Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104709 articles
Browse latest View live

This is What Zari Post On Her Instagram Account....

$
0
0

This is What Zari Post On Her Instagram Account....



Mr Blue: Siwezi Kueleza Jinsi Ninavyompenda Mke Wangu

$
0
0
Diamond Platnumz hana maneno ya kuwaeleza walimwengu ili wajue ni kwa kiasi gani anampenda mchumba wake, Zari the Bosslady. Lakini inaonesha kuwa siku za hivi karibuni wanawake wamekuwa na mchango mkubwa zaidi katika ustawi wa maisha ya wapenzi wao. Mr Blue pia hana maneno ya kueleza ili watu waelewe anavyompenda mke wake Wahyda.

Blue amepost picha Instagram akiwa na mke wake huyo na kuandika,” Morning ig…@wahyda_bysers_heart …siwezi kuelezea jinsi gani nampenda mke wangu….##kumekucha#lifeisgud.

Hivi karibuni Mr Blue byser alitangaza hadharani kuwa sasa sio mfuasi tena wa vilevi vya aina yoyote, na ashukuriwe mke wake kwa kuwezesha hilo. Kupitia akaunti yake ya Instagram, hit maker huyo wa ‘Pesa’ alikiri kuwa sasa ana furaha zaidi baada ya kufanikiwa kuacha kuvuta bangi, sigara (fegi) mirungi na pombe. Alimshukuru mama mtoto wake kwa kumwezesha kuacha kutumia vilevi hivyo.

Hiki ndicho aliandika Blue:

Alhamdulilahi ..nimeamka salama nikiwa mwenye furaha ahsante mungu ..na nashukuru pia kwa kufaulu mtihani ahsante mke wangu@wahyda_bysers_heart kwa kunifanikisha kuacha vilevi vyote..(bangi, fegi, mirungi, pombe) na kuishi km binadamu wa kawaida..nawashauri ndugu zangu kuwa makini na marafiki wengine wapo kwa ajili ya kukuharibia maisha yako ..kuwa makini… “

Kenyan socialite Vera Sidika buys herself 2015 Range Rover Sport as a birthday present

$
0
0

Popular Kenyan socialite Vera Sidika is making headlines again! She has acquired the 2015 Range Rover Sport as her own early birthday present.

The controversial socialite unveiled the new ride through her social network accounts with the caption:
“Bought myself an early Birthday present. From me to me. Single girl problems. #RangeRoverSport2015 #Grateful”

On another post she wrote:

“Expect more from yourself…not others! Because if you succeed, you will be happy! But if you fail, you will be wiser! Remember that the only people who never fail are the ones who never try to succeed! God will surely Bless those of us who take actions with Good intentions 🙏 👑QVB👑”

Shilole na Nuh Mziwanda Kwenye HekaHeka ya Leo, Wana Ugomvi?…(Audio)

$
0
0
Shilole na Nuh Mziwanda wameachiaSingle yao inayojulikana kama ‘Ganda la Ndizi’ kabla ya kutoa wimbo huo walionekana kama kutofautiana kwenye mtandao wa kijamii wa @Instagram huku kila mmoja akiweka ujumbe wa kumkashifu mwenzake.

Hekaheka ya leo imefanya mahojiano na wawili hao na kuamua kuzungumzia utata wao ambao ulizua gumzo kwenye mtandao wa Instagram.

Shilole amesema hawakuwa wamegombana lakini wanashukuru kwa support ya mashabiki wao katika kukuza muziki wao.

Shilole anasema waliamua kufanya hivyo kama sehemu ya kuutangaza wimbo waohuo mpya unaoitwa.

Wasikilize hapa mtu wangu…

Amini Aipuuzia imani Kuwa Msanii Akioa Hushuka Kimuziki

$
0
0
Msanii na mtunzi wa nyimbo za Bongo Flava, Amini amesema haamini kuwa msanii akioa hushuka kimuziki.

Amini ameiambia Clouds FM kuwa anashukuru kumpata mke ambaye wanaendana katika kazi zake.

Unajua kila mtu ana mtazamo wake, wengi wanasema hivyo kuwa msanii ukioa unashuka. Hapana kwangu nakataa na mimi sijaoa useme labda muuza duka au ana dili na mambo mengine, ila nimeoa msanii tena mke wangu ana kipaji kikubwa tu hasa cha kuandika,” amesema Amini.

Sasa kwa upande wangu mimi amekuwa akinisaidia sana na kunishauri hasa katika suala la uandishi. Nadhani hiyo ni mitazamo tu ya watu wengine. Unajua kutosikika kwangu mara kwa mara ni sababu muziki ni lazima kupeana nafasi. Hatuwezi wasanii wote kutoa nyimbo pamoja.”

Sijui kwanini watu wamepaniki baada ya kuona mjengo wangu – Linah

$
0
0
Linah Sanga amejikomboa kwa kukaribia kukamilisha mjengo wake japo anadai watu wengi wamekuwa wakijaribu kumkatisha tamaa.


Linah alifanya ukaguzi kwenye nyumba yake inayoendelea kujengwa

Muimbaji huyo ameiambia Bongo5 kuwa haikuwa rahisi kujenga nyumba hiyo kutokana na kipato chake kidogo na hivyo kuamua kuijenga taratibu.

“Yeah ile ni nyumba yangu, ipo Mbezi sehemu moja inaitwa Mpiji Magoe,” amesema. “Ile sio nyumba ambayo natarajia nitaishi mimi, nataka kuifanyia biashara halafu nijenge nyingine ambayo itakuwa maalum kwaajili ya kuishi. Naona watu wengi kama wamepaniki, ile nyumba nimejenga kidogo kidogo mpaka pale ilipofika na ikiisha tu ile naanza yangu,” ameongeza.

‘Nimekuwa nikiijenga taratibu, nikipata milioni mbili nanunua tofali mpaka inakamilika. Unajua watu wengi kwenye mitandao wapo kwaajili ya kuku-challenge, mimi ninaweza nikawa nimechukia na kukata tamaA lakini nagundua hawa watu wapo kwaajili ya kutukatisha tamaa. Lakini unaamka na nakusonga mbele nikihakikisha nakipata kile nilichokipanga.”

Kwa upande mwingine Linah amesema ataachia video yake mpya wiki ijayo.

Wanaume wa Dar es Salaam Katika Kashfa Nyingine Tena Baada ya ile ya Panya Road

$
0
0
Mmoja wa Abiria Aliyoshambuliwa Juzi na Mtu Huyo kwenye Daladala
Juzi nilireport hapa kuhusu Mtu mmoja aliyewachoma watu kwa kisu kwenye daladala jijini Dar es Salaam , Sasa leo nimesikiliza clip ya dada mmoja anaeelezea mtu alie choma watu kisu ndani ya Daladala. Eti wanaume watu wazima walikuwa wanakanyagana kukimbia.

Hadi mama mmoja jasiri alipo jitolea na kukishika kile kisu cha mvamizi hadi kikamkata vidole.Eti ndipo wanaume wakajitokeza.

Kweli jamani wanaume wa Dar! Hadi msaidiwe na kina mama!

Aibu iliyoje hii

CHADEMA Kutangaza Mgombea Urais Mwezi Ujao

$
0
0
Chama cha CHADEMA watatangaza mgombea Wa kiti cha urais mapema mwezi ujao.Hii imethibitishwa na katibu mkuu Wa chama.

Chanzo: DW - SWAHILI

Lowassa kutangaza kuhamia CHADEMA Julai 26, Mwembe Yanga ambako Dr Slaa alimtangaza kuwa Fisadi Papa

$
0
0
Zipo tetesi kwamba Edward Lowasa, Waziri Mkuu aliyejiuzulu kwa kashfa ya ufisadi wa Richmond anatarajia kuzungumza na waandishi wa habari Jumapili tarehe 26 Julai 2015 Jijini Dar es Salaam. Katika mkutano huo, Lowasa anatarajiwa kueleza mambo mengi juu ya mchakato wa uchaguzi ndani ya CCM uliopelekea jina lake kukatwa.

Pia katika mkutano huo, Lowasa anatarajiwa kutangaza rasmi kujivua uanachama wake ndani ya CCM na kujiunga na CHADEMA ambapo baadaye jioni ataelekea viwanja vya Mwembeyanga ambako ataungana na viongozi wengine wa CHADEMA kwenye mkutano wa hadharaza. Mtakumbuka kuwa uwanja huo wa Mwembeyanga uliopo Temeke Dar es Salaam ulitumika kutaja orodha ya mafisadi 11 na Katibu Mkuu wa CHADEMA, Wilbroad Slaa mwaka 2007 ambapo jina la Lowasa lilikuwa miongoni mwa majina yaliyopo kwenye orodha hiyo.

Uamuzi wa Lowasa kwenda CHADEMA umetokana na kutimiza makubaliano ya kupeleka shilingi bilioni 10 ambapo fedha hizo zimekabidhiwa Jana Alhamis Tarehe 23 Julai 2015. Aliyekabidhi fedha hizo kwa Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe ni Apson Mwang'onda na makabidhiano yamefanyika kwenye Hotel ya Sea Cliff huku tukio hilo likishuhudiwa na Kingunge Ngombale Mwiru na wengine ambao sitawataja kutokana na sababu maalum.

Taarifa zinasema kuwa kumekuwa na shinikizo kubwa kutoka kwa watu walioathirika na kukatwa kwa Lowasa hasa kutokana na fedha nyingi na muda kwa matumaini kuwa watakuwa "UPPER" baada ya Lowasa kushinda Urais. Miongoni mwao ni pamoja na Prof Juma Kapuya, Nazir Karamagi, Parseko Kone, Mgana Msindai, Kingunge Ngombale Mwiru, Mchungaji Gwajima, Andrew Chenge nk.

Hata hivyo, inadaiwa pia kuwa watu walio karibu na Lowasa akiwemo mfadhili wake mkuu Rostam Aziz ambaye amegoma kutoa fedha za kufadhili harakati za kwenda upinzani wanaendelea kumsihi kuwa asiende huko kwani atakuwa amejimaliza kabisa kisiasa. Pia inadaiwa kuwa mkewe Regina Lowasa amekuwa bitter sana na mpango wa mumewe kwenda upinzani na kwamba kwa siku kadhaa sasa amekuwa akiwafukuza wageni waliokuwa wanaenda nyumbani kwake hasa wale wa upinzani.

Hata hivyo, uamuzi wa Lowasa kwenda CHADEMA unatokana na msukumo wa maslahi binafsi baina ya Lowasa, Freeman Mbowe na wale waliomzunguka Lowasa na kwamba mpango huo ni hatari kubwa kwa ustawi wa CHADEMA. FREEMAN MBOWE anamtaka Lowasa kwa tamaa ya fedha ambapo matamanio yake yamekamilika baada ya kukabidhiwa shilingi bilioni 10 alizohitaji. Hata hivyo, upo uwezekano kuwa fedha hizo zikamtokea puani hasa pale atakaposhindwa kushawishi viongozi wa UKAWA kumteua Lowasa kupeperusha Bendera yao kwa mujibu wa makubaliano ya Lowasa na Mbowe.

Pia mtakumbuka kuwa Lowasa ameenguliwa CCM kutokana na kukiuka kanuni na taratibu za chama huku kashfa za ufisadi zikitumika kama kigezo kikuu cha kuenguliwa kwake. Lowasa huyu anayeenda CHADEMA ni Lowasa yule yule wa Kashfa za Richmond na kwamba CHADEMA wanapokea mtu ambaye taifa limemkataa.

Aidha, viongozi wa CHADEMA wamekuwa na kauli tofauti juu ya Lowasa huku Tundu Lissu na Wilbroad Slaa bila kumsahau Godbless Lema wakiongoza mashambulizi dhidi ya Lowasa. Mathalan, hotuba za viongozi hawa wakati wa Uchaguzi Mdogo wa Arumeru Mashariki ambapo Nassari alikuwa anapambana na Sioi Sumari, Mkwe wa Lowasa zilitawala kashfa za Lowasa na kashfa hizo ndizo zilizopelekea Nassari kushinda. Pia, Dr Slaa amemtaja Lowasa kwenye list of shame na hajajitokeza kwenye vyombo vya habari na kutangaza kuwa amemuondoa kwenye Orodha hiyo.

Vilevile, shinikizo la Lowasa kwenda CHADEMA linafanywa na watu ambao image yao kwenye public ni mbaya. Watu kama Prof Kapuya, Nazir Karamagi, Andrew Chenge na wengineo hakika wanawakilisha kikundi cha watu ambao hawana taswira nzuri kwenye jamii.

CHADEMA wana wakati mgumu sana katika kumnadi Lowasa. Siku zote wamekuwa wakijipambanua kuwa chama chao kinapambana na ufisadi. Inashangaza kuwa wanaojinasibu kuwa wanapambana na ufisadi ndo wanapokea rushwa na wanakaribisha mafisadi kwenye chama chao.

Natambua kuwa CHADEMA wanataka kumtumia tu Lowasa katika uchaguzi Mkuu ujao na baada ya hapo watamtema. Hata hivyo watambue kuwa uamuzi huo si tu utakuwa na athari kwa Lowasa bali hata wao CHADEMA watakuwa wamejimaliza.

Nimalizie kwa kusema kuwa Lowasa huyu ambaye ameonekana mchafu ndani ya CCM hawezi kuwa msafi ndani ya CHADEMA.

Mpenzi Wangu Amenitenda Aaada ya Kujiunga Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam

$
0
0
Nina mpenzi ambaye nilianza mahusiano naye wakati yeye yupo kidato cha Sita shule ya Kajumulo inayomilikiwa na Mama wa hela ya Mboga, Bukoba.

Binti ni Mnyarwanda kwa jina la Ishimimana, kiukweli ni mzuri sana kaenda hewani sekunde ukicheki nyoro inakuita.

Tulipendana sana na tulikuwa tukiongea kila siku jioni,pia nilikuwa nikiongea na marafiki zake sana,mimi nilikuwa Dar na yeye Bukoba.Nilifarijika nikajua ndoto ya kuoa mnyarwanda inatimia.Pesa ndogo ndogo za matumizi nilikuwa nampatia.Ilifika hatua hadi DP ya facebook akaweka picha yangu.

Alimaliza kidato cha sita na kujiunga chuo shahada ya sheria,

Miezi ya kwanza ya chuo mapenzi yalikuwa matamu na ndipo tukapata hata muda wa kula tunda la peponi.Mara ya kwanza sikutaka kumgegeda sababu alikuwa analindwa na sheria ya wanafunzi.

Hali ilibadilika baada ya kuzoea chuo na jiji,mtoto akawa hakamatiki,mapenzi akapunguza,mawasiliano akapunguza.Hostel aliyokuwa anaishi akahama bila kunitaarifu.

Facebook na Instagram akawa anaweka picha anakula bata na matozi na friends zake,picha wanazoweka ni za kuonesha makalio yalivyoumbika,ukweli kama kalio analo tena halisi la kinyarwanda.

Niliumia sana ukizingatia nilimpenda sana,nilipoteza muda wangu kwake lakini sasa hauthamini.

Kilichosababisha niandike uzi huu ni kuomba ushauri nifanye jambo gani niweze kumrudisha kwenye himaya yangu,ukweli nimemiss mapenzi yake,nakiri bado nampenda sana.

Basi hata nikishindwa kumrejesha basi nimshauri kuwa anapotea kwa mambo anayofanya, labda atanikumbuka kwa hilo.

Ushauri wenu ni muhimu

Wakenya Nao Wanadeki na Kusafisha Barabara Ujio wa Obama

$
0
0
Nimeona kwenye taarifa zao za Habari Barabara zinadekiwa, vibanda vinaondolewa omba omba wa mitaani nao marufuku kuonekani Mjini.

Nilidhani ni Sisi.

Ila jamaa zetu wanamuabudu sana Obama, rejea wanavyomzungumzia Ujio wake.

ACT-Wazalendo Kuvuna Wabunge Kutoka CCM na CHADEMA

$
0
0
Baada ya vumbi la uchaguzi mkuu kuanza kumtika tumeona kura za maoni zinazoendelea kupigwa kutoka Chadema na CCM kwenye kila jimbo.

Chadema wanachagua wagombea ili baadae watakapokubaliana na wenzao CUF, NCCR Mageuzi, NLD, itabidi baadhi ya Majimbo wapewe vyama hivyo ambavyo vipo kwenye umoja huo UKAWA.

Na hapo ndiyo utazuka mgogoro mkubwa wa baadhi ya wagombea ambao majimbo yao watapewa UKAWA, hapo ndipo ACT-Wazalendo watakapojipatia wagombea wanaokubalika na kuwasimamisha kama wagombea wa ACT-Wazalendo.

Vile wagombea wa CCM ambao watakatwa pia kuna uwezekano mkubwa wakakimbilia ACT-Wazalendo.

Hapo ndiyo kauli ya Zitto kuwa wagombea hamsini watahamia ACT-Wazalendo itatimia.

Huu ndiyo ukweli ingawa unauma kuusoma hii hali kwenye siasa uwa inatumika sana.

Wale wote waliofanyiwa fitna watatumia mbinu hii ambayo imewahi kutumiwa na Dr.W.Slaa wakati yupo CCM kabla ya kutimkia Chadema na kushinda ubunge.

Wimbo Mpya wa Allykiba Uliovuja, Wageuka Kuwa Hit Song...Usikilize Hapa

$
0
0
Wakuu wimbo huu ambao upo in form of demo, umeendelea kupata downloaders wengi kwenye web na blogs mbalimbali East Africa, na blogs mbalimbali za Nigeria. Wimbo huu unakwenda kwa jina la "School baby" japokuwa hakuwa umekamilika hata balance ya sauti na beat kuwa haijakamilika lakin umegeuka kuwa hit song.

Hongera kingkiba.

http://www.jimmcarter.com/2015/07/usikilize-huu-wimbo-wa-alikiba.html

Wema Sepetu Apigwa CHINI kwenye Kura za Maoni Ubunge wa viti Maalum Singida

$
0
0

Msanii  wa  Filamu  za  kibongo  anayeongoza  kwa  urembo  ndani  ya  tasnia hiyo, Wema Abraham Sepetu, aliyekuwa anagombea Ubunge wa Viti Maalum jimbo la Singida amebwagwa chini baada ya kupata kura 90 tu katika uchaguzi huo. 

Mgawanyo wa kura ulikuwa  hivi;
1. Aysharose Mattembe (311)
2. Martha Mlata(235)
3. Diana Chilolo(182)
4. Wema Sepetu(90)
  

Mwigizaji Lulu Michael Amwambia Wema Sepetu Haya Baada ya Jina Lake Kukatwa Ubunge viti Maalum

$
0
0

Baada  ya  matokeo  ya Ubunge viti maalamu Singida kutoka na Wema Kupigwa chini, Lulu  Michael  amemtia  moyo  Wema  Sepetu  kwa  Kuandika  ujumbe  huu;
  
Kuna matokeo ya aina 3 
>>Kushinda
>>Kushindwa
>>Kudroo. 
  
Mpka hapa ulipofika Leo umethubutu kitu ambacho wanawake wengi ni waoga kujaribu wewe ni mshindi Dada yawezeka Kuna kingine zaidi Mungu amekuandalia 


Shinikizo la Lowassa Kuhamia CHADEMA Lazidi Kupamba Moto......Mkewe Ampigia Magoti Akimsihi Asihame!!

$
0
0

Shinikizo dhidi ya Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa, la kumtaka akihame Chama Cha Mapinduzi (CCM) linazidi kuongezeka na katika timu yake ya ndani ni watu wawili tu wanaonekana kumtaka abakie ndani ya chama hicho.

Habari za ndani ya vikao vya kujadili hatua za kuchukuliwa na Lowassa baada ya jina lake kukatwa kwenye mchakato wa kugombea urais kupitia CCM, zinasema kuwa wandani wake wanaamini kuwa hana atakachopata kama ataendelea kubaki kwenye chama hicho tawala.

"Kaka sikiliza, inavyoelekea shinikizo dhidi ya Lowassa ni kubwa sana. Watu wake wa ndani wanataka aondoke CCM. Wanaona kama amedhalilishwa mno,"kilisema chanzo chetu ndani ya vikao hivyo.

Chanzo hicho kilichoomba kutokutajwa jina kwa sasa, kilisema kuwa watu wake wa ndani wanaamini Lowassa akiendelea kubaki CCM atakuwa amewavunja moyo wale wote waliompigania, hasa vijana waliojaa matumaini ya kumuona akiongoza taifa hili.

Wandani wa Lowassa wanaamini kuwa kama akiamua kujiunga na chama chenye nguvu cha upinzani anaweza kutimiza ndoto yake ya kuwatumikia Watanzania kama rais wa awamu ya tano.

Chanzo chetu kinasema kuwa Lowassa mwenyewe amekwisha kuamua kufanya uamuzi mgumu, ila kuna msuguano juu ya namna ya kuondoka CCM.

Taarifa zaidi zinasema kuwa watu wawili katika timu ya ndani ya Lowassa ndio wanaelekea kuwa na mawazo tofauti. Hawa ni Rostam Aziz, mwanasiasa na mfanyabiashara mashuhuri nchini na mtu mwingine anayetofautiana na mkakati huu mpya wa kung'oka CCM ni mkewe, Mama Regina Lowassa.

Chanzo chetu kinasema kuwa wawili hao wanaamini mapigo ambayo Lowassa amekumbana nayo ni mengi na yanatosha, kwa maana hiyo ingefaa tu apumzike.

"Sijui ni kwa nini RA (Rostam Aziz) anakuwa skeptical (shaka). Si unakumbuka ndiye aliyesema amechoshwa na siasa uchwara... sasa sijui kwa nini anapunguza makali,"chanzo kilisema.

Hata hivyo, vyanzo vyetu vinaongeza kuwa pamoja na upinzani huo Lowassa anadaiwa kuwa amekwisha kuamua na kinachosubiriwa sasa ni muda tu wa kutamka anakokwenda.

Wakati hali ikiwa hivyo ndani ya kambi ya Lowassa, kuna taarifa za kuaminika kuwa kumekuwa na mashauriano baina ya watu wake na viongozi waandamizi wa kambi ya upinzani juu ya mwelekeo wake wa kisiasa.

Mwandani mwingine katika kambi ya Lowassa alisema kimsingi yeye (Lowassa) amekwisha kuamua, anachofanya ni kuona kwamba watu wake wa karibu hawadhuriki na uamuzi wake huo.

Chanzo hicho kilisema kuwa wenye msimamo mkali katika kambi ya Lowassa wanaamini utabiri wa Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere kuwa upinzani utatoka ndani ya CCM utatimia mwaka huu.

"Mnakumbuka ya Mrema (Augustino) alipoondoka CCM siasa za Tanzania zilibadilika mpaka leo? Sasa safari hii ni zaidi," alisema.

Takriban wiki mbili sasa, Lowassa amekuwa na jambo kubwa moyoni analitaka kuwaambia Watanzania.

Mara ya kwanza alikuwa afanye mkutano na waandishi wa habari Julai 13 mwaka huu mjini Dodoma majira ya asubuhi, lakini mkutano huo ukahamishiwa Dar es Salaam ambako pia ukaahirishwa kwa muda usiojulikana.

 

Tangu wakati huo kumekuwa na tetesi kuwa alikuwa atangaze kujiondoa CCM.

Lowassa ni miongoni mwa makada 38 waliojitosa kuwania kuteuliwa kuwa wagombea wa nafasi ya urais wa CCM katika uchaguzi mkuu utakaofanyika Oktoba 25, mwaka huu. 

 

Hata hivyo, jina lake halikuwamo katika orodha ya makada watano waliopitishwa kwenye vikao vya juu vya chama hicho ambavyo mwishowe vilimteua John Pombe Magufuli kuwa mgombea urais atakayekabiliana na wagombea wa upinzani katika uchaguzi mkuu huo.

Easta Bulaya ni Moto wa Kuoteka Mbali........Apata mapokezi ya kishindo Bunda, Amchamba na Kumlipua Wassira

$
0
0

ALIYEKUWA Mbunge wa Viti Maalumu mkoani Mara kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Bi.Esta Bulaya ambaye juzi alitangaza kujiunga na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), amepata mapokezi makubwa Mjini Bunda jana akitokea jijini Mwanza akiwa na viongozi wa CHADEMA mkoani humo na Kanda ya Ziwa.

 

Akiwahutubia wananchi katika Viwanja vya Stendi ya Zamani, Bi.Bulaya aliwapongeza wananchi kwa mapokezi makubwa waliyompa na kumlipua mbunge wa jimbo hilo aliyemaliza muda wake, Bw. Stephen Wassira akisema muda wake wa kukaa serikalini unatosha.

 

Alisema katika Serikali ya Awamu ya Tano, viongozi kama Bw. Wassira hawafai kwani amekuwa Waziri muda mrefu lakini jimbo hilo bado halina maendeleo yaliyotarajiwa na wananchi.

 

"Wazazi wangu mimi ni mwanachama wa CCM na mimi nimekulia ndani ya chama hicho hivyo mkiona nimekimbia, mjue mambo yamenifika shingoni, katika mkoa huu kuna rasilimali nyingi ambazo hazijatumika vizuri ili ziwaondolee wananchi umaskini," alisema.

 

Akizungumzia uwazi na uwajibikaji, alisema viongozi wengi wa CCM hawataki kuwatetea wananchi na kushindwa kuwasimamia watendaji wa Serikali akitolea mfano mradi mkubwa wa maji mjini humo ambao umechukua miaka tisa bila Bw.Wassira kuukamilisha.

 

"Leo hii Wassira atakuja na sera gani kwa wananchi wakati ameshindwa kutekeleza wajibu wake kama mbunge na kiongozi wa Serikali, tuwakatae viongozi wa ngazi zote wanaotokana na CCM," alisema.

 

Aliongeza kuwa, umefika wakati wa majimbo yote mkoani humo kuchukuliwa na wagombea wa CHADEMA ambao watatimiza ahadi zao kwa wananchi na kutatua kero walizonazo.

 

Bi.Bulaya aliweka wazi dhamira yake ya kuwania ubunge wa Bunda Mjini kwa tiketi ya CHADEMA ambapo leo atashiriki kura ya maoni ya kumpata mgombea ubunge wa jimbo hilo kwa tiketi ya CHADEMA.

 

Naye mbunge wa Kahama, Bw. James Lembeli, alidai kuchoshwa na ufisadi uliopo ndani ya CCM na kuwataka wananchi wakubali kuiunga mkono CHADEMA kwa kuwaweka madarakani na kushika dola katika Uchaguzi Mkuu Oktoba 25, mwaka huu.

 

Mbunge wa Musoma Mjini, Bw. Vicent Nyerere, alilitaka Jeshi la Polisi kutoa ushirikiano katika Uchaguzi Mkuu na kuacha kuitetea CCM huku akidai jeshi hilo ni sehemu ya Watanzania ambao wote wamepigika.

OBAMA Tells UHURU and Kenyans to Accept GAYs as the Latter Declares it a Non-Issue

$
0
0


President Uhuru Kenyatta has today let the cat out of the bag by telling US President Barrack Obama that Kenya is a nation that is focused on development and believes that homosexuality is a non-issue.

Responding to an AFP journalist in a joint press conference at State House, Nairobi, tough speaking Kenyatta said though Kenya and US share many values, there are some  that the two countries never shares.

“Kenya and the United States share so many values but there are others that we don't. The gay issue is a non issue,” Uhuru said.

The father of the nation said Kenyans have so many problems to tackle and homosexuality is not one of them.

On whether, Kenya is looking East or West, Uhuru said Kenya is neither looking East of West but looking for progress.

Obama on his part congratulated President Uhuru Kenyatta for his braveness towards fighting corruption which he said has derailed Kenya’s economic growth.

He said his Government will help Kenyatta’s administration in fighting corruption that has infiltrated Kenya’s public and private sectors.


Rushwa ya Ngono iliniondoa Kaole-Batuli

$
0
0
Msanii wa bongo movie Batuli ameweka wazi kuwa alikimbia kundi la Kaole sanaa Group baada ya kukutana na changamoto nyingi ikiwepo changamoto ya rushwa ya ngono, Batuli amefunguka hayo leo alipokuwa katika kipengele cha Kikaangoni kinachofanyika kila siku ya Jumatano kupitia ukurasa wa facebook wa EATV.

Batuli alifunguka na kusema kuwa moja ya sababu kubwa ambayo ilimfanya kuondoka katika kundi hilo ilikuwa kuombwa rushwa ya ngono ili aweze kupewa kipaumbele zaidi kuliko wasanii wengine jambo ambalo kwa upande wake hakuwa tayari kulifanya na kuamua kuondoka katika kundi hilo.

Batuli anasema kabla ya kuweza kutoka kupitia mkono wa Kanumba alishasota sana katika kundi hilo na alikuwa akibaniwa nafasi kutokana na kutokubaliana na watu ambao walikuwa wakimtaka kingono ili waweze kumpa kipaumbele zaidi, ndipo hapo alipoamua kuondoka na baadaye msanii Kanumba ndipo alipoamua kumpa nafasi na kuweza kumtoa kisanaa.

"Nilijiunga kaole lakini baadae Kanumba aliniona nafaa kwenye filamu chini ya kampuni ya Game 1st Quality ndivyo nilivyotoka ila kabla ya hapo nilisota sana kwa sababu ya changamoto mbalimbali ikiwepo kubaniwa kazi, na kutakwa kimapenzi au kuombwa rushwa ya ngono moja ya jambo lililofanya niondoke Kaole ni changamoto ya rushwa ya ngono, nilikutana na changamoto hiyo nilipojiunga na kikundi cha kaole nikaamua kuhama kikundi kabisaa"

"Nilijiunga kaole baadae Kanumba alinishika mkono" Aliongeza Batuli

Mbali na hilo Batuli alisema kuwa kwa sasa yeye ni mtalaka na ana watoto wawili na katika kipindi chake cha ndoa hakuwahi kuchepuka hata siku moja sababu huwa anapenda kutulia na mtu mmoja, na kuweka wazi kuwa katika maisha yake hajawahi kugombanisha wanaume sababu huwa anapenda kuwa na mtu mmoja anayempenda.

"Hapana haijawahi kutokea nimegombanisha wanaume au wanaume wamegombana kwa sababu yangu kwa kuwa huwa sina mahusiano mengi natulia na mmoja"

Tunatambua katika tasnia ya filamu na movie nchini wasanii wengi wamekuwa wakitumia kiki na skendo mbalimbali kama njia ya kujitangaza na kujiongezea umaarufu zaidi katika sanaa husika jambo ambalo kwa Batuli limekuwa kinyume chake yeye anaamini kuwa skendo na kiki zinamfanya msanii adharaulike kila na kushusha heshima ya msanii huyo jambo ambalo yeye ameweza lifananisha na vazi baya au chafu katika tasnia ya filamu na sanaa kiujumla.

"sio kweli huwezi kuheshimika na kuwa na scandal kuwa na scandals kuna mfanya msanii adharaulike kila aendapo naweza kusema scandals ni vazi baya na chafu kwenye tasnia yetu"

Niaje Wasee? Hawayuni? Obama Afungua Mkutano wa GES jijini Nairobi kwa Salamu ya Sheng (Video)

$
0
0
Rais wa Marekani, Barack Obama yupo nchini Kenya kwa ziara ya kwanza ya rais wa Marekani aliyepo madarakani kuwahi kufanyika nchini humo.

Obama amefungua mkutano wa ujasiriamali wa dunia, GES asubuhi hii kwa salamu ya Sheng. “Niaje Wasee, Hawayuni,” aliwasamilia wajumbe wa mkutano huo waliomuangushia shangwe za kutosha.

Jana usiku Obama alishiriki chakula cha usiku na ndugu upande wa baba yake.

Waliokuwepo kwenye dinner hiyo iliyofanyika Villa Rosa kwenye hoteli ya Kempinski jijini Nairobi ni pamoja na bibi yake, Mama Sarah na dada yake Auma Obama.
Viewing all 104709 articles
Browse latest View live




Latest Images