Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104789 articles
Browse latest View live

Only God will save Kenya, This was captured in a city Club, Sodom & Gomorrah (VIDEO)

$
0
0
The city of Nairobi has been turned into another Las Vegas thanks to the hundreds of clubs that are spread all over the town.

What happens in most of city clubs can be compared to Sodom and Gomorrah.

Ladies do the unthinkable and it’s clear that most of the city residents are only surviving under the Lord’s mercy.

After watching the video below that was captured in one of the city clubs, you will just go down to your knees and pray for our nation.

Click play and watch the action.


Ally Kiba will faints after seeing these photos.....Just read what Jokate wrote on this photo

$
0
0
This is what Jokate captioned this photo; Business Meeting In Nairobi With Fareed Khimani At His Restaurant Monikos at Valley Arcade. Check It Out Once In Nairobi-Kenya. Usengwile.

Trending Photo on INSTAGRAM, This Kajala and Chuchu Hans's Photo received more than 1000 likes just in 20mins on INSTA

$
0
0
Trending Photo on INSTAGRAM, This Kajala and Chuchu Hans's Photo received more than 1000 likes just in 20mins on INSTA

Lowassa: Mimi Ndiyo Nitaleta Mabadiliko CCM

$
0
0
Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa jana alisema kuwa muda wa mabadiliko aliyotabiri Baba wa Taifa, Mwalimu Nyerere ni sasa na kwamba yeye ndiye anayeweza kuyaongoza.

Wakati Lowassa akisema hayo mjini Iringa, kada mwingine anayewania urais kwa kupitia chama hicho, William Ngeleja alikuwa mkoani Mwanza ambako alisema kuwa ana dhamira ya dhati na nia ya kuleta mabadiliko kwa maisha ya Watanzania.

Mjini Iringa, Lowassa alisema kuwa kwa sasa CCM inahitaji mabadiliko makubwa na akanukuu kauli ya Mwalimu Nyerere aliyoitoa mwaka 1995 alipozungumzia haja ya chama hicho kujisahihisha.

“Baba wa Taifa alisema kuwa Watanzania wanahitaji mabadiliko na wasipoyapata ndani ya CCM watayatafuta nje ya CCM,” alisema mbunge huyo wa Monduli kwenye hafla hiyo iliyofanyika Uwanja wa Samora mjini Iringa.

“Huu ni wakati wa mabadiliko. CCM ikijipanga inaweza kuleta mabadiliko na mtu wa kuleta mabadiliko hayo ni mimi,” alisema.

Lowassa alisema aliamua kuingia kwenye mbio za urais kwa sababu tatu, ambazo ni kufanya mabadiliko ndani ya CCM, kufanyia kazi tatizo la umaskini na kushughulikia tatizo la ajira kwa vijana.

Kocha Mkwasa na Julio kocha msaidiz sasa ndani ya Taifa Star! Wazungu Hatutaki Tena......

$
0
0
Habari! naandika hivi kwasababu zifatazo.

1. Mkwasa ni kocha mzuri sanaa, anajua kufundisha mpira wa kibongo na wakimataifa (yanga) anaufahamu sanaa.

2. Julio ni kocha msomi, ana beji za kimataifa, ni mtaalamu wa mpira wa fitina nje ya uwanja, na mpira wa bongo anaujua sanaaaa.

SASA.
Namba moja anatasaidia sanaa kufundisha mpira ndani ya uwanja kimataifa na ndani. na namba mbili atasidia kusaka vipaji kila kona ya nchi na kumpa mkwasa na kuweka sawa plus vitina zake nje ya uwanja

Tiafa star hapo itakuwa bora, kuliko sasa bora taifa star.

Tukiweza kwa style hii, baadaye ndio tutaleta mzungu kufundisha mpira wa darasani.

Jamani Housegirl wangu Huyu, Ananitafuta ubaya! (STRICTLY KWA WANAUME TU)

$
0
0
Jamani naomba ushauri kuhusu hili.

Mimi ni mume wa mke mmoja na watoto wanne. Hivi karibuni tumepata housegirl mpya kutoka Singida, amemaliza form four hakubahatika kuendelea na masomo kwa sababu ya kukosa sifa za shule za serikali. Ni mzuri wa kawaida, yaani hana muonekano ule wa mahousegirl-naamaanisha muonekano choka mbaya kweli anafaa hata kuwa mke wa mtu. Katika historia yangu sijawahi hata siku moja kutembea na housegirl na mpaka sasa nishaajiri hao h/girl si chini ya 6, huwa niko very serious na sitaki mazoea nao hata kidogo.

Huyu amekuja naona anataka kuniangusha katika msimamo wangu huu. siku ya kwanza kutambulishwa kwake alionekana kushituka sana ingawa na mimi kwa ndani nilimkubali kuwa mzuri. Maisha yakaendelea na siku zikafunguka. Sasa toka siku hiyo amekuwa anakosa sana sana tu confidence ninapokuwa nyumbani, mara atajikwaa, mara ataogopa kuja mbele yangu n.k mbaya zaidi ninapokuwa peke yangu lets say wengine wapo mbali ananichangamkia sana na kutabasamu muda wote kila nitakalooongee yeye anatabasamu hata kama si la kufurahisha, nikimtuma kitu ataniletea wakati napokea anainua kichwa kuniangalia kiuchokozi halafu anatabasamu, basi na mimi nikawa natabasamu. Ikitokea labda nimerudi nyumbani na nahitaji chakula mapema atanipikia vizuri sana wakati mwingine anongeza kitu ambacho hakikupangwa kwenye ratiba ya chakula cha siku hiyo, anaweza kunkaangia mayai au akachemsha chai ya maziwa akaweka na viuongo haraka haraka na kunipatia chakula.

Tatizo, wife keshamshitukia hizo nyendo zake, amekuwa kila mara ananiuliza kuhusu mtu huyu, anasema mbona fulani ukiwepo anakuwa hana confidence nikamwambia mi sijui embu muulize alipomuuliza akamjibu wife kuwa eti ananiogopa kwa sababu aliambiwa na mlinzi mi ni mkali sana achunge asinikorofishe. Lakini ukiangalia mapozi yake kwangu si ya mtu anayemuogopa. Si hizi ameongeza zaidi, kunisalimia/kuniamkia kwake imekuwa ngumu sana ni mara mojax2 sana. Mi kwa ujumla ni mtu nisiyejali vitu vidogo vidogo na nilichojaribu kufanya ni kuwa mbali nae, nimeongeza kuwa serious, na wakatui mwingine nakuwa mkali ninapoongea nae ili awe mbali nami au afute hicho anachofikiri au kukitafuta, Lakini nahisi ananitafuta ubayaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa aaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa!

Nimfanyeje? au nifenye lakini nahisi kujidhalilisha kwa mah/girl!

Le Mutuz Amfagilia Tena Wema...Ataka Watu Waache Chuki na Wivu Juu ya Wema Sepetu.....'Matatizo yako ya maisha ni yako mwenyewe pigana nayo'

$
0
0
PEACE JAMANI AMANI PEOPLE hata kama humpendi yeye lakini HESHIMU NYOTA YAKE cause tatizo sio yeye ila NYOTA and guys lets support her MBUNGE MTARAJIWA and yes I said it STOP HATING I mean guys TUPENDANE LIIFE IS TOO SHORT narudia huwezi KUMCHUKIA MTU USIYEMJUA NA ASIYEKUHUSU KAMA WEWE BINAFSI SIO A DEAD MAN WALKING mazafantazz ndio maana unataka na WENGINE WAFWE KAMA WEWE ...and wacha hizo CHUKI NA.WIVU WAKO matatizo yako ya maisha ni yako mwenyewe pigana nayo mwenyewe kila mtu ana yake na usieme mambo ya Chuki kayaleta fulani ina maana utaenda mbele ya Mungu useme niliambiwa KUCHUKIA WENGINE NA FULANI? people STOP HATING NOW...IT IS WRONG AND IT IS A SIN! Now Imagine unajaza.bundle kwa hela nyingi ili UKANUNUE DHAMBI hahahaha that is LE MBURULAZZZZ STOP IT NOW! - le Mutuz

@lemutuz_nation on Instagram

Mzee Majuto Amuunga Mkono Wema Sepetu, Diamond Amtaka Wema Abadilike Kama Kweli Anautaka Ubunge

$
0
0
Mzee Majuto  kwa mara ya kwanza ameamua kufunguka kumuunga mkono Wema Sepetu kwa nia yake ya kutaka kuwa mbunge.Kupitia ukurasa wake mtandaoni, Mzee Majuto ameandika;

Nisingependa kuyaongea haya kwenye mfungu mtukufu ila kiundani ningependa kuonyesha umoja na kumuunga mkono wazo na lengo la Mwanangu kwa kuwa anaweza na amethubutu sasa isitokee wale wasiopenda maendeleo ya watu na taifa hili kuvuruga misingi na mipango madhubuti ya kuwapa nafasi vijana na hasa wanawake kushika hatamu na kuleta mabadiliko.Kapeleke mabadiliko Singida na Tanzania nzima.

Muhimu ni kuwa na juhudi uwezo imani pamoja na uzalendo. Ujumbe huu pia ni kwa kila kijana na mwanamke mwenye lengo na nia ya udhubutu. Inshallah. Ramadhan Maqbul Waislam wote. Mzee Majuto alimaliza na kumtag Wema.

Moja kati ya waliochangia kwenye andiko hili la Mzee Majuto, ni Diamond Platnumz ambaye alimtaka Wema abadilike kama kweli anautaka ubunge.


  • “Swala siyo watu kumvunja moyo ,..ila yeye abadilishe akili ya mambo ya kushabiki migogoro ya watu wengine mitandaoni aache..katia aibu sana jana ,katangaza ubunge na bado ana shadadia ugomvi wa Diamond na Davido ,...mbunge ndo wakuwa na akili hii kweli,...watu wanahasira na upuuzi unaofanya na team yake na bado yeye mwenyewe anachochea ...watu watamuachaje....abadilike kama kweli anataka kugombea ubunge”


Wewe mdau unakipi cha kusema hapa.

Mwanamuziki Diamond Ampa Makavu Live WEMA SEPETU..Adai Anaitaji Kubadilika..'Jana Katangaza Kuwania Ubunge Lakini Bado Anashadadia Ugomvi wa Diamond na Davido'

$
0
0
Dimond: Wema and Her Team Must change- Wema for MP...
This is Diamond comment on Wema regarding her motives to MJENGONI

For those who love VERA SIDIKA, she's back & this is what she wants you to see

$
0
0
Well endowed socialite, Vera Sidika who has of late been keeping a low profile of herself is now back.
The lass, who is never afraid when it comes to flaunting what her mama gave her, recently took to social media to give “team mizigo” the best view of her giant bo0ty

Habari Njema Kwa Waathiriwa wa picha za ngono katika mtandao wa Google......Google sasa yakubali kuondoa picha za uchi

$
0
0
Waathiriwa wa picha za ngono katika mtandao wa Google wataruhusiwa kutuma ombi kwa kampuni hiyo la kuziondoa picha hizo.
Picha hizo zitaendelea kuwa katika mtandao huo lakini hazitaorodheshwa katika picha wakati wateja watakapozitafuta.
Makamu wa rais wa kampuni hiyo Amit Singhal amesema kuwa mpango huo utashirikisha picha za uchi na zile zenye uchafu mkubwa.
Google hapo awali ilikataa jaribio la kuitaka kuondoa picha kama hizo katika picha zilizoorodheshwa katika mashine yake ya utafutaji.
Mpango huo mpya unatarajiwa kuanza kufanya kazi katika kipindi cha wiki chache zijazo.

Lowassa Azidi Kupata Mapokezi Makubwa Kila Anakoenda.......Songea Alazimika Kukaa Juu ya Paa la Nyumba, Asema Jina Lake Haliwezi Kukatwa

$
0
0
WAZIRI Mkuu Mstaafu,Edward Lowassa amesema hana shaka na swala la kukatwa jina lake katika vikao vya Chama cha Mapinduzi(CCM), kwani anaamini Chama chao kitatenda haki kwa kurudisha jina lake kuwa mgombea urais wa Tanzania.

Lowassa aliyasema hayo jana wakati akizungumza na wanachama wa CCM na wananchi wa Mkoa wa Ruvuma katika ofisi kuu za CCM Mkoani humo, wakati akitoa shukrani baada ya kudhaminini na wanaCCM zaidi ya elfu 52.

"Nimekuwa mwanaCCM tangu mwaka 1977 nilipomaliza chuo kikuu, sijawahi kufanya kazi nje ya CCM hivyo nakijua chama na hakuna mgombea atakayeweza kuvunja rekodi ya utendaji wangu katika chama, sasa leo anayetaka kukata jina langu anatoka wapi? anakata kwa sababu gani? Sioni kosa la kukatwa jina na Watanzania hawaoni, kwa hiyo msiwe na wasiwasi jina litarudi tu". alisema Lowassa.

Lowassa aliwasili Mkoani Ruvuma mapema  jana mchana akitokea Mkoani Iringa kwaajili ya kusaka wadhamini katika mbio zake za kusaka urais kwa tiketi ya chama hicho, ambapo umati wa watu ulifurika kumlaki na kupelekea kufunga barabara kuu ya mjini, hali iliyompelekea Lowassa kupanda juu ya paa la  jengo la ofisi ya CCM Mkoa ili aweze kuzungumza nao.

Risasi Zarindima Vituo Vya BVR Arusha, Godbless Lema Atiwa Mbaroni

$
0
0
MILIO ya risasi ilisikika katika vituo vya uandikishaji kura katika kata ya Sokoni One jijini hapa, baada ya kuibuka kwa vurugu zilizohusisha vijana wa Chadema na wenzao wa CCM, chanzo kikitajwa madai ya kuwepo kwa watu ambao sio wakazi wa eneo hilo kutaka kujiandikisha.

Vurugu hizo zilisababisha takribani watu 15 kukamatwa akiwemo Mbunge wa Jimbo la Arusha Mjini, Godbless Lema (Chadema) ambaye hata hivyo baadaye aliachiwa huru. Alishikiliwa kuanzia saa 1:30 usiku hadi saa 4:00 usiku juzi.

Patashika hiyo ilichukua zaidi ya saa moja, kwani baadhi ya polisi waliokuwa na silaha za moto aina ya bastola walifyatua risasi hewani kwa lengo la kutawanya vurugu hizo, lakini hali ilikuwa mbaya zaidi hadi polisi walipoongezwa na kufanikiwa kutuliza ghasia hizo.

Wakati hayo yanatokea Lema alisisitiza kuwa kamwe hawezi kukubali kutohamasisha wananchi kwenda kujiandikisha katika Daftari la Kudumu la Wapigakura licha ya kudai kuwa, kundi la vijana wanaosadikiwa kuwa wa CCM wamempiga mawe sambamba na watu wengine waliojitokeza kujiandikisha katika kata mbalimbali.

Hata hivyo, upande wa vijana wa CCM, umedai wenzao wa Chadema ndio chanzo cha vurugu, kwani wameonekana wakisambaza makundi ya vijana wasiostahili kuandikisha katika vituo mbalimbali.

Lema ajitetea
Akizungumzia kukamatwa kwake na polisi wa kata ya Osunyai kutokana na vurugu zilioibuka, alidai alikuwa akitoa taarifa za uongezwaji wa mashine za BVR kwa wananchi na kuwapa moyo kuwa watulivu wakati wa uandikishwaji sambamba na kutunza vitambulisho hivyo kwa ajili ya kupiga kura mwaka huu katika uchaguzi mkuu wa rais, wabunge na madiwani.

Alisema wakati akiendelea kuwapa moyo wananchi na kusema Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imeongeza mashine za BVR, ghafla aliona vijana anaodai wamekodishwa kufanya vurugu kwenye vituo mbalimbali vya kujindikisha na ndipo alitoa taarifa Polisi, lakini badala ya kukamata vijana hao alikamatwa yeye na vijana wengine na kuwekwa mahabusu.

NEC iliruhusu uandikishaji kuendelea hadi saa mbili usiku kutokana na wingi wa watu wanaostahili kuandikishwa.

Hata hivyo mmoja wa wafuasi wa CCM aliyejitambulisha kwa jina la Abdi Marijani maarufu kwa jina la ‘`Mutu’ alisema Chadema wamekuwa wakileta watu ambao sio wakazi wa Jiji la Arusha kutaka kujiandikisha hali iliyopingwa na vijana hao.

Mutu alisema CCM ilikuwa imepewa taarifa juu ya njama za Chadema za uchomekeaji watu katika kila kata na chama kikaweka vijana imara katika kila kituo wakiwa na mabalozi ambao ndio wenye jukumu la kujua mkazi wa eneo husika.

Akizungumza na waandishi wa habari mjini hapa jana, Lema alisema juzi akiwa kata ya Osunyai alishangaa kuona kundi la vijana wakiwa kwenye gari aina ya Toyota Land Cruiser lenye namba za usajili T 122 ATR ambalo alidai wakati mwingine gari hilo lilibadilishwa namba na kusomeka T 122 ABR wakishuka ghafla na kuanza kumpiga mawe na kuwapiga vijana wengine 25 ambao walikuwa katika kituo hicho.

Alisema wakati tukio hilo likitokea alitoa taarifa kwa Mkuu wa Upelelezi wa wilaya OC/CID, Faustine Mwafele ili kuwaelezea tukio hilo, lakini polisi walifika eneo la tukio badala ya kuwakamata vijana hao walimkamata yeye na vijana waliokuwepo kisha kuwaweka chini ya ulinzi.

Alisema inaonekana kundi hilo linaonekana lipo juu ya sheria watu wanafanya fujo za waziwazi, huku mbunge akigeuziwa `na kusulubiwa.

Alisema kwa kuwa yeye ni mbunge, hawezi kuacha kuhamasisha wananchi wake kujiandikisha badala yake chama chao na viongozi wa chama wataendelea kuhamasisha watu kujitokeza kujiandikisha sambamba na kuhamasisha watu wasikate tamaa katika kujiandikisha kwa sababu ni wajibu wao wa kisheria, kisiasa na kidemokrasia.

Aliongeza kuwa udhalilishwaji sasa umefika mwisho, hivyo alitoa rai kwa vijana wa chama hicho kuchukua hatua ya kuwalinda viongozi wao, kulinda demokrasia na mali zao.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Liberatus Sabas hakupatikana kuzungumzia tukio hilo, licha ya kutafutwa kupitia simu yake ya mkono ikiwa ni pamoja na kutumiwa ujumbe mfupi wa maandishi.

Wasemavyo CCM
Akizungumzia hilo, Katibu wa CCM wa Wilaya ya Arusha, Feruz Banno alisema vurugu zilianzishwa na vijana wa Chadema kwa kuwapiga vijana wa CCM na kupiga risasi hewani hovyo bila ya sababu za msingi.

Banno alisema dola Arusha inapaswa kuwa makini, kwani hali inaweza kuwa mbaya zaidi iwapo hilo halitadhibitiwa na kuwafanya watu wengine kushindwa kwenda kujiandikisha kwa kuogopa vurugu.

Alisema kutokana na vurugu zinazofanywa kwenye baadhi ya vituo vya kujiandisha na baadhi ya viongozi wa Chadema ili kudhibiti wazee na akinamama wanaokwenda kujiandikisha kwenye vituo hivyo.

Alisema kwa sasa uandikishaji unafanyika katika kata za Terati, Murieti, Olusunyai, Moshono, Sinoni na Sokoni One, lakini baadhi ya vijana wa chama hicho wamekuwa wakisafirishwa kwa magari kutoka kata tofauti na hizo na kupelekwa eneo hilo kwa ajili ya kujiandikisha .

Ulinzi
Kwa upande wake Marijani, alisema kutokana na udhibiti uliowekwa na makamanda wa CCM vituo vya kupigia kura wamebaini kuwa viongozi wa Chadema na vijana wao wamekuwa wakileta vurugu katika kila kituo ili zoezi hilo lisiweze kufanikiwa.

“Tumeweka ulinzi kila kituo na hiyo itakuwa ikifanyika katika kata zote za Jiji la Arusha kwani hiyo itasaidia kupata wakazi halisi wa eneo husika na sio mamluki,” alisema Mutu

Mwandosya Atoa Mpya..Amtaka Lowassa Amuunge MKONO yeye Mbio za Urais ili Mambo yaishe Mapema

$
0
0

WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais, Kazi Maalumu, Profesa Mark Mwandosya amemuomba mgombea mwenzake katika kinyang’anyiro cha kutafuta ridhaa ya kuteuliwa kuwa mgombea kupitia CCM, Edward Lowassa asisite kumuunga mkono kama walivyofanya watangaza nia wengine ili mambo yaishe mapema.

Aidha, amewaonya wanaotishia kukihama chama endapo hawatapitishwa, akisema huo ni upuuzi na pia vitisho kwa Mwenyekiti wa Chama na wanaCCM kwa ujumla, hivyo wanaojiona wao ni maarufu kuliko chama wanajidanganya.

Mwandosya alitoa kauli hiyo mwishoni mwa wiki wilayani Mbozi alipokuwa akizungumza na wanaCCM waliomdhamini katika mbio zake za urais, pamoja na wanachama wengine waliojitokeza katika Ofisi za CCM Wilaya.

Mgombea huyo alisema amefarijika kusikia anaungwa mkono na wagombea wenzake, Waziri Mkuu, Mizengo Pinda na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Benard Membe pamoja na kupata taarifa za Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Stephen Wassira naye kusema anamuunga mkono.

Alisema pamoja na kuungwa mkono na wenzake hao watatu, anamuomba pia Lowassa naye kumuunga mkono ili kuipunguzia kazi Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya CCM).
 
“Nimesikia Membe amesema hapa Mbeya asipopitishwa yeye basi atamuunga mkono Profesa Mwandosya, nikasikia tena na Waziri Mkuu akisema hata kama asipopitishwa yeye atafarijika kama Profesa Mwandosya atakuwa mgombea, nikasikia tena na Wassira naye kupitia kwa mtu wake wa karibu ataniunga mkono, sasa namuomba mwenzangu naye Edward au maarufu kama Edo naye aseme Profesa ndiyo wangu, ili kazi iishe na tuipunguzie kazi Halmashauri Kuu,” alisema Profesa na kushangiliwa.

Awali Profesa Mwandosya aliwaeleza wanachama hao kuwa mwaka huu wa uchaguzi ni mwaka mgumu sana kwa CCM na kuwataka wanachama kutofanya mchezo katika kujibu mapigo ya wapinzani.

“Watatuuliza kuhusu EPA, wataendelea kutuuliza kuhusu Richmond, watatuuliza kuhusu Escrow, kubwa zaidi watatuuliza kuhusu Vodacom ingawa hili halizungumzwi lakini linakuja, lazima tujitayarishe.

“Sasa nani huyo ataweza kutusafisha, wananchi wakimtazama watasema huyu atatusaidia na atajibu, kila ninakopita naambiwa na wananchi kuhusu ufisadi na rushwa vinatuumiza."

"Kama chama lazima tukabiliane na hilo na hapa hatumzungumzii mtu lazima kama chama tuyaeleze kwa wananchi. Nani atafanya hivyo wakubwa wanajua,” alisema Profesa.

Akizungumzia wanaotishia kuhama chama, alisema wanajidanganya kwani CCM ni maarufu zaidi ya mtu mmoja mmoja, akisema mtu pekee aliyewahi kuhama na kukitikisa chama alikuwa Augustine Mrema, Waziri wa zamani wa Mambo ya Ndani.

Zitto Awapiga Dongo CCM ..Adai Hawaaminiani wala Kuthaminiana Wenyewe kwa Wenyewe

$
0
0
Kiongozi wa Chama cha ACT-Wazalendo Zitto Kabwe, amesema utitiri wa wagombea urais kupitia CCM kunaonyesha dalili ya wao wenyewe kutoaminiana, kutothaminiana na kimepoteza hazina ya viongozi.

Aidha, alisema kazi ya urais ingekuwa inachukuliwa kwa uzito wagombea wa CCM wasingefikia 10 badala yake imeonekana nikazi nyepesi na imerahisishwa na CCM.

Kabwe alisema sifa 13 pekee za wagombeawa CCM ni nyepesi ndio maana kila mmoja anajiona anaweza kuwa kiongozi wa nchi.

Akizungumza jana mjini Sumbawanga mkoani Rukwa, Kabwe alisema moja ya sifa ya chama cha ACT-Wazalendo ni wagombea kufuata masharti kwa kutangaza mali na madeni ikiwamo kufuata miiko ya viongozi iliyotangazwa na Azimio la Tabora.

Kabwe aliwataja viongozi hao kuwa ni wa kitaifa wa chama, rais, mawaziri, wabunge na madiwani watakaotokana na chama hicho.

Aliongeza kuwa ili kubomoa mfumo wa kinyonyaji na kifisadi miongoni mwa viongozi, chama hicho kimeamua kurejesha miiko ya uongozi na kuishia ambayo imehusishwa kutokana na Azimio la Arusha.“Chama kinamtaka kiongozi katika uongozi wa umma asiwe mkurugenzi katika kampuni au shirika la umma, awe wazi na vyanzo vyake vya mapato, mali alizonazo kwa kuzingatia utaratibu wa sheria ya nchi na kanuni za mwenendo na maadili ya viongozi,” alisema Kabwe.

Pia, alisema kiongozi anatakiwa asiwe mfanyabiashara wa aina yoyote katika chama na serikali anapokuwa kwenye nafasi ya uongozi.

Alisema tangu wagombea hao waanze kutangaza nia hakuna mgombea urais aliyetamka neno miiko isipokuwa Samuel Sitta pekee, licha ya kuahidi kupambana narushwa pamoja na ufisadi.“Nitolee mfano nchi ya Canada, Uingereza, Marekani wana miiko lakini Tanzania tunageuza uongozi kuwa kichaka cha wezi kwa kutupa miiko pembeni,” alisema Kabwe.

Chanzo: NIPASHE

ALI KIBA Atangaza Vita na Mwanamuziki Diamond Platnumz

$
0
0

Brighton Masalu
VITA! Saa chache tu baada ya kutua kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA), Dar akitokea nchini Marekani kwa shughuli za kimuziki, staa wa Bongo Fleva, Ali Saleh Kiba ametangaza kile kinachotafsirika kuwa ni vita dhidi ya hasimu wake kwenye anga la muziki huo, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’, Ijumaa Wikienda lina ‘full’ stori.
 cdeaw3
TUJIUNGE ENEO LA TUKIO

Ali Kiba alitema cheche Alhamisi ya wiki iliyopita ndani ya Hoteli ya Sea Cliff, Masaki jijini Dar, kulikokuwa na uzinduzi wa kampeni ya kupinga vita ujangili, iliyoratibiwa na Wizara ya Maliasili na Utalii, huku akiwa ni mmoja wa mabalozi sanjari na mlimbwende wa zamani, Jacqueline Ntuyabaliwe Mengi ‘K-Lyin’.


USO KWA USO NA PAPARAZI

Baada ya shamrashamra za ‘event’ hiyo, haraka sana kama mshale wa Mmakonde, mwandishi wetu alimfuata Ali Kiba, lengo kuu likiwa ni kusikia chochote juu ya ushindi wa Tuzo za Kili ambapo alizoa tano binafsi na moja ya kushirikishwa.

Kiba alisema anaamini alistahili kushinda tuzo zote kwani vigezo na sifa anazo na amejiandaa kikamilifu kupambana na yeyote anayedhani kuwa ni mfalme wa muziki huo.

JINA LA DIAMOND LAMCHEFUA!

Katika mahojiano hayo, mwandishi wetu alimkumbusha Ali Kiba uwepo wa Diamond ambapo kwa haraka sana alimkata kauli mwandishi kwa kusonya na kuweka wazi kuwa miongoni mwa mambo ambayo humpa kichefuchefu, ni pamoja na kusikia jina la Diamond likitajwa mahali popote penye uwepo wake!

“Kaka, sitaki kabisa kulisikia jina hilo, linanipa kichefuchefu, unajua kwa kipindi ambacho nilikaa kimya, nilikuwa nausoma mchezo lakini hakuna aliyeweza kuchukua kiti changu na kuamua kurejea ulingoni kwa kishindo na kuanzia sasa hivi ni mapambano mwendo mdundo,” alisema  Kiba na kuongeza:

“Simaanishi kuwa hakuna msanii mzuri kama mimi, naomba nisieleweke vibaya, wapo lakini siyo huyo dogo (Diamond), muziki ni zaidi ya mbwembwe, niko kikazi na sasa nimedhamiria kweli, kama anaamini yuko fiti, kazi zitaweka wazi ukweli na si drama za kitoto.”

 VIPI KUHUSU YEYE NA WEMA?

Mwandishi wetu alitaka kujua kulikoni msanii huyo alimuweka Wema Sepetu kwenye ukurasa wake wa Instagram akimmwagia shukrani lukuki na si mtu mwingine?

“Wema amekuwa ni shabiki wangu wa siku nyingi mno, alianza kunipenda kupitia wimbo wangu wa Hands Across the World (kwenye Project ya One-Eight) na kuanzia hapo amekuwa akinipa sapoti kubwa sana, siwezi kukaa naye mbali eti kisa huyo jamaa (Diamond).

“Naamini kwa asilimia nyingi sana hata huu ushindi wangu wa tuzo, umechangiwa na sapoti yake pamoja na wadau wangu wengine,” alisema Kiba.

 AFUNGUKA KUHUSU VIDEO YA MWANA!

Pia, mwandishi wetu alimtaka staa huyo kufafanua madai ya kutoitendea haki video ya Wimbo wa Mwana, ambapo alisema, watu wengi walitarajia aifanye kulingana na mawazo yao ndiyo maana akaamua afanye vile anavyoaamini ingekuwa bora.

“Kila mtu alikuwa ameshatengeneza picha ya jinsi video ya wimbo itakavyokuwa, halafu sifanyi kazi kwa kushindana na mtu, ndiyo maana ilionekana tofauti na mawazo ya wengi, namalizia kwa kusema salamu zimfikie jamaa (Diamond) kuwa mapambano ndiyo kwanza yameanza,” alisema Kiba.

 DIAMOND ANASEMAJE?

Hadi tunakwenda mitamboni, jitihada za kumpata Diamond aweze kuzungumzia vita hiyo iliyofufuka upya hazikuzaa matunda kufuatia simu ya staa huyo aliyekuwa nchini Afrika Kusini kikazi, kuita bila majibu.

 TUJIKUMBUSHE

Kwa muda mrefu sasa, Kiba na Diamond wamekuwa wakiripotiwa kuwa na bifu la chini kwa chini linalotokana kugombania ufalme wa muziki Bongo.

Makongoro Nyerere Ametumwa na Nani Urais 2015?

$
0
0
Hakuna kipindi ambacho CCM imeingia katika Uchaguzi Mkuu ikiwa na makundi hatarishi na pia matatizo ya kiutawala kama uchaguzi Mkuu ujao.

Ujio wa Abdulrahman Kinana kama Katibu Mkuu kwa kiasi kikubwa umekichelewesha chama kumeguka vipande vipande kabla ya Uchaguzi Mkuu ujao.

Wataalam wa kisiasa wanaendelea kujiuliza maswali mengi kuhusu hatima ya makundi na uhasama unaorutubika kila siku ndani ya CCM.

Udhaifu wa viongozi wakuu wa chama umesababisha baadhi ya wanachama kufanya watakacho kwa kukiuka kanuni, maadili na taratibu za chama mpaka kufikia hatua ya kutaka kumuondolea Rais Kikwete kofia ya Mwenyekiti wa CCM-Taifa.

Kuibuka kwa Makongoro Nyerere katika kundi la wanachama ambao wanaomba kuteuliwa kuwa wagombea Urais wa Tanzania kumeufanya uwanja wa siasa ndani ya CCM kubadilika hasa ikichukuliwa kuwa, hakuna mwanaCCM ambaye alikuwa akiongea na kusikilizwa kwa makini na wanachama wa CCM kuhusu kile kilichokua kinaendelea ndani ya CCM.

Makongoro amewashambulia vikali baadhi ya watia nia kama Edward Lowassa, Mwigulu Nchemba na Stephen Wasira kama ndiyo baadhi ya wale wanaleta maradhi ndani ya CCM pamoja na kwamba CCM bado ni chama bora nchini.

Pamoja na mambo mengine, Makongoro aliwatuhumu kwa kuja na Ilani yao ya uchaguzi badala ya kusubiri Ilani ya CCM itakayopitishwa na Mkutano Mkuu wa CCM-Taifa.

Alisema ndani ya chama hicho kumekuibuka pia genge la watu wachache ambao utajiri wao ni wa shaka na umejijenga kwa fedha chafu.

“Ndani ya chama tawala wamekuwapo ‘vibaka’ wachache… unajua kibaka ni kibaka tu hata kama kapewa gari la Serikali lina bendera ya taifa mbele atabaki kuwa kibaka tu. Hawa ndiyo wanaotuvurugia chama na hawamheshimu Mwenyekiti wa chama, Rais Jakaya Kikwete’’, Makongoro alisema.

Makongoro ameamua kuchukua jukumu la viongozi wakuu wa CCM ili kupambana na makundi yanayohatarisha uwepo wa CCM katika uwanja wa siasa.

Sauti ya Makongoro ukiichunguza kwa makini ni kama sauti ya mtu aliaye nyikani!

Kwa sauti hii, ni nani amemtuma Makongoro ili kupambana na wanachama anaowaita ni vibaka wanaosababisha baadhi ya viongozi wa CCM kuishi maisha ya kusukumwa kwa upepo wa makundi yanayomilikiwa na watoa fedha.

Je, inawezekana sauti ya Makongoro ni sauti ya viongozi wakuu wa CCM?


Makongoro atauweza mfupa uliowashinda viongozi wakuu wa CCM?.

Sugu Amfikisha Mkewe Kortini..Kisa Kuvaa Nusu Utupu na Kupiga Picha za AIBU

$
0
0
KINDUMBWENDUMBWE! Mbunge wa Mbeya Mjini kwa ‘leseni’ ya Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Joseph Osmund Mbilinyi ‘Sugu’ amemfikisha kortini aliyekuwa mkewe,  Faiza Ally akitaka apewe mtoto wao, Shaa (2) ili amlee kwa vile mama yake huyo si mwadilifu.

Aliyekuwa mkewe na mbunge wa mbeya mjini Joseph Osmund Mbilinyi ‘Sugu’,  Faiza Ally akiwa katika pozi.

Ijumaa iliyopita, saa 2:00 asubuhi, Faiza alipanda kwenye kizimba cha Mahakama ya Mwanzo, Manzese/ Sinza iliyopo Sinza-Makaburini jijini Dar kwa ajili ya kukabiliana na madai hayo.

 Alieyekuwa mke wa mbunge wa mbeya mjini Joseph Mbilinyi "Sugu" akiingia mahakamani.

ZILIPO HASIRA ZA SUGU

Kwa mujibu wa chanzo chetu kilichomwaga ‘ubuyu’ huo, Mheshimiwa Sugu alifikia hatua hiyo baada ya kuchukizwa na tabia mbaya za mwanamke huyo hasa ya kuvaa nguo zinazomuacha nusu utupu na kupiga picha za aibu, akiamini kuwa, tabia hizo zinaweza kuathiri makuzi ya mtoto huyo.

Mnyetishaji huyo aliendelea kusema kuwa, kwa kipindi kirefu, Sugu amekuwa akimvumilia Faiza, lakini hivi karibuni uzalendo ulimshinda baada ya picha zake akiwa amevaa kigauni kifupi na makalio nje kusambaa mitandaoni.

PALIPOKOLEZEA HASIRA

Faiza alivaa kivazi hicho hivi karibuni kwenye hafla ya ugawaji wa Tuzo za Kili Music iliyofanyika Ukumbi wa Mlimani City, Dar.

 SUGU MBELE YA HAKIMU

Akizungumza mbele ya hakimu mfawidhi wa mahakama hiyo, Patrick Vaginga, Mheshimiwa Sugu alidai kuwa mbali na mzazi mwenzake huyo kuwa na tabia ya kuvaa nusu utupu pia ana mtindo wa kupiga picha zisizo na maadili na kuziweka mtandaoni yeye mwenyewe.

 Joseph Mbilinyi akionekana kwa mbali katika maeneo ya mahakama.

KUHUSU MTOTO

Sugu alikwenda mbele zaidi kwa kudai kwamba, pia mwanamke huyo amekuwa na tabia ya kumpiga picha mbaya mtoto wao na kuzimimina humohumo mitandaoni jambo ambalo alisema linamharibu mtoto huyo.

 FAIZA HANA PESA

Mbali na sababu hizo, pia Sugu aliongeza kuwa, Faiza hana kipato kizuri cha kuweza kumlea mtoto na mara kwa mara amekuwa akisafiri jambo ambalo husababisha mtoto huyo kutopata malezi ya mama kwa muda mrefu hivyo kuiomba mahakama impe haki yeye ya kuishi na mwanaye.

 FAIZA AJIBU MAPIGO

Naye Faiza akijibu mapigo katika utetezi wake alisema kuwa, Sugu hafai kumlea mtoto huyo kwa sababu naye ana tabia ya kusafiri kwa muda mrefu hivyo kuishi mbali na mtoto ambapo aliiomba mahakama hiyo isimruhusu baba mzazi huyo kuishi na mtoto kwa kuwa atamharibu.

KESI YAPIGWA KALENDA

Mheshimiwa Hakimu Vaginga akasema kwa vile kesi hiyo ndiyo imeanza kusikilizwa kwa mara ya kwanza aliiahirisha hadi baadaye mwezi huu ambapo hukumu itatolewa.

 SUGU NJIA YAKE, FAIZA NJIA YAKE

Ijumaa Wikienda lililokuwa mahakamani hapo, liliwashuhudia wazazi hao, kila mmoja akiondoka na njia yake.

KWA NINI FAIZA NI MKE WA SUGU?

Kwa sheria za Kitanzania, mwanamke na mwanaume wakiishi pamoja kwa zaidi ya miezi sita, hao tayari ni mke na mume kama ilivyokuwa kwa Faiza na Sugu ambao waliishi pamoja kwa zaidi ya miaka miwili.
GPL

Shilole:Sasa Namzalia Nuhu Mziwanda Mtoto

$
0
0
Chande Abdallah
Kutoka kwenye mtima! Staa wa Bongo Fleva, Zuwena Mohamed ‘Shilole’ amefungukia ishu ya kumbebea mimba mpenzi wake, Naftal Mlawa ‘Nuh Mziwanda’ ili kuwafunga midomo wanawake wa mjini ambao wanamzengea jamaa huyo.

Staa wa Bongo Fleva, Zuwena Mohamed ‘Shilole’ akiwa katika pozi na mpenzi wake Nuhu Mziwanda.

Akizungumza na Ijumaa Wikienda, Shilole alitiriria kuwa, kwa muda mrefu amekuwa akibanwa na kazi zake za muziki ambazo anafanya na mpenzi wake huyo kiasi kwamba hawakufikiria kuhusu kupata mtoto mapema.

“Kwa sasa nimepanga kumbebea mimba na kumzalia Nuh,” alisema Shilole au Shishi Baby.
GPL

Jack Patrick Akirudi, Vanessa Atakuwa na Nafasi Kwa Jux?

$
0
0
Super model ambaye yupo gerezani kwa sasa kutokana na ishu ya kukamatwa na madawa ya kulevyia nchini China Jack Patric .

Awali mwana dada huyo aliwahi kuwa na mahusiano yakimapenzi na mwanamuziki wa bongo fleva Juma Jux ,lakini baada ya mwanadada huyo kutupwa garezani kwa miaka kumi ,Jux ameamua kunzisha mahusiano na Vanessa Mdee  huku wakiwa wanaponda raha za  kufa  mtu. .

Awali jux alinukuliwa na kituo kimoja cha redio kuwa hatakama mpenzi wake Jack yupo jela ila bado atalilinda penzi lao mpaka akaamua kumtungia nyimbo ‘’Nitasubiri’’

Je, Jux ameamua kumsaliti Jack nakuwa na Vanessa au kaona soo kuwa na Jack kisa kapatwa na skendo hiyo??? Jack akitoka jela atakuwa ana nanafasi gani kwa jux au Vanessa atapigwa chini ???

Jack awalii aliwahi kuolewa na  mwanume afahamikaye kwa jina la  Fundikila lakini ndoa yao  ilivunjika kutokana na  mwana dada huyo kumsaliti mumewe kwa Jux hadi kupelekea kila mtu kushika time yake .

Je kwa hali ya kawaida Jux ameonyesha kutokuwa mvumilivu nakuvunja ahadi au yupo na Vanessa kwa short time ???

Funguka
Viewing all 104789 articles
Browse latest View live




Latest Images