Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104785 articles
Browse latest View live

Dr Kessy Anakuletea Dawa za Kutengeneza Hips, Makalio, Nywele na Nguvu za Kiume Kwa Kutumia Dawa za Asili zisizo na Kemikali

$
0
0


Kifaa cha Kurefusha uume Kinachouzwa 160,000
Pendeza na Dr Kessy Products 
Ni dawa za Asili zisizo na Kemikali wala madhara yoyote kwa Binadamu, zimetengenezwa kwa kutumia mimea na matunda mbali mbali kukupa matokeo ya Haraka

1.Refusha Nywele na zisikatike  45,000/
2.Ondoa Mvi Sugu kichwani  45,000/
3.Toa Michirizi Mapajani, Chunusi na Madoa mwilini 40,000/
4.Punguza tumbo na Manyama uzembe 45,000/
5.Mkanda wa Kufunga Kupunguza tumbo 70,000/
6.Tengeneza Shepu Hips na Makalio  45,000/ ,Vidonge 80,000/
7.Ongeza Nguvu za Kiume  Jelly 45,000/ , Vidonge 60,000/
8.Ongeza Ukubwa wa Maumbile ya kiume Jelly 80,000/ , Mashine 160,000/
9.Kuongeza Mwili Mzima 40,000/
10.Kupunguza Mwili 45,000/
11.Kupunguza Maziwa na Kuyasimamisha 40,000/
12.Ongeza Mguu uwe wa Kupendeza 45,000/
13.Rudisha usichana ama Bikira 55,000/
14.Ongeza Hamu ya Kula 40,000/
15.Ongeza Hamu ya Kufanya Mapenzi 55,000/
16. Fanya mwili Kuwa Soft 60,000/
17. Dawa ya kutoa Michububuko kwenye mapaja 45,000/
18. Dawa ya kutoa maji maji sehemu ya siri na kukuacha mkavu 55,000/

TUNAPATIKANA DAR NA MIKOA YOTE, HUDUMA ZINAFIKA POPOTE ULIPO , 
DAR TUPO KARIAKOO MSIMBAZI NA POSTA  MPYA

PIGA SIMU: 0719955528, 0756259180 au 0785371237

Nuh Mziwanda Ajibu Tuhuma za Kumtongoza Wema Sepetu

$
0
0
Baada ya kusambaa sauti ya Nuh Mziwanda akimtongoza Wema Sepetu, muimbaji huyo ameibuka na kukanusha kuwa sauti hiyo sio yake na kumtuhumu Wema kuitengeneza sauti hiyo.

Akizungumza na mtandao  wa  Bongo5  akiwa na mpenzi wake Shilole, Nuh amesema kitendo kilichofanywa na Wema pamoja na timu yake sio cha kistaarabu.

“Mimi nimetake easy, ni mambo ya dunia kwa sababu ni mambo ya dunia ambayo yapo duniani. So wameamua tu kufanya vile sio suala ambalo lipo na sio suala sahihi,” amesema Nuh.

“Ile sio sauti yangu watu tu wameamua kufanya ili kunichafulia mimi labda na mpenzi wangu. Kwa sababu ukisikiliza mwishoni kuna mtu amejitaja jina lake. Ni kitu ambacho kimepelekwa studio wakaiweka sawa ili wapate kitu kibaya kije kwangu na Shishi. Hiki kitu sikukitegemea kwa sababu watu waliofanya kitu kama hicho ni watu ambao kwenye vitu vingi, kwenye mambo ya kampeni yaani mimi sijategemea,” ameongeza.

“Mimi hili suala nalichukulia kawaida na naona ni ushamba na upu*vu na hawana akili hata kidogo. Kama ni kweli, angemfuata Shishi akamwambia kwamba ‘mpenzi wako kafanya kitu fulani fulani kwangu’ sio kutangaza.

"Na kama kweli, kwanini asingesema wengine wanaomtongoza na akawaweka mtandaoni? Ni Wema pamoja na watu wake wote ndio wamefanya hivi! Siku ya kwanza Shishi alilipokea vibaya lakini baada ya kumuelewesha kanielewa,” amesisitiza.

Kwa upande wa Shilole amekiri kulipokea jambo hilo kwa mshtuko lakini tayari ameshamsamehe Nuh na maisha yanaendelea.

“Mimi sina ugomvi na mtu katika maisha yangu,” amesema Shilole.

“Kama wametengeneza ili wafanye hayo yote mimi sijali, watajua wenyewe, of course limeathiri mapenzi yetu. Sasa hivi tupo fresh, kwasababu mwenyewe ameshaniomba ‘mpenzi wangu samahani kwa kilichotokea lakini sio kweli.’ Nimeshamsamehe, mimi nimemuelewa alichosema Nuh basi.”

Kikwete: CCM Si Chama Cha Mchezo.......Wapinzani Watakiona cha Mtema Kuni Mwaka Huu

$
0
0
MWENYEKITI wa Taifa wa CCM, Rais Jakaya Kikwete amesema chama hicho sio chama cha mchezo na kuvionya vyama vya upinzani kuwa watakiona cha mtema kuni katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba mwaka huu.

Amesema CCM itapata ushindi katika uchaguzi huo kwa kuwa imejipanga kwa hoja na imeleta maendeleo nchini, huku akieleza kuwa wapo watu wenye tamaa ya uongozi ambayo imekithiri.

Aliungwa mkono na Mgombea Urais wa CCM, Dk John Magufuli aliyesema chama hicho kitashinda na haoni wa kuwashinda, huku akiahidi kuwa atakuwa mtumishi wa Watanzania kwani anazijua shida zao.

Rais Kikwete aliyasema hayo jana katika Ofisi Ndogo za CCM, Mtaa wa Lumumba, Dar es Salaam ambako alikuwapo kumpokea Dk Magufuli na Mgombea Mwenza Samia Suluhu Hassan baada ya kutoka kuchukua fomu katika Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) katikati ya Jiji ili kuomba kuidhinishwa kuwa wagombea.

“Sasa kazi ndio imeanza rasmi. Dodoma zile zilikuwa rasharasha. CCM sio chama cha mchezo. Watakiona cha mtema kuni. Kama ni mpira wa miguu, basi tumefunga bao wakiwa wamesimama. Tumejiandaa vya kutosha na kushinda tutashinda. Uzoefu, maarifa na uwezo wa kushinda tunao,” alisema Rais Kikwete na kuongeza:

 “Nawataka wanaCCM kujipanga, msimdharau yeyote hata mpinzani akiwa mdogo shughulikeni naye. Tumejipanga kwa hoja, tunazo hoja za kuzungumza. Nchi tulivu na maendeleo yanaonekana na duniani kote wanajua kuwa Tanzania inafanya vizuri. Tunao utawala bora, demokrasia na uhuru wa habari.

“Hata duniani wanajua hilo na wanaona fahari kushirikiana na Tanzania. Lakini wapo watakaokuwa na tamaa tu, duniani wapo watu wameumbwa hivyo, wengine wanayo tamaa hadi imekithiri, imevuka mipaka,” alieleza Rais Kikwete mbele ya maelfu ya viongozi, wanachama na mashabiki wa chama hicho tawala.

Rais Kikwete aliyefuatana na mkewe Mama Salma, alikatiza hotuba yake na kuliomba kundi la Tanzania One Theatre (TOT) kuimba wimbo wa “Waache waseme CCM ina wenyewe,” ambao alishiriki kucheza na mwisho wa wimbo huo, alisema: “Ni ushindi wa uhakika, hauna hatihati. CCM shangilia ushindi unakuja.”

Kabla ya kumkaribisha Dk Magufuli na Samia, Mwenyekiti huyo wa CCM alisema uzinduzi wa kampeni za urais kwa chama hicho utafanyika Agosti 22, mwaka huu na watatangaza wapi uzinduzi huo utafanyika kwani Viwanja vya Jangwani kwa sasa havina fursa hiyo kwa kujengwa miradi ya mabasi ya haraka na wafanyabiashara wadogo.

Alishuka jukwaani saa saba kamili mchana baada ya kuwatambulisha wagombea hao wawili, ambapo Samia kwa upande wake alisema haoni sababu ya CCM kushindwa kutokana na jinsi kazi ya jana ya kwenda kuchukua fomu ilivyokusanya maelfu ya wanachama, wapenzi na mashabiki wa chama hicho tawala.

Lakini, Dk Magufuli ambaye aliwasili Lumumba saa 4.47 asubuhi ili kwenda kuchukua fomu hizo, alisisitiza kauli ya Rais Kikwete kuwa CCM itashinda kwani chini ya uongozi wa rais huyo anayemaliza muda wake kikatiba, mambo mengi mazuri yamefanywa ambayo yanawafanya watembee kifua mbele.

“Kujitokeza kwenu kwa wingi leo ni ushahidi mwingine kuwa CCM itaendelea kutawala. Niwathibitishie kuwa shida za Watanzania nazijua, mategemeo ya Watanzania ninayo, na ipo misingi mizuri imewekwa chini ya Rais Kikwete.

“Nawaahidi nitakuwa mtumishi wenu sababu ninazijua shida za Watanzania. Watanzania wana tatizo la ajira, hawataki kero za ovyo kama kukimbizana na mama ntilie na bodaboda. Wanataka uchumi wao uwe mzuri, wanataka maisha mazuri zaidi. Nitayasimamia, nawahakikishia sababu kero hizo nazijua,” alisema Dk Magufuli.

“Nimekuwa mbunge kwa miaka ishirini na nimekuwa Waziri. Nimepata uzoefu kwa Rais Kikwete, Mzee Mwinyi, Mzee Mkapa, Mzee Nyerere, na viongozi wengine. Niko tayari kukipokea kijiti kwa mikono miwili. Nataka Mwenyekiti kukuhakikishia kuwa tutashinda, sioni wa kutushinda,” alisema Dk Magufuli huku akirudia maneno ya “sioni wa kutushinda” mara tatu.

Alisema atakuwa mtumishi wa Watanzania wote bila kujali dini, kabila, itikadi kwa sababu maendeleo ni ya wote, lakini akawataka wadumishe umoja na amani, na kuwaahidi kuwa hatawaangusha.

Napata shida sana kujua dhamira ya Mh Lowassa kwa Taifa la Tanzania na katika Siasa za Tanzania

$
0
0
1: Aliangaika sana kwa hali na mali kwa kutumia Pesa nyingi sana ndani ya CCM ili siku moja aweze kuwa Rais.

2: Kama angefanikiwa ndani ya CCM angetawala nchi kwa kufuata Sera za CCM na kudumisha Muungano wa Tanzania.

3: Leo hii amewakana CCM kwa kusema 'CCM si baba yangu wala mama yangu' kwa kutumia Pesa nyingi saana na kuhamia CHADEMA. Kama leo hii CCM imekanwa basi na wewe ukiwa kama mwanachama wa CHADEMA/UKAWA au Mwananchi wa kawaida wa Tanzania basi na wewe jiandae kukanwa wakati wowote.

4: Ametumia Pesa nyingi sana kuwashawishi CHADEMA na wengine (kuwanunua) ili awe mgombea pekee wa Urais kupitia UKAWA. Hii inaonesha wazi wazi ni jinsi gani Mh Lowassa hasivyopenda Demokrasia ya kweli na kupenda Uditekta kwa chochote atakacho.

5: Hivi Sasa amehamia CHADEMA kwa matumaini kwamba atashinda Urais na kama akifanikiwa basi atakuja kutawala nchi kwa kutumia sera za CHADEMA/UKAWA na kuvunja Muungano wa Tanzania na kuweka Serikali tatu.

Nikiwa kama Mwananchi nisiye na Chama chochote cha Siasa hapa Tanzania, napata shida saana kujua dhamira ya Mh Lowassa katika Siasa za Tanzania, napata shida sana kujua dhamira yake ndani ya Tanzania kitu ambacho kinanifanya KAMWE siwezi kumuamini chochote asemacho kuhusu swala lolote ndani ya Tanzania, kitu ambacho kinanifanya kutoamini chochote wasemacho CHADEMA/UKAWA maana kama wanaweza kununuliwa kwa mabilioni machache basi ata rasilimali za nchi na Serikali yao siku wakishika madaraka inaweza kununuliwa na Mataifa ya nje kwa pesa ndogo sana.

Kwa kutumia uzoefu wangu wa kutambua watu, Vitu vyote afanyavyo na matendo yake nayaona ni kama mchezo wa kuigiza and its too Good to be true haswa haswa sura yake ukiiangalia kwa makini sana you will see theres something fishy going on.

Kama kweli anauchukia Umasikini na anauchukia umasikini wa Watanzania basi katika mabilioni aliyoyapoteza kwenye Kampeni za kutaka kuwa Rais kupitia tiketi ya CCM na mpaka sasa CHADEMA/UKAWA basi kwanini asingetoa kiasi kidogo kwa Wananchi wa Tanzania na kuwasaidia??!

Je Mh Lowassa una dhamira gani ndani ya Tanzania, Je ni nani anayekutumia kuusaka Urais kwa namna hiyo?? Kwa malengo gani haswa??!

Watanzania, CHADEMA/UKAWA na vyama vyote vingine vya Siasa nchini muogopeni Mh Lowassa zaidi ya Ukoma, CCM wameona basi nanyi kuweni makini sana.

Asanteni.

Maoni Binafsi Toka Kwa Infinite wa JF

Matokeo CCM yazidi Kuwa Mwimba kwa Wabunge...Waziri Mwingine, wabunge 4 Waanguka Kura za Maoni CCM

$
0
0
SIKU mbili baada ya mawaziri watano kushindwa katika kura za maoni ya ubunge ndani ya CCM, waziri mwingine, Gaudentia Kabaka anayeshughulikia Kazi na Ajira, naye amedondoshwa katika jimbo la Tarime Mjini.

Kabaka, kabla ya kujitosa katika siasa za majimbo, alikuwa mbunge wa muda mrefu wa viti maalumu. Aidha, katika kura hizo zilizofanyika kote nchini, zimewaacha katika hali mbaya wabunge wanne, baada ya kushindwa katika kura za maoni majimboni mwao.

Hao ni Nyambari Nyangwine, Gaudence Kayombo, John Lwanji na Salome Mwambu.

Matokeo ya Tarime Mjini na Tarime Vijijini ambako Nyangwine ameanguka, yamethibitishwa na Kaimu Mkurugenzi wa Uchaguzi ambaye pia ni Katibu Wazazi Wilaya ya Tarime, Mathias Lugola aliyetangaza rasmi matokeo ya majimbo hayo.

Awali, matokeo hayo ya kura za maoni yaliahirishwa kutangazwa kutokana na kuwepo kwa tuhuma za kuwapo kwa wizi wa kura. Kwa jimbo la Tarime Mjini, Lugola alifafanua kuwa Michael Kembaki ndiye aliyeibuka mshindi kwa kura 3,908 akifuatiwa na Kabaka aliyepata kura 2,411.

Katika Jimbo la Tarime Vijijini, Mkuu wa Wilaya ya Arusha, Christopher Kangoye ambaye amejaribu zaidi ya mara tatu kuusaka ubunge, lakini bila mafanikio aliibuka mshindi akivuna kura 15,928 dhidi ya 12,205 za John Gimunta ambaye ni Mweka Hazina wa CCM wilayani Tarime.

Nyangwine na Gimunta, baadaye walilalamikia matokeo hayo wakisema mchakato wa kura za maoni ulitawaliwa na hujuma.

Kayombo azidiwa Mbinga
Katika Jimbo la Mbinga Vijijini, matokeo yaliyotangazwa saa 5:45 usiku baada ya mvutano wa kutangaza matokeo unaodaiwa kudumu kwa takribani saa 12, yameonesha kuwa mbunge wa jimbo hilo aliyekuwa amejitokeza kutetea kiti chake, Gaudence Kayombo ameshindwa katika kura za maoni ndani ya CCM.

Aliyeibuka mshindi ni Martin Msuha, aliyepata kura 13,354 dhidi ya 12,068 za Kayombo, ambaye pia kwa mwaka mmoja na nusu kati ya Januari 12, 2007 na Agosti 2, 2008 alikuwa Naibu Waziri wa Mipango, Uchumi na Uwezeshaji.

Wengine walioshiriki katika mchakato wa ubunge jimboni humo na kura zao kwenye mabano ni Humphrey Kisika (545), Dk Silverius Komba (1,289), Edesius Kinunda (2,355), Deodatus Mapunda (2,532), Benaya Kapinga (3,941) na Deodatus Ndunguru.

Wabunge Singida hoi
MCHUANO wa makada mbalimbali wa CCM kuwania nafasi za ubunge katika mkoa wa Singida umekamilika, huku wabunge waliokuwa wakitetea nafasi zao na baadhi ya vigogo kwenye chama hicho wakiwa wamebwaga vibaya.

Kwa mujibu wa Kaimu Katibu wa CCM mkoa wa Singida, Mary Maziku, wabunge wawili waliokuwa wakitetea nafasi zao hawakuweza kupata kura za kutosha kwenye kura za maoni. Nao ni Salome Mwambu wa Jimbo la Mkalama na John Lwanji wa Manyoni Magharibi.

Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Singida, Mgana Msindai ambaye aligombea jimbo la Mkalama alifanikiwa kushika nafasi ya pili kwenye kinyang’anyiro hicho kwa kupata kura 3,908 nyuma ya Allan Kiula aliyezoa kura 5,823. Jimbo hilo lilikuwa na wagombea 16.

LOWASSA: Tutachukua Nchi Asubuhi Asubuhi 'Hatuko Tayari Kuibiwa Kura'

$
0
0
EDWARD Lowassa ambaye ni mgombea urais kupitia Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), amesema chama hicho kwa ushirikiano na vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA) watashika dola Oktoba 25 mwaka huu saa 2:30 asubuhi. Anaandika Jimmy Mfuru … (endelea).

Akizungumza na wajumbe wa chama hicho kwenye Mkutano Mkuu leo jijini Dar es Salaam Lowassa amesema, hakuna sababu ya kutoa lugha za matusi huku akiwasihi kuimarishwa kwa amani wakati wa uchaguzi huo.

“Muungano huu una nguvu kubwa ya kwenda kuchukua dola saa 2:30 asubuhi, na tutachukua dola asubuhi,” amesema Lowassa na kuongeza; “hatuko tayari kuibiwa kura na hatutafanya fujo lakini wasiibe kura zetu.”

Amesema kuwa, katika maisha yake hana msamiati wa kushindwa isipokuwa ana msamiati wa kushinda huku akiwataka wana Chadema na UKAWA kuwa wamoja katika kukidondosha Chama Cha Mapinduzi (CCM) madarakani.
Lowassa amesema, wakati akiwa CCM safari yake ya kwenda Ikulu ilikuwa ‘Safari ya Matumaini’ na sasa ndani ya Chadema kwa usaidizi wa UKAWA safari hiyo inaitwa ‘Safari ya Mabadiliko nje ya CCM.’

Akiwa mwenye kujiamini amesema, changamoto kubwa ipo katika UKAWA kutokana na walio nje ya umoja huo kwa maana ya CCM kufikiria kuuvuruga.
Hata hivyo ameabainisha kuwa, hatua ya Chadema na UKAWA kumwamini na kumkabidhi bendera ya kupeperusha kwenye Uchaguzi Mkuu ujao ni nzito.

“Kazi miliyonipa ni nzito, nasisitiza kuwa sitawaangusha, nitawajibika kwa vitendo,” amesema Lowassa huku akiwahakikishia wajumbe hao kuwa chama hicho na UKAWA watashika dola.Lowasa ambaye ni Waziri Mkuu wa zamani na Mbunge wa Monduli amesema, hakukurupuka kufikia uamuzi wa kuhamia Chadema na kwamba, alifanya mashauriano na mkewe pamoja watu wanaomzunguka.
Amesema, “sikujiunga Chadema kwa bahati mbaya, nilikaa na mke wangu, familia yangu pamoja na watu wanaonizunguka na kufikia uamuzi huu. Nasema kuwa, kazi ya chama ni kushika dola na tumejiandaa kushika dola. Nitapita kila jimbo la nchi hii kuhakikisha tunachukua majimbo yote, kajiandaeni huko, nakuja.”

Upaja Wangu Ndio Silaha Yangu, Nikivaa Nguo Ndefu Sijiamini Kabisa Nakosa Confidence

$
0
0
Admin
Nimeona Nikuandikie e-mail Udaku Special Watu Wanipe Ushauri , Mimi ni Msichana Bado Mbichi Sana ila Tatizo langu ni Mavazi yaani Sijui inakuwaje kila nikitoka out ama Kwenda kazini nikivaa nguo ndefu sijiamini hata kidogo nakosa amani na hata furaha , ila siku nikiwa nimevaa nguo fupi basi najiamini si mchezo naweza kumface mtu yoyote , alafu napenda vile Kila mtu anavyoniangalia nikitembea with my High Heels..

Je Nitakuwa nimeathirika kisaikologia kimavazi ama ni Kawaida hata wadada wengine inawakuta hivyo?

Kigogo Ikulu Aokoa Jahazi...Azuia Nyumba ya Mwanamuziki Lady Jide Dee Kuuzwa

$
0
0
KISMATI! Ile nyumba ya nyota wa muziki wa kizazi kipya nchini, Judith Wambura Mbibo ‘Jide’ iliyopo Mivumoni, Kinondoni jijini Dar es Salaam, iliyowekwa mnadani zaidi ya mwezi mmoja uliopita, imezuiwa kupigwa bei na kigogo mmoja wa ikulu, Risasi Mchanganyiko lina full data.

Habari kutoka chanzo cha kuaminika zinasema kigogo huyo ambaye kutokana na hadhi yake hawezi kutajwa jina, mara baada ya kupata taarifa za mnada huo, alimuagiza mmoja wa wasaidizi wake kutafuta namba ya msanii huyo, ambaye wakati huo alikuwa China kwa shughuli zake binafsi.
Mzee alisikia kama nyumba ya Jide inauzwa, akawa anatafuta namba yake ili azungumze naye ajue tatizo nini, anaonekana anataka kumsaidia ili jambo hilo limalizike, bado sijajua kama atamsaidia hela au kumuombea muda zaidi wa kulipa deni hilo,” kilisema chanzo chetu.

Baada ya kupata ‘ubuyu’ huo, gazeti hili lilitaka kujiridhisha na ukweli wa habari hizo na lilipowasiliana na mmoja wa maofisa wa kampuni ya udalali ya Mem Auctioneers And General Brokers Ltd, waliotangaza mnada huo, alikiri kusitishwa kwa zoezi hilo.

Ni kweli zoezi limesitishwa, tulitaarifiwa na wateja wetu, taasisi ya fedha ya EFC TANZANIA LTD kwa kuambiwa kuwa wameshamalizana na msanii huyo, hatujui kama alilipa au kulikuwa na makubaliano mengine, lakini hilo suala la mkubwa kuzuia sisi hatulifahamu,” alisema ofisa huyo, aliyejitambulisha kwa jina la Mushi Dalali.
GPL

Isabela Achekelea Adhabu Aliyopewa Mwanamuziki Shilole na Basata

$
0
0
BAADA ya msanii na muigizaji Zuwena Mohamed ‘Shilole’ kufungiwa na Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) kwa kitendo chake cha kucheza nusu utupu jukwaani, msanii mwenzake Isabela Mpanda amechekelea adhabu hiyo na kusema liwe fundisho kwa wengine.

Akipiga stori na gazeti hili, Isabela alisema pamoja na kumhurumia juu ya maisha atakayoishi bila kufanya kazi kwa mwaka mzima wa kutumikia adhabu yake, lakini hatua hiyo ni nzuri kwani wapo wengi wenye tabia ya kucheza na kuacha matiti nje.

Mimi huwa sivai nguo inayoniacha matiti wazi, kwa nini wasanii hawafanyii majaribio kwanza ya nguo kabla hawajavaa na kutoka? Ninamhurumia na nampa pole maana sijui atawaleaje watoto wake watatu, maana anautegemea muziki katika kuendesha familia yake,” alisema Isabela.

UKAWA ipo Imara Sana Kuliko Kawauda Lazima itachukua Nchi- Ester Bulaya

$
0
0
Aliyekuwa Mbunge wa Viti Maalumu wa CCM aliyehamia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Ester Bulaya amefunguka na kusema kuwa

Umoja ya Katiba ya Wananchi (UKAWA) upo imara na utachukua dola japo amekiri kunachangamoto mbalimbali kutoka kwa chama tawala kutaka kuvuruga umoja huo.
Ester Bulaya ameyasema haya leo alipokuwa aki-chat live katika ukurasa wa facebook wa EATV katika Kipengele cha Kikaangoni ambacho huwa kinawakutanisha wananchi na watu mashughuri kila siku ya Jumatano kuanzia saa nane mchana mpaka kumi alasiri.

Katika zoezi hilo watu wengi walitaka kujua iwapo UKAWA unaweza kuchukua nchi na kukishinda Chama cha Mapinduzi (CCM) ndipo Ester Bulaya alipotoa mtazamo wake juu ya umoja huo ambao anadai ni tishio kubwa kwa CCM hivi sasa.
"Ukawa upo imara na utachukua nchi, ingawa changamoto hazikosekani pale ambapo mafanikio yapo karibu, kwani dola imejitahidi kuhakikisha Ukawa unasambaratika lakini kwa nguvu za Mungu bado umoja huo umesimama imara," alisema Ester Bulaya

Licha ya hayo Ester Bulaya aliweza kuweka wazi kilichomsukuma kukihama CCM na kwenda Chadema na kudai aliamua kufanya maamuzi hayo magumu kwa kuwa anachokiamini yeye na kukisimamia ni sawa na misingi na itikadi za Chadema, hivyo kutokana na maamuzi yake hayo anaamini yupo sehemu sahihi na yupo huru. Bulaya pia amedai misimamo yake pamoja na anachokiamini kilikuwa kinawakwaza CCM.

"Niliziona kasoro baada ya kuwa mbunge wa viti Maalum (CCM), kwani nikiwa umoja wa vijana ndani ya CCM moja ya mambo mnayofundishwa kwamba vijana ni watetezi wa taifa hili na sauti ya chama na kukemea maovu, nilipo anza kufanya vile nilivyofundishwa ikaonekana ni tatizo, hivyo nikagundua CCM inahubiri vitu tofauti na inavyoviamini, mdomoni unapaswa kusema vingine moyoni uamini vingine," alifafanua Ester Bulaya.
Katika hataua nyingine Ester Bulaya amedai kujifunza mambo mengi ndani ya muda mfupi alipohamia Chadema, kwani amegundua wazi kuwa viongozi na wananchama wake wapo tayari kujitolea kujenga na kuleta mabadiliko kwa watanzania.

"Kila chama kina utaratibu wake, lakini nilichojifunza Chadema viongozi na wanachama wake wapo tayari kujitolea kujenga chama na kuleta ukombozi wa kweli kwa watanzania na pia Chadema wanachokiubiri na kukiamini ndicho wanachokisimamia," alisema Ester Bulaya.

Amesema malengo yake ndani ya chadema ni kuungana na jeshi la ukombozi kuleta mageuzi ya kweli, siasa safi za demokrasia ya kweli na kuwakomboa watanzania kwa kuwaletea maendeleo ya kweli kutokana na rasilimali zao ambazo kwa miaka 50 ya utawala wa CCM wameshindwa kuyapata.
Ester Bulaya alikuwa mbunge wa kwanza kutoka katika Chama Cha Mapinduzi na kuhamia Chadema pamoja na aliyekuwa mbunge wa jimbo la Kahama James Lembeli ambao walitambulishwa na kukabidhiwa kadi za Chadema katika mkutano wa Chadema uliofanyika Jijini Mwanza.

Baada Sauti ya Mziwanda Akimtongoza Wema Sepetu Kuvuja, Shilole Kayaandika Haya mtandaoni

$
0
0
Nakukutanisha na msanii wa bongofleva Shilole ambaye aliingia kwenye headlines baada ya boyfriend wake msanii Nuh Mziwanda kunaswa kwa sauti akimtongoza mwigizaji Wema Sepetu.

 Ilionekana kama baada ya kusambaa hadharani kwa sauti hiyo kungefanya mapenzi yao yayumbe au waachane lakini imekua tofauti na matarajio kwani Shilole alithibitisha kuendelea kwao pamoja kwa kupost hiyo picha hapo juu na kuandika ‘Mi siachani nawe na ntakupenda zaidi

Licha ya Kupata Bwana Mpya; Johari: Siachani na Ray!

$
0
0
Ray na Johari Katika Pozi
SIKU chache baada ya kupenyezwa kwa madai ya kupata bwana mpya, staa wa filamu Bongo, Blandina William Chagula ‘Johari’ ameibuka na kuweka wazi kuwa kamwe hafikirii wala hana mpango wa kuachana na msanii mwenzake, Vincent Kigosi ‘Ray’ katika masuala ya kazi.

Akianika mwanya’ na Risasi Jumamosi hivi karibuni ndani ya ofisi zake, Sinza-Mori jijini Dar, Johari alisema hawezi kuruhusu mapenzi yatawale maisha yake na kusahau kazi.

“Siondoki RJ, kama kuna mtu anatarajia nitoke hapa eti kisa mambo ya mapenzi, anajidanganya kabisa, sifikirii kuachana na Ray kikazi, ni mtu muhimu sana, mapenzi hayawezi kutawala maisha yangu, yeye atabaki na mpenzi wake na mimi nitaendelea na mpenzi wangu,” alisema Johari.

Ray kwa sasa ameshaonesha upande na kukiri kukolea kwenye penzi la mwigizaji  Chuchu Hans na tayari ameshajipambanua kuwa wana mipango endelevu maishani mwao.

Chanzo: GPL

Ripoti iliyomng’oa Dk. Slaa Chadema yavuja....Ipo Hapa

$
0
0
Ripoti ya utafiti iliyokabidhiwa kwa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) inayomtaja Dk. Willibrod Slaa, kama mwanasiasa mwenye mvuto miongoni mwa wapinzani anayestahili kuwania urais kupitia Ukawa, hatimaye imepatikana; JAMHURI linathibitisha.

Kutupwa kwa ripoti hiyo kunatajwa kuwa ndiyo chachu iliyomfanya Dk. Slaa aachane na shughuli zote za kisiasa ndani ya Chadema. RIPOTI YOTE IMECHAPISHWA UK. 15-20 katika toleo hili la JAMHURI.

Utafiti huo uliofanywa na taasisi ya Tanzania Development Initiative Programme (TADIP) ambayo ni mali ya Chadema, unaonyesha kuwa Dk. Slaa anaongoza dhidi ya Edward Lowassa.

Ilikabidhiwa kwa uongozi wa juu wa Chadema Julai 26, mwaka huu, lakini chama hicho hakitaki kuitoa hadharani.

TADIP ni taasisi ya Chadema ambayo kazi yake kubwa ni kufanya utafiti na kutoa ushauri wa kitaalamu kwa chama hicho. Ripoti iliyokabidhiwa wiki mbili zilizopita, ni matokeo ya utafiti uliofanywa Mei na Juni, mwaka huu.

Kumekuwapo sintofahamu kati ya Dk. Slaa na viongozi wenzake ndani ya Chadema na Ukawa kwa jumla, lakini habari za uhakika zinasema mwanasiasa huyo amejiondoa Chadema kama njia ya kuonyesha kutokubaliana na wenzake kwa kumruhusu Lowassa kukaribishwa na hatimaye kupata ridhaa ya kukiwakilisha chama hicho na Ukawa kwenye uchaguzi wa rais.

Uongozi ndani ya Chadema unajitahidi kukanusha taarifa hizo, lakini uchunguzi uliofanywa na JAMHURI na vyombo vingine vya habari umethibitisha pasi na shaka kuwa Dk. Slaa amejiondoa Chadema.

Kaimu Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya TADIP, George Shumbusho, amekabidhi ripoti ya utafiti kwa Chadema baada ya kufanya utafiti/kura ya maoni katika mikoa minane ya Tanzania Bara, kata 113 na kuwafikia wapigakura 1,727.

“Utafiti huu ulilenga kujua utayari wa wananchi kushiriki uchaguzi wakati wa kupiga kura, wagombea urais na vyama vya siasa vinavyokubalika pamoja na vipaumbele vya wananchi,” amesema Shumbusho kwenye barua yake ya kukabidhi ripoti ya utafiti huo.

Nafasi ya Urais 2015

Kwa mujibu wa utafiti, Dk. Slaa anaongoza kwa asilimia 24.6 huku akifuatiwa kwa ukaribu na Waziri Mkuu mstaafu Edward Lowassa ambaye alipata asilimia 22.9. Wanasiasa wengine walionekana kukubalika katika nafasi ya urais ni Profesa Ibrahim Lipumba kwa asilimia 9.6, Benard Membe aliyepata asilimia 7.6 na Dk. John Magufuli ambaye anakubalika kwa asilimia 4.3 kwa mujibu wa utafiti huo.

Wanasiasa wengine waliobaki wakiwamo wengi wa waliokuwa wametangaza nia kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Kiongozi Mkuu wa chama kipya cha ACT walionekana kukubalika katika nafasi hiyo chini ya asilimia 3. Hata hivyo, kuna kundi la wananchi (asilimia 17) ambao hawakuwa wameonyesha kuwa tayari kumchagua kiongozi yeyote atakayewafaa.

“Pia, hali hii ya kukubalika inaweza ikaendelea kubadilika haswa ikizingatiwa kuwa utafiti huu ulifanyika kabla vyama havijafanya uteuzi rasmi wa wagombea. Kukubalika kwa wanasiasa katika nafasi ya urais kunaonyesha kutofautiana baina ya mikoa iliyohusishwa. Dk. Slaa na Lowasa ambao ndio wanasiasa wanaonekana kukubalika zaidi katika utafiti huu walikaribiana katika mikoa yote iliyohusishwa; isipokuwa walitoafutiana kidogo,” inasema ripoti hiyo.

Dk. Slaa analionekana kukubalika zaidi katika mikoa ya Mbeya na Kigoma; huku Lowassa akikubalika zaidi katika mikoa ya Arusha, Dar es Salaam na Singida. Profesa Ibrahim Lipumba na Membe walionekana kukubalika zaidi katika Mkoa wa Mtwara (mikoa ya Kusini) huku Profesa Mark Mwandosya akiwa anakubalika zaidi mkoani Mbeya. Dk. Magufuli anakubalika zaidi katika mkoa wa Mwanza ikilinganishwa na mikao mingine.

Matokeo haya yanaashiria kwamba mgombea wa urais atapata kura kwa kuzingatia eneo anakotoka na nguvu ya chama katika baadhi ya maeneo (mikoa).
“Utafiti huu pia umegundua kuwa watu rika tofauti tofuati wana mitizamo tofuati kuhusu nani anakubalika nafasi ya urais. Dk. Slaa na Lowassa wanaonekana kukubalika miongoni mwa Watanzania wenye umri tofauti tofauti,” inasema ripoti.

Hata hivyo, Dk. Slaa anaonekana kukubalika zaidi miongoni mwa vijana wenye umri kati ya miaka 27 mpaka 33 na watu wenye umri wa kati (miaka 38 mpaka 45) pamoja na watu wazima wenye umri wa miaka 51 mpaka 56.

Vijana wadogo, kati ya umri wa miaka 15 mpaka 26 wanaonekana kumkubali zaidi Lowassa wakifuatiwa na wazee zaidi ya miaka 56 ambao hata hivyo si wengi. Mbali na wanasiasa hao wawili, Profesa Lipumba, Membe na Dk. Magufuli walionyesha kukubalika zaidi kwa watu wazima wenye umri wa miaka 50 na kuendelea.

“Kutokana na matokeo haya, Dk. Slaa na Lowassa ndio wanasiasa wanaokubalika na makundi ya kiumri yenye asilimia kubwa zaidi ya wapiga kura,” inasema ripoti.

Ufuasi/uanachama wa Siasa

Vyama vyenye uwakilishi mkubwa bungeni vya CCM, CHADEMA na CUF vilionekana kuwa na wafuasi/wanachama wengi ikilinganishwa na vyama vingine. CCM ikiongoza kwa kuwa na asilimia 31.3 ikifuatiwa kwa karibu na CHADEMA kikiwa na asilimia 28.2 na CUF ilikuwa na asilimia 6.6 ya wafuasi/wanachama.

Vyama vingine vina asilimia chini ya 5 ya wafuasi/wanachama kwa mujibu wa utafiti huu.
Hata hivyo, kuna kundi kubwa la wananchi- sawa na asilimia 30 ambao walikiri kutokuwa na ufuasi/uanachama wa chama chochote.
“Hii inamaanisha kuwa vyama vyote vinahitaji kura za wafuasi/wanachama wao na za Watanzania ambao hawana chama chochote ili wapate viongozi bora. Sambamba na hilo, matokeo haya yanaashiria kwamba vyama vya upinzani vitakuwa na nguvu zaidi ama sawa na chama tawala endapo vitaunganisha nguvu zake,” umesema utafiti huo.

Chama gani kinakubalika 2015?
Matokeo yanaonyesha kuwa asilimia 42 ya wananchi wangechagua CCM; huku asilimia 37.8 wangechagua CHADEMA; na asilimia 10.1 wangepigia kura CUF.

Chama cha ACT kingepigiwa kura na asilimia 2.9 ya wananchi kikifuatiwa na NCCR-Mageuzi kwa asilimia 1.3; huku TLP na UDP vikiwa vya mwisho kwa asilimia 0.2 na 0.1.

“Kwa haya matokeo ni dhahiri kuwa umoja wa vyama vya upinzani (UKAWA) unaweza kupata ushindi ama kuleta upinzani mkubwa kwa chama tawala tofauti vile ambavyo kila chama kingeshiriki uchaguzi kwa kujitegemea.

Sambamba na hilo, wananchi wengi walioonyesha kutokuwa na ufuasi wa chama chochote wana uwezekano wa kupigia kura vyama vitatu ambavyo ni CCM, CHADEMA na CUF,” imesema sehemu ya utafiti huo.

Chama kitakachochaguliwa 2015
Wanachi walioshiriki katika utafiti wametoa sababu mbalimbali juu ya nini kitawasukuma kuchagua chama cha siasa.

Asilimia 27.7 wamesema wangechagua chama cha siasi kutokana na uongozi bora na sera makini, aslimia

18 walisema wangechagua chama kutokana na uwezo wake wa kuboresha maendeleo ya nchi. Wengine asilimia 14.3 walionyesha kuwa tayari kuchagua chama kutokana na uwezo wake wa kuleta mabadiliko kiuongozi na kiuchumi huku asilimia 10.8 wakioonekana kuchagua chama kutokana na kwamba kimekuwa madarakani tangu ukoloni, hawa ni wale ambao wangechagua chama tawala. Wanachi wengine walitoa sababu mbalimbali ambazo zinahusiana na uongozi bora, maendeleo na amani ya nchi.

“Matokeo haya yanadhihirisha kuwa wananchi watachagua chama kutokana namna kitakavyojinadi kushughulikia masuala ya maendeleo na uongozi bora. Hata hivyo, wapo wananchi ambao huenda wakapiga kura kutokana na mazoea ya chama tawala,” umesema utafiti.

Sababu za kuchagua chama
Kukubalika kwa vyama kunaonekana kuwa na tofauti mikoa mbalimbali. CCM iliongoza kwa kukubalika katika mikoa ya Arusha, Dar es Salaam, Mwanza na Singida. CHADEMA inakubalika zaidi katika mkoa wa Mbeya na kukaribiana na CCM katika mikoa mingine saba iliyohusika katika utafiti huo. Chama cha CUF kinaonekana kukubalika zaidi katika mkoa wa Mtwara huku ACT wakionekana kukubalika japo kwa kiasi kidogo katika mikoa ya Singida na Kigoma.

Kukubalika kwa chama kimikoa
“Kwa upande wa makundi rika, CCM inaoneka kukubalika zaidi kwa watu wenye umri wa utu uzima kuanzia miaka 45 na kuendelea huku CHADEMA kikionekana kukubalika zaidi miongoni mwa vijana na watu wenye umri wa kati. Kwa maneno meingine, CHADEMA itapigiwa kura zaidi na watu wenye umri chini ya miaka 45. CUF pia inakubalika zaidi kwa wazee wenye umri zaidi ya miaka 50. Hata hivyo, watu wenye mkubwa kwa mujibu wa sensa na kwa kujibu wa utafiti huu ni wachache chini ya asilimia 5,” utafiti umebaini.

Matokeo yanaonyesha kuwa CCM inakubalika zaidi kwa watu ambao hawana kiwango chochote cha elimu, na watu wenye elimu stashahada huku ikiwa imekabana koo na CHADEMA kwa kukubalika na watu wenye elimu ya msingi, sekondari na shahada ya kwanza. Vyama vya upinzani- CHADEMA, CUF na NCCR-Mageuzi vinaonekana kukubalika zaidi kwa watu wenye elimu ya juu, hasa shahada ya uzamili na shahada ya kwanza na kukubalika kwa kiasi kidogo miongoni mwa watu ambao hawana kiwango chochote cha elimu.

Utafiti unaonyesha kuwa makundi ya watu ambao hawajasoma na kundi la watu wenye elimu ya juu zaidi (shahada ya uzamili) yalikuwa na uwakilishi mdogo katika utafiti huo. Wengi wa wapigakura mwaka 2015 watakuwa na elimu ya msingi, sekondari na shahada ya kwanza.
Elimu na kukubalika kwa vyama

Mbali na makundi ya kielimu, utafiti huu pia umegundua kuwapo kwa tofuti juu ya kukubalika kwa vyama baina ya wanawake na wanaume. CCM ilionekana kukubalika zaidi kwa wanawake kuliko wanaume; huku chama wa CHADEMA kikionekana kukubalika zaidi wa wanaume. Vyama vya CUF na NCCR-Mageuzi viilikuwa na takribani asilimia sawa za kukubalika baina ya wanaume na wanawake.

Hitimisho na Mapendekezo
“Utafiti huu unaonyesha kuwa wananchi watakaoshiriki Uchaguzi Mkuu mwaka 2015 wengi wao watakuwa na umri wa ujana na umri wa kati (miaka 18 mpaka 40). Wengi wa wapigakura watakuwa na elimu ya msingi na sekondari na pia wengi watakuwa ni watu wanaojihusisha na kilimo, biashara na ujasiriamali. Kuna uwezekano pia wanaume wakawa na ushiriki mkubwa katika uchaguzi huu ikilinganishwa na wanawake.

“Asilimia kubwa ya wanachi wana utayari wa kupiga kura na asilimia ndogo wanaonekana kutokuwa tayari. Hata hivyo, ushiriki wa wapiga kura unaweza ukaathiriwa na sheria, kanuni, taratibu na taasisi zenye jukumu la usimamizi wa uchaguzi.

“Wanasiasa wakongwe watatu yaani Dk. Wilbroad Slaa, Edward Lowassa na Profesa Ibrahim Lipumba wa CUF ndio wanasiasa ambao wanakubalika zaidi katika nafasi ya urais. Hata hivyo, kuna uwezekanao kwa mitizamo ya wananchi juu ya nani anakubalika urais kwa kuwa utafiti huu ulifanywa kabla uteuzi rasmi wa wagombea haujafanywa na vyama vya siasa.

“CCM inaonekana kukubalika zaidi ya vyama vingine ikifuatiwa karibu na CHADEMA ambacho kinafuatiwa kwa mbali na vyama vingine vya upinzani vya CUF, ACT na NCCR-Mageuzi. Kwa mantiki hiyo, muugano wa vyama vya siasa vya upinzani ndio njia kuu kwa kuimarisha nguvu ya vyama hivyo na kuviwezesha kupata ushindi mwembamba ama kuleta upinzani mkubwa.

“Mbali na mambo ya wagombea na vyama vya siasa, wapigakura wangependa serikali ijayo iboreshe hali ya huduma za kijamii ikiwamo elimu, afya, na maji. Kujenga uchumi imara utakaoboresha sekta za kilimo na viwanda ili kuleta tija katika utoaji wa ajira. Wapigakura wangependa kuona serikali itakayosimamia rasilimali za umma na kuwekeza katika mapambano dhidi ya rushwa,” utafiti umebaini.

Mapendekezo kwa Vyama vya UKAWA
Taasisi ya TADEP imetoa mapendekezo yafuatayo kwa Chadema na Ukawa kama kweli wanataka kuishinda CCM. Mapendekezo hayo ni:
• Vyama viendelee kuwahamasisha wananchi kuendelea kujiandikisha katika Daftari la Kudumu la Wapigakura. Elimu juu ya sheria na kanuni za uchaguzi iendelee kutolewa ili kuwafanya wananchi wawe na ufahamu wa kutosha wasije wakanyimwa kupiga kura kutokana na wasimamizi wenye maslahi na chama tawala.

• Dk. Slaa ni mwanasiasa ambaye anakubalika zaidi kusimamishwa na UKAWA katika kiti cha urais ikizingatiwa kuwa Lowassa amekoswa kuteuliwa CCM katika kinyang’anyiro hicho. Pamoja na Mgombea Mweza kutoka CUF, viongozi wa CUF na NCCR- Mageuzi watamwongezea hamasa Dk. Slaa kwakushiriki katika kampeni za kumnadi.

•Ikiwa vyama vya UKAWA vitaendelea na ushirikiano wake wakati wote wa uchaguzi, kuna uwezekano kwa wapinzani kushinda uchaguzi mkuu japo kwa asilimia ndogo.

•Kwa kuwa bado kuna wananchi wanaonekana kutokuwa na ufuasi wa chama, kwa kuwa utafiti huu unadhihirisha kuwa watu watapiga kura kwa itikadi za kisiasa, ni muhimu vyama vya UKAWA vikaendelea na jitihada za kuingiza wananchama wengi zaidi katika vyama vyao.

•Mikakati UKAWA ni muhimu ikalenga kuwafikia watu wenye elimu ndogo/uelewa wa kawaida, watu wazima na wazee, pamoja na akina mama.
Vipaumbele vya wagombea na ilani za vyama vinavyounda UKAWA zinapaswa zizingatie vipaumbele vya wananchi ikiwa ni pamoja na umuhimu wa kuboresha huduma za kijamii za elimu, afya, upatikanaji wa maji safi na salama. Ilani zizungumzie mipango ya kujenga uchumi imara utakaojikita katika sekta za kilimo na viwanda. Mbali na hayo, wananchi wangependa kuona serikali itakayosimamia vyema rasilimali za taifa kwa kupambana na rushwa, hivyo ni muhimu ilani za vyama washirika wa UKAWA kuzunguzia mambo haya.

Pembe za ndovu 50 kutokea Tanzania, zanaswa zikielekea China

$
0
0

Customs officials at Zurich airport have seized 262 kilograms (578 pounds) of ivory that three Chinese men had dispatched from Tanzania, contraband that may have come from up to 50 elephants, Swiss authorities said Tuesday.
The ivory was found during a security check on July 6 and packed in eight suitcases, Switzerland's customs authority said. It put the estimated black market value at about 400,000 francs ($413,000).

The elephant tusks had been sawed into 172 pieces to fit into the luggage, which was being transported from Tanzania's capital, Dar es Salaam, to Beijing via Zurich. The head of the customs operation at the airport, Heinz Widmer, said officials estimate that the pieces came from 40 to 50 elephants.

Demand from China's rising middle class has been fueling elephant poaching in Africa and illegal trade in ivory, which is turned into jewelry and other decorative items.

The Chinese men were temporarily detained in Zurich and questioned, Widmer said. They could face large fines for violating customs and animal protection rules.

The suitcases also contained 1 kilogram (2.2 pounds) of lion fangs and claws — 21 fangs and 35 claws. They could be used as jewelry or talismans, or as a symbol for strength in Chinese traditional medicine, Widmer said.
The ivory haul, while sizeable, is below the 500-kilogram (1,100-pound) threshold considered to be a large-scale seizure that indicates the likely involvement of organized crime, according to TRAFFIC, a wildlife trade monitoring organization.

The group, which said that it doesn't speculate on the black-market value of ivory as a matter of policy, said the frequency of large-scale seizures has increased greatly since 2000, with 18 such hauls reported in 2013.
In May, a senior Chinese official made an unexpected pledge to halt the ivory trade inside the country, though it isn't clear how and when that ban might take effect.
Copyright 2015 The Associated Press. All rights reserved. This material may not be published, broadcast, rewritten or redistributed.
Swiss customs seize 578 pounds of ivory en route to China - US News

Makapi Aliyosema Mh. Kinana Haya Hapa

$
0
0
“Nchi yetu inakwenda kwenye uchaguzi ikiwa na wagombea na makapi, sasa kati ya mgombea na makapi nani mshindi? - Kinana 04/08/2015

Wadau kutokana na kauli ya Mh Kinana aliyoitoa wakati akihutubia wanaCCM waliofika Lumumba kumsindikiza Mh Dr John Pombe Magufuli kuchukua fomu ya uraisi wa JMT, alimaanisha kwamba kila aliyetia nia ya uongozi CCM na hakupata fursa hiyo ni makapi. Nijuavyo makapi ni mabaki yeyote baada ya mchujo/mchakato.

Katika mchakato ule kulikuwa na watia nia 42 na baadae 38 walifanikiwa kurudisha fomu. Katika mchujo ule ni Magufuli pekee aliibuka kidedea baada ya michujo kadhaa. Kwa mantiki hiyo aliyepita kwenye chujio ni Magufuli na wengine waliobaki ndiyo MAKAPI. Kama nilivyomwelewa Mh Kinana ina maana hao MAKAPI hata wakishindana na mgombea wao sehemu yeyote ile hawatashinda.
Kwa mujibu wa Mh Kinana alimaanisha hivi:

A. Mgombea
1. John Pombe Magufuli

B: MAKAPI ( Waliobaki baada ya mchujo)Kwa kuwa hakuna mgombea yeyote aliyefukuzwa CCM baada ya mchakato wa kumtafuta mgombea uraisi kwa Chama Cha Mapinduzi kukamilika, neno MAKAPI linabaki kuwahusu wale wote waliochujwa kwenye mchakato na yeyote (makapi) akishindana na mgombea popote pale watashindwa.
Ifuatayo ndiyo listi ya MAKAPI kulingana na kauli ya Mh Kinana:

Bilal
Lowasa
Pinda
Mwakyembe
Sitta
Nyalandu
Mwigulu
Makamba
Kigwangwala
Chikawe
Ali Karume
Mwandosya
Amina Salum Ally
Asha Rose
Membe
Wassira
Makongoro
Ngeleja
Mpina
Sumaye
Muhongo
Sanoko
Mahiga
Jaji Ramadhani
Dr Mwele
Murenda
Boniface Ndembo
Bw Bilohe (Mkulima)
Peter Nyalali
Helen Elinewinga
Anthony Chalamila
Dk Muzamil Kalokola nk.

Hatimaye Dr. Slaa Aonekana Baada ya Takribani Wiki Mbili Mafichoni

$
0
0
Mbunge mstaafu wa Moshi Mjini, Mzee Philemon Ndesamburo, maarufu kama "Ndesa Pesa", amekutana jijini Dar es Salaam leo na Katibu Mkuu wa CHADEMA ambaye ilielezwa hapo awali na chama chake kuwa kwa sasa yuko mapumzikoni, Dkt. Wilbrod Slaa, nyumbani kwake jijini Dar es Salaam.

Ndesamburo alifuatana na makada wenzake wa chama hicho, baadhi yao ni Meya wa Manispaa ya Moshi ambaye pia ni mgombea ubunge (mtarajiwa), wa jimbo hilo, Japhary Michael.

Hakuna taarifa yoyote iliyotolewa ya nini wamezungumza, ingawa makada hao wa CHADEMA walikuwa jijini kuhudhuria mkutano mkuu maalum wa chama hicho uliomteua Waziri Mkuu wa zamani Mhe. Edward Lowassa, kuwa mgombea wa kiti cha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, chini ya mwavuli wa muungano wa vuguvugu la Umoja wa Katiba ya Wananchi, UKAWA. Mgombea mwenza aliyeteuliwa ni Mhe. Juma Duni Haji.

Edward Lowassa Aendelea Kugawa DOZI!! Nguli Mwingine wa CCM Atua CHADEMA.

$
0
0
Edward Lowassa aendelea kugawa DOZI!!
Nguli mwingine wa CCM atua CHADEMA.
Aliyekuwa Mbunge wa KYELA na Mkuu wa Mkoa Mbeya - Ndugu John Mwakipesile ametangaza rasmi kuihama CCM leo na kujiunga na CHADEMA.

Nipo njia panda kuchukua uraia wa Tanzania – Christian Bella

$
0
0
Christian Bella aka ‘King of Best Melodies’ amesema bado yupo njia panda kuchukua uraia wa Tanzania huku akiimarisha zaidi makazi ya nyumbani kwao.


Bella anayetamba kwa sasa na video ya Nashindwa, ameiambia Bongo5 leo kuwa ingawa amekuwa akipokea ushauri kutoka kwa watu wa karibu lakini bado anaona kwa sasa sio muda sahihi.

Kupata uraia sio kitu rahisi,” amesema. “Naichukulia Tanzania kama nyumbani kwangu, tena najisikia furaha zaidi kwa sababu ni sehemu ambayo imenipa nafasi ya kufanya kile ninachokipenda maishani mwangu. Umaarufu nilionao Tanzania sio umaarufu nilionao Kongo. Wengi wamekuwa wakinishauri nichukue uraia lakini naogopa nisije nikajuta baadaye. Acha niendelee kutafakari kwanza, ikifika wakati basi hakuna kinachoshindikana,” ameongeza.

Pia Bella amesema kitu kingine kinachomuumzia ni kukaa mbali na mke wake pamoja na mtoto wake wanaoishi nchini Sweden.

Hii inanicost sana ninavyotaka kuonana nao. Sipendi niache familia yangu huko Ulaya na mimi nipo Bongo, yaani mtoto na mama yake wananimiss sana na mimi nawamiss sana. Lakini kikwazo ni mtoto anasoma na serikali ya kule inafuatilia sana watoto, huwezi kumtoa mtoto wako akae nje ya shule kwa miezi mitatu. Mtoto wanachukulia kama wa kwao hivi na mimi najua sio kitu kizuri kuacha familia yangu mbali na mimi nipo huku lakini ndo maisha,” amesema.

“Mimi muziki wangu unapendwa huku na sio kule. Hata nikienda kule na rangi hii nyeusi wataleta dharau,.”

Mwenyekiti wa CUF Profesa Ibrahim Lipumba Akana Kujiuzulu Uenyekiti CUF

$
0
0
Kufuatia kutokea sintofahamu iliyopelekea mkutano wa Mwenyekiti wa CUF Profesa Ibrahim Lipumba na Waandishi wa  Habari  kuahirishwa jana  asubuhi hatimaye, mida  ya  saa  nane  mchana  Prof. Lipumba alijitokeza na kukana kujiulu.

Katika mitandao mbalimbali ya kijamii kuanzia juzi zilienea taarifa kuwa Prof. Lipumba amejiuzulu, suala lililopelekea jana kuitishwa mkutano na Waandishi wa Habari katika ofisi zao zilizopo Buguruni jijini Dar es salaam lakini  ghafla mkutano huo uliahirishwa.

Sababu ya kuahirishwa mkutano huo inadaiwa kuwa  ni wazee wa  chama  hicho kumtaka Prof. Lipumba kuwaeleza kile alichopanga kuzungumza na waandishi .

Wazee kadhaa walichaguana na kwenda kuonana naye kujua alichokuwa amekusudia kuzungumza na waandishi wa habari hasa baada ya kuwapo kwa tetesi za kutaka kujiuzulu.

Akizungumza mara baada ya kufanya kikao na wazee hao Prof. Lipumba alisema kuwa hajajiuzulu  na kuwataka wanachama   kuhakikisha   kuwa  wanakijenga  chama  cha CUF.

“Mwaka 1995 nilikuwa mwanachama wa kawaida nilipogombea urais kwa tiketi ya CUF na mwaka 1999 nilikuwa mwanachama wa kawaida nilipoongoza kampeni za Jimbo la Temeke na Ubungo ambapo tulishinda lakini wakatuibia kura.

“Chama ni taasisi na tukijenge kama taasisi, ni wajibu wa kila mwanachama bila kujali nafasi aliyonayo kukijenga,” alisema na kuhitimisha kwa salamu ya; “hakiii” na kujibiwa “kwa wote,”

Funny: Jionee Wakenya walivyomshambulia Huddah baada ya kugundua shamba alilopost sio lake!

$
0
0
Socialite Huddah Monroe was not a lucky lass after a claim she had made on her instagram turned out to be fake according to KOT. It all started after the socialite posted pictures of a vegetable farm she claimed to be hers and went ahead to say that it is from it that she gets all the money to foot her bills as well as finance her international flights.

Keen Kenyans quickly revealed that she had just picked pictures from the internet and then created a photo-collage to make the farm appear to be hers. Below is a compilation of how KOT bashed Huddah for lying about her source of income.


Viewing all 104785 articles
Browse latest View live




Latest Images