Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104416 articles
Browse latest View live

Ushahidi wa Lowassa Kujiunga Chadema:Kikao cha Kamati Kuu CHADEMA, Edward Lowassa ndani

0
0
Waziri Mkuu Mstaafu wa JMT Mh. Edward Ngoyai Lowassa, akisalimiana na viongozi na wanachama wa CHADEMA

Waziri Mkuu Mstaafu wa JMT Mh. Edward Ngoyai Lowassa akiwa Meza Kuu na viogozi wa CHADEMA

Edward Lowassa ni Msafi, Lakini Kwanini Aliitwa Fisadi?

0
0
Kwa nini lowasa aliitwa fisadi, hii ni kwa sababu yeye kama waziri mkuu, msimamizi mkuu wa serikali alitakiwa akemee inshu zote za richmond, lakini, yeye alipata shinikizo kutoka kwa Mkulu. Ndiyo maana Kuepuka Mkulu asianguke ilibidi Lowasa ajiuzuru. Vinginevyo Mkulu angetawala Miaka mitatu tu, Na serikari yake ingehanguka. Sasa leo Loawasa ataongea Ukweli kuhusu Richmond,ataongea Vitu vyote ambavyo Mwakyembe aliviacha Kuongea katika Riport yake ,Kwa kuilinda Ikulu.Hata Ongea hayo tu, Pia ataongea kuhusu wamiliki Halisi wa IPTL, pia atagusia Mambo ya Escrow ni nani aliyeengeer Mchakato wote wa Escrow, Ataelezea ni nani Anamiliki Kampuni ya Simba Trust, iliyochukua Bilion 75 kwenye Kashifa ya Escrow. Riport yote ya Takukuru ipo hewani kuhusu Esrow. Ndugu yetu Lowasa anatubu na anarudi kundini, Kundi la makamanda, kundi la Kutetea nchi. The same apply hata Pinda angejiuzuru kwenye kashifa ya Escrow naye angeitwa Fisadi. (Tatizo la lowasa ni Kukubali kujiuzuru kwa manufaa ya Serikali ya CCM)

Lowasa atatuambia Fisadi mkuu wa Hii nchi ni nani? Kaeni Mkao wa kura , watu wameshaanza kukimbilia nje ya nchi kuangalia pesa zao kama zipo Salama. Na ninawambia Kuwa SIKU LOWASA ANAAPISHWA RASMI kama RAISI wa nchi hii.

kuna Watu watakimbia hii nchi, kwa sababu Uozo wote utawekwa Wazi ,hatutangalia Mtu,wa cheo chake Sijui alikuwa nani, Wote ni MAHAKANI.

Tutaendelea kuijenga hii nchi, kila mtanzania afaidike na Rasilimali za nchi yake.
Karibu Lowasa, karibu Ukawa.

Ahsanten.
Bintiwangara.

Diamond Amliza Amliza Wema Sepetu Kwa Maneno ya Kejeli

0
0
Wema Sepetu
Musa Mateja
Inasikitisha! Mrembo Wema Isaac Sepetu ‘Madam’ amejikuta akiangua kilio baada ya kupewa maneno ya kejeli na aliyekuwa mpenzi wake, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ kufuatia kupigwa chini kwenye kura za kuwania Ubunge wa Viti Maalum mkoani Singida kupitia Tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM).
wemasepetuMrembo kunako Bongo movie aliyekuwa akiwania ubunge wa viti maalum Ikungi Singida, Wema Isaac Sepetu ‘Madam’.

TUJIUNGE NA CHANZO
Chanzo makini kililiambia Ijumaa Wikienda kwamba, Julai 24, mwaka huu Wema alijikuta akiangua kilio cha aina yake kufuatia maneno ya kumshambulia kutoka kwa watu mbalimbali akiwemo Diamond muda mfupi baada ya kuangushwa katika kinyang’anyiro hicho cha ubunge kilichofanyika katika Wilaya ya Ikugi, Singida.

Kiliendelea kunyetisha kwa sauti ya upole kwamba, miongoni mwa vitu vilivyosababisha Wema kudondosha chozi ni pamoja na maneno ya Diamond aliyoandika muda mfupi tu katika ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa Instagram huku akijua wazi kwamba mwanadada huyo alishapoteza fedha nyingi ili apate nafasi ya kuingia mjengoni, Dodoma.

“Ujue watu wengi hawakujua kilichomuuma zaidi Wema ila mimi kaniambia kwamba, kilichomuuma si kukosa nafasi hiyo ila ni maneno ya Diamond aliyoandika kwenye ukurasa wake wa Instagram maana yamemchoma na hakutarajia kama ‘ex’ wake huyo angefikia hatua ya kuonesha chuki zake wazi kiasi hicho.

“Wema alikuwa na matumaini makubwa ya kuibuka mshindi kwenye mchakato huo kutokana na kujulikana kwake na namna wajumbe walivyokuwa wanampa matumaini ila hali imekuwa ndivyo sivyo.
“Baada ya matokeo, sisi tulimuona akiwa kawaida tu lakini baadaye alibadilika na kuwa mnyonge hali iliyonifanya nimuulize kisa cha kuwa vile ndipo akaniambia maneno ya kwenye mitandao yanamchoma.

KUMBE ALITUMIA FEDHA NYINGI
“Unajua amekuwa wa mwisho kwa kupata kura 90 hivyo ni wazi kuwa hana chake tena katika kuwania nafasi hiyo na alitumia fedha nyingi kwenye kuomba kura kwa wanachama (haikufafanuliwa kivipi kwa madai kwamba alitoa hongo), hawezi tena kuingia mjengoni kwani nafasi tatu zimechukuliwa na wenzake hao, hivyo anachotakiwa kuanzia sasa ni kujipanga ili kama itawezekana baada ya miaka mitano ijayo agombee tena,” kilisema chanzo hicho.
WEMA ANASEMAJE?
Ijumaa Wikienda, kama kawaida yake, baada ya kupata ‘unyunyuzi’ huo lilimtafuta Wema ili aweze kuanika hisia zake baada ya matumaini yake kuishia njiani ambapo alisema kwamba  anaamini kila jambo limepangwa na Mungu hivyo haikuwa bahati yake zaidi ataendelea kujipanga kwa kipindi kingine.
“Namuachia Mungu maana kila jambo hupangwa na yeye, hakuna mtu anayeshindana akashindwa halafu awe ‘happy’ tu, nimeumia isipokuwa Mungu ndiye jibu la kila kitu,” alisema Wema na kuongeza:
“Nilipoamua kugombea nilijua kuna kupata na kukosa. Awamu hii nimekosa lakini dunia inazunguka.
“Nawashukuru wote walionipinga kwa sababu waliniongezea ujasiri.”
Kwa upande wa Meneja wa Wema, Martin Kadinda aliweka ujumbe kwenye ukurasa wake wa Twitter: “Haikuwa vile tulivyotarajia….hongera Aysharose Mattembe.”
Maneno ambayo aliyaposti Diamond yaliyomchoma Wema hadi kufikia hatua ya kumwaga chozi yalisomeka: “Sitaacha kuwashukuru Wanasinginda kwa mapenzi yenu ya dhati mliyonioneshea, Moshi tukutane Kili Home.”
Wema alikuwa ni miongoni mwa wagombea wa Viti Maalum kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM), katika Wilaya ya Ikungi, Singida ambapo mchakato wa kura za maoni ulifanyika Julai 24, ambapo aliambulia kura 90 akishika nafasi ya nne huku mtu wa kwanza Aysharose Mattembe alikipata kura 311, nafasi ya pili ikichukuliwa na Martha Mlata aliyezoa kura 235 na ya tatu akichukua Diana Chilolo kwa kura 182.

SABABU ZA KUSHINDWA
Wikiendi iliyopita mjadala mkubwa kwenye mitandao ya kijamii ilikuwa ni ishu ya Wema kukosa ubunge ambapo miongoni mwa sababu hizo ni skendo mfululizo na picha zisizokuwa na maadili zilizojaa mitandaoni na kwamba CCM kwa sasa ipo kwenye mkakati mkali wa kusimamia maadili ya chama.

Kusambaa Kwa Kauli Hii Ya Eddo Kumwembe Kuhusu Lowassa Ni Pigo Kubwa Kwa CCM

0
0
".....CCM kuongelea ubaya wa Lowassa kwa sasa ni sawa na mtu kujichungulia nyeti zake...Chadema kuongelea uzuri wa Lowassa kwa sasa ni sawa na mtu kujitekenya na kucheka mwenyewe....Vyote vinahitaji uso usio na soni"-Edo kumwembe.

Nimevumilia Nimechoka Bora Niwe Mkweli...Mpenzi Kanikimbia na Mtoto Wangu

0
0
Kuna Vitu Ambavyo Unaweza Kukutana Navyo Katika Maisha Yako ya Kila Siku na Ukavihifadhi Katika Moyo Wako Na Kufanya Siri Kubwa Ambayo Kamwe Hutataka Kumwambia Mtu Yoyote Yule. Katika Maisha Ambayo Nimeishi Hapo Kabla ikiwa Bado Sijakutana na Huyu Mpenzi Niliyenae Sasa Nilibahatika Kuzaa Na Msichana Mmoja Aitwaye Sheila. Alikuwa Ni Msichana Ambaye Nilikutana nae Kibahati Mbaya Sana, Nasema Kibahati Mbaya Sana Kwa Kuwa Mazingira Tuliokutana Yalikuwa ni Mazingira Ya Msaada Zaidi Baada Ya Kumkuta Maeneo Ya Posta Mpya Saa Tano Za Usiku Akiwa Amejiinamia. Sikujua Nikitu Gani Ambacho Kilinisogeza Pale Lakini Nilijikuta Tayari Nikiwa Mbele Yake Huku Nikionyesha Roho Ya Ubinadamu Ikiwa ni Pamoja na Kuuliza ni lipi Tatizo Ambalo Linamsibu. Binti Yule Hakutaka Kunijibu Wala Kunisikiliza Alichokuwa Anakifanya Ilikuwa ni Kunitazama tu na Kunibinulia Mdomo Kwa Dharau Kubwa. Kusema Kweli binti Alikuwa ni Mrembo Sana na Alikuwa Anavutia Sana.. Kijana Nikaona nitangaze Msaada Huku Moyoni Nikiwa na Mipango Yangu Mingine. Kweli Baada Ya Vuta Nikuvute Binti Akakubali Kuondoka na Mimi Kuelekea Kigamboni Ninakoishi Huku Akiweka Angalizo La Kutokumsumbua Tukifika Huko. Mdomoni Nikakubali Lakini Moyoni Nilikuwa Mbali Sana.... Kifupi Siku Hiyo Hiyo Ndio Siku Ambayo tulifungua Ukurasa Wa Penzi Letu Na Tukawa Kama Kumbikumbi Kila Wakati tuko Wote Huku nikiwa Sijui Chochote Kuhusu Alikotoka na Kwa Wazazi Wa Huyu Mwenzangu.

Ndani Ya Kipindi Cha Uhusiano Wote mwenzangu Akapata Ujauzito Ambao Kila Mmoja Aliufurahia Sana Huku Mapenzi Yetu Yakiongezeka Maradufu. Sasa Kilichonifanya Kuja Hapa Kwenu Wanajamvi Wenzangu Ni Kwamba Licha Ya Kumhudumia Kwa Kila Kitu Kama Mwenza Wangu Lakini Baada Ya Kujifungua Binti Akanambia Alichokuwa Anakitaka Ameshakipata Hivyo Nisimjue na Nisimfuatilie Tena.... Mwanzo Niliona Ni Kama Utani Lakini Baada Ya Siku Chache Akatoroka na Mtoto Mimi Nikiwa Kazini na Hata Niliporudi na Kuwauliza Majirani Hawakuwa na Jibu La Maana. Na Hata Namba Zake Za Simu Kila Nikipiga Hazipatikani Tena Lakini kuna Siku NIlitumiwa Sms Kwa Namba Ngeni Akinipa Hongera Ya Kumpatia Mtoto... Lakini Nilipoipiga Haikupatikana na Mpaka Leo Haipatikani..... Ombi langu Kwenu Wanajamvi Wenzangu Nifanyeje Niweze Kuipata Damu Yangu? Imefikia Kipindi Nahitaji Kumuona Mwanangu Lakini Sijui Wapi Nitampata Huyu Mwanamke.

Msaada Wanajamvi Wenzangu

Mwanamuziki Jennifer Lopez asherehekea bethidei yake na kinguo cha ajabu

0
0
MWANAMUZIKI na mwigizaji, Jennifer Lynn Lopez ‘JLO’ mwishoni mwa wikiendi alisherehekea miaka 46 ya kuzaliwa kwa kutupia kinguo kilichoacha sehemu ya maungo yake wazi na kumfanya aonekane binti wa miaka 20.
Sherehe hiyo ya miaka 46 ya staa huyo ilifanyika huko Hamptons nchini Marekani. Katika sherehe hizo, JLO aliambatana na mpenzi wake mwenye miaka 28 aitwaye Casper Smart sambamba na French Montana.

Upepo Umegeuka, Marafiki wa Lowassa Wapinga Swahiba wao kwenda CHADEMA, Apson Matatani

0
0
Kambi ya Lowasa kwa sasa tumbo joto kutokana na mgawanyiko mkubwa uliojitokeza. Kambii hiyo imegawanyika na kuzaa timu mbili. Timu ya kwanza inaundwa na wastaafu akiwemo Apson Mwang'onda na viongozi wa CCM wa Mikoa na wilaya. Wengi wa wanaounda kundi hili ni wachovu kifedha na wanaishi kwa kutegemea Marafiki wa Lowasa.

Timu ya Pili inaundwa na Marafiki wa Lowassa ambao ndio wenye fedha. Taarifa za uhakika kutoka kambi hiyo zinasema kuwa Marafiki wa Lowasa wakiongozwa na Rostam Aziz pamoja na Mke wa Lowasa Regina Lowasa hawataki rafiki yao aende upinzani. Hoja wanazotoa ni pamoja na hizi zifuatazo;

1. Marafiki wa Lowassa wanasisitiza kuwa Apson Mwang'onda ni mpotoshaji. Kwamba, ni Apson ndiye aliyetoa ushauri mbaya kwa Lowassa mpaka akapoteza muelekeo ndani ya CCM hali iliyosababisha jina lake kukatwa katika hatua za awali. Kwamba, Apson alikuwa anawahakikishia kuwa hakuna mwenye jeuri ya kukata jina la Lowassa na kwamba wakithubutu kufanya hivyo hapatakalika. Hata hivyo, kilichotokea ni kinyume chake.

2. Vyama vya upinzani havina dhamira ya dhati kwa Lowasa. Wao wanachokihitaji ni fedha zake na mashabiki wake ili waongeze idadi ya viti vya wabunge na kura za Rais. Kwamba, siku zote vyama hivyo vilikuwa vinamtukana Lowassa na kumtolea kila aina ya maneno machafu. Sasa wanashangaa vyama hivyo hususan CHADEMA wanamuona Lowassa kama malaika.

3. Marafiki wa Lowasa wametumia fedha nyingi wakati wa mchakato ndani ya CCM. Lowasa aliwahakikishia kuwa atabaki ndani ya chama na kwamba hata asipoteuliwa kupeperusha bendera hatahama chama na badala yake atatafuta haki ndani ya chama hicho. Hata hivyo, wanashangaa kuona rafiki yao akiendelea kukaa kimya badala ya kuchukua hatua ndani ya chama kama alivyoahidi. Kwamba, tangu jina lake likatwe, hajachukua hatua stahiki ikiwa ni pamoja na kupeleka malalamiko kwenye vyombo husika. Kutokana na hali hiyo marafiki hao wanaona kuwa uamuzi uliochukuliwa na chama ulikuwa ni sahihi isipokuwa rafiki yao alikuwa na agenda ya siri kwa kushirikiana na Apson Mwang'onda.

4. Wafuasi wengi waliokuwa upande wa Lowassa wameridhika uteuzi uliofanywa na CCM ambapo wamemteua John Magufuli kuwa Mgombea Urais. Wanasema kuwa wao walichokuwa wanahitaji ni CCM kumteua mtu mwenye maamuzi na mwajibikaji. Magufuli ana sifa zote walizohitaji. Hivyo wanasema kuwa Lowasa asijidanganye kuwa wafuasi wake watamfuata upinzani.

Kutokana na hoja hizo, marafiki wa Lowassa wamesema kuwa hawapo tayari kuendelea kupoteza fedha kumgharamia mtu ambaye hana msimamo. Hata hivyo, wanasema kuwa wapo tayari kumsaidia Lowasa kwa namna atakayotaka ikiwa atafanya maamuzi ya kuachana na siasa.

Kundi la Apson Mwang'onda kwa upande wake linasisitiza kuwa ni lazima Lowassa aende upinzani ambako ameahidiwa kupata nafasi ya kuwa mgombea Urais. Kwamba, hata kama Lowasa hatachaguliwa kuwa Rais, atakuwa amewatuliza wafuasi wake ambao wamepoteza muda na fedha nyingi kumfikisha hapa alipo.

Mvutano huo umemuacha Lowassa njia panda. Afuate ushauri wa marafiki zake ambao wamemsaidia kwa kila hali na kwamba wameahidi kumsaidia katika maisha yake nje ya siasa au kuendelea kushikamana na Apson ambaye siku zote amekuwa akimponza kutokana na ushauri wake.

Kutokana na hali hiyo, Lowassa ameshindwa kukamilisha deal lake na CHADEMA kama alivyopanga na badala yake anaendelea kuwapiga danadana huku akiwaacha tumbo joto.

Ni dhahiri sasa kuwa Lowasa atafuata ushauri wa marafiki zake kuliko ushauri wa Apson. Katika hili, mchango wa Rostam unaonekana dhahiri na anaonekana kuwa ndiye rafiki wa dhati wa The White Hair. Wengine walikuwa kimaslahi zaidi.

Tetesi: Rais Kikwete Apigiwa Simu Ya Dharura Arejee Ofisini

0
0
CCM walipoambiwa hawawezi kuzuia mafuriko kwa mkono walidharau,Sasa manyunyu yameanza wanaanza kukimbia ovyo ovyo.

Ni vema kama ni watu majasiri wasubiri mafuriko kamili na ndipo tuone wanakabiliana nayo vipi.

Taarifa zilizopo kwa sasa ni kuwa Lumumba hapakaliki tena,Kila mtu anamtupia lawama mwenzake,JK nasikia kapigiwa simu ya dharura arejee kuokoa jahazi.

LOWASSA Atua Rasmi CHADEMA.......Kutangazwa Muda Wowote Ndani ya Wiki Hii

0
0
Mpango wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kumtangaza kada wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Edward Lowassa, kujiunga na chama hicho uliotarajiwa kutekelezwa jana, umekwama huku kukiwa na taarifa za mgawanyiko ndani ya Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa).

Wiki iliyopita, Mtandao huu uliandika taarifa kwamba Chadema walipanga kumtangaza Lowassa Jumapili ya jana baada ya kumaliza mazungumzo naye, lakini hilo lilishindikana.

Taarifa kutoka ndani ya Chadema zinadai kuwa huenda kada huyo ambaye mustakabali wake ndani ya CCM uliingia dosari baada ya jina lake kuondolewa alipokuwa akisaka urais, sasa huenda akatangazwa rasmi wakati wowote wiki hii.

“Kwamba anakuja Chadema hiyo si siri tena, lakini ule mpango wa kumtangaza leo (jana) haukufanikiwa kutokana na kuwapo kwa vikao tofauti muhimu vya vyama viwili ndani ya Ukawa, Chadema na CUF,” alisema mtoa habari wetu ndani ya Chadema.

Jana, Chadema waliitisha mkutano wa dharura wa Kamati Kuu jijini Dar es Salaam wakati ambapo CUF nao walikuwa na mkutano wa Baraza Kuu huko Zanzibar, wote wakijadiliana suala moja tu; urais ndani ya Ukawa.

Vikao hivyo vilivyogubikwa na usiri mkubwa vilitarajiwa kumalizika jana mchana na kisha jioni wenyeviti wenza wa Ukawa walipanga kuzungumza na wahariri wa vyombo vya habari, lakini mkutano huo uliahirishwa kutokana na kushindwa kumalizika kwa wakati vikao hivyo nyeti.

Akizungumza na mtandao huu jana, Mkurugenzi wa Habari wa CUF, Abdul Kambaya, alisema kwa ufupi kuwa kilichokuwa kikijadiliwa na chama hicho kitawekwa hadharani leo, huku Makamu Mwenyekiti wa Chadema Zanzibar, Said Issa Mohamed naye akisema: “Tutawafahamisha kinachozungumzwa baada ya kikao kumalizika.”

Watu wa karibu na CUF wanadai kuwa uongozi wa juu wa chama hicho, hasa Mwenyekiti Profesa Ibrahim Lipumba, hadi jana hakuwa akiafiki ujio wa Lowassa Ukawa.

“Sijui itakuwaje lakini kama msimamo wa Profesa ukiendelea hivi, sioni namna gani CUF itaendelea kuwamo ndani ya Ukawa. Kwanza kura ambazo huwa anazipata kwenye urais nazo ni muhimu sana kwani husaidia chama kupata ruzuku.

“Sasa iwapo hatagombea na labda akagombea Lowassa kupitia Chadema ndani ya Ukawa, basi suala la ruzuku litaleta balaa kwani ndizo fedha zinazosaidia kuendesha ofisi za CUF Tanzania Bara,” alisema mwanachama mmoja wa CUF, akizungumzia utata uliokigubika chama hicho unaohatarisha maisha ya Ukawa kuelekea kwenye Uchaguzi Mkuu Oktoba mwaka huu.

Kwa upande wa Chadema, mtandao huu ulihakikishiwa jana kuwa wao hawana shaka na ujio wa Lowassa, wakiandaa mazingira ya kumsafisha mbele ya wananchi kwa madai kuwa kilichofanya aonekane mchafu ni mfumo ndani ya CCM na wala si yeye kama Lowassa.

Ingawa kumekuwapo madai kuwa wanafamilia ya Lowassa na marafiki zake wachache wamekuwa wakimshauri kutohama CCM, lakini Lowassa ndiye mwenye uamuzi wa mwisho na kwamba mmoja wa rafiki zake wakubwa na mfanyabiashara maarufu nchini amewahi kusikika akikiri kuwa ameshindwa kumshawishi rafiki yake huyo kubaki CCM.

Hii ndio sababu iliyofanya Mbunge Andrew Chenge hajafika leo kuhojiwa na Kamati ya Maadili Dar…

0
0
Andrew Chenge
Ni zaidi ya miezi saba imepita toka Bunge litoe mapendekezo kwamba wahusika wote wa ishu ya ESCROW wawajibishwe, kazi ikaanza kwenye Kamati ya Maadili ambapo Viongozi mbalimbali walianza kuhojiwa ikiwemo Mbunge Anna Tibaijuka, Andrew Chenge na William Ngeleja.

Kwa upande wa Andrew Chenge Kamati hiyo ilisimamisha kumhoji kwa vile alikuwa amepeleka ombi Mahakama Kuu kuzuia kuhojiwa, baadae Mahakama hiyo ikatoa amri kwamba Kamati ya Maadili inaweza kuendelea na kumhoji.

July 27 2015 ilikuwa Mbunge huyo afike kwenye Kikao cha Kamati ya Maadili Dar kwa ajili ya kuhojiwa na kuhusika kwake kwenye ishu ya ESCROW, lakini ripota wa millardayo.com kafika kwenye Ofisi za Kamati hiyo.

Mbunge huyo hakufika na taarifa iliyotolewa ni kwamba Andrew Chenge ameomba Kamati ya Maadili ipeleke mbele tarehe ya kusikiliza shauri lake kwa vile ratiba hiyo inaingiliana na majukumu yake ambayo CCM imemkabidhi Jimboni kwake Bariadi Magharibi wakati huu wa maandalizi ya Kampeni za Uchaguzi Mkuu 2015.

Shuhuda KITUKO CHA Rais Obama Alichokifanya Alivyoondoka Nchini Kenya

0
0
RAIS wa Marekani, Barrack Obama leo jioni amekamilisha ziara yake ya siku tatu nchini Kenya ambapo alifungua kongamano la kibiashara, akawahutubia Wakenya katika Uwanja wa Kasarani na baadaye kuzungumza na viongozi wa mashirika ya kijamii katika Chuo Kikuu cha Kenyatta. :

What This Curvaceous Kenyan LADY Did To Her Boyfriend Will Leave You Shocked (VIDEO)

0
0

To all those who claim that Kenyan ladies don’t know how to shake it, there’s this hot video of a Kenyan lady shaking her assets vigorously for her boyfriend in their  room.

The s3xy lady can give the likes of Vera Sidika and Huddah a run for their money with her s3ductive moves that are irresistible.

Just click play and watch her doing it.

MEN Only! This Private VIDEO Of a Hot LADY Doing Bad Things is a Must Watch

0
0

Let’s put aside those twerking videos from local socialites like Vera Sidika and her fellow city socialites. There’s this bootylicious lady who was caught on camera doing “bad things” in her room.

The well endowed lady left little for imagination as she displayed her madness infront of the camera.  Just observe privacy and see what she did.

Have You Ever Salivated on a Pregnant Woman? Just Look at ZARI (PHOTOs)

0
0

Despite her pregnancy, aging Ugandan socialite, Zari Hassan, has managed to maintain her s3xiness. Unlike most pregnant women who dress in boring maternity dresses, Zari always kills it and most men can’t get enough of her gorgeous body.

Below are some of her pregnancy photos that will leave men salivating.




Lowassa Akaribishwa Rasmi UKAWA......Hapa kuna picha na kilichojiri Leo Katika mkutano wa UKAWA na Waandishi wa habari

0
0
“Watanzania wanataka mabadiliko, wasipoyapata ndani ya CCM watayatafuta nje”. Hii ni moja ya kauli  ambayo Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Monduli, Edward Ngoyai Lowassa aliziongea Arusha May 30 2015 alipotangaza nia ya Kugombea Urais kupitia CCM.
CCM ilikuwa na Wagombea zaidi ya 40 ambao walitangaza nia na kuchukua fomu za Kugombea Urais 2015 lakini baadae Chama hicho kikampitisha Dk. John Pombe Magufuli kugombea nafasi hiyo, baada ya hapo kukawa na  taarifa nyingi sana kuhusu ishu ya Edward Lowassa na UKAWA.
Viongozi wa Umoja wa UKAWA wamekutana Dar  leo  na mmoja wa Viongozi hao, James Mbatia amesema wamekubaliana kumkaribisha Mbunge Edward Lowassa ndani ya UKAWA na wako tayari kumpa nafasi na kushirikiana nae.
Mbatia  ameongeza kuwa Lowassa ni mchapa kazi makini na mfuatiliaji wa karibu wa kiutendaji katika majukumu anayokabidhiwa.

Alipoulizwa kuwa Lowassa atakuwa mgombea Urais Mbatia amesema kila chama kina utaratibu wake  hivyo mchakato ukishakamilika  atatangazwa mgombea urais wa UKAWA mmoja  mwanzoni mwa mwezi agosti.

While Lowassa and Ukawa is Trending everywhere on Social Media… Here are Magufuli’s Recent Messages on Twitter to You

0
0
While everyone on the social Media is talking about Lowassa and his “Unexpected” decision to join UKAWA, here are the most recent tweets from Hon. John Pombe Magufuli


Shindano la Big Brother Africa kutofanyika mwaka huu?

0
0
Kuna uvumi uliosambaa kuwa reality Tv show ya Big Brother Africa (BBA) ambayo huziunganisha nchi mbalimbali za Africa haitafanyika mwaka huu.

Meneja wa Multichoice Ghana, Anne Sackey amethibitisha uvumi huo na kusema kuwa ni kweli Multi Choice Ghana wamepokea ujumbe kutoka MNET kuwa shindano hilo halitafanyika mwaka huu.

Sackey ameongeza kuwa MNET hawakutoa sababu za kusitisha msimu mpya lakini yeye binafsi anahisi ni kutokana na ukosefu wa wadhamini.

Hata hivyo, watu wengi wanaamini kuwa hii inaweza kuwa ni ‘public stunt’ ya kuwaandaa watu na msimu mpya.

Picha: Zari the Bosslady Aonesha Ujauzito Wake Ulivyokua Kwa Mipasho ya Haja!

0
0
Zari The Bosslady ameshakuwa mswahili na huenda Taarab ikawa ni muziki anaousikiliza sana kwa sasa. Hiyo imeonekana kwenye picha nne alizopost (moja akiwa na mchumba wake, Diamond Platnumz) kwenye mtandao wa Instagram kuonesha jinsi ujauzito wake ulivyokuwa mkubwa. Tazama picha hizo na kile alichoandika.
11260430_123341838006995_1936020447_n
Alichoandika: Namaumivu yakizidi………. Wishing you all blessed week ahead, Good nyt
11373653_943084819082779_1562587470_n
Alichoandika: They say when you have it, flaunt it. Kwani kuna mtu kaibiwa??? Keeping it sexy and classy. #BabyBumpPhotoShoot
11351999_104770406541206_1765468179_n
Alichoandika: Kwa raha zetu…… vaeni madera, fungeni mikanda mpite kimya kimya Keeping it sexy and classy
11352117_525804417568038_2127135778_n
Alichoandika: Keeping it sexy and classy. #BabyBumpPhotoShoot


Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumanne ya July 28

0
0























Hapa nimekuwekea Habari  Zilizopo  Katika  Magazeti  ya  Leo  Jumanne  ya  July  28 kwa Ufupi kwa Kupitia kurasa za mbele za magazeti hayo...
Tembelea kila siku website yetu uweze kupata habari zinazo make headlines kila siku bila kukosa

IKULU Yaukana Mshahara Wa Rais Kikwete........Yasema Gazeti La Mwananchi Limepotosha

0
0
Gazeti la Mwananchi la Jumatatu, Julai 27, 2015, kwenye ukurasa wake wa 26 limechapisha habari yenye kichwa cha habari, “Marais watano wanaotajwa kuongoza kwa mishahara minono barani Afrika ni hawa hapa”.

Katika habari hiyo ambayo gazeti hilo linadai chanzo chake ni “uchambuzi wa mtandao wa African Review” inadaiwa kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete, anashilikia nafasi ya tano miongoni mwa viongozi 38 wa nchi za Afrika wanaolipwa mshahara mnono zaidi.

Gazeti hilo linadai kuwa Rais Kikwete analipwa Dola za Marekani 192,000 kwa mwaka, ikiwa ni malipo ya Dola za Marekani 16,000 kwa mwezi.

Habari hizi siyo za kweli. Ni uongo na uzandiki. Ni uzushi mtupu na ni uzushi wa hatari.

Mshahara wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa mwezi ama kwa mwaka haufikii na hata wala kukaribia kabisa kiwango kinachotajwa na Gazeti la Mwananchi.

Tangu Uhuru, mwaka 1961, Rais wa Tanganyika na baadaye tangu mwaka 1964 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania amekuwa miongoni mwa viongozi wanaolipwa mishahara ya chini kabisa duniani.

Mshahara wa Rais wa Tanzania kwa mwezi ni wa chini kiasi cha kwamba mshahara wake unazidiwa, tena kwa mbali, na mishahara wanayolipwa baadhi ya watendaji wakuu wa baadhi ya taasisi za umma nchini.

Aidha, ni jambo la kushangaza kwamba Gazeti la Mwananchi, linalochapishwa hapa nchini, linaweza kupata kiasi cha uongo anacholipwa Rais wa Tanzania katika mitandao ya nje badala ya kuuliza rasmi na kupewa majibu sahihi.

Kwa kujiingiza katika uzushi wa kupindua kiasi hiki, Gazeti la Mwananchi haliwezi kuwa na nia nyingine yoyote isipokuwa nia ya kuwachochea wananchi na kuwajengea chuki dhidi ya Serikali yao na Kiongozi wao Mkuu.

Ni matarajio yetu, kuwa Gazeti la Mwananchi litafanya jitihada za makusudi, kama taaluma ya uandishi wa habari inavyoelekeza, kutafuta usahihi wa jambo hili na kuwaambia Watanzania ukweli.

Imetolewa na;

Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu – Dar es Salaam.
27 Julai, 2015
Viewing all 104416 articles
Browse latest View live




Latest Images