Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104698 articles
Browse latest View live

Mchezaji Ramadhani Singano Ashinda Kesi Dhidi ya Simba Kuhusu Mkataba Feki..Sasa Nimchezaji Huru

$
0
0
SHIRIKISHO la Soka Tanzania (TFF), leo limeamua kuwa, mchezaji Ramadhani Yahya Singano 'Messi' ni huru na sasa anaweza kujiunga na timu yoyote.

Taarifa kutoka kwenye kikao cha Kamati ya Sheria Maadili na Hadhi za Wachezaji ya TFF kilichofanyika leo, imesema kwamba Simba SC walishindwa kutekeleza baadhi ya vipengele vya Mkataba, hivyo wanapoteza haki za kummiliki mchezaji huyo.

Chini ya Mwenyekiti wake, Richard Sinamtwa, Kamati hiyo imejiridhisha Messi hakuwahi kupewa nyuma ya kuishi na Simba SC jambo ambalo ni kinyume cha Mkataba baina yake na klabu hiyo.
Simba SC iliwakilishwa na Mwenyekiti wake wa Kamati yake ya Usajili, Zacharia Hans Poppe na Mjumbe wa Kamati ya Utendaji, Collins Frisch wakati Messi alifika na Mwenyekiti wa Chama cha Wachezaji Tanzania (SPUTANZA), Mussa Kisoky.

Maamuzi haya ni faraja kwa Messi ambaye anahusishwa kwa kiasi kikubwa na kuhamia Azam FC. Messi aliyeibukia timu ya vijana ya Simba SC miaka minne iliyopita, hivi karibuni ameibua shutuma dhidi ya klabu yake hiyo kwamba imeghushi Mkataba wake. Messi anadai Mkataba wake halali ulikuwa unamalizika mwaka huu, na si huu wa sasa ambao inaelezwa utamalizika mwakani.

Lakini Simba SC imeendelea kusistiza mchezaji huyo alikuwa ana Mkataba wa miaka mitatu. Awali, Sekretarieti ya TFF, chini ya Katibu wake, Selestine Mwesigwa ilizikutanisha pande zote mbili, mchezaji na Simba SC na kuamuru waketi chini na kutayarisha Mkataba mpya baada ya kuona huu wa sasa una mushkeli. Hata hivyo, Messi akakataa na kuamua kulihamishaia suala hilo Kamati ya Sheria ambayo leo imempa kile alichotaka ‘kuwa mchezaji huru’.

Safari FIFA?; Hans Poppe amesema kwamba watakwenda mbele kusaka haki zao

Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Simba SC, Hans Poppe amesema kuwa, baada ya matokeo hayo, wanakwenda kukutana ili kujua hatua zaidi za kuchukua, lakini dhahiri hawataishia hapo.
“Tuliwasilisha ushahidi wote mbele ya Kamati, tumeonyesha mshahara wake ulikuwa kiasi gani na tumeonyesha kwa nini alikuwa anapewa laki moja (100,000) zaidi.

Ili akalipie kodi ya nyumba, lakini bado hatukueleweka. Tunaamini hapa si mwisho, vipo vyombo vingine ambavyo vitatupa haki yetu, tunakwenda kukutana kuangalia uwezekano wa kulipeleka suala hili huko,”amesema Kapteni huyo wa zamani wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ).

JUSTIN BIEBER Atupia Picha ya Uchi Mtandaoni, Yapata Likes 719,000 Ndani ya Lisaa Limoja

$
0
0
MWANAMUZIKI raia wa Canada asiyeishiwa vituko, Justin Bieber kwa mara nyingine ametengebeza vichwa vya habari mitandaoni baada ya kutupia picha yake ya utupu katika akaunti yake ya Instagram.

Staa huyo ameachia pia hiyo ikionyesha sehemu za makalio yake wakati akijiachia katika Kisiwa cha Bora Bora kilichopo nchini Ufaransa.

Ndani ya saa moja baada ya kutupia picha hiyo, tayari ilikuwa na 'likes' zaidi ya 719,000.

Diamond: Hakuna Msanii Ambaye Nimewahi Kumlipa Wala yeye Kunilipa Kufanya Collabo

$
0
0
Diamond Platnumz amesema kuwa ameshafanya collabo na wasanii A-list karibu wote wanaofanya vizuri Afrika, lakini hakuna hata mmoja ambaye amewahi kumlipa wala wao kumlipa kwaajili ya collabo hizo.

“Nimefanya collabo na wasanii tofauti tofauti, karibuni A-list wote ya wanaofanya vizuri Afrika nimeshafanya nao.” Alisema kupitia XXL ya Clouds Fm.

Ameongeza kuwa mwanzoni haikuwa rahisi kufanya nao kutokana na kwamba wengi walikuwa hawamfahamu tofauti na ilivyo sasa.

“Kiukweli sijawahi kufanya malipo ya mtu yoyote kufanya naye nyimbo. Mwanzoni wakati naanza kufanya ilikuwa kidogo tabu kwasababu mtu alikuwa hajafahamu anafanya nyimbo na nani, lakini sasa hivi wanafahamu kwamba…nikifanya nyimbo na Diamond, East Afrika mimi kwangu inakuwa kiurahisi nyimbo yangu, na upande wangu mimi inakuwa ni rahisi kwa West, kwahiyo tukichanganya inakuwa rahisi zaidi.

"Kwahiyo hakuna mtu ambaye nimeshawahi kumlipa wala yeye mimi kunilipa hii ni uongo sijawahi kufanya hivyo.”

Msichana Anayemzimikia Diamond Platnumz Kimapenzi Awaomba Watanzania Wamuuonge Mkono..Adai yeye ni Natural Kuliko Zari

$
0
0
Watanzania munisuport Mimi Tanzania mwenzenu...... uyo Mgandaa ni 360 watanzania wotee ni nduguu mali za watanzinia zitumiwee na wataniaa iwejee MTU from no where atuchukulie kijana wetuu mnajua Tanzania hairuhuruu urai wa nchi mbili what if diamond akiamua kufunga ndoa na zari Diamond akachukua Uraia wa South ili wamlee mtoto hamuoni atakua tumepoteza icon... muni support nimpate dai tuoanee atabakia kwetu..... nipigieni kura Mumtagg Diamond najua akiniona niko natural atanitongoza....By Baby_ake

Pia amepost picha hii na kuandika haya:
Mrs and mr D..... Msinitukanee eti mnasema nimechanganyikiwa.. yes nimechanganyikiwa kimapenzi you cant tell me nothing.. yaani MTU akinivunja moyo now ntamtukama matusii yanguoni sijawahi mtukana MTU but mnanilazimisha
Basi mwenzenuu Leo nimeota niko Kitanda kimoja na Diamond ..... haha nimeonja muogo wake wa jangombe  ni mtamu . .... yaani tume last 45 kiu yoote kaikata. . .. kushtuka ni ndoto but i hope. Itakua kweli. I LOVE you D
Team baby ake mpooooooooooooo?


WEMA SEPETU Agundulika na Gonjwa la Ajabu..Mwenye Adai Lamkosesha Raha

$
0
0

Musa Mateja
Habari mbaya ikufikie kuwa Mkurugenzi wa Kampuni ya Endless Fame Films Productions ambaye yupo kwenye harakati za kuwania Ubunge wa Viti Maalum kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM) mkoani Singida, Wema Isaac Sepetu amegundulika kuwa na gonjwa la ajabu linalomsababishia kukosa raha ambalo linakua kadiri siku zinavyosonga.

Staa wa filamu Bongo, Wema Isaac Sepetu.

Gonjwa hilo limegundulika hivi karibuni machoni mwa paparazi wetu baada ya kumuona mlimbwende huyo wa Tanzania mwaka 2006 akiwa na bonge la nundu nyuma ya shingo, jambo lililomfanya paparazi ashindwe kujizuia na kuamua kumuuliza Wema.

MIAKA 26 MWILINI
Bila kupepesa macho Wema alisema kuwa ‘uvimbe’ huo upo mwilini mwake kwa zaidi ya miaka 26 sasa na umekuwa ukiongezeka siku hadi siku.

Wema alilazimika kufunguka zaidi baada ya paparazi wetu kumuona sehemu hiyo ikiwa imemvimba bila kujua kama ni tatizo lake la miaka yote.

Sehemu ya shingo iliyoonekana kuvimba.

HATA MAMA YAKE?
Wema alitolea ufafanuzi jambo hilo kwa kusema kuwa huo si uvimbe bali ni nundu ambayo amekuwa nayo tangu mwaka mmoja baada ya kuzaliwa na hata mama yake mzazi, Miriam Sepetu pia yuko hivyo.“Huu siyo uvimbe mpya, ujue mimi niko hivi na hii nundu ipo siku nyingi, sema imekuwa ikiongezeka kadiri siku zinavyosonga.

LAMKOSESHA RAHA
“Kweli tatizo hili linanikosesha raha. Nimekuwa nikisuka nywele ndefu na mara nyingine mawigi yangu ni marefu hivyo watu huwa hawanigundui.“Nadhani hili ni tatizo la kifamilia maana mama yangu pia yuko hivihivi isipokuwa mimi linaonekana kuwa kubwa sana,” alisema Wema.

MTU WA KARIBU
Paparazi wetu aliendelea kuchimba kwa watu wa karibu wa Wema ili kujua kama ni kweli hiyo nundu ipo siku zote au alipata ajali, jambo ambalo lilikuwa hivyo kutokana na majibu ya Petit Man ambaye alisema kuwa wao hata hawamshangai tena Wema maana hiyo nundu ipo kitambo na kuna muda huwa wanamtania kwa kumuita jina la Kinundu.

“Haaa! Wewe ulikuwa hujui kama Wema ana nundu, mbona ipo siku nyingi tu, sema huwa anaifunika na nywele na ndiyo maana haionekani sana, muda mwingi watu wamekuwa hawaigundui kwa kuwa ipo nyuma ya shingo, labda ingekuwa mbele au pembeni nadhani kila mtu angekuwa anaiona,” alisema Petit Man.

DAKTARI AFAFANUA
Akizungumza na gazeti hili, daktari maarufu jijini Dar, Godfrey Chale ‘Dokta Chale’ alifafanua kwamba ugonjwa huo kitaalam unajulikana kwa jina la Lipoma na huwa ni mkusanyiko wa nyama ya mafuta kwa ndani hivyo ukubwa wake ukizidi huwa ni gumu.

“Uvimbe huo ukishakuwa na ugumu huo unaotokana na kuwa kubwa husababisha mishipa ya damu kugandamizwa, hali inayomsababisha mgonjwa kuumwa na kichwa kwa upande wa nyuma.
“Pia huaribu muonekano wa kawaida wa mtu,” alisema Dk. Chale na kuongeza:
“Inabidi Wema amuone daktari kwa vipimo na upasuaji ili kuondoa uvimbe huo.”

SIRI IMEFICHUKA: Baada ya Kuficha Ujauzito, Snura Adaiwa Kufunga Ndoa Kimya Kimya..Soma Hapa

$
0
0
Staa wa Bongo Fleva alieanzia uigizaji, Snura Mushi amedaiwa kufunga ndoa ya siri na mchumba wake wa siku nyingi ambaye pia ni mzazi mwenziye,DJ maarufu mjini Mbeya,Hunter.

Habari zinasema kuwa katika sherehe ya ndoa hiyo walialikwa watu wachache kutoka kwenye pande mbili za familia ya wanandoa hao na ilifungwa kwa siri jijini Dar.

Kupitia U heard na Soudy Brown amezungumza na Snura ambaye amekana kufunga ndoa,lakini alipoulizwa kama aliweza kuficha mimba hadi alipojifungua je? Hawezi kuficha kufunga ndoa?

‘’Jamani sijafunga ndoa kama nimefunga muulize mpenzi wangu Hunter au meneja wangu HK,’alisema Snura.

Hata hivyo Hunter alipoulizwa kuhusu suala hilo alijibu kwa ufupi kuwa hajafunga ndoa na Snura.

Cloudsfm.com

Mzazi Mwenza wa Nay wa Mitego SIWEMA Anaswa na Kidume Kingine Uganda..Walala Hotel Moja..Hana Habari na Mtoto wake Mchanga

$
0
0
Gladness Mallya
KABAANG! Zilipendwa wa staa wa Bongo Fleva, Emmanuel Elibariki ‘Nay wa Mitego’, Siwema Edson amezua gumzo la aina yake baada ya kunaswa na ‘kidume’ kingine nchini Uganda.

Zilipendwa wa staa wa Bongo Fleva, Emmanuel Elibariki ‘Nay wa Mitego’, Siwema Edson.

Kwa mujibu wa chanzo chetu makini kilichowafuatilia wawili hao hatua kwa hatua, mpango mzima ulianzia jijini Mwanza ambapo Siwema alionekana akiwa na mwanaume huyo (jina halikupatikana mara moja) wakipeana kampani utadhani ni wapenzi.

Chanzo hicho kilizidi kumwaga ubuyu kuwa, wawili hao walipanda basi la Friends jijini Mwanza ambapo Siwema na mwanaume huyo walikuwa beneti nje na ndani ya gari.

Kilieleza kuwa, wakiwa mpakani Mtukula wawili hao walikuwa wakipiga stori, kula chakula na vinywaji pamoja ambapo walipofika Kampala, Uganda walikatiza mitaani na kufikia kwenye Hoteli ya HBT.

“Nimesafiri na Siwema na mwanaume wake huyo kutoka Mwanza hadi Kampala yaani ni mahaba niue, kwani hata pochi alikuwa amebebewa na huyo mwanaume na kule walifikia hoteli ya HBT, nami nilikuwepo hapo kama siku nne hivi nikaondoka na kuwaacha, naona waliamua kwenda kupumzika huko,” kilisema chanzo hicho ambacho hata hivyo, kilishindwa kuthibitisha kama wawili hao walilala chumba kimoja.


Baada ya kuzinyaka habari hizi paparazi wetu alimtafuta Nay wa Mitego ambaye ni mzazi mwenzake na kumweleza kuhusu hilo ambapo alisema mwanamke huyo siyo mkewe hivyo anao uhuru wa kuishi vile anavyojisikia.

“Nimesikia hizo habari, mimi sidhani kama kuna tatizo kwa sababu kitu muhimu kwangu ilikuwa ni mtoto ambaye tayari ninaye, kwake imebaki stori, mawazo yangu hivi sasa ni jinsi ya kumlea mwanangu na si vinginevyo,” alisema.

Alipotafutwa Siwema ili kusikia anazungumziaje picha hizo zilizonyetishwa na chanzo chetu, simu yake haikuwa hewani. Jitihada zinaendelea.

Siwema na Nay wa Mitego walikuwa ni wapenzi wa muda mrefu na walijaaliwa kupata mtoto mmoja ambapo miezi kadhaa iliyopita walimwagana baada ya Nay wa Mitego kumfumania mwanadada huyo na mwanaume mwingine.

Diamond Asema Yuko Tayari Kufanya Collabo na Msanii Yeyote Tanzania Lakini Mwenye Vigezo Hivi

$
0
0
Diamond Platnumz amesema kuwa yuko tayari kufanya collabo na msanii yeyote wa Tanzania, ambaye atakuwa anakidhi vigezo vyake.

Muimbaji huyo wa ‘Nana’ ameyasema hayo baada ya kuulizwa kwanini hafanyi collabo nyingi na wasanii wa Tanzania.


  • “Mimi sina tatizo as long as nijue hiyo kazi unayotaka kufanya na mimi itafika wapi,” alisema Diamond kupitia Clouds E.



  • “umejipanga vipi project yako na umeiandaa vipi, kwasababu sitaki nifanye tu nyimbo mwisho wa siku halafu iishie tu ndani unaiskiliza wakati natumia muda kukaa kuandika kupoteza muda studio.“


Aliendelea kwa kujitolea mfano yeye anapofanya collabo na msanii wa nje, lengo kubwa huwa ni kujitangaza zaidi kule anakotoka msanii anayemshirikisha.


  • “Na ukiangalia kwa mfano kama nje nakuwa nafanya collabo na wasanii tofauti tofauti kwasababu inasaidia pia muziki wetu kutanua kiurahisi[…] Lakini haimaanishi kwamba sitaki kufanya collabo na wasanii wa Tanzania […] yaani unavyokuja kufanya collabo lazima ufanye kuonesha qualification za kufanya tufanye collabo.”

CCM Kumtangaza Mgombea wake Tarehe Hii.......Tukio Hilo Litarushwa Na Vituo Mbalimbali ya TV Live kwa masaa Sita

$
0
0
Juzi  tarehe 7 mwezi wa saba tumeanza vikao vya mchakato wa mkutano mkuu wa taifa wa CCM ambao unnategemewa pamoja na mambo mengine utapitisha ilani ya uchaguzi ya mwaka 2015-20 20.
 
Pia utateua mgombea wa urais wa jamhuri ya muungano wa tanzania kupitia CCM, na pia kutakuwa na kikao cha halmashauri kuu ambacho kitateua jina la mgombea wa urais kwa chama cha mapinduzi kwa upande wa Zanzibar.
 
Ratiba ya vikao
Leo tarehe 8 tunategemea kufanya kikao cha kamati ya usalama na maadili cha chama, ambacho kitakuwa chini ya mwenyekiti wa Taifa  Dk.Jakaya Mrisho Kikwete.

Tarehe 9 kichama kutakuwa na shughuli kuu mbili ya kwanza asubuhi, kutafanyika uzinduzi au ufunguzi wa ukumbi mpya wa chama cha mapinduzi na ofisi zake ambao upo njia ya kwenda chuo kikuu cha Dodoma bila shaka baadhi yenu mtakuwa mmeona, mwenyekiti wa chama Rais Kikwete alipokwenda kutembelea.

Kwahiyo ufunguzi wake utafanyika tarehe 9, majira ya asubuhi kabla mheshimiwa rais hajaenda kuvunja bunge, kama ratiba itabadilika tutawaambia lakini tarehe 9 tunahiyo shughuli ya kwanza baadaye mchana kutakuwa na kikao cha Kamati Kuu ya Halmashauri kuu ya Taifa ya chama cha mapinduzi ambayo nayo ni muendelezo wa vikao vya awali kuelekea mkutano mkuu.

Tarehe 10 tunategemea kuwa na kikao cha Halmashauri kuu ya chama cha Mapinduzi ambacho kikao hichi kitafanya mambo makubwa matatu ambacho kitafanya.
 
Kwanza kitateuwa jina la mgombea urais kwa upande wa Tanzania zanzibar, halmashauri kuu ya taifa kwa mujibu wa katiba ndio inayoteua jina la mgombea urais wa Zanzibar kwahiyo hiyo itakuwa ni kazi mojawapo itakayofanywa na Halmashauri kuu ya Taifa
 
Pili, watapitia pia ilani ya uchaguzi ya chama cha mapinduzi ambayo ndiyo itakayotumika kuombea kura na ndio itakayotumika kwa kipindi cha 2015-2020, na kutoka kwao hiyo ilani itapelekwa katika mkutano mkuu kwaajili ya kuhitimishwa.

Tatu, halmashauri kuu hii itapokea majina matano kutoka kamati kuu ambayo yatakuwa yameteuliwa na kamati kuu, tarehe 9 na hapo watafanya kazi ya kupiga kura kupata majina matatu ya wanachama wa CCM walioomba kupitishwa na chama cha mapinduzi kuwa wagombea wa nafasi ya urais kwa upande wa jamhuri ya muungano wa Tanzania.

Majina matano haya yatapigiwa kura kupata matatu na tarehe 11 ndio siku ya mkutano mkuu wa Taifa wa chama cha mapinduzi ambao una kazi kubwa mbili.
 
Moja ni kupitisha hiyo ilani ambayo itakuwa imepitishwa na halmashauri kuu ya Taifa na maandalizi ya ilani hiyo yamekamilika.
 
Tuliunda timu kama mnakumbuka tumewahi kuitangaza ipo chini ya Wasira imefanya kazi nzuri ya kutengeneza ilani nadhani safari hii tutakuwa na ilani nzuri sana ambayo itaendeleza mafanikio yaliyopatikana katika awamu zote zilizopita lakini pia itatupeleka sasa kwenye hatua kubwa zaidi ya maendeleo ya nchi yetu.

Pili, ni kupiga kura katika majina matatu yatakayowasilishwa katika mkutano mkuu ili kupata jina moja la mwanachama wa CCM ambaye ndiye atakuwa mgombea wa urais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania kupitia chama cha mapinduzi.
 
Tarehe 11 itakuwa ni siku ya mkutano mkuu na mkutano mkuu huu utakuwa wa siku moja,lakini mkutano mkuu huu utaoneshwa moja kwa moja kupitia vyombo mbalimbali vya habari hapa nchini.
 
Tv zote zitaonesha kuanzia ufunguzi ratiba ile mpaka wakati fulani halafu baadaye wakati wa matokeo na ufungaji wa mkutano karibia masaa sita au saba hivi tutauonesha moja kwa moja.

Ninachotaka tu ni kuwathibitishia watanzania tumejipanga vizuri,chama chetu tupo wamoja tunaamini tutamaliza vikao hivi salama, na tutatoka tukiwa na ushindi, tutatoka tukiwa na nguvu, tutatoka tukiwa wamoja na bila shaka vikao hivi vitajenga msingi wa kushinda uchaguzi kwa kishindo sana mwaka huu.

-Nape Nnauye,
Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi CCM.

CCM Ina Kashfa ya Escrow Tu, asema Msekwa...Atakaye Katwa Jina Anaruhusiwa Kuhama Chama

$
0
0

Makamu mwenyekiti mstaafu wa CCM, Pius Msekwa amesema kashfa ya uchotwaji fedha kwenye Akaunti ya Tegeta Escrow imekijengea chama hicho chuki kwa wananchi na hivyo kinahitaji mgombea anayekubalika ili kishinde kwenye Uchaguzi Mkuu wa Oktoba.

Msekwa, ambaye ni mmoja wa viongozi wa zamani wanaotarajiwa kutoa mapendekezo yatakayokuwa msingi wa kupata mgombea wa urais wa CCM, alisema hayo kwenye kipindi cha Dakika 45 kinachorushwa kila Jumatatu na Kituo cha Televisheni cha ITV.

CCM imeshaanza mchakato wa mwisho wa kumpata mgombea wa urais kwenye Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 25 kwa ajili ya kuwania kuongoza Serikali ya Awamu ya Tano na pia mrithi wa Jakaya Kikwete kwenye nafasi ya mwenyekiti wa chama hicho. Mchakato huo utakamilika Jumapili wiki hii wakati Mkutano Mkuu utakapochagua mgombea wa nafasi hiyo ya juu ya kisiasa nchini.

Akizungumza kwenye kipindi hicho, Msekwa alisema katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2010, ushindi wa mgombea urais wa CCM, Rais Kikwete, uliporomoka kutoka asilimia 82 hadi 61 kwa sababu kulikuwa na matukio mengi yaliyowafanya wananchi wajenge chuki dhidi ya chama hicho.

“Lakini uchaguzi wa mwaka huu, kuna jambo moja tu la escrow,” alisema Msekwa.

Msekwa, ambaye alikuwa Spika wa Bunge la Nane, alisema sakata la Akaunti ya Tegeta Escrow limejenga chuki na hasira mpya kwa wananchi, hivyo CCM lazima iwe na wagombea wanaokubalika katika jamii.

Msekwa alitoa ufafanuzi huo baada ya kuulizwa kama matukio ya aina mbalimbali yaliyotokea miaka ya nyuma yanaweza kuwa sababu ya wananchi kuwa na chuki na CCM, kukifanya chama hicho kuwa na wakati mgumu katika chaguzi mbalimbali.

“Hayo ni maamuzi ya wananchi. Mimi siwezi kutabiri chuki hiyo ni kubwa kiasi gani. Wakati ule chuki ilikuwa kubwa sana na tuliiona hata viongozi wa dini walikasirishwa sana. Hiyo ndiyo ilifanya CCM ipate ushindi wa asilimia 61,” alisema.

“Sasa hivi suala lililopo mbele yetu ni escrow tu, hivyo siwezi kupima ukubwa wake ukoje na itatupa ushindi kwa asilimia gani. Ila nina imani kuwa tutashinda lakini sijui ni asilimia ngapi maana inategemea ukubwa wa chuki dhidi ya CCM.”

Katika sakata hilo, zaidi ya Sh306 bilioni zilichotwa kutoka kwenye Akaunti ya Tegeta Escrow iliyokuwa Benki Kuu ya Tanzania (BoT) na fedha hizo zilionekana zikiingia kwenye akaunti za baadhi ya mawaziri, wabunge, majaji na watendaji waandamizi serikalini.

Sakata hilo lilimlazimu Rais Kikwete kumwengua Profesa Anna Tibaijuka katika wadhifa wa Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi huku Profesa Sospeter Muhongo, aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini sambamba na aliyekuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jaji Frederick Werema, wakilazimika kuachia ngazi.

Wizi wa mabilioni hayo uliwekwa wazi katika ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), ambayo iliibua mjadala mkubwa bungeni.


Kuhusu mchujo wa kumpata mgombea urais wa CCM mwaka huu, Msekwa alisema hauwezi kukigawa chama licha ya kuwapo kwa makundi mengi yanayowaunga mkono makada tofauti.

“Huwezi kuepuka makundi katika uchaguzi kwa sababu hakuna anayetoka nyumbani kwake peke yake na kwenda kutafuta uongozi. Lazima atakuwa na wanaomuunga mkono na muungaji mkono wa kwanza atakuwa mke wake,” alisema Msekwa.

Alisema kila mwanachama wa CCM anakula kiapo cha kuwa mwaminifu kwa chama, hivyo anayetafuta uongozi lazima atii uamuzi wa chama na kusisitiza huo ndiyo uaminifu. “Tunategemea wanachama wetu watatii kiapo chao. Hatuwafungi kamba shingoni. Ambaye ataona hakubaliani na uamuzi atatoka na wamewahi kutoka na waliobaki tukabaki,” alisema Msekwa.

Alisema uchaguzi wa mwaka 2010 wapo baadhi ya makada wa chama hicho walijiunga na vyama vya upinzani baada ya kutoswa katika kura za maoni za ubunge CCM.

Alisema CCM ni kama maji ya Mto Rufiji, akisisitiza kuwa huwezi kuchota maji yake katika ndoo na kujisifu kuwa umeyamaliza yote... “Maji yatabaki mengi tu. CCM kina mamilioni ya wanachama, wataondoka 10 au 20 lakini wengi watabaki.”

Jibu la Linah Baada ya Shabiki Kuuliza Uhusiano wake na Kaka yake Zari (Bosi Mutoto).

$
0
0
Kama wewe ni mtu wa stori za mastaa kutoka kwenye mitandao ya kijamii inawezekana ikawa imekufikia hii ya Linah kutajwa kuwa mapenzini na kaka yake Zari The Boss lady ambaye ni girlfriend wa Diamond.

Kwenye Exclusive Interview Linah ameongea na Millard Ayo alipotembelea studio za TZA na hilo swali kuulizwa na shabiki, tazama hii video hapa chini…

Baba yangu alinipa pesa ya kusokota dreads na kutoboa masikio – Sheria Ngowi

$
0
0
Mbunifu wa mavazi nchini, Sheria Ngowi amesema mafanikio aliyoyapata yametokana baba yake mzazi aliyemuunga mkono kwenye kila japo analolifanya.

“Baba yangu alikuwa ananipa uhuru wa kufanya kila kitu nilichokuwa nataka kufanya,” Ngowi ameuambia mtandao wa Dar City Center.

“Hata nilipotaka kuwa mbunifu wa mavazi alinipa support, pesa ya kusokota dreads na kutoboa masikio alinipa yeye.”

Producer Manecky na Diamond Platnumz Wamaliza Tofauti zao, Waamua Kufanya Kitu Hichi Pamoja

$
0
0
Mtayarishaji wa muziki wa AM records, Manecky na Diamond Platnumz wamemaliza tofauti zao.

Manecky ameiambia Bongo5 kuwa ameanza kurekodi tena na Diamond baada ya miaka takriban miwili ya kutofanya kazi pamoja.

“Unajua kuna mzingira fulani yalijitokeza kati yangu mimi na Diamond tukawa muda mrefu sana hatujaongea na kuonana na kufanya kitu,” mtayarishaji huyo ameiambia Bongo5.

“Unajua kuna time inafika kila mtu anagundua ana mapungufu yake, sasa mnapoamua kuachana na mambo hayo mnaachana nayo. Sasa mimi sioni kama kuna sababu ya kukaa tena chini na kumuangalia nani alikosea. Sasa hivi tunasonga kwenda mbele, sasa hivi tupo fresh ndio maana tumeshaanza kurekodi ngoma mpya na Nay wa Mitego ili kutengeneza kitu kizuri,” ameongeza Manecky.

Hata hivyo Manecky amesema bado anapata wakati mgumu kuitafuta chemistry yake na Diamond kwakuwa ni kipindi kirefu hawajafanya kazi pamoja.

“Sasa hivi napata wakati fulani mgumu, unajua tumekaa muda mrefu hatujaonana wala kuongea/ Utajikuta unafanya kazi kwa mazingira fulani ili upate kitu kizuri ili kazi iwe nzuri.”

Msanii H baba Kuichezea Toto African?, Maneno yake Nimekuwekea Hapa

$
0
0
Good news ninayotaka kukusogezea ni hii kutoka kwa msanii wa Bongo Fleva, H Baba ambaye ametangaza rasmi sasa hivi kurudi kwenye soka na kujiunga na timu ya Toto African.

‘Kupitia kwenye kipindi cha AMPLIFAYA cha Clouds FM july 7, 2015 alifunguka na kusema’Ni kweli kwamba mimi nina vipaji vingi sasa ubora wa vipaji ni kuvionesha kwasababu nilishawahi kucheza soka na hii ni timu ya nyumbani timu nyingi zilishawahi kunihitaji sema muda mwingi sana nilikua kwenye kazi zangu za muziki kwa hiyo kwasasa hivi najipanga kwa mambo mengi wasishangae nikafanya vitu tofauti’– H Baba

‘Hapana siwezi kuacha muziki siwezi kuacha mpira siwezi kuacha filamu ni vitu vyote ambayo ninavyovipenda na siwezi kuja kuviacha mimi umri wangu bado mdogo unaniruhusu kuingia kwenye soka kwasasa hivi mimi niko Toto African watu wajiandae tu wafahamu kuwa niko Toto ila bado tupo katika harakati kwamba tutakapokaa sawa kuzungumza yakifikia sasa maafikiano ila Yanga na Sima wajiandae’ – H baba

Msichana Anayempenda Diamond Platnumz Aja Tena Na Mpya Leo ..Adai Zari ni Mzee na Ajiamini pia ni Gogo Kitandani....

$
0
0
Msichana anayejiita Baby ake huku instagram anazidi rusha hisia zake kwa Diamond Platnumz..Sasa leo amekuja na mpya na kusema haya hapa chini kuhusu Zari ambae ndio mchumba wa Diamond Kwa sasa:

Nimeaminii kwelii uyu mwanamkee ni mzeee ajiamini.... etii kaona nimetangaza nia ya u Mrs Diamond kani block.... we demu ujiaminii live ni Rambo nini?... sasa ata ukiniblock bwanakoo ntampata tuu... namimi ntapikiwa na kubebewa mapochi... khaa kizuri kula na wenzio we kwanza sio mtz iweje ujimilikishe..... embu jiangalie unifikii ata nusuu uwoo weupe tuu.... kwanza mademu weupe sio ata watamu.... au waringia miguu... kwa mange alisema ni ugojwa.... au iyoo mimbaa..... sasa kama umembebea D mimba mie ntampa nyumaa tuone atamchagua nani.. unifii we we.... mie black beauty mi hasilia siweki mokope na situmii 360 siweki miywele.... bandia wala mikope kama wewe.... kwanza diamond upenda vitu asili.... mie mwepesi kitanda sioo wewe gogoo

Sijali mabaya mnayoyaonga kwangu Hata kama yatakuwa machungu na mazito kiasi gani,kumpenda mtu sio dhambi na wala sio kosa la jinai ila tu najua nachukiwa sababu nampenda mtu ambaye anapendwa na wengi sababu na jua miongoni kwa watu wanaonichukia na kunktusi kwa sababu ya D ndo hao hao ambao nafsi zao zinawauma na Kukereka pale ninapoeleza hisia zangu ila mimi hayo yote hayanitishi sababu haja ya moyo wangu naijua,na nyie mnaosema mimi natafuta followers kazaneni kusema lakini hakuna niliyemfata nikamwambia njoo kwangu ni kwa hiari zenu na bado mkiamua mnayo nafasi ya kuniufollow ili nisizidi kuwakera,sitaacha kumpenda D nampenda nampenda nampenda Hata kama sitakuwa nae ila kitendo tu cha yeye kujua kama nampenda basi kwangu ni faraja na inatosha,mchana mwema kwenu


Nassari Afunguka.......Asema Ajali ya Helikopta Aliyopata ni ya Kishirikina, Ndesamburo Asema Atanunua Nyingine

$
0
0

Wakati Mbunge wa Arumeru Mashariki, Joshua Nassari akisema anashindwa kuamini kilichotokea na kunusurika katika ajali ya helikopta juzi, mmiliki wa chopa hiyo, Philemon Ndesamburo amesema atanunua nyingine haraka kabla ya kuanza kampeni za Uchaguzi Mkuu. 

 

Kauli hizo zilitolewa jana ikiwa ni siku moja baada ya helikopta hiyo inayomilikiwa na Ndesamburo kupitia kampuni yake ya Keys Aviation kupata ajali wakati ikitumiwa na Nassari na baadhi ya viongozi wa Chadema.
 

Wakati ikipata ajali, ilikuwa imekodishwa na Kampuni ya General Aviation Services (T) Ltd inayomilikiwa na Kapteni William Slaa.
 

Katibu wa Ndesamburo, Basil Lema alisema ilipata ajali baada ya kupigwa na kimbunga wakati anga likiwa limefunikiwa na wingu zito.
 

“Mheshimiwa Ndesamburo amemshukuru Mungu kwa kuwanusuru watu waliokuwa kwenye ndege hiyo ambao ni pamoja na Mbunge Joshua Nassari.
 

“Ameweka wazi kwamba atalazimika kununua nyingine mapema kwa ajili ya kuongeza nguvu kwenye kampeni za Uchaguzi Mkuu mwaka huu,” alisema Lema akimnukuu Ndesamburo.
 

Lema alisema rubani aliyekuwa akiendesha helikopta hiyo alifanikiwa kuielekeza juu ya miti alioutumia kupunguza kasi ya kushuka chini na kusaidia abiria kutoka salama.
 

“Imeharibika lakini abiria wote ni wazima. Walikuwamo wanne,” alisema na kuongeza kuwa helikopta hiyo ndiyo iliyotumiwa na Chadema katika Uchaguzi Mkuu wa 2010 na Uchaguzi wa Serikali za Mitaa mwaka jana na chama hicho kilitegemea kuitumia katika Uchaguzi Mkuu ujao.
 

Pia, imewahi kutumiwa na makada mbalimbali wa CCM akiwamo Naibu Katibu Mkuu wa CCM, Mwigulu Nchemba na kada maarufu wa Moshi mjini, Buni Ramole.
 

Kauli ya Nassari

Akizungumza na waandishi wa habari katika wodi alikolazwa kwenye Hospitali ya Seliani – Arusha, Nassari alisema waliporuka kutoka Leguruki, hakukuwa na dalili zozote za kuchafuka kwa hali ya hewa, lakini dakika chache baada ya kuruka angani wingu zito lililoambatana na upepo mkali liliwafunika ghafla.
 

“Wingu lile na upepo ule sijawahi kuona katika maisha yangu yote zaidi ya kusoma kwenye vitabu vya simulizi vya mambo ya ushirikina. Namshukuru Mungu wote tuko salama kwani hatukuwa na matumaini ya kupona ajali ile,” alisema Nassari.

Mbunge huyo aliyekuwa katika ziara ya kuhamasisha wananchi kujiandikisha kwenye Daftari la Wapigakura, alimwagia sifa rubani Slaa kwa uwezo na ustadi aliouonyesha hadi wakanusurika.
 

“Kama siyo ustadi wake, naamini watu wangeokota vipande vya nyama tu kwenye eneo la ajali, ila Mungu ni mkuu leo tuko hai wote licha ya madhara madogo,” alisema.
 

Nassari alisema muda mfupi kabla ya kuruka saa kumi na moja jioni, wakati akihutubia mkutano huko Leguruki, alipokea simu kutoka kwa mchungaji mmoja akimtaarifu kupata maono kuwa anakabiliwa na hatari ya kukutwa na jambo kubwa na baya akimtaka adumu katika sala.
 

“Dakika 15 baadaye nikaruka na kupata ajali. Naamini kilichotuokoa ni nguvu ya sala niliyosali baada ya kupokea ujumbe wa mchungaji na maombi ya wachungaji wangu wanaoniombea kila siku,” alidai Nassari.
 

Rubani Slaa alisema alishangaa lilipotokea wingu na upepo uliosababisha ndege kuanguka ikiwa njiani kuelekea Ndoombo na Ngureserosambu.
 

“Kabla ya kurusha ndege nilijiridhisha na hali ya hewa. Hakukuwa na kiashiria chochote cha hali ya hatari kama maeneo mengine ambako tulishindwa kutua kutokana na mvua zilizokuwa zikinyesha."
 

Kaimu Mkurugenzi wa Hospitali ya Seliani, Dk Paul Kisanga alisema hali za majeruhi si mbaya, isipokuwa Eva Kayaha aliyevunjika mbavu mbili.

Biashara ya NGONO Yashamiri Mkoani Dodoma.........Makahaba Wazagaa Kila Kona

$
0
0

BIASHARA ya ngono imeshamiri mkoani Dodoma wakati huu ambao vikao vya kumpata mgombea urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) vimekwisha kuanza.

 

Uchunguzi uliofanywa  katika baadhi ya kumbi kama  Club Maisha, Club Laazizi na Matei Lounge, Chako ni Chako, umebaini kuwapo idadi kubwa ya kina dada wakiwa wamevaa nusu uchi.

 

Katika maeneo ya katikati ya mji wa Dodoma zilikuwapo hekaheka za wasichana wanaojiuza ambao walionekana wakitafuta wateja bila ya wasiwasi wowote na wengine walisikika wakisema  wako kibiashara na siyo kuuza sura.

 

Eneo maarufu la Chako ni Chako kuanzia jioni mpaka usiku kucha  akina dada hao wamekuwa wakijazana hadi kwenye taa za kuongozea magari huku wakitafuta wateja wenye magari.

 

Baadhi yao ambao hawakutaka kutaja majina yao halisi mmoja wao alisema,‘’Kaka sema una shilingi ngapi habari ya majina unataka kutupeleka wapi…?

 

‘’……wewe unaona shimo limetema hapa kila nikigeuka mwanaume na wanatoa ‘mpunga’ nadhani huyu rais ajaye atakuwa na neema.’’

 

Dada mwingine ambaye aliyekuwa   Dodoma Carnival karibu na Kituo Kikuu cha Mabasi, alisema ametoka Arusha akiwa na marafiki zake kwa lengo la kuwafuata wateja wa msimu walioko Dodoma.

 

Alisema hadi sasa ana   siku tatu akiwa  Dodoma na tayari amekusanya zaidi ya Sh 700,000 huku akiwatumia madalali  ambao huwaunganisha kwa wateja 

Mrembo Ester wa Bongo Movies Adai Marafiki zake ni Wavulana tu..Asema Wanawake ni Masnichi Wakubwa

$
0
0

Deogratius Mongela 
MUIGIZAJI mwenye mvuto anayekuja kasi katika tasnia ya filamu Bongo, Ester Kiama ameweka bayana kuwa hapendi kuwa na marafiki wa kike na hana.

Muigizaji mwenye mvuto anayekuja kasi katika tasnia ya filamu Bongo, Ester Kiama.

Akifunguka kiunagaubaga, Ester alisema kutokana na malezi na maisha yalivyo sasa inabidi aepuke marafiki ambao wengi wao ni wanafiki.

“Wengi wanajua naringa sana lakini ukweli sipo hivyo ndiyo maana muda mwingi nautumia katika kufanya shughuli zangu na kujiepusha na makundi kwani najua madhara yake, washikaji zangu ni wanaume kwani najifunza mengi kupitia kwao,” alisema Ester. 

Tano Bora ya Urais CCM Itatoka Ndani ya Kundi Hili.......Majina yao Kuanikwa leo, wengine 33 Kufyekwa

$
0
0

WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya RaisKamati Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) leo inakutana kuchuja majina ya makada wake 38 waliorejesha fomu za kuomba kuteuliwa kuwania urais kupitia chama hicho na majina 33 ni lazima yapigwe panga ili kupeleka majina matano kwenye kikao cha Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) kupigiwa kura.

Kwa mujibu wa habari kutoka mitandao ya kijamii, kwenye vijiwe na mijadala sehemu mbalimbali, majina hayo matano yanaaminika kwamba yatatoka miongoni mwa watiania 10 ambao wametajwa zaidi katika mijadala hiyo.

Sababu kuu mbili ambazo zimekuwa zikitolewa kwenye mijadala hiyo na hata na baadhi ya wachambuzi wa mambo ya siasa Tanzania ni mbili. Mosi, uzoefu wao ndani ya ungozi wa serikali na pili, nafasi yao ndani ya chama, ama kama wajumbe wa NEC au Kamati Kuu.

Majina ambayo yanatazamiwa kwamba yanaweza kupenya Kamati Kuu ni pamoja na Makamu wa Rais, Dk. Mohamed Gharib Bilal; Waziri Mkuu wa zamani na Mbunge wa Monduli, Edward Lowassa; Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Stephen Wasira; Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe; Waziri wa Sheria na Katiba, Dk. Asha-Rose Migiro; Waziri Mkuu Mizengo Pinda; Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Kazi Maalum), Profesa Mark Mwandosya; Jaji Mkuu Mstaafu, Augustino Ramadhani; Waziri Mkuu Mstaafu, Frederick Sumaye na Waziri wa Ujenzi, John Magufuli;.

Kwa ujumla kundi la makada hao (hapo juu) kila mmoja ana nafasi ya kupenya kwenye mchujo wa Kamati Kuu, lakini pia anakabiliwa na changamoto kadhaa.
 

Bilal

Dk. Bilal ni Makamu wa Rais, katika hali ya kawaida ni vigumu msaidizi namba moja wa rais aliyeko madarakani kukosa nafasi ya kupenya ngazi hiyo hata kama ni kwa sababu tu za kiprotokali .

Mbali na wadhifa wake, Bilal anayetoka Zanzibar amepata kuwa Waziri Kiongozi na ana uzoefu wa kuendesha serikali, kwa maana hiyo anawakilisha kundi la upande mmoja wa Muungano na hivyo siyo rahisi jina lake kutokuzingatiwa.
  
Hata hivyo, Bilal ana changamoto ya umri kwani kwa umri wa miaka 70 alio nao sasa inakuwa ni kazi kubwa kukimbizana na changamoto za sasa katika nafasi hiyo.

Lowassa

Lowassa ni mbunge wa Monduli, lakini pia alipata kuwa Waziri Mkuu hadi alipojiuzulu Februari 2008 kutokana na kadhia ya Richmond juu ya mkataba wa kufua umeme. 
  
Hata hivyo, kadri muda ulivyosonga hadi sasa kadhia hiyo ilikuja kujidhihirisha kusukumwa zaidi na misuguano ya ndani ya CCM hasa juu ya chuki za nafasi ya uwaziri mkuu.

Kama walivyo watia nia wengi, ni mjumbe wa NEC, amekuwa waziri katika serikali ya Mzee Ali Hassan Mwinyi na ya Rais Benjamin Mkapa, anaijua serikali vizuri.

Lowassa amekuwa gumzo kubwa miongoni mwa watia nia wote kiasi cha kuandamwa hata na wapinzani wake ndani ya chama kwa kuwa tu kila wakati kura za maoni zimeonyesha kuwa ni chaguo la kwanza la wananchi katika kundi la wawania urais wote, ndani ya CCM na hata ndani ya upinzani.

Mwanasiasa huyo ambaye wengi waliamini kwamba kadhia ya Richmond ilikuwa imemmaliza, aliigeuza hali hiyo kiasi cha kuonekana kuwa mtu anayestahili kuwa Rais wa Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
  
Mvuto wake kwa wananchi wengi, umefanya wapinzani wake wajipange kumwandamana kwa tuhuma mbalimbali, ambazo amezipuuza.

Wakati wa mchakato wa kutafuta wadhamini ndani ya CCM, Lowassa alionyesha kwa vitendo halisi jinsi anavyoungwa mkono na wanaCCM wenzake, kwani mikutano yake iligeuka kuwa ‘mafuriko’ kila mkoa alikokwenda. Alidhaminiwa na wanachama zaidi ya laki nane.

Lowassa anaungwa mkono na wananchi wengi kwa sababu ni miongoni mwa viongozi wa serikali wachache ambao wanatenda kwa vitendo halisi kuliko kupiga kelele kwenye majukwaa ya kisiasa.

Anakumbukwa kwa ufuatiliaji wa karibu kwenye kila wizara aliyokuwa, anakumbukwa kwa kusaidia Tanzania kunufaika na maji ya ziwa Victoria na wakati akiwa Waziri Mkuu alianza kubadili mfumo wa utendaji serikalini kutoka ‘business as usual’ na kuibua ari ya kufanya kazi kwa bidii zaidi miongoni mwa watumishi wa umma.

Wassira

Wasira ni miongoni mwa makada wa siku nyingi wa CCM, amehudumu kama waziri katika serikali za awamu tatu, ya Mwalimu Nyerere; ya Mzee Mwinyi na ya awamu ya nne, inayoongozwa na Rais Jakaya Kikwete.

Ni miongoni mwa wanasiasa wakongwe, akiwa amejizolea umaarufu ndani ya CCM na hata kwenye upinzani kwani mwaka 1995 alihamia NCCR-Mageuzi na kugombea ubunge jimbo la Bunda na kumshinda, Jaji Joseph Warioba.
  
Hata hivyo, baadaye mahakama kuu ilitengua ubunge wake na kumtia hatiani kwa kuhusika na vitendo vya rushwa katika uchaguzi.

Ingawa kiutendaji Wasira anaonekana kama mmoja wa watu wanaojituma, kitendo chake cha kuhama CCM na kurejea tena kinaweza kuwa moja ya sababu za kutumika dhidi yake.

Membe

Amekuwa Waziri wa Mambo ya Nje tangu mwaka 2007 alipoondoka Dk. Migiro kwenda kuwa Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa (UN).
  
Membe aliingia bungeni mara ya kwanza mwaka 2000 wakati wa utawala wa Mkapa, lakini ni chini ya Kikwete alipata nafasi ya kuwa Naibu Waziri, akianzia Mambo ya Ndani na baadaye Nishati na Madini kabla ya kuibukia Mambo ya Nje kama waziri kamili.

Ni mjumbe wa NEC kama walivyo makada wenzake. Kwa miaka mingi ya utumishi wake Membe ambaye pia ni ofisa wa usalama wa taifa, alifanya kazi nje ya nchi.

Duru za kisiasa nchini zinasema kuwa ingawa hana mizizi mirefu ndani ya chama, kukaa kwake wizara ya Mambo ya Nje kwa muda huo kumempa uzoefu wa uendeshaji wa serikali. 
  
Hata hivyo kumekuwa na maoni kuwa Membe anabebwa na wakuu serikalini.

Migiro

Huyu ni mwanamke pekee anayepewa nafasi ya kufika mbali miongoni mwa watia nia wote kwa sababu ya nafasi yake, kwanza ndani ya nchi na nje alipokuwa UN. Anaelezwa kuwa na uzoefu wa ndani na wa kimataifa.

Katika kipindi hiki ambacho Rais Kikwete amekuwa anatoa fursa nyingi zaidi kwa wanawake katika vyombo vya maamuzi, Dk. Migiro anaweza kupenya kwenye kundi la tano bora hivyo kusaka kura za NEC kama anataka kufika kwenye tatu bora kwenye mkutano mkuu.

Pinda

Huyu ni waziri mkuu tanu Februari 2008 alipojiuzulu Lowassa. Pinda amekuwa mbunge tangu awamu ya pili ya Rais Mkapa na kuwa waziri wa Tamisemi.

Muda wake mwingi wa utumishi alikuwa ndani ya Ikulu kama ofisa wa serikali. Ni mwanasiasa ambaye kimsingi hajawa na kishindo sana licha ya nafasi yake kubwa ya uwaziri mkuu.

Pinda amekuwa miongoni mwa mawaziri wakuu wapole ambao hawajaacha kishindo kama alivyokuwa Waziri Mkuu pekee wa Rais Mkapa, Sumaye ambaye alikaa kwenye nafasi hiyo kwa miaka 10, lakini hakuacha kishindo chochote pia.

Hata hivyo, kwa sababu za itifaki kama ilivyokwa Dk. Bilal, itakuwa ni vigumu kumpiga panga jina lake katika ngazi ya Kamati Kuu, ingawa wote umri nao umesogea, Bilal miaka 70 na Pinda miaka 67.

Mwandosya

Mwandosya ni mwanasiasa aliyeweka rekodi mwaka 2005 kwa kuingia tatu bora katika kinyang’anyiro cha urais, akiachwa nyuma na Kikwete na Dk. Salim Ahmed Salim.

Amekuwa moja ya nguzo ya siasa ya CCM kwa miaka mingi na ndiye alianzisha mkakati wa harambee ya kuchangia chama kabla ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2005.

Amehudumu katika awamu mbili kama waziri, awamu ya tatu na ya nne. Kwa kitambo alikuwa ndiye nguzo ya wanaCCM mkoani Mbeya, lakini kuibuka kwa Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dk. Harrison Mwakyembe, kama mmoja wa watia nia, kumeibua maswali mengi kama Profesa Mwandosya bado anashikilia nafasi hiyo Mbeya na kanda yote ya nyanda za juu kusini. 
  
Hata hivyo, umri wa miaka 66 wa Mwandosya siyo haba katika dunia ya leo inayohitaji mchakamchaka.

Sumaye

Sumaye aliweka rekodi ya waziri mkuu aliyekalia kiti hicho mfululizo kwa muda mrefu zaidi ya mawaziri wakuu tisa kuwahi kuteuliwa tangu uhuru.

Hakuna ubishi kwamba Sumaye ana uzoefu wa kuendesha serikali, amekuwa naibu waziri, waziri na waziri mkuu kwa miaka 10. Alishikilia ubunge wa jimbo la Hanang hadi alipoamua kustaafu mwaka 2005 baada ya kuliwakilisha kwa miaka 20.

Ingawa Sumaye hana kikwazo chochote cha kisiasa kupenya hatua ya Kamati Kuu, nguvu zake za kisiasa jimboni kwake zimepungua ndiyo maana mwaka 2012 alibwagwa katika nafasi ya UNEC na Mary Nagu, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Mahisiano na Uratibu).

Magufuli

Dk. Magufuli amekuwa ni miongoni mwa mawaziri wachache wachapakazi tangu awamu ya Rais Mkapa na hata sasa.
  
 Amekuwa Naibu Waziri wa Ujenzi na kisha Waziri wa Ujenzi wakati wa Mkapa na chini ya Kikwete amekuwa Waziri wa Uvuvi na Mifugo, kisha wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi. Kila alikopelekwa amejitahidi kuchapa kazi.
 

Ni kati ya mawaziri wanaozijua wizara na majukumu yao sawasawa, ni mfuatiliaji. Kwa utendaji huo, Magufuli amejijengea sifa ya kuwajibika kama kiongozi.

Hata hivyo, kuna jambo kubwa ambalo limekuwa likiibuka kila wakati juu ya kuhusika kwake na uuzaji wa nyumba za serikali.
  
Ingawa inadaiwa kuwa ulikuwa uamuzi wa baraza la mawaziri, bado wananchi wengi wamekuwa wakihoji uamuzi wa kuuza nyumba hizo.

Mbali ya kuwa mbunge wa Chato tangu mwaka 1995, Magufuli hajawahi kugombea nafasi nyingine ya kuchaguliwa ndani ya CCM. 
  
Siyo mjumbe wa NEC na hakuna kumbukumbu zozote kwamba alipata kuomba nafasi hiyo.

Mwanamuziki Mwingine wa Bongo Flava Ambae ni Albino Atangaza Nia ya Kuingia Kwenye Siasa..Adai Anajipenda na Kujiamini..

$
0
0
Msanii wa Bongo Fleva  ambaye ameshawahi kuigiza kwenye filamu kadha ya kupinga mauwaji ya Albino, Keisha  amefunguka kupitia ukurasa wake wa kwenye mtandao wa  Instgram sababu na nia yake ya kuingia bungeni mwaka huu,na kwamba wao kama walemavu wa ngozi (Albino) lazima wawe na wawakilishi wa kutosha bungeni ili sauti zetu zisikike ili sheria itungwe na kutekelezwa pia.
Kesha ameandika;

Habari za asubuhi ndugu zangu rafiki zangu mashabiki zangu na media zote nchini.najua wengi mnajiuliza maswali mengi sana juu yangu kwanini nimeamua kuingia kwenye siasa lakini leo naomba nifunguke na kuwaambia kitu.

Mimi kama mlemavu wa ngozi najikubali najipenda na ninajiamini lakini yote tisa napigana kwa uhuru na amani ambayo tunastahili kuipata kutoka nchini kwetu.

Nilipoanza kupost picha zangu za siasa kuna ambao walinipongeza na kuna ambao walinisema kwamba sina uchungu na wenzangu kwakuwa wanahisi nimeingia huku kwa ajili ya kujinufaisha mwenyewe mimi ni mpiganaji na ndomana siku zote nimekuwa nikiwaza kuhusu amani yetu.fimbo ya mbali haiui nyoka na kidole kimoja hakivunji chawa nikimaanisha kwamba lazima tusimamie sheria ambazo zitatusaidia kuendeleza amani hivyo basi lazima tuwe na wawakilishi wa kutosha ndani ya bunge ili sauti zetu zisikike ili sheria kutungwa na kutekelezwa pia.hivyo mimi kama mtanzania mwenzenu nahitaji support yenu ili niweze kufikia malengo yetu kwa yeyote ambaye anaupendo nasi na mimi na harakati zangu anisaidie kwa chochote ambacho kitanifikisha nnapoataka.

this is my tigo no 0718785045 na hii ni account number yangu ya crdb 011 2022295800 jina ni hadija shabani Taya unaweza kuchangia humo na kwa upendo kabisa naomba u repost hii post kadri muwezavyo ahsanteni shukrani.

Tumuunge mkono jamani.
Viewing all 104698 articles
Browse latest View live




Latest Images