Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104756 articles
Browse latest View live

Agness Masogange Ajibu Maswali Kuhusu Tuhuma za Kufukuzwa South Africa, Kazi Anayoifanya South Africa, Kuhusu Mtoto Wake na Kuhusu Boifriend

$
0
0
Q1. Tulisikiaga umepata uraia wa south na ulisema hutorudi bongo ....mbona umerudi ghafla na kuna madai umetimuliwa ukweli ni upi?
.
AGGY:Hapa ni home hata iweje so ninapojiskia hamu ya kurudi narudi lkn sauz ndo sehemu ya kufanyia biashara zangu..
.
Q2: unafanya biashara gani ambayo watu hawaioni?.
.
AGGY:Sio lazima kila unachofanya lazima watu wajue, unachotakiwa kujua ni kwamba nafanya biashara zangu kule.
.
Q3: Tulisikia umepata mchumba huko south na ndo anayekupa jeuri ya kwenda na kuishi south.
.
AGGY:Ni kweli nina mchumba lakini hata nikienda kule siishi kwake nakaa kwangu na najilipia kodi mwenyewe
.
Q4: ulikuwa na mwanaume wako hapa bongo ambaye alikuwa anakupenda sana anaitwa Evance ilikuwaje ukammwaga??.
.
AGGY:Unajua kila mtu anapoamua kufanya jambo anakuwa ana sababu zakw mi naona Mungu tu akuamua tuwe pamoja hadi leo.
.
Q5: Hivi karibuni mtandao mmoja ulikuandika ww ndiye mwanamke mwenye shepu hatari africa mashariki je uliichukuliaje ile habari?
.
AGGY:Ahahahaaa nilijiskia vizuri na pia nilicheka sana nikajiuliza walinijuaje?
.
Q6: unasema sshv makazi yako ni south je ukipata mchumba bongo utakubali kurudi na kufunga nae ndoa?
.
AGGY: Hakuna mtu anayenizuia huko south km ntaridhika nae kwanini nisirudi?
.
Q7: wewe una mtoto lkn hujawahi kumpost hata siku moja km unavyopost zako na km mastar wenzio wanavyopoa watoto zao kwanini?
.
AGGY: Unajua unapozaa mtoto anakuwa sio mali yako pekeyako kuna babake pia ..siwezi kufanya hivyo kwa kuwa babake hapendi..
.
Q8: Hili suala la wewe kukamatwa na unga limewashitua wengi unawashauri nini wasichana wanaoifanya au wanaotaka kufanya hii deal?.
.
AGGY: Ni suala la kujitambua na kufikiri kabla ya kufanya ile sio kazi ya kufanya kwakuwa ukikamatwa majuto ni lazima
.
Q9: Tunajua ww hauna ttzo la kutozaa sbb tayari una mtoto je una mpango wa kupata mwingine?
.
AGGY: Kwa sasa sina mpango huo labda baadae sanaaa..
.
Q10: kwa sasa huonekani ktk video za muziki km zaman (video queen)vp au umeacha hii kazi
.
AGGY: Sijaacha na siwezi kuacha sema tu sijapata hilo deal kikubwa ni maslahi tu


Mwanamke Apata Aibu ya Mwaka..Haja Kubwa Yamtoka Bila Kujijua Kisa Mchezo Mbaya Anaofanyiwa na Wanaume

$
0
0
Kina dada muogopeni mungu pia jioneeni huruma jamani mwanaume mwenye mapenzi na wewe kamwe hawezi hawezi kukuingilia uani hata siku moja ndio maana hizo mambo huwezi kuzisikia jamaa kafanya na mkewe unasikia kwa michepuko tu au gelofriends....kama mwanaume hakupendi basi hakupendi tu usijidanganye kwenda kumpitisha uani ukadhani ndio atakupenda au hutoachwa atakutifua na kuachwa utaachwa tu...hebu huyu dada jamani katikati ya mtoko anaadhirika sijui alijua amejamba tu kumbe kashusha na limzigo bila habari sasa mateso yote yanini hayo??..najua humu mpo wengi tu...full kujikausha lkn ujumbe utakuwa umewafikia acheni tabia hizo mungu hapendi pia utajipa mateso bureee..nanyi wanaume mtakuja kuziba huko matokeo yake ukienda kukojoa ova unakojoa vidagaa kumbe umeziba njia na mim..vi..."
By Usipojipanga

Tetesi za Ndoa ya Wema Sepetu zazua Gumzo Mjini

$
0
0
Ubuyu Mpya unaoenea kwa siri kwenye mitandao ya kijamii kwa sasa, ni kuhusu ndoa ya super star wema sepetu inayotarajiwa kufungwa ivi karibuni. Chanzo cha ubuyu kinaeleza kuwa hatua zote muhimu zimeshachukuliwa, kinachosubiriwa tu ni bwaba harusi huyo mtarajiwa kuchukua jiko lake bila kipingamizi chochote. Mpaka sasa ivi bado mume huyo mtarajiwa wa staa huyo hajawekwa wazi kwa kuogopa watu wabaya kumfanyia fitna.

Mpaka sasa management yake inafanya siri kubwa kuhusu tukio hilo muhimu litakalobadilisha title na heshima ya msanii huyo.

Diamond kuzindua TV station yake mei 1 Mlimani City

$
0
0
Kupitia kwenye kipindi cha XXL kinachorushwa clouds fm, msanii Diamond platnums, amezungumzia uzinduzi wa Tv station yake binafsi atakayoizindua mei 1 kwenye party ya zari inayofahamika kama zari all white party itakayofanyika mlimani city.

All the best kama sio kick.

This is What Really Led To Lady Jay Dee's Break-Up With Her Husband,This Is What She Told Mzazi Willy Tuva, Kenyan Radio Station

$
0
0

Tanzanian songstress Lady Jay Dee has been in Kenya she was doing rounds in Kenyan radio stations to introduce her new song and also give an insight about her life; music life and love life.

It was late last year that Lady Jay Dee finally broke up with her husband of many years, Gadner G Habash a radio presenter with a Tanzanian radio station.

It was early rumored that Lady Jay Dee had failed to give her husband a child and perhaps this could be the reason behind their break-up.

However, the singer has come out to paint a clear picture of what really led to the infamous break-up. Contrary to what we have known for years, Jay Dee who was speaking to Mzazi Willy M Tuva when she visited Kenyan Radio called Citizen yesterday said that her husband was not only a drunkard but also a cheat and a lzy fellow.

“I quit my marriage because my husband was a cheat and a drunkard. He was also very lazy and I realized I did most of the work,” Jay Dee told the radio presenter.

On whether she will marry again, Jay Dee said: “I will for now take my time and see what comes my way. I will definitely fall in love at some point but not soon. I need a lot of time to compose myself.”

Here is the interview as it went down courtesy of Mambo Mseto:

Kadinda: Sipendi ‘Drama’ za Wema, Team Wema Msinitusi

$
0
0
Meneja  wa staa mrembo, mjasiliamali  na mwigizaji  wa filamu, Wema Sepetu , Martin Kadinda ametoboa kuwa anapenda kila kitu kuhusu Wema isipokuwa  ‘drama’  zake na kuwasihi watu ambao ni mashabiki na watetezi wa Wema Sepetu kwa kila jambo huko mtandaoni maarufu kama Team Wema wasimtukane .

Meneja huyo ambaye ni mbunifu wa mavazi aliyasema hayo hivi juzi kati kwenye ukursa wake mtandao mara baada ya kubandika picha ya Wema akiwa ndani ya ofisi ya Hospitali ya kimataifa ambayo imeingia mkataba na Wema kuwa Balozi wa hospital hiyo.

Sichoki Kumwomba Mungu... Naamini ipo siku tutafika kileleni.....  I love Every thing Abou tHer kasoro drama tu  team wema msinitusi”- Kadinda aliandika.

Na kweli team Wema walimstahi meneja huyu.

UKAWA Washindwa Kuafikiana.......NCCR Mageuzi Yawasilisha Hoja Ya Kujitoa, CUF Watoa Masharti Mazito

$
0
0


KIKAO cha viongozi wa vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), kimeshindwa kuendelea baada ya baadhi ya wajumbe kushindwa kuafikiana kuhusu hoja iliyowasilishwa na Chama cha NCCR-Mageuzi, ya kutaka kujitoa kwenye umoja huo, imefahamika.
 

Viongozi hao walikutana jijini Dar es Salaam jana katika Ofisi Kuu ya Chama cha Wananchi (CUF), ambapo pamoja na mambo mengine walikuwa wakijadili hatima ya kuachiana majimbo kuelekea Uchaguzi Mkuu wa Oktoba.
 

Katika kikao hicho ambacho kilitarajiwa kuanza saa 4 asubuhi kama ilivyokuwa imepangwa na badala yake kilianza saa 6 mchana, ajenda kuu zilikuwa ni kujadili namna ya kuachiana majimbo ambayo bado mwafaka haujapatikana pamoja na utaratibu wa kumpata mgombea urais kupitia Ukawa.
 

Chanzo cha kuaminika kutoka ndani ya kikao hicho kilichokuwa chini ya Mwenyekiti mwenza wa Ukawa, ambaye pia ni Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba, kilishindwa kutoa mwelekeo wa majimbo 18 yenye mvutano huku kila chama kikitaka kugombea kivyake.
 

Hata hivyo hoja hiyo iliibua mvutano mkali baina ya wajumbe wa kikao hicho ambapo kwa upande wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), ujumbe wake uliongozwa na Mwenyekiti Freeman Mbowe, Katibu Mkuu Dk. Willibrod Slaa na Mwanasheria Mkuu wa chama hicho Tundu Lissu.
 

Kwa upande wa CUF, ujumbe wake uliongozwa na Profesa Lipumba, Naibu Katibu Mkuu Bara, Magdalena Sakaya na Naibu Mkurugenzi wa Mipango na Uchaguzi, Shaweji Mketo.
 

NCCR-Mageuzi kiliongozwa na Mwenyekiti wake James Mbatia ambaye baada ya kuwasilishwa hoja ya chama chake alishindwa kuendelea na kikao na kulazimika kutoka nje ya ukumbi wa mikutano.
 

“Mwanzo tulianza kujadili suala la uandikishaji wapigakura kwa mfumo wa BVR na changamoto zake zilizojitokeza pamoja na hatima ya uwezekanao wa kuwapo kwa Uchaguzi Mkuu Oktoba, mwaka huu.
 

“Pia tulijadili kwa kina mwendelezo wa ugawaji wa majimbo yaliyobaki, lakini hata hivyo tuliacha ajenda hiyo kutokana na kuibuka kwa hoja nzito kwa kila upande,” kilisema chanzo chetu ambacho hakikutaka kuandikwa jina lake.
 

Taarifa kutoka ndani ya kikao hicho zinapasha kuwa ilipotimu saa 7 mchana, aliingia Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi, Mbatia, ambaye alishiriki katika hatua za awali za majadiliano hayo, lakini ilipofika saa 9:20 aliondoka kabla kuwasilishwa hoja ya chama chake kutaka kujitoa Ukawa.
 

Hata hivyo wajumbe walishindwa kuendelea na kikao hicho kutokana na NCCR-Mageuzi kutokuwa na mjumbe ambaye angeweza kueleza kwa undani sababu za kutaka kuchukua uamuzi wa kujitoa.
 

“Hoja iliyokuwa katika ajenda ni ya NCCR-Mageuzi waliyowasilisha ya kutaka kujitoa Ukawa na dai lao kuu ni kutotendewa haki kwa baadhi ya mambo, hasa katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa uliopita.
 

“Na hili jambo si geni kwani mnapokuwa kwenye jumuiya yoyote inawezekana ikatokea hali ya kutoelewana kwa baadhi ya wajumbe kwa kuona kuna sehemu kuna mmoja anaona hajatendewa haki.
 

“Na jambo ambalo lilitakiwa ni kuzungumza na kulimaliza ili watu wasonge mbele, na NCCR-Mageuzi walileta kama malalamiko… siwezi kulizungumzia vizuri kwa sababu halijazungumziwa kwa undani kwenye kikao,” kilisema chanzo chetu.
 

Mtoa habari wetu alisema kikao hicho kilitarajiwa kumalizika jana usiku, lakini kutokana na hoja ya NCCR-Mageuzi, ilimlazimu Mwenyekiti wa kikao hicho Profesa Lipumba kukiahirisha saa 11 jioni hadi leo ambapo kitaendelea.
 

Ukawa inaundwa na vyama vya Chadema, CUF, NCCR-Mageuzi na NLD kinachoongozwa na Dk. Emmanuel Makaidi.
 

Hivi sasa joto la kuwatangaza wagombea urais ndani ya vyama vinavyounda Ukawa pamoja na Chama Cha Mapinduzi (CCM) linazidi kupanda huku kila upande ukimvizia mwenzake katika kutangaza mgombea nafasi hiyo.
 

Hatua hiyo imekuja baada ya viongozi wa Ukawa katika mkutano wao na wanahabari kueleza kuwa mgombea wao atatangazwa Machi mwaka huu, lakini hadi sasa imepita miezi miwili bila kumtangaza.
 

Wakati hayo yakiendelea ndani ya Ukawa, CCM nayo hadi sasa imeshindwa kueleza ni lini atapatikana mgombea wake pamoja na kutangazwa kwa hatima ya makada sita wa chama hicho ambao wanadaiwa kuanza kampeni kabla ya wakati.

Credit: Mtanzania

Godbless Lema Amshambulia Zitto Kabwe......Amtuhumu Kuikosesha CHADEMA Ushindi Mwaka 2010

$
0
0

CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kimewatoa hofu wanachama wake mkoani Shinyanga kikidai propaganda zinazoenezwa na Kiongozi Mkuu wa Chama cha ACT-Wazalendo, Bw. Zitto Kabwe, anayedai chama hicho kimepoteza mwelekeo si za kweli bali ni uongo.

Mbunge wa Arusha Mjini ambaye pia ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya CHADEMA Taifa, Bw. Godbless Lema, aliyasema hayo hivi karibuni mkoani Shinyanga kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika katika Viwanja vya Mahakama ya Mwanzo.

Alisema chama chao bado kipo imara na hakitagawanyika kama inavyodaiwa na Bw. Kabwe ambaye CHADEMA kilimfukuza katika chama baada ya kukisaliti hivyo kukiuka Katiba ya chama hicho.

"Ndugu zangu wana Shinyanga, CHADEMA tupo imara na tutaendelea kuwa imara hadi tukamate dola na kuwakomboa Watanzania ambao wanateseka tangu tupate uhuru.

"Zitto hana ubavu wa kukigawa chama chetu kama anavyofikiri na kuamini...anahangaika bure, alitaka kukiua tukamshtukia na mimi ndiye mtu wa kwanza kubaini njama zake na wenzake akiwemo Samson Mwigamba na Profesa Kitila Mkumbo; hivyo hawatubabaishi kwa lolote," alisema.

Bw. Lema aliongeza kuwa, Bw. Kabwe alikuwa chanzo cha kufifisha ushindi wa CHADEMA katika baadhi ya majimbo katika Uchaguzi Mkuu wa 2010 baada ya kutoa taarifa za uongo kwa wasimamizi wa uchaguzi katika majimbo ya Katavi, Musoma Vijijini na Singida Mjini na kusababisha wagombea wa CCM wapite bila kupingwa.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa chama hicho Taifa (BAVICHA), Patrobass Katambi, aliwataka wanachama wa CHADEMA kusimama imara ili kukiimarisha chama chao na waachane na Bw. Kabwe aliyeonesha dhahiri usaliti wake baada ya kujiunga na Chama cha ACT-Wazalendo.

"Huyu Bw. Kabwe alikana katakata kujihusisha na Chama cha ACT-Tanzania kama kilivyofahamika awali; lakini siku chache baada ya kutimuliwa CHADEMA akajiunga nacho.

"Anawadanganya Watanzania kuwa yeye ni mjamaa na moja ya sababu iliyomtoa CHADEMA ni kutokuwepo demokrasia ya kweli...kama kweli anathamini demokrasia mbona baada ya kujiunga na ACT ghafla amejitangazia madaraka ya Kiongozi Mkuu wa chama," alihoji Katambi.

Katika hatua nyingine, CHADEMA kimetoa wito kwa wakazi wa Mkoa huo kujitokeza kwa wingi ili kujiandikisha kwenye Daftari la Kudumu la Wapigakura waweze kupata haki yao ya kuchagua viongozi waadilifu katika Uchaguzi Mkuu.


Baby Madaha: Natamani Zitto Kabwe Anioe, Pia Natamani Kujiunga na Freemason

$
0
0
NYOTA wa muziki na filamu Bongo, Baby Joseph  Madaha amesema kuwa anatamani kuolewa na Kiongozi Mkuu wa Chama cha ACT Wazalendo, Zitto Zuber Kabwe, akisema ni mwanaume mwenye sifa zote za kuwa mume kwa mwanamke anayejiamini.

Akizungumza katika mahojiano maalum na gazeti la Risasi wiki iliyopita jijini Dar es Salaam, Baby Madaha ambaye alizungumzia masuala mbalimbali ya sanaa na kijamii, alisema Zitto ni mwanasiasa anayejiamini anayejua kusimamia hoja zake, hivyo kumpata mtu wa namna hiyo, ni kitu anachokitamani kitokee. 
“Nafikiri Zitto ni mwanaume anayenivutia sana ambaye ningetamani anioe, licha ya kujiamini kwake, pia ana akili na ujasiri wa hali ya juu, kitu ambacho wengi hawana. 
  
"Ukiangalia mambo ambayo ameyafanya akiwa bungeni, yanaonyesha ni jinsi gani yeye ni mtu jasiri ambaye yupo tayari kufa kwa kupigania anachokiamini,”alisema Baby.

Kuonyesha kuwa anamfuatilia mwanasiasa huyo kijana, aliorodhesha mambo kadhaa yaliyosimamiwa na Zitto bungeni bila kuogopa, la mwisho kabisa likiwa ni sakata la upotevu wa fedha katika akaunti ya Tegeta Escrow, ambalo liliishia kwa wanasiasa kadhaa kupoteza nyadhifa zao, akiwemo aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo, aliyekuwa Waziri wa Nyumba, Ardhi na Maendeleo ya Makazi, Profesa Anna Tibaijuka, Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Fredrick Werema na Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Eliakim Maswi.

Licha ya kumpenda Zitto, Baby Madaha pia alisema anahusudu kujiunga na jamii ya Freemason, akisema anavutiwa na jinsi wanavyojitoa katika kusaidia watu wa jamii mbalimbali, tofauti na imani ya wengi kuwa watu hao ni wabaya.

Alitoa kauli hiyo kufuatia swali lililomuuliza imani yake kwa mambo ya kishirikina, tabia inayosemwa kufanywa na baadhi ya waigizaji na wanamuziki hapa nchini.

“Ukiniambia Freemason kweli, uchawi? Napenda Freemason maana iko wazi na kiongozi wake anajulikana, tofauti na imani za giza ambazo wahusika hawaonekani, achilia mbali kuwa wengi wao ni wachafu na wenye maisha ya shida.

“Muangalie mtu kama Chande (Alex, Kiongozi wa Freemason Tanzania) ni mtu mwenye maisha mazuri na yupo watu wanamuona, anaendesha taasisi kwa uwazi, haijalishi wako vipi, mimi ninawaelewa na ninawakubali,” alisema msanii huyo na alipoulizwa kuhusu usiri wa baadhi ya masharti ya kujiunga kama yana ishara mbaya, aliongeza;

“Siyo kila kitu mtu ajue, lazima yawepo baadhi ya mambo mnayojua wenyewe tu, angalia hata shoo ya Diamond, ameweka kiingilio kikubwa kwa sababu siyo kila mtu lazima aingie, wengine wa oyaoya waishie hukuhuku, huko kuna wenyewe, binafsi nitafurahi sana nikipata chansi, hao waliomo humo mbona hatuoni watoto wao wamekufa au wazazi wao?,”alisema kwa kuhoji Baby.

Ommy Dimpoz: Hakuna kitu ninachokipenda kama kurusha fedha, mikufu kwa mashabiki wangu nikiwa jukwaani

$
0
0
Kila msanii hua na mzuka wake awapo jukwaani, hasa mashabiki wakiwa nyomi na shangwe zikitawala. Kwa upande Omary “Ommy Dimpoz” Nyembo mzuka wake huwa ni kuwarushia zawadi mashabiki wake.

Muimbaji huyo wa ‘Wanjera’ amesema kuwa hupenda kuwarushia vitu vyake mashabiki awapo jukwaani, kama ishara ya upendo wake kwao kutokana na kusupport kazi zake.

“Hakuna kitu ninachokipenda kama kurusha vitu vyangu mashabiki wangu nikiwa jukwaani hii inaonyesha jinsi gani nawapenda, lakini pia inaongeza burudani kwao huku wakiendelea kupenda shoo yangu na muziki wangu kwa ujumla,’’ Dimpoz aliliambia gazeti la Mtanzania.

Aliongeza kwamba kufanya hivyo kunamuongezea mashabiki na ufuatiliaji wa muziki anaofanya na wengi wao humfuatilia ili kujua maisha yake kwa ujumla.

Source: Mtanzania

Jini Kabula Ataja Mchawi wa Soko la Filamu

$
0
0
Staa mrembo wa Bongo Movies,  Mariam Jolwa ‘Jini Kabula’ amesema kuwa anguko la soko la filamu za Bongo asitafutwe mchawi, kwani wasanii wengi wanaigiza chini ya kiwango na ndiyo maana kazi zao hazifanyi vizuri, licha ya kutumia gharama kubwa kuziandaa.                                      

Akizungumza na gazeti la Mtanzania, Dar es Salaam jana, Jini Kabula alisema kuwa ni filamu chache zinazofanya vizuri sokoni, ikiwemo ya Chozi la Wanjaa iliyochezwa na Aunt Ezekiel, Kulwa Kikumbi ‘Dude’ na wasanii wengine ambazo zinaonekana kuwafurahisha watu, isipokuwa nyingi zinatengenezwa kwa kulipuliwa.
Hakuna haja ya kumtafuta mchawi wa anguko la filamu nchini, kwani wengi wanatengeneza kwa kulipua, endapo waandaaji wasipobadilika, fani hii itakuwa haina maana tena kwa waigizaji,” alisema.

Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Kimefikia Tamati yake

$
0
0
Maoni Kutoka Kwa Mdau
Si kificho tena, bali ni uhalisia, Chama cha Demokrasia na Maendeleo, kimefikia tamati yake kabla hata ya uchaguzi mkuu wa oktoba kufikia.

Ni jambo ambalo wenyewe wanaweza lipinga lakini viashiria vyote vya chama hai havionekani kwa Chadema.

Hakuna uibuzi wa hoja zenye kuleta suluhisho la changamoto tulizonazo kama taifa, bali tunasikia tu mipasho kila kona ya nchi hii toka kwa viongozi wake.

Safu ya juu ya chama imekosa ubunifu na kubaki kulaumu kila mtu mpaka wale wasiohusika.

Si kificho tena bali ni uhalisia, Chadema imeishia njiani, kutokana na ulafi wa madaraka na ubinafsi.

Chadema kinapumulia mwavuli wa UKAWA na hoja ya katiba mpya , bila hiyo hawana la kutuambia watanzania.

By  Stroke/JF


Nimemtongoza Jana, Leo Anataka Nimtumie Hela

$
0
0
Kuna msichana niliwahi kuonana nae mara1 ni rafiki wa dadaangu, tulionana nilipoenda kumtembelea sista nikahisi kumpenda, jumapili kulikuwa na event ya kifamilia nikaonana naye, safari hii nikawa siriaz kumbana nimsomeshe hadi kieleweke.

Bahati nzuri tulipotoka kwenye event tulisafiri pamoja nikakaa naye kwenye siti zinazofatana, nilimtongoza though hakunipa jibu la moja kwa moja kunikubalia but alikuwa anaonyesha kuelekea kukubali, nilimwomba namba yake akanipa. Kesho yake ambayo ni jana akanichokoza kupitia msg, akanisalimia nami nikarespond.

Si nikahisi mtoto kashakolea, ile nataka nianze kumchokoza anipe jibu langu mara akatuma meseji 'Nasikia njaa', duh ile kuendelea kuchat nikagundua anamaanisha nimtumie hela. Eti ndugu wananchi, huyu ni wife material kweli au najiingiza kwenye majanga? Maana mtu mwenyewe hela za kuokoteza.

Kumbe mimba ya Lotus Kyamba wa Nirvana.....Kapewa na Roma Mkatoliki?

$
0
0
LOTUS KYAMBA kathibitisha kupitia kipindi chake cha Nirvana kwamba mimba aliyonayo msababishaji ni mwanahiphop Roma Mkatoliki na anampenda sana. Big up Roma kwa kutarajia kuongeza kiumbe kingine, but vipi kuhusu yule bibie uliyekuwa unamrusha sana fb umempiga chini au?

Shamsa Ford:Mnikome Kuanzia Leo Naishi Nitakavyo Mimi na Kufanya Kile Ambacho Nahic Kinafaida Kwangu

$
0
0
Ustaa kazi: Baada ya kuchoshwa na maneno ya watu kuhusu maisha yake binafsi, staa mrembo wa Bongo Movies, Shamsa Ford ameamua kuweka wazi msimamo wake kwa mashabiki zake wote.

Siku zote nimekuwa muoga kuishi maisha yangu kwa kuogopa watu but hao watu naowaogopa hata siku moja hawajawahi kuogopa kuishi maisha yao kwa kuniogopa mm..from today nitaishi nitakavyo mimi na kufanya kile ambacho nahic kinafaida na kunifurahisha katika maisha yangu.Mashabiki wangu wa ukweli kabisaa alionipangia Mungu hata niweje hawawezi Kunitoka na nitaendelea kuwapenda na kuwaheshimu kila siku..I love my family….” –Shamsa ameandika hayo leo kwenye ukurasa wake mtandaoni.

Mimba ya Zari, Familia ya Diamond Wadai Wanashaka na Ujauzito Huo, Kauli ya Penny na Mume wa Zari Ndio Chanzo

$
0
0
SHAKA! Familia ya ‘President’ wa Kruu ya Wasafi, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ imeamua kuweka kikao kummbana staa huyo aweke wazi kama ni kweli ana uhakika mimba aliyonayo mjasiriamali Zarinah Hassan ‘Zari’ ni ya kwake au magumashi, Risasi Mchanganyiko linakupa mchapo kamili.

TUJIUNGE NA CHANZO

Kwa mujibu wa chanzo kilicho karibu na familia ya staa huyo, ndugu wa karibu akiwemo mama, binamu yake Romy Jons, wajomba zake, mameneja na marafiki wa karibu wa familia, waliamua kuweka kikao hicho usiku  hivi karibuni ili Diamond athibitishe kama kweli kiumbe kinachoripotiwa kuwa ni cha kwake magazetini ni chake kweli.
“Ndugu walichachamaa, walitaka kujua kama kweli mimba inamhusu Diamond au ni magumashi ya kiki za vyombo vya habari.

“Kwenye hicho kikao walimualika na Diamond mwenyewe ili aweze kufunguka kama ana uhakika kweli mimba ni yake,” kilisema chanzo hicho

 WALITAKA ATOE MSIMAMO

“Mbali na kutaka kujua kama mimba ni yake, walitaka pia kujua ana msimamo gani na Zari maana kila kukicha wanasikia mambo tofauti katika mitandao na vyombo vya habari,’’ kilisema chanzo hicho.

SABABU ZAZIDI KUANIKWA

Chanzo hicho kilipobanwa na mwanahabari wetu kuhusiana na sababu zilizowafanya ndugu wa Diamond watilie shaka mimba hiyo, kilisema ni kauli ambazo ziliwahi kusemwa na aliyekuwa mpenzi wake Penniel Mungilwa ‘Penny’ na aliyekuwa mume wa Zari, Ivan Semwanga.

“Walishitushwa na kauli ambayo aliwahi kuitoa Penny kwamba Diamond hana uwezo wa kumpa mwanamke mimba lakini kama hiyo haitoshi, waliitafakari kauli ya mume wa Zari ambaye alidai Zari hawezi kumzalia Diamond ndiyo maana wakataka wapate uhakika,” kilisema chanzo hicho.

 MUAFAKA WA KIKAO

Chanzo hicho kikizidi kumwaga ubuyu mbele ya kinasa sauti cha Risasi Mchanganyiko kwamba, baada ya Diamond kubanwa na nduguze, alithibitisha kuwa Zari ndiyo kila kitu kwake kwa sasa, hivyo wasiwe na shaka yoyote juu ya kiumbe kinachotarajiwa kuzaliwa.

“Diamond aliwahakikishia kwamba mzigo ni wake, na msimamo wake ni kufika katika hatua ya ndoa Mungu akijalia.

 KUMVISHA PETE

“Kuonesha yupo serious baada ya Diamond kuwatoa hofu ndugu zake, alisema atafanya sapraiz siku ya Mei Mosi katika shoo ya mrembo huyo, All White Party itakayofanyika kwenye Ukumbi wa Mlimani City jijini Dar,” kilisema chanzo hicho na kudokeza kuwa Diamond atamvisha pete mrembo huyo.

DIAMOND AFUNGUKA

Ili kuweza kupata ukweli, mwanahabari wetu alimtafuta Diamond ili aweze kuweka wazi juu ya kikao hicho na kama ni kweli anatarajia kumvisha pete Zari. Diamond alifunguka:

“Yeah ni kweli ndugu zangu walikuwa na shaka lakini nimewahakikishia kwamba kiumbe kilichomo tumboni mwa Zari ni mali yangu, kuhusu kumvisha pete ni mapema kidogo kulizungumzia lakini watu wahudhurie kwa wingi katika shoo ya Zari White Party Ijumaa hii pale Mlimani City kwani nimeandaa sapraizi nyingi sana.

“Mei Mosi itakuwa ni siku ya kihistoria sana kwake kwani kuna mambo muhimu mengi natarajia kumfanyia mpenzi wangu Zari, watu watajua rasmi nia yangu kwa Zari maana ni mwanamke ambaye ameamua kujitoa kwa ajili yangu, hivyo sina budi kumuonesha upendo stahiki, nitafanya kila linalowezekana kumuonyesha namna gani nampenda.”

 SHOO YA KIHISTORIA

Kwenye shoo hiyo ya Zari, watu mbalimbali mashuhuri wanatarajiwa kuhudhuria akiwemo dairekta mkubwa Afrika, Godfather wa Afrika Kusini na Top Ten ya Washiriki wa Shindano la Big Brother ‘Hot Shot’ 2014.
GPL

Picha ya Ommy Dimpoz iliyozua Gumzo Mitandaoni Siku ya Leo..Embu iangalie kwa Makini alafu Uniambie ina Shida Gani

$
0
0
Picha ya Ommy Dimpoz iliyozua Gumzo Mitandaoni Siku ya Leo..Kama macho yako ni Mazima Embu iangalie Picha hiyo hapo juu kwa Makini alafu Uniambie ina Shida Gani

Mwanafunzi auawa baada ya kukutwa na barua ya mapenzi

$
0
0
MWANAFUNZI wa Kidato cha Pili, Jofrey Robert Mwakatenya (15) Ameuawa kikatili na baba yake mzazi, Robert Mwakatenya (35) baada ya kumkuta akiwa na barua ya mapenzi, inayodaiwa aliandikiwa na rafiki wake wa kike.

Mzazi huyo ambaye ni mfanyabiashara na mkazi wa eneo la Majengo ‘D’ Manispaa ya Sumbawanga, anadaiwa kumwadhibu mwanafunzi huyo, ambaye ni mtoto wake wa kwanza kwa kupiga ngumi na mateke mfululizo kwa zaidi ya saa tatu.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Rukwa , Jacob Mwaruanda alithibitisha tukio hilo, lilitokea usiku wa kuamkia Jumapili iliyopita. Alisema bado wanamtafuta mtuhumiwa huyo kwani baada ya kufanya kitendo hicho alitokomea.

Akizungumza na mwandishi wa habari hizi, Mwenyekiti wa Serikali Majengo D, Antony Nyambo alidai kuwa mzazi huyo alikuwa na tabia ya kumwadhibu mwanawe huyo, akimtuhumu kuwa ni mtoro wa shule .

“Nilitaarifiwa juu ya kisa hiki Jumapili saa mbili asubuhi baada ya kutoka katika ibada na raia mwema, ndipo niliamua kufika nyumbani kwa marehemu, nilimkuta akiwa amelazwa chumbani, nilipomfunua niliona akiwa ametapakaa vumbi mwili mzima huku akiwa amevaa nguo ya ndani tu,” alidai mwenyekiti huyo wa mtaa.

Inadaiwa kuwa usiku huo wa tukio, mtuhumiwa alianza kumwadhibu kumpiga ngumi na mateke kuanzia saa mbili usiku hadi usiku wa manane.

Mtoto huyo baada ya kupata kipigo hicho, alizimia ambapo baba yake alimwagia maji mwilini hadi akazinduka, kisha akamwamuru alale chumbani humo pamoja na mdogo wake.

Mzazi wa mtoto huyo alidamka alfajiri na kwenda kwenye chumba walicholala watoto hao na kugundua kuwa Jofrey alikuwa mfu.

“Ndipo baba huyo alipoaga nyumbani hapo, akidai kuwa anaenda kutafuta gari ili Jofrey aweze kupelekwa hospitalini kwa matibabu. Mzazi huyo hakurudi tena nyumbani kwake hadi sasa,” alibainisha.

Kajala Awapoza Walioshindwa, Shindano la EFM

$
0
0
Staa wa Bongo Movies, Kajala Masanja hivi majuzi aliwapoza washiriki walioshindwa kwenye shindano la Shika Ndinga  lililoandaliwa na Kituo cha Redio cha EFM cha jijini Dar es Salaam.

Ambapo mkazi wa Ilala, Stela Robert (26) na Gabriel Geoffrey (36) wa Temeke wameibuka washindi wa gari na kukabidhiwa funguo za magari yao katika viwanja vya Tanganyika Pekas Kawe  ambapo lilifanyikia shindano hilo.

Kwa mujibu wa ofisa Uhusiano wa EFM, Lydia Moyo alisema shindano hilo lilikuwa na raundi nne ambapo washiriki walitakiwa washike kitu huku wakiwa wamesimama kwa miguu miwili, kisha wasimame kwa mguu mmoja na mwingine ukiwa umekunjwa kwa nyuma.

Alisema washiriki waliovumilia maumivu katika mizunguko hiyo minne walikuwa wawili ambao ndiyo walioibuka washindi ambapo mmoja kwa upande wa wanaume na mwingine kwa wanawake.

Kutokana na ugumu na shangamoto za shindano hilo akiwa ni moja kati ya waalikwa wa kwenye shindano hilo, Kajala Masanja ‘Kajala’ aliwapoza washiriki wote walioshindwa kushinda gari kwa kuwapa pole yake ya Sh 10,000 kila mmoja.

Barua Nzito: Wastara Omba Radhi‭, ‬Badilika‭!‬

$
0
0
KWAKO mwanamke unayejua kuuvaa vyema uhusika katika sinema za Kibongo, Wastara Juma. Za siku nyingi? Uko poa mama!?

Ukitaka kujua afya yangu mimi ni mzima wa afya, naendelea na mishemishe zangu za kila siku kuhakikisha mkono unakwenda kinywani. Nimekukumbuka hapa leo maana ni kitambo kidogo hatujaonana. Nikaona ni vizuri kukuandikia barua.

Dhumuni la barua hii ni kwanza kutaka kukukumbusha juu ya heshima niliyokuwa nakupa. Nilikuwa nakuheshimu kama mama wa watoto wawili, mtu mzima mwenye busara za kutosha.

Kwa levo ya heshima niliyokuwa nakupa, sikuwahi kuwa na shaka kwamba labda kuna siku unaweza ukabadilika. Niliamini kadiri siku zilivyozidi kusonga ndivyo busara zaidi zingeendelea kujaa katika kichwa chako.

Nilikuheshimu kama mama jasiri sana. Historia ya maisha yako inaonesha umepitia mitihani mingi, kwa namna ambavyo umepambana na kuvuka viunzi hivyo, hakuna ambaye anaweza kuwa na shaka na wewe zaidi ya kukupongeza na kukuona ni mfano wa kuigwa.

Ulipambana sana kutetea uhai wa mumeo hadi pale Mungu alipomchukua. Nikwambie Watanzania walikupa heshima ya juu. Mimi mwenyewe nilikuheshimu sana. Sikuwahi kutarajia kama siku moja unaweza kushusha heshima yako kirahisi kama wafanyavyo baadhi ya wasanii.

Sikuwahi kuwaza kama kuna siku ninaweza kukuona umevaa mavazi ya ajabu kama wafanyavyo baadhi ya wenzako, achilia mbali ulevi wa kupindukia.

Niliamini wewe ndiye mtu wa kukemea wenzako wanaotoka nje ya mstari wa kujiheshimu.

Licha  ya kukuheshimu huko kwa muda mrefu, juzikati ulifanya tukio ambalo nilipoliona, akili yangu ilishindwa kuamini kama ni wewe yule ninayekuheshimu. Nazungumzia matusi mazito uliyoyaporomosha kwenye mtandao wa Instagram.

Ulimtukana mmoja wa mashabiki wako matusi mazito ya nguoni. Najua kabisa kwamba alikuudhi na kama binadamu unakasirika, lakini siku zote kabla ya kufanya jambo lolote lazima kwanza uangalie nafasi yako katika jamii.

Huwezi kumuona chizi anakutukana eti na wewe ukamtukana ili kumkomoa. Mwenye busara na hekima, akitukanwa na chizi, hukaa kimya na mwisho wa siku watu hubaini nani ni chizi!

Kwa matusi uliyomlipizia yule shabiki wako, waungwana walikujadili wewe uliyejibu badala ya shabiki wako.

Walikuona hukutumia busara. Kwa nafasi yako katika jamii, ukisema umjibu kila atakayekutukana, utawatukana wangapi? Jamii nayo itakuelewaje?

Nikuambie tu dada yangu hukufanya kitu kizuri hata kidogo, wewe ni staa mwenye heshima kubwa, huwezi kutukana matusi mazito kiasi kile hadharani, tena kwenye akaunti yako ambayo unaitumia kufanya biashara mbalimbali.

Binafsi tangu siku ile niliposoma posti yako nilijisikia vibaya, sikutegemea. Ningekushauri, ili kurejesha heshima yako, omba radhi na kubadilika. Kwa leo ni hayo tu.

Wasalaam

By GPL
Viewing all 104756 articles
Browse latest View live




Latest Images