Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104417 articles
Browse latest View live

Wingi wa Swala Haukimbizi Simba Porini....Wewe Kijana Unayemkimbilia Kumfuata LOWASSA Ukawa Unajua Unajifungia Opportunities Mwenyewe?

0
0
" WINGI WA SWALA HAUMKIMBIZI SIMBA PORINI". TUKUTANE TAREHE 26/10/2015......
KIDUMU CHAMA CHA MAPINDUZI:- Now FACT is Picha ya kushoto ni CCM na Kulia ni Muungano wa vyama Vingi vya UKAWA against Chama Kimoja tu CCM..the FACT is Lowasa ndani ya CCM alipata wadhamini 800,700 lakini toka aingie UKAWA waliotoka kumfuata hawazidi 2,000...another FACT ni kwamba Lowasa alisindikizwa na Wenyeviti wa CCM Mikoa 15 kwenye kurudisha Fomu yake ya CCM mpaka leo waliomfuata UKAWA hawazidi 4....

Another FACT Meneja Mkuu wa kampeni za Lowasa CCM alikuwa Bashe mpaka leo amegoma kabisa kumfuata Boss wake UKAWA... another FACT Wabunge 150 wa CCM walikuwa wanamuunga mkono Lowasa akiwa CCM mpaka leo hakuna Mbunge aliyeshinda Kura za maoni CCM aliyemfuata Lowasa amefuatwa na wasiozidi 10 na wote wameshindwa kura za Maoni kwanza ndio wamemfuata hahahahaha...another FACT ni kwamba Dr. Nchimbi, Sophia Simba na Adam Kimbisa waliomtetea sana Lowasa Kamati Kuu kwenye mchujo wa Urais wameapa kwamba hawatakuja kumfuata Lowasa huko UKAWA....INFACT the FACT is jana Dr. Nchimbi kwenye kikao cha Baraza Kuu la UVCCM alisema "Watuwazima mkisha kaa kwenye kikao na kukubaliana kama tulivyofanya Dodoma kwenye kuchagua mgombea, halafu wewe ukatoka hapo ukaenda kinyume na makubaliano hufai kuwa Kiongozi wa Taifa ni Msaliti"....

FACT Lowasa amejitoa CCM kwa sababu at his age and time hakuwa na alternative ya kusubiri Miaka 5 ya uchaguzi tena NOW WEWE KIJANA UNAYEMKIMBILIA KUMFUATA LOWASA UKAWA unajua unajifungia opportunities mwenyewe cause unachokifanya ni "Point of no return" I mean yaani unaaamini Bashe Manager wa Lowasa hana akili wewe unazo zaidi? THINK.ABOUT IT TAFAKARI KABLA HUJARUKIA TRENI KWA MBELE! jamani I was just thinking aloud! Hahaha kama una tatizo jibu na FACTS PLEASE! ONLY FACTS HERE BABY!....WINGI WA MBUZI HAUMKIMBIZI SIMBA U KNOW - le Mutuz 


Nanyimwa Haki Yangu ya Tendo la Ndoa Kisa Mimi ni Mwana UKAWA

0
0
Imepita takribani week tatu tokea mheshimiwa waziri mstaafu ENL ajiunge na UKAWA na kusema ukweli mimi ni mmoja wa watu niliyekuwa natamani na naendelea kutamani mheshimiwa Mamvi ashike hatamu ya urais wa nchi hii tokea akiwa CCM.

Sasa alivyohama CCM na mimi nilihama nae na kuwa Mwana Umoja Wa Katiba ya Wananchi. Tokea hapo shemeji na wifi yenu ameninunia kwa kuwa yeye ni mwana ccm na ni mgombea wa viti maalum mkoa fulani. Sipewi unyumba na ndani hatuongeleshani. Ila majukumu mengine anayatekeleza kama kawaida. Nimejaribu kukaa nae kuongea nae kwa kituo lakini hataki kabisa kuweka maelewano baina yetu.

Na mimi kama mwanaume nahitaji huduma ya mke wangu mpenzi. Hivyo basi wanabodi naombeni ushauri wenu nifanyeje na mimi siwezi kuitema UKAWA.

Mtoto Tiffah wa Diamond Platnumz Apewa Zawadi ya Benz la Mil. 200

0
0
Musa mateja
Kazi ipo mwaka huu! Ndugu wa mzazi mwenzake na Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’, Zarinah Hassan ‘Zari The Boss Lady’ wamempa zawadi mtoto wa mastaa hao, Latiffah Nasibu ‘Princess Tiffah’ ndinga aina ya Mercedes Benz MSL Benz lenye thamani ya dola 100,000 (zaidi Sh. milioni 200).

Habari za uhakika kutoka ndani ya familia ya Diamond zilieleza kwamba, ishu hiyo ilijiri juzikati mara tu baada ya Zari ambapo baadhi ya ndugu wa mwanamama huyo walichanga na kumletea Tiffah gari hilo ili Zari alitumie katika mishemishe zake anapotoka na mwanaye Tiffah ikiwa ni pamoja na kumpeleka kliniki.

Kikisherehesha kwa kina stori hiyo, chanzo hicho kiliweka bayana kuwa ndugu wa Tiffah wameamua kumletea gari hilo ikiwa ni moja ya zawadi ambazo waliahidi kipindi akiwa majamzito, lakini pia wameamua kufanya hivyo kwa kuwa hawataki mtu achangie gari na Tiffah.
“Ni kweli ndugu wa Zari wameamua kumnunulia Tiffah gari aina ya Benz na tayari limewasili Bongo na Ijumaa iliyopita lilitumika kumpeleka Tiffah kliniki,” kilisema Chanzo hicho cha ndani.
GPL

Penny Agoma Kuulizwa Kuhusu Mtoto wa Diamond Platnumz na Zari ..Kisa Hichi Hapa

0
0
Yamekuwa hayo? Aliyewahi kuwa mwandani wa staa wa Bongo Fleva Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’, Penniel Mwingilwa `DVJ Penny’ amegoma kuulizwa chochote kuhusu kitendo cha zilipendwa wake huyo kupata mtoto wakati yeye alidaiwa kukataa kumzalia.
Akizungumza na Ijumaa Wikienda, wikiendi iliyopita, Penny alifunguka kwamba, haoni kama kuna sababu ya kumzungumzia Diamond na mtoto wake (Tiffah) kwani walishaachana zaidi ya miaka miwili sasa.

Jamani, huyo mtu kwa sasa hanihusu na sioni kama kuna sababu ya kumuongelea mtoto wake, anayepaswa kuulizwa mambo ya Diamond ni Zari, kwa hilo mnisamehe (no comments), nikiulizwa niulizwe mambo yangu tu,” alisema Penny.
GPL

Mpenzi Wangu Alikuwa Anafanya Sana Musterbation, Sasa Jogoo Hapandi, Nimsaidiaje?

0
0
Nilikutana nae chuo kwenye masomo ya degree ya pili ni mwanaume mwenye umri miaka 30 (mimi 24) ni kijana mtanashati mcha Mungu mwenye upendo na malengo ya maisha. Safari yetu ya mahusiano ilianza baada ya masomo yetu kuisha

Tulipoanza kukutana faragha ndipo nilipogundua kwamba ana tatizo la erectile dysfunction(jogoo hawiki) yani kama akiwika basi erection inakuwa very weak nikamuuliza nini tatizo hakunificha akanielezea tatizo lake kwamba alikuwa anafanya sana masturbation toka yupo primary mpaka amemaliza chuo for about 15 years and it has affected him psychologically. Naelewa jinsi gani being able to satisfy a partner is to a man na kama akishindwa inamuaffect kwa kiasi gani so i understood his struggle basi nilimuelewa na akaniambia ni tatizo linatibika ila nikamshauri asijekujaribu short cuts za madawa ya waganga wa kienyeji just bcz of the pressure ya kupona haraka

Nikaahidi kumpa muda na support alishughulikie tatizo lake (meaning abstaining from porn n masturbation) na alisema alivoona madhara yake with his previous gf's akaanza kulishughulikia kama 2 years ago kabla ya sisi kuanza uhusiano tatizo linakuja kwamba sasa yapata miezi 9 naona tatizo bado lipo,, I play my part as a partner kumfanya mawazo yake yote yawe kwangu yani anione mimi desirable n apate proper erection instead of kuvuta hisia za porn.

Na pia tatizo jingine ni kuwa ame loose confidence kiasi kwamba ana doubt mapenzi yangu kwake kwahiyo muda wote he questions my true feelings jambo hili hunikera sana japo nimeshamueleza ila bado haachi najaribu kumuelewa kwasababu yote hii ni a result of his ED problem.

Sasa wadau swali langu ni je hili tatizo huwa linatumia muda gani kupona yani mtu kuweza kurudia katika hali yake ya kawaida??na akiweza kurudia hali yake ya kawaida are the results permanent??

(This is serious question) thanks in advance

NAPE-Lowassa Amepewa Hiyo Nafasi ya Kugombea Urais Baada ya Kuinunua Kwa Viongozi wa Ukawa

0
0
Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM Nape Nnauye amesema Lowassa hapendwi na wafuasi wa vyama vya upinzani, isipokuwa alipewa nafasi hiyo baada ya kuinunua kwa viongozi wa Ukawa, ambao wana tamaa ya fedha.
"Kila mtu anajua kuwa huyu bwana ameinunua hii nafasi kwa viongozi wa Ukawa, ndiyo maana watu wenye akili zao, wameamua kujiweka pembeni wamewaachia wenyewe na mzigo wao usiobebeka, inashangaza kuwa sisi tunawafukuza mafisadi wao wanawapokea, sasa wakipewa nchi si itakuwa hatari zaidi. Hivi umeshawasikia tangu ajiunge nao wanazungumza kuhusu ufisadi? Wanaona aibu kwa sababu katika nchi hii, ukitaja fisadi na mafisadi huwezi kumweka kando. Unafikiri Watanzania ni wajinga kiasi kwamba hawaoni huu usanii??” alihoji Nape.

Source GPL

Nini maoni yako?

LOWASSA:Mkiendelea na Mchezo wa Kupiga Watu Mabomu Tukimaliza Uchaguzi Tutawapeleka The Hague Mkakipate cha Moto na Huko Hamtarudi

0
0

Mgombea urais kwa tiketi ya Chadema, Edward Lowassa amesema anawatakia kila la heri wanaobeza nguvu ya umma.

Kutokana na umati wa watu waliojitokeza jana kumlaki kuanzia Uwanja wa Ndege wa Mwanza alikowasili saa saba mchana, iliuchukua zaidi ya saa mbili msafara wake kuingia Viwanja vya Furahisha saa tisa alasiri, ambako ni takriban kilomita nane.

Katika hotuba yake iliyochukua dakika 14 kuanzia saa 11.53 hadi 12.07 jioni, Lowassa alisema anawasikitikia wanaobeza nguvu hiyo ya umma.

“Haya siyo mapenzi, haya ni mahaba. Wanaobeza nguvu hii ya umma nawatakia kila la heri,” alisema Lowassa huku akishangiliwa na umati huo.

Akizungumzia idadi hiyo ya wananchi, mke wa mgombea huyo, Regina Lowassa alisema haijawahi kutokea maeneo yote waliyotembelea Dar es Salaam, Mbeya na Arusha.

“Mwanza nimewapenda, nafikiri baba (Lowassa) akitoka hapa atalala usingizi mzuri mzito,” alisema Regina.

Lowassa aliwataka polisi kutoingilia mchakato wa uchaguzi na kutumiwa na CCM kupambana na wapinzani na kwamba, wakiendelea watakuwa wanajitafutia tiketi ya kupelekwa Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu (ICC), mjini The Hegue.

“Nimesikitishwa sana kuwa watu wamepigwa mabomu asubuhi. Mkiendelea na mchezo huu tukimaliza uchaguzi tutawapeleka The Hague mkakipate cha mtoto na huko hamtarudi tena,” alisema.

Polisi mkoani hapa jana walilazimika kutumia mabomu ya machozi, kuwatawanya wafuasi wa vyama vinavyounda Ukawa ambao walifurika Uwanja vya Ndege wa Mwanza kumpokea Lowassa.

Lowassa aliwasili akiwa ameambatana na mgombea mwenza, Juma Duni Haji, Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe na Mwenyekiti wa NCCR Mageuzi, James Mbatia, Kaimu Mwenyekiti wa CUF, Twaha Taslima na Mwenyekiti wa NLD, Dk Emmanuel Makaidi.

Mabomu ya machozi yalianza kurindima saa tano asubuhi, baada ya baadhi ya wafuasi wa Ukawa kutaka kuingia kwenye lango la uwanja wa ndege, huku wengine wakijaribu kuwatunishia misuli polisi kwa kuwatupia mawe.

Hekaheka za mapokezi ya Lowassa zilianza saa mbili asubuhi, baada ya maelfu ya wafuasi wa Ukawa wakiwa na mabango yenye ujumbe mbalimbali ikiwamo: “Oil chafu ni kiboko ya mchwa” kutanda kwenye barabara inayoelekea uwanja wa ndege.



Msafara wa Lowassa kutoka uwanja vya ndege uliongozwa na pikipiki ambazo zilikuwa zinapeperusha bendera za vyama vya CUF, Chadema ,NCCR Mageuzi na NLD, huku viongozi hao wakiwa kwenye magari ya wazi.

Lowassa alisema ziara yake hiyo inahusu kujitambulisha na asingependa kuwapa nafasi wapinzani wake kumtafsiri kuwa hajui sheria, lakini kero za Mwanza anazifahamu hivyo akaahidi kurejea na mikakati ya kuzitatua.

Mwenyekiti wa CCM Rais Jakaya Kikwete Atoa Tamko Baada ya Mafuriko ya Lowassa Kumfunika Vibaya Mgombea wa CC Magufuli

0
0
Mwenyekiti wa CCM Rais Jakaya Kikwete amesema uamuzi wa nani agombee urais kupitia chama hicho ulifanyika kwa pamoja kwa kufuata taratibu, hivyo anayetoka katika chama hicho kwa sasa ni hiari yake na mapenzi yake.

Aliyasema hayo jana wakati wa mazungumzo na wajumbe wa Baraza Kuu la Umoja wa Vijana wa CCM Dar es Salaam na kuongeza kuwa uamuzi huo ulifanyika kwa mujibu wa Katiba ya CCM na ulipigiwa kura ndani ya Halmashauri Kuu ya Taifa baada ya mjadala mrefu na uamuzi ulichukuliwa kwa pamoja. 6
Read more at http://websta.me/n/cloudsfmtz#6Q3vB75cS6Midxpu.99

Nchimbi Avunja Ukimya CCM........Sadifa Ampa Makavu Lowassa

0
0
Mmoja wa makada wa CCM aliyekuwa rafiki  wa  karibu na Edward Lowassa  wakati  wa  mchakato  wa  urais  ndani  ya  CCM, Dk Emmanuel  Nchimbi, ameibuka na kudai kuwa, hana kinyongo na yaliyotokea Dodoma huku akionesha kuwashangaa wanaoendelea kunung’unika, akisema watu wa aina hiyo hawakuwa pamoja na chama.

Aidha, Nchimbi, mmoja wa makada vijana waliokulia katika mfumo wa kisiasa ndani ya CCM alikoshika nyadhifa mbalimbali zikiwemo Mwenyekiti wa Taifa wa Umoja wa Vijana (UVCCM), Mkuu wa Wilaya, Mbunge na Waziri, amesema sasa si wakati wa kuendelea kuwa na makundi, bali kujenga umoja kwa lengo la kukipa chama ushindi.

Aliyasema hayo mwishoni mwa wiki wakati wa mkutano wa Baraza Kuu la UVCCM jijini Dar es Salaam.

Nchimbi ambaye tangu baada ya uteuzi wa mgombea wa urais wa CCM amekuwa kimya, ikiwa pamoja na kutojitokeza kuwania ubunge katika jimbo lake la Songea Mjini na hata kuhusishwa na mpango wa kukihama chama, amesisitiza hana kinyongo, bali anaunganisha nguvu zake na WanaCCM wengine kuhakikisha ushindi wa Dk John Magufuli, Waziri wa Ujenzi aliyepewa jukumu la kupeperusha bendera ya CCM katika urais.

Alisema ndani ya UVCCM, umoja huo umekubaliana kumaliza makundi na kwamba hivi sasa wapo kitu kimoja kwa ajili ya ushindi wa CCM.

Sadifa  Amvaa  Lowassa
Kwa upande wa Mwenyekiti wa Taifa wa UVCCM, Sadifa Juma Hamisi, ameendelea kutetea uamuzi wa CCM wa kutompitisha Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa kuwa mgombea urais kupitia chama hicho, akidai alipoteza sifa ya kuwa Rais tangu enzi za Baba wa Taifa, Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.

Akifungua Baraza Kuu la UVCCM, Dar es Salaam juzi, Sadifa alisema makada wanaohama chama na kujiunga na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), walipoteza sifa za uongozi tangu enzi za Mwalimu Nyerere.

Sadifa alisema Lowassa ambaye ni mgombea urais wa Chadema, alipoteza sifa ya kuwa rais tangu enzi za Mwalimu Nyerere na kwamba dhamira yake hiyo haitafanikiwa milele.

Aliongeza kuwa, umoja huo haushtushwi na wimbi la wanasiasa maslahi wanaohama chama. Sadifa alisema vijana wa CCM wamejipanga kuueleza umma udhaifu wa wanasiasa hao.

“Hatutatishwa na watu wanaotumia fedha zao kusaka madaraka. Tumeamua kuvunja makundi yetu na tutaeleza uchafu wote…,” alisema Sadifa ambaye inaaminika alikuwa akimuunga mkono Lowassa kuwania urais ndani ya CCM.

Alisema umoja huo utashirikiana na chama, kuhakikisha Mgombea Urais wa CCM, Dk John Magufuli anapata ushindi mkubwa.

Alisema mwaka huu, umoja huo utawadhihirishia wote wanaodhani chama ni uso wa mtu wakisahau kuwa ni taasisi kwa kukipa ushindi wa kishindo kwenye nafasi zote za uongozi.

Alisema CCM imepata mgombea makini na kwamba hana dosari wala hakuna sababu ya kutafuta sabuni ya kumsafisha.

Sadifa alisema Rais Jakaya Kikwete ambaye ni Mwenyekiti wa Taifa wa CCM aliendesha vikao vya Chama kwa umahiri mkubwa.

NEC Yawatoa Hofu Watanzania......Yasema Hakuna Wizi wala Uchakachuaji wa Kura Mwaka huu

0
0
Tume ya Taifa ya Uchaguzi (Nec), imesema kuwa imeunda timu ya ushindi ya kuhakikisha matokeo ya uchaguzi mkuu wa Oktoba, mwaka huu yanatangazwa kwa wakati, ya kweli na haki kwa pande zote.

Akizungumza na gazeti  la Nipashe jana lililotaka kujua mipango ya Tume ili kuondoa malalamiko ya wananchi, vyama vya siasa, wagombea na wadau kuhusu kucheleweshwa matokeo na kuzua hofu ya uchakachuaji, Mkurugenzi wa Nec, Ramadhani Kailima, alisema timu hiyo itakuwa na wajibu mkubwa na hakuna kulala hadi matokeo yote yawe wazi.

“Tutakuwa na timu ya ushindi kutangaza matokeo yote mapema, hakuna kulala hadi tutoe matokeo kwa wakati, ya haki na kweli na yanayoaminika kwa wapigakura,” alisema.

Alisema malalamiko ya kupendelewa kwa chama chochote hayana msingi wowote kwa kuwa Tume haina chama na haitapendelea chama zaidi ya kuweka wazi matokeo yote itakayoyapata kwa wakati kwa kuwa watakuwa wanafanya kazi kisasa zaidi.

Alipoulizwa juu ya uzoefu wa Tume miaka ya nyuma kuhusiana na kuchelewesha matokeo hata ya maeneo ya mijini kunakofikika kirahisi, Kailima alisema kama kutakuwa na ucheleweshaji sababu zitawekwa wazi na wapigakura watatangaziwa bila kificho.

“Ya 2010, yasizungumziwe sasa kwa kuwa tunafanya kazi kisasa kuhakikisha matokeo yanakuwa wazi na kila hatua wananchi watatangaziwa,” alisema na kuongeza:

“Tunawaomba wananchi mara baada ya kupiga kura wakae mbali na ikiwezekana waende nyumbani kwa kuwa kila kituo cha kupigia kura kutakuwa na mawakala kama kuna tatizo lolote la kufanya matokeo yasitangazwe kwa wakati, watajulishwa mapema.”

Kailima alisema Nec iko huru na inatekeleza majukumu yake kwa mujibu wa sheria na kanuni na haiingiliwi kokote kwani katika kugawa majimbo, Chama Cha Mapinduzi (CCM) ambacho kinadaiwa kubebwa na Tume, kimelalamika na kama wangekuwa wanapendelewa, ni wazi kuwa malalamiko yao yangesikilizwa, lakini Tume imeamua kufanya kazi zake kwa uhuru.

“Uhuru wetu siyo jina, bali ni kutekeleza majukumu ya kikatiba na sheria bila kuingiliwa, kiwe chama au mtu hawaruhusiwi kutangaza matokeo ya uchaguzi, bali msimamizi wa uchaguzi wa kata atatangaza ya kata, ubunge yatatangazwa na Mkurugenzi wa Manispaa, mji au halmashauri na Tume itatangaza matokeo ya urais,” alisema.

Alisema watumishi wote wa Tume kabla ya kufanya kazi huapishwa kujiondoa au kukana itikadi ya chama chake na kuanza kutekeleza majukumu yake ili kusiwe na upendeleo kutokana na itikadi.

Alipoulizwa kuhusu matukio kadhaa yaliyotokea katika uchanguzi mkuu wa mwaka 2010 ikiwamo wasimamizi wa baadhi ya majimbo mfano, Shinyanga mjini kutoroka baada ya kutangaza matokeo yenye utata yaliyompa ushindi mgombea wa CCM na kuzua vurugu, Kailima alisema:

“Tuko 2015, tumejipanga kikamilifu, ndiyo maana tuna timu ya ushindi kuhakikisha hakuna ucheleweshwaji wa matokeo. Itakuwa Tume tofauti na ya miaka mingine.”

Msamaha Umetolewa Kwa Shindano la Miss Tanzania, Maelezo Kuhusu Msamaha Huo Nimekuwekea Hapa

0
0
December 2014 baada ya shindano la Miss Tanzania kukamilika liliingia kwenye headlines baada ya Baraza la sanaa la Taifa kutangaza kulifungia shindano hilo kwa miaka miwili baada ya kujiridhisha kwamba limekiuka taratibu lakini leo August 17 2015 Miss Tanzania imeingia tena kwenye headlines baada ya Basata kutoa msamaha.

Hii hapa chini ndio taarifa iliyotolewa na BASATA.

Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) limelifungulia shindano la urembo la Miss Tanzania baada ya mwandaaji wake Kampuni ya LINO International Agency Limited kufuata taratibu, kuomba radhi na kuyafanyia kazi baadhi ya mapungufu yaliyojitokeza na kutekeleza masharti aliyopewa.

Itakumbukwa kuwa mnano tarehe 22/12/2014 BASATA liliwaandikia barua LINO International Agency Limited ya kulisimamisha shindano la Miss Tanzania kwa miaka miwili (Mwaka 2015 na 2016) na kuwaagiza kujipanga upya na kurekebisha kasoro ambazo zimekuwa zikijitokeza mara kwa mara.

Mapungufu yaliyobainishwa ni pamoja na; mosi, kutokufuata Sheria, Kanuni na Taratibu za uendeshaji matukio ya Sanaa nchini, pili kutokuwasilisha nyaraka mbalimbali za shindano lake hususan mikataba ya washiriki. Tatu kutumia mawakala wasiosajiliwa na kupewa vibali vya BASATA.

Miongoni mjwa mapungufu ambayo Kampuni ya LINO imeyafanyia kazi ni kuanza mchakato wa usajili wa mawakala – BASATA na kufanyia marekebisho kanuni na taratibu za uendeshaji wa Mashindano ya Urembo ya Miss Tanzania. Aidha, LINO imewasilisha muundo wa kamati ya uendeshaji wa shindano yenye muelekeo wa kuzingatia jinsia.

Katika kuboresha na kurudisha hadhi ya shindano la Miss Tanzania, LINO International Agency Limited imepewa kibali cha muda kisichozidi miezi minne (4) kwa ajili ya maandalizi ya awali ikiwemo kukamilisha usajili wa mawakala katika ngazi zote husika.

BASATA linapenda kuwafahamisha wadau wote wa Sanaa hususan wale wa shindano la urembo la Miss Tanzania kwamba Kampuni ya LINO imetekeleza maagizo ya msingi iliyopewa kama masharti ya kufunguliwa. Na kwamba baada ya kufanyia kazi changamoto zilizokuwa zimejitokeza BASATA limeyafungulia mashindano ya Miss Tanzania kwa masharti ya kukamilisha changamoto zilizobakia.

Ni matarajio ya BASATA kwamba kampuni ya LINO itazingatia taratibu zote za uendeshaji wa matukio ya Sanaa nchini na kwamba haitarudia tena makosa yatakayopelekea kuliweka shindano hili katika hali ya kushuka hadhi na kuzua sintofahamu katika jamii.

Sanaa ni kazi, tuipende na kuithamini

Godfrey Mngereza

KATIBU MTENDAJI

Maajabu Niliyoyaona Mwanza Kwenye Mkutano wa LOWASSA Hayajapata Kutokea.....Watu Walipigwa Mabomu bila Kukoma, Wengine Walizimia

0
0

Haijawahi kutokea. Siyo mabomu ya machozi wala polisi wenye silaha walioweza kuzuia halaiki ya wananchi kufika kwenye viwanja vya Furahisha kuhudhuria mkutano wa mgombea urais wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Edward Lowassa.

Hii ni kwa sababu umati uliojitokeza kuanzia Uwanja wa Ndege wa Mwanza ambako polisi walilazimika kupiga mabomu yasiyohesabika kuwatawanya wananchi ambao walifunga barabara inayoingia uwanjani hapo, kutozaa matunda.

Msafara wa Lowassa anayeungwa na mkono na vyama vinavyounda Ukawa vya Chadema, NCCR-Mageuzi, NLD na Cuf, ulilisimamisha Jiji la Mwanza kwa takriban saa tatu kutokana na msafara kutembea kilomita sifuri kwa saa.

Pamoja na polisi kupiga mabomu mita chache kutoka uwanjani hapo, Lowassa alipotoka tu uwanjani, umati mkubwa wa wafuasi wake na wa Ukawa, waliokuwa wamejificha waliibuka wakiwa na chupa za maji; mbele ya askari waliokuwa kwenye magari wakiwa na silaha za moto na mabomu ya machozi.
Kilichochangia msafara kutembea mwendo mdogo ni baadhi yao kumwaga maji barabarani kama ishara ya kupiga deki ili Lowassa apite huku wengine waliokuwa na fagio za chelewa, wakifagia.

Wananchi wengine walikuwa na mabango yenye ujumbe mbalimbali ikiwamo ‘Richmond ilikuwa ni maagizo ya juu’; ‘pombe mwisho kaunta, Ikulu ni Lowassa’‘kufuli mwisho mlangoni’; na ‘Tanzania bila Lowassa haiwezekani.’

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Charles Mkumbo, akizungumza na waandishi wa habari uwanjani hapo, alisema polisi hawajawazuia wananchi kushiriki mkutano bali wamepiga mabomu kuzuia wale ambao wamekwenda uwanja wa ndege ambako siyo eneo la mkutano.

“Hatuna nia ya kuzuia mkutano, wananchi tumewaambia kwamba waende Furahisha kwa sababu wakija huku watasababisha usumbufu kwa watumiaji wengine wa uwanja,” alisema.

Ikiwa uwanjani hapo, Mpekuzi ilisikia milipuko ya mabomu zaidi ya 30 yaliyopigwa kwa takriban saa moja kabla msafara wa Lowassa haujaondoka kuelekea Furahisha.

Tofauti na mikoa mingine, maandamano ya Mwanza hayakuwa na pikipiki, bajaj wala magari zaidi ya yale ya viongozi wa Ukawa taifa na wabunge wa Chadema kwenye mikoa ya Kanda ya Ziwa, bali ni wananchi wasiohesabika ambao walilazimisha mkutano kutembea kilomita sifuri kwa saa.

Idadi ya watu waliojitokeza kwenye uwanja wa Furahisha, nusura usababishe mkutano kuahirishwa baada ya watu kuanza kuzimia na kupoteza fahamu, jambo ambalo lilisababisha kikosi cha Msalaba Mwekundu uwanjani kuzidiwa nguvu.

Kutokana na hali hiyo,  Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe, aliwaambia wananchi warudi nyuma na wengine wakae chini ili kutoa nafasi kwa viongozi, waandishi na wapigapicha wafanya kazi yao.

Hata hivyo, tangazo hilo halikufua dafu kwani baadhi ya wananchi waliokuwa mbele, walikaa chini lakini halaiki hiyo iliendelea kusababisha usumbufu mkubwa kutokana na idadi ya watu walioendelea kupoteza fahamu.

Baada ya kuanza kusukumana, wananchi wengine walianza kulia na kusema kuwa walilala uwanjani kumsubiri Lowassa na viongozi wa Ukawa, lakini wanasikitika kusukumwa na kukanyagwa.
By Mpekuzi blog

Picha ya Mtoto wa Diamond Akiwa Amefungwa Kitu Cheusi Mkononi yazua Mabishano Instagram...Wengine Wadai ni Hirizi

0
0

Kwenye Page ya Instagram @udaku_Special Tulipost picha hiyo na kuuliza hili jambo ?

Eti jamani hicho hapo mkononi kwa mtoto Tiffah ni nini?
Kuna mabishano eti wengine wanadai ni hirizi? Mie nimebisha aisee kwa udhungu alio nao mama ake sidhani kama anaamini hayo mambo!! Embu nijuze basi...

Majibu ya Wadau yalikuwa Haya:

mossyfimbo
Hiyo sio hirizi ni kitu kina itwa MVUJE unaufunga kwenye kitambaa cheusi kisha wamfunga mtoto mkononi ni imani tu kuwa mtoto asisumbuliwe na mapepo machafu kwa kuwa unanuka vibaya unaharufu mbaya sana kwa hiyo pepo chafu au baya haliwezi kumkaribia mtoto ni imani za miaka nenda rudi sasa kaka bibi kamfunga Dai au Zari hawezi sema chochote lakini ukifunga kwenye kitambaa ile harufu huwezi isikia kabisa. Hata mimi nilisikia kwa wazazi wangu nami na copy kuandika hapa labda kuna mwingine anajua kwa maana tofauti.

mbucheche
 mwambie mlinzi ni mungu tu na si vya kutengenezwa na wanadam yeye ndio mwenye nguvu zote na kila goti linapigwa mbele zake .

yohanampenzume
mwenyewe iliiona nkajiuliza kumbe bado watu wako kwenye digital huku wakiishi kianalogia??? @udaku_special km wanaamin uchawi na wa wana ela si waajiri waganga wa sumbawanga na tanga wakae kumlinda mtoto?? NI WAZO TU MAZEE MXJENGE CHUKI

mbucheche
mbona wengine hawavalishwi na wamekua jaman tuachage haya mambo ya kumsubstute mungu na kizizi huezi ukasema unamtegemea mungu huku unavaa vitu vingine sasa hapo imani si inakua hapo kwenye icho kidude badala ya mungu.tunahitaji tuwe wa kwel kama tunajiita tunamwamin mungu tusimfananishe na kitu.kama unamwamini amini kama unaamin kizizi basi kiamini.

mabuttocks
Jamani sio hirizi, watoto wengi wanasomewa sura tul yaasin afu anafungiwa mkononi iwe ina mlinda. Wanaosema hirizi ndo wenye imani potovu

mbucheche
 hao wanavitoa wapi mnajua au mnavalisha watoto tu bila kujua kwa iyo icho ndo kinamlinda badala ya mungu ambae tunasema tunamwamini kumbe tuna yetu mengine.watoto wanakua bila kuvalishwa icho kidude mbona?


mbucheche
 waambie yani badala ya kuwapeleka watoto wakaombewe kwenye nyumba za ibada mnarelax na uo upupu kwel tunapotea kwa kukosa maarifa hee.

datimaa
Mungu pekee ndie anaetulinda hvo vitu vingine ni ziada@mbucheche


saidastambul
 Wasenge wte mnaojifanya hamjui mvuje halafu watu hawa ni wanafiki ajabu eti ushirikina?umejua je?kama ni shirikina?kama ww sio kiongozi mungu awauwe nyote wanafikii

 nasriyathabit_alkhanan
ata watoto wa mashekhe wanavaa mivuje
Watu wengne wanataka 2 umbea wkt hiko kwa tz makabila meng umfunga mtoto akiwa mchanga nais ata wao wenyewe walfungwa now wanajfanya wamekua wanashangaa fyuu

amonizabroni
 Maana kila mnachokiona mnadis ..kwetu kigoma mkitaka kujuwa maana yake njooni kigoma

Je wewe Una Maoni Gani?

Jokate Amtambulisha Ali Kiba Apigwa Chini Kwao

0
0
Imevuja! Gumzo la ndoa ya staa mwenye jina kubwa Bongo, Jokate Mwegelo ‘Kidoti’ na Mbongo-Fleva Ali Saleh Kiba ‘King Kiba’ inadaiwa kupigwa zengwe kama ilivyowahi kutokea kwa Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ kufuatia madai ya mwanadada huyo kumtambulisha jamaa huyo kwao kisha kukataliwa.


MINONG’ONO

 Habari kutoka chanzo cha kuaminika ambacho ni mtu wa karibu wa wawili hao, tukio hilo lilijiri hivi karibuni ambapo wawili hao walihudhuria kwenye harusi ya dada wa Jokate hivyo kuibua minong’ono kwamba huenda harusi inayofuata itakuwa yao.

 Chanzo hicho kiliendelea kudai kwamba, habari mbaya ni kuwa baada ya Jokate kumtambulisha Kiba kwa ndugu, jamaa na marafiki baadaye kumpeleka kwao, wazazi wa mwanadada huyo walikuja juu wakidai jambo hilo haliwezekani huku sababu nne zikianikwa.

KIGEZO CHA DINI

Madai yalishushwa kuwa, sababu ya kwanza ni kwamba, familia ya Jokate hasa wazazi wake ni watu walioshika sana Dini ya Kikristo (Kanisa Katoliki) huku Kiba akiwa ni Muislam kama ilivyokuwa kwa Diamond aliyeshindwa kumuoa Jokate kwa kigezo hichohicho.

NDOA ZA MASTAA NI TATIZO?
Ilidaiwa kuwa, sababu ya pili iliyotolewa na wazazi hao ni kwamba, hawataki binti yao kuolewa na msanii mwenzake kwa kuwa wanajua ndoa za mastaa zinavyokuwa na ‘drama’.

KIGEZO CHA KABILA

Kigezo kingine kilichotajwa ni kabila ambapo wazazi hao wanataka Jokate aolewe na mtu wa kabila lake la Wangoni tofauti na Kiba ambaye ni Muha.

KIGEZO CHA BONGO FLEVA
Chanzo kilikwenda mbali zaidi na kudai kuwa, wazazi hao wanaamini kwamba baadhi ya wasanii wa Bongo Fleva ni wahuni hivyo kuwawia vigumu kukubali binti yao kuolewa na Mbongo-Fleva.Pia habari za ndani zilidai kwamba, Jokate na Kiba walikuwa kwenye harakati za kuoana kabla ya mwaka huu kumalizika ila zengwe limekuwa kubwa upande wa familia hasa kwenye suala la dini ambapo kila mmoja amekuwa akitaka mwanaye abadili dini.

KAMA DIAMOND

“Unajua kilichompata Kiba ni kama kile kilichomfika Diamond kipindi kile alipotaka kumuoa Jokate.
“Ilikuwa ni ishu hiyohiyo ya dini maana wazazi wa Jokate walikuwa wakimwambia kila siku kama kweli anampenda mtoto wao basi abadili dini lakini Diamond hakuweza kufanya hivyo na kujikuta wakishindwa kufikia lengo la kufunga ndoa,” kilitambaa chanzo hicho.

KIBA KAMA KAWA

Kama kawaida yake, Kiba alipoulizwa juu ya ishu hiyo alikanusha vikali akidai kwamba hajawahi kuwa na mipango hiyo na mrembo huyo.“Ulishawahi kunisikia nikizungumzia ishu hiyo? Siyo kweli bwana…hakuna kitu kama hicho,” alisema Kiba akionekana ‘kumaindi’ kwa kuulizwa juu ya jambo hilo.Kwa upande wake Jokate hakupatikana hewani na hata alipotumiwa ujumbe mfupi hakujibu hivyo jitihada za kumpata zinaendelea.

TUJIKUMBUSHE

Kwa muda mrefu, Jokate na Kiba wamekuwa wakiripotiwa kuwa ni wapenzi lakini Kiba amekuwa mstari wa mbele kukanusha huku Jokate akikiri kuwa jamaa huyo ni mtu wake.

Chanzo: GPL

Shamsa Ford Na Nay wa Mitego Wakiri Uhusiano Wao wa Kimapenzi

0
0
Msanii wa filamu nchini, Shamsa Ford amekiri kuwahi kutoka kimapenzi na Nay wa Mitego na baadaye wakaachana.

Shamsha na Nay wa Mitego walikuwa wakizungumza kwa pamoja ndani ya Global TV hivi karibuni. “Ukweli ni kwamba finally nilikuwa na mahusiano ya kimapenzi na Emanuel (Nay) lakini tumeachana,” alisema Shamsa.

Kwa upande wake Nay alisema uhusiano ulikuja baada ya kuwa marafiki.

“Tulikuwa washkaji, mahusiano yetu yalianza hivyo,” alisema rapper huyo.

“Tulienda Masaki baada ya kukaa mida fulani wakati wa kuondoka kusema kweli, kidogo nikaanza kuvutiwa na Shamsa Ford, katika kuagana nikaomba mimi nikamwambia mimi mwenzako matatizo yangu ni haya.

Bahati nzuri yeye pia hakuwa mzito, nahisi na yeye alikuwa amesoma kitu kwangu labda ambacho kilimvutia. Tuli-kiss na for the first time tulikuwa tumeonana siku hiyo na kwamba kila mtu alikuwa tayari kwa lolote litakalotokea. So tukaanza hivyo, kilichotufanya tuendelee kuwa connected ni lile kiss la siku ya kwanza,” aliongeza Nay.

Chanzo: Bongo5

Jamani Zari Hajawahi Kuolewa – Diamond Platnumz

0
0
Diamond Platnumz amesema Zari hajawahi kuolewa na kwamba hadi sasa hajapokea barua yoyote kutoka mahakamani ikimtaka kuchukua vipimo vya DNA vya mtoto wake, Tiffah.

Kwa mujibu wa Diamond, barua iliyowekwa kwenye akaunti ya King Lawrenc ni moja ya njia ya swahiba hiyo wa ex wa Zari, Ivan ya kujipatia umaarufu.

“Sijapokea barua yoyote,” Diamond ameiambia 255 ya XXL kupitia Clouds FM leo.

“Unajua lazima tujue kila mtu anatumia mitandao kwa njia zake. Wengine wanatumia kutafutia umaarufu kama hivyo which is not bad but kupata umaarufu ni kazi sio, mtu anatafuta njia yoyote kutafuta umaarufu na watu wakamsikiliza na kupata pongezi kwa sababu amekaa amebuni kitu mpaka watu wakamsikiliza,” amesema Diamond.

“Zari hajawahi kuolewa kwanza, ni story tu hizo, lakini hajawahi kuolewa, ukimuuliza mwenyewe anasema hajawahi kuolewa kabisa,” amesisitiza staa huyo.

“Unapokuwa na mahusiano na mtu huwezi kufuatilia vitu vyake vya nyuma. Tumeanza maisha yangu mimi na yeye sidhani kama umeshaona post yangu yoyote ya kumzungumzia vibaya ndio maana nikiona vitu ambavyo navisikia naona ni uongo, mimi sifuatilii maisha ya mtu.”

Utani Huu: Mpambe wa Ex wa Zari Anataka DNA ya mtoto wa Diamond, Anadai yeye ni Baba, Juzi Alidai Ivan Ndio Baba!

0
0
Guys kuna mambo mengi sana feki yanaendelea kwenye mitandao ya kijamii. Tena zaidi ni kuwa mengi yanakuja na picha zinazoashiria ukweli lakini katika maisha ya chuki na visasi, kila kitu kinawezekana.

Bahati mbaya tunaishi kwenye dunia ambayo watu huamini haraka mambo hasi ambayo kwa kawaida husambaa haraka zaidi kuliko yale chanya. Na kwakuwa mitandao ya kijamii katika miaka ya hivi karibuni imekuwa chanzo kikubwa cha habari, blogs zimekuwa zikiwahiana kuandika habari na wakati mwingine bila kuzitafakari na kuzichuja vyema kupata uhalali wake.

Habari ya mpambe wa ex wa Zari, King Lawrenc, imetawala magazeti na blogs nyingi za Afrika Mashariki leo.


Lawrenc alipost kwenye akaunti ya Instagram kile kinachoonekana kuwa ni barua ya kutaka kufanyika vipimo vya DNA ili kujulikana ukweli wa nani ni baba wa Latiffah, ambaye ni binti wa Diamond Platnumz.

Lawrenc ametumia kampuni maarufu ya wanasheria ya nchini Uganda iitwayo WEB Advocates & Solicitors kumtaka Zari achukue vipimo vya DNA vya Tiffah katika nchi tatu tofauti ili kubaini nani ni baba wa mtoto huyu!

The funny part of this story is; Katika barua hii Lawrenc anadai kuwa yeye ndio baba wa mtoto huyu wakati katika post mbili zilizopita amekuwa akipost vijembe kuwa Tiffah ni mtoto wa Ivan, ex wa Zari. Ivan na Lawrenc ni marafiki!

Katika post ya kwanza, King aliweka picha ya Ivan na mtoto mchanga na kuandika, “No DNA Needed. The best revenge has shown itself after 9months.” Katika picha nyingine ambayo anaonekana akifurahia Cigar na Ivan, jamaa aliandika, “Chilling with @princess_tiffah’s father.”

Habari ya kuwa Ivan ndio baba wa Tiffah imebadilika, na sasa yeye ndiye anayelalamika kuwa ‘amenyimwa haki ya kumuona mtoto’ ambaye anaamini kuwa ni wake!

King Lawrenc ni mtu anayejulikana kwa njaa ya umaarufu na yupo radhi kufanya lolote ili aupate hata ikiwa ni kusema kuwa amewahi kulala na mke wa zamani wa rafiki yake, Ivan! Kinachowashangaza zaidi watu wengi ni kuwa Ivan anaruhusu yote haya.

Ivan yuko sawa kumuona mpambe wake akitangaza hadharani kuwa naye amewahi kutembea na Zari! Urafiki gani huu? Uhusiano wa Ivan na Lawrenc unatia mashaka sana!

Inavyoonekana Ivan na Lawrenc wamedhamiria kuhakikisha kuwa Zari na Diamond hawaipati ile furaha ya kupata mtoto. Hata hivyo hakuna chochote kati ya haya yanayoendelea kinachoonesha kuwaumiza Zari na Diamond.


Hatujui kinachoendelea ‘behind closed doors’ lakini picha za kwenye Instagram zinaonesha kuwa familia ipo katika kilele cha furaha. Diamond anaonekana kuwa baba anayejivunia kwa binti yake Tiffah.

Mungu akiepushe kichanga hiki na drama za watu wasiokuwa na mshipa wa aibu! Ama kweli umaarufu ni mzigo wa miiba!

Chat ya Instagram kati ya Diamond na Wema ni ‘Feki’ – Meneja

0
0
Meneja wa Diamond Platnumz, Sallam Sharaff amedai kuwa screen shots ya kile kinachoonekana kuwa ni mazungumzo kati ya Wema na Diamond kupitia DM za Instagram ni feki.

Katika mazungumzo hayo, Wema anamueleza Diamond kuwa apuuzie kile mashabiki wake wanachokisema kuhusiana na Zari na mtoto wao Tiffah na kwamba bado anampenda staa huyo wa ‘Nana.’

Diamond naye anaonekana kupagawa na ujumbe huo na kumuomba waonane.

Hata hivyo Sallam Ambae ni Meneja wa Diamond kupitia Twitter amepuuzia screenshot hiyo kwa kudai kuwa ni feki.

Jerry Muro Katoa Sababu za Kushindwa Katika Kura za Maoni ya Ubunge CCM

0
0
Jina la Jerry Muro sio geni masikioni mwa walio wengi kwani aliwahi kufanya kazi ya uandishi wa habari za uchunguzi kwa muda mrefu na zilizofanya jina lake kukua na watu kumtambua, Jerry ambaye kwa sasa ni mkuu wa idara ya habari ya klabu ya Dar Es Salaam Young African.

Mwaka 2015 aliamua kuingia rasmi katika siasa kwa kuanza harakati za kutaka kulirudisha jimbo la Kawe kwa chama tawala, Jerry alikuwa ni miongoni mwa makada 21 wa CCM waliojitokeza kuomba ridhaa ya kugombea ubunge wa jimbo la Kawe kupitia kwa chama cha mapinduzi (CCM).



Kwa bahati mbaya kura hazikutosha kumuwezesha Jerry Muro kupata ridhaa hiyo ya kupata nafasi ya kugombea ubunge wa Kawe kupitia chama cha mapinduzi, ila ameeleza sababu za yeye kukosa nafasi hiyo na nini kilipelekea yeye kushindwa katika kura za maoni, hii ni exclusive interview aliofanya na millardayo.com Jerry Muro ana haya.


Kweli nilikuwa mgombea wa jimbo la Kawe kupitia tiketi ya chama cha mapinduzi CCM nilikuwa miongoni mwa wagombea 21, tukiwa katika mchakato nilipata changamoto mbili ya kufiwa na baba yangu na kuvunjiwa nazi na mayai lakini kubwa ni kufiwa  na baba yangu mzee Muro alifariki tarehe 31 wakati sisi tunaelekea ukingoni wa kuitimisha kampeni na alivyofariki mzee wangu nilisitisha kila kitu

Hadi sasa Halima Mdee wa chama cha demokrasia na maendeleo CHADEMA ndiye mbunge rasmi wa jimbo hilo hadi pale Oktoba 25 uchaguzi mkuu utakapofanyika wa kuchagua wabunge, madiwani na Rais, Halima Mdee alishinda katika uchaguzi mkuu mwaka 2010 na kufanya awe mbunge wa jimbo hilo.

Haya Ndio Majibu ya Diamond Platnumz Kuhusu ishu ya Mtoto Kupimwa DNA…

0
0
Kumekuwa na stori ambayo imechukua sana headlines kuanzia mitandaoni mpaka kwenye Magazeti inayomhusu Diamond, Zari na mtoto wao.

Diamond amepatikana na kutolea majibu ishu hiyo, barua ya kudai mtoto wake akapimwe DNA bado haijamfikia na kama ni ishu ya Kisheria inayohusu Mahakama amesema ingepitia kwa Wakili au Mwanasheria na sio kupitia Mitandaoni.

Kingine amesema kwamba Zari hajawahi kuolewa na wao wameamua kuishi maisha yao na hawezi kufuatilia maisha ya mtu wala wao kufuatilia maisha ya watu.


Viewing all 104417 articles
Browse latest View live




Latest Images