Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104756 articles
Browse latest View live

Picha za Mauji ya Polisi na Raia yaliyofanywa na Majambazi Usiku wa Kuamkia leo Jijini Dar

$
0
0



Picha zanatisha :Picha za Mauji ya Polisi na Raia yaliyofanywa na Majambazi Usiku wa Kuamkia leo Jijini Dar

Minong'ono Kuhusu Shilole Kuwa Mjamzito Hizi Hapa..Mwenyewe Aibuka na Kusema Haya

$
0
0
Mussa Mateja
Minong’ono! Tumbo la staa wa Bongo Fleva, Zuwena Mohamed ‘Shilole’ limezua maswali kwa wadau kibao kama ni la kawaida au tayari mwandani wake, Naftal Mlawa ‘Nuh Muziwanda’ ameshampachika ujauzito.

Shilole au Shishi Baby alizua minong’ono hiyo wikiendi iliyopita nyumbani kwa mwigizaji, Aunt Ezekiel Grayson maeneo ya Mwananyamala jijini Dar ambapo kulikuwa na shughuli ya 40 ya mtoto wa Aunt, Cookie iliyokwenda sambamba na futari huku mastaa kibao wakijumuika katika tukio hilo.

Akiwa kwenye tukio hilo, Shilole alizua maswali baada ya tumbo lake kuonekana limejaa kama mjamzito.
“Dah nipo kitambo sasa lakini sijapata picha kama tumbo la Shilole ni mimba au kashiba tu, maana kwa uzoefu wangu jinsi anavyoonekana atakuwa na mimba,” alisema mmoja wa mashuhuda.

Baada ya kuona hali hiyo, mwanahabari wetu alimfuata Shilole kwa lengo la kumtaka azungumzie ishu hiyo kama ni tumbo tu au ameshanasa ujauzito, ambapo alisema:

“Ni kweli nina mwanaume rijali lakini sijabahatika kupata mimba, nadhani muonekano wa tumbo ni kwa sababu ya nguo niliyovaa ila natamani kupata mtoto,” alisema Shilole.

Diamond na Penny Uso Kwa Uso...Ni Kwenye 40 ya Mtoto wa Aunt Ezekiel, Wakumbushia Enzi zao...

$
0
0
Musa Mateja na Imelda Mtema
Ule usemi wa kwamba milima haikutani, binadamu hukutana umejidhihirisha baada ya staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’, kukutana uso kwa uso na aliyekuwa mchumba’ke, Penniel Mwigilwa ‘Penny’ kwenye shughuli ya 40 ya mtoto wa mwigizaji, Aunt Ezekiel hivyo kupata fursa ya kukumbushia enzi zao.


Tukio hilo lililoshuhudiwa na Ijumaa Wikienda lilijiri wikiendi iliyopita nyumbani kwa Aunt, Mwananyamala, Dar ambapo pati hiyo ilihudhuriwa na mastaa kibao.

Katika tukio hilo, Diamond ndiye aliyeanza kumuona Penny akamwita kwa lengo la kumsalimia ambapo naye alitii akionekana mwenye furaha kisha walikumbatiana huku baadhi ya waalikwa wakiwataka kukumbushia enzi za mapenzi yao.

Baada ya salamu, waliendelea kuzungumza ‘mambo yao’ huku muda wote wakicheka.
Baadaye, Penny aliwasalimia baadhi ya watu waliokuwa wamekaa na Diamond na kwenda kukaa pembeni yao huku akitazamana na Diamond kwa shauku kubwa.

Ijumaa Wikienda liliendelea kufuatilia kila jambo juu ya wawili hao ambapo muda mwingi walikuwa wakitaniana huku Romy Jones akichagiza utani huo.Hata hivyo, baadaye Romy alinyanyuka alipokuwa ameketi na kwenda kwa Penny kama mtu aliyeagizwa jambo na Diamond ambapo walizungumza kwa kirefu.

Alipoulizwa Penny kulikoni yeye na Diamond kuwa gumzo mahali hapo, alisema kuwa hana sababu ya kununa maana hakuna kibaya ambacho kipo kati yake na jamaa huyo kwani wamekuwa wakiwasiliana na kuongea vizuri ingawa kila mtu ana mambo yake.

“Hapa tumealikwa na kila mtu amekuja kivyake, sasa si rahisi ukawaona watu usiwasalimie au uchukie maana hakuna sababu ya kufanya hivyo, sina ugomvi na Diamond na sina mipaka yoyote ya kusalimiana au kuongea naye,” alisema Penny.

Kwa upande wa Diamond alisema kuwa alikuwa pale kwa ajili ya kufuturu na kumfurahia kila mtu hivyo hakuna dhambi yoyote kwake kusalimiana na Penny.

Taarifa zaidi za kuvamiwa kwa kituo cha polisi Stakishari-Ukonga,polisi wanne kuuawa na kuporwa silaha

$
0
0
WATU wanaodhaniwa kuwa majambazi wamevamia Kituo cha Polisi Stakishari kilichopo Ukonga jijini Dar es Salaam, jana usiku na kuua askari na raia kisha kupora silaha.

Kwa mujibu wa taarifa kutoka eneo la tukio zinasema kuwa watu hao walifika kituoni hapo wakiwa katika pikipiki wakidai kwamba walikuwa wamembeba mtu aliyepata ajali wakihitaji msaada wa polisi kabla ya kuwabadilikia ghafla na kuanza kuwashambulia kwa risasi.

Inadaiwa kuwa askari wanne wamepoteza maisha katika tukio hilo, wananchi wawili na mmoja wa magaidi hao.

Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Suleiman Kova amesema atakuwa na mkutano na wanahabari kati ya saa 5 au 6 leo kwa ajili ya kutoa taarifa rasmi juu ya tukio hilo la kigaidi.

LULU MICHAEL Amchokoza Wema Sepetu, Ampiga Dongo la Wazi wazi Kuhusu Ubunge Viti Maalum, Soma Hapa Vijembe Alivyotoa kwa Wema

$
0
0
Kupitia Account yake ya Tweeter Mrembo na Mwigizaji wa Bongo Movies Lulu Michael Amerusha Kijembe kikali kwa Wanaowania Ubunge kupitia Viti Maalum, Kijembe hicho kimetafsiriwa na Wadau kuwa ni Special kwenda kwa Wema Sepetu ambae nae yumo katika wagombea kupitia Singida...
Soma Hapa alichoandika:

Lulu atolea ufafanuzi wa ‘Kijembe’ Alichoandika Twitter kuhusu ‘viti maalum’ Ambacho Wengi Wanadai Amemlenga Wema Sepetu

$
0
0
Baada ya muigizaji mrembo wa filamu za Bongo, Elizabeth “Lulu” Michael kuandika tweet iliyotafsiriwa kuwa huenda ni kijembe kwa mrembo fulani, amefafanua alichokimaanisha.

Lulu amesema kuwa alichokiandika kwenye post hiyo ilikuwa ni utani, na wakati huo huo kukubali kuwa inaweza kuwa na ukweli ndani yake.


  • “It was a joke, but sort of ukweli pia kwa sababu mara nyingi kumekuwa na dhana watu wa nje wanachukulia kama vile viti maalum ni vya kupeana” alisema kupitia The Playlist ya Times Fm.


Hiki ndicho alipost:


Lulu aliendelea kwa kusema:


  • “…probably watu wameichukulia kama nimemsnitch mtu, mimi siko hivyo na sinaga hayo mambo kabisa. Ni kwamba nimefanya kama utani, lakini watu wasichukulie poa kwamba kila anaewekwa pale kwamba ana sura nzuri, kila anaewekwa pale ana umbo zuri.”

Tundu Lissu: I don’t See Lowassa Crossing Over From CCM to Join With UKAWA

$
0
0

A Tanzanian opposition lawmaker says tension within the ruling Chama Cha Mapinduzi (CCM) party will boost the chances of the opposition coalition to win the presidential vote.

The CCM has ruled the country since the country gained independence in 1961.

Tundu Lissu of the Chadema party says the opposition parties' Ukawa coalition will take advantage of the apparent split among supporters of the ruling party to win.

His comments came after senior officials of the CCM Central Committee excluded former Prime Minister Edward Lowassa, from the list of aspiring candidates to lead the party in the October 25 general election.

Lowassa was seen as a front-runner in the presidential race because of the crowds that welcomed his campaign across the country. His opponents however accuse him of being divisive and tainted with corruption. Lowassa denies the accusations.

The ruling party’s central committee led by outgoing President Jakaya Kikwete excluded Lowassa from a five-member list of candidates ahead of the October vote.

Opposition Hopeful

Analysts say Lowassa’s exclusion could split the ruling party, and give the opposition coalition a chance to win the presidential vote. Lissu agrees with the assessment.

“This is the end game for CCM and it has been this way for quite a while,” said Lissu. “The fact that Edward Lowassa has been taken out of the race will definitely cause even bigger tension and divisions within the CCM. It will surely put us in a much better position to win power in October.

“Our chances are very good,” said Lissu. “They were very good with Lowassa and they are very good with whoever comes… [Lowassa] has not been able to win the people within his party. We know the reasons why he was drawing huge crowds [because] his campaign has been very well financed. He spent billions to get people on the streets to get people to show support to him.”

Some supporters of the former prime minister say Mr. Lowassa should consider joining an opposition party to challenge the ruling party due to what they said is his popularity. Lissu disagreed.

“I don’t see Lowassa crossing over from CCM to join with Ukawa. Firstly, because he is not the type of politician who has the boldness required to cross over. It is also a fact that if he crosses over to the opposition, there is no way he can be our flagbearer in the coming election in October. So, I don’t see any incentive for him to cross over except for the maybe retaliation,” said Lissu.

He said the reaction of supporters from the opposition coalition has been quiet. Lissu however says the group has been focused on intensifying its nationwide campaign ahead of the vote.

“We have been preparing ourselves so whoever comes from CCM... we are being prepared. So the fact that it is not Lowassa does not in any way lower our level of preparation,” said Lissu.

Picha Hii Inatufundisha Nini Kuhusu Watawala Wetu Wanao Omba Kupewa Mamlaka kwa Muhula wa Pili au zaidi?

$
0
0
Monduli Wakati shule nyingi nchini zinafunguliwa baada kumalizika kwa likizo Wanakijiji wa kijiji cha Donyonaado kilichopo wilaya ya Monduli mkoani Arusha wameeleza wasi wasi juu ya uchakavu wa jengo la shule ya Msingi Idonyonaado huenda linaweza kuanguka na kusababisha maafa kwa wanafunzi.

Shule hiyo iliyoko umbali wa kilomita 64 kutoka Monduli mjini iliyojengwa kwa udongo na mawe na wanakijiji waliojitoa haina milango na madirisha hivyo wanafunzi kupata adha ya vumbi na baridi kali hasa kipindi cha mvua. Wanakijiji hao wamesema kuwa hali mbaya ya miundombinu ya shule hiyo imewafanya wazazi wengi kusita kuwapeleka watoto mashuleni hivyo ameiomba serikali na mashirika binafsi yajitokeze kusaidia kutatua changamoto hizo.

Mwenyekiti wa kijiji cha Donyonaado ,Malulu Kutetei amesema kuwa licha ya changamoto za shule hiyo bado wanakabiliwa na tatizo la ukosefu wa nyumba bora za walimu pamoja na uhaba wa maji jambo linalokwamisha maendeleo ya taaluma shuni hapo.

Mkurugenzi wa Shirika lisilokuwa la kiserikali la Wafugaji la Monduli Pastodalist Development Initiative (MPDI) ,Erasto Sanare ameeleza kusikitishwa na changamoto zinazoikabili shule hiyo hivyo kushiriki katika ujenzi wa shule ya kudumu ,ameieomba serikali isaidia shule hiyo ambayo ni tegemeo kwa wafugaji.

Licha ya Jamii ya Wafugaji kuamka katika masuala ya elimu tofauti na miaka iliyopita bado kuna mazingira duni ya elimu ikiwemo kukosekana kwa shule za kutosha,miundombinu mibovu,uhaba wa maji na vifaa vya kufundishia na nyumba za walimu

My take
Swali: Kweli Kabisa tunaamini watu hawa wanaweza saaaana kuongoza? Kabisa wapo wanaosema tuwape miaka mingine mitano tena kwa macho makavu kabisa....


Tujiulize Maswali Haya Juu ya Uporaji wa SILAHA na Mauji ya Askari Vituo vya Polisi..

$
0
0
Hii hali ya polisi kuporwa silaha vituoni inatisha sana kwa sasa.

Hapa kuna maswali machache nimejiuliza bila majibu

1.Ni kwanini waporaji hupendelea vituo vya mjini tu?Hususani Dar na Pwani

2.Kwa nini waporaji hawajishughulishi na vituo vya wilayani huko mkoani,Ingali kwao inakuwa rahisi kutoroka?

3.Kwa nini wanatumia riski kubwa kupora hizo silaha ukizingatia tetesi zilizopo zipo silaha haramu zinauzwaga kwa bei rahisi?

Hili ni jambo la kufanyia utafiti na uchunguzi wa kina,Inawezekana nyuma ya huu uharamia lipo jambo kubwa limejificha.

Emmanuel Mbasha Akutwa na Hatia ya Kesi ya Ubakaji

$
0
0
MAHAKAMA ya Wilaya ya Ilala imesema mfanyabiashara na muimbaji wa muziki wa injili Emmanuel Mbasha ana kesi ya kujibu katika shtaka linalomkabili la ubakaji linalomkabili.
 
Katika shtaka hilo Mbasha anadaiwa kumbaka binti mwenye umri wa miaka 17 (jina linahifadhiwa) ambaye ni shemeji yake.
 
Mbele ya Hakimu Flora Mjaya, mwendesha Mashtaka Munde Kalombola alidai mahakama imemkuta Mbasha na hatia baada ya kupitia ushahidi wa pande zote mbili.
 
Mbasha ambaye ni mume wa muimbaji maarufu wa muziki wa injili Flora Mbasha anadaiwa kumbaka shemeji yake huyo kati ya Mei 23 na 25 mwaka huu eneo la Tabata ambako alikuwa akiishi naye.
 
Kesi hiyo ilianza kusikilizwa mahakamani hapo Septemba 5, 2013 ambapo binti huyo aliieleza Mahakama kuwa alibakwa na shemeji yake (Mbasha) kwa awamu mbili tofauti kabla ya kufanikiwa kukimbia.
 
Kwa mujibu wa Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai ya mwaka 2003 sura ya 20 kifungu cha 186, kifungu kidogo cha tatu, kesi hiyo inasikilizwa na Mahakama ya siri ili kulinda haki ya binti huyo.
 
Kesi hiyo itatajwa tena mahakamani hapo Julai 23, mwaka huu ambapo Mbasha anatakiwa kufika na mawakili wake ili kujitetea dhidi ya shtaka hilo

UKAWA Wasema Magufuli Hawatishi na Hawamuogopi...Wadai Hawezi Kuleta Mabadiliko yoyote ni Wale wale

$
0
0
Dakika chache baada ya CCM kumpitisha Dk John Magufuli kuwa mgombea wake wa urais, viongozi wa vyama vya upinzani wamesema hawatishwi na Dk Magufuli na wanamuona kama kada wa kawaida miongoni mwa wengi waliopo CCM na kwamba hawezi kuleta mabadiliko yoyote.

Wamesema vita yao ni kuondoa mfumo wa uongozi uliopo na si ya mtu mmojammoja.

Wakizungumza jana viongozi hao, hasa wanaounda Ukawa, walisema wanajipanga kumtambulisha mgombea wao kesho na kila Mtanzania atapata fursa ya kumfahamu.

Katibu Mkuu wa NCCR-Mageuzi, Mosena Nyambabe alisema CCM inakabiliwa na tatizo la mfumo mbovu, hivyo vita iliyopo inaelekezwa katika kukiondoa madarakani ili kuruhusu kitu kipya kuchukua nafasi na kuwapa Watanzania uzoefu mwingine.

Alisema Ukawa haimhofii mgombea huyo kwa kuwa hata sifa zilizotumika kumpata ni za chama chake na kwamba suala linalozingatiwa ni hoja zenye mashiko mbele ya wananchi ambao wamechoshwa na taratibu za siku zote kushughulikia kero zao.

“Ajenda na hoja tulizonazo ndizo zitakazotubeba mbele ya wananchi… tutawapelekea ili waamue wakiwa na taarifa sahihi. Kama ni kutowajibika au ufisadi ndani ya CCM, suala hilo linaanzia ngazi ya juu mpaka kwa mwanachama wa kawaida,” alisema na kuongeza:

“Hatutegemei kashfa kama kigezo kikuu cha kumshinda mgombea wa CCM kwa kuwa hilo ni tatizo la mfumo wa chama kizima,” alisema.

Mwenyekiti mwenza wa Ukawa, Dk Emmanuel Makaidi alisema endapo wananchi wataachana na dhana ya kufuata itikadi na wakaelekeza fikra na akili zao katika hoja za kampeni, watakuwa kwenye nafasi nzuri ya kumchagua kiongozi bora.

“Hatustushwi na (Dk John) Magufuli kwa lolote na mashambulizi yetu yatakuwa makubwa. Lengo letu la kuiondoa CCM madarakani liko palepale,” alisema Dk Makaidi ambaye pia ni Mwenyekiti wa NLD.

Naibu Katibu Mkuu wa Chadema (Bara), John Mnyika alisema mabadiliko ya mfumo mbovu wa utawala hayawezi kufanywa na mteule yeyote wa CCM kwa kuwa chama hicho kimeahidi kufanya mambo yaleyale.

Alisema baada ya chama hicho kumaliza harakati zake za kumpata mgombea urais, kazi yake ya kwanza ilikuwa ni kumteua Samia Suluhu Hassan aliyeshiriki uongozi wa kuichakachua Katiba Mpya.

“Hii inadhihirisha kuwa nchi itaongozwa na watu walio nyuma ya pazia kuendeleza uchakachuaji badala ya kuheshimu matakwa ya wananchi. Ufisadi utaendelea iwapo CCM itaendelea kutawala,” alisema Mnyika.


Mwenyekiti wa Tanzania Labour (TLP), Augustine Mrema alimpongeza Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete pamoja na kamati ya maadili ya chama hicho kwa kuwaondoa watu wenye kashfa za rushwa na ufisadi na kutaka wembe huo uendelee hata kwa ngazi za ubunge na udiwani.

“Chama kimejivua gamba na wafanye hivyo kwa ngazi zote zilizosalia,” alisema Mrema na kuongeza kuwa:
 
 “Nitafanya kazi kwa ushirikiano mzuri na Dk Magufuli kwani ameshafanya kazi kubwa hapa Vunjo. Namtakia mafanikio katika safari yake.”

Natamani mngeelewa jinsi ninavyompenda Zari – Diamond

$
0
0
Diamond Platnumz anatamani watu waelewe jinsi anavyompenda mpenzi wake Zari Tlale aka The Bosslady.

Wawili hao wanatarajia kupata mtoto wao wa kwanza mwezi ujao.

Hitmaker huyo wa ‘Nana’ amepost picha kwenye Instagram inayomuonesha akilibusu tumbo la mpenzi wake huyo na kuandika, “I wish you can understand how Much i Love this Woman… Thanks God for the life have always prayed for."

Msanii huyo amemaanisha, “Natamani mngeelewa jinsi ninavyompenda huyu mwanamke. Asante Mungu kwa maisha niliyokuwa nikiyaomba siku zote.”

Mkuu wa Jeshi la Polisi Azungumzia Tukio La Majambazi Kuvamia Kituo Cha Polisi Jana.......Asema Waliouawa ni Polisi 4 na Wananchi 3

$
0
0
Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, Ernest Mangu akizungumza na waandishi wa habari leo katika kituo cha Stakishari Ukonga jijini Dar es Salaam, kutokana na Askari wa Jeshi la Polisi  na raia wa eneo hilo kuuwawa na majambazi waliovamia katika kituo hicho usiku wa kuamkia leo.

Viongozi wa Jeshi la Polisi nchini wakiongozwa na Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, Ernest Mangu, wakitembelea maeneo mbalimbali ambayo majambazi walidhuru, katika kituo cha Stakishari Ukonga jijini Dar es Salaam leo.

*****
ASKARI wa nne wa Jeshi la Polisi na raia watatu wamefariki dunia  katika tukio la ujambazi lililotokea katika kituo cha Polisi cha Stakishari kilichopo Ukonga jijini Dar es Salaam.

Katika tukio hilo watu wapatao nane wamesadikika kuingia katika kituo hicho cha Polisi eneo la Stakishari majira ya saa 4 usiku wa kuamkia leo.

Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo, Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, Ernest Mangu amesema lengo la la watu hao ni kutaka kuiba silaha zilizokuwa katika kituo hicho cha Stakishari.

Aidha, amesema wananchi wanapaswa kutoa ushirikiano kwa kutoa taarifa zinazohusu uharifu kwa Jeshi la Polisi.

Pia, kuhusu uvamizi wa Majambazi, Mangu amesema watajitahidi kuanza kuimarisha ulinzi kwa upande wao hususani katika vituo vya Polisi ndiyo baadae kwenda kuimarisha usalama wa  wananchi.

Tukio la Kituo cha Polisi Kutekwa: Viongozi Wa Dini Wacharuka.......Wamtaka Rais Kikwete Afanye Mabadiliko ya Jeshi la Polisi

$
0
0
VIONGOZI mbalimbali wa dini nchini wameandaa maandamano  kwa lengo la kumuona Rais jakaya kikwete ili kumuomba alifanyie mabadiliko makubwa Jeshi Polisi.

Mabadiliko hayo ni pamoja  na kubadili mawaziri  wote wa mambo ya ndani,  mkuu wa jeshi hilo (IGP)  na  MA-CP wawili ambao wametajwa  kuendesha jeshi hilo  kimtandao  kinyume  na taratibu za kijeshi.

Maandamano hayo yamefikiwa na Maaskofu na Mashekhe 160 wa mjini Dodoma jana chini ya Mwenyekiti wa Kamati ya  Maadili, amani na haki za binadamu ya Madhehebu ya Dini Nchini Askofu William Mwamalanga.

Mwamalanga alisema  viongozi hao wamepokea taarifa ya kuuwa  kwa  askari polisi  wanne wa kituo cha stakishari cha jijini Dar es Salaam  kwa masitikito.

“Tumepokea taarifa ya vifo vya askari hawa kwa masikitiko, hali hii haikubaliki kila mara vituo vimekuwa vikivamiwa na hadi sasa takriban Askari 47 wameuwawa,” alisema Mwamalanga.

Huku akibubujikwa na machozi ya Uchungu Askofu Mwamalanga amehoji ukimya wa  Waziri wa Mambo ya Ndani Mathias Chikawe na IGP Erinest Mangu kwa vifo vyote ambavyo vimekuwa vikitokea tangu mwaka huu uanze.

“Uvamizi huu na mauaji ya askari wa chini unatisha   na hatuoni hatua yoyote ya maana  iweje wahalifu wawe na nguvu kuliko jeshi hasa kipindi hiki ambacho dunia inakabiliana  na makundi ya wahalifu hatari wakiwemo al shabab,” alihoji.

Kufuatia hali hiyo, ASkofu  Mwamalanga  amemuomba  Rais kikwete  kuwaongeza askari  wangazi ya  chini  mishahara   kwa kiwango cha Millioni moja ili  walingane na wenzao wa  nchi za afrika mashariki na kusini.

Alisema hatua hiyo itawawezesha askari hao kukabiliana na changamoto za maisha kama  ilivyofanya kwa wafanyakazi Mamlaka ya Mapato nchini (TRA) ambapo ilisema hiyo itawaondolea tamaa za Rushwa.

“Kwa Polisi ni zaidi kwani kitendo cha kuuwawa kama tembo porini bila mshahara mzuri kunawakatisha tamaa na ari ya kufanya kazi,” alisema.

Askofu  Mwamalanga  ambaye ni Mwanaharakati  Mtafiti wa haki  za jamii  alisema idadi kubwa ya Maaskofu na Maashekhe nchini wamelaani Mauaji  hayo yanayoendelea dhidi ya polisi.

“Tayari zaidi ya askari 47 wameuwawa na wengine wamebaki vilema, silaha  lukuki zimechukuliwa vituoni na kutokomea kusikojulikana, hili lina dhihirisha kuwa Taifa letu lipo pabaya. Ndiyo maana tunaona ipo haja tena muhimu kwa rais kwachukilia hatua za haraka  wanaosababisha uzembe huo ikiwa ni pamoja na kulifanyia ukarabati jeshi hili,” alisema.

Aliwakumbusha watanzania kuliona jeshi hilo kuwa ni chombo chao cha kuwalinda  wao wawe salama dhidi magenge ya uhalifu  duniani hivyo wana wajibu kama  raia wema  kuhakikisha wanawalinda askari  hao kwa hali na mali ikiwa ni pamoja na kuwapa taarifa muhimu ili kuwakamata  wauaji wote pamoja  na silaha zote zilizoporwa.

Aidha  viongozi hao  walihoji kuondolewa kwa vizuizi [ berial] barabarani kulikuwa na maslahi gani kwa usalama wa nchi kwani hivi sasa  wahalifu  wametumia nafasi kutoroka kirahisi pale wanakuwa wamefanya uhalifu.

“Tunataka vizuizi hivyo virudishwe mara moja kwa barabara zote nchini,” alisema.

Kwa upande wake shekhe  Athumani Mukambaku   ambaye ni  Mwenyekiti mwenza wa Kamati  hiyo  na mjumbe wa BAKWATA halmashauri ya mkoa wa dar es Salaam alishauri serikali itunge sera mahususi ya  raia  wote kuwalinda  polisi  baadala  ya dhana iliyojengeka kuwa ni polisi pekee ndiyo wenye wajibu wa kulinda  raia, jambo linalojenga chuki pale ambapo  polisi wanaposhindwa  kusimamia haki za raia sawasawa.

“Katika kipindi hiki cha kulelekea uchaguzi mkuu jeshi linapaswa kuimarisha vituo vyake vyote ikiwa ni pamoja na kufunga kamera maalumu za cctv ili kuweka rekodi ya watu wote wanaotembelea vituo hivyo pamoja kuvunja kanda maalumu za kipolisi ambazo hazionesha juhudi ya kupambana na uhalifu na baadala yake zimeongeza gharama  kwa jeshi  hilo,” alisema Shekhe Mukambaku.

Alisema rais anapaswa ateue makamanda wabunifu wanaokwenda na wakati na kwamba  kila mkoa uwe maalumu kwa kuimarisha vitendea kazi vya askari ikiwa ni pamoja kuwapatia  motisha wale walio ngazi ya chini ambao hukesha  vituo kuimarisha ulinzi.

Dr Slaa: Nikiwa Rais Nitamtia Magufuri ndani kwa Kuuza nyumba za Serikali

$
0
0
Dr Slaa akihojiwa na Radio five ya Arusha Jana jioni nini maoni yake kuhusu uteuzi wa Magufuri kuwania Urais.

Ameongelea mengi lakini amesema iwapo UKAWA wakimpa nafasi na Watanzania wakampa kura za kutosha kushinda Urais atamtia Magufuri ndani ili kujibu tuhuma za uuzwaji wa Nyumba kwa bei ya kutupa.

Source: Radio five, Arusha

Lowassa: Je, Alikosea Wapi? Akiamua Kuendelea, Arekebishe Wapi?

$
0
0
Mchakato wa kutafuta mgombea urais kwa tiketi ya CCM umeshakamilika, na mgombea aliyepatikana ni John Pombe Magufuli. Pamoja na hayo, ukweli unabakia kwamba katika mchakato wa kutafuta wadhamini, ni Edward Lowassa ndiye aliyeungwa mkono na wanachama na makada wengi wa CCM kuliko mgombea mwingine yoyote.

Edward Lowassa aliungwa mkono na wanachama karibia milioni moja wa Chama Cha Mapinduzi. Pamoja na jina la Edward Lowassa kutorudishwa na vikao vya ngazi za juu ya CCM, kuelekea uchaguzi mkuu, suala la Lowassa kupata wadhamini karibia milioni moja ni suala ambalo halitakiwi kuchukuliwa kimasihara au kubezwa, kote - ndani na nje ya CCM. Kwanini tunasema hivyo:

1. Wadhamini hawa karibia milioni moja ni mchanganyiko wa wanachama na viongozi wa ngazi mbali mbali wa CCM. Wanatoka katika kona mbalimbali za Tanzania. Ni hawa ambao kwa kawaida, ndio wanaochukuaga jukumu la kumbeba na kumnadi mgombea urais (CCM) baada ya jina la mgombea kupatikana.

2. Kwa kuzingatia historia inavyotueleza, upinzani umeweza kunyakua makada wengi wa CCM baada ya makada hao kuenguliwa majina yao na vikao vya juu vya chama, licha ya makada husika kukubalika na kuwa chaguo la wanachama na makada wengi wa ngazi za chini. Kilichofuatia ni kwamba, CCM ilikuja kupoteza majimbo kadhaa kwa upinzani.

Kama ilivyotokea huko nyuma kwa makada kadhaa kuenguliwa katika vinyang’anyiro cha ubunge hivyo safari yao ya matumaini kuzimishwa na vikao vya juu vya CCM licha ya kukubalika na makada wengi wa ngazi za chini za CCM, hali hii imejitokeza kwa mara ya kwanza katika kinyang’anyiro cha kutafuta mgombea urais (CCM) ambapo, Safari ya matumaini ya Edward Lowassa kubeba bendera ya CCM (urais) 2015, Safari hiyo imezimwa rasmi na vikao vya juu vya chama cha mapinduzi. Je:

· Edward Lowassa alikosea wapi katika safari yake ya matumaini ndani ya CCM?

Na iwapo itatokea akashawishika kuendelea na safari yake ya matumaini kupitia chama kingine cha siasa kama ilivyotokea kwa makada wengine walioenguliwa kwenye vinyang’anyiro vya ubunge (CCM), ili kutimiza safari yake ya matumaini nje ya CCM, je:

· Edward Lowassa arekebishe wapi ili kufika safari yake ya matumaini nje ya CCM?

Baada ya Jina Lake Kukatwa, Haya Ndiyo Yanayomsumbua Edward Lowasa Mpaka Anashindwa Kula

$
0
0

Nimepata taarifa kutoka kwa watu walio karibu na Lowasa kuwa tangu juzi chakula hakijapanda kwa mzee. Kwamba kila akiwekewa chakula mezani, anachokonoa kidogo tu na inachukua muda mrefu kati ya tonge moja hadi jingine. Pia mdau huyo kanidokeza kuwa Mzee Lowasa kwa sasa ana mawazo mengi sana na hajui afanye nini. Wapo waliomshauri kuwa akae kimya katika kipindi hiki kigumu ili apate muda wa kutosha kutafakari na kufanya maamuzi. Hata hivyo, ushauri huo ameutupa kwani anahisi kwamba muda ukipita atasahaulika na yale aliyopanga kuyatekeleza hayatatimia. Wapo waliomshauri kwamba aende kwao Monduli akatulie japo kwa wimbi mbili na asiruhusu watu wamtembelee ili mawazo yake yapungue. Wapo pia wanaomshauri kuwa aende kwenye vyombo vya habari na kueleza kwa nini amekatwa. Wanaomshauri hivyo wanaona kuwa hiyo ndo njia sahihi kwani kukaa kwake kimya kunaacha sintofahamu kwa wapenzi wake.

Hata hivyo, nimetafakari sana juu ya hatma ya Lowasa na nimebaini kuwa anasumbuliwa na mambo yafuatayo;

1. JINSI YA KUREJESHA FEDHA ZA WAFADHILI WAKE
Lowasa ametumia kiasi kikubwa cha fedha tangu aanze mchakato wa kwenda Ikulu, vyanzo vyangu vimebaini kuwa Lowasa ametumia zaidi ya shilingi bilioni 50 hasa kuanzia mwaka 2012 alipojitokeza hadharani kuchangia huduma za kijamii, mashirika ya kidini, watu binafsi na taasisi mbalimbali. Kati ya fedha hizo, shilingi bilioni 30 zimetumika kwa kipindi cha 2014 hadi alipokatwa rasmi Julai 9. Inaelezwa kuwa kiasi kingine cha fedha kipo mikononi mwa watu na kingine hakijulikani kimeenda wapi ijapokuwa bill imeenda kwa Lowasa. Hiki ni kiasi kikubwa cha fedha. Ni fedha ambazo alipewa kwa wafadhili wake kwa mategemeo kuwa zitarejeshwa baada ya yeye kwenda Ikulu ambapo walikubaliana kuwa watapewa miradi ya serikali. Hata hivyo, baada ya kukatwa, Lowasa hana namna tena ya kurejesha fedha hizo. Baadhi ya wafadhili wake kama akina Karamagi, Rostam, Manji na Reginald Mengi wameanza kumnunia na kwamba tangu juzi, baadhi yao hawajapiga hata simu kumsalimia tofauti na hapo awali ambapo kila mara walikuwa wanapiga simu kujuliana hali na kubadilishana mawazo. Jambo hili linamtatiza sana Lowasa.

2. HATMA YA MAISHA YAKE BAADA YA KUKATWA.
Lowasa alikuwa na uhakika wa asilimia 100 kuwa ndiye Rais ajaye. Ubongo wake aliutune usipokee aina nyingine ya maisha tofauti na majukumu ya mkuu wa nchi. Kitendo cha kukatwa hata kabla ya kuingia tano bora, hakika kinamnyima raha sana.

3. KUKIMBIWA NA WATU WALIOKUWA KARIBU NAYE.
Baadhi ya watu ambao mara zote walikuwa karibu naye inasemekana kuwa wamemkimbia. Miongoni wa watu hao ni pamoja na Emmanuel Nchimbi, Hamisi Mgeja, Jerry Slaa, Sophia Simba, Adam Kimbisa, Apson Mwang'onda, Mohamed Abdulaziz, Kingunge Ngombale Mwiru, Msukuma na wengineo wengi. Eneo ambalo amepoteza watu wengi ni kanda ya ziwa ambako aliwekeza fedha nyingi. Hakika kitendo cha watu hao kumkimbia ni pigo kubwa sana kwake. Sasa anakumbuka msemo wa kiswahili kwamba mgaa gaa namupwa hali wali mkavu. Kumbe waru wale hawakuwa na mapenzi mema kwake na kilichokuwa kinawapeleka ni fedha zake tu. sasa bahari imekauka wameamua kuikimbia lwani na kwenda kuishi bara.

4. MATAMSHI YA BAADHI YA WAFUASI WAKE KUMUUNGA MKONO MAGUFULI.
Baadhi ya wafuasi wake wamenukuliwa wakitoa matamshi ya kumuunga Mkono Mgombea wa CCM, JOHN POMBE MAGUFULI. Miongoni mwao ni Emmanuel Nchimbi ambaye ndiye alimuandaa kuwa Waziri Mkuu wake. Watu hao wamesikika wakisema kuwa hawana budi kumuunga Mkono Magufuli kwa vile anauzika kuliko wagombea wengine waliochukua fomu. Maneno hayo yamemkasirisha sana Lowasa na yanaendelea kumtesa kila akisoma kwenye mitandao ya kijamii. Ina mana yeye Lowasa hauziki?

5. WANACHAMA WALIOMDHAMINI WAKATI WA KUOMBA RIDHAA YA CHAMA
Lowasa alipata wadhamini zaidi ya laki nane na hivyo kuwa kinara kuliko wagombea wengine. Mgombea aliyepata wadhamini wachache, Magufuli ndiye kaibuka kuwa mshindi. Hilo linamtesa sana Lowasa. Kinachomsumbua zaidi ni zile pesa alizotumia kuwapa wadhamini hao. Lowasa anajua kuwa wadhamini hao wanajua siri hiyo na wakati wowote wataiweka hadharani. Ikiwa siri hiyo itawekwa hadharani, ni wazi kuwa ataendelea kuumbuka na hata kama atahama chama, huko atakakoelekea hatakuwa wa maana tena.

Kuna orodha ya mambo mengi sana yanayomtesa Lowasa. Hata hivyo, kukaa kimya anaona kuwa siyo suluhisho kamili. Njia anayoona muafaka ni ile aliyotumia awali. Yaani kuitisha press conference na kutoa ya moyoni. Yaani kati ya wagombea wote 38 waliorejesha fomu, huyu pekee ndiye anayeteseka baada ya kukatwa. Wengine wametulia tulii na wamekubaliana na matokeo. Hata hasimu wake kisiasa Benard Membe na hata Sammuel Sitta wameamua kukaa kimya na kutokuwa waropokaji. Wameheshimu maamuzi ya vyombo halali vya chama vilivyoundwa kwa kazi hiyo. Kazi ya KUKATA waliochukua fomu kwa vile masharti ni kwamba kuwe na wagombea watano tu wanaoenda NEC.

Kwa kumalizia, nawakumbusha Msemo wa JK kwamba UKITAKA KULA KUBALI NA WEWE KULIWA. Ndicho kinachomtesa hasa Lowasa. Kala sana vya watu na sasa anahofia kuliwa. Anajua kuwa watu kama akina Karamagi, Manji, Rostam hawatakubali kuona fedha zao zimeteketea. Lazima zirudi kwa njia yoyote ile.

JF...

Pesa Aliyolipwa Diamond Platnumz Baada ya Video yake Kuchezwa kwenye TV ya Marekani.

$
0
0
Ni utamaduni wa kawaida kwenye nchi zilizoendelea au nchi kubwa duniani Wasanii kulipwa pesa kutokana na nyimbo zao kuchezwa kwenye TV na Radio ambapo hii imemtokea Mtanzania Diamond Platnumz baada ya wimbo wake kuchezwa kwenye TV maarufu kwa burudani, BET ya Marekani.

Tazama hii video hapa chini ujue hizo milioni alizozichukua Diamond.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumanne ya July 14

$
0
0























Habari  Zilizopo  Katika  Magazeti  ya  Leo  Jumanne  ya  July  14

Mwigizaji Riyama Ally Alazwa..Aombe Mwenye Dawa ya Gonjwa Lake Linalomsumbua Ajitokeza na Kumtibu

$
0
0
Alhamdulilah sijambo kiasi na mshukuru MUNGU NINA MALARIA WADUDU WAWILI na tumbo la chango chamoto nimekiona kwa muda mfupi tu waungwana wangu mwenye dawa nzuri ya tumbo la chango tusaidiane dah nimebebwa wallah nguvu zote kwisha asante sana kwa familia yangu na kwa mume Wangu mtarajiwa @leomysteriotz pia shukran kwa Mikumihospital Mungu awajazekheri ishalah Amin duwa zenu vipenzi vyangu

Riyama Ally on instagram
Viewing all 104756 articles
Browse latest View live




Latest Images