Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104684 articles
Browse latest View live

Busu la Kajala Lilinifanya Nilale Usingizi Mnono- Senga

$
0
0
Mchekeshaji maarufu Bongo, Joseph Senga ‘Senga’ amefunguka kuwa busu alilompiga staa wa kike wa filamu, Kajala Masanja lilimfanya alale usingizi mnono sana ukizingatia kuwa hajawahi kubusu shavu laini kiasi hicho kwasababu warembo wengi wanazingua.

Akizungumza na Centre Spread, Senga alisema alipata fursa hiyo ya kumpiga busu wakati wakiigiza filamu matata ya Pishu iliyoandaliwa na Kajala Entertainment, itakayoingia sokoni Mei Mosi, ambapo alisema anajikubali katika filamu hiyo ambayo anaamini itavunja watu mbavu.

Wewewee umpige busu Kajala utashindwa kulala kweli jamani,yaani nilishtuka kumeshakucha kabisa lakini pamoja na yote mimi ni mchekeshaji ila kwa filamu ya Pishu nimeinua mikono,” alisema Senga.

Check Out Linnah Sanga's New S3xy Photos..Is She Really Pregnant??

$
0
0
May be she had just eaten a lot, she never said she was pregnant, watanzania with their speculations ..

Below are the new photos...

Kama Rais Uhuru wa Kenya Leo Ameweza, Kwetu Rais Kikwete Tatizo Nini?

$
0
0
Leo hii raisi wa kenya amewasimamisha kazi wa kuu wa chombo kinacho simamia udhibiti wa ufisadi pale nchini kenya,yaani mwenyekiti na makamu wake.Sababu kuu ni moja tu,wameshindwa kuwajibika ipasavyo kupambana na ukosefu wa maadili na kukithiri kwa ufisadi kenya. swali? hapa Tanzania tatizo lipo wapi? Vyombo vya Kudhibiti  vimelala ufisadi sana zaidi ya sana ....

Kwa Kasi Hii, Zitto Kabwe kwa sasa ni Moto wa Kuotea Mbali katika Chaguzi Kuu

$
0
0
Kwa sasa ACT-Wazalendo ni Zitto Kabwe, bila Zitto Kabwe hata uhai wa ACT-Wazalendo haupo!.

Ziara ya Viongozi wakuu wa ACT-Wazalendo katika mikoa ya Ruvuma, Njombe, Iringa, Morogoro, Dodoma, Singida, Tabora, Shinyanga, Mara na Mwanza imeangaza picha na kutoa majibu mengi.

Ni ukweli kuwa, kuingia kwa ACT-Wazalendo kwenye uwanja wa siasa nchini umewatikisa UKAWA na unaifanya CCM kujitathmini na kuwa waangalifu katika mchakato wa kuwapata wagombea wake.Kabla ya ACT-Wazalendo, nguvu ya kisiasa ilikuwa mikononi mwa CCM na UKAWA.

ACT-Wazalendo unaifanya UKAWA kukosa kwa kiwango kikubwa umuhimu wa Muungano wao kama nia yao ni kutaka kuunganisha idadi ya kura ili kuishinda CCM na siyo kuunganisha philosophy, policies and manifesto.

ACT-Wazalendo unaifanya CCM kuachana na politics as usual katika mchakato wa kupata wagombea kwa sababu ACT-Wazalendo ni zaidi ya Independent candidate katika nguvu za CCM. CCM wangeweza kuendelea kufanya politics as usual kama nguvu ya kisiasa ingebakia ni UKAWA pekee kwa sababu wale wangefanyiwa vitimbwi ndani ya CCM wasingepata nafasi tena ya kukimbilia UKAWA na kupata nafasi ya kuwa wagombea kwa sababu muungano wa UKAWA umeishafukia nafasi tatu kati ya nne za wagombea kutoka vyama vinavyounda muungano wa UKAWA kuanzia udiwani, Ubunge mpaka Urais.

ACT-Wazalendo imeingia kwenye uwanja wa siasa na clear-cut central idea and programme soundly ikisaidiwa kwa kiwango kikubwa na vyombo vingi vya mawasiliano nchini kwa sababu imebeba majibu ya mapungufu ya UKAWA na CCM katika siasa za Tanzania lakini kikubwa zaidi, inafanya siasa zake nje ya confrontational environment ukilinganisha na vyama vikubwa hasa ikichukuliwa kuwa, Watanzania wengi hawapendi siasa za vurugu.

Wananchi wengi watakaojiunga na ACT-Wazalendo kutoka CCM watakuwa ni wale wanaamini CCM imeacha misingi ya uanzishwaji wake na vile vile rushwa imekuwa ni kigezo cha kupata uongozi ndani ya chama na serikali yake.

Wananchi wengi watakaojiunga na ACT-Wazalendo kutoka UKAWA watakuwa ni wale wanaamini Muungano wa CHADEMA, CUF, NCCR-Mageuzi na NLD umewanyima demokrasia ya kuchaguliwa ndani ya vyama vyao baada ya kuwekesha nguvu na pesa katika vyama hivyo na pia kuna wengine watafanya hivyo kwa sababu wanaamini ni wahanga wa uongozi wenye hekima na busara za makengeza.

Ninaamini huu ni ukweli unaonekana na wachache kwa kutumia naked eye na katika ukweli huu, ndiyo nguvu ya ACT-Wazalendo kupitia kwa Zitto Kabwe inakuwa ni power broker.

Ni wajinga na wapumbavu watakaopuuza na kubeza uwepo wa ACT-Wazalendo iliyo chini ya Zitto Kabwe katika mstakabali wa chaguzi za Tanzania Bara katika mazingira ya siasa za ndani ya UKAWA na CCM.

Kuna baadhi ya wananchi wameanza kuja na hoja nyepesi za kisiasa kuhusiana na ujio wa ACT-Wazalendo wakiamini ni hoja mbadala au ni hoja zinazotuliza ombwe lao la fikra pevu.

Kuna baadhi ya wananchi wameanza kudai eti haka ni kachama kadogo. Fine!.

Hoja ya msingi hapa, Ziara walizofanya katika mikoa kumi imetoa majibu ya maana ya ''haka kachama kadogo''.


Kuna baadhi wanadai ACT-Wazalendo ni chama cha wasaliti. Fine!.

Hoja ya msingi hapa, wasaliti wa nani katika taifa Iinalokadiriwa na National Bureau of Statistics (NBS) office kuwa ifikapo siku ya uchaguzi, Tanzania itakuwa na watu wapatao 48,522,228, ambapo watakaokuwa na umri wa kupiga kura mwaka huu watakuwa ni watu 24,253,541.

Kuna wengine wanadai, ACT-Wazalendo ni tawi la CCM. Fine!.

Hoja ya msingi hapa, vyama vingine ni matawi ya nani kwa faida ya nani?

Kuna wengine pia wanakuja na hoja wakisema, ACT-Wazalendo imekuja kugawa kura za UKAWA. Fine!.

Hoja ya msingi hapa, kura hazigawanywi kama njugu. Kinachogawa kura ni philosophy, policies and manifesto, labda kama misingi hii ya ACT-Wazalendo inafanana na UKAWA lakini kikubwa zaidi, Tanzania hivi sasa ina zaidi ya vyama 22 vyenye usajili wa kudumu chini ya Rais aliyechaguliwa na wananchi 5,276,827 kati ya wananchi 20,137,303 waliojiandikisha kupiga kura.

Wahenga walisema, ‘Mchelea mwana kulia hulia yeye’ na ‘Mdharau mwiba mguu huota tende’ lakini kwa wale wanafahamu maana yake, this is an opportunity to step back, reflect and refocus.

Kwa mtaji huu, ACT-Wazalendo is a force to be reckoned with. Be prepared to deal with any mischief.

By Ng'wamapalala

Jokate Reveals The Secret to Her S3XY Looks!!

$
0
0
The secret is quite simple.....I work out every morning....

Woman Dies After Mistakenly Taking Poisoned Soup She Had Been Told to Prepare For Her Cheating Husband by The Witch Doctor

$
0
0
An attempt by a frustrated housewife to get her husband to fulfill his conjugal duties backfired after she reportedly ate the soup laced with a poisonous charm she had procured from a witch doctor.

Her neighbors reported that she had complained of abandonment -that her husband has not been making love to her since they got married two years ago.

The wife, instead of seeking the family’s intervention, allegedly sought the help of a witch doctor who prepared a charm for the man to have a change of heart.


The man had told some persons that he was involved in extra-marital affairs because of an odour that oozes from his wife.

On her return from the witch  doctor’s place on that fatal evening, she immediately applied the charm but unfortunately the man was nowhere to be found. She was said to have mistakenly mixed the charm in her own soup not knowing it was poisonous. She ate it, went to bed and died.

Reacting, the husband said: “My wife had threatened to make me impotent when I stopped making love to her for obvious reasons and I found some fetish items in her room, including the soup she ate before her death its sad enough that she had to die like that”

Siwema, Nay wa Mitego's Ex Girlfriend Spotted Doing This with This New Boyfriend..Has She Really Moved On ?

$
0
0

Meet The New Boyfriend of Siwema After the Break up With Nay wa Mitego ...Has She Really Moved On..Or its just a Rebound after Nay wa Mitego Spotted Kissing Bongo Movie Actress Shamsha Ford ?

Nape Akanusha: Hatukisaidii Chama cha ACT Wazalendo

$
0
0
Katibu wa itikadi na uenezi wa CCM Nape Nnauye amesema chama chake hakikisaidii kwa fedha chama kipya cha ACT wala kiongozi wake mkuu Zitto Kabwe kama inavyoenezwa ktk mitandao mingi ya kijamii

Source: Raia Tanzania

My take:
Nani amemuuliza Nape hayo anayokanusha? Kama yanaandikwa kwenye mitandao na hayana ukweli kwa nini asiyapuuze? Anataka kitwambia kila kinachoandikwa kwenye mitandao huwa anakikanusha? Mbona wanaodaiwa kusaidiwa hawakanushi?

Nikinywa Pombe na Kuvuta Bangi ndio Napata Raha Sana Wakati wa Kufanya Mapenzi

$
0
0

Nadhani wapenzi wa hayo mambo hapo juu watakubaliana nami kuwa ukinywa pombe au kuvuta bangi na ukamkamata mwanamke hakika kuna starehe ya ajabu isiyo na mfano, konyagi ndio kiboko ya yote, kunywa konyagi halafu ugegede ndio mwanamke atalijua jiji.

Hata kama ni mgumu kiasi gani kufika kileleni lazima siku hiyo ataomba poo.Kuna mwanamke wa kijaluo mrembo alikuwa kila akienda na mwanaume haridhiki.

Siku hiyo akaingia kwenye anga zangu nikiwa nimekunywa nusu mzinga wa konyagi na safari mbili,wee wee, alishinda anaongea kijaluo,hadi leo hataki kuniacha najilia viji cent vyake.

Kwa kweli konyagi na mapenzi ni sawa na pikipiki na petrol.Wasiokunywa pombe wana hasara kubwa sana hapa duniani na hawajui mautamu tunayopata.Tusker Bariiidi hebu waambie.

Je wewe Kwako ikoje ?

By Mdau

Jack Dustan: Sisi Mastaa wa Kike Ndio Vinara wa Kuchukua Waume za Watu Bongo Tusipobadilika Watatuua

$
0
0
Staa aliyepata umaarufu kupitia Shindano la Maisha Plus, Jacqueline Dustan amefunguka kuwa mastaa wamepachikwa nembo ya kuwa ni vinara wa kubeba waume za watu jambo ambalo linawapa sifa mbaya.

Akizungumzia mwenendo wa mastaa wengi kuhusishwa na skendo ya kutembea na waume za watu, Jack alisema:

Yaani sisi mastaa tumepachikwa nembo ya kupora waume za watu. Imefika wakati hata kama umempata mpenzi wako mtu anakuuliza umempora nani. Huwa inaniuma sana.

Kimsingi tuna sifa mbaya na tusipobadilika waume za watu hawa watatuua.”

Askofu Pengo: Nasumbuliwa na uti wa mgongo, Watanzania Chagueni Rais Masikini

$
0
0
Hatimaye Askofu wa Kanisa Katoliki Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo amewatoa hofu Watanzania kuhusu afya yake kwa kueleza kuwa anaendelea vizuri baada ya kufanyiwa uchunguzi wa matatizo yake ya uti wa mgongo.

Kardinali Pengo pia amegusia nafasi ya urais katika Uchaguzi Mkuu ujao kwa kuwataka watanzania kumchagua rais fukara kuliko anayetafuta nafasi hiyo kwa rushwa.

Alitoa kauli hiyo katika mahafali ya Saba ya Chuo Kikuu cha Mtakatifu Joseph, Dar es Salaam jana.

Alisema maradhi ya uti wa mgongo ambayo yamekuwa yakimsumbua kila yaligundulika Agosti mwaka 2013 baada ya kufanyiwa uchunguzi wa afya, Ujerumani.

“Hospitali ya Ujerumani ndiyo waligundua kuwa nyuzi mbili ndani ya uti wa mgongo zimechanika zinabana mashipa ya neva, kwa hiyo zikawa zinanisababishia maumivu ya mgongo.

“Kule Ujerumani walizirudisha katika nafasi yake lakini kwa bahati mbaya hawakufunga huku wakitegemea kuwa mambo yatakwenda vizuri kwa njia ya kawaida.

Lakini kwa sababu ya kurukaruka nikajiona kama nimepona ila baada ya muda kidogo maumivu yasio ya kawaida yalirudi tena,” alisema kiongozi huyo wa kiroho.

Alisema maumivu yalipozidi Juni mwaka jana alisafiri kwenda Hospitali ya Manipal, Bangalore, India kwa uchunguzi zaidi.

Walinihudumia vizuri na kwa sasa naendelea vizuri … kwa wale wanaojali uhai wangu nilipokwenda mara ya mwisho kwenye uchunguzi waliniambia kila kitu kimekaa kwenye nafasi yake.

Madaktari walinielezea kuwa nisishangae maumivu ya mara kwa mara kwa sababu operesheni ilikuwa kubwa.

Kwa sababu operesheni ya sasa itachukua muda kati ya miaka miwili hadi mitatu niweze kujisikia mzima kabisa. Kwa sasa naendelea vizuri sina tatizo zaidi,” alisema.

Kuhusu Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba mwaka huu, Kardinali Pengo alisema ni kitu kibaya kama viongozi wanaowania nafasi ya urais wanatoa rushwa.

“Uongozi wa Taifa hauwezi kununuliwa kwa gharama yoyote… wanaoelekea kutoa rushwa baadaye watataka sisi wananchi tulipe zile gharama ambazo walikuwa wametugawia katika kutoa rushwa, afadhali waache kabisa.

Ni vizuri tupate rais anayekuwa fukara lakini anayependa nchi yetu na hatatudai gharama ya kumchangua kama si hivyo gharama inaweza kuwa kubwa ikatusababishia matatizo,” alisema.

Kardinali Pengo pia alizungumzia matukio ya ugaidi na kuwataka wanaosambaza ujumbe fupi wa vitisho kuacha mara moja tabia hiyo kwa vile inawaweka wananchi katika hofu.

Wanaweza kusababisha taharuki na mikanganyiko na kuleta madhara kwa wengi kwa kitu ambacho hakipo.

Kama kuna hofu ya usalama sehemu yoyote inabidi tuwaachie wataalamu wa usalama waweze kuishughulikia kwa namna wajuavyo,” alisema.

Hata hivyo, aliitaka serikali kupitia Idara ya Usalama kuwa ya kwanza kuwahakikishia wananchi kuwa hakuna matukio hayo amani na utulivu viendelee kuwapo.

Pia aliwashauri wahitimu wa Chuo Kikuu cha Mtakatifu Josesph kuwa wasisome kwa ajili ya kuajiriwa na serikali tu.

Kuna nafasi za wataalamu wa sayasi na sanaa za kujiajiri katika chuo hiki … Chuo kikuu kizuri ni kile kinachoandaa wanafunzi kujiajiri,” alisema.

Mkuu wa Chuo hicho, Padre Aru Raji alisema chuo kinazidi kupanuka na mwaka huu kinatarajia kufungua Chuo Kikuu Sumbawanga na Chuo cha Afya na Tiba, Boko, Dar es Salaam.

Zitto: ACT Hatutaki Anasa, Usafiri Wetu Ziarani ni Treni na Mabasi

$
0
0
Zitto Akiwa Ndani ya treni
Kama Watanzania tunataka chama cha siasa chenye nidhamu ya matumizi ya pesa, basi ACT ndio chama sahihi!

Zitto ameendelea kuonyesha tabia yake ya kujali raslimali kwa kuzitumia kwa uangalifu mkubwa huku akifikiria wanyonge wa nchi hii ambao wengi wao wako kijijini.

Katika kutekeleza hilo, Zitto ameamua kufanya ziara za chama hicho (kwa awamu ya pili) kwa kutumia treni kwa kuwa itapita maeneo ambayo ACT imeyakusudia kwa awamu ya pili!

Watanzania, matukio haya ambayo tunayoyaona ndani ya ACT ni ukumbusho wa ujamaa wa Mwalimu wakati wa CCM ile ya enzi za azimio la Arusha.

Mwigizaji Lulu Michael Arudi Tena Instagram Baada ya Kujitoa siku ya Kifo cha Secky

$
0
0
Siku ya Jana Accounts Mbali mbali  Maarufu za Instagram zimeshinda zikipost kuwa Lulu michael amerudi instagram kwa jina la lizymichael Baada ya Kujitoa siku Secky alipofariki Dunia Baada ya watu kuanza kumuhusisha lulu na Kifo Hicho kitu ambacho hakikuwa Kweli ....

Baadhi ya Meseji huku instagram kuhusu kurudi kwa lulu Insta hizi Hapa:

lulunation_ Lulu amerudi instagram asante Mungu kwa yote account yake org ni @lizymichael
@lizymichael @lizymichael
@lizymichael
@lizymichael
follow  13h

sephoramwakalinga Karibu swthrt..saiz kua na moyo km wa jambaz @lizymichael hao shain wasikupe shida coz hakuna jipya chini ya jua, ishi utakavyo...hao machokoraa wanaojiropokea acha waendelee kujifurahisha coz hawawez kua wewe. 11h

proudoflulumichael Mungu amekuchaguwa wewe ili uwakomboee na wengine @lizymichael @lizymichael ...


proudoflulumichael She is Back again my Queen Lizy now you can follow her .Her new account is @lizymichael @lizymichael @lizymichael @lizymichael ..Wellcome baq


Mwigizaji Johari Amkana Ray Laivu!

$
0
0
Staa wa Bongo Movies na mmiliki mwenza  wa kampuni ya filamu nchini ya ‘RJ Company’, Blandina Chagula ‘Johari’, ameibuka na kushangaza wengi kwa kauli yake kwamba hakuwahi kuwa na uhusiano wa kimapenzi na mwigizaji mwenzake, Vicent Kigosi ‘Ray’.

Staa huyo aliwahi kukiri kuwa na uhusiano huo na msanii huyo na kwamba walishaachana kwa amani, ndiyo maana waliweza kuendelea na kampuni yao ya masuala ya filamu ya Rj Company.

Juzi Johari ameliambia gazeti la Mtanzania kwamba, muda mrefu alikuwa akisikiliza wanaodai hana uelewano mzuri na Ray kutokana na kuwa na uhusiano wa kimapenzi na mwigizaji Chuchu Hans na sasa ameamua kuweka wazi suala hilo.

“Ni kwa kipindi kirefu sana yamezuka maneno yanayodai mimi na Ray tulishawahi kuwa wapenzi, kitu ambacho si cha kweli, tena kibaya zaidi wameongeza kuwa hatuna maelewano mazuri kikazi,” alieleza Johari.
Aliendelea kufafanua: “Sikuwahi kuwa na uhusiano naye wa kimapenzi kama wengi wanavyofikiria na kama ningekuwa na uhusiano wa kimapenzi na Ray na tumeachana, hata kampuni yetu ingeshavunjika kwa kuwa tungekuwa na chuki, nawaambia hatutegemei kutengana kikazi wala kirafiki,” alisema Johari

Tatizo la Kushindwa Kuzaa Kwa Wema Sepetu Waganga wa Kienyeji na Madaktari Kila Kona Wajitokeza Kumsaidia, Wema Adai Yupo Tayari

$
0
0
Kufuatia  tatizo la kushindwa kupata ujauzito alilonalo msanii maarufu Bongo, Wema Sepetu, hivi karibuni waganga wapatao 26 kutoka sehemu mbalimbali nchini walijitokeza na kuomba kuunganishwa na staa huyo ili wamtibu.

Waganga hao wa tiba asilia pamoja na madaktari kutoka hospitali mbalimbali kwa nyakati tofauti walipigia simu  na kueleza kuwa, wanashangaa kuona Wema anakosa amani wakati wao wanaweza kumtibu na kuweza kuitwa mama kama wenzake.

Unajua wapo wanawake ambao wanakosa amani kwa mambo ambayo hawastahili, hili la Wema kutopata mtoto linatibika, mpeni namba yangu kisha anitafute,” alisema mmoja wa wataalam hao aliyeomba jina lake lisiandikwe.

Katika kujua Wema anapokeaje ofa aliyopewa na waganga hao, alitafutwa na alipopatikana alikubali mara moja kutibiwa tatizo alilonalo lakini akatoa angalizo.

Kuna watu wengi sana ukiacha ambao wamejitokeza kwenu, mimi nina meseji zaidi ya 400 ambazo nimetumiwa kwenye namba yangu ya WhatsApp na simu kibao nimepigiwa watu wakijitolea kuja kushughulikia tatizo langu, kiukweli kabisa nipo tayari.

Lakini ni vizuri wakati naanza kutibiwa tayari nikawa na mwenza wangu ambaye tutakuwa tumekubaliana na pale tatizo litakapoisha, iwe rahisi kuzaa mara moja,” alisema Wema.

January Makamba 'Urais Nautaka Sasa na si Kipindi Kingine Chochote, Hizi Kauli Kuwa Natumiwa na watu zinaniumiza Sana'

$
0
0
Mbunge wa Bumbuli (CCM) na Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, January Makamba amesema haweki utani katika suala la kugombea urais na akikosa kiti hicho kipindi hiki itakuwa vigumu kukipata miaka ijayo.
Makamba ameliambia  gazeti  la  Mwananchi, hivi karibuni , kuwa kauli zinazotolewa na watu, ikiwemo ile ya yeye kutumiwa kutangaza nia ili baadaye aje kumuunga mkono mgombea mwingine wa urais kwa tiketi ya chama hicho, inamkera na ‘kumnyima usingizi’.

Urais nautaka sasa na si kipindi kingine chochote, na niseme tu wazi kwamba, hizi kauli kuwa natumiwa na watu zinaniumiza sana. Naamini kuwa ninaweza. Kama atakayepewa sasa (urais) ataharibu, ni vigumu sana kugombea tena urais na kuupata,” alisema Makamba ambaye amewahi kuwa mwandishi wa hotuba za Rais Jakaya Kikwete.
Kauli hiyo ya Makamba aliyetangaza nia ya kuwania urais mwaka jana akiwa London, Uingereza imelenga kuwajibu wanaodhani kuwa anatumika kutibua harakati za vigogo wa chama hicho wanaoutaka urais.

Julai 9, mwaka jana Rais Kikwete alizungumzia nia ya Makamba kutaka kuwania urais, akisema mwanasiasa huyo kijana “anataka mambo makubwa, lakini hajamshirikisha”, na kwamba “asilazimishe” kwa kuwa wakati ukifika atapata kile anachokitaka.
Nasikia kuwa bwana mdogo January anataka mambo makubwa. Mie hajaniambia, na mie nasikia. Hata alipogombea ubunge hakuniambia nilisikia baadaye... asilazimishe, wakati ukifika atapata, na akikosa asilete nongwa,” alisema Kikwete.

Rais Kikwete alitolea mfano wake aliposhindwa katika uteuzi wa mgombea urais wa CCM mwaka 1995, wakati akiwa na miaka 45 (miaka minne zaidi ya umri wa Makamba), akisema kuwa hakukata tamaa na aliendelea kusikiliza ushauri wa wazee hadi alipofanikiwa kukalia nafasi hiyo ya juu mwaka 2005.
Kauli hiyo ilikuwa ya kwanza kutolewa na Rais Kikwete kuhusu wanachama wa CCM wanaotaka kuwania urais, baada ya chama hicho kuwaonya makada sita kwa tuhuma za kuanza mapema kampeni za kutaka nafasi hiyo kubwa.
Akifafanua zaidi nia yake hiyo, Makamba ambaye ni mtoto wa Katibu Mkuu mstaafu wa CCM, Yussuf Makamba alisema, “Wapo wanaosema kuwa ninautaka urais kwa sababu ninatumiwa na watu. Wapo pia wanaosema kuwa ninautaka urais kwa ajili ya kujitangaza ili niweze kupata nafasi nyingine za uongozi.”

Aliongeza: “Wanasema kuwa ninautaka urais sasa kwa ajili ya kujiwekea mazingira mazuri ya kugombea (urais) mwaka 2025. Unajua kama CCM ikiweka mgombea ambaye si mzuri, mwaka 2025 utakuwa mgumu sana.
Makamba alisema anaamini kuwa yeye ni miongoni mwa makada wasafi wa chama hicho tawala.
“Kuhusu suala la maadili sina shaka kabisa. Moja ya changamoto kubwa iliyopo nchini kwa sasa ni mmomonyoko wa maadili. Wapo viongozi wengi wanaoomba nafasi ya urais huku kukiwa na mashaka makubwa kuhusu uadilifu wao,” alisema.
Alisema wapo viongozi wanaotumia pesa nyingi kutafuta nafasi hiyo kwa kuzigawa nchi nzima ila anaaamni viongozi hao hawawezi kuleta mabadiliko yoyote katika nchi hii yakiwamo ya kupambana na rushwa ambayo ni kansa inayoirudisha nyuma na kuitafuna nchi.

Afande Sele: Nikichaguliwa Kuwa Mbunge Nitakataa Posho na Mishahara Mikubwa

$
0
0
Mwana hip hop na Bongo Fleva nchini, Afande Sele, ameweka wazi kwamba hata kama atakuwa mwakilishi wa wananchi katika bunge la mwakani, hataweza kuacha kufanya muziki kwa kuwa ndiyo njia ya kumuingizia kipato.

Alisema licha ya kuwa bungeni, atakuwa akitegemea zaidi fedha zinazotokana na muziki wake badala ya kufikiria mishahara minono na posho zinazopatikana bungeni.

Kazi yangu ya muziki siwezi kuiacha, ndiyo itakayoniongoza katika maisha yangu, kwa kuwa nitakapokuwa bungeni licha ya kuwa na utetezi mwingine kwa wananchi, lakini pia nitapinga na kukataa posho na mishahara minono wanayopata wabunge kiasi kwamba wanasahau walipotokea,’’ alieleza Afande

Afande, ambaye sasa ni mwanachama wa chama Kipya ya ACT, aliongeza kwamba ili wasanii waweze kuwatumikia vema wananchi, baada ya kuwa wabunge lazima wakatae posho na mishahara minono.

Wasanii wengi waliopo bungeni wanajisahau kwa kuwa wanapopata posho na mishahara minono wanasahau walipotoka na kujitofautisha na wananchi na ukishachukua fedha hizo huwezi kuwatetea wananchi, lakini mimi nikienda huko nitapiga vita dhidi ya posho na mishahara hiyo minono ili fedha hizo zielekezwe kwenye shughuli nyingine za maendeleo,’’ alieleza.

Aliongeza kwamba hatajali hata akilipwa kiasi kidogo cha mshahara kwa kuwa lengo lake la utetezi litakuwa limekamilika na wananchi wengi Tanzania watanufaika nalo kama posho na mishahara minono itapunguzwa ama kufutwa kabisa.

Mama Kanumba na mama Lulu Kimenuka, Mama Kanumba Adaiwa Kumtumia Mwenzake Meseji Mbaya

$
0
0
Taarifa zilizotua kwenye dawati la gazeti hili zinadai kuwa, wale wamama wa mjini ambao walikuwa mashosti hadi kufikia hatua ya kusema ni kama ndugu, mama wa aliyekuwa staa wa Bongo Movies, marehemu Steven Kanumba, Flora Mtegoa na mama wa mwigizaji Elizabeth Michael ‘Lulu’, Lucresia Karugila, sasa kimenuka!

DALILI KUWA PAKA NA CHUI
Chanzo chetu cha kuaminika kilidai kuwa, dalili za wawili hao kuelekea kugeuka kuwa paka na chui zilianza muda mrefu lakini hali ikazidi kuwa mbaya Siku ya Kumbukumbu ya Kifo cha Kanumba, Aprili 7, mwaka huu alipokuwa akitimiza miaka mitatu kaburini.

CHANZO NI LULU
Ubuyu ulidai kwamba, siku ya kumbukumbu ya kifo cha Kunumba, Mama Kanumba alimtuhumu Lulu kutotoa ushirikiano na kufikia hatua ya kutoa maneno makali zaidi yaliyomkera mama Lulu

MAMA KANUMBA NA SMS MBAYA KWA MAMA LULU
Ilidaiwa kwamba, siku ya kumbukumbu ya kifo cha Kanumba, mama Kanumba alimtumia mama lulu sms mbaya ya kejeli (kuiandika hapa siyo busara) ndipo mama Lulu ‘alipofyumu’ na kuona kwa hali hiyo bora kama mbwai na iwe mbwai.“Ile sms mama Kanumba alimtumia mama Lulu siku ile (Aprili 7) majira ya saa 11:00 alfajiri.

HAIKUWA YA KIUNGWANA
“Kwa kweli ilikuwa meseji mbaya mno. Alikuwa akimuagiza mama Lulu amuamshe Lulu kwa ajili ya kwenda kaburini kwa Kanumba lakini haikuwa ya kiungwana.“Hata hivyo, ukweli mama Lulu alitumia busara kwa kutomjibu lakini akadhamiria kuchukua hatua za kisheria,” alidai mtoa ‘ubuyu’ huyo.

Ilizidi kudaiwa kwamba, wakati mama Lulu akitafakari sababu ya shosti wake huyo ambaye walikuwa wakitembea mjini kama kumbikumbi kumtumia sms hiyo, akashangaa kusoma tena kwenye gazeti mama Kanumba akimpa vipande vyake Lulu, jambo lililozidi kumchefua mama Lulu.

KUBURUZANA KORTINI?
“Kimsingi hali ni mbaya sana sasa hivi, inavyoonekana mama Lulu kamchoka mama Kanumba na anataka kuchukua hatua zaidi ikiwemo kuburuzana kortini,” alidai sosi huyo.

MAMA LULU AFUNGUKA
Baada ya kunyetishiwa ishu hiyo, gazeti hili lilimtafuta mama Lulu ambapo alipopatikana alikiri kupokea ujumbe na kwamba hali ni mbaya sana.“Nimeumizwa sana na sms ya mama Kanumba lakini siwezi kuwapa kwa sababu nataka kuifanyia kazi,” alisema mama Lul


MAMA KANUMBA VIPI?
Kwa upande wake mama Kanumba aliendelea kusisitiza kuwa yeye ataendelea kumlilia mwanaye na hana mpango na familia hiyo ya Lulu.“Mimi kwa upande wangu nitamlilia mtoto wangu mpaka siku ya kufa kwangu lakini kinachoniuma ni Lulu kufanya sherehe ya mdogo wake siku ya kumbukumbu ya mwanangu.

“Jamani hata kama mtu ana roho gani, hawezi kufanya hivyo,” alisema.
Alipoulizwa kuhusu sms aliyomtumia mama Lulu na kwamba mama huyo yupo mbioni kumchukulia hatua za kisheria hakuwa tayari kuzungumza chochote.

Source:Global Publishers

Ajabu na kweli Ng'ombe Awala Kondoo Kenya, Akataa Kula Majani

$
0
0
Mkulima mmoja nchi Kenya anasema kuwa mmoja wa ng'ombe wake amesusia lishe yake ya kawaida na kuanza kuwala kondoo.

Charles Mamboleo, ambaye anamiliki shamba kusini magharibi mwa kaunti ya Nakuru aligungua kuwa ng'ombe wake amemla kondo siku moja asubuni.
Jitihada zake za kumpa ng'ombe huyo chakula na maji hazikufua dafu, na siku iliyofuata ng'ombe huyo alimla kondoo mwingine.

Kulingana na afisa mmoja wa kilimo ni kuwa , huenda tabia ya ng'ombe huyo huenda imetokana na ukosefu wa madini yanayopatikana kwa mimea mbichi.
Hali ya kiangazi ambayo ilimalizika hivi majuzi huenda imesababisha mifugo kukosa madini yanayopatikaan kwenye nyasi mbichi. Mwaka 2007 ndama mmoja nchini India alinaswa kwenye mkanda wa video akila kuku.

Simba ina Waganga Wengi wa Kienyeji Kuliko idadi ya Wataalamu Waliopo Benchi la Ufundi

$
0
0
Na Shaffih Dauda

MTANDAO huu kwa muda mrefu sasa umekuwa ukifanya tafiti na kufuatilia mwenendo wa klabu ya Simba katika mechi za ligi kuu soka Tanzania bara msimu huu.

Mwishoni mwa juma lililopita, Simba ilifungwa magoli 2-0 na Mbeya City fc katika uwanja wa Sokoine, Mbeya na kuifanya klabu hiyo kongwe nchini kuendelea kukaa nafasi ya tatu kwa pointi 35 walizokusanya baada ya kushuka dimbani mara 22.

Machi 18 mwaka huu walifungwa magoli 2-0 na Mgambo JKT katika uwanja wa CCM Mkwakwani Tanga, lakini wakashinda 2-1 ugenini dhidi ya Kagera Sugar uwanja wa CCM Kambarage, Shinyanga na ilikuwa aprili 6 mwaka huu (jumatatu ya pasaka).

Katika mechi hizo tatu, mtandao huu ulikuwa unachunguza mwenendo wa Simba na namna wanavyoiandaa timu kwa ajili ya mechi.

Katika mechi ya Tanga waliyochapwa na Mgambo, timu iligoma kuingia kwenye vyumba vya kubadilishia nguo, wachezaji wakakaguliwa ndani ya basi nje ya geti karibu na vyumba vya kubadilishia nguo.

Simba walifanya hivyo wakihofia kurogwa na wenyeji wao, lakini mwisho wa siku wakafa mbili bila na walipoenda Shinyanga kucheza na Kagera walifanya hivyo hivyo, walikataa kuingia vyumbani na kukubali kutozwa faini na TFF.

Simba waliendeleza tabia yao ya kutoingia vyumbani kwa madai ya kuogopa kurogwa huku wakisingizia vyumba ni vibovu. Inawezekana kweli ni vibovu, lakini dhahiri walikuwa na mawazo mengine kichwani mwao kwani viongozi walionekana kuwapangia wachezaji maeneo ya kupita wakati wanaingia uwanjani.

Baada ya safari ndefu ya uchunguzi, hatimaye jibu limepatikana kule Mbeya ambako Simba amekufa tena mbele ya Wagonga nyundo wa Mbeya, Mbeya City fc.

Tulipiga kambi jijini Mbeya na kugundua kuwa Simba wameharibikiwa kwasababu wanawatumia Waganga wa kienyeji kwa muda mwingi wakiamini watawasaidia kupata matokeo ndani ya uwanja.

Dunia ya leo klabu kongwe ya Simba, mfano wa kuigwa inaendekeza imani za kishirikina kwa kiwango cha juu namna hii, inasikitisha sana.

Chakusikitisha zaidi ni kwamba, tunaamini viongozi waliopo madarakani ni vijana wa kidijitali yaani wa kisasa au kileo. Imefika wakati tunaamini wazee kama vile Hassan Dalali na wengineo hizi si zama zao, lakini hayo ni maneno tu, inawezekana wale wazee wakawa na mafanikio makubwa kuliko  vijana ambao tunaamini wanaweza kuiendesha timu kileo au kisasa, vijana ambao ukiwaangalia ni watanashati,  lakini matendo wanayoifanyia klabu ni mabaya mno.

Kwa aina ya viongozi wa sasa wa Simba, ni jambo la aibu kutumia muda mwingi kuwekeza katika uchawi , kutumia waganga au ndumba wakiamini watasaidia kupata matokeo kuliko kujikita katika maandalizi ya kitaalamu na kiuweledi.

Simba wamefungwa na Mbeya City kwasababu hawakutoa nafasi ya kiuweledi katika maandalizi yao, waliwekeza nguvu kwa mambo ya nje ya uwanja wakiamini yatawasaidia kupata matokeo.

Utaratibu ulivyo, unapoenda uwanja wa ugenini, siku moja kabla ya mechi,  timu inatakiwa kufanya mazoezi kwenye uwanja ambao watachezea mchezo, kwahiyo Simba walitakiwa kwenda kufanya mazoezi Sokoine siku ya ijumaa, lakini kutokana na kuamini mambo ya kishirikina hawakwenda kufanya mazoezi siku hiyo, matokeo yake ilibidi wafanye mazoezi kwenye bustani (Garden) ya Hoteli waliyofikia, wanafanyia mazoezi ‘Garden’ eti kwa sababu wanaogopa kurogwa na Mbeya City.

Hii ilikuwa kinyume, mwalimu na benchi la ufundi walitaka timu ikafanye mazoezi uwanjani, lakini baadhi ya viongozi walioandama na timu waliona timu ikienda kufanya mazoezi Sokoine wataenda kupoteza mchezo wa jumamosi.

Mwisho wa siku wakafanya mazoezi uani, wakafanya mazoezi ‘Garden’, na wakawa ‘wamefeli’ rasmi.

Ikaja siku ya mechi, badala ya kupita kwenye mlango wa kawaida wakapitia mlango wa nyuma, wachezaji wakashuka na kuingilia mlango wa nyuma,  wakashindwa kuingia kwenye vyumba vya kubadilishia nguo, wakakaa pembeni kwenye kona kulia kwa jukwaa kuu la Sokoine, sehemu ambayo maaskari Polisi wanapenda kuweka magari yao.

Baadaye kidogo wakaenda karibu na sehemu ya vyumba vya kubadilishia nguo na kukaa nje upande wa kulia kwenye chumba chao , lakini wachezaji wakaamuriwa waondoke tena.

Muda huo wachezaji wa Mbeya City walikuwa wanapasha moto misuli ‘Warm-up) na walikuwa wameshafanya kwa muda mrefu, Simba wao walichelewa hata kupasha moto misuli kutokana na mambo yao ya kishirikina.

Wakati wanaingia kwenye ‘Warm-up’ badala ya kuingilia kwenye benchi ambalo watakaa upande wa kushoto kwasababu kulia walikuwa wamekaa Mbeya City kinyume na taratibu zinazowataka wenyeji kukaa benchi la kushoto na wageni kulia, Simba wakarudi kwenye kona waliyoingilia mara ya kwanza

Simba walifuata taratibu kwamba wenyeji wanakaa benchi la kushoto, wageni kulia, lakini kulia ni sehemu ambayo Mbeya City wanakaa kila siku na Simba walikataa kukaa kushoto wakiamini pameshapigwa misumari. Walipotaka kukaa kulia Mbeya City wakagoma na ndipo ikatokea vurumai kati ya watu wa Mbeya City na Simba, ikabidi Simba wawe wapole na kukubali kukaa kushoto.

Wakati huo wachezaji walikuwa wamekaa chini nyuma ya lile benchi la ufundi na ilibidi wakafanye ‘warm-up’, kwa itikadi hizo hizo za kishirikiana wakashindwa kuingia uwanjani kupitia eneo hilo, wakaambiwa watembee na kurudi goli la kusini wazunguke kwenye kibendera cha kona na waingie uwanjani na mstari ule wakafanye ‘warm-up’.

Ukiangalia kwa undani,  wachezaji hawataki mambo hayo, wanakasirika, wanaingia uwanjani hawana raha, lakini kwasababu wamelazimishwa na wapambe wanaojifanya wanajua  kila kitu, timu iingilie wapi, wakanyage wapi na kamwe hawataki kukiuka maigizo ya waganda wa kienyeji.

Siku ya mechi hakika wachezaji hawakuwa sawa kisaikolojia, waliingia kupasha misuli na kuanza mechi, wakati wanacheza Mbeya City waliwazidi Simba, walikuwa wamechangamka, walionesha kabisa wanahitaji matokeo, lakini Simba walikuwa wanacheza tu kama vile mtu anayetaka kutekeleza jukumu lake na kuondoka.

Jonas Mkude, Abdi Hassan Banda, Said Ndemla wakawa wanazunguka tu, wanageuka nyuma na mipira, hawaoneshi nia ya kwenda mbele, Elius Maguli, Ibrahim Hajibu wakaonekana vimeo kwasababu walikuwa hawapati huduma kutoka kwa viungo.

Mbeya City walicheza vizuri sana ukiachana na mambo ya kupiga misumari kwa wale wanaoamini hivyo, lakini kwasisi ambao hatuamini hivyo, tukiamini kuwa maandalizi ya mechi ni mazoezi, Mbeya City walicheza zaidi ya Simba, walitengeneza nafasi nyingi na kilichosababisha Simba washindwe kucheza ni imani za kishirikina.

Kuna baadhi ya wachezaji ambao sitaki kuwataja hawafurahishwi na vitendo vya kuendekeza vitendo vya kishirikina, walienda Tanga kuchuana na Mgambo, kuna mtu mmoja wa kamati ya utendaji (jina tunalo) anapenda sana mambo ya kishirikina, alienda na waganga karibia nane (8) Mkwakwani, wakapigwa 2-0 na Mgambo.

Pointi yetu ni kuwakanya Simba na timu nyingine za ligi kuu kuachana na mambo ya kuamini waganga . Hata tabia ya Mbeya City kulinda uwanja, kuchimbua uwanja na kufukia vitu ni ya kishamba, matokeo hayapatikani kwa njia ya Waganda. Mbona kuna mataifa yanasifika kwa uchawi lakini wanaboronga katika soka?

Hata hapa Tanzania maeneo yanayosifika kwa uchawi mfano Sumbawanga mbona hawana hata timu ya ligi kuu?

Inawezekana waganda wanatumika kwasababu ya mila na desturi za kizamani, lakini hayatakiwi kufanyika kwa kasi ya ajabu kama wanavyofanya Simba na timu nyingine.

Kama yanafanyika kwasababu za kitamaduni basi yafanyike kwa siri pasipokuwahusisha wachezaji, haiwezekani eti wamekuja waganga usiku Hotelini, wachezaji wanaamushwa usiku kusikiliza maelekezo ya Waganga.

Unawachosha wachezaji, hawapumuziki vizuri, matokeo yake wanapoteza malengo, inatakiwa mchezaji alale mapema, akae kitandani awaze mechi ya kesho, ajiandae na mechi kisaikolojia, lakini unapomuamsha usiku unamnyima muda wa kupumzika, pia unamnyima nafasi ya kuuwaza mchezo wa kesho na matokeo yake analala na msongo wa mawazo na hasira juu kutokana na kusumbuliwa usiku.

Matokeo yake wanaingia kwenye mechi bila kuwa sawa kisaikolojia na wanafungwa si kwasababu ya kukosa uwezo bali ni miundombinu ya viongozi kushindwa kuwaandaa wachezaji kiuweledi.

Waganga hawasaidii katika soka, maandalizi ya kitaalamu, kiuweledi ndiyo yanatoa nafasi ya kupata matokeo. Simba na timu nyingine zote badilikeni!

Nawatakiwa jumatatu njema, tukutane tena jumatano ya wiki hii!!
Viewing all 104684 articles
Browse latest View live




Latest Images