Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104709 articles
Browse latest View live

Vurugu Burundi: Polisi wapambana na Waandamanaji Wanaompinga Rais Nkurunzinza kugombea Urais tena.......Katiba ya Nchi hiyo hairuhusu mihula mitatu

$
0
0
WAPINZANI wa Serikali nchini Burundi, wameitisha maandamano makubwa leo ya kupinga hatua ya Chama Tawala cha CNDD-FDD kumtangaza Rais Pierre Nkurunziza, wa nchi hiyo kuwania mhula wa tatu katika uchaguzi ujao (Katiba ya Nchi hiyo hairuhusu mihula mitatu).

Mkuu wa Chama cha FNL kilichipigwa marufuku nchini humo, Agathon Rwasa, amepinga vikali uamuzi huo na kusema kwamba unaenda kinyume na Katiba ya Burundi.

Rwasa, amesisitiza kuwa, kuteuliwa kwa Rais Nkurunzinza kw aajili yam hula wa tatu utaitumbukiza nchi hiyo katika matatizo makubwa. Rwasa ndiye aliyekuwa mpinzani mkuu wa rais Pierre Nkurunziza katika uchaguzi mkuu wa mwezi Juni, 2010.

Kufuatia hatua hiyo, wapinzani hao wa serikali kwa nyakati tofauti, wameitisha maandamano makubwa leo Aprili 26, 2015 kupinga hatua hiyo ya chama tawala.

Akimtangaza rasmi Rais Nkurunzinza, Mwenyekiti wa Chama Tawala nchini humo, Pascal Nyebenda, aliwataka wapinzani wa serikali kuwa watulivu na kuachana na Rais Nkurunzinza katika masanduku ya kumipigia kura.

Mzozo wa kisiasa unaendelea kutokota nchini humo ambapo taarifa zinaeleza kuwa hivi sasa kumezuka ghasia katika mji wa Bujumbura nchini humo kati ya maafisa wa Polisi na waandamanaji wanaoishtumu serikali kwa kufanya mapinduzi ya kikatiba.

Waandamanaji walirusha mawe na kuchoma matairi huku maafisa wa Polisi wakilazimika kurusha mabomu ya machozi na risasi bandia hewani ambapo ghasia hizo zinafuatia tangazo lililotolewa siku ya Jumamosi kwamba Rais wa Nkurunziza ameteuliwa na chama chake kuwania muhula wa tatu wa urais.Serikali imesema kuwa maandamano hayo si halali.

Kumbukumbu zinaonyesha kwamba maelfu ya raia wa Burundi wamelitoroka taifa hilo katika majuma ya hivi karibuni wakihofia kuongezeka kwa ghasia hizo, huku taifa hilo likijiandaa kwa uchaguzi mnamo mwezi Juni, 2015.

Wakati hayo yakitokea, mrengo wa upinzani nchini humo unaoundwa na vyama 9, Aprili 21, 2015 ulimtangaza Jean de Dieu Mutabazi, kuwa ndiye atayapeperusha bendera yao katika uchaguzi ujao wa rais nchini humo.
 
Muungano huo unaojulikana kwa jina la Participatory Opposition Coalition in Burundi (COPA), umemteua Mutabazi kuwa mgombea wake katika uchaguzi huo utakaofanyika Juni mwaka huu.

Check Out Romantic Diamond Kissing Zari's Baby Bump....So Cute!!

$
0
0
When i saw this pic i went like, awwwwwww this is so cute and romantic, Diamond seems to be very happy. Love is an amazing feeling!!

Kabla ya Uchaguzi Mkuu Mangula Aamua Kuwasaka Wasaliti CCM..Adai Kila MTU awe Mlinzi wa Mwenzie Kwani CCM imejaa Wasaliti

$
0
0
MAKAMU Mwenyekiti wa CCM Tanzania Bara, Philip Mangula amemaliza ziara yake katika majimbo ya Mkoa wa Dar es Salaam, na kuagiza kila mwanachama awe mlinzi wa mwenzake, amchunguze ili kuepuka wasaliti.

Akizungumza na waandishi wa habari jana, Mangula alisema kuna wanachama wamekuwa wakikisaliti chama hicho tangu mwaka 2010 na wengine bado wapo, ambao wamekuwa wakisababisha CCM kushindwa uchaguzi katika baadhi ya maeneo.

Kila mtu awe mlinzi na ukigundua kwamba kuna anayesaliti chama atoe taarifa na atakapobainika kweli ni msaliti atafukuzwa ndani ya chama... CCM ina viongozi wengi kila mtu ni kiongozi ila nyakati za kuongoza zinatofautiana,” alisema.

Mkakati wa Ushindi Akizungumzia mkakati wa ushindi, Mangula alitaka wanachama wake kuhakikisha kwamba mgombea atakayesimamishwa anakuwa mgombea wa chama, ili kusaidia chama hicho kupata ushindi katika Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba mwaka huu.

Tunaandaa chama chetu ili kupata ushindi, hivyo mgombea atakayesimamishwa atakuwa wa chama, kwa sababu kinaposhindwa chama hatusemi fulani kashindwa, bali chama kimeshindwa vivyo hivyo na mgombea akishinda ni ushindi wa chama.

Wakati wa kura za maoni ni wakati ambao mwanachama anagombea ili kuwakilisha chama na pale ndipo anakuwa na kundi, lakini baada ya mgombea kuteuliwa ni chama kinachogombea hivyo makundi yanatakiwa kuvunjwa na kumuunga mkono mgombea aliyeteuliwa, ili kukipatia chama ushindi.

Tunatakiwa kumpa ushirikiano mgombea wetu tutakayemsimamisha na tunahitaji nguvu ya ziada na kuunda umoja, ili kufanya mgombea wetu ashinde… mtu anatakiwa kutangaza sera za chama na siyo sera zake,” alisema Mangula.

Amani Aidha aliwaasa wanasiasa wasitumie mtego wa kuingia kwenye uchaguzi kuvuruga amani ya nchi, kwa kuwa katika nchi zote zilizo na machafuko, mara nyingi huchangiwa na baadhi ya wanasiasa na baadhi ya viongozi wa dini.

Pia aliwataka wana CCM kujipanga kuimarisha ulinzi katika vituo vya kupigia kura na kuweka tahadhari bila kupigana, ili kuepusha vurugu zinazochangia kura nyingi kupotea kutokana na watu kuogopa kwenda vituoni kwa kuhofia usalama wao.

Awali kabla ya kuzungumza na waandishi wa habari, Mangula alikutana na wajumbe wa Halmashauri ya CCM Mkoa wa Dar es Salaam. Naye Meya wa Jiji la Dar es Salaam, Didas Masaburi alisema wametekeleza ilani ya CCM kwa vitendo katika miundombinu ya barabara, elimu na maji.

Mbali na mafanikio katika miundombinu hayo, Masaburi pia alisema wapo katika mchakato kuhakikisha kila Manispaa inakuwa na dampo lake ili kudhibiti usafi wa mazingira.

Ukweli Kuhusu Kupotea Kwa Shilingi MIA TANO ya Sarafu..Wajanja wa Mjini Watumia Kutengeneza CHENI..

$
0
0
Ndani ya wiki moja nimekutana na watu watatu wakitafuta sh.500/= ya sarafu kwa sh.2500/= kwa sarafu moja ya mia 5, mwanzoni nilipuuzia lakini baada ya kutulia na kufanya utafiti nimegundua kwanza hii sarafu imekuwa adimu na inatafutwa kwa udi na uvumba 
Pili ni kwamba wale wapenzi wa SILVER sasa unaweza kupata cheni halisi ya silver kwa bei poa kabisa ! sababu ni kwamba zile sarafu za mia tano ndio zinayeyushwa na kutengeneza vidani siku hizi

Hii ni KASHFA nyingine kubwa kuhusiana na pesa yetu na mamlaka zinazohusika ziko kimya kuhusu hili lakini hii ndio hali halisi inayoendelea mitaani TUGUTUKE

Muuguzi Aliyemchapa Viboko Mjamzito Baada ya Kushindwa Kujikakamua ili Mtoto Atoke Asakwe na Kuchukuliwa Hatua Kwa Kusababisha Mauaji ya Mtoto Tumboni

$
0
0
Katika toleo letu la jana kulikuwa na habari iliyomuhusu mwanamke mmoja wa Dodoma ambaye alikuwa amepelekwa kituo cha afya cha Muungano wilayani Chamwino kwa ajili ya kujifungua, lakini akakutana na vitendo vya kikatili vilivyochangia mtoto afie tumboni.

Kwa mujibu wa habari hiyo, muuguzi aliyekuwa zamu siku hiyo aliamua kumchapa viboko mjamzito huyo baada ya kumuona anashindwa kujikakamua ili kumsukuma mtoto atoke na alikuwa akifanya hayo akidai kuwa mwanamke huyo ni mzembe na anadeka ndio maana alikuwa anashindwa kujifungua.

Muuguzi mkuu wa Hospitali ya Mkoa wa Dodoma alikiri kuwapo kwa taarifa za mama huyo kuchapwa viboko akiwa chumba cha kujifungulia na kwamba wameagiza uchunguzi ufanyike ili kupata taarifa sahihi za tukio hilo na hatua zichukuliwe.

Wakati uchunguzi huo ukifanyika, hatutaki kuamini kuwa kifo cha mtoto huyo kimesababishwa na kupigwa kwa mama yake, lakini kinachotushangaza ni jinsi mama huyo alivyoshughulikiwa hadi kupoteza kiumbe hicho alichokitunza tumboni kwa miezi tisa.

Muuguzi huyo ni mmoja tu kati ya wengi ambao wamekuwa wakiwafanyia vitendo visivyo sahihi wagonjwa wanapoenda hospitalini kwa ajili ya kupata tiba, hasa wajawazito ambao hulundikiwa mzigo wa maneno kuanzia wanapofika hadi wanapojifungua. Imekuwa ni kawaida kwa kina mama wajawazito kusimangwa, kutolewa maneno machafu na kucheleweshewa huduma na matokeo yake baadhi hujikuta wakipoteza watoto na wengine kulazimika kujifungua kwa kufanyiwa upasuaji.

Wengine wamekuwa wakilalamika kuwa wauguzi huwaomba rushwa na wasipotoa, hufanyiwa vitendo hivyo vya kikatili na kudhalilisha.

Mambo hayo husababisha wanawazito wanaoishi kwenye maeneo ya nje ya miji, kuona ni heri kujifungulia majumbani au kwa waganga wa jadi ambako wanaona hakuna unyanyasaji kama wanaofanyiwa hospitalini na matokeo yake hukumbana na athari kubwa zaidi.

Tunatambua kuwa wauguzi wanafanya kazi katika mazingira magumu kutokana na Serikali kutotenga fedha za kutosha kwenye sekta hiyo, lakini hatuamini kuwa hali hiyo ndiyo inayosababisha wauguzi wafanye vitendo vya unyanyasaji kwa wagonjwa, na hasa wajawazito.

Tunaamini kuwa katika mazingira hayo magumu, bado wauguzi wanaweza kuonyesha moyo wa upendo, kufanya kazi kwa weledi na maadili angalau kwa kiwango kinacholingana na mazingira waliyonayo ili juhudi za kuhimiza kina mama wajifungulie hospitalini au kwenye vituo vya afya zizae matunda.

Itakuwa ni kitu cha ajabu kama Serikali inapiga kelele kuhimiza wananchi kwenda kwenye vituo vya afya au hospitalini wakati wauguzi nao wanafanya vitendo ambavyo vinakatisha tamaa wananchi kwenda sehemu hizo.

Wakati mama huyo akiendelea kupata matibabu kwenye Hospitali ya Mkoa ya Dodoma, ni vizuri kwa uongozi wa mkoa kufanya uchunguzi wa kina kama ulivyoahidi ili kupata taarifa sahihi za tukio hilo lililotokea Aprili 3 mwaka huu, takriban siku 20 zilizopita.

Imekuwa ni kawaida kwamba tukio lolote baya likiripotiwa na vyombo vya habari, wahusika huwa wepesi kusema wanafuatilia kupata taarifa kamili na wanapoona hali imepoa, nao wanachana nalo na hakuna hatua zinazochukuliwa. Matokeo yake ni vitendo hivyo kuendelea kuwa sugu

atutarajii kwamba uongozi wa mkoa wa Dodoma utaingia kwenye mkumbo huo wa kusubiri hali ipoe, bali utatekeleza ahadi yake ya kufanyia kazi taarifa hizo ili wahusika wachukuliwe hatua.

Na kwa kuwa huduma duni ni tatizo sugu hospitalini na kwenye vituo vya afya na hospitalini, Serikali haina budi kufuatilia vitendo hivyo ili kuvikomesha.

Tafadhali: MWANAUME Anayeuliza Maswali Haya Mawili ni wa Kumuepuka Kama Ukoma

$
0
0
Kama we mwanamke umekuwa na mwanaume ambaye hamjawahi kusex hata mara moja lakini ndio mnaanza uhusiano then katika chatting za hapa na pale mwanaume akakuuliza haya maswali mawili ujue mbovu wa wabovu, hajui kugegeda na anakibamia. Mkimbie kabisa

MASWALI YENYEWE HAYA HAPA:

1. Huwa unatumia muda gani kufika kileleni?
Ukiona mwanaume kakuuliza swali hilo, ujue yeye ni ''ONE MINUTE MAN'' yaani akiingiza tu kamwaga na mgegedo wake hausimami tena. Sasa anawaza huyu mwanamke kama muziki wake ni wa nusu saa mpaka saa zima nitauweza kweli hivyo anakuuliza mapema ajijue. Ukimtajia dakika nyingi, utaona hana hata nguvu ya kukulazimisha mkagegedane.

2. Huwa unapenda mgegedo wa aina gani?
Hili pia ni moja ya swali ambalo wanaume vibonde huwauliza mademu ambao hawajawahi kusex nao. Mwanaume anayeuliza swali hilo mara nyingi huwa anakuwa ana kibamia hahahaha.

Posted by: MCHUNGUZI HURU (Associate Professor)

Nay wa Mitego Ampoza Gwajima, Watu Wataka Majibu ya DNA ya Mtoto wa Flora Mbasha

$
0
0
Week Kadhaa zimepita sasa toka Nay wa Mitego alipotoa majibu ya DNA ya mtoto wake baada ya Utata kutokea kuwa Mtoto si wake, Majibu ya DNA yalitoka na yakaonyesha kweli mtoto ni wa Nay wa Mitego ..
Kutokana na uamuzi wa Nay wa Mitego wa kwenda kuhakikisha  kama mtoto ni wake watu wameanza kuongea chini chini kuwa lazima na Emmanuel Mbasha aende kumpima mtoto wake na Flora Mbasha kwani naye ana utata baada ya mume wa Flora kumtuhumu Askofu Gwajima kuwa anamahusiano na Mke wake na ndio chanzo cha ndoa yao kuvunjika.....

Je wewe unamshaurije Emmanuel Mbasha?

Mwanamuziki H-Baba Amchungulia Mkewe Wakati Akijifungua...Baada ya Hapo Akaamua Kumwandikia Waraka huu

$
0
0
Msanii mkubwa Bongo Hamis Baba Maarifu Kama H Baba kwenye Music Amemuandikia Waraka wa kumpa hongera mke wake Frora Mvungi baada ya kumshuhudia laivu akijifungua mtoto wa Pili hospitalini..

Flora amejifungua mtoto wa pili ambae amepewa jina la Afrika huku H baba akishihudia jinsi mkewe huyo aliyokuwa anamleta Africa Duniani.

"Huyu ni mtoto wa pili mke wangu anajifungua nashuhudia mwanzo wa uchungu mpaka kujifungua kwake kwa kweli heshima kubwa kwa mama Tanzanite ulijitahidi sana nakupa hongera kwa kweli wewe ni shujaaa na ni mfano wa kuigwa" ulisomeka waraka huo

Waraka huo uliendelea kusema:

"Kuna muda nilikuwa navumilia na kutamani kutoka nje ili nisione unavyojifungua lakini nilijikaza na kuangalia mpaka mwisho wake Asante mungu kwa watoto hawa wawili mungu awajalie wakue vizuri"

Hongera Sana H-baba na Flora Mvungi

Ommy Dimpoz Aikana 'KICK' ya Wema Sepetu ,Adai Hawezi kuwa Mapenzini na Wema Kwasababu Anaweza Kuharibu Mambo yake ya Maana

$
0
0
Msanii mkubwa Bongo Omary Nyembo maarufu kama Ommy Dimpoz amesema kuwa hawezi kuwa na uhusiano wa kimapenzi na Wema Sepetu kwa sababu anaweza kuharibu mambo yote ya maana ambayo anapanga kuyafanya.
Dimpoz aliweka wazi hayo kwa Dia wa ala za Roho na kusema kuwa Wema ni staa na ni mzuri hana tatizo lakini mazingira yanachangia awe mbali nae kwani akiweka mapenzi kutakuwa hakuna kazi.

"Unajua ukiwa na rafiki alafu mkaweka mapenzi basi patakuwa hakuna kazi zaidi ya kuharibu kazi , hata kama palikuwa na project basi mwishowe inaharibika, Nasisitiza sina uhusiano wa kimapenzi na Wema Sepetu" Alisema Dimpoz

LIST ya Mastaa wa BONGO Wanaongoza Kwa Kushusha Matusi Mtandaoni

$
0
0
Imekuwa ikielezwa kuwa wasanii ni kioo cha jamii. Kwa maana hiyo wanatakiwa kufanya mambo ambayo yanaweza kuigwa na wale wanaowatazama. Hata hivyo, maisha wanayoishi baadhi ya wasanii hayaakisi msemo huo.

Wengi wamekuwa wakikumbwa na skendo mbalimbali zinazowafanya wasiwe na vigezo vya kuitwa kioo cha jamii.

Miongoni mwa mambo yanayowafanya wakati mwingine wadharaulike ni kutoa maneno machafu, ‘live’ au kupitia kwenye mitandao ya kijamii.

Katika makala haya nitawazungumzia mastaa wanaoongoza kwa kutukana mitandaoni

Wastara Juma
Huyu Wastara amekuwa akiheshimika kwenye jamii kwa muda mrefu na alikuwa ni miongoni mwa mastaa wa kike ambao wangesimama na kuamua jambo wangesikilizwa kutokana na jinsi alivyokuwa amejiweka na kuwaaminisha watu.

Lakini katika siku za hivi karibuni alichafuka kwa kuingia katika orodha ya mastaa wanaotukana mtandaoni baada ya kumvaa mmoja wa mashabiki wake aliyemsemea mbovu na kumtukana matusi mazito

 “Iweje anakubali kushushwa na mtu mmoja ambaye alikaa na kuamua kumvuruga, anasahau kama kuna kundi la watu linamheshimu?”  Aliandika mmoja wa mashabiki wake kwenye mtandao wa Instagram baada ya kuona matusi hayo.

 Amanda Posh

Wafuatiliaji wa mambo na hasa wale ambao wapo Facebook watakumbuka jinsi staa huyu wa filamu alivyomshambulia jamaa mmoja aliyefahamika kwa jina la Joel.

Haikuwa ustaarabu kabisa kwa staa huyo kufanya hivyo kwani jambo lililomkasirisha angeweza kulipuuza na angebaki na heshima yake huku yule aliyemtukana akionekana mjinga.

Lakini ukiacha hilo, Amanda amekuwa akisifika kwa kutoa maneno machafu pale anapochokozwa, tabia inayomfanya afiti kwenye makala haya.

Isabela Mpanda

Katika mastaa micharuko, huyu yumo! Hajivuni, hajisikii lakini ukimchokoza lazima akushikishe adabu kwa matusi.

Posti zake zenye lugha chafu kwenye mtandao wa Instagram zipo nyingi lakini pia kwa wale wenye kumbukumbu watakumbuka kuwa staa huyu aliwahi kumtukana mwanamitindo Belina Mgeni na mpaka sasa hawaongei.

Hao ni baadhi ya mastaa ambao katika siku za hivi karibuni wameshika chati kwenye suala la kutukana mtandaoni.

Majambazi Wavunja Kaburi....Wamvua Marehemu Nguo Na Viatu, Watimka Na Mabegi Aliyozikwa Nayo

$
0
0
Watu wanaosadikiwa kuwa ni majambazi wamebomoa kaburi la Napegwa Kishaluli (75) mkazi wa Mailimoja Kibaha mkoani Pwani aliyezikwa Aprili 20 mwaka huu na kumvua nguo zote pamoja na kuchukua mikoba aliyokuwa amezikwa nayo.

Tukio hilo lilitokea Aprili 24 mwaka huu katika Kata ya Tangini jirani na soko la Loliondo ambako baada ya mazishi kaburi hilo liliwekewa mlinzi kwa muda wa wiki moja.

Mkataba wa mlinzi huyo ulipomalizika aliondoka na siku iliyofuata kaburi hilo lilivunjwa.

Watu wa karibu na familia ya marehemu wamesema kuwa baada ya mazishi ulikuwapo uvumi kwamba marehemu alizikwa na vitu vya thamani zikiwamo fedha, simu, pete na mikufu ya dhahabu pamoja na nguo zenye thamani kubwa.

Hata hivyo, taarifa zinasema marehemu Kishaluli alizikwa na mikoba miwili ya nguo na vitu vyake vingine na kwamba kabla ya kifo chake aliagiza azikwe na vitu vyake.

Akizungumza na Mwandishi wetu jana,ndugu wa marehemu,Bartholomew Mwanjile alisema baada kuzika walilazimika kuajiri mtu wa kulinda kaburi hilo la ndugu yao kwa wiki moja lakini siku moja baada ya mkataba kumalizika kaburi hilo lilivunjwa.

Tuliweka mlinzi alinde kaburi hilo kwa wiki moja tukiamini litakuwa limekauka kwa sababu lilitengenezwa kwa zege"

Tuliamini watu wenye nia mbaya watashindwa kulivunja jambo ambalo limekuwa kinyume kwa vile baada ya muda huo kumalizika kaburi lilibomolewa na watu wasiojulikana ambao waliamini ndani ya mikoba hiyo kulikuwa na fedha,” alisema Mwanjile.

Mwanjile alisema baada ya kuvunja kaburi hilo majambazi walifungua jeneza na kupekua ndani kwa kuligeuza na kuliweka tofauti na lilivyokuwa awali, baada ya kumvua marehemu nguo zote na viatu alivyokua amevalishwa na hata soksi nazo walichukua.

Alisema tukio la kuvunjwa kwa kaburi hilo limetokea baada ya uvumi kuwa ndugu yao alizikwa na nguo na vitu vingine zikiwamo fedha, kiasi cha Sh milioni 8, cheni ya dhahabu,simu za gharama na kompyuta mpakato(laptop),jambo ambalo si la kweli.

Tulimzika ndugu yetu na mikoba ya nguo zake ambazo aliagiza kabla ya mauti kumkuta na kaburi tulijenga kwa zege lakini tukashauriana tuweke mlinzi, hapo ndipo watu wakaanza kutia shaka wakadhani kuna vitu vya gharama jambo ambalo si kweli,” alisema Mwanjile.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani, Jafari Mohamedi alithibitisha kutokea kwa tukio hilo na kwamba uchunguzi unaendelea na watakaobainika watachukuliwa hatua za sheria.

MBOWE Apigilia Msumari Kauli Ya Mnyika.....Asema Hawatamruhusu Kiongozi wa ACT Zitto KABWE Kujiunga na UKAWA kwa Madai Kuwa Atavujisha SIRI Zao

$
0
0
Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe, amesema hawatamruhusu Kiongozi wa Chama cha ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe, kujiunga na Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa).

Kauli ya Mbowe imetolewa siku chache baada ya Zitto kutangaza kuwa ACT ipo tayari kujiunga na Ukawa kama wanavyotaka Watanzania wakiwamo baadhi ya viongozi wa umoja huo.

Alitoa kauli hiyo jana wilayani Kyerwa alipozungumza na Mwandishi wetu.

Mbowe alisema kuwa hawamwamini tena Zitto kwa madai kuwa akiingia Ukawa atakuwa akivujisha siri za umoja huo kwenda Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Hatuwezi kumruhusu Zitto na chama chake kiwe miongoni mwa Ukawa. Tukiruhusu Zitto awepo siri zote zitakuwa zikiwafikia CCM,” alisema Mbowe.

Aprili 15 mwaka huu, Chama cha Alliance for Change and Transparency (ACT-Wazalendo), kilitangaza kuwa kipo tayari kushirikiana na vyama vingine vya siasa kwa lengo la kuleta mapinduzi ya uchumi na kubomoa mfumo unaowanyonya wananchi.

Zitto alisema hivi sasa taifa limekuwa na shauku ya ACT kushirikiana na vyama vingine kama njia ya kufanikisha malengo ya kukitoa CCM madarakani.

SIWEMA Ajibu Mapigo Amuonyesha Serengeti Boy aliyefumaniwa Naye..Ni Baada ya Nay wa Mitego Kuanza Kuishi na Shamsa Ford

$
0
0
Ni kama Vile Kujibu Mapigo..Mrembo Siwema ambaye alikuwa Mpenzi wa Nay wa Mitego na kumzalia mtoto mmoja na kisha kupigana chini kwa tuhuma za kumfumania laivu akiwa na Kiserengeti Boy ameanza kumuweka wazi katika mitandao kijana ambae ni mpenzi wake kwa sasa..

Inasemekana mapenzi na Kijana huyo hayakuanza jana wala leo ili yapo muda mrefu ila walikuw wakifanya kwa siri mpaka siku Nay wa mitego alipofumania mchezo na kuamua kuchukua mtoto wake na Kusema...

Kijana huyu ambae anaonekana ni mdogo watu wengi wa huko mwanza wamempa jina la kiserengeti boy..Kwa sasa anaonekana kila kona akiongozana na Siwema bila kificho kama zamani..
Siwema Akiwa na Serengeti Boy na Rafiki yao

Wema: Mama Yangu Amepoteza Uwezo wa Kuona Kwa 75%!

$
0
0
Staa wa Bongo movies, Wema Isaac Sepetu ‘Madam’ amefunguka kuwa mama yake mzazi, Miriam Sepetu anasumbuliwa na macho ambapo madaktari wamegundua kwamba amepoteza uwezo wa kuona kwa asilimia sabini na tano (75%).

Kwa mujibu wa Wema, aliamua kumpeleka mzazi wake huyo hospitalini (hakuitaja) ndipo alipohakikishiwa tatizo hilo ambalo limekuwa likimsumbua kwa muda mrefu.

“Kumnusuru mama yangu asipate upofu wa moja kwa moja inabidi afanyiwe operesheni ya macho,” alisema Wema kwa huzuni kwa kuwa hakuna kama mama.

Kwenye ukursa wake mtandaoni  Wema aliandika "My mumumu anaumwa macho and she is abt to have an eye surgery... You'll be fine inshallah my love... I love u with all my heart..."mara baada ya kuweka picha hiyo hapo juu akiwa na mama yake.

Pole sana mama Wema.

Picha za Diamond Platnumz na Mpenzi Wake Zari Wakila BATA Visiwani Zanzibar

$
0
0


Diamond akilibusu tumbo la mpenzi wake Zari ambaye ni mjamzito.
Mwanamuziki Nasibu Abdul 'Diamond' akijiachia na mpenzi wake Zarinah Hassan 'The Boss Lady' Visiwani Zanzibar.
Zari na Diamond wakizidi kula maisha huko Zanzibar walipokwenda kwa ajili ya shoo iliyofanyika Juni 25, mwaka huu.
******* 
STAA wa Bongo Fleva nchini, Nasibu Abdul 'Diamond' na mpenzi wake Zarinah Hassan 'The Boss Lady' wamezidi kuonyesha kuwa penzi lao linazidi kuimarika baada ya Zari kuachia picha Instagram wakiwa 'close' walipokwenda Visiwani Zanzibar juzi.
  
Wapenzi hao walikuwa Zanzibar kwa ajili ya shoo ya Diamond iliyofanyika Jumamosi (Aprili 25, mwaka huu) usiku huko Ngome Kongwe.
  
Mojawapo ya picha za wapendanao hao ambayo imeenea mitandaoni ni ile ambayo Diamond analibusu tumbo la Zari mwenye ujauzito unaodaiwa kuwa wa staa huyo.

Urais 2015: CCM Imejiandaa na Changamoto za Kumkubali au Kumkataa Edward Lowassa?

$
0
0
Ni ukweli usio na shaka kwamba Mheshimiwa Waziri Mkuu wa zamani, Ndugu Edward Ngoyai Lowassa ana dhamira ya kugombea kiti cha urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia chama chake cha CCM.

 Ni ukweli usio na shaka pia kwamba ili afikie hatua ya kuwa mgombea urais wa CCM ni lazima kwanza ashinde kwa kuruka na kuvuka “viunzi” na “vigingi” vya Kamati ya Maadili, Kamati Kuu, Halmashauri Kuu na Mkutano Mkuu, ambavyo vyote hivyo ni vyombo vya Chama cha Mapinduzi (CCM).

Kwa mujibu wa hali ya hewa ya kisiasa katika nchi yetu kwa sasa, inaonekana wenye “nia” ya kuiomba CCM ikubali kuwakilishwa na wao kwa nafasi ya urais katika Uchaguzi Mkuu utakaofanyika, inshaa-Allah, mwishoni mwa mwaka huu, wako wengi pengine wakaizidi idadi ya “wasaka urais” wa CCM waliojitokeza mwaka 1995 na 2005.

Hapo tunaona kwamba “ushindani” ndani ya CCM juu ya ni nani haswa aiwakilishe, utakuwa mkali na mgumu mno.

Swali ambalo ni muhimu na lazima litafutiwe majibu mapema ni kumtafakari kila mgombea atakayeomba “ridhaa” ya CCM kuiwakilisha ni ipi faida ya kuiwakilisha CCM na yapi madhara ya kutokuiwakilisha; hiyo ni tafakuri ambayo ni muhimu kila mmoja wao kufanyiwa.

Kalamu yangu kwa leo imeona iikumbushe CCM kufanya tafakuri hiyo kwa Mheshimiwa Edward Lowassa kabla ya hao watarajiwa wengine. Ninapendekeza tafakuri hiyo ianze kwa Mheshimiwa Lowassa kwa sababu:

(a) Ndiye mgombea mtarajiwa pekee ambaye anaonekana kuwa na wapenzi na mashabiki wengi mpaka hivi sasa.

(b) Ndiye mgombea mtarajiwa pekee ambaye tayari ameshatamka kwamba katika uongozi wake ataanzia pale ambapo Mheshimiwa Rais Jakaya Kikwete atakapoishia (hiyo ni dalili kwamba “piga ua” atagombea tu).

(c) Ndiye mgombea mtarajiwa pekee ambaye tayari amefuatwa na kushawishiwa na makundi kadhaa wa kadhaa.

(d) Ndiye mgombea mtarajiwa pekee ambaye wasifu wake na historia yake inamtofautisha na wagombea watarajiwa wengine.

Si sahihi hata kidogo kumdharau au kuidharau jamii hiyo ya kitanzania iliyojenga imani kwake, na ndipo nikaonelea nianze “uchokozi” mapema kwa njia ya swali kwamba: Je, CCM imejiandaa na changamoto za kumkataa au kumkubali Lowassa?

Katika hali ya kawaida na kwa kutumia akili tu ya kuzaliwa, endapo Chama cha Mapinduzi (CCM) kitamptisha Mheshimiwa Edward Lowassa kuwa mgombea wake wa urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Uchaguzi Mkuu ujao, itapambana na changamoto kadhaa.

Lakini hata kama CCM watakataa kuwakilishwa na Mheshimiwa Lowassa, bado pia zitakuwepo changamoto kadhaa. Kwa muktadha huo, kumkubali Mheshimiwa Lowassa ni tatizo, na hata kumkataa ni tatizo pia.

Mfano wa Mheshimiwa Lowassa katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu ni kama “tonge tamu” la chakula cha moto ambalo ukilimeza utaungua na kulitema huwezi kwa sababu ni tamu na unalihitaji.

Kazi kubwa sana ambayo watapambana nayo viongozi wa CCM ni kuyapima madhara na faida kwa kutumia kipimo huru kisichohusishwa na “shinikizo” lolote lile.

Pamoja na kwamba CCM ndio wanaowajibika na kazi ya kuufanya utafiti huo, lakini kutokana na mazingira ya siasa za kitanzania kwa sasa tunaweza kuyapima yale ya “juu juu” ambayo muonekano wake uko wazi. Halafu yale ambayo ni ya “ndani zaidi’ yatatamkwa na wenyewe (makada na makomredi wa CCM).

CCM ikithubutu kufanya “mizengwe” na hila yoyote kumkataa Mheshimiwa Lowassa kiasi kwamba, yeye Lowassa na wafuasi wake wakajiaminisha kwamba “wameonewa”, basi CCM ijiandae kuzikabili changamoto zifuatazo:

(i) Kwanza Mheshimiwa Lowassa, yeye mwenyewe haonekani kama atayapokea matokeo hayo japo kwa shingo upande, bali upo uwezekano mkubwa wa kukubali “maombi” ya kujiunga na chama pinzani chenye nguvu ili agombee kupitia upinzani.

Na hapo ni lazima CCM “ijiandae” kupambana na nguvu kubwa ya upinzani ambayo itakuwa imeunganishwa na nguvu kutoka ndani ya CCM ya wale “CCM Lowassa” ambao watakuwa wamekasirishwa sana kutokana na “kuenguliwa” kipenzi chao, Mheshimiwa Edward Lowassa. Kwa mtazamo wa wafuasi hao, “Lowassa kwanza, CCM baadae”.

Japokuwa Wapinzani wamekuwa wakitamka hadharani mara kwa mara hawatohitaji “makapi” ya CCM, lakini kamwe tusijidanganye kwamba Wapinzani watadharau nguvu ya Mheshimiwa Lowassa katika kuwafanya Wapinzani wafungue ukurasa mpya wa kuiondoa CCM madarakani kwa kutumia nguvu ya mwana CCM huyo “mstaafu”.
 
Je, CCM wamejiandaa kukabiliana na nguvu hiyo ya Mheshimiwa Lowassa iliyounganishwa na nguvu ya vyama vya upinzani?

(ii) Jambo la pili ambalo CCM wanatakiwa wajiandae nalo baada ya “kumuengua” Mheshimiwa Lowassa katika kukiwakilisha chama kwenye kugombea urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Uchaguzi Mkuu ujao, ni namna ya kuishi na wana CCM ambao watakuwa ni “mamluki” wa Lowassa.

Na kwa kuwa watakuwa hawajulikani, wanaweza “kuvuruga” mbinu zote za ushindi za CCM na hatimaye CCM kushindwa au kushinda kwa ushindi “mwembamba” mno ili wawaonyeshe Watanzania umuhimu wa Lowassa.
 
Je, CCM imejiandaa vipi kulikabili kundi la wafuasi wa Lowassa ambao wamo ndani ya CCM? Je, ni vipi wataweka mbele maslahi ya CCM kwanza wakati mgombea wao Lowassa hakupita?

(iii) Jambo la tatu ambalo CCM wanapaswa kujiandaa kukabiliana nalo baada ya “kumkataa” Mheshimiwa Lowassa ni kitendo cha kunyimwa kura kwa mgombea wa CCM au kitendo cha wafuasi wa Mheshimiwa Lowassa kupeleka kura zao kwa mgombea wa Upinzani (hata kama atakuwa si Mheshimiwa Lowassa).

Wafuasi wa Lowassa watachukua uamuzi huo wa hasira kwani hata ukiwasikia baadhi yao hivi sasa, unaona wazi kwamba hawakujiandaa hata kidogo kushindwa bali wamejiandaa kushinda kwa asilimia mia moja.

CCM itapata wakati mgumu sana baada ya kumnyima Lowassa nafasi ya kugombea urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia CCM kwani Mheshimiwa Lowassa ameshajijengea “mazingira” yanayoonyesha kwamba anapendwa sana na idadi kubwa ya Watanzania wakiwemo baadhi ya Masheikh waliothubutu kwenda kumuomba akubali kugombea cheo hicho cha urais.

Pia baadhi ya viongozi wa dini ya Kikristo ambao wamekwenda kumuomba agombee pamoja na kumfanyia “maombi” nyumbani kwake Dodoma. Wengine ni baadhi ya waendesha “bodaboda” pamoja na wajasiriamali kadhaa.

Kwa bahati mbaya sana, Mheshimiwa Lowassa bado hajawaambia wapenzi na wafuasi wake kwamba ili kura ya mwendesha bodaboda au mamalishe au kiongozi wa kidini iwe na thamani, ni lazima kwanza Kamati ya Maadili ya CCM, Kamati Kuu ya CCM, Halmashauri Kuu ya CCM na Mkutano Mkuu wa CCM; wajiridhishe kwamba Mheshimiwa Lowassa “anauzika” na anaweza kuongoza katika cheo hicho cha juu cha urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Kwa ujumla, CCM ina mtihani mgumu sana katika kazi ya kuchuja wagombea na ni lazima ijiandae kwa faida na hasara kwa kila mgombea kutokana na kumkataa au kumkubali kwao.
 
Lakini kwa kuanzia tathmini hiyo, waanze na huyu Mheshimiwa Lowassa. Je, CCM imejiandaa vyema na changamoto za kumkataa au kumkubali Lowassa? Kama haijajiandaa, inapaswa iamke kutoka katika “usingizi mzito” na ifanye tahtmini hiyo sasa.

Changamoto ambazo CCM wanatakiwa kujiandaa nazo kwa kumkataa au kumkubali Mheshimiwa Lowassa zipo nyingi sana, cha msingi ni kuwakumbusha wana CCM kuwa makini kwani ni CCM pekee ndiyo inayoonekana kuwa kimbilio la Watanzania kwa nafasi ya mgombea urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Baadhi ya Watanzania huwa wanajaribu kubadilisha vyama katika ngazi ya serikali za mitaa, udiwani na ubunge; lakini katika ngazi ya urais bado wanaiamini CCM kuwaletea kiongozi bora.
 
Kwa muktadha huo, CCM nayo inalazimika kujipima na kutafakari mapema yote yanayotarajiwa kujiri katika Uchaguzi kwani uchaguzi sio tukio la ghafla bali ni tukio linalojulikana mapema hivyo mipango ipangwe mapema pia.

Kanisa Langu Halitakufa, Anayetaka Kuliangamiza Ataangamia yeye- Gwajima

$
0
0
Askofu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima, amesema kuna watu wanaotaka kuua kanisa lake lakini kamwe halitakufa na litang’aa hadi katika kizazi cha mwisho.

Akizungumza katika ibada yake iliyofanyika katika Viwanja vya Tanganyika Packers, Dar es Salaam jana, Askofu Gwajima alisema watu hao wamekuwa wakisema kuwa hawalipendi Kanisa la Ufufuo na Uzima na kutaka life.

Alisema kanisa lake lina mamlaka na linaungana na sauti ya damu ya mwana kondoo.

Damu ya Yesu ina sauti kubwa ingawaje ilimwagika miaka mingi iliyopita hivyo watu hao wanapaswa kutambua kuwa wanalindwa na Mungu kwa njia ya damu ya Yesu.

“Hili ni kanisa la Wakristo wa Agano Jipya wasioogopa mambo ya ajabu ajabu na ya upuuzi puuzi na anayetaka kuliangamiza kanisa hili aangamie mwenyewe na ashindwe kwa damu ya Mwanakondoo,” alisema.

Hivi karibuni Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mathias Chikawe, alitishia kuzifutia usajili taasisi mbalimbali zikiwamo za dini ambazo alisema zinajihusisha kutoa matamko na kushawishi waumini wao kutekeleza matakwa ya siasa.

Waziri Chikawe alisema atatumia Sheria ya Vyama vya Jamii Sura ya 337 na kanuni zake zinazosimamia uendeshaji wa taasisi hizo.

Alikiba ni Mmoja ya Mwanamuziki Mzuri Ambaye ana Management iliyoshindwa Kulikabili Soko la Muziki?

$
0
0
Ni ukweli ulio wazi kabisa Alikiba ni mmoja wa waimbaji/wanamuziki bora kabisa na mwenye kipaji cha aina yake hasa kuimba!

Ni wazi soko la muziki limebadilika sana na limekuwa na ushindani wa hali ya juu na pengine uwezo wa msanii unaweza usipimwe kwa kipaji chake bali uwezo wake wa kulikabili soko na kuendana na mahitaji ya soko la muziki! Na hapa kwenye mipango ndipo watu hushikana uchawi na kuanza kutuhumia ooh fulani ana bebwa ooh fulani anatumia nguvu za giza ..kumbe muda mwingine ni mipango tuu...
kuna jamaa wa futuhi husema "Mjini mipango.

Nami naamini soko hili hasa la sasa lina hitaji mipango na uthubutu wa hali ya juu kinyume na hapo soko litakushinda!

Alikiba ni mmoja ya wasanii wenye uwezo mkubwa sana na mwenye ushawishi sokoni lakini naamini ni mmoja wa wasanii mwenye management mbovu na iliyo choka kufikiri kabisa!
Management ya Alikiba haijawai kumbadilisha alikiba wala kumfanya Alikiba kuwa msanii mkubwa kama matarajio ya watu!

Wakati Alikiba anarudi nilitegemea atarudi huku akiwa amejiandaa kulikabili soko la muziki ambalo kwa sasa lina changamoto nyingi na halitegemei kipaji tuu!

Hivi management ya Alikiba haifahamu kuwa kwa sasa Video ina mtangaza msanii kuliko audio?
Hivi management ya Alikiba imeshindwa kumpandisha thamani Alikiba?
Hivi kweli Alikiba nae hadi sasa ana stahili kujumuishwa kwenye show zisizo na tija hasa zile zinazo onekana kabisa hazilipi?
Tangu Alikiba amerudi sijaona cha kipekee ambacho amerudi nacho kuweza kupambana na soko la muziki na ukweli ni kwamba Alikiba hakujipanga au kuna tatizo kubwa kwenye management yake!

Kusema kweli ni wazi ana hitaji kuitazama upya management yake pengine kuibadilisha kabisa maana haina tija kwakwe na ina mdanganya sana!
Hivi Alikiba na management yake wameshindwa kujua kuwa video inafanya wimbo huduma milele?

Pengine sio dhambi na sijawai kuhisi ni dhambi kuiga kwa wengine...kuanzia thamani ya show na kumbrand msanii na bila shaka mashabiki wa Alikiba wanatamani kuona Alikiba anaonekana kuwa ni msanii mkubwa si masikioni tuu bali hata machoni mwa watu..!

Watanzania pamoja na shida walizo nazo linapokuja swala la kutumia hela kwa burudani huwa wako tayari kabisa tatizo wasanii wetu wanashindwa kutumia fursa..kwakweli Alikiba ni msanii aliye shindwa kuchukua hela ambazo watanzania wanazo kwaajili yake na kipaji alicho nacho!

Nimeamua kuyasema haya kwasababu nimegundua kuna mambo Alikiba na management yake hawaambiwi kabisa na bila shaka wata jitazama upya kama kweli hii ndio thamani ya Alikiba tunaye msikia kila leo!

Karibuni wana jamvi!

Majibu ya mwigizaji Rose Ndauka baada ya kuhusishwa na matatizo ya ndoa ya Shetta

$
0
0

Taarifa zilizomfikia Soudy Brown ni kwamba ndoa ya msanii Shetta imevunjika baada ya taarifa kumfikia mke wake kuwa Shetta anamahusiano na mwigizaji Rose Ndauka.
Soudy aliamua kumtafuta Rose Ndauka, majibu yake yalikuwa hivi; “Kwanza kitu ambacho ningependa kumuambia asipende kusikiliza watu.. la pili kitu chochote ambacho kinahusiana na mahusiano sio vizuri kupeleka kwenye public… hata ingekuwa ni ukweli kile ambacho amesikia ni ukweli yeye kama mwanamke anapaswa kuwa strong asiondolewe nyumbani kwake kwa sababu ya mwanamke mwingine..“
Kusikiliza stori yote ya U Heard bonyeza play hapa chini..

Hivi ndivyo Eric OMONDI alivyoirudia wimbo wote wa Diamond PLATNUMZ- Nasema Nawe (VIDEO)

$
0
0
Mara ya kwanza niliona vipisi vya hii video kwenye ukurasa wa Eric Omondi wa Instagram.. nikaviweka hapa alafu nikawa na hamu sana kuiona video kamili.
Katika pitapita zangu nimekutana nayo video kamili, Eric Omondi kaifanya REMIX ya wimbo wa ‘Nasema Nawe‘ ya Diamond Platumz, yeye yake ameiita ‘Nabeba Mawe‘

Viewing all 104709 articles
Browse latest View live




Latest Images