Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104698 articles
Browse latest View live

Diamond ndiyo Habari ya Nigeria!! Ali Kiba Upo Wapi? Diamond ameachia Video nyingine na IYANYA Itazame Hapa

$
0
0
Diamond ndiyo Habari ya Nigeria!! Ali Kiba Upo Wapi? Diamond ameachia Video nyingine na IYANYA Itazame Hapa

MSHTUKO!!!Mwakyembe Nitapambana Kufa na Kupona LOWASSA asiingie Ikulu

$
0
0
WAZIRI wa Afrika Mashariki, Dk. Harrison Mwakyembe, ameapa kupambana kufa au kupona, kumzuia Edward Lowassa, kuingia Ikulu kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Katika andishi lake alilolituma kwenye mitandao ya kijamii, Dk. Mwakyembe anasema, Lowassa hana sifa ya kuwa Rais wa Jamhuri. Amesema, “…namuona Lowassa kama mtu ambaye anatapatapa huku akiujua ukweli kwamba hana nafasi hata kiduchu ndani ya CCM.

lisema hili bila kukemea jicho wala kuwa na wasiwasi wowote na maisha yangu kwani najiamini na mwenyezi mungu ananilinda na watanzania wananiombea daima na najisikia furaha kuwa miongoni mwa wabunge wa CCM ambao hatukuufumbia macho ufisadi wa kampuni feki la kuzalisha umeme iliyomuhusisha waziri mkuu ambaye mimi namuita aliyejiuzulu na sio kustaafu.
Nakushauri ujitafakari vizuri kwani CCM haitoweza kumkabidhi nduli nchi hii.
Unahaha kutumia mabilioni kuhonga na kusafirisha watu kwenye tendo la kutangaza nia tu, hivi unafijiri kamati zote za CCM zina njaa ya pesa zako za kifisadi?

Hivi hujui watanzania wakushangaa unasema safari ya matumaini wakati safari hiyo ni ndani ya bahari iliyojaa majoka na mizimu ambayo imejivika ngozi ya kondoo ili iwameze katikati ya bahari?
Nitakuwa wa kwanza kujitafakari na kuitafakari CCM na kuchukua hatua ambayo najua watanzania wasiouza utu wao kwa dhamana ya fedha.
Ninakusubiri kwa hamu ili nikusikie utakavyokuwa unabadili jihanam kuwa peponi, kwa manufaa ya watanzania nitaanika hadharani uozo wako wote kwa ujasiri na bila hata chembe ya woga ili watanzania wasipotoshwe tena kwa njia ya nbwembwe za fedha. Eh mwenyezi mungu nipe uthabiti kwa hilo.

Rai yangu kwa wana CCM na watanzania tuchague viongozi bora na sio kwa nguvu ya fedha, wapambe na kutembelea nyota ya mtu.
Utauficha wapi uso wako wakati ambapo CCM itakapokuangusha kwa kishindo na kuchagua wawakilishi walio safi? Utapata kiharusi na shock bure kwa kupoteza fedha za madili uliyopiga RICHMOND na ufisadi mwingine.

Hon Dr. Harison Mwakyembe (Mb) Waziri wa Jumuiya ya Ushirikiano wa Afrika Mashariki.
Mungu ibariki Tanzania, Mungu ibariki Afrika.

Pole Sana Edward Lowassa Maadui Wako ni Wana CCM Wenzako

$
0
0
Ni mmoja wa vijana ninayemkubali sana Lowassa tangu akiwa waziri wa maji na baadae waziri mkuu. Maskini Pamoja kuugwa mkono na kila rika lakini kwa hotuba za makada wawili wanaoitaka hii nafasi ya uraisi ni dhahiri maadui wako wako ndani ya CCM na si UPINZANI kama nilivyokuwa najidaganya hapo awali!! pamoja na hotuba ya kistaarabu uliyoitoa juzi wenzako hawana hilo. Lakini mungu ni mwema tutashinda.

Mtoto afa baada ya mama yake kumnywesha sumu ya mende badala ya dawa ya minyoo

$
0
0
Tukio la kusikitisha sana limetokea eneo la Mbezi kwa Musuguli eneo la Bwaloni ambapo mama kwa bahati mbaya amemnywesha mwanae wa kike wa umri wa mika 3 sumu ya mende badala ya dawa ya minyoo hivyo kusababisha kifo chake. Hii ni kwasababu mama aliweka dawa ya minyoo pamoja na sumu akaamka saa 11 alfajiri ili awahi kumpa mtoto dawa ya minyoo. Kwa bahati mbaya badala ya kuchukua ile ya minyoo akachukua ile ya mende na kumpa mtoto kisha mtoto akaenda kulala.

Kulipokucha vizuri wakashangaa mtoto haamki ndipo walipoenda na kumkuta katika hali mbaya. Wakamkimbiza katika hospitali ya Bochi iliyopo Mbezi kwa Msuguli barabarani lakini walipofika waliambiwa wamechelewa sana hivyo mtoto akafariki. Amesafirishwa Jumamosi kwenda Moshi kwa mazishi. Wazazi wa mtoto ni watu waliookoka wakisali katika kanisa la KKKT Mtaa wa Bwaloni. Inasikitisha sana.

Ili kuzuia tukio kama hili kujitokeza nashauri wazazi na watu wote kuweka mbali kabisa dawa za binadamu na dawa za wanyama na wadudu iwe za kutibu au kuua wadudu. Pembeni ya hapo nimewaza sana kuwa kama tukio hili lingekuwa limefanywa na House girl kwa bahati mbaya vile vile sijui ingekuwaje?

Angeeleweka na ingeeleweka kuwa ni bahati mbaya? Katika tukio hilo mama naye alitikiswa kidogo kwani alikuwa ameilamba kidogo kabla ya kumpa mwanae.

Mungu ailaze roho ya mtoto mahali pema peponi, Ameni.

Destined To Musically Conquer Africa; the Amazing Tale of Diamond Platnumz

$
0
0
Whether you cognize Swahili or not, you sure have fallen in love with one of his songs or one of his exquisitely crafted videos. I’m talking about Diamond Platnumz, East Africa’s most selling artist and one of Africa’s most progressive musicians.

From Afro-pop to Afro folk, Diamond Platnumz has set himself apart as talented, versatile, unique, focused and destined to musically conquer Africa; a journey that is rather deliberate not fortuitous.

Before I excavate deep into the startling journey of East Africa’s hottest music export to the world, let’s take a brief look at who he is. Born Nasibu Abdul Juma on the 2nd of October 1989 in Tanzania, Diamond is a Bongo Flava recording artist and singer who has won numerous awards world over including Channel O and the Prestigious HiPipo Music Awards.

He has performed in different parts of the world, with some of his hottest songs including Kamwambie, Nalia na mengi, Mbagala, Nitarejea, Binadamu, Kizaizai, Lala Salama, Moyo Wangu, Mawazo, Kipofu, Kisa, Nimpende nani, Chanda Chema, Ukimwona, Nkifa Kesho, Nataka Kulewa, Kesho, Mapenzi Basi, Number One, Number One Remix (Ft.Davido), Mdogo mdogo, Bum Bum (Ft. Iyanya), Lala Ukisinzia, Ntampata Wapi, Nasema Nawee and Nana (Ft. Flavor).

One of the things that have elevated Diamond is his deliberate choice to craft stunning music videos. Whether you like his music or not, you’ll agree that his videos speak volumes of effort and creativity.

His Nana video (Ft. Flavor), for example, is such a beauty! Nana was shot in Cape Town, South Africa by God Father and it sure is well thought out, right from concept, story, casting and costuming to choreography! It feels like a movie and that’s what I mean when I say that Diamond’s rise to the top is well thought out.

In addition to his talent and uniqueness, it is such videos that have endeared him to music fans all over the continent. He doesn’t craft music videos just for the sake of having a music video out there, but rather to deliver masterpiece products; products that would appeal to a music fan in any part of the world!

His eye for the right collaborations has also helped him spread across the continent at such an amazing speed. Projects like Number One Remix (Ft. Davido), Bum Bum (Ft. Iyanya) and Nana (Ft. Flavor) have helped him spread beyond his East African market.

At this rate, Diamond Platnumz is obviously destined to musically conquer the African continent.

Kisa Lowassa,Mzee Mengi alalamika kutukanwa, Aweka hadharani namba ya mbaya wake na Kuandika Ujumbe Huu

$
0
0
Baada ya ITV kurusha matangazo ya moja kwa moja siku ndugu Lowassa alipotangaza nia, Mzee Mengi amelalamika kupitia ukurasa wake wa twitter kuwa wapo watu walimtukana sana, haswa mtu mmoja ambaye namba yake kaiweka hadharani.

Kwanini Mengi atukanwe? Mbona ni vituo vingi vilikuwa Live? Mbona hata watangaza nia kama Wassira na Mwigulu ITV walirusha Live?


Shamsa Ford anamlea mtoto wa Nay Wa Mitego?

$
0
0
Picha iliyosambaa mtandaoni ikimuonyesha staa wa Bongo Movies, Shamsa Ford akiwa amembeba mtoto wa staa wa Bongo Fleva,Nay Wa Mitego, Curtis imezua maswali kwa mashabiki wao kuwa huenda mwigizaji huyo kwa sasa anamlea mtoto huyo.

Miezi ya hivi karibuni Nay Wa Mitego aliamua kumchukua mtoto wake kutoka kwa mama yake Siwema aliyekuwa akiishi jijini Mwanza baada ya kutoelewana kati yao na minong’ono ilisambaa kuwa msanii huyo anatoka kimapenzi na Shamsa Ford.

Hata hivyo wote wawili walikana kutoka kimapenzi na kwamba ni marafiki wa kawaida,Clouds Fm imezungumza na Nay kuhusu picha hiyo alisema kuwa mwigizaji huyo ni rafiki wa dada yake alienda kumtembelea na kumbeba mtoto huyo na kupiga naye picha.

‘’Siyo kweli kwamba mtoto wangu analelewa na Shamsa namlea mwenyewe na mama yangu alienda kumtembelea dada yangu akapiga picha na Curtis,’alisema Nay.

Cloudsfm.com

Mshiriki wa BBA Kutoka Namibia Amwagia Sifa Wema Sepetu

$
0
0
Mshiriki wa Big Brother Afrika ‘BBA’ Hot Shot 2014 kutoka nchini Namibia, Luis Munana, amemwagia sifa aliyekuwa Miss Tanzania 2016, Wema Sepetu kuwa ni mwenye mvuto wa kipekee.

Lakini licha ya kutoa sifa hizo, mshiriki mwenzao ambaye ndiye mwenyeji wao, Idris Sultan, hakutokea katika sherehe hiyo jambo lililozua minong’ono kwa watu baada ya tetesi kwamba ana ugomvi na Wema Sepetu.

Wema alimwagiwa sifa hizo alipokuwa katika sherehe za Instagram Party katika viwanja vya Posta Kijitonyama jijini Dar es Salaam.

“Wasanii ninaowakubali kutoka Tanzania ni Wema Sepetu, ni mrembo sana nampenda, wasanii wengine ambao nawakubali ni Shilole, Ommy Dimpoz pamoja na wimbo wake wa Wanjera,” alisema.
Washiriki wengine wa BBA waliohudhuria sherehe hizo ni Nhalanhla na Samantha wote kutoka nchini Afrika Kusini.

Wasanii wa Tanzania waliohudhuria sherehe hiyo ni Ben Paul, Izzo Bizness, Shelta, King Majuto, Stan Bakora, JJ Band, huku mshereheshaji akiwa Adam Mchomvu, B Dozen na DJ Ommy.
Hata hivyo, Wema alishukuru kupendwa na Luis. “Jamanii sina hata la kusema jinsi ulivyonisifia, nashukuru sana sana,” alijinadi Wema akishukuru.

Mtanzania

Mchezaji Yaya Toure Afanya Maamuzi Magumu

$
0
0
Uongozi wa klabu ya Man city umefanikiwa katika suala la kumshawishi kiungo kutoka nchini Ivory Coast, Yaya Toure aliyekua mbioni kutimka klabuni hapo mara baada ya msimu wa 2014-15 kufikia kikomo.

Juma lililopita uongozi wa Man City ulitangaza kupingana na hatua za kiungo huyo kuwa katika mipango ya kutaka kuondoka klabuni hapo na kwenda kusaka mahala pengine pa kucheza soka lake.

Toure amethibitisha kuendelea kubaki Etihad Stadium, baada ya kuandika katika mitandao ya kijamii, na kupokelea vyema na mashabiki wake waliouona ujumbe huo.

Naye wakala wa kiungo huyo mwenye umri wa miaka 32, Dimitry Seluk amethibitisha taarifa hizo, baada ya kuulizwa na vyombo vya habari ambavyo vilihitaji kujua ukweli wa taarifa zilizotolewa na Toure.

Seluk alitangaza kuanza mchakato wa kumtafutia klabu nyingine mchezaji wake majuma matatu yaliyopita, huku akitoa sababu za hali ya kutoelewana baina ya Toure na baadhi ya viongozi wa Man City ambao walimuonyesha dharau mwaishoni mwa msimu uliopita kwa kushindwa kumtakia kheri kwenye siku yake ya kuzaliwa.

Tayari klabu ya Inter Milan ya nchini Italia pamoja na Chelsea ya England zilikua zinahusishwa na mipango ya kutaka kumsajili kiungo huyo.

Aliyetaka Kumuua Mwanamuziki Lil Wayne Kwa Risasi Akamatwa na Polisi

$
0
0
Polisi kutoka Mji wa Atlanta waperipoti kumkamata mtu aliyejaribu kumuua Mkali wa Hipohop Lil Wayne kwa kupiga risasi basi lake la safari.

Kwa mujibu wa ripoti ya Polisi wamemtaja mtu huyo anayejulikana kwa jina la Jimmy Carlton Winfrey na ni mtu wa karubu wa Young Thug.

Kwa Mujibu wa maelezo aliyoyatoa kwenye kituo cha polisi baada ya kufanyiwa mahojiano, Jimmy Carlton Winfrey alisema aliamua kupiga basi hilo ili pate heshima ndani ya kundi lake la Bloods Gang.

Bado hukumu yoyote haijatolewa na polisi wamesema wanaendelea na uchunguzi ambapo kesi hiyo itapandishwa mahakani kwa ajili ya kutoa hukumu.

Wiki kadhaa zilizopita iliripotiwa kupigwa risasi basi la Lil Wayne lillokuwa likipita kwenye mji wa Atlanta huko Marekani, mji ambao anaishi hasimu wake mkubwa kwa sasa Young Thug.

Kumekuwa na taarifa za kupeana vitisho vya kutoana uhai kwa wasanii Lil Wayne na Young Thug ambao wanaonekana kuingiliana kwenye biashara za muziki wanao ufanya.

Profesa Muhongo Nae Kutangaza Nia Ya Kuwania Urais LEO

$
0
0
WAKATI makada watano wakiwa wamejitokeza kutangaza nia ya kuwania urais kwa tiketi ya chama tawala, CCM, leo ni zamu ya Waziri wa Nishati na Madini aliyejiuzulu, Profesa Sospter Muhongo.

Kwa mujibu wa kambi ya mwanajiolojia huyo maarufu duniani, atatangaza dhamira yake hiyo akiwa katika ukumbi wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania (OUT) Tawi la Musoma mkoani Mara.

Muhongo aliyejipatia umaarufu mkubwa wa uchapaji kazi akiwa waziri, anatajwa kujielekeza zaidi katika kuiweka Tanzania kuwa nchi ya uchumi wa kati, hasa kwa kutumia rasilimali ya nishati ya gesi iliyogunduliwa nchini.

Kiongozi huyo ambaye kwa sasa amebaki na kofia yake ya mbunge wa kuteuliwa na Rais Jakaya Kikwete, aliachia ngazi hivi karibuni kutokana na sakata la Escrow.

Hata hivyo, tume zilizoundwa kuchunguza sakata hilo, zilimsafisha yeye na Katibu Mkuu wake, Eliakim Maswi.

Muhongo anatarajiwa kuungana na Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa, Waziri wa Kilimo, Chakula la Ushirika, Stephen Wassira, Naibu Waziri wa Fedha, Mwigulu Nchemba, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Kazi Maalumu) Profesa Mark Mwandosya na Mbunge wa Afrika Mashariki, Charles Makongoro Nyerere waliotangaza nia.

Kesho itakuwa zamu ya Waziri wa zamani wa Nishati na Madini, ambaye kwa sasa ni Mbunge wa Sengerema, William Ngeleja. Ngeleja anatarajiwa kutangaza nia jijini Mwanza.

Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Dk Titus Kamani anatarajiwa kutangaza nia wakati wowote wiki hii. Aidha, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe anatarajiwa kutangaza nia kijijini kwake Rondo mkoani Lindi Jumamosi wiki hii.

Akizungumza wakati wa Tamasha la Kaswida jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki, Membe aliyekuwa mgeni rasmi siku hiyo alithibitisha kutaka kutangaza nia hiyo na kuwaomba wananchi wamsikilize kwa makini siku hiyo, kwa kuwa ataeleza kwa kina nini anataka kufanya nchi iweze kuondoka ilipo na kuendelea kudumisha amani na utulivu uliopo.

Nisha awaumbua Ommy Dimpoz na Martin Kadinda Kwa Kuonyesha Maumbile ya KIUME fake Kwenye Suruali zao ili Wasifiwe

$
0
0
Baada ya wiki chache kupita toka msanii wa bongo fleva, ommy dimpozi, kupost picha kwenye ukurusa wake wa instagram, ikimuonyesha staa huyo akiwa amevaa suruali inayoonyesha kitu chenye muonekano kama maumbile ya kiume , picha iliyozua gumzo kwenye mitandao ya kijamii, uku wengi wakimsifia staa huyo kwa kujaliwa na maumbile. Ata hivyo haikujulikana ni kwa nin staa huyo wa hit song ya wanjera aliamua kufanya kioja hicho.

Hivi karibuni tena , mwanamitindo na manager wa muigizaji Wema Sepetu aitwaye Martin Kadinda, alifanya kioja cha aina yake ambapo kama ilivyokuwa kwa Ommy Dimpozi, na yeye aliamua kupiga picha huku akiwa amevaa suruali iliyoonyesha kitu mfano wa maumbile ya kiume, hali iliyozua maswali ya sintofahamu.

Leo hasubuhi kupitia ukurasa wake wa Instagram, muigizaji na mchekeshaji maarufu bongo, Salma Jabu, maarufu kama Nisha , naye amepost picha ikimuonyesha amevaa surual inayoonyesha maumbile ya kiume wakati yeye ni mwanamke, hali iliyozua mijadala uku wengi wakidai mastaa hao(martin na ommy ) wanafanya mchezo huo mchafu wa kuweka vitu vinavyofanana na viungo vya kiume na kuwadanganya watu, kuwa ni maumbile yao, either kwa kutaka KICK au njia mojawapo ya kujitafutia wanawake kama ilivyo kwa mastaa wengi wa kike, wanavyo post picha instagram, ikiwaonyesha wana makalio makubwa ili wawavutie wanaume wakati sivyo walivyo, wengi wao wamekuwa wakitumia application maalumu ya kubadili maumbile yao.

Baadhi ya wadau mbali mbali wamewataka mastaa hao kuacha huo mchezo mara moja, licha ya kujishushia heshima zao, mastaa hao wametakiwa kuwa mstari wa mbele kukemea matendo yaliyo kinyume na maadili yetu na sio kuchochea maadili mabovu.

Bifu la Emelda Mwamanga wa Bang magazine na Reginald Mengi Kwa Kuvujisha Picha za Mengi na Familia yake

$
0
0
Mwanamama mjasiriamali, na managing director wa jarida maarufu nchini , Bang magazine , aitwaye Emelda Mwamanga amefunguka kuhusu bifu lake na mfanyabiashara maarufu nchini, Reginald Mengi, kupitia kwenye moja ya mahojiano ya kwenye kipindi maarufu cha Tv Hapa nchini .

Mbali na kuelezea experience yake kwenye biashara yake, pia alizungumzia changamoto mbali mbali anazokabiliana nazo kwenye biashara zake, moja ya changamoto alizozielezea ni ile ya kushtakiwa na mfanyabiashara maarufu nchini, Reginald Mengi, ambaye ni mume wa aliyekuwa miss Tanzania, Jackline Ntuyabaliwe maarufu kama K-Lyn.

Akielezea chanzo cha kushtakiwa, mwenyewe anadai ni kuvujishwa kwa picha za mfanyabiashara huyo akiwa na familia yake, kitendo ambacho mfanyabiashara huyo hakukipenda hivyo aliamua kumshtaki mwanamama huyo kama adhabu na fundisho.

Akielezea kwa masikitiko mwanamama huyo alielezea jinsi ya picha hizo zilivyosambaa mitandaoni, ambazo zilipigwa mahsusi kwa ajili ya kupambwa kwenye jarida maarufu la mwanamama huyo, hata hivyo inasemekana baadhi ya wahariri wa jarida hilo walizivujisha picha za Mengi huyo kwenye mitandao ya kijamii either kwa bahati mbaya au kwa kukusudia , kitendo kilichomkera Mengi na kuamua kumshtaki.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumanne ya Tarehe 2 Juni 2015

$
0
0
























Habari  Zilizopo  Katika  Magazeti  ya  Leo  Jumanne  ya  Tarehe 2 Juni 2015

Mtoto Wa Nyerere Avuruga Urais CCM.....Adai Lowassa, Pinda, Wassira na Mwigulu ni WEZI na Wanahonga.....Atangaza Nia ya Urais Butiama

$
0
0

Mbio za kusaka urais kwa makada wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) zimezidi kushika kasi baada ya mtoto wa tano wa Hayati Baba wa Taifa, Mwalimu Nyerere, Charles Makongoro Nyerere kujitosa kwenye kinyang’anyiro hicho.

 

Wakati Makongoro akichukua uamuzi huo kwa mara ya kwanza katika historia ya familia ya Mwalimu Nyerere, mkoani Mbeya Waziri wa Nchi,Ofisi ya Rais Kazi Maalumu, Profesa Mark Mwandosya naye ameingia kwenye mbio hizo.

 

Makongoro

Akitangaza nia yake katika eneo la Mwitongo kijijini Butiama jana, Makongoro aliwashambulia makada wenzake ndani ya CCM ambao wanaongoza makundi ya kuwania urais kwa kuwaita ni ‘vibaka’ wanaokivuruga chama hicho kwa maslahi yao binafsi.

 

Akitoa mfano kwa baadhi ya makada wanaoongoza makundi ndani ya chama hicho, Makongoro aliwataja kwa majina kuwa ni Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa, Naibu Waziri wa Fedha,Mwigulu Nchemba na Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Steven Wasira.

 

Alisema makada hao kwa muda mrefu wamekuwa wakitumia fedha nyingi kuendesha makundi ya urais na akahoji sababu za kutafuta cheo hicho cha juu kwa fedha.

 

"CCM irudishwe kwa wazalendo kwa sababu vibaka wamekuwa na mlengo mbaya wa kukiendeleza chama hicho,"alisema.

 

Alisema ndani ya chama hicho kumekuwa maradhi ya rushwa ambayo yameiambukiza nchi nzima.

 

Makongoro alisema yeye ni mzalendo wa kweli na anataka kuirudisha nchi katika misingi ya uadilifu endapo CCM itampa ridhaa ya kupeperusha bendera katika uchaguzi mkuu wa Oktoba mwaka huu.

 

Alisema ndani ya chama hicho kumekuibuka genge la watu wachache ambao utajiri wao ni wa shaka na umejijenga kwa fedha chafu.

 

“Ndani ya chama tawala wamekuwapo ‘vibaka’ wachache… unajua kibaka ni kibaka tu hata kama kapewa gari la Serikali lina bendera ya taifa mbele atabaki kuwa kibaka tu.

 

“Wananijua vizuri huwa siwaonei haya kuwaambia ukweli, hawa ndiyo wanaotuvurugia chama na hawamheshimu Mwenyekiti wa chama, Rais Jakaya Kikwete,” alisema Makongoro.

 

Katika hotuba yake ambayo alitumia saa mbili, Makongoro alijikita kuzungumzia madhara yanayotokana na rushwa ndani ya CCM.

 

Alisema baadhi ya makada wanaotumia rushwa wamezalisha makundi na mipasuko isiyo ya lazima huku akisisitiza kuwa anachukia kuwapo makundi ndani ya chama hicho.

 

Kwa mujibu wa Makongoro, hali hiyo imechochea badhi ya viongozi wa CCM katika ngazi mbalimbali wakiwamo wenyeviti wa mikoa na wajumbe wa Halmashauri Kuu ya chama hicho kuishi kama mifugo.

 

Alisema hali hiyo imesababisha baadhi ya viongozi hao kuishi maisha ya kusukumwa kwa upepo wa makundi yanayomilikiwa na watoa fedha.

 

“Vibaka waturudishie CCM yetu, watambue wao ni wachache na sisi wazalendo ni wengi, hawatushindi na fedha zao na kitaeleweka tu.

 

“Leo hii viongozi wetu wa CCM wamekuwa ni watu wa kuendeshwa na vibaka hawa wanahongwa fedha ovyo…wao wana mifugo yao ndani ya NEC basi mimi sijafuga hata kuku, nasema kitaweleweka,” alisema Makongoro.

 

Alisema yeye hawezi kufanya hivyo kwa sababu rasimu ya ilani ya chama hicho bado haijapitishwa na chama, hofu yake ni kwamba anaweza kutoa ahadi na zikawa kinyuume na ilani ya chama chake.

 

“Nimewasikia wanajinadi,nawashangaa sana, najiuliza kwani wao ni akina nani watoe ahadi kabla ya ilani ya chama? Ikitokea ahadi yako ikaenda kinyume na ilani si ndiyo mwanzo wa kuwa na rais muongo…sitaki kuwa rais muongo nitaheshimu chama changu kwa kila mchakato na maelekezo,” alisema Makongoro.

 

Aliwaasa Watanzania wawaogope watu wanaoonekana kuwa na haraka ya kukimbilia kutawala nchi.

  

“Ukiona watu kazi inatangazwa ifanywe kwa utaratibu wake na mtu aliyeiomba kazi hiyo anakiuka taratibu, muogopeni sana huyo hafai kukukuongoza maana hata akikuongoza ataendelea kukiuka taratibu ili ajinufaishe,” alisema Makongoro.

 

Wanawake wananipenda

Makongoro alisema anakerwa na siasa chafu dhidi yake zinazoenezwa na baadhi ya wanasiasa wenzake ndani ya CCM.

 

Alizitaja siasa hizo kuwa ni tuhuma za kulaaniwa na baba yake, ulevi na mtu anayependa wanawake.

 

Akijibu tuhuma hizo, Makongoro alihoji umati uliomiminika kumsikiliza kwamba,“jamani naonekana nimelaaniwa? Naelekea kuokota makopo? Jamani mnanionaje, naonekana mlevi? na umati ulikataa kwa kusema, “hapana”.

 

“Eti wanasema Makongoro anapenda wanawake sasa wanataka nipende wanaume? Wanawake wananipenda na mimi nawapenda, hizi siasa chafu wanazonituhumu hazinisumbuilangu ni moja tu vibaka rudisheni nchi yetu,”alisema. 

 

Nimrod Mkono

Naye Mbunge wa Musoma Vijijini , Nimrode Mkono alisema atakuwa bega kwa bega na Makongoro kuanzia sasa katika safari yake ya kuwania urais mpaka hatua ya mwisho.

 

“Wapo wengi walionifuata niwe nao katika harakati zao za kuwania urais, sasa nawaambia ‘bye bye’ nipo na Makongoro na wasijihangaishe kunitafuta,” alisema Mkono.

 

Shyrose

Mbunge wa Bunge la Afrika Mashari, Shyrose Banji na mwanamuziki wa kizazi kipya, Judith Wambura ‘Lady J Dee’ nao walihudhuria kikao hicho.

 

Makongoro afananishwa na Daudi

Awali kabla ya Makongoro kutangaza nia ya kugombea urais,baadhi ya viongozi wa dini walimuombea ambako Mchungaji wa Kanisa la Anglikana, Jackob Ngagani alimfananisha na Daudi.

 

Alisema anaamini Mungu atamuongoza Makongoro kushinda ushindani wa kupata mgombea urais kupitia CCM.

Kabla ya dua ya viongozi wa dini, wazee wa kabila la Wazanaki, walimvisha vazi la asili la kabila hilo na kumkabidhi fimbo kwa ajili ya kuwaongoza Watanzania.

 

Naye Chifu wa Kabila la Wazanaki, Japhet Wanzagi alisema Makongoro ni simba na kusisitiza kuwa kabila lao huwa halibahatishi.


Mwanamuziki NAKAAYA Sumari Amjibu MANGE Kimambi Baada ya Kuandika Kuwa Nakaaya na Nancy Sumari Wana Ugomvi Mkubwa

$
0
0
Nakaaya Sumari Katika Pozi
Baada ya Mange Kimambi kuandika Kwenye Blog kuwa Nakaaya na Mdogo wake Nancy Sumari Hawapatani na Wana Ugomvi Mkubwa... Nakaaya Ameamua Kuandika Haya Kama Jibu la Post aliyoandika Mange:

Nakaayasumari Dear Mange. I trust all is well. It is important that I address post uliyoweka kwenye blog yako. If you trully know me like you said you do, utajua kuwa nawapenda sana wadogo zangu wote. Sio tu Nancy. I think what you have planted on peoples minds is a bit too much. The comments are unbeliavable and I dont think you fully understand the impact of your post. LET ME SAY- MY SISTER HAS NEVER HAD AN AFFAIR WITH ANY OF MY PARTNERS. NEVER. We were not raised that way. I do not appreciate the pictures you have painted of me and my sister. Kuwa she is the devil and i am the poor victim. You should do a little more research before stressing families and harming people's reputations. Yeye sio ulivyomuandika.
Na mimi sio victim ulivyosema. We are mothers living in different parts of the country with different paths and interests. It doesnt mean we hate each other! On the contrary!!! You forget kuwa we are blood. Ni familia ipi haina issues? Yes we fight. But we make up. Like other sisters. We are both stubborn and strong heads. We are bound to kwaruzana. Ni kitu cha kawaida sana.

You have let derrogatory comments loose, and make it seem kuwa success yake ni mbaya. Kuwa hatupendi. Naomba nikuambie anatupenda sana. She does so much na sijui kama alihitajika kutangaza. Mange, you were right about one thing. Nawapenda sana wadogo zangu. I will not stand and let you tarnish her like that. I am not where I want to be, but I am certainly not where I used to be. Jamani is that a crime? You made me out to be a sad victim!! You have hurt the family sana. Kama kuna shida, ambayo haipo basi wazazi wetu watamaliza. Asante.


Bongo Movies Fan Claims That Kajala Has Bigger and More Beautiful Goodies Than Wema....

$
0
0
There's a debate here about who has bigger and better goodies between Wema and Kajala?
What do you think??

DIVA Loveness Atangaza Kuitaji Mwanaume wa Kuzaa Nae..Masharti Haya Hapa Bila Kusahau Kuwa Uwe Unaiweza Shughuli Kitandani

$
0
0
Nahitaji Mwanaume wa Kuzaa Nae Mtoto Mzuri Kama Huyu Maana Nina Baby Fever n sina Bwana chuChuchu ' tototoo .. ajiginjiginjiiii ...  dem eyes tho . damn It! There Goes My baby' what a Diva ... dah anyways Ntafanya Audition Tho at escape1 soon. terms and Conditions muhimu .. nataka .5 Moja Look alike ya @chrisbrownofficial afu shughuli awe ana iweza afu awe na Cheda. i dnt need some broke ass , dumb ass Mofo! i jus need A real Man.. Shababi afu Mashaallah .. Sio Some Pretty Boy anivunje moyo wangu Coz he is annoying Mofo who thinks Money runs his Own D! yaan inshort sio Some Lito boy wit lots of love n pretty face but thirsty ass .. sitaki' sitaki some cute Man like ... (mute) maana nshalia sana kisa some .... cute baby boo sitaki tena afu good looking basi awe msafi kama Chris Breezy. nataka handsome mmoja ajabu' a goon with some Mullah lalaa - so i can floss na yeye .. By Diva

Breaking News:Lori la Mafuta Langonga Treni Jioni Hii Maeneo ya Buguruni..Njia zafungwa

$
0
0
Jinsi hali ilivyo katika maeneo kati ya Buguruni na Tazara mara baada ya Lori la mafuta kugonga Treni la mizigo na kuburuza nje ya Reli....hivyo njia imezibwa hakuna mawasiliano kati ya magari yatokayo Temeke kuja Buguruni wala kutoka Ubungo kuelekea Temeke au Buguruni kwa kupitia Mandela Road jioni hii

Alichokiongea Profesa Muhongo LEO Wakati Akitangaza Nia Yake ya Kugombea Urais Kwa Tiketi ya CCM

$
0
0
1.Niko mbele yenu sio kufanya kampeni ya urais, niko mbele yenu kuomba ridhaa ya yenu kugombea nafasi ya urais muda ukifika.
 
2. Siko hapa kumlaumu mtu au ukimshambulia kwa sababu ukimlaumu mtu umAsikini bado uko palepale. Nikisema historia yangu yote muda hautatosha, kisomo nimesoma mpaka mwisho wa kusoma, kama ni taalumu nimefikia mwisho.
 
3.Nimepata bahati ya kusoma vyuo vikubwa sana duniani na sehemu kubwa nimepatia Ujerumani ndio maana wengine wanasema nafanya kazi kijerumani.

4. Nimefanya utafiti kwa miaka 30,chama cha majiologia wamerekani kilichoanza mwaka 1988, mimi niko ngazi ya juu pia kwa waingereza na wachina niko ngazi ya juu kabisa.

5.Kwenye uasisi mwaka 1976, CCM inaanza 77 sisi ndo waasisi, kadi hii hapa. Kama nimeweza kutunza kadi ya CCM tangu 75 basi mimi ndio naweza kutunza rasilimali zenu.

6.Toka tunapata uhuru tuna vikwazo, ujinga, maradhi na umasikini Mwl alitueleza. Nil lazima matatizo yatakuwepo kwenye jamii.

7.Rushwa kubwa na ndogo, ukosefu wa ajira, siasa imekwenda kila mahala, taifa linanyemelewa na uvuvu na utegemezi, dhulma, upungufu wa upatikanaji wa takwimu sahihi, tumepungukiwa ushindani kama taifa, tumeshindwa kujiamini.
 
8. Haya ndio nataka kuyashughulikia mimi. Upungufu wa mshikamano wa taifa letu. Kwetu asilimia 51 waislamu na 49 wakristo hivyo matatizo ya madhehebu hapa ndipo mahala pake. Afrika ina nchi 54, mimi nimeeenda 52 kasoro Mauritania na Chad. Ningekua sio muaminifu nisingepokelewa huko, ulaya nimezunguka.

9.Lazima Tujue hali halisi ya uchumi wetu, chukueni kalamu na karatasi. Lazima useme unatoka wapi unaenda wapi! India asilimia 74 wanajua kusoma na kuandika. Nchi inayoongoza kwa watafiti ni Finland.(Anataja takwimu za nchi ambazo tulikuwa tunafanana uchumi baada ya vita ya pili ya dunia ikiwemo India, Brazil, China na Kenya.) Sipendi sana kujilinganisha na Kenya kwa sababu sote ni maskini.

10.Dira ya maendeleo inasema miaka kumi kutoka sasa Tanzania isiwe nchi masikini, tusikae pembeni, tusogee juu kidogo. Hakuna mwenye uwezo huo ni mimi tu ili tufikie pato la dola bilioni 200 kutoka dila bilioni 40. Mwaka 2025 tutakuwa milioni 60, nataka tule miogo na viazi kwa hamu na sio kwa shida.

11.Siwezi kukupa ahadi ya mishahara wakati sijakuza uchumi, siwezi kukupa ahadi ya kukujengea shule wakati sijakuza uchumi, tukuze kwanza uchumi.

12.Naombeni ridhaa yenu nisimamishe deni la taifa lisiongezeke, mwenye dawa ya umaskini ndani ya CCM, CHADEMA, NCCR ni profesa Muhongo tu. Elimu kuiboresha lazima tuongeze bajeti, haiwezekani darasa limerundikana ukafundisha. Anaeweza ni mimi tu sababu wengine utafiti wanausoma kwenye magazeti tu.

13.Wana CCM mnae mwanasayansi wa dunia, si mnipe tu! Tutatumia rasimali, madini yetu tumeyachimba kwa asilimia 10 kitu, mimi ndio nimetengeneza ramani ya madini ya Tanzania, Africa na duniani nikiwa vice president. Nilizunguka hii nchi kuchora ramani ya madini kwa uzalendo, ningiweza kuja na ramani na kuuzia serikali.

14. Mimi mtu anidanganyi, unakuja tunajadiliana, hii sio dunia ya kuandikiwa tu, inabidi na wewe ujiandikie. Niliweka mipango ya kuwapunguzia bei ya umeme. Ilibidi nitoke kidogo mpate machungu mnichague.
 
15. Nawaomba ifike mahala ifike mahala tuachane na matumizi ya kuni na mkaa, ni aibu sana. Tutajenga mabomba nchi nzima gesi itumike majumbani. Kila nyumba iwe na mabomba mawili, la maji na la gesi.

16.Wengine mnaweza kuwadanganya, mimi hamuwezi kunidanganya, gesi yenu ipo kwenye mikono ya uhakika kwa professa Muhongo tangu nimeanza kusoma wakati niko chuo kikuu cha Dar es Salaam na nimefanya maisha yangu yote.

17.Mapato ya gesi yasiende hazina, tutafungua mfuko maalumu na bunge litakua linaizinisha asilimia ngapi iende kwenye bajeti. Mtanzania yoyote asiwe na maamuzi ya kutumia hizo fedha bila idhini ya watanzania.

18.Mimi sipendi wawekezaji wababaishaji na si kwamba sipendi wawekezaji wa ndani, haya yote ya ujenzi wa uchumi lazima tuwe na umeme. Na umeme wa bei nafuu ndio kazi niliyokuwa naianza. Umeme ulikuwa haukatiki mara kwa mara, muda umefika tusijidharau, lazima tushinde.

19.Lazima watanzania zaidi ya asilimia zaidi ya 75 wawe wanatumia umeme, tutatumia vyanzo vyote vya umeme. Lazima mtembee kifua mbele professa Muhongo amitimiza ahadi ya CCM, hata ilani mpya inayokuja mtekelezaji atakaetekeleza kwa uhakika ni professa.

20.Ni lazima tupambane na rushwa, na sio maneno kupambana nazo na nyie wananchi muwe na uelewa na haki zetu. Mnaombwa rushwa kwa sababu hamjui haki zenu. Naomba ridhaa yenu mniteue niwe mgombea wenu. Wakulima na wafugani ni mwisho wa kuuana chini ya prof Muhongo, tatizo sio ardhi, ni technologia.

21.Uwezo ninao, maarifa ninayo, jinsi ya kutafuta fedha ndani na nje, ambacho sina ni nyinyi kuniteua tu.
Viewing all 104698 articles
Browse latest View live




Latest Images