Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104709 articles
Browse latest View live

UDAKU'Z HOT GIRL OF THE DAY...

$
0
0
Anajiita Rita Kutoka Dar .......

HII KALI KWA DIAMOND PLATNUMZ!!! AAMUA KUJIITA 'DOMO' INSTAGRAM...CHEKI HAPA

$
0
0

Diamond Platnumz aka Prezident wa WCB ametoa kali na mpya kwa kuamua kujiita 'DoMo' kupitia ukurasa wake wa Instagram kama unavyo ona hapo chini. Yawezekana amefikia hatua hiyo baada ya watu wengi kumkashifu mara nyingi sababu ya mdomo wake. 
Kwangu mimi sioni tatizo maana ndivyo alivyo umbwa na je alikuwa anauliza wakuandika hivyo kweli? Au ndo kutupa cha kuongela? All in all he rocks big time being one of the most successful artists in East Africa pamoja na 'DoMo'

MWAIGULU NCHEMBA ANENA MAZITO KUHUSU SAKATA LA ZITTO KUVULIWA MADARAKA

$
0
0
Jisomee Mwenyewe Hapo Juu ....Dahhh

CANDY RECORDS WAMEONYESHA JEURI YA PESA TENA BAADA YA KUFUNGUA ONLINE RADIO INAYOITWA CANDY VIBES FM

$
0
0
CANDY N CANDY TENA

NI NOMAA……SANA!!!!,ILE CREW NZIMA KUTOKA JIJINI NAIROBI KENYA CANDY N CANDY MUSIC RECORD LABEL AMBAYO MAJUZI TU ILIMWAGIA MWANADAFADA TOKAPANDE HIZI BABY MADAHA MAMILIONI YA PESA KAMA SHAVU LA MKATABA KUFANYA MUSIC CHINI YAO
WAMEONYESHA JEURI YA PESA TENA BAADA YA KUFUNGUA ONLINE RADIO INAYOITWA CANDY VIBES FM,AMBAYO IKO WORLD WIDE NA INACHEZA MUSIC VIDEO LIVE KUPITIA TOVUTI YAKE.NI MAPINDUZI KATIKA SEKTA HII YA BURUDANI HASA KWA HAPA AFRIKA MASHARIKI……
MBALI LA HILO WAMETOA SHAVU KWA MADJs WOTE WANAOJIAMINI WANAWEZA KU HYP GOOD MIXING MUSIC KUTUMA APPLICATION S ZAO KUPITIA ACCOUNT ZAO ZA FB”Candy n candy records” NA TWITTER@candy n candy rec…..
KAZI KWENUUU, AND BIG UP SANA KWA CANDY N CANDY MUSIC RECORD LABEL KEEP IT UP!!!

UTAMU WA MKE WA MTU BALAA..USIOMBE HILI LIKUKUTE ACHA KABISA MCHEZO HUU

$
0
0



Utamu wa Mke wa Mtu ni balaa
Usiombe hili likukute ... acha kutembea na wake za watu......

SERIKALI YA ANGOLA YAZUIA DINI YA KIISLAM NA KUVUNJA MISIKITI YOTE

$
0
0
Angola bans Islam and shuts down all mosques across the country because it 'clashes with state religion of Christianity'


Minister of culture described Islam as a 'sect' which is banned as counter to Angolan customs and culture
Nation's president said: ‘This is the final end of Islamic influence in our country'



Angola has reportedly declared Islam illegal and ordered for all of the country’s mosques to be closed down.

Minister of culture Rosa Cruz e Silva said that mosques in the largely Christian country would be closed until further notice.

She described Islam as a ‘sect’ that would be banned as counter to Angolan customs and culture.

Angola (capital, Luanda, pictured) has reportedly declared Islam illegal and ordered for all mosques to be closed

There are unconfirmed reports that mosques across the African country are being destroyed, according to the International Business Times.

President Jose Edurado dos Santos reportedly told the Osun Defence daily: ‘This is the final end of Islamic influence in our country.’
Along with Islam, which is a religion associated with less than 1 per cent of the population of 19 million, 194 other ‘sects’ have been banned in the nation, where more than half the population is Christian.

Ms Cruz e Silva said: ‘The legalisation of Islam has not been approved by the Ministry of Justice and Human Rights [and] their mosques will be closed until further notice.’

Clashes between Christians and Muslim people are frequently reported in the local media.

source.Angola bans Islam and shuts down all mosques | Mail Online

YALIYOJIRI:MKUTANO WA CHADEMA NA WAANDISHI WA HABARI

$
0
0
Mheshimuwa John Mnyika, Tundu Lissu na Benson Kigailla ndio wazungumzaji wakuu.

Mnyika - amewaleeza waandishi kuwa sekritarieti ya chama ilikaa kikao chake jana kujadili mambo kadhaa ndani ya chama.

Ameeleza kuwa wahusika wamesha andikiwa barua zenye tuhuma zao 11 wanazotakiwa kuzijibu ndanj ya siku 14.

Ameeleza kuwa press conference waliyofanya wamejitungia tuhuma ambazo kimsingi sizo zilizo wavua nafasi zao.

Benson Kigailla anaeleza mikakati inayoendelea kwenye kanda ambayo kimsingi ripoti zililetwa kwenye kamati kuu.

Anasema mpango na programu ya chadema ni msingi pamoja na M4C kanda unaendelea kwa mafanikio makubwa kwani misingi inaendelea kuundwa na mpaka sasa zaidi ya wakunzi elfu tisa kutoka katika kanda mbalimbali wameshafundishwa.

Wakufunzi waliokwisha fundishwa.

Taifa 30

Kanda 40

Majimbo 956

Kata 19,408

Vijiji/Mitaa 72,000

Anaeleza kuwa kuna timu nne zimeundwa kwenda kwenye kanda mbalimbali kukagua misingi iliyokwisha simikwa.

Ziwa Mashariki misingi 3069 kati 7098

Ziwa Magharibi 3840 kati 9757

Kaskazini 3278 kati ya 8417

Juu kusini 2113 kati ya 10,857

Magharibi Kata 235 kati ya kata 315

kanda ya Kati Kata 363 kati ya 495

Kanda Kusini 219 kati ya 387

Kanda ya Pwani misingi 846

Tundu Lissu.

walichokifanya kina Zitto na Kitilla ni "Diversion" mashtaka yao yanatokana na waraka wa kihaini wa mabadiliko ambao ni kinyume na katiba na maadili ya uongozi, kuvuliwa kwao nafasi zao hakuhusiani na mambo ya PAC wala kuuza nafasi zetu za wagombea kwa maccm, wala kutokushiriki kwenye ziara za chama.

anawaambia waandishi, "wamevuliwa nafasi zao na kamati kuu kwa sababu ya waraka wenye nia ovu"

Anasema chadema haijaanza kufanya maamuzi magumu leo, ilishafanya hivyo kwa Dr Walid Kaburu na kwa Chacha Wangwe na mara zote vyombo vya habari vimekuwa vinaandika kuwa CHADEMA yapasuka, mara CHADEMA inakufa lakini kipindi chote haijawahi kufa wala kupasuka, na hata kwenye hili haitakufa kama ikitokea kamati ikiwafukuza.

Lissu alieleza kuwa - Kitilla amepotosha kuwa kamati kuu haina mamlaka ya kumvua yeye nafasi yake ya ujumbe wa kamati kuu maana amechaguliwa na baraza kuu. Amesema Zitto alipaswa kumkumbusha rafiki yake maana yeye (Zitto) alikuwepo kwenye kamati kuu iliyo mvua ukatibu mkuu Dr Walid kaburu, na makamu mwenyekiti bara Chacha Wangwe. kama iliweza kwa Kaburu na Chacha Wangwe (Katibu mkuu na Makamu mwenyekiti) imeweza na kwake pia ambaye hana vyeo hivyo, hivyo aache kupotosha umma kwa makusudi.

Mwandishi mmoja aliuliza kuhusu vurugu za kuchana bendera huko Kigoma, majibu yalikuwa - kurugenzi ya ulinzi na usalama ya chama imewasiliana na viongozi wa chama Kigoma na watalitolea wao taarifa lakini taarifa za awali ni kwamba ulikuwa mpango wa kuigiza ulioandaliwa na watu waliotumwa na wameshajulikana na hatua zaidi ziko chini ya uongozi wa tawi husika.

====================
Jamii Forums

JB: MLOKOLE MWENYE KICHAA CHA MUZIKI

$
0
0
AKISIKIA muziki unapigwa mahali fulani vinyweleo humsisimka, kichwa hutingishika na kama yuko mahali ambako anaweza kujiachia basi lazima aingie kati kuchangamsha mwili kwa kusakata rhumba.

Haijalishi ni muziki wa aina gani unapigwa wakati huo isipokuwa anachoangalia ni mazingira tu. Ukimpigia Bolingo, R&B, Country, Bongo Fleva zote zitamkuna. Yote kwa yote mwanamuziki anayeikonga roho ya JB duniani kote ni Don Williams.

“Ninapenda kusikiliza na kucheza muziki, lakini inategemea wakati huo nipo kama nani, nikiwa kama JB yaani mwigizaji kuna aina ya muziki huwa napendelea halikadhalika nikiwa Jacob,” anasema JB.

Anasema kutokana na kazi yake amejikuta akizijua aina nyingi za muziki na kujiongezea orodha ya nyimbo katika maktaba yake, lakini hii haijambadilisha kuwa yule mtu wa kawaida mwenye chaguo la kipekee.

“Unaniona kwenye majukwaa ya muziki, kumbi za starehe na kwingineko nikijirusha vilivyo, lakini huyo ni JB na si Jacob, Jacob anaenda kanisani na kucheza nyimbo za Injili,” anasema JB.

JB anasema yeye ni mlokole, hivyo katika maisha ya kawaida hupendelea kusikiliza nyimbo za Injili kwa kuwa ndivyo imani yake inavyomruhusu.

“Nimeokoka, mara nyingi huwa ninasikiliza nyimbo za Injili, lakini kwa sababu ninapenda aina nyingine ya muziki huwa ninasikiliza zile ambazo zina mafundisho,” anasema JB.

Anasema mbali na kusikiliza nyimbo za Injili, huwa anapenda kuwasikiliza wanamuziki kama Jose Chameleon, Ben Pol, Profesa Jay, Lady Jay Dee, Twanga Pepeta na wengineo wa nyimbo za kidunia.

“Ninapenda sana muziki, maisha yangu yametawaliwa na kusikiliza au hata kucheza pale ninapopata nafasi iwe nyumbani, kanisani hata kwenye hadhira,” anasema.

Anasema pamoja na kuwa huonekana katika kumbi za starehe na klabu za usiku, haimaanishi kuwa anakwenda huko kucheza muziki bali hufanya hivyo kujifunza mambo mbalimbali.

“Kama utakumbuka kabla ya kutengeneza filamu yangu ya ‘Senior Bachelor’, nilikuwa naenda sana klabu, sikwenda kule kufuata muziki ingawa kiukweli nilikuwa nafurahia, lengo langu lilikuwa kujifunza namna mapedeshee na madj wanavyojirusha ili niweze kuicheza nafasi hiyo vizuri,” anasema JB.

Akizungumzia ujio wake mpya katika filamu, mwigizaji huyo amesema yupo mbioni kuachia kazi mfululizo huku akisisitiza kuwa filamu yake mpya aliyoshirikisha mwanamitindo, Jokate Mwegelo, itatoka baada ya miezi sita.

“Napigiwa simu nyingi, kila mtu anataka kuiona filamu aliyocheza Jokate, lakini siwezi kuitoa mpaka mwezi wa nne mwakani kwani nina kazi nyingi ambazo inabidi zitoke kwanza,” anasema.

Akizungumzia sababu za kumshirikisha Jokate katika filamu hiyo iliyopewa jina la ‘Mikono Salama’, anasema ni kutokana na umbo lake ambalo lilionekana kuwa lingefaa katika nafasi hiyo.

“Unajua Jokate ana kaumbo fulani kazuri ambako unaweza kukachezesha nafasi yoyote, wasanii wengi wamezeeka kuna nafasi huwezi kuwachezesha tena,” anamalizia.
-Mwanaspot

BAADA YA ZITTO KUVULIWA UONGOZI VIJANA CHADEMA WACHAPANA MAKONDE NA KUCHANA BENDERA MKOANI MBEYA

$
0
0
Uamuzi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) wa kuwavua nafasi za uongozi vigogo wake watatu akiwamo aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu, Zitto Kabwe, umepokelewa vibaya na baadhi ya wafuasi wao ambao wameamua kupigana ngumi na  kuchana  bendera  za  chama  hicho. 
Zitto ambaye ni Mbunge wa Kigoma Kaskazini, alivuliwa nyadhifa zake sambamba na aliyekuwa mjumbe wa Kamati Kuu, Dk. Mkumbo Kitila na aliyekuwa Mwenyekiti wa Chadema Mkoa wa Arusha, Samson Mwigamba. 
Kamati Kuu ya chama hicho ilichukua hatua hiyo Ijumaa iliyopita, baada ya kubaini waraka wa usaliti waliouandaa ukiibua tuhuma mbalimbali dhidi ya chama na viongozi wake ngazi ya taifa. 
NGUMI ZAPIGWA MBEYA
Kundi la vijana wanaodaiwa kuwa ni wafuasi wa Zitto jijini Mbeya wanadaiwa kuchana  bendera  za  chama  hicho  na kurushiana makonde na viongozi wa Chadema katika ofisi ya chama hicho Wilaya ya Mbeya Mjini kwa madai ya kutofautiana msimamo kuhusiana na uamuzi wa Kamati Kuu. 

Mwenyekiti wa Chadema Wilaya ya Mbeya Mjini, David Mwambigija maarufu kwa jina la ‘Mzee wa Upako’, alithibitisha kutokea kwa vurugu hizo juzi mchana.

Mwambigija alisema kuwa chanzo cha vurugu hizo ni vijana zaidi ya 18 wanaodaiwa kuwa ni wafuasi wa Zitto kuanza kufanya vikao vya siri mjini Mbeya kwa nia ya kukihujumu chama. 
  Alisema uongozi wa chama ngazi ya wilaya ulipopata taarifa hizo alizodai kuwa ni za kiintelijensia na kuwa yeye (Mwambigija) ambaye ni Mwenyekiti wa Kamati Tendaji ya chama hicho wilaya, aliamua kuwaandikia barua ya kuwaita ofisini kwa lengo la kuwahoji. 

Alisema vijana hao walipofika ofisini kwake huku wajumbe wa Kamati Tendaji wakiwa tayari wameketi kwa ajili ya kuwahoji, waliingia ndani ya ofisi na kulazimisha wahojiwe kwa pamoja badala ya kuhojiwa mmoja mmoja. 

Alisema walipotakiwa watoke nje ili kila mmoja ahojiwe kwa wakati wake, waligoma na kukataa kutoka ofisini na ndipo yeye kama Mwenyekiti alipoamuru kikosi cha ulinzi wa chama hicho maarufu kwa jina la Red Bridged kuwatoa nje kwa nguvu na ndipo vurugu hizo zilipoanza. 
  “Ni kweli kumetokea vurugu kubwa ofisini kwetu wakati kikao cha kamati ya utendaji kikihitaji kuwahoji vijana wanaoendesha vikao vya siri kutaka kukihujumu chama kutokana na uamuzi wa Kamati Kuu kumvua Zitto madaraka, tumepata taarifa hizi kwa njia zetu za kiintelijensia kuwa vijana hawa wapo kwenye kundi la Zitto,” alisema Mwambigija. 

Hata hivyo, Mwambigija alipotakiwa  kuonyesha uthibitisho juu ya tuhuma dhidi ya vijana hao, alisema kuwa ushahidi bado ni siri kwa vile wametumia njia zao za kiintelijensia kubaini mtandao wa vijana hao. 

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Baraza la Vijana Mkoa wa Mbeya, Joseph Kasambala ambaye ni mmoja wa vijana walioitwa kuhojiwa na kamati ya utendaji alikanusha madai hayo na kusema kuwa vurugu hizo hazikuwa na uhusiano hata kidogo na  usaliti  wa  chama. 

Alisema chanzo cha vurugu hizo ni Kamati hiyo kumuita na kutaka kumuhoji kinyume cha katiba ya Chadema yeye (Kasambala) ambaye ni kiongozi wa mkoa, hivyo hawezi kuhojiwa wala kuwajibishwa na kamati hiyo ambayo ni ngazi ya wilaya. 

Alisema kuwa Katiba ya Chadema inaeleza wazi kuwa kingozi wa mkoa mamlaka yake ya nidhamu ni Kamati Kuu ya Chadema Taifa, hivyo kitendo cha ngazi ya wilaya kumuita na kutaka kumuhoji ni ukiukwaji wa Katiba. 
  “Mimi baada ya kupata barua ya kuitwa na Kamati hiyo ikinieleza kuwa nina tuhuma ambazo hazikuandikwa kwenye barua waliyoniletea, nilikwenda ofisini ili nipewe tuhuma zangu kwa maandishi kama ambavyo Katiba inaelekeza, lakini nikashangaa eti wanataka wanihoji, nikakataa walipotaka kunishinikiza vijana wakawajia juu wakipinga nisidhalilishwe na ndipo vurugu zile zilipoanza,” alisema Kasambala. 

KAMA KUNA WANAWAKE WANAO TAKA KUZAA NA MIMI WAJITOKEZE"BABA KANUMBA"

$
0
0
BABA wa marehemu Steven Kanumba, Charles Kusekwa amefunguka kuwa baada ya kutangaza kuwa wanawake wanaotaka uzao wake wajitokeze azae nao, wamejitokeza kumi lakini akawapa masharti, yakawashinda.

Akizungumza na mwandishi wetu, baba Kanumba aliweka bayana kuwa warembo hao waliojitokeza aliwapa sharti la kwenda kupima Ukimwi lakini ajabu wote waliingia mitini.
“Wamejitokeza vizuri lakini nashangaa wote wamekuwa wazito katika suala la kupima Ukimwi wameingia mitini, kama wapo wengine watakaolimudu sharti hilo, nawakaribisha,” alisema baba Kanumba

WARAKA HALISI WA MKAKATI WA MADILIKO 2013 CHADEMA UTATA MTUPU

$
0
0

Utata mkubwa umeibuka kuhusu waraka halisi wa ‘Mkakati wa Mabadiliko 2013’ uliosababisha Zitto Kabwe kuvuliwa wadhifa wake wa Naibu Katibu Mkuu wa Chadema na kikao cha Kamati Kuu ya chama hicho kilichofanyika Novemba 20 - 22, mwaka huu.

Baada ya juzi, Mkurugenzi wa Habari na Uenezi wa Chadema, John Mnyika kuwaeleza wanahabari kuwa waraka uliochapishwa katika magazeti na mitandao ya kijamii, siyo halisi, aliyekuwa Mwenyekiti wa chama hicho Mkoa wa Arusha, Samson Mwigamba amejitokeza na kuutetea huku akidai kwamba huo unaodaiwa na uongozi kuwa ndiyo halisi umeghushiwa.

Zitto ambaye pia ni Mbunge wa Kigoma Kaskazini (Chadema), alivuliwa uongozi pamoja na aliyekuwa Mjumbe wa Kamati Kuu, Dk Kitila Mkumbo na Mwigamba kutokana na madai ya kuandaa waraka huo ambao Chadema kimesema ulikuwa unaeleza mbinu za uasi za viongozi hao ambazo zingetumika wakati wa uchaguzi mkuu wa ndani wa chama hicho jambo ambalo ni kinyume na katiba, sheria na itifaki zake.

Katika tamko alilotoa jana, Mwigamba alidai kwamba

kuna njama zinazofanywa na baadhi ya viongozi wa Chadema ili kuubadili waraka halisi wa ‘Mkakati wa Mabadiliko 2013’ kwa lengo la kupoteza maana yake, huku akisisitiza kuwa waraka halisi hauna tatizo lolote.

Katika madai yake, Mnyika alisema waraka huo unaosambazwa na kuchapishwa, si ule uliowasilishwa na kujadiliwa katika kikao cha Kamati Kuu na kuahidi kuutoa waraka halisi ambao una mambo makubwa na mengi zaidi.

“Waraka utakaotumika katika mashtaka yao siyo huo. Sisi tutautumia ule ambao uliwasilishwa katika Kamati Kuu ambao una mambo makubwa na mengi zaidi kuliko huo unaochapishwa sehemu mbalimbali, ikibidi tutautoa huo waraka halisi,” alisema.

Hata hivyo, jana Mwigamba alisema waraka halisi ni ule ambao upo katika kompyuta mpakato (Laptop) aliyonyang’anywa na wanachama wa Chadema, Oktoba 25, mwaka huu, katika mkutano mjini Arusha.

“Waraka uliosambazwa kwenye vyombo mbalimbali vya habari na mitandao ya kijamii ni sahihi neno kwa neno kama nilivyousoma katika magazeti ya jana (juzi), pamoja na nakala iliyopo katika mtandao wa kijamii wa Jamii Forums.”

Aliongeza: “Ili kuthibitisha kwamba waraka ule ndiyo wenyewe, nawatumieni ‘soft copy’ kutoka kwenye kompyuta yangu kwani waraka huo uliibwa kutoka katika kompyuta hiyo ambayo nilirudishiwa baada ya wao kuikagua na kukuta waraka huo halisi.”

Mwigamba alisema waraka wake unatofautiana kwa kiasi kikubwa na ule ambao Chadema kinasema kuwa ndiyo halisi: “Lissu na wenzake wana mpango wa kuuchakachua waraka huu, lakini wamekwama.”

Alisema kuandaa waraka huo siyo uhaini kama ambavyo imekuwa ikielezwa na viongozi wa Chadema na kusisitiza kuwa ni waraka wa kusaka ushindi katika uchaguzi halali ndani ya chama hicho uliopangwa kufanyika Desemba mwaka huu na baadaye kusogezwa hadi Juni mwakani.

“Wakati wa uchaguzi si ajabu kuwepo kwa wanachama wanaounga mkono wagombea tofauti. Nimekuwa karibu na Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe kwa miaka mingi, najua hata yeye ana mikakati na wanaoshiriki mkakati wake ni Lissu na Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema,” alisema.

Alisema anashangazwa kwa kitendo cha Chadema kuusambaza waraka huo, wakati ulikuwa ni mpango wa siri kati yake, Dk Kitila pamoja na mtu mwingine anayetajwa kwa jina la M2.

“Baada ya kugundua madhara ya kusambaza ovyo waraka huo, sasa wameamua kuukana, waraka wangu ni sahihi na unaeleza ukweli. Binafsi nimefanya kazi ofisi ya makao makuu ya chama kama Mhasibu Mkuu ningeweza kuanika mengi lakini sijafanya hivyo kwa masilahi ya chama,” alisema na kuongeza:

“Tunatambua kwamba viongozi wetu wanamchukia Zitto na tangu siku nyingi walipanga kumfukuza. Nawashauri watafute sababu nzuri za kumfukuza uongozi na hata uanachama. Zitto hahusiki na mkakati huu pamoja na kwamba alikuwa ndiye mhusika mkuu, alikuwa hajui lolote.”

Jumamosi iliyopita, mama yake mzazi Zitto, Shida Salum ambaye ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema alisema waraka huo ulikuwa umeongezwa maneno.

“Hata ule waraka uliongezwa maneno baada ya baadhi ya wanachama kumpora Mwigamba `laptop’ yake alipokuwa mkoani Arusha katika kikao cha Chadema,” alisema bila kutaka kufafanua ulibadilishwa vipi, licha ya kuwataja kwa majina waliohusika kuubadili wakiwamo wabunge wawili wa chama hicho na viongozi wa ngazi za juu.

Sitoki Chadema

Kuhusu hatima yake ndani ya Chadema, Mwigamba alisema hana mpango wa kuondoka hata baada ya kuvuliwa uongozi, huku akisisitiza kuwa hakusudii kuomba radhi kutokana na kuandaa waraka huo.

Alisema hakusudii kuhama kwa kuwa ana historia ndefu na Chadema na anaamini kuwa ndicho mkombozi wa Watanzania.

“Nimekuwa kiongozi wa kata, wilaya, mkoa hadi taifa. Nimetumia muda wangu mwingi na hata kuhatarisha maisha yangu kwa ajili ya chama hiki, siwezi kuondoka kutokana na tofauti za kimitazamo na viongozi wangu,” alisema.

Mwigamba, ambaye alikuwa mfanyakazi katika Mahakama ya Kimataifa inayosikiliza Kesi za Mauaji ya Halaiki ya Rwanda (ICTR) na baadaye kujiondoa ili ajikite kwenye siasa, alisema ana imani yanayotokea sasa katika chama hicho yatapita salama.
Mwananchi

SIKILIZA NA DOWNLOAD WIMBO MPYA WA AMINI:USINIPE ROBO

$
0
0
Sikiliza na Download Wimbo huo Hapa chini :

RAIS WA MALAWI JOYCE BANDA ASHITAKIWE UMOJA WA NCHI ZA AFRICA

$
0
0
Taasisi isiyo ya kiserikali inayoshughulikia mambo ya utawala bora na maendeleo nchini (The Center for Good Governance and Development in Tanzania -CEGODETA), imeitaka Serikali ya Tanzania kumshtaki Rais wa Malawi, Joyce Banda Umoja wa Nchi za Afrika (AU).

Taarifa ya taasisi hiyo iliyosainiwa na Mkurugenzi Mtendaji wa taasisi hiyo, Thomas Ngawaiya ilisema uamuzi huo ni kutokana na kauli za dharau za Banda dhidi ya viongozi wanaoshughulikia mgogoro wa Ziwa Nyasa.

“Serikali imshtaki kiongozi huyo wa Malawi AU ili aulizwe ana dhamira gani kwa Tanzania na Afrika kabla hajaleta madhara makubwa kwa nchi yetu na Bara zima la Afrika.

Waswahili husema ‘Mchelea mwana kulia hulia yeye’ na ‘Mdharau mwiba mguu huota tende’, maana yake ni kuwa inawezekana huyu mtu ana mtandao mbaya sana tusioujua, tufanye uchunguzi kuubaini,” inasema taarifa hiyo.

Inasema kuwa, mara tu baada ya kuingia madarakani Rais Banda alidai kuwa Ziwa Nyasa ni mali ya Malawi kwa asilimia 100 na Tanzania haina haki ya kulitumia ziwa hilo kwa njia yoyote ile.

Taarifa hiyo inasema kuwa, mgogoro huo kwa sasa uko kwenye jopo la usuluhishi la marais wastaafu wa nchi za Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) chini ya Rais Mstaafu, Joachim Chissano wa Msumbiji.

MWIGAMBA:SITOKI CHADEMA NA WALA SIOMBI RADHI -ATOA UFAFANUZI KUHUSU WARAKA WA MKAKATI WA MABADILIKO 2013

$
0
0
TAARIFA YA SAMSON MWIGAMBA KWA WAANDISHI WA HABARI KUHUSU WARAKA WA MKAKATI WA MABADILIKO 2013


Jumatano, 27 Novemba 2013

Jana katika taarifa kwa waandishi wa habari, Mhe. Tundu Lissu na Mhe. John Mnyika waliudanganya umma kuhusu waraka unaohusu Mkakati wa Mabadiliko 2013. Katika maelezo yao waheshimiwa hawa, pamoja na mambo mengine, walidai kuwa waraka uliosambazwa kwenye vyombo mbalimbali vya habari ni feki. Ukweli ni kwamba:

Ninathibitisha kwamba waraka uliosambazwa kwenye vyombo mbalimbali vya habari na mitandao ya kijamii ni sahihi neno kwa neno kama nilivyousoma katika magazeti ya HabariLeo, Jamhuri na Rai, pamoja na nakala iliyopo Jamii Forum. Ili kuthibitisha kwamba waraka ule ndio wenyewe, nawatumieni ‘soft copy’ kutoka kwenye kompyuta mpakato (laptop) yangu ambako ndiko ulikoibwa na viongozi wa chama baada ya kunipora kwa nguvu laptop yangu Oktoba 25 na kukaa nayo hadi jioni ya Oktoba 28. Naomba kila mtu asome neno kwa neno waraka ninaowapa leo halafu afananishe na ule uliopo kwenye magazeti na kwenye mtandao ili mjiridhishe kama kweli sio wenyewe. Kama Lissu na wenzake wana mpango wa kuuchakachua waraka huu wamekwama!
Waraka huu si wa uhaini wala mapinduzi wala usaliti kama inavyodaiwa na akina Lissu. Huu ni waraka wa kusaka ushindi katika uchaguzi halali ndani ya chama ambao ulikuwa ufanyike Desemba 2013, na ambao sasa umesogezwa mbele.
Napenda ijulikane kwamba wakati wa uchaguzi si jambo la ajabu kuwa kwa wanachama kuwaunga mkono wagombea tofauti. Nimekuwa karibu na Mwenyekiti Mbowe kwa miaka mingi na ninajua kwamba yeye naye anao mkakati tena unaohusisha mbinu haramu za kuhakikisha anammaliza Zitto na yeye kupita bila kupingwa kwenye uchaguzi huo. Wanaoshiriki mkakati wake ni pamoja na Lema, Lissu na wakurugenzi kadhaa waliopo makao makuu.
Waraka huu ulipaswa kuwa siri ndani ya watu watatu tu (M1, M2 na M3) na haikutarajiwa kwamba ungevuja kwa jamii. Bahati mbaya viongozi wa chama baada ya kuunasa waraka huu kutoka kwenye komputa yangu mpakato (laptop), na baada ya kikao cha Kamati Kuu, waliamua, kwa jazba na bila kutumia busara ya kiuongozi, kuusambaza waraka huo kwenye vyombo vya habari kwa lengo la kuwakomoa na kuwadhalilisha waandaji. Sasa baaada ya kugundua madhara ya waraka huo machoni pa jamii wameamua kuukana. Ni ajabu kwamba wanaukana waraka ambao waliusambaza wenyewe.
Nasisitiza kwamba mambo yaliyopo kwenye waraka ni bayana na dhahiri. Sibahatishi kwa sababu mimi nimefanya kazi makao makuu kama Mhasibu Mkuu hadi Mwezi Aprili 2012. Ni kwa kutambua uozo uliopo katika uongozi wa chama makao makuu niliona umuhimu wa kubadilisha uongozi kwa njia za kidemokrasia ili tukiokoe chama na hatukuwa na nia wala sababu za kuanika haya yote kwenye umma. Kwa sababu za chuki na kukosa busara za kiuongozi huyo anayeitwa Mwanasheria Mkuu akawashauri viongozi wetu kijinga wauanike waraka mbele ya macho ya watanzania. Wangekuwa na akili na busara baada ya yote haya kutokea wangejiuzulu au kuitisha uchaguzi mara moja.
Tunatambua kwamba viongozi wetu wanamchukia Mheshimiwa Zitto Kabwe kwa siku nyingi sana na wametamani kumfukuza siku nyingi. Hata hivyo, ninawashauri watafute sababu nzuri za kumfukuza uongozi na hata uanachama kwa sababu yeye hahusiki na waraka wetu wa Mkakati wa Mabadiliko 2013 hata chembe, pamoja na kwamba yeye ndiye alikuwa na bado ndiye mlengwa mkuu, kama atakubali.



Samson Mwigamba (M3)
Arusha
Jumatano, 27 Novemba 2013.

UDAKU'Z PHOTO OF THE DAY-UMOJA NI NGUVU UTENGANO NI UDHAIFU

$
0
0
Umoja ni nguvu utengano ni udhaifu.....umoja wetu utatufanya tumuondoe our COMON ENEMY!

CHIDI BENZ AMEVURUGWA KWELI..!! TAZAMA ALICHOKIONGEA KATIKA HII POST YAKE

$
0
0

Hakuna tena kitu kizuri kwa Chidi Benz siku hizi. Kwa muda mrefu rapper huyo ambaye hivi karibuni ametokea kukubalika sana nchini Kenya (thanks kwa mashavu anayopewa na Nonini) ameonekana kutoa yake ya rohoni yanayomuumiza kupitia Twitter.

Yeye na Wakazi kuna tatizo?
Picha lilianza jana, baada ya Wakazi kutweet: Na ningependa kusema pia AY, Dimpoz, Ally Kiba, FidQ, Shaa, Cpwaa, Black Rhino, Remi Ongala, Profesa Jay & Lady Jaydee ni other Local heros!
Baada ya kuona ujumbe huo wa Wakazi, Chidi alimuuliza kishari ‘nini?’
Wakazi alichuna. Chidi akaamua kuandika: Hujui kuongea huwezi muoga..unaweza kuandika hapa twitter. Nyie ndio mkianza kushindwa mnasifia maadui.#umal** tuu.”
Ujumbe huo ulivuta hisia za watu wengi akiwemo Madee aliyeuliza: Rasheeed nani tena kazingua?  Chidi alijibu:Mazafanta wanahisi wanajua kuliko wewe wakati mwenyewe saa zingine unaona hujijui..2
Hata hivyo hatuwezi kuthibitisha kama maneno hayo yalikuwa yakimlenga Wakazi ama mtu mwingine kwakuwa kabla ya hapo tayari alikuwa ameanza kuandika tweets za hasira.
“Game ilipo now na propaganda zake inaua vitu vingi tu.sisi tunaonekana tunalalamika ujinga but hatuna maisha mabaya. Viongozi wa nchi sio lazima mdil na bongo freva..haiongezi wewe kufatwa but unatuongezea uadui usio na lazima. Mi natangazwa kwa ubaya tuuuuu.ila nina marafiki bado na wengi wanaongezeka hata hapa.#nakaza roho,” aliandika Chidi.
Kunani?

TANZANIA, CONGO NA BURUNDI WAUNDA MUUNGANO WAO BAADA YA KUTENGENGWA

$
0
0

Wakati Kenya, Rwanda na Uganda zimeunda umoja unaoitwa `Umoja wa Walio Tayari’ , Tanzania, Burundi na Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo (DRC) nazo zimeanzisha ushirikiano baina yao.
  
Katika siku za karibuni kumekuwa na mtikisiko ndani ya Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) baada ya Tanzania na Burundi kutengwa na wenzao wa Kenya, Rwanda na Uganda katika baadhi ya masuala muhimu ya ushirikiano hasa wa kiuchumi.

Tanzania, Burundi na DRC nazo zimekutana ikiwa ni utekelezaji wa ahadi ya Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta ambaye aliliambia Bunge lililopita kuwa Tanzania inafikiria kushirikiana na nchi hizo.
Mkutano wa ujirani mwema
Akizungumza na waandishi wa habari baada ya mkutano wa Ujirani Mwema uliofanyika mjini Bujumbura, Burundi jana, Sitta alisema Tanzania, Burundi na Kongo zimekubaliana kuendeleza miundombinu ya barabara, reli, anga na usafiri wa maji katika Ziwa Tanganyika.
Alisema mkutano huo ulilenga kuboresha miundombinu ya usafiri katika Ziwa Tanganyika ambalo linaziunganisha Burundi Tanzania, DRC na Zambia.
Pia tumepanga kuendeleza reli ya kati kutoka eneo la Uvinza, Tanzania hadi Msongati, Burundi na pia kuunganisha Barabara ya Manyoni - Tabora - Kigoma kupitia Bujumbura hadi Kivu ya Kusini, DRC,” alisema Sitta.
Mkutano huo ulihudhuriwa na Sitta pamoja na Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki wa Burundi, Leontine Nzeyimana na Waziri wa Uchukuzi wa DRC, Jack Lukeba.
Pia tulitembelea Bandari ya Kalindo iliyoko katika Ziwa Tanganyika upande wa Burundi kwani tunataka kuboresha bandari za ziwa hilo,” alisema Sitta.
Waziri huyo alisema Tanzania na Burundi zitaunganishwa na Barabara ya Manyoni – Tabora - Kigoma na Barabara ya Manyovu - Mgina, Mabanda - Bujumbura itakayounganishwa mpaka Kivu ya Kusini, DRC.
Kuhusu usafiri wa anga, Sitta alisema nchi hizo zinaangalia uwezekano wa kuanzisha safari za ndege za Dar es Salaam mpaka Bujumbura.

DIAMOND "PICHA ZA ZOEZI LA KUWAFANYIA INTERVIEW WALE WALIOTUMA MAOMBI YA KAZI"

$
0
0


Siku ya jana tulifanya zoezi la kuwafanyia interview
 baadhi ya watu waliotuma maombi yao kwa
 mujibu wa ,tangazo la kazi nilillolitoa
                                                                      juzi,mwitikio
 wa watu ulikuwa mkubwa,watu waliotuma
 email zao pamoja simu,kiasi ilituwia vigumu 
kuwataka wote waje kwenye interview,ilitubidi
 tuchague baadhi ya watu ambao tulihisi wanaweza
 kukidhi sifa tulizozihitaji ingawa nao pia tulipata
 changamoto ya wengi wao kuja pasipo kuzingatia maelekezo 
 na maagizo ya tangazo lilivyotaka,hivyo jana 
nikishilikiana na wataalamu wa hizo sekta tulisaili
 na mwisho wa siku tutachukua wale wenye viwango
 tunavyovihitaji na kuungana na team ya WCB-WASAFI,.....
Ahsanteni sana.

RAY NA CHUCHU HANS SASA LIVE LIVE..WAOMBA WASIINGILIWE PENZI LAO

$
0
0
Stori: Gladness Mallya
AMA kweli penzi ni kikohozi kulificha huwezi! Hatimaye uliokuwa uhusiano wa chini kwa chini wa nyota wawili wa sinema za Kibongo, Vincent Kigosi ‘Ray’ na Chuchu Hans, siyo siri tena baada ya wahusika hao wakuu kujiachia ‘live’, Ijumaa limeshiba.

KIMAHABA ZAIDI
Ishu hiyo ilitokea mapema wiki hii ambapo Chuchu alitundika picha kwenye ukurasa wake wa Instagram akiwa na Ray chumbani kimahaba.
Kufuatia tukio hilo kuliibuka gumzo kubwa na kulifanya jambo hilo kuwa ndiyo habari ya mjini katika ulimwengu wa mastaa wa filamu za Kibongo.

Katika picha hiyo, Chuchu anayetumia jina la Chukichuku kwenye Instagram aliambatanisha na maneno yaliyosomeka ‘Me n U’ akimaanisha yeye na Ray hivyo kutoa fursa kwa mashabiki wao kusema chochote.
Kwa mujibu wa mashabiki hao, Ray na Chuchu kwa sasa ndiyo love bird au ‘maua’ yanayopendezesha tasnia hiyo.
“Mmependezaaa…mapenzi waziwazi,” ilisomeka komenti ya mmoja wa mashabiki hao.

“Nilikuwa simuelewi Ray lakini hapa nimemsoma. Wamependeza sana,” ilisomeka komenti nyingine iliyoungwa mkono na mashabiki wengi kwa kupata ‘likes’ nyingi.
Mwingine aliandika: “Sasa walichokuwa wanagombea Mainda (Ruth Suka) na Johari (Blandina Chagula) kipo wapi? Ona sasa wamekosa wote… hahahaaa… wawaache miaka isiyohesabika.”

HAKUNA KIFICHO TENA
Katika kunogesha mambo, baadaye Chuchu aliweka picha ya Ray akimsifia jambo lililodhihirisha kuwa kwa sasa hawafanyi tena kificho kama miezi kadhaa iliyopita.
Habari za chini ya kapeti kutoka kwa wasanii wenzao wanaokuwa nao lokesheni zilieleza kuwa wawili hao wamekuwa wakionesha waziwazi kuwa wao ni item (kitu kimoja).

“Kuna siku tulikuwa tuna-shoot maeneo ya Sinza-Mori (Dar), yaani ungewaona wala usingeuliza maana kama hujui kusoma, ungeangalia hata picha. Yaani mapenzi kama njiwa!
“Sasa hivi ndiyo uhusiano ambao upo ‘hoti’ kwenye tasnia yetu, sema ndiyo hivyo wenyewe walikuwa hawapendi ijulikane lakini naona wameshindwa kuendelea kujificha,” alisema mwigizaji huyo kwa sharti la kutotajwa gazetini.

CHUCHU ATAKA WASIINGILIWE
Baada ya kujikusanyia data, Ijumaa lilimtafuta Chuchu akiwa mmoja wa wahusika wakuu ambapo alipopatikana alikuwa na haya ya kusema: “Hayo ni mambo yetu binafsi, naomba tusiingiliwe katika mambo yetu.”
Ijumaa: Chuchu wewe ni kioo cha jamii na mashabiki wako wanataka kujua ukweli juu ya uhusiano wako na Ray. Unalizungumziaje hilo?

Chuchu: Weweee…sikia! Nimeshasema sitaki mtu aniingilie mambo yangu. Kwani mnataka nini nyiye?
Ijumaa: Je, hiyo picha mliyopiga chumbani ni hotelini au nyumbani?
Chuchu: Siwezi kukuelezea tumepiga wapi, iwe hotelini au nyumbani haiwahusu, naomba mniache jamani mbona hivyo? Kwani vipi? (kisha akakata simu).

KAKA MKUBWA VIPI?
Jitihada za kumpata Ray ‘Kaka Mkubwa’ katika tasnia ya filamu za Kibongo ili kupata neno lake juu ya ishu hiyo ziligonga mwamba baada ya simu yake ya kiganjani kuita bila kupokelewa na hata alipofuatwa ofisini kwake, RJ Productions pale Sinza-Mori, Dar hakupatikana.

KABLA YA PICHA
Kwa muda mrefu kumekuwa na madai mazito kuwa Ray na Chuchu wanatoka lakini habari hizo zilikosa mashiko kwa kuwa hakukuwa na ushahidi wowote.
Ilidaiwa kuwa hata ile vita ya hivi karibuni ambapo Johari na Chuchu walizichapa kavukavu ilitokana na kugombea penzi la Ray.

JOHARI ASARENDA
Hata hivyo, baadaye Johari alinyoosha mikono kuashiria ‘kusarenda’ na kumwachia Chuchu atawale ulingo ambao ulimshinda pia Mainda.
Ilidaiwa kuwa katika kutekeleza kile walichokiita mpango wa siri, Chuchu na Ray waliunda kampuni yao na kuipa jina la kolabo la Chura wakimaanisha Chuchu na Ray.

TATIZO KUBWA
Wakati hayo yakiendelea, taarifa rasmi ni kwamba bado Chuchu ni mke wa ndoa wa bosi wa Kampuni ya 2 Eyez Productions, Frank Mtao anayeishi ughaibuni huko Australia akiwa ni mwenyekiti wa Wabongo waishio pande hizo.

Mbali na kuwa mke wa mtu, pia Chuchu ni mama wa watoto wawili hivyo uhusiano wake tata na Ray unalenga kuzalisha tatizo kubwa kwenye ndoa ya Chuchu ikiwa ni miezi kadhaa tangu wawili hao walipodaiwa kufumaniwa na mwanaume mwingine wa Chuchu.
-Global Publishers

PROFESA BAREGU AITAHADHARISHA CHADEMA KUHUSU ZITTO

$
0
0
Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema, Profesa Mwesiga Baregu amewataka viongozi wa chama hicho kutafakari na kudhibiti madhara yanayoweza kukikumba hasa baada ya hatua yake ya hivi karibuni ya kumvua nyadhifa zote, Naibu Katibu Mkuu, Zitto Kabwe na wenzake wawili.

“Bahati nzuri wamevuliwa uongozi siyo uanachama, binafsi nadhani  viongozi wanatakiwa kutafakari na kudhibiti madhara zaidi kwa chama, wakishupaza shingo, lolote litakalotokea watakuwa ni sehemu ya lawama,” Profesa Baregu alisema Dar es Salaam jana.

Zitto, aliyekuwa Mjumbe wa Kamati Kuu, Dk Kitila Mkumbo pamoja na aliyekuwa Mwenyekiti wa Chadema mkoani Arusha, Samson Mwigamba walivuliwa uongozi Novemba 22 mwaka huu, kwa tuhuma za kuandaa waraka wa Mkakati wa Mabadiliko 2013, uliolenga kufanya mabadiliko makubwa ya kiuongozi wakati wa uchaguzi mkuu wa ndani wa chama hicho kinyume na katiba, sheria na itifaki za chama.

Profesa Baregu alisema pamoja na viongozi hao kuvuliwa madaraka, mema waliyokifanyia chama hicho hayawezi kuyeyuka na kwamba makosa yao yasikuzwe kiasi cha kufuta mazuri yao katika kujenga chama hicho.

“Ni vigumu kuamini kwamba makosa ya Zitto, Dk Kitila na Samson Mwigamba yanaweza kuyeyusha mema waliyokifanyia chama kama barafu inavyoyeyuka juani.”

Profesa Baregu ambaye alikuwapo katika kikao kilichowavua uongozi Zitto na wenzake alisema kinachotakiwa kufanyika sasa ni kujenga uhusiano ndani ya chama na hasa kipindi hiki cha mpito kuelekea uchaguzi mkuu wa ndani ambao umeanza Novemba 22 na unatarajiwa kumalizika Juni mwakani.

Alitaka hatua dhidi yao zizingatie Katiba ya chama hicho ili kuhakikisha kuwa hazivurugwi na mamlaka nyingine zilizopo ndani ya Chadema akisema mkutano wa Baraza Kuu unaweza kubadili uamuzi wa Kamati Kuu.

“Kinachotakiwa kufanywa ni kuwatangazia wanachama misingi, taratibu na kanuni za kuzingatia katika harakati zao  ili kuondoa hali ya watu kufanya mambo kwa kificho,” alisema na kuongeza:

“Ni wazi wengi wapo katika kampeni, ichukuliwe kuwa walioshughulikiwa wamebambwa na iwe njia ya kuonyesha ukomavu katika kustahamiliana.”

Alisema asingependa kuona siasa za kulipizana visasi na kusisitiza kwamba hata kama mwanachama ana chuki binafsi na mwenzake, hatakiwi kutumia chuki hiyo kumhukumu.

“Tuhuma zinazotolewa dhidi ya Zitto na wenzake kwamba wamenunuliwa na chama fulani cha siasa zinahitaji maelezo na vielelezo vya kina ili kuwaaminisha wengi. Nasema hivi kwa sababu historia yao inadhihirisha kuwa wana uchungu na chama chao. Chama kinachoongozwa kwa demokrasia na kinachotarajiwa kushika madaraka ya kuongoza nchi, lazima kionyeshe uwezo mkubwa wa kuvumiliana, kutafakari, kusamehe, kuaminiana na kujenga umoja wenye lengo la kuelekea kusudio lake.”

Lwakatare

Mkurugenzi wa Ulinzi na Usalama wa Chadema, Wilfred Lwakatare alisema chama hicho kipo imara na hakiwezi kuyumba kwa sababu ya uamuzi huo.

Lwakatale ambaye pia ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya chama hicho alisema: “Mfumo wa ulinzi ndani ya chama upo imara, yakitolewa maelezo na ngazi za juu kinachofuata baada ya hapo ni utekelezaji.”

Alisema kilichotokea ni kitu cha kawaida na ni mwanzo wa chama kujiimarisha.

Temeke wapinga

Baadhi ya wajumbe wa Mkutano Mkuu na Baraza Kuu la Chadema hicho Wilaya ya Temeke wamepinga hatua iliyochukuliwa na Kamati Kuu ya kuwavua nyadhifa viongozi hao.

Mwenyekiti wa Vijana Mkoa wa Temeke, ambaye pia ni Mjumbe wa Baraza Kuu na Mkutano Mkuu, Joseph Patrick aliwaambia waandishi wa habari jana kuwa mgogoro huo haulengi kujenga chama, bali unakibomoa.

“Chama chetu kimekuwa na tabia ya kuingia kwenye migogoro kila panapokaribia uchaguzi wa ndani. Hii inasababisha kuchafuana na kutukanana miongoni mwetu kiasi cha kuitana wahaini, wasaliti na wengine kuwaita wenzao wanatumika kwa lengo la kuwadhoofisha mbele ya wanachama,” alisema na kuongheza:

“Tumeona mifano mingi ya namna hii. Wakati Chacha Wangwe akiwa hai alipotangaza kuwania uenyekiti, mgogoro wa namna hii ulijitokeza, aliitwa majina yote na hakuwahi kusemwa vizuri kwenye chama, hakuchafuliwa na watu walio nje ya chama, bali viongozi wenzake waliotofautiana kimsimamo.”

Alisema hali hiyo ilijitokeza pia kwa Zitto alipotangaza kuwania uenyekiti kama ilivyokuwa wakati wa chaguzi za viti maalumu na mabaraza ya chama.

Alisema ni vyema viongozi wakaitisha mkutano mkuu wa dharura na kuwaeleza wanachama mambo mbalimbali ikiwamo ni kwa nini wameamua kusambaza waraka ambao alisema unakidhalilisha chama badala ya waliouandika.

Katibu Chadema ahojiwa


Katibu wa Chadema Mkoa wa Dar es Salaam, Herry Kilewo amehojiwa na Polisi kwa kile kilichodaiwa kuwa ni kutokana na madai ya Zitto kutishiwa kuuawa.

Katika mahojiano hayo, Kilewo aliongozwa na Mwanasheria wake, Mussa Mfinanga, Mwanasheria wa Chadema John Malya na pia alikuwapo Diwani wa Ubungo, Boniface Jacob. Mfinanga alisema Novemba 11 mwaka huu, chombo kimoja cha habari kiliripoti kuwa Zitto ametishiwa kuuawa na mteja wake Kilewo.

Mfinanga alisema baada ya madai hayo, Jeshi hilo lilimwita Zitto kutoa maelezo yake na kisha kuona haja ya kumhoji Kilewo shutuma hizo. Alisema mteja wake amejidhanini mwenyewe na yupo nje kwa dhamana bila ya masharti yeyote.

Msemaji wa Polisi, Advera Senso alikiri kuhojiwa kwa Kilewo akisema ni kawaida kwa jeshi hilo kumuita mtu na kumhoji kwa mujibu wa taratibu na sheria zake.


Imeandikwa na Fidelis Butahe, Beatrice Moses, Pamela Chilongola na Editha Majura.
Viewing all 104709 articles
Browse latest View live




Latest Images