Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104785 articles
Browse latest View live

Makabila ya Pwani Wanawezana Wenyewe Ndoa zao, ni Shidaaa!

$
0
0
Wadada wakicheza Ngoma Maarufu Pwani ijulikanayo kama Kigodoro
Watu wa Pwani wanawezana wenyewe kwa wenyewe ndoa zao,mtu wa bara utachemka tu.Ukanda wa pwani kuanzia Tanga, Pwani, Dar, Lindi, Mtwara, Ruvuma na hata Morogoro pia ni walewale tu tabia, mila na desturi zao.

Vigodoro kwa sana, kushinda ngomani, shule kwao ni kama adhabu, vitabia vya ajabuajabu tu,ni shida...Yaani imefikia hata maendeleo katika Sehemu zao yapo duni sana ..Kama ukiangalia Bagamoyo kwa sasa Wahamiaji ndio wanaoleta maendeleo kwa kununua mashamba na viwanja vya wazaramo na kuwaacha wenyeji hawana kitu ..

Hili Ndo Jukwaa Ambalo Edward Lowassa Atalitumia Kutangaza Nia LEO Ya Kugombea Urais 2015........Hapa kuna picha 5

$
0
0
Leo Mbunge wa Monduli Edward Lowassa atatangaza nia ya kugombea Urais katika uwanja wa Sheikh Amri Abeid  jijini Arusha.Maandalizi mbalimbali yanaendelea huku ilinzi ukiimarishwa kila kona.

Mamia ya wananchi wanaendelea kuingia katika uwanja huu kutoka mikoa mbalimbali nchini Tanzania ikiwemo Dares salaam,Arusha,Dodoma,Kagera,Mwanza na Mbeya

Kila mtu katika uwanja pamoja na Watanzania wana shauku ya kutaka kufahamu Edward Lowassa atasema nini kuelekea katika uchaguzi wa Rais utakaofanyika wiki ya mwisho ya mwezi oktoba mwaka huu 2015.

Video mpya ya Diamond Ft. Mr. Flavour-Nana

$
0
0

Video mpya ya Diamond Ft. Mr. Flavour-Nana

Wema Sepetu na Idris Nusura Wazichape

$
0
0
Malkia anayemiliki Kampuni ya Endless Fame Production, Wema Isaac Sepetu na Mshindi wa Big Brother Africa 2014/15, Idris Sultan ambao wamekuwa marafiki wakubwa katika siku za hivi karibuni, nusu wazichape kavukavu baada ya kupishana kauli huku wivu wa kimapenzi ukitajwa.

Tukio hilo lilijiri mwishoni mwa wiki iliyopita nje ya Hoteli ya Hyatt Regency Dar es Salaam, The Kilimanjaro iliyopo Posta jijini Dar ambapo kwa pamoja walikuwa wamehudhuria sherehe ya utoaji Tuzo za Watu.

Kwa mujibu wa shuhuda wetu, tafrani ya wawili hao kutaka kukunjana ilitokea baada ya kumalizika kwa shuguli hiyo ambapo Idris alimpora Wema tuzo yake aliyoshinda na kwenda nayo kwenye gari lake.

Ugomvi huo ulipamba moto na kusababisha watu waliokuwa wakiwashuhudia kutaharuki ambapo Wema alikwenda kwenye gari lake lililokuwa likiendeshwa na Petit Man lakini Idris alimfuata akionekana kumuonea wivu na kumtaka apande gari lake waondoka jambo ambalo Wema alilitolea nje na kumfungia kioo.

Baada ya kuona Wema amemtolea nje, Idris alikwenda kwenye gari lake na kuliegesha mbele ya gari la Wema ‘kum-block’ ili asiondoke ambapo alishuka na kumwambia Petit Man ahakikishe anamfuata kwa nyuma jambo ambalo Petit Man alishindwa kulitekeleza baada ya Wema kukataa.

Baada ya kushuhudia vurugu hizo, mwanahabari wetu alimfuata Wema ili kujua kilichotokea ambapo mwanadada huyo alisema kuwa haelewi ni kitu gani ambacho kilimkuta Idris siku hiyo maana kama angekuwa anakunywa pombe, angesema labda alizidiwa lakini kwa kilichotokea hadi leo hajui ni kipi kilimkuta.

“Yaani hata sielewi Idris alifikwa na nini maana amefanya mambo ya ajabu sana na mara ya kwanza nilijua utani lakini nilimshangaa zaidi baada ya kukomaa hadi kufikia hatua ya kuni-block na gari lake huku akitaka niondoke naye wakati kila mtu alikwenda pale kimpango wake.

“Mimi nadhani kuna utoto fulani bado anao na unamsumbua,” alisema Wema lakini Idris hakupatikana kusema chochote.

Credit: Gpl

Hawa Ndio wasanii wa Bongo Fleva Wenye Sauti Mbaya

$
0
0
Kabla sijamwagika, ieleweke tu kuwa mimi nipo kwenye hii industry pia, na ninakaribisha walio kwenye hii game wachallenge hoja, simaanishi mashabiki au wasikilizaji wa muziki, bali producers na waimbaji.

Kwanza nitoe somo kuhusu sauti:
Kuna aina 2 za sauti kwenye uimbaji - 1) Long Wave na 2)Vibrating Wave. Waimbaji wote wenye sauti nzuri wanaangukia kwenye hizi category 2 na wale wenye sauti mbaya wanaangukia kwenye category ya kwanza (Long wave) ila wakiwa na kasoro hasa za kibailojia upande wa makoo, pua na sauti zao kwa ujumla.


Long wave: Hii ni sauti iliyonyooka bila mawimbi. Mfano wa wasanii wenye sauti ya hivi hapa bongo ni Vanessa Mdee, Lady Jay Dee, Ommy Dimpoz, Bob Junior na Ulaya ni Chris Brown, Justine Bieber, Taylor Swift n.k.

Vibrating Wave: Hii ni sauti yenye mawimbi hasa mwishoni mwa maneno/sentesi na ndio sauti tamu zaidi duniani. Kibongongo tunao Ali Kiba, Diamond, Ben Pal, Linah, Vumi na Ulaya ni kv; Rihanna, Beyonce, Adele, Bruno Mars n.k.

Sauti mbaya ya muimbaji husababishwa na vifuatavyo:
Haimbi kwa sauti inayotoka tumboni, anaimbia kwa kutumia koo la sauti ambalo matumizi yake ni sauti ya kuongea katika hali ya kawaida...na mwingine huharibu zaidi kwa kuipitishia hiyo sauti puani, na kwa ujumla wako kwenye category ya Long wave. Wengi nyimbo zao zimejaa Autotune (ubadilishaji wa uhalisia wa sauti unaofanywa na Producer) na Voice-overs nyingi (unaskia ni kama kwaya wakati anayeimba ni mmoja), yote hii ni kuficha ubaya wa sauti. So sauti zingine huenda ziliumbwa kwaajili ya fani ya kutangaza mpira au kuongoza jeshi la mgambo, sema ndio hivyo...riziki popote.

Sasa kwa hapa bongo wafuatao ndio wenye sauti mbaya:
Shetta
Aika (huyu namjua kwa ukaribu zaidi maana few months back nilikuwa "friends with benefit" na dada yake mkubwa pale Arusha)
Shilole
Mina
Snura
Joh Makini (huyu ni ngumu kufocus kwenye ubaya wa sauti yake kwasababu ana art kwenye uimbaji wake, anacheza maneno, illa ubaya wa sauti yake ni kuitolea puani. Na hili swala liko nje ya uwezo wa mtu kiujumla maana ndio maumbile ya sauti yake)


Karibuni kwa mchango/kuongezea wengine.

Lemutuz 'siwezi kuoa Mbebezz wa Instagram NEVER cause Maisha yetu Yatakuwa ni Instagram tu Mkigombana Kidogo Instagram Nzima Wanajua'

$
0
0
EXTRA LIVE TALK:- People unajua unakuwa mjinga kama una AKILI KUBWAZZ halafu hujijui no mimi ni AKILI KUBWAZZ na ninajijua ninafanya mambo yangu kwa strategies zamani nilikuwa naandika sana ujinga cause nilishajua ndicho Wananchi wa Tanzania wnachopenda na ili kuwaonyesha ni AKILI KUBWAZZ kwanza lazima nitafute their100% FULL ATTENTION now nimeshaipata ndio maana siku hizi naandika 90% serious ishuz na bado 10% naandika pumba cause nisipochanganya AKILI KUBWAZZ na PUMBA nitakosa watu hapa...ndio maana nashindwa.kuoa tena unatakiwa kuoa mpenzi mnayefanana akili japo hata 75% cause siwezi kurudia makosa n almost kila mbebebzz anafikiria PESA na WATU WATAMUONAJE KWENYE JAMII sio moyo wake unamwamabia nini ukikuta Mbebez ana akili na.pesa ni MSAGAJI au HATAKI MAPENZI KABISA siwezi kuoa Mbebezz wa Instagram NEVER cause maisha yetu yatakuwa ni Instagram tu mkigombana kidogo Instagram nzima wanajua hahha so I am stuck....zamani wabongo tulikuwa na akili sana sijui kilitutokea nini yaani mbongo akienda majuu watu kama FREDDY MACHA au ATHUMANI MAGOMA walikuwa wanaishi majuu wanandika AKILI KUBWA kwenye Social Media jamani tazama siku hizi wale wote maarufu I mean wabongo wanaoandika Social Media ni mabingwa wa matusi tu kama.nasema uongo hebu mtaje mbongo mmoja.tu aliye majuu anayesifika kwa kuandika Sense? wote wanaofahamika ni MABINGWA wa matusi I mean huwa inanishangaza mbongo yupo majuu anatukana watu wanaoishi Tanzania mpaka.na.details zao za.jana walikuwa wapi na juzi walikuwa wapi Mungu wangu mtu unaishi First World badala ya kusaidia wenzio waliobaki wewe ni kuwatumia MATUSI.TU halafu watu wanalalamikia Viongozi kwa.nini Taifa haliendelei hahahahah tutakufwa wote hapa hamna maendeleo.mpaka.tutakapobadilika sometimes huwa nafikiria kuiomba Serikali inipe.ruhusa niwapitishe waya wa umeme vichwani Wananchi wote mtaani labda wataamuka mazafantazzz I mean dead people walking tumetoka kuadhibiwa na mvua majuzi kisa miaka 53 ya uhuru.hatuna serious Miundo Mbinu leo watu wamesafiri kwenda kuunga mkono wagombea Urais waliowahi kuwa Serikalini for the last 40 years ungetegemea wananchi wenye akili wapige kelele kwamba wagombea wote hawafai mazafantazzz! CHANGE! - le Mutuz

Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Paul Makonda Afunguka Kutembea na Mrembo wa Bongo Movies, Kajala Masanja

$
0
0
BAADA ya kuzagaa kwa habari kwamba Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Paul Makonda ‘kutembea’ na mrembo wa Bongo Movies, Kajala Masanja, mheshimiwa huyo ameibuka na kuzungumzia tuhuma hizo kuwa hazina ukweli wowote zaidi ya kutaka kumchafua katika uongozi wake.

Mapema wiki hii, mitandao mbalimbali ya kijamii ilimtuhumu mheshimiwa huyo kwamba ana uhusiano na muigizaji huyo kwa kudai amekuwa akionekana naye mara kwa mara.Makonda ambaye ameonesha uchapakazi uliotukuka baada ya kuteuliwa na rais Jakaya Kikwete kuwa mkuu wa wilaya hiyo mapema mwaka huu, ameweka bayana kuwa kwa muda mrefu kuna watu wenye nia mbaya ambao wanaendesha kampeni ya kumchafua.

“Ni muda mrefu tu, walianza kipindi kile wakati wa Bunge la Katiba nilipokwenda Bungeni na mwigizaji Yobnesh Yusuf ‘Batuli’, wakasema natembea naye, wakanyamaza. Sasa wamehamia kwa Kajala baada ya kufanya naye kazi.

Hakuna ukweli wowote wanatungatunga tu mambo, watakuwa na sababu zao kwa sababu mtu kama Kajala, maneno yameibuka baada ya kufanya naye project ya kutafuta vipaji vya wasanii.“Nimeshirikiana na wasanii wengi wa kiume katika project hiyo lakini kwa kuwa wameona mwanamke ni Kajala peke yake, wanasema vitu ambavyo havina kichwa wala miguu. Najua kuna wengine wanaoeneza haya mambo wanatumika kisiasa lakini mimi sijali.

Waniache nifanye kazi, najitoa kwa wasanii kwa nia njema ya kutafuta wasanii ambao baadaye wataweza kujitegemea kwani sanaa ni ajira, kamwe hawawezi kurudisha nyuma juhudi zangu,” alisema Makonda ambaye amejiwekea utaratibu wa kukutana na wakazi wake kila Ijumaa kutatua migogoro ya ardhi.
GPL

Mimba ya Zari yawa LULU Yamwingizia Diamond Mamilion

$
0
0
Musa Mateja
Imebainika kuwa mimba ya mwandani wa mwanamuziki Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’, Zarinah Hassan ‘Zari The Boss Lady’ inamwingizia jamaa huyo mamilioni ya fedha, Ijumaa limebaini mchezo mzima.
KUMBE!

Imeelezwa kwamba, katika kila shoo anayokwenda na mama kijacho huyo amekuwa akilamba dau kubwa kwani wengi wanahudhuria burudani inayotolewa na Diamond ili kumuona Zari akiwa na kibendi.Uchunguzi wetu ulibaini kwamba, ujauzito wa Zari kwa sasa unamuingizia mkwanja mrefu Diamond kufuatia kila shoo anayohitaji kwenda kufanya, mapromota wengi wamekuwa wakimtaka aende na Zari ili tu mashabiki wamshuhudie.

TUJIUNGE NA CHANZO
Katika uchunguzi wake, Ijumaa lilizungumza na vyanzo mbalimbali akiwemo mtu wa ndani ya Wasafi Classic Baby (WCB) ambaye alithibitisha kuwa ni kweli uwepo wa mimba ya Zari kwa sasa umeongeza mamilioni ya fedha kwa Diamond kupitia shoo ambazo amekuwa akihitajika na mapromota kwenda na Zari.

DIAMOND ASHTUKIA 
Chanzo hicho kilimwaga ‘ubuyu’ kuwa, Diamond ameshalishtukia jambo hilo kiasi kwamba kuna sehemu sasa analazimika kwenda na Zari kwa siri.

ZARI AFICHWA MWANZA
Ilifahamika kwamba, kwenye Shoo ya Jembeka iliyofanyika mwishoni mwa wiki iliyopita jijini Mwanza, Diamond alikwenda na Zari kwa kificho kikubwa kiasi kwamba hata umati uliyojitokeza kumpokea uwanja wa ndege jijini humo hawakuweza kumuona kwa kuwa makubaliano yake na waandaaji hayakumhusu Zari.

“Alichokifanya Diamond ni kumficha hotelini kwa kuwa katika shoo hiyo mapromota walikuwa hawakuelewana naye kwenda na Zari kama ilivyo kwenye shoo nyingine anazofanya kwa sasa,” kilisema chanzo hicho cha kuaminika na kuongeza:

“Ni kitu ambacho Watanzania wengi hawakijui lakini ukweli uko hivyo kwamba, Diamond kwa sasa anavunja mkwanja mara mbili anapokuwa na Zari.”

BEI MARA MBILI?
Ilidaiwa kwamba kama Diamond alikuwa anachukua Sh. milioni 25 kwa shoo za ndani, kwa sasa akiwa na Zari ni mara mbili yake kwa hiyo inakuwa si chini ya Sh. milioni 50.

SHOO ZA KUMWAGA ZA NJE
Chanzo hicho kilieleza kwamba kwa shoo za nje ndiyo usiseme na tayari ameshaingia mikataba ya fedha ndefu kwenye nchi mbalimbali akiwa na Zari zikiwemo, Afrika Kusini ‘Sauzi’, Nigeria, Ghana, Cameroon, Togo, Angola na nyingine kibao.

DIAMOND ABANWA, AFUNGUKA
Baada ya kunyetishiwa ubuyu huo, mwanahabari wetu alimtafuta Diamond na kumbana ili afunguke juu ya hilo ambapo alipopatikana alikiri kwamba ni kweli kwa sasa mapromota wengi wamekuwa wakimhitaji kwenye shoo akiwa na Zari.
Diamond alisema kuwa, jambo hilo ni zuri ila kila mmoja ana malipo yake kwa maana wakitaka aende naye bei inakuwa tofauti ukilinganisha anapokwenda mwenyewe au na timu yake ya Wasafi.

Diamond: Nikiwa naenda kwenye events (matukio) namuuliza kwanza promota kama atahitaji niende na Zari? Akinijibu ndiyo, gharama inaongezeka.Ijumaa: Kwa hiyo unamaanisha kwa sasa ukienda kwenye shoo bila Zari kuna bei yake na ukienda naye unatakiwa ulipwe bei tofauti?

Diamond: Naam, namaanisha kwamba nikienda na Zari, lazima kuwepo na gharama za uwepo wake.
Ijumaa: Ni jambo gani lililokufanya kushtukia hilo hadi unasema hivyo?
Diamond: Ujue sasa hivi imefikia hatua nikiposti kwenye peji yangu kwamba kuna shoo nitaenda na Zari, idadi ya watu inaongezeka hata kama sitaingia naye ukumbini.

Ijumaa: Zari anajisikiaje mimba yake kufanywa ya maonesho?
Diamond: Zari ni mtu wa hekaheka hivyo hana tatizo kwani usalama wake upo wa kutosha.

DIAMOND Getting All Cozy with Pregnant ZARI’s bo0ty in Public

$
0
0
DIAMOND getting all cozy with pregnant ZARI’s b@@ty in public

Check out VERA’s well curved ‘money maker’! Every man needs these PHOTOs in his room

$
0
0




Check out VERA’s well curved ‘money maker’! Every man needs these PHOTOs in his room

Amber Rose Shares Half Nude sultry Photo in the Pool...

$
0
0
Ms. Amber Rose shared this sultry photo of her chilling in the Pool half nude.

Baada ya Mwaka Moja, Leo Monalisa Atoboa Mazito Kuhusu Kilichotokea Kwenye Msiba wa George Tyson

$
0
0
Leo ikiwa ni mwaka mmoja toka aliekuwa muongozaji wa filamu na vipindi vya TV hapa Bongo, George Tyson kufariki dunia, mwigizaji  Yvonne Cherrie ‘Monalisa’ ambaye alizaa na marehemu  afunguaka mazuto kupitia ukurasa wake mtandaoni.

Mara baada ya kubandika picha hiyo hapo juu monalisa akiwa na marehemu Tyson na mtoto wao, monalisa aliandika;

Wiki 78 zilizopita @jojityson alipost hii pic na kuandika
My family @monalisatz @soniamonalisa

Leo ni mwaka mmoja toka uondoke George..bado ni ngumu sana kwetu.Ulipoondoka mengi huku nyuma yamesemwa kama unavyowajua wabongo kwa kuongea,wengine waliniporomoshea matusi eti najishaua nalia nini?mmh!wabongo bana.wanaojifanya ndugu zako eti nao wakaanza kukimbilia mali,bila hata kujua zilitoka wapi,umezipataje..kweli nilikuwa naonaga hivi vitu kwenye muvi ila bwana yametokea baada ya ww kuondoka.Ila nakushukuru sana sehemu ulizoandika mwenyewe ulimkumbuka sana Sonia na Eugene,watoto ambao mm nawafahamu.Mali zingine hadi leo watu wamesepa nazo ila tumeamua kuwaachia maana ni mali tu zinapita.Sonia is doing good shuleni japo mwanzoni alikuwa anatoka nje na kulia peke yake,ss hv amemove on na bado pia anasoma shule ya music na siku ya kuagwa kwako alikuahidi she ll never stop singing for you...nitarudi kukupa story zingine maana najua mwaka mmoja ni mwingi na umepitwa na mengi japo naamini kwamba Umepumzika kwa Amani...George

Monalisa akaadika tena

Eti leo nasikia kuna ibada ya kukuombea.Duh!hii kali nimeisikia kwenye social media tu.walivyoona wameharibu naanza kutumiwa sms kwa fujo.Mmh!tunashukuru wanakukumbuka hata kukuombea lakini isiwe tu ni namna nyengine ya kujipatia ela.Maana siku ya kuagwa kwako pale Leaders Club watu waliombwa kutoa sadaka kwa ajili ya watoto ila ziliishia tumboni mwa wanaojua kula ela..wengine waliahidi kwa jinsi ulivyowasaidia wangemsaidia Sonia..loh!ilikuwa ni gia ya kuondokea hakuna mtu aliyemsaidia narudia HAKUNA.si ndugu zako,si rafiki nasema HAKUNA.
Nitarudi tena George..nina mambo mengi ya kukueleza..Pumzika kwa amani

ARUSHA KWALIPUKA, Hakuna pa Kukanyaga... Na Wazungu pia Wamo..

$
0
0
ARUSHA KWALIPUKA, HAKUNA PA KUKANYAGA... Na wazungu pia wamo.......leo ni Mh. Edward Lowassa ndani ya Arusha ataongea leo mchana kwenye uwanja wa Shekh Amri Abeid.
Read more at http://websta.me/n/mrekebishatabia#7fObsFL71sKRgPjO.99

Kundi la UHURU la Sauzi Afrika Lamuomba Diamond Platnumz Kufanya Remix ya Wimbo wa Nana Uliotoka Jana na Kuwa Gumzo Afrika.

$
0
0
Diamond ni Star Africa kuliko watanzania tunavyomchukulia wakati Kundi la Uhuru Kutoka Sauzi Afrika wakiomba kufanya Remix ya Wimbo wake Mpya wa Nanaa, Usiku wa kuamkia leo nchini Nigeria video ya nana ilikuwa gumzo kwenye mitandao. Wabongo sijui kwanin hatupendi vya kwetu siku Diamond Platnumz mungu amemchukua hawa wanao mbeza na kumtukana ndo wanafiki wa kwanza kujifanya kulia hadi kuzimia huku wakimsifia......

Diamond ni kiboko..Hakunaga.......

Mashabiki Wamvaa IRENE PAUL Baada ya Kutoa Kauli ya Kuudhi ..Wasusia Movie zake

$
0
0
Baada ya siku kadhaa muigizaji irene paul, kupokea Tuzo ya muigizaji bora wa kike mwaka 2015 (TAF) , Msanii huyo amejikuta kwenye wakati mgumu baada ya ivi karibuni kufanyiwa mahojiano na kituo kimoja cha television ,ambapo aliulizwa swali na mwandishi, ni movie ipi ya kibongo anayoikubali?, ndipo msanii huyo alipofunguka bila kumung'unya maneno kuwa sio muangaliaji wa bongo movie, hivyo hajui chochote. kauli hiyo ilizua tafrani kwa baadhi ya mashabiki zake ambao walimjia juu muigizaji huyo mwenye makeke ya aina yake awapo mbele ya camera.

Baadhi ya Comments 

# 1: Huyu dada anajisikia sana, hajui kuwa sisi ndio tuliomfanya awe mtu, bila kuigiza nani angemjua apa mjini? Sijapenda kauli yake ata kidogo.

# 2: Najuta kabisa kwa nini nilimpigia kura, kama yeye msanii haangalii bongo movie, sasa sisi tuangalie ili iweje? Atakula jeuri yake mwaka huu, hiyo tuzo ndio ya mwisho.

# 3: Kwanza mie sionagi uigizaji wake zaidi ya kupiga kelele ovyo na kujitutumua kama anataka kukata roho, mimi simkubali huyo dada anajisikia sana.

# 4: Kuna siku nilikutana nae mlimani nikamuomba kupiga nae picha akaniambia yeye sio irene Paul nimemfananisha, ata hivyo niliomba tu kupiga nae picha kwa kuwa nilimpenda, jibu alilonipa eti mi msumbufu sana ,yeye yupo busy na mambo yake, kweli anatujibu hivyo mashabiki zake? Nilisikia aibu sana kwa kweli aliniaibisha mbele za watu,sitakaa nimpende.

# 5: Kama haangalii kazi wanazofanya wenzie atajuaje changamoto zilizopo kwenye filamu na kuzifanyia kazi? Kauli yake sio nzuri, kwa hiyo anatuona tunaoangalia kazi zao hatuna akili?

# 6: MUongo mkubwa anajishaua tu, anajifanya anafanana na angelina jolie na mishavu yake kama panya, simpendi huyo dada.

# 7: Mi namkubali sana irene paul, ila hiyo kauli sio nzuri, ata kama ni kweli aangalii ni bora anfefikiria kabla ya kuongea, by the way mi namkubali tu.

#8 : Kwanza hiyo tuzo kapewa kwa uigizaji upi? Mi sijaona anachoigiza zaidi ya kutumia nguvu kuliko akili, kama haangalii bongo movie anaigiza ili iweje? Basi akaigize ulaya

# 9: Huyu dada anajiona mzuri wakati kakomaa kama nazi, kwanza kuigiza hajui, kanichefua sana, tutakua hatuangalii movie zao tuone hizo jeuri watapatia wapi

# 10: KWa hiyo kapata tuzo ndo anajidai kuropoka? Sasa akipata oscar si ndio ataikana kabisa Kuwa yeye sio muigizaji wa Tanzania?

Hotuba Ya Mh. Edward Lowassa Aliyoitoa LEO jijini Arusha Wakati Akitangaza Nia Ya Kuomba Kuteuliwa na CCM Kuwa Mgombea Urais Wa Tanzania

$
0
0
UTANGULIZI:

Ndugu zangu wana-CCM na Watanzania wenzangu,

Hii ni siku muhimu kwangu na kwa nchi yetu. Leo nimeamua kuwaita ili kuwatangazia rasmi Watanzania wenzangu azma yangu ya kutaka kuomba ridhaa ya chama chetu, Chama Cha Mapinduzi (CCM), niweze kuteuliwa kuwa Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Nasema hii ni siku muhimu kwangu kwa sababu naamini historia yangu itainakili kama ni siku ambayo kwa mara ya pili katika maisha yangu nimejitokeza kuwania kuiongoza nchi yetu kupitia chama chetu. Mara ya kwanza ilikuwa ni mwaka 1995 wakati wa uchaguzi wa kwanza wa vyama vingi hapa nchini nilipojitokeza nikiwa pamoja na Rais Jakaya Kikwete; wakati ule sote tulikuwa wanasiasa vijana. Tulikwenda pamoja kuchukua fomu ndani ya Chama na baadaye tukafanya mazungumzo ya pamoja na waandishi wa habari. Tulileta hamasa kubwa pale tulipofanya jambo ambalo halikuzoeleka kwa Watanzania kwa kutangaza kwamba yeyote atakayepita kati ya wawili sisi basi mwenzake ambaye hatafanikiwa angemuunga mkono.

Ningeweza kujitokeza tena mwaka 2005 lakini nikaamua kwa dhati kabisa kumuunga mkono moja kwa moja Rais Jakaya Kikwete.
 
 Nikiwa Mwenyekiti wa Kampeni niliwaongoza wenzangu kufanikisha ushindi mkubwa wa mgombea tuliyemuunga mkono na baadaye ushindi mkubwa wa asilimia 80 wa Chama Cha Mapinduzi kwenye uchaguzi mkuu wa 2005.

Nitaeleza kwa nini nimeamua kujitokeza tena mwaka huu na kwa nini naamini mimi ndiye mtu sahihi wa kuiongoza nchi yetu wakati huu. Mpaka hapa itoshe tu kuwaeleza ni kwa kwa nini naamini leo ni siku muhimu kwangu.

Lakini nasema ni siku muhimu kwa nchi yetu pia. Nasema hivyokwa sababu naamini inajibu wito wa mahitaji ya sasa ya uongozi wa Taifa letu wa kumpata kiongozi imara atakayewaongoza Watanzania kujenga taifa imara. Na hili pia nitalieleza kwa kina.

Hali  ya  Nchi  na  Matarajio  ya  Watu:
Miaka 48 iliyopita katika jiji hili la Arusha, Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage alianzisha mchakato wa kujenga taifa huru kiuchumi na kupiga vita maadui umaskini, ujinga na maradhi kwakutumia silaha ya kujitegemea. 
 
Leo hii, wakati taifa likijiandaa kwa Uchaguzi Mkuu ujao, hatuna budi kutafakari tulikotoka, tulipo na tunapotaka kwenda ili tuweze kubuni upya mikakati ya kuhitimisha azma aliyo kuwa nayo Mwalimu, ili tujenge taifa huru, lenye utulivu, mshikamano, amani na maendeleo.

Nchi yetu hivi sasa inapita katika kipindi kigumu cha mpito katika maeneo yote makuu ya maisha yetu – katika siasa, katika uchumi na katika maisha ya kijamii.

Kisiasa, tumeshuhudia kuongezeka kwa vuguvugu la mfumo wa vyama vingi ambapo ushindani kati ya vyama vya siasa unazidi kuwa mkali na kwa bahati mbaya kufikia sura ya kuonekana kama vile ni mapambano ya watu binafsi badala ya mapambano ya sera na dira ya kuongoza nchi. 
 
Tunashuhudia kuongezeka uhasama binafsi kati ya wanasiasa ndani ya chama kimoja kimoja na pia kati ya wanasiasa wa chama kimoja dhidi ya kingine. Kadiri siku zinavyokwenda, hali inazidi kuzorota na ikiachiwa kuendelea nchi yetu inaweza kujikuta mahali pabaya. 
 
Kukua kwa ushindani ni jambo jema linalokomaza na kurutubisha demokrasia yetu na tukiwa na ushindani wenye afya unaweza kuwa chachu ya kuleta mabadiliko mema kwa wananchi na kupelekea kuongezeka kwa kasi ya maendeleo ya kiuchumi na kijamii katika nchi yetu. 
 
Kinyume chake ushindani unaochukua sura ya chuki binafsi au kukomoana na hata kulipizana visasi si ushindani wenye tija na tunapaswa kuutafutia tiba. 
 
Tunahitaji uongozi imara kusimamia kipindi cha mpito kutoka siasa muflisi za aina hii na kuelekea kwenye siasa mpya zinazoimarisha ushindani wenye tija unaojikita katika kushindana katika kuwapatia huduma bora Watanzania.

Kiuchumi, tumeshuhudia ukuaji mzuri na kuongezeka kwa mapato ya ndani ya Serikali na uimarishaji wa mfumo wa uwajibikaji na ulipaji kodi.
 
 Kwa upande mwengine, Serikali ya Rais BenjaminiMkapa na Rais Jakaya Kikwete imefanya kazi kubwa katika uendelezaji wa sekta ya mafuta na gesi asilia ambapo kiwango kikubwa cha gesi asilia kimegunduliwa.
 
 Tanzania sasa imekuwa ni miongoni mwa nchi zinazovutia uwekezaji mkubwa katika sekta hiyo ambayo inatajwa kwamba inaweza kuja kubadilisha kabisa maisha ya Watanzania. 
 
Hata hivyo, kipindi hiki cha mpito kuelekea ujenzi wa uchumi wa kisasa kimeshuhudia kuongezeka kwa hofu na wasiwasi miongoni mwa wananchi kwamba hawatonufaika naukuaji huu wa uchumi na ugunduzi wa utajiri mkubwa wa gesi asilia.
 
 Kwa upande mwingine, vijana wanataka kuona ukuaji wa uchumi na ugunduzi wa utajiri huo unakwenda sambamba na uzalishaji wa ajira zenye maana ili waweze kukabiliana na changamoto za maisha yao.
 
 Niliwahi kusema kwamba tatizo la ukosefu wa ajira likiachiwa bila ya kutafutiwa ufumbuzi imara ni bomu linalosubiri kulipuka. 
 
Vijana wasio na ajira hupoteza matumaini na ni rahisi kughilibiwa kuingiza nchi katika machafuko.Tunahitaji uongozi imara kuweza kuikabili hali hiyo na kuitafutia suluhisho maridhawa.

Kijamii, kipindi cha karibuni tumeshuhudia mabadiliko makubwa ya tabia miongoni mwa raia katika hali ambayo haijawahi kuwa sehemu ya utamaduni wa Watanzania.
 
 Kumekuwa na ongezeko la kutisha la matukio ya uhalifu linalokwenda sambamba na wananchi kuonyesha wanapoteza imani na taasisi zinazosimamia sheria na usalama na kuamua kujichukulia sheria mikononi mwao. 
 
Kumeripotiwa matukio mengi yakiwemo ya kuvamiwa vituo vya polisi, askari kupigwa na kuporwa silaha, matumizi makubwa ya nguvu katika utatuzi wa migogoro mbalimbali hasa ile ya kijamii, mathalani migogoro ya wakulima na wafugaji, mivutano ya kidini na pia mivutano baina ya viongozi wa dini wenyewe kwa wenyewe na baina ya viongozi wa dini na wale wa Serikali.
 
 Matokeo yakemshikamano wa taifa nao unaingia majaribuni. Mara nyingine wananchi wanatuuliza viongozi iwapo hii ndiyo nchi tuliyoachiwa na waasisi wetu. Tunahitaji uongozi imara wa kukabiliana na changamoto hizi na kurudisha mshikamano wa taifa letu na watu wake.


Watanzania  Wanataka  Mabadiliko;
Ndugu zangu, mnaweza kujiuliza kwa nini nimeyaeleza yote hayo na yana mahusiano gani na dhamira yangu ya kutangaza nia ya kutaka kuiongoza nchi yetu kupitia CCM?

Nimeyaeleza haya kwa sababu haya na matukio mengine yanayoendelea nchini yamepelekea Watanzania kutaka mabadiliko. 
 
Watanzania wanataka mabadiliko yatakayowawezesha kuzishinda changamoto hizi na kuwaongoza kujenga Taifa imara ambalo kila mwananchi wake anaishi akiwa na uhakika wa mahitaji yake muhimu na papo hapo akijiridhisha kwamba leo yake ni bora kuliko jana yake, na kesho yake itakuwa bora zaidi kuliko leo yake.
 
 Kwa maneno mengine, Watanzania wanahitaji mabadiliko yatakayowapa uongozi imara unaoweza kuwaongoza kujenga taifaimara. Hii ndio Safari ya Matumaini.

Chama chetu, Chama Cha Mapinduzi (CCM), na watangulizi wake, TANU na ASP, kimepata bahati ya kuungwa mkono na Watanzania tokea enzi za kupigania uhuru, wakati wa Uhuru wa Tanganyika na Mapinduzi ya Zanzibar, na pia miaka yote tokea Uhuru, Mapinduzi na hatimaye Muungano wetu. Watanzania hawajawahi kushuhudia chama kingine kikiongoza Serikali zetu zaidi ya CCM. Wamekiamini na wanaendelea kukiamini.
 
 Hata katika yale majimbo machache ya nchi yetu ambayo hatukufanya vizuri katika uchaguzi, ukiangalia kwa undani utaona si kwamba watu wa maeneo hayo wana matatizo na CCM kama Chama bali wana matatizo na baadhi ya viongozi ambao walishindwa kukiwakilisha vyema Chama na kutambua matakwa ya wananchi hao.

Mimi naamini kwamba hata katika kipindi hiki ambapo Watanzania wanaonekana kutaka mabadiliko bado wanaendelea kuamini kwamba watayapata mabadiliko hayo ndani ya CCM. 
 
Lakini kama alivyotupa wasia Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere, mwaka 1995 wakati wa uchaguzi mkuu wa kwanza chini ya mfumo wa vyama vingi hapa nchini, Watanzania wasipoyapata mabadiliko hayo ndani ya CCM watayatafuta nje ya CCM. 
 
Mimi naamini kwamba CCM tunao uwezo wa kuwapa Watanzania mabadiliko wanayoyataka. Tuwape imani na imani hiyo iwe ni ya dhati na ya ukweli kwamba CCM inao uwezo wa kuwapa uongozi imara wanaouhitaji kwa ajili ya kujenga taifa imara.

Vyama vya siasa vinajumuisha watu na vinaongozwa na watu. Moja ya hulka ya binadamu ni kubadilika kulingana na mahitaji ya mazingira anayoishi.
 
 Kwa maneno mengine, binadamu ni ‘dynamic’. Kwa sababu hiyo basi, hata vyama vya siasa vinapaswa kuwa ‘dynamic’.
 
 CCM haijapata kuwa na upungufu wa sifa ya ‘dynamism’. Kwa zaidi ya miongo mitano sasa, CCM (na kabla yake TANU na ASP) iliweza kubadili dira na mwelekeo wake ili kwenda sambamba na mahitaji ya Watanzania ya wakati husika. 
 
Ndiyo maana tumepita katika vipindi tofauti vya mpito kwa mafanikio makubwa licha ya changamoto nyingi zilizotukabili. 
 
Tanzania imeendelea kuwa nchi ya amani licha ya kubadili mfumo wetu wa siasa kutoka ule wa chama kimoja kuja vyama vingi; licha ya kubadili mwelekeo wa uchumi wetu kutoka ule wa dola kumiliki njia zote kuu za uchumi kuja katika uchumi wa soko unaozingatia ushiriki mpana wa Watanzania wa matabaka yote; na hata karibuni kabisa katika mchakato wa kuipatia nchi yetu Katiba mpya.
 
Tanzania tumeweza kufanya mabadiliko ya uongozi mara nne katika hali ya amani na maelewano, jambo ambalo nchi nyingi za Afrika zimeshindwa.
 
 Ni imani yangu kwamba tukijikubalisha tunaweza tena kuwapa Watanzania wanachokitaka katika zama hizi za sasa.
 
 Lakini ni lazima tuoneshe dhamira hiyo kwa dhati ili, kama alivyotuasa Mwalimu Nyerere, Watanzania wasiyatafute mabadiliko hayo nje ya CCM. 
 
Nasisitiza tena kwamba CCM inao uwezo wa kuwapa Watanzania mabadiliko wanayoyataka, lakini pia wananchi wana hiali kuchagua mabadiliko wanayoyataka.

Uongozi  unaohitajika  kuleta  mabadiliko  yanayotakiwa:
Rais Jakaya Kikwete amefanya kazi kubwa katika kipindi chake na kama ambavyo amekuwa akisisitiza mara kwa mara katika hotuba zake za karibuni ni kwamba yeye ametekeleza wajibu wake kwa kuweka misingi imara ya ujenzi wa Taifa la kisasa lenye uchumi madhubuti na unaoweza kukua kwa kasi.
 
 Amesema anamwachia atakayemkabidhi uongozi wa nchi yetu baada ya yeye kumaliza muda wake kuendeleza pale atakapoachia.

Kwa maoni yangu ili kuifanya kazi hiyo na kuzikabili changamoto nilizozieleza, nchi yetu inahitaji uongozi wenye sifa zifuatazo:

-  Uongozi wenye uthubutu, usioogopa kufanya kufanya maamuzi magumu;
-    Uongozi thabiti na usioyumba;
-    Uongozi makini na mahiri;
-    Uongozi wenye ubunifu na wenye upeo mkubwa;
-   Uongozi utakaozikabili changamoto kifua mbele na siyo kuzikimbia;
-    Uongozi unaoamini katika mfumo shirikishi katika ujenzi wa Taifa;
-    Uongozi unaozingatia muda katika kutekeleza majukumu yake.

Naamini pia kwamba wananchi wanataka Rais ajaye wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania awe na sifa kuu zifuatazo:

-    Aweze kuwaunganisha Watanzania (kukabiliana na viashiria vya migawanyiko ya aina mbali mbali inayoinyemelea Tanzania);

-    Aweze kuja na sera na mikakati ya kuinua uchumi wa Tanzania na kukuza pato la Mtanzania;ikiwemo kupunguza tofauti ya kipato kati ya aliyekuwanacho na wasiokuwanacho;

-     Aweze kuja na sera na mikakati ya kuzalisha ajira kwa vijana wetu;

-     Aweze kutokomeza mianya ya rushwa kwa vitendo;
-    Aweze kuwa mfano wa kuchapa kazi na kuwajibika;
-     Asimamie nidhamu ya matumizi ndani ya Serikali;
-     Aweze kusimamia ukusanyaji wa mapato ya Serikali;
-     Aweze kutumia fursa yetu ya kijiografia kibiashara

Uongozi  Imara,Taifa  Imara
Naamini kwamba uongozi wa juu wa nchi katika nafasi ya Urais si kazi ya lelemama na unahitaji utashi. Kabla hata ya kutakiwa na wenzako ni lazima kwanza wewe mwenyewe uamini na uwaaminishe wenzio kwamba unao uwezo wa kuwaongoza wananchi wenzako. Na katika hilo, rekodi yako ni lazima izungumze na kulithibitisha hilo.

Binafsi nina hazina ya uzoefu na rekodi njema ya matokeo ya kazi nilizozifanya katika uongozi na utumishi wa umma ndani ya CCM na ndani ya Serikali. Nilianza kazi nikiwa Katibu Msaidizi wa CCM katika mikoa ya Shinyanga, Arusha na Moshi.
 
 Nimekuwa Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa na Kamati Kuu ya CCM. Niliingia Bungeni mwaka 1985 na baadae mzee wangu, Rais Ali Hassan Mwinyi, akaniamini kwa kuniteua kuwa Waziri. 
 
Nimekuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Waziri wa Ardhi, Makaazi na Maendeleo ya Miji, Waziri wa Mazingira, Waziri wa Maji na hatimaye Waziri Mkuu.

Miongoni mwa mafanikio ninayojivunia katika uongozi na utumishi wangu, na ambayo Watanzania wanayatambua na naamini wanayathamini, ni pamoja na:

-    Nikiwa Waziri wa Maji chini ya uongozi mahiri wa Rais Mkapa,tulithubutu kushawishi na kuongoza hatua za kukataa kufungika na makubaliano yaliyowekwa na wakoloni ambayo yalikuwa yanazizuia nchi zilizopakana na Ziwa Victoria zisiweze kufaidika ipasavyo na maji ya Ziwa hilo. Leo hii ndugu zangu wa Kanda ya Ziwa wanafaidika na ujasiri wetu katika kukabiliana na suala hilo zito.

-    Nikiwa Waziri wa Mazingira, tulipanda miti mingi zaidi kuliko wakati mwingine wowote tokea Uhuru na pia kuwakabili kikamilifu na kuwachukulia hatua waliochafua na kuharibu mazingira.

-    Nikiwa Waziri Mkuu, tulisimamia agizo la Rais Kikwete na kufanikisha utekelezaji wake ndani ya miaka miwili kwa kujenga shule nyingi za sekondari kuliko wakati mwingine wowote tokea Uhuru.

-    Kipindi hicho hicho, tulisimamia agizo la Rais Kikwete la kuanzisha Chuo Kikuu cha Dodoma na kuhakikisha kinakamilishwa kwa wakati. Leo hii Chuo Kikuu hicho ni fahari ya Tanzania.

Tunapomtafuta Rais wa Jamhuri ya Muungano ni lazima tukumbuke kwamba tunamtafuta mtu ambaye atakuwa pia ni Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama katika nchi yetu. Na kwa Chama Cha Mapinduzi tunamtafuta mtu ambaye atakuwa pia Mwenyekiti wa Chama chetu.

Naamini kwa vigezo vyote, nina kila sifa ya kubeba dhamana hizo nzito. Katika mambo ambayo najivunia na sitoyasahau katika historia yangu ni kushiriki kwangu kuilinda nchi yangu pale ilipohitajika. 
 
Nilishiriki kikamilifu katika Vita vya Kagera nikiwa miongoni askari wa mstari wa mbele wa mapambano. Nikiwa Mbunge nilipata heshima ya kuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama. Naamini Watanzania hawatakuwa na wasiwasi wa usalama wao nikiwa Amiri Jeshi Mkuu.

Nimeeleza uzoefu wangu kwenye Chama na huo hauhitaji maelezo zaidi. Ninakijua vyema Chama Cha Mapinduzi kiasi cha kutosha kabisa kukiongoza kama Mwenyekiti wake pale wakati utakapofika.
 
 Wana-CCM wanajua nikikabidhiwa uongozi, Chama chetu kitakuwa chini ya nahodha madhubuti, mzoefu na asiyeyumba.

Kutokana na rekodi yangu hii, naamini ninazo sifa za kuwaongoza Watanzania wenzangu katika zama mpya za ujenzi wa Taifa la kisasa lenye watu wazalendo walioshikamana na lenye uchumi imara unaomnufaisha kila Mtanzania. Naamini ninao uwezo wa kuwapa Watanzania Uongozi imara kwa ajili ya ujenzi wa Taifa Imara.

Dira  yangu  na  Matarajio  ya  Watanzania
Mfumo tuliojiwekea hapa nchini unaelekeza kila chama cha siasa kinachosimamisha mgombea Urais na kinachowania kuongoza nchi yetu kuja na Ilani ya Uchaguzi ambayo ndiyo inayoweka misingi ya sera zitakazofuatwa na Serikali itakayoongozwa na chama hicho pale kinapopewa ridhaa ya kuongoza nchi.
 
 Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimekuwa ni cha kupigiwa mfano katika kutayarisha Ilani bora na ndiyo maana mara zote kimepewa ridhaa ya kuongoza nchi yetu. Tumefanya hivyo tokea enzi za mfumo wa chama kimoja na tumeendelea kufanya vizuri katika mfumo wa kushindanisha sera kupitia vyama vingi. 
 
Najua kwamba Ilani ya CCM ya mwaka 2015 imo katika hatua za mwisho za kukamilishwa na itakapopata baraka za vikao vya Chama itakuwa ndiyo msingi wa utendaji wa Serikali ya Awamu ya Tano itakayochaguliwa Oktoba mwaka huu. 
 
Hata hivyo, naamini pia kwamba mgombea mwenyewe anayetaka ridhaa ya Chama na ya Watanzania kuongoza nchi naye anapaswa kueleza dira yake.

Mimi, baada ya kutafakari kwa kina changamoto tulizo nazo na matarajio na matumaini waliyo nayo Watanzania, naamini kwambaUongozi imara unaolenga kujenga Taifa imara unapaswa kuwa na dira yenye malengo yafuatayo:

-    Kuimarisha Muungano wetu kwa kuyashughulikia yanayotutenganisha na kuyafanyia kazi ili yasivuruge yale yanayotuunganisha ambayo ni mengi zaidi na makubwa zaidi.

-    Kushughulikia matumizi mabaya ya siasa za udini na ukabila kwa kuimarisha siasa zilizoshiba uzalendo na zenye kutuelekeza kwenye Utanzania wetu.

-    Kujenga uchumi imara na wa kisasa, na ambao ni shirikishi unaomnufaisha kila Mtanzania aliyeko mjini au kijijini. Tunapaswa kubadili hali tuliyo nayo sasa ambapo Kilimo kinaonekana kama kimesahauliwa na wakulima wetu wanaonekana wanakata tamaa.
 
Wafugaji na wavuvi nao wanahisi sekta zao hazijapewa umuhimu unaostahiki. Tunahitaji kuondokana na hali iliyopo sasa ya kuwa Taifa linalouza malighafi na badala yake kuwa Taifa linalosindika na kusarifu mazao na kutengeneza wenyewe bidhaa zitokanazo na malighafi yake. 
 
Ndani ya miaka mitano ijayo tutahakikishatunaiondolea Tanzania sifa ya kusafirisha malighafi na badala yake kusindika mazao yanayozalishwa hapa nchini kama pamba, kahawa, chai na korosho na kuyaongezea thamani (value addition).Mkakati huu utazalisha ajira nyingi na kuongeza mapato ya fedha za kigeni nchini.
 
 Tunahitaji kujielekeza kwenye kujenga viwanda na kuleta ajira. Tuna vivutio vingi sana vya utalii lakini bado Tanzania inapitwa na nchi kama Afrika Kusini katika kuingiza idadi kubwa ya watalii.
 
 Kwa nini nchi kama Dubai iweze kuvutia watalii kwa mamilioni na Tanzania tushindwe? Tunapaswa kukabiliana kikamilifu na hisia zilizopo miongoni mwa wananchi kwamba Tanzania hainufaiki ipasavyo na utajiri wa rasilimali zake nyingi ilizo nazo. 
 
Tutajipanga zaidi kuhakikisha tunanufaika kama nchi na rasilimali zetu kama madini na gesi asilia. Hii ndio Safari ya Matumaini

-    Kukuza kipato cha wananchi na kunyanyua hali za maisha ya watu wetu. Tunapaswa kuhakikisha kuwa ukuaji wa uchumi tunaouzungumzia unamnufaisha Mtanzania aliyeko mjini au kijijini na kwamba hali za Watanzania wa matabaka yote zinanyanyuka na kwamba wanaridhika na kuuona uhalisi wa ukuaji wa maendeleo tunayoyazungumzia.

-    Kuondokana na sifa mbaya ya kuwa Taifa ombaomba. Kwa wingi wa rasilimali tulizo nazo na neema ya ardhi, maziwa, mito na bahari Tanzania tuna kila sababu ya kuacha kuwa ‘bakuli la ombaomba’ na badala yake kuwa ‘mkoba wa neema’ katika Afrika.We can transform our nation from being the begging bowl to become the bread basket of Africa.

- Kujenga mfumo mpya wa elimu unaojielekeza kuwatayarisha vijana wetu waweze kuajirika, kujiajiri na kushindana katika soko la ajira. 
 
Tumepiga hatua kadhaa katika elimu lakini kiwango cha elimu bado ni hafifu. Pamoja na kuwa na shahada (degrees), bado wahitimu wetu hawawezi kushindana kwenye soko la ajira. 
 
Wakati tunazungumzia kuunganisha soko la ajira katika Afrika Mashariki,hatuna budi kujikita kubadili mfumo wetu wa elimu na kuuelekeza kwenye mafunzo ya ufundi na stadi yanayowajenga wahitimu wetu kuwa wabunifu na wenye kujiamini katika kukabiliana na changamoto za maendeleo duniani.

-    Kuhakikisha tunakabiliana ipasavyo na kulipunguza kwa kiasi kikubwa kama si kulimaliza kabisa tatizo la upatikanaji wa maji safi na salama. Ni jambo la kusikitisha kwamba tumezungukwa na mito na maziwa lakini bado watu wetu hawana maji ya kunywa hata ndani ya Dar es Salaam.

-    Kujenga na kusimamia mfumo imara wa kutekeleza sera na sheria tunazozitunga na kuzipitisha kwa lengo la kumtumikia Mtanzania na kumjengea uwezo wa kubadili maisha yake ili tuweze kwenda sambamba na viwango vya kimataifa. Tanzania imepata sera na sheria nzuri sana lakini utekelezaji wake umekuwa hafifu. 
 
Tumekuwa wepesi wa kutunga sera na sheria lakini wazito mno wa kuzitekeleza na kuzisimamia. Uongozi imara wenye kulenga ujenzi wa Taifa imara utahakikisha tunakuwa mfano wa utekelezaji wa sera na sheria tulizo nazo na mpya zitakazotungwa kukabiliana na malengo tuliyojiwekea.

Mambo haya niliyoyaeleza hapa ndiyo yatakayokuwa msingi mkuu wa utendaji wa Serikali nitakayoiongoza pale nitakapopewa ridhaa ya kubeba bendera ya CCM katika nafasi ya Urais na pia nitakapopewa ridhaa ya kuliongoza Taifa letu kupitia uchaguzi mkuu wa mwaka huu.

Ramani  ya  Uongozi  Imara  Ninaouamini 9 Leadership Roadmap)
Kama nilivyotangulia kusema, kazi ya kuongoza nchi si lelemama na hasa unapoongozwa na dhamira ya dhati na msukumo wa ndani ya nafsi unaojielekeza kubadilisha maisha ya wananchi wenzako waliokuamini uwaongoze. Kwa vyovyote vile, hiyo haiwezi kuwa kazi ya mtu mmoja. Ni kazi ya pamoja.
 
 Lakini ili muweze kufanya kazi kama timu moja iliyojipanga kisawasawa kuleta mabadiliko yanayohitajika na ili muweze kweli kutoa Uongozi imara unaojikita kujenga Taifa imara hapana budi kiongozi mkuu anayeongoza timu hiyo aweke ramani anayokusudia kuifuata katika kutoa uongoziimara anaoukusudia yaani ‘Leadership Roadmap’.

Pamoja na kuwa sehemu ya uongozi huko nyuma, kutakuwa na maamuzi na matumaini mapya. Ramani ya uongozi imaraninayokusudia kuutoa kwa wenzangu na ambayo nitaitumia kuiongoza timu yangu katika kuwatumikia Watanzania wenzangu itajikita katika maeneo yafuatayo:

1. Kurejea kwenye Katiba katika kuainisha nia, dhamira na malengo yetu ya kujenga jamii inayozingatia misingi ya demokrasia, udugu na amani. Muhimu katika hili ni kukemea tabia mbaya zinazochochea mfarakano katika jamii kama vile matumizi mabaya ya siasa za udini na ukabila.
 
Aidha moja ya misingi muhimu ya Katiba ni Muungano wetu. Itakuwa dhamira yangu kuimarisha misingi ya Muungano pamoja na udugu wa damu nahistoria ya ushirikiano iliyojengwa na waasisi wetu, Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere na Hayati Sheikh Amri Abeid Karume na kuyaenzi Mapinduzi matukufu ya Zanzibar.

2. Kujenga fikra mpya za kurejesha kujiamini na kufufua azma ya kujitegemea kama Taifa. Ni dhahiri kuwa pamoja na rasilimali zetu, bado Tanzania ni taifa tegemezi. Bado tunajidanganya kuwa wafadhili watatujengea nchi. Tukumbuke, nchi zinajengwa nawananchi wake. 
 
Nasi pia lazima tujikomboe kifkra na tuondokane na utamaduni wa kuwa tegemezi. Tuanze kwa kujipiga kifua kwa kujiamini kuwa tunaweza kujitegemea na kuijenga Tanzania sisi wenyewe.Kujiamini na kujitegemea ndio uhuru wa kweli.

3. Kujenga uzalendo, uadilifu ikiwa ni pamoja na kuimarisha uwazi katika shughuli zote za serikali na kupambana na rushwa.Watanzania tumepoteza uzalendo kwa kiasi kikubwa. Kuna vitendo vinavyoashiria kuwa hatuipendi tena nchi yetu. 
 
Tunashabikia wizi na rushwa. Inabidi turejee kwenye misingi ya taifa letu misingi ya uadilifu na uzalendo. Tukumbuke kuwa hatuwezi kujenga uchumi wa kisasa kama tutaruhusu rushwa ishamiri.
 
 Wawekezaji hawataleta mitaji yao kwa wingi kama rushwa itaendelea kutawala katika huduma serikali na wananchi hawawezi kupata huduma bora kama rushwa itaendelea kutawala. Ni lazima tuipinge rushwa kwa vitendo sio maneno.

4. Kujenga Serikali madhubuti, makini na yenye nidhamu inayoendeshwa kwa misingi ya sheria, uwazi na uwajibikaji.Maendeleo ya watu hayawezekani bila serikali kusimamiautekelezaji sera na miradi na kuleta ufanisi katika kutoa huduma na kusimamia maendeleo. Tumekuwa wepesi wa kutunga sera lakini wazito wa kuzitekeleza na kuzisimamia.


5. Kuleta msukumo mpya wa ushirikiano kati ya serikali na sekta binafsi katika ujenzi wa uchumi wa kisasa na unaojitegemea. Sekta binafsi ndiyo nyenzo ya uchumi imara. Inazalisha mali, ajira na kuchangia kwa kiasi kikubwa katika pato la taifa kwa kulipa kodi.
 
 Ilisekta hii itoe mchango unaotakiwa katika maendeleo ni lazima ifanye kazi na serikali kwa karibu. Tukumbuke, bila uchumi imarahakuna huduma bora!


6. Uwekezaji katika huduma za jamii. Elimu na afya bora, mazingira, makazi safi na maji salama ndiyo mihimili ya maendeleo ya watu.
 
 Hii inawezekana tu iwapo serikali itakuwa na sera na utashi wa kuutambua uboreshaji wa huduma za jamii kama ndiyo lengo kuu la maendeleo ya nchi. Serikali nitayoiongoza itahakikisha kuwa kila Mtanzania anapata elimu bora na inayogharamiwa na serikali kama mimi na wenzangu tulivyopata. 
 
Wakatitunazungumzia kuunganisha soko la ajira katika Afrika Mashariki, hatuna budi kurekebisha mfumo wetu wa elimu na kuuelekeza kwenye mafunzo ya ufundi na ustadi yanayowajenga wahitimu wetu kuwa wabunifu, wenye kujiamini, wenye uwezo kushindana katika soko la ajira na wa kujiajiri. Napenda kusisitiza kuwa elimu ndiyo muhimili wa maendeleo, ndiyo mkombozi wa kweli wa binadamu. Mimi ni mfano hai wa ukombozi wa elimu. 
 
Elimu ndiyoimenivusha kutoka kijijini kwetu Ngarash na kunipa upeo wa kitaifa. Mama akiwa na elimu atajua umuhimu wa kumpeleka mwanae shule, anapata lishe bora na chanjo stahili na kuwa anaishi katika mazingira safi. Elimu ndilo jibu la umaskini, maradhi na ujinga.Taifa lililo elimika ni taifa lenye maendeleo.
 
7. Kujenga uchumi shirikishi unaolenga kuondoa umaskini.Mkakati wa kuondoa umaskini Tanzania lazima ujikite kwenye nguzo za ushiriki wa kila Mtanzania katika uchumi wa taifa. 
 
Kwa misingi hii, tukiweza kupunguza umaskini, tutaweza pia kupunguzatofauti za kipato ambazo tukiziacha ziendelee kukua kwa kiasi cha sasa, zinaweza kuhatarisha utulivu na amani katika jamii yetu.Uchumi shirikishi ndio silaha dhidi ya umaskini.

8. Kuimarisha ulinzi wa nchi na usalama wa raia na ujirani mwema.Itakuwa nia yangu kuimarisha misingi iliyojengwa kulinda na kudumisha umoja na amani nchini. 
 
Kadhalika, nitahakikisha kuwa usalama wa mipaka ya Tanzania unaimarishwa kwa misingi ya ujirani mwema na kutanzua migogoro na matatatizo yoyote na nchi jirani, kwa njia ya diplomasia na mazungumzo.

Hitimisho:
Hii ndiyo misingi na dira ya uongozi wangu. Nachelea kusema kuwa haitakuwa kazi rahisi. Lakini kwa ushirikiano wa kila mmoja na maamuzi magumu, yote yanawezekana.
 
 Tumeona nchi nyingi zilizosimamiwa na utawala thabiti wa serikali za kimaendeleo zikikabili na kupunguza umaskini katika kizazi kimoja. Kama mataifa mengine yamefanikiwa, tena bila raslimali kama zetu, kwa nini sisi tushindwe? 
 
Tuna kila sababu ya kufanya maamuzi magumu sasa ili kuwajengea Watanzania matumaini mapya ya maendeleo. Naomba nisisitize kuwa katika uongozi wangu hakutakuwa na nafasi ya majungu, na visasi. Hatutaangalia nyuma bali tutasonga mbele kwani ndicho Watanzania wanakitarajiakutoka kwa uongozi uliojengwa kwenye misingi bora.

Ndugu Watanzania:-
Ni maono yangu kuwa siku si nyingi nchi yetu itaanza safari yenye uelekeo wa matumaini na neema tele kwa wananchi.

Ni maono yangu kuwa siku si nyingi sisi kama Watanzania kwa umoja wetu tutajivunia kuishi katika nchi tunayoipenda na inayoendeshwa kwa misingi ya utawala bora, chini ya serikali ya kimaendeleo iliyojengwa kwenye fikra mpya za uzalendo, uadilifu, utendaji na uwajibikaji.

Ni maono yangu kuwa Peke yangu sitaweza, lakini kwa maamuzi magumu na ushirikiano wa kila mmoja wetu ikiwa ni pamoja na wagombea wenzangu ndani ya CCM, inawezekana kuanza safari hii ya Matumaini Mapya.

Kabla ya kumaliza hotuba yangu hii fupi, kuna mambo matatu ningependa kuyaweka wazi hapa.

La kwanza, linahusu msingi wa uongozi ninaouamini na ambao nimeusema mara kadhaa hapa. Msingi huo ni UWAJIBIKAJI.Watanzania wananifahamu mimi si mtu wa maneno, ni mtu wa vitendo. Naamini kwa dhati kabisa kwamba huwezi kuwa na Uongozi imara utakaoweza kusimamia ujenzi wa Taifa imara iwapo huna ujasiri wa kuwajibika. Mimi nimeongoza kwa mfano, na pale ilipobidi, nilikubali kuwajibika na kubeba dhamana ya uongozinilipojiuzulu nafasi ya Waziri Mkuu.

La pili, mimi si mtu wa visasi. Siamini katika kuangalia ya nyuma. Yaliyopita si ndwele, tugange yajayo. Na kwa nini tuangalie nyuma wakati kama taifa tuna kazi kubwa sana mbele yetu inayohitaji kufanywa? Mimi ni Mkristo; najifunza kutoka kwa Bwana Yesu ambaye alipoulizwa: “Nisamehe mara ngapi?” Alijibu, “Samehe mara sabini mara saba”. Nitaenzi na kudumisha utamaduni huu wenye sura ya utu na heshima.

La Tatu, natambua kwamba dhamana ya Urais ni shughuli nzito hasa kwa taifa ambalo lina changamoto nyingi. Nataka niwahakikishie Watanzania wenzangu kwamba afya yangu ni njema kuweza kuwatumikia katika jukumu hili zito. Pamoja na vijineno vinavyosemwa pembeni, mimi mwenyewe ndiye ninayejijua zaidi. Nawahakikishia kuwa nisingekuja hapa leo na kueleza nia yangu hii ingekuwa sina uhakika na afya yangu.

Natoa RAI kwa Chama changu cha CCM, nadhani umefika wakati kwamba tutende tofauti na mazoea, watu wote walionyesha nia ya kutaka kuongoza, liundwe jopo la madaktari wa ndani na nje ya nchi tupimwe afya zetu, kwa hili najitolea kuwa wa KWANZA KUPIMWA afya yangu

Safari tuianze leo, hatuna kesho nyingine.
Ahsanteni sana kwa kunisikiliza

Wolper Ampongeza Aunty kwa Kuwaacha Matajiri na Kufuata Kiuno cha Moses Iyobo

$
0
0
Staa wa Bongo Movies, Jacqueline Wolper amefunguka na kumpogeza staa mwenzake Aunt Ezekiel ambaye amezaa na mcheza dansi, Moses Iyobo kwa kuamua kuwaacha matariji na kuamua kuzaa na mcheza dansi huyo.

Penzi la Aunt Ezekiel na Moses Iyobo limekuwa likitazamwa kwamitazamo tofauti tofauti hasa miongoni mwa mashabiki huko mitandaoni, Wolper amevunja ukimya na kuanddika haya kwenye ukurasa wake mtandaoni mara baada ya kuweka picha hiyo hapo juu.

Kiukweli na hamu yakulishwa keki kama kwenye hii picha hapo huduma hzii zinapatikana wapi?? au paka upendwe kama huyu dada lol.. kikubwa ni mapenzi ya kweli sasa mkiwa mnapiga porojo ooh viuni sijui kunengua hayo ni maneno tuu ata kwenye khanga yapo sasa ukiwa gwijii wamaneno kamaa kina sisi hapa ndo kwanza zile kelele zinakua kma instrument huku blues inaendelea kma hvii Maneno yote nimeongea kwa sababu ya kina  baba insta, mamainsta, paroko insta, masheeh insta  wachungaji insta, washauri inatsta na wazazi wainsta .

Wolper akaendelea;

Huyu dada now yupo happy na ana amani ya moyo nayo ni hii hapa ukiona mtu kaacha matajiri wote kafwata kiuno basi hcho ndo kinachomfaa .hongera sana mama coukie na baba coukie shem langu mose iyogo kwa kupata bint Mungu awasimamia kwakila jambo asikwambie mtu akuna asiyependa kuwa na chake vyauwizi navyo vinachosha mtu chake sokoni anakua ndo pochi outing anakuwa ndo kiatu kitandani ndo usiseme anakua shuka kabisa  hlw fans i love uu & Tanzani iz country, jumamosi njema.

Mzee wa Ubuyu

Aunty Ezekiel Responds To Her Haters Who Say Moze Iyobo Isn't The Daddy of Her Daughter Cookie

$
0
0
Few days ago some of Aunty Ezekiel's friends  went to media to say that Aunty's daughter Cookie doesn't look like Moze Iyobo who is Aunty's boyfriend. Her friends whose names were withheld think the father of her daughter is someone else and not Moze Iyobo claiming the baby is white while both Moze and Aunty are black.
But through instagram Aunty posted the photo above sharing hot kiss with Moze and insisted Moze is the daddy of her child...

Afungwa miaka 30 kwa kumbaka mtoto wa miaka tisa

$
0
0
Mkazi wa Malampaka mkoani Simiyu, Benedictor Bulobo (30) , ametupwa gerezani atakakotumikia kifungo kwa miaka 30 baada ya kupatikana na hatia ya kumbaka binti wa miaka tisa.

 Alihukumiwa  na Mahakama ya Wilaya ya Maswa juzi na Hakimu Mwandamizi Mfawidhi  Agatha Chigulu, baada ya kuridhishwa  na ushahidi uliotolewa na upande wa mashtaka.

Akitoa hukumu hiyo hakimu huyo alisema kuwa anatoa adhabu hiyo ili kukomesha vitendo hivyo na kuwaonya wenye nia  mbaya ya kutaka kutenda kosa kama hilo wajifunze na kuacha mwenendo huo.

Chigulu alieleza kuwa kosa hilo ni kinyume na kifungu cha 131 cha sheria ya kanuni ya adhabu sura ya 16 iliyofanyiwa marekebisho mwaka 2012.

 Awali mahakama iliambiwa na  Mwendesha Mashitaka wa Polisi, Nassibu Swedy kuwa mshitakiwa alitenda kosa hilo Februari 23 mwaka jana  saa 5:00 asubuhi.

Alimnajisi mtoto huyo  maeneo ya nyumbani kwake baada ya kumkamata  kwa nguvu binti huyo mwanafunzi wa darasa la kwanza katika Shule ya Msingi Malampaka na kumwingiza chumbani kwake alipombaka.

Alisema mtoto huyo  alipata maumivu makali  baada ya kuumizwa  sehemu za siri,  alipiga kelele kuomba msaada na watu walifika katika eneo la tukio,  kumkamata  na kumfikisha Bulobo katika kituo cha polisi Malampaka.

Dudu Baya kurudi rasmi kwenye muziki kwa jina jipya, ‘Dudu Mamba’

$
0
0
Msanii wa Hip Hop wa muda mrefu, Godfrey Tumaini aka Dudu Baya amedai kujipanga kurejea rasmi kwenye muziki wa Hip Hop na kuahidi kuweka ushindani mkubwa na wasanii wenzake wakiwemo Fid Q na Young Killer Msodoki.

Dudu Baya ameimbia Bongo5 kuwa si kwamba anarudi na muziki mpya tu bali pia akiwa na jina jipya – Dudu Mamba.

“Ushindani nitauweza najua kuna wasanii kama Fid Q, Young Killer na wengine wanafanya vizuri lakini mimi sasa hivi nimekuja kushindana,” amesema Dudu Mamba.

“Unajua hii miaka miwili nilionekana kutokuwa serious na muziki lakini sasa hivi tayari nimeshaingia studio za Mona Gangster. Mona ndo kamtoa Young Killer ngoma zote na wasanii wengine, kwahiyo tayari silaha ya kwanza katika kurudi kwangu ni kufanya kazi katika studio bora chini ya producer bora Mona Gangstar.

Silaha ya pili ni mpangilio wa promotion ya ngoma yangu mpya. Nimeshazungumza na wadau mbalimbali wa media kuangalia jinsi gani tunawezafanya kazi kwa kushirikiana, kwahiyo matumani ya kurudi katika level zangu yapo. Ngoma yangu inaitwa ‘Kuwachora kwa Jicho’ ngoma ambayo natumani itakuwa poa sana kwa sababu ngoma ni ya kuchezeka.”
Viewing all 104785 articles
Browse latest View live




Latest Images