Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104712 articles
Browse latest View live

LEMUTUZ Aelezea Sababu ya Kutosomeshwa na Baba yake Ambae Alishawahi Kuwa Waziri Mkuu wa Tanzania Mzee Malecela

$
0
0
William Malecela, maarufu kama Lemutuz Nation au "King of All Bongo Social Networks" kama anavyofahamika katika mitandao mbalimbali ya kijamii ameeleza sababu za yeye kutosomeshwa na baba yake mzazi.

Le Mutuz Nation ambaye ametumia muda mwingi kusoma na kuishi nchini Marekani na Belgium, ameweka bayana katika kipindi cha Mlimanidotcom cha Mlimani TV kuwa alijisomesha kwa kupitia fedha ambazo zilitokana na kazi mbalimbali ambazo alikuwa akifanya kama vile udereva wa mabasi makubwa huko jijini New York pamoja na kukaanga kuku.

Alipoulizwa kuhusu taarifa za yeye kujisomesha kupitia kuendesha malori na kukaanga kuku, Le Mutuz alisema “Liko sawasawa, unajua ni la ajabu Tanzania lakini si la ajabu nchi nyingine kwasababu mimi wakati nakua, tulikuwa kwenye siasa ya ujamaa kwa hiyo mambo mengi yalikuwa yamebana na mimi nilikuwa nataka ubaharia”

Alieleza kuwa sababu kuu ni kuwa yeye alitaka ubaharia lakini baba yake hakutaka yeye asome masomo hayo katika ngazi ya chuo kikuu, Lakini pia ameeleza kuwa baba yake ambaye ni Waziri mkuu wa zamani wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania hakumsomesha kwasababu kipindi yeye anakua ilikuwa ni kipindi cha ujamaa na mambo mengi yalikuwa yamebana hivyo baba yake asingeweza kumlipia kusoma nje ya nchi.

Pamoja na kueleza hayo, Lemutuz alizungumzia sababu za yeye kuliburuza gazeti la Kiu mahakamani na pia kwanini anapenda kupiga picha na wanawake na kuweka Instagram



Video ya Alikiba ‘Chekecha Cheketua’ yafikisha views zaidi ya laki 1 ndani ya saa 24

$
0
0
Video ya Alikiba ‘Chekecha Cheketua’ iliyokuwa ikisubiriwa kwa hamu na mashabiki wa muziki ndani na nje ya Tanzania imepata mapokezi mazuri toka ilipooneshwa kwa mara ya kwanza na Trace Urban.

Baada ya video hiyo iliyoongozwa na director Mnigeria, Meji Alabi na JM Films kuwekwa mtandao wa Youtube kwenye channel ya Alikiba, imepata views zaidi ya laki moja ndani ya saa 24.

Haya ni mafanikio kwa Alikiba ambaye kwa sasa yuko jijini Nairobi, Kenya akishiriki kwenye msimu mpya wa CokeStudio.

‘Chekecha Cheketua’ ni wimbo wa pili baada ya ‘Mwana’ kutoka kwa Alikiba akiwa chini ya ROCKSTAR4000.

Mwanamke Aliyefanya Kazi ya Umalaya Kwa Miaka 25 Aelezea Masaibu Aliyoyapitia Kwenye Kazi Hiyo

$
0
0
Brenda Myers-Powell alikua mtoto wakati alipoanza kufanya ukahaba katika miaka ya sabini. Alizaliwa eneo la Chicago, Marekani na mamake mzazi alifariki dunia akiwa na miezi sita pakee.
Hapo ilimlazimu kusalia na bibi yake. Aligundua baadaye kwamba mamake alikufa kutokana na ulevi wa kupindukia.Kwa sababu bibi yake alikua mfanyikazi wa ndani ilimlazimu Brenda kujipeleka shule na kurejea nyumbani wenyewe licha ya kwamba alikua kwenye chekechea.

Baadhi ya watu walimdhulumu kingono mtoto huyo wakati alipokua akitoka chekechea.
Mwanamama huyu alifanya ukahaba kwa miaka 15, wakati huu wote hakuwahi kujiingiza katika mihadarati. Lakini kutokana na mazingira magumu kwenye madanguro ya ukahaba, hakuwa na budi kuanza kutumia mihadarati ili kusahau maisha aliyokua akiishi.
Baadaya ya miaka 25 kama kahaba, siku moja alikutana na mteja ambaye alikua katili.Alimtupa nje ya gari lake huku likienda kwa muendo wa kasi. Brenda alipata majeraha mabaya kiasi cha kupelekwa hospitalini akiwa mahututi.

Lakini madaktari waliokua wakimhudumia walimdhihaki kwamba alipata alichotaka na kumsuta kwamba alikua kahadaa mteja ndiposa akapata adhabu. Hapo wakawaita polisi kumkamata.

Wateja wakaribia kahaba barabarani
Lakini kwa bahati nzuri daktari mmoja alizungumza na Brenda na kumshauri afike katika kituo cha huduma ya jamii maarufu kama Genesis House. Msimamizi wa kituo hiki alikua Bi Edwina Gateley raia wa Uingereza.

Ni katika kituo cha Genesis Brenda alipata maisha mapya na kuanza safari ya kupona machungu, adhabu na kero za ukahaba. Hakupata shinikizo za kuondoka hadi pale alipohakikisha maisha yake yalikua shwari.
Kwa sasa Brenda anawasaidia wanawake na wasichana wanaokimbia ukahaba. Aidha alijaaliwa kuwa na familia, mume na wanawe wawili wa kike. Ana pia wajukuu. Maisha yake ni kuwafundisha soka watoto na kuhakikisha wanaishi kwa maadili mema.

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Alhamisi Ya Tarehe 2 July 2015

$
0
0





























Habari  Zilizopo  Katika  Magazeti  Ya  Leo  Alhamisi  Ya  Tarehe  2 July  2015

Hii Nayo Mpya ..Watuhumiwa wa EPA Waachiwa Huru

$
0
0
MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu, imewaachia huru Kada wa CCM Rajabu Maranda na wenzake waliokuwa wanakabiliwa na kesi wizi wa Sh milioni 207 katika Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA) kutoka Benki Kuu ya Tanzania (BoT).

Jopo la mahakimu watatu likiongozwa na Hakimu John Utamwa, Ignas Kitusi na Eva Nkya liliwaachia washitakiwa hao baada ya upande wa Jamhuri kushindwa kuthibitisha mashitaka dhidi ya washitakiwa hao.

Mbali na Maranda washitakiwa wengine walioachiwa huru ni Farijala Hussein na waliokuwa wafanyakazi wa BoT, Ester Komu, Bosco Kimera na Imani Mwakosya.

Akisoma hukumu hiyo Hakimu Utamwa alisema washitakiwa waliokuwa wanakabiliwa na mashitaka manne kula njama, kughushi, kuwasilisha nyaraka za uongo BoT na wiziwa Sh milioni 207.2 wako huru kutokana na upande wa Jamhuri kushindwa kuthibitisha mashitaka hayo bila kuacha shaka kama inavyotakiwa kisheria.

Alisema upande wa Jamhuri umeshindwa kuithibitishia mahakama jinsi Maranda na Farijala walighushi makubaliano ya kukusanya deni kati ya Kampuni ya General Marketing ya India kwenda Kampuni ya Rashas (T) ya Tanzania.

Katika hukumu hiyo iliyosomwa bila Mwakosya kuwepo mahakamani, Hakimu Utamwa alisema upande wa Jamhuri wameshindwa kumleta mpelelezi wa kesi hiyo ili aweze kuithibitishia Mahakama saini ambazo zinadaiwa kuwepo katika makubaliano hayo hivyo udhaifu huo hauwezi kuwatia washitakiwa hatiani.

Aliongeza kuwa, upande wa Jamhuri ulishindwa kuthibitisha shitaka la kughushi, kwa hiyo shitaka la kuwasilisha nyaraka za uongo litakuwa limekufa,kwa sababu wameshindwa kuonesha kweli nyaraka ni za kughushi.

Aidha alisemwa wameshindwa kuonesha ni jinsi gani fedha hizo zilihamishwa kama wanavyodai kuwa mchakato huo ulifanikiwa kwa sababu Maranda na Farijala walitumia nyaraka za kughushi.

“Hakuna shahidi aliyeweza kutoa ushahidi ukaenda sawa na hati ya mashitaka iliyofunguliwa mahakamani hapo dhidi ya washitakiwa,” alisema Hakimu Utamwa.

Nyaraka zinazodaiwa kughushiwa ni hati za makubaliano ya kuhamishiwa deni kutoka Kampuni ya General Marketing ya India kwenda Kampuni ya Rashas (T) ya nchini Tanzania, ambazo walizutumia na kuiba fedha hizo.

Baada ya Hukumu hiyo, Farijala alirudishwa rumande kwa sababu anatumikia kifungo cha miaka miwili jela alichohukumiwa katika kesi nyingine na Maranda aliachiwa lakini bado ataendelea kwenda mahakamani kwa kuwa anakabiliwa na kesi nyingine.

Ndugu na marafiki waliokuwepo katika eneo hilo la mahakama walishukuru mahakama kutoa uamuzi wa haki na kusema kweli Mungu ametenda miujiza.

Diamond Kuwasha Moto Miss Kilimanjaro

$
0
0
Tareheh 24 julai 2015 miss Kilimanjaro inatarajiwa kufanyika katika ukumbi wa ”KILI HOME MOSHI”ambapo Daimond atawaburuudisha wageni watakao fika katika ukumbi huo .

Ofa Ofa Kutoka James Cosmetics..Je Unahitaji Kuwa na Umbo Zuri la Kuvutia, Nywele Ndefu, Makalio Makubwa ya Mviringo na Ngozi ya Kuvutia?

$
0
0
OFA! OFA! OFA JAMES COSMETIC CO.LTD inawatangazia ofa ya punguzo la bei kwa mwezi huu mtukufu kwa kila bidhaa
pia usisahau hizi ni bidhaa za mimea na matunda kutoka viwandani na zimedhibitishwa hazina kemikal zenye madhara 1) kutoa chunusi na madoa = 50,000

2)kushep hips na figure = 60,000

3) kuongeza unene na uzito wa mwili = 60,000

4) kupunguza unene na uzito wa mwili = 70,000


5) kuondoa kitambi na nyama za kiunoni kwa (1) mkanda wa kawaida = 70,000 (2) dawa ya kupaka = 60,000 (3) micro kumputer belt = 150,000

6) kuondoa mvi zisirudi tena = 80,000

7) kuongeza nguvu za kiume na maumbile kwa (1) jeli ya kupaka = 60,000 (2) kwa vidonge maalum = 70,000 (3) kwa hand some up (pump og) = 170,000

8) kusoftisha ngozi na kuifanya laini mwili mzima = 70,000
9) kuondoa michirizi na mipasuko mwilini = 60,000

10) kubana uke na kuleta ham ya tendo la ndoa = 60,000

11) kushep miguu kuwa chupa ya bia = 60,000

12) kuondoa makunyanzi yani ngozi ya uzee = 60,000

13) kurefusha nyele na kuzuia kukatika ovyo = 60,000
TUPO KARIAKOO MSIMBAZI POLICE PIA TUNATUMA MIZIGO MIKOA YOTE NA NJE PIA NA KWA DAR DELIVER WAPO NI BURE CALL 0653 074067. 0659 404750. 0752 923461.
NB hakikisha unapata bidhaa bora na njema kwa afya yako.

Wastara: Nimeamua Kumpa Bond Nafasi ya Kunioa, Mimi Bado Damu Changa Nikisema Siwezi Kuolewa Tena Najidanganya..Nimempa Bond Sharti Hili...

$
0
0
Wastara na Bond Mapenzini
Brighton Masalu

WASTARA Juma Issa Abeid amekiri kuzidiwa na hisia za kuwa na mwenza kutokana na ukweli kwamba damu yake bado changa, hivyo suala la kuolewa halikwepeki huku akimpa nafasi kubwa msanii mwenzake, Bond Bin Sinan endapo atakidhi vigezo na masharti.

Akifungulia ‘koki’ ya maneno mbele ya paparazi wetu kwa njia ya simu mwanzoni mwa wiki hii, Wastara ambaye kwa sasa yuko bize kusaka ubunge nyumbani kwao Morogoro Vijijini, alisema hawezi kudanganya kwamba ataishi bila kuwa na mume kwa kuwa amekamilika kimaumbile.
Wastara na Bond Katika Pozi

“Mimi ni mwanamke, nimekamilika tena nakula na ninashiba. Damu bado changa. Nikisema siwezi kuolewa, nitakuwa nadanganya. Nimekaa muda mrefu kwa sababu kila mwanaume anayenihitaji ananitamani tu.

“Bond namuona ni mwelewa. Lakini nimempa sharti la kutonigusa hadi siku ya ndoa. Kama atakidhi na hayo mengine ambayo ni siri yetu, niko tayari kuolewa naye,” alisema Wastara.
GPL

Watano wanashikiliwa na Polisi kutokana na wizi wa Milioni 200, uliotokea katika Benki ya NMB Mkuranga, Mmoja ni Polis Aliyokuwa Akilinda Bank Hiyo

$
0
0
Five people, including a National Microfinance Bank (NMB) employee, have been arrested following a recent bank robbery of more than TZS 200 million at the bank’s branch in Mkuranga district, Coast Region.

According to Coast Regional Police Commander (CP), Jafari Ibrahim, four of the arrested people are workers of a private security company that was responsible for transporting the money from NMB Bank House in Dar es Salaam to Mkuranga.

The police commander further said one of the apprehended persons, who is the NMB employee (names and position withheld), is still being interrogated by the police officers, as investigation continues.

Three bandits equipped with a Short Machine Gun (SMG) are said to have killed one police officer and left two injured on June 26, before taking off with more than TZS 200 million at NMB Bank Mkuranga branch.

The robbery took place a few minutes after the arrival of the cash delivery van from Dar es Salaam.

The murdered police officer was not on duty on the day of the event, but was on his way to the bank for a night shift before he met his death.

Two other people were injured in the scuffle and were rushed to the hospital. However, they have since been released from the hospital after getting better.

“I miss ugali a lot but I can’t cook it” admits Lupita Nyong’o

$
0
0
Oscar Award winning actress Lupita Nyong’o admitted that one of the things she misses most while away from Kenya is ugali, she also confessed that even though she owns a mwiko (wooden stirring spoon) she doesn’t know how to cook the popular dish.

Here is the excerpt from the interview with NTV’s Larry Madowo:
LARRY MADOWO: Do you miss living here? Is there anything you miss about Kenya?
LUPITA: I miss ugali a lot, because I also don’t know how to cook ugali.
LARRY: What do you mean you don’t know how to cook Ugali?
LUPITA: Yeah, I don’t know how to cook Ugali.
LARRY: That’s terrible.
LUPITA: I know it’s really, really bad. I have a mwiko but I don’t know how to cook ugali.

The actress is currently on a homecoming tour that will include art mentorship activities, as well as an awareness campaign on wildlife conservancy efforts in the Kenya.

Despite her love for ugali and the fact that Lupita can’t cook it, she does have more than enough money to hire the best cooks available!

Askofu: Serikali ya CCM ilikabidhiwa kwa mizimu wakati wa Uhuru na Nyerere

$
0
0
Katika kipindi cha Asubuhi cha cha jana ITV alialikwa Askofu wa kanisa Katoliki ambaye alinishangaza kwa jambo jipya.

Alisema wala tusishangae yanayo fanywa na serikali ya CCM ni matokeo ya Mwalimu Nyerere kwenda kwa mashehe fulani wa Bagamoyo ambao walifanya tambiko ili Nchi ipate uhuru chini ya mwalimu Nyerere kwa kibali cha mizimu.

Kusema ukweli hata mimi niliwahi kumsikia Mwalimu akisema hao wazee walimwambia aruke shimo moja lililo fanyizwa dawa kisha akaambiwa mkoloni hakuwezi.

Sasa kwa mjibu wa mtumishi huyo wa Mungu anasema hata Uhuru ulipo patikana nchi ili kuwa chini ya laana kubwa kiasi kila jitihada zilikuwa zikienda mrama daima.

Yeye ansema ameoteshwa juzi tu kuhusu mkasa huo na kuambiwa Watanzania wasipotubu tuta kuwa tuna shuhudia viongozi wetu wakifanya vituko.

Aliongeza kuwa tabia ya mtu aliye laaniwa inajulikana anakuwa haelewi anafanya nini.Mkimlaumu atakuwa ana washangaa ninyi.

Anasema madudu yote ya CCM mathalani kutoa nguzo za umeme toka mafinga kupelekaKenya na kisha kurudisha Nchini kwa kununua kwa fedha za kigeni ni jambo linalo weza kufanywa na waliolaaniwa tu.

Chanzo: ITV

Zitto Kabwe Atamba 'ACT Lazima Tushinde Majimbo yote 8 ya Kigoma'

$
0
0
Akizungumza na clouds TV, bwana Zito amesema Kigoma ndio base ya ACT hivyo ni lazima washinde majimbo yote ya Kigoma na kwamba yeyote anayetaka kushinda jimbo Kigoma lazima apitie ACT. Yeye binafsi anagombea Kigoma mjini kumtoa Serukamba. Amesema Lowasa hawezi kujiunga na ACT anaipenda sana CCM na pia ACT haitaki mtu anayechanganya biashara na siasa.

Source: Clouds Tv

Hofu ya Mtoto wa Zari the Lady Boss Kufia Tumboni yatanda

$
0
0
HABARI ya mjini kwa sasa ni mjadala mzito mitaani na kwenye mitandao ya kijamii kwamba, mpenzi wa sasa wa Mbongo-Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’, Zarinah Hassan ‘Zari The Boss Lady’ anaweza kumuua motto aliye tumboni kutokana na tabia yake ya kuvaa viatu vyenye visigino virefu (high hills) katika kipindi hiki cha ujauzito.

WALICHOKISEMA MASHABIKI

Baadhi ya mashabiki, hasa watoto wa mjini wanaosadikiwa kuwa na mapenzi makubwa na Miss Tanzania 2006 aliye pia nyota wa sinema za Kibongo, Wema Isaac Sepetu (Team Wema), ambaye aliwahi kuwa na uhusiano wa kimapenzi na Diamond, wamemnanga Zari wakisema kuvaa kwake high hills ‘kokoko’ kunaweza kumminya tumbo wakati wa kutembea hivyo kukifanya kitoto hicho kufia tumboni.

DOKTA AZUNGUMZA, AFAFANUA

Kufuatia madai hayo mazito, juzi Amani lilizungumza na daktari maarufu jijini Dar, Godfrey Chale ‘Dokta Chale’ ambaye alilazimika kueleza kuhusu madai hayo.

Amani: “Samahani dokta, tumelazimika kukutafuta kutokana na maneno yaliyosambaa kwa sasa hapa mjini. Diamond ana mpenzi wake ni mjamzito. Sasa pamoja na ujauzito wake, anavaa viatu virefu.

“Kwa hiyo wanamnanga kwamba anaweza kukiua kitoto kilichopo tumboni kwa sababu anapovaa viatu hivyo, misuli ya

miguu inakaza na anabana tumbo. Kuna ukweli?”

Dokta: “Kwanza kabisa siyo kweli. Mwanamke anapovaa viatu virefu wakati wa ujauzito hakusababishi mtoto tumboni kufa.

“Ila, inashauriwa wajawazito

wasiwe wanavaa viatu virefu kwa sababu, wanapovaa, wanatanua misuli na kujiongezea uzito. Kwa hiyo inakuwa kama mtu aliyebeba mzigo kichwani huku akiwa na mimba.”

ATAJA MAGONJWA YANAYOMKABILI ZARI

Dokta Chale aliendelea kuweka wazi kuwa, mjamzito anapopendelea kuvaa viatu virefu, akishajifungua na mwili ukapoa, atakabiliwa na magonjwa manne.

“Kwanza ataugua miguu. Pili, atasumbuliwa na matatizo kwenye visigino. Tatu atapata matatizo ya magoti na nne ataugua mgongo. Ndiyo maana unaweza kukuta mwanamke anakuwa mrembo, miguu mizuri lakini kama alikuwa akibeba mizigo au kuvaa viatu virefu wakati wa mimba, miguu inaota nyama kwa nyuma ‘kiazi’.”

AONDOA HOFU

“Kwa hiyo, kama jamii ina hofu kwamba huyo mjamzito atamuua mtoto aliye tumboni kwa sababu ya kuvaa viatu virefu, hofu hiyo iondoke bali yazingatiwe hayo matatizo manne niliyoyasema,” alisema daktari huyo.

KWA WANAWAKE WOTE

“Lakini madhara haya si kwa wajawazito tu. Utafiti wa kitaalam umegundua kuwa, mwanamke ana uwezo wa kutembea wastani wa hatua 10,000 kwa siku. Kwa hiyo kuvaa viatu vyenye visigino virefu hufanya nguvu inayotumika kutembea hatua moja kuwa kubwa zaidi. Sasa utaona madhara ya kutembea hatua 10,000. Hii haijalishi anayetumia gari.

“Matokeo yake husababisha misuli na mishipa ya kwenye miguu, kiuno, mgongo na shingoni kufanya kazi kubwa ya kujaribu kusawazisha uzito. Kazi ambayo kwa kawaida hufanywa na visigino,” alimalizia dokta huyo.

DIAMOND ALIVYOSEMA

Amani, juzi lilimtafuta Diamond kwa njia ya mtandao wake wa WhatsApp na kumuuliza anachukuliaje madai ya ‘wabaya’ wa Zari:

“Hao wapo tu. Unajua dunia hii ukishakuwa maarufu kila jambo litakuandama. Lakini mimi naangalia mbele zaidi, nini nafanya na nini nitafanya. Kama maneno hata kwenye kanga yapo.”
GPL

Lowassa: "Nimechoka Kuitwa Fisadi .......Mwenye Ushahidi wa Rushwa dhidi Yangu Ajitokeze Ili Aeleze nilitoa lini, wapi na kwa nani."

$
0
0
Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa jana aliwataka wanaomhusisha na ufisadi kuacha mara moja kwa sababu hakuna hata chembe ya ukweli katika tuhuma hizo.


Lowassa, aliyeonekana kuzungumza kwa hisia, alisema hayo jana mara baada ya kurejesha fomu ya kuwania kuteuliwa na CCM kugombea urais katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 25.

Mbunge huyo wa Monduli alikuwa mmoja kati ya makada tisa waliorudisha fomu jana, ikiwa ni siku moja kabla ya kuisha kwa muda uliowekwa na chama hicho.

Wengine waliorejesha fomu jana ni Elidephonce Bilohe, Mwigulu Nchemba, Luhaga Mpina, Dk Hamisi Kigwangalla, Hassy Kitine, Mariki Marupu, Dk Asha Rose Migiro na Lazaro Nyalandu.

Hadi sasa, tayari wanachama 32 kati ya 42 wa CCM walioomba kuteuliwa na chama hicho kugombea urais wamerudisha fomu na kazi hiyo itahitimishwa leo.

Hakuna mtu ambaye amejitokeza hadharani kumtuhumu Lowassa kwa ufisadi, lakini tuhuma hizo zimekuwa zikisambaa kwenye mitandao ya kijamii, hasa kutokana na mbunge huyo wa Monduli kujiuzulu nafasi ya Waziri Mkuu mwaka 2008 baada ya kuibuka sakata la mkataba wa ufuaji umeme wa dharura baina ya Serikali na Kampuni ya Richmond RDC ya Marekani ambayo ilionekana haina uwezo.

Wakati huo, Lowassa alisema kwenye hotuba yake ya kujiuzulu kuwa amefanya uamuzi huo “ili kuonyesha dhana ya uwajibikaji, lakini kutokubaliana na utaratibu uliotumika wa kusema uongo ndani ya Bunge kwa kumsingizia mtu.”

Akizungumza jana kwenye ofisi za makao makuu ya CCM, Lowassa alirudia wito wake wa kutaka wenye ushahidi wa tuhuma hizo wajitokeze hadharani.

“Nataka nitumie fursa hii kuwataka wale wote ambao wamekuwa wakinituhumu kwa miaka kadhaa sasa na kunihusisha na suala zima la rushwa, nawaambia waache mara moja, kwani hakuna chembe hata ya ukweli wa maneno hayo,” alisema.

“Natoa changamoto kwa yeyote mwenye ushahidi wa tuhuma hizo za kipuuzi, autoe na aeleze kwa ushahidi rushwa yoyote inayonihusu, aseme nimechukua lini, kwa nani, kwa lipi na kiasi gani?”

Alisema yeye ni mwadilifu na anaposema atasimamia vita dhidi ya rushwa atafanya hivyo kwa vitendo bila kumuonea mtu na bila kumuonea haya yeyote.

“Ndugu wanachama wenzangu na wananchi kwa jumla, ni lazima sasa tufike mahali tuseme imetosha. Majungu yametosha, upotoshwaji umetosha, rushwa imetosha na kwa pamoja tunaweza kukomesha haya. Tutayakomesha kwa kusimamia ukweli, uadilifu, uaminifu na kutenda kwa haki,” alisema.

Alisema tuhuma hizo zimeendelea hata wakati wa kutafuta wadhamini kwa baadhi ya watu kuzieneza.

“Tumefanya kazi ya kutafuta na kuomba udhamini kwa uadilifu na umakini mkubwa. Na hapa nitumie nafasi hii pia kuwashukuru makatibu na viongozi wote wa Chama katika mikoa na wilaya kwa maandalizi mazuri katika kuifanikisha zoezi hili,” alisisitiza.

Alisema kuwa walifanya kazi yao vizuri kinyume kabisa cha vijimaneno vilivyoenezwa kwamba kulikuwa na matumizi ya fedha katika kuwatafuta wadhamni.

“Hivi kweli, unahongaje watu zaidi ya laki nane?” alihoji.

Lowassa ambaye pia ni mbunge wa Monduli, alisema tuhuma hizo zimekuwa zikitolewa na watu ambao wamekosa hoja na zinatolewa bila ushahidi wowote.

Alisema akifanikiwa kushika wadhifa wa urais, ataendesha nchi kwa kufuata katiba na sheria.

Kuhusu safari ya kusaka wadhamini, Lowassa aliwashukuru wana-CCM waliomdhamini na kwamba walijitokeza kwa wingi jambo ambalo limempa picha ya kuungwa mkono na kukubalika.

Alisema wanachama waliojitokeza kumdhamini walifanya hivyo kwa utashi wao na bila kishawishi chochote cha fedha au fadhila nyingine yoyote.

Alisema kuwa udhamini alioupata ni kielelezo cha vitendo kwamba wapo naye katika Safari ya Matumaini.

“Nina matumaini na imani kubwa kwamba mtaendelea kuniunga mkono ndani ya Chamna chetu ili kwa pamoja na mshikamano ndani ya Chama niweze kuteuliwa kugombea kiti cha urais,” alisema.

Lowassa alisema: “Kwa mafanikio haya ya hatua ya awali nina imani kwamba ni ishara njema kueleke hatua zilizobakia na uweza wake Mwenyezi Mungu Mungu, na kwa ushirikiano wenu kwa pamoja tutalivuka daraja ili hatimaye niwatumikie kwa utumishi uliotukuka nikiwa Rais wa Awamu ya Tano.”

Aliongeza kuwa: “Nina shauku kubwa ya kuunganisha nguvu na uwezo ya kila Mtanzania katika kupambana na umasikini wa nchi hii. Umasikini wa watu wetu siyo amri ya Mwenyenzi Mungu. Nina imani kabisa kwa pamoja tunaweza kutumia rasilimali tulizo nazo kwa bidii, maarifa na ufanisi zaidi ili kutokomeza umasikini huu.”

Ukumbi wa Whitehouse, jana ulijaa wana-CCM ambao walifika kushuhudia Lowassa akirudisha fomu tofauti na idadi iliyowahi kutokea kwa wagombea wengine kadhaa waliomtangulia.

Hali hiyo ilisababisha foleni kwenye Barabara ya Mtaa wa Kuu unaopita mbele ya ofisi za CCM, na kusababisha usumbufu kwa wapita njia.

Lowassa alifika akiwa ameongozana na mwanasiasa mkongwe nchini, Kingunge Ngombale Mwiru na wenyeviti wa chama hicho wa mikoa kadhaa pamoja na wabunge.

Wabunge hao ni Andrew Chenge (Bariadi Magharibi), Peter Serukamba (Kigoma Mjini), Diana Chilolo (Viti Maalumu), Profesa Juma Kapuya (Urambo Magharibi), Mary Chitanda (Viti Maalumu), Naibu Waziri wa Kazi na Ajira, Dk Makongoro Mahanga na Mary Mwanjelwa (Viti Maalumu).

Baadhi ya wenyeviti wa CCM wa mikoa waliomsindikiza ni Jesca Sambatavangu kutoka Iringa, Ramadhan Madabida (Dar es Salaam), Khamis Mgeja (Shinyanga), Mgana Msindai (Singida) na Joseph Msukuma (Geita).

Chris Brown Akimbilia Mahakamani, Mama wa Mtoto wake Anataka zaidi ya Milion 30 Kwa Mwezi ya Matunzo ya Mtoto wao

$
0
0
Chris Brown who has been spending so much time with his daughter Royalty, says he has had it with his baby mama Nia Guzman's child support and custody demands, so he's asking a judge to intervene.

Chris and Nia have been at war over 1-year-old Royalty for a long time now. She's demanding $15,000 a month in child support, but Chris Brown doesn't think it is a fair amount.

Due to this reason, he has filed legal documents in Houston to establish paternity of baby Royalty. That will give him the right to fight Nia over support and custody.

Chis who has been paying Nia $2,500  per month, believes it is a fair amount. If he ascertains that he is Royalty's father, he will then go to court to file for custody and a fair amount for child support to Nia.
He says Nia has been denying him the right to see his daughter, so he wants a judge to get involved and set guidelines for both of them

Makongoro: Lowassa sikumuona Vita ya Kagera, Labda alikuja baada ya vita kuburudisha wanajeshi

$
0
0
CHARLES Makongoro Nyerere (CMN) ni miongoni mwa wanachama wa CCM waliotangaza nia ya kutaka kuchaguliwa kuwania urais kupitia chama hicho mwaka huu. Raia Mwema lilifanya naye mahojiano wiki hii nyumbani kwake jijini Dar es Salaam. Endelea

-RAIA MWEMA: Kwanini wana CCM wanatakiwa wakuchague wewe uwe mgombea wao na si mwingine miongoni mwa wenzako 41 waliojitokeza kuwania nafasi hiyo?

MAKONGORO: Mimi si mwizi, wala mla rushwa. Nina uzoefu wa kutosha na nakijua chama changu. Pia ni mtu ambaye napenda kufuata utaratibu. CCM sasa inahitaji mtu wa namna hiyo.

-RAIA MWEMA: Kwanini unadhani uadilifu ndiyo sifa kuu ya Rais ajaye wa Tanzania?

MAKONGORO: Naamini kuwa ni mtu mwadilifu pekee ndiye ambaye ataisaidia nchi yetu kuondokana na matatizo tuliyonayo. Ufisadi, wizi wa mali ya umma na matatizo yote tuliyonayo yataondoka endapo tutampata kiongozi ambaye ni muadilifu.
Kinachotakiwa ni kwa chama kujisafisha chenyewe kwanza. CCM ikiwa safi, serikali itakuwa safi tu. Lakini serikali haiwezi kuacha kuwa ya kifisadi wakati chama chetu kina mafisadi na tunawavumilia.

-RAIA MWEMA: Ina maana kama utafanikiwa kuwa Rais na hatimaye Mwenyekiti wa CCM unaweza kuwafukuza wanachama wote wenye tuhuma za ufisadi?

MAKONGORO: Hapana, siwezi kumfukuza mwanachama kutoka CCM. Tunachoweza kufanya ni kuwatoa kutoka katika nafasi zao za uongozi. Nitakupa mifano miwili kueleza hili.

Kwa mfano wewe ni Mwislamu. Dini yako inataka uwe unaswali swala tano kwa siku. Sasa pale msikitini kwako una Imamu ambaye kwa siku anahudhuria swala moja au asihudhurie kabisa. Lakini kila siku unaambiwa anaonekana klabu ya pombe akinywa.
Sasa huyu imamu dawa yake si kumvua Uislamu wake. Unachofanya ni kumtoa kwenye uimamu na kumpa mtu mwingine ambaye hatawakwaza.

Kama wewe ni Mkristo na una Paroko ambaye kila kukicha ana kashfa za ngono na wake za watu ingawa hajawahi kukutwa huyo si paroko. Sasa ikitokea siku akanusurika kufumaniwa hadi akaacha mavazi yake ya uparoko kule Guest House lakini akachoropoka bila kukamatwa; huyo humvui Ukristo wake. Unachofanya ni kumtoa kwenye Uparoko wake.

Chama ni imani kama zilivyo dini. Huwezi kumwondoa mtu kwenye chama lakini unaweza kumwondoa kwenye nafasi za uongozi. Kwa kifupi, kuna maparoko na maimamu wa aina hiyo ndani ya CCM ambao ni lazima kuwaondoa kwenye nafasi zao kama kweli tunaitakia mema nchi yetu.

-RAIA MWEMA: Unasema chama ni imani lakini wewe uliondoka CCM na kuhamia NCCR Mageuzi kwenye miaka ya 1990. Ilikuaje ukahama chama chako?

MAKONGORO: Mojawapo ya matatizo ya chama chetu ambayo ni lazima Rais ajaye apambane nayo ni ukweli kwamba kuna majimbo ya uchaguzi hapa Tanzania ambayo kama mtu hutoi rushwa huwezi kupita.

Arusha ni mojawapo ya maeneo hayo. Yaani kama hula hela sahau kuhusu kuchaguliwa. Utafanyiwa mizengwe na viongozi wala rushwa hadi mwenyewe utachoka na kukata tamaa.

Mimi mwaka ule wa 1995 nilikumbwa na tatizo hilo. Nilitaka ubunge pale Arusha lakini mtandao wa rushwa ulikuwa ukiniwekea vikwazo. Sasa wazee wawili wa pale; mmoja amefariki dunia na mwingine yuko hai, wakanishauri kuwa kwa vile wananchi wananitaka na shida yao ni kiongozi mzuri, nihamie kwenye chama kingine. Ndiyo nikaenda NCCR Mageuzi na nikapata ubunge.

Haya ndiyo mambo ambayo yamenifanya niingie kwenye kinyang’anyiro kwa sababu hali inazidi kuwa mbaya. Kama hali ikiachwa hivi basi hata kwenye urais atakayeshinda atakuwa ni mla rushwa tu na nchi itakwenda vibaya sana.

-RAIA MWEMA: Kuna taarifa kwamba Rais mstaafu, Benjamin Mkapa, aliwahi kutaka kukuteua kuwa mbunge wakati akiwa Rais lakini wewe ulikataa. Kuna ukweli gani katika hili?

MAKONGORO: Katika watu ambao nawaheshimu sana kama viongozi hapa nchini, Mzee Mkapa ni mmoja wao. Aliikuta nchi ikiwa na hali mbaya sana lakini akaicha pazuri. Aliikuta inanuka madeni lakini akaondoka akiiacha na akiba kubwa ya fedha za kigeni.

Sasa miezi 18 kabla hajamaliza urais wake, aliniambia anataka kuniteua kuwa mbunge. Ni kweli kuwa nilikataa nafasi hiyo. Nilikataa kwa sababu ingeonekana anampendelea mtoto wa Nyerere. Ingeonekana kama anatoa zawadi. Na pengine ingeweza kujenga picha kuwa nimebebwa.

Nilikataa kwa sababu sikutaka mtu ambaye ninamuheshimu sana anyooshewe vidole kwa ajili yangu. Nilimueleza sababu zangu na nashukuru mzee yule alinielewa vizuri.

-RAIA MWEMA: Ni kweli kwamba baba yako, Mwalimu Julius Nyerere, hakujua kwamba uko vitani Uganda wakati wa Vita ya Kagera hadi baada ya vita kumalizika?

MAKONGORO: Ni kweli. Unajua mimi nilikwenda vitani nikiwa na umri wa miaka 18 tu ambao ndiyo ulikuwa umri mdogo zaidi kuruhusiwa kwenda vitani wakati huo.

Wakati vita inaanza mimi nilikuwa kwenye mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) kwenye Operesheni iliyojulikana kama Chakaza. Wale waliokuwa JKT walipatiwa mafunzo kidogo na kisha kupelekwa vitani.

Mimi pia nikaenda lakini sikumwambia baba. Ulikuwa ni uamuzi wangu binafsi. Kuna kaka zangu walikuwa jeshini tayari wakati huo lakini mimi nilikuwa mdogo sana.

Baba alikuwa na mambo mengi ya kufanya wakati wa vita na nadhani alijua naendelea na JKT. Kwa bahati nzuri pale nyumbani Msasani kulikuwa na simu na baada ya vita askari tulikuwa tukirusiwa kupiga simu nyumbani.

Sasa nikaanza utaratibu wa kupiga simu nyumbani mara kwa mara kila ilipofika saa kumi jioni. Baba alikuwa na utaratibu wa kurudi nyumbani saa tisa na akirudi moja kwa moja anakwenda mezani ale chakula.

Baada ya muda akabaini kuwa kila saa kumi wadogo zangu wakisikia tu simu wanakimbilia ilipo kwenda kusikiliza. Siku moja akawauliza, mbona mnakimbilia simu kila inapofika saa kumi na saa nyingine hamkimbilii?

Ndiyo wakamwambia tunaongea na kaka Mako (Makongoro). Akashangaa, akawaambia mnaongea naye kutoka wapi? Wakamwambia yuko Uganda. Nalisikia alishtuka sana na moja kwa moja akaja kwenye simu.

Mara nikasikia sauti ya Mwalimu ikiuliza Uko wapi Makongoro? Nikamwambia niko vitani Uganda? Akaniuliza uliendajeendaje? Nikamuuliza kwani vijana wenzangu kama mimi waliendajeendaje?

Basi, nikasikia anapumua na akaanza kuniuliza kuhusu habari za Uganda na mambo mengine. Nilikuwa sijawasiliana na baba yangu kwa muda wa miaka miwili tangu kuanza kwa vita.

-RAIA MWEMA: Mmoja wa washindani wako kwenye kinyang’anyiro hiki cha kuwania urais, Edward Lowassa, amewahi kuhadithia namna alivyoshuhudia watu wakifa vitani wakati wa vita hiyo. Je, mliwahi kukutana mkiwa Uganda?

MAKONGORO: Sikumbuki kukutana na Lowassa wakati wa Vita ya Uganda. Lakini kulikuwa na askari wengi na inawezekana nilipokuwa mimi yeye hakuwepo. Siwezi kujua askari wote waliopigana vita ile.

Baada ya vita kumalizika, wasanii wengi kama vile Zahir Ally Zorro walikuja Uganda kututumbuiza lakini Lowassa pia sikumuona. Nasikia yeye alisomea sanaa Chuo Kikuu labda alikuja wakati huo lakini pia sikumuona.

Zorro na marehemu Kapteni John Komba niliwaona wakati ule. Lakini Lowassa sikumbuki kumuona. Labda alipigana mji mwingine au alikuja na wasanii kutumbuiza baada ya vita, lakini mimi sikumbuki kumuona.

-RAIA MWEMA: Washindani wako wanadai kuwa wewe hufai kupewa urais kwa sababu ni mlevi na unapenda kunywa pombe. Unazungumziaje shutuma hizi?

MAKONGORO: Mimi pombe nakunywa lakini hilo la kusema kwamba mimi ni mlevi halipo. Mimi si mlevi. Wapo wapinzani wangu ambao ni walevi kiasi kwamba pombe zimeharibu afya zao na sasa wanaumwa.

Wanaumwa kwa sababu ya kunywa pombe. Mimi kama unavyoniona niko fiti na sina tatizo lolote la kiafya. Sasa wale ambao ulevi umewasababishia matatizo hawasemwi na kibao kinageuzwa kwangu. Hiki ni kichekesho kwelikweli.

-RAIA MWEMA: Kwa hiyo uko tayari kwenda kupimwa afya ili uthibitishe utimamu wa afya yako kama alivyopendekeza mgombea mmoja kwamba wagombea wote mpimwe afya zenu?

MAKONGORO: Tupimwe afya kwani tunataka kwenda kuchezea Real Madrid au Manchester United? Wachezaji wanaotaka kwenda kucheza mpira ndiyo wanapimwa afya zao lakini sijasikia popote watu wanaotaka urais wanaenda kupima afya.

Kwani Watanzania hawawezi kuangalia tu wenyewe na wakajua huyu ana afya njema na yule hana?

-RAIA MWEMA: Una wito gani kwa wana CCM wenzako kuelekea kuchagua mgombea urais kupitia chama chenu kwenye Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu?

MAKONGORO: Mimi nasema wana CCM wanatakiwa watutendee haki wagombea, chama chao na taifa lao. Kwenye uchaguzi huu, CCM inaweza kuamua kufanya mabadiliko chanya au hasi.

Wakichagua mtu ambaye dunia nzima inajua ni mwizi, wajue kwamba Watanzania watawaona na dunia pia itawaona pia.

Wana CCM wasibabaike na kauli za vitisho zinazotolewa na baadhi ya wagombea kwamba wasipopitishwa wao, basi patachimbika.

Sasa nauliza, patachimbika kwani kuna madini gani yanayotafutwa? CCM imekuwa Mererani ambako wachimba madini wanachimba kutafuta Tanzanite?

Kama wana CCM watafanya makosa safari hii, wajue kwamba hawakuwa na wa kumlilia isipokuwa wao wenyewe.

Chanzo: Raia Mwema

Ray C : Naomba kuwatangazia kuwa natafuta mchumba wa kuishi naye milele! Atoa vigezo 10 vya mume amtakaye

$
0
0
Msanii wa muziki Rehema Chalamila aka Ray C amefungua mlango kwa mwanaume yoyote anayetaka kumuoa ajitokeze ilimradi awe na vigezo 10 ambavyo ameviainisha.


Kupitia ukurasa wake wa instagram Ray C ameandika:

“Habari zenu wapendwa wote dunia nzima!Leo na habari nzuri sana kwenu,Naomba kuwatangazia kuwa natafuta Mchumba wa kuishi nae milele!nataka niwe nae milele na nimzalie watoto wawili wa kike na wakiume!!!!

Ila naomba niwambie kabisa masharti

1.Awe mpole ili nikikasirika anibembeleze
2.Awe anapenda muvi za kihindi ili nikiwa na stress aniwekee nyimbo za kihindi maana ndio raha ya moyo wangu.
3.Asiwe muongeaji sana sababu huwa sipendi makelele.
4 Anipende na ubonge wangu huu asije akaanza kunambia baby anza mazoezi au dah baby zamani ulikuwa bomba au rudisha kiuno hapo hatutaelewana.
5.Awe ananipikia nikichoka maana navutiwa nikimuona mwanaume anapika.
6.Awe na Mimi muda wote maana na wivu sana ikiwezekana tufanye kazi ofisi moja au awe ofisi ijengwe hapo hapo nyumbani.
7.Awe mvumilivu maana nikiwa na hasira huwa naongea kwa sauti ya juu sana.
8.Asiwe na rafiki wengi,na akitaka kuonana nae na mi niwepo maana si mnajua wanaume tena wakikutana huwa wanashaurina mabaya.
9.Awe anajua nyimbo zangu zote ndio ntaamini kweli ananipenda.
10.Sharti la mwisho kabisa ambalo ni muhimu sana kwangu ni hili tuwe tunatumia simu moja na Namba moja, maana kanisani tunafundishwa kuwa ndoa maana yake tumeungana na kuwa kitu kimoja kwahiyo kama mume na mke tunalala pamoja kitanda kimoja na kuishi pamoja kwanini tusitumie simu moja!Sioni tatizo!

Kama una ndugu,jamaa.kaka,rafiki yuko single basi mjulishe tangazo hili huezi jua unaeza ukashangaa nimekuwa shemeji yako au wifi yako”.

Wema: Nachukizwa na ‘Artwork’ Ambazo Sina Taarifa Nazo

$
0
0
Nachukizwa sana pale napoona mtu kaenda kutengeneza Artwork ambayo mimi binafsi sina taarifa nayo... Nimeona Artwork yenye picha yangu niliovaa bazee la njano ikisema Wema Sepetu Vyiti maalum 2015 -2020... Kwanza kakosea neno Viti maana sio Vyiti... Naomba aliopost hio artwork aitoe kwa heshima na taadhima... Pale zitakapokuwa tayari za kwangu basi nadhani mtaanza kuiona kupitia ukurasa wangu ambao ni huu hapa... Ile picha kwanza ni picha ya zamani sana na pale ambapo wameweka rangi ya Green palikuwa Royal Blue... Watanzania muda utakapofika basi naamini nitatoa posters zenye kueleweka na sio hizi zinazosambazwa... Ahsanteni sana...

Wema Sepetu on Instagram

Aunt Ezekiel: Nitamuunga Mkono Wema Sepetu Katika Safari Yake ya Kugombea Ubunge

$
0
0
Diva  wa filamu Bongo ambaye kwa sasa ni mama wa mtoto mmoja anayetambulika kwa jina la Cookie, Aunt Ezekiel, amefungukia kuhakikisha anampa sapoti ya nguvu shosti wake, Wema Sepetu katika harakati zake za kuwania ubunge.

unt amesema kuwa pamoja na kwamba yeye hafahamu siasa hata kidogo na hatarajii kujiingiza huko, lakini anatambua Wema ameamua kutangaza nia ya kugombea, hivyo kama rafiki yake mkubwa atahakikisha anazunguka naye kila sehemu ili kumsaidia atimize ndoto zake za kuingia mjengoni na kuwatumikia wananchi wa Singida.

“Kama rafiki wa Wema nitahakikisha nampa sapoti ya nguvu rafiki yangu hadi aingie mjengoni, japo kuwa mimi binafsi sipendi siasa na sitaki kujiingiza huko,” amesema Aunt Ezekiel.

Wema ni mmoja kati ya wasanii waliojitokeza katika kinyang’anyiro cha kutangaza nia ya kugombea ubunge wa viti maalumu jimbo la Singida Mjini kwa tiketi ya CCM.

Angalia Video Kilichotokea Bungeni mpaka Bunge likaahirishwa leo July 02 2015

$
0
0
Kikao cha Bunge kilianza kama kawaida leo July 02 2015, baada ya kipindi cha maswali na majibu yaliyoulizwa kwa Mawaziri, Mbunge John Mnyika akaomba mwongozo.

“Tumekabidhiwa orodha ya shughuli za leo.. kimsingi imekiuka kanuni, uamuzi wa kuileta hii miswada mitatu kwa pamoja kama hati ya dharura umekiuka kabisa msingi wa makubaliano ya kwenye Semina ambapo Wabunge kwa kauli moja tulikataa Miswada hii isiletwe kwa hati ya dharura“


“Naomba Mwongozo, hili jambo linahitaji majibu sasa” >>> Mbunge John Mnyika.

Spika Makinda akaanza kutoa ufafanuzi kuhusu hiyo ishu >>> “Toa kwanza maneno ya kuniamrisha mimi cha kufanya… Hakuna mtu anayeweza kuniamrisha” >>> Anne Makinda.

Spika akaendelea >>> “Tumefanya mara nyingi sana wala sio leo tu, hakuna kanuni iliyovunjwa na sio mara ya kwanza kujadili kitu kinachofanana kwa pamoja”>>> Spika Anne Makinda.

Hakukuwa na suluhu ya hilo, Wabunge wa Upinzani wakagomea Mjadala huo kuendelea ikabidi Kikao cha Bunge kiahirishwe saa nne asubuhi. Angalia Video Hapa:
Viewing all 104712 articles
Browse latest View live




Latest Images