Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104774 articles
Browse latest View live

Wanajeshi Walioongoza Mapinduzi Yaliyoshindwa Burundi Wakamatwa

$
0
0
Majenerali watatu waliojaribu kufanya jaribio la mapinduzi nchini Burundi wamekamatwa, lakini kiongozi wao aliyeongoza jaribio hilo la kumpindua Rais Pierre Nkurunziza bado “yuko mafichoni“

Baada ya makabiliano makali ya udhibiti wa makao makuu ya redio na televisheni ya taifa kushuhudiwa jana, barabara za mji mkuu Bujumbura zimesalia kuwa tulivu hii leo.

Rais Nkurunziza ambaye alirejea jana nchini humo kutokea Tanzania, ambako alikuwa akihudhuria mkutano wa viongozi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, wakati jaribio la mapinduzi likiendelea nchini mwake, anatarajiwa kulihutubia taifa wakati wowote kuanzia hivi sasa.

Msemaji wa rais Gervais Abayeho amesema Jenerali mmoja wa polisi na majenerali wawili wa jeshi walikaamtwa kwa kuhusika katika mapinduzi hayo yaliyoshindwa. Ameongeza kuwa mmoja wao alikuwa Waziri wa zamani wa Ulinzi Cyrille Ndayirukiye.

Lakini kiongozi wa mapinduzi hayo Goedfrpid Niyombare ambaye alitimuliwa na Nkurunziza kama mkuu wa ujasusi, hajakamatwa maana hajulikani aliko. Jenerali Niyombare ameliambia shirika la habari la AFP kwa njia ya simu kuwa anataka kujisamilisha, akitaraji kuwa hawatauliwa na vikosi vya serikali.

Jenerali Niyombare aliyeongoza jaribio la mapinduzi Burundi amekwenda mafichoni

Msemaji wa kundi lililoongoza mapinduzi, Zenon Ndabaneze, amezungumza na AFP akithibitisha kuwa wanamapinduzi waliamua kujisalimisha baada ya kukamatwa na polisi. Afisa mmoja wa polisi amesema wamewaweka kizuizini wanajeshi hao waasi ili wawafungulie mashtaka.

Jaribio hilo la mapinduzi linafuatia wiki mbili za maandamano mjini Bujumbura, ambayo waandamanaji kila mara walipambana na polisi, ambao walionekena wakiwafyatulia risasi za moto. Zaidi ya watu 20 waliuawa huku wengine wengi wakijeruhiwa.

Kundi moja la mashirika ya kiraia ambalo liliongoza maandamano hayo ya kumpinga rais Nkurunziza limetoa wito leo wa kuendelea maandamanao.

Gordien Niyungeko naibu kiongozi wa Focode, mojawapo ya mashirika ya kiraia 300 yaliyoandamana, amesema manaandamano yao yataendelea maana kundi lake halihusiki kwa vyovyote vile na jaribio lililoshindwa la mapinduzi.

Kundi moja la vijana katika kitongoji cha Cibitoke, cha mji mkuu Bujumbura, eneo ambalo lilikuwa kitovu cha maandamano, limesema wameonywa na polisi kuwa watachukuliwa kuwa wao ni waasi na watafyatuliwa risasi ikiwa wataandamana.

Nayo Marekani imewaonya raia wake kutokwenda nchini humo na kuwataka wale walioko kule kuondoka haraka iwezekanavyo.

Katika taarifa, Wizara ya Mambo ya Kigeni imesema Burundi inakabiliwa na hali mbaya ya usalama. Imesema kundi la kigaidi la Al-Shabaab limetishia kufanya mashambulizi nchini Burundi na pia huenda likawalenga raia wa Marekani.

Chanzo:DW

Picha ya Waziri Nyalandu Akiwa Amempakata Askari Yafika Bungeni.......Msikilize Mbunge Nassari akiongelea sakata hilo

$
0
0
Waziri Nyalandu akiwa amembeba mmoja wa askari wa  kike.

Kitendo  hicho  kimeonekana  kuwakera  wabunge  ambao  wamepaaza  sauti  na  kuhoji  uhalali  wa  waziri  kumshika  kiuno  Askari  wa  kike....

Hapo  chini  kuna  audio  ya  Mbunge  Nassari  akiongelea  sakata  hilo

Jacqueline Wolper Massawe Anaswa Laivu Bila Chenga Akitoka Ndani ya Jumba la Freemason Dar es Salaaam

$
0
0
Mshtuko! Staa wa sinema za Kibongo, Jacqueline Wolper Massawe ameibua maswali kwa mashuhuda walimuona ‘live’ akiingia kwenye hekalu la watu wa Jamii ya Siri (Secret Society) ya Freemasons yenye nguvu duniani inayohusishwa na imani za kishetani.

TUJIUNGE MTAA WA SOKOINE
Tukio hilo lililoibua kizaazaa kwa mashuhuda waliomuona Wolper, lilijiri juzikati, mishale ya jioni kwenye hekalu hilo lililopo Mtaa wa Sokoine mkabala na Hoteli ya Hyatt Regency, The Kilimanjaro jijini Dar jirani na Benki Kuu ya Tanzania (BoT).

SIMU ZAMIMINIKA
Likiwa kwenye majukumu ya kusaka habari kama kawaida yake, gazeti hili lilipokea simu kadhaa kutoka kwa mashuhuda hao wakiwataka wanahabari wetu kuwahi eneo la tukio.
Kufuatia umbali waliokuwa mapaparazi wetu, ilibidi kuwaomba mashuhuda hao ‘kumfotoa’ picha ambapo mmoja wao alifanya hivyo na kuziwasilisha kwenye meza ya gazeti hili.

ALINASWAJE?
Akidadavua mazingira aliyonaswa Wolper, shuhuda huyo alikuwa na haya ya kusema:
“Kwanza mwanzoni hatukumjua kama ni Wolper lakini kuna dada ambaye anamjua vizuri na ni shabiki wake mkubwa ndiye aliyetuhakikishia kuwa ni Jacqueline (Wolper).

“Kuna waliomuona akiingia. Nilipofika mimi nilimkuta getini anatoka. Walisema hakukaa muda mrefu kwani alitumia dakika kadhaa kisha akatoka na kwenda kwenye gari lake aina ya Prado (Toyota) alilopaki mbali kidogo na lango hilo,” alisema shuhuda huyo kwa sharti la kutotajwa jina na kuongeza:
“Baada ya hapo alitoka nduki maana nzi (watu) walikuwa wameanza kumjalia na kulizingira gari lake.”

WOLPER AJITETEA
Baada ya kuzikagua picha za Wolper akiwa katika mazingira hayo na kujiridhisha kuwa ni yeye, gazeti hili lilimbana mwigizaji huyo ambapo alijitetea:

“Jamani nilikuwa sina hili wala lile. Kuna jengo nilikuwa nalitafuta ndiyo nikajikuta nimetokea maeneo hayo.
“Mimi mwenyewe nilishtuka kuona watu wananiangalia sana kumbe ndiyo nikagundua nipo kwenye lango la Freemasons.”
Risasi Jumamosi: Mbona kuna mashuhuda walikuona wakati unaingia na wakati unatoka?
Wolper: Unajua mimi sikuona kibao chao lakini sikuingia kabisa hadi kule ndani.

Risasi Jumamosi: Lakini kuna madai kwamba wewe ni mwanachama. Unasemaje?
Wolper: Mimi siyo Freemasons, nakumbuka kuna siku watu walinifuata wakaniambia nijiunge Freemasons nitakuwa na mafanikio lakini sijakubaliana nao.

TUJIKUMBUSHE
Mwaka 2012 wakati wa kifo cha aliyekuwa mwigizaji mkubwa Bongo, marehemu Steven Kanumba ‘The Great’ kuliibuka madai ya baadhi ya wasanii ambao ilisemekana ni ‘memba’ wa Freemasons

Mbali na Kanumba, wengine waliotajwa kwenye listi hiyo mwaka huo alikuwepo Wolper na mwanamuziki Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ ambaye madai hayo yamekuwa yakiendelea kumganda huku wengi wakiwa na imani potofu kuwa ukijiunga na jamii hiyo unapata utajiri wa ghafla.

Source:GPL

Baada ya Kupotea kwa Muda: Wema Sepetu Arudi tena Mzigoni Akiwa na JB

$
0
0
Staa mrembo wa Bongo Movies, Wema Sepetu ameshare nasi kipande kidogo cha video ya kazi mpya  inayokwenda kwa jina la  Chungu Cha Tatu akiwa na Staa mwenzake, Jacob Stephen  'JB' wakiwa 'lokesheni'.

Kwa muda mrefu sasa Wema Sepetu amekuwa afanyi filamu, Bila shaka mashabiki wake wana hamu kubwa sana ya kumuona tena kwenye filamu.

Kajala Amrushia Ujumbe Wema Sepetu Ambae Amekuwa Mgumu Kusamehe “Love will save us”

$
0
0
Brigthon Masalu
KAJALA Masanja ambaye ana bifu na aliyekuwa shosti wake mkubwa, Wema Sepetu ‘Madam’ amedaiwa kumpa rafiki yake huyo wa zamani ujumbe unaoashiria upendo kwa kuvaa gauni lenye maandishi yaliyosomeka “Love will save us” yakimaanisha upendo utatuokoa.

‘Katukio’ hako kalinaswa na mwandishi wetu mwishoni mwa wiki iliyopita ndani ya Ukumbi wa New Maisha, Masaki jijini Dar kulikokuwa na onesho la Mrs. Mabeste Charity (mke wa msanii Mabeste) ambayo ilikusanya wasanii wengi wakiwemo Kajala na Wema.

Baada ya mwandishi wetu kushuhudia ujumbe huo mgongoni mwa Kajala huku marafiki zake wakidai ni maalum kwa Wema ambaye amekuwa mzito kusamehe ugomvi wao, alimuuliza kama amemlenga Wema au ni vazi tu alivaa?
“Jamani mimi nimevaa tu, sikumkusudia mtu,” alisema Kajala.Wema na Kajala wamekuwa kwenye bifu la kuchukuliana bwana na bado hawajafikia muafaka.

GPL

Siwema wa Nay wa Mitego Yazidi Kumkuta..Apandishwa Kizimbani Kwa Kosa la Kujipatia Mali na Pesa Kwa Vitisho

$
0
0
Musa mateja
MAJANGA yamezidi kumkuta mzazi mwenzake na Mbongo Fleva, Emmanuel Elibariki ‘Nay wa Mitego’, Siwema Edson ambapo jana alitarajiwa kufikishwa  katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Mwanza, kujibu shitaka la kujipatia mali kwa njia vitisho.

Siwema anatuhumiwa kujipatia mali kwa kumtishia kigogo mmoja serikalini (jina tunalihifadhi) ambaye inadaiwa alikuwa mchumba wake na baada ya kuachana, mrembo huyo kwa nyakati tofauti akawa anamtishia kuwa ana picha zake za utupu hivyo asipompa fedha ataziweka mitandaoni hivyo kigogo huyo alikuwa akilazimika kumpatia.

Chanzo cha habari hii kimeeleza kwamba, baada  ya polisi kujiridhisha na uchunguzi wa madai hayo, waliamua kumpeleka mahakamani ili kujibu shitaka hilo linalomkabili.

“Kesho (jana) wanampandisha mahakamani akajibu shitaka linalomkabili maana polisi tayari wameshamaliza uchunguzi wao hivyo sakata hilo linahamia mahakamani,” kilisema chanzo chetu.

 Alipotafutwa Siwema kwa njia ya simu, simu yake iliita bila majibu lakini alipopigiwa msaidizi wake wa dukani aitwaye Zuhura, alisema:

“Dada (Siwema) jana alikuwa polisi hivyo sijajua kama wamempeleka mahakamani au la!”

Mwishoni mwa wiki iliyopita, Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Mwanza, Naibu Kamishna wa Polisi, Charles Mkumbo alikiri kumkamata Siwema kwa kosa la kujipatia mali kwa njia ya vitisho kisha kumuachia kwa dhamana.

Lowassa Alitikisa Jiji La Arusha.....Mitaa Yafungwa, 'Safari ya Matumaini' Kutangazwa Rasmi Mei 24 Mwaka huu

$
0
0
Shughuli mbalimbali jijini Arusha jana zilisimama kwa muda wakati umati wa watu ulipofurika kumlaki Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa aliyewasili mkoani hapa kwa ajili ya kuendesha harambee ya ujenzi wa Msikiti wa Patandi ulioko wilayani Arumeru.

Lowassa, ambaye jana aliweka bayana kuwa atatangaza rasmi nia yake ya kuwania urais kwa tiketi ya CCM, alienda kuendesha harambee kwenye msikiti huo baada ya kutumwa kumwakilisha Makamu wa Rais, Dk Mohamed Gharib Bilal.

Katika shughuli hiyo ya harambee, Lowassa alifanikiwa kuchangisha Sh235 milioni, ikiwa ni zaidi ya makisio ya msikiti huo ya kukusanya Sh200 milioni.

Harambee zimekuwa zikichukuliwa kama uwanja wa kampeni wa makada wanaowania urais kupitia chama tawala cha CCM na tangu apewe adhabu na wanachama wengine watano, Lowassa hakuwahi kuonekana kwenye uchangishaji fedha hadi wiki mbili zilizopita alipoalikwa na wagombea wengine wa urais wa CCM kwenye hafla iliyofanyika Zanzibar.

Jana, mbunge huyo wa Monduli alipokelewa kwa mbwembwe kwenye Uwanja wa Ndege wa Arusha ambako alilakiwa na umati wa watu, wakiwepo waendesha pikipiki ambao waliongoza msafara hadi viwanja vya msikiti mkuu wa Arusha.

Lowassa alifanya kazi hiyo ya harambee ya kuchangia mradi wa ujenzi wa jengo la ghorofa tano la msikiti huo litakalokuwa na shule ya sekondari, msikiti na kituo cha watoto yatima.

Barabara ya Uhuru, ambayo msafara huo ulipita ukiongozwa na pikipiki za polisi, ilifungwa na wafuasi wa Lowassa, ambao magari yao yalikuwa na nembo za ‘Team Lowassa’ na ‘Lowassa FU’ huku, wengine wakiwa na magari binafsi na waendesha pikipiki.

Lowassa alitua uwanja mdogo wa Arusha saa 7:30 mchana na alifika viwanja vya msikiti mkuu, saa 8:35 mchana na kulifanyika harambee ya kuchangia kituo cha elimu cha kiislam na msikiti wa Patandi na kupokelewa na umati huku wakiimba “rais, rais, rais” na kupokelewa na sheikh wa mkoa wa Arusha, Sheikh Shaaban Juma.

Katika msafara huo, Lowassa aliambatana na kaimu mkuu wa mkoa, Christopha Kangoye, mkuu wa wilaya ya Arumeru, Hasna Mwilima, mbunge wa Kigoma Mjini, Peter Serukamba na mbunge wa viti maalum (CCM) mkoa wa Arusha, Namelock Sokoine.

Pia walikuwepo baadhi ya Wajumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM (NEC) wa wilaya, wafanyabiashara wakubwa wa mkoa wa Arusha, Mwanza na Kilimanjaro, sambamba na watu kadhaa wanaotarajiwa kugombea ubunge katika majimbo ya Arusha mjini, Arumeru Mashariki, Arumeru Magharibi, Monduli, Londigo na Ngorongoro.

Amshukuru Dk Bilal
Akizungumza katika harambee hiyo, Lowassa alisema si jambo dogo kupewa fursa kumwakilisha makamu wa Rais Dk Bilal katika hafla hiyo.


Baada ya Makamu wa Rais kuniomba kuja kumwakilisha hapa,  nilisita kidogo kwanza kutokana na kuwa  hapa ni nyumbani, pia bado nipo kifungoni na pia nimekuwa nikialikwa katika harambee kadhaa za misikiti mkoani hapa na kushindwa kufika,” alisema ambaye amefungiwa kujihusiaha na shughuli za uchaguzi pamoja na makada wengine watano.

Alisema hata hivyo, baadaye alikubali kwa kutambua jambo ambalo anamwakilisha Makamu wa Rais ni la maendeleo kwa wananchi wa mkoa mzima wa Arusha na Taifa.

Avunja ukimya
Lowassa akizungumza na mamia ya watu waliohudhuria katika hafla hiyo, alisema amekuja Arusha akiwa na taarifa njema kuwa, Mei 24 atazungumza neno kwenye Uwanja wa Sheikh Amri Abeid.

Aliwataka wakazi wa Arusha kumuunga mkono, siku hiyo kwa kujitokeza kwa wingi  kumsikiliza.

Mei 24 nitatoa neno siku hiyo na mtu akikuuliza unakwenda wapi mjibu nakwenda kwenye safari ya matumaini,” alisema Lowassa huku akishangiliwa na umati wa watu.

Lowassa alipongeza wakazi wa Arusha kwa umoja wao, wanaoendelea kuuonyesha bila kujali itikadi zao, dini wala rangi, kutokana na kuhudhuria kwa wingi katika harambee hiyo.

Hii ndio Arusha ninayoijua mimi, tumeishi kwa upendo na amani miaka mingi, tusikubali kugawanywa kwani sote ni binadamu tulio sawa,” alisema

 Achangisha 235 milioni
Katika harambee hiyo, zaidi ya Sh235 milioni zilichangwa, wakati Lowassa, Makamu wa Rais na marafiki zake, walichanga Sh105 milioni.

Lowassa alikabidhi Sh50 milioni taslimu kwa sheikh wa mkoa wa Arusha, ikiwa ni mchango wake, makamu wa Rais na marafiki zake huku na kuahidi Sh50500 milioni.

Katika  harambee, hiyo Sheikh wa mkoa, alijisahau na kumuita Lowassa ‘Mh Rais’, na kusababisha umati wa watu kushangilia. Fedha nyingine Sh130 milioni zilichangwa.


Baadhi ya wachangiaji walikuwa ni marafiki wa Lowassa walioongozwa na Mathias Manga, ambaye ni mjumbe wa NEC wa wilaya ya Arumeru, ambao walitoa Sh20milioni, Hussein Gonga Sh7 milioni na Mkandarasi Jeremiah Ayo alitoa Sh5milioni.

Mgombea watarajiwa wa ubunge, Mustapha Panju alitoa Sh6 milioni, Sioyi Sumari (Sh7 milioni), Kim Fute (Sh3 milioni), Philemon Mollel (Sh5 milioni), mbunge Peter Serukamba (Sh3 milioni) na mjumbe wa NEC kutoka jimbo la Busega, Dk Raphael Chegeni alichanga Sh1 milioni sawa na mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema na Namelock Sokoine.

Gharama
Awali akizungumza kabla ya kuanza kwa harambee hiyo, katibu wa Bakwata mkoani Arusha, Juma Masoud alisema kuwa mradi wa ujenzi wa msikiti huo unatarajiwa kugharimu Sh1 bilioni hadi kukamilika.

Alisema kuwa mradi huo ni miongoni mwa miradi mikubwa ambayo wanatarajia kuitekeleza na kwamba ujenzi utahusisha ghorofa tano na ndani yake kutakuwa na kituo cha watoto yatima.

Waumini katika msikiti huu kwa sasa wanakbiliwa na changamoto ya sehemu ya kufanyia ibada hivyo kukamilika kwa mradi huo kutasaidia kuokoa tatizo hilo,” alisema.

Alisisitzia kuwa awamu ya kwanza ya mradi huo unataraji kugharimu jumla ya kiasi cha Sh200 milioni na alimpongeza Lowassa kwa kujitoa katika juhudi za kusaidia maendeleo ndani ya jamii.

Naye Sheikh Shaaban alisema harambee hiyo inahusu wakazi wote wa Arusha kwani sekondari itakayojengwa haitakuwa ya dini moja hivyo, aliwashukuru wote waliochangia na mungu atawalipa.

Nyingine Kali ya Shilole Kiuno Bila Mfupa Hii Hapa

$
0
0

Pozi Kali Kutoka kwa Shilole Kiuno Bila Mfupa Akiwa na Shabiki Wake ...
Una maoni Gani ....

Lulu Asema Nyumba Aliyomzawadia Mama yake si ya Kuhongwa, Amejenga kwa Miaka Minne

$
0
0
Mwanzoni mwa mwaka huu (2015) mrembo na muigizaji wa filamu, Elizabeth “Lulu” Michael aliwa-surprise watu wengi pale alipomzawadia mama yake nyumba aliyojenga Kimara, jijini Dar es- Salaam.

Je Lulu aliwezaje kufanya mambo makubwa kama hayo katika umri mdogo na kwa kipato cha kuigiza peke yake? Hayo ni maswali ambayo wengi walijiuliza, kiasi cha kuwafanya wengine waamini kuwa labda amehongwa.

Lulu amesema kuwa nyumba hiyo alianza kuijenga kidogo kidogo miaka minne iliyopita kwa kile alichokuwa anakipata kupitia kazi yake ya uigizaji, lakini watu wengi hawakufahamu mpaka siku alipoitoa kama zawadi kwa mama yake.

Kiukweli ile nyumba nimeanza kujenga nikiwa bado mdogo sana, ni nyumba ya chini ya kawaida lakini nilikuwa najenga kidogo kidogo, kwamba leo nikipata laki nampa mama leo kaongezee hiki…kwahiyo ni kwasababu mtu hajui atashangaa Lulu kapata wapi hela za vuuup, lakini ni kitu ambacho kimeenda kidogo kidogo imechukua hata miaka minne..kwahiyo mtu atashtuka kwasababu ameiskia leo sasa ndo hivyo mtu ataanza kusema kahongwa hajui background.” alisema Lulu kupitia The Sporah Show.

Wema Sepetu Aeleza Kwanini Hampendi tena Diamond na Kwanini Zari Hamtishi Kwenye Fashion

$
0
0
Wema Sepetu hampendi tena Diamond Platnumz na anasema kila anapoukumbua uhusiano wao, anakumbuka mambo mabaya zaidi kuliko mazuri.

Hapana simpendi [Diamond], yalishaisha hayo, nilishampendega, niliwahi kumpenda sana, lakini hamna tena, yaani hata sishtuki,” Wema alikiambia kipindi kifupi cha Kabali cha EFM.

Nikimkumbuka Diamond most of the things ambavyo ninavikumbuka sio vitu vizuri na ndio maana hata sasa hivi imekuwa hivyo. Vizuri vilikuwepo lakini mtu anaweza akafanya vizuri akaja kufanya kimoja tu kibaya na akaharibu vyote tisa,” aliongeza.

Katika hatua nyingine Wema alisema Zari the Bosslady hamtishi katika sekta ya fashion.

[Zari] hanitishi kwasababu yeye ana taste yake, mimi nina taste yangu, yeye ni Zari mimi ni Wema,” amesema muigizaji huyo. “I got my own, I like to play along with anything and she got her own.

Bar ya Lady Jay Dee ijulikanayo Kama MOG Kufungwa Mwisho wa Mwezi Huu..Mwenyewe Afunguka Haya

$
0
0
Habari iliyotufikia leo hii, kutoka kwa mwanamuziki mkongwe wa r n b nchini, Judith Wambura Mbibo au maarufu kama Lady Jaydee, ni kuhusu kufungwa kwa biashara yake ya Bar n Restaurant aliyokuwa akiifanya kwa takribani mwaka wa nne sasa toka mwaka 2011, bar hyo iliyotambulika zamani kama nyumbani lounge na baadae kubadilishwa jina kuwa Mog n bar restaurant .

Msanii huyo alifunguka kupitia ukurusa wake wa Instagram kuwa ifikapo mwisho wa mwezi huu atafunga biashara hiyo na kuahidi kuja na kitu kizuri zaidi baada ya miezi mitatu ijayo, pia alimshukuru mwenye eneo hilo kwa kumpangishia na kumpa ushirikiano mzuri toka aanze kupanga eneo hilo.

Diamond Amuita Jokate Makombo, Mwacheni Ali Kiba Ajilie

$
0
0
DONGO! Mkali wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’ amemuita mpenzi wake wa zamani Jokate Mwegelo kuwa ni makombo na kudai kama zilipendwa huyo anatembea na hasimu wake Ali Kiba, hakuna jipya kwani anakula makombo.

Diamond ametoa kauli hiyo Jumatano iliyopita wakati mwanahabari wetu alipotaka kujua anajisikiaje kuona wapenzi wake wa zamani Jokate na Wema Sepetu ‘Madam’ wanamuunga mkono Ali Kiba.

Pamoja na kudaiwa kuwa Jokate ana uhusiano wa ‘kimalovee’ na Ali Kiba na mwenyewe kutokubali, ameungana na Wema kuendesha kampeni ya nguvu kwenye mitandao ya kijamii kuhamasisha watu wampigie kura Kiba kwenye Tuzo za Kili 2015 kwa kile kinachoelezwa kuwa ni kampeni ya kuuangusha ufalme wa Diamond kimuziki.

Baada ya mwanahabari wetu kuujua ‘mchezo huo’ uliopamba moto kama moto wa kifuu mitandaoni ndipo alipomuuliza Diamond anauzungumziaje ambapo kwanza alikiri kuufahamu na kudai ameudharau maana hauna jipya.

Hamna jipya waache waendelee kumpigia kampeni (Kiba) lakini mimi nafanya muziki wangu, mashabiki wanafahamu. Kwa hao watoto wa kike, hakuna kipya kwangu si kimuziki hata maisha yao binafsi.

Wema namjua vizuri, Jokate ndiyo usiseme. Mwache huyo Kiba aendelee kula makombo kwa Jokate kama ameamua kipita njia nilizopita si mbaya, inaruhusiwa,” alisema Diamond.

Jitihada za kumpata Jokate ili aweze kufunguka kuwa anajisikiaje kuitwa makombo na Diamond hazikuzaa matuda kufuatia simu yake kuita bila kupokewa, jitihada zinaendelea.

Chanzo: GPL

My Take,
Huku ni kudhalilishana kwa sababu wasanii wa kibongo kuchukuliana ndio fashien. Naye anayemtumia mke wa mtu hali makombo? Ifike hatua nao hawa wasanii wa mwaka 2006 waolewe wawapishe vijana wapya enzi zoo zimeisha wasije kukutwa na ndala wakati wa kuolewa.

Afande Sele: Wabunge Wengi wa Tanzania Wanavuta Mmea

$
0
0
Afande Sele kafunguka kupitia ‪#‎YouHeard‬ ya Power Breakfast Clouds Fm na kusema kuwa wabunge wengi wa Tanzania wanamfuata na kumuomba 'Mmea' wakidhania kuwa yeye bado anavuta. "Mimi huwa nawaelekeza kwa washikaji zangu nnaowajua kisha wao wanaenda kuchukua"

Pia amedai kuwa kuna nchi zilizoendelea na zimepitisha matumizi ya 'mmea' na zinaingiza ushuru wa kutosha kupitia mimea hiyo.

OMG: Batuli Blasts Zari, Aunty Ezekiel And Hamisa Mobeto For The Show Off of Their Naked Baby Bumps

$
0
0
Batuli Yobnesh Yusuph isn't happy with fellow female celebs who put their baby bump on display on social media. Apparently Globalpublishers had a post on their Instagram account asking whether pregnant women showing off their naked baby bump on social media is fashion or just provincialism(ushamba).
Batuli went to comment by blasting Aunty Ezekiel, Zari and Hamisa Mobeto on the post which had the photos of three celebs. Batuli said it is unacceptable and bad behavior for pregnant women showing off their undressed baby bump. Some fans replied Batuli with negative comments but the actress insisted it is not good and there are good things to praise not those ones. Below is what Batuli said........

Andiko Hili la Zamaradi Mtetema Lawagusa Wengi

$
0
0
MAISHA NI SAFARI na lazima WOTE tufike.. haijalishi kwa njia gani sababu kila mtu ana njia yake ya kupita ili kukamilisha safari hii.. kumbuka njia hazifanani sababu kila mtu ana MWISHO WAKE tofauti, hivyo katika hii safari unatakiwa kuwa makini na kuangalia NJIA YAKO TU na sio kuwa na wasiwasi na njia za wengine ama kujaribu kupita/Kuiga njia walizopita wengine..kufanya hivyo Hakutafanya ufike unapotakiwa kufika (kwako) ila utajikuta umefika kwa WENGINE ambako si kwako mwisho wa siku inabidi uanze moja ili kujaribu kufika kwako..

KWANINI USINDIKIZE WENZIO!! ni sawa na kwako kuwe ILALA halafu kwa kukwepa mashimo ukaona upite MBEZI BEACH ambapo uliskia njia ni nzuri kwa kutegemea ufike ILALA, IMPOSSIBLE! Kitakachotokea MBEZI utakaa kwa muda mfupi tu kusubiria MUDA uanze tena safari ya kupatafuta/kurudi ILALA!! WASTAGE OF TIME! This is the BIG reason in my life SIJAWAHI KUSHINDANA NA SISHINDANI, ila NAFANYA..Nafanya kile nachotakiwa kufanya.. bila PRESSURE wala wasiwasi sababu naamini safari ya kwangu ni YANGU!! Ina njia zangu na mwisho wangu..

 Kwa wanaonijua huwaga SINA STRESS NA VITU!! kushindana ni kupoteza mwelekeo wa ya kwangu.. siangalii nani anafanya nini ili nifanye but naangalia natakiwa kufanya nini kwa muda husika,Sioni vibaya kwa mafanikio ya yeyote yule, Naamini nna ya kwangu..SIIGIZI maisha wala kuweka TASWIRA ama ATTITUDE nisiyokuwa nayo..I am who I am!! Nataka mtu anitambue kwa cha kwangu.. kunichukia ama kunipenda iwe kutokana na tabia yangu ya ukweli na sio ile plastic ya kujivisha.. Na kama kuna chochote nnachotakiwa kukipata basi nikipate kwa NILIVYO na sio kwa sira nisiyokuwa nayo ambapo baadae itakapogundulika tofauti ikawa tofauti!! KIKUBWA Dont stress over someone else's life..

RELAX!! sababu hata siku moja Huwezi kubadili ukweli wa KWAKO!! KWAKO HAPABADILIKI.. na hata ushinde na kulala nyumba za jirani lakini mwisho wa siku lazima urudi KWAKO..TENGENEZA KWAKO!! Hakuna mwisho mbaya.. Ila tunautengeneza tunapopita njia tofauti na tunazotakiwa kupita ili tufike, NJIA ZA WENZETU.. Lazima utokee pasipokuhusu ambapo automatic hapatakuwa pazuri KWAKO ila kwa PANAEMUHUSU.. NATAKA NIFIKE KWANGU.

Zamaradi mtetema ambaye ni mtangazaji na muaandaaji wa filamu za kibongo aliandika hayo kwenye ukurasa wake mtandaoni na kungwamkono na watu wengi.

Mwigizaji Riyama Ally Nae Aonyesha Ujauzito Wake...

$
0
0
Staa wa Bongo Movies, Riyama Ally ambaye ni mama wa mtoto mmoja , hivi juzi kati aliwaacha njia panda mashabiki wake mtandaoni baada ya kuweka picha hiyo akionyesha ujauzito na mpenzi wake akiwa ana ubusu.

Riyama alibandika picha hiyo kuandika “………?” kitu ambacho kiliwafanya mashabiki kupoteana kabisa, wapo ambao wadai kuwa mwanadada huyo yupo lokesheni anatengeneza muvi na wenngine kudai kuwa hiyo sio muvi bali ni kweli staa huyo kwasasa ni mjamzito.

Kwa siku za hivi karibuni staa huyo amekuwa akitupia picha kadhaakwenye ukurasa wake  akiwa na jamaa huyo (alimuita  Baba Fatma kwenye moja ya posti zake) akimtambulisha kuwa ndio mwandani wake.

BongoMovies.com imejaribu kumtafuta Riyama ili atoboe ukweli juu ya jambo hili bila mafanikio.

Kama ni kweli, tunakupongeza na kukutakia kheri kwani ni jambo jema.

Mzee wa Ubuyu

Kashfa ya Uchotwaji Fedha za Umma 'Escrow' Yarudi Bungeni kwa Kishindo Baada ya Ikulu Kuwashafisha Baadhi Kiana

$
0
0
KASHFA ya uchotwaji fedha za Umma katika Akaunti ya Tegeta Escrow Sh. 306 bilioni, iliyofunguliwa kwenye Benki Kuu ya Tanzania (BoT) bado haijazimika, licha ya Serikali kujaribu kuwasafisha baadhi ya watuhumiwa ikidai hawahusiki. Anaandika Edson Kamukara … (endelea).
Mbunge wa Kigoma Mjini, Peter Serukamba (CCM) ndiye ameifufua bungeni akisema, kitendo hatua ya Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue, kuwasafisha baadhi ya watuhumiwa wa kashfa hiyo ni ubaguzi na usanii usiokubalika.
Wiki iliyopita, Ikulu ilitangaza kuwasafisha aliyekuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Eliachim Maswi na waziri wake, Prof. Sospeter Muhongo kwamba tume iliyoundwa kuchunguza tuhuma dhidi yao, haikuwakuta na hatia katika suala la miamala ya fedha za Escrow.

Pia, Ikulu kupitia kwa Balozi Sefue, iliwasafisha mawaziri watatu waliojiuzulu kwa shinikizo la Bunge katika kashfa ya oparesheni tokomeza, ikisema licha ya wananchi kupoteza maisha, kuteswa na mifugo kuuawa na askari waliotekeleza oparesheni hiyo, lakini viongozi hao hawakuhusika moja kwa moja.

Mawaziri hao ni Dk. Emmanuel Nchimbi (Mambo ya Ndani), Balozi Khamis Kagasheki (Maliasili na Utalii) na Dk. Mathayo David (Mifugo na Uvuvi).
Ikumbukwe kuwa sakata la escrow liliibuliwa bungeni na mbunge wa Kigoma Kusini, David Kafulila (NCCR-Mageuzi) na baada ya ukaguzi wa Mdhibiti na Mkaguzi wa Fedha za Serikali (CAG) kufanyika, ilithibitika kwamba miamala hiyo ilifanyika kinyume cha sheria huku baadhi ya viongozi wakiwa wamenufaika na mgawo wa fedha hizo.

Akichangia hotuba ya makadirio ya mapato na matumizi kwa ofisi ya Waziri Mkuu kwa mwaka wa fedha 2015/16, katika eneo la utawala bora, Serukamba amesema “hii staili inayojaribu kutumika ni ya kizamani ya kusafisha watu kiani, imepitwa na wakati”.

Huku akisikilizwa na kushangiliwa na wabunge wengi, Serukamba amesema “kama Balozi Sefue anasema Maswi na mawaziri hao ni safi, basi atwambie Andrew Chenge (Bariadi Magharibi), Prof. Anna Tibaijuka (Muleba Kusini), William Ngeleja (Geita), uchafu wao ni upi wakati walipata mgawo halali?"

Chenge, Ngeleja na Victor Mwambalaswa (Lupa), walivuliwa uenyekiti wa kamati za Bunge baada ya kuthibitika kuwa walipokea mgawo wa fedha hizo kutoka kwa mmoja wa wamiliki wa IPTL, James Rugemalira bila kutangaza maslahi kama sheria ya maadili ya viongozi wa umma inavyotaka.

Katika mtiririko huo, mawaziri Tibaijuka, Muhongo na aliyekuwa Mwanasheria Mkuu, Jaji Fredrick Werema walijiuzulu kutokana na kashfa hiyo huku baadhi ya watendaji katika mamlaka mbalimbali za serikali wakifikishwa mahakamani na kwenye Baraza la Sekretarieti ya Viongozi wa Umma.

Akizungumza kwa masikitiko kuhusu uamuzi huo wa Ikulu, Serukamba alishauri kuwa, “Chenge, Ngeleja, Werema, Mwambalaswa na mawaziri wengine waliowahi kujiuzulu kama sehemu ya uwajibikaji nao wasafishwe na kurudishwa katika nafasi zao.”

Bunge hapa tuliomba ripoti ya oparesheni tokomeza lakini haijawahi kuletwa ila anajitokeza katibu mkuu kiongozi kusafisha baadhi ya watu. Huu ni usanii wa kuwasaidia watu wachache na kuumiza wengine kwa malengo binafsi. Hatuwezi kuwa na serikali yenye“double standards”.

Lazima wakina Chenge, Tibaijuka na wengine wote mawaziri waliojiuzulu huko nyuma kwa kashfa ya Richmond nao waundiwe tume wasafishwe kama wakina Maswi, vinginevyo mna ajenda binafsi ya kujisafisha,” amesema.

Serukamba ameongeza kuwa, wako watumishi wa Ikulu (akina Gurumo na wenzie) wenye tuhuma za escrow lakini bado wanaendelea kubaki kazini huku watumishi wengine wa umma katika taasisi zingine wakifikishwa mahakamani kwa jambo hilohilo na hivyo kuhoji hii ni serikali gani yenye ubaguzi wa aina hiyo?

“Kama ni kuunda Judicial Inquiry (Tume ya kimahakama), basi ifanyike kwa watuhumiwa wote. Hiki si Chama Cha Mapinduzi tunachokijua. Sasa kinachofuata hata hao mliowapeleka mahakamani kwa suala hilo watawashinda kutokana na uamuzi huu wa kusafisha baadhi ya watu.

Katibu Mkuu Kiongozi anasema hiyo ripoti ya tokomeza hawezi kuileta bungeni badala yake anaisoma nusu nusu na kuwasafisha baadhi ya watu. Huu ni ubaguzi na labda tuambiwe kuna watu mnaowalenga lakini haitawezekana,” alisisitiza Serukamba na kushangiliwa.

Vera Sidika- My ‘assets’ were not as big when I came to Nairobi

$
0
0
Vera first came to Nairobi in 2008 
I was accompanied by my mother when I first came to Nairobi in September 2008 to join Kenyatta University. On arrival, we went to a restaurant where shockingly, we were served food in foolscaps and nylon papers and had to eat using toothpicks! I thought Nairobians were so selfish and were hiding the forks and plates.

 I mean, we had paid for the food, right? I later came to learn that this was the fast food culture in the city. I had never been to such a busy town. Everyone seemed to be in a hurry, headed somewhere. Honestly, I did not have intentions of staying. My plan was to go back to Mombasa as soon as I finish my studies and ‘chill.’ That changed when I saw how almost everyone around me was juggling day jobs, studies and a myriad of other side hustles.

I also joined the bandwagon and got into modelling. Although my ‘assets’ were not as big as they are presently, people still found me attractive, thanks to my coastal accent. Nairobi men, however, did not impress me.
 They only wanted to get into your pants! And boy, were they aggressive? At first, I thought that the girls in my class were ‘shady’ since they all went to class in high heels. A classroom, for me, was a laid back place where jeans and flat shoes would be ideal. But you know what they say, if you can’t beat them, join them! I did, and outdid them. I was the flashiest of them all! Vera Sidika spoke to Cate Mukei

Photos: Aunty Ezekiel Sharing passionate Kisses With Boyfriend Moze Iyobo

$
0
0
Some say Aunty Ezekiel didn't do justice to herself by dating Moze Iyobo who is a dancer of Diamond Platnumz but Aunty herself doesn't care since she gets what she wants from Iyobo. Aunty went far by getting Moze's pregnancy and she recently had a baby shower in Bagamoyo, guess what...they gifted hot kisses to one another. These are some pics...

Here Moze showing other men how to hold and touch woman's baby bump.......

Photos From Diamond Platnumz' Interview With BBC In London

$
0
0
Superstar Diamond Platnumz took flight from Dudai to London, and while in London he had interview with BBC. Here are some pics .......

Viewing all 104774 articles
Browse latest View live




Latest Images