Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104768 articles
Browse latest View live

Baada ya Clouds FM Kumzengua Mtangazaji Maarufu Dina Marios, Sasa Ajiunga na Redio Pinzani EFM...

$
0
0
Dina Marios Aliyekiwa Mtangazaji wa Kipindi cha Leo Tena Clouds FM Amepost Picha Akiwa Redio za EFM ikiwa na Maana tayari Ameshahama Redio Clouds Ambayo kwa sababu wanazozijua wao walimweka Bench kwa Muda Mrefu Kiasi cha Mwenyewe Kulalamika Kitendo hicho...

Dina Marios Ameandika Haya Katika Ukurasa wake wa Facebook na Kuambatanisha na Hiyo Picha Hapo Juu:

"I believe if you keep your faith, you keep your trust, you keep the right attitude, if you’re grateful, you’ll see God open up new doors.”
– Joel Osteen

Tetesi za Wakongwe wa CCM Kuhama Chama na Kujiunga na UPINZANI Zaanza Kunukia..Hali ni Tete CCM

$
0
0
Hali ni "TETE" CCM !
Tetesi za wakongwe wa CCM kuhama chama na kujiunga na UPINZANI zaanza kunukia!
Mafuriko ya Lowassa hayazuiliki.
Sumaye na Bilali wanategemewa kufanya maamuzi magumu wakati ukifika.
Tusubiri tuone!

Jiji la Dar Lasimama: Hapa Kuna Picha 5 za LOWASSA Akisindikizwa Ofisi za NEC na Maelfu ya Wananchi Kuchukua Fomu ya Urais

$
0
0
Picha  5  za  LOWASSA  Akisindikizwa  Ofisi  za  NEC  na  Maelfu  ya  Wananchi  Kuchukua  Fomu  ya  Urais




Selfie imefanya Wanaume Tushindwe Kuona Makalio ya Wanawake Kama Zamani

$
0
0

Mtakumbuka kipindi cha hapo nyuma kidogo ilikuwa kila mwanamke anayepiga picha basi lazima ajibinue nyuma atuonyeshe alilozawadiwa na Mungu.

Lakini hivi sasa habari ya mjini ni selfie tu, yaani wakipiga picha tunaishia kuona tu sura lakini nyuma hatukuoni.

Kusema ukweli, tangu selfie iwe habari ya mjini sisi wanaume tunaopenda makalio tumekuwa tukinyanyasika sana. Yaani ukiingia Instagram tunaishia kuona style za nywele na lips tu.

Tafadhali kina dada acheni selfie, rudini enzi zenu za kutuonyesha makalio ili nasisi wapenda makalio nafsi zetu zisuuzike.

Posted by: MCHUNGUZI HURU (Associate Professor)

CCM Tutulize Vichwa, Lowassa ni Tatizo Tulilojitengenezea Wenyewe, Hakujitengeneza-LEMUTUZ

$
0
0
Wamarekani wana Kanuni moja muhimu sana kwenye Rehab zao za kusaidia Wanaotumia Madawa ya Kulevya kwamba kabla ya kuwachukua kwenye Makazi yao ya msaada ni lazima waathirika wajitokeze wenyewe kwenye ofisi za hayo makazi kuomba msaada baada ya kukubali kwa maandishi chini kwamba wana MATATIZO, ndipo wanaweza kupokelewa na kupewa msaada sio vinginevyo. Now wakati umefika CCM tunatakiwa kukubali katika nafsi zetu kwanza kwamba tuna TATIZO na hili tatizo tumejitengenezea wenyewe I mean tatizo la Lowasa kugombea Urais kupitia Upinzani, kuacha mengine yote ya muhimu tuna tatizo moja kubwa sana nalo ni Wananchi wa Tanzania wamekosa kuona Upinzani wa kweli toka Mrema aliposhindwa ku-fit the hype aliyo create mwenyewe ambayo sababu yake kubwa ilikuwa hakuwa na elimu kubwa na uzoefu wa siasa kama Lowasa kwa hiyo ndio maana this time around ninasema CCM tuna TATIZO KUBWA kuliko la Mrema. MWalimu Baba wa Taifa hayupo tena kumzima Lowasa kama alivyomzima Mrema, this time tunatakiwa tuungane na kuwa kitu kimoja tupigane kushika Dola. Hapa mjini kuna bendi moja inaitwa FM Academia Wazee wa Ngwasuma ni bendi inayomilikiwa na mtu mwenye akili sana anawajua vizuri sana Wa-Congo kuwa wakipata sifa kidogo ni watu wa kuhama hama so yeye hajawaruhusu kwa Mwanamuziki mmoja kupata sifa individually bila ya bendi nzima na ameajiri wapigaji wengi sana kiasi kwamba hata mmoja asipokuwepo huwezi kujua kuwa kuna dosari ndio maana ni moja ya bendi chache sana hapa Tanzania yenye Wa-congo wengi lakini imeweza kudumu kwa muda mrefu wakiwa pamoja. CCM tulifanya kosa hili kubwa sana la kuruhusu Kiongozi mmoja wa chama chetu akawa almost bigger than chama tukashituka very late now we are about to pay the price ya makosa yetu wenyewe, ndipo ninaposema cha muhimu sio kulaumiana au kuwalaumu wanaotoka hapana ni kukubali kwanza kwamba kuna makosa tumefanya ila kwa sababu CCM ni kubwa kuliko wanaojitoa tutafute majibu mazuri na mazito yenye busara ndani yake bila ya ku panic tuweze kushika tena Dola!!

- LOWASA:-
Kuingia kwake UKAWA kunabadilisha Completely the picture ya siasa zetu kwa sababu kwenye haya maisha hakuna kitu perfect kila kitu kina mapungufu yake so are our politics na hasa our fragile Democracy now Lowasa offers a sweet package kwa wale wote walioumizwa na mapungufu ya Demokrasia yetu hasa ya ndani ya CCM. UKAWA na Lowasa wana matatizo mengi sana Politically kuelekea Avenue ya kutafuta Urais kwa sababu mpaka sasa hawajaweza kuwachukua kutoka CCM Viongozi wenye Credibility na Public, so far wamechukua Viongozi wengi waliokuwa none effective ndani ya CCM hilo ni la kushukuru sana kwa sababu so far linawasumbua sana na pia kutoka kwa Lipumba na kitendo cha Dr. Slaa kukaa pembeni na ujio wa Lowasa ni pigo kubwa sana kwa UKAWA. Lakini bado Lowasa ni a big threat kwa sababu moja ya pungufu kubwa la CCM madarakani ni Ajira kwa Vijana wengi walioko mijini, ina maana kwamba hawa Vijana wote mjini wasiokuwa na Ajira Lowasa ni jawabu lao sio kwa sababu ana ajira hapana ni kwa sababu ana present a political threat kwa establishment kwa hiyo kwa sababu Vijana hawa hawana anything to lose kwa kumfuata Lowasa aslimia kubwa kati yao watamfuata ingawa wengi wao sio wapiga kura kwa kawaida lakini kwa vile Waziri Mkuu wa zamani wa CCM atakuwa majukwaani anaishambulia CCM it offers excitement kwa Vijana wanaokaa bure bila kazi na huku wameenda Shule. Sio siri kwamba Lowasa atakusanya watu wengi sana kwenye majukwaa yake, ambao watajaa kujionea wenyewe kwa macho yao the history being unfold, pia Wastaafu wa Serikali wengi watamfuata now hawa ni hatari sana kwa sababu ni wapiga kura na wana hasira sana na Serikali ya CCM ambayo kwa mawazo yao haiwajali kwa sababu inawapa penshioni ambayo haikidhi matakwa yao ya maisha the good newz ni kwamba sio wengi isipokuwa kwa kuwa wana tabia ya kuishi sehemu moja kama Kimara sehemu kama hizo ni ngumu sana kwa CCM kukubalika. Viongozi mbali mbali watakaoumizwa kwenye process ya uchaguzi wa sasa wa Kura za maoni watamfuata 20% yao watatuumiza CCM hasa kwenye Serikali za Mitaa na Udiwani na hata kwenye Ubunge, kwenye Urais Lowasa does not present a big threat kwa sababu most of the times of this Campaign atakuwa kwenye ropes kujitetea zaidi kuliko kushambulia on that CCM tunatakiwa kumpa kamba ya kujinyongea yeye mwenyewe ingawa hili linahitaji serious brains behind it. But all and all bado Lowasa anatuletea CCM the best changamoto ever infact this is the fisrt serious challenge CCM we are going to face since our existance 1977, hatuwezi kumchukulia Lowasa kuwa ni poa hapana he is a threat lakini managerable only kama tutatuliza akili chini na kupigana back kistaarabu.

- CCM:-
Ni Chama kikubwa sana na kumekuwepo kabla hata Lowasa hajafikiria kuwa Mwanasiasa, Mwalimu the greatest Leaders ever in the history of our Nation alikuwa ni Binadam mwenye mapungufu pia kwa maoni yangu ni FACT kwamba mapungufu makubwa 2 ya Mwalimu yalikuwa ni SHERIA na UCHUMI na ni matatizo yanayotutesa sana hili Taifa mpaka leo. Mwalimu alikuwa na Tabia ya kuyepeleka mambo ya Kisheria kwenye Kamati Kuu ya CCM badala ya mahakamani, Kiongozi wa Taifa anaharibu Mwanza anahamishiwa Mtwara haya ni mapungufu yaliyoishia kumtengeneza Lowasa our CCM's problem now. Simlaumu Mwalimu kwa sababu Miaka karibu 30 toka Mwalimu apumzike Urais CCM tulikuwa na muda mwingi wa kulirekebisha hili la kulindana ndani ya CCM, lakini tukalipuuzia na kuendelea kushi nalo sasa linataka kutuumiza wenyewe. Pamoja na ukubwa wa political threat ya Lowasa bado sio kubwa sana mpaka akiweza kuwachukua some serious Leaders ndani ya CCM ambao so far ameshindwa ingawa pia kubaki kwa ndani ya CCM wale wote ambao wanajulikana ni wafuasi wake nako kunatuletea tatizo kubwa sana ndani ya CCM.

HOWEVER:- Lowasa na UKAWA, wanapigika tena bila tatizo kwenye uchaguzi only kama CCM ikituliza vichwa chini na kupigana na hili tatizo kwa kutumia akili kubwa na maarifa pamoja na busara kubwa, kwa mfano CCM ni lazima i avoid kupigazana makelele hewa na Lowasa pamoja na UKAWA we should stick to the POLITICAL FACTS. Kwa mara ya kwanza Upinzani watatumia muda mwingi kujitetea kama CCM tukiweza kutengeneza a serious Political Package ya mapungufu ya Lowasa kwa kutumia lugha yao wenyewe Wapinzani ambao wamekuwa mstari wa mbele kwa muda mrefu sana kumshambulia Lowasa akiwa ndani ya CCM. Zipo Video za Viongozi wakuu wa Chadema na UKAWA wakimshambulia Lowasa bila huruma kwamba anatakiwa kunyongwa kutokana na mapungufu yake akiwa Waziri mpaka Waziri Mkuu, now Mwananchi mwenye akili timamu akionyeshwa hizo video bila kuombwa kuangalia kwa matusi na makelele halafu akaonyeshwa tena video za sasa za Viongozi wale wale wa Upinzani wakipigana kumsafisha Lowasa ninaamini mwananchi hatakuwa na tatizo kuamua kati ya CCM na UKAWA nani ni waigizaji wa Sinema na nani ni Chama cha Siasa. CCM tutathimini seriously nani wametoka na effect yao kwenye maeneo waliyotoka na kufanyia kazi matokeo ya tathmini hizo, pia tuwa identify wale wote ambao hawajatoka lakini ni wafuasi wake Lowasa maana hawa ni hatari sana kuliko waliotoka kabisa, tujue wapo wapi, wanafanya nini na namna ya kuwathibiti bila kuanzisha misuguano ambayo ni unnessesary kisiasa. Na kubwa kuliko yote CCM tukatae kata kata kuchukuwa Hostage na hawa wanasiasa mamluki watakao tokea kutaka kujifanya kutaka kutoka ili wabembelezwe kubaki ni muhimu tukajiwekea policy mapema kwamba anayetaka kutoka aende now na hatutambembeleza mtu.

- Wamarekani walilitengeneza tatizo la Binladen alipokuwa tatizo wakaishia kulimaliza wenyewe, halafu wakatengeneza tatizo la General Abacha Nigeria na wakaishia kulimaliza wenyewe, and then wakalitengeneza tatizo la Chief Abiola na wakalimaliza wenyewe, Panama walitengeneza tatizo la Noriega and then wakaishia kulimaliza wenyewe, sisemi tutumia njia zao kumaliza tatizo la Lowasa tulilolitengeneza wenyewe CCM HAPANA, infact uwepo wa Lowasa unatusaidia sana CCM kujibu tuhuma na majungu ya muda mrefu sana kwenye our political arena kwamba kuna Viongozi wa CCM waliokufa kutokana na kutaka kwao kuingia Upinzani. Sababu kubwa ni kwamba kati yao wote hakuna aliyekuwa Mkubwa na mwenye Nguvu kama Lowasa sasa kama CCM huwa ina tabia ya kuwaondoa mbona yupo mpaka leo na anagombea urais kupitia Upinzani? CCM tutulize akili, tujiepushe kujibu jibu makelele ya Lowasa na watu wake kila wakati mengine hayahitaji kujibiwa kabisa kama vile juzi Wasanii walipomuaga Rais JK, Lowasa amepiga kelele hakuna aliyemjibu ila FACTS zilizosemwa na Wasanii wenyewe kwa kusomwa na Msanii Niki wa pili, ile risala imejibu maswali yote ya Lowasa kuhusu Hatimiliki za Wasanii yote Rais JK aliyowafanyia Wasanii toka ashike madaraka mpaka leo anajitayarisha kuyaacha.

- Pia CCM, tukumbuke kwamba kutoka kwa Lowasa na kuingia Upinzani ni good for our Nation Democracy so hata tunaposema sema tuwe tunaweka na akiba ya maneno for the interest of our Nation's Democracy, this is just a test kwa CCM je ni chama kweli cha Mapinduzi na kinachokubalika na wengi kuliko Upinzani? Majibu yake ni rahisi sana lakini only kama CCM itatuliza akili chini na infact CCM bado tunahitaji sana ku explore na kuitumia our biggest political asset yaani Wakinamama, Siasa za Chadema na Upinzani kwa ujumla kwa kawaida hapa Tanzania bado hazijawahi kuwashawishi sana kina mama ambao bado wanaiamini CCM ni wengi na ni wapiga kura. Tumewapoteza Vijana wengi sana kutokana na ukosefu wa ajira lakini the good news ni kwamba Vijana wasio na ajira kwa kwaida sio wapiga kura huwa ni wapiga kelele tu mtaani na kujaa kwenye majukwaa ya Wapinzani.

- Social Media ni muhimu sana kuna wakati Chadema walikuwa wametupiga bao kabisa kwenye hizi area, lakini not now sasa hivi CCM tunawapita kwa at least 10%, kwa sababu converting Lowasa into Chadema bado inawasambua sana operators wao wa Social Media maana it sounds very backwards kulinganisha na jinsi walivyokuwa wanamshambulia sana Lowasa now kwa mara ya kwanza wanajikuta wapo kwenye kamba I mean kwenye kumtetea Lowasa it is a shock itakayowasumbua sana kwa muda huu wa mwanzoni. Now you know kwamba kwenye siasa Kujitetea ni Dalili za kushindwa tayari so CCM tukiwashambulia hawa mapema sana na kuwaweka kwenye kamba kama ilivyo sasa, itawachukua muda sana kurudi kwenye nafasi yao ya zamani ya kushambulia tu huenda wakiamka usingizini Vita itakuwa imekwisha tayari, lakini otherwise bado na wao ni a threat kwa sababu wanasomeka sana mijini ila kama kawaida tunatakiwa kuwajibu with FACTS na safari hii tumepata a golden chance ya kuwashambulia constantly hahahahaha I love it!!

- MUHIMU KULIKO YOTE NI TATIZO LA LOWASA LINATUPA CCM NAFASI YA KUJIKUSANYA KWA PAMOJA TUKIJUA KWAMBA NI TISHIO KWENYE KUSHIKA KWETU DOLA SO NI LAZIMA TUPIGANE PAMOJA KUMSHINDA NA TUTAMSHINDA TU!!

MUNGU AIBARIKI TANZANIA

Le Mutuz Nation

Hofu ya Lowassa, CCM Wakutana Ghafla Dodoma

$
0
0
Katika kile kinachoonekana hali mbaya ndani ya Chama kuelekea Uchaguzi Mkuu hapo Oktoba, Kamati Kuu ya CCM inakutana Mjini Dodoma chini ya Uongozi wa Mwenyekiti Jakaya Kikwete.

Ripoti za ndani zinadai ajenda kuu ni Kuzuia Kasi ya Edward Lowassa ambae anaonekana kuwatesa kila uchao.

Tutaendelea kujuzana yanayojiri huko, Usicheze mbali.

Nuh Mziwanda Afunguka Makubwa Amtuhumu Idris wa Big Brother Kumsumbua Demu wake Shilole

$
0
0
Picha limeanzia kwenye post ya Instagram ya mshindi wa Big Brother Africa Hotshots, Idris Sultan ambayo aliweka picha ya girlfriend wake Samantha wa Afrika Kusini.

Miongoni mwa watu walio comment kwenye picha hiyo ni pamoja na mmiliki wa ‘moyo’ wa Shishi Baby, Nuh Mziwanda ambaye alimchimba ‘biti’ Idris, akidai kuwa amekuwa akimsumbua mpenzi wake Shilole kwa kumtumia ujumbe ambao hapendezwi nao.

“Nikianza kumsumbua demu wako, kaam unavyomsumbua wangu utafurahi, nimekuvumilia sana bro, sasa imekuwa too much, tuheshimiane @idrissultan msg zako sijazipenda.”


WEMA SEPETU Awapiga Mkwara TEAM WEMA Kuto Weka Habari yoyote ya LOWASSA kwenye page zao za Instagram...

$
0
0
Wakati wagombea mbalimbali wa vyama vya Siasa nchini Tanzania wakiwa na wafuasi wao wakiendelea kuingia kwenye headlines mbalimbali Aug 10 nakukutanisha na hii post ya Mrembo Wema Sepetu.

 Kama unamfatilia Wema Sepetu kwenye mitandao yake ya kijamii leo kupitia mtandao wa Instagram kapost picha inayomuonyesha Waziri wa ujenzi John Magufuli akisalimiana na Steve Nyerere pamoja na Rais Jakaya Kikwete.

Kwenye post yake ameipa maneno haya  “Wamoja havai Mbili…. Alafu nina msg to Team Wema … Please my darlings… kama kuna mtu anatumia account yenye jina langu naomba msimpost Lowassa tafadhal… Kama unashindwa then badili tu jina… Dont use my name kumpost Lowassa …. Jamani Iam Not Team Lowassa…. Thank u… CCM tu hapa… TeamMagufuli to death … Nilishasema mi ni CCM Damu Kabisa… Sidanganyiki…

UKAWA mtaenda msojielewa…”

Lowassa Amtuhumu Rais Jakaya Kikwete Kwa Kuuharibu Uchumi wa Tanzania...... Asema Vitu vimepandishwa na Tembo Wanauawa Hovyo

$
0
0
EDWARD Lowassa, mgombea urais wa Chadema amesema, Rais Jakaya Kikwete ameharibu uchumi wa Tanzania.

Akizungumza na wafuasi wa Chadema pia UKAWA katika ofisi za Chadema mara baada ya kuchukua fomu ya kuwania urais kupitia chama hicho jana mchana, Lowassa  alisema;

“Rafiki yangu Jakaya Kikwete ameuharibu uchumi wa nchi yetu,”

“Wakati Rais Mkapa anaondoka madarakani kilo ya sukari ilikuwa Sh. 600 leo ni Sh. 2,300. Mchele ulikuwa Sh. 550 leo ni Sh. 2,300. Sembe ilikuwa Sh. 250 leo ni Sh. 1,200.”

Aidha Lowassa alisema, katika kipindi cha utawala wa Rais Kikwete ndipo Tembo na kila aina ya wanyama wameuwawa kuliko kipindi chochote katika historia ya Tanzania.

“Katika utawala wa Rais Kikwete, Tembo wameuwawa kuliko kipindi chochote katika historia duniani kote.

“Kila aina ya mnyama ameuwawa kuliko kipindi chochote katika historia ya nchi yetu. Nitaijenga serikali yenye uchumi kwa speed (kasi), ambaye hawezi akae pembeni,” alisema Lowassa.

 Angalia video hii hapo chini  umsikie  Lowassa  akitoa  tuhuma  hizi.:-

Magufuli Aahidi Ushindi wa Tsunami CCM......Asema Wapinzani Wataishia Kupiga Kelele Tu, Mwigulu Nchemba Naye Apigilia Msumari wa 'Moto'

$
0
0
MGOMBEA urais kwa tiketi ya CCM, Dk John Magufuli, amewahakikishia wana-CCM na Watanzaia kwa ujumla kuwa mwaka huu, chama kitapata ushindi wa Tsunami na si wa kishindo wala kimbunga.

Dk Magufuli alisema hayo nje ya ofisi ya chama hicho mkoani Mtwara juzi alipokuwa akizungumza na wanachama wa chama hicho ambapo alisisitiza kuwa wapinzani watapiga kelele sana, wataongea sana lakini ushindi kwa CCM ni lazima na upo pale pale.

Alisema ushindi huo unatokana na matawi yaliyoanguka ndani ya chama na kuhama na kwamba watu hao wameiacha CCM ikiwa safi na salama zaidi.

Alisema watu hao walikuwa wakitumia fedha nyingi kurubuni watu wakati wa mchakato wa kumpata mgombea urais wa CCM ambapo chama kiliwakata na kukimbilia vyama vingine vya upinzani.

Aliwataka wana-CCM wasikatishwe tamaa na watu wa aina hiyo na badala yake washikamane, wawe kitu kimoja na kwamba mwaka huu, chama kitafanya kampeni za kisayansi.

Aidha, Mbunge wa Iramba Magharibi, Mwigulu Nchemba alisema ni kazi rahisi kumnadi Dk Magufuli kutokana na vigezo na sifa alizonazo.

Mwigulu, ambaye pia ni Naibu Waziri wa Fedha, alisema walioshindwa kwenye mchakato wa kura za maoni na kuhama ndani ya chama, hivi sasa wanahaha kutafuta urais wenyewe ambapo wanatoa mpaka hela ili kutafuta uongozi, lakini wataumbuka mapema.

Akizungumza na mamia ya wana-CCM waliojitokeza kumpokea katika hiyo ofisi ya chama ambapo alifika kwa ajili ya kuwasalimia na kuwashukuru kwa kumchagua kuwa mgombea na kumdhamini, Dk Magufuli aliwataka makada hao na Wtanzania kwa ujumla kutoyumba kwa kuwa Watanzania walio wengi bado wanakipenda Chama.

“Ushindi wa mwaka huu wala si wa kimbunga ni wa Tsunami, watapiga kelele sana, watakuja na propaganda nyingi sana, lakini ushindi wa CCM ni lazima. Ni lazima tupate ushindi wa rais, wabunge, wawakilishi na madiwani,” alisema.

Alisema walikuwa watu 42, wakati wakiomba kuteuliwa na chama hivi sasa, CCM ina kundi moja tu la ushindi.

“Hako ka tawi kamoja ndio kakameguka kwenda uko mbali, mti ambao unataka upate mbao zake nzuri matawi kudondoka chini ni vizuri ili upate mbao safi.

 “Lakini baada ya kudondoka hilo ni jambo la kawaida kwa chama kikubwa kama CCM.

"Hata ukiangalia tangu enzi za Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere wapo waliotoka wako akina Kambona walitoka na wengine walifukuzwa na wengine walijua watafukuzwa wakakimbia wenyewe kabla ya kufukuzwa kama hao,” alisema.

Alisema iwapo atachaguliwa kuongoza dola atapenda awe mtumishi wa watu, asiyekuwa na majivuno ili aweze kuwatumikia wananchi na atimize matarajio yao.

 Dk Magufuli alisema wakati wa kampeni ukifika zitafanyika za kistaarabu na kisayansi na kwamba zitakuwa za shina kwa shina, tawi kwa tawi, kata kwa kata, jimbo kwa jimbo, wilaya, mkoa na taifa.

Aliwataka wana-CCM wasimame imara kwani wananchi wengi wanakipenda Chama.

 Dk Magufuli akizungumzia uzoefu wake ndani ya CCM, alisema alikuwa mbunge katika kipindi chake cha miaka 20, ambapo vipindi viwli alipita bila kupingwa na alikuwa waziri kwa miaka 20 katika wizara mbalimbali.

Alisema anaifahamu vizuri Mtwara, Tanzania, CCM na kero za Watanzania anazifahamu vya kutosha hivyo akipewa nafasi watashudia wenyewe kasi ya utendaji kwa maendeleo ya taifa.

 “Nilichaguliwa na mkutano mkuu kutoka kila kona ya nchi kwa asilimia 87, wale walionichagua waliwakishia Watanzania wote. Niwahakikishie kuwa mwaka huu, tutashinda zaidi,” alisema.

Aliwataka wana-CCM katika umoja wao kutulia na kutoyumbishwa na maneno ya porojo kwa kuwa chama kinajiuliza kwa kile walichofanya kwa wananchi na si maneno matamu bila vitendo.

“Chama nakifahamu, shida za wana-CCM nazifahamu, matarajio yao nayafahamu, shida za wananchi nazifahamu hivyo kama nitachaguliwa nitawatumikia kwa uadilifu mkubwa ili kuwaletea maendeleo,” alisema.

Alikiba Athibitisha Ujio wa Collabo yake na Davido, Aelezea Ngoma itakuwaje

$
0
0
Habari kuhusu ujio wa collabo kati ya superstar wa Nigeria, Davido na superstar wa Tanzania Alikiba tuliisikia kutoka kwa Davido mwenyewe wakati wa tuzo za 2015 MTV MAMA zilizotolewa huko Durban, Afrika Kusini.

Hatimaye Alikiba naye amezungumzia collabo hiyo kwa mara ya kwanza, kwa kuthibitisha kuwa alichokisema Davido ni kweli hivyo watu wajiandae kupokea kazi hiyo hivi karibuni.

“Davido ameongea na Millardayo kwamba anataka kuja kufanya featuring na Alikiba, which is tayari tulikuwa tumeshaongea muda mrefu, kwahiyo watu wasubirie tu ngoma inakuja kutoka lini.” Alisema King Kiba kupitia 255 ya XXL ya Clouds Fm.

Alikiba pia ameelezea kile ambacho wanatarajia kukiimba katika wimbo huo ambao bado haujarekodiwa.

“Track iko vizuri, lakini idea bado haijakamilika, lakini kiukweli mi hua nafanya ngoma nikiwa studio, tutazungumzia kuhusu goodtime, party, mapenzi flani you know, yaani nyimbo flani ya kuhamaishisha watu katika raha.”

Rais Kikwete Atua mjini Dodoma Kuendesha Vikao vya Chama cha Mapinduzi

$
0
0
Mwenyekiti wa CCM Taifa Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Dodoma Adam Kimbisa muda mfupi baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa Dodoma ambapo ataongoza vikao vya Kamati ya Maadili na Kamati kuu ya CCM vitakavyofanyika katika ukumbi wa White House Makao Makuu Dodoma.
 
Alhaj Kimbisa amekanusha uvumi uliosambazwa katika mitandao ya kijamii kuwa ameihama CCM. Kushoto ni Katibu mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana

Mwenyekiti wa CCM Taifa Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na KAtibu Mkuu wa CCM Ndg Abdulrahmana Kinana baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa Dodoma ambapo ataongoza vikao vya Kamati ya Maadili na Kamati kuu ya CCM vitakavyofanyika katika ukumbi wa White House Makao Makuu Dodoma.

Nuhu Mziwanda Amshutuma WEMA SEPETU Kwa Kuvuruga Uhusiano Wake na Shilole Kwa Makusudi...Aandika Haya Kwa Uchungu

$
0
0
Nuhu Mziwanda Ameshindwa Kuvumilia na Kuamua kumfungukia Wema Sepetu Ambaye alihusika kusambaza Audio ambayo Nuhu Mziwanda anasikika akimtongoza Wema....

Kaandika Haya Hapa:

'Nakupa hongera kwa kufanikiwa kutoa amani katika mapenzi yangu mimi Na zuwena'maana hukua na nia njema wewe pamoja na team yako'na hata kama ingekua kweli ungemfata pembeni zuwena na kumweleza kua bwana ako anantongoza na sauti zake hizi hapa'lakini ukaona sio ishu na kuachia mitandaoni'mradi kuniaibisha mimi pamoja na na huyo unaesema unampenda sana na ni shoga yako'kingine Wema umetongozwa na wangapi hapa duniani kwann usiweke Voic note zao?yani moja kwa moja umetaka kusambalatisha mapenzi yetu na now naona mnaanza kutumana kumtongoza shishi'well madam nakupa salute zako'najua unaishi kwa amani na raha 'ila huku umekiwasha mpka mtu unakua hauna amani ya moyo na ukizingatia sijawahi hata kukaa na ww tukapga stor wala kuona undani wa mwili wangu'kipindi una kampeni uling'ang'ania sana niingie kwenye group yako ya whatsup for supporting you'kumbe unanichekea kinafiki na ulikua na mabomu yako umeyapanga kuyalipua 'sawa mama angu ila mimi nimetoa ya moyoni mwangu kwako na naamini ujumbe utakufikia mana nimeshindwa kukaa na duku duku'sisi wote binadam na hatuna garantee ya kuishi'salute kwako kwa ulichofanya' Mziwanda

WEMA SEPETU Amjibu Nuhu Mziwanda..Amtaka Ajishughulishe na Aache Umarioo

$
0
0
'Naitwa Wema Sepetu na ntabaki kuwa Wema Sepetu... Iam Number One... Sina muda wa kubishana na watoto...Nina muda wa kufanya kazi na kwa sasa jicho langu limeelekea kwa Wanyaturu wangu Singida na kwenye siasa yangu pamoja na kazi zangu za maana bila kusahau entertainment niliokuwa ninayo from 2006 ... Kumbe wakati mi nimelala nyie mnaandika Instagram... Ntapata dhambi kugombana na watoto wadogo-ambao nimewazidi sio pesa tu hadi dhambi pia nimewazidi.... Mstafute kick kupitia jina la Wema jamani... Jitume, amka, usibweteke, fanya kazi.... Umarioo mwisho Chalinze maana Dar wote tuna Hustle... Ama nene....' Wema Sepetu

Haya ndio majibu ya Petit Man kwa Soudy Brown kuhusu tetesi ndoa yake na Esma kuvunjika

$
0
0
Kwenye mtandao wa kijamii wa @Instagram kulikuwepo na uvumi kuwa ndoa ya dada wa Diamond, aitwaye Esma na Petit ipo kwenye ugomvi baina ya wawili hao.

Leo Soudy Brown kaamua kupiga Stori na Petit kutaka kujua ukweli wa taarifa hizo lakini mwenyewe hakuonesha utayari wa kuzungumzia undani wa ishu hiyo.

Ukibonyeza play hapa utamsikia Soudy na Petit Man ilivyokuwa kwenye U Heard.



BREAKING: Dr. Slaa aibuka tena kupitia Ukurasa wake wa Twitter na kusema Mambo Mazito kuhusu Lowassa

$
0
0
 BREAKING: Dr. Slaa aibuka tena kupitia Ukurasa wake wa Twitter na kusema Mambo Mazito kuhusu Lowassa...Hapa Chini unaweza Kusoma Mambo yote aliyosema kuhusu Lowassa na Chadema...





BREAKING: Dr. Slaa aibuka tena kupitia Ukurasa wake wa Twitter na kusema Mambo Mazito kuhusu Lowassa

Habari Mpya Kutoka MUHIMBILI Ambako Freeman Mbowe Amelazwa Baada ya Kuugua Ghafla

$
0
0
Hali ya mwenyekiti wa CHADEMA taifa na mbunge wa jimbo la Hai anayemaliza muda wake, mh Freeman Aikae Mbowe, imeendelea kuimarika.

Akizungumza na waandishi wa habari muda mfupi uliopita katika Hospitali ya taifa ya Muhimbili, anakopatiwa matibabu, mh Mbowe, amesema anaendelea vizuri na kwamba bado anaendelea kupumzika hospitalini hapo, kama alivyopangiwa na madaktari wanaoangalia hali yake.

''Hali yangu imeendelea kuimarika na kilichonipata jana kwa mujibu wa uchunguzi wa madaktari ni uchovu wa muda mrefu, uliobainishwa kutokana na shughuli za muda mrefu bila kupumzika katika shughuli zangu za kisiasa'' amesema Mbowe.

Mh Mbowe ameongeza kwamba, madaktari wamemtaka kuendelea kuwa chini ya uangalizi wao mpaka hapo watakapo mruhusu kuendelea na shughuli zake za kwawaida.

Mmoja kati ya madaktari wanaoangalia afya ya mh Mbowe, Dr Tulizo Sanga(daktari bingwa wa magonjwa ya moyo) ,amewaambia waandishi wa habari hospitalini hapo kwamba, mh Mbowe alipokelewa jana akitokea Hospitali ya Doctors Plaza ya Kinondoni,jijini Dar Es Salaam, kwa ajili ya uangalizi na uchunguzi zaidi kutokana na kuugua ghafla wakati akiwa katika msafara wa mgombea urais wa CHADEMA, Edward Lowassa.

Mh Mbowe amelazwa katika hospitali ya Muhimbili, kitengo cha moyo, baada ya kuugua ghafla jana na kukimbizwa hospitalini hapo.
 
Nae James Mbatia mwenyekiti wa NCCR Mageuzi, ambaye pia ni mwenyekiti mwenza wa UKAWA, amefika hospitalini hapo kumjulia hali mh Mbowe, na amesema pamoja na hali ya kuumwa ya mh Mbowe, wao bado wanaendelea kufanya kazi na kwamba ratiba mbalimbali za vikao vya UKAWA ziko palepale, na amewaomba watanzania kuwa watulivu na kuendelea kumuombea mh Mbowe, apone haraka.

Tofauti Kati ya Mrema na Lowasa Kwenye Ugombea Uraisi

$
0
0
Tofauti kati ya Mrema na Lowasa wote wakiwa wametokea CCM na wote wakiwa wagombea uraisi kupitia upinzani walikoingia bila kujua sera za vyama walivyoingia kwa kuwa waliingia chap chap ni kama ifuatavyo

1.Mrema alikuwa akiungwa na makundi ya wasomi waliobobea wakiwemo maprofesa walikuwa tayari kumbeba na kusukuma gari lake kuonyesha upendo wao kwake.Lowasa wasomi wamekaa naye mbali wengi hata kumsikia hawataki kuanzia wasomi wakubwa hadi wadogo.Slaa alikuwa kipenzi cha wasomi

2.Mrema aliungwa na watu wengi wa hali ya chini (walalahoi) ambao walimpenda bure bila gharama yeyote kwa kuwa alijitambulisha kama mlalahoi mwenzao wakawa wanamwunga mkono na kumsindikiza kwa makundi makubwa ya kutisha wakihemka kwa mihemko ya dhati ya kumwunga mkono mgombea wao.Lowasa haungwi mkono na walalahi wengi kwa kuwa kajitanabaisha kama mtu mwenye pesa anayetaka kumkomboa mlalahoi!! Walalahoi wazo la kukubali kuwa tajiri aweza kuwakomboa wengi wanalikataa hivyo Lowasa kumfanya akose waunga mkono kutoka kundi la walalahoi.Walalahoi wengine ambao wako tayari kumfuata ni wale ambao wanaamini kuwa Lowasa ana hela na wanataka pesa zake kwanza ili waandamane naye ana WAFUASI MASLAHI WENGI MNO ambao hawamwungi mkono kwa dhati kama ilivyokuwa kwa mrema.

3.Mrema alipoondoka CCM aliondoka na wafanyabiashara wengi wazawa kibao ambao walikuwa wakinyionyesha wazi na kumchangia hasa kwa ajili ya mbio za uraisi bila woga na kwa mapenzi ya dhati kwa mrema.Lowasa anaoondoka nao CCM ni watu maslahi si watu wenye hela wanaotaka kumsaidia bali wengi ni wale omba omba wavizia pesa za Lowasa wanaosubiri Lowasa atafute pesa awagawie!! Ziwasaidie ubunge,udiwani au katika mishe mishe za maisha yao.Ni watu wenye tamaa ambao wangependa wapenye waingie ndani ya Team lowasa kule kwenye fuko la hela hasa walibomoe.
Makundi ya wengi wanaohama CCM kumshabikia Lowasa ni wachovu kipesa na kimaisha wamepigika.Wanavizia LOWASA

4.Mrema alibebwa na vyombo vya habari bure hakutoa hata thumuni na misafara ya wasindikizaji ilikuwa ni ya bure hakuwapa chochote.Lowasa kuanzia vyombo vya habari visivyokuwa na haya kutwa vinawinda hela yake na wasindikizaji kuanzia bodaboda wanasema HAPENDWI MTU NI POCHI TU alete pochi tuingie barabarani.

5.Mrema alijipambanua kama mpiganaji wa wazi wa ufisadi Lowasa kauli mbio yake ni ya kuondoa CCM ,ufisadi ulimi wake unashindwa hata kutamka

Kwa ujumla Mrema alikuwa na nguvu kubwa kuliko Lowasa ya uungwaji mkono wa dhati.Kwa kuangalia aina ya waunga mkono Lowasa sisiti kusema uwezo wake wa kushinda Uraisi ni mdogo mno.Angekuwa na Sifa za mrema angalau angefurukuta.

Maoni Binafsi Kutoka Kwa YEHODAYA -JF

Majimbo Matano Kurudia Kupiga Kura za Maoni CCM

$
0
0
Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CC) imeagiza kurudiwa kwa uchaguzi katika majimbo matano yaliyopo Tanzania Bara kutokana na dosari mbalimbali zilizojitokeza katika mchakato wa kura ya maoni.

Majimbo yanayotakiwa kurudia uchaguzi wa kura ya maoni ni pamoja na Makete, Busega, Ukonga, Rufiji na jimbo la Kilolo.

Akizungumza na waandishi wa habari leo mjini Dodoma Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye amesema mchakato huo utarudiwa siku ya Alhamisi Agosti 13 mwaka huu.
Amesema baada ya uchaguzi huo matokeo yatapelekwa katika vikao vinavyoendelea kwa ajili ya uamuzi.

Akizungumzia kuhusu vikao vinavyoendelea katika ukumbi wa NEC mjini Dodoma amesema vikao hivyo vinaendelea vizuri ambapo jana kikao cha kamati ya maadili kiliendelea mpaka usiku.
Amesema leo wanatarajia kumaliza kikao cha Kamati Kuu ambapo kesho na kesho kutwa watamaliza na kikao cha halmashauri kuu ya chama hicho (NEC) kama ilivyopangwa.

Gazeti la Uhuru: Vijana waliomsindikiza Lowasa kuchukua fomu jana ni VIBAKA

$
0
0
Ni kitambo sana gazeti dada la chama Cha Mapinduzi limekua likinanga Harakati za vyama pinzani. Yote tisa kumi ni ripoti zilizomo kwa gazeti hili tar 11/08/2015 siku moja baada ya MTETEMO WA UKAWA JIJINI DAR.

"Ati Kundi la vibaka latikisa Ukawa. " hao vibaka mliwaona wapi, hizo fedha walizolipwa mliziona kwa nani, na hizo Pombe walizokunywa mliwanywesha?

Mmeanza kukata mauno hata ngoma bado haijaanza kudunda? Mtachoka mapemaaa. Kama Gazeti ni la kimapinduzi wapeni watu habari zenuu, msiwapotoshe watu kwa vitu walivyovishuhudia.

Niwaulize kidogo.

Hiviii Wizi wa kura katika michakato ya majimboni si habari? Semeni hayo.

Na je Rushwa iliyoota mizizi katika Harakati za uteuzi si habari? Andikeni hiyo.

Viewing all 104768 articles
Browse latest View live




Latest Images