Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104684 articles
Browse latest View live

TEN THINGS TO NEVER POST ON FACEBOOK AFTER BREAK UP WITH UR LOVER

$
0
0
It’s over. Before you take to Facebook to let the world know of your newfound singledom, remember these simple rules about what not to post online following a breakup.

1. Rants. Don’t complain about this and that or recount every event. Facebook is not your diary. .  Just because you’re on an emotional roller coaster doesn’t mean that those ups and downs should be available for public consumption. Journal in private. Cry with close friends. Just stay away from your computer when you’re tempted to chronicle every stage of the breakup.

2. Sappy breakup songs. Put them on your iPod or our fan. More so listen to some hip hop or dub step instead. No one listens to breakup songs apart from the hurting ones.  Don’t keep quoting song lyrics, hoping that people might note and sympathize with you.  No one actually cares. Everyone has their life to live. So just stay calm and relax

3. Denial photos and messages. Take down that profile pic with you as a couple. Don’t post a message on their wall as if you’re still friends. Remove your relationship status (with as little fanfare as possible).

4. Resist the Facebook rebound. Don’t post photos of you with cute members of the opposite sex. Don’t message other exes or cute single “friends” out of discomfort for your new singleness. If you catch yourself posting anything that you hope will make your ex jealous, don’t do it. It’s a transparent move that will only make you look bad.

5. Cryptic notes about your ex or your emotional state. In fact, as a general note, don’t post cryptic notes on Facebook ever. If you don’t want people to know why you’re sad, don’t insinuate that you’re blue.

6. Don’t get friends involved. Don’t comment on wall posts by any of his/her friends. Don’t force mutual friends to defriend him in order to stay in your good books. If you have to hide statuses for a time, do so.

7. Revenge posts or attacks. Keep it classy. Repeat this motto: No slander, no revenge posts — ever. Do not attack your ex. Don’t be a psycho.

8. Don’t try to convince them to return, or publicly beg for forgiveness. This never works. It only shows desperation. If the two of you really need to talk, do so in person.

9. Don’t use statuses and photos to announce that you’re having the best or worst time ever. Don’t try to make your ex miserable. (Nor should you be assuming that they are reading your Facebook wall. You shouldn’t be reading theirs. It’s a waste of time.) If the two of you are meant to be back together, you will. Don’t force it.

10. Never admit to Facebook stalking. If you find yourself checking out their Facebook page, never comment that you’ve been there. Better yet, don’t check their page or timeline. Don’t write a status about the picture they just posted or the life they are leading without you.

JAGUAR NOMA..AWATOA JELA WALE WAFUNGWA ALIYO FANYA NAO VIDEO YA KIOO GEREZA NI

$
0
0
Mwanamuziki Jaguar wa Kenya Amefanya jambo la Maana baada ya kuwatoa wafungwa wawili jela ambao aliomba afanye nao Video ya Kioo Wimbo wake unao tamba sasa...Alifanya hivyo kwa kuwalipia Fine ambazo walikuwa wana dai na hivyo Serekali kuwaachia Huru....Big Kaka

KALA JEREMIAH"FILAMU TANZANIA HAZILIPI SINA SABABU YA KUINGIA HUKO"

$
0
0
Mwanamuzi wa Bongo Flava Ajulikane kama Kala Jeremiah aliye tamba na wimbo wake wa Dear God Amehabarisha kuwa Tasnia ya Filamu Tanzania Hailipi Kabisa kutoka na Muda mwingi wanaoinvest huko wakati malipo yake ni kidogo sana kiasi wengine wanahamia kwenye mziki kama wakina Shilole......Amesema anapenda sana kuingiza japo hawezi kwa sasa kutokana na malipo madogo.

WEMA SEPETU"SIUMIZWI NA NAIMA KUNICHUKULIA BWANA AISHI MAISHA YAKE"

$
0
0
Mwanadada Wema Sepetu Leo Amefunguka kwenye Segment ya U-heard ya Clouds FM na Suddy Brown kuwa Haumizwi kabisa na kitendo cha Rafiki yake ajulikanae kama Naima Kumchukulia Bwana "Clement" Amesema hana Beef nae kabisa kwa kuwa na yeye ana wake kwa sasa "Diamond i Guess" , Niko Happy kabisa na Nimeshamwambia Aishi Maisha yake Tuko Fresh kabisa nae.....

MZEE MAJUTO APIGILIA MSUMARI KAULI YA KALA JEREMIAH.."SOKO LA FILAMU HALILIPI BONGO BORA NIKALIME"

$
0
0
Mzee Small Ameliambia Gazeti Moja la Michezo Hapa Bongo kuwa Tasnia ya Filama Bongo Hailipi kabisa kwani walio shikilia soko wana Masharti magumu sana hivyo kujikuta msaanii hapati chochote ...Amezidi kusema kuwa ni bora aende akalime..Amesema kuwa akipata mfadhili wa kumpa Trekta basi atahama mjini na kwenda kulima kijijini...
Kauli hiyo inapigilia msumari kauli nyingine alie itoa msaani Nguli wa Bongo Flava Kala Jeremiah aliyosema kuwa hana sababu ya kuingia kwenye Tasnia hiyo kwani Hailipi hapa Bongo.....
Unaonaje ?
Udaku Specially.com 

MCHEZAJI WA YANGA WA ZAMANI ANYONGWA DAR

$
0
0
OMAR Changa, straika aliyekuwa na umbo la mwili lililokuwa likiendana na nafasi yake hatunaye, na habari kutoka kwa ndugu zake zinasema alinyongwa na watu wasiojulikana pamoja na kuchomwa na kitu chenye ncha kali maeneo ya kichwani na ubavuni.

Mchezaji huyo aliyetamba na Yanga alizikwa jana Jumatatu jioni katika makaburi ya Mwinyimkuu, Magomeni Dar es Salaam huku kifo chake kikiacha maswali mengi ya utata kuliko majibu.

Kwa mujibu wa kaka wa Changa, ambaye alikuwa mchezaji wa Moro United iliyoshuka daraja, kaka wa marehemu Idd Kambi, ameliambiaa Mwanaspoti kuwa kwa mujibu wa ripoti ya daktari aliyokabidhiwa baba wa marehemu, inaonyesha kuwa Omar Changa alichomwa na kitu chenye ncha kali mgongoni na kilichotokeza mbele ye tumbo huku pia shingo ikionekana kulegea.

“Mpaka sasa tumemaliza mazishi, lakini bado tuna huzuni kuhusu hii ripoti tuliyopewa, tunachofanya tunafuatilia ni timu gani aliichezea mara ya mwisho kwa sababu inaonekana inafichwa, lengo ni kujua mazingira ya mchezo yalikuwaje.”

Mdogo huyo wa marehemu alisema Omar Changa alimpigia simu Jumamosi iliyopita, akimtaka kwenda naye kushuhudia anavyocheza ndondo mchangani maeneo ya Kigamboni nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam.

Katika mchezo huo Changa alifunga bao moja la ushindi kwa penalti.

Mchumba wake marehemu aliyetambulika kwa jina la Sarah Mahemba alisema Changa hakurudi kwake tangu alipoondoka Jumamosi kuelekea Kigamboni katika mchezo huo, jambo ambalo liliwapa shaka wapangaji wenzake siku ya Jumapili na kuamua kumtafuta kupitia simu yake ya mkononi lakini haikupatikana ingawa yeye aliijaribu na kuwa inaita bila kupokelewa mpaka alipopata taarifa za kifo kupitia mdogo wa mshambuliaji wa Mbeya City, Omari Kijuso.

Mwili wa marehemu ulipatikana katika mtaro, maeneo ya Jangwani jijini Dar es Salaam.

SHILOLE AACHIA PICHA MTANDAONI AKIWA KATIKA KHANGA MOKO

$
0
0

STAA wa mduara Bongo, Zuwena Mohamed ‘Shilole’  ameamua  kuachia  picha  adimu  akiwa  kitandani  na  kanga  moja  tu  bila  chochote  kama  ishara  ya  kuwashukuru  mashabiki  wake  kwa  sapoti  kubwa  ambayo  wamekuwa  wakimpa  na  kumfanya  awe  juu  kimuziki…

URAIS CCM NI KAMA VITA-MPASUKO NDANI YA CHANA WAZIDI ONGEZEKA

$
0
0
Mpasuko ndani ya CCM unazidi kuongezeka baada ya viongozi wa chama hicho Mkoa wa Arusha na Wilaya ya Monduli kuibuka na kukemea ‘siasa za vitisho na hofu’ dhidi ya Mbunge wa Monduli, Edward Lowassa.

Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Arusha, Onesmo Ole Nangole, akiambatana na Mwenyekiti wa Wilaya ya Monduli, Reuben Ole Kuney na Katibu Mwenezi wa CCM Mkoa wa Arusha, Isaack Joseph alieleza kuchoshwa na kauli za vitisho dhidi ya Lowassa zinazotolewa na baadhi ya viongozi wa chama hicho, wakati wanachama wote ni sawa na hakuna mwenye ukubwa mithili ya tembo wa kumtisha mwenzake.

Kauli ya kiongozi huyo, imekuja siku mbili baada ya Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete kukemea vitendo vya rushwa kwa watu wanaotaka kuwania urais na kuiagiza Kamati ya Maadili ya chama hicho inayoongozwa na Makamu Mwenyekiti wa CCM, Philip Mangula kuwashughulikia.

Akizungumza katika mkutano wa utekelezaji wa Ilani ya uchaguzi katika Kata ya Monduli Mjini ambao pia ulienda sambamba na maadhimisho ya miaka 37 ya CCM, Nangole alisema wanachama wote wa CCM wana haki sawa na hakuna wa kuogopwa kama tembo, wala mdogo wa kunyanyaswa kama sisimizi, ili mradi hakuna ambaye anavunja sheria na taratibu za chama hicho.

“CCM ni yetu sote, hakuna mtu wa kuogopwa kama tembo wala sisimizi, mimi binafsi sijaona kosa alilofanya Lowassa hadi sasa. Kwa nini wanamfuatafuata na kumshambulia kupitia vyombo vya habari?” alihoji Nangole.

Alisema anawashangaa baadhi ya viongozi kuanza kutoa kauli za kumshambulia Lowassa na kumtishia kumpeleka katika Kamati ya Maadili ya chama hicho kwa tuhuma  kuwa, ameanza kampeni za urais, jambo ambalo sio kweli, kwani tangu mwaka 1993 amekuwa akiendesha harambee mbalimbali na amekuwa akifanya sherehe kila mwaka nyumbani kwake.

“Nakumbuka Rais Jakaya Kikwete mwenyewe alihudhuria sherehe nyumbani kwa Lowassa mwaka 2006 na alimpongeza kwa sherehe hiyo kwa kuwaalika marafiki zake wengi na kupokea mwaka mpya, lakini nashangaa sasa sherehe yake kuwa nongwa,” alisema Nangole.

Alisema anaamini kuna ajenda ya siri dhidi ya Lowassa, kwani hata makada wengine wa chama hicho wameonyesha nia ya kuwania urais, lakini hakuna ambaye anawasema.

“Kwani hatujuani? Tunajuana, wapo wanaopita wanasema hawajaoteshwa wanangoja kuoteshwa, wengine wanasema afya zao nzuri na wanaweza kuongoza miaka mitano, wengine wamesambaza kalenda nchi nzima na wengine wanapigiwa kampeni na viongozi wa juu wa chama, lakini hakuna anayesemwa zaidi ya Lowassa,” alisema Nangole.

Nangole alisema wao wanajua taratibu za chama, hivyo hawawezi sasa kuanza kampeni kabla ya muda mwafaka.

Alisema Tanzania ni ya watu wote na waliongia CCM ni kutokana na kuwa na imani ya chama hicho, hivyo hakuna sababu za ubabe na baadhi kujiona bora zaidi ya wengine.

Alisema Lowassa tangu mwaka 1993/4 alipokuwa waziri katika Ofisi ya Waziri Mkuu, alianza utaratibu wa harambee kusaidia wazazi waliokuwa na watoto wanaokosa nafasi ya shule na kuanzisha mifuko na alikuwa akienda kanisani na misikitini, iweje leo iwe nongwa?


“Mungu amempa uwezo akisimama watu humfuata nyuma katika kusaidia wanyonge, yeye ana nguvu za Mungu, nadhani hiyo ndiyo inamletea taabu. Sasa mimi niulize kuna kamati za maadili sawa, tangu mwaka 1993 ameanza harambee leo wanasema ameanza kampeni?” alihoji Nangole.

Alisema Lowassa amekuwa akisaidia kila pembe ya nchi katika nyumba za ibada na hafanyi kampeni, kwani hao wanaosaidiwa siyo wajumbe wa Mkutano Mkuu wa CCM.

Amshambulia Malecela

Alisema anamheshimu sana Makamu Mwenyekiti mstaafu wa chama hicho, John Malecela na alidhani angetumia busara zake kumsaidia Rais Kikwete ili kukabiliana na matatizo ya kijamii kuliko kuibua suala la fulana za kuashiria Lowassa ameanza kampeni.

“Tuna matatizo ya ajira, elimu, afya, ajali, rais anahangaika usiku na mchana, ningedhani huyu mzee mwenye umri mkubwa ameongoza nchi kama Makamu wa Rais, Waziri Mkuu na Makamu Mwenyekiti wa CCM, angemshauri Rais kwani tuna matatizo mengi kuliko  fulana. Mimi nadhani busara zake zingesaidia taifa kuliko fulana ambazo hata wanamichezo wanapewa. Nimesikitika sana,” alisema Nangole.

Nangole amekuwa mwenyekiti wa tatu wa CCM mkoa kujitokeza hadharani na kutoa matamshi ya kutetea kinachoelezwa kama mienendo ya Lowassa.

Wengine ni Khamis Mgeja wa Shinyanga na Mgana Msindai wa Singida wanaoungana na wabunge, John Komba wa Mbinga Magharibi na Beatrice Shellukindo wa Jimbo la Kilindi.

Lowassa asiwe na hofu

Kwa upande wake ole Kuney alisema anashangaa watu wanaomshambulia Lowassa bila sababu za msingi hasa kuhusiana na mbio za urais ambazo hata hajatangaza.

“Mbona watu wengi wanasema wanataka kugombea na wanajulikana, mbona hawasemwi. Tunamwomba Lowassa asiwe na hofu awapuuze hawa watu, wanatapatapa kama wafamaji,” alisema Ole Kuney.

Alisema lazima ijulikane Lowassa ana watu, ana marafiki wa kila aina, kwa hiyo akizunguka na wajasiriamali hakuna tatizo.


RAISI WA RWANDA KAGAME AZIDI KUICHOKONOA TANZANIA..CHADEMA WAJITOSA

$
0
0
*Sasa amgeukia Membe
*Chadema nayo yajitosa 
GAZETI la The New Times Rwanda ambalo linatajwa kuwa mshirika wa karibu wa Serikali ya Rais Paul Kagame, nalo limeingia kwenye propaganda za kuwachafua baadhi ya viongozi wa Tanzania.

Baadhi ya vyombo vya habari vya nchi hiyo, vimekuwa vikitumika kumchafua Rais Jakaya Kikwete, ambapo wiki iliyopita gazeti la News of Rwanda liliandika taarifa iliyodai kuwa Rais wa Tanzania amekutana na wapinzani wa Rais Kagame.

Hata hivyo taarifa hiyo ilikanushwa vikali na Serikali ya Tanzania, ambapo iliweka wazi kwamba Rais Kikwete hajawahi kukutana na watu hao waliotajwa na News of Rwanda na kwamba siku zilizotajwa kuwa rais alikutana na watu hao hakuwepo nchini.

Wakati Tanzania ikikemea propaganda hizo chafu, wiki hii gazeti la The New Times Rwanda, limehamishia uchokozi kwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wa Tanzania, Bernard Membe, kwamba alikutana kwa siri na mmoja wa waasi wa nchi hiyo alipokuwa jijini Washington DC nchini Marekani.

Gazeti hilo katika toleo lake la juzi, liliandika kuwa Membe alikutana na mmoja wa waanzilishi wa Chama cha Upinzani nchini humo cha Rwanda National Congress (RNC), Dk. Theogene Rudasingwa jijini Washington DC mwishoni mwa mwaka jana.

Habari iliyoandikwa na gazeti hilo, imebainisha kuwa kikao hicho cha Membe na Dk. Rudasingwa kilikuwa na lengo la kumwomba Membe amshawishi Rais Kikwete aonane na waasi hao kwa ajili ya kufanya mazungumzo.

Gazeti hilo lilidai kuwa limepata taarifa hizo kutoka kwenye vyanzo vyake vya habari vilivyokuwapo nchini Marekani mwaka jana, ambapo Membe alikwenda kuhudhuria mkutano ambao haukuwekwa wazi.

Ilielezwa kuwa baada ya Membe kuonana na kiongozi huyo, Januari 23 mwaka huu viongozi wa RNC walifanikiwa kukutana na Rais Kikwete.

Waliotajwa kukutana na Rais Kikwete ni Mratibu wa chama hicho, Dk. Rudasingwa na Mshauri wake, Condo Gervais.

Kabla ya gazeti hili kuandika uzushi huu, gazeti la News of Rwanda lilidai kuwa kundi la waasi la FDLR lilifanikiwa kukutana na Rais Kikwete nchini Tanzania na kwamba waliwakilishwa na Katibu Mtendaji wake, Luteni Kanali Wilson Irategeka na Kanali Hamadi ambaye ni kamanda wa operesheni.

Siku chache baadaye, mtandao wa AllAfrika uliandika kwenye ukurasa wake taarifa zilizokuwa zikimkariri, Faustin Twagiramungu akikiri kufika Tanzania na walionana na Rais Kikwete.

Baada ya uzushi huo gazeti dada la hili, MTANZANIA Jumapili lilifanikiwa kufanya mazungumzo na Twagiramungu ambaye ni Rais wa Chama cha RDI-Rwanda (Rwiz Party of Rwanda), ambaye alisema taarifa hizo za AllAfrika ni za uzushi wa hatari uliofinyangwa na makachero wanaofanya kazi kwa maslahi ya Serikali ya Rwanda. 

Mbali ya Twagiramungu, pia Dk. Theogene Rudasingwa ambaye alitajwa na News of Rwanda kuwa alikutana na Rais Kikwete, katika mahojiano yake na MTANZANIA Jumapili kwa njia ya simu akiwa nchini Afrika Kusini, alipuuza taarifa hizo na kudai kuwa ni mkakati wa Serikali ya Rais Kagame kutaka wapinzani wake wafungwe.

MTANZANIA Jumatano lilifanikiwa kuzungumza na Ofisa Habari wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Ushirikiano wa Kimataifa, Mkumbo Ali, ambaye alisema hafahamu kama Membe alikutana na Dk. Rudasingwa.

“Kwakweli sina uhakika na hilo na sifahamu kama kuna siku Membe alikutana na Dk. Rudasingwa,” alisema Mkumbo.

CHADEMA YAJITOSA 

Wakati huo huo, Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kupitia kwa Waziri Kivuli wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Ezekiah Wenje, ambaye pia ni mbunge wa Nyamagana wamejitosa kwenye chokochoko hizo za Rwanda kwa kuishauri Serikali ya Tanzania kutafuta jinsi ya kulimaliza suala hilo.

Mbali na ushauri huo pia, Wenje aliishauri Serikali kuhakikisha Waziri Mkuu wa zamani wa Rwanda, Faustin Twagiramungu anaiomba radhi Tanzania.

Wenje amemtaka Twagiramungu aombe radhi baada ya kunukuliwa na mtandao maarufu wa habari za Afrika wa AllAfrika, akisema katika kile kinachoelekezwa kuwa ni mkutano wa ndani uliofanyika katika mji wa Lyon nchini Ufaransa, jinsi alivyosafiri kwa siri kuja Tanzania na kukutana na Rais Kikwete.

Wenje alieleza kushangazwa na kauli za Twagiramungu kukana kukutana na Rais Kikwete, wakati kuna video ambayo inamuonyesha akizungumza nchini Ufaransa akieleza namna alivyosafiri kwa siri kuja Tanzania.

“Tunaiomba Serikali imtake huyu Twagiramungu aombe radhi kutokana na kauli zake, pia apewe barua ya ‘official demand aje open clearly’ na kutueleza ni kwanini anakanusha, wakati kuna video iliyokuwa inamuonyesha akizungumza hayo.

“Pengine watu wa aina ya kina Twagiramungu ndio wanaosababisha migogoro hii kwa maslahi yao binafsi, sasa tunaomba aje akanushe na aombe msamaha,” alisema Wenje.

Aidha Wenje alisema idara ya uhamiaji ni moja ya idara zilizooza hapa nchini, ambapo alihoji kuwa inawezekanaje hao waasi watumie hati ya kusafiria ya Tanzania wakati ni kinyume na mkataba wa Umoja wa Afrika (AU).

Katika kutaka suluhu ya mvutano huo, Wenje alipendekeza Bunge kupitia Kamati yake ya Mambo ya Nje, liunde kikundi kidogo kitakachopewa jukumu la kulizungumzia tatizo hilo na kufikia suluhu, kwani Watanzania wa kawaida hawajui tatizo la mgogoro.

“Sisi Chadema hatutaki kuona nchi jirani ya Rwanda inaingia katika mgogoro na Tanzania, ikumbukwe kuwa vita ni vita hata kama ni kidogo inaweza kuathiri kiuchumi na kijamii. “Tunajua leo ikitokea vita Rais hataumia atalindwa kwa mitutu ya bunduki, lakini atakayekuja kuumia ni Mtanzania wa kawaida, ni vyema tukaimarisha uhusiano wetu na hizi nchi jirani,” alisema Wenje.

UTATA KESI YA MTANZANIA AFRIKA KUSINI..NI ALIYE TISHIA KUTOA SIRI ZA MKE WA ZUMA

$
0
0
Kesi ya Mtanzania Stephen Ongolo anayeshikiliwa na polisi Afrika Kusini akituhumiwa kutishia kutoa siri za mke wa pili wa Rais wa nchi hiyo, Jacob Zuma, Nompumelelo Ntuli Zuma (MaNtuli), imeibua mabishano ya kisheria ya kuhusu mahali anapotakiwa kushtakiwa.

Gazeti la The Star la Afrika Kusini liliripoti kuwa baada ya Ongolo kupandishwa kizimbani kwenye Mahakama ya Camperdown jijini Durban, Jumatatu wiki hii, ilibainika kuwa Mwendesha Mashtaka wa Serikali, Ndoda January hakueleza ni wilaya gani ya kimahakama ambayo Ongolo alitenda kosa hilo. January alisema kuwa walishindwa kujua eneo alilofanya makosa Ongolo, kwani alikuwa akitumia ujumbe mfupi wa simu alioutuma kwa vyombo vya habari vya nchi hiyo.

“Tunashindwa kuelewa eneo gani ambalo mshtakiwa amefanya kosa kwa sababu mlalamikaji anaweza kuwa sehemu yeyote kati ya Camperdown na Nkandla ambako alipeleka ujumbe huo,” alisema January.

Kukamatwa kwa Ongolo

Ongolo alikamatwa na polisi jijini Durban mwezi uliopita kwa madai ya kumtishia mke wa pili wa Rais Zuma kuwa angetoa siri zake. Siri hizo zinahusiana na kifo cha mlinzi wa Rais Zuma, Phinda Thomo, ambaye alidaiwa kujiua bafuni kwake mwaka 2009.

Ongolo alikaririwa na Gazeti la Sunday Independent la Afrika Kusini akieleza kuwa Thomo hakujiua bali kifo chake kilipangwa baada ya siri kati yake na MaNtuli kubainika.

Gazeti la The Star la nchini humo, jana liliripoti kuwa hakimu anayesikiliza kesi hiyo, Thys Talijaard wa Camperdown alisema ili Ongolo apate dhamana hapo Camperdown, alitakiwa awe ameshtakiwa kwa makosa aliyofanya kwenye mahakama ya wilaya ambayo kosa limetendeka.

Ongolo alitakiwa kuomba dhamana Jumatatu lakini mwanasheria anayemtetea, Lekoa Le-koko hakuwapo mahakamani, na hivyo mashtaka kupangwa kusikilizwa tena jana.

Wakati mshtakiwa huyo akiwa mahakamani hapo ulizuka mjadala mzito kati ya January na Mdu Thuketana ambaye alishika nafasi ya Le-koko, wakijadiliana ni wapi mshtakiwa anaweza kushikiliwa wakati kesi yake ikiendelea kusikilizwa.

Thuketana aliomba Ongolo awe chini ya ulinzi wa polisi kutokana na afya yake kwani anasumbuliwa na maradhi ya pumu na pia walikuwa wakihofia usalama wake.

Wiki iliyopita, Ongolo alishindwa kwenda mahakamani baada ya kuugua pumu na kupelekwa hospitali.

Hata hivyo, January alisema mshtakiwa anaweza kuwekwa chini ya ulinzi wa polisi kwa siku saba tu, na baada ya hapo atapelekwa kwenye mahabusu za kawaida, jambo ambalo liliafikiwa na Hakimu Talijaard.

NJIA MPYA YA KUSAFIRISHA MADAWA YA KULEVYA NJE YA NCHI YAGUNDULIKA

$
0
0

Wauza sembe wamegundua njia mpya ya kusafirisha sembe kupitia JNIA kwa kutumia kampuni zinazosafirisha vifurushi. Naibu Waziri wa Uchukuzi Charles Tizeba ameimbia Kamati ya Bunge ya Miundombinu iliyotembelea JNIA kuwa wiki iliyopita mamlaka husika uwanjani hapo zimekamata jumla ya vifurishi nane vilivyokuwa na dawa za kulevya. 

Amesema jumla ya watuhumiwa nane wameshakamtwa kuhusiana na vifurishi hivyo na kuongeza kuwa wamiliki wa vifurushi hivyo bado hawajapatikana. 

Amesema moja ya vifurishi hivyo kinapelekwa nchini Nambia huku kikionyesha kuwa kulikuwa na kitabu cha biology. Lakini kilipochunguzwa kilikutwa kikiwa na kiasi kikubwa cha heroin iliyokuwa imewekwa ndani ya kusasa za kitabu hicho. 

Waziri ameongeza kuwa wauza unga pia wamekuwa wakitumia sandals na pakti za majani ya chai kusafirisha dawa za kulevya. Ameongeza kuwa vifurishi vingi vyenye dawa za kulevya vilikuwa vinaelekea nchi za Afrika Magharibi. 

Habari kwa mujibu wa gazeti la Shanghai Daily la China.

WINNIE MANDELA AAMBULIA PATUPU URITHI WA MANDELA, GRACA ARITHI ASILIMIA 50

$
0
0
Mke wa zamani wa Nelson Mandela, Winnie Madikizela-Mandela ameambulia patupu katika wosia wa kinara huyo wa vita dhidi ya ubaguzi wa rangi, imebainika.
Rais huyo wa zamani wa Afrika Kusini amegawanya mali zake zenye thamani ya Pauni za Uingereza milioni 2.5 kati ya wanafamilia yake, wafanyakazi na chama tawala cha African National Congress.
Hatahivyo, ameamua kutompatia chochote Winnie - mke wake wa pili, ambaye alizaa naye watoto wawili, Zenani na Zindziswa.
Wakati huohuo, mke wake wa tatu, Graca Machel, ametajwa kama mrithi mkuu wa wosia huo sababu ndoa yao ilikuwa 'kwenye mali ya jamii', kwa mujibu wa msimamizi wa mirathi, Naibu Jaji Mkuu Dikgang Moseneke.
Hivyo amethibitishwa kupata asilimia 50 ya mali zake, ambayo imethaminishwa kufikia Randi milioni 46 (sawa na Pauni za Uingereza 2.5), bila kuhusisha mirabaha.
Wosia huo wa Mandela wenye kurasa 40 - ulioandikwa mwaka 2004, na kufanyiwa maboresho mwaka 2005 na 2008 - ulisomwa mjini Johannesburg jana asubuhi.
Mgawanyo huo wa mali zake ulitarajiwa kuibua mgogoro mkubwa miongozi mwa watoto zake 30, wajukuu na vitukuu.
Lakini inaaminika kuwa umekubalika na familia yake bila pingamizi lolote mpaka sasa.
Kama mrithi mkuu, Mama Graca lazima adai nusu yake ya utajiri huo ndani ya siku 90, alisema Moseneke, ambaye aliungana na wasimamizi wa mirathi George Bizos, mwanasheria wa haki za binadamu ambaye alikuwa rafiki wa siku nyingi wa Mandela, na Themba Sangoni, jaji mkuu kutoka jimbo la Eastern Cape.
Aliongeza kwamba ingawa Winnie hakuwa ametajwa katika wosia huo, wajukuu zake kila mmoja atapata Dola za Marekani 9,000 (sawa na Pauni za Uingereza 5,500).
Moneseke alisema usomwaji wa wosia huo kwa ndugu wa Mandela 'ulienda vizuri' - lakini aliongeza 'kulihitajika ufafanuzi mara kwa mara'.
Utajiri wa shujaa huyo wa mapambano dhidi ya ubaguzi wa rangi umegawanywa kati ya taasisi tatu alizoanzisha, ikiwamo moja iliyoundwa kwa ajili ya kuhudumia ndugu wa familia yake, alisema.
Mandela, mfungwa wakati wa utawala dhalimu wa weupe wachache ambaye alikuja kuwa rais wa kwanza mweusi wa Afrika Kusini, alifariki Desemba 5 akiwa na umri wa miaka 95 - na kufuatiwa na kipindi cha siku 10 za maombolezo nchi nzima na kufurika salamu za rambirambi kutoka kote duniani.
Ameacha mali ambazo zinahusisha jumba la thamani kubwa mjini Johannesburg na nyumba ya wastani ya makazi kwenye kijiji chake alikozaliwa katika jimbo la Eastern Cape. 
Pia unahusisha mrabaha kutoka mauzo ya vitabu, vikiwamo 'Mandela's autobiography' na 'Long Walk to Freedom'.
MUHTASARI WA WARITHI WALIOTAJWA KATIKA WOSIA WA MANDELA:
Takribani watu 50 au taasisi zimetajwa kama warithi kwenye wosia wa Nelson Mandela, kwa mujibu wa muhtasari maalumu.
Warithi wakuu ni:
-        Mke Graca Machel, ambaye amekabidhiwa asilimia 50 ya utajiri wake, wenye thamani ya takribani Dola za Marekani milioni 4.1. Anatarajiwa kupata haki hiyo kwa kupokea vitegauchumi vinne nchini Msumbiji, magari, michoro, vito na mali nyinginezo.
-        Watoto wa Mandela kila mmoja atapata takribani Dola za Marekani 300,000, au kama waliwahi kukopa kiasi hicho kutoka kwake wakati wa uhai wake, deni lao litafutwa.
-        Watoto wa Graca, Josina Machel na Malengane Machel, kila mmoja atapata takribani Dola za Marekani 270,000.
-        Wajukuu wanne wa Mandela kwa marehemu mtoto wake wa kiume Makgatho kila mmoja atapata 300,000 na wameruhusiwa kutumia nyumba yake iliyoko Houghton, Johannesburg.
-        Chama cha ANC, kitapata kati ya asilimia 10 na 30 ya mrabaha kutoka kwenye miradi yake mbalimbali. 
-        Makazi ya Mandela katika kijiji alichokulia cha Qunu yatatumiwa na familia ya Mandela, na pia mjane Graca na watoto zake wawili.
-        Wajukuu kutoka katika ndoa yake ya kwanza Evelyn Mase na ndoa ya pili kwa Winnie kila mmoja atapata Dola za Marekani 9,000. Haikuwekwa wazi mara moja kama kuna chochote kimerithishwa kwa Winnie.
-        Wafanyakazi, akiwamo msaidizi wake binafsi wa muda mrefu Zelda la Grange, watapata Dola za Marekani 4,500 kila mmoja.
-    Mashule na vyuo vikuu alivyosoma na kuweka sawa maisha yake ya kisiasa kila kimoja kilitunukiwa Dola za Marekani 9,000.

BILL CLINTON NDANI YA KASHFA NYINGINE YA KUTOKA NJE YA NDOA NA KIMADA

$
0
0
Bill Clinton rais zamani wa Marekani aliwahi kuingia kwenye kashfa kubwa ya kuwa na mahusiano ya kimapenzi na Monica Lewinsky ambaye alikuwa na miaka 22 kipindi hicho akifanya kazi kama intern ndani ya White house.
Skendo hiyo ilivyoendelea kuwa kubwa ilimpelekea hadi Bill Clinton kukanusha waziwazi kwa kusema kwamba hakuwa na mahusiano ya kimapenzi na miss Lewinsky kama ilivyokuwa inasemekana.

Kitu kipya ni kwamba mtandao mmoja huko Marekani ambao hutoa habari za kuaminika, umetoa habari na kusema kwamba Bill Clinton alicheza faulo nje ya ndoa yake na actress/model Elizabeth Hurley.

Ripoti ya mtandao huo unasema kwamba Bill Clinton alikuwa na uhusiano na model huyo kwa muda wa zaidi ya mwaka mzima bila mke wake Hillary Clinton kujua.
Ripoti hizi kama zikithibishwa ukweli ndani yake, zinaweza kuharibu harakati za Hillary Clinton ambaye anajiandaa kugombania urais mwaka 2016.
Hata hivyo mwanamitindo/muigizaji Elizabeth Hurley hakukaa kimya na kuandika tweet akikanusha taarifa hiyo na kusema kila kitu ameshawakabidhi wanasheria wake washughulikie hili swala.

UJUMBE KUTOKA KWA WASTARA SAJUKI KUJA KWAKO

$
0
0
Tweet
"..Maisha ni mapambano na katika kupambana nayo kuna vizingiti vingi tena virefu utanue mguu kwa hatua kubwa kuvuka hivyo vizingiti, ukiamua kusonga mbele usigeuke nyuma pambana na kilichopo mbele yako kutimiza malengo yako katika maisha.." by - Wastara Sajuki

BAADA YA MIEZI 9 URIANI KAJALA AIBUKA TAJIRI WA KUTISHA

$
0
0
MIEZI tisa baada ya Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar kumhukumu staa wa filambu za Bongo, Kajala Masanja kifungo cha miaka mitatu jela au faini ya shilingi milioni 13 kwa kosa la utakatishaji fedha na Miss Tanzania 2006, Wema Sepetu kumlipia hivyo kuwa huru, hali ya maisha ya msanii huyo imebadilika ghafla na sasa ameibuka katika utajiri wenye maswali na majibu.

Kajala Masanja.
Chanzo makini kimeliambia gazeti hili kwamba, Kajala ambaye alitoka mahabusu ya Segerea jijini Dar, Machi 25, 2013 akiwa hana mbele wala nyuma kiasi cha kutia huruma, sasa anazikamata za kutosha kiasi cha watu wake wa karibu kumshangaa.

MANUNUZI YAKE 
Chanzo kimebainisha kuwa, Kajala ameagiza kutoka China kontena lenye urefu wa futi 20 likiwa limesheheni  samani za ndani. Samani za ndani ni fenicha mbalimbali.

Wema na shosti wake Kajala.
“Hivi mnajua kwamba Kajala yuko juu. Naweza kusema ni tajiri kwa sasa, maisha yake ni poa. Hivi ninavyoongea kuna kontena la futi arobaini linakuja Dar, ndani mna samani tu,” kilisema chanzo hicho.

AMWAGA MILIONI 90 KUTENGENEZA FILAMU
Katika hali inayoendelea kutafsiriwa kuwa ni kuzidi kuonesha ukwasi alionao, msanii huyo ameshatumia shilingi milioni 90 kwa ajili ya kutengeneza filamu zake tatu, kila moja ikitumia bajeti ya milioni 30 za Kibongo.
Filamu ya Kajala ambayo iko njiani kutoka inaitwa Laana. Inadaiwa mpango wake ni kutengeneza filamu 10 ambazo atakuwa akiziuza kwa nyodo. Kama ni hivyo atatumia shilingi milioni 300 kwa filamu hizo kumi.

ATUMIA MILIONI 11 KUNUNUA VITO VYA THAMANI
Mbali na kuvaa magauni na viatu vya bei mbaya, hivi karibu staa huyo alitua Dar akitokea China ambapo alipigilia vito vya gharama ya maisha ya familia nzima.
“Juzikati Kajala katoka China na cheni ya dhahabu kainunua dola za Marekani elfu tatu, bangiri pia ya dhahabu ya dola elfu mbili na mia tano na hereni za gold (dhahabu) za dola elfu moja mia tano,” kilisema chanzo.
Kwa mahesabu ya sasa, kiasi hicho cha dola kikibadilishwa na shilingi ya Tanzania, Kajala alitumia kama milioni 11 kununua vito hivyo tu. 

ANAYEMPA JEURI ATAJWA
Inadaiwa mcheza filamu huyo amekuwa akipata jeuri hiyo kutoka kwa mwanaume bilionea wa Ghana aliyejulikana kwa jina moja la Safara ambaye walikutana nchini China. Inadaiwa Safara anaishi Marekani lakini ndiye anayeshika tenda ya kuinunulia serikali ya Ghana vitu mbalimbali.

MWISHO DESEMBA KUISHI NYUMBA YA KUPANGA
Habari zikazidi kumiminika kwamba, Safara amemwambia Kajala mwisho Desemba mwaka huu kuishi kwenye nyumba ya kupanga, mwakani mjengo wake utakuwa umekamilika.
Hata hivyo, haijaelezwa kama ameshapata kiwanja cha kujengea au la! Ingawa habari zinasema nyumba anayoishi sasa Kajala imeshalipiwa kodi ya mwaka mmoja na tajiri huyo wa Ghana.

MFADHILI WEMA
Ikazidi kudaiwa kuwa, katika ziara ya baadhi ya mastaa jijini Arusha hivi karibuni wakiongozwa na Wema ambako kulikuwa na shoo ya muziki wa Kizazi Kipya, Kajala alimsaidia Wema mambo mbalimbali zikiwemo pesa ili kufanikisha shughuli hiyo iliyohitaji umakini wa hali ya juu.
“Mbali na fedha hizo, Kajala wa zamani si huyu wa sasa, ila ninashomsifu bado anamheshimu sana Wema, anajua ndiye amechangia mafanikio yake, kama siku zile asingetoa zile milioni kumi na tatu Kajala angekuwa gerezani,” kilisema chanzo hicho.

ALIPOTOKA GEREZANI
Inadaiwa baada ya kutoka Segerea, Kajala aliishi maisha ya kuwa na shida hata shilingi elfu kumi ilimsumbua, Wema ndiye aliyekuwa akimbeba kwa vijisenti vya matumizi na baadaye alimwajiri kwenye kampuni yake ya filamu ya Endless Fame kama sekretari. Kampuni hiyo kwa sasa imesimama.

HUENDA CHINA KINYEMELA?
Baada ya kuona safari zake zimezaa matunda na kuhisi watu wanafuatilia nyendo zake, likiwemo gazeti hili, Kajala ambaye husafiri mara kwa mara, amekuwa akidai anakwenda Zanzibar licha ya hati zake za kusafiria kuoneshwa zimegongwa mihuri ya China na Dubai.

KAJALA SASA
Alipoulizwa kwa njia ya simu juzi kuhusiana na ukwasi wake kwa sasa, Kajala alisema anachojua yeye anaishi maisha ya kawaida, tafsiri kwamba amekuwa tajiri ghafla inafanywa na watu  wanaomuona.
“Mimi naishi kawaida tu, huo utajiri wanauona wao. Unajua haya ni maisha, leo unakuwa hivi, kesho unakuwa vile ndicho ninachoweza kukisema, siwezi kusimulia kila kitu,” alisema Kajala.

Imeandikwa na Musa Mateja na Imelda Mtema.

GPL

ZITTO AIBUKA NA DVD, INAYOWANANGA VIONGOZI WA CHADEMA

$
0
0
Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe.
WAKATI Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe, akijipanga kuanza ziara katika mikoa kadhaa nchini kujibu mapigo ya tuhuma dhidi yake zilizotolewa na baadhi ya viongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kwenye ziara ya Operesheni M4C Pamoja Daima, mbunge huyo ameibuka na DVD inayowananga viongozi wa CHADEMA.
Vyanzo vyetu vya habari vilisema kuwa DVD hizo zitasambazwa kwenye mikoa na maeneo yote atakayofanya mikutano ya hadhara mbunge huyo, kama moja ya harakati na mikakati ya kujisafisha na tuhuma za usaliti zinazomkabili ndani ya chama.
Uchunguzi uliofanywa na gazeti hili umebaini kuwa DVD hizo zinatengenezwa kwenye kampuni moja iliyopo eneo la Kariakoo ambayo imepewa tenda ya kuchapa nakala 10,000 na kampuni nyingine zaidi ya tatu, nazo zimepewa tenda ya kuchapa DVD hizo kwa idadi tofauti.
Hata hivyo jambo la kushangaza ni kwamba katika jaradio la DVD hizo kuna rangi ya njano, nyeupe, bluu nyepesi, bluu nzito pamoja na bendera ya taifa.
Rangi zilizotumika kwenye jaradio hilo hazina uhusiano na rangi za bendera ya CHADEMA wala chama chochote cha siasa nchini.
Mbali ya jaradio hilo kupambwa na rangi hizo, pia limepambwa na picha kadhaa za mikutano aliyopata kuifanya mwanasiasa huyo katika maeneo mbalimbali na nyakati tofauti nchini, huku picha kubwa ikimwonyesha Zitto akiwa amevalia suti huku akitabasamu.
Jaradio hilo pia limezungukwa na maandishi mbalimbali ambayo yanasomeka:
‘Uadilifu, Uzalendo na Uwajibikaji, ndio silaha yetu katika kutetea wanyonge na maskini wote wa Tanzania, tuungane kwa pamoja.’  ‘Tanzania Kwanza’
Maandishi mengine makubwa yanamtambulisha mbunge huyo ambayo  nayo yanasomeka:
‘Zitto Zuberi Kabwe, Mtetezi wa Wanyonge, Tumaini la Maskini wa Tanzania”
Jaradio hilo pia limeweka mawasiliano ya mbunge huyo ya simu ya mkononi, barua pepe, Facebook na Twitter.
Hakuna maelezo yanayoonyesha kama DVD hizo zinauzwa au zinatolewa bure.
Ndani ya DVD
DVD hizo ambazo nakala tunayo, zinaonyesha picha ya mikutano ya hadhara ya mbunge huyo aliyoifanya mkoani Kigoma mara baada ya Kamati Kuu (CC) ya CHADEMA kumvua nyadhifa zake na Mahakama Kuu kushikilia hatima ya uanachama wake baada ya kukabiliwa na tishio la kuvuliwa uanachama.

Kwa mujibu wa DVD hizo, katika moja ya mikutano ya mkoani Kigoma, Zitto anasikika akiuambia umati wa wafuasi wake waliofurika kumsikiliza akieleza chanzo cha mgogoro wake na CHADEMA ni msimamo wake wa kuhoji hesabu za fedha za vyama vya siasa, kikiwemo CHADEMA na kumuagiza Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), kufanya uhakiki.

Kama ambavyo amepata kukaririwa mara kwa mara, Zitto ambaye ni Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) anasema CHADEMA ilimtaka awajulishe kwanza kabla ya kumuagiza CAG kufanya ukaguzi ili kutoa fursa ya kuweka hesabu zao vizuri.

DVD hiyo pia inamuonyesha Zitto akisema sababu nyingine ya ugomvi wake na CHADEMA ni dhamira yake ya kutaka kuwania uenyekiti wa CHADEMA, nafasi ambayo kwa sasa inashikiliwa na Freeman Mbowe, Mbunge wa Hai na Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni.

Huku akishangiliwa na maelfu ya wafuasi wake, baadhi wakiwa na mabango ya kumsifia, Zitto anasema hajawahi kupewa fedha na CCM kuisaliti CHADEMA na kuongeza kwamba atakuwa wa mwisho kutoka ndani ya chama hicho alichojiunga nacho akiwa na umri wa miaka 16.

Dk. Kitila Mkumbo naye yumo

DVD hiyo pia inamuonyesha aliyekuwa Mjumbe wa Kamati Kuu na Baraza Kuu la CHADEMA, Dk. Kitila Mkumbo, akieleza sababu za yeye kutaka kujiuzulu kabla ya Kamati Kuu kuamua kumvua uanachama.

Dk. Kitila pia anaonekana  kwenye DVD hiyo akielezea waraka ulioandikwa na Samson Mwigamba ambao ulinaswa ukielezea mikakati ya kutaka kuung’oa uongozi wa Mbowe kwenye nafasi ya uenyekiti.

Kwa kifupi maelezo ya Dk. Kitila ni  yale aliyopata kuyatoa siku yeye na Zitto walipofanya mkutano na vyombo vya habari katika Hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam wakitetea waraka huo kwamba haukuwa wa uasi kama ilivyotafsiriwa na CHADEMA.

Wiki iliyopita gazeti hili liliibua mkakati  unaodaiwa kufadhiliwa na  Chama Cha Mapinduzi (CCM) wa kutaka kumtumia Zitto kupambana na CHADEMA waziwazi.

Katika mkakati huo CCM inadaiwa kutaka kukodisha helikopta ya kumpeleka Zitto katika mikoa minne kwa gharama ya sh milioni 50, mara tu baada ya CHADEMA kuhitimisha Operesheni yao ya M4C Pamoja Daima.

Kwa mujibu wa taarifa kutoka vyanzo vilivyo karibu na Zitto na CCM, yeye na chama hicho sasa wana adui mmoja – CHADEMA; na wameamua kujibu mapigo baada ya kuridhika kwamba kwa vyovyote Zitto amekwisha kupoteza uanachama wake katika CHADEMA.

Nia yao ni kumtumia Zitto kuleta mpasuko katika CHADEMA, na kufunika mjadala wa mgogoro wa CCM, kero za wananchi na mchakato wa Katiba mpya.

Zitto ambaye alivuliwa nyadhifa zake zote ndani ya CHADEMA – Naibu Katibu Mkuu Bara, Mjumbe wa Kamati Kuu, Mjumbe wa Baraza Kuu na Naibu Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni – anatarajia kutumia helikopta yenye uwezo wa kubeba watu wanne, ambayo inadaiwa kukodishwa na wapinzani wa CHADEMA.

Kwa mujibu wa habari hizo, lengo la ziara ya Zitto ni kujibu mapigo ya CHADEMA, hasa katika maeneo ambayo baadhi ya makada na viongozi wa chama hicho wamepita na kuzungumzia hatima yake kisiasa, hasa walipojibu maswali ya wananchi kuhusu sakata lake kuvuliwa uongozi kwa tuhuma za usaliti, na hatimaye Zitto kwenda mahakamani kuzuia chama kujadili uanachama wake.

Katika kesi ya msingi, Zitto aliyewahi kuwa maarufu akiwa kiongozi wa CHADEMA, anaomba arudishiwe nyadhifa zake zote, na apatiwe nakala za uamuzi wa Kamati Kuu (CC) ili aweze kukata rufaa Baraza Kuu.
CHANZO NI TANZANIA DAIMA

MADAM RITA AWAPONDA VIBAYA WANAUME WASIO JUA KUWA WATANASHATI

$
0
0
Madam Rita Kaamua kufunguka kama hivi kwa wale wanaume wasio jua nini maana ya Utanashati..jisomee mwenyewe hapa chini

MISS TANZANIA FARAJA KOTA AMSIFIA MUMEWE WAZIRI NYALANDU..AELEZEA WALIPOKUTANA

$
0
0
Msikilize hapa chini Faraja Kota Akielezea kuhusu mumewe ambae ni Waziri Katika Bunge la Tanzania Pia Asema walipo kutana:

KWA WALE WANAUME WAHUNI HUU UJUMBE UNAKUHUSU

INGIA HAPA KUANGALIA PICHA ZA WATOTO MAPACHA WA MENGI NA JACKLINE WALIVYO WAZURI

$
0
0

Jamani  so so cute .....Au unasemaje Mdau wangu ..Embu tupia comment Basi ...
Viewing all 104684 articles
Browse latest View live




Latest Images