Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104689 articles
Browse latest View live

Lulu Akiri na Kutoa Sababu ya Kupenda Kutoka na Wanaume Waliomzidi Umr

$
0
0
Staa mrembo wa Bongo Movies, Elizabeth ‘Lulu’ Michael amekili kupenda kuwa na mahusiano na ya kimapenzi na wanaume waliomzidi sana umri.

Akizungumza kwenye The Sporah Show, Lulu amezitaja sababu za kupendelea kutoka na wanaume waliomzidi umri.

SPORAH: Watu wanahisi kwamba Lulu anapenda sana kutembea na watu waliomzidi umri sana,

LULU: That’s true, sio uongo, sio sana, Napenda kudate mtu ambaye anayeweza kusimama kama mpenzi, kama kaka, kama baba, kama kiongozi. Sitakuwa tayari kuwa na ile relation leo tumeamka na Maisha Club, kesho tumeamka na Billicanas, kesho tumeamka pale tunakula chips, I need to gain from you, nje ya upenzi unanifundisha nini kwa sababu haimaanishi kwamba mi ntaishi na wewe milele, itafikia siku labda we utaondoka au mi ntaondoka, we ukiondoka mi nikibaki nimejifunza nini kutoka kwako na ntaendelea kuishi vipi.”

“Haimaanishi kwamba napenda kutembea na watu walionizidi umri labda miaka hamsini, napenda kuwa na mtu ambaye angalau ananizidi umri, anauzoefu zaidi yangu, amepitia vitu vingi, anajua vitu vingi kwamba i’ll be there as a girlfriend lakini nakuwa naiba iba kidogo […] na vitu vingine vya kitoto kitoto vingi vinakuwa hamna.” alisema Lulu.

Bongo 5

Ikulu: Nkurunziza Hayupo Tanzania, Alishaondoka, Tanzania haina cha kusema juu ya alipo Nkurunziza.

$
0
0
Mkurugenzi wa Kurugenzi ya Habari Ikulu,Salva Rweyemamu amenukuliwa na Redio BBC Swahili akisema kuwa Rais wa Burundi,Pierre Nkurunziza hayupo Tanzania. Akizungumza na BBC Swahili, Rweyemamu amesema kuwa Nkurunziza alishaondoka Tanzania na hivyo Tanzania haina cha kusema juu ya alipo Nkurunziza.

The saga continues!

Msemaji wa Nkurunziza amethibitisha kuwa Nkurunziza ameondoka Tanzania. Lakini,amekataa kusema alipo kwa sababu za kiusalama. Msemaji huyo amedai kuwa Rais Nkurunziza bado anadhibiti utawala wa Burundi

Ni kweli Linah anapaka Vipodozi vya kumfanya awe ‘Mweupe’?… #Uheard

$
0
0
Baada ya comment kadhaa kutoka kwa mashabiki na watu wanaomfuata Linah kupitia mtandao wa Instagram, mwenyewe aliamua kuandika maneno ambayo yametafsiriwa kama ni majibu kwa zile comment ambazo si nzuri kwake.

kwenye post yake Linah alianza kwa kuandika ‘Jamanii nimechoka Na kufuru zenu, hivi naomba niulize ufupi wangu, kukomaa kwangu, mkorogo wangu vinawahusu nini? Ni naomba mfatilie kazi zangu tu vingi be ni vitu vya kawaida kila binadamu kuambiwa kasoro zake!
Kwenye sentensi nyingine ameandika ‘Hvi wale ambao Hawana mikono Na miguu Na wao walie vipi kwa Mungu? Namshukuru hivi nilivyo. Mbona mnapenda kutoa hukumu kama nyie ndyo Israeli?! Ifike kipindi tukumbuke kila mtu anamaisha yake! Naona mnaandamana sana Na maisha yangu’

Mwisho aliandika ‘Kuna ambae hata alimsaidia mama yangu wakati anapush hospitali? Hivi kumbukeni mnawazazi pia Na nyinyi mlizaliwa pia,kama nyie Mungu basi nibadilisheni mniumbe mtakavyo, nyie ni kina baba Na kina mama wa badae kumbukeni mtazaa Na nyinyi then tuone! Chozi langu hili haliendi bure!! U will pay it back maana nimechoka Na masimango yenu’

Ndipo Soudy Brown wa Clouds Fm aliamua kumpigia simu na maongezi yao unaweza kuyasikia mtu wangu kwa kubonyeza play hapo chini lakini unaweza kuisikiliza Clouds Fm ukiwa Shinyanga kupitia 87.5.

We ni Miongoni Mwawatu Waliyopitwa na Mahojiano ya Wema Sepetu na EFM Radiao? Unaweza Kuisikiliza Hapa

$
0
0
Msikilize Mrembo Wema Sepetu akijitetea baada ya kupigwa kabali na 93.7 EFM.

I Have Never Been Pregnant, I Always use Protection - Vera Sidika Dismisses Claims She is 'Paged'

$
0
0
The world celebrated Mother’s Day on May 10 and many Kenyans went online to honour their mummies. International celebs too paid tribute to their mothers as others celebrated the gift of motherhood.
Closer home, the flashy Vera Sidika claims she called her mother since she was out of the country, even as speculations were rife that she is also a mum. Towards the end of last year, a photo of a seemingly ‘paged’ Vera surfaced online, shocking her fans, as she has never talked about a child or pregnancy.

“Did u know Vera Sidika was once pregnant? Now ask yourself where is the baby,” read a caption from Igwe Sonko SK on Facebook, who posted the picture, igniting debate among Kenyans on Twitter and Facebook. Some wondered whether the photo was real and the whereabouts of the baby and the father.

Now, Vera has come out to deny these allegations claiming that the picture was Photoshopped. “I have never been pregnant, I have always used protection. That photo was fake!” Vera said, but confessed that she hopes to have children some day

Aliyemng’ata na Kumtesa ‘House Girl’ Avamiwa na Majambazi

$
0
0
KESI ya kumtesa mfanyakazi wa ndani inayomkabili mkazi wa Mwananyamala, Amina Maige (42), imeahirishwa katika Mahakama ya Wilaya ya Kinondoni jana kutokana na mshtakiwa kuvamiwa na watu wasiojulikana na kumkata kwa mapanga.

Shauri hilo litakuja tena Juni 16, mwaka huu endapo hali ya mshtakiwa ikiendelea vizuri.

Mbele ya Hakimu Yohana Yongolo, Wakili upande wa Jamhuri ulidai kwamba shauri hilo lipo mbele ya mahakama hiyo kwa ajili ya kuendelea kusikilizwa ushahidi upande wa mlalamikaji.

Mdhamini wa pili wa mshtakiwa Chausiku Maige, aliiambia mahakama hiyo kwamba Amina ameshindwa kufika mahakamani kwa kuwa alivamiwa na watu wasiojulikana ambapo tukio hilo lilitokea nyumbani kwake Mei 7, mwaka huu.

Mheshimiwa mtuhumiwa kwa sasa yupo katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili Taasisi ya Mifupa (MOI), akiendelea na matibabu baada ya tukio hilo lililotokea nyumbani kwake alfajiri wakati akitoka ndani kuelekea kazini.

Tulitoa taarifa katika Kituo cha Polisi Osterbay kisha tulipewa RB/7647/2015. Amina amepata majeraha makubwa sehemu za mkononi pamoja na kichwani,” alidai Chausiku.

Hakimu alimhoji mtuhumiwa huyo kama  eneo analoishi mtuhumiwa huyo ana uhasama na jirani zake, ambapo shahidi huyo alijibu kuwa hajui kwa kuwa haishi naye karibu.

Amina Maige kwa mara ya kwanza alipandishwa kizimbani katika mahakama hiyo Juni 13, mwaka jana akikabiliwa na tuhuma za kumchoma pasi na kumng’ata mfanyakazi wake wa ndani, Yusta Kashinde (20) hali iliyosababisha maumivu makali mwilini.

Rais Pierre Nkurunziza Arejea Burundi Baada ya Jaribio la Kumpindua..Wanajeshi Watiifu Wadhibiti Maeneo Muhumu

$
0
0
Rais wa Burundi Pierre Nkurunziza  amerejea nchini humo, huku naibu kiongozi wa mapinduzi akikiri kuwa jaribio la kumuangusha Nkurunziza limeshindwa. Umoja wa Mataifa umetaka kurejeshwa haraka utawala wa sheria.

Mshauri mwandamizi wa mawasiliano wa rais Willy Nyamwitwe, alisema Nkurunziza amerejea nchini humo, lakini hakutoa maelezo zaidi kwa kile alichosema ni sababu za kiusalama.

Nkurunziza alikuwa nchi jirani ya Tanzania kwa ajili ya mazungumzo ya kikanda siku ya Jumatano wakati mapinduzi yalipotangazwa na Jenerali Godefroid Niyombere, na kufunika wiki kadhaa za maandamano dhidi ya jaribio la rais kutafuta muhula wa tatu.

Taarifa za kurejea kwa rais Nkurunziza hazikuweza kuthibitishwa na duru huru hata hivyo, na uwepo wake umeendelea kuwa kitendawili usiku wa Alhamisi.

Lakini tangazo kwamba amerudi lilifuatia haraka na kukiri kwa naibu kiongozi wa mapinduzi Cyrille Ndayirukiye kwamba mapinduzi hayo yameshindwa.

Ndayikuriye aliliambia shirika la habari la Ufaransa AFP, kuwa binafsi anatambua kuwa vuguvugu lao limeshindwa.

Wanajeshi Watiifu wadhibiti vituo muhimu
Mapema Alhamis, wanajeshi watiifu kwa rais walisema walizuwia mashambulizi mawili makubwa yaliyofanywa na wapinzani katika mapambano makali ya kudhibiti kituo chenye umuhimu wa kimkakati cha redio ya taifa.

Miili ya wanajeshi watatu ilionekana ikiwa imelala mitaani karibu na eneo la mapigano hayo, ishara ya kwanza ya maafa katika kadhia hiyo ya mapinduzi.

Kufikia mchana, mkurugenzi wa kituo hicho Jerome Nkokirantevye alisema wanajeshi watiifu ndiyo walikuwa wanakidhibiti kituo hicho.

Afisa mwanadamizi wa polisi alithibitisha taarifa hizo na kusema jana jioni kuwa wanajeshi wanaounga mkono mapinduzi walisambaratika baada ya mashambulizi yao dhidi ya Televisheni ya taifa RTNB na jengo la redio katika mji mkuu kukandamizwa. Alisema baadhi ya waasi tayari wamejisalimisha na wengine walikimbia.

Tangazo la mapinduzi la Jumatano lilisababisha ukosoaji kutoka sehemu mbalimbali za dunia, na kuibua hofu ya kurejea katika vurugu kubwa katika taifa hilo maskini, ambalo bado linaendelea kuhisi athari za vita vya wenyewe kwa wenyewe vya miaka 13 vilivyomalizika mwaka 2006, na kugharimu maisha ya maelfu ya Warundi.

Baraza la Usalama laonya
Marekani ilisisitiza Alhamis kuwa Nkurunziza ndiye rais halali wa Burundi . Nalo Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa lililokutana katika kikao cha dharura siku ya Alhamis, lililaani jaribio hilo la mapinduzi, na kutaka kurejeshwa haraka kwa utawala wa sheria na kufanyika kwa uchaguzi kwa kuzingatia makubaliano ya Arusha.

Katika taarifa iliyosomwa na Raimonda Murmokaite, balozi wa Lithuania katika Umoja wa Umoja wa Mataifa, na rais wa barala hilo kwa mwezi wa Mei, baraza hilo lenye wanachama 15 lilieza utayarifu wake kuchukulia hatua vitendo vya vurugu nchini Burundi vinavyotishia amani na usalama.

"Wanachama wa baraza la usalama wamelaani machafuko nchini Burundi na hasa wamewalaani wanaochochea vurugu za aina yoyote dhidi ya raia, na wale wanaotaka kutwaa madaraka kwa njia zisizohalali," alisema Murmokaite.

"Wanachama wa baraza la usalama wametoa wito kwa pande zote kutotumia vurugu na kutoa kipaumbele kwa amani na usalama. Baraza pia limerejelea uungaji wake mkono wa juhudi la mjumbe maalumu wa Umoja wa Mataifa Said Djinnit, Umoja wa Afrika na Jumuiya ya Afrika Mashariki."

Chanzo: DW

Nyumba ya Diamond Katika Hati Hati..Mafuriko Yaizengea ,Yazungukwa na Mifereji ya Maji ya Mvua

$
0
0
MAFURIKO yanayotokea katika sehemu mbalimbali nchini kutokana na mvua  zinazoendelea kunyesha, yanaizengea nyumba ya nyota wa muziki wa kizazi kipya nchini, Diamond Platnumz iliyopo Tegeta Madale, nje kidogo ya Jiji la Dar.

Kwa mujibu wa majirani wa staa huyo, nyumba hiyo imejengwa katika njia ya maji (mkondo), jambo ambalo hakulielewa hapo mwanzo, kwani ndiyo sababu kubwa iliyodondosha ukuta wa uzio wake muda mfupi baada ya Diamond kuhamia wiki kadhaa zilizopita.

Kabla ya ujenzi, kiwanja hiki kilikuwa na njia kuu mbili za maji ambazo wakati wa mvua, zilikuwa zinatiririsha maji kuelekea bondeni, lakini baada ya ujenzi, nguvu ya yale maji yakadondosha ukuta.

Sasa ukiacha ukuta uliobomoka mwanzoni, kuna njia nyingine ambayo inapitisha maji mengi zaidi ambayo inapita kwenye ukuta wake mwingine na tayari yameanza kuuchimba kwa chini. Mnaweza kuja kuangalia,” alisema jirani mmoja aliyekataa kutaja jina lake.

Waandishi wetu walifika nyumbani hapo na kumkuta fundi ujenzi akijaza kifusi nyuma ya ukuta uliovunjika mwanzo huku upande mwingine wa ukuta  maji yakionekana kutiririka kwa kasi.

Wema Sepetu " Sina Bahati na Marafiki Kabisa, Nawapenda kwa Moyo Wote ila Wananigeuka..Sasa Nimeamua Kufuata Ushauri wa Mama Yangu"

$
0
0
Na Imelda Mtema
Beautiful Onyinye wa Bongo, Wema Sepetu amefunguka kuwa, anajua siku zote yeye hana bahati ya kuwa na marafiki kwa kuwa hata akiwa nao mwishowe kunatokea mgogoro na kuachana huku kila mmoja akimuona mbaya

Akizungumza na gazeti hili juzi, Wema alisema anaumia sana kwa kuwa mara nyingi anawapenda sana rafiki zake kwa moyo mmoja lakini mwisho wa urafiki wao huwa ni mbaya sana tena huvunjika kwa kugombana.

“Mimi nimeshajiona siku nyingi sina bahati kabisa, hata nikiwa na marafiki ambao nawapenda kutoka moyoni, mara nyingi wananigeuka na mama yangu amekuwa akinisihi mara nyingi sana, sasa naona bora nifuate ushauri ambao mama yangu ananishauri wa kuangalia watu wa kuanzisha urafiki nao,” alisema Wema.

5 Reasons Why Curvy LADIES Are the Best in Bed, Do You Agree?

$
0
0
1) BO0BS

Not every curvy girl has large bo0bs but the chances are 80% are favored with big bo0bs are everything and more. There is hardly any man that doesn’t fancy bo0bs as this is usually the first step of foreplay before s3x.

2) BO0TY

Big bo0ty in children are as a result of Omega 3 fatty acid they store and there is NO curvy girl without a big bo0ty . Being with a curvy girl is your subconscious way of ensuring healthy kids.

3) A PLACE TO REST

After long pleasurable s3x, the soft womanly curves is the perfect place to rest your post-shagging head. There is really no difference between her bo0ty  and the pillow.

4) HEALTHY S£X APPEAL

There is really nothing more appealing than a curvy full figured lady. Curvy girls have long been associated with beauty and s3x appeal and thousands of years of history can never be wrong. A curvy girl is easily appealing to the eyes at first sight which in turn creates a healthy appetite.

5) CONFIDENCE

Having bo0bs, a massive backside or something to grab hold of is not only what makes a curvy woman s3xy, it goes beyond that to knowing how best to rock it. Beauty has everything to do with confidence and confidence has everything to do with amazing s3x.

Sababu Zilizosaidia Ndege ya Nkurunzinza Isitunguliwe Bujumbura

$
0
0
Pierre Nkurunzinza janja janja sana huyu bwana,hata jana nchini mwake hakuondoka na ndege ya nchi yake...ili kuwapoteza maboya maadui wake alikodi ndege toka South Africa ikaja kumchukua Bujumbura - Dar es Salaam.Hata "Call Sign" yake haikuwa inaita kama "Burundi 001" ilikuwa inaita kwa Registration number yake ambayo ni ya South Africa,maana nasikia alipanda LearJet45(LJ45) yenye usajili wa ZS-OPR ambayo ni usajili wa Afrika Kusini

Sasa kama Rais alifikia kukodi ndege toka Afrika Kusini maanake alianza kunusa harufu za uasi toka kwa watu wake,ambao pengine angekuja na ndege ya Serikali kwayo Marubani wake ni Wanajeshi wangeweza kumuhujumu kwa namna yoyote ile.Hii kukodi ndege ya nchi nyingine na kuendeshwa na marubani ambao ni raia wa nchi nyingine ya Afrika kusini ndio imemuokoa jana Rais Pierre Nkurunzinza,laa sivyo kama angekuwa amekuja na ndege ya Serikali ya Burundi basi historia ya mwaka 1994 ingejirudia jana ktk uwanja wa ndege wa Bujumbura kwa Nkurunzinza kuripuliwa na ndio ingekuwa mwanzo wa machafuko kati ya wale wanaomuungu Nkurunzinza na wale wasio watiifu kwake


Kwenye usafiri wa anga kuna kitu wanaita "Call Sign",huu huwa ni muito wa ndege au utambulisho wake inapokuwa ktk safari zake,utambulisho huu unaweza kuwa ni namba ya usajili ya ndege,au jina la kampuni ya ndege au jina "mahalia" linaloambatana na "flight number"...kwa mfano wa jina "mahalia" kwa ndege za shirika la umma la Afrika Kusini ni "springbok",huyu ni mnyama mwenye sifa na heshima kwa S.Africa,British Airway wao ni "Speedbird",wakati mashirika kama Fly 540 hujiita kama "swift Tango" n.k

Kwa mfano Tanzania shirika la ndege la fast jet "call sign" yake hujiita kama "Greybird" kutokana na picha ya ndege wa kijivu kama alama ya ndege pale mkiani mwa ndege zao.Kwa hiyo hata watu mashuhuri duniani huwa na "call sign" zao wawapo angani au ardhini iwe tu ni ndani ya ndege,mfano Rais wa Marekani akiwa ndani ya ndege ya Rais "call sign" yake huwa ni "Air Force One", akiwa ndani ya meli ataitwa kama "Marine One";kwetu hapa Tanzania ndege ikiwa imebeba rais hujitambulisha kama "Tanzania One",akiwa makamu wa Rais "Tanzania Two" na akiwa Waziri mkuu rubani huita "Tanzania Three".

Tukirudi kwenye mada ya Nkurunzinza Pierre,jana wakati akiondoka Bujumbura kuja Tanzania hakujitambulisha kama "Burundi One" bali marubani wa kukodiwa toka Afrika Kusini waliita kwa "Call sign" ya "ZS-OPR",kitu ambacho kilifanywa kuwa siri ya nani alikuwa ndani ya ndege hiyo,kwa aina ya usajili wa ndege maadui wa Nkurunzinza iliwawia vigumu kujua hasa ni nani yupo ndani ya ndege hiyo na wasingefanya lolote sababu usajili wa ndege ilikuwa ni Afrika Kusini.

Mara baada ya mkutano hapa DSM,Nkurunzinza alitaka kurudi kwa lazima Bujumbura ili akahutubie Taifa kupitia Radio na Tv za Serikali,kujiamini kwako kulikuwa na sababu ya aina ya ndege aliyotumia ili kutua ktk uwanja wa Bujumbura,kitu ambacho aliamini maadui zake hawawezi "kuitungua" kwa sababu zifuatazo:

(1)Ilikuwa ni ndege ya kiraia toka Afrika Kusini

(2)Ilikuwa ndege inayoongozwa na marubani raia wa S.Afrika.

Kuitungua ndege hii yenye marubani wa Afrika Kusini tena "raia" waliombeba "mteja" aliyeikodi,ingeamsha mgogoro mpya wa kidiplomasia ambao "maadui" zake wasingeweza kukubali mtego huo

Nkurunzinza aliondoka Dar es Salaam milango ya saa 1815hrs,lakini baada ya kama saa moja na nusu alirudi tena kutua kwenye uwanja wa ndege wa Dsm,hii ni baada ya kujaribu kutua mara mbili katika uwanja wa Bujumbura kwa "Call sign" ya " ZS-OPR" badala ya "Burundi One".Hata baada ya rubani kuulizwa mara kadhaa "status of souls on board" alisisitiza kuwa ni "customers" waliomkodi toka Bujumbura-Dsm-Bujumbura.

Baadae Rubani wa ndege akaambiwa "Clear to land at your own risk"...hii ni baada ya chumba cha waongoza ndege kuwa tayari mikononi mwa wanajeshi wasio watiifu kwa Nkurunzinza,hali hii ilimfanya Rubani kugeuza na ku-opt Entebbe International Airport,ambapo Mseven hakuwa tayari,ndipo Pierre akaamua kurudi kwa "Baba" zake Tanzania,mpaka sasa hajulikani amefikia sehemu gani ktk jiji la Dsm,hata Waziri Membe alipooulizwa leo kuwa Nkurunzinza yupo Tz sehemu gani,hakutaka kusema mahali alipo

Hiki ndio kitu pekee kilichomuokoa Brother Nkurunzinza,vinginevyo maadau zake waliokuwa wamefunga mipaka na kutawala viwanja vya ndege wangefanya lolote endapo tu ndege aliyokuwa anatumia ingekuwa ni ile ya Rais ambayo huitumia mara kwa mara,maana kwa maadaui zake kurudi kwa Nkurunzinza toka Dsm na kuhutubia Taifa ingekuwa ni pigo kwani ingezuia vuguvugu na harakati za kumuondoa madarakani zilizokwisha anza.

Lakini mbadala mwingine kama Nkurunzinza angekuwa ametumia ndege ya Rais kurudi Bujumbura kwa kulazimisha ni ima maadui zake wangeitungua ndege yake au wangeruhusu itue na kumshikiria Pierre kwa nguvu,lakini kwa sababu ya "mbeleko" ya ndege ya "kiraia" yenye marubani " raia" toka nchi ya Afrika Kusini,Maadui zake walizingatia diplomasia ya kimataifa na kumsihi rubani asitue Bujumbura "if and only among the souls on board,the soul of Nkurunzinza was boarded"...hii ndio ilikuwa nafuu ya Bro Nkurunzinza na "ujanja" wa team yake ya kijasusi,vinginevyo leo tungekuwa tunaongea mengine na pengine kama yale ya mwaka 1994 ambapo baada ya mkutano wa Dsm,watu walipokuwa wanarudi Makwao wakatunguliwa.

Mchungaji Gwajima Avamiwa.....Apigwa Panga Kichwani na Kulazwa ICU

$
0
0
MCHUNGAJI wa Kanisa la Ufufuo na Uzima jijini Mwanza, Samson Gwajima na Ofisa wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), Amin Neigwa, wamevamiwa na majambazi ambao wamewajeruhi vibaya kwa kuwakata mapanga vichwani.

Tukio hilo lilitokea usiku wa kuamkia jana katika Mtaa wa Lyila, Kata ya Buhongwa, Wilaya ya Nyamagana, jijini Mwanza.

Akizungumza kwa taabu na mwandishi wetu akiwa wodini kwenye Hospitali ya Rufaa ya Bugando (BMC), alikolazwa kwa matibabu, Neigwa, alisema akiwa sebuleni nyumbani kwake na mkewe, ghafla walimuona msichana wa kazi aliyekuwa nje akichota maji, akiingia ndani kwa kasi na kukimbilia chumbani.

Alisema wakati akitahamaki kilichotokea, watu wanaosadikiwa kuwa majambazi waliingia ndani wakiwa na silaha za jadi kama mapanga, nyundo, vitu vyenye ncha kali na kutaka fedha.

"Walikuwa sita na baadhi yao walifunika sura zao kwa vitambaa, walinitaka niwape pesa...nilipata ujasiri wa kumrukia mmoja wao aliyekuwa na panga na kumkaba ndipo wengine wakanishambulia kwa kutumia silaha zao hadi nikapoteza fahamu," alisema.

Aliongeza kuwa, wakati wanamshambulia wengine walikuwa wanamlazimisha mkewe awape pesa lakini aliwakatalia na baadaye aliamua kuwapa sh. 10,000 ambayo ilikuwepo wakaichukua.

"Kelele nilizopiga wakati tumevamiwa zilisikika kwa majirani ambao walijitokeza ndipo wavamizi wakakimbia," alisema Neigwa ambaye alijeruhiwa kichwani ambapo hadi jana alikuwa akitokwa na damu masikioni.

Baada ya watu hao kukimbia, walienda kuvamia nyumbani kwa Mchungaji Gwajima na kumjeruhi kichwani kwa panga ambapo hivi sasa amelazwa katika hospitali hiyo kwenye Chumba cha Wagonjwa Wanaohitaji Uangalizi Maalumu (ICU).

Mchungaji Gwajima ni kaka wa Kiongozi wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Askofu Josephat Gwajima, ambaye alivamiwa alipokuwa amelala na familia yake eneo la Lyila na kulazimishwa kutoa fedha.

Akizungumza na mwandishi wetu, Mchungaji wa kanisa hilo, John Kiula,  alisema Mchungaji Gwajima alivamiwa usiku ambapo baadhi ya mashuhuda walidai baadhi ya meno yake yameng'oka.

"Hadi sasa bado hajajitambua, tumetoka kwenye kipimo cha CT-Scan lakini majibu bado hatujapewa tumeambiwa yakiwa
tayari watatujulisha," alisema Mchungaji Kiula.

Mkuu wa Idara ya Dharura hospitalini hapo, Dkt. Derick David, alikiri kuwapokea majeruhi hao usiku na kusema Mchungaji Gwajima alifikishwa akiwa na hali mbaya zaidi kuliko Neigwa.

"Gwajima ana jeraha kubwa kwenye paji la uso ambalo ni kama sentimita mbili hadi tatu kwa urefu kwenda ndani, kipimo cha X-Ray kimeonesha hajapasuka mfupa ila hali yake si nzuri.

"Hadi sasa bado hajitambui, tunatarajia kumfanyia kipimo kikubwa cha CT-Scan ambacho kitaonyesha ameumia kiasi gani lakini Neigwa anaendelea vizuri ingawa naye anahitaji kupimwa na CT-Scan ili kuona majeraha yake kama amepata athari ndani ya kichwa, tunaendelea kuokoa maisha yao," alisema.

Kamanda wa Polisi mkoani humo, Naibu Kamishna wa Polisi, Charles Mkumbo, alikiri kutokea kwa matukio hayo na kuahidi kuyatolea ufafanuzi ambapo baadhi ya watu wamekamatwa wakihusishwa na matukio hayo.

"Mkuu wa Upelelezi Mkoa na timu yake walikuwa wanaendelea na uchunguzi, wakiukamilisha nitalizungumzia kwa undani na kuwataja walioshikiliwa, baadhi ya majambazi hao wametambuliwa na majirani," alisema.

Padri wa Kanisa Katoliki Anaswa Kichakani Ndani Ya Gari Akiwa Na Mrembo UCHI

$
0
0
KAMA mti mbichi unatenda haya, itakuwaje kwa mti mkavu?! Ndivyo inavyoweza kutafsiriwa kwa Katibu Mtendaji wa Idara ya Mawasiliano wa Baraza la Maaskofu wa Kanisa Katoliki Tanzania (Tanzania Episcopal Conference, TEC), Padri Anatoly Salawa kufuatia kunaswa kichakani akiwa na mrembo.

Kiongozi huyo wa dini alinaswa hivi karibuni majira ya saa 8: 02 usiku akiwa ndani ya gari aina ya Toyota RAV 4 lenye nambari ya usajili T 674 ADA kwenye kichaka kilichopo maeneo ya viwanda na gereji za magari makubwa, Kurasini jijini Dar.

Huku mvua kubwa ikinyesha na baridi ikipuliza vilivyo achilia mbali baadhi ya maeneo ya jiji kutotulia kwa mafuriko na foleni, waandishi wetu  walipigiwa simu na mlinzi mmoja wa Kimasai wa kwenye gereji hizo na kunyetisha juu ya gari lililosimama karibu na eneo lao la lindo huku likinesanesa.

Mlinzi huyo alieleza kuwa yeye na wenzake walilichunguza kwa makini gari hilo na kuona kuwa ndani yake kulikuwa na watu wawili wa jinsi tofauti lakini walishindwa kujua wazi kilichokuwa kikiendelea.

Mlinzi huyo alisema kuwa mara kwa mara gari kama hilo  limekuwa likifika hapo majira ya usiku wa manane hivyo kuwafanya kuingiwa na shaka.

Waandishi walifika eneo la tukio ndani ya muda mfupi na kuwakuta polisi nao wakiwasili kisha kuchukua kwanza maelezo kwa walinzi hao bila kuwashtua wahusika kwenye gari.

Baada ya mahojiano na walinzi hao, walilifuata gari hilo na kulipekua ambapo hawakuamini macho yao baada ya kumkuta mtu mzima huyo katika gari hilo akiwa na mrembo aliyekuwa mtupu.

Huku mvua ikiendelea kumwagika, padri huyo alionekana akiwa ametaharuki ndani ya gari asijue la kufanya.

Mara baada ya kuwanasa wawili hao, padri alijitetea kwa kusema kuwa, alikuwa ameingiliwa na wahuni katika starehe zake hivyo aliingia kwenye gari na kutimua na mrembo wake.

Jana  padri  huyo  alitafutwa  tena ili kama ana la ziada la kusema alitoe lakini simu yake ya kiganjani iliita bila kupokelewa na baadaye ikazimwa kabisa.

Baada ya muda simu hiyo iliwashwa tena na ndipo  alipotumiwa ujumbe mfupi wa simu ya mkononi (SMS) . Hata hivyo, SMS hiyo haikujibiwa.


Baada ya SMS hiyo, padri huyo aliendelea kupigiwa simu lakini bado iliita bila kupokelewa ndipo akatumiwa ujumbe mwingine uliosomeka hivi; ‘mkuu tumepata tukio lako ukiwa kichakani ndani ya gari usiku na mrembo akiwa mtupu. Wewe unalizungumziaje tukio hili? Kwa maana nyingine unajiteteaje? Tunaomba maelezo yako’.

Kama ilivyokuwa kwa ujumbe wa kwanza, nao huo haukujibiwa.

Chanzo:  Gazeti  la  Ijumaa/Gpl

James Lembeli Aitaka Ikulu Imsafishe Pia Lowassa Kama Ilivyowasafishwa Watuhumiwa Wa Escrow

$
0
0
Aliyekuwa Mwenyekiti wa Kamati Ndogo ya Bunge kuchunguza madhara ya Operesheni Tokomeza, James Lembeli, amekosoa ‘mchezo mchafu’ wa serikali kuwasafisha baadhi ya viongozi wanaotuhumiwa kwa kashfa mbalimbali.

Amehoji kama suala ni kusafishana, kwanini juhudi kama hizo zisitumike kuwasafisha wengine pia kama Waziri Mkuu Mstaafu, Edward Lowassa.

Lowassa alijiuzulu wadhifa wake kutokana na sakata la mtambo wa kufua umeme wa kampuni ya Richmond, mwaka 2007.

Wengine waliojiuzulu kufuatia sakata hilo ni Dk. Ibrahim Msabaha na Nazir Karamagi ambao wote walikuwa mawaziri wa Nishati na Madini kwa nyakati tofauti wakati sakata hilo lilipoibuka bungeni mwaka 2008.

Akichangia hotuba ya mapitio na mwelekeo wa kazi za serikali na makadirio ya matumizi ya fedha ya ofisi ya Waziri Mkuu kwa mwaka 2015/16 bungeni jana, Lembeli alisema, tabia hiyo italeta giza. Alisisitiza tabia ya kuwasafisha viongozi wachache na kuwaacha wengine ni mbaya.

“Kama kusafishana basi tusafishane wote na siyo watu wachache tu. 
 
“Nchi hii sasa inaenda kubaya, watu wanawekwa kwenye makundi…kama kusafishana tusafishane wote na kama siyo hivyo huko tunakoenda kuna giza. Tabia iliyozuka sasa ya kusafishana na kuwaacha wengine ni mbaya,” alisema Lembeli ambaye ni Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Mazingira.

Alisema licha ya kuwa alikuwa mmoja wa wajumbe wa Kamati Teule ya Bunge iliyochunguza sakata la Richmond lililomlazimisha Lowasa ajiuzulu, kwa sasa haoni sababu za kiongozi huyo ambaye pia ni Mbunge wa Monduli naye kutosafishwa.

Tokomeza
Alisema ripoti ya kamati yake ya Tokomeza, haikuwatia hatiani waliokuwa mawaziri watatu, Dk. Emmanuel Nchimbi-Mambo ya Ndani ya Nchi, Balozi Hamis Kagasheki-Maliasili na Utalii na Shamsi Vuai Nahodha- Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, isipokuwa waziri mmoja, Dk. Mathayo David Mathayo-Mifugo na Uvuvi.

“Nimeshtuka kusikia ripoti ya Tume ya Kimahakama ya Uchunguzi kuhusu sakata la Operesheni Tokomeza imesema mawaziri hao hawana makosa…kamati yangu iliweka bayana kwamba hao hawakuwa na makosa, kuna siri gani hapo,” alihoji na kuongeza:

“Lakini ripoti hiyo haizungumzii namna ya kuwalipa fidia ndugu wa watu waliokufa, waliojeruhiwa na kupata ulemavu au kuharibiwa mali zao.”

Alimtaja pia Ezekiel Maige, aliyekuwa Waziri wa Maliasili na Utalii, kwamba naye pia anahangaika na anastahili kusafishwa.

Tegeta  Escrow
Kuhusu sakata la Akaunti ya Tegeta Escrow, alisema, matokeo ya uchunguzi uliofanywa na serikali umewasafisha aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini, Prof. Sospeter Muhongo na Katibu Mkuu wake, Eliakim Maswi na kuwaacha wengine.

Alisema tatizo kubwa la sakata la Akaunti ya Escrow ni wale walioidhinisha fedha hizo kutolewa na siyo waliwekewa fedha kwenye akaunti zao. Kiasi cha Sh. bilioni 301 zilichotwa katika akaunti hiyo.

Alisema wakati akina Prof. Muhongo na Maswi wanasafishwa, akina Prof. Anna Tibaijuka wanahangaika kwa kutiwa hatiani na sakata hilo.

Alisema wakati Prof. Tibaijuka anahangaika kutokana na kuwekewa fedha kwenye akaunti yake, waliohusika kuidhinisha fedha hizo kutoka hawajachukuliwa hatua yo yote.
 
Alidai Mbunge wa Bariadi Magharibi, Andrew Chenge, naye anahangaika kwa kuwekewa fedha hizo, lakini kwa mujibu wa maelezo yake fedha hizo ni malipo ya kazi aliyokuwa ameifanya ya kutoa ushauri ambayo ni haki yake.

Ezekiel Wenje
Kwa upande wake, Mbunge wa Nyamagana, Ezakia Wenje, (Chadema), alirusha kijembe kwa watuhumiwa wa sakata la akaunti ya Tegeta Escrow, akisema haiwezekani kwa mtu ambaye yumo kwenye ‘dili’ la kashfa za fedha asafishwe.

“Kosa la escrow ni wale walioidhinisha fedha hizo zitoke. Nikisikia mbunge yumo katika kila dili halafu anajisifia nje kuwa yeye ni ‘nyoka wa makengeza’ huyo huwezi kumsafisha,” alisema.

 Sugu
Mbunge wa Mbeya Mjini (Chadema), Joseph Mbilinyi, amehoji sababu za serikali kununua magari 700 ya deraya na ya maji ya kuwasha badala ya kuipa fedha Tume ya Uchaguzi (NEC) isajili wapiga kura.

NEC iko taabani kifedha na imeshindwa kusajili wapiga kura na kununua vifaa vya kusajili kielektroniki (BVR).  

Akiongea kwa mbwembwe na vibwagizo wakati wa kuchangia hotuba hiyo, Mbilinyi alisema inashangaza kuona kuwa hakuna kipaumbele. Alisema kati ya deraya (magari yasiyopenya risasi) 700 yanayonunuliwa  anaomba 500 yapelekwe Mbeya ili wayafanyie kazi.

Sugu alisema wapinzani hawana ugomvi na serikali lakini wanachozungumzia ni masuala ya kutetea umma.

Alitoa mfano wa kura ya maoni wapinzani walisema haitafanyika, lakini serikali ikang’ang’ania kuwa itapigwa Aprili 30 jambo ambalo halikufanyika.

Aliongeza kuwa kuna msemo kuwa namba hazidanganyi, lakini watu huongopa hivyo serikali ya CCM ikubali kuwa hakuna sababu ya kuwadanganya wananchi kwa vile ukweli unaonekana.

“Wanawake  au wanaume wanadanganya, lakini namba haziongopi 2+2 ni sawasawa na 4,” alisema Sugu na kutamba kuwa atashinda uchaguzi wa Oktoba.

Akizungumza kwa kuweka lugha za kimziki kama ‘yaah men’‘kamooni’ aliitaka CCM na serikali wasipate hofu (kupaniki) bali wawasikilize na wapinzani kwa vile nia ni kupeleka mbele maslahi ya nchi. 
 
Mbunge mmoja alikifananisha Chama Cha Mapinduzi (CCM) na ng’ombe anayesubiri kuchinjwa.

CCM inaelekea kibla kama ng’ombe anayesubiri kisu, tumechoka tunataka kunufaika na rasilimali zetu. Ikifika Oktoba tunaichinja,”alisema Kuluthum Mchuchuri  (CUF Viti Maalum).

Alisema Watanzania wanaishi kwa kudra za Mwenyezi Mungu na si sera, bajeti  wala mipango ya CCM.

Akitaja baadhi ya mambo yanayoipeleka CCM kibla ni pamoja kujenga maabara wakati hakuna walimu wa sayansi.
 
Alisema shule kama Mwara, Mwaseni na Umwe mkoani humo hazina walimu lakini maabara zinashinikizwa kujengwa.
 
Lakini pia vijembe viliendelea  pale Zarina Madabida (Viti Maalum CCM), alipowafananisha wapinzani na wake wenza wa CCM, akisema hawawezi kuisifia CCM kwani kufanya hivyo ni sawa na mke mwenza kumsifia mwenzake.
 
Mbunge wa NCCR-Mageuzi Kasulu Mjini, Mosses Machali, alipinga kuwa serikali ya CCM haiwezi kujenga maabara bali ni wananchi ambao wanachangishwa fedha na wanashiriki kujenga majengo hayo.

Mbunge wa Kinondoni (CCM), Idd Azzan, aliulipua ujenzi wa barabara ziendazo haraka jijini Dar es Salaam (Dart) kuwa ni chanzo cha mafuriko. 
 
Alisema barabara hizo zimegeuza Jangwani kuwa uwanja wa mafuriko na kusababisha maji kujaa juu ya barabara kutokana na ujenzi na vifusi vilivyomwagwa.

Mbunge wa Arusha Mjini (Chadema) Godbless Lema, alisema siasa zinazotumia propaganda za udini na ukabila zinatumika kuichafua Chadema.
 
Aliyasema hayo kufuatia maelezo ya Mohamed Amour Chombo (CCM) Magomeni, aliyesema Ukawa wanashangaza kudai wataondoa ubaguzi wakati ndiyo vinara wa kubagua.

Chombo alieleza kuwa Cuf ni wabaguzi kwa asilimia 100, akitaja kuwa huko Pemba kiongozi akiomba uongozi hawezi kupewa kama anatokea Unguja. 
 
Na hata Unguja ndicho wanachofanya ni wabaguzi na wanachaguana kwa misingi ya U-Cuf na Upemba.

Aliendelea kusema kuwa, kwa Chadema mtiririko wa uongozi wao unaonyesha jinsi walivyo watu wa eneo moja, baada ya kumaliza maelezo hayo ilifika fursa ya Lema kuchangia na akasema Chombo anastahili kupigwa risasi.

Akimshambulia zaidi, alisema ingekuwa ni Korea Kaskazini mbunge kama huyo Waziri wa Ulinzi, angeamuru apigwe risasi.

Alionya kuwa kuendelea kuendesha nchi kwa utaratibu wa udini na ukabila kutasababisha taifa kuparaganyika.

Waziri wa zamani wa elimu, Prof. Athumani Kapuya, ametahadharisha kuwa sera ya elimu inayoelekeza Kiswahili kuwa lugha ya kufundishia taasisi zote za elimu itahatarisha amani ya taifa.
 
Alisema sera ya elimu itateketeza amani ya Tanzania  na kwamba yanahitajika  mapinduzi ya elimu.

Here’s What Happened in Nairobi After a MAN Refused to Pay a PROSTITUTE After S£X

$
0
0
Some Kenyan men think that prostitutes do their business for fun but in the real sense, most ladies who trade their flesh in town are single mothers struggling to make ends meet.

A man decided to seek s3x services from a middle aged prostitute in Nairobi and after enjoying the “honey pot”, he vanished without paying his dues.

When the young prostitute decided to chase the shameless man, he vanished in a crowd like lightning. The poor prostitute went berserk and couldn’t believe that she had been duped as eager city residents milled around.

Just watch all the drama that happened in the video below.
Take Care......

Nigerian Godfather or Tanzanian Hanscana To Direct Mapenzi Au Pesa By Nay Wa Mitego ft Diamond

$
0
0
Mapenzi au Pesa(Love or Money) is the new song by Nay Wa Mitego featuring Diamond Platnumz which is currently enjoying airwaves in and outside Tanzania. And two video directors are considered to shoot it's video.
In a new interview with Clouds fm Diamond and Nay said that in Tanzania they have Hanscana in their minds while for outsider director they consider Nigerian Godfather so one of them will work with Diamond and Nay because they want the video to be in great standards.

Aunty Ezekiel na Kajala Masanja Wamseng'enya Wema Sepetu

$
0
0
MASTAA wa filamu Bongo, Aunt Ezekiel na Kajala Masanja, juzikati walikutana na kutumia muda wa takriban nusu saa (dakika 30) kumsengenya aliyekuwa shosti wao, Wema Sepetu.

Tukio hilo lilijiri  hivi karibuni kwenye Bustani za Ndoto Polepole zilizopo Bagamoyo, ambapo mastaa kibao walihudhuria sherehe ya Baby Shower ya Aunt, iliyokuwa imesheheni vituko kibao huku gumzo likiwa ni kutokuwepo kwa Wema.

Awali paparazi wetu aliwashuhudia wawili hao wakimzungumzia Wema tena huku watu wengine wakisikia, kubwa likiwa kumshangaa kwa namna anavyotaka kila anayekuwa rafiki yake, awe adui wa maadui zake.Mjadala huo ulikuwa mkubwa, ambapo Kajala kuna wakati alimuuliza Aunt sababu ya Wema kutokuwepo eneo hilo ndipo alipompa mkasa mzima.

Mazungumzo hayo ya Kajala na Aunt yaliwafanya hata waalikwa wengine kumteta Wema, wakidai kuwa anatakiwa kujiangalia kwani ni staa ambaye hadumu na marafiki zake na mara nyingi wakiachana, huachana kwa ubaya.Ijumaa lilijaribu kuingilia mazungumzia hayo ili kujua kisa cha wao kutumia muda mwingi kumjadili Wema lakini wote waliishia kuguna kisha kuendelea na sherehe hiyo.

Kocha Hans Van Der Pluijm Aacha Ripoti yenye Siri Nzito Yanga Kuhusu Usajili

$
0
0
UKISIKIA fagio la chuma ndilo hili ambalo limepitishwa katika kikosi cha Yanga na kocha mkuu wake, Hans Van Der Pluijm ambaye ameacha ripoti yenye siri nzito.
Kocha huyo Mholanzi ambaye anatarajia kuondoka nchini keshokutwa kuelekea Ghana kuungana na familia yake kwa ajili ya mapumziko, amesema kwamba amekamilisha kila kitu ikiwa ni pamoja na orodha ya wachezaji ambao hawahitaji kwenye kikosi chake msimu ujao.
“Nimetoa ripoti yangu lakini siwezi kukwambia nini nimesema kwa kuwa sina ruhusa ya kufanya hivyo hadi uongozi utakapoipitia na kisha tukashauriana,” alisema kocha huyo.
Hata hivyo, habari kutoka ndani ya klabu hiyo zinasema kuwa moja ya mapendezo ya kocha huyo ni kubakisha wachezaji wawili tu wa kimataifa kati ya waliopo na kufanya usajili mpya wa wachezaji wa kimataifa.
Tayari wachezaji Haruna Niyonzima, Mbuyu Twite mikataba yao lakini taarifa mbalimbali zinadai kuwa Niyonzima tayari amesaini mkataba mpya huku Twite naye akiwa katika hatua za mwisho
Pia Mliberia, Kpah Sherman yeye anatarajia kuondoka kwenda nchini Uswisi hivyo kubaki Amiss Tambwe na Coutinho ambao bado wana mikataba na timu hiyo.
Aidha, chanzo chetu kutoka Yanga kimeeleza kuwa kwa wachezaji wa ndani panga la Pluijm limewakuta wanane (8) huku wengine watatu akishauri watolewe kwa mkopo kutokana na kuwa bado wana mikataba.
Chanzo:Bingwa

I'm Now Dating GK But I Would Love To Have a 2nd Child With Chris Brown: Diva Loveness Malinzi

$
0
0
Hot Radio presenter from Tanzania, Diva Loveness Malinzi wants to have a 2nd child with American superstar Chris Brown. Diva believes her child will be so cute if the father is Chris Brown. Through instagram the controversial presenter who is currently dating Bongofleva artist King Crazy GK shared video of Chris Brown's daughter and she had the below to write.....
What do you think considering Diva is currently in a relationship with GK.....?

Uwoya: Siogopi Maneno ya Watu, Ila Mwacheni Mwanangu..

$
0
0
Kufuatia kitendo cha baadhi ya mashabiki kuwashambulia mastaa kwenye kurasa zao mitandaoni kushamili, Staa wa Bongo Movies, Irene Uwoya ameibuka na kuweka angalizo hili kwa followers wake.

Mamboz! Nataka niulize swali hivi kunamtu nilimlazimisha kuni follow au ni kwa mapenz tuuu? sasa kwanini mtu anataka kuchukua jukumu la mzazi wangu kujifanya anajua sana maisha yangu wakati toka nizaliwe hajawahi kuninunulia ata pipiii!!!

Sasa ni hivi kusemwa mimi siogopi na matus pia siogopi kabisa coz nimeanza kusemwa toka nipo tumboniii!!! Ila naomba sanaaa mwanangu awe pembeni hausiki ata kidogo tena naomba sanaaa fanyeni yote lakin mwanangu chondechondeee!!!

Wewe unaesema na nyota ya mchanga ni kweli ujakosea kwasababu mchanga unadhamani kubwa sana ndomana ukizikwa lazima uwekewe mchanga!

Sasa ambaye anaona amekuja huku ili anitukanie mwanangu naomba atoke haraka staki kuwa nawatu wengi wanafiki nibora kuwa na wachache wenye mapenzi ya kweli na ukikosea wanakwambia kuliko kuwa na wengi kazi yao umbea na majunguuu!!!

STAKI kama unajijua ni mmoja wao fanya usepeee!!!!!

Nadhani ameeleweka, tubadilike jamani
Viewing all 104689 articles
Browse latest View live




Latest Images