Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104432 articles
Browse latest View live

Picha: Jokate Habanduki kwa Kiba, Amfuata Kenya, Ashuhudia Wakirekodi na Sauti Sol

0
0
Jokate Mwegelo hatoki begani mwa mahabuba wake, Alikiba.
11910136_147181532285484_807925537_n
Wawili hao wapo jijini Nairobi, ambapo Kiba yupo kurekodi kipindi cha Coke Studio na Jokate ameamua kuungana naye kumsaidia kumpunguzia baridi la jiji hilo ambalo kipindi hiki linadaiwa kuwa katika kilele chake.
Jokate ameshare picha kadhaa kwenye Instagram zikimuonesha akiwa na hitmaker huyo wa Mwana na pia kumshuhudia mwandani wake huyo akirekodi wimbo anaofanya na kundi Kenya, Sauti Sol.
11925835_863410010403993_1708931298_n
Hata hivyo huenda Jokate akawa ameenda pia kufanya kazi zake binafsi kwakuwa katika picha moja anaonekana akiwa na mtangazaji mrembo wa TV wa nchini humo, Sarah Hassan.
11356856_1476774022622816_64077804_n

Zari Asema Wataionesha Sura ya Tiffah Baada ya Siku…

0
0
Shauku kubwa ambayo mashabiki wa Diamond Platnumz na Zari the Boss Lady wako nayo kwa sasa ni kuiona sura ya mtoto wao wa kike Latiffah Naseeb a.k.a Princess Tiffah.

Hii ni kutokana na maneno mengi ambayo yanaendelea hivi sasa kwenye mitandao ya kijamii, wengi wanahamu ya kujua mtoto anafanana na nani kati ya baba na mama yake.

Picha zote za Tiffah zilizowekwa kwenye mitandao ya kijamii zinamuonesha mikono, miguu, mdomo lakini amekuwa haoneshwi sura yake.

Shabiki mmoja alimuuliza swali Zari kupitia ukurasa wake, ni lini wana mpango wa kuionesha sura ya Tiffah, na jibu la Zari lilikuwa “Baada ya siku 40”.

Hadi sasa ukurasa wa Instagram wa Princess Tiffah una followers 87,650.

KIMENUKA..Wana CCM 704 Toka Jimbo Analogombea Nape Ubunge Wahamia CHADEMA

0
0
Aliyekuwa mgombea wa kura za maoni kupitia chama cha mapinduzi jimbo la mtama SELEMANI METHEW amekihama chama hicho na kuondoka na wana CCM wapatao 704 na kuhamia chama cha demokrasia na maendeleo CHADEMA kwa kile anachodai hakutendewa haki katika mchakato mzima wa kura za maoni.

METHEW amesema kuondoka ndani ya CCM kumetokana na maamuzi ya wananchi ambao wameona haiwezekani na haitawezekana kiongozi wanayemuitaji kufanyiwa hila na mizengwe,kudhulumiwa haki yake ya msingi ya kuwaongoza wananchi wa jimbo la mtama.

Amesema jimbo la mtama halihitaji usanii bali linaitaji mgombea shupavu atakayeweza kupambana na mgombea wa CCM Nape Nnauye huku akisisitiza uwezo huo anao.

Mkutano huo umeudhuriwa na wanawake wengi ambao kwa sehemu kubwa ndiyo waliorudisha kadi za CCM.

Mkutano huo ulipambwa na vimbwanga mbalimbali likiwemo tambiko rasmi lililotumika kumzindika mgombea huyo ikiwa ni pamoja na kumpa nguvu na kumkinga na majanga ili aweze kufanikisha kampeni na kuibuka na ushindi.

Kutoka Diamond: Mapokezi ya Magufuli baada ya kurejesha fomu NEC

0
0
Kikwete: CCM haibahatishi, ni chama kikubwa kinawajua watu wake vizuri, sasa nataka nimlete ndugu Magufuli. Anaimbisha wimbo wa kumkaribisha Magufuli. Watu wajue leo CCM ndio imeanza, kama walikuwa wanchukua picha na kuunganisha kwenye computer, sasa zinakuja picha za kweli. John Magufuli ndio Rais na Samia ndio makamu


Magufuli: CCM oyeee, Ali nselema...

Sikutegemea kama patakua na wananchi wakereketwa ndani ya mioyo yao na wenye nyuso za furaha na wamependeza kweli kuhudhuria muda huu. Nimeomba kukutana na wazee wa Dar es Salaam kwa niaba ya wazee wa Tanzania, nafahamu ukitaka kupata busara, utapata kwa wazee. Uzuri leo wazee wamesindikizwa na vijana, ninawashukuru sana. Kabla sijaendelea niwashukuru wazee na wananchi wa Dar kwa kunikaribisha, niliingia mara ya kwanza 1978 wakati naenda kujiunga kidato cha tano, nilikaa siku mbili kisha nikaelekea Iringa. Nilipokuja tena kwa masomo ya chuo kikuu sijawahi kuulizwa dini wala kabila langu. Ninawashukuru sana wana-Dar es Salaam na watanzania.

Ninyi wazee wa Dar mna historia kubwa katika taifa hili, baba wa taifa wakati akiwa kwenye harakati za kudai uhuru alifika Dar es Salaam na akakutaa na wazee, mkamuombea dua na kumbariki na hatimae tukapata uhuru bila kumwaga damu, wakati wa Idd Amin, Nyerere alikutana tena na wazee wa Dar es Salaam, akazungumza nao na mkampa uwezo wa kwenda kushina na yeye akatamka nia tunayo, uwezo tunao. Idd Amin akakimbilia huko alipokimbilia.

Leo wazee wangu nami nimewaita ili nije nipate busara zenu na dua zenu kwa sababu natambua nikizungumza na wazee wa Dar es Salaam mambo yangu yatakua safi kabisa. Mara baada ya kuteuliwa na kupata kura nyingi kabisa na baada ya kumpata Mh Samia kuteuliwa nafasi ya makamu urais kwa mara ya kwanza. Ninachowaomba watanzania na Dar kwa ujumla tuwe wamoja, kura zimeshamalizika, sasa jukumu letu kubwa tulilonalo ni kuhahakikisha tunafanya kampeni nyumba kwa nyuma, kutanda kwa kitanda, uvungu kwa uvungu mpaka tunashinda. Ndugu zangu wa Dar leo haya nilikuwa nachomekea tu, kwa sababu nafahamu tar 23 pale Jagwani itakuwa ndio siku yenyewe ya kuzungumza lakini niwaambie, mimi ninatosha kila mahali. Mbele natosha, nyuma natosha, ubavuni natosha na kila mahali natosha. Shida za wana-Dar es Salaam nazifahamu na kwa bahati nzuri katika uzoefu wa miaka 20 niliokaa serikali, sijawahi kushindwa mahali, mtuamini na hatutawaangusha. Mungu awabariki sana, yatakayokuja kwetu kama changamoto tutayakamilisha kwa nguvu ya hali ya juu. Na vyama vishindwe na vilegee.

Ali nselema, CCM nselema........

Tatizo la kukataliwa na wasichana Kila Ninapotongoza..Naombeni Ushahuri

0
0
Ndugu zangu kila ninapotongoza wasichana wananikataa.
Sijui sababu ya kukataliwa mwishowe huwa naishia kupiga punyeto au kununua dada poa
Nisaidien ndugu nipate technic nataka niwe na msichana wangu Peke yangu.

JIBU KUTOKA KWA AUNTY MAPENZI RAHA:
Hebu chunguza yafuatayo.
Unapiga mswaki?
Unanuka kikwapa?
Au unafuaga nguo vizuri?
Unapiga pasi?
Miguu yako inatoa harufu ukivaa viatu?
Unanyoaga nywele za kichwani na kidevuni na mashavuni?
Una mkwanja?
Kama majibu ya maswali yote haya ni NDIO basi nadhani inabidi ukasafishiwe Nyota yako kanisani.
Sio Bagamoyo.
Tuanzie hapo kwanza
Halafu kumbuka kuweka umri wako hapa wakati unajibu maswali haya.
Vigezo na masharti kuzingatiwa

Je wewe una mshauri nini Huyu Jamaaa?

Kwanini Wanaume Wengi Walioko Kwenye Ndoa Hufa Mapema na Kuwaacha Wake zao ?

0
0
(Kwanini wajane ni wengi kuliko wagane??)
1. Umri mdogo wa kikomo cha maisha “life expectancy” – Kama unafahamu hili jambo linaloitwa “life expectancy” utakubaliana na mimi kwamba umri wa mwanaume wa kuishi ni mdogo sana ukilinganisha na mke wake, hususani kusini mwa jangwa la sahara. Kwa hiyo wanawake wanapewa nafasi kubwa ya kuishi muda mrefu kuliko waume zao.

2. Ugumu katika kufunguka – Utakubaliana na mimi kwamba wanaume ni wagumu sana ten asana kufunguka na kushirikisha mambo yao, wao wako tayari wafe na tai shingoni wakijifanya hawaumii au hawasikii shida. Mkiwa na ishu kwenye ndo mkaitwa sehemu muyaongee yeye kamwe hamumpati, anakwambia mambo yetu tutasuluhisha wenyewe wakati ndani yanamla na kummaliza. Na kwa mtaji huu watakufa sana tu

3. Ugumu katika kusamehe – Kusamehe sio tu kwa faida ya anayesamehewa bali pia kwa afya yaw ewe unayesamehe. Mzigo unaotokana na kusamehe hutuumiza sana mioyo yetu, hata kama mara nyingine tunajifanya hatuna shida yeyote. Unaposamehe unaachilia mzigo mkubwa, wanaume wao ni wagumu sna kusamehe. Wako tayari wakubebe moyoni miaka, na tena watakukumbusha uchungu wao kila wanapokuona. Hii inawala sana bila wao kujua.

4. Tabia hatarishi – Wanaume wengi kwenye ndoa ndio wanaoongoza kushiriki tabia hatarishi kama vile ulevi, anasa, ngono holela na hii huwaweka karibu zaidi na jeneza kuliko wake zao waliowaacha nyumbani wakiwadanganya kuwa wako mkutanoni mkoani.

5. Ugumu katika kujali afya – Ni rahisi sana mwanaume akajisikia vibaya lakini asiende hospitalini kuangalia afya, hata pale anapohimizwa kwenda bado anaweza kukwepa au kubisha au hata kusema kuwa ameshakwenda au ameshakunywa dawa kumbe mwongo. Wako pia ambao wanaweza kupewa dawa na wasizitumie.

6. Msongo wa mawazo – Wanaume ndio wabebaji wakubwa wa shehena za msongo wa mawazo “stress” ingawa kwa nje wanajitahisi sana kuonyesha kuwa mambo yako shwari wakati wanatafunwa ndani. Kaulize hospitalini, wanaokufa kwa presha ya kupanda au ya kushuka, stroke, kusimama kwa moyo, kupasuka kwa mishipa ya damu, matatizo ya mifupa, au kuumwa sana kichwa, halafu uliza ni jinsia gani.

Maisha sio mabaya kiasi hicho, maisha ni mazuri. Chagua kuishi – Chris Mauki

Walinzi wa CHADEMA Walioongoza Msafara wa Lowassa Jijini Mbeya Watakiwa Kujisalimisha Polisi Kwa Ajili ya Mahojiano

0
0
Mnamo Tarehe 14.08.2015 Mgombea Urais Kwa Tiketi Ya Chadema Alikuja Mkoa Wa Mbeya Akiwa Ameandamana Na Viongozi Wa Vyama Vya Cuf, Nccr – Mageuzi Na Nld Kwa Dhumuni La Kumtambulisha Na Kuomba Udhamini Wa Kupeperusha Bendera Ya Chadema Kwa Nafasi Ya Urais.

Katika Msafara Wake Kutoka Uwanja Wa Ndege [songwe] Kulionekana Gari Moja (pichani) Aina Ya Land Cruiser – Pick Up Yenye Rangi Nyeusi Na Ndani Yake Lilikuwa Limebeba Vijana Ambao Walikuwa Wamevaa Mavazi Meusi, Kofia – Bereti Nyeusi Na Miwani Nyeusi Na Mabuti.

Watu Hao Walikuwa Na Muonekano Kama Askari Na Shughuli  Waliyokuwa Wakifanya Ya Kuongoza Msafara, Ulinzi Na Kazi Nyingine Zifanyazo Na Jeshi La Polisi.
 
Kutokana Na Muonekano Wao Na Shughuli Walizokuwa Wakizifanya Ilikuwa Ikitafsirika Kuwa Ni Jeshi Lifanyazo Kazi Hizo Ambalo Halikuwa Likifahamika.

Kutokana Na Sintofahamu Hiyo Wananchi Wengi Walikuwa Wakihoji “hilo Ni Jeshi Gani” Sambamba Na Kutuma Picha Kwa Njia Ya Mtandao Wa Kijamii [whatsapp] Wakionyesha Wasiwasi Waliokuwa Nao Dhidi Ya Kikundi Hicho.

Kufuatia Hali Hiyo, Ofisi Ya Mkuu Wa Upelelezi Wa Makosa Ya Jinai Mkoa Wa Mbeya Ilifungua Jalada La Uchunguzi Ili Kuwapata Vijana Wale Kwa Lengo La Kuwahoji Na Kukamilisha Upelelezi Ili Jalada Lipelekwe Kwa Mwanasheria Wa Serikali Kwa Ufafanuzi Wa Kisheria.

Hii Ni Kutokana Na Kuibuka Kwa Makundi Ya Aina Hii Hasa Kwa Vyama Vikubwa Vya Siasa Hapa Nchini.

Katika Kufanya Ufuatiliaji Huo, Wapo Watu Wawili Walikamatwa Alfajiri Ya Leo Tarehe 18.08.2015 Kwa Mahojiano Na Baada Ya Maelezo Yao Kuchukuliwa Walipewa Dhamana.

Baadhi Ya Viongozi Wao Waliokuja Polisi Wameelezwa Kuhitajika Kwa Vijana Wale Waliokuwa Katika Gari Lile Ili Wahojiwe Na Kukamilisha Upelelezi Wa Jalada Hilo Mapema Ili Mwanasheria Wa Serikali Alitolee Mwongozo Wa Kisheria.
 
           Imesainiwa Na:
[ahmed Z. Msangi – Sacp]
Kamanda Wa Polisi Mkoa Wa Mbeya.

Rose Ndauka: Nipo Tayari Kuolewa na Yeyote Japo Awe ni Mume Bora Alie toka kwa Mungu

0
0
ROSE Donatus Anjelus Ndauka ‘mtata’ amesema kama mwanamke aliyekamilika na mwenye kuhitaji heshima katika jamii, yupo tayari kuolewa na kuishi kama mama na mwanaume yeyote.
Akichonga na Amani, Rose alisema japo mume bora anatoka kwa Mungu na kwamba anangojea aliye chaguo lake, lakini amechoshwa na hali ya kuishi bila ndoa.

“Mimi kama mwanamke ninayetoka kwenye familia yenye maadili, inafika wakati natamani kuishi katika ndoa, natamani kuwa na familia yangu na mume wangu na kwa sasa akitokea yeyote, nikajihakikisha kuwa anavyo vigezo ninavyovihitaji, hakika niko tayari kuanzisha naye safari ya maisha,” alisema Rose.
Awali Rose alikuwa na uhusiano na msanii wa Bongo Fleva, Malick Bandawe ‘King Chiwaman’ na kufanikiwa kupata mtoto mmoja na mwishoni mwa mwaka jana waliachana.

Lowassa Funguka Kila Kitu Kuhusu Richmond, CCM Wanapanga Kukuanika

0
0
Wakati umefika kwa Lowassa kujibu mapigo na kuwaeleza watanzania kila kitu(A-Z) kuhusu Richmond maana kwa mujibu wa gazeti la Uhuru la leo tarehe 19/08/2015,CCM wanapanga kutumia kile kinachoitwa "file chafu" la Lowassa kukuchafua hivyo nawe jibu mapigo bila kuficha chochote vinginevyo itaku-cost.

Kichwa kimoja kidogo cha habari katika ukurusa wa mbele kinasomeka, "faili chafu lenye lundo za kashifa kufunguliwa J'pili".

Tukumbuke J'pili ndio CCM nao wanazindua campaign zao.

Yangu ni hayo tu.

By Salary Slip /JF

Easter Bulaya Apewa Fomu ya Ubunge kwa Mbinde...'Kwanini Awe Yeye Badala ya Mshindi wa Kwanza".

0
0
Ester Bulaya, mshindi Wa Tatu kura za maoni CDM, Amepitishwa na chama kupeperusha bendera ya chama kama mgombea Wa Ubunge -BUNDA. Alipokwenda kuchukua Form yake msimamizi Wa uchaguzi akamgomea. Kisa .."kwanini uwe wewe badala ya mshindi Wa kwanza".

Mtanange haukuishia hapo, mwenyekiti Wa chama plus mshindi Wa kwanza kwenye kura za maoni wote wakavamia offisi ya msimamizi huyo kushinikiza Ester Bulaya apewe Form, bado msimamizi akagoma kwa madai Yale Yale kwanini wakupe wewe sio yule. Mtifuano ulipozidi akaachia form.

Watanzania hii Tafsiri yake nini? Kiongozi sampuli hii huko mbeleni itakuwaje.. Na wako wengi type hiyo..

TAFAKARI AISEE..

Utafiti Mpya: Lowassa Kuibuka Mshindi kwa asilimia 51.2%, Magufuli kuambulia 47.9%

0
0
Utafiti wa awali uliotolewa na shirika la Kimataifa umeonyesha kwamba Lowassa atashinda kwa asilimia 52.1% Dhidi ya Magufuli 47.9..... (see attached document).... Utafiti huu umefanywa kwa mikoa 29 Tanzania

Kwa upande wa wabunge inaonyesha CCM wataongoza kwa kuwa na wabunge wengi dhidi ya Ukawa.....

Mytake:... Lowassa Hazuiliki...

Shilole: Nikiiba mume wa mtu nisilaumiwe

0
0
Mwanamuziki wa miondoko ya mduara ambaye kwa hivi sasa anatumikia kifungo cha mwaka mmoja kilichotolewa na  Baraza la Sanaa Basata  ya kutojihusisha na shughuli za kisanaa mpaka mwaka mmoja, kitu ambacho kimemuumiza sana na kudai kuwa akiiba mume wa mtu atakuwa anakosea pia!
Akizungumza na paparazi wetu, Shilole alisema kuwa adhabu aliyopewa ni kubwa mno kiasi ambacho  anashindwa kuelewa kwa kuwa sanaa ndiyo kazi inayompatia kula na hata kuwasomesha watoto wake hivyo kumfungia mwaka mzima ni kama kumtuma kutembea hata na waume za watu  ili maisha yake yazidi kusonga mbele.

“ Mimi naona sasa wananituma kuanza kusaka waume za watu kwa kweli kwa sababu mwaka mzima kweli na ni kazi ambayo naitegemea kwa kila kitu katika maisha yangu kwa nini  mtu usiwaze vitu vingine kama huna kazi ya kufanya jamani, yaani inaniuma sana,” alisema Shilole.

Kasoro DART: Milango ya Mabasi ya Mwendokasi milango yake iko kushoto wakati vituo viko kulia!

0
0
Hii ndio Tanzania bwana. Mabasi yaendayo kasi milango yake iko kushoto na vituo viko kulia. Sasa sijui wamefanya kinyume. Najaribu kuwaza kwa sauti.

Serikali Yakataa Ombi la UKAWA Kutumia Uwanja wa Taifa kwa ajili ya Uzinduzi wa Kampeni Za Uchaguzi Mkuu

0
0
SERIKALI imekanusha taarifa zilizojitokeza kwenye Vyombo vya habari yakiwemo magazeti na mitandao ya kijamii kwamba Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kitafanya mkutano hadhara Uwanja wa Taifa Dar es Salaam tarehe 22 Agosti, 2015.

Akizungumza na vyombo vya habari jana, Mkurugenzi wa Idara ya Habari (MAELEZO), Assah Mwambene alisema serikali haijatoa ruhusa kwa chama chochote cha siasa kutumia uwanja wa taifa kwa ajili ya shughuli za kisiasa

Alikiri kwamba ni kweli kwamba CHADEMA waliiandikia Wizara tarehe 12 Agosti, 2015 kutaka kutumia uwanja wa taifa katika uzinduzi wa kampeni lakini ombi lao lilikataliwa kwa maelezo kwamba uwanja ule kwa mazingira ya sasa hauruhusiwi kutumika kwa ajili ya mihadhara ya vyama vya siasa

“Kwa kipindi haturuhusu uwanja wa taifa kutumika kwa mihadhara ya kampeni za vyama vya siasa. Uamuzi huu unalenga kuweka uwanja katika mazingira rafiki ya michezo na kuepuka athari zozote zinazoweza kujitokeza kutokana na mihemuko ya kisiasa” alisema Bwana Mwambene.

Mwambene ameeleza kuwa, Serikali imeamua uwanja huo ubaki kwa ajili ya kufanyia shughuli zake za msingi za kimichezo ili kuepuka mihemuko na athari yoyote inayoweza kujitokeza kutokana na hamasa za kisiasa.

“Ni kweli kwamba tulipata barua ya Chadema kuomba Uwanja kutumika kwa ajili ya mhadhara ya kisiasa wa CHADEMA hasa kuzindua Kampeni zao kwenye Uwanja tayari tumeshawaandikia kuwaarifu kuwa Uwanja ule hauwezi kutumika kwa ajili ya shughuli zozote za kisiasa” alisema Bwana Mwambene.

Alisema vyama vyovyote vitakavyoomba kutumia Uwanja ule kwa shughuli za kisiasa havitaruhusiwa.

Kikwete: Picha za mafuriko ya UKAWA ni za kutengeneza

0
0
Hiyo ni kauli ya raisi Kikwete kama ilivyonukuliwa na gazeti la TanzaniaDaima la leo.

My take:
Kukata roho ni shiiida!

Ukame wa wana CCM Maguli kuhamia CHADEMA, Je Lowassa Amefilisika au Ameuziwa Mbuzi Kwenye Gunia?

0
0
Wakati Lowasa anahamia CHADEMA, alienda kwa tambo nyingi huku akiwaahidi viongozi wa CHADEMA kuwa kuna mafuriko ya wana CCM kuhama chama chao na kujiunga na CHADEMA.

Hata hivyo, mpaka sasa, ni takriban wiki tatu sasa tangu mwanasiasa huyo ahamie CHADEMA na hakuna dalili za yale mafuriko aliyoahidi wakati anajiunga na CHADEMA. Mpaka sasa ni wenyeviti wawili tu wa mikoa wa CCM waliojiunga na Lowasa ilhali aliahidi kuwa zaidi ya nusu ya wenyeviti wa mikoa na wilaya watatangaza kujiunga na CHADEMA. Pia alitangaza kuwa kuna wakuu wa mikoa na wilaya watajiunga na CHADEMA ambapo mpaka sasa, hakuna mkuu wa Mkoa wala wilaya aliyejiunga na CHADEMA.

Pia, hakuna mbunge aliyepitishwa na CCM ambaye ametangaza kujiunga na CHADEMA. Waliojiunga na chama hicho ni wale waliokatwa kwenye kura za maoni kutokana na kushindwa kutimiza matarajio ya wananchi kwenye majimbo yao.

Kwa upande wa wanachama wa kawaida, hapa ndipo hofu ya Lowasa ilipo. Mpaka sasa hakuna lile wimbi la wanachama wa CCM kwenda CHADEMA, baadhi waliokuwa na hasira kutokana na watu wao kukatwa hali imetulia baada ya kuujua ukweli.

Swali la kujiuliza, je Lowasa ameshindwa kufikia dau la kuweza kuwanunua wana CCM zaidi au ameuziwa mbuzi kwenye gunia?

Wimbi Kubwa la Wanawake Wengi Kuwa na Watoto Bila Kuwa na Baba wa Mtoto

0
0
Kumekuwepo na wimbi kubwa kwa hawa dada zetu, kuwa na watoto bila mume.Ukimuuliza anakwambia tumeachana na hawakotayari kuweka wazi sana.

Sasa mimi nashindwa kuelewa tatizo ni sisi wanaume, au ni hawa dada zetu?

Na je mwanaume inakuweje mpaka unafikia hatua ya kumwachia watoto mzazi mwenzio?

Na wewe dada inakuweje uone unaweza muishi na watoto bila mume hata kama hela ya kuwalea unayo?

Yaani jaribuni kuchunguza katika wasichana kumi hapa Bongo, wenye umri 25-35 saba wana watoto na ukiuliza kuhusu baba wa mtoto, au watoto utapewa ngonjera tu!

Tatizo liko wapi? Ebu fungukeni kina dada au sababu ni sisi wanaume?

Jokate Afunguka Baada ya Kukataliwa Ukweni: Wazazi Wasiingilie Mapenzi ya Watoto

0
0
SIKU chache baada ya gazeti dada ya hili la Ijumaa Wikienda kuripoti juu ya wazazi wa Jokate Urban Mwegelo ‘Kidoti’ kumkataa Ali Kiba kama mchumba wake, binti huyo ameibuka na kuwataka wazazi kote nchini kuacha kuwaingilia watoto wao katika masuala ya kimapenzi, akidai jambo hilo ni vema wakiachiwa wenyewe.

Akizungumza na gazeti hili, Jokate alisema ni vyema kama wazazi wakawaacha watoto wao waoe au kuolewa na watu wawapendao, kwani vinginevyo ni kuwaingilia maisha na uhuru wao binafsi, jambo ambalo si jema.

“Unajua nimelala, madai ya Ally (Kiba), sitaki kuyazungumza sana, unajua mimi ni binti mtu mzima, ninao uhuru wa kumchagua nimpendaye kwa ajili ya maisha yangu, ifike mahali wazazi wawape uhuru watoto wa kufanya mambo yao, awamu hii siko tayari kuona naumizwa tena na familia juu ya uhusiano wangu,” alisema binti huyo kwa njia ya simu juzi.

Chanzo: GPL

Ester Bulaya Hakuwa na Mpango wa Kuhama CCM ila….

0
0
Najua nina watu wangu wanaopenda stori za siasa sasa stori ninayotaka kukusogezea ni hii kutoka kwa aliyekuwa mbunge wa viti maalumu kupitia CCM Ester Bulaya pamoja anaonekana kwenye headlines mpya za Chadema baada ya kuhamia chama hicho anasema hakutegemea kuhama chama cha Mapinduzi (CCM).

Kuhama inatokea na mazingira lakini mimi sikuwahi kufikiria kama nitakuja kuhamia Chadema lakini mienendo, tabia, future  ya kuwatumikia wananchi ilikuwa imepotea mimi nimekulia CCM na am proud for that  wamenilea lakini walinilea kwenye misingi ya uwazi na ukweli kile walichonifunza nikitaka kukitumia hawataki sasa kama kuna wengine kile nilichofundishwa huku wao wanakiaminia kutoka moyoni na midomo mwao niende kujiunga nao lakini wote tukiwa na ndoto za kuwatumikia wananchi’ -Ester Bulaya


Unajua kuna tofauti ya utumishi na mtu kufikiri utumishi ni cheo wanaofikiri ubunge ni cheo ni wale ambao hawatimizi wajibu wao wanataka ubunge kutaka madaraka Fulani, mimi ni mtumishi naenda kuwatumikia wananchi mabosi wangu ni wananchi ukiwa unadhani ya kwamba ubunge ni cheo utavimba kichwa na utashindwa kutimiza wajibu wako, bunge bosi wake ni wananchi‘ – Ester Bulaya.

SBL Yapeleka Uzinduzi wa Tuzo za Ubora wa Thamani Kwa Wakazi wa Mwanza na Moshi

0
0


Mkazi wa Kona ya Bwiru jijini Mwanza Bw. Godfrey Urio akionyesha zawadi ya fedha taslim alizopokea mara baada ya kuibuka mshindi wa shindano la “Serengeti Masta” wakati wa kusherekea uzinduzi kampeni ya tuzo ya dhahabu ya ubora wa thamani ya Monde Selection ambapo kwa mwaka huu bia ya Serengeti Premium Lager toka SBL imejinyakulia medali tatu za dhahabu kutokana na ubora wake. (Kushoto) ni Meneja Masoko kwa wateja wa Kampuni ya bia ya Serengeti kanda ya Mwanza Bw. Denis Tairo na kulia ni mshereheshaji wa tukio hilo aliyefahamika kwa jina la MC Bebe. Hafla hiyo ambayo ilikua mahususi kwa wakazi wa kanda ya ziwa, ilifanyika katika baa ya “The dreams” iliyopo Kona ya Bwiru jijini Mwanza. Shindano la “Serengeti Masta” litafanyika Tanzania nzima na kuibua Mshindi mmoja kwa kila kanda na mwisho kumuibua wa taifa. Kauli mbiu ya kampeni hii ikiwa ni “TUNAIJUA BIA NA SERENGETI PREMIUM LAGER NDIO YENYEWE”.

Mdau wa bia ya Serengeti Premium Lager Ben Rockman akijaribu kuitambua bia ya Serengeti Premium Lager ,aliposhiriki kwenye shindano la kumtafuta “Serengeti Masta” wa baa ya “The dreams” ya jijini Mwanza wakati wa kusherekea uzinduzi kampeni ya tuzo ya dhahabu ya ubora wa thamani ya Monde Selection ambapo kwa mwaka huu bia ya Serengeti Premium Lager toka SBL imejinyakulia medali tatu za dhahabu kutokana na ubora wake. Kauli mbiu ya kampeni hii ikiwa ni “SERENGETI PREMIUM LAGER. TUNAIJUA BIA NA HII NDIO YENYEWE”.

 Wakazi wa Majengo mjini Moshi wakiburudika kushangilia Tuzo ya Dhahabu ya Monde waliyoipata kwa Bia ya Serengeti Premium Lager mwaka 2015 kutambua ubora wa kiwango cha juu wa iliyopata Bia ya Serengeti Premium Lager ambayo iliambatana na mashindano ya kutambua bia ya Serengeti Premium Lager mwishoni mwa wiki katika Baa ya Oriental.

Wafanyakazi wa kampuni ya Serengeti Brewieries Limited wakiwa na Mabalozi wa kinywaji hicho wakati wa kutambulisha Tuzo ya Dhahabu ya Monde inayotambulika kimataifa baada ya bia ya Serengeti Premium Lager kukidhi viwango vya juu vya ubora katika hafla iliyofanyika katika Baa ya Oriental ,Majengo mjini Moshi mwishoni mwa wiki.
Viewing all 104432 articles
Browse latest View live




Latest Images