Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104423 articles
Browse latest View live

Huddah Monroe Apagawishwa na Mtoto wa Mahita Mpaka Ashindwa Kuhudhuria Party ya Zari All White Party

0
0
Kama unakumbuka mmoja wa Wageni wa Party ya Zari all White Party pale mlimani City alikuwa pia Mrembo Huddah Monroe , Lakini Pamoja na Kuweka picha kwenye Instagram Akiwa Ameshatua Bongo kwa Party hiyo akiwa hotelini pale Hyatt zamani Kempinski Mrembo huyo hakuweza hudhuria hiyo Party ..

Sasa ubuyu uliopo mtaani ni kuwa sababu za yeye kushindwa kuhudhuria party hiyo ni mtoto wa Mahita  a.ka Tajiri mutoto, inasemekana walikutana pale Hotelini na kuanza kupagawishana na kusahau kila kitu ..Mwendelezo wa hao wawili ulihamia kwenye visiwa vya Zanzibar kama Picha zinavyoonyesha hapa chini kwenye picha ambapo kila mmoja alikuwa akipost picha wakiwa kwenye Boti..ukiangalia kwa makini hilo ni Boti Moja Japo Hawakupiga Picha ya Pamoja...




Pamoja Na Kumaliza Mgomo, Makonda Jana Alinusurika Kupigwa Mawe Na Madereva Ubungo

0
0
MKUU wa Wilaya ya Kinondoni, Paul Makonda na maofisa wa Jeshi la Polisi jana walijikuta katika wakati mgumu baada ya kunusurika kupigwa mawe na vijana waliokuwa wamejazana katika Kituo Kikuu cha Mabasi Ubungo jijini Dar es Salaam.

Makonda na maofisa hao, walifika eneo hilo kwa nia ya kuwaomba madereva wa mabasi yaendayo mikoani kusitisha mgomo waliouanza juzi.

Maofisa wa polisi walionusurika kupigwa mawe ni Kamanda wa Polisi Kikosi cha Usalama Barabarani, Mohammed Mpinga na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, Camilius Wambura.

Tukio hilo lilitokea kituoni hapo saa 4:00 asubuhi, wakati Makonda alipokwenda kuzungumza na viongozi wa Chama cha Madereva kuhusu namna ya kumaliza mgomo uliodumu tangu juzi.

Makonda alipofika kituoni hapo, alikwenda moja kwa moja kufanya mazungumzo na uongozi wa madereva, huku akilindwa na askari polisi na wengine waliovaa kiraia.

Wakati mazungumzo yanaendelea, askari wengine walifika katika eneo hilo wakiwa na mbwa kwa ajili ya kuimarisha ulinzi.

Askari walianza kutumia mbwa kuwatishia madereva pamoja na umati mkubwa wa watu uliotaka kusikiliza kilichokuwa kikizungumzwa na baadaye mbwa alimrukia kijana mmoja na kumjeruhi mkono wa kulia.

Tukio hilo liliamsha hasira kwa baadhi ya madereva ambapo walianza kuzomea na kurusha mawe mfululizo katika eneo ambalo Makonda alisimama pamoja na maofisa wa polisi.

Hali hiyo iliwafanya viongozi wa polisi, wakiwamo Kamanda Mpinga, Wambura na wengine kujikusanya na kumkinga Makonda kwa kutumia mikono.

Kisha walifanikiwa kumweka chini Makonda ili mawe yaliyokuwa yakirushwa ovyo yasimfikie.

Watu wengine wakiwamo waandishi wa habari, walilazimika kukimbilia maeneo mengine ili kujinusuru na adha hiyo.

Vurugu hizo ziliwalazimu askari wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU) kufyatua mabomu ya machozi na risasi za moto hewani ili kutawanya kundi kubwa la vijana.

“Hapa tumekuja kutafuta suluhu, wao wanatuletea mbwa na mabomu yao ya nini? Waandishi wa habari mnajionea wenyewe polisi ndio wanaoanzisha vurugu, si madereva,” alilalamika mmoja wa madereva hao.

Baada ya dakika kadhaa, Makonda aliendelea na mazungumzo na viongozi wa madereva hao.Makonda alisema anaunga mkono mgomo huo kwa sababu ni haki ya raia kudai haki yao.

“Mimi naunga mkono mgomo huu, kwa sababu ni haki ya kila raia na huu ndiyo msingi wa kupata haki yako kwa mtendaji asiyefanya kazi yake sawa sawa.

“Njia hii inasaidia kuwakumbusha viongozi kufikiri zaidi kwa niaba ya wale wanaowatumikia ili kutatua matatizo yaliyopo,” alisema Makonda huku akishangiliwa.

Baada ya Makonda kuzungumza hayo, Katibu wa madereva hao, Rashid Salehe, alisema lengo lao ni kutaka makubaliano yao na Serikali yawekwe kwenye maandishi.

“Si lengo letu kugoma kila mara, tunataka makubaliano tunayofikia yawekwe kwenye maandishi si kama vile alivyofanya Kabaka (Waziri wa Kazi na Ajira) ili tukiona hayajatekelezwa tudai kwenda mahakamani,” alisema Salehe.

Baada ya kauli hiyo, Makonda alikubaliana na sharti hilo, hivyo alikwenda hadi katika ofisi za madereva hao kituoni hapo ili kuyaweka makubaliano hayo kwenye maandishi.

Katika Maongezi yake na madereva hao, Makonda alisema: “Tumeambiwa kwamba kuna tume imeundwa na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, haiwezekani tume ikaundwa hewani, lazima tujue mambo matatu kuhusu tume hiyo.

“Lazima tuwajue viongozi waliomo ndani ya tume hii, muda ambao watafanya kazi yao na hadidu za rejea ambazo watazitumia.

“Lakini wanasema mnyonge mnyongeni haki yake mpeni. Ingawaje mnadai haki yenu nawasihi leo wapelekeni abiria hawa makwao, halafu kesho saa 4 nitaongozana na viongozi wenu kwenda kwa Waziri Mkuu tukajue mambo haya matatu kuhusu tume hiyo.”

Alisema iwapo watayaona majina ya wajumbe wa tume hiyo na kukosa imani nao, ataomba waongeze viongozi wawili wa madereva ambao wanawaamini.

“Iwapo leo hatutapata jibu katika madai yenu, nawaahidi nitakuja hapa na kuendelea na mgomo pamoja nanyi kwa muda wa siku saba hadi tupate mwafaka,” alisema.

Uso Kwa Uso na Mke Wa Rafiki yangu Gesti

0
0
Wakuu weekend iliyopita nilimuaga mke wangu kuwa Nina semina nje ya dar kikazi maana hiyo ndo huwa mbinu yangu ya kwenda kwenye dhambi zangu kwa siku tatu NNE
Nilikua nime import mchepuko wangu kutoka arusha so nika check in kwenye hotel moja bagamoyo tukajipumzisha hapo alhamisi,Ijumaa, Jumamosi jumapili asubuhi tuka check out

Wakati nafunga mlango wa room nashtuka kumuona mke Wa Rafiki yangu akitoka Chumba mkabala na changu akiongozana na zee moja hivi nao wakifunga Chumba chao shemeji alitetemeka na kupata mshtuko mkubwa hadi yule Mzee kumuuliza kuna nini

Mchepuko wangu ulishatangulia kwenye gari nikamsalimia shemeji nikamwambia mm ndo na check out nilikua semina ya siku tatu ndo imeisha, akaitikia kwa kichwa tu,
Nikapiga hatua za haraka kwenda kwenye Gari ili asiuone mchepuko wangu ambao ulishatangulia kwenye gari

Jumatatu akanipigia simu mwenyewe akaniambia shemeji naomba unifichie siri sitarudia tena
Nikamwambia naomba tuongee baadae kwa sasa nipo busy

Mchana wake akanitumia meseji inasomeka hivi "" Shem naomba kama vipi tafuta sehemu nije tumalizane kiutu uzima and you stay silence forever "" naomba unijibu i can't afford to loose this marriage

Wakuu nipo njia panda, ingawa mm ni mzinzi na sina utakatifu lakini siwezi kutembea na mke Wa Rafiki yangu kipenzi tulieshibana miaka nenda miaka Rudi
Na nilishawahi kukaa kwake sana wakati sijapata kazi yy alianza kuja dar kabla yangu

Kwa sasa huyu jamaa yupo mkoani kikazi alihamishiwa huko mke alishindwa kumfuata kwa yy mwenyewe ana kazi hapa dar .

Jana kanitumia M-PESA laki tano ikisindikizwa na msg kuwa vipi shemeji lile suala letu umeamuaje ukimya wako unaniumiza.
Sikujibu kitu

Wakuu naomba muongozo wenu
Kweli nisimwambie Rafiki yangu kuhusu uzinzi Wa mkewe?

Na mm ndo nimepewa jukumu la kumuangalizia familia yake kwa mambo mbali mbali kwa kuwa yupo mbali

Nawasikiliza wakuu

By Montana

Barua Nzito Wema Kuna Kitu cha Kujifunza kwa‭ ‬Zari‭!

0
0
KWAKO mtoto mzuri, Beutiful Onyinye, Wema Sepetu !'Madam'. Vipi uko poa? Ukitaka kujua afya yangu, mimi ni mzima namshukuru Mungu, hofu na mashaka ni kwako wewe uliye mbali na upeo wa maisha yangu.

Kitambo kidogo hatujaonana, nimeona si mbaya kama nitakukumbuka kwa barua maana najua kutokana na majukumu yako na yangu kuwa mengi, wakati mwingine tunaweza tukafikisha hata miezi sita hatujaonana.

Dhumuni la barua hii ni kutaka kukushauri kwamba unaweza kujifunza kitu kutoka kwa mpenzi wa sasa wa aliyekuwa mpenzi wako, Nasibu Abdul !'Diamond, Zarinah Hassan !'Zari!

Naomba usinielewe vibaya. Sina nia ya kukupambanisha wala kutaka kukukejeli kwa namna yoyote. Kuna kitu kidogo tu cha kujifunza kutoka kwa binti huyo wa Kiganda.
Achana na maneno yanayosemwa mtaani, kila mmoja ana upungufu wake lakini binadamu tunashauriwa kuiga yale mazuri kutoka kwa wenzetu.

Iko hivi Wema, wewe na yeye mna nafasi moja nzuri katika jamii. Nyinyi ni maarufu. Mnapendwa na watu kupita maelezo. Mna ushawishi mkubwa sana katika jamii hivyo mnaweza kufanya jambo na likapata mafanikio makubwa sana.

Umaarufu wenu ni biashara. Kwa nini uendelee kubaki chini wakati umezungukwa na fursa kibao? Umaarufu wako ni biashara kama utaamua kuwa !٪serious!& na kila hatua unayoipiga.
Nikwambie ukweli bila unafiki, unapaswa kuiga jambo moja tu la msingi kutoka kwa Zari, kuwekeza na kuheshimu fedha.

Mwenzako anaijua fedha. Anajua namna ya kuitafuta na namna ya kuiwekeza katika maeneo ambayo yatazidi kuzizalisha. Akili yake inawaza pesa na si starehe zisizokuwa na msingi.
Mfano mdogo tu ni !٪idea!& kama ya All White Party aliyofanya Zari kule Uganda. Alifanikiwa, anaendelea kufanya na wiki iliyopita aliifanya pale Mlimani City jijini Dar na kupata mafanikio makubwa.

Kwangu mimi kile ni kitu kikubwa sana ambacho kinaingiza fedha nyingi kwa wakati mmoja. Si vibaya kama utaiga vitu vya namna hiyo. Nisikufiche, nafasi ya umaarufu uliyonayo Kibongobongo, unaweza kufanya zaidi ya shoo ile kama utaamua na kupata watu wazuri wa kufanya nao kazi.

Na unapofanya mambo makubwa kama hayo, lazima pia udhibiti matumizi yako. Starehe zipo lakini wakati mwingine unapaswa kuheshimu fedha. Yale mambo ya kwenda kuzimwaga ukumbini eti kuwa kama kina pedeshee !٪nanilii!&, si mazuri.

Jeuri ya fedha ifanye kwa kufungua miradi mikubwa ambayo hata utakapozeeka utainjoi matunda yake. Kuigiza kuna mwisho, huwezi kuwa mwigizaji milele, kuna wakati utatakiwa kuwa msimamizi wa miradi yako tu binafsi na mkono uende kinywani kiulani tu.

Usikubali kushikiwa akili na wapambe, unayoshauriwa na wapambe yachuje maana si yote yanakuwa na manufaa. Tumia kipaji na jina lako vizuri, una nyota ya kupendwa basi kupendwa huko kuwe na faida.
Natambua una idea zako ambazo tayari umeanzisha kama kipindi chako cha In My Shoes, usiishie hapo fanya makubwa zaidi.
Kwa leo acha niishie hapo. Ni matumaini umenielewa.
Wasalaam

BY: Eric Evarist/ GPL

Ray na Davina Kidogo Wazichape Ukumbini!

0
0
Mastaa wa Bongo Movies, Vincent Kigosi ‘Ray’ na Halima Yahaya ‘Davina’ nusura wazichape kavukavu katika Ukumbi wa Mlimani City, jijini Dar baada ya Ray kudaiwa kumshika mwenzake huyo sehemu nyeti, Risasi Mchanganyiko lina mchapo kamili.

Kwa mujibu wa chanzo makini cha gazeti la Risasi, ambacho kilikuwa shuhuda wa tukio hilo, Davina alikuwa amekaa na wasanii wengine pamoja na Mlezi wa Bongo Movies, mama Loraa wakipata vinywaji ndipo Ray alipofika na kuharibu shughuli.


“Wakati Davina anaendelea kupata kinywaji na mama Loraa, alitokea Ray akiwa tayari ‘ameshakula vyombo’ na kumshika Davina kalio kitendo kilishomkasirisha sana msanii huyo na kuanza kumcharukia Ray,” kilisema chanzo hicho na kuongeza:

“Davina alinyanyua glasi ya kinywaji chake, akammwagia Ray huku akimuuliza kwa nini alimshika makalio ndipo Ray naye alipopandisha hadi wakataka kukunjana.”
Baada ya vurugu hizo kuanza kushika kasi, alitokea mwigizaji Steven Mengere ‘Steve Nyerere’ na wenzake ambao waliwasihi wawili hao waachane na mambo hayo.


Baada  ya kupata habari hiyo, gazeti hilo liliwatafuta wahusika ambapo lilianza na Davina.
“Jamani mi nafikiri nisizungumzie hilo tukio maana naona ni la aibu, si kitendo kizuri na kinaniumiza mno kwa maana ni udhalilishaji mno na kwa nini mtu akufanyie hivyo?,” alisema Davina. Simu ya Ray iliita bila kupokelewa.

Nilipofukuzwa CHADEMA nilitamani kujiunga na Chama cha NCCR Mageuzi

0
0
Kiongozi wa Chama cha ACT Wazalendo Zitto Kabwe amefunguka na kusema kuwa alipofukuzwa wanachama katika chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) alitamani kujiunga na Chama Cha NCCR-Mageuzi kwani ndicho chama ambacho kilikuwa kinaendana na itikadi yake anayoifuata na kuiamini ambayo ni itikadi ya Ujamaa. Zitto Kabwe amefunguka haya leo alipokuwa akichat Live kupitia ukurasa wa facebook wa EATV katika kipengele cha KIKAANGONI ambacho kimeanza upya katika msimu wa pili na kitakuwa kikifanyika kila Jumatano kuanzia saa nane mchana mpaka kumi Alasiri.
Zitto Kabwe alisema kuwa alishindwa kujiunga na Chama hicho cha NCCR-Mageuzi kutokana na kuwepo kwa matatizo hivyo aliona siyo vyema kujiunga nacho, ndiyo maana alifikiri kuwa na chama cha siasa ambacho kitakuwa na misingi na itikadi ambayo yeye anaiamini na kuisimamia.

Ubuyu:Wema Sepetu, Aunt Ezekiel Kimenuka Kisa Zari, Kisa White Party ya Zari

0
0
Gazeti la Risasi la leo limeripoti kuwa Mataa wa bongo movies ambao ni  mashosti wa kufa na kuzikana, Wema Isaac Sepetu na Aunt Ezekiel Grayson wanadaiwa kugombana baada ya Aunt ‘kuposti’ kwenye ukurasa wake wa Instagram tangazo lililohusiana na pati ya mwandani wa mwanamuziki Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’, Zarinah Hassan ‘Zari The Boss Lady’ iliyofanyika Mlimani City jijini Dar wikiendi iliyopita.

Kwa mujibu wa mtu wa karibu wa mastaa hao wa sinema za Kibongo, baada ya Aunt kuposti tangazo hilo akiwalaumu watu wa mtandao wa huduma za simu waliomtumia ndipo Wema akaona na kuja juu.
Ilielezwa kwamba baada ya Aunt kutupia picha ya tangazo hilo, Wema alichukizwa na kitendo hicho huku akimuona Aunt kuwa amemsaliti.

Ilisemekana kwamba katika utetezi wake, Aunt hakupendezwa na tangazo hilo alilotumiwa na mtandao huo wa simu.
“Wema alivyoona alichukia na kusema Aunt alikuwa akimsaliti na alitumia tangazo lile kijanja kwa ajili ya kuwatangazia watu kuhusu pati ya Zari wakati anajua kabisa kuwa Wema hazipandi na Zari kwa sababu anatoka na aliyekuwa mchumba’ke (Diamond),” kilisema chanzo hicho.

Katika sakata hilo, kuna watu ambao waliona Aunt hakuwa na kosa lakini wapo walioona hakuwa sahihi, jambo ambalo lilichochea ugomvi wao huku wakidaiwa kukesha wakitukanana.

Gazeti hilo lilipozungumza na Aunt kuhusiana na sakata hilo, alikiri kutokea akisema kuwa hakuwa na maana mbaya kuposti tangazo hilo lakini kila mtu ana mtazamo wake.

“Mimi sikumaanisha chochote kibaya kuhusu hilo tangazo na wala sikujua kama kuna mtu anaweza akalichukulia tofauti kabisa na hapo na mimi ndiyo nashindwa cha kuzungumza,” alisema Aunt.
Alipopigiwa Wema simu yake iliita bila kupokelewa.

Mjue Body Guard wa Mwanamuziki Diamond -Kumbe ni Komandoo wa Kuogopwa Hasa

0
0
Bodigadi wa Diamond Mwarabu Seleman Mirundi akifanya mazoezi ya kikomandoo kwenye msitu wa chuo kikuu kuhofia watu wasione mazoezi yake.

Juu picha za wanajeshi wa Irani ambao pia ni makomandoo ambao awefanyanao mazoezi.
Hapa akiwajibika kumlinda boss wake nchini Burundi.

Mwarabu Seleman Mirundi akiwa nchini Iran hivi karibuni alipokwenda kwa mara ya kwanza kushiriki michezo ya mapigano ya hatari ambayo hufanywa na wanajeshi hasa walifuvu ukomandoo. Mwarabu Seleman Mirundi akiwa nyuma ya bendera ya Tanzania tayari kupambana na Komandoo wa Iran ambae hata hivyo alimchakaza vibaya na kuokolewa raundi ya kwanza
Hiki ni cheti alichotunukiwa nchini Iraq baada ya kumsambaratisha Komandoo wa nchi hiyo ambae hakumtaja jina. Hiki pia cheti alichotunukiwa na nchini Mozambique baada ya kuwatandika wanajeshi kadhaa nchini humomaskanibongotz Mwarabu akifanya mazoezi mepesi na mmoja wa maofisa usalama wa nchini Tanzania .

Jamaa huyu hakuwa anafahamika sana hata kwenye matamasha mbalimbali ulikuwa huwezi kumkuta lakini baada ya kupata kazi ya kumlinda staa wa Bongo Flava nchini Naseeb Abdul Diamond alianza kujulikana zaidi huku watu wakimchukulia kama mtu wa kawaida sana kama mabaunsa wengine.

Jina lake halisi anaitwa Mwarabu Suleiman Mirundi huyu baada ya kupata taarifa za kuwa huyu jamaa si mtu wa kawaida kwenye jamii ilifanyajitihada za kumtafuta huku kupatikana kwake huwa ni kwa nadra sana huwezi kumkuta mitaani kama tuwaonavyo mabaunsa wengine wanazurura mitaani. baada ya kutonywa sehemu anapoweza kupatikana kijana huyo ambapo ni msitu wa chuo kikuu ndiko anakofanyia mazoezi mara nyingi akiwa na mwanamuziki na bondia Zora D ndipo nilipofunga safari hadi huko na kumkuta kijana huyo akifanya mazoezi ya hatari kuyaona. Mwarabu alianza kuelezea ingawa hakupenda watu wajue kama yeye ni mtu wa aina hiyo lakini alianza kufunguka kama ifuatavyo " Dada mimi ni Komandoo lakini sio wa JWTZ hapana nimefuvu mazoezi haya ya mapigano nchini Iran toka mwaka 2010 baada ya kwenda kule kuchgeza mchezo wa kutumia mabavu ndipo niliposhinda kwa kumchakaza vibaya Komandoo wa Iran" Alisema Mwarabu Baada ya hapo Jeshi la nchi hiyo baada ya kumuona sio mtu wa kawaida kuwa raia wa kawaida ndipo alipochukuliwa Kambini humo kwa ajir ya kufanya mazoezi hayo ya hatari duniani hadi mwaka juzi 2013 ndipo walipompatia cheti cha kuhitimu kama kinavyoonekana pichani.

Hata hivyo Mwarabu anasema kwa jinsi alivyo na mazoezi aliyoyapata chini ya watu kumi hatakiwi kupigana nao hata wakija na shoka isipokuwa zaidi ya hapo ndipo kidogo atawapiga makofi tu na kuwaacha lakini sio aseme atoe kichapo kwani pigo lake moja mtu anabadilishwa jina mara moja na kuitwa marehemu. Mwarabu ambae kwa sasa ameajiriwa na mwanamuziki Diamond na analipwa mshara mnono kwa kazi ya kumlinda ambapo hadi sasa amenunua viwanja kadhaa na ujenzi unaendelea na si nyumba za kitoto huku akiwa na usafari zaidi ya gari tatu ambapo moja boss wake alimnunulia na mbili amenunua kwa mshahara anaomlipa na hadi sasa anakafikisha kilo 190 wastani wa kilo 200.

Jinsi ya Kumtambua Mwanaume Asiye na Pesa

0
0

Zifuatazo ni dalili za mwanaume asiye na pesa;

1. Kila siku appointment zake yeye ni gheto kwake au anang'ang'ania kuja kwako, hakuna hata kwenda beach wala hotelin.

2. Siku ukiwa unaenda kwake, anakwambia njoo kwenye saa tisa au kumi. Ujue amekadiria hiyo mida utakuwa umeshapata lunch.

3. Ukiwa unaenda kwake hasemi ukikaribia nishtue nitoke kukupokea, ujue anaogopa akifika kabla yako itabidi alipie bajaji.

4. Ukiwa unaondoka kwake anasema sijisikii vizuri kwahiyo siwezi kukusindikiza, ujue anaogopa unapopanda bajaji itabidi akulipie.

5. Ukimwambia umefulia, anakwambia "pole mpenzi ndio maisha hayo" ujue hana cha kukupa.

6. Mkiwa mpo mahali inabidi kila mtu aondoke peke yake ukasikia anasema mi ntapanda bajaji pale mbele kuna sehemu napitia, ujue hana hela anaenda kupanda daladala.

7. Kila mkienda kula restaurant jamaa anasema "mi nimetoka kula sio mda njaa haiumi" haagizi hata maji ya kunywa ujue jamaa hana kitu.

8. Kama upo mtandao tofauti na yeye kila siku ye anatuma tu sms, siku akitaka kupiga simu anakwambia "weka line ya tigo tuongee" ujue hana kitu huyo.

9. Ukiona anasisitiza kwamba hapendi wanawake wanaopenda vitu vya gharama kama simu n.k, ujue kaishiwa huyo akaoe ma house girl.

10.Ukiona kila siku ukikaa nae anakupa wosia kwamba mapenzi sio pesa, ujue hana kitu huyo.

Posted by: SUPU YA MAWE

Mwigizaji Lulu Michael Afunguka "Mimi Sina Jini Mauti Jamani"

0
0
MSANII nyota wa filamu, Elizabeth Michael `Lulu’ amekanusha uvumi kuwa matatizo yanayowatokea wanaume aliowahi kuwa nao yanatokana na yeye kuwa na Jini Mauti anayesababisha hali hiyo kutokea, Amani linakujuza.

Akizungumza na gazeti hili juu ya madai ya wadau mbalimbali kuhusiana na matukio mengi yanayomtokea, muigizaji huyo wa filamu ya Foolish Age, alisema maisha yake ya siku hizi ni ya kusali sana, hivyo anaamini kutokana na maombi yake, hali yake iko vizuri kutokana na Mungu kumpa anachokihitaji.

“Ninasali sana kwa sasa aisee, mara nyingi nafanya hivyo mara tatu kwa siku, ninao uwezo wa kukemea mapepo na yakaondoka, hayawezi kukaa mwilini mwangu,” alisema muigizaji huyo ambaye miaka michache iliyopita, aliondokewa na mpenzi wake, Steven Kanumba aliyeanguka na kufariki mbele yake.

Mtabiri mmoja maarufu jijini Dar es Salaam, Maalim Hassan Yahya Hussein, alisema tatizo kubwa linalomsumbua binti huyo ni jini mauti ambalo baada ya kumpenda, halitaki kuridhia uhusiano wake wa kimapenzi na binadamu.“Hapa nimshauri tu, achukue hatua ya matibabu haraka iwezekanavyo vinginevyo hali hiyo itaendelea, anatakiwa afanye kafara kwa kuchinja mnyama yoyote ili

Mbunge wa Arusha Mjini Lema Atamba Kushinda Tena Ubunge Bila Kampeni uchanguzi Mkuu 2015

0
0
Mbunge wa Arusha mjini kwa tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Godbless Lema amesema kuwa atashinda tena ubunge kwa tiketi ya chama hicho, hata asipopiga kampeni.

Aidha amesema ni vyema wananchi wa Jiji la Arusha na maeneo mbalimbali nchini kujitokeza kwa wingi kujiandikisha kwenye daftari la wapiga kura, ili waweze kupiga kura na kuchagua wagombea wanaotaka kuongoza.
Lema amesema hata asipopiga kampeni za kutetea kiti hicho yeye bado ni mbunge na uchaguzi huu ataendelea kushinda kwani wagombea wanaopitapita kutangaza nia na baadhi yao kugawa unga, bila mboga anawafananisha na bendera zinazoendelea kupepea bila kuwa na mafanikio yoyote.
Amesema ni vyema wananchi wakajitokeza kuhakikisha daftari hilo la wapiga kura likitangazwa kufika mkoani Arusha, wanajitokeza kwa wingi kujiadikisha ili waweze kutumia haki yao siku ya uchaguzi na kuongeza idadi ya wabunge na madiwani wengi kupitia Chadema.
Lema amesema kwa jinsi anavyoona hadi sasa maandalizi ya uchaguzi mkuu yanasuasua, hivyo yawezekana daftari hilo likitangazwa kuhamia
mkoani Arusha siku zinaweza kuwa chache hivyo ni vyema wananchi wakawa makini, wakisikia daftari linapita mkoa fulani wajitokeze kwa wingi kujiandikisha, ili waweze kuchagua wabunge wengi kutoka Ukawa.

Aunty Ezekiel Is Fond of Zari And Wants To Be Her Friend But Fears Her Friendship With Wema Sepetu Will Go Kaput.

0
0
Hot gossip is that Aunty Ezekiel is a big fan of Zari and she wants to be her friend but the problem is Wema Sepetu. Wema is Aunty's best friend while Zari is Wema's arch rival as we all know Zari  is now with Diamond Platnumz who used to be Wema's boyfriend for more than three years before their separation.

An insider from Aunty and Wema further told Swahiliworldplanet that Aunty likes how Zari uses well opportunities which come her way to earn money so she want to learn from her too, Plus Aunty wants to be Zari's friend believing they can exchange maternal experiences as they are both pregnant but Aunty has been hiding it just because she will jeopardize her friendship with Wema Sepetu.

"Aunty is very fond of Zari, she wants to be her close friend so that they can exchange maternal experiences too but Aunty is afraid her friendship with Wema won't be strong anymore because Wema won't be happy with it" said the source

Lady Jaydee Looking Lovely In a New Photo Shoot

0
0
Lady Jaydee looking so lovely in these new photos.................


Jackie Chandiru Avunja Ndoa ya mtu..Afunga Ndoa na Mume wa Mtu

0
0
Siku chache tu baada ya msanii wa muziki Jackie Chandiru wa nchini Uganda kufunga ndoa na mumewe ambaye ni raia wa kigeni Van Vliet, imegundulika kuwa, mwanaume huyo tayari alikuwa na ndoa na mrembo Adut Mawien.

Taarifa hizi zimeibuka na kuwaacha midomo wazi mashabiki wa Jackie, hasa kutokana na kurasa za mitandao ya kijamii za mumewe huyo mpya, kuendelea kuwa na picha na kumbukumbu za Adut ambaye ni mwanamitindo kutoka Sudan Kusini ambaye mpaka sasa, hakuna kithibitisho kuwa waliachana.

Kuibuka kwa taarifa hizi, kunamrudisha Jackie katika historia ya kutoka na waume za watu, rekodi zikionesha kuwepo kwa ugomvi mkubwa kipindi cha nyuma kati yake na mke wa Caleb Alaka, mwanaume ambaye aliingia naye penzini licha ya kuwa ni mtu mwenye familia.

MAPYA: Waajiri Waanza Kuwafukuza Madereva Waliogoma......CHAKUA, UWAMATA,CHAMAMATA Watoa Matamko

0
0
BAADHI ya madereva waliogoma katika mgomo wa juzi uliodumu kwa siku mbili wameanza kufukuzwa kazi na wamiliki wa mabasi hayo.

Mhasibu Mkuu wa Umoja wa Madereva Tanzania(UWAMATA) Issa Regan aliwataka matajiri kuwarudisha kazini dereva huyo na kama hawatawarudisha watawaambia madereva wote wa kampuni hiyo kugoma.

Regan aliongeza kuwa makosa sio ya madereva hao kwa kuwa walitii umoja huo na viongozi wao ndio waliwaambia kugoma hivyo kumfuza dereva sio sawa.

“Nasikitika kwa kitendo hicho na kama hawa matajiri wanataka vita basi tupo radhi kufanya hivyo lakini sisi tunataka kujenga mahusiano mazuri kati ya madereva na mabosi wao suala letu lilikuwa ni suala la msingi mtu ashindwe kuelewa mi sijui wanatutaka nini” alisema Regani.

Alimtaja dereva aliyefukuzwa na mmiliki wake kuwa ni Seif Kitumbo wa basi la kwenda Musoma, ambaye ni wa kampuni ya Osaka.

Regan alieleza kuwa wameshatoa taarifa kwenye vyombo vya  usalama kuwa endapo akipotea kiongozi yeyote wa chama chetu cha madereva bila mawasiliano (kutekwa) sisi tutashughulika na matajiri.

Naye dereva aliyefukuzwa katika gari hilo kwa sababu ya mgomo, Kitumbo alisema kuwa chanzo cha yeye kufukuzwa ni kwa sababu aligoma na tajiri wake alimwambia kuwa amemsababishia hasara.

“Nimekuja kwenye chama chetu hiki ili niweze kusaidiwa nimefanya kazi kwa muda wa mwaka mmoja na miezi 11 sijawahi kusababisha ajali yoyote”alisema Kitumbo.

Naye Katibu Mkuu wa UWAMATA,Abdala Lubala alisema athari za kutoajiriwa ndizo hizo kama Kitumbo angekuwa anamkataba asingefukuzwa kirahisi kama hivyo.

“Wamiliki wanatutafuta sisi tuligoma kwa haki yetu madereva tutafata sheria za kuweza kumsaidia huyu dereva arudishwe kazini lakini dunia imekubali madai yetu kuwa ni ya msingi”alisema Lubala.

Amri  ya  Kurudi  Shule  Yafutwa
Akizungumza na waandishi wa habari jana kituoni hapo, Katibu wa Umoja huo Abdul Lubanda alisema kero moja kati ya madai yao tayari limefanyiwa kazi na Serikali.

Alisema kero hiyo ni ile ya madereva kurudi shule kusoma kila baada ya miaka mitatu ambayo walikuwa wakiipinga.

“Baada ya kikao cha jana (juzi)tuliondoka na Mkuu wa Wilaya, Paul Makonda hadi kwa Waziri Mkuu kwa ajili ya kushughulikia masuala ambayo tulikuwa tunayalalamikia pamoja na kujua tume iliyoundwa.

“Tulikuwa pia na Waziri wa Uchukuzi, Samuel Sitta tulikuta tayari kero ya kurudi shule imeondolewa kimaandishi kama ambavyo tuliomba,” alisema.

Alisema walielezwa muundo wa tume (kamati) iliyoundwa na Waziri Mkuu Mizengo Pinda kwamba itajumuisha makatibu wakuu wa wizara nne pamoja na taasisi mbalimbali zinazohusiana na mambo ya usafirishaji.

Alitaja Wizara hizo ni pamoja na Ujenzi, Uchukuzi, Kazi na Ajira na Miundombinu na vyama hivyo ni Chama Cha Wamiliki wa Malori (TATOA), Chama cha Wamiliki wa Mabasi (TABOA), Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (SUMATRA), Chama cha Madereva, Chama cha Kutetea Abiria (CHAKUA).

 Alisema kamati hiyo itakuwa ikikutana mara moja kila mwezi na kwamba ital;azimika kukutana mara kwa mara iwapo kuna tatizo kama lililojitokeza hivi sasa la mgomo ili kulipatia ufumbuzi.

“Chama cha Madereva tumepatiwa nafasi tano za wajumbe ndani ya kamati hiyo leo (jana) tumekuwatana ili kuwateua wawakilishi wetu, kamati itakapoanza kazi  itashughulikia suala la mikataba ndani ya siku 30, tunataka kila dereva apatiwe mkataba bora na si bora mkataba na mwajiri wake,” alisema.

Alisema kutokana na mgomo uliomalizika wanaimani kwamba kilio chao kimewafikia wahusika na kwamba kamati hiyo itasimamia kwa weledi ili kuendelea kutatua changamoto zilizokuwa zikiwakabili.

Hali  ya  Kituo
Meneja wa kituo hicho, Juma Idd alisema idadi kubwa ya watu waliokuwa ndani ya kituo hicho kipindi chote cha mgomo iliwapa changamoto kubwa.

“Watu walikuwa wengi kupita kawaida, kwa sababu wengi ni wageni hawajui kama hapa kituoni tuna majengo matano ya vyoo ambayo yanajumla ya matundu…. Ilibidi tuwaelekeze watu sehemu hizo,” alisema.

Idd alisema anamshukuru Mungu kwamba licha ya mgomo huo kuwepo kwa takriban siku mbili, huduma ya maji ilikuwepo katika kipindi chote na hivyo vyoo hivyo kufanyiwa usafi kila mara kwani hali ingeweza kuwa mbaya zaidi.

Akizungumzia juu ya kupanda kwa gharama za vyakula kituoni hapo alisema Halmashauri haihusiki na jambo hilo kwani huduma hiyo hutolewa na watu binafsi.

“Watu walikuwa wakilalamika kupanda kwa gharama za chakula, kuna msemo wanasema kufa kufaana pengine wapo baadhi ya wafanyabiashara ambao waliona watumie mwanya huo kujipatia faida na labda kwa sababu bidhaa zilikuwa hazipelekwi sokoni ikapelekea kupanda kwa gharama za manunuzi,” alisema.

CHAKUA watoa  Wito
Katibu Msaidizi wa Chama cha Kutetea Abiria (Chakua) Godwin Ntongeji alitoa wito kwa wamiliki wa mabasi kutochukua nauli kwa abiria iwapo wanajua madereva wao watafanya mgomo.

Aliwataka wamiliki hao kufunga kabisa vituo vyao ili abiria wasikate tiketi kuliko kuwasababishia usumbufu kama huo walioupata kituoni hapo katika kipindi hicho cha mgomo.
 
“Vyakula vilipanda bei, wengine walikuwa wanakwenda msibani ikashindikana, na  kuna mwanamke mmoja alikuwa mjamzito akapatwa na uchungu ghafla usiku ilibidi wanawake wenzake wamsaidia walikwenda naye pembeni wakamzingira, wakamzalisha kisha akakimbizwa hospitalini,” alisema.

Chama cha Madereva  wa  Maroli
Mwenyekiti wa Chama cha Madereva wa Maroli (Chamamata), Clement Masanja, alisema watawashtaki wamiliki wote ambao watawafukuza madereva wao.

Alisema kitendo cha wamiliki kuanza kuwafukuza madereva ni cha uonevu kwani walikuwa wanadai haki zao za msingi.
 
“Tutafuatilia kujua kama huyo dereva aliyefukuzwa aliajiriwa kwa mkataba na kama hakuwa nao sisi kama chama tunao uwezo wa kumshtaki,” alisema Masanja.

Kauli nisiyopenda Kuisikia "Wenye akili wako Chuo cha UDSM, Huko Kwingine Utachelewa Sana Kuajiriwa Ukimaliza Chuo"

0
0
Nikiwa mwaka wa kwanza Chuo Kikuu Cha Tumaini- Iringa(sasa wanakiita University Of Iringa); nilikutana na "brother" mmoja aliyekuwa ndio kwanza ametua nchini baada ya kumaliza digrii yake katika chuo kikuu cha Makerere cha nchini Uganda. Akaniambia kauli ya ajabu sana, akasema, "Kwa nini umeenda kusoma chuo hicho?(akimaanisha Tumaini). Wenye akili wako UDSM, huko Tumaini umeingia choo cha kike, utachelewa sana kuajiriwa". Nikamwangalia weeee, (nikamuhurumia na kumdharau ndani kwa ndani) halafu nikamjibu; "Brother, wenye akili ni wale wenye hela za maana; wanaweza kuwa wamesoma huko UDSM ama chuo chochote na wanaweza kuwa hawakusoma kabisa!. Kujidhania una akili za kufaulia mitihani halafu usiwe na hela za maana(au atleast za kutosha) huo ni ujuha." Akiwa bado anashangaa-shangaa nilichomwambia, nikamuongezea;

"Kwanza wanaohangaika na CV za mavyuo ni wale wanaotaka kuwavutia wenye akili(waajiri) ili wawaelekeze cha kufanya(yaani wawaajiri). Mtu mwenye maono ya kujiajiri hahangaiki na CV za mavyuo bali anaangalia maarifa ya kumsaidia na kimsingi anaweza hata asiende shule bali akayapata maarifa hata mtaani tu". Akaniuliza, "Unamaanisha nini?" Nikamwambia, "Umesoma chuo Kikubwa lakini bado una akili za kikoloni zinazowaza kuwa hakuna maisha ya maana mpaka uajiriwe. Kusoma ni jambo zuri na kuajiriwa sio jambo baya lakini usikariri kuwa hakuna maisha pasipo kuajiriwa; na usifikiri kila anaefika chuo kikuu anawaza kuajiriwa tu. Siku hizi mafanikio kimaisha hayamo katika CV ya chuo ulichosoma na kamwe hutatajirika (au atleast kuwa na pesa za maana) kwa kutegemea mshahara pekee". Ikiwa imepita miaka sita sasa, sijajua hali ya kiuchumi na kimaisha ya yule brother; lakini ikiwa hajabadilisha ile "mentality" nina uhakika atakuwa "ni mbangaizaji tu" kiuchumi na kimaisha kwa ujumla licha ya kuwa anamiliki cheti cha digrii kutoka Makerere!

By Albert Nyaluke Sanga

Kutana na Mwanaume Mwenye Hips Kubwa Kuliko Wanaume Wote Dunia

0
0
20-year-old Micah is a man but his body features will amaze you! He has hips that are larger than life, the type of hips that most women will go under the knife to get.

The guy who has the eyes of many through his Instagram account says he is an upcoming singer and songwriter from Chicago. From the photos he posts on Instagram, it is obvious he enjoys and loves who he is and all the attention that comes with it.

Qoute of the Day
'You've gotta dance like there's nobody watching,
Love like you'll never be hurt,
Sing like there's nobody listening,
And live like it's heaven on earth.'

DIRTY! Campus Ladies Doing The Unthinkable, You Need PRIVACY Please (+21 ONLY VIDEO)

0
0
Some of the things ladies do in private are just shocking and disgusting.
In-fact, most campus hostels have been turned into Sodom and Gomorrah where all manner of evils take place.

Below is a video taken in one of Tanzania’s leading Universities that shows ladies getting wild and teaching each other bad manners. You need privacy on this before you click play.

Profesa Lipumba Aieleza Mahakama ya Kisutu kuwa Polisi WALIMPIGA, Akana Kufanya Maandamano

0
0
MWENYEKITI wa Chama cha Wananchi (CUF), Profesa Ibrahim Lipumba, ameieleza Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam kuwa, hawakufanya maandamano wala kupata barua ya zuio badala yake alipigwa na polisi.

Prof. Lipumba aliyasema hayo mahakamani hapo jana wakati yeye na washtakiwa wengine waliposomewa maelezo ya awali, mbele ya Hakimu Mkazi, Cyprian Mkeha.

Mawakili wa Serikali, Tumaini Kweka, Joseph Maugo na Mohamed Salum, walidai kesi hiyo imekuja mahakamani hapo kwa ajili ya washtakiwa kusomewa maelezo ya awali.

Akisoma maelezo hayo, Salum alidai CUF waliandika barua Januari 22, mwaka huu, kwenda kwa Kamishna wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Suleiman Kova kutoa taarifa ya kufanya maandamano kuanzia Ofisi za CUF Wilaya ya Temeke kwenda Mbagala Zakhiem.

Alidai mshtakiwa wa kwanza, Prof. Lipumba ndiye aliyepanga kuongoza maandamano na baadaye kuhutubia kwenye mkutano wa hadhara uliokuwa ufanyike Viwanja vya Zakhiem.

Aliongeza kuwa, Januari 26, mwaka huu, Jeshi la Polisi lilijibu barua hiyo na kuwataka wasitishe maandamano kutokana na sababu mbalimbali zilizoelezwa ndani ya barua hiyo.

Baada ya maelezo hayo, Prof. Lipumba alisema barua hiyo ilifika saa 12:30 jioni hivyo hakupata ujumbe wowote kama wamezuiwa kufanya maandamano hayo.

Alisema Januari 27, alifika katika Ofisi ndogo za CUF zilizopo Temeke kuzungumza na maofisa wa chama hicho na baadaye walianza maandamano kuelekea Zakhiem.

Hata hivyo, upande wa Jamhuri ulidai kabla ya maandamano hayo hayajaanza, polisi walitoa onyo la kuwataka wasitishe maandamano na kutawanyika kwani wanachokifanya ni kinyume cha sheria.

Licha ya kutolewa kwa onyo hilo, washtakiwa walikaidi amri hiyo,kuendelea na maandamano na walipofika eneo la Mtoni Mtongani, walikutana na polisi ambao walitoa ilani ya  kusitishwa kwa maandamano hayo lakini waliendelea kukaidi.

Baada ya washtakiwa kukaidi amri ya polisi, waliwakamata, kuwapandisha kwenye gari na kupelekwa Kituo cha Polisi Kati ili kutoa maelezo.

Hata hivyo, baada ya kusomewa maelezo na upande wa Jamhuri, mshtakiwa wa kwanza hadi 29, walikana na kudai hawakukaidi amri hiyo wala kufanya maandamano.

"Hatukufanya maandamano, huo ni uongo mtupu kwanza sikupata hiyo barua, isipokuwa polisi waliamua kutukamata na kutupiga tu," alidai Prof. Lipumba.

Upande wa Jamhuri ulidai kuwa, mshtakiwa wa 30 na 31 walikamatwa katika Viwanja vya Zakhiem wakiwa wamekusanya watu kwa ajili ya kufanya mkutano shtaka ambalo walilikana.

Kweka aliieleza mahakama kuwa, upelelezi wa kesi hiyo umekamilika, hivyo aliomba ipangwe tarehe ya kusikilizwa.

Baada ya kueleza hayo, upande wa utetezi ukiwakilishwa na Wakili Twaha Taslima aliomba apatiwe maelezo ya mlalamikaji.

Hakimu Mkeha aliahirisha shauri hilo hadi Juni 4, mwaka huu kwa ajili ya kesi hiyo kuanza kusikilizwa na kuutaka upande wa Jamhuri kuja na mashahidi wawili.

Hivi karibuni, viongozi wa CUF na wafuasi wao walifikishwa mahakamani hapo na kusomewa mashtaka matatu ikidaiwa kosa la kwanza walilitenda Januari 27, mwaka huu, eneo la Temeke ambapo wote kwa pamoja walikula njama ya kutenda kosa la kufanya mkusanyiko kinyume cha taratibu.

Katika shtaka la pili, inadaiwa siku hiyo ya tukio, washtakiwa, wakiwa katika Ofisi ya CUF karibu na Hospitali ya Wilaya ya Temeke bila ya kuwa na uhalali, walifanya mkusanyiko kwa nia ya kufanya maandamano kwenda Mbagala Zakhiem.

Shtaka la tatu, ilidaiwa siku hiyo ya tukio katika eneo la Mtoni Mtongani, waligoma na kutojali tangazo halali lililotolewa na polisi likiwataka wasiandamane na kutofanya mkusanyiko usio halali.

Washtakiwa hao ni Shabani Tano (29), Shabani  Abdallah (40), Juma (54), Athuman Ngumwai (40), Shaweji Mohamed, Hassan Said (37), Mohamed Ibrahim (31), Allan Ally (53) na Abdina Abdina (47).

Wengine ni Allawi Msenga (47), Abdi Hatibu (34), Abdallah Ally (32), Said Mohamed (40), Salim Mwafisi, Salehe Rashid (25), Rehema Kawambwa (47), Salma  Ndewa (42), Athuman Said (39), Dickson Leasson (37) na Nurdin Msati (37).

Baada ya Kupata Mamilioni, Diamond na Zari Ndoa Yafungwa Rasmi, Yadaiwa ni Kujibu Ndoa Aliyojitangazia Wema Sepetu

0
0
HUKU wakidaiwa kuogelea kwenye utajiri wa mabilioni ya fedha, nyota  wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’ ameibukia kwenye Gazeti la Amani na kusema kuwa, amefunga ndoa ya kimyakimya na mpenzi wake wa sasa, Zarina Hassan ‘Zari’ ambaye ni nyota wa muziki wa kizazi kipya, nchini Uganda na Afrika Kusini.

Diamond aliyasema hayo juzi jijini Dar es Salaam alipofanya mahojiano na waandishi wetu baada ya kumuuliza kama ana mpango wa kufunga ndoa na Zari.

SIKIA MAHOJIANO HAYO
Amani: “Zari ameshakubebea ujauzito, ameshaandaa shoo ya nguvu ile ya Zari All White Party hapa kwenu Tanzania na ameonekana kukubalika na baadhi ya mashabiki wako. Je, una mpango gani wa kufunga naye ndoa sasa?
Diamond: “Khaa! Mbona kama ni ndoa na Zari nimeshafunga kimyakimya!”
Amani: “Si kweli bwana! Lini na wapi?”

Diamond: “Hapahapa Dar. Lakini siwezi kusema ni wapi kwani tulishaamua iwe kimyakimya na imepita tayari, siku chahe kabla ya ile shoo ya Mlimani City.”Amani: “Kama ni kweli kwa nini haikuwa na mashamsham kama ndoa za mastaa wengine?”

KISA CHA KIMYAKIMYA
Diamond: “Unajua bi mkubwa (mama yake mzazi, Sanura Kasim) alikuwa anaumwa, kidogo ana nafuu kwa sasa. Ndiyo maana sikutaka mashamsham.”Amani: “Zari mwenyewe amekubaliana na uamuzi wa ndoa ya kimyakimya?”
Diamond: “Hakuwa na shida.”

KUHUSU DINI YA ZARI
Amani: “Amebadili dini? Maana ilisemekana alikuwa Muislam, akabadili kuwa Mkristo.”
Diamond: “Ilikuwa rahisi kurudi kwenye imani yake ya kwanza kwa hiyo ataendelea kuitwa Zarina.”

DIAMOND SASA
Rafiki wa karibu wa Diamond ambaye hakupenda jina lake kutajwa gazetini lakini wengi wanamjua, alipoulizwa kuhusu ndoa ya Diamond na Zari alisema:
“Jamani! Jamani! Jamani! Hivi kweli mnavyomjua Dangote (Diamond) nyie anaweza kufunga ndoa kwa siri au kimyakimya?”

Amani: “Amesema kwa sababu mama yake bado hajakaa sawasawa kiafya?”
Rafiki: “Mbona kaenda kutumbuiza kwenye Zari All White Party, Mlimani City, si angekaa na mama yake nyumban? Hivi Dangote mnamjua, mnamsikia? Acheni kabisa.

“Dangote anapenda kiki! Kila siku anawaza kiki. Kwa hiyo kusema amefunga ndoa na Zari sidhani kama ni kweli inaweza kuwa ni kiki. Tena afadhali kama Zari asingekuwa na mimba, lakini ameshambebea ule mzigo ndiyo kabisa maana Dangote yeye hana cha kupoteza. Lakini anyway, labda kweli.”

NI SIKU CHACHE BAADA YA WEMA KUDAI AMEFUNGA NDOA
Hivi karibuni, mpenzi wa zamani wa Diamond aliye pia Miss Tanzania 2006 na staa wa sinema za Bongo, Wema Sepetu naye alitupia kwenye mtandao wa Instagram picha inayomwonesha amefunga ndoa kwa siri.

Baada ya picha hiyo kuwa gumzo, baadhi ya vyombo vya habari, hasa vya kielektroniki vilimpigia simu Wema ili kumuuliza kama kweli amefunga ndoa kwa siri kama inavyoenea kwenye mitandao, Wema alikiri.
Kwa ile sauti yake ndogo: “Yeah! Nimefunga kweli ndoa.”

Swali: “Sasa Wema wewe ni supastaa, kwa nini ufunge ndoa kwa siri mpaka wadau wako wasijue?”
Wema: “Mume wangu hapendi ijulikane. Hata mimi sipendi ijulikane.”

YALIYOMKUTA WEMA BAADA YA KUKIRI
Amani lilizungumza na mtu mwingine wa karibu na Wema ambapo alisema:
“Jamani Wema amejitakia matatizo, ndugu zake, dada yake na mama yake wamemjia juu. Kwanza walimuuliza kama ni kweli amefunga ndoa bila wao kujua, akasema hajafunga.

“Mama yake alimwambia alichokifanya cha kukiri kwenye redio ni nuksi kubwa kwake na Watanzania hawatamwamini tena hata akisema ukweli.“Unajua ndugu zake waliweka kikao. Walikubaliana kwamba, kama ndoa yake ilikuwa kwenye filamu si mbaya lakini walilaani kile kitendo cha kuulizwa na watangazaji wawili wa redio tena kwa muda tofauti akakiri. Pale ndipo penye tatizo. Leo hii Wema atazungumza ukweli gani kwa watu wakamuelewa?”

WEMA NA GAZETI LA AMANI
Wema alipotafutwa juzi na gazeti hili na kuulizwa kuhusu ndoa hiyo alikiri kuwa ilikuwa filamu ambayo itatoka hivi karibuni.
Viewing all 104423 articles
Browse latest View live




Latest Images