Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104712 articles
Browse latest View live

Dr Slaa: Niko Salama, Wakati Ukifika Ntazungumza Kila Kitu

$
0
0
Siku tatu baada ya Baraza Kuu la Chadema kuridhia kumpumzisha kwa muda Katibu Mkuu wa chama hicho, Dk Willibrod Slaa baada ya kutofautiana na Kamati Kuu kwa kumkaribisha waziri mkuu wa zamani, Edward Lowassa, kiongozi huyo amesema yupo salama na wakati mwafaka ukifika atazungumza ya moyoni.

Akizungumza kwa mara ya kwanza na gazeti la Mwananchi tangu Chadema imkaribishe Lowassa na hatimaye kumpitisha kuwania urais kupitia muungano wa Ukawa, Dk Slaa amesema amekuwa akisikia mengi yakisemwa juu yake lakini yote yamekuwa yakimchekesha tu.

Hakuhudhuria vikao muhimu vya chama hicho na vile vya Ukawa, vikiwamo; wakati Lowassa akitambulishwa rasmi, akichukua fomu, kikao cha Baraza Kuu na juzi Mkutano Mkuu na hakuwa akipatikana kwa simu yake ya mkononi.

Wakati kimya kikitawala juu ya hatima yake, baadhi ya vyombo vya habari vimekuwa vikiandika kuwa amejivua uanachama Chadema.

Lakini jana alisema: “Naangalia mambo mengi yanayoendelea kwenye mitandao halafu ninacheka tu, usifikiri sifuatilii, nafuatilia kinachoendelea na ninabaki nikicheka.”

Kuhusu hatima yake kisiasa na madai ya kujiuzulu uanachama ndani ya Chadema, alisema hawezi kuzungumza lolote kwa sasa na atafanya hivyo wakati mwafaka ukifika.
 
“Usijali wakati wangu wa kuzungumza ukifika nitasema tu, sasa hivi nawaachia mzungumze, lakini nitazungumza,” alisema.

Kadhalika, alipoulizwa kuhusu taarifa zilizozagaa kuwa maisha yake yapo hatarini kwa kuwa anatishwa, Dk Slaa alisema hata hilo pia atalizungumzia wakati mwafaka ukifika.

“Ndiyo hayohayo ninayosema, wala msijali nitazungumza wakati ukifika,” alisema na kusisitiza: “Nipo salama.”

Dk Slaa alisema kwa sasa yupo mapumzikoni nje ya jiji la Dar es Salaam ingawa hakutaka kueleza ni eneo gani.

Juzi, Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe alifafanua tofauti iliyojitokeza kati ya Kamati Kuu ya Chadema na Dk Slaa wakati wa mchakato wa kumpokea Lowassa.

Katika mkutano huo wa Baraza Kuu la Chadema, Mbowe alisema wamekubaliana katibu mkuu huyo apumzike kwa muda... “Nina hakika kwa tabia na hulka za Dk Slaa… kwa sababu anajua tunampenda na yeye anakipenda chama hiki, tunamwombea kwa Mungu ampe nguvu na ujasiri wa kuona kwamba kauli ya wengi ni kauli ya Mungu.”

Ndesamburo na siri nzito
Mbunge wa Moshi Mjini, Philemon Ndesamburo na makada wengine wa Chadema, jana walikwenda kuonana na Dk Slaa nyumbani kwake na kufanya naye kikao cha faragha.

Picha zilizomuonyesha Ndesamburo akiwa na Dk Slaa na makada wengine akiwamo Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema, Jaffar Michael, zilisambaa kwa kasi katika mitandao ya kijamii jana na kuibua mijadala.

Baadhi ya waliochangia mijadala hiyo walidokeza kuwa huenda Ndesamburo anayeheshimika ndani ya chama hicho alikwenda kujaribu kusawazisha hali ya mambo.

Mkuu wa Idara ya Habari wa Chadema, Tumaini Makene alikiri kuwa picha hizo ni halisi, baadhi zilipigwa juzi na nyingine jana mchana, lakini hakutaka kuingia undani wa mkutano wa wanasiasa hao.

Ndesamburo alithibitisha kukutana na Dk Slaa: “Ni kweli tulikwenda, kwani kuna tatizo gani? Si mzee mwenzangu? Halafu bado ni mwanachama wetu, hajatoka Chadema, hivyo tuna kila haki ya kwenda kumsalimia.”

Alipoulizwa kama alikwenda kumsihi Dk Slaa arejee kuendesha mapambano ya kuing’oa CCM, Ndesamburo alisisitiza kuwa walikwenda kumsalimia.

Michael alipoulizwa nia ya safari hiyo alijibu kwa kuuliza; “Dk Slaa ni katibu mkuu wetu kwani tunazuiwa kwenda kumsalimia?”

Dk Slaa aligombea urais mwaka 2010 na kushika nafasi ya pili baada ya Rais Jakaya Kikwete na ndiye aliyekuwa akitajwa kuwania tena nafasi hiyo kupitia Chadema na Ukawa kabla ya “kubadili gia angani” na kumteua Lowassa.

Creepy! – These Kenyan Ladies Followed Diamond to His Hotel Room – VIDEO - See

$
0
0

On Saturday night, a group of Kenyan ladies who could not stomach the absence of Diamond Platnumz  after the MAMA’s After Party performances, decided to pursue him inside the hotel room where he was sleeping all in the name of taking selfies with the high flying Bongo sensation.

Raining knocks on his door, Diamond had to oblige and come out to meet, greet and take pictures with his diehard Kenyan female fans. His stripping incidence while on stage must have rippled the ladies’ interest to see him in person.

Well, below are video clips of the chics having their time with the nana hit-maker.

Welcome Inside Diamond Platnumz’s Daughter’s Room – VIDEO

$
0
0
Being born into a rich family is one of the best privileges any child can get in this life, and such is the case of Diamond and Zari’s unborn child whom they have been busy preparing to welcome into the world.

Apart from shopping for her from the best baby shops in the world, the East African power couple has now designed and decorated a room in one of their mega mansion to be hers. From their social media, below  is a short video clip of the princess about to be born to Platnumz’s family.


Zari Ateseka saa 48, Siku Zimeshafika na Kupitiliza...

$
0
0
Zari
HALI ni tete! Nyota wa Muziki wa Kizazi Kipya wa Uganda, Zarina Hassan ‘Zari’ (pichani) ambaye ni mpenzi wa Mbongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’ anasemekana kuteseka kwa saa arobaini na nane (siku mbili) akisubiri kujifungua kutoka katika ujauzito wake, Amani lina mchapo wote.
zariKwa mujibu wa chanzo cha ndani kutoka katika familia ya Diamond, Jumatatu na Jumanne zilikuwa siku mbaya kwa Zari baada ya hali yake kuwa tete kwa maumivu makali hali iliyoashiria kwamba, sekunde za kupata uchungu wa kuzaa zilishafika.

SIKU ZA MATARAJIO
Taarifa za awali zilidai kuwa, Jumamosi ya Agosti Mosi, mwaka huu ndiyo ilikuwa siku ya makadirio ya Zari kujifungua lakini siku hiyo jua likachomoza mpaka likazama, kukakucha. Siku ya pili ikaingia, Jumapili, ikafika Jumatatu, Zari akiwa bado hajajaliwa kupata mtoto ndipo hali ilipobadilika.

DIAMOND AMKIMBIZA HOSPITALI
“Hali ilikuwa mbaya sana. Ikabidi Diamond amkimbize kliniki anayotumia Zari iliyopo Masaki (Amani linaijua ni Hospitali ya Ami, Masaki, Dar),” kilisema chanzo hicho huku kikiomba hifadhi ya jina lake.

DAKTARI ATIA NENO
Habari zaidi zinadai kuwa, daktari wa Zari alimwambia Diamond kuwa, itabidi mjamzito huyo akomalie mazoezi, hasa yale ya kujaza pumzi kifuani ili aweze kujifungua kirahisi na ndivyo alivyofanya Zari.

HALI YAKE
“Ilibidi Zari arudishwe nyumbani lakini hali yake kiafya ikiwa ya kusuasua kwani hayuko kawaida. Si unajua wajawazito. Wakianza maumivu ya tumbo (uchungu) wanakuwa kwenye mateso makubwa. Hali yake ni ya kumtazamia sana.” Chanzo.

MAMA WA ZARI ATUA DAR
Habari zilizolifikia gazeti hili Jumanne iliyopita zilisema kuwa, mama wa Zari, Halima Hassan tayari yupo Dar nyumbani kwa Diamond baada ya hali ya Zari kuwa tete.
“Mama Zari ametua Dar tayari kwa dharura. Kaja tayari kwa kumsaidia mama Diamond (Sanura Kasim) katika harakati za kuhakikisha mzazi huyo (Zari) anahudumiwa sawasawa,” kiliongeza chanzo.

HOFU YA KUFICHA HABARI
Wakati hayo yakiendelea, tayari kuna hofu kwamba, habari za Zari kujifungua zinadaiwa haziwezi kuwafikia mashabiki moja kwa moja ili kumuepusha mtoto na watu wabaya.

DIAMOND AZUNGUMZA
Amani lilipata nafasi ya kuzungumza na Diamond juzi ambapo aliulizwa kuhusu Zari kujifungua.
“Teh! Teh! Nyie watu kwa kutafuta habari bwana…Teh! Teh!”

KUHUSU USIRI
Diamond alisema hakuna usiri wowote wa Zari kujifungua kwani ni jambo la heri kabisa.
“Usiri wa nini sasa? Kwani kujifungua ni jambo baya? Mbona ni tukio jema tu. Hakuna usiri wowote ule,” alisema Diamond.

Breaking News:Profesa Lipumba Kashindwa Kuvumilia, Haya Ndio Maamuzi yake Magumu

$
0
0
Kumekuwa na stori nyingi ambazo zimeandikwa sana Magazetini kuhusu Umoja wa Vyama vya UKAWA, baada ya Mbunge wa Monduli kukaribishwa CHADEMA na UKAWA stori nyingine zikaanza kuchukua headlines kuhusu baadhi ya Viongozi waliopo Vyama vya UKAWA.

August 06 2015 nimeipata taarifa rasmi kutoka kwenye Kikao ambacho Prof. Lipumba amekifanya Dar, ametangaza rasmi kujiuzulu nafasi yake ya Uenyekiti wa Chama hicho.

Kunani?

Hatimaye Diamond Na Mpenzi Wake Zari Wapata Mtoto Wa Kike.

$
0
0
Staa wa Bongo Fleva ambaye jina lake limebeba uzito mkubwa Afrika, Diamond Platnumz amepata  mtoto  wa  kike  toka  kwa  mpenzi  wake  Zari  Hassani.

Mtoto huyo ameingia duniani saa 10 na dakika 40 Alfajir, Alhamis hii.

Haijaweza kufahamika kwa mara moja ni hospitali gani mtoto huyo amezaliwa kwa kile meneja alichosema ‘usalama wa mama na mtoto’ kwakuwa bado wapo hospitali.

Sura ya mama yangu inatosha kueleza ni kiasi gani najiskia ndani ya Moyo wangu, karibu kwenye ulimwengu @princess_tiffah,” ameandika Diamond kwenye picha hiyo juu aliyoiweka Instagram.

Awali Diamond alisema kuwa Zari angejifungulia Tanzania.

Wema Sepetu Amtangazia Kiama Tundu Lissu......Asema Siku Zake za Ubunge Zinahesabika

$
0
0
MSANII maarufu wa filamu nchini,Wema  Sepetu, amemtangazia kiama mbunge wa jimbo la Singida mashariki Tundu Lissu wa CHADEMA,kwamba siku zake za ubunge zinahesabika.

Wema miss Tanzania 2006, aliyasema hayo wakati akizungumza na waandishi wa habari juu ya safari yake ya kisiasa ambayo ameianzisha baada ya kushindwa kwenye uchaguzi ubunge viti maalum (CCM) mkoa wa Singida uliofanyika hivi karibuni.

Alisema matunda ya safari yake ya kisiasa yataanza kuonekana kuanzi oktoba mwaka huu baada ya kumalizika kwa uchaguzi mkuu, kwani jimbo la Singida mashariki,litakuwa mikononi mwa CCM  chama tawala.

“Mimi nimerudi Singida kwa kazi maalum, nimekuja kushiriki upigaji kura za maoni CCM.Tumemchagua mgombea wetu Jonathan Njau…..tutahakikisha Njau anamgaragara Tundu Lissu”,alisema Wema kwa kujiamini.

Akifafanua,alisema hivi sasa maandalizi ya kuing’oa CHADEMA jimbo la Singida mashariki,yameanza na yanaendelea vizuri.

Wema alisema kazi ya kuing’oa CHADEMA mwaka huu, itafanywa kwa ushirikiano wa karibu na wana CCM wote na kuungwa mkono na kundi la wasanii maarufu kutoka jijini Dar-es-salaam.

Kwa upande wake katibu wa CCM wilaya ya Ikungi, Aluu Segamba,amesema Wema ameonyesha amekomaa kisiasa kwa kitendo chake cha kurudi Singida mapema,licha ya kuangushwa kwenye uchaguzi wa ubunge viti maalum CCM hivi karibuni.

“Tunaendeleaa kushuhudia wana CCM wengi wanaoangushwa kwenye chaguzi mbalimbali,huwa na chuki na chama na wangine wamefikia uamuzi wa kukihama chama. Lakini Wema ndio kwanza mapenzi yake kwa chama yameimarika na sasa anaelekeza nguvu zake kulikomboa jimbo la Singida mashariki kutoka CHADEMA na kulirudisha CCM”, alisema Segamba.

Jacqueline Wolper ana mimba ya miezi mitatu? ‘Mine is on the way 5 months to go’

$
0
0
Jacqueline Wolper ni mama kijacho – at least kwa maneno yake mwenyewe aliyoandika Instagram wakati akiwapongeza Diamond na Zari kwa kupata mtoto wao wa kwanza, Latiffah.

Congratulations dad and mom MTV, God is always great, Congrats Wasafi President for the little princes. Mine is on the way 5 months to go!!,” ameandika Wolper.

“Sema mtoto wa kwanza bwana unaweza kujikuta unataka kum’beba wewe tuu na kazini usiendee, utunyime mashabk haki yetu ukaacha kututungia viburudisho ukawa unalea. Hongera mtani wangu one love @diamondplatnumz,” ameongeza.

Tusubiri kama taarifa yake ina ukweli!

Mtoto wa Diamond Latiffah Naseeb Abdul Aanza Maisha ya Ustaa Akiwa Hajamaliza Hata Siku Tangu Azaliwe

$
0
0
Latiffah aka Tiffah hajamaliza hata siku moja lakini tayari ni staa si tu kwenye mitandao ya kijamii na vyombo vya habari bali hata kwenye midomo ya watu wanaofuatilia burudani barani Afrika.

Wazazi wake mwenyewe wanamuita ‘The Next Most Famous Daughter in Africa.’ Kwa ukubwa wa Diamond Platnumz na mama yake Zari Ttale, hakuna ubishi kuwa Tiffah ana kila sifa ya kuja kuwa ‘binti maarufu zaidi barani Afrika.

Ikiwa ni saa chache tu tangu kuzaliwa kwake, akaunti yake ya Instagram iliyofunguliwa imefikisha followers zaidi ya 16,000.

Picha yake ya kwanza kuwekwa kwenye akaunti hiyo ina zaidi ya comments 860.

“Welcome to the next most famous daughter in Africa… my dad and mom decided to call me Latiffah but I wanna be called Latty or Tiffah #princesstiffa #lattyplatnumz,” yanasomeka maelezo kwenye picha hiyo.

Makadirio ni kuwa akaunti hiyo inaweza kuvuka followers laki moja ndani ya siku mbili au zaidi ya followers 200k hadi wiki inaisha. Hiyo ni speed kubwa sana kwa akaunti ya Instagram kupata followers kiasi hicho.

Mashabiki wa Diamond na Zari na wana shauku kubwa ya kuiona sura ya malaika huyo. Hakuna uwezekano wa wawili hao kuiweka sura yake mapema. Hamu ya watu kutaka kumuona mtoto huyo inaweza kutumiwa kama fursa ya kibiashara na wazazi wake.

Na pengine Diamond na Zari wanaweza kuwa miongoni mwa mastaa wachache wa Afrika (kama wapo) waliowahi kuingiza fedha kupitia picha za mtoto wao. Kipaji cha Diamond na Zari cha kutengeneza fursa za kibiashara kinaweza kuwasaidia kumfanya mtoto wao kuanza kutengeneza fedha akiwa na umri mdogo.

Kufunguliwa akaunti ya Instagram ni hatua ya kwanza katika kumbrand mtoto huyo na kwakuwa mtandao huo umekuwa ukitumika kuwaingiza fedha wasanii duniani, usishangae siku za usoni, makampuni makubwa hasa yanayojihusisha na bidhaa za watoto, yakaichukua akaunti hiyo (retain) ili waitumie kwenye promotion za bidhaa zao. Na isitoshe deals zimeshaanza kuingia.


Umaarufu wa mtoto wa kwanza wa Diamond si kitu ambacho hakikutarajiwa. Habari kuhusu wapenzi hao kumkaribisha duniani mtoto wao kwa siku kadhaa itatengenezwa vichwa vya habari katika bara zima la Afrika.

Kwenye mitandao ya kijamii hasa Instagram kwa siku mbili hizi Tiffah atakuwa haepukiki.

Nuh Mziwanda: Wengi Walimshauri Shilole Aniache

$
0
0
Msanii wa Bongofleva ambaye kwa sasa anafanya vizuri na wimbo wake wa 'Ganda la Ndizi' Nuh Mziwanda akiwa na mchumba wake Shilole amefunguka na kusema watu wengi walimshauri mpenzi wake huyo amuache.

Nuh amesema watu walimpatia ushauri huo Shilole, baada ya hivi karibuni kusambazwa sauti yake katika mitandao ya jamii akisikika kumtaka kimapenzi msanii wa Bongo Movie Wema Sepetu, mazungumzo yao yalikuwa yamerekodiwa kwa njia ya simu na kusambazwa na mtu asiyejulikana.

Nuh Mziwanda amesema baada ya sauti hiyo kusambazwa watu wengi walikuwa wakimpigia simu Shilole na kumshauri aachane naye lakini anamshukuru Mungu, Shilole hajaweza kuwasikiliza na wanaendelea poa na maisha yao kama wapenzi na kudai Mungu ana kusudio lake kufanya waendelee kuwa pamoja.

"Wengi mlishauri aachane na mimi, ila Mungu ana kusudio lake kufanya tuendelee kuwa pamoja na nampenda sana Shishi wangu na sifikirii kumuacha," alisema Nuh Mziwanda.

Baada ya kauli hiyo ya Nuh Mziwanda mashabiki wake katika mitandao ya jamii walimbadilikia na kusema kuwa anapenda sana mteremko na kutafutiwa ndiyo maana anahangaika na watu ambao wamemzidi umri, huku wengine wakionyesha kutopenda mambo yake ya ndani anavyoanika katika mitandao ya kijamii hususani kuhusu mapenzi yake na mchumba wake.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya August 7

$
0
0



















Habari  Zilizopo  Katika  Magazeti  ya  Leo  Ijumaa  ya  August 7

Audio: Chadema yatoa kauli juu ya kuondoka Prof. Ibrahim Lipumba kwenye uwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF)

$
0
0
Hapo  chini  kuna  sauti  ya  Tundu  Lissu  akizungumzia  sakata  la  Lipumba  kujiuzulu  uenyekiti  CUF

CUF Wamjibu Lipumba.....Wasema Chama Chao Kiko Imara Na Kamwe Hakiwezi Kuyumba, Pia Wameapa Kuilinda UKAWA Kwa Nguvu Zote

$
0
0
TAARIFA KWA WAANDISHI WA HABARI

Leo tarehe 6 Agosti, 2015 Profesa Ibrahim Lipumba aliitisha mkutano na waandishi wa habari katika Hoteli ya Peacock, mjini Dar es Salaam na kutangaza kwamba amejizulu nafasi yake kama Mwenyekiti wa Taifa wa Chama Cha Wananchi (CUF).

Sisi kama Chama tumezipokea taarifa hizo na tunayaheshimu maamuzi yake. Ni haki yake ya kikatiba na haki ya kidemokrasia kufanya maamuzi anayoyaona yana maslahi kwake.

Bila shaka, Profesa Ibrahim Lipumba amekifanyia kazi kubwa Chama chetu katika miaka 16 ambayo alikuwa Mwenyekiti wetu, nafasi iliyomfanya awe kiongozi wetu mkuu. Kwa nafasi yake hiyo, pia ametoa mchango mkubwa katika ujenzi wa demokrasia katika nchi yetu. Tunaithamini kazi hiyo na tutaendelea kumheshimu kwa utumishi wake mkubwa kwa Chama chetu na nchi yetu. Tunamtakia kila la kheri katika mipango yake ya baadaye.

Chama Cha Wananchi (CUF) ni taasisi na kinaendeshwa kitaasisi. Ndiyo maana maamuzi yake yote yamekuwa yakifanywa kitaasisi kwa mujibu wa Katiba na Kanuni za Chama. Kwa msingi huo, pamoja na ukweli kwamba kuondoka kwa Profesa Lipumba katika safu ya uongozi kutaacha pengo hasa katika kipindi hichi ambacho tunaelekea kwenye Uchaguzi Mkuu, tunawahakikishia wanachama na wapenzi wa CUF na wananchi wa Tanzania kwa ujumla kwamba Chama hichi hakitayumba.

Katika historia yake, CUF imepita katika dhoruba na misukosuko mingi lakini mara zote kimeonesha uwezo mkubwa wa kuhimili dhoruba na misukosuko hiyo na kukabiliana na athari zake. Hatuna chembe ya wasiwasi kwamba hata mtihani huu tutauvuka na tunaamini tutaibuka tukiwa Chama imara zaidi.

Katibu Mkuu ameagiza kuitishwa kwa vikao vya dharura vya Kamati ya Utendaji ya Taifa na Baraza Kuu la Uongozi la Taifa siku ya Jumapili, tarehe 9 Agosti, 2015 ili kujadili hatua hiyo na kufanya maamuzi juu ya hatua muafaka zinazopaswa kuchukuliwa katika kipindi hiki hadi hapo Chama kitakapomchagua mwanachama mwengine kujaza nafasi hiyo ya Mwenyekiti.

Katika kipindi hiki, Chama kinawataka wanachama na wapenzi wake wote kuwa watulivu na wavumilivu na kusubiri maelekezo ya vikao vya juu vya kitaifa vya Chama.

Mwisho kabisa, tunawahakikishia wanachama wetu na Watanzania wote kwa ujumla kwamba CUF itaendelea na shughuli zake kama Chama na pia kama mshirika katika UKAWA ambayo CUF ilikuwa ni katika waasisi wake. 
  
Tunawahakikishia wanachama wetu na Watanzania wote kwa ujumla kwamba CUF itatumia nguvu, uwezo, juhudi na maarifa yake yote kuhakikisha kwamba inaulinda UKAWA ambao unaonekana kuwa mwiba kwa CCM.
  
Tunatambua kwamba kuna njama na mbinu kubwa na nyingi zinazofanywa na watawala kutaka kuuvuruga na kuuhujumu UKAWA wakidhani kwamba watapata manusura.
  
Tumesema na tunaendelea kusema CCM mwaka huu hawana manusura. 
  
Watanzania wameamua kuwan’goa, na watan’goka Tanzania Bara na Zanzibar kupitia sanduku la kura tarehe 25 Oktoba, 2015. Wimbi hili kubwa la mabadiliko halizuiliki tena.

HAKI SAWA KWA WOTE

ISMAIL JUSSA
KAIMU MKURUGENZI WA HABARI, UENEZI NA MAWASILIANO NA UMMA
06 AGOSTI, 2015

Madiwani 18 wa CCM Wahamia CHADEMA

$
0
0
Madiwani 18 wa Halmashauri ya Wilaya ya Ngorongoro kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) wametangaza kuhama chama hicho jana jijini Arusha.

Madiwani hao waliotangaza kuihama CCM walikuwa katika ofisi za Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) wilayani Arumeru.

Huku aliyekuwa Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo, Elias Ngorisa aliyefuatana na Diwani wa Kata ya Engusero Sambu, Kagil Mashati Ngukwo, ambaye pia alikuwa Katibu wa Fedha na Uchumi wa CCM Wilaya ya Ngorongoro naye pia amejiunga na Chadema.

Walikuwepo wazee wa mila wa Kabila la Wamasai (malaigwanani) Laurence Ngorisa na Lekakui Oleiti, wote kutoka Engusero Sambu. Mbunge wa Arumeru Mashariki, Joshua Nassari, ndiye aliyewapokea makada hao na kuwapatia kadi za Chadema.

Akizungumza baada ya kupokea kadi, Elias Ngorisa, alisema wapo madiwani 18 kati ya 28 ambao tayari wamechukua kadi za Chadema na kuondoka CCM na watatetea nafasi zao kupitia Chadema katika uchaguzi wa Oktoba mwaka huu.

Alisema yapo mabadiliko makubwa na Watanzania hawana budi kuyakubali na ameshawishika kubadilisha mwelekeo toka CCM kwenda Chadema.

Kwa upande wake, Diwani Ngukwo, alisema, amekihama chama hicho kwa sababu anahitaji mabadiliko na anaamini wengi watawafuata ili waweze kuondokana na manyanyaso mengi ya Loliondo wanayopata.

Rais JAKAYA KIKWETE, Ametangazwa Kuwa SHUJAA na Umoja wa Wasanii Nchini

$
0
0
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Dkt Jakaya Kikwete akizungumza mbele ya wageni waalikwa mbalimbali (hawapo pichani),waliofika ndani ya ukumbi wa Mlimani City  katika hafla ya kuagwa kwake ilioandaliwa na Muungano wa Wasanii kwa ajili ya kumshukuru kwa namna alivyowasaidia tangu alivyoingia madarakani kwa miaka 10 na pia kumtambulisha Mgombea wa Urais wa chama cha CCM Dkt John Pombe Magufuli,Dkt Jakaya Kikwete alizungumza mambo mbalimbali zikiwemo haki na hatimiliki za wasanii wa muziki pamoja na Bongomovie na pia alikubali kuwa mlezi wa tasnia hizo na kuhakikisha mambo yanakwenda sawa ndani ya tasnia hizo mbili adhimu kwa sasa hapa nchini.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Dkt Jakaya Kikwete katikati pichani akiserebuka na wadau wa muziki na huku akipiga nao picha,ndani ya ukumbi wa Mlimani City  katika hafla ya kuagwa kwake ilioandaliwa na Muungano wa Wasanii kwa ajili ya kumshukuru kwa namna alivyowasaidia tangu alivyoingia madarakani kwa miaka 10 na pia kumtambulisha Mgombea wa Urais wa chama cha CCM Dkt John Pombe Magufuli.

 Mgombea Urais wa CCM Dkt John Pombe Magufuli akipiga ngoma huku akishirikiana na Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akipiga gitaa ndani ya ukumbi wa mlimani City jijini Dar.
Mwanadada Wema Sepetu akimtunza midola Dkt John Magufuli alipokuwa akipiga ngoma jukwaani kwa ustadi mkubwa.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Dkt Jakaya Kikwete akiwa ameambatana na Mgombea Urais wa chama cha CCM Dkt John Pombe Magufuli pamoja na Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana,Katibu wa NEC Itikadi na Uuenezi Nape Nnauye na pamoja na Januari Makamba wakifurahia jambo kwa pamoja na wageni waalikwa mbalimbali waliofika ndani ya ukumbi wa Mlimani City kushiriki hafla ya kuagwa kwake ilioandaliwa na Muungano wa Wasanii kwa ajili ya kumshukuru kwa namna alivyowasaidia tangu alivyoingia madarakani kwa miaka 10.

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Dkt Jakaya Kikwete akiwa ameambatana na Mgombea Urais wa chama cha CCM Dkt John Pombe Magufuli pamojoa na Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana  (mwisho kushoto) na Mkuu wa Wilaya ya Ilala Mh.Paul Makonda wakiwasili ndani ya ukumbi wa Mlimani City kushiriki hafla ya kuagwa kwake ilioandaliwa na Muungano wa Wasanii kwa ajili ya kumshukuru kwa namna alivyowasaidia tangu alivyoingia madarakani kwa miaka 10.
Rais Dr. Jakaya Kikwete akifurahia jambo  na Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr John Pombe Magufuli kupitia CCM wakati alipowasili Mlimani City jijini Dar es salaam kwa ajili ya kushiriki hafla ya chakula cha jioni kilichondaliwa na Muungano wa wasanii Kumshukuru Mh. Dr. Jakaya Kikwete kwa jinsi alivyowasaidia katika uongozi wake wa miaka 10 kama Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Kumkaribisha Mgombea wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia CCM Dr. John Pombe Magufuli, Kushoto ni Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Kinana pia akishiriki tukio hilo.Hafla hiyo imehudhuriwa na wasanii mbalimbali  wakiwemo waigizaji wa filamu, wachezaji na wanamuziki wakishiriki kwa pamoja kumshukuru Dk.Jakaya Kikwete.
 Baadhi ya Wadau wa muziki wakifurahia jambo wakati Rais Dkt Jakaya Kikwete alipokuwa akiwasili ndani ya ukumbi wa Mlimani City.
 Rais Jakaya Kikwete akisalimiana na baadhi ya wadau wa muziki nchini ndani ya ukumbi wa mlimani City usiku huu.
 Dkt Jakaya Kikwete akisalimiana na Mkurugenzi wa Mawasiliano wa kampuni ya Vodacom,Kelvin Twisa.
 Dkt Kikwete akisalimiana na baadhi ya Wasanii wa muziki wa bongofleva.
 Rais Jakaya Kikwete akisalimiana na Mkuu wa Mkoa wa Dar Es Salaam,Mh Said Meck Sadick ndani ya ukumbi wa mlimani city usiku huu.
Wanauziki wakongwe pia walikuwepo kumshukuru Rais Kikwete kwa mambo mengi aliyoyafanya katika uongozi wake wa miaka kumi ndani ya tasnia ya muziki. 

Mtoto wa Diamond Platnumz Amburuza Mtoto wa Ali kiba Ndani ya Siku Moja Mtandaoni

$
0
0
Mtoto wa Diamond Priness Tiffah amabaye Ana siku moja toka aje duniani ame mburuza na kumgaragaza mtoto wa pili wa Kiba, Kiba Jr kwa idadi ya followers Instagram ikumbukwe Princess Tiffah account yake ya Insta gram siku moja wakati ya kiba Jr ina 76 weeks.

Angalia Hapa Chini:


Dr Kessy Anakuletea Dawa za Kutengeneza Hips, Makalio, Nywele na Nguvu za Kiume Kwa Kutumia Dawa za Asili zisizo na Kemikali

$
0
0


Kifaa cha Kurefusha uume Kinachouzwa 160,000
Pendeza na Dr Kessy Products 
Ni dawa za Asili zisizo na Kemikali wala madhara yoyote kwa Binadamu, zimetengenezwa kwa kutumia mimea na matunda mbali mbali kukupa matokeo ya Haraka

1.Refusha Nywele na zisikatike  45,000/
2.Ondoa Mvi Sugu kichwani  45,000/
3.Toa Michirizi Mapajani, Chunusi na Madoa mwilini 40,000/
4.Punguza tumbo na Manyama uzembe 45,000/
5.Mkanda wa Kufunga Kupunguza tumbo 70,000/
6.Tengeneza Shepu Hips na Makalio  45,000/ ,Vidonge 80,000/
7.Ongeza Nguvu za Kiume  Jelly 45,000/ , Vidonge 60,000/
8.Ongeza Ukubwa wa Maumbile ya kiume Jelly 80,000/ , Mashine 160,000/
9.Kuongeza Mwili Mzima 40,000/
10.Kupunguza Mwili 45,000/
11.Kupunguza Maziwa na Kuyasimamisha 40,000/
12.Ongeza Mguu uwe wa Kupendeza 45,000/
13.Rudisha usichana ama Bikira 55,000/
14.Ongeza Hamu ya Kula 40,000/
15.Ongeza Hamu ya Kufanya Mapenzi 55,000/
16. Fanya mwili Kuwa Soft 60,000/
17. Dawa ya kutoa Michububuko kwenye mapaja 45,000/
18. Dawa ya kutoa maji maji sehemu ya siri na kukuacha mkavu 55,000/

TUNAPATIKANA DAR NA MIKOA YOTE, HUDUMA ZINAFIKA POPOTE ULIPO , 
DAR TUPO KARIAKOO MSIMBAZI NA POSTA  MPYA

PIGA SIMU: 0719955528, 0756259180 au 0785371237

Diamond Ajivunia Deal la Milioni 50 Alilopewa Bintiye Tiffah, ni Pamoja na Kuvalishwa Bure na Duka Kubwa la Nguo za Watoto

$
0
0
Mtoto wa Diamond Platnumz, Latiffah amepewa endorsement ya shilingi milioni 50 na duka la nguo za watoto ambalo kumvalisha nguo bure ni sehemu ya mkataba huo.


Akiongea jana kwenye hafla iliyoandaliwa na wasanii kumuaga Rais Jakaya Kikwete, Diamond alidai kuwa hayo ni sehemu ya maendeleo kwenye muziki yaliyotokea katika mihula miwili ya uongozi wake.

“Katika miaka hii 10 na mtoto nimepata. Mheshimiwa mtoto amezaliwa leo (jana) lakini amepata endorsement leo leo karibuni milioni 50 katika duka tu la kuwa anadhaminiwa kama mtoto anavalishwa na hilo duka, sio maendeleo hayo jamani,?” alihoji Platnumz.

Diamond hakusita pia kuzungumzia rekodi ilivyovunjwa na akaunti ya Instagram ya mwanae, ambayo hadi sasa ina followers zaidi ya elfu 45 siku moja tu baada ya kuzaliwa.

“Katika Afrika ndio mtoto wa kwanza huyo aliyepata followers wengi Afrika nzima, anatokea Tanzania sio maendeleo hayo?

Hii Ndio Picha ya Kwanza ya Diamond Akiwa na Mtoto wake Latiffah

$
0
0
Latiffah Naseeb Abdul a.k.a Tiffah Dangote au kama wazazi wake Diamond na Zari wanavyomuita ‘The African Royal Princess’, anaendelea kupata umaarufu kwenye mitandao ya kijamii akiwa na umri wa siku moja tu.

Kupitia akaunti yake ya Instagram @princess_tiffah iliyofunguliwa jana baada ya kuzaliwa, imepostiwa picha ya kwanza ya baba na mwana, Diamond akiwa na mtoto wake kitandani. Hata hivyo mtoto anaonekana mkono tu.

Hii ndio caption iliyoandikwa katika post hiyo:

My Dad Couldn’t seep last night, he was staring at me the whole night #MyFirstDayInTheStateHouse”.

Mpaka sasa akaunti ya @princess_tiffah imefikisha followers 44,357 ikiwa ni siku moja toka ifunguliwe.

Sijifananishi na Drake, nina muonekano mzuri kuliko yeye – Hemedy PHD

$
0
0
Kama unamfollow msanii wa filamu na muziki Tanzania, Hemedy PHD katika akaunti yake ya Instagram, utakuwa umekutana na post zake nyingi kuhusu rapper/muimbaji wa Canada, Drake.

Hemedy amesema kuwa yeye ni shabiki mkubwa sana wa Drake, na ndiye msanii wa nje anayemu-inspire kwa kiasi kikubwa ndio sababu huwa anampost sana kwenye akaunti zake lakini sio kwasababu anajifananisha naye.

Ninamkubali sana drake lakini sijifananishi na Drake” alisema Hemedy kupitia Clouds’E’ ya Clouds TV.

Lakini kama kawaida yake hakuacha kujifagilia kidogo, kwa kusema kuwa licha ya kumpenda Drake lakini bado yeye (Hemedy) anamzidi Drake mambo mengi ikiwemo muonekano wake na kuvaa.

Nina muonekano mzuri kuliko Drake, navaa vizuri kuliko drake” – Hemedy PHD

Hemedy ambaye hivi karibuni ameachia video mpya ‘Imebaki Story’, pia amezungumzia maana ya ‘Papi Nation’ kuwa ni jina la kampuni yake anayotarajia kuisajili hivi karibuni.

BONGO 5
Viewing all 104712 articles
Browse latest View live




Latest Images