Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104701 articles
Browse latest View live

Lulu Amchokonoa Zari...Ajibebisha Kwa Diamond Platnumz

$
0
0

UCHOKOZI! Staa wa sinema za Kibongo, Elizabeth Michael ‘Lulu’ anatengeneza kichwa cha habari kwa mara nyingine baada ya kudaiwa ‘kujibebisha’ kwa staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’, kitendo kilichotafsiriwa kuwa ni kumchokonoa mwandani wa jamaa huyo, Zarinah Hassan ‘Zari The Boss Lady’.


Tukio hilo lilijiri usiku mnene Jumapili iliyopita kwenye Ukumbi wa House Club uliopo Masaki, Dar ambapo kulikuwa na sherehe ya bethdei ya DJ wa Diamond, Rommy Jones.
Kwa mujibu wa shuhuda wetu aliyeweka kambi ukumbini humo, Lulu, bila kujali kwamba, Diamond alimwacha Zari nyumbani akimnyonyesha ‘baby girl’ wao, Latifah Nasibu a.k.a ‘Princess Tiffah’, alionekana akijiachia naye kimahaba huku akionesha ‘kummisi’ kinoma jamaa huyo.
LIANZA HIVI
Lulu, alikuwa wa mwishomwisho kuingia ukumbini ambapo baada ya kuzunguka kusalimiana na mastaa wengine alitua kwenye sofa alilokuwa amekaa Diamond ambapo walianza kufanya yao bila kujali ëwavimba machoí waliokuwa wakiwakodolea.
Kwa kuwa Diamond alikuwa host (mwendeshaji) wa shughuli hiyo, Lulu alikuwa akimwaga mauno huku akimshangilia Diamond kufuatia muziki wake wa nguvu uliokuwa unarindima ukumbini humo.
Kutokana na hali hiyo, Lulu aliendelea kucheza zaidi kwa madai kwamba anaupenda mno muziki wa Diamond hasa ulipodondoshwa ule wa Mdogomdogo.
WAONESHANA MAHABA
Ilifika wakati Diamond alionekana akimpiga Lulu busu mdomoni huku watu wakishangilia ëoyoooí lakini wao hawakuwa wakijali chochote kwani waliendelea kufanya yao.
Kuna wakati walikuwa wakitaniana na kucheka huku wakigongesha glasi zao za mvinyo na kukumbushana mambo mbalimbali ya siku za nyuma.
Baadhi ya watu walisikika wakisema kwamba, Lulu anamchokonoa mama Tiffah ‘Zari’ kwani kwa usiku huo yeye alikuwa tu nyumbani akinyonyesha wakati baba mtoto wake akijiachia na kimwana huyo.
“Naona Lulu anatafuta matatizo kwa Zari kwani mahaba wanayooneshana hapa ukumbini siyo ya kawaida, yaani hawa mastaa wetu mbona majangaaa,” alisikika mmoja wa wahudhuriaji wa shughuli hiyo iliyokuwa ya kistaa kwani hakukuwa na ‘watoto wa mbwa’.
SHETTA AMWAGA FEDHA
Katika sherehe hiyo ilipambwa na mastaa kibao wa fani mbalimbali na mapedeshee wa mjini, walimmwagia Rommy mvua ya fedha huku mwanamuziki, Nurdin Bilal ‘Shetta’ akimzawadia fedha taslimu Sh. milioni moja ambapo shughuli iliendelea hadi majogoo.
Wakati hayo yakitendeka mmoja wa marafiki wa karibu wa Zari alimtumia ujumbe mfupi wa maneno (sms) kumfahamisha juu ya tukio hilo.
MASTAA KIBAO
Ukiacha Lulu na Shetta, baadhi ya mastaa wengine waliojiachia vya kutosha ni pamoja na Aunt Ezekiel na baba mtoto wake, Moses Iyobo, dada wa Diamond, Mwajuma Abdul ‘Queen Darleen’, Khaleed Mohamed ‘TID Mnyama’, Vanessa Mdee ‘Vee Money’ sambamba na Juma Musa ‘Jux’, Hamad Ally ‘Madee’, Zuwena Mohamed ‘Shilole’ na wengine kibao.
LULU ANASEMAJE?
Akizungumzia hali hiyo, Lulu alisema kuwa ilikuwa ni pati na kupiga picha na Diamond haikuwa ishu kubwa kwani ni watu wengi waliopiga naye picha.
“Siamini wala sihisi kama Zari anaweza ‘kumaindi’ ishu kama hiyo. Kama akimaindi atakuwa na lake jambo,” alisema Lulu.
TUJIKUMBUSHE
Kabla ya tukio hilo, Lulu aliwahi kudaiwa kutoka na Diamond lakini alikanusha vikali ishu hiyo huku akionesha kuwa jamaa huyo hana ubavu wa kumsogelea wala kufaidi penzi lake.
Chanzo:GPL

Diamond Platnumz Aamua Kuungana na Wema Sepetu Kumpigia Kampeni Mgombea wa CCM John Magufuli

$
0
0
Kutokana na demokrasia kila mtu ana haki ya kumchagua kiongozi ambaye anadhani kuwa anafaa bila shinikizo la mtu, hii imetokea pia kwa baadhi wasanii ambao wamegawana katika makundi ambapo kuna baadhi wapo team Lowassa na wengine team Magufuli.

Hadi sasa kuna baadhi ya mastaa wa Tanzania, wameweka wazi watu wanaowakubali kati ya wagombea wawili, miongoni mwao ni Wema Sepetu aliyeweka wazi kumsupport Magufuli, muigizaji Jacqueline Wolper na Aunty Ezekiel wanamsupport Edward Lowassa na sasa ni Diamond ameweka wazi kuwa yupo team Magufuli.

Kupitia mtandao wa kijamii Diamond ameandika “Iwe Msanii, Mtangazaji, ama Mwanamichezo, ila Kila Mtanzania anahaki ya Kuchagua kiongozi anaeamini ni Bora, Mchapa kazi, Mwenye Afya na Msimamo ili kutuendelezea Nchi yetu… Kwa Uchunguzi na tathmini niliyoifanya tangu hizi mambo za Kampeni zianze nimegundua na kuamini kuwa huyu ndio Jembe,”.

Akamalizia “Nitakuandikia na kukupostia ushahidi kukuthibitishia kwanini nimeona John Magufuli Pombe ndie anaefaa… unapohisi na wewe una fact za kumtetea umtakaye karibu uniambie hapo halaf na mi nikumwagie zangu, ila usijisumbue Matusi coz hayatokusaidia wala kunisaidia kunibadilisha akili yangu kwa sababu sanasana ntakuona Huna akili Maana nishayazoea, nipe fact zako nami nikupe zangu ili pamoja Tujenge nchi….. #HapaKaziTu #Ccm,”.

Mshindi wa Kura za Maoni CHADEMA Bunda Aliyekatwa na Nafasi yake Kupewa Ester Bulaya, Ahamia CCM

$
0
0
Wakuu, hatimae Pius Masului yule mshindi wa kura za maoni CHADEMA jimbo la Bunda mjini amehamia CCM akidai kutoridhishwa Na maamuzi ya CC ya CHADEMA Taifa kukata jina lake na Kumpa Mshindi wa Tatu Ester Bulaya

Chanzo: Radio Mazingira FM

TETESI MTANDAONI..ETI Wasanii Wasioiunga Mkono CCM Kukosa Airtime Clouds FM

$
0
0
Nimepata taarifa kuwa kuna amri imetolewa kwa wasanii kumsuport mgombea wa CCM na CCM kiujumla, na atakaye kaidi hilo basi asahau kuwekwa hewani na chanel hiyo. Sina hakika maana mi si mmoja wa wasanii na wala sijapokea amri hiyo. Ila kwa haraka haraka nimejaribu kupitia account za wasanii wengi na kuanza kuamini hilo . Hapa chini nimeambatanisha baadhi ya screen short toka kwenye account za wasanii....

JE MWENZAGU UMEYASIKIA HAYO?




DR Slaa Kuibukia CCM, Apangwa Kujitokeza Kwenye Mkutano wa CCM Jagwani.....

$
0
0
USHAWISHI mkubwa umefanywa na Chama Cha Mapinduzi (CCM) kuhakikisha kuwa, katibu mkuu aliye mapumzikoni wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk. Wallboard Slaa anashiriki kwenye kampeni ya chama hicho tawala, Uwazi Mizengwe limeambiwa. Chanzo kutoka ndani ya CCM kilisema hivi karibuni kuwa, mazungumzo yamefanikiwa kwa kiwango kikubwa na kwamba upo uwezekano wa asilimia 90 kwa Dk. Slaa kupanda jukwaani siku ya ufunguzi wa kampeni za CCM uliopangwa kufanyika kwenye Viwanja vya Jangwani, Dar keshokutwa Jumapili. “Ili kukabili nguvu ya upinzani tulipanga kuwa Dokta atoke mafichoni ashiriki nasi kwenye uzinduzi, tuna imani hilo litafanikiwa na utakuwa ni mtaji mkubwa kwa chama chetu kipindi hiki cha kuelekea kwenye uchaguzi mkuu,” kilisema chanzo chetu.

Gabo:Sijaona Muigizaji wa Kushindana Naye Bongo Movies

$
0
0
Msanii wa filamu aliyejizolea umaarufu miaka ya hivi karibuni, Salim Ahmed maarufu kwa jina la Gabo amesema haoni msanii anayempa changamato.

Akizungumza kwenye kipindi cha Take One cha Clouds TV, Gabo alisema wengi wamekuwa wakimwambia anaringa kutokana na kuwaambia ukweli.

“Kwa hapa Tanzania sijui ndio maana wanasema mimi naringa,” alisema Gabo alipoulizwa ni msanii gani anayempa changamoto.

“Nyuma alikuwa Single Mtambalike, sasa hivi sijaona wa kumtazama na kunipa changamoto tuweze kushirikiana kupeana nguvu. Kwa single sijui nisene vitu vinakwenda vinaisha! Lakini simuoni tena yule, sasa hivi amekuwa akifanya kazi anakuwa ni yule yule, hakuna mabadiliko. Lakini nikimwangalia yule single wa filamu za nyuma nasemaga yule jamaa, amebadilika kabisa na kuwa wa kawaida,” aliongeza.

Gabo amesema kuwa pamoja na filamu za Tanzania kuwa na changamoto, amefanikiwa kupata mafanikio mengi.

“Mimi kama ningekuwa nchi nyingine ningekuwa mtu mkubwa sana,” alisema.

“Ukiangalia uwezo wangu mimi na jinsi ninavyoishi havilingani. Nimekuwa nikitembelea nchi kama Afrika Kusini na Jumatatu kama Mungu akipenda naenda Botswana, watu wanakuona huyooo kumbe maandazi tu hamna chochote! Kitu kikubwa ambacho nilikuwa nakihitaji kwa sasa ni kampuni yangu ya Sarafu Media, nilitamani iwe strong mtu akija anaogopa, lakini sasa ipo kampuni jina, mtu akija anaona huyu naye anaanza.

Kingine mimi nimejenga nje ya sanaa, hata kwangu pale nikilala najiona bado. Ndioa maana nikapangisha kule nikaja kukaa Kinondoni ili nitafute kwa jasho la filamu. Mimi ninachojivunia kwa sasa kilichopatikana kutokana na filamu ni gari (Passo), ndio maana sasa hivi naboresha zaidi kazi zangu hata mtu akinihitaji kufanya filamu yake aandae milioni 8,” alisisitiza.

Rais Kikwete Amjibu Lowassa 'Kimtindo'.

$
0
0
Rais Jakaya Kikwete, amefunguka na kusema hatishwi wala hashtushwi na maneno ya watu wanaosema serikali yake kwa miaka 10 haijafanya kitu.

Badala yake amesema kitakachomshtusha ni taarifa zozote za uchochezi kwa kutumia kivuli cha dini ama ukabila kwa kuwa vitu hivyo ni hatari na vinaweza kuliingiza Taifa katika machafuko.

Rais Kikwete aliyasema hayo jijini Dar es Salaam jana alipotembelea Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora  (THBUB) na kuzungumza na watumishi wake ambao walitumia nafasi hiyo kumuaga.

Alisema watu wanaobeza mafanikio ya serikali yake hawezi kuhangaika nao kwa kuwa anajua kuna mafanikio mengi yamepatikana katika kipindi cha miaka 10 mpaka sasa na wanao uhuru na kusema chochote wanachotaka.

“Kuna watu wanasema sana serikali yangu haijafanya chochote, lakini hawa sitahangaika nao kwa kuwa najua kuna mafanikio mengi yamefanyika katika uongozi wangu,” alisema  Rais Kikwete.

Alisema mtu atakayehangaika naye ni yule atakayetoa kauli za kuashiria uchochezi kwa kutumia dini na ukabila kwa kuwa vitu hivi ni hatari kwa amani ya nchi na kwamba kwa hilo atakuwa mkali.

“Kuna uhuru wa kutoa maoni na kama kuna mtu anataka kusema au kukosoa serikali yangu, mimi sina tatizo na yeye aende hata pale Jangwani aseme siku nzima sina tatizo naye, lakini atakayejaribu kuleta uchochezi kwa kutumia dini na ukabila, huyo tutashughulika naye," alisema.

Ingawa Rais Kikwete hakumtaja mtu yeyote, Julai 29, mwaka huu, Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa, anayegombea urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa tiketi ya Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), alisema kuwa Serikali ya Rais Kikwete imeshindwa kuwapatia wananchi maendeleo.

Lowassa baada ya kuchukua fomu za kuwania urais, akiwahutubia wafuasi wa Chadema na wananchi katika ofisi za chama hicho mtaa wa Ufipa, Kinondoni, Dar es Salaam pamoja na mambo mengine, alisema Serikali ya Rais Kikwete imeshindwa kusimamia uchumi kiasi cha bei za vitu kupanda kila uchao vikiwamo vibiriti, mafuta na vyakula.

Katika ziara zake za kutafuta wadhamini kwenye mikoa ya Mwanza, Arusha, Mbeya na Zamzibar, Lowassa alirudia kauli hiyo na kusema kuwa Serikali ya Awamu ya Tatu chini ya Rais Benjamin Mkapa, ilisimamia vizuri uchumi kuliko Serikali ya Awamu ya Nne.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya Agosti 21

$
0
0
















Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya Agosti 21, 

Kanisa Lagoma Kumbatiza Mtoto wa Aunt Ezekiel

$
0
0
Kanisa Katoliki limemzuia staa wa Bongo Movies, Aunt Ezekiel kumbatiza mwanaye kutokana na kutokidhi matakwa ya kanisa.

Tukio hilo limetokea hivi karibuni mara baada ya mwigizaji huyo ambaye imani yake ni ya Kiislamu, kutaka kumbatiza mwanaye huyo ambaye baba yake ( Moze Iyobo) ni Mkatoliki.

“Alikuwa amejipanga kumbatiza Kikristo kutokana na imani ya baba mtoto wake lakini alipokutana na padri Paul Ruwaaich wa Parokia ya Uparo Moshi aliyekuwa Dar kikazi akamtaka akaanzie kusali kwenye Jumuiya Ndogondogo (mtaani kwake), abadilishe dini ndipo mtoto huyo abatizwe kwani ndizo taratibu za Kanisa Katoliki.

“Alipopewa sharti hilo, lilikuwa gumu kwa Aunt, ikabisi ageuze zake,” kilisema chanzo chetu.

Mwanahabari wetu alipomuuliza Aunt kuhusu suala hilo, alisema amebaki njia panda na anatafakari cha kufanya.

Diamond Platnumz Noma Sana..Amdaka NEYO Nairobi na Kufanya Nae Collabo Moja Matata...Kiba Je ?

$
0
0
Huwa nawashangaa sana wanao semega eti Diamond ni freemanson wakati juhudi zake za kupita kiasi zinaonekana ..Unaambiwa Neyo amekuja kufanya Coke Studio na Kiba ila Diamond hapo hapo akachukua fursa bila kupoteza muda na kumburuza NEYO studio kutoa kitu kipya..ANGALIA PICHA HIZO USHAHIDI WAKIWA STUDIO NA SHEDDY CLEVER YULE PRODUCER WA NGOLOLO.. Hahah
Natumaini kiba na yeye atakamata fursa...ole wako urudi bongo bila collabo

Wasanii Wazindua Kampeni Kuipigia Debe CCM na Tamasha la 'Mama Ongea na Mwanao'

$
0
0
WASANII ambao ni makada wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wameandaa Tamasha kubwa kuzunguka nchi nzima kwa pamoja na kukinadi chama hicho tawala pamoja na Sera zake ili kiweze kushinda Uchaguzi Mkuu onaotarajia kufanyika Oktoba Mwaka huu (2015).
 
Tamasha hilo litakalojulikana kama “MAMA ONGEA NA MWANAO 2015″ limeandaliwa na baadhi ya wasanii makada wa CCM wapatao 250 ambao watazunguka mikoa zaidi ya 10 kukipigia kampeni chama hicho tawala ili kiweze kupewa ridhaa tena na Wananchi ya kuendelea kuongoza nchi.
 
Akizungumza jana jijini Dar es Salaam na waandishi wa habari Mwenyekiti Msaidizi wa tamasha hilo, Wema Sepetu alisema madhumuni ya tamasha la Mama Ongea na Mwanao 2015 ni kulinda mazuri yote yalioasisiwa na CCM kupitia viongozi wake akiwemo Baba wa Taifa Mwalimu Julias Nyerere na Sheikh Abeid Aman Karume.
 
Msanii Sepetu akiyataja masuala hayo yalioasisiwa na CCM kupitia viongozi hao kuwa ni pamoja na amani na utulivu uliopo hadi sasa, maendeleo ya kijamii na kiuchumi yalioletwa hadi sasa, masuala ambayo yanastahili kuendelezwa na wala si kubezwa.
 
Tamasha hilo linajumuisha wasanii kama Odama, Davina, Wastara Juma, Keisha, Wellu Sengo (Matilda), Bi. Mwenda, Mama Lolaa, Mama Nyamayao, Herieth Chumila, Thea, Maya, Chuchu Hans, Steve Nyerere pamoja na wasanii wengine wengi.
 
Aidha alisema kupitia tamasha hilo wasanii hao pamoja na wenzao watazunguka katika mikoa zaidi ya 10 kwa pamoja kufanya kampeni kumnadi mgombea wa urais kupitia CCM, Dk. John Pombe Magufuli, mgombea Mwenza, Samia Hassan Suluhu pamoja na viongozi wengine ngazi mbalimbali wanazogombea kupitia chama cha Mapinduzi.
 
Madhumuni ya tamasha la Mama Ongea na Mwanao 2015 ni kulinda mazuri yote yalioasisiwa na CCM kupitia viongozi wake akiwemo Baba wa Taifa Mwalimu Julias Nyerere na Sheikh Abeid Aman Karume ambayo bila amani mama awezi kujifungua salama, Bila mama hakuna familia, amani inapotoweka mama hawezi kukimbia kilometa kadhaa na kuiacha familia yake, bila mama hakuna ujasiliamali, mama ni kimbilio la baba, kaka, dada na watoto…ikumbukwe kuwa mama ndio mpiga kura ndio maana tunasema mama ongea na mwanao,” alisema Wema Sepetu.
 
“Na leo hii kuanzia sasa tunatambulisha kampeni yetu tunayoifanya kuhamasisha vijana, kinamama, kinababa, mashabiki wetu wale wote wenye sifa za kupiga kura wapige kura kwa kumchagua kiongozi bora anayetoka Chama Cha Mapinduzi…chagua Dk. Magufuli, Samia Suluhu, wabunge na madiwani wa Chama Cha Mapinduzi,” alisema Sepetu.
 
Aidha wasanii hao wamempongeza Mwenyekiti wa CCM na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jakaya Kikwete kwa kuongoza vizuri vikao vyote vya chama hicho hadi kupatikana kwa mgombea bora wa urais kupitia chama hicho (Dk. Magufuli), hivyo kuwataka wanaCCM wote ambao waligombea na hawakupata nafasi kuungana na kukitumikia chama.
 
“…Mimi Wema Abraham Sepetu nikiwa na baadhi ya wasanii wenzangu ambao tuligombea tunasema muda bado tunao na siku tunazo kwa kukitumikia chama tukipewa ridhaa kwa njia yoyote na kwa nafasi yoyote ndio maana hatuja teteleka tupo imara kuwatumikia wananchi katika nafasi nyingine ndani ya CCM,” alisema Sepetu.
Kada wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Mratibu wa Tamasha la MAMA ONGEA NA MWANAO 2015 litakaloipigia kampeni CCM, Steve Mengele a.k.a Steve Nyerere akizungumza na waandishi wa habari leo juu ya tamasha hilo.
Kada wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Mratibu wa Tamasha la MAMA ONGEA NA MWANAO 2015 litakaloipigia kampeni CCM, Steve Mengele a.k.a Steve Nyerere akizungumza na waandishi wa habari  juu ya tamasha hilo.
Mwenyekiti Msaidizi wa Tamasha la MAMA ONGEA NA MWANAO 2015 litakaloipigia kampeni CCM, Wema Sepetu (kulia) akizungumza na wanahabari leo jijini Dar es Salaam juu ya tamasha na kampeni zao. Kutoka kulia ni Wellu Sengo (Matilda) na Yobnesh Yusuph (Batuli).
Mwenyekiti Msaidizi wa Tamasha la MAMA ONGEA NA MWANAO 2015 litakaloipigia kampeni CCM, Wema Sepetu (kulia) akizungumza na wanahabari  jijini Dar es Salaam juu ya tamasha na kampeni zao. Kutoka kulia ni Wellu Sengo (Matilda) na Yobnesh Yusuph (Batuli).
Mwenyekiti Msaidizi wa Tamasha la MAMA ONGEA NA MWANAO 2015 litakaloipigia kampeni CCM, Wema Sepetu akizungumza na wanahabari leo jijini Dar es Salaam juu ya tamasha na kampeni zao. Kulia ni Yobnesh Yusuph (Batuli) na kushoto ni Steve Mengele a.k.a Steve Nyerere wakiwa katika mkutano huo.
Mwenyekiti Msaidizi wa Tamasha la MAMA ONGEA NA MWANAO 2015 litakaloipigia kampeni CCM, Wema Sepetu akizungumza na wanahabari jana jijini Dar es Salaam juu ya tamasha na kampeni zao. Kulia ni Yobnesh Yusuph (Batuli) na kushoto ni Steve Mengele a.k.a Steve Nyerere wakiwa katika mkutano huo.
Baadhi ya wasanii na makada wa CCM ambao watajumuika katika tamasha la MAMA ONGEA NA MWANAO 2015 litakaloipigia kampeni CCM wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya mkutano na waandishi wa habari.

Mpekuzi blog

Unbelievable!! HUDDAH MONROE Doing This To Her ‘Sehemu Ya Siri’ All in The Name of Men

$
0
0

Huddah Monroe says she is tired of waxing and shaving her private hair and has now decided to get rid of it via laser hair removal.
                       
This is what she wrote;

Huyu Ndo Mgombea Urais wa ACT-Wazalendo baada ya Kitila Mkumbo Kukataa

$
0
0
Hatimaye Chama cha ACT – Wazalendo kimempitisha mwenyekiti wake, Anna Mghwira (56) kuwania urais baada ya mshauri wake, Profesa Kitila Mkumbo aliyekuwa amechukuliwa fomu kukataa kubeba jukumu hilo.

Sambamba na Mghwira, mkutano mkuu wa chama hicho uliokutana jana ulimpitisha Hamad Mussa Yusuf kuwa mgombea mwenza.

Chama hicho kimefikia hatua hiyo baada ya kusota kwa siku kadhaa kutafuta mgombea na pigo kubwa lilikuwa juzi baada ya Profesa Mkumbo kukataa.

Akisoma maazimio ya Halmashauri Kuu katika mkutano mkuu jana usiku, mshauri wa chama hicho, Profesa Mkumbo alisema wameamua kumpitisha Mghwira kwa kuwa anazo sifa za kuwania urais.

Alisema mwenyekiti huyo anao uwezo na sifa za kuwa rais, kwa kuwa kazi za rais ambazo ni kufikiri, kuwa mlinzi mkuu wa umoja, tunu za Taifa na kuwa mfano bora wa ubinadamu anazimudu.

Alisema Mghwira anaweza kufikiri na amekuwa akiandika makala mbalimbali, jambo ambalo baadhi ya wagombea hawaliwezi kwa kuwa hata hotuba wanaandikiwa.

Baada ya kumtangaza, wajumbe wa mkutano huo walishangilia kwa mbwembwe kumpata mgombea huyo.

Kwa uteuzi huo, Mghwira atalazimika kuachia ule wa awali wa kuwania ubunge katika Jimbo la Singida Mjini na atakuwa na kibarua ya kutafuta wadhamini nchi nzima na kukamilisha kazi hiyo kabla ya kurejesha fomu kwa muda aliopangiwa wa saa 7.30 mchana leo.

Akiwashukuru wajumbe wa mkutano huo, Mghwira alisema Taifa linahitaji kiongozi mwenye moyo wa nyama, mwenye upendo, uadilifu na mwenye uwezo wa kuwaunganisha watu wote bila upendeleo.

Alisema wamechelewa kumtangaza mgombea kwa kuwa walikuwa wanatafakari kauli ya Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere ya “Ikulu ni mahali patakatifu”, hivyo wamempata rais mtakatifu.

Kiongozi wa ACT – Wazalendo, Zitto Kabwe alisema ilani ya uchaguzi ya chama hicho imejikita katika mambo matano ambayo ni hifadhi ya jamii, elimu, afya, ajira na utalii.

Hali Tete Bunda, Viongozi CHADEMA Wajiuzulu...Kisa Ester Bulaya

$
0
0
SIKU chache baada ya mgombea ubunge wa Jimbo la Bunda Mjini kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Esther Bulaya kuteuliwa na chama hicho na kuchukua fomu ya kuwania nafasi hiyo, hali ndani ya chama hicho wilayani Bunda imekuwa tete.

Hatua hiyo inatokana na uamuzi wa aliyekuwa mpinzani wa Bulaya katika kura za maoni ndani ya chama hicho, Pius Masururi, kujitoa katika chama hicho na kujiunga na Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Tayari Masururi ametangaza kumuunga mkono Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Stephen Wasira katika mbio za ubunge huku viongozi 11 wa Chadema katika jimbo hilo wakisimamishwa uongozi.

Inaelezwa kuwa sababu ya kusimamishwa kwa viongozi hao kunatokana na kile kilichodaiwa kuwa kusimamisha wagombea mamluki katika nafasi ya ubunge na udiwani.

Akizungumza jana mjini hapa kupitia Redio ya Kijamii ya Mazingira FM, Masururi alitangaza kujiunga na CCM jana muda mfupi kabla ya kuondoka na kurejea jijini Nairobi nchini Kenya.

Alisema Kamati Kuu haikutenda haki kwa kumteua Esther Bulaya na kumwacha yeye ameshinda katika kura za maoni licha ya kushiriki kwake kukijenga chama hicho kwa kipindi cha miaka minne.

Kutokana na hali hiyo, Katibu wa Chadema Wilaya ya Bunda, Rita Ikandire kwa niaba ya viongozi wanzake wanaotuhumiwa kukihujumu chama hicho wametangaza kujiuzulu nafasi zao za uongozi huku wakidai ofisi ya katibu wa Mkoa wa Mara na Taifa wamevunja katiba ya chama hicho.
“Mimi pamoja na viongozi wa jimbo na kamati ya utendaji Jimbo la Bunda tumejiuzulu baada ya kutoridhika na uamuzi wa Kamati Kuu lakini pia baadhi ya makatibu na wenyeviti katika kata 20 za jimbo hili wamejiuzulu na watabaki kuwa wanachama wa kawaida wa Chadema,” alisema Rita.

Waliotangaza kujiuzulu mbele ya waandishi wa habari ni pamoja na Alfred Imanani(Mwenyekiti wa Jimbo), Emmnuel Malibwa(Katibu Mwenezi), Dickson Kujerwa(Mwenyekiti BAVICHA), David Abogast (Mjumbe Kamati ya Utendaji), Mwenge Webiro (Katibu BAWACHA jimbo) na Mjumbe wa Mkutano Mkuu wa Taifa, Juma Omari.

Wengine ni Ng’wena Mwita (Mwenyekiti Baraza la Wazee jimbo), Damas Kunju, Kibago Kibago(Red Brigedia Mkuu) ambao wote wamedai kujiuzulu na kubaki wanachama wa kawaida.

Wakati viongozi hao wakidai kujiuzulu, mmoja wa kiongozi wa Chadema, Kaunya Yohana, alisema viongozi 11 tu ndio wamesimishwa uongozi na chama baada ya kupandikiza wagombea wasiokuwa na sifa.
“Viongozi hao hawakujiuzulu kama wanavyodai isipokuwa wamesimamishwa uongozi mpaka mambo yatakapokuwa sawa tangu tarehe 15/8/2015,” alisema Yohana.

Alisema viongozi hao wamesimamishwa kwa barua yenye kumb. Na.C/HQ/ADM/KK/08 ya tarehe 19/08/2015 iliyosainiwa na Julius Mwita Katibu wa Vijana Taifa kwa niaba ya Katibu Mkuu wa Chadema Taifa.

Aliwataja baadhi ya waliosimamishwa kuwa ni pamoja na Alfred Imanani, Rita Ikandiro, Emanuel Malibwa, Damas Kunju, Dickson Kujerwa, David Abogast, Matara Athumani na Noa Laurent.

Alisema wakati viongozi hao wakitumikia adhabu hiyo chama kimeunda nguvu kazi itakayosimamia shughuli zote za chama na kuratibu mchakato mzima wa uchaguzi katika majimbo matatu ya Bunda Vijijini, Bunda Mjini na Mwibara.
CREDIT: MTANZANIA

Wema Sepetu Adaiwa Kuvunja Ndoa ya Esma Platnumz na Petit Man

$
0
0
HALI si shwari kwenye familia ya Kampuni ya Endless Fame Productions kufuatia madai mazito yanayomgusa mkurugenzi wake, Wema Isaac Sepetu akihusishwa na kuvunjika kwa ndoa ya mdogo wa mkali wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ almaarufu kwa jina la Esma Platnumz aliyeolewa na Hamad Manungwa ‘Petit Man’.

Mdogo wa mkali wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ almaarufu kwa jina la Esma Platnumz akiwa na mume wake  Hamad Manungwa ‘Petit Man’ siku walipofunga ndoa.

MAI NDANI
Katika sakata hilo, mtangazaji maarufu Bongo, Maimartha Jesse ‘Mai’, Esma na Mtangazaji Nasra Rajesh ‘Lady Naa’ wanadaiwa kuunda kundi lenye lengo la kuwasuta wezi wa waume za watu (Wema aliwekwa kwenye tageti) lililopewa jina la Al-Shabaab.

Esma Platnumz akiwa na mume wake  Hamad Manungwa ‘Petit Man’.
Wakati mpango huo ukiendelea, Mai anadaiwa alielezea mkasa wa kuvunjika kwa ndoa ya Esma na Petit Man kwenye Instagram huku akimtaja Wema kuhusika kwa mafumbo, jambo lililomfanya staa huyo wa filamu (Wema) aogelee matusi ya kutosha.

MADAI YA WEMA KUHUSIKA
Madai kamili yanamhusisha Wema na uvunjifu wa ndoa hiyo akituhumiwa ‘kuchepuka’ na Petit Man kwa muda mrefu sasa huku mwenyewe akikanusha vikali.

USHAHIDI WA MESEJI
Madai yalizidi kushushwa kwamba, sakata hilo lina ushahidi ikiwa ni pamoja na Esma kubamba meseji zisizo na dalili njema kutoka kwa Wema zikiwa kwenye simu ya Petit Man.
“Ukibahatika kukutana na Esma halafu umkute kwenye ‘mood’ ya kuongea, atakueleza jinsi mume wake alivyokuwa na ukaribu wa kupitiliza kwa Wema. Yawezekana hawakuwahi kuchepuka lakini ukaribu wao ulikuwa wa kupitiliza kiasi cha kuibomoa ndoa hiyo.

SIMU ZA WEMA HADI USIKU WA MANANE
“Esma anadai kuwa kuachana kwake na Petit Man hakuhusiani sana na meseji za Diva (Mtangazaji wa Clouds FM, Loveness Malinzi) kwani hizo zilisherehesha ugomvi wao tu, ila kilichomfanya hadi akaamua kubwaga manyanga ni utitiri wa meseji za wanawake na simu kibao za Wema kumhitaji Petit Man hadi usiku wa manane wakati ni mume wa mtu,” kilidai chanzo hicho.

WEMA ANASEMAJE?
Kufuatia madai hayo, Ijumaa lilimtafuta Wema  alipopatikana alisema: “Mimi nimekuwa nikimsapoti Petit kwenye mambo yake na Esma, sasa kama kuna watu wanasema maneno ya kunifanya nionekane mbaya, hao ni watu wasio na nia njema na mimi.
“Nakaa na Petit kama mwanangu lakini pia ni mfanyakazi wa Endless Fame na Esma sina tatizo naye, zaidi watu wanaibua tu mambo yao. Sipendi kabisa…”
ESMA KIMYA
Esma alipotakiwa kufunguka juu ya madai ya Wema kuhusika kwenye kuvunjika kwa ndoa yake alisema kwa kifupi: “Hilo suala liko kwenye ngazi ya kifamilia, siwezi kuliongelea kwa sasa.”

WEMA AKEREKA
Kufuatia maneno ya kuuma kwenye mtandao aliyokuwa akiendelea kuandika Mai, Agosti 18, Wema alishindwa kuvumilia hivyo kwenda kumripoti kwenye Kituo cha Polisi cha Kijitonyama.
Paparazi wetu aliponyetishiwa ‘ubuyu’ huo wa Wema kulifikisha ‘soo’ hilo polisi, alinyanyua mguu hadi kituoni hapo ambapo alikutana na askari wakiongozana na Wema hadi Mitaa ya Sofani, Kijitonyama ambako kuna duka la Mai lakini hawakumkuta hadi kesho yake (Jumatano asubuni) alipotiwa mbaroni.

MSIKIE MAI
Baada ya Mai kufikishwa kituoni hapo alishikiliwa kwa saa kadhaa akihojiwa na alipotoka na kutakiwa kusema chochote kuhusiana na tukio hilo alisema:
“Huu ni mziki mnene, Wema amechokoza moto.”

PETIT MAN NA ESMA
Katika ndoa yao, Petit Man ambaye ni mmoja wa wafanyakazi wa Endless na Esma wamedumu kwa takriban miaka miwili na kujaliwa mtoto mmoja kabla ya mambo kwenda mrama hivi karibuni.
GPL

Wagombea Rasmi wa Urais ni 8 Tu, Wengine Wahawajakidhi Vigezo Hivyo Wamekataliwa

$
0
0

WAGOMBEA RASMI WA URAIS NI 8 TU, WENGINE HAWAJAKIDHI VIGEZO.
Hatimaye katika vyama 12 vilivyochukua fomu za kugombea urais, ni vyama 8 tu ambavyo wagombea wake wamekidhi vigezo vya kugombea urais mwaka huu Tanzania. Vyama hivyo ni
CCM, CHADEMA, TLD, ADC, CHAUMA, ACT- WAZALENDO, NRA na UPDP.
Wagombea hao 8 na vyama vyao ni
1. John Magufuli (CCM)
2. Edward Lowassa (CHADEMA)
2. Anna Mghwira (ACT)
4. Fahmi Dovutwa (UPDP)
5. Chifu Lutalosa Yemba (ADC)
6. Janken Kasambala (NRA)
7. Hashim Rungwe (CHAUMA)
8. macmillan lyimo (TLP)
Wagombea wa vyama vitatu hawajakidhi vigezo vya kugombea urais wa Tanzania, vyama hivyo ni CCK, DP , TADEA.. Chama cha AFP chenyewe hakijafika kabisa katika ofisi za NEC kuleta fomu zake.

Christopher Mtikila, Chipaka na Malisa Waenguliwa Mbio za Urais.......NEC Yasema Hawajatimiza Masharti. Lowassa,Magufuli WAPETA!!!

$
0
0
Wanasiasa wakongwe nchini, Christopher Mtikila na John Lifa- Chipaka wametupwa nje ya kinyang’anyiro cha kugombea kiti cha urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kutokana na kushindwa kutimiza vigezo vya kisheria.

Mchungaji Mtikila anawakilisha Chama cha Democratic Party (DP) na Chipaka anawakilisha Tanzania Democratic Alliance (TADEA). Vyama vyote hivyo vilianzishwa mara tu Sheria ya Usajili wa Vyama vya Siasa, Na. 11 ya 1992, ilipopitishwa na Bunge la Jamhuri ya Muungano.

Kupitia sheria hiyo, ndiyo ilitolewa ruhusa ya kisheria ya kuanzishwa kwa mfumo wa vyama vingi vya siasa nchini Tanzania. Kabla ya sheria hiyo, masuala ya siasa yalikuwa si katika mambo ya Muungano.

Pigo la kukosa kuteuliwa kugombea urais, pia lilimpata Dk. Godfrey Malisa Kahangwa aliyewakilisha Chama cha Kijamii (CCK), chama kilichoanzishwa miaka michache iliyopita, baada ya uchaguzi mkuu wa 2010.

Akitangaza matokeo ya maombi ya vyama hivyo vitatu jioni hii, Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), Jaji mstaafu Damian Lubuva alisema ombi la Mchungaji Mtikila limekataliwa kwa sababu ameshindwa kuwasilisha tamko la kiapo la Mahakama Kuu, ingawa yeye aliapa lakini mgombea mwenza wake ambaye hakutajwa jina, hakufika na hakuna kiapo chake.

Jaji Lubuva ambaye alifikia ngazi ya jaji wa Mahakama ya Rufaa Tanzania, amesema Dk. Kahangwa hakutimiza idadi ya watu wanaotakiwa katika udhamini na amekosa mgombea mwenza kutoka upande wa Zanzibar.

Kwa Lifa-Chipaka, ilielezwa kwamba hakutimiza vigezo kwa vile alishindwa kuwasilisha orodha ya wadhamini kutoka Zanzibar. kisheria walitakiwa watu 200 wenye kadi za kupigia kura.

Wakati Chipaka amekosa wadhamini Zanzibar, upande huohuo chama hicho kimesimamisha mgombea urais, ambaye ni Juma Ali Khatibu, Naibu Katibu Mkuu.

Mchungaji Mtikila alilalamika mara tu alipotangaziwa uamuzi na Jaji Lubuva, kwamba alicheleweshwa kwa utaratibu tu wa ofisi ya Tume kwani alifika mapema na kuripoti ofisini kwa Mkurugenzi wa Uchaguzi, Kailima Kwemboy.

Mtikila alidai kuwa hakufika na mgombea mwenza wake kwa wakati kwa kuwa amepata tatizo la kuumiwa mkewe na kulazwa chumba cha wagonjwa mahututi na kuamua kuahirisha safari.

“Tulijitahidi hata kumtumia tiketi ya ndege lakini hakuwahi hapa. Hili tatizo ni la asili ambalo mtu analifahamu linaweza kutokea wakati wowote. Lakini mimi nimewahi hapa na jaji alinikubalia kuapa na kushauri nije kukujulisha kuwa mkinipa muda kusubiri kidogo nitakamilisha na kurudia kwake niape na mgombea mwenza akiwa amewasili,” alisema Mtikila katika kilio ambacho hakikuzingatiwa na Tume.

Jaji Lubuva alisema kwa wote walioshindwa kutimiza masharti, maana yake wamekosa kuteuliwa kwa mujibu wa sheria kwa kuwa kwa utaratibu ulioandaliwa, hakuna muda wa kuwasubiri kukamilisha taratibu.

Vyama vilivyofuzu kuteuliwa wagombea wao ni pamoja na Chadema, Edward Lowassa (mgombea mwenza Juma Duni Haji) wanaowakilisha Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA); ACT-Wazalendo Anna Mghwira na mgombea mwenza Hamad Mussa Yussuf na Dk. John Magufuli (na mgombea mwenza Samia Suluhu Hassan) wa CCM.

Kampeni za urais zinaanza rasmi kesho.

Mwanafunzi Kidato cha II Auawa Akimwokoa Mwenzake Asibakwe

$
0
0
Mwanafunzi wa kidato cha pili wa Sekondari ya Nyasubi, Ally Jacob ameuawa baada kuchomwa na kitu chenye ncha kali shingoni alipokuwa akijaribu kumwokoa mwanafunzi mwenzake asibakwe.

Tukio hilo lilitokea juzi saa 9:00 alasiri maeneo ya Nyasubi, Wilaya ya Kahama mkoani Shinyanga. alikuwa akirejea nyumbani kutokea shuleni.

Kamanda wa Polisi mkoani Shinyanga, Justus Kamugisha alidai kuwa mwanafunzi huyo aliuawa kwa kuchomwa na kitu chenye ncha kali sehemu ya shingoni na mwenzake anayesoma Sekondari ya Kishimba.

Kamugisha alisema sababu za Jacob kuuawa ni kujaribu kumsaidia mwanafunzi mwenzake mwenye umri wa miaka 16 (jina linahifadhiwa) ambaye anasoma kidato cha pili Sekondari ya Nyasubi ili asibakwe na mtuhumiwa ambaye alitaka kufanya unyama huo kwa kushirikiana na mkazi mmoja wa Nyasubi.

Alisema watuhumiwa wote wamekamatwa na watafikishwa mahakamani baada ya upelelezi kukamilika.

Lowassa Akwama Kuzindua Kampeni Baada ya Kukosa Uwanja wa Kutosha 'Mafuriko' Yake

$
0
0
Wakati mgombea Urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), John Magufuli, akitarajiwa kuzindua kampeni zake kesho jijini Dar es Salaam, mgombea kupitia Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), Edward Lowassa amekwama kuzindua kampeni zake  kama ilivyotangazwa awali.

Ukawa unaoundwa na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), National Convention for Construction and Reform – Mageuzi (NCCR-Mageuzi), Chama cha Wananchi (CUF) na National League for Democracy (NLD) umeahirisha uzinduzi kutokana na kukosa mahali patakapotosha ‘mafuriko’ ya watu watakaohudhuria.

Lowassa alitarajiwa kufungua pazia kwa kuzindua kampeni zake kwenye Uwanja Mkuu wa Taifa jijini Dar es Salaam, lakini serikali imekataza uwanja huo kutumika kwa kampeni za vyama vya siasa.

Mkurugenzi wa Idara ya Habari (Maelezo), Assah Mwambene, akiongea na waandishi wa habari Jumatano wiki hii, alisema serikali imefikia hatua hiyo kwa vile kusudio la ujenzi wa uwanja huo ni shughuli za michezo pekee na si vinginevyo.

Kampeni zinazoanza kesho  pia zitahusisha wagombea urais kupitia vyama vingine vya siasa vikiwamo ambavyo wagombe wake hawapewi nafasi kubwa ya kuibua ushindani kama itakavyokuwa ama kukaribia kwa CCM na Ukawa.

Pia kuanza kwa kampeni hizi kutawahusisha wagombea ubunge na udiwani watakaoshiriki Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 25, mwaka huu.

Afisa Habari wa Chadema iliyo mshirika katika Ukawa, Tumaini Makene, amesema kuwa, Lowassa anayewania Urais akiwa na mgombea mwenza Juma Duni Haji, ameahirisha kuzindua kampeni zake mpaka itakapotangazwa baadaye.

Alisema kuahirishwa kwa uzinduzi huo kunalengo la kutoa fursa kwa Ukawa kujiweka sawa hasa katika kupata uwanja wenye uwezo wa kuwajumuisha watu wengi na nafasi za kuegesha magari.

“Mgombea wetu hatazindua kampeni leo wala kesho, waache hao wengine waanze sisi tunajipanga kupata eneo zuri litakalotosha kwa idadi kubwa ya watu tunaowatarajia ikiwamo na maegesho ya magari,” alisema.

Makene alisema kutokana na uzeofu uliojionyesha wakati mgombea wao akitafuta wadhamini ama kutambulishwa mikoani, wanaamini kuwa mkutano wao utahudhuriwa na watu wengi, hivyo ni muhimu wakatafuta eneo kubwa la kutosha watu wengi na maegesho ya vyombo vya usafiri.

Wakati ikitarajiwa kuzindua kampeni zake kesho, CCM imeshatangaza kamati ya watu 32 kwa ajili ya kutafuta ushindi, ikiongozwa na Katibu Mkuu wa chama hicho, Abdulrahaman Kinana.

Kamati hiyo ilitangazwa na Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye, Jumanne  wiki hii ambaye alimuita Kinana kama mwanaharakati wa kivita anayefahamu medani za ushindi.

Uchaguzi wa mwaka huu ambao unatarajiwa kuwa na changamoto kubwa hasa kutokana na mgombea anayeungwa  mkono na Ukawa (Lowassa) akitokea CCM, kuonyesha upinzani mkubwa dhidi ya  CCM alichokuwa mwanachama wake tangu mwaka 1977.

Licha ya kuwa mwanachana, Lowassa ameshika nafasi tofauti ndani ya CCM na serikalini ikiwamo Uwaziri Mkuu aliojiuzulu mwaka 2008.

Lowassa alikuwa pia katika timu ya kampeni za mwaka 2005 ambapo Rais Jakaya Kikwete aliwania nafasi hiyo kwa mara ya kwanza na kupata ushindi wa kishindo.

Hata hivyo, Julai 29, mwaka huu, Lowassa aliamua kujiunga na Chadema ikiwa ni siku chache baada ya jina lake kukatwa katika hatua za awali za kuwachuja watia nia waliotaka kuwania Urais kupitia CCM.

Jumla ya makada 42 wa CCM walijitokeza kwenye kinyang’anyiro cha kumtafuta mgombea urais ambapo 38 walirejesha fomu na Magufuli aliibuka kuwa mshindi atakayegombea Urais katika ‘kumrithi’ Rais Kikwete.

Macho na masikio ya wapiga kura wengi kuanzia kesho yataelekezwa kwenye uzinduzi wa kampeni hizo kusikia sera za vyama hivyo vikubwa vinavyoshindana kumpata Rais wa awamu ya tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Serikali Yakanusha Mabasi Yaendayo kasi DART ni ya KICHINA: Ni kiwanda kilicho Assemble Mabasi

$
0
0
Kuna upotoshaji wa Makusudi uliozagaa kwenye Mitandao ya Kijamii kuwa Mabasi Yaliyozinduliwa Tarehe 17/08/2015 kuwa.

1. Ati ni ya Kichina

2. Milango ya kushukia na kupandia Abiria Iko kushoto hivyo hayaendani na Miundombinu iliyojengwa.

HUO NI UZUSHI WENYE LENGO LA KUWAPOTOSHA WATANZANI WALIOCHOSHWA NA MSONGAMANO UNAOONGEZEKA SIKU HADI SIKU

TAARIFA SAHIHI KUTOKA KWENYE MAMLAKA HUSIKA HII HAPA:

1. Kiwanda Kilicho Assemble (Kuunganisha) Mabasi haya kinaitwa Golden Dragon cha China.

2. Aina ya Injini ni CUMMINS ya Marekani (USA)

3. Aina ya Giaboksi ni VOITH ya Ujerumani.

4. Mfumo wa Stelingi ni ZF ya Ujerumani.

5. Mgumo wa Difu ni kutoka Marekani (USA).

6. Aina ya Suspension (Za upepo) Air Suspension kutoka Marekani (USA).

7. Mfumo wa Breki ni WABCO

8. Aina za Mabasi ziko mbili. Articulated Mita kumi na nane almaarufu (Ikarusi) Kutoka Hungary zitakazopita kwenye barabara Maalumu za zege zilizojengwa na Mabaai ya mita kumi na mbili yanayoitwa (Feeder) Mabasi Mlisho yatakayotumia vituo vilivyoko nje ya mfumo Mfano Kituo cha Shekilango, Moroco Hotel, Mwanamboka na Magomeni Mapipa kuwapeleka na kuwaleta kwenye Mfumo.

9. Milango ya kupanda na kushukia Abiria ipo kulia na kushoto ili kukidhi mahitaji ndani na nje ya mfumo ambayo idadi yake ni Minne kila upande ila itatumika mitatu na mmoja niwa dharula kila upande.

10. Urefu kutoka ardhini kwa milango ya kushoto ya Basi ni Sentimita thelathini (30) ambayo hata mtoto anaweza kushuka bila msaada wa mtu mzima.

11. Urefu wa Milango ya kulia ni Sentimita tisini (90) sawa na urefu wa Platform za kila kituo cha DART unaomuwezesha hata mtu mwenye mahitaji maalum Kuingia na kutoka ndani ya basi bila msaada wa mtu.

12. Ndani ya basi kuna eneo la kukaa watu wenye Mahitaji maalum.
Walemavu, Wazee na Mama wajawazito.

13. Mfumo wa ulipaji nauli unafanyika vituoni kama ilivyo kwenye kivuko pale Kivukoni hivyo basi hili halina Kondokta. Makondakta wapo vituoni.

14. Muda wa Safari kutoka Kivukoni hadi kimara ni wastani wa dakika thelathini (30) ikihusisha muda wa kushusha na kupakia kwenye Vituo vya DART.

15. Ni marufuku kwa chombo ama mwananchi kutumia barabara maalum za Mabasi. Wananchi watumie maeneo yaliyotengwa maalum kulingana na mahitaji. Watumiaji wa Bodaboda wanatakiwa kupita kwenye barabara zinazotumiwa na magari ya Kawaida na siyo eneo lililotengwa kwa ajili ya Watembea kwa Miguu.

HIZI NDIZO TAARIFA MUBIMU NA RASMI KWA WATANZANIA
Viewing all 104701 articles
Browse latest View live




Latest Images