Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104698 articles
Browse latest View live

Ladies: 10 Men You Shouldn't Even Bother Dating

$
0
0
People aren’t always who they appear to be. After dating a guy for a little while or after getting to know a man for a few weeks, you may realize that he isn’t exactly what you thought or expected him to be. And in the dating pool, there are definitely some men that you want to avoid dating at all costs, here are 15 of them

THE PLAYER

No woman really wants to date a player, but for some reason a lot of females are attracted to them. Newsflash: a player has and wants no future with you. As the name entails, he’s doing nothing but playing you, wasting your time, and letting you go whenever he’s found a new lady to mess with. Players only want side pieces, and we’re all worth a lot more than that.

THE JOBLESS MAN

A man without a job should have no use to you. A man who is jobless obviously lacks a lot of ambition, skill, or maybe both. Unless you find that he has a good excuse, i.e. he just got laid off and he’s looking consistently for a new job, you’ll want to stay away from guys with no income. Unemployment doesn’t count and in the end he may try to reel you in and have you pay his bills.

THE EXTREMELY INSECURE MAN

We all have our insecurities and often times we work towards them to help eliminate them altogether. Dating a man with a lot of insecurities is extremely time consuming and in the end, it can be really tough. You have to deal with a lot of jealousy, insecurity, trust issues, and so on. A relationship with an insecure man is bound to be a chore.

THE WANNABE KING

Ahh, a king without his crown. You may one day run into a guy who expects to be treated like royalty. He wants you to cook, clean, and do his laundry for him. All the while he isn’t helping one bit. A guy with such high expectations isn’t likely to be one who treats you right. You deserve to be treated like a queen, or at least like a princess, not the other way around.

THE DAD TO TOO MANY

When a guy is 25 with three children by three different women, you better have a huge red flag going off in your head. Men with a lot of kids by various different women usually aren’t worth dating. Chances have it that you’ll get caught up in the already existing baby mama drama, and we all know how that turns out. Avoid the guy with several baby mamas, you’ll thank yourself later.

THE NARCISSIST (SELF CENTERED)

Dating a narcissist is never wise. There’s nothing worse than a man who is completely self-centered and unconcerned about anyone but himself. Though narcissists are likely to look nice and dress nice, they’re only worried about themselves. His care for you is more than likely non-existent.

THE ONE-NIGHT-STANDER

One night stands can have their perks, especially if you’re in needy mode. But, dating a guy who wants nothing but bedroom time with you is a mere waste of time. What good is a man if he only wants to get you in bed and then find his way out of it as quickly as possible? If he’s having one-night stands with you, he’s more than likely doing it with others.

THE HEAVY DRINKER

There’s nothing wrong with drinking, especially when you know your limits. However, dating a guy who loves to drink and drinks almost every night will only smells like trouble..and liquor.  A man who lives to drink and drinks to live will be costly in the end. What’s the fun in getting drunk every weekend? Guys tend to act like fools when they’re drunk anyway!

THE OVERLY EMOTIONAL MAN

A man who readily expresses and shows his emotions is rare to find, but an overly emotional man isn’t such a great pick. Men who are overly emotional tend to go the extreme with lots of crying and a lot of anger. Usually this men will tick at the drop of a pin. A man who has no control over his emotions isn’t usually a good guy to date.

THE OVERLY-CONTROLLING MAN

He expects you to abide by his rules, and what he says goes. He doesn’t want you to have a lot of male friends. After your first date he urges you to delete your dating profile and change your Facebook status. These are all signs of a man who is very controlling. This type of guy will only lead to a lot of trouble.


Zari is So Beautiful Diamond Can't Resist Her Beauty...Look at her Showing off Her Natural Hair

$
0
0
Zari is So Beautiful Diamond Can't Resist Her Beauty...Look at her Showing off Her Natural Hair

This is what she captioned this photo on social media:

Skin so flawless he can't resist....Blessed week ahead to all.

Zitto Kabwe awanyima usingizi CHADEMA, viongozi wahaha nchi nzima kuzima moto wa ACT

$
0
0
Wadau, hakika sasa si siri tena kwamba kitendo cha uongozi wa CHADEMA kumfukuza uanachama aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu wa chama hicho, Zitto Kabwe kumekigharimu chama.

Mtakumbuka kuwa baada tu ya Tundu Lissu kutangaza kuwa Zitto Kabwe si mwanachama tena wa chadema baada ya Mahakama kufuta kesi aliyoifungua dhidi ya uongozi wake, Zitto Kabwe alitangaza kuachia madaraka ya ubunge na hatimaye kujiunga na ACT ambapo amechaguliwa kuwa Kiongozi Mkuu wa chama hicho.

Kitendo hicho cha Zitto kuhamia ACT kilipokelewa kwa dhihaka na makada wa CHADEMA wakidhani kuwa Zitto Kabwe ndo anajimaliza kisiasa. Hata hivyo, baada ya Zitto Kabwe kuhamia ACT na kuchaguliwa kuwa kiongozi wa chama hicho, alifanya ziara katika mikoa 10 nchini akiwa na viongozi wengine akiwemo Katibu Mkuu Samson Mwigamba. Umati uliofurika kuhudhuria mikutano ya ZITTO umewashtua sana viongozi wa CHADEMA. Kilichowashtua zaidi ni maelfu ya wafuasi wa chadema walioacha chama hicho na kujiunga na ACT.

Hakika Zitto Kabwe amechafua hali ya hewa ya Kinondoni Mtaa wa Ufipa. Sasa viongozi wanaona viti vinawaka moto. Sasa wanaona kuwa chadema inaelekea kwa Buriani. Ni kutokana na amsha amsha ya Zitto Kabwe na mchaka mchaka aliouanza, Viongozi wa CHADEMA hawana namna nyingine zaidi ya kukabiliana naye kwenye majukwaa na njia za siri.

Kwa upande wa majukwaani, Kamati Kuu ya chama hicho imeagiza kuwa viongozi wote wasambae mikoani kuzima moto wa Zitto Kabwe. Haijapata kutokea viongozi wakuu wote wakaikimbia ofisi ya CHADEMA kama ilivyo sasa. Kuanzia Mwenyekiti, Makamu Mwenyekiti, Katibu Mkuu na Manaibu Katibu wakuu wote wanapita maeneo aliyolisha sumu Zitto Kabwe ili kujaribu kutoa maziwa ambayo wanaamini pengine yanaweza kukata sumu hiyo. Lakini wapi.

CHADEMA sasa wanalia na kusaga meno. CHADEMA wanajutia maamuzi waliyofanya. Wataalam wa masuala ya siasa wanaona kuwa nguvu ya Zitto Kabwe katika kushawishi inazidi mara dufu uwezo wa viongozi wote wa UKAWA. Washauri wa CHADEMA akiwemo Saed Kubenea wanaona kuwa Zitto Kabwe akiachwa aendelee atasababisha nguvu ya UKAWA kumezwa na ACT.

Kwamba ACT itageuka kuwa chama kikuu ya Upinzani baada ya uchaguzi wa Oktoba 2015 ambao bila shaka CCM itashinda kwa kishindo. Aidha, jaribio la kumshawishi Zitto Kabwe kujiunga na UKAWA zinaelekea kugonga mwamba hasa baada ya John Mnyika kujichanganya alipotangaza kuwa Zitto Kabwe ni adui namba moja wa CHADEMA.

Imeandikwa na  Lizaboni/JF

Muswada wa Sheria ya Mtandao 2015 : Ikulu Yasema Hauna Tatizo Lolote.......Yaweka Wazi Kuwa Rais Kikwete Atausaini

$
0
0
Ikulu imesema Rais Jakaya Kikwete atasaini Muswada wa Sheria ya Makosa ya Mtandao ya mwaka 2015, kwa kuwa umepitia taratibu zote. Pia, Ikulu imesisitiza kuwa sheria hiyo ni nzuri na itadhibiti matumizi mabaya ya mtandao.

Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu, Salva Rweyemamu alitoa taarifa hiyo jana, alipozungumza na waandishi wa habari, Ikulu jijini Dar es Salaam. Rweyemamu alisema sheria ya Makosa ya Mtandao itasainiwa na rais muda wowote.

Hii ni sheria nzuri, kwanza inadhibiti matumizi mabaya ya mitandao, wote watakaohusishwa ama kutuma au kutumiwa vitu au picha mbaya sheria itawabana wote, na kama umetumiwa bila idhini yako, toa taarifa polisi, ili uwe kwenye upande salama,” alisema Rweyemamu.

Alisema madai ya wadau kwamba inanyima uhuru wa kupata taarifa, hayako sahihi kwa kuwa hiyo si sheria ya habari.
 
Alisema kutokuwa na sheria hiyo, si jambo jema kwa usalama wa nchi.

Muswada wa Sheria ya Makosa ya Mtandao ulipitishwa katika mkutano wa 19 wa Bunge, uliofanyika Dodoma hivi karibuni.
 
Katika mjadala, wabunge wengi walikemea vitendo vilivyokithiri vya uhalifu wa mtandao nchini, na kutaka sheria hiyo itakaposainiwa, itumike ipasavyo kudhibiti.

Wabunge wengi walisema viongozi, watu maarufu na jamii kwa ujumla, wamekuwa waathirika wakubwa wa matumizi hayo mabaya ya mtandao, kutokana na kutukanwa, kutishiwa kuuawa, kuzushiwa uongo na hata wakati mwingine kutapeliwa.

Hata hivyo, baada ya kupitishwa muswada huo, kumekuwapo na kauli za ukosoaji kutoka kwa watu binafsi na makundi mbalimbali, wakitaka rais asisaini hadi baadhi ya vifungu virekebishwe.

Miongoni mwa mambo yaliyokosolewa ni pamoja na sheria kubana pia mtu anayetumiwa vitu au picha mbaya . Wakati huo huo, Rweyemamu akizungumzia Muswada wa Sheria ya Takwimu kuhusu maombi ya wadau ya kutaka ziangaliwe pande zote mbili wakati wa kutiwa hatiani, kutokana na kutoa au kuandika takwimu zisizo sahihi. Alisema maombi hayo yatazingatiwa.

Kuhusu Muswada wa Sheria ya Habari, uliopelekwa pia katika mkutano wa Bunge uliomalizika hivi karibuni, Rweyemamu alisema;

 “Mimi naomba wadau wa habari wauunge mkono muswada huu, madai kuwa umepelekwa bungeni chini ya hati ya dharura sio kosa, na pia madai kuwa haujajadiliwa na wadau nalo sio sahihi, kwani muswada huu umejadiliwa zaidi ya miaka 10, na mimi pia nilishiriki kwenye moja ya mkutano wa wadau kuujadili miaka hiyo pale Morogoro.

Aidha alisema kuendelea kupinga muswada huo ni kusababisha kuendelea kuwa na sheria ya zamani, jambo ambalo linafanya kukosa sheria mpya. Alisisitiza wadau wa habari kuunga mkono .

Ugaidi
Akizungumzia masuala ya ugaidi, Mkurugenzi huyo wa Mawasiliano Ikulu alishukuru vyombo vya habari kwa kuandika na kuripoti habari za ugaidi kwa kuhabarisha wananchi mbinu za kujihami, iwapo tukio hilo litatokea.

Aliomba viendelee kuhabarisha umma taarifa za kujenga na kujihami dhidi ya matukio hayo, bila kuongeza chumvi na ushabiki.
 
Navishukuru vyombo vya habari vimefanya kazi yao ya kuhabarisha umma kuhusu masuala ya ugaidi na mbinu za kujihami, ila kuna baadhi wamekuwa wakiandika habari hizo kwa ushabiki na kuongeza chumvi, jambo ambalo siyo zuri,” alisema.

Leo ni Zamu ya Kuwajua Mastaa wa Bongo Wanaoongoza Kutukanwa Mtandaoni

$
0
0
Kwa upande wa wale ambao wanashika nafasi za juu kwa kutukanwa, wapo wengi lakini leo tutawazungumzia wahanga watatu.

Kajala Masanja:

Tangu aingie kwenye bifu na Wema Sepetu, kuna kundi ambalo linajiita Team Wema limekuwa likimshambulia kwa kumtukana na kumshutumu kwa mambo ambayo mengine hayana ukweli.

Hata hivyo, Kajala anaonekana kuwa mstaarabu kidogo kwani licha ya kutukanwa mtandaoni, yeye amekuwa mkimya akijua kujibizana na watu hao ambao wala hawana majina ni sawa na kuzidi kujichafulia.

Elizabeth Michael ‘Lulu’:
Huyu naye ni mhanga wa matusi mtandaoni. Kuna kundi la watu ambao linaonekana kuwa na chuki dhidi yake, huenda kutokana na mafanikio aliyonayo akiwa kwenye umri mdogo.

Lakini sasa, licha ya matusi anayoyaoga mtandaoni, amekuwa mvumilivu wa kuyaacha yapite. Watu wake wa karibu wanaeleza kuwa, licha ya kutukana sana mwenyewe wala hajui kwamba anatukanwa kwani si mtu wa kufuatilia nani kasema nini kibaya juu yake

Wema Sepetu:

Kama ilivyo kwa Kajala, huyu naye anashambuliwa sana na Team Kajala. Hawa ni watu ambao wamejitenga kuhakikisha wanamkosesha amani staa huyu.

Amekuwa akitukanwa kwa mengi lakini kwa kuwa anajua ustaa ni kama jalala, huwa hajali na anachukulia poa.

 Ni mara chache sana amekuwa akinyanyua mdomo wake kuwajibu wale ambao wamekuwa wakimsema vibaya sambamba na kumtukana.

Kwa uchache hao ndiyo mastaa ambao hivi karibuni wametia fora kwa

 kutukana na kutukanwa mtandaoni.

Tahadhari

Mastaa ambao ni wepesi kutukana mtandaoni  wajue kwamba endapo Rais wa Jamhuri ya Muungano, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete atasaini ile sheria ya makosa ya mtandaoni ya mwaka 2015, watajikuta wanaenda jela hivi hivi.

Mchezaji wa Yanga Hamisi Tambwe Ashinda Kesi na Kuvuna Mamilion ya Hela Simba

$
0
0
Kamati ya Sheria na Hadhi za Wachezaji ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), limeitaka Simba kumlipa mshambuliaji wa Yanga, Amissi Tambwe

kiasi cha Dola 7,000 (Sh 13,545,000) anazoidai klabu hiyo.

Simba jana ilipandishwa kizimbani kwa kesi tatu za madai ya fidia kwa waliokuwa waajiriwa wake ambao ni wachezaji Amissi Tambwe na Haruna Chonongo pamoja na kocha Zdravko Logarusic.

Kamati ya sheria na hadhi za wachezaji chini ya mwenyekiti wake Richard Sinamtwa ilisikiliza shauri la Tambwe ambaye alikuwa anaidai Simba jumla ya kiasi cha Dola 7,000 zilizotokana na klabu hiyo kuvunja mkataba wake.

Simba ilitakiwa kumlipa Mrundi huyo fidia ya Dola 6,000 (Sh 11,610,000), pamoja na dola 1,000 (Sh 1,935,000) zikiwa ni malimbikizo ya mshahara wake.

Katika shauri hilo Simba iliyowakilishwa na Katibu wake Steven Ally, ilikubali kudaiwa na Tambwe, ambapo kamati ikiagiza malipo hayo yafanyike kwa awamu mbili ikitakiwa Aprili 30 kulipa Dola 5000 (Sh 9,675,000) kabla ya Alhamisi hii na kumalizia Dola 2,000 (3,870,000) ifikapo Mei 10, 2015.

Aidha kamati hiyo imeitaka Simba kuhakikisha inasimamia utekelezaji wa makubaliano hayo kama watashindwa kufanya malipo hayo mapato ya mechi zake za mwisho yatashilikiliwa kulipa madeni hayo.

Mbali ya Tambwe, mwingine anayetarajia kuvuna fedha kutoka Simba ni winga wao Chanongo anayecheza kwa mkopo Stand United anayedai kutolipwa nusu mshahara wake kama ilivyokuwa katika makubaliano ya mkataba wake.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumanne ya Tarehe 28 April 2015

$
0
0

















Habari  Zilizopo  Katika  Magazeti  ya  Leo  Jumanne  ya  Tarehe  28  April  2015

Mgomo...! Mgomo..! Mabasi Yote Ya Abiria Yapanga Kugoma Nchi Nzima

$
0
0
WAMILIKI wa Mabasi yaendayo mikoani wameitunishia misuli Mamlaka ya usafiri wa nchi kavu na majini (SUMATRA )na kusema kuwa hawatashusha nauli kutokana na bei ya mafuta kupanda.

Wamesema kama SUMATRA hawatatoa  majibu mapema kuanzia  Aprili 29 mwaka huu hawatokata tiketi kwa wasafiri na badala yake wataendelea na mgomo huo kwa  siku saba.

Akizungumza Jijini Dar es Salaam jana  katika kikao cha dharura cha wamiliki wa mabasi yaendayo mikoani , Katibu Mkuu wa TABOA, Enea Mrutu, alisema SUMATRA ilikurupuka  kushusha nauli bila kufanya mchanganuo na kuda.

Wamiliki hao waliafikiana kuwa yeyote atakayetoa gari lake kufanya biashara kabla hawajapata muafaka kutoka SUMATRA watamchukulia hatua za kisheria.

TABOA wameitaka serikali kurudisha viwango vya nauli za mabasi ya mikoani kwenye hali yake ya kawaida iliyokuwepo miezi michache iliyopita kwasababu bei ya mafuta imerudi juu, baada ya kushuka kwa kisingizio cha bei ya mafuta kushuka

Breaking News: Majina Ya Walimu Waliopangiwa Kufundisha Shule Za Sekondari YAMESITISHWA Kwa Muda Kutokana Na Kasoro Za Kiufundi Zilizojitokeza

$
0
0
Orodha ya wahitimu wa shahada na stashahada waliopangiwa katika halmashauri mbalimbali inafanyiwa marekebisho baada ya kubainika kuwa uongozi wa Chuo Kikuu cha Sebastian Kolowa (Sebastian Kolowa University College-SEKUCO) cha Lushoto uliwasilisha orodha ya wahitimu wapatao 491 wa mwaka 2013 ambao walishaajiriwa badala ya wahitimu wa mwaka 2014.

Kutokana na sababu hiyo, orodha tajwa imesitishwa kwa muda ili kufanyiwa marekebisho na kuwekwa orodha sahihi itakayojumuisha wahitimu wa SEKUCO wa mwaka 2014.

Tunaomba radhi kwa usumbufu uliojitokeza kutokana na kasoro hiyo.

Imetolewa na;
OFISI YA WAZIRI MKUU - TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA

Wanawake Hupata Wakati Mgumu Jeshini Kuliko Wanaume?

$
0
0
Moja ya maeneo ambayo katika siku za karibuni yamekuwa yakitoa ajira nyingi nchini na mataifa mengine ulimwenguni ni majeshi.

Wanawake ni sehemu ya wanaonufaika na ajira ya taasisi hiyo nyeti kwa nchi zote ulimwenguni, huku idadi yao ikitajwa kuongezeka kwa kasi katika kazi hizo za ulinzi wa mataifa yao huku swali kubwa likiwa je, wanawake hupata wakati mgumu zaidi ya wanaume jeshini?

Swali hilo linajibiwa na utafiti wa hivi karibuni unaobainisha kuwa taasisi hizo si rafiki kwa wanawake tofauti na ilivyo kwa wanajeshi wanaume.

Utafiti wa Taasisi ya Women’s Rights uliopewa jina la Changamoto zinazowakabili wanawake jeshini, unabainisha kuwa wengi wa wanawake walio jeshini wamekuwa wakikabiliwa na changamoto nyingi kuliko wanaume.

Utafiti huo unaeleza kuwa wanawake wana wakati mgumu jeshini kutokana na kukumbwa na visa tofauti vya unyanyasaji vinavyowanyima haki.

Utafiti huo ambao uliakisi pia jinsi wanajeshi wa kike wanavyotumika wakati wa vita, unabainisha kuwa mara nyingi wanajeshi wanawake hutumika katika kazi za kutoa huduma na kuonekana kama ‘wauza sura’ wakati wanaume wakiwa mstari wa mbele, jambo ambalo linawapunguzia thamani ikilinganishwa na wanajeshi wanaume.

“Wanakabiliwa na changamoto nyingi kama vile talaka, ukosefu wa huduma bora za afya kulingana na jinsia zao. Pia, kubughudhiwa kimapenzi na visa vingine vya namna hiyo, ingawa wana umuhimu wa kipekee katika medani hiyo,” unabainisha utafiti huo.

Utafiti huo unasisitiza kuwa pamoja na changamoto zote wanazokabiliana nazo, wanawake wamekuwa na umuhimu wa kipekee.

Matokeo ya utafiti huo yametangazwa ikiwa ni wiki chache tangu Msemaji wa Wizara ya Ulinzi ya Marekani, Leon Panetta atangaze nia ya jeshi la nchi hiyo kurudisha mfumo liliouacha miongo miwili iliyopita wa wanawake kupelekwa mstari wa mbele jeshini.

Hatua hiyo imekuja huku nchini humo kukiwa na wastani wa matukio 19,000 ya mashambulizi ya kingono kwa wanajeshi wanawake kila mwaka.

Hata hivyo, hali hiyo inapuuzwa na Panetta, anayesema kuwa malengo ya idara ni kupata wanajeshi wazuri wenye sifa kwa ajili ya mstari wa mbele bila kujali jinsia.

“Wanawake wameonyesha ari na moyo mkubwa wa kujitolea,” anasema Panetta na kuongeza kuwa atahakikisha mpango huo wa kuwarudisha wanawake jeshini unawapata wenye sifa na weledi wa hali ya juu katika uwanja wa mapambano.

Anasema awali mpango huo ulishindikana kutokana na sera za nje za Marekani hasa baada ya kuingia katika vita nchini Afghanistan na kuonywa kuwa utekelezaji wa mpango huo utakuwa mgumu kwa wanawake kupelekwa vitani katika nchi hiyo.

‘Kuna ambao walipelekwa kwa ajili ya kuhudumu katika kambi zilizokuwa nchini Afghanistan na kuna ambao walipoteza maisha kutokana na sababu mbalimbali ikiwamo maradhi ya kuambukiza.

Kuzuiwa kwa wanajeshi hao wa kike kulitokana na sababu nyingi, lakini baadhi ya wadadisi wa masuala ya kijeshi wanailaumu Pentagon kwa kutowajali askari wa kike, badala yake kutoa kipaumbele kwa wanaume.

“Pentagon ina utamaduni wa kutowajali askari wa kike ambao pia hawapewi fursa sawa na wenzao (wanaume), wanachukuliwa kama ni watu wa daraja la pili, wakiwa ni watu wa kuwastarehesha wengine kambini,” anasema Helen Benedict, mwandishi wa Kitabu ‘The lonely Soldier’ ambaye pia ni mwandishi wa habari na profesa katika Chuo Kikuu cha Columbia.

Anasema kukosa kuthaminiwa kwa wanawake wanajeshi ni tabia ya muda mrefu na huchangia udanganyifu katika utoaji wa taarifa za matukio ya mashambulizi kingono.

Anafafanua kuwa huo ni utamaduni utakaochukua muda mrefu kubadilika na kwamba kaulimbiu kuwa watu wote ni sawa, huenda ikabadili mtazamo.

“Naamini kunapokuwa na kundi la watu katika madarasa mawili tofauti, moja kwa ajili ya mashujaa na jingine kwa watu wa kundi jingine ni wazi kuwa unaelekea katika vitendo vya namna hiyo,” anasema Dempsey na kuongeza kuwa kadri watakavyowatendea kwa usawa, ndivyo nao watakavyotendeana.

Kauli ya JWTZ

Mkurugenzi wa Habari na Mawasiliano wa JWTZ, Joseph Masanja alikataa kuzungumzia utafiti huo. “Siwezi kuzungumzia utafiti huo wala kueleza hali halisi ilivyo” alisema na kukata simu.

Hata hivyo, kimtazamo, wanawake hawaonekani kuwa na jukumu la kuwapo mstari wa mbele, ingawa baadhi ya nchi za Kiafrika zimekuwa na utaratibu kwa wanawake kushiriki vitani.

Sierra Leone kupitia azimio lililofikiwa nchini Ghana la Accra-based Women Peace Security (WISPEN) ni moja ya nchi ambazo wanajeshi wanawake hushiriki vitani na kuwa mstari wa mbele. Mpango huo unafadhiliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Mfuko wa Maendeleo kwa Wanawake (UNIFEM) ambao umefanya hivyo ili kuvunja mila na imani potofu zinazowabagua wanawake.

Shinikizo jingine la kufanya mapinduzi hayo ni kutokana na kuwapo kwa visa vingi baada ya ghasia za mwa 1991-200o zilizosababisha wanawake na wasichana wengi kubakwa na kudhalilishwa kijinsia na wanajeshi wa makundi yaliyokuwa hasimu.

Mke wa Hussein Machozi Aibuka na Kusema Haya Baada ya HUSSEIN MACHOZI Kusema Hakuwahi Kuoa Huko Mombasa

$
0
0
Yule dada aliyedai kufunga ndoa na Hussein Machozi ameibuka na kusema haya Maneno kwa Uchungu baada ya Hussein Machozi Kudai Anatafuta Kick na si kweli kwamba walifungua ndoa :

"Hey jameni hebu msinidhalilishe. mimi ndie mke wa Hussein. nasidhani nikwanini niseme nilifunga ndoa ya kiislam kama niuongo.mimi namuogopa sana Mungu. Ndoa nikitu ambacho nibaraka.
mume wangu amenidhalilisha kisa chakufanya hivyo sikijui. ila mm niko thayari kama akisema aniacha i will say fine. cause haina haja kua na mtu anaekukana ama anaekana Ndoa. Yamenisikithisha sana haya maneno. na kwaujumbe wenu yeye hakuthoroka ndoa. Bali mm ndie nnaeishi nje ya Africa. so yy alirudi kwao tu baada ya muda mrefu kua kenya mm nlipomuacha huko. ulizeni pande zothe mbili kabla kuandika haya maneno ati mwanamk athafutha kiki. kiki gani nithafuthe africa? Nimwaka gani tulifunga ndoa kama ni kiki mbona sikuithafutha wakathi huo? Muogope Mungu mumewangu. Usikufuru. ila kama ndoa inkushinda iepuke usiikane. duniani utaikana , je mbele yaa Mungu pia waezaikana nakuniita mm huyo mwanamke wakimombasa?
Am sorry realy. mm sina shida yakukimbilia mtu. Namshkuru Mungu Alhamdhulillah"

Hiyo meseji imeandikwa Hapa :http://www.udakuspecially.com/2015/04/husein-machozi-mimi-sijaoa-bado.html

Angalia Hii Video Jinsi Hussein Machozi Alivyosema Hajawahi Kuoa huko Mombasa

Wema Sepetu Apata Deal la Ubalozi wa Hospitali ya Kimataifa

$
0
0
Miss Tanzania 2006 na muigizaji wa filamu, Wema Sepetu ameteuliwa kuwa balozi wa hospitali ya kimataifa ya macho.

Taarifa hiyo imetolewa na meneja wake, Martin Kadinda kwenye Instagram:

Mrembo wa Tanzania, muigizaji na mjasiriamali Wema Sepetu, Amesign makubaliano ya kuwa Balozi wa Hospital Ya Kimataifa Ya macho Iliyopo Ali hassan mwinyi Road katika jengo la Tropical House…..#mkataba huu wa ni wa mwaka mmoja.. Wema amehaidi kuwa balozi wa hospitali hiyo iliyokuja na mitambo mpya ambayo itawezesha vijana wenye umri chini ya miaka 35 wanaotumia miwani kuacha kabisa utumiaji wa miwani kwakuwa wanauwezo wa kuondoa swala la uvaaji miwani kwa vijana..

Mke Achinjwa na Mume na Kufa Kisa Kapata Wapi Hela ya Kwenda Saloon..Wivu wa Mapenzi Wachangia

$
0
0
HII ni zaidi ya ukatili! Jiji la Tanga bado linazizima kufuatia mauaji ya kutisha yanayodaiwa kufanywa na mwanaume aitwaye Khalfan  Hamad (46), dhidi ya mkewe, Mary Lucas (20) kwa kumchinja na panga kisa kikidaiwa ni wivu wa mapenzi, Uwazi lina mkasa mzima.

Tukio hilo lililoacha simulizi ya kushangaza miongoni mwa wanandoa na wanaotarajia kuingia, lilijiri Aprili 18, mwaka huu nyumbani kwa mwanaume huyo, Mtaa wa Mapinduzi ‘A’ Kata ya Duga jijini hapa.

WANACHOKIJUA POLISI WA TANGA

Kamanda wa Polisi Mkoa  wa Tanga, ACP Zuberi Mwombeki alitangaza kwa waandishi wa habari kwamba, mauaji hayo yalitokea saa nne na nusu asubuhi ya Aprili 18 mwaka huu.

Alisema chanzo cha tukio hilo ni wivu wa kimapenzi kati ya wawili hao  ambapo marehemu alimuomba mumewe pesa kiasi cha shilingi elfu kumi aende saluni kutengeneza nywele lakini mwanaume akasema hana.

“Mwanaume hakumpa pesa marehemu lakini baadaye alimkuta amesuka na ndipo ugomvi ulipoanzia hapo hadi kutokea mauaji hayo,” alieleza kamanda huyo.

UWAZI LAANZA NA MAJIRANI

Mengi yamesemwa kufuatia mauaji hayo, lakini kama kawaida ya Gazeti la Uwazi ni kufuatilia kwa kina ili kujua chanzo cha kila habari inayotakiwa kuandikwa gazetini.

Ili kujua nini kilitokea kabla na baada ya mauaji hayo, Uwazi lilizungumza na baadhi ya majirani wa nyumbani kwa mtuhumiwa huyo ambaye kwa sasa anashikiliwa na polisi chini ya ulinzi mkali.

“Jamani sisi wenyewe tumeshtuka sana kwa kifo cha Mary, mimi nimeongea naye akiwa anakwenda saluni na hata aliporudi. Kama angejua ndiyo siku yake ya kufa naamini asingekwenda. Inauma sana!

“Mary alitoka saluni akiwa amependeza maana alitengenezwa nywele vizuri sana. Mimi mwenyewe nilimsifia. Kufika nyumbani kwake, mzozo ukaanza.

“Mumewe alitaka kujua alikotoa shilingi elfu kumi ya kuendea saluni maana yeye hakumpa. Mzozo ulikwenda hadi mwanaume akachukua panga na kumchinja. Naamini ni wivu,” alisema jirani mmoja.

 KUMBE WALIKUWA NA HISTORIA YA UGOMVI

Jirani mwingine, Shaban Juma yeye alisema: “Hawa watu wameishi katika hali ya kutoelewana na walikuwa wakigombana kila wakati, lakini hatukujua kama litatokea hili kwani mara zote katika kugombana kwao, mwanaume ndiye aliyekuwa akipigwa jambo ambalo liliwafanya watu wa karibu yake kumshauri  kuvunja uhusiano wao kulikoni aibu ya kupigwa na mke.”

Jennifer   Charles yeye pia ni jirani, alisema: “Siku ya tukio Mary alimwomba mumewe hela ya kwenda kutengeneza nywele saluni  lakini mume hakuwa na pesa siku hiyo lakini baada ya kuondoka nyumbani,  marehemu naye alikwenda saluni.

“Baadaye mume aliporudi  nyumbani hakumkuta  Mary lakini mara alirudi akiwa ametengenezwa nywele jambo lililomfanya  bwana  kuhisi kuwa fedha hizo amehongwa na mwanaume  mwingine  tofauti na  yeye na hivyo kuzuka ugomvi  huo.”

 MUME ALITOKA NJE AKITAMBA KUUA

Baada ya Jennifer kumaliza kusimulia hayo, Juma  Ally, naye ni jirani, akaendeleza: “Hatukujua kilichoendelea katika mzozo wao, lakini baadaye ukimya ulitawala. Muda mfupi mbele mume alitoka nje na kutuambia kwamba ameshaua  huko ndani  kwani amechoka kupigwa na sasa amejibu mapigo.

“Kwanza tulijua anatutania lakini  tulivyoona kimya kimezidi tukaamua kuingia ndipo

tulipomkuta marehemu akiwa chini, akitoka damu nyingi. Tuliogopa kwa kweli. Mary mrembo tunayemjua sisi, amelala chini na damu chapachapa.

“Alikuwa ana majeraha  makubwa sehemu ya shingo na kichwani  yaliyotokana na kupigwa na panga. Ilionekana panga lilikuwa kali sana na panga lenyewe lilikuwa pembeni yake. Ndipo tulipoamua kumkimbiza Hospitali ya Mkoa, Bombo ambapo alipoteza maisha wakati madaktari wakihangaika kuokoa uhai wake.”

ASINGEKUFA MKE

Naye, Fatuma Ramadhani alisema kutokana na ugomvi wa mara kwa mara kati ya wawili hao na mwanaume kupigwa kila wakati, majirani waliamini siku moja mume  huyo ndiye angekuja kupata madhara hata kufa kutokana na alivyokuwa akipigwa.

MTUHUMIWA KUPANDA MAHAKAMANI WAKATI WOWOTE

Kamanda Mwombeki alisema upelelezi unaendelea ili kuweza kumfikisha mahakamani mtuhumiwa huyo.

Marehemu Mary alizikwa katika eneo la Mwakizaro jijini Tanga, siku ya pili baada ya tukio hilo la kuhuzunisha.

Hivi Mke Wangu Anajiandaa Kuachana na Mimi Baada ya Miaka 10 ya Ndoa au?

$
0
0
Husika na kichwa cha habari, nimekua nikijiuliza hili swali kwa kipindi kirefu sana bila majibu. Mimi na mke wangu tulifunga ndoa ya Kanisani miaka kumi iliyopita, tuna watoto watatu, sisi sote ni wafanyakazi na sote ni masters holders.

Miaka saba iliyopita mke wangu alinifumania na rafiki yake kipenzi. Huyo rafiki alikua anaishi mkoani mara nyingi akija Dar es salaam alikua akifikia kwetu, so akawa amekuja kwa mambo yake.Jumapili moja wife na familia walienda kanisani akabaki rafiki na mimi, baadae nikaenda bar kupata supu, then nikazimua bia kadhaa hadi mchana nikaenda home nilale kidogo nitoke tena.

Nilipofika home nikafungua geti dogo, nilipaki Gari nje. Nikasikia kilio cha mahaba sebuleni naingia hivi namkuta shemeji akiwa na top tu chini hana chochote akijihudumia kwa mkono huku alilia kwa sauti kubwa, nilishindwa kujizuia nikaanza kuvua nguo kama nafukuzwa nikamrukia kochini na akanipokea kwa mikono miwili.

Ikawa ndo mchezo wetu, kumbe housegirl aliunyaka mchezo mzima na kumshtua wife na wakatuwekea mtego ambapo tulinasa, nilikua nimeamka usiku wa nane nikaenda kwa shemeji tukiwa katikati wife akaingia na kutuma na kumtimua rafiki usiku huo huo.Nikamwangukia na kuomba msamaha na nikasamehewa.Miaka michache tangu fumanizi hilo wife akaanzisha tabia ya usiri na kutonishirikisha mambo yake hasa ya maendeleo

(1) Tukio la kwanza:-
Alijenga nyumba sehemu flani hapa Dar es salaam bila mimi kujua, fundi wake alinipa hizo taarifa accidentally
Nilipom confront akakiri na kukosa majibu ya maana.

(2)Tukio la pili:-
Akafungua duka la nguo kimya kimya nikabaini kupitia intelligence info nilizopata akaruka sio duka lake
Ila baadae nilithibitisha ni la kwake.

(3)Tukio la tatu.
Alinunua shamba bagamoyo worth 10 million niligundua baada ya yy kudhulumiwa kumbe Dalali alimtapeli shamba halikua lake.Kesi ikaenda polisi hatimaye mahakamani ikafika pahala ikashindikana kuficha nikagundua, nikaingilia kati kumsaidia mke wangu akarudishiwa pesa zake tukafuta kesi

(4)Tukio la nne
Alinunua Gari 35 million dream car yake, tangu anadunduliza hizo hela akawa anatuma Japan kwa binamu yake kidogo kidogo lakin kimya kimya hadi likafika, nikastukia tu siku amekuja nalo home badala ya kufurahi kwa kweli nilihuzunika

Gari hilo ilibaki kidogo tu liibiwe nikaingilia kati halikuibiwa ilikuaje? Ni hivi:-
Kumbe kijana aliemfanyia clearance bandarini wife hakumlipa yule kijana wakatofautiana
Janki alitaka 1.5 million wife akadai ni laki tano dogo akagomea hela akasema utaona

Baada ya mwezi hilo Gari likaibiwa kibo complex tegeta wife alilia kama mtoto mwanaume nikaingia kazini. Nikatenga kama 1 million kwa polisi, kwa kutumia technolojia ya mawasiliano na kwa ku mtrack yule dogo na mawasiliana yake hatimaye gari ikapatikana dogo yupo nyuma ya nondo hadi leo.

Hata hivyo wife hajaacha hii tabia, hivi sasa ana biashara ya kukopesha watu kwa riba anaifanya kwa siri kubwa ila mimi naijua nimeamua kumuacha tu aendelee maana nimeshachoka.Wadau huyu mtu ana mpango gani na ndoa hii? Au ndo anajiandaa kuishi kivyake baadae? Nimefañya kosa gani lisilokua na msamaha? Kama lipo naomba mnisaidie majibu ya haya maswali.

Kwa upande wangu, biashara zote nazofanya mbali na kazi yangu anazijua.Hata nyumba nilizojenga nimempeleka kote. Nina guest kijijini kwetu ambayo mama yangu mzazi anaisimamia pia Mke wangu anaijua ingawa ningeweza kumficha na asingejua nipo njia panda najiuliza huyu mtu ni Wa kufa na kuzikana kweli?
Je safari yetu ya maisha ni moja kweli?

Sincerely naomba kwa moyo wenu wa dhati mnisaidie mawazo.

NB: Sijazini tena tangu nizini na Rafiki yake miaka saba iliyopita nae sijawahi kumshika wala kumshuku kwa uzinzi.

Here is the amount of money DIAMOND charges per One Show Outside Tanzania

$
0
0
Here is a letter Diamond wrote to promoters in Kenya giving them conditions that they must meet before he performs.

 “First of all the team is going to Include 10 people.

You will have to manage Local transport during our staying there, return Air transport and Accomodation for the whole team.

=> TRANSPORT

8 Economy and 2 Business class return air tickets

=> ACCOMMODATION

4 double rooms

One Single Room

And one Presidantial Suit Room

=> PERFORMANCE FEE

Our performance fee is 40,000$ per show at the Moment bt if you delay to book us until we release our new Track on the middle of this Month there will be an increase of 5,000$

=> TECHNICAL RIDER

Our Technical rider includes two wireless Sure Brand Microphones, a glass stage (the size will depend on your venue size) with trussing having LED lights, and moving heads, moreover the plot stage shall have a backstage well equipped with air condition and eight personnel six being security, one waitress, and one representative from the organizers side…the backstage shall have water, juices , and snacks, please avoid beacon or any form of pork oriented meals…Please do note that the performance fee mentioned earlier is a very discounted rate aiming at establishing our good and pure business relationship.
Our performance will be 2 and a half hours to be precise.

Please do note that we won’t allow any figure on stage except for two security and our Dj during performance.

Any form of video shooting is unacceptable unless there can be special agreements between WCB and the client.

Thank You in advance.


Diamond Platnumz Management.”


Ikulu Yakana Kuwepo kwa Njama za Kutaka Kumdhuru Dr. Reginald Mengi Zilizodaiwa Kuandaliwa na Rais Jakaya Kikwete

$
0
0
Ikulu imekana kuwapo njama zozote za kutaka kumuangamiza Mwenyekiti Mtendaji wa IPP, Dk. Reginald Mengi, zilizodaiwa kuandaliwa na Rais Jakaya Kikwete, kwa kile kilichodaiwa kuwashughulikia wanaoihujumu serikali yake na kupanga kumshughulikia.

Njama hizo ziliripotiwa na baadhi ya vyombo vya habari, ambavyo vilidai kunasa mazungumzo kati ya Rais Kikwete na Kiongozi wa chama cha ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe, ambaye anadaiwa kumchongea Dk. Mengi kwamba, ndiye kinara anayesababisha serikali yake iyumbe kila mara.

Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, Ikulu, Salvatory Rweyemamu, aliwaambia waandishi wa habari jana kuwa Rais Kikwete hawezi kushiriki katika njama za kumdhuru raia na kwa hiyo, habari hizo ni za kutengenezwa kwa nia mbaya ya kutaka kuharibu urafiki uliopo kati ya Rais na Dk. Mengi.

Alisema Rais Kikwete alizisikia habari hizo akiwa nchini Jordan, Jumamosi ya wiki iliyopita na kushangazwa nazo.

Hata hivyo, alisema Zitto, ambaye ndiye wa kwanza kushutumiwa kuhusiana na habari hizo alikwishazijibu kwa kuzikanusha na kwamba, juzi Dk. Mengi alihudhuria sherehe za kutunuku nishani Ikulu, hivyo haamini kwamba, mahali pabaya kiasi hicho, ambako kuna watu wanamsubiri ili kumdhuru, anaweza kwenda.

Alisema madai kwamba, Zitto na Rais Kikwete walikutana Ikulu na kuzungumzia suala hilo, hayana ukweli, kwani hakuna mkutano wa ana kwa ana au mazungumzo ya simu, yaliyofanyika kati ya viongozi hao wawili katika miezi ya hivi karibuni.

Hata wakati huo, ambao ingetegemewa wangewasiliana labda kwa namna ya mazingira ya wakati huo wa matatizo ya Escrow na nini na nini, hawakuwasiliana kwa sababu Rais alikuwa anatibiwa nje ya nchi. Kwa hiyo, hapakuwapo na mkutano wa namna hiyo wa mbinu sijui za kupanga mbinu za kumuumiza mtu,” alisema Rweyemamu.

Alisema pia Rais huapa kulinda raia wote na mali zao, hivyo hawezi kugeuka na kuanza kula njama za kujaribu kumdhuru raia yeyote nchini.

Rweyemamu alisema pia Rais Kikwete na Dk. Mengi huwasiliana sana, kwani anayo simu yake na amekuwa akimpigia mara nyingi na kuzungumza naye, hivyo alidhani busara bora zaidi kwenye jambo hilo, ingeongoza kwamba, Dk. Mengi angempigia Rais na kutaka kujua ukweli kuhusiana na habari hizo.

Wakazungumza wote wawili, watu wazima, wazee wenye busara sana wakaelewana, kwamba tumeliruhusu hili suala kutoka pale lilipotakiwa kuja, tukalitumbukiza kwenye ukumbi wa kila mtu wa hadhara inakuwa jambo gumu kidogo kueleweka,” alisema Rweyemamu.

Aliongeza: “Ndio maana nikasema tulipopata habari, sisi hatukujua tu-react (tujibu) vipi. Yaani kwa sababu jambo halipo, jambo limetungwa, limefinyangwa finyangwa hivi likatupwa hivi mbele ya watu, hatujui limeanzia wapi. 

"Hata unapoiambia Ikulu, Kurugenzi ya Mawasiliano sijui, Mkurugenzi wa (Idara ya) Habari (Maelezo) hawakujibu. Tujibu nini? Hatujui.

"Kwa hiyo ndio maana sasa tukaanza sasa kuwasiliana jamani kuna hili tufanye nini? Tena kuna watu wengine walikuwa wanasema bwana hata ukiulizwa usiliseme. Kwamba, ni jambo halipo, halina maana, tuachane nalo lipite.”

Hata hivyo, alisema jana alilazimika kulizungumzia kwa kuwa aliulizwa na waandishi wa habari, pia kwa vile anayeshutumiwa ni Rais na shutuma zinahusu usalama wa raia wake, hivyo alifanya hivyo ili wananchi wapate kupumua japo kidogo.

Aunty Ezekiel's Baby Bump is so Huge Can Somebody tell Us How Many days are left?

$
0
0
Aunty is really pretty, even heavily pregnant she still looks beautiful, May God bless her journey and give her a bouncing beautiful baby.

David Kafulila atunukiwa Tuzo kwa hoja ya Escrow

$
0
0
Mbunge wa Kigoma Kusini David Kafulila anapewa award na taasisi ya HUMAN RIGHTS DEFENDERS kwa kazi ya escrow.

Mgeni rasmi ni balozi wa Jumuiya ya ulaya. Shughuli hiyo itafanyika asubuhi hii katika ukumbi wa Blue Pearl Ubungo Plaza.

Akihutubia huko Muhambwe Kigoma juzi David Kafulila alilaani wanasiasa wanaotaka kudandia hoja ya Escrow ili kujipatia umaarufu huku wakiwa hawana hadhi yoyote kuzungumzia hoja hiyo.

Kafulila pia aliwataka wananchi kuhakikisha wanachagua wagombea wote wanaotokana na UKAWA kwenye uchaguzi mkuu ujao.

Nashangazwa na Msimamo wa Mbowe Kuhusu UKAWA - Zitto

$
0
0
Katika gazeti la changamoto katika ukurasa wake wa kwanza unasomeka "Zitto azidi kuwaumiza CHADEMA" na habari hiyo ukiifuatilia ndani inaeleza kuhusu kauli ya mwenyekiti wa CHADEMA, mhe Mbowe na jinsi Zitto alivyoipokea.

Kwa mujibu wa gazeti hilo ni kwamba, Zitto hakutarajia mtu ambae yeye anamuheshimu katika siasa kuwa na misimamo isiyo tanguliza maslahi ya taifa mbele na badala yake kushikilia matatizo yao yaliyojitokeza huko nyuma ambayo kimsingi yalihusu nafasi za kiuongozi.

Zitto alieleza kuwa kwa sasa hayupo tayari kujibizana na viongozi tena kwa kuwa amekuwa akisema hivyo kila mahali anapokwenda kufanya mikutano yake na amewekeza nguvu nyingi katika kukitangaza chama chake kipya. Pamoja na malengo hayo, ila kwa kauli ile ya jana ameona hana budi kuitolea maelezo!

Zitto alisisitiza kuwa matatizo yake binafsi na viongozi wa chama chake cha zamani yasipewe kipaumbele kuliko maslahi ya taifa. Ameeleza kuwa mara kadhaa ameomba chama chake kijiunge na UKAWA lakini CHADEMA wamekuwa wakigoma. Kauli ile ya jana sio ngeni masikioni pangu. Alieleza Zitto.

Zitto aliongezea kuwa, "kama ni matatizo basi ni kati yangu na viongozi wa CHADEMA na yasifanywe ya taifa zima. ACT-Wazalendo tuna nia ya dhati ya kuwaondoa CCM madarakani. Pia UKAWA wana nia hiyo hiyo. Kwa hali hiyo hatuna budi kushirikiana kummaliza CCM na hilo litafanyika kama kweli tumetanguliza utaifa mbele badala ya matatizo yetu binafsi na viongozi wa chama changu cha zamani."

My Take,

Zitto amekomaa kisiasa na ana ngozi ngumu sana. Pamoja na mihasira na Mbowe na maneno yake ya ovyo kuhusu Zitto, lakini kijana Zitto amemjibu kistaarabu sana na bado ameonyesha nia ya kutaka ushirikiano na UKAWA.

Joketi 'Kuna Mtu Namtamani Sana Kimapenzi na Ninamvutia Kasi Nimpate'

$
0
0
Aliyekuwa miss Tanzania nambari mbili Jocate Mwegelo “jojo” amefunguka kuwa kuna mtu anamtamani sana kimapenzi na anamvutia kasi kumpata

Kupitia bonge moja la show weekend “the playlist” Kidoti, alisanuka hayo akihusisha ukweli huo na kile alichokiimba kwenye hit single yake “Leo leo” na Ice Prince

“Yah nyimbo inahusiana coz kuna mtu namtamani sana yani, ila akizingua tu nambwaga bado namuangalia” alisema Jojo

Hata hivyo Jocate hakuwa tayari kumtaja mtu huyo anayemvizia.
Viewing all 104698 articles
Browse latest View live




Latest Images