Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104417 articles
Browse latest View live

Diamond Amzuia Zari Kujifungulia Afrika Kusini, Ataka Ajifungulie Bongo, Amuanzisha Clinic Hapa hapa

0
0
Habari zilizosambaa leo mitandaoni moja wapo ni hii ya Diamond Kumzuia Zari Ambae ni mama Kijacho wake kwenda kujifungulia Sauz Afrika...Inasemekana Diamond Anataka ajifungulia hapa hapa Bongo Muda utakapo fika ili iwe rahisi familia nzima kufurahi nae badala ya kusafiri mpaka Sauz.

Tayari Diamond Ameshamuanzishia Zari Clinic ya Hapa Bongo kwenye Hospitali ijulikanayo kama AMI iliyoko Masaki 

Gwajima Akana Utajiri Wake, Adai Alivyonavyo Kwa Sasa ni Baraka za Mungu Lakini si Utajiri

0
0
ASKOFU Josephat Gwajima wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, amesema yeye si tajiri kama inavyodhaniwa, bali alichonacho ikiwa ni pamoja na nyumba, magari na helikopta ni baraka tu za Mungu, lakini kama ni utajiri, anatarajia siku moja utamshukia.

Aliyasema hayo jana wakati akihubiri kanisani kwake Kawe, Dar es Salaam, ambako alisema anawashangaa watu wanaomfuatilia maisha yake huku wakisema yeye ni tajiri mkubwa.

“Wanaodai mimi ni tajiri wana wivu tu na wananionea, mimi si tajiri, bali ni masikini kama walivyo masikini wengine. Natarajia kutajirika hapo baadaye waumini wangu wakiwa matajiri, siwezi kutajirika kama waumini wangu bado ni masikini, nitatajirika pamoja nao,” alisema Gwajima.

Kuhusu mgogoro unaoendelea baina yake na Jeshi la Polisi, Askofu Gwajima alisema yeye anauona kama ni vita vya kiroho na hivyo ataendelea kumwomba Mungu ili amsaidie kupambana na kilichopo mbele yake na anaamini kuwa atashinda vita hiyo kwa uweza wa Mungu anayemtegemea.

“Mungu wangu na awasamehe wote wanaonituhumu kuwa mimi ni tajiri na kuamua kudhoofisha huduma, nasema huduma yangu haitakufa kamwe na wala hatutayumba katika mipango yetu ya kuhubiri injili. Tutapigana kwa uweza wa Mungu na tutashinda kama alivyosema kuwa tutapigana pamoja naye na tutashinda,” alisema Gwajima.

Akizungumzia afya yake, Askofu Gwajima alisema kwa sasa anaendelea vizuri na anaweza kusimama na kutembea, kuhubiri kama ilivyokuwa hapo awali na hatarajii kurejea tena kwenye kiti cha baiskeli ya magurudumu matatu bali atasimama imara daima.

Kuhusu kupeleka nyaraka kadhaa anazotakiwa aziwasilishe polisi siku ya mahojiano Aprili 16, mwaka huu, Askofu Gwajima alisema suala hilo bado wanasheria wake wanalishughulikia na wataendelea kufuata taratibu zote zinazotakiwa na jeshi hilo.

Gwajima anatakiwa kuwasilisha nyaraka muhimu za hati ya usajili wa kanisa lake, namba ya usajili wa kanisa, hati ya umiliki wa helikopta, hati ya nyumba anazomiliki, idadi ya makanisa yaliyopo chini yake pamoja na hesabu za fedha za kanisani kwake zinazohusu mapato na matumizi.

Nyaraka zingine ni majina ya Bodi ya Udhamini wa kanisa, mpiga picha za video kanisani kwake siku ya ibada na shughuli zingine za kanisani hapo pamoja na waraka wa Maaskofu uliosomwa makanisani ambao Mwadhama Polycarp Kadinali Pengo alioupinga na kusababisha yeye kumkashifu kiongozi mwenzake huyo wa dini.

Akionekana kuwa makini sana na lugha anayotumia wakati wa kuhubiri, Gwajima aliwaomba waumini wake waendelee kufuatilia kila sehemu na kuchunguza mambo yote mabaya yanayosemwa juu yake na kanisa lake na kuyaripoti kwake au kwa uongozi wa kanisa ili wayafanyie kazi mara moja kabla hayajaleta madhara.

“Nawaombeni sana mfuatilie kila chanzo cha habari na kuchunguza mambo yote yanayosemwa juu yangu au kuhusu kanisa na kuyaleta mara moja hapa kanisani ili tuyafanyie kazi kabla hayajaleta madhara makubwa,” alisema Gwajima.

Aliongeza kuwa, “tuendelee kuwa na umoja katika kipindi hiki ambapo shetani anataka kupigana nasi ili tuweze kushinda. Tukifarakana hatutaweza bali tukiwa kitu kimoja tutasonga mbele na kuwa huru”.

Utajiri wake

Wakati akikana kuwa tajiri, mwanzoni mwa mwaka jana alifanya mahojiano na gazeti hili na kukiri Mungu anambariki, ndiyo maana mambo yake yanamnyookea.

Aliyasema hayo alipokuwa anazungumzia mpango wake wa kununua helikopta kwa ajili ya huduma za injili ndani na nje ya nchi.

Alikiri kutokana na utajiri anaosema unatokana na baraka za Mungu, anamiliki jumba la ghorofa nne eneo la Mbezi Beach katika Manispaa ya Kinondoni.

Pia amewanunulia wachungaji wake 40 magari ya kutembelea kwa bei tofauti, yakiwemo ya chini ya Sh milioni 10 na mengine ya zaidi ya Sh milioni 20.

“Ni kweli nimewanunulia magari, unajua moja ya misingi yangu ya maisha ni kwamba, mimi siwezi kuishi maisha mazuri, wakati wachungaji wangu wanadhalilika, nimewanunulia magari karibia 40. Lakini nina wachungaji wa ngazi mbalimbali, hawa ni wale wa juu, wengine wachungaji wadogo wapo zaidi ya 670, hawa ni watenda kazi muhimu na wanatofautiana kwa ngazi zao, ndio maana kazi ya Mungu inasonga mbele hata nisipokuwepo,” alisema Gwajima.

Tanzania tuliivamia DRC kuwatoa M23 mbona kigugumizi kuwang'oa Alshaabab?

0
0
Nimekuwa nikishawishi serikali yetu mara kadhaa kuwa kuna haja ya Tanzania kuivamia Somalia kijeshi kwa kushirikiana na majeshi mengine ya Afrika yaliyoko Somalia ili kuwang'oa Alshaabab.

Kuna haja ya sisi watanzania kufanya hivyo kwani kwa sasa ni dhahiri ndugu zetu wa Kenya wanakaribia kuzidiwa nguvu na hawa alshaabab.

Ikumbukwe wakati alshaabab wanaanza harakati zao walikuwa wanateka meli tu ambazo zilikuwa zinapita pwani ya Kenya na Somalia na kuteka watalii kisha kutoa rai ya kubadilishana mateka na fedha.

Kwa sasa wamejipanua na kutaka kuanzisha jamuhuri yao hivyo kuwa tishio zaidi huku wakijipambanua kwa mgongo wa uislamu!

Na endapo wakiachwa watawale kama wanavyofanya sasa baada ya muda pwani nzima ya Afrika mashariki haitokuwa salama tena.

Kuna vitisho kadhaa ambavyo hufanya alshaabab endapo unaenda kwenye ardhi yao kuwapiga kama vile kutoa maneno ya vitisho, kufanya mashambulizi ya kushtukiza kwa raia na kutesa wanajeshi wanaowakamata/kuwateka.

Mfano, Marekani ilipoivamia Somalia kuwapiga alshaabab, kwa bahati mbaya alshaabab wakamkamata askari mmoja wa Marekani, wakamuua kikatili kisha kuanza kumburuza akiwa amefungwa nyuma ya gari mitaani Mogadishu. Baada ya kuona tukio lile raia wa Marekani wakapiga makelele serikali yao iwaondoe askari walioko Somalia. Kweli askari wengi wakarudishwa Amerika. Kitisho kile kikawa kimefanikiwa.

Wametoa vitisho pia mara kadhaa kwa serikali ya Kenya na Uganda kwa kuwavamia na kuua raia wao mara kadhaa kama ile ya westgate, Garissa, nk.

Tusiogope vitisho tuna jeshi imara ambalo halina shaka na tumelipa sifa kila uchao.

Twendeni Somalia!!

Shukrani A. Ngonyani,

Dar Es Salaam,

April 9, 2015.

00255784 37 97 99

MALI ZA GWAJIMA ZAANIKWA: Akisiwa Kuwa Mchungaji Tajiri Afrika!

0
0
Sakata la Gwajima limechukua sura mpya baada ya mchungaji huyo kutakiwa na jeshi la polisi kupeleka nyaraka mbalimbali zinazohusu umiliki wa mali zake!

Mchungaji Gwajima katika kupingana na amri hiyo halali ya jeshi la polisi, amekimbilia kwa mawakili, ili tu kuweka pingamizi la yeye kuthibitisha umiliki wake wa mali alizonazo na namna alivyozipata.

Itakumbukwa kuwa jeshi la polisi lilimtaka Gwajima apeleke nyaraka zifuatazo: Hati ya usajili wa kanisa lake, namba ya usajili wa kanisa lake, hati ya umiliki wa helikopta, hati za nyumba anazomiliki, idadi ya makanisa yaliyopo chini yake na taarifa za mapato na matumizi ya makanisa yake.

Nyaraka zingine ni: majina ya bodi ya udhamini wa kanisa na waraka wa maaskofu uliosomwa makanisani ambao Kardinali Pengo aliupinga!

Taarifa kuhusu mali za Gwajima ni hii hapa:

...Gwajima ana miliki nyumba nne za ghorofa Mbezi beach na kwa mujibu wa ripoti ya uthamini wa nyumba hizo jumla zina thamani ya bilioni 11 na milioni 400 (11.4 bilioni) pesa za Kitanzania.

...Pia ana nyumba nyingine kadhaa kwenye maeneo mbalimbali nchini ila hadi hivi sasa taarifa za uhakika za thamani ya nyumba hizo bado hazipo wazi.

...Gwajima ana miliki helikopta moja na magari ya kifahari kama vile Hammer, Range rover. Magari mengine ni Nissani Murano, Land Rover 4 na Land Cruiser V8.

...Gwajima pia amenunua magari mengine 40 yenye thamani kati ya Tshs 10 milioni na Tshs 20 milioni na kuwapatia wachungaji wake kote nchini kwa ajili ya shughuli zao binafsi na magari yote hayo yapo chini ya umiliki wake.

...Inakadiliwa kuwa akaunti binafsi za Gwajima zilizopo hapa nchini zina zaidi ya Tshs 20 bilioni ikiwa ni fedha zilizopo nje ya fedha za akaunti ya kanisa.

Aidha, pamoja na yeye mwenyewe kutaarifu juu ya mali zake kama ambavyo zimeorodheshwa hapo juu, lakini siku ya jana akiwa anahubiri kanisani kwake alikana kuwa yeye sio tajiri! 

Gwajima alikaririwa akisema kwamba mali zote anazomiliki ni baraka tu za Mungu na sio kwamba yeye ni tajiri. Gwajima alisisitiza kuwa yeye ni maskini kama walivyo maskini wengine wakiwemo wahumini wake, na wanaosema yeye ni tajiri wanawivu na wanamuonea. 

Source: HabariLeo

Look what Zari is Doing with her sons

0
0
Look what Zari is Doing with her sons..
Happy People...

Pole Aunty Ezekiel kwa hili. Msamehe bure. Ni elimu tu Hana Huyo na ni Limbukeni wa Mitandao

0
0
Kweli mitandao ya kijamii ina kazi. Ukiwa na moyo mwepesi mitandao hii inaweza kuwa sio wazo zuri sana kwako.

Leo kupitia mtandao, mwanadada Aunty Ezekiel amepata na jambo ambalo kwa upande wetu tunaona si la kiungwana hata kidogo baada ya jamaa mmoja kuandika maneno yasio ya kibinadamu hata kidogo kwenye picha moja aliyoiweka mwanadada huyo ambaye ni mjamzito .

Aunty Ezekiel aliweka picha yake akiwa na Wema Sepetu ambaye hapo jana aliamua kufungua juu ya tatizo lake linalomsumbua la kutoweza kushika ujauzito, na baada ya kuweka picha hiyo ndipo alipopatwa na dhahama hiyo baada ya jamaa huyo kuandika kuwa anatamani aunty Ezekiel akijifungua tu afe pamoja na mtoto wake huyo, jambo ambalo si la kibinadamu kabisa kumuombea mtanzania mwenzako

Yani ukijifungua naomba ufe na mimba yako maana utakachozikaa kimelaaniwa” Hayo ndio yalikuwa maneno ya kijana huyo.

Baada ya kauli hiyo Aunty Ezekiel aliamua kuandika haya yafuatayo…

Ukiacha yote ktk Maisha naamini Duniani tunapita na kila mmoja wetu yupo ktk safari ugumu ni kutangulia na Mwenyezi Mungu si wa kwako wala wakwang na ndio mana kila mmoja anatimiziwa haja zake kwa nafasi yake Nataka nikwambie tuu ww kaka uliyeandika maneno hayo kwang leo kuwa ww ni wa Mwenyezi Mungu pia dua lako linawezekana kusikilizwa na likasikilizwa haraka couse wala haupo peke yako ila ww ndie pekee uliepata ujasiri wa kuandika wengine watakuwa wanaomba kwa chini ila wote tumuombae hayo ni huyo huyo mmoja hvyo bac tumuachie yy Inshaalah ndio anajua mwisho wa kila mmoja wetu.Furaha ni ya zamu utakapokuwa unafurahia Umauti wang Familia yang itakuwa ikilia kwa hilo na ifikapo kwako ww unaeniombea hilo kila kukicha ni hvyohvyo pia kwa familia yako.Hvyo nina Aman yakutosha tu kwakuwa mm ni wakwake pia Sikujiumba.WHN JESUS SAY YES NO BD CAN SAY NO....love u all.....

Pole sana Aunty Ezekiel. Tunakuombe ujifungue salama.

Nini maoni yako?

High Performance Debt Collection Course, 23rd – 24th April, Colosseum Hotel, Dar es Salaam…

0
0
Credit Debt Masters Ltd.
Due to a high a demand, the most successful training course on Credit/Debt Management that maximizes cash flows will be repeated on 23rd to 24th April at Colosseum Hotel & Fitness Club, Dar es Salaam.
We have only allocated a few seats for a greater one to one approach, group discussions, presentations and lots of fun…don’t miss the great opportunity to turn your debts into once again cash flows and improve your systems for a higher results…call us on 0763 200 332 for the few reservations left…

How Come Hizi Ajali Zitokee Kwa Kiasi Kikubwa Hivi Kipindi Hichi na Kuua Watu Wengi ?

0
0

Siku hizi ajali zimekuwa nyingi sana barabarani tena nyingi zikihusisha mabasi ya abiria kugongana na lori au basi kwa basi na kusababisha ndugu zetu wengi kupoteza maisha.. Ukifatilia kwa makini utaona nyingi zinasababishwa na Madereva wetu ku-overtake gari la mbele yake sehemu zenye hatari.. Hiii inasikitisha sana maana watu wengi wanapotea kwa uzembe mdogo tu.

Je haya pia ni mapenzi ya Mungu kuwa watanzania wapoteze maisha kwa ajali zisababishwazo na uzembe barabarani pamoja na mwendokasa? 
Kwa upande wako wewe, una lipi la kusema juu ya hili?

Gwajima:Nitaendelea Kuwapa VIDONGE vyenu Kila Mtakapo potoka, Nafanya kazi ya Bwana, Mbona Wengine Wakitoa Misimamo yao Hamuwafuati?

0
0
Madaktari, wanasiasa, wafanyabiashara wamekuwa wakitoa misimamo yao lakini hawabughudhiwi iweje Gwajima tu? Nitaendelea kuwapa vidonge vyenu kila mtakapopotoka, nafanya kazi ya bwana,” alisema Gwajima

Kuhusu utajiri wake pia Gwajima amesema anashangazwa na vyombo vya Serikali vinavyohoji utajiri alionao bila kujua anaongoza idadi gani ya waumini. Alisema anaongoza kanisa lenye waumini zaidi ya 70,000 ambao akiwaomba kila mmoja ampe Sh1,000 tu atakuwa na Sh70 milioni, na kama wakiamua kutoa elfu 10, 000 basi atakuwa na milioni 700.

Nini mtazamo wako katika hili? Na unapenda mwambia nini Gwajima?

Wanachama wa Chama Kipya Cha ACT- Tanzania Wapigwa Marufuku Kushabikia UKAWA'

0
0
Chama cha ACT-Wazalendo kimesema kila mwanachama anapaswa kuwaunga mkono wagombea watakaopitishwa na chama hicho katika nafasi mbalimbali katika Uchaguzi Mkuu ujao, kwani kinyume chake ni kukisaliti na adhabu yake ni kufukuzwa.

Mwenyekiti wa chama hicho, Anna Mghwira alisema mwishoni mwa juma kuwa katika kipindi hiki cha kuelekea kwenye Uchaguzi Mkuu, chama hicho kinahitaji nguvu za pamoja.

“Sisi bado hatujajiunga na Ukawa, hivyo wanachama wetu wanapaswa kulitambua hilo na kuepuka kushiriki kwenye ushawishi wa kufanya kampeni za wagombea wa vyama vingine. Hata kwenye katiba yetu tunasema sasa tunalenga zaidi katika kujiimarisha ili kutoa ushindani mzuri wa kisiasa katika uchaguzi huu,” alisema.

Katiba ya ACT, imeeleza wazi kuwa pamoja na sababu nyingine na kwa mujibu wa kanuni zitakazotungwa na Halmashauri Kuu, mwanachama yeyote ambaye atasaidia kushawishi, kujiunga, kutoa tamko la kuunga mkono chama kingine au mgombea wakati chama kimeweka mgombea wake kwa mujibu wa sheria za nchi, atakuwa amepoteza uanachama wake.

ACT- Wazalendo tayari imetoa ilani yake ya uchaguzi ikionyesha kwamba iwapo itaingia madarakani, itawajibika kwa wananchi kwa kuweka kipaumbele katika maeneo manne ambayo ni hifadhi ya jamii, uchumi shirikishi wenye kuzalisha ajira nyingi na bora, afya na elimu.

Kauli hiyo ya ACT linakuja huku kambi ya vyama kadhaa vya upinzani vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), ikiwa kwenye mchakato wa kuunganisha nguvu ili kusimamisha mgombea mmoja wa urais na kuachiana majimbo katika baadhi ya maeneo.

Mwenyekiti mwenza wa Ukawa, James Mbatia amewahi kunukuliwa akisema kuwa umoja huo unaoundwa na Chadema, CUF, NCCR-Mageuzi na NLD umehamishia nguvu zake kwenye Uchaguzi Mkuu wa 2015.

Mbatia alisema tayari umoja huo umeunda kamati maalumu kutafuta namna ya kumsimamisha mgombea mmoja wa urais na kuachiana majimbo.

Mbatia ambaye pia ni Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi, alisema tayari kamati zimeundwa na zinaendelea na kazi ya kuratibu mpango huo mahsusi, unaolenga kuiondoa CCM madarakani.

Lengo letu ni kuhakikisha Ukawa ina nguvu ya kushika dola katika Uchaguzi Mkuu wa 2015 na katika mpango huo, vyama vitaachiana majimbo na viti vya udiwani kulingana na nguvu ya chama katika sehemu husika,” alisema.

Mkakati huo uliopangwa na Ukawa, unaelezwa na wachambuzi wa masuala ya kisiasa kuwa ni kombora kwa CCM, kwani endapo utafanikiwa, utakiweka chama hicho tawala katika wakati mgumu katika Uchaguzi Mkuu uliopangawa kufanyika Oktoba mwaka huu.

Nay wa Mitego aeleza kwanini alinunua sanamu ya shetani kwa shilingi milioni 5

0
0
Nay wa Mitego ni mtu wa maamuzi na mapenzi tofauti na wengine. Ndio maana ukiingia ndani kwake utakutana na sanamu isiyo ya kawaida – ni sanamu ya shetani!

Rapper huyo ameiambia Bongo5 kuwa sanamu hiyo ni moja ya vitu anavyovipenda zaidi ndani mwake.

“Mimi naipenda na niliinunua hela nyingi tu, ni dola elfu tatu,” amesema Nay.

“Nilitokea tu kuipenda, ni moja kati ya vitu muhimu ninavyovipenda ndani ya nyumba yangu. Kuna sehemu niliinunua sio Tanzania. “Mimi nilitokea kukipenda yaani naipenda sana tena sana na hata ukiingia ndani kwangu utaanza kuiona hiyo,” amesisitiza rapper huyo.

Miili 15 ya Waliokufa Katika ajali ya Basi na Lori Kilosa yazikwa Kwenye Kaburi Moja Baada ya Miili yao Kutotambulika

0
0
Miili ya watu 15 kati ya 19 waliopoteza maisha katika ajali ya basi na lori mkoani Morogoro imezikwa leo katika makaburi ya Pamoja ya Msanvu wilayani Kilosa mkoani humo.

Mamia ya wakazi wa wilaya za Kilosa na Kilombero wamejitokeza katika mazishi ya pamoja ya watu 15 kati ya 19 waliofariki katika ajali ya basi ya Nganga ambalo liligongana na fuso kisha kuwaka moto katika eneo la Iyovi na kuzikwa katika kaburi la pamoja kwenye makaburi ya Msamvu Ruaha wilayani Kilosa mkoani Morogoro.
Wakizungumza kwa niaba ya serikali ya mkuu wa wilaya ya Kilosa John Henjewele amesema serikali imewalazimu kufanya mazishi ya pamoja ya watu waliofariki kwenye ajali hiyo ambao miili yao haijatambulika.
Pia amesema serikali itaendelea na zoezi la ukaguzi wa magari mkoani wa Morogoro ili kudhibiti ajali za mara kwa mara na kupoteza maisha ya watu huku wengine wakiachwa na vilema vya maisha.
Naye mkuu wa wilaya ya Kilombero Lephy Gembe amewataka wananchi kuwa na uvumilivu katika msiba mkubwa walioupata.
Kwa upande wake diwani wa kata ya Ruaha Rahel Nyangasa amesema wamepokea msiba huo kwa masikitiko makubwa kwani umekuwa ni pigo kubwa kwa wakazi wa wilaya hizo.
Ndugu na waombolezaji nao wamesema msiba huo si wakusahaulika kwani umewashtua sana na muinjilisti wa kanisa la kiinjili la kilutheri Issaya Chura akiomba serikali kuendelea kukabiliana na madereva wabovu.

Mama Ajifungua Mtoto na Kisha Kumtupa Katika Shimo la Takataka ( Jalala) jijini Mwanza

0
0
Mama mmoja mkazi wa kata ya Mkuyuni-Sokoni wilayani Nyamagana jijini Mwanza (jina lake halikufahamika mara moja) amejifungua mtoto wa kiume na kisha kumtupa kwenye shimo la kutupa taka (jalala) eneo a Mkuyuni jijini hapa.
 
Akizungumza na waandishi wa habari, mmoja wa watoa taarifa kwa viongozi wa serikali aliyetoa sharti la kutotajwa jina lake amesema:
 
“Mimi ni mfanya usafi hapa Mkuyuni, wakati ninaenda kumwaga uchafu pale dampo nikakuta kitoto kichanga kimetupwa maeneo hayo ndipo nilipoenda kutoa taarifa kwa Mwenyekiti wa Mtaa wa Mkuyuni-Sokoni ili wafanye utaratibu wa kukitoa hapo:”
 
Naye mwenyekiti wa mtaa wa Mkuyuni, Godwin Peter  Kyangara,  amesema: “Mimi nimeletewa hizi taarifa za mtoto huyu aliyetupwa maeneo haya mida ya saa 2:30  asubuhi, baada ya kupokea taarifa hizo ikabidi nikatoe taarifa kwa Jeshi la Polisi ndipo walipokuja kuuchukua mwili wa mtoto huyo.”
 
Inasemekana kwamba mtoto huyo alikuwa tayari ana umri wa miezi tisa hivyo mzazi wake alikuwa tayari amejifungua ndipo alipoamua kumtelekeza kwenye shimo hilo la kutupa takataka.
 
Kwa upande wake, diwani wa kata ya Mkuyuni, Charles Fashion, ameeleza kuwa ameshangazwa na kitendo hicho cha mwanamke kujifungua mtoto na kumtupa jalalani ambapo alisema inabidi atafutwe na apewe adhabu iwe fundisho kwa akina mama wengine wenye tabia kama hizo katika jamii.
 
Aidha, Jeshi la Polisi jijini Mwanza limethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kuongeza kuwa bado juhudi za kumtafuta mwanamke huyo aliyetenda unyama huo zinaendelea ili afikishwe mahakamani  kujibu mashtaka yanayomkabili.




Mpekuzi blog

Irene Uwoya Aumizwa na Maneno ya Wema, Ampongeza Wema kwa Moyo Wakishujaa

0
0

Irene Uwoya  Aumizwa na Maneno ya Wema, Ampongeza Wema kwa Moyo Wakishujaa
 
Minashindwa kuwaelewa watu ni kwanini mnapenda sana kutaka kutoa kibanz kwenye jicho la mtu wakat kipande chamti kiko kwenye jicho lako.....nimeumia sana na maneno ya wema,mtoto anapanga MUNGU sio binadamu .....Embu mwachen mtoto wa watu sasa awenaaamani kila siku mnamsema yeye mmnazan anachuma nin Ana moyo,afu kunawatu wanapenda sana kudandia mambo ........mmedandia weweee mme mtukana mtoto wawatu minaomba niwape namba ya MUNGU mumulize yeye kwanin na mumuache mtoto wa watu!sipendag kuingilia mambo ya watu lakin imezid sasaaaaa!!!!!sio vizuri jiweken nafas yake muone kama hamjajinyonga!WEMA kiukweli unamoyo wa kishujaaa sana napenda sana mwanamke awe hivyo MUNGU ndoanamajibu yote achana nao wenye kudandia yasiyo wahusu maana watajikuta wapo kama pweza wanamiguu lakin kusimama hawawez.....”-Irene Uwoya ameandika kwenye ukurasa wake mtandaoni.

Hii ni baada ya Wema hivi majuzi kufunguka mtandaoni kuwa anatamani sana kuwa mtoto lakini huwezo  hana.

Hofu ya Mbowe na CHADEMA juu ya Zitto Kabwe na Chama chake Kipya

0
0
Kwa takribani kipndi kama cha mwezi mzima uliopita kumeibuka msuguano mkubwa sana hasa kwenye mitandao ya kijamii kati ya wafuasi wa CHADEMA dhidi ya wafuasi wa chama cha ACT.

Msuguano huo hasa unahusisha wale wafuasi wa CHADEMA kurusha tuhuma nzito dhidi ya aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu wa CHADEMA ndugu Zitto kwa kumuita -------, Anatumiwa na CCM kuuwa upinzani, Anaandaliwa mikutano yake na CCM na shutuma nyinginezo nyingi nyingi tu sina haja ya kuzirudia hapa.

Lakini kwa upande wa huyo aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu wa CHADEMA yeye alishapigia mstari kule alikokuwepo na ameanza safari yake mpya katika chama kipya na ambacho amakiasisi yeye mwenyewe wakati akiwa bado na kesi dhidi ya CHADEMA na hatukuwai kumsikia ama haijathibitishwa ya kwamba huko ACT alipohamia amekuwa akiwatuhumu ama kuwashambulia viongozi wa chama chake cha zamani lakini pia chama chake cha zamani.

Sasa nirudi katika hoja ya kwanini Mbowe, Slaa na baadhi ya wanachama wa chadema walio watiifu kwa Mbowe na wale wafuata mkumbo wanahofu dhidi ya ZITTO?

Ni ukweli usiopingika Mbowe na Zitto ndio waliotumia muda mwingi kukijenga chama hicho na kuwaaminisha Watanzania kwamba muarubaini wa matatizo yao umepatikana na katika pilika za kukujenga chama hicho ndugu Zitto aliwavutia vijana wengi sana kuipenda siasa hasa ikizingatiwa kipindi kile hakukuwa na vijana waliokuwa wanavutiwa na siasa.

Kwa mantiki hiyo ndani ya CHADEMA kuna viongozi wengi ambao wamekuwa wakinungunika muda mrefu sana kutokana na aina ya uongozi wa mabavu ambao mwenyekiti na katibu wake pamoja na wale vipenzi vyao wanaoutumia.

Na wamekuwa hawana sehemu ya kusema kwa kuwa wako ndani ya chama lakini wametengwa na ni wanamageuzi wa ukweli kabisa nikiwa na maana hawawezi kuhamia chama tawala kwa hiyo wamekuwa kwa muda mrefu wakivumilia vurugu zote na mabavu ya Mwenyekiti na genge lake.

Sasa hofu inakuja zaidi kwa Mwenyekiti na genge lake kwa kuwa wale Makamanda sasa wanamahali pakuelekea na hasa baada ya kuona mwanzo wa ziara za ACT na hali yakuwa Makamanda hao wanaushawishi mkubwa sana katika jamii inayowazunguka.

Wasalaam

Nimeshindwa Kuwa Rubani wa NDEGE Sababu ya Filamu-Uwoya

0
0
Mwigizaji katika tasnia ya filamu Tanzania Irene Uwoya amesema kuwa filamu zimeharibu mipango yake ya miaka mingi ya kutaka kuwa mwongozaji wa ndege yaani Rubani.

Irene alisema hayo weekend hii kupitia kituo cha Radio cha East Africa Radio na kudai kuwa miaka yote aliyokuwa akisoma lengo lake kubwa lilikuwa ni kuja kuwa muongozaji wa ndege Rubani kwani ndiyo kazi aliyokuwa akiipenda na alianza kusoma masomo ambayo aliamini moja kwa moja yangeweza kumfanya kufikia ndoto hizo.
Amesema ndoto yake hiyo iliingia ukakasi baada ya kuanza kufanya filamu za bongo na kujikuta sasa maisha yake yapo kwenye filamu zaidi.

Irene uwoya ambaye alikuwa ni mke wa ndoa wa mchezaji mpira Sulemani Yamin Ndikumana alisema kati ya mwaka 2007 na 2008 ndipo alipoingia katika tasnia ya filamu ambapo anadai kuwa hakuichukulia serious kazi hiyo, sababu tayari alikuwa na mipango ya kusoma na kuja kuwa rubani lakini aliamua kuingia katika tasnia hiyo kufuatia kushawishiwa na baadhi ya watu ambao waliamini kuwa anaweza kuigiza.

"Katikati ya mwaka 2007 na 2008 ndipo niliingia katika tasnia ya filamu nchini tena kwa kushawishiwa na baadhi ya watu, ila mimi nilikuwa nafanya tu sikuwa serious kabisa maana mimi malengo yangu yalikuwa nisome nije kuwa rubani, lakini baada ya kuanza kufanya nikaona watu wananikubali na kupenda kile nikifanyacho na nilipoanza kupata mafanikio nikaona okay kumbe hii ni kazi nikaanza kufanya kazi sasa."

"Nikajikuta sasa maisha yangu yote yameegemea katika filamu na nikaanza kufanya filamu kama maisha mpaka sasa, ingawa kuna kipindi nilikuwa kimya kidogo kutokana na matatizo ya ndoa yangu, maana hakuna kitu kilikuwa kinanitesa kama maneno ya watu, ilifika kipindi nilikuwa siwezi kufanya jambo lolote kwa kuhofia watu, maana nilikuwa naona kama watu wananizungumzia mimi, hivyo kipindi kile kilinirudisha nyuma kidogo, lakini nashukuru Mungu baadaye niliona ni suala la kawaida, maana kuna watu wengi walikuwa katika ndoa na mwisho wa siku ndoa zao zilivunjika na maisha yaliendelea kuanzia hapo ndipo nilipata nguvu na kurudi kuendelea na kazi kama awali, ila kipindi hicho kwa kweli kimenipa taabu sana" Aliongeza Irene Uwoya.

Mbali na hapo Irene alizidi kuweka wazi kuwa kupitia filamu amefanya mambo ya maendeleo mengi sana ikiwepo kuishi maisha yake ayatakayo yeye pasipo kumtegemea mtu yoyote, lakini pia filamu zimeweza kumjengea nyumba ambayo anadai nyumba hiyo inakamilika muda si mrefu tokea sasa.
Amesema hiyo ni mbali na ziara nyingi na mialiko mingi aipatayo nje ya nchi ambayo nayo humjenga na kumpa nafasi zaidi katika kukutana na watu ambao nao wanakuwa na msaada katika kumtengenezea network nzuri ya kazi yake ya sanaa.

Licha ya kuzungumzia mambo mazuri ambayo ndani ya tasnia ya bongo movie lakini Uwoya alisema kuwa kwa sasa tasnia hiyo inaingiliwa na watu ambao wengi wao hawana vipaji wala uwezo wa kuigiza na wanapewa nafasi jambo ambalo linasababisha tasnia hiyo kushuka chini, hivyo anadai kuwa kwa sasa ana mpango wa kukaa na wasanii wenzake.
wakubwa ili waweke mpango wa kuona jinsi gani wanaweza kuzuia watu wasio na vipaji kutoingia katika tasnia hiyo na kuiharibia jina tasnia ya bongo movie ambayo imeweza kubadili maisha ya vijana wengi na kutoa ajira pia kwa vijana wengi.

Wanawake Wanaojiona Warembo Sana Uishia Kusimamia Harusi za Wenzao Wengi Hawaolewi

0
0
Nimeenda harusi nyingi wanawake wanaoolewa ni wale wa kawaida na wenye kujitambua,hawa wanaojiita warembo wengi wao hawaolewi na huishia kusimamia harusi za wanawake wenzao tu.

Pia wengi huishia kuwa nyumba ndogo,sababu kuu zinazofanya wasiolewe ni wengi wanakuwa wanataka kuishi maisha ya tamthilia za ng'ambo anataka mwanaume tajiri awe mtanashati sana.

Pia wanapenda sana matumizi makubwa story zake ni kuhusu matumizi ya hanasa,wanaume wengi ushtuka na kuishia ku hit na kusepa.

Hawaridhiki anakuwa anajiona mzuri sana hivyo mkikorofishana kidogo na akatongozwa nje basi uishia kwenda nje. Wengi huishia kutumiwa tu na kuachwa kwa sababu ya tabia zao na tamaa.

Kisa cha Wema Sepetu Kilichomfanya Aandike Ujumbe wa Kusikitisha Kuwa Hana uwezo wa Kuzaa Hichi Hapa

0
0
Ilianza Hivi:
Muigizaji maarafu wa filamu nchini Tanzania,Wema Sepetu alizomewa kwenye mtandao wa kijamii wa Instagram baada ya kuweka picha ya mlimbwende Hamisa Obetto akiwa mjamzito na kuandika maneno ya mshangao

”Jamani my mdogo umezaa.!wewe ni mwanamke sasa”.

Ujumbe huo ulizusha tafrani kwa baadhi ya watu na kumjibu Wema kwa maneno makali yenye kebehi ya kwa nini yeye hazai anakaa kushabikia watoto wa wenzie tu.
Gumzo hilo lilifwata mkondo tofauti pale ambapo mchumba wake wa zamani mwanamuziki Diamond Platinum akitarajia kupata mtoto na bi.Zari kutoka Uganda ambaye ni mpinzani wake mkubwa Wema.

Wema Sepetu aliweza kujibu tuhuma hizo kwa kusema yeye si mpanga wa yote,''ningekuwa na uwezo wa kuzaa angezaa siku nyingi ila ni Mungu ndiye anapanga'',

Alisema kuwa ''nimekuwa nikihangaika kupata mtoto usiku na mchana''

aliongezea kusema kuwa si rahisi kwa yeye kuwaambia kila kitu,kwani yeye pia ni binadamu na kuwa
''anaumia sana na maneno makali watu wanayoandika au kusema kumhusu''.
Ujumbe wa simanzi kutoka kwa muigizaji huyo ulirudiwa na baadhi ya waigizaji kama Iren Uwoya na mashabiki wengine
ukionya tabia ya watu kutoa matusi makali kwa Wema bila kuangalia upande wa pili,maana siku hizi kuna team kwenye mtandao pia zikijiita team Wema na Team Zari

Zari Is Not 41 Years Old! Diamond Platnumz Reveals Her Real Age

0
0
Bongo flava star Diamond Platnumz has jumped to the defense of his Ugandan lover, Zari over her age.

In a recent media interview in Tanzania, “The Ntampata Wapi” hitmaker disclosed that she’s 34, putting an end to rumors that she was 41 years old. This comes months after the two have overcome criticism for their huge age difference. They are rumored to have wed in a secret ceremony.

Diamond, 25, also revealed that they will be expecting the birth of their child either in July or August.

Shutuma za Albert Msando Kukimbia na Kutelekeza Wananchi Wake Walio Mchagua Kama Diwani Moshi

0
0
Nimekutana na Hili Jamii Forums....Nikaona si la Kupuuzia ..Alberto Msando Ana la Kujibu Hapa

"Akiwa kijana mdogo, msomi na mwenye mvuto wa kisiasa wakazi wa mabogini walikupa heshima ya kuwa diwani wao.

manispaa ya moshi ndio yenye madiwani wengi wa CDM kati ya nyingi nchini. Msando aliaminiwa.

Ajabu na kweli amekimbia kata, haonekani, wananchi wana hasira sana na huyu jamaa.

kama ni kukikomoa chama cha Chadema kwa kutokufanya kazi ulioomba wananchi na kukiri unaiweza basi umejimaliza mwenyewe.

Ukiwa kijana unapokwenda mbele ya wananchi uwe mkweli, wananchi huchagua mtu mara nyingi sana kabla ya chama. ndio maana hupiga kura. Kura zilipigwa na watu wote kukuchagua bila kujali itikadi ya kisiasa.

Leo umewaacha wananchi wako kama huwajui vile.

Diwani wa mabaogini Albert Msando umetia aibu kubwa sana - Mungu akuonyeshe kweli huko ulipo sasa"

Written By Chief Mkwawa- 360 degreee via JF
Viewing all 104417 articles
Browse latest View live




Latest Images