Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104429 articles
Browse latest View live

Kiwango Stars Stars Chakera Watanzania..Wadau Wataka Kocha Afukuzwe..Sasa Wamkumbuka Maximo

0
0
Taifa Stars Imefungwa Michezo yote mitatu kwenye michuano ya Mataifa ya Kusini mwa Afrika (Cosafa) ,Matokeo hayo yamewaumiza Watanzania wengi nchini, ambapo mara baada ya kumalizika mechi hiyo kwenye mitandao mbalimbali ya kijamii, watu wengi wamelaumu kiwango kibovu kilichoonyeshwa na Stars.

“Siku zote kila mtu anavuna alichopanda, Taifa Stars wamevuna walichopanda, timu inachaguliwa kwa upendeleo, wachezaji waliofanya vizuri na wenye uwezo hawachaguliwi ukiuliza au ukiongea wanasema kocha anajua tumwachie, hebu tujiulize huyu kocha ana uchungu kweli na kipigo anachopata kuliko sisi Watanzania?” alihoji Charles Mayilla kupitia mtandao wa facebook.

Kipigo hicho kinakuja wiki chache mara baada ya wapenzi wengi wa soka nchini kulalamikia uteuzi wa kikosi wa Kocha Mkuu, Mart Nooij, ambaye ameendelea kuwaita baadhi ya wachezaji wanaokaa benchi kwenye timu zao huku akiwaacha wale waliofanya vizuri.

Baadhi ya wachezaji aliosafiri nao na wamekuwa wakiwekwa benchi kwenye mechi nyingi za timu zao msimu uliopita wa Ligi Kuu Tanzania Bara (VPL) ni kipa Deogratius Munishi ‘Dida’ (Yanga), Mwadini Ally (Azam), Hassan Dilunga (Yanga) na John Booco (Azam), aliyesumbuliwa na majeraha ya mara kwa mara.

Makocha wanena

Akizungumza na MTANZANIA kocha mkongwe visiwani Zanzibar, Hemed Morocco, anayeinoa timu ya taifa ya huko ‘Zanzibar Heroes’, alisema hakuna njia ya mkato ya mafanikio kwa Stars, amedai lazima iachane na wachezaji wazee na kutengeneza kikosi bora cha vijana.

“Kila siku matokeo yetu yamekuwa ni kufungwa, mimi naona bado tunakurupuka, tunakumbatia timu ile ile ya wazee, Tanzania ina wachezaji wengi vijana waliobarikiwa vipaji, tukitaka kufika mbali tutengeneze kikosi bora cha vijana wenye umri wa miaka 17 ambacho baada ya miaka minne kitatupa mafanikio,” alisema.

Naye kocha mzoefu nchini, Kennedy Mwaisabula, alisema matokeo ya Stars dhidi ya Swaziland yametokana na kupwaya eneo la ushambuliaji waliopoteza nafasi kadhaa za wazi, huku akipata shaka kwenye safari ya timu hiyo kufuzu Mataifa ya Afrika (AFCON) 2017 na Mataifa ya Afrika kwa Wachezaji wa Ndani (CHAN).

“Uteuzi wa kikosi ndio unaiangusha timu, si vibaya kocha kuita kikosi chenye sura zile zile, lakini lazima tuangalie ya kuwa kikosi anachoendelea kukiita kina mafanikio, kama hakina mafanikio kocha lazima abadili kikosi na kujaribu wachezaji wengine, tunaona hapo amewaacha wachezaji bora kwenye ligi kama mshambuliaji Mandawa (Rashid), Malimi Busungu yule wa Mgambo, full back Kessy (Hassan),” alisema.

Alisema ipo haja kwa kocha wa Stars, Nooij kupata usaidizi mzuri wa ushauri kwa makocha wazawa ambao wanawajua vizuri wachezaji wa hapa, huku pia akieleza lazima Mholanzi huyo awe na mahusiano mazuri na makocha wa timu za Ligi Kuu.

“Kuna makocha wakongwe kabisa nchini kama mzee Kibadeni (Abdallah) na Mshindo Msolla, lazima watumiwe kwenye ushauri kwani wameipatia nchi mafanikio, kingine kocha inaonekana hana mahusiano mazuri na makocha wa ligi, kwani hata uteuzi wake amekuwa akiita wachezaji wagonjwa, hivyo lazima aimarishe mahusiano kwani wachezaji wanatoka kwenye klabu,” alisema.

Taifa Stars enzi za Maximo ilikuwa Team ya Kuogopwa sana yaaani mpaka sasa wadai tunataka kocha afukuzwe tu hata wapewe watanzania labda mambo yatabadilika...

JB Atoa Tahadhari Kuhusu ya Matapeli Hawa

0
0
Tahadhari: kuna watu wametengeneza akaunti feki yenye picha zangu.na wanasema kwamba Jerusalem inahitaji wasanii wapya.na wanawapigia simu watu huku wakiwatoza kiasi cha tsh 45000 hadi laki kama ada ya kujiandikisha.watu hawa ni matapeli.na wamechukua hela nyingi kwa watu.jamani hatuna utaratibu huo na usikubali kutoa pesa...Fb watu wanaitumia vibaya sana..

By:JB on Instagram

Washindi wa Tuzo za Watu Hawa Hapa, Wema Sepetu na Ali Kiba Ndani

0
0

Hii ni orodha kamili ya washindi

Mtangazaji wa redio anayependwa

D’Jaro Arungu – TBC FM

Kipindi cha redio kinachopendwa

Papaso – TBC FM

Mtangazaji wa runinga anayependwa

Salim Kikeke – BBC Swahili

Kipindi cha runinga kinachopendwa

Mkasi – EATV

Blog/Website inayopendwa

Millardayo.com

Muongozaji wa video anayependwa

Hanscana

Muongozaji wa filamu anayependwa

Vincent ‘Ray’ Kigosi

Muigizaji wa kike wa filamu anayependwa

Wema Sepetu

Muigizaji wa kiume wa filamu anayependwa

Hemedy PHD

Mwanamuziki wa kike anayependwa

Lady Jaydee

Mwanamuziki wa kiume anayependwa

Alikiba

Filamu inayopendwa

Kigodoro

Video ya muziki inayopendwa

Nani kama Mama – Christian Bella f/ Ommy Dimpoz

Anayolalamikia Reginald Mengi Kama ni Kweli, Tunaelekea Kwenye Udikteta Usiomithilika

0
0
Serikali inaweza kuingia katika mgogoro usio wa lazima na vyombo vya habari wakati huu nchi inapokaribia kufanya uchaguzi Mkuu, iwapo miswada ya Huduma ya Vyombo vya habari na wa Sheria ya Haki ya kupata Habari itapitishwa bila kufanyiwa marekebisho.

Mwenyekiti wa Wamiliki wa vyombo vya Habari nchini – MOAT Dr Reginald Mengi ametoa tahadhari hiyo jijini Dar es salaam wakati akizungumza na waandishi wa habari baada ya mkutano wa Mashauriano ya Amani na Utulivu nchini, na kusisitiza kuwa kupitishwa kwa miswada hiyo kutasababisha ukiukwaji mkubwa wa Uhuru wa Habari, uvunjifu wa amani, na ni kifo kwa vyombo vya habari binafsi nchini.

Akitolea mfano, Dr Mengi ambaye pia ni Mwenyekiti Mtendaji wa IPP amesema kifungu nambari 14 cha muswada wa sheria ya Huduma za Vyombo vya habari kinatoa amri kwa vituo binafsi vya Utangazaji kujiunga na chombo cha habari cha umma kwa ajili ya Taarifa ya habari ya kila siku saa mbili usiku, kinyume na ilivyo sasa, na ni dalili za kurudi tulikotoka.

Nimewahi Kuwa Changudoa wa Kujiuza ili Nipate Pesa za Kujikimu Nairobi, Sasa Nataka Kuolewa, Je Nimjulishe Mchumba Wangu?

0
0
Ilikuwa hivi baba na mjomba waliwekwa korokoroni kwa kesi ya ujambazi tukiishi na kusoma arusha mimi na wadogo zangu wawili kuna siku gafla kama saa nne mama akaja shuleni (day skuli) akatuchukua (wawili, mdogo alikuwa hasomi) bila kupitia nyumbani tukaelekea tanga tukakaa hotelini for two weeks then tukaelekea Kenya Nakuru ambapo mama alinunua nyumba na gari tukaanza maisha bila ya baba na mjomba.

Wote watatu tukapelekwa boarding skuli Nairobi-Kenya, mama akarejea nakuru miaka minne baadae mama akakamatwa akarejeshwa arusha kuunganishwa kwenye kesi, mimi ndiye nlikuwa mtoto wa kwanza na woote hatukuwa tumejua kama mama kakamatwa mpaka tuliporudi nyumbani likizo.

Majirani walitushangaa na kuanza kutuuliza alipo mama, kwa msaada tukavunja mlango gari ilikuwepo kuna chumba ilikuwa inafungiwa nliwaambia wadogo zangu mama kaenda kumsalimu mjomba atarejea. Nikaanza misele Nakuru mjini na kiboyfriend changu, siku mmoja akaja mama fulani nlipokuwa nimepaki kigari mjini akajitambulisha ni Mtanzania mmarangu na aliongea kichagga nikazuga simsikii.

Akaniambia amenitambua kwa kuwa anaifahamu gari ya mama na anajua mama na nimefanana na mama.Akanieleza kuhusu mjomba,baba na akaniambia mama alikuwa gerezani arusha kwa kesi. Akanitaka niiuze gari na nyumba fasta kabla havijakamatwa. Akaniambia nsiwe narudi rudi kukaa muda mrefu pale nyumbani mpaka atakapoachiwa mama nlikuwa form three-Nairobi, four days baadae niliuza gari, nyumba ikagoma kwa kuwa collateral ya mkopo alichukua mama benki. Nikawaamuru Madogo tuondoke tuwahi kurudi shuleni mama anatusubiri Nairobi.

With time hata mwaka haukuisha hela ikakata nikashawishiwa na a classmate Elizabeth-Mkenya mkamba wa Nairobi
tukaanza kujiuza likizo and life ikasonga na nikawa nawalipia wadogo na mimi ada. Nilijiuza mpaka nikasoma chuo na wadogo wakaingia sekondari thank god mama aliachiwa baada ya mitatu miaka kuna wakati tuligombana sana na wadogo zangu wakiamini mama amenipa access ya akaunti zake za benki na natumia hela nyingi kivyangu huku nikiwapa wao kidogo.

Tatizo: Kwa sasa tupo Arusha nina boyfriend mmasai na kila wakati wa semina kanisani mchungaji husema ni bora wapenzi wachumba muwekane wazi kuhusu maisha yenu hata ya nyuma ili isiwagharimu baadae. Naogopa sana kumwambia jamaa kuwa niliwahi kuwa nilikuwa changudoa.

NOTE:KUNA WADADA WAKENYA AMBAO NLIJIUZA NAO WAMEHAMIA ARUSHA NA HAWANA KAZI ZA MAANA, nlilazimika kuhama kanisa ambalo mimi nlikuwa kiongozi wa vijana baada ya baadhi yao kuanza kusali pale kanisani uamuzi ambao BF na mchungaji wanaushangaa mpaka leo.Kwa sasa nasali kikanisa kidogo njee ya mji kwa kuwaogopa washirika uchangudoa wenzangu wa NAIROBI...nateseka sana kuwaza

Zari wa Diamond Ateswa na Picha Inayoonyesha Akiwa Beneti na Pedeshee Katunzi

0
0
MUSA MATEJA
MCHUMBA wa Mbongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’,  Zarina Hassan ‘Zari’ amedaiwa kuangua kilio baada ya kuvuja kwa picha yake na mfanyabiashara maarufu jijini Dar, Mzamili Katunzi ambayo ilidaiwa kuwa ni mtu wake na kusababisha gumzo mjini.

Mtu wa karibu na Zari amefunguka kuwa Zari alijisikia vibaya sana baada ya kuona picha hiyo na kukasirika hivyo kuanza kuwasaka watu walioivujisha kwani walikuwa na nia mbaya ya kumgombanisha lakini wamechemka.
Zari kamaindi kweli, anajiuliza huyo aliyeivujisha alikuwa na lengo gani?” alisema mtu huyo

Jitihada za kuzungumza na Zari hazikuzaa matunda lakini bahati nzuri Diamond alipatikana na kufafanua:
 “Ni kweli zimemsumbua baby lakini nimemuweka sawa kwa kuwa najua ni mambo ya mitandao, hakuna ukweli wowote.”

Kajala 'Skendo za Kutengenezwa Juu Yangu Zinamnyima Raha Mtoto Wangu, Wenzake Humnyooshea Vidole Kila Wakati Kwa Taarifa zisizo Sahii'

0
0
Staa wa Bongo Movies, Kajala Masanja ameweka wazi kuwa mipango yake ya kuzaa watoto iko palepale na kwamba safari hii angependelea kuzaa watoto mapacha.

licha ya kwamba Kajala ana binti yake aitwae Paula,atahakikisha anamtafutia wadogo zake kwani hata yeye amekaa kweny falimia ya watoto wengi na angependelea na yeye kuwa na familia kubwa.Kajala amebainisha kwamba hafikirii kupata mtoto na mme wake ambae kwa sasa yuko gerezani bali anatafuta mwanaume mwenye malengo ya maisha na mwenye kujali familia.

Licha ya kuwa na mipango yote hiyo Kajala ameelezea ugumu anaoupata katika lengo lake la kuilea hiyo familia kwani hadi sasa binti yake paula anakosa raha kutokana na skendo zinazotengenezwa dhidi yake.Amesema hali hyo iimekua inamnyima raha binti yake huyo hata anapokua shuleni kwani wenzake humnyooshea vidole kila wakati kutokana na taarifa ambazo alisema si sahihi kuhusu mama yake..

Mwananchi

Nyumba Anayoishi Ali Kiba Yazua Utata..Yadaiwa si yake Bali Kapewa Kuishi tu na Mrembo Amazing Anayeishi Singapore

0
0
Musa Mateja
Mjengo anaoishi mkali wa Bongo Fleva anayetamba na ngoma yake ya Chekecha Cheketua, Ali Saleh Kiba uliopo Kunduchi-Mbezi Beach jijini Dar, unadaiwa kuzua utata mkubwa hivyo kulilazimu Risasi Jumamosi kuchimba na kubaini kuwa nyumba hiyo si ya msanii huyo bali amepangisha.

Awali, Kiba alikaririwa akisema kuwa, mjengo huo wa kifahari ni wa ndugu yake aliyepo nje ya nchi ambaye alimpa ili aishi na ndugu zake (wa Kiba) wakati yeye (mmiliki) akiwa hayupo.Siku kadhaa mbele, baada ya Kiba kuvamiwa nyumbani hapo na watu kupora vitu huku akinusurika kuuawa, jamaa huyo alikaririwa redioni na kwenye mitandao ya kijamii akisema kuwa nyumba hiyo ni yake.

Ilidaiwa kwamba, mara tu baada ya Kiba kutangaza kumiliki nyumba hiyo, ilidaiwa kuwa aliibuka mwanamke aliyetajwa kwa jina moja la Mariana ikisemekana eti ndiye mmiliki halali wa nyumba hiyo.Madai mazito yaliendelea kushushwa kwamba, Mariana, akiwa mwandani wa Kiba ndiye aliyemuweka Kiba aishi kwenye nyumba hiyo wakati yeye (Mariana) kwa sasa anaishi nchini Singapore barani Asia.

Ninyi mnasema ule mjengo ni wa Ali (Kiba)? Acheni hizo, kwa taarifa yenu hiyo nyumba kapewa na mrembo f’lani hivi amazing, anaitwa Mariana, ni Mbongo anayeishi Singapore.

Muulizeni huyo Kiba awaambie ukweli,” kilisema chanzo chetu kikisisitiza: “Hata Mariana aliposikia eti nyumba ni ya Ali (Kiba) alishangaa na akamaindi ile mbaya hivyo kwa sasa sidhani kama wanaelewana kwa ajili hiyo.

Baada ya kukutana na mkanganyiko huo, gazeti hili lilimtafuta Kiba ambaye alikiri kwamba kweli nyumba hiyo siyo yake bali amepangisha huku akikana kusema kuwa anaimiliki.Alipoulizwa juu ya madai ya kupewa nyumba hiyo na mwanamke aitwaye Mariana, Kiba alisema hayo ni maneno tu kwani anachojua yeye amepangisha.

“Kwanza hebu nitumie picha nijue ni nyumba gani?” aliomba Kiba ambapo alitumiwa picha kwa WhatsApp ndipo akajibu:
Okey, kama ni hiyo nimepangisha lakini siyo kwamba sina nyumba.”
Source:GPL

Here Is The Name of Aunty Ezekiel And Moze Iyobo's Daughter.

0
0
Yesterday actress Aunty Ezekiel who was pregnant of Moze Iyobo gave birth to a baby girl. Their daughter is named Cookie...

Congratz to them.......

Photos: Wema Sepetu's Look At Tuzo Za Watu 2015

0
0
Here is what Wema Sepetu wore to Tuzo Za Watu 2015, she also won favorite actress award.....

Atimae Zitto Kabwe Achukua Form ya Kugombea Ubunge..Unataka Kujua Atagombea Wapi ? Soma Hapa

0
0
Safari ya mbunge wa zamani wa Kigoma Kaskazini kwa tiketi ya Chadema, Zitto Kabwe kurejea bungeni imeanza rasmi baada ya kiongozi huyo wa chama kipya cha ACT-Wazalendo kuchukua fomu za kuwania kuongoza jimbo la Kigoma Mjini.

Uamuzi huo wa kulitaka jimbo hilo unathibitisha kauli zake ambazo amekuwa akizitoa kwa muda mrefu kuwa hatarudi tena Kigoma Kaskazini kwa kuwa alishawatimizia kila kitu na haoni sababu za kuwawakilisha tena wananchi wa eneo hilo.

Kauli yake iliibua ubashiri kuwa Zitto anataka kubadilishana jimbo na mbunge wa Kigoma Mjini (CCM), Peter Serukamba, uvumi ambao aliukanusha akisema hadhani kama CCM inaweza kupata jimbo Kigoma.

Zitto, ambaye alijiondoa Chadema baada ya kukiuka katiba kwa kufungua mashtaka dhidi ya chama hicho, hakufanya mbwembwe wakati akienda kuchukua fomu kwenye ofisi za ACT Ujiji jana, badala yake aliita viongozi wa kata na matawi bila ya kutaarifu vyombo vya habari.

Nimeamua kugombea ubunge wa Kigoma Mjini ili niwatumikie ndugu zangu ambao wamekuwa wakipata tabu katika kupigania haki zao za msingi ambazo walistahili kuzipata kama ilivyo katika mikoa mingine,” alisema Zitto alipoongea na mwandishi wa Mwananchi kwa simu.

Nitakapokuwa mbunge wa Kigoma Mjini nitahakikisha barabara za mitaani zinapitika katika kipindi chote cha mwaka, nitahakikisha watu wanaacha tabia ya kulima mashamba katikati ya mitaa na makazi, lakini nitahakikisha kila mmoja anajiunga na mifuko ya kijamii ili kujiwekea akiba ya uzeeni pamoja na kupata huduma ya matibabu, elimu na nyinginezo zinazopatikana kwa kutumia mifuko hiyo.”

Mwenyekiti huyo wa zamani wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC), alisema bonde la Mto Luiche bado halijatumika ipasavyo kuzalisha chakula kwa wingi.

Nakusudia kuibana Serikali ijenge skimu ya umwagiliaji maji ili wakulima walime kilimo cha mpunga kwa mwaka mzima bila kupumzika, jambo ambalo litainua uchumi wa wakulima na kuongeza chakula hapa Kigoma,” alisema.

Kuhusu umeme wa gridi ya Taifa, Zitto alisema lazima upatikane ili kusaidia jitihada ya ujenzi wa viwanda vya kusindika mazao ya uvuvi na kilimo kwa kuwa hivi sasa mji wa Kigoma Ujiji unategemea umeme wa jenereta ambao hauwezi kuendesha shughuli za viwanda, hali inayochangia mkoa kuendelea kuwa masikini licha ya kuzungukwa na rasilimali nyingi.

Katibu wa ACT wa Jimbo la Kigoma Mjini, Azizi Ally alisema Zitto alichukua fomu hiyo jana kwa malipo ya Sh100,000 mbele ya viongozi 72 wa kata na matawi kutoka jimboni humo.

“Kwa hali ya sasa Kigoma Mjini inahitaji kupata mbunge anayeweza kufuatilia mambo kwa kina ili kuleta maendeleo ya wananchi baadala ya yule anayekwenda bungeni kujifunza,” alisema Ally.

Watu wanakabiliwa na kero mbalimbali kama ubovu wa barabara za mitaani, uhaba wa umeme wa uhakika unaoweza kuendesha viwanda vikubwa na vidogo, pamoja na wengi kufanya kilimo cha kujikimu zaidi.“

Zitto alitofautiana na uongozi wa juu wa Chadema uliomtuhumu kuwa alikuwa amefanya uasi na kwamba alishaanzisha chama kingine akiwa ndani ya chama hicho kikuu cha upinzani na kusababisha avuliwe nyadhifa zote, ikiwamo ya unaibu katibu mkuu.

Hata hivyo, wakati Chadema ikijiandaa kumjadili na pengine kumvua uanachama, Zitto alifungua kesi akitaka mahakama imuamuru katibu mkuu wa Chadema ampe nyaraka za mwenendo wa vikao vilivyomvua madaraka na kuomba amri ya kuzuia vikao hivyo visimjadili.

Katika hukumu ya kesi hiyo, mahakama ilitupilia mbali hoja zake, uamuzi uliotafsiriwa kuwa umefungua njia ya kutimuliwa kwake kwa kitendo cha kufungua kesi mahakamani kinyume cha katiba.

Mkazi wa Gungu mjini Kigoma, Zuberi Mrisho alisema ujio za Zitto kugombea Ubunge wa jimbo hilo utaamsha ari ya wananchi kujiandikisha kwa wingi katika Daftari la Wapigakura na kujitokeza kupiga kura tofauti na chaguzi zilizopita.

Mwaka 2010 Vijana wengi hatukupiga kura hapa kwa sababu tulikosa imani na baadhi ya wagombea wa nafasi mbalimbali, lakini kwa ujio wa Zitto sasa nina hakika wengi tutajitokeza kupiga kura ili tupate viongozi makini kwa maslahi ya mji wetu,’ alisema Mrisho.

KENYA:RUTO’s Lawyer Wants to Marry OBAMA’s Daughter - Here is What He is Offering as Bride Price

0
0
A lawyer associated with Deputy President William Ruto is preparing to propose to US President Barrack Obama’s daughter, Malia, when the Obamas visit Kenya in July.

Speaking to one of the local dailies, Felix Kiprono Matagei said that he is ready to meet Barrack Obama and Michelle Obama to discuss the matter when the US President visits in July.

“I got interested in her in 2008. As a matter of fact, I haven’t dated anyone since and promise to be faithful to her. I have shared this with my family and they are willing to help me raise the bride price,” Kiprono said.

The young lawyer, who hit the headlines when he moved to court seeking to have William Ruto sworn in as President when Uhuru travelled to The Hague for his International Criminal Court (ICC) case, claims his love for Malia is real and not infatuation.

“People might say I am after the family’s money, which is not the case. My love is real,” Kiprono said adding that, “I am currently drafting a letter to Obama asking him to please have Malia accompany him for this trip. I hope the Embassy will pass the letter to him. I will hand it over to the US Ambassador with whom we have interacted several times.”

The controversial lawyer said he is ready to pay 50 cows, 70 sheep and 30 goats as bride price.


The Kenyan DAILY POST

Diamond: Tumeshapima DNA na kujua mtoto ni wa kike

0
0
Bwana mdogo Huyu alipokuwa anahojiwa na mtangazaji wa BBC na kuulizwa swali kama ameshajua Jinsia ha mtoto kwa kushangaza kabisa alijibu yes tumeshapima DNA na kujua mtoto wa ni wa kike.ushauri wangu kwa Dogo kwa kusema ukweli ame emprove sana kwenye Lugha Ila tatizo ni mbwembwe na uongo akiacha Uongo na mbwembwe lazima tutegemee makubwa zaidi toka kwake.

Lemutuz Apinga Matokeo ya Tuzo za Watu Adai Matokeo Yamepangwa..Ali Kiba Hawezi Mshinda Diamond Kwa Kupendwa

0
0
Kama mjuavyo hakuna tunzo inayo kosa mikasa na maneno na hii uonesha jinsi tunzo zinavyo wagusa wengi!

Na Tunzo iliyokuwa ina wagusa wengi ni tunzo ya msanii wa kiume anaye pendwa na wengi ambayo imekwenda kwa msanii Alikiba!
Baada ya utoaji wa tunzo huo wengi wamesema na kunena lakini leo hii kuna kitu kipya kimezuka ambacho kinaweza kuwa kivutio kwa wengi na wengi watatamani kujua kilicho nyuma ya haya yote!

Mh Lemutuz au Sauti ya Umeme amesema wazi kabisa kwenye Tunzo za watu haki haikutendeka kabisa na hakuna msanii anayependwa Tanzania zaidi ya Diamond!

LEMUTUZ AMEANDIKA HAYA KUHUSU TUZO HIZO:

Well, thank "Tuzo za Watu" for the best Show but I have a big problem kuamini kwamba1. Millardayo hakupata zawadi zote isipokuwa ya Blogu tu 2. Ali Kiba ameshinda Tuzo ya Mwanamuziki anayependwa against The King Of Pop in East Africa 3. Mzee Majuto kashindwa kupata hata zawadi moja.....nilichokiona ni Manouver and Manipulation by somebody very powerful behind the scene anayetaka ku create a balance katika Field ambayo ni unbalanced by Nature and TALENT in the end ni kuvuruga competititon ambayo tayari ipo na kuwakatisha tamaa waliofanikiwa kwa VIPAJI VYAO...the Idea inatakuwa kuwa ni kupiganisha Vipaji uwanjani sio ku balance the Field from somebody's Office....mapokezi ya Diamond leo Mwanza na LONDON WIKI ILIYOPITA ni EVIDENCE ya kutosha kwamba HAKUTENDEWA HAKI NA TUZO ZA.LEO.....ninawaheshimu sana watayarishaji wa Show ya leo lakini NAOMBA KUKUBALI KUTOKUBALIANA NANYI na we remain kool SIAMINI KWAMBA MATOKEO YA LEO YALIKUWA FAIR na nitashukuru sana kuona process iliyotumika kufikia matokeo ya leo!

...UPDATE: well nimesoma arguments nyingi against my prior post kuna wachache sana wanaojaribu ku make a sense lakini at the end of the heart of all the TRUTH STANDS alone kwamba kulikuwa na unfairness I mean eti KING MAJUTO ana mpinzani Tanzania? Please eti Millardayo ana mpinzani Tanzania? Diamond Platznumz ana mpinzani Tanzania? hahahahahahah that is a joke infact the biggest joke of my life...I mean wananchi wanajaa kwenye Show za Diamond kuliko za Wasanii wote Tanzania lakini hawakumpigia kura? hahahahha ninasema that is.the biggest joke of all the times Diamond ana followers wengi Instagram na FACEBOOK kuliko MTANZANIA YOYOTE ALIYEWAHI KUISHI.HAPA NCHINI lakini hawakumpigia kura? hahahahahha kuna mtu hukoooo anataka niamini that! hahahahah wanannchi wamekubali kununua meza kwa Shillingi Millioni Tatu kumuona Diamond lakini hawakumpigia kura? Ipi ni kazi ngumu kupiga kura kwenye simu au kulipia meza Shillingi Millioni Tatu?......I mean hata aliyetaja washindi alikuwa anatetemeka kutaja kushindwa kwa Diamond WHY? hahahahaha baada ya Category ya Diamond kupita ilikuwa ni rahisi kutabiri the rest of the TUZOS kila mtu alijua mapema kuwa Millard ameshinda blog WHY?....KIPAJI kinatakiwa kushindanishwa na KIPAJI sio otherwise....sina muda wa kujibu low arguments za Yanga na Simba eti mtumzima.na akili zako.unaweza kusimama na kusema Mwanamuziki anayependwa Tanzania sio Diamond eti kuna mwingine! hahahahahahahha namshukuru Mungu kwa kunijalia kwenda Shule niliyoyaona leo ni aibu tupu na ndio mwanzo wa kuua vipaji soon tutaanza tena kuwarudia kina Kandabongo Man ambaye huko kwao huwa.anapiga bure kwenye harusi...sio kosa la Diamond kwamba amewaacha wasanii wenzie maili 20 ni kosa la KIPAJI CHAKE kipaji hakitengenezwi na TUZO ila kukubalika na wnanchi ninasema DIAMOND NDIYE MWANAMUZIKI ANAYEKUBALIKA.KULIKO WOTE TANZANIA NI FACTS NA MIFANO IPO WAZI ni maoni yangu kama huyakubali andika FACTS sio ushabiki wa Yanga na Simba! - le Mutuz

Lemutuz: Aliyevuruga Matokeo ya Jana Tuzo za Watu Yupo Busy Pia Kuvuruga Matokeo ya KTMA, Nitamtaja Laivu

0
0
lemutuz_nation 'Well, huwa ninaongea na FACTS with EVIDENCE toka jana Usiku nimesema I smell fish kama nilivyo smell Fishy kwenye matokeo ya Miss Tanzania ya Mwaka jana kuna wajinga akili ndogo walioanza kunirushia matusi LE AKILI KUBWAZZZZ now ninasema jana HAKI HAIKUTENDEKA kuna wanaojaribu kuninyamazisha na matusi...great ninarudia tena sikuenda Shule kuwa mjinga so toka jana niliingia kwenye uchunguzi wa FACTS and EVIDENCE of WHO IS BEHIND LAST NIGHT MESS tayari nimeshaanza kupata the TRUTH....tena the TRUTH ni aliyevuruga jana yupo busy pia kuvuruga Matokeo ya KMTA....soon nitakuwa na "LE TAMKOZZZ FOUR LIVE" and I mean it...stay tuned hahahaha U know makelele yangu toka jana yameleta kizungu zungu behind the scene wameshaanza kuvurugana na kunipigia niache hahahaha..now stay tuned NITAMTAJA ALIYEVURUGA SHOW YA JANA NA FACTS and EVIDENCE....na I HOPE NITASAIDIA KUTOVURUGWA KWA KTMA maana ni huyo huyo gademu mazafantazzz! Na the good thing watayarishaji hawakuhusika kabisa so stay tuned! - le Mutuz


Mwalimu na Wenzake Watano Wakamatwa na Mifupa ya Albino Walikuwa Wakiiuza Milioni Mia Sita

0
0
WATU sita, akiwemo Mwalimu wa Shule ya Msingi Katunguru iliyoko Kata ya Wendele, Tarafa ya Msalala wilayani Kahama, wamekamatwa mjini hapa wakiwa na vipande sita vya mifupa inayodhaniwa kuwa ya albino.

Taarifa zilizopatikana mjini hapa zimeeleza kwamba, mwalimu huyo Bahati Kilungu Maziku (56), Msukuma na mkazi wa Mtaa wa Mbulu katika Halmashauri ya Mji wa Kahama, amekamatwa akiwa na watu watano, wakiwemo waganga wa jadi watatu, katika harakati za kuuziana mifupa hiyo.

Wengine waliokamatwa ni mganga wa jadi Bi. Elizabeth au Shija Makandi Sweya (42), mkazi wa Busongwahala, Wilaya ya Nzega mkoani  Tabora, Bilia Masanja Mhalala (39), Msukuma, mkulima na mkazi wa Mogwa wilayani Nzega, mke wa Biria ambaye ni mganga wa jadi Regina au Tatu Kashinje Nhende (40), Msukuma na mkazi wa Mogwa.

Aidha, watuhumiwa wengine waliokamatwa ni Muhoja John Shija (24), Mnyamwezi na mkazi wa Isagenhe wilayani Nzega pamoja na mganga wa jadi na mfanyabiashara Abubakar Ally Magazi (25), Mrundi na mkazi wa Nzega.

Taarifa za uchunguzi wa awali zinaeleza kwamba, Mwalimu Bahati ndiye aliyesuka mpango mzima akishirikiana na waganga wa jadi Bi. Shija Makandi ambaye ndiye aliyeitafuta mifupa hiyo na Abubakar Magazi ambaye alikuwa apelekewe ili ‘kuibetua’ (kuitengeneza) na kuzalisha fedha.

Watuhumiwa watano wanadaiwa kwamba walifunga safari kutoka Nzega hadi Kahama kwa Mwalimu Bahati, ambaye kwa mujibu wa maelezo ya awali, ndiye aliyejua ni wapi ambako mifupa hiyo ingeuzwa, hivyo walikuwa wanakutana hapo kwa ajili ya kugawana fedha.

Mifupa hiyo inadawa kuhusishwa na tukio la kukatwa mkono wa kulia Bi. Muungu Masaga Gedi (35) mwenye albinism, mkazi wa Kitongoji cha Mkuyuni, Kijiji cha Buhekela, Kata ya Igoweko wilayani Igunga, ambalo lilitokea Mei 16, 2014 na kufunguliwa Jalada Namba IGU/IR/1070/2014.

Katika tukio hilo, mume wa majeruhi huyo, Mapambo Mashili, aliuawa kwa kukatwa mapanga na watu wasiofahamika wakati akipambana na watu hao wasimdhuru mkewe.

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Shinyanga, SACP Justus Kamugisha, amethibitisha kutokea kwa tukio hilo Mei 21, 2015 na kwamba watu hao walikamatwa saa 7:00 mchana katika nyumba moja ya kulala wageni inayofahamika kwa jina la Maji Hoteli iliyopo Phantom, Kata ya Nyasubi mjini Kahama baada ya Polisi kuweka mtego kufuatia taarifa za wasamaria wema.

Taarifa ya Kamanda Kamugisha imesema kwamba, mnamo Mei 19, asubuhi, mkuu wa upelelezi wa Wilaya ya Nzega alipata taarifa kuwa kuna mtu anauza viungo vya albino, ndipo walipoweka mtego. Hata hivyo, alisemai kuwa walishindwa kuwakamata na baadaye mtu huyo alihamishia biashara hiyo wilayani Kahama.

Hata hivyo, jeshi la polisi bado linaendelea na msako dhidi ya watu wengine wanaotajwa kwamba ndio walioitafuta mifupa hiyo, na kwa mujibu wa taarifa za awali, ndio waliohusika na mauaji pamoja na kumjeruhi mama huyo.​


Bilia Masanja Mhalala.
Mwalimu wa Shule ya Msingi Katunguru wilayani Kahama, Bahati Kilungu Maziku.
Abubakar Ally Magazi.
Elizabeth au Shija Makandi Sweya na Regina au Tatu Kashinje Nhende.
Muhoja John Shija.

Unajua Wema Sepetu Kazaliwa lini? Na Johari Je?......Unataka kujua Wanatoza Shilingi Ngapi Kucheza Muvi Moja?? Bofya hapa

0
0
Kila mwanamichezo au mwanamuziki hulipwa mshahara kulingana na kiwango chake, hali hii ipo hivyo pia kwa waigizaji na watu wengine wa kawaida.
 
Hali hii imekuwa ikiwapa morali zaidi wale wanaofanya kazi kujituma ili wapate mshahara mkubwa zaidi au kupewa kazi ya ziada tofauti na pale ulipozoea.

Hii pia imekuwa ikifanyika kwa wasanii wa filamu za Tanzania wenye umoja wao maarufu kama Bongo Movies. Hao wamekuwa wakilipwa madau kama wachezaji ili wafanye kazi za wenzao, hii imekuwa ikileta changamoto kubwa kwa wasanii kuhakikisha wanapanda dau kutokana na uwezo binafsi.
 
Asilimia kubwa ya mashabiki wa filamu za kibongo wamekuwa wakitoa fedha za kununua kazi zao bila kufahamu muhusika ‘anayemnunua’ amelipwa kiasi gani cha fedha kucheza ‘movie’ aliyoinunua. Tazama bei zao hapa chini:

Vincet Kigosi ‘Ray’
Inadaiwa kuwa huyu jamaa ni mgumu sana kukubali kucheza filamu za watu. Alishawahi kupewa Sh Milioni 10 ili cheze filamu moja (jina kapuni) lakini aligoma na amekuwa na msimamo mkubwa katika kazi zake lakini badala yake hizo fedha zikawalipa wasanii wengine watatu.
 
Inaaminika ndiye msanii mwenye gharama kubwa licha ya kuwa mpaka sasa bado amekuwa akigoma kucheza filamu za wenzake, ishu kubwa akidaiwa kujiona ni ‘staa’ zaidi ya wenzake.

Wema Sepetu
Kipaji chake kiliibuliwa na marehemu Steven Kanumba kupitia Filamu ya ‘A Point Of No Return’ baada ya hapo akapata mashavu kibao na hadi sasa amefanikiwa kucheza filamu na msanii mkubwa Van Vicker raia wa Ghana. 
 
Wema  Sepetu
Za mjini zinasema kabla hajaachana na aliyedaiwa kuwa ni mpenzi wake, Clement alikuwa akitoza kuanzia Sh Milioni Tano kwa filamu moja lakini sasa anapokea hata chini ya hapo kwa kuwa fedha zimeanza ‘kumkatikia’. 
 
Wema ambaye pia ni Miss Tanzania mwaka 2006, alizaliwa mwaka 1988, Dar anamiliki kampuni yake inayofahamika kama Endless Fame Films na ndiye mkurugenzi mtendaji.

Kajala Masanja
Ana kampuni yake ya uzalishaji wa filamu inayoitwa Kay Entertainment na tayari ameshafanya kazi zake zinayofahamika kwa majina ya Mbwa Mwitu pamoja na Pishu.
 
Lakini linapokuja suala la kufanya kazi za watu inakulazimu kuzama katika pochi au ‘waleti’ ukitoa mkono uwe na Sh Milioni Mbili lakini kwa kiasi hiki awe anakufahamu na kama ‘ndo’ mnaona kwa mara ya kwanza jiandae kuachia Sh Milioni Tatu hadi 2.5 zaidi ya hapo hakuna maneno maneno kazi inapigwa kwa kiwango kikubwa tu na binti huyu aliyezaliwa mwaka 1983.

Jacqueline Walper ‘Wolper’
Ninja, dada mkubwa, anaweza kucheza ‘sini’ zote ziwe za kijambazi, mke mwema na hata changudoa, amekuwa na mashabiki wengi sana Bongo na hata nje ambao wamekuwa wakipenda kazi zake. 
 
Mshkaji huyu ambaye alizaliwa mwaka 1987 huko Moshi, Kilimanjaro, yupo kishkaji tu kwani anakubali kupokea kuanzia Sh Milioni 2 hadi 2.5 hapo haipungui labda iongezeke ndipo atakufanyia kazi zako. Mpaka sasa amecheza filamu zaidi ya 20.

Mzee Majuto
Licha ya kuzaliwa mwaka 1948 huko Tanga, Amri Athuman ‘King Majuto’ au Mzee Majuto bado inaaminika kuwa ndiye msanii mwenye mashabiki wengi zaidi Bongo kutokana na uimara wa kuigiza hususan kwenye filamu za kuchekesha.
 
Mzee wa watu hana makuu ukitaka achekeshe weee filamu nzima jiandae kumkatia Sh Milioni 1.5 hadi 2 tu, hicho ndicho kiwango chake na atakufanyia kazi kwa umakini mkubwa zaidi ya hapo hashuki. Nje ya fani anamiliki daladala mbalimbali huko kwao Tanga ambazo pia zinamuongezea kipato.

Riyama Ally
Anaigiza kwa hisia kali sana katika kila filamu, ukitaka alie na machozi yatoke kwa wingi au acheze filamu za kimbea, majungu, vigodoro na nyinginezo wala hana makuu dada wa watu anapokea hata Sh Milioni 1.5.
 
Riyama ambaye alianza kujihusisha na maigizo mwaka 2000 akiwa na kundi la Taswira, mara nyingi katika filamu alizocheza anasifika kwa kuigiza kwa uhalisia mkubwa pengine ukimtoa Johari wa enzi za Tamthilia ya Johari basi huyu ni namba mbili kwa wepesi wa kutoa machozi. Mpaka sasa amecheza  filamu zaidi ya 40.

Blandina Chagula ‘Johari’
Alipata jina kupitia Tamthilia ya Johari kabla ya kuhamia kwenye filamu. Ni Mkurugenzi wa Kampuni ya RJ akisaidiana na msanii mwenzake Ray, katika kuindesha. Diva huyu wa movie za Kibongo alizaliwa mwaka 1983 huko Shinyanga.
 
Hana makuu katika kusaidia wenzake na mara nyingi amekuwa akijitoa kwa moyo kucheza filamu yoyote. Dau lake ni la ki-upendo zaidi kwani anapokea hata Sh Milioni Moja, hii yote anafanya kwa lengo la kusaidia wenzake. 
 
Anasifika zaidi kwa kucheza filamu za kulialia kwani kwake kutoa machozi si lolote hata sekunde mbili hazipiti anakuwa kayatiririsha hatari.

Lulu: Wanaonipenda Kweli, Wanafiki na Wale Baby Baby NAWAJUA

0
0
Staa mrembo wa Bongo Movies, Elizabeth Michael ‘Lulu’ ameandika haya kwenye ukurasa wake mtandaoni, bila shaka na wewe ANAKUJUA.

Mnaonipa Moyo na Kunipenda kiukweli....NAWAJUA
Wakuongea Nao Ya Moyoni....NAWAJUA
Wale wa kuni baby baby on IG kumbe Hakuna lolote....NAWAJUA
Wale mnajifanya shoulders to cry on ili mpate kunijua kirahisi...NAWAJUA ila SIWEZI KUWAPA HIYO CHANCE AISEEE...I'm Soleeeeee
Wale tunaochekeana kinafki...NAWAJUA I hope MNANIJUA PIA yani TUNAJUANA
Wale Waukweli kbsa ....NAWAJUA
Wale wa kuwaamini na wale wa kutowaamini....NAWAJUA
Wale mlio karibu yangu kwa sababu Fulani....NAWAJUA na msiniamini sana Hata mm nimewaruhusu kuwa Karibu yangu kwa sababu zangu flani
Kwa ufupi tu....JUA NAKUJUA
TafakariChukuaHatua
OkyBye"-Lulu on Instagram

New Video: Hussein Machozi – Ulikuwa Wapi

0
0

‘Ulikuwa Wapi?’ hilo ni swali, lakini pia ndio jina la wimbo ambao msanii Hussein Machozi ameachia rasmi video yake mpya.
Video ya wimbo huo wa Machozi ambao ulivuja mwaka jana mwishoni ukiwa na jina la ‘Mdogo Mdogo’ kabla hajauruhusu uendelee kupigwa, imefanywa na kampuni ya Kwetu Studios ya jijini Dar es salaam.

MARKSON BEAUTY PRODUCTS Inakuletea Dawa za Kurefusha Nywele, Kukuza Makalio, Kupunguza Tumbo, Kung'arisha Ngozi na Zingine Nyingi

0
0


Je, unapenda kuwa mrembo na mwenye mvuto kwa haraka? MARKSON BEAUTY PRODUCTS inakuletea bidhaa zenye ubora na matokeo ya haraka zisizo na kemikali wala madhara kwa mtumiaji. Tuna uzoefu wa miaka 15 na bidhaa zetu zote zimethibitishwa.                

TUNAZO ZA:-
1.Kurefusha nywele na kuzuia kukatika ovyo @80,000/=
2.Kutengeneza shepu (hips na makalio) @90,000/=. 
3.Kuwa mweupe na softi mwili mzima @80,000/=. 
4.Kuondoa mvi milele zisirudi @90,000/=. 
5.Kuongeza maumbile na nguvu za kiume kwa:-(1)Gely ya kupaka @70,000/=  (11)Vidonge maalum@90,000/=      (111)Mashine original ya Handsome up@200,000@/=     
6.Kupunguza unene na uzito wa mwili mzima @80,000/=.  
7.Kushepu maziwa na kuyasimamisha @70,000/=   
8.Kuongeza unene na uzito wa mwili mzima @80,000/=  
9.Kupunguza tumbo na nyama za pembeni kwa:- (1)Dawa @80,000/=  (11)Mkanda wa kawaida @80,000/= (111)Mkanda wa umeme (Micro computer belt) @200,000/=   
10.Kushepu miguu na kuwa minene (Chupa ya bia) @70,000/=    
11.Kuondoa mipasuko (Michirizi) mwilini @70,000/=                                
12.Kubana Uke na Kuongeza Hamu ya Tendo la Ndoa kwa Mwanamke @80,000/=

NB. Hakikisha unapewa risiti yenye muhuri halisi wa MARKSON BEAUTY PRODUCTS pamoja na garantii ili kukuhakikishia kufanikiwa kwako.      

Wasiliana nasi kwa no (+255 ) 0767-447444 na 0714335378.
Viewing all 104429 articles
Browse latest View live




Latest Images