Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104756 articles
Browse latest View live

Mpenzi wa Facebook Afanya Mauaji Kwa Kumnyonga Mke wa Mtu Gesti House

$
0
0
KWELI mchepuko siyo dili! Kauli hii imedhihirika kufuatia mwanadada, Ashura Maulid, mkazi wa Ilala jijini Dar, kukumbwa na mauti kwa madai ya kunyongwa ndani ya gesti na mwanaume mmoja anayejulikana kwa jina la Charles ambaye inasemekana ni mpenzi waliyekutana kwenye mtandao wa kijamaii wa Facebook.

Tukio hilo lililojaa majonzi tele na kuacha maswali mengi, hasa kwa mume wa marehemu, Suleiman Othman, lilijiri  Mei 19, mwaka huu kwenye nyumba ya kulala wageni (jina lipo) iliyopo kandokando ya barabara ya kutoka Sinza Afrikasana kwenda Kijitonyama kupitia Kituo cha Polisi cha ‘Mabatini’, Dar.

Chanzo kinadai kuwa, enzi za uhai wake, mwanadada huyo alikuwa akijihusisha na biashara ya kuuza duka la friji maeneo ya Sinza ya Afrikasana na inasemekana amekuwa ndani ya ndoa na mumewe, Suleiman kwa miaka 15 na kujaliwa kupata watoto wawili, wa mwisho akiwa na umri wa mwaka mmoja na nusu.

Akizungumza na Uwazi, Ijumaa iliyopita huku akiwa katika majonzi mazito, mume huyo alisema Jumanne ya Mei 19, mwaka huu, mkewe alimuaga anakwenda kazini huku akiumwa, alimtaka apumzike lakini mwanamke huyo akasema anajiona amepona hivyo ana uwezo wa kumudu majukumu yake.

Ilipofika saa moja usiku akanitaarifu kuwa ameshatoka kazini. Cha ajabu mpaka saa nne usiku alikuwa hajafika nyumbani na nilipompigia simu hakupokea.“Mara kwa mara mke wangu alipokuwa akimaliza kazi na kuanza safari ya kurudi nyumbani alikuwa ananitaarifu, nachati naye kila wakati mpaka anafika. Siku hiyo nilikuwa nina majukumu mengi aliponitaarifu kamaliza kazi ndo’ anarudi sikuwa na presha.

“Sasa ilipofika saa nne mimi nikiwa nyumbani na simu hapokei, nikashangaa. Mbaya zaidi, baadaye simu yake ikawa haipatikani kabisa.“Nilifanya jitihada za kumtafuta kwa ndugu na jamaa, vituo vya polisi na hospitali mbalimbali, ikiwemo Muhimbili kuulizia kwenye wodi za wagonjwa lakini sikumkuta.



Juzi (Mei 20), nilishtuka kupigiwa simu na polisi wa Kijitonyama, wakaniambia kuna maiti imekutwa mahali (walimficha kama ilikuwa gesti) na aliyehusika na mauaji ni mwanaume ambaye walianza kufahamiana na mke wangu kupitia Facebook. Walisema marehemu alionekana alikufa kwa kunyongwa.

“Waliniambia huyo mwanaume alikimbia baada ya kufanya mauaji hayo. Palepale ndo’ wakaanza jitihada za kumtafuta mpaka wakamkamata,” alisema mume huyo.Akiendelea kuelezea tukio hilo alisema kisa cha kugundua kuwa Charles alikutana na mke wake kwenye Facebook ni siku ya tukio baada ya mawasiliano waliyoyafanya kwa kipindi kirefu bila yeye kujua.

Alisema ilionesha kuwa, siku hiyo waliamua kuonana laivu ambapo alimkaribisha dukani kwake na kuondoka naye baada ya kumaliza kazi na kufunga duka huku akiwa amemtaarifu bosi wake (si mumewe) fedha zilizopatikana siku hiyo.
“Niliambiwa na rafiki wa mke wangu kuwa siku hiyo mwanaume huyo alifika dukani kwa mke wangu akawatambulisha mashosti zake kuwa ni rafiki yake waliyejuana Facebook. Wakiwa hapo, mke wangu  alimpigia simu bosi wake kumwambia siku hiyo aliingiza shilingi milioni moja na laki saba. Huenda hicho ndo’ kilimfanya jamaa amgeuke na kumuua kwa tamaa ya zile fedha,” aliongeza.

Mumewe huyo alisema, haamini kama mkewe alishindwa kuiheshimu ndoa yake na kuwapa nafasi wanaume wengine tena kwa kwa mtu ambaye hakufahamiana naye ila kwa kukutana naye kwenye mtandao na kuanzisha uhusiano kwani yeye alimtosheleza kwa kila jambo.

Kwa upande wake, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, Camillus Wambura alipotafutwa ili aulizwe kuhusiana na tukio hilo, simu yake iliita bila kupokelewa.Uwazi lilipofika kwenye gesti hiyo ambayo marehemu alifia chumba Namba 4 lakini wahusika  waligoma kutoa ushirikiano na kudai hakukuwa na tukio hilo.

Kesi  hiyo ipo katika Kituo cha Polisi Kijitonyama ‘Mabatini’ faili Namba KJN/RB/5081/15 TAARIFA YA KIFO huku mtuhumiwa akishikiliwa hapo baada ya kukamatwa akiwa na gari aina ya Toyota Carina

GPL

Suala la usajili Yanga sasa lawa 'serious' Mwaka Huu...Hichi Ndicho Walichoamua Hakuna Mzaha Tena

$
0
0
KLABU ya Yanga imesema kutokana na mkakati wao wa kusuka kikosi cha kufa mtu cha msimu ujao, hawatakuwa na mzaha katika usajili wao kwa kusubiri kuletewa wachezaji na wanaojiita mawakala.

Badala yake, Wanajangwani hao wameamua kujitosa ‘jumla jumla’ kufuatilia wachezaji waliong’ara katika timu zao msimu uliomalizika hivi karibuni na kuona kama wanaweza kuwasajili.
Katibu Mkuu wa Yanga, Jonas Tiboroha, alisema jana kuwa wamebaini wachezaji wengi wanaoletwa na wanajiita mawakala kufanya majaribio hapa nchini, si lolote zaidi ya kuja kuganga njaa.
Alisema kwa kutambua hilo, wamejipanga kuhakikisha wanasafiri katika eneo lolote la Bara la Afrika kumfuata mchezaji ambaye atabainika kuwa na kiwango cha juu.

“Hatutasubiri kuletewa mchezaji na wakala, wengi wanaokuja kufanya majaribio hawana viwango vya kutisha kama ilivyojionyesha kwa waliopita,” alisema Katibu huyo. 
Tiboroha alisema mikakati yao ni kuwa na wachezaji ambao watawawezesha kutamba katika Soka la Afrika na kuwa klabu tishio barani humo, jambo ambalo halitawezekana kwa kusubiri wachezaji wa ‘mafungu’.
Baadhi ya wachezaji wa kigeni ambao waliwahi kutua nchini baada ya kuletwa na mawakala, lakini mwisho wa siku walichemka ni Mcameroon, Jama Mba (Yanga), Komal Bill Keita (Simba) na wengineo wengi.
Kwa sasa klabu za Ligi Kuu Bara zipo katika mchakato wa usajili wa wachezaji, zikianzia na makubaliano ya mikataba kabla ya kusaini fomu za usajili zitakazotolewa na TFF baadaye mwaka huu.
Chanzo:Bingwa

Siku ya Kwanza Kunywa Kiroba Ndio Siku Safari ya Mapenzi Hadi Ndoa ilianza..Soma Kisa Kizima Hapa

$
0
0
Safari yangu ya ndoa ilianza kwa namna yake! nikiwa mitaa fulani ya kijitonyama' baada ya kuhitimu na kuamua kuacha kazi ili nijikite kwenye ujasiriamali nilikutana na ukata ambao sikuwahi kufikilia kama ungewahi nitokea' hata hivyo mtembea bure si sawa na mkaa bure' maana mkate ulikuwa unapatikana!!

Nilikuwa na kibanda cha huduma fulani pembezoni mwa barabara' hivyo watu wakishuka mitaa ya sayansi walikuwa wanapita usoni mwa banda langu lakutafutia liziki kwenye ile barabara yakuelekea Kwa Ally Maua(watu wa k'nyama wananielewa vizuri hapa)

Kumbe kati ya wale wapita njia ambao huwa nawaona asubuhi na jioni wakiwa wanaenda na kutoka maofisini moja wao ni ubavu wangu lakini kwa hali yakawaida ilikuwa fumbo zito kwangu. Mara mojamoja ilinipa wakati mgumu hasa pale nilipokuwa naona wapendanao wakiwa wanasindikizana na wamependezana'' kilichokuwa kinaniumiza ni maswali mengi niliyokuwa nayo kichwani yasiyokuwa na majibu' lini mambo yangu yatanyoka? Lini takuwa na mtu ambaye tutamatch tukiongozana mtaani watu watutolee macho? Lini takuwa na familia yangu?

Jioni moja nikiwa na jamaa yangu
Kwenye mgahawa karibu na akachube road' baada ya msosi si tukaagiza safari ili kukata kiu' nikahisi kama vile haitoshi na mfukoni nimebaki na buku, kwakujitutumia mhudum lete kiroba' nikachanganya kiroba na safari!! Bwana kilichofuatia..

Wakapita wadada wawili walipendeza sana lakini sura ya mmoja wao ilikuwa imezoeleka machoni kwangu' kwakuwa kiroba kilikuwa kimeanza kazi nikashindwa kukumbuka kwaharaka (kumbe alikuwa ni mmoja kati ya wale ambao huwa wanapita mbele ya kibanda changu na sometimes huwa anakuja kupata huduma kibandani kwangu). Ila mara nyingi huwa anavaa earfone na anakuwa anaongea na sim mda wote akipita' na leo yupo casual tofauti na muonekano niliozoea kumuona!!

Basi bwana kiroba kikiwa kimechanganya dada si akapita karibu yetu'
Mimi; dada karibu
Dada; Asante
Mimi; agiza moja
Dada; Asante' situmii!!
Nikadakia ina maana niharam kwako? Dada akamuita mwenzake fanya haraka tuondoke'
Mimi' dada acha dharau mim nakukaribisha wewe ndo kwanza kama vile huniskii!
Dada; samahani kaka yaishe!

Basi akili ya kiroba ikaanza kazi' mimi; unajifanya jeuri sio' takuonyesha leo! Nikamkunja dada wawatu kichapo kichapo' mamwela sijui walitokea wapi wakakuta dada anachezea kichapo wakanianzishia sikufanya ajizi nikamdaka alikua na kihelehele chakushuka kwenye gari nikampa kichapo akaangukia mtaroni' bwana wee kama nilichokoza nyuki nilishambuliwa nawale jamaa na virungu' na sikujielewa kuja kutahamaki nipo mabatini kwenye kasero kadoogo!

Nisijue kumbe nilimsababishia jeraha yule dada' baadae nikayaweka sawa pale kituoni na nikatakiwa kulipa gharama za matibabu! Basi nikaenda kumuona yule dada na kumuomba msamaha' nashukuru nilikuta anaendelea vizuri' ikanibidi niulize gharama za matibabu ingawa nilikuwa sina chochote mfukoni' dada akaniambia atagharamia mwenyewe! Nikajifanya kumbembeleza pale kumbe moyoni nashukuru kwelikweli maana navyowajua wale jamaa dada angekomaa alipwe nao wangeongeza chao!

Mazoea yakaanza' kati yangu na yule dada katika kipindi ambacho alikuwa anauguliwa maana ikanibidi niwe mtu wa matunda juice juice kuonyesha kwamba kilichotokea sio hulka yangu ilikuwa bahati mbaya tu na ndio ukweli!! Lakini kwakipindi hicho nilijifunza kitu kwake na akaendelea kunivutia zaidi na zaidi lililokuwa kubwa zaidi sikuwahi kukutana na mtu ambaye ningehisi au kutambulishwa kama shemeji(yaani mpenzi wake) kila nilipokuwa nikienda kumuona!!

Siku zikasogea, miezi ikaenda, mwaka ukakatika!! Nikagundua kwamba Ana sifa zote na vigezo vyakuwekwa ndani... Issue ikawa taanzaje kumueleza hisia zangu juu ya hilo!! Nikajipa moyo mimi mtoto wa kiume woga wangu waweza kuwa umaskini wangu nikajitutumua' bwana wee ikawa kama nimetaka kuvunja urafiki!!
Basi nikajituma mwanaume miezi ikakatika' akaanza kuniekewa taratibu tukawa wapenzi' siku zikaenda mara nikatangaza ndoa! Hatimaye sasa nimama wa mtoto mmoja na nampenda sana na sijawahi jutia kuwa naye!!

Yote kwayote tunapaswa kujua mambo mengine yanatokea kwasababu fulani! Mimi sio mlevi na wala sikuwa mnywaji au mtumiaji wa pombe lakini siku hiyo nilikunywa safari tena nikaongeza na kiroba kumbe ulikuwa ndo mwanzo wa safari yangu ya ndoa!! Siisahau siku hiyo maana ndo ilikuwa siku yangu ya kwanza na mwisho yakutumia pombe lakini pia ndo ilikuwa mwanzo wa mahusiano hatimaye mke!!

Hivyo ndio namna safari yangu ya ndoa ilivyoanza' wewe ulie kwenye mapenzi ilikuwaje paka umefika hapo ulipo? Nawewe uliye kwenye ndoa safari yako ilikuwaje?

By JJ10

K-Lynn azungumzia maisha yake kama mama, kwanini hawezi kurudi kwenye muziki na kazi ya interior design

$
0
0
Ni nadra sana kukutana na Jacqueline Ntuyabaliwe Mengi maarufu kama K-Lynn lakini kupitia tuzo za watu tulifanikiwa kupiga story mbili tatu.

K-Lynn ameiambia Bongo5 kuwa maisha akiwa kama mama watoto wawili mapacha yamekuwa ya aina yake na anayafurahia kila sekunde.

“Nimejifunza kuwa mvumilivu, nimejifunza upendo ambao sijawahi kujisikia kabla. Jinsi unavyompenda mtoto ni tofauti ambavyo unaweza kumpenda mtu yoyote yule katika maisha yako,” alisema.

Katika hatua nyingine Miss Tanzania huyo wa zamani alisema hakuna uwezekano wowote wa yeye kurejea tena kwenye muziki.

“Kwa bahati nzuri sana baada ya kufanya uamuzi wa kutokuwa kwenye muziki, niliweza kupata kitu kingine ambacho kimeuteka moyo wangu. Kufanya interior design kunanifurahisha kuliko hata muziki.

"Nafurahi sana kujua kwamba kuna watu wangependa kunisikia ama kusikia nikiimba lakini nafikiri moyo wangu umehamia kwenye sanaa nyingine.”

Rais Kikwete Awatolea Uvivu Vijana wa CCM.....Awataka Waache Ukuwadi

$
0
0
RAIS Jakaya Kikwete, amesema Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), umegeuka kuwa jukwaa la watu wanaotaka kugombea urais kwa kuwa makuwadi, mawakala wa kuhonga fedha vijana wenzao badala ya kufanya mijadala ya kukijenga chama.

Alisema lazima vijana wa UVCCM wawe wapiganaji, wapambanaji na wanaharakati wa kukiimarisha chama kwani hatima ya CCM iko mikononi mwao.

Rais Kikwete ambaye ni Mwenyekiti wa CCM Taifa, aliyasema hayo Mjini Dodoma jana wakati akifungua Mkutano Mkuu wa Shirikisho la Wanafunzi wa Vyuo vya Elimu ya Juu nchini.

Alisema badala ya umoja huo kukaa na kuzungumza mambo ya mustakabali wa chama na Taifa, baadhi ya viongozi wake huchukua fedha kwa wazee na kuwagawia vijana.

"Vijana hampaswi kuwa makuwadi na mawakala wa kuhonga wenzenu, katika Kikao cha NEC, nilimuita Sixtus Mapunda (Katibu Mkuu wa UVCCM Taifa) na wenzake nikamwambia mnakoenda siko rudini huku...sisi tunategemea miaka 30 ijayo Rais atoke miongoni mwenu hivyo lazima tufanye kazi ya kuwaandaa vijana ili wawe viongozi wazuri.

"Utakuta viongozi wanasafirishwa ili kuwasindikiza wazee wanaotaka urais jambo ambalo haliwezekani vijana kuhusishwa na ugawaji rushwa, enzi zetu hoja za vijana zilikuwa zina nguvu lakini sasa hivi vijana si tishio tena," alisema.

Aliongeza kuwa, hivi sasa vijana hawatoi hoja za kukijenga chama hivyo aliwataka warudishe misingi ya uanzishwaji wake na kusisitiza kuwa, anaamini shirikisho hilo litakipa uhai CCM na kutoa mawazo ya kujenga chama.

Rais Kikwete alisema, jukumu la shirikisho hilo ni kukitafutia chama wanachama, marafiki na kuhakikisha kinaungwa mkono na wanafunzi wa elimu ya juu na wengine.

"Shirikisho hili lina wajibu wa kuwa chombo cha uwakilishi wa masilahi ya wanafunzi, kuwa wepesi kuyatambua mambo yenye masilahi kwa wanafunzi na kuyasemea.

"Muwe tumaini na kimbilio la wanafunzi, tatueni changamoto na kuzisemea kwa chama na Serikali badala ya kuacha mambo yakaharibika...shirikisho hili ni tanuru la kupika viongozi wa baadaye hivyo lazima muwe na mipango madhubuti," alisema.

Aliwataka kuchagua viongozi wazuri, waaminifu, waadilifu, wabunifu na wachapa kazi ndani ya shirikisho ambao watakuwa na uwezo wa kujenga hoja.

"Chama kinasema jitokezeni kugombea, nasubiri hiyo Juni 3, mwaka huu nione watajitokeza wangapi maana ninavyosikia
wako wengi zaidi ya 20 wanaotaka urais.

"Lazima tushirikiane kujenga chama chetu na shirikisho, mimi nilijaribu mwaka 1995 kugombea urais lakini kura hazikutosha na sikumnunia Mzee Mkapa," alisema Rais Kikwete.

Awali, akimkaribisha mgeni rasmi, mlezi wa shirikisho hilo Bw.January Makamba, alisema shirikisho lina matawi 137 katika mikoa mbalimbali nchini ambapo changamoto zinazowakabili vijana ni mikopo ya wanafunzi, ushirikishwaji katika kampeni na suala la ajira hivyo alimwomba Rais Kikwete kuyatafutia ufumbuzi.

Maelezo Ya KINA Ya Edward Lowassa Kuhusiana Na Sakata La Richmond, Afya Yake, Utajiri Wake Na Kwa Nini Alikuwa Kimya Kwa Miaka Yote 7

$
0
0
Hatimaye  Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa, jana alivunja ukimya wa muda mrefu alipofanya mahojiano ya ana kwa ana na wahariri wa vyombo mbalimbali vya habari.

Katika mkutano huo,Lowassa aliitumia nafasi hiyo kutangaza msimamo wake wa siasa ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Lowassa aliitumia fursa ya mahojiano hayo, yaliyofanyika nyumbani kwake eneo la Area C mjini hapa, kuwaeleza wahariri kuwa hana mpango wa kuhama CCM licha ya kuwapo shinikizo la chini kwa chini la kumtaka aondoke na kwamba wale wote wanaomtaka au wanaotamani aondoke, wanapaswa kuondoka wao.
 

 Sakata  La  Richmond:
Kuhusu sakata la Richmond, ambalo lilimfanya ajiuzulu uwaziri mkuu, Lowassa alisema tatizo kubwa halikuwa kuhusu mitambo hiyo ya umeme ila uwaziri mkuu.

“Ajenda haikuwa kuhusu Richmond, ila uwaziri mkuu ndiyo maana niliwaachia. Tunajifunza  nini katika hilo, wakubwa wawili wa Marekani, aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Nje (Hillary) Clinton na Rais wake (Barack) Obama, wote wamekuja Tanzania na wamethibitisha kuwa ile mitambo ni mizuri. Lakini jingine tulilojifunza katika ubishi ule umeisababisha nchi hasara ya Dola 120 milioni,” alisema Lowassa.

“Moja ya ushauri wangu wakati ule ilikuwa ni kutaka kuvunja mkataba wa Richmond nikaita wataalamu, nikawaelezea kuhusu habari za magazeti kuwa zinasema hawa jamaa (Richmond) hawana fedha, hebu angalieni, nikaita wataalamu na mwanasheria mkuu, nikawaambia kuna hii habari kuweni makini.
 
"Pamoja na hayo nikaweka kwa maandishi kwa mwanasheria mkuu, pia kulikuwa na timu ya mashauriano ya Serikali iliyokuwa chini ya makatibu wakuu nao walikuwa na vikao vyao, ilikuwa inaongozwa na (Katibu Mkuu Wizara ya Fedha (Gray Mgonja) nao wakakutana chini ya Katibu Mkuu Kiongozi na baada ya kukutana wakatoa uamuzi ambao sina haja ya kuujadili. Lakini ubishi ule umetugharimu Dola 120 milioni."

“Nilipotaka mkataba uvunjwe nilikuwa nimetoa uzoefu wangu kwani kabla ya kuwa waziri mkuu nilikuwa nimekuwa waziri wa maji na mifugo ambako nilivunja mkataba wa kampuni ya Kiingereza iliyokuwa imewekeza katika mradi wa maji Dar es Salaam ya City Water.

“Chini ya uongozi wa Rais (Benjamin) Mkapa tukagundua hawa jamaa (City Water) ni matapeli…tulifanya kikao saa tisa alasiri, tukachukua kibali cha kumkamata yule Mzungu wa City Water na tukamfukuza akaondoka siku hiyohiyo kwa ndege kurudi kwao, tulifanya saa tisa alasiri ili asiende mahakamani kupata zuio, kwa hiyo tulivizia muda huo ili asije kwenda kupata zuio."

Nini tofauti ya Lowassa nje ya Serikali na ambaye angeendelea kuwa waziri mkuu na kisha kugombea urais?

 “…Naamini kuwa kama tungeanza kwa kasi ile tuliyoanza nayo nikiwa waziri mkuu, sasa ningepita napunga mkono ningepata kura zote… lakini kinachonisikitisha tumekuwa hatufanyi maamuzi magumu au rahisi, kila kitu kinakwenda legelege.
 
"Rais amefanya jitihada kubwa, lakini kuna mambo katika nchi hayaendi, matokeo yake Uganda, Kenya na Rwanda zinatupita sasa, haifai, lakini nawaachia uhondo nitaelezea vizuri Jumamosi, Arusha.”

Kwa  nini  Alikuwa  Kimya  Kwa  Miaka  Yote 7?
Lowassa aliyejiuzulu uwaziri mkuu mwaka 2008 kutokana na kashfa ya mtambo wa kufua umeme wa Richmond, alisema kimya chake baada ya tukio hilo kilitokana na siasa nyingi za uhasama na kutishiana.

“Kwa miaka saba, niliona ni hekima kunyamaza, askofu mmoja alinifundisha kuwa ukimya ni hekima kutoka kwa Mungu. Nilichagua kuwa kimya.
 
"Nilinyamaza kwa sababu ilikuwa salama kunyamaza, ningezungumza ningeweza kutibua mambo kwenye nchi na kusababisha mambo ambayo hayapo.

“Nilinyamaza ili kuipa muda Serikali ifanye kazi yake.... sikupenda kuzungumza kwa sababu ya siasa nyingi za uhasama na kutishiana kwingi, kuna kusingiziana kwingi, kufitiniana kwingi.

"Kukaa kimya ni jambo gumu sana kwa mwanasiasa, lakini nashukuru Mungu niliweza hilo,” alisema Lowassa ambaye Jumamosi atatangaza nia ya kuwania urais mjini Arusha.
 
Ni Kweli  Afya  Yake  Ni  Mbovu?
Alipoulizwa kuhusu madai kuwa afya yake inaterereka, alisema anaamini yupo fiti na akashauri wagombea urais wote wakapimwe.

“Hata nikikimbia kilomita 100 watasema mimi mgonjwa. Hivi karibuni nilitembea kilomita tano na albino jijini Dar es Salaam, kuna watu wakasema nimechoka sana, nimepata ‘stroke’ na nimekimbizwa Ujerumani kutibiwa, huo ni upuuzi mtupu.
 
"Kuna chuki imeingia katika siasa zetu na kutakiana mabaya. Afya ni neema kutoka kwa Mungu tu. Napenda kuwahakikishia kuwa nipo fiti na nipo fiti na kwa lolote.
 
"Nadhani ni wakati sasa kwa chama chetu waweke utaratibu wanaogombea nafasi hii ambayo nitaitangaza Jumamosi, tukapime wote afya na mimi nitakuwa wa kwanza kujitokeza kwenda kupima.

“Twendeni tukapime tuone nani mgonjwa. Tuonane kwenye uwanja wa mapambano katika mchakamchaka wa maendeleo, ninajua nitawashinda kwa mbali,” alisema.

Utajiri wake
Alipoulizwa ana utajiri kiasi gani na fedha anazochangia kwenye harambee makanisani na misikitini zinatoka wapi, Lowassa alisema anatamani angekuwa tajiri, lakini anachukia umaskini.


“Tatizo siku hizi kuna maneno mengi, kila nyumba nzuri wanasema ya Lowassa. Mimi nina nyumba chache na ng’ombe kati ya 800 na 1,000.
 
"Kwetu Umasaini unapokuwa kiongozi unapewa ng’ombe ili usipate taabu kwa ajili ya kuwakarimu wageni wanapokuja wala usiwe ombaomba au usichukue rushwa. Lakini kama kuna mtu mwenye shaka na utajiri wangu aende Sekretarieti ya Maadili kule ataona kila kitu,” alisema.


“Nachukia umaskini, napenda utajiri, natafuta uongozi wa nchi hii ili kuwasaidia Watanzania kuwa matajiri na si kukumbatia umaskini. Hii kudanganya watu kwamba nikiwa maskini ndiyo nafaa kuwa kiongozi ni ujinga ambao inabidi tuuache.
 
"Nataka watu wawe matajiri, tuache kuwabeza matajiri, matajiri wawe ni mfano kwa wengine, watu kama (Reginald) Mengi, (Said) Bakhressa na (Nazir) Karamagi wanatakiwa kuwa mfano kwa wengine, tungekuwa na watu kama hawa 20,000, nchi hii ingekuwa haikopi nje. Naukataa umaskini na nauchukia umaskini. Nakataa umaskini na ninataka watu wanihukumu kwa hilo,” alisema.

Kuhusu kushiriki harambee nyingi na anakopata fedha alisema: “Sina fedha ila nina marafiki wengi, nikipata mwaliko wa kuchangia nawatafuta marafiki zangu wanachanga. Mfano ‘juzi’ nilipomwakilisha Makamu wa Rais mjini Arusha, marafiki zangu walichangia Sh100 milioni, Makamu wa Rais alichangia Sh10 milioni na watu wa Arusha wakatoa Sh100 milioni. Hizo hazikuwa fedha zangu, ila ni watu walichangia.
 
"Nafurahia kufanya harambee, harambee zangu zinasaidia misikiti, makanisa na shule, hivi ni vitu vya maendeleo ya watu, nawashauri na wabunge wafanye hivyo kwenye majimbo yao. Hata shule za kata zilichangiwa kwa harambee, tusionee aibu ni jambo jema,” alisisitiza.

What's Wrong With This Picture??

$
0
0
‘Thirsts’ are dangerous things to have as they always lead to some strange habits. Mix the thirst with booze and it gets difficult to keep one’s hands to themselves.

Like this two revellers who were spotted in Machakos. Scratch my back and I scratch yours must be their motto.

Wauza Sura Wamtesa Batuli...Wengi Huja na Sura Nzuri Lakini.....

$
0
0
Staa wa Bongo Movies, Yobnesh Yussuf ‘Batuli’ amekiri kuteswa na suru nzuri za wanaume ambao huwa wanamfuata kwa ajili ya uhusiano wa kimapenzi huku wengine wakimuahidi kumuoa na kuwakubalia ombi lao na kuelekeza mapenzi yake yote kwao.

Azungumza na tanuru la fulamu hivi karibuni  batuli alisema kuwa yeye huwa anapenda mwanaume mpole na mwenye kujiheshimu ili watengeneze maisha yao na penzi linapo kolea na kujiachia kimahaba sura hizo hubadilika na kuwa mwiba kwake hali ambayo humfanya  akimbie.

“Nina watoto wawili  ambao nimezaa na wanaume wawili tofauti, niliwahi kuolewa na mwanaume aliekuja na lugha nzuri na sura yenye  kuonyesha  ana mapenzi ya dhati lakini baada ya kuingia ndani ya ndoa akakunjua makucha nikaamua  kukimbia  vivyo hivyo  na wapili nilimpata kwa staili hiyo naye akawa mchungu” alisema Batuli.

Staa huyo alisema kwamba kwasasa ana mchumba ambaye badoanamwangalia kama naye ni kama aliowahi kuwakubali na  na kuingia nao kwenye ndoa kasha wakawa mbogo ndiao mana ameweka ngumu kuolewa sasa mpaka ajue tabia yake kwani amechoka kuumizwa na wanaume.

Lulu Arudi Instagram Kwa Kishindo..Atupia Picha hizi ...Zitazame Hapa

$
0
0
Baada ya kuifunga akaunti yake kwenye mtandao picha wa Instagram iliyokuwa na followers zaidi ya laki nne, na kuamua kufungua tena akaunti kwenye mtandao huo, staa mrembo wa Bongo Movies, Elizaberth Michael ‘Lulu’ ametupia picha hizi mpya kwenye ukarara wake huo mpya  unaopatikana kwa anuani ya @ elizabethmichaelofficia kitendo ambacho kimewavutia mashabiki wengi waliommiss mrembo huyo ambaye ni mpenzi wa fasheni.

Mashabiki wengi wamemsifia kwa kutokeleza bomba na kuonyesha furaha zao kwa juio wake tena mtandandaoni humo kwani wanampenda na kumkubali sana.

Karibu tena Lulu

Diamond Platnumz's Fame and Love in east africa, Haters Have a Long way to Go as Diamonds Fame is Like a Forest Fire Which Can"t be Put Off with a Mere Bucket of Water

$
0
0
The Tanzanian music superster as he calls himself the Rolls royce musician from East Africa Diamond platnumz has continues prooving that fame and love are seen and not rumored around, Recently this month after overseas Live shows in Dubai and London, Soon after the mission complete of these shows the East african super star went back to his home country(Tanzania) with his wcb (wasafi classic baby) crew, Soon after touching down in Tanzania the superstar caused a disastrous situation when he landed to mwanza airport in Nothern Tanzania, Hundreds of thousands of his fans stormed at the airport trying to get even a minor chance to see their superstar who mercilessly dominates the Tanzanian territory leaving only a small share to his fellow artists ,

The superstar was escorted by way so many motorcycles as he was waving at the countless fans beside the road as he took his time in the "HUMMER", The die hard hardcore fans of Diamond did not want to leave his side untill they reached the hotel where they were forced to leave him, Due to this situation one of the Tanzanian artists felt jealous and posted on instagram a ---- of hateful bla blas, It is no joke that Diamond success causes him to have manyfans and haters in Tanzania, There has recently been a network of his haters in tanzania who somehow mingled up the votes which made Diamond loose the award of the most loved Tanzanian artist to a less famous fellow artist "ALI KIBA" Many Tanzanians were shocked by the awards and thought there was a mistake but it was later known that his haters used much time and miney to promote the other artists, However his haters have a long way to go as Diamonds fame is like a forest fire which can"t be put off with a mere bucket of water

OKEY back to the topic, after his succesfull show s in Dubai, London and mwanza (Northen Tanzania) Diamond is expected to tour for the shows expected to be perfomed live in South Africa, nigeria, ghana, cameroon, togo and angola, In may 1 It has to be remembered that diamond hosted a party for his rich billionaire pregnant girlfriend "ZARI" For the first time in the History of Tanzania there were tickets CLASS A which costed as much and likely 1452 american dollars, these tickets had all finished by the time the part started

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatano ya Tarehe 27 May 2015

$
0
0
















Habari  Zilizopo  Katika  Magazeti ya  Leo  Jumatano  ya  Tarehe  27  May  2015

VERA SIDIKA is still a s*x goddess….. The Guy Behind the Camera Must be the Luckiest Man Alive

$
0
0
VERA SIDIKA is still a s*x goddess….. The guy behind the camera must be the luckiest man alive

Sitti Mtemvu Aongea Kwa Mara ya Kwanza Baada ya Kujivua Taji la Miss Tanzania, Aongelea Mahusiano na Lundenga, Umri wake, Mtoto na Sababu ya Kujivua Taji la Miss Tanzania

$
0
0
Sitti Abbas Mtemvu alishinda Taji la Miss TZ mwaka 2014, muda mfupi baadae alitangaza kujivua Taji hilo baada ya mengi kusikika.. watu wakaandika na kuhoji kuhusu umri wake, elimu yake, madai mengine ni yale kwamba ana mtoto… aliwahi kuyajibu kwa nyakati tofauti, leo alikuwa Live kwenye show ya Nirvana @EATV hii ni sehemu ya majibu yake.

Niko sawa, nilikubaliana na changamoto nilizopitia.. namshukuru Mungu kwa kila kitu.. nina amani na furaha." Sitti Mtemvu.

Kilichomfanya akaamua kuvua taji “Ilikuwa inaniathiri mimi na familia yangu… nikaamua nirudishe maana maneno yalikuwa mengi“

Sitti anasema mdogo wake aliumizwa pia na kila kilichomkuta yeye  “Ilifikia hatua marafiki zake shule wanamtania, walikuwa wanamwambia wewe ni mtoto wa ‘bibi bomba

Kwani alilazimishwa kuvua Taji? Uhusiano wake na Kamati ya Miss Tanzania ukoje?  “Hapana, niliamua acha nivue taji.. mimi na wao hatuna tatizo kabisa"

Iliwahi kuandikwa kwamba ana uhusiano na Hasheem Lundenga, jibu lake je? “Hamna uhusiano wowote kati yangu na Hasheem Lundenga, mengi yaliandikwa kama ilivyoandikwa mimi na mtoto, it’s okay… yamepita

Swali la umri je?  “Nimeamua kufunga huo ukurasa kwa sababu chochote nitakachokisema kitafunua mambo yaliyopita.. nimeendelea mbele mimi sio Miss Tanzania nimeufunga huo ukurasa.. umri wangu ni kitu binafsi

Exclusive hiyo nimeirekodi @EATV, hapa unaweza kuplay ukasikia sauti ya nterview yote mtu wangu.

Eti wakili Mkenya ataoa mtoto wa Obama?? Ona mipango yake sasa aliyojipanga !!

$
0
0
Kila mtu ana ndoto na mtu ambaye anamhitaji awe mpenzi wake kwa maisha yote, sio ajabu mtu akawa na ndoto za kumuwaza mtu ambaye ni ngumu sana kwenye mazingra ya kawaida kuonana nae, pata picha ya huyu jamaa ambaye yeye macho na akili yake ni kwa Malia Obama.

Kiprono Matagei kazi yake ni wakili Kenya, ndoto yake ni yeye na Malia Obama damdam, alianza kumpenda tangu mwaka 2008.. moyoni mwake akaweka ahadi kwamba hatokuwa na uhusiano na mwanamke yoyote mpaka siku ampate Malia wake !!

Jamaa kajiongeza kabisa, amesema mahari aliyopanga kutoa ni hii>>> ng’ombe 50, kondoo 70 na mbuzi 30.

Kiprono kasema yuko serious kabisa na aliwashirikisha familia yake, wako tayari nao kumsaidia mpaka afanikiwe !!

Obama atakuwa Kenya mwezi wa saba, ziara yake haitachukua muda mrefu lakini jamaa amesema atajitahidi aitumie nafasi hiyo hiyo kumuona ‘baba mkwe huyo mtarajiwa’ !!

Dr. Slaa: Sitakula Sahani Moja na Mafisadi, UKAWA Hawapo tayari Kupokea Mafisadi

$
0
0
Kufuatia uvumi kuwa Edward Lowassa waziri mkuu aliyeng'oka kwa kashfa za ufisadi kutaka kuhamia UKAWA, Dr. Willbrod Slaa katibu mkuu wa CHADEMA amesema kuwa hayupo tayari kula sahani moja na mafisadi.

Akijibu tuhuma hizo Dr. Slaa amesema wazi kuwa Chadema na UKAWA hawapo tayari kupokea mafisadi kwani itakuwa ni kinyume kabisa na dhamira ya UKAWA ya kuwatumikia watanzania wanaotegemea mabadiliko makubwa.

"Watanzania wapo tayari kwa mabadiliko na wameonyesha nia ya dhati kutuunga mkono, hatupo tayari kuchafuka na mafisadi" amesema Dr. Slaa

Kutokana na hali halisi ilivyo mdani ya CCM, chama hicho kinatarajiwa kukumbwa na mgogoro mkubwa kutokana na msuguano mkali wa makundi mawili makubwa yanayowania urais huku kundi hasimu na Lowassa likiungwa mkono na rais Kikwete.

Lowassa tayari ametoa hotuba huku akiainisha vipaumbele vyake ambavyo vinaenda kinyume kabisa na ilani ya CCM mwaka 2015-2020 jambo linalohashiria kuwa ndani ya chama hicho hali si shwari.

The big 3: Lowassa, Chenge na Rostam kuhakikisha wanashika Ikulu?

$
0
0
Mbio za kutinga Ikulu mwaka huu zina mvuto aina yake huku zikionekana kutekwa zaidi na kundi la mafisadi ambao baada ya uchaguzi mkuu uliopita Andrew Chenge, Rostam Azizi na Edward Lowasa walitangazwa kwamba ni mafisadi papa na hivyo kuwataka wajiengue chama kabla hawajachukuliwa hatua za kufukuzwa kwa kukichafua chama.

Aliyetii ni Rostam Azizi kwa kujivua ubunge wa Igunga na nyadhifa nyingine chamani akiita ni siasa za maji taka, wengine Lowasa na Chenge wakavuta subira iliyowapa ahueni kutoenguliwa na bila maelezo ya kuridhishwa kwamba zile siku tisini hazikuwekwa bayana lini zinaanza.

Hatimaye Lowasa aliporejea toka kuombewa huko Nigeria aliita press comference na tishio alilosema wakati huo ni kuwa atakayeendelea kumchafua atamchukulia hatu za kisheria mahakamani, hata hivyo bungeni amekuwa mkimya wala kutoonyesha msimamo wake juu ya kashfa nzito nzito zotokeazo serikalini.

Lowasa Kujipitishapitisha kwenye mikusanyiko na mtukio aonwe na wapita kura
Kilichoendelea ni kujipitishapitisha kwenye matukio na mikusanyuiko ambayo vyombo vya habari huwepo na pia uchangiaji usiokoma katika nyumba za ibada jambo ambalo awali hakuwa analifanya.

Lowasa kukiri marafiki wanamchangia pesa za kampeni
Maswali ya wengi anapata wapi pesa hizo anazotoa misaada na kufanya kampeni, jibu alilotoa hadharani ni kuwa anachangiwa na marafiki wake, hata hivyo hakubainisha marafiki wake ni nani wala kutaja majina yao.

Chenge kuteka Rasimu ya katiba ya Warioba/Rostam kuuza hisa zake VODA
Kilichoendelea ni matukio mawili yasiyo kawaida ambapo CCM iligeuka ghafla na kuikataa Rasimu ya Warioba ambaye ni kada wa Chama cha Mapinduzi pamoja na timu yake ambayo iliwekwa na kutawazwa na serikali ya CCM yenyewe kuendesha mchakacho wa katiba, kisha Andrew Chenge akajitwisha mzigo kuileta rasimu ya katiba aliyoiandaa na kufuta vifungu vyote vilivyokuwamo kwenye Rasimu ya Warioba kuhusu kuwabana mafisadi.

Miezi michache iliyopita Rostam Azizi ameuza baadhi ya hisa zake za Voda Com kitendo kinachoweza kuzua maswali mengi wakati tukielekea uchaguzi mkuu, kama si kuongeza mtaji wa pesa za kampeni za Lowasa au ni kibiashara tu?

Kwa kuunganisha dot kufanya msitari hakuna shaka mashaka kwamba hawa mapacha watatu kuna ushirikiano wa hali na mali na ndio maana tumeona Lowasa kuwa na nguvu sana ya pesa katika safari ya kwenda MAGOGONI. Pia marafikiwa wanaomchangia pesa Lowasa hawa marafiki wenzake vigumu kuchomoka maana ni kundi moja la mafisadi papa watu walioanikwa bayana na chama chao.

Chama kutowasafisha tuhuma za ufisadi wa kukichafua chama
Tuhuma za kuwa mafisadi papa hawa watatu chamani na kwamba wanakichafua chama bado hazijasafishwa kwa watanzania wakati suala hilo limezimika kiaina bila kujua nini kitaendelea, papo hapo fisadi mojawapo ndani ya hao watatu kuwa katika mbio za kupeperusha bendera ya CCM kugombea kiti cha Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Kauli ya Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi wakati akifungua kikao mojawapo cha kichama safari hii Dodoma, licha ya hotuba yake kukubaliwa na wasomi kuwa ameonyesha ukomavu kisiasa, jambo jingine alilosema kimafumbo kuwa Bwana mmoja anajiona yuko juu ya wote na hivyo tuwe makini kuchagua atakayeuzika chamani.

Hii ni dalili wazi kuwa CCM sasa hivi ipo mikononi mwa mafisadi, na ndio maana uwezo wao kifedha unawafanya kuwanunua au kuwagawa wajumbe na hivyo kuwashika wale ambao wanaona ndio watakaofanikisha timu ya mafisadi kuingia Ikulu.

HITIMISHO
Timu ya mafisadi inatumia nguvu nyingi ya pesa, pesa hizo wakishakuwa madarakani watahitaji kufidiwa, je nani atakayeumia kama si mpiga kura. Mtindo anaotumia Lowasa na timu yake kuingia Ikulu haitofautiani na ule uliyotumiwa na Kikwete, matokeo tumeyaona taifa kubebeshwa zigo la madeni, pesa za umma kushindaniwa na watumishi kutia mifukoni mwao, ufisadi kukirithi, uvunjaji haki za binadamu kushamiri, unyanyasaji vyama vya upinzani kushika kasi, vyombo vya dola kuingia katika kashfa ya kunyanyasa wananchi, nk.

Source:By Candid Scope- JF

Mwanamuziki Diamond Adaiwa Kuwatelekeza Watoto Shule..Akwama Kuwalipia Ada..Ni wale Walioshinda Kucheza Ngololo na Kuahidi Kuwasomesha

$
0
0
Gladness Mallya
KABANG! Staa anayevuna fedha nyingi kupitia kipaji chake cha muziki, Bongo, Nasibu Abdul ‘Diamond’ amewatelekeza watoto katika Shule ya East Africa International jijini Dar ambao aliahidi kuwalipia ada, Risasi Mchanganyiko linakuwa la kwanza kukudondoshea.

Chanzo makini kililiambia gazeti hili juzi kwamba, baada ya Diamond kuwashindanisha watoto hao, Hillary na Hamis (katika picha no. 1 na 2 zilizoko ukurasa wa mbele walipelekwa shule na Diamond) katika shindano la Ngololo lililonyika Januari, mwaka jana katika Viwanja vya Leaders Club, Dar na kushinda aliamua kuwapeleka katika shule hiyo na kuahidi kuwalipia ada kila mwaka lakini kuanzia hapo aliwatelekeza.

“Jamani Diamond kila kukicha anafanya shoo za mamilioni lakini ameshindwa kuwalipia ada wale watoto ambao aliahidi kuwasomesha. Wamesoma mwaka mmoja tu,  mwezi uliopita walitimuliwa na sasa wako nyumbani. Inauma sana kwani hawa watoto walitolewa kwenye shule za kawaida na yeye ndiyo akawapeleka kule,” kilisema chanzo hicho.

WAZAZI WANASEMAJE?
Akizungumza na gazeti hili, mmoja wa wazazi wa wanafunzi hao, Fadhili alisema watoto wao walitimuliwa shuleni tangu April mwaka huu kwa kuwa, Diamond hakuwahi kuwalipia ada tangu alipowaingiza pale.“Inauma sana, kwani tangu watoto wetu watimuliwe tumekuwa tukifuatilia kwa mtu tuliyeambiwa ni msimamizi wa Diamond (jina lake linahifadhiwa kwa sasa) lakini hatupi jibu la kueleweka.

“Tulipewa namba za simu za mameneja wa Diamond, Hamis Taletale ‘Babu Tale’ na Said Fella lakini kila tukiwapigia simu tunaambiwa msanii huyo hayupo Dar, mara amesafiri, mara yuko kwenye shoo, yaani kila siku tunazunguka tu hatujui tufanye nini.

“Tunaomba sana jamani, mtusaidie na nyie waandishi maana watoto wanapitwa na masomo na isitoshe kabla ya hapo walikuwa wakisoma kwenye shule za kawaida,” alisema mzazi huyo.

MSIKIE MWALIMU MKUU
Paparazi wetu alifunga safari mpaka shuleni hapo maeneo ya Mikocheni, Dar na kufanikiwa kuzungumza na Mwalimu Mkuu, Mercy Githirua ambapo alithibitisha watoto hao kusimamishwa masomo kutokana na kukosa ada.“Tulivumilia kwa muda mrefu sana kwani tulimwamini Diamond tukawapokea watoto hao na kuanza masomo. Siku aliyokuja kuwakabidhi hapa shuleni aliomba ‘invoice’ kwa ajili ya kututumia  ada lakini yuko kimya mpaka leo.

“Hata fedha ya kuwashonea sare za shule ilibidi niwasiliane na (linatajwa jina, linasitiriwa) maana tunafanya naye kazi nyingi, akatoa hizo fedha lakini ada ndiyo ikawa tatizo. Hivyo ilipofika Aprili 14, mwaka huu ilibidi niwarudishe nyumbani mpaka kieleweke kwa kweli.

“Sijapenda tabia ya Diamond, hivi anajua watoto wakimchukia itakuwa ni hatari sana kwake? Watoto wa watu walikuwa wanasoma huko akaenda kuwatoa na kuwaleta hapa lakini amewatelekeza, siyo vizuri kabisa,” alisema mwalimu mkuu huyo.

WANADAIWA SHILINGI NGAPI?
Kwa mujibu wa mwalimu mkuu huyo, watoto hao tangu walivyoingia Januari 21, 2014 hawakuwahi kulipiwa ada yoyote hivyo kila mmoja anadaiwa shilingi milioni moja na laki sita (1,600,000).

DIAMOND, MAMENEJA WAKE!
Juzi, gazeti hili lilifanya jitihada za kumtafuta Diamond kwa njia ya simu lakini ilikuwa imesetiwa kwamba inafanya kazi muda wote ‘bize’ hata alipotumiwa meseji hakujibu. Vivyo hivyo kwa mameneja wake, Fella na Bab Tale simu zao ziliita bila kupokelewa.

TUJIKUMBUSHE
Mwaka jana, Diamond aliandaa shindano la Nani Anaweza Kucheza Staili ya Wimbo wa Ngololo ambapo watoto kibao walijitokeza Leaders Club. Watoto hao wawili waliibuka kidedea kwa kuonesha uwezo mkubwa wa kucheza na ndipo zawadi yao aliamua kuwapeleka kwenye shule hiyo na kukutwa na yaliyowakuta!

GPL

Mi ni Team Kiba But I Still love Diamond’s Music, That Boy Can Really Sing – Wema Sepetu

$
0
0
This is a love and hate type of sh*t. Wema Sepetu amekiri kuwa upande wa Alikiba lakini bado anazipenda nyimbo za mpenzi wake wa zamani, Diamond.


Unakipata kizungumkuti cha kauli hiyo sio? Hivi karibuni Wema alitengeneza vichwa vya habari kwa kuonesha support kubwa kwa Alikiba (hasimu wa Diamond) katika kumuombea kura za KTMA. Kwa wengi hiyo ilitafsiriwa kama kisasi cha Wema kwa ex wake. Na wengine walihisi Kiba na Wema wana lao jambo! Lipi?

Hata hivyo kupitia kipindi cha Ala za Roho cha Clouds FM, Jumatatu hii, Wema alisema Kiba ni mtu wake wa karibu tangu siku nyingi na humuita jina la utani ‘bichwa’.

Ali and I are very good friends,” alisema Wema. “Ali alinitumia meseji kwenye whatsapp akanitumia picha (za KTMA) kama nne, nikamuambia ipi? Akaniambia zote, nikapost zote, akaniambia ntakutumia zingine. Nikamuuliza ‘hivi umetajwa kwenye category ngapi kwenye Kili? Akaniambia saba. Nikamwambia fresh nitumie zote nitakupost. Akaniambia poa na wewe nitumie post zako za Tuzo za watu and I took it as a support, namsupport mshkaji wangu. Mimi ni team Kiba.

Hata hivyo Wema alisema haoni kama kuna tatizo kama akiwa team Diamond pia.

I love his [Diamond] music. Mtu akikaa leo akisema kwamba Diamond anaimba vibaya huyo atakuwa ni hater tu, the boy can really sing.”

Actress Shamsa Ford Shares New Hot and Sexy Photos wearing a Boyfriend Shirt like Faiza Ally Did on Zari's White Party

$
0
0
 Actress Shamsa Ford Shares New Hot and Sexy Photos wearing a Boyfriend Shirt like Faiza Ally Did on Zari's White Party...


Wema Sepetu Would faint if she saw this photos...Idriss and his Bae, Samantha

$
0
0

Check out Iddris Having Fun with his Bae Samantha, What do u think, is it cute or not?


Viewing all 104756 articles
Browse latest View live




Latest Images