Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104789 articles
Browse latest View live

Bond: Jamani Nibembelezeeni Wastara Nimuoe!

$
0
0
KUTOKANA na ugumu wa masharti aliyopewa na mwigizaji Wastara Juma juu ya kumuoa, msanii Bond Suleiman ‘Bond’ ameomba msaada kwa watu wa karibu hususan upande wa Wastara kumsaidia kumuweka sawa ili atimize lengo lake la kumuoa.

Akizungumza na mwandishi wetu hivi karibuni, Bond alisema Wastara ni mwanamke mwenye kila sifa ya kuwa mke, hivyo endapo atamkosa litakuwa ni pigo kubwa maishani mwake.

Jamani, amenipa masharti magumu sana, ni mwanamke thabiti ambaye nisingependa kumkosa, najaribu kuwatumia watu wetu wa karibu kumuweka sawa, maana ana kila sifa za kuitwa mke, nimekaa naye muda mrefu kama meneja wake, nimegundua mambo mengi sana, nahitaji msaada jamani,” alisema Bond.

Chanzo: GPL

Kampuni ya Bia ya Serengeti Kudhamini Uzinduzi wa Video Mpya ya Msanii Linah Sanga

$
0
0
1.    Meneja wa Msanii wa Muziki wa kizazi kipya, Estelina Sanga maarufu kwa jina la “Linah”, Doreen Noni toka Kampuni ya Panamusiq inayosimamia kazi za msanii huyo (wa kwanza kulia) akiongea na waandishi wa Habari (Hawapo Pichani) kuhusu udhamini wa video ya msanii wake walioupata toka Kampuni ya bia ya Serengeti kupitia kinywaji chake cha Jebel na kufafanua zaidi juu ya uzinduzi wa video hiyo mpya itakayotambulika kwa jina la “No Stress” anayotarajia kuzindua hivi karibuni. Wa pili kulia ni msanii Linah na wa tatu ni Meneja chapa wa pombe kali SBL, Shomari Shija  na kushoto ni Meneja uvumbuzi SBL , Attu Mynah. Hafla hiyo imefanyika makao makuu ya kampuni hiyo Chang’ombe jijini Dar es Salaam.

2.   Msanii maarufu wa Muziki wa kizazi kipya, Estelina Sanga maarufu kama “Linah” (wa kwanza kulia) akifafanua jambo kwa waandishi wa habari hawapo pichani juu ya Video yake mpya ijulikanayo kama” No Stress” inayotarajiwa kuzinduliwa hivi karibuni chini ya udhamini wa Kampuni ya bia ya Serengeti kupitia kinywaji chake cha Jebel Coconut, katikati ni Meneja chapa pombe kali toka SBL, Shomari Shija na Meneja uvumbuzi SBL, Attu Mynah. Tukio hilo limefanyika makao makuu ya kampuni hiyo Chang’ombe jijini Dar es Salaam.

3.    Msanii maarufu wa muziki wa kizazi kipya, Estelina Sanga maarufu kama “Linah” (kulia) akifafanua jambo kwa waandishi wa habari hawapo pichani juu ya ujio wa video yake mpya itakayokwenda kwa jina la “No Strees” ambayo inatarajiwa kuzinduliwa hivi karibuni kwa udhamini wa Kampuni ya Bia ya Serengeti kupitia kinywaji chake cha Jebel Coconut ambapo yeye ni balozi wa Kinywaji hicho. (Wa pili) ni Meneja chapa wa pombe kali SBL, Shomari Shija, Mkutano huo ulifanyika makao makuu ya Kampuni hiyo, Chang’ombe jijini Dar es Salaam.
4.    Meneja chapa wa pombe kali SBL, Shomari Shija (katikati) akiongea na waandishi wa habari (hawapo pichani) juu ya udhamini wa uzinduzi wa video mpya ya msanii Estelina Sanga “Linah” itakayokwenda kwa jina la “No Stress” kupitia kinywaji chake cha Jebel Coconut. Kushoto ni Meneja uvumbuzi SBL, Attu Mynah, na kulia ni msanii Linah. Tukio hilo lilifanyika makao makuu ya SBL Chang’ombe jijini Dar es Salaam.

5. Meneja chapa pombe kali toka SBL, Shomari Shija (kushoto) akiongea na waandishi wa habari hawapo Pichani juu ya udhamini wa uzinduzi wa video mpya ya msanii maarufu Estelina Sanga a.k.a” Linah”(katikati) wimbo ukijulikana kama “No Stress”. Wimbo huo umedhaminiwa na Kampuni ya bia ya Serengeti kupitia kinywaji chake cha Jebel Coconut ambapo msanii huyo ni balozi. (wa kwanza kulia) ni Doreen Noni Meneja wa msanii huyo toka Kampuni ya Panamusiq inayosimamia kazi za Linah. Tukio hilo lilifanyika makao makuu ya SBL Chang’ombe jijini Dar es Salaam.

6.   Meneja uvumbuzi SBL, Attu Mynah, (kushoto) akiongea na waandishi wa habari hawapo pichani kuhusu udhamini wa video mpya ya msanii “Linah” kupitia chapa ya Jebel coconut toka SBL chapa ambayo msanii huyo ni balozi. Video hiyo inatarajiwa kuzinduliwa hivi karibuni na itakwenda kwa jina la “No Stress” (Wa pili) ni msanii Linah na wa kwanza kulia ni Meneja wa msanii huyo Doreen Noni toka kampuni ya Panamusiq inayosimamia kazi za msanii huyo. (Wa pili) kushoto ni Meneja chapa pombe kali toka SBL, Shomari Shija.

7.    Meneja chapa pombe kali toka SBL, Shomari Shija (kushoto) akiongea na waandishi wa habari hawapo pichani juu ya udhamini wa uzinduzi wa video mpya ya msanii maarufu Estelina Sanga a.k.a Linah” (katikati) itakayojulikana kwa jina la “No Stress”. Udhamnini wa msanii huyo unafuatia ahadi ya Kampuni ya bia ya Serengeti kusapoti kazi zake baada ya msanii huyo kupata mkataba wa ubalozi wa kinywaji cha Jebel Coconut toka SBL. (Kushoto) ni Meneja wa msanii huyo Doreen Noni toka Kampuni ya Panamusiq inayosimamia kazi za msanii huyo. Tukio hilo lilifanyika makao makuu ya SBL Chang’ombe jijini Dar es Salaam.

Kampuni ya bia ya Serengeti kupitia kinywaji chake cha Jebel Coconut imetangaza rasmi siku ya leo dhamira yake ya kudhamini uzinduzi wa video mpya ya msanii Estelinah Sanga maarufu kwa jina la kisanii “Linah” itakayo kwenda kwa jina la “No Stress”.
Video ya wimbo huo imefanyika nchini Kenya na Afrika ya kusini ambapo kwa kushirikiana na menejimenti ya msanii huyo, SBL imeweza kudhamini utengenezaji wa video hiyo ambayo hadi sasa imeshakamilika huku Kampuni hiyo ikisubiria kuizindua rasmi kwa wananchi.
Hatua ya SBL kudhamini video ya wimbo huo ni njia mojawapo ya Kampuni hiyo kutambua sanaa ya muziki hapa nchini ambapo pia hapo awali Kampuni hiyo iliahidi kumsapoti msanii huyo mara baada ya kupata mkataba wa mwaka mmoja wa kuwa balozi wa kinywaji cha Kampuni hiyo cha Jebel coconut.

Akizungumza na waandishi wa habari wakati wa utoaji wa taarifa hiyo kwa umma, Meneja Uvumbuzi wa kampuni hiyo Attu Mynah alisema “Kampuni ya bia ya Serengeti inatambua umuhimu wa Sanaa ya muziki hapa nchini na siku zote inalenga kumuwezesha msanii aweze kufikia malengo ya ndoto zake. Tumeamua kudhamini utengenezaji na uzinduzi wa video ya wimbo wa msanii Linah kwa kuwa tunatambua uwezo wake na tungependa afike mbali zaidi kimuziki”.
, alisema “Tunafuraha kwa kuwa Kinywaji chetu cha Jebel coconut kinaendelea kujizolea mashabiki wengi kupitia ubalozi wake ambapo ameendelea kuitangaza chapa hii sehemu mbalimbali za Tanzania. Kama SBL tunajivunia kudhamini baadhi ya kazi zake na ni matumaini yetu kuwa kupitia udhamini huu ataendelea kufanya vizuri zaidi katika ngazi za kimataifa”.

Jebel coconut ni aina ya pombe kali yenye ujazo wa 250ml inayotengenezwa nchini Tanzania na Kampuni ya bia ya Serengeti ambayo imebuniwa na kutengenezwa kwa ladha ya nazi ambazo zinapatikana kwa wingi hapa nchini. Jebel pia ni kati ya pombe kali zaidi ya 10 za kimataifa zinazosambazwa na kampuni ya bia ya Serengeti huku walengwa wa kinywaji hiki wakiwa ni watu wazima na wenye umri wa kati.
**MWISHO**

Wasomi waelezea tetesi za Dk. Slaa kujiuzulu siasa......Yadaiwa ni Shinikizo la mkewe

$
0
0
Wakati uvumi wa kujiuzulu cheo na kujivua uanachama wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema),  Dk. Wilbroad Slaa, ukiwa umetawala kupitia mitandao ya kijamii na magazeti, taarifa zinadai kuwa sababu ya kuchukua hatua hiyo ni shinikizo kutoka kwa mkewe.

Taarifa zilizochapishwa na gazeti moja likimnukuu Dk. Slaa mwenyewe, zilisema ameachana na siasa na kujivua wadhifa wake na atabaki kufanya shughuli zingine.

Dk. Slaa  amedaiwa hakubaliani na namna chama chake kilivyompokea Waziri Mkuu wa zamani Edward Lowassa.

Lowassa aliyekuwa Mbunge wa Monduli alitangaza kuhamia Chadema, Julai 28, mwaka huu  baada ya kutoridhishwa na mchakato wa CCM wa kumpata mgombea wa urais.

Habari za uhakika kutoka vyanzo vyetu vya habari ndani ya Chadema zinadai, Dk. Slaa alishiriki katika mchakato mzima wa kumpokea na kuridhia Lowassa, kusimamishwa kuwa mgombea urais kupitia Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa).

Hata hivyo, chanzo kingine cha habari kinadai kuwa mke wa Dk. Slaa, Josephine Mashumbusi, alitoa shinikizo kwa mumewe la kujiuzulu baada ya kuruhusu kusimamishwa mgombea mwingine (Lowassa).

"Josephine alikuwa na uhakika mume wake ndiye atakayesimama ugombea urais kwa upande wa Ukawa, hali ilivyobadilika, akakasirika na kumwambia mumewe ama yeye au Chadema," chanzo kilidokeza.

Kupitia ujumbe uliosambaa kwenye mitandao ya kijamii, unaoonyesha kutoka kwa Mashumbusi, aliandika "Ni kweli Frida na kwa hili Dk. Slaa amejivua wadhifa wake wa ukatibu mkuu na kuachana na siasa. Hamtamsikia tena kwani hawezi kupinga anachokiamini".

Hata hivyo, Dk. Slaa alipotafutwa kupitia simu yake ya mkononi kuthibitisha madai hayo, iliita mara moja na kuzimwa. Juhudi za kumpata ziligonga mwamba baada ya simu yake kutopatikana hali kadhalika simu ya Mashumbusi.

Wakizungumza na mtandao huu, baadhi ya wasomi walisema kama Dk. Slaa amejiuzulu nafasi yake  na kujivua unachama atakuwa amejijengea heshima na uaminifu na kwamba Chadema kitapata pigo.

Mhadhiri wa Chuo kikuu cha Dar es Salaam, Dk. Benson Bana, alisema  kwa upande wake aliamini kitu kama hicho kitatokea kutokana na tukio hilo kuwa la haraka na kulifananisha sawa na mapinduzi ya ghafla ndani ya chama.

“Nafikiri kama kweli Dk. Slaa amejivua uanachama itakuwa ni jambo zito na pigo kwa Chadema, lakini ni uamuzi wa busara na kumjengea heshima kwa jamii,” alisema Dk. Bana.

Alisema kitendo cha Lowassa kuhamia chama hicho kwa haraka kilileta mashaka na mijadala kwa baadhi ya viongozi.

“Ninavyojua mimi ndani ya Chadema kuna watu wenye misimamo na wapo tayari kuilinda kwa nguvu zote, kujitoa kwake sawa na kutaka kusimamia kile anachokiamini na kukaa kwake kimya katika jambo hili lazima kutakuwa na mshindo mkuu,” alisisitiza.

Mhadhiri huyo alisema anaamini Slaa aliweza kukifufua chama hicho mwaka 2010 kwa kuweka misingi yake ya kukemea ufisadi, hivyo hawezi kurudi nyuma kwa kuivunja.

Dk. Kitlya Mkumbo kwa upande wake alisema anaheshimu maamuzi ya pande zote mbili kwani zinaonyesha demokrasia na ukomavu wa kisisa.

Alisema Dk. Slaa amechukua uamuzi sahihi wa kujiuzulu kwa sababu ni haki yake kikatiba na Chadema wamechukua hatua ya kumkaribisha Lowassa walikuwa na njia njema kukuza upinzani na kuiondoa CCM madarakani.

Kauli  za  Slaa  Dhidi  ya  Lowassa
Septemba 15 mwaka 2007 katika viwanja vya Mwembe Yanga jijini Dar es Salaam, Dk. Slaa alimtaja Lowassa kuwa miongoni mwa mafisadi 11 waliochota fedha Benki kuu katika akaunti ya Epa.

Kauli hiyo alikuwa akiitamka kila mahali alipokwenda na  kusisitiza kwamba Lowassa na viongozi wenzake wa CCM wamechafuka kwa ufisadi.

Akiwa katika kampeni ya urais mwaka 2010, Wilayani Monduli Dk. Slaa alimshambulia Lowassa, kwa kushindwa kudhibiti vitendo vya kifisadi vilivyotokea jimboni na serikalini.

Akizungumza katika mkutano uliofanyika katika viwanja vya Bomani, alisema binafsi hana ugomvi  na Lowassa kwani ni mmoja  wa viongozi aliofanya nao kazi kwa karibu na ni rafiki yake, lakini wanatofautiana katika masuala ya msingi yanayohusu maslahi ya Taifa.

Naibu Waziri wa Kazi na Ajira , Dk. Makongoro Mahanga Atangaza Kuihama CCM......Asema Atahamia CHADEMA

$
0
0
Naibu Waziri wa Kazi na Ajira na Mbunge wa Segerea anayemaliza muda wake,Mh. Dkt. Makongoro Mahanga, ametangaza kuihama CCM na  kuhamia  CHADEMA kutokana na kutokuwepo Demokrasia ya Kweli ndani ya CCM.

Dr. Mahanga ambaye ni Mbunge anayemaliza muda wake  kwenye Jimbo la Segerea  kwa  tiketi  ya  CCM  ametangaZA azma hiyo leo mchana baada ya  rufaa yake ya kupinga ushindi wa aliyekuwa Diwani wa Kata ya Kipawa mama Kivela kutupiliwa mbali na Ofisi ya CCM mkoa wa Ilala.

Duru za Kisiasa zinasema kilichomponza Dr. Mahanga ni kitendo chake cha yeye kuhusika katika mpango wa kumnadi Waziri mkuu wa zamani Edward Lowassa kwenye nafasi ya Urais wa CCM, ambaye kwa  sasa ametangaza kugombea urais kupitia Chadema.

Kura za Maoni CCM: Mawaziri Watano Waanguka.......Yumo Chikawe,Sillima,Mahanga na Makalla.......Aden Rage Pia Kaanguka!!

$
0
0
Matokeo ya awali ya kura za maoni kwa wagombea udiwani na ubunge kupitia chama tawala, yameanza kuanikwa, huku yakionesha kuwa baadhi ya mawaziri, wabunge na watendaji katika chama na serikali wameangushwa.


Kwa mujibu wa matokeo ambayo mtandao huu umeyapata, kwa upande wa mawaziri walioshindwa ni pamoja na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mathias Chikawe.
 
 Hayo yamethibitishwa na Katibu wa CCM mkoa wa Lindi, Adelina Gefi aliyesema kura za Chikawe katika jimbo lake la Nachingwea alikokuwa anatetea kiti chake, hazikutosha mbele ya Hassan Masalla, Mkuu wa Wilaya ya Kilombero aliyepata kura 6,444. Chikawe amepata kura 5,128.
 
Wakati Chikawe, mmoja wa wanasiasa mahiri na mwanasheria aliyepata kuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Utawala Bora na pia Waziri wa Katiba na Sheria akikwama katika mchakato wa kurejea bungeni, naibu wake katika Wizara wa Mambo ya Ndani, Pereira Silima naye ameanguka katika kura za maoni huko jimbo la Bumbwini, Unguja.

Mwanasiasa mwingine aliyekwama katika kura za maoni ni Mahadhi Juma Mahadhi ambaye ni Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.
 
Mahadhi ameanguka katika kura za maoni katika Jimbo la Paje, Unguja huku mshindi akiibuka kuwa Jaffar Sanya Jussa.
 
Mambo yamekuwa mabaya pia kwa Naibu Waziri wa Fedha, Adam Malima ambaye ameripotiwa kuanguka katika kura za maoni katija Jimbo la Mkuranga mkoani Pwani.

Hali kama hiyo imemkuta Naibu Waziri wa Kazi na Ajira, Dk Milton Makongoro Mahanga ambaye ndani ya saa 24 tangu ashindwe kura za maoni katika jimbo alilokuwa analitumikia la Segerea katika Manispaa ya Ilala, Dar es Salaam, jana alitangaza kuihama CCM na kujiunga na Chadema.

Katika Jimbo la Mvomero mkoani Morogoro, habari zinasema aliyewahi kuwa mbunge wa zamani wa jimbo hilo, Suleiman Saddiq `Murad’ amefanikiwa kumwangusha mshindani wake wa siku nyingi, Amos Makalla ambaye alilitwaa jimbo hilo mwaka 2010 na baadaye kuteuliwa kuwa Naibu Waziri, akianzia Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo kabla ya kuhamishiwa Wizara ya Maji ambako yupo mpaka sasa.

Ingawa Katibu wa CCM wa wilaya ya Mvomero, Amos Shimba hakuthibitisha hilo, akisema kwa kiasi kikubwa matokeo yamepatikana, isipokuwa katika baadhi ya maeneo, hivyo matokeo rasmi yatatangazwa leo, tayari kambi za Murad na Makalla zilithibitisha matokeo ya kura za maoni katika jimbo hilo, kwamba hali ya Makalla haikuwa nzuri katika kura hizo.
 
Mshtuko mwingine wa kisiasa umesikika katika Jimbo la Uzini ambako mwanasiasa nguli aliyepata kuwa waziri katika wizara mbalimbali za Serikali ya Muungano, Muhammed Seif Khatib ameshindwa katika kura za maoni.
 
Khatib ambaye kwa sasa ni Katibu wa Oganaizesheni ya CCM, amepata kura 1,333 dhidi ya mpinzani wake, Salum Mwinyi Rehani aliyepata kura 1,521.

Khatib amekuwa mbunge wa jimbo hilo kwa miaka 20 na katika kipindi hicho alikuwa waziri wa wizara mbalimbali zikiwemo Habari na ile ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
 
Rage `out’, Adadi, Nape safi
Ukiachilia mbali mawaziri hao, baadhi ya wabunge wamekuwa na wakati mgumu majimboni kwao, akiwemo Ismail Aden Rage wa Tabora Mjini. Aidha, Zainabu Kawawa, binti wa Waziri Mkuu wa zamani, Rashid Mfaume Kawawa hakufua dafu mbele ya Mbunge wa Jimbo la Liwale, Faith Mitambo.

Awali, Zainabu alikuwa Mbunge wa Viti Maalumu kwa tiketi ya CCM.
 
Mbunge mwingine aliyeshindwa katika kura za maoni ni Mtutura Abdalla wa Tunduru Kusini, kama ilivyokuwa kwa wabunge watatu wa mkoa wa Tanga, Herbert Mntanga wa Jimbo la Muheza aliyeangushwa na Balozi wa zamani wa Tanzania nchini Zimbabwe, Adadi Rajab ambaye pia alikuwa Mkurugenzi wa Makosa ya Jinai Nchini (DCI).

Saleh Pamba, Katibu Mkuu wa zamani wa Wizara ya Maliasili ambaye anamalizia ubunge wake katika Jimbo la Pangani, amethibitika kukwama mbele ya Jumaa Awesso, kwa mujibu wa Katibu wa CCM mkoa wa Tanga, Shija Othman.

Mbunge wa Korogwe Mjini, Yussuf Nasri naye kura zake hazikutosha, baada ya wanachama wa CCM kumpa kura nyingi Mary Chatanda kuwa ndiye chaguo lao katika kura za maoni ya ubunge.
 
Naye Gregory Teu, Mbunge wa Mpwapwa aliyewahi kuwa Naibu Waziri wa Fedha, ameripotiwa kuanguka na mbunge wa zamani wa Jimbo hilo, George Malima Lubeleje.

Katia Jimbo la Kilombero, Abdul Mteketa amegota mbele ya Abubakar Asenga, wakati katika Jimbo la Igalula mkoani Tabora, Naibu Waziri wa zamani wa Uchukuzi, Athuman Mfutakamba anaburuzana na Mussa Ntimizi, ambapo kufikia jana Ntimizi alikuwa na zaidi ya kura 75,000 dhidi ya 3,400 za Mfutakamba.

Kibamba ni Dk Mukangara
Kwa upande wa baadhi ya majimbo ya Dar es Salaam, walioshinda kwa upande wa CCM ni pamoja na Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Dk Fenella Mukangara aliyeshinda kura za maoni katika jimbo jipya la Kibamba lililogawanywa kutoka jimbo la Ubungo, huku Ramesh Patel aking’ara Jimbo la Ukonga alikowabwaga washindani kadhaa, akiwemo Meya wa Manispaa wa Ilala, Jerry Silaa.

Katika jimbo la Ubungo, kura zimempa nafasi Meya wa Jiji la Dar es Salaam, wakati Abbas Mtemvu ameshinda katika jimbo la Temeke analoliongoza tangu mwaka 2005.
 
Nape apeta Mtama
Nako katika Jimbo la Mtama lililoongozwa kwa miaka 15 na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe kabla ya mwaka huu kujitosa katika mbio za urais, kijiti kinaelekea kumwangukia Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM Taifa, Nape Nnauye aliyewabwaga washindani wake kadhaa, akiwemo Suleiman Mathew aliyekuwa Diwani wa Kata ya Vijibweni, Kigamboni

Huwezi Amini Watanzania Tuna Maamuzi Magumu Sana...Embu Jisomee Hapa Uone.....

$
0
0

1. Huna uhakika wa kula na elfu moja pekee uliyonayo unaamua kuinywa Kiroba - Ni maamuzi magumu.

2. Huna kitanda na unaamua kuoa - Hayo pia ni maamuzi magumu.

3. Huna uwezo wa kumlisha mkeo kazi yako ni kumjaza ujauzito - Ni maamuzi magumu.

4. Shule haina waalimu unampeleka mwanao - Pia ni maamuzi magumu....

5. Daladala imejaa mpaka mlangoni na unaamua kupanda - Ni maamuzi magumu.

6. Unalipwa laki mbili unamhonga binti laki moja - Hayo ni maamuzi magumu.

7. Kama utasoma hapa na kushindwa kuweka maamuzi magumu unayoyajua - Utakuwa unamaamuzi magumu mnoo...!

8. Mdada unaweka brazillian ya laki saba mshahara laki 2- Hayo ni maamuzi magumu

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatatu ya August 3

$
0
0




















Habari  Zilizopo  Katika  Magazeti  ya  Leo  Jumatatu  ya  August   3

DJ Fetty Awachana BASATA Kuhusu Kumfungia Shilole...Akumbushia Mixtape za Matusi za ANTI VIRUS

$
0
0
@Thebestfetty;
"Zilitoka mixtape za matusi za ANTI VIRUS vol 1 na 2, BASATA ilikaa kimya na ilitoa kibali cha uzinduzi wa anti virus volume 2, Viwanja vya posta, licha ya kuwepo kwa malaamiko. SWALI ni, kifungu kilichotumika kumhukumu ni kuwa UCHI au ni UVUNJAJI WA MAADILI????".

Msikilize Nuhu Mziwanda Akimtongoza Wema Sepetu..Nimekuwekea Audio Hapa....Usipitwe na Hili...

$
0
0
YELEUWIII! Katika hali ya kushangaza, sauti ya mpenzi wa staa wa muziki na filamu Bongo, Zuwena Mohamed ‘Shilole’, Naftal Mlawa ‘Nuh Mziwanda’ inayosikika akimtongoza Wema Sepetu imemfikia Shilole na kusababisha azimie

Nuh kajipambanua ileile. Kaimbisha mistari yote ya kimahaba, utafikiri alikaririshwa. Alijitahidi kushusha vesi tamu ili  kumuingiza Wema kwenye himaya yake. Huwezi amini jamaa alizidisha mbwembwe kiasi cha kumwambia amkubalie kwani hamtaki Shilole tena.

WEMA AMTOSA
“Wema amesikika akikataa, akamwambia hawezi kuwa naye kwani ni shemeji yake na anamheshimu Shishi,” kilisema chanzo hicho.

SHILOLE AMFUATA NUH
Chanzo hicho kilieleza kuwa, baada ya kuusikiliza ujumbe huo, Shilole alimfuata Nuh kwa ajili ya kumsikilizisha lakini Nuh alijibu ‘mbovu’ ndipo Shilole alipomuomba ufunguo wa gari waliyokwenda nayo, akarudi alipokuwa amekaa awali.

APOTEZA ‘NETIWEKI’
“Aliporudi alipokuwa amekaa, Shilole alijikuta akiishiwa nguvu na kuzimia ambapo Aunt Ezekiel na kina JB (Jacob Stephen) walipofanya kazi ya ziada kumpepea, huku wengine wakihangaika kummwagia maji kunusuru afya yake.
“Walifanikiwa kumpandisha kwenye gari lake. Joto lilikuwa kubwa kufuatia hali hiyo maana kila mtu alishindwa kuelewa kilichotokea, hivyo Shilole, baada ya kuzinduka aliulizwa kilichomfanya azime ambapo aliwasikilizisha sauti hiyo kila mmoja akabaki ameduwaa,” kilieleza chanzo.

AUNT AOKOA JAHAZI
Ilielezwa kuwa, mwigizaji Aunt Ezekiel ndiye aliyeokoa jahazi kwa kulazimika kuendesha gari la Shilole na kumpeleka nyumbani huku Nuh akipandishwa kwenye gari la JB kumpeleka kwa ndugu zake.
MSIKIE SHILOLE
Paparazi wetu, baada ya kupenyezewa ubuyu huo, alimtafuta Shilole ili kupata habari kamili ambapo alikiri kupokea ujumbe huo wa sauti huku akiainisha kuwa umemkera kwani kuna maneno yanasikika akimponda yeye.
“Inaniuma sana, Nuh kuendelea kunidhalilisha kiasi hicho wakati ni mwanaume ambaye ninamheshimu, tunakoelekea uzalendo utanishinda.
“Nilipousikiliza ujumbe ule kwa mara ya kwanza sikuamini nilichokisikia. Pamoja na Wema kuonesha wazi msimamo wa kumkataa Nuh ila mimi naona kama fedheha kubwa kwangu kwani ninamheshimu sana.
“Watu wananiona mimi mkorofi lakini kama ningekuwa napenda kuweka kila jambo wazi, hakuna mtu angeendelea kunifikiria vibaya.“Siwezi tena kuendelea kuumiza moyo wangu kila kukicha,” alisema Shilole ambaye anatumikia kifungo cha Basata kwa kutojishughulisha na sanaa kwa takriban mwaka mmoja kwa kosa la kucheza nusu utupu jukwaani.

Nimekuwekea hii Audio Hapa:


Kampeni ya Tusker Fanya Kweli Kiwanjani Sasa Kutimua Vumbi Mikoani....

$
0
0
Kampeni maarufu ya Tusker Fanyakweli Kiwanjani inatarajia kutimua vumbi wiki hii kwa wakazi wa jiji la Dar huku ikitanua wigo wake mikoani baada ya kufanya vizuri kwenye kipindi chake cha kwanza.

Kampeni hii inayoletwa kwenu na Kampuni ya bia ya Serengeti imejipanga kusaidia baa mbalimbali za mitaa tunayoishi na kuzipigia promo ya huduma zake kwa wapenzi mbalimbali wa kinywaji cha Tusker.

Akizungumza kuhusiana na mchakato mzima  wa Kampeni hiyo Meneja chapa bia ya Tusker Bi. Sialouise Shayo alisema SBL kupitia chapa yake ya Tusker imejipanga kutembelea baa zaidi ya 1000 kwenye miji yote mikuu nchini ikiwemo Dar es salaam, Arusha, Morogoro, Moshi, Mbeya na Mwanza.

“Uamuzi wa kuongeza muda wa promosheni hii ya Fanyakweli Kiwanjani ni kutokana na maombi mbalimbali hasa toka baa za mikoani kufanyiwa promo/shindano kama hili kwenye baa zao”…alisema Sialouise.



Akifafanua zaidi kuhusu ratiba ya promosheni hiyo kwa wakazi wa Dar na mikoani, Sialouise alisema taarifa rasmi ya maandalizi ya promosheni hii itatangazwa kwenye vyombo vya habari vya mikoa husika ili kuwajulisha wapenzi wote wa kinywaji cha Tusker kuhusiana na nini kinaendelea.

Aliongeza kuwa utaratibu wa kuchagua na kuorodhesha baa mbalimbali ili zipite kwenye kampeni hii haujabadilika ambapo wapenzi wa Kinywaji cha Tusker wanatakiwa kuzipigia kura baa wazipendazo ambapo anachotakiwa mtu kufanya ni kutembelea baa ya mtaani kwake na kunywa bia ya Tusker, kupiga picha na kisha kuweka picha hizo kwenye kurasa za mitandao ya kijamii (Facebook na Twitter) za Tusker au kusikiliza redio E-fm kwa wakazi wa Dar es salaam na wa mikoani wasikilize redio zifuatazo kwa maelezo zaidi. Redio 5 (Arusha), Kili fm (Kilimanjaro), Metro fm (Mwanza), Planet fm (Morogoro) na Bomba fm (Mbeya).
***MWISHO***

Zari Awapiga ‘Stop’ Ndugu wa Mwanamuziki Diamond Platnumz

$
0
0
Imelda Mtema
Stop! Wakati akisubiriwa kujifungua muda wowote, mwandani wa staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’, Zarinah Hassan ‘Zari The Boss Lady’ anadaiwa kuwazuia baadhi ya ndugu wa jamaa huyo kuingia kwenye chumba maalum kilichoandaliwa ili kuepuka kisiingie vumbi na kiwe safi wakati wote.

Chanzo chetu ambacho ni mmoja wa ‘memba’ wa familia hiyo kilipenyeza kuwa, kwa sasa nyumbani kwa mwanamuziki huyo maeneo ya Madale-Tegeta, Dar, wana bashasha wakimsubiria mtoto huku chumba hicho kikiwekewa uangalizi mkubwa.
“Yaani Zari hataki mchezo kabisa na haruhusu mtu kuingia chumbani humo hovyo kwa sababu ya kuepuka vumbi kwa mtoto kwa maana chumba hicho hakihitaji msongamano wa watu wengi,” kilisema chanzo hicho.

Mpashaji huyo aliweka wazi kuwa, Zari alitia ngumu na kusema ni sheria aliyoiweka mwanamama huyo na haitakiwi kukiukwa na mtu yeyote kwa kuwa wanafahamu fika kuwa chumba cha mtoto hakihitaji msongamano wa watu hivyo ndugu hao imebidi wawe wapole.
Kilidai kwamba, kwa sasa kila mtu anayefika nyumbani hapo anahojiwa na kwamba kama siyo ndugu wa ndani zaidi kwenye familia haruhusiwi hata kuingia getini.Akizungumza na Ijumaa Wikienda kuhusu maandalizi hayo, Diamond alisema kila kitu kipo sawa na kwamba, anamuomba Mungu mambo yaende kama alivyopanga.

Whattttttt........Martin Kadinda Kuoa Soon....Huamini? Soma Hapa....

$
0
0
Mbunifu wa mavazi Bongo, Martin Kadinda, amesema kuwa baada ya kuishi bachela kwa miaka mingi amepanga kuoa ‘ soon’ mwanamke ambaye ni mpenzi wake wa siku nyingi ili kumaliza maneno ya watu kuwa hajiwezi.

Akizungumza na Amani, Kadinda alisema kuwa mwanamke anayemuoa si aliyezaa naye mtoto bali ni mwanamke aliyekuwa naye kwenye uhusiano kwa muda mrefu na tayari anatambua tabia zake hivyo hana shaka juu ya kuishi kwao pamoja.

Wazazi wako tayari juu ya hilo nadhani na sitaki kumweka hadharani sasa hivi maana watu hawakawii kuharibu kwa maneno yao machafu, lakini wale ambao walidhani sitaweza kufanya hivyo watambue kuwa mwakani naoa,” alisema Kadinda.

Mbowe: Tumuombee Dr. Slaa kwa Mungu ampe moyo wa ujasiri!

$
0
0
Mwenyekiti wa CHADEMA amewataka wanachama kumuombea kwa Mungu Dr. Slaa ampe moyo wa ujasiri katika kipindi hiki kigumu ambacho chama kinafanya mkutano wa kumpitisha mgombea wake wa urais!

Mbowe amesema Dr.Slaa hatashiriki katika mkutano huo kwa kuwa atakuwa kwenye mapumziko!

Hata hivyo Dr. Slaa bado ndiye Katibu Mkuu wa CHADEMA na ataendelea na kazi zake baada ya likizo yake!

Source:EA Radio

CHADEMA Wadai wamempa Likizo DR Slaa kwa muda..Ni Kweli ? Wapi Alipo ?

$
0
0
CHADEMA wampa likizo dk Slaa kwa muda....Mbowe aweka wazi kwamba wamekubaliana nae awe likizo nafasi yake katika chama iko pale pale... Kuna mwenye swali mpaka hapo.

Kunani?

Maneno ya Mbowe Haya:

Mbowe-Tumekubaliana na Katibu Mkuu apumzike kwa muda, kwamba sis tuendelee na atakapokuwa tayari ataungana nasi mbele ya safari.

Mbowe-Chama hiki hatukiendeshi kwa siri, tunakiendesha kwa mikakati.

Mbowe-Tulilazimika kutumia kila mbinu halali ambayo inakiwezesha chama chetu kusaka matumaini na matarajio ya wananchi.

Mbowe-Tuliridhika pasipo shaka kwamba ugeni wa Edward Lowassa katika chama chetu ni mpango wa Mungu.

Mbowe-Umoja wetu ndio ushindi, fursa iliyojitokeza ni nadra.

Mbowe-Mtikisiko huu umekuja kwa CCM kipindi ambacho Watanzania wanamatamanio ya mabadiliko

Mbowe-Hatuwezi kuwa chama cha kuendelea kuhubiri mabaya ya jana tukashindwa kuhubiri maendeleo ya kesho

Mbowe- Kipigo wanachopata CCM, hawajawahi kukipata tangu tuanze siasa za vyama vingi

Mbowe-Kila tunayeweza kumpokea kutoka vyama vilivyo nje ya UKAWA tutamchukua

Mbowe-Mungu ameamua kutumia chama chetu kujeruhi na kuangusha CCM.

Mbowe-CHADEMA ni chama cha siasa, ni chama makini, chama makinI ni chama cha watu, chama kisichokuwa makini ni chama cha viongozi.

Diamond anyakua tuzo mbili za NAFCA 2015 nchini Nigeria

$
0
0
Staa wa Bongo fleva nchini anayetamba kwa sasa na wimbo wa ‘Nana’ huku akiitambulisha Tanzania Kimataifa zaidi katika tasnia muziki, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ wikiendi hii staa huyo wa ‘Nana’ ameshinda vipengele viwili kwenye tuzo za Nollywood and African People’ Choice Awards
Diamondss (1)Vipengele alivyoshinda Diamond kwenye NAFCA ni Msanii bora wa mwaka na Wimbo bora wa mwaka.

Tuzo hiyo ni mafanakio zaidi kwa Diamond na tasnia nzima ya muziki nchini ikiwa ni siku chache tangu staa huyo anyakue tuzo za MTV MAMA 2015 katika kipengele cha Mtumbuizaji bora.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumanne ya August 4

$
0
0















Habari  Zilizopo  Katika  Magazeti  ya  Leo  Jumanne  ya  August  4

Hapa na Pale: Hii ndiyo Mistari ya Nuh Mziwanda Alipokuwa Anamtongoza Wema Sepetu, Utavunja Mbavu

$
0
0
Kwa jinsi teknolojia ilivyokua watu wanapaswa kuwa makini sana kwa simu wanazopiga na maneno wanayoongea

Nuh Mziwanda amejikuta akiumbuka vibaya baada ya Wema Sepetu kuvujisha sauti anayosikika akimtongoza mrembo huyo. Mazungumzo hayo yanachekesha sana hasa kutokana na mistari anayompa Miss Tanzania huyo wa zamani. Haya ni maongezi yaliyofanyika mwezi June (siku moja kabla ya KTMA 2015). Tunafahamu wapo wasioweza kusikiliza clip yote hivyo tumekuandikia mazungumzo hayo.

Nuh Mziwanda: Kuna ua moja lilikuwa limefuatwa sana na vipepeo pamoja na nyuki kwaajili ya kutengeneza asali, unanielewa?

Wema Sepetu: Yeah

Nuh: Kwahiyo lile ua yule mama alikuwa anapenda sana kulitunza na kulifanya special kuliko maua yote. Mama yupo radhi maua yote yakauke lakini lile ua alimwagilie maji ili likue.

Wema: Hilo ua lilikuwa nyumbani kwenu?

Nuh Mziwanda: Yeah nyumbani kwetu Ilala Posta, alipokulia Shetta kwa akina Shetta pale kwetu hapa. Ua hilo hadi leo hii lipo. Ua ambalo mama analipenda na kulithamini kwakuwa lililikuwa linavutia. Kwahiyo katika kuvutia kwake, vipepeo walikuwa wanalipenda lile ua. Ni mfano wako wewe, you’re so beautiful!

Wema: Thank you lakini unanitafutia matatizo, wewe unataka mimi Shilole anifanye nini? Nuh mbona hivyo?

Nuh Mziwanda: Sijamalizia kuongea! Kwanza wewe ni mwanamke mzuri sana na wa kuvutia na mwanaume akikuona, anatamani aje kwenye ua kwakuwa wewe ni mfano wa ua. Na sisi ni mfano wa vipepeo na mfano wa nyuki.

Wema: Sasa hizo tattoo unazifanya nini?

Nuh: Eeeh!!

Wema: Hizo tattoo zako za Shishi Beibe unazifanya nini?

Nuh: Unajua kila kitu kinatokea kwa sababu kwenye hii dunia. Wema ulikuwa haujui mimi ni nani? Lakini hatujui Mungu alipanga nini kwenye muziki wangu na maisha yangu. Baada ya mimi kuchora tattoo nimejulika mimi ni nani. Kwahiyo namshukuru Mungu sasa hivi mashabiki wangu wanajua kwamba mimi naitwa Nuh! Nina mashabiki wachache lakini hao hao ndo wananifanya mimi niwe Nuh. Naamini nilichora tattoo kwa sababu ya Mungu na kila kitu kinatokeaga kwa sababu. Mimi naishi kama binadamu haya mambo yanatokeaga kwa binadamu yoyote. Vitu vingapi ulikuwa navyo leo hauna? Sisi tunaishi kama binadamu, haya mambo yalikuja na yanaweza kutokea kwa binadamu yoyote. Huwezi kujua mambo mangapi ya kipuuzi umeyafanya katika maisha yako. Lakini unaangalia unafanya nini ili uendelee na maisha, natamani niwe na wewe, natamani uwe mpenzi wangu serious!

Wema: Utanituliza akili yangu na wewe na Shilole itakuwaje mbona unataka kunifanyia vitu vya ajabu vya kunigombanisha mimi na rafiki yangu? Shilole is not my best friend lakini ni mshkaji sawa. Ni msichana ambaye namjua na ni rafiki yangu yaani. Itakuwa vibaya halafu mimi sipendi maneno sawa. Mimi napenda tunakutana mambo poa vipi, everybody is happy. Sasa hapo sasa hivi tunataka kuanza kubadilishana dunia tena. Mimi sipendi Nuh, mimi sipendi maneno na Shilole alishanitamkia na tena alisema mbele yako na umemsikia, kwamba hataki, mimi sitaki tuishi kama washkaji, Nuh unakosea kwa sababu kuna kesho kesho kutwa.

Nuh: Nikwambie kitu Wema?

Wema: Uniambie nini Nuh? Uniambie kitu gani sasa hivi it’s not possible yaAni ni kitu ambacho kipo very impossible. Sio nakuvunja moyo nakwambia kweli, nakwambia ukweli unajua in love sio kila kitu unachokitaka unakipata si unajua hivyo?

Nuh: I know!

Wema: Kwamba katika maisha sio kila kitu unachokitaka utakipata. Basi mimi namheshimu sana Shilole na ninakuheshimu wewe pia. Nimekubali umenipigia simu na umeniambia lakini it’s something ambacho hakiwezekani tokea. Yaani haiwezekani kutokea. Najua sio rahisi ku-accept lakini jitahidi kuikubali kwa sababu ndio hali halisi, haiwezekani icho kitu.

Nuh: Nikwambie kitu?

Wema: Utaniambia kitu gani Nuh na nimeshakwambia kwamba haiwezekani!

Nuh: Kama unanikatisha tamaa kihivyo, unadhani nitakwambia kitu gani?

Wema: Haya kitu gani? Niambie nakusikiliza kitu gani?

Nuh: Kitu ninachotaka nikwambie ndio hicho tu, nothing new, kila siku unatongozwa lakini mimi naongea kwa mapenzi na kama mwanaume na kwa kujiamini pia. Lakini inawezekana pia nikawa nimekukwaza.

Wema: Hamna haujanikwaza kwa sababu kumwambia mtu hisia zako sio kitu kibaya. Kusema hisia zako it’s not very bad. Tena it’s a very good thing kwa sababu umeshow kitu umekuwa jasiri. Halafu mpaka umenipigia simu na umeniambia yaani umetumia ujasiri sana, unaona so I appreciate it, and thank you. Kupendwa raha lakini unapopenda hapawezekani kwa sababu mimi siwezi siko kwenye nafasi ya kukukubalia what you are talking me. Ushanielewa kwamba nafasi yangu hairuhusu kukubali, kwa sababu moja nakuheshimu wewe kama shemeji yangu, wewe ni shemeji yangu, wewe ni boyfriend wa rafiki yangu. Mimi siko hivyo, mimi sio mtu wa kumchukulia rafiki yangu mwanaume, yaAni siko hivyo!

Nuh: Mimi najua kila kitu, najua nimejichora matatoo, najua ya mwanamke usinijudge kwa yale, ila nijudge kwa akili yako.

Wema: Sikia nikwambie Nuh, apart from everything mimi siwezi kukudanganya. Mimi siwezi kukukataa sijui, yaani kitu itanishusha. Kuingia mabifu na Shilole, unaanza kusikia Wema sasa hivi yupo na bifu na Shilole.

Nuh: Au wewe utatangaza kwa watu?

Wema: Akaa, no hakuna kitu kama hicho. Hakuna kitu ambacho kinafichika kama kuna mapenzi, mapenzi kitu kizito sana.

Nuh: Nikwambie kitu?

Wema: No, Nuh niache nilale, naomba niache nilale naomba niache nilale. Kesho naamka asubuhi sana natakiwa nijiandae na Kilimanjaro, si unaenda kwenye KTMA? .

Nuh: Unajua mimi nafikiria pia akilini mwangu na nina mawazo yangu kama binadamu na kila kitu kinatokea kwenye maisha kama vile nilivyokwambia, kuna vitu vingi vilitokea kwenye maisha yako,lakini inafika wakati unasahau. Na mimi nilifiwa na ndugu zangu lakini nikasahau, kwahiyo vyote vinaweza kutokea.

Wema: No! tutaongea kesho.

Ray Awashangaa Wanaobeza Ushindi wa Uwoya Ubunge Huko Tabora

$
0
0
Nimekaa Hapa Ofisini Kwangu Nikitafakari Mengi Sana kuhusu Baadhi Ya Watanzaia Kuwakatisha Tamaa Wasanii Wao Sasa Cjui Ni Roho Mbaya Ama Nini Maaana Leo Irene Uwoya Kashinda Kwenye Viti Maalum Tabora Lkn Coments Zimekuwa Nyingi Sana Kuwa Heti Baba Wa Taifa Nyanyuka Maana Chama Chako Kinaangamia. Hapana Hakuna Sehemu Yotote Inayopinga Mtu Kugombania Ubunge Maaana Ni Haki Ya Kila Mtanzania Mwenye Kukidhi VigezoYa Katiba Ya Nchi Ye2 .

Tuache Roho Mbaya Na Kuwadharau Wasanii Nakuwaona Kama Wa2 Wasiostahili Kuingia Kwenye Siasa Hivi Niulize Swali? Kuna Shule Yoyote Inayofundisha Siasa? Nadhani Kila m2 Atakuwa Na Jibu Lake Kichwani Tumeona Mifano Mingi 2 Kwa Wasanii Waliongia Kwenye Siasa Na wakafanikiwa Ndani Ya Africa Na Nje Ya Africa Marekani. ARNOLD SCHWARZENEGGER GAVANA , DESMOND ELIOT MUIGIZAJI TOKA NIGERIA ALISHIDA PIA UGAVANA, PIA YUPO RICHARD MOFE DAMIJO WENGI WANAMJUA KWA JINA LA PASTOR OKEMY TOKA NIGERIA Pia Ni Gavana Nk. Why Sisi Tusithubutu Wapeni Nguvu Wasanii Wenu Na Kuwatia Moyo Pale Wanapothubutu Kufanya Jambo Lolote. Waswahili Wanasemaje Kulegalega C Kufa Kufa Ni Kuoza Utumbo. Utabaki Kuwa Mtazamo Wangu Over...

Vicent Kigosi ‘Ray’ ‘@raythegreatest’ on instagram

Hongera sana Irene Uwoya, na kila la kheri  kwenye harakati zako.

Nisha Awekwa Chini ya Ulinzi Chin...Kisa Madawa ya Kulevya...

$
0
0
Yamemkuta! Staa wa Bongo Movies, Salma Jabu ‘Nisha’ ameonja joto ya jiwe baada ya kuwekwa chini ya ulinzi mkali huko Hong Kong, China ambapo alidhaniwa kuwa amebeba madawa ya kulevya ‘unga’.

Akizungumza na Ijumaa Wikienda, wikiendi iliyopita, Nisha alisema kuwa alijikuta akiichukia nchi ya China baada ya kupata wakati mgumu alipowekwa chini ya ulinzi kwa muda wa saa nne.

“Yaani China si mchezo, ukienda uwe na sababu, bila sababu unaweza kujikuta unaishia jela, kwa sasa Watanzania hatuaminiki kabisa, mwenzenu nilikamatwa na kupekuliwa mpaka walipojiridhisha ndipo wakaniachia,” alisema Nisha.

Adam Juma ataja sababu za kwanini video zake hazioneshwi MTV na Trace

$
0
0
Director Adam Juma amejibu lawama ambazo amekuwa akizipata kwa muda mrefu kuhusu video zake kutochezwa na vituo vya kimataifa kama MTV na Trace licha ya kuwa na ubora mkubwa.

Adam amesema kuwa sababu kubwa ya video nyingi anazofanya kushindwa kuchezwa zinaanzia kwa wasanii wenyewe.

Hiki ndicho amekisema kupitia 255 ya XXL ya Clouds Fm:

“Mi mtaendelea kunilaumu mpaka mtafika sehemu mtakuja kugundua, hata akija kufanya mtu mwingine mwisho wa siku hamuwezi mka solve, lazima mjue source ya matatizo…mnaweza mkafikiri labda mimi sitaki hizo video ziende huko, lakini swala sio hilo video zisiende huko, wasanii wenyewe pia sio wavumilivu…Alikiba kafanya video akaja akaitoa, kachelewa sana kuitoa, Trace wanatumia wiki tatu kui review video…hawakubali kupiga video baada ya watu wengine kupiga wanataka wao waanze kupiga wao, kwahiyo kuna wasanii wengine wajanja, wanaipeleka kule video miezi miwili mitatu mpaka ije kupita wakishapewa hiyo exclusive baada ya siku mbili tatu ndio wanaaachia bongo…Sasa mtu anataka ashut leo leo ipigwe Tanzania halafu iende ikapigwe na Trace…sasa mtu mwingine anakua ananilalamikia mimi bila sababu utafikiri mimi nafanya kazi bure tu. “– AJ
Viewing all 104789 articles
Browse latest View live




Latest Images