Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104689 articles
Browse latest View live

Utoaji wa Mimba Wakithiri Dar....Wasichana 400 Dar Waripotiwa Kwa Utoaji wa Mimba

$
0
0
Zaidi ya wasichana 400 wenye umri kati ya miaka 19-30 wametajwa kufika katika vituo vya afya katika kipindi cha mwezi July hadi Augost mwaka huu kwa ajili ya matatizo ya utoaji mimba

Jambo linalosabisha ongezeko la tatizo la ugumba na vifo vya watoto chini ya miaka mitano nchini Tanzania.
Takwimu hizo zimezotolewa hii leo katika hospitali ya Mwananyamala Jijini Dar es Salaam na Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Kinamama na Afya ya Uzazi Dkt. Luzango Maembe, ambapo zinaonyesha asilimia kubwa ya wanawake hutoa mimba mitaani kwa kutumia njia za kienyeji pia wataalamu wasio na ujuzi hali inayopelekea wapate matatizo ya kudumu.

Dkt. Maembe amesema kila siku wanapokea wagonjwa wawili wenye tatizo la kuharibika kwa mimba licha ya kuwepo wengine ambao huwa hawaripoti hospitalini na kuitaka jamii kuzingatia elimu ya afya ya uzazi pamoja na kuondokana na tabia ya kutumia njia zisizo salama.
"kati ya wagonjwa 200 wanaoletwa katika wodi ya wakinamama zaidi ya sitini au sabini wanakutwa na tatizo la mimba kuharibika au kutoa mimba kwa njia za kienyeji" alisema Maembe
Akizitaja baadhi ya njia zisizo salama zinazotumika kuwa ni pamoja na spoku za baiskeli utomvu wa mti wa muhogo, vyuma vyenye ncha kaali na vidonge, na kuwa utaratibu huo hufanyika bila kufuata maelekezo ya madaktari.
Aidha Dkt. Maembe amesema takribani kila siku wanapokewa wagonjwa wawili ambao wanamatatizo ya kuharibika kwa mimba na kuwa kati ya wasichana 25 kati yao watano wanatajwa kutoa mimba kwa njia rasmi na zisizo rasmi.

Katika zahanati na hospital kuwa za wilaya jijini Dar es salaam zinaonyesha asilimia kubwa ya wanawake hutoa mimba mitaani kwa kutumia njia za kienyeji pia wataalamu wasio na ujuzi.
Kulingana na utafiti uliofanywa na chuo kikuu cha afya Muhimbili mwaka 2012 kuhusu utoaji wa mimba uliofanyika katika kata za wilaya ya Temeke ulionyesha asilimia 33 ya wasichana walipata mimba zisizotarajiwa . Kati yao asilimia 26 walizitoa, asilimia 87 zilitolewa kwa njia zisizo salama.
Wasichana zaidi ya 400 wenye umri kati ya miaka 19 na 25 waliohojiwa na kukiri kutoa mimba kwa msaada wa marafiki wa kiume, ndugu au wahudumu wa afya.

Kitaifa takwim zinaonyesha asilimia 18 ya mimba 2, 430,000 zilitolewa kiholela zilisababisha vifo.
Katika hospitali ya Amana na Temeke wanawake 444 walifikishwa kutokana na kesi za utoaji mimbavichochoroni tangu Januari hadi Juni mwaka huu.huku miongoni mwa wanaotoa mimba hizo ni wasichana wadogo na wanafunzi.

Uchunguzi unaonesha idadi kubwa ya wanaotoa mimba kiholela, hupata madhara mbalimbali ikiwamo kutoboka utumbo, kuchanika kwa kizazi, kuoza na wengine kuharibu figo.
Dkt. Chande Makaranga kwa uponde wake yeye analeza vitendo hivyo kuwa ni hatari kwa wanawake wanaotegemewa kuchangia kiasi kikubwa cha ukuaji wa uchumi wa taifa kwani wakipatwa na madhara hayo ni vigumu kuchangia katika uchumi hata kujenga familia kwa kupata watoto.

Lowassa Avunja REKODI Jijini Mbeya..Ni Mafuriko ya Watu Haijawahi Tokea

$
0
0

Hii Ni Zaidi ya mafuriko Angalia Jinsi Watu walivyojazana Uwanjani Kumshuhudia Mgombea wa Chadema Edward Lowassa Mbeya...

JWTZ Wakanusha Kunyang'anywa Kadi Zao za Kupigia Kura

$
0
0
Mkurugenzi wa Habari na Uhusiano wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ), Kanali Ngemela Lubinga (katikati), akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari Dar es Salaam leo.

JESHI la Wananchi Tanzania (JWTZ), limekanusha kuwanyang'anya kadi za kupigia kura maofisa na askari wake kama ilivyodaiwa na mmoja wa viongozi wa chama kimoja cha siasa na kutolewa katika vyombo vya habari na mitandao ya kijamii.

Akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari Dar es Salaam leo asubuhi Mkurugenzi wa Habari na Uhusiano wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ), Kanali Ngemela Lubinga alisema madai hayo siyo ya kweli na  kuwa jeshi hilo halijafanya hivyo na wala haliwezi kufanya hivyo.

"Wanajeshi hawaruhusiwi kuwa wanachama wa chama chochote cha kisiasa na kuwa mwanajeshi haruhusiwi kuwa shabiki wa chama chochote cha kisiasa."

Lubinga alisema Jeshi la Wananchi Tanzania linafanya kazi zake kama 'professional state organ duniani na kuwa mwanajeshi anayekiuka huchukuliwa hatua za kinidhamu za kijeshi wala si za kiraia.

Alisema Jeshi la Wananchi Tanzania limesikitishwa na kauli hiyo iliyotolewa na kiongozi huyo.

"Wananchi na viongozi wa kisiasa mnaombwa mfanye kazi zenu za kisiasa na zisianzishwe hoja nje ya maeneo hayo ya kisiasa kwani lugha hizo za upotoshaji zinaweza kuleta hofu, ukakasi na wasiwasi kwa wananchi" alisema Kanali Lubinga.

Kanali Lubinga alisema jeshi hilo linaendelea na shughuli zake kama kawaida halipendi litolewe kauli za upotoshaji, kusikoeleweka ufuatwe utaratibu wa kuuliza kupata majibu ya uhakika kwani wananchi wanaimani na jeshi lao.

CCM Wakanusha Habari Iliyoenea Kuwa Mgombea Wake, Dr John Magufuli Ameahidi Kugawa Laptop Kwa Walimu Wote Nchini

$
0
0
Chama cha Mapinduzi (CCM) kimekanusha uvumi ulioenea sehemu mbalimbali kuwa Mgombea wa Urais kupitia tiketi ya Chama hicho,Dkt.John Pombe Magufuli amewaahidi Walimu kuwapa Kompyuta kama CCM itapita madarakani.

Akizungumza na Waandishi wa Habari katika Ofisi ndogo ya Makao Makuu ya Chama hicho,Katibu wa NEC,Itikadi na Uenezi,Nape Nnauye amesema kauli hiyo siyo ya kweli na haikutolewa na Mgombea huyo wa Urais,Dkt.Magufuli.

Hatahivyo,Nape amesema kauli hiyo imetolewa kwa nia mbaya kuonyesha Chama cha Mapinduzi kimeanza ziara ya kampeni mapema.

Amesema watu walioinukuu kauli hiyo wamesema imetoka katika Ilani ya Uchaguzi ya Chama hicho.
 
" Ilani ya Uchaguzi ya CCM imetoka jana Agosti 13,2015 katika Mkutano wa Chama uliofanyika jana mjini Dodoma na inatarajiwa kuzinduliwa Agosti 23 mwaka huu katika uzinduzi wa Kampeni,hivyo kauli yoyote iliyotoka kwa chama hicho ikidaiwa imetoka katika Ilani yetu ya Uchaguzihiyo siyo ya kweli,kwani Ilani hiyo itazinduliwa wakati wa uzinduzi wa kampeni Agosti 23" alisema na Nape kwa msisitizo.

Kuhusu msimamo wa Chama cha Mapinduzi kwa wanachama wanaohama chama hicho,Nape amesema wanachama hao wanahama kwa mapenzi yao binafsi wengine wamehama kwa sababu ya kushindwa katika kura za maoni za chama.


Diamond: Nipo tayari kwa kifo! Ndoto Yangu Imetimia

$
0
0
Staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’ akiwa na mtoto wake Latifah ‘Princess Tiffah’.
SIKU chache baada ya staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’ kupata binti na kumwita Latifah ‘Princess Tiffah’ na kuanza maisha mapya ya familia na mzazi mwenzake, Zarina Hassan ‘Zari’, nyota huyo anadaiwa kutoa ya moyoni kwa kusema kuwa sasa yupo tayari kwa kifo kwa vile ndoto yake kubwa ya kupata mtoto imekamilika na ana chata duniani.

KWANZA ANAMSHUKURU MUNGU
Kwa mujibu wa chanzo chetu makini, Diamond alisema anamshukuru Mwenyezi Mungu kwa kumtimizia ndoto yake ambayo amekuwa akiiota usiku na mchana na kwa miaka mingi tangu kuingia ‘ukubwani’ hivyo, bahati mbaya yoyote ikitokea akapoteza uhai itakuwa poa tu kwake.

NDICHO KITU ALICHOBAKIZA
Chanzo kilikwenda mbele zaidi kwa kusema kuwa kuhusu mafanikio ya kimuziki na kimaisha, nyota huyo anaamini alishafikia malengo, alibakiza kimoja tu, mtoto.
“Unajua katika maisha, ukipata mali au mafanikio mengine ujue tatizo kubwa litabaki kwenye familia na familia yenyewe si kupata mke au mume bali kupata mtoto.
“Sasa jamaa siku zote alikuwa akisema, pesa kwake si tatizo, nyumba ya kuishi nzuri anayo, gari la kutembelea pia. Kilichokuwa kikiuchakaza moyo wake ni kutopata mtoto ili awe kama wengine. Hicho ndicho kitu alichokuwa amebakiza hapa duniani,” kilisema chanzo.

ZARI NAYE HANA FURAHA YA MTOTO
Chanzo kikazidi kudai kuwa, wakati Diamond akifurika machozi ya furaha kwa kupata mtoto, mzazi mwenziye, Zari yeye hana furaha kufuatia baba wa watoto wake watatu au aliyekuwa mumewe, Ivan Ssemwanga kumpiga madongo kupitia mtandao wake wa Instagram.
Mfano, juzi kwenye mtandao wake, jamaa huyo ametupia picha akiwa na mtu anayedaiwa kuwa eti, ndiye baba wa mtoto Tiffah.
“Zari anaujua ukweli kwamba mtoto ni wa Diamond. Sasa wale jamaa kuendelea kutangaza si wa Diamond wao wanajuaje wakati siri ya mtoto ni wa nani anaijua mama? Hayo ndiyo maneno ya Zari kila kukicha.

“Yeye ni mtu mzima, ana akili timamu. Hawezi mtoto wa huyu akampa yule. Nadhani maneno ya aliyekuwa mumewe ndiyo yanamkosesha raha. Lakini Diamond mwenyewe ni peace tu.” Chanzo.
Baada ya kujazwa ubuyu huo, paparazi wetu alifanikiwa kukutana uso kwa macho na Diamond mwenyewe ambaye kweli alionekana mwenye furaha muda wote na hata alipogusiwa hilo alimshukuru Mungu akisema maombi yake yamekubaliwa.

STUDIO YA DIAMOND HAIKALIKI
Habari zaidi zinasema kuwa, nyota huyo kupata mtoto imekuwa ‘nongwa, watu hawali wala hawanywi’. Hapatikani kwenye studio yake ya Wasafi Record iliyopo Sinza Mapambano.
Amani lilifika juzi na kumkosa lakini mmoja wa wafanyakazi wake alisema: “Weee! Chezea kichanga wewe. Baba Tiffah anakuja lakini si kama zamani. Unajua kwa sasa muda mwingi yupo na mwanaye.”

MSIKILIZE
Baadaye Amani lilimpata Diamond kwa njia ya simu na kumuuliza kuhusu madai hayo ambapo alisema: “Kusema kweli namshukuru Mungu kwa kila jambo ila zaidi kunipatia huyu Princess Tiffah. Kwani uwepo wake ni furaha kwangu na ni historia kubwa katika maisha yangu.
“Leo hii ikitokea nikafa basi watu watanikumbuka zaidi wakimuona mwanangu, maana huyo ndiye mrithi wa kila kitu kwangu.“Nilikuwa najiuliza nikifa sina mtoto itakuaje? Ina maana sitaacha kumbukumbu. Lakini kwa sasa nipo tayari kwa kifo kama Mungu amenia-ndikia.
GPL

Nape Afunguka: Wanao Hama CCM Sasa ni Sawa na OlL Chafu ya Gari..

$
0
0
Katibu Mwenezi wa CCM Nape Amekaririwa Akisema kuwa CCM ina Wanachama Wengi sana, Hao wawili watatu mnaosikia wanahama chama kila siku ni sawa na Oili chafu ya Gari ....Hawana Tena Thamani.....


Wema Sepetu akijitetea Skendo ya kujiuza kwa Mkongo kisha kukimbiwa bila malipo

$
0
0
Chanzo chetu ambacho ni makini kilipenyeza kuwa, katika tukio hilo la hivi karibuni, staa huyo alikuwa hafahamiani na mwanaume huyo, lakini kuna kijana mmoja ambaye mara nyingi anawakuwadia mastaa wa Bongo kwa matajiri, alidaiwa kumtonya Wema kuwa kuna ‘mchati’ anataka kutoka naye.

Kilifunguka kwamba, baada ya Wema kung’atwa sikio juu ya Mkongomani ambaye ana ‘hela chafu’, alidaiwa kuonekana kuchachawa hivyo eti alikubali kupelekwa kwake akajazwe ‘mihela’.

Baada ya Wema kufika hotelini hapo, alitambulishwa kwa Mkongo huyo ambapo baada ya kusalimiana tu, walikaa pamoja na kuanza ‘kufanya yao’.

Baada ya Wema na Mkongo huyo kukutana na kumaliza ‘shida’ zao, kila mtu alichukua hamsini zake huku jamaa huyo ‘akim-block’ Wema kwenye simu.

Pamoja na Wema mwenyewe Kukanusha kupitia instagram kwamba hizo picha ni za 2011, ushahidi wa simu za mezani umemuumbua kwani simu inayoonekana ikimpiga picha ni samsung galaxy s6 edge na simu inayoonekana ipo mezani ni iphone 6 ambazo ni simu zilizotoka juzi juzi tuu.

Haya.....

Irene Uwoya Yupo Hatarini Sana Kupoteza Ubunge Viti Maalum

$
0
0
Muigizaji wa bongo movies Irene Uwoya aliyejiunga na ccm na kuchaguliwa kuwa mbunge wa viti maalum tabora yupo hatarini kupoteza cheo chake cha ubunge wa viti maalum na huenda wabunge viti maalum wengi sana wa ccm nao wataachia ngazi.

Mbunge viti maalum aliechaguliwa kwa sasa ataingia mjengoni mpaka ifikapo oktoba baad ya kampeni na uchaguzi ambapo kila
jimbo litapata mbunge(sio wa viti maalum) wake ambapo hawa wabunge wa viti maalum waliochaguliwa saizi italazimu idadi yao ilingane sawa na idadi ya wabunge wawakilishi wa majimbo wa vyama vyao, mfano kwa ccm mwaka 2010 kabla ya kampeni walikuwa na wabunge viti maalum 92 ila baada ya kampeni na uchaguzi ilipata wabunge 60, kutokana na kupoteza majimbo mengi hivyo ikabidi idadi ya wabunge wa ccm wa viti maalum ipungue toka 92 hadi 60, na wakati wao ccm waliandaa wabunge 92 wa viti maalum wakijua watapata majimbo mengi , matokeo yake ikabidi chama kiwapunguze hadi 60 na baada ya hapo nafas zilizobsaki 22 za wabunge viti maalum wakapewa chadema.

Kwa sasa ni wazi kabisa tembo yupo shambani ambayeaneyejifanya hamuoni aende mahututi, kwa upepo huu wa siasa
ni wazi kabisa ukawa, act na vyama vingine watachukua majimbo mengi sana kwenye nafasi za ubunge(sio ule wa viti maalum), hivy basi endapo CCM itapata wabunge kwenye majimbo machache asilimia hiyo ya wabunge itabidi ilingane na wabungewataopitishwa kwenda kuwakilisha majimbo kwa nafasi za viti maalum na kukilazimu chama kukata wabunge viti maalum wawe wachache

Ben Paul & Belle 9 amkeni usingizini , Mmelala Sana Aise....

$
0
0
Toka wimbo wa NIKIKUPATA mpaka SOPHIA.Ben paul ameendelea kuthibitisha ubora wa kipaji chake maridhawa.Belle 9 ni kipaji kingine adhimu katika ardhi ya nchi yetu.Wasanii hawa wawili mpaka leo hawapati thamani na hadhi zao sahihi.

Napenda kuwaamsha usingizi kuwa wanatakiwa kuwekeza katika kazi zao ili watoke kimataifa.Katika dunia ya sasa hivi ili uwafanikiwe unahitaji kuwa na kipaji na management nzuri, vijana hawa ni kama wameridhika hivi,lakini ukweli ni kuwa lazima waamke ili kufika juu zaidi.

Nakaribisha hoja zaid,

LOWASSA Aahidi Kuunda Serikali Makini Itakayofanya Kazi Masaa 24 Kuwahudumia Wananchi

$
0
0
Mgombea urais kwa tiketi ya Chadema na Ukawa, Edward Lowassa jana alipokewa na maelfu ya watu mjini Mbeya ambao kwenye uwanja wa Ruanda, Nzovwe, aliwaambia wananchi kuwa hatataka mchezo katika serikali atakayoiongoza.

Pamoja na Jeshi la Polisi kutangaza kuzuia msafara wakati wa ziara ya waziri huyo mkuu wa zamani, hali ilikuwa tofauti jana wakati zaidi ya magari 20 yalimsindikiza kutoka Uwanja wa Ndege wa Songwe huku wananchi wakijitokeza barabarani kumshangilia hadi kwenye uwanja huo, ulio nje kidogo ya mji wa Mbeya ambako alihutubia.

Polisi walinda msafara
Msafara wa Lowassa uliwasili mjini hapa kwa kutumia ndege mbili, ya kwanza ikiwa imebeba waandishi wa habari wapatao 10 na nyingine iliyombeba mbunge huyo wa Monduli ambayo iliwasili saa  8:20.

Umati wa watu ulikuwa ukimsubiri nje ya uwanja huo na alipotoka ilianza safari ya kuelekea katikati ya jiji na msafara wa zaidi ya magari 20 pamoja na pikipiki.

Polisi walitanda barabarani, huku vijana wa Red Brigedi waliovalia sare nyeusi na miwani wakiwa wamesambazwa barabara yote.

Maeneo ambayo msafara ulipita kwa shida kutokana na umati wa watu kufurika ni Mbalizi, Mafiati Mwanjelwa, lakini polisi walifanya kazi ya ziada kuwaondoa watu waliokuwa wakitaka kuandamana kuusindika msafara huo.

Lowassa aliambatana na mgombea mwenza, Juma Haji Duni, mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe, mwenyekiti wa NCCR Mageuzi, James Mbatia na kulakiwa na viongozi wa mkoa pamoja na mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi, maarufu kwa jina la Sugu.

Akizungumza baada ya kukaribishwa kuhutubia na Duni Haji,  Lowassa alianza kwa kibwagizo cha “mchakamchaka  chinja” na kabla ya kuwashukuru wananchi wa mikoa ya Nyanda za Juu Kusini kwa kufurika hadi pomoni kwenye uwanja huo.

“Sitaki mchezo,” alisema Lowassa ambaye amekuwa akizungumzia uendeshaji wa Serikali kwa mtindo wa mchaka mchaka.

“Nataka maendeleo. Nataka Jiji la Mbeya liwe la kimataifa wakati wa Serikali yangu na litakuwa kama nchi ya Swaziland,’’ alisema akilifananisha jiji hilo na nchi hiyo ndogo iliyozungukwa pande zote na Afrika Kusini.

“Nitahakikisha Uwanja wa Ndege wa Songwe unakuwa wa kimataifa.”

Lowassa, ambaye alipata zaidi ya watu 50,000 mjini hapa wakati alipokuwa akisaka wadhamini wa urais kwa tiketi ya CCM, alisema Serikali yake pia itawajali walimu na wakulima, huku akisisitiza kwamba watakaochelewesha pembejeo watakiona cha moto.

Akizungumza polepole, Lowassa alisema katika Serikali yake hatataka mchezo katika kazi  na kwamba mawaziri wake watachapa kazi saa 24  kuwahudumia wananchi.

Kuhusu kiu ya wananchi waliotaka kujua kauli yake kwa polisi, alisema polisi wanatenda kazi huku wakitaka mabadiliko ya kupata mshahara mnono na kwamba ataboresha mahitaji ya wafanyakazi kwa ujumla.

Awali akiwakaribisha wageni, Sugu aliwashukuru wakazi wa Mbeya kwa kile alichokieleza kuwa ni kuleta mizuka kwenye uwanja huo kutokana na kufurika watu wengi. “Karibu Mbeya wageni, hapa siyo mafuriko ni gharika... kilichobaki ni kupiga kura ya kukuchagua wewe Rais Lowassa,’’ alisema.

Sugu alisema goli la mkono la CCM litazuiwa na beki makini Lowassa  na kutoa onyo kwamba CCM wasidiriki kutumia kadi bandia za wapiga kura.

Naye Mbatia  alisisitiza suala la Watanzania kulinda amani na upendo na kuwasihi wakazi wa Mbeya wasikubali kufanya vurugu katika kipindi chote cha kampeni na uchaguzi.

Wabunge wawili wajiunga Chadema.
Wakati Lowassa akipata wadhamini, Chadema ilipata neema tena wakati wabunge wawili wa CCM,  Dickson Kilufi  wa Mbarali na Luckson Mwanjale wa Mbeya Vijijini walipotangazwa kujiunga na chama hicho kikuu cha upinzani.

Hata hivyo, Mbowe alimkabidhi kadi Kilufi pekee baada ya Mwanjale kutofika eneo hilo licha ya kuonekana uwanja wa ndege.

Mtabiri: Kifo cha Mgombea Urais Mwaka Huu Kipo Palepale

$
0
0
MTABIRI maarufu Bongo, Maalim Hassan Yahya ameibuka na kusema kwamba utabiri aliowahi kuutoa kwamba kuna mgombea urais atafariki, bado upo palepale.

Maalim Hassan alisema kuugua ghafla kwa Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe ni dalili tu za ukamilifu wa utabiri wake lakini suala la mgombea urais kudondoka na kufa akiwa jukwaani akifanya kampeni linakuja.

“Kuugua kwa Mbowe hakujatimiza utabiri kama ulivyosema ila hizo ni dalili tu lakini kuna mgombea atadondoka jukwaani akifanya kampeni na atakufa lakini haioneshi ni wa chama gani na hii ni kutokana tu na mwaka huu ulivyoanza kinyota,” alisema mtabiri huyo.

Mwaka huu mwanzoni mtabiri huyo alitoa utabiri uliyoonyesha kwamba kutakuwa na kifo cha mgombea urais pamoja na mambo mengine ikiwemo kuibuka kwa magonjwa ya kushangaza

LOWASSA Ahamishia Mafuriko Jijini Arusha..Hapa Nimekuwekea Picha Kadhaa Uone Jinsi Mambo yalivyokuwa

$
0
0

LOWASSA Ahamishia Mafuriko Jijini Arusha..Hapa Nimekuwekea Picha Kadhaa Uone Jinsi Mambo yalivyokuwa

Busu la Wema Sepetu na Makamba Lazua Jambo..Wadau Wasema Wamependezeana

$
0
0
Musa Mateja
BUSU walilopigana mrembo wa Bongo Movies, Wema Sepetu ‘Madam’ na Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, January Makamba lilizua gumzo la aina yake huku wambea wakisema; “wamependezana.”

‘Katukio’ hako ka’aina yake kalitokea wiki iliyopita katika Ukumbi wa Mlimani City jijini Dar kulipokuwa na hafla ya umoja wa wasanii waliokuwa wakimuaga Rais Jakaya Kikwete, anayemaliza madaraka yake, Oktoba 25, mwaka huu.

Wakati shamrashamra zikiendelea, muda wa kucheza muziki, Madam alikutana uso kwa uso na Makamba ambaye anapenda kucheka na kila mtu, wakakumbatiana na kubusiana ‘kiaina’ hali ambayo iliwafurahisha watu wengi.
“Wamependezana. Makamba mtu poa, imenishtua kidogo walipochelewa kuachiana lakini najua ni salamu ya kumisiana tu,” alisikika shuhuda mmoja.
Wawili hao kila mmoja ana mtu wake, kukumbatiana huko na kubusiana kulikuwa ni kwa Kawaida tu

Shamsa Ford: Natamani Kuolewa na Mtu Ambaye Si Maarufu

$
0
0
Muigizaji wa filamu za Bongo, Shamsa Ford ameweka wazi hisia zake za kutaka kuingia kwenye ndoa.

Shamsa ambaye kwa miezi kadhaa iliyopita amekuwa akikanusha kuwa na uhusiano na Nay Wa Mitego licha ya kuwepo kwa dalili nyingi zinazoashiria kuwa ni wapenzi, amesema sasa umefika muda anatamani kuolewa.

Muigizaji huyo wa ‘Chausiku’ ambaye ni mama wa mtoto mmoja, ameongeza kuwa licha ya kutamani kuwa mke wa mtu lakini nafasi hiyo hawezi kumpa mtu maarufu, kwa lugha nyingine hawezi kuolewa na Nay Wa mitego.

“Sijui hizi hisia zimetoka wapi…kwa sasa natamani kuolewa na nipo tayari kuolewa ila na mtu ambae si maarufu. Maisha ya usingle nimeshayachoka,” aliandika kupitia akaunti yake ya Instagram.

Wiki mbili zilizopita wawili hao walionekana wakibadilishana mate kwenye birthday ya Shamsa kama inavyoonekana picha hapo juu.

Ushauri: Mumewe ana Maumbile Makubwa, Mkewe Anaumia Wakati wa Tendo la Ndoa

$
0
0
Habarini wadau,

Nitakuwa wazi sana na kwa anayeweza kunisaidia anisaidie ila kama mtu hajui/ hawezi kutoa msaada basi ni bora akaacha kuchangia kuliko kutusi/ kudhihaki.

Nina kaka yangu kabisa ambaye kiukweli alizaliwa na uume mkubwa kupita kiasi, namaanisha sote tuna maumbile makubwa lakini wa kwake umekuwa na matokeo mabaya kwa mkewe.

-Mke wake (shemeji yangu) amekuwa akilalamika mara kwa mara wakati wa tendo la ndoa, na kiasi kwamba kaka anasema huwa haridhiki afanyapo tendo hilo na mkewe kwani hamalizi hamu na anaishia njiani.

Ilifikia mahali kama kaka akirudi kutoka safari naye mkewe anaondoka kwenda kwao kwa sababu isiyo ya msingi, ila kuna siku alimtumia bro meseji kuwa "sina kizazi cha kuharibiwa hapo kitandani" ila sasa wana mtoto mmoja.

Mkewe anasema alikuwa anapata nafuu akifanya wakati akiwa mjamzito ila baada ya kujifungua akifanya anaumia sana kama zamani. Mwaka 2010 kaka alienda hospitali akapewa vi rubberband vya kuvalisha kwenye uume na alivileta home

Ila anasema akivaa na uume ukasimama haswa anaumia sana. Hata hivyo kuna daktari mwingine alimwambia asiivae kwani inazuia flowing ya damu vizuri katika uume.

Huyu shemeji siku hizi hata akienda harusini au katika shughuli yoyote basi ataunganisha mpaka kwao na anamkwepa mumewe mara kwa mara ila kwa bahati nzuri hasemi kwa watu wa nje.

Ila sasa nafikiri mama yake pamoja na dada zake wanajua,na kiukweli ni kama hana hata wivu akisikia mumewe ana mwanamke wa nje.

Naombeni mtusaidie katika hili wadau

Natanguliza shukrani

By Awsom-JF

Mwanamitindo Fraviana Matata Afunga Ndoa...Nimekuwekea Picha Kadhaa Hapa

$
0
0
Mwanamitindo Fraviana Matata amefunga ndoa katika kanisa la St.Joseph na mpenzi wake wa siku nyingi aitwaye Deogratius Massawe.
11363943_614978965271610_490778977_n[1]
11849047_1031723616852156_1648758899_n[1]
11910322_1687559864807151_1741215753_n[1]

NEC Yapiga Marufuku Maandamano Urudishaji Fomu za Urais, Watu Saba tu Kuruhusiwa Kumsindikiza Mgombea

$
0
0
Tume ya Taifa ya Uchaguzi (Nec), imetangaza siku ya urejeshaji fomu za Urais na Makamu wa rais kuwa ni Alhamis ijayo.

Aidha, imepiga marufuku maandamano na badala yake watu saba tu ndio wataruhusiwa kusindikiza wagombea.

Taarifa ya Nec kwa vyombo vya habari jana na kusainiwa na Mkurugenzi wa NEC, Ramadhani Kailima, ilisema urejeshaji fomu utaanza saa 1:30 asubuhi hadi saa 10:00 jioni.

Alisema wagombea wote wanatakiwa kufika kwenye ofisi za Tume wakisindikizwa na watu hao na majina yao yawasilishwe Tume kabla ya Agosti 20, ili kuratibu kazi hiyo.

“Wagombea hawaruhusiwi kuja Tume kwa maandamano, shamrashamra, nderemo wala vifijo. Hii ni kwa sababu siku hiyo vyama vya siasa vitakavyowasilisha fomu za kuomba uteuzi vitakuwa vingi hivyo kila chama kikija Tume kwa maandamano na shamrashamra kunaweza kutokea uvujifu wa amani,” alisema.

Alisema sababu nyingine ni kuwawezesha wananchi wengine kuendelea na shughuli zao na sababu ya tatu ni kuimarisha amani na utulivu na kwamba ni vyem vyama vikafuata maelekezo hayo.

GHARIKA KUU ARUSHA!!!! EDWARD LOWASSA Aiteka kaskazini Mamilion ya Watu Wamlaki, Viongozi wa CCM Kilimanjaro na Arusha Waitosa CCM na Kujiunga CHADEMA.

$
0
0
GHARIKA KUU ARUSHA!!!!
EDWARD LOWASSA aiteka kaskazini
Mamilion ya watu wamlaki, viongozi wa CCM Kilimanjaro na Arusha waitosa CCM na kujiunga CHADEMA.
Aliyekuwa Waziri wa mambo ya ndani Laurence Masha ajisalimisha CHADEMA kabla ya ujio wa LOWASSA huko MWANZA.
UKAWA KIMEELEWEKA!!


NAPE Unapotuambia Hii ni OIL Chafu, Haifai, Tunaweza Kukupa Utitiri wa Matumizi Yake...na Utashangaa

$
0
0
Wakati wa utoto kule Moshi tulikuwa tunatumia maguta (magari ya miti), kilainishi cha beringi (bearing) zake tulikuwa tunatumia OIL CHAFU, pia ili mbao ama nguzo isiliwe na MCHWA tulikuwa tunaipaka OIL CHAFU. Siku hizi hata kinyesi cha Ng'ombe kule Moshi wanatengenezea gesi (bio gas), nacho ni dili pia. Wajerumani maji ya kuflashia chooni yanachujwa yanarudi tena mtaani kwa matumizi mengine. Unapotuambia hii ni OIL chafu, haifai, tunaweza kukupa utitiri wa matumizi yake.

By Bwana Mushi

Rais Kikwete Ammwagia Sifa MAGUFULI.........Awafananisha Wapinzani na Moto wa Mabua ambao Hauwaki Ukadumu

$
0
0
RAIS Jakaya Kikwete amesema ukiona Waziri anajisifia kafanya mambo kadhaa kwa uwezo wake, huyo ana matatizo ya ufahamu na ni mpenda sifa, kwa sababu mambo anayoyafanya anatekeleza majukumu aliyopewa na Rais na kwa mujibu wa muongozo aliopewa.

Alisema hayo jana wakati akiagwa jijini Dar es Salaam na taasisi zilizopo chini ya Wizara ya Ujenzi, huku akiongeza kuwa vuguvugu za kisiasa zinazoendelea, ni moto wa mabua ambao hauwaki ukadumu.

Kwa mujibu wa Rais Kikwete, Waziri wa Ujenzi, Dk John Magufuli ambaye pia ndiye mgombea wa urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), angekuwa kama mawaziri hao, angejisifia kwa mafanikio yote yaliyopatikana katika Wizara alizoziongoza, ikiwemo Wizara hiyo ya Ujenzi.

Katika hotuba hiyo amesema sifa moja ya Dk Magufuli ni kutambua kuwa akiwa Waziri, anafanya kazi kwa niaba ya Rais kwa mujibu wa muongozo na rasilimali alizopewa, ambavyo vimeeleza nini anatakiwa kufanya kama waziri.

“Sijawahi kukusikia ukijisifia binafsi maana na wewe ungeweza kabisa kufanya hivyo kwa sababu barabara zote hizi ungeweza kusema ni mimi nimejenga na sio Rais… Sasa bila Rais kukuteua na kukupa muongozo na rasilimali ungepata nafasi ya kujenga hizo barabara?”Alihoji Rais Kikwete.

 Alisema baadhi ya watu wamediriki kusema waliyoyafanya ni wao na sio Rais aliyewapa muongozo huo kufanya yoliyofanyika na kuongeza:

“Unadhani Rais atakuja kujenga nyumba? Amekwambia nimekupa hivi hapa na kila mtu niliyemteua nafanya hivyo na inatangazwa kwenye gazeti la Serikali.”

Rais Kikwete alisema Rais hana ushindani na Waziri wake na pia Waziri hana mashindano na Rais kwa sababu Waziri anafanya kazi kwa niaba yake maana ndiye aliyemteua.

Moto wa mabua
Alisema CCM imemteua Dk Magufuli kugombea nafasi ya Urais kupitia chama hicho na ana imani atapita salama kwa sababu ni mtendaji kazi mzuri na kwamba vurugu zinazoendelea za kisiasa ni moto wa mabua tu

. “Nina imani chama chetu kimekuteua kuwa mgombea wa urais kwa sababu ni mtendaji… Taifa litanufaika likipata kiongozi kama wewe, hao wengine ni moto wa mabua tu hauwaki ukadumu,” alisema Rais Kikwete.

Rais Kikwete alisema ana imani Mungu akijalia Magufuli kuwa Rais basi yale mambo mazuri aliyoyafanya katika Wizara ya Ujenzi na sekta ulizopata kuongoza, atatumia maarifa na uzoefu huo kusukuma mbele gurudumu la taifa mbele.

Alisema Dk Magufuli kila wizara aliyopelekwa alifanya vizuri, ikiwa ni pamoja na Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Miundombinu na Ardhi ambapo alisaidia kuondoa ujanja ujanja na kuimarisha nidhamu lakini hakuwahi kusema ni yeye binafsi ameleta manufaa hayo.

“Kuna wakati sehemu fulani ina matatizo watu wanasema jamani kwa nini msimlete Magufuli, tunasema hawezi kuwa kila mahali… Na sekta hii ya ujenzi ni sekta muhimu na kubwa, nashukuru chini ya uongozi wako tumeifikisha mahali pazuri,” alisema Rais Kikwete.

 Aidha Rais Kikwete alisema anajivunia kuunganishwa kwa barabara zote za mikoa na Wilaya nchini katika kipindi cha uongozi wake na hiyo ni kwa jitihada na usimamizi uliofanywa na Waziri Dk Magufuli.

“Katika uongozi wangu tumefanikiwa kuunganisha karibu mikoa yote nchini kwa kiwango cha lami. Jambo hili limewezekana kwa ushirikiano na wafanyakazi wote pamoja na wataalam wa wizara hii ya ujenzi.”

 Kikwete alisema alipoingia madarakani, bandari ya Dar es Salaam ilikuwa inasafirisha jumla ya tani milioni 6.7 za mizigo kwa mwaka, lakini hivi sasa bandari hiyo inasafirisha mizigo zaidi ya tani milioni 15 hadi mwishoni mwa mwaka huu, bandari ya Dar es Salaam itakuwa na uwezo wa kusafirisha zaidi ya tani milioni 18, kitu ambacho kitaongeza ukuaji wa uchumi na kuongezeka kwa pato la taifa.

Aidha alisema kukamilika kwa barabara zote nchini kwa kiwango cha lami kutawezesha uchumi kukua kwa haraka zaidi na kuifanya nchi kupiga hatua kubwa ya kimaendeleo kwa siku za usoni.

Rais Kikwete pia alisema katika kipindi chote cha uongozi wake ameweza kupambana na changamoto zilizokuwa zikiikabili wizara ya ujenzi na ndio maana mafanikio haya yamepatikana.

Hata hivyo, Rais Kikwete alisema mara baada ya kumaliza muda wake na kukabidhi madaraka kwa rais ajaye, ataondoka na kurejea kijijini kwao Msoga na kuendesha shughuli za kilimo, ikiwemo kilimo cha mananasi, mahindi na mazao mengine.

 “Nikimaliza muda wangu wa uongozi na kukabidhi madaraka, nitarudi kijijini na kwenda kuendesha shughuli za kilimo, na wala sitaki nikiwa kule mnifuatefuate. Niacheni nikawe mkulima hodari,” alisema Kikwete.

Alisema sasa taifa linahitaji kiongozi bora zaidi yake ili aweze kuendeleza pale alipofikia yeye kwani likipata kiongozi dhaifu hata haya mafanikio yaliyopo yatarudi nyuma.

 Kwa upande wake, Waziri Dk Magufuli alisema katika kipindi chote cha uongozi wake katika wizara ya ujenzi, ameweza kuyatekeleza vyema majukumu aliyopewa na rais kwa kushirikiana na wafanyakazi wenzake ndio maana wamepata mafanikio.

Alisema japokuwa wizara yake bado inakabiliwa na changamoto kadhaa, lakini imeweza kupambana nazo na kufanikisha ujenzi wa miundombinu yote muhimu iliyokuwa ikihitajika, Magufuli alisema anatumaini atakapokuwa Rais atatatua changamoto hizo zaidi kwa sababu anazifahamu vizuri.

 Awali wakiwasilisha mafanikio yaliyofikiwa na taasisi zao zilizopo chini ya wizara ya ujenzi, watendaji wa taasisi hizo walisema awamu ya nne imeweza kufanya mambo mengi na ya kuingwa.

Mtendaji Mkuu wa Tanroads, Patrick Mfugale alisema barabara zenye urefu wa kilomita 5,568 zimejengwa kwa kiwango cha lami katika serikali ya awamu ya nne na kugharimu Sh trilioni 4.9.

Mfugale alisema barabara zinazoendelea kujengwa hadi hivi sasa zina urefu wa kilomita 3,875 ambazo pia zitagharimu Sh trilioni 4 na bilioni 535 na kwamba jumla ya barabara zenye urefu wa kilomita 8,600 zimejengwa kwa kiwango cha lami nchini nzima ambazo ni sawa na asilimia 86 na nyingine ziko katika hatua mbalimbali za ujenzi. Imeandikwa na Regina Kumba na Emmanuel Ghula.
Viewing all 104689 articles
Browse latest View live




Latest Images