Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104747 articles
Browse latest View live

Aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani, Lawrence Masha Aachiwa Kwa Dhamana

$
0
0

Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imemuachia huru aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani nchini, Lawrence Masha (45) baada ya kukamilisha masharti ya dhamana.

Masha alifikishwa mahakamani hapo jana nyakati za saa 6:49 mchana na kuhifadhiwa mahabusu na ilipofika saa 9:31 alasiri alipelekwa mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Waliarwande Lema kwa ajili ya kukamilisha masharti ya dhamana.

Masha aliachiwa huru baada ya nyaraka za wadhamini wake wawili wanaoaminika ambao kila mmoja alisaini bondi ya Sh 1milioni kuhakikiwa na Wakili wa Serikali, Wankyo Simon kuithibitishia mahakama kuwa nyaraka hizo ni halali.

Kufanyika kwa uthibitisho huo wa nyaraka za wadhamini ndio uliopelekea jana Masha kupelekwa mahabusu katika gereza la Segerea.

Baada ya kumaliza kukamilisha taratibu hizo za dhamana ilipofika saa 9:46 alasiri Masha, mkewe, mawakili wanaomtetea katika kesi hiyo, Peter kibatala na Albart Msando pamoja na ndugu zao wengine waliondoka mahakamani hapo kwenda nyumbani.

Awali Agosti 25, 2015 Masha alipandishwa kizimbani akikabiliwa na shtaka la kutumia lugha ya matusi kwa maofisa wa Jeshi la Polisi.

Masha aliyekuwa amevaa tisheti jeusi, suruali ya jinsi ya rangi ya Bluu na viatu aina ya Sendo anadaiwa kuwa Agosti 24,2015 katika kituo cha polisi cha Osterbay alitoa lugha ya matusi kwa maofisa wa jeshi la polisi.




KIMENUKA! Wananchi Ambao Ndio Wapiga Kura Wamtaka Rais Mstaafu Benjamin Mkapa Aombe Msamaha

$
0
0
MUUNGANO wa wapiga kura Tanzania (TANVU), umeiomba Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) kumchukulia hatua, Rais Mstaafu, Benjamin Mkapa, kwa kitendo alichokifanya kuvitukana vyama vya upinzani kwa kuwaita viongozi na wanachama wake malofa, vibaka na wapumbavu.

Kauli ya TANVU inakuja ikiwa ni siku chache baada ya Mkapa kutoa maneno ya kuvihadaa vyama vya upinzani wakati Chama cha Mapinduzi (CCM) kilipokuwa kinazindua kampeni za uchaguzi mkuu uliofanyika kwenye viwanja vya Jangwani, Dar es Salaam.

Pia muungano huo umekipatia CCM muda wa siku saba kuanzia leo kuwaomba radhi watanzania kwa kutumia Shirikisho la vyama vya watu wenye ulemavu nchini (SHIVYAWATA) kwenye uzinduzi wa kampeni hizo huku kikitambua ni makosa kisheria kwa vyama vya siasa kutumia Taasisi zisizokuwa za serikali kwenye kampeni za uchaguzi.

Kauli hiyo ya TANVU imetolewa leo jijini Mwanza na Rais wake, Militon Lutabanana wakati akizungumza na wandishi juu ya hali ya kisiasa nchini, demokrasia na kuelekea kwenye uchaguzi Mkuu wa mwaka huu.

Amesema hatua ya SHIVYAWATA kushiriki kwenye uzinduzi wa kampeni za kisiasa za CCM ni makosa kwa kuwa kwa mujibu wa sheria za nchi taasisi yoyote isiyo ya serikali hairuhusiwi   kujiingiza kwenye shughuli za kisiasa.

“Kwa kitendo hicho wote wanamakosa CCM na SHIVYAWATA lakini kama CCM haitaomba radhi tutatoa tamko lingine ambalo sisi kama muungano wa wapiga kura nchini hatupendi tufike huko,” amesema na kuongeza.

“Tunaiomba Tume ya Taifa ya Uchaguzi itende haki kwa kumchukulia hatua stahiki Rais Mkapa kama ambavyo jana tumeshuhudia aliyewahi kuwa waziri wa mambo ya ndani ya nchi Laurence Masha alivyoshughulikiwa,” amesema.

Amesema wapiga kura hawahitaji kusikia matusi wala vijembe kutoka kwa wagombea, viongozi au wanachama wa vyama vya siasa wanachotaka kusikia ni sera za vyama hivyo vya siasa na sio vinginevyo.

“Tunawaomba makada wa CCM waache kuendesha kampeni kwa mabavu, Magufuli (John) hatuna tatizo naye tunamshauri asikubali kuombewa kura na watu wanaotumia matusi,” amesema.

Aliongeza kuwa kitendo cha Rais Mkapa kutoa lugha za matusi kitamharibia mgombea wa CCM na kumpunguzia idadi ya kura kwa kuwa yeye alikuwa kama mdhamini wake kwa wapiga kura.

Baada ya Kunyimwa Uwanja wa Jagwani..Ukawa Yapata Piga Jingine..Serekali Yawapiga Marufuku Matumizi ya Helkopta Kwenye Kampeni

$
0
0
  1. UTANGULIZI
    1. Tangazo hili linatolewa kwa lengo la kutoa mwongozo kwa watoa huduma za helikopta, marubani wake na umma kwa ujumla kuhusiana na hatua za kiusalama zinazopaswa kuzingatiwa inapolazimika kutoa huduma ya usafiri wa helikopta hapa nchini, hususan, maeneo ya mbali (vijijini) ambapo huduma za uongozaji ndege hazipo au sio maeneo maalum yaliyotengwa kwa ajili ya helikopta kutua (mahsusi kwa helikopta au viwanja vya ndege kwa ujumla). Tangazo hili limetolewa baada ya Mamlaka kugundua kwamba kumekuwa na matumizi mabaya ya huduma hizi kinyume na kanuni za usafiri wa anga nchini na weledi unaozingatia taratibu za kitaaalamu na miongozo katika usafiri wa anga.
      .
    2. Mamlaka inatambua kwamba matumizi ya helikopta wakati wa kampeni za uchaguzi mkuu wa mwaka 2015 yanatarajiwa kuongezeka na kuna uwezekano wa kuleta athari za kiusalama kwa maisha ya watu na mali pamoja na watumiaji wa vyombo hivi. Pia vitendo vya kuning’iniza vitu kama mabango ya matangazo mbalimbali kwa kutumia ndege (helikopta ikiwemo) yanaweza kuleta hatari endapo sheria na taratibu zinazohusiana na matumizi hayo hazitazingatiwa.
    3. Tangazo hili linatolewa kwa mamlaka aliyopewa Mkurugenzi Mkuu chini ya Sheria Namba 80 ya Usafiri wa Anga na kanuni zake zinazohusiana na masuala ya usafiri wa anga nchini zilizowekwa kwa lengo, hususan, kuhakikisha usalama katika matumizi ya vyombo vya usafiri wa anga sambamba na kulinda usalama wa umma na mali wakati wa matumizi ya vyombo husika.
    4. Watoa huduma za usafiri wa helikopta au ndege na marubani wake wanaokodishwa kutoa huduma wakati wa kampeni, na mtu yeyote anayetarajiwa kutumia huduma hiyo wanakumbushwa kuhakikisha wanazingatia kanuni za usafiri wa anga na ikibidi kuomba kibali kutoka kwa Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania. Kanuni zinapatikana kupitia tovuti yetu kwa anuani ya:www.tcaa.go.tz; na endapo utahitaji maelezo ya ziada au miongozo zaidi usisite kuwasiliana na Mamlaka.
  2. CHETI CHA NDEGE KWA USALAMA WA KURUKA – AIRWORTHINESS CERTIFICATE
    1. Helikopta yeyote itakayotoa huduma katika kampeni za kisiasa lazima iwe ina cheti halisi cha usalama wa kuruka kilichotolewa na mamlaka husika ya helikopta ilikosajiliwa. Kwa hapa nchini cheti hicho ni lazima kiwe kimetolewa na Mamlaka ya Usafiri wa Anga. Na cheti hicho ni lazima kiwe kimetolewa kwa ajili ya helikopta yenye usajili na mahsusi kwa kazi ya kubeba abiria ambayo inaweza kutumika kwa shughuli nyingine zozote. Kwa tangazo hili helikopta nyingine yeyote ile isiyokuwa na sifa hiyo haiwezi kutumika kufanya biashara ya usafiri wa abiria katika kampeni.
    2. Endapo helikopta itakuwa ina usajili wa nje ya Tanzania, mtu anayetarajia kuitumia hapa nchini ni lazima apate kibali cha kuiingiza nchini na kuitumia kwa usajili wa nchi iliyotoka kama ilivyoainishwa katika Waraka wa Mamlaka unaoainisha taarifa za usafiri wa anga – Aeronautical Information Circular (AIC 08/09). Hakikisha unapoomba kibali uwe umekidhi vigezo vya waraka huu ikiwa ni pamoja na kuwasilisha nakala za nyaraka zinazopaswa kuwasilishwa zikiwemo cheti cha usajili wa ndege, cheti cha ndege kwa usalama wa kuruka, cheti cha leseni za radio za ndege, cheti cha bima, makubaliano/mkataba wa kukodisha ndege hiyo, utaratibu wa kufanya matengenezo ya ndege hiyo, leseni za marubani, na ushahidi wa karibuni wa matengenezo ya ndege hiyo.
  3. TARATIBU ZA USALAMA WA UENDESHAJI
    1. Mahitaji ya jumla ya kiuendeshaji

      Matakwa ya marubani na uendeshaji unatakiwa kufuata maelekezo husika yaliyomo kwenye Kanuni inayohusiana na uendeshaji, yaani, The Civil Aviation (Operation of Aircraft) Regulations. Rubani Mkuu anawajibika kuhakikisha kwamba vituo vya Mamlaka vya kuongoza ndege vinavyohusika katika eneo atakalokuwepo au kwa utaratibu wa uongozaji ndege, wanakuwa na taarifa za mpango wake mzima wa safari husika kwa siku au wakati husika.

      Njia itakayotumiwa na rubani izingatie matakwa ya kuepuka kuruka chini ya kiwango cha umbali unaotakiwa hasa katika maeneo yenye watu wengi yakiwemo maeneo yaliyopangwa kufanyika kwa mikutano husika.

      Tahadhari ni lazima zichukuliwe wakati wa kuelekea kutua, kutua kwenyewe na hata wakati wa kuondoka, hasa ikizingatiwa kuwa kuna uwezekano wa wananchi kuikimbilia helikopta au eneo la utuaji. Katika hali yeyote ile rubani hapaswi kutumia chombo chake kukusanya wananchi kwa ajili ya mkutano au kuitumia kwa utaratibu wowote mwingine kinyume na matakwa ya kiurukaji kwa ndege husika.
    2. Usalama wa eneo la kutua na kuruka

      Maeneo yote yatakayotumika kwa ajili ya kutua ama kuruka ni lazima yafahamike mapema. Maeneo ya kuruka ama kutua ni lazima yawe mbali na eneo mkutano utakapofanyika ili kuweza kutoa eneo salama kwa ajili ya kuruka ama kutua kutoka katika mikusanyiko ya watu.

      Maeneo ambayo yatatambuliwa kama ni ya kuruka ama kutua hasa yale ambayo hayajatambulika kisheria kwa kufanyia shughuli hiyo ni lazima yawekewe alama maalum na uzio ili kuzuia watu wasiohusika kusogelea eneo hilo.

      Eneo husika ni lazima lilindwe; rubani mkuu ahakikishe helikopta itakayokuwa imetua eneo hilo inalindwa dhidi ya uvamizi kutoka kwa watu wasiohusika. Hatua maalum za kiulinzi ni vyema kuchukuliwa endapo kutakuwa na ulazima wa chombo hicho kulala katika eneo husika usiku mzima. Kila wakati rubani anapotaka kuruka ni vyema ahakikishe amekagua chombo chake kwa mujibu wa taratibu zinazohusika kwa umakini kabla ya kuanza safari.
    3. Usiamizi wa Chombo kikiwa ardhini na usalama kwa umma

      Mtu mwenye wajibu wa usimamizi wa chombo kikiwa ardhini lazima awe ni mwenye mafunzo ya kutosha na awe anajua madhara yanayoweza kusababishwa na mapanga ya helikopta yanapozunguka. Kwa marejeo zaidi kuhusiaha na hilo tafadhali zingatia yaliyomo kwenye Waraka wa Mamlaka AIC33/2000 unaoelezea masuala ya madhara yanayoweza kusababishwa na mapanga ya helikopta yanayozunguka.

      Ni wajibu wa Rubani mkuu na mhusika aliyekodisha helikopta kuhakikisha wananchi wanakuwa salama na mbali na helikopta. Matumizi ya kizembe na yasiyo ya kiweledi ya helikopta yatakayohatarisha usalama wa wananchi yatachukuliwa kama ukiukwaji wa kanuni za usafiri wa anga na Mamlaka itawachukulia hatua kama ilivyoanishwa kwenye kanuni hizo.
    4. Kuchukua na kuangusha vitu ardhini na kupeperusha mabango angani

      Huduma hizi zinaweza kufanywa na helikopta na hata ndege zingine za kawaida. Kabla ya kufanya shughuli za namna hiyo, mmiliki wa chombo ni lazima ahakikishe anakidhi vigezo vya Kanuni za Usafiri wa Anga kwa huduma hizi, yaani, The Civil Aviation (Aerial Work) Regulations na pia awe amepatiwa kibali kutoka Mamlaka ya Usafiri wa Anga kwa kazi hiyo. Mmiliki wa ndege yeyote anayefanya shughuli za namna hii bila ya kuzingatia vigezo vya Kanuni hizi atachukuliwa hatua.
    5. Kutoa taarifa za matukio

      Rubani Mkuu ni lazima aandike taarifa ya matukio na kuiwasilisha Mamlaka ya Usafiri wa Anga kama ilivyoanishwa kwa mujibu wa kanuni za usafiri wa anga hususan, kanuni za 52, 74,75 na 76 zilizomo kwenye Kanuni ya The Civil Aviation (Operation of Aircraft) Regulations. Wananchi nao wanatakiwa kutoa taarifa ya tukio lolote waliloliona hatarishi kwa mujibu wa kanuni namba 262 ya Kanuni iliyotajwa.

      Mamlaka itafuatilia na kuchunguza taarifa inazozipokea na kuchukuwa hatua stahiki ili kuhakikisha kuwepo kwa usalama wa kiuendeshaji, watu na mali.
  4. HITIMISHO
    Ili kulinda usalama wa wananchi, wamiliki na marubani wote wanapaswa kuhakikisha wanazingatia Sheria ya Usafiri wa Anga pamoja na Kanuni zake. Rubani anayeendesha chombo ni lazima ahakikishe anatumia weledi wa hali ya juu katika matendo yake.

    Mamlaka inawahakikishia wananchi/umma kwa ujumla kwamba haitosita kuchukuwa hatua stahiki kama zilivyoanishwa kisheria na kanuni za usafiri wa anga iwapo mapungufu ya usalama yatajitokeza.
Imetolewa na
Charles M. Chacha
Kaimu MKURUGENZI MKUU
MAMLAKA YA USAFIRI WA ANGA TANZANIA

Ni zamu ya Nay wa Mitego kaonesha kumsupport Mgombea wa Urais 2015…

$
0
0
Mwaka huu ni headlines za Uchaguzi 2015 tumeona baadhi ya wasanii wameonesha kutoa support kwenye kipindi hiki kwa wagombea Urais wawili ambao ni John Pombe Magufuli atakaegombea CCM na Edward Lowassa kupitia CHADEMA.

Miongoni mwa wasanii waliojitokeza na kutangaza rasmi kumsupport mgombea Urais kupitia CCM, Dkt.John Pombe Magufuli, kuna Wema Sepetu, Batuli, Snura, Linex, Steve Nyerere, Diamond Platnumz, Shetta, Barnaba,Bushoke, Kysher, Wastara na wengineo huku mwigizaji Aunty Ezekiel na Jackline Wolper wanamsupport Edward Lowassa na sasa ni zamu ya Nay wa Mitego.

Nay wa Mitego anamsupport Edward Lowassa kayaandika haya….>>>>Huwezi zuia Mvua ikiamua kunyesha inanyesha tu! Tuna Imani na Lowassa. Ccm wote bado wana Imani na Lowassa hata Kura za Urais ni kwa Lowassa.Nilikua sipost chochote coz Nilikua nataka nisikie CCM labda wana jipya juu ya sera yao mwaka huu coz upinzani umekua mkali, wangenishawishi kidogo. Dooh ndo wameongeza uozo mara dufu.Watanzania wameamka si kwa uongo ule wa jana 😂😂 Milioni Hamsini kila Kijiji. Tanzania ina vijiji vingapi? Piga Hesabu ya haraka kadilia, si chini ya bilioni 600 na zaidi.Watanzania sio mazoba kiasi hicho tumeshtuaa…Hamjajipanga mwaka huu mmetukosa..#Mabadiliko2015


Hatimae Polisi Kutoa Tamko CCM Kuzidisha Muda wa Kampeni Baada ya NEC Kudai ilikuwa Kazi yao Kuwazuia CCM

$
0
0

Kamishna wa operesheni mafunzo wa Jeshi la Polisi nchini Paul Chagonja
Jeshi la Polisi nchini Tanzania limesema kuwa litatoa tamko la jeshi hilo juu ya Chama cha Mapinduzi kuzidisha muda wakati wa Uzinduzi wa Kampeni za chama hicho wiki iliyopita.

Akizungumza na waandishi wa habari wakati wa mdahalo wa wadau wa uchaguzi leo jijini Dar es salaam Kamishna wa Mafunzo na Operasheni wa Jeshi la Polisi CP Paul Chagonja amesema kuwa wanashughulikia suala hilo na muda ukifika watatoa tamko.
Ameongeza kuwa ili uchaguzi uwe wa Amani ni lazima watu wote watimize wajibu wao.
Kwa upande wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi iliwakilishwa na Jaji Mstaafu John Mkwawa amevitaka vyama vya siasa kuzingatia maadili ya uchaguzi waliosaini ili kulinda amani na kuepusha migogoro na uvunjifu wa Amani.
Kwa upande wa mwakilishi toka chama cha ADC Mwanaisha Yemba amevitaka vyama vyenye vikundi vya ulinzi kuwapa sare na alama maalum walinzi wao ili watambuliwe na kila mtu ili wakifanya vujo iwe rahisi kutambulika.

Sheddy Clever: Nimelipwa pesa nyingi sana kutayarisha wimbo wa Diamond na Ne-Yo

$
0
0
Producer Sheddy Clever wa Burn Records amesema kuwa amepata pesa nyingi alizolipwa na Diamond kutengeneza collabo yake na Ne-Yo, kiasi ambacho ingemchukua miezi mitatu kuipata kwa kazi zake za kawaida za production.

Sheddy ambaye ndiye producer anayepika collabo ya Diamond na Ne-Yo inayosubiriwa kwa hamu na mashabiki wa muziki wa Afrika, ameiambia Bongo5 kuwa hajawahi kulipwa kiasi hicho cha pesa toka ameanza kufanya production.

“Hii kazi tuliyoenda kufanya juzi nimelipwa, na nimelipwa vizuri tu…sijawahi kulipwa hivyo kwakweli yaani nafurahi sana,” alisema kwa furaha.

“Diamond ni msanii tofauti sana na haogopi kuwekeza katika kazi zake kwasababu anajua nini anachokifanya…Nimelipwa vizuri japokuwa kazi bado sijamaliza lakini nimelipwa pesa nyingi tu nzuri nimefikia hoteli nzuri.” alisema Sheddy.

Sasabu wengi huwa hawapendi kusema kiwango wanacholipwa, nilipomuuliza kama amelipwa zaidi ya shilingi milioni 1 alijibu;
Sheddy:[kicheko] Inazidi milioni 1 hata milioni 3 inazidi kabisa nimelipwa vizuri

Nikaendelea kumuuliza kama amelipwa zaidi ya shilingi milioni 5?

Sheddy:[kicheko na kigugumizi] labda nisiongelee sana hilo ila nimelipwa pesa nyingi kwakweli nisiwe muongo wala nisiwe mnafiki, mwenyezi Mungu ananiona hata kama nikiongea uongo nimelipwa pesa nyingi SANA (akasisitiza) kiasi cha kwamba ninaweza nikakaa studio kwa muda hata wa miezi miwili au mitatu ndo nikaipata pesa hiyo lakini nimeipata kwa kazi moja na kazi bado sijamaliza na kuwakabidhi bado sijawakabidhi.

Kizazaa cha fedha za Kampeni Lowassa, CHADEMA na UKAWA

$
0
0
Kwa mujibu wa habari nyeti nilizotonywa sasa hivi kuna kizazaa cha fedha za kampeni zinazowafanya
Lowassa, Chadema na UKAWA kwa ujumla kuwa katika mtafuruku mkubwa na mpaka sasa uliopelekea kuchelewa kuanza uzinduzi wa kampeni ya Urais wa ukawa.

Vyama vinayounda UKAWA vinasema Lowassa aliahidi kuwa atatowa fedha zote za kampeni kwa hiyo wao wasiulizwe. Lowassa anasema alizotowa zinatosha (hasemi katowa kampa nani na za nini), Chadema nao wanavunga kuwa mpaka sasa akaunti ya kutowa kiasi kikubwa cha fedha ni lazima saini ya Katibu Mkuu iwepo na Katibu Mkuu wa chadema alipofatwa kusaini yeye kagoma ( huu ni ungo wa chadomo) wanasema eti Katibu Mkuu wao anataka kwanza taratibu za kubadili saini yake zikamilike kama watatowa fedha watowe wenyewe akikamilisha zoezi la kubadili kuwa ndiyo anawakwamisha.

Kizungumkuti kinaendelea wakati marafiki matajiri waliokuwa wanampa fedha azitakazo Lowassa wameona mambo yanakuwa magumu na badala ya fedha wameanza kumpa ahadi za kesho, kesho, kesho huku wakitazama upepo unapovuma.

Kuna habari nyingine kuwa kuanzia jana kuna ng'ombe zaidi ya 3,000 wanapakiwa wapelekwe sokoni kutoka kwenye ranchi moja kubwa sana iliyopo huko Handeni, sijuwi nayo inahusiana na Lowassa?

Kwa mujibu wa mtonyaji wangu anasema, Ndesamburo nae kagoma kutowa fedha, anasema Lowassa aliahidi atatowa fedha zote za kampeni yake yeye mwenyewe kwa hiyo asiulizwe yeye.

Mzee Mtei yupo mbioni kuwasiliana na Lowassa, Lowassa hapatikani kwa muda mrefu kwenye simu

Jamii Forums-Written By FaizaFoxy

Baba Diamond Akataliwa Kumuona Mjukuu wake Tiffah

$
0
0
Baba mzazi wa mwanamuziki huyo, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’, Abdul Jumaa ‘Baba D’.
MSHTUKO! Baada ya hivi karibuni staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ kupata mtoto wa kike, Latifah Nasibu ‘Princes Tiffah’ kupitia kwa mwandani wake, Zarinah Hassan ‘Zari The Boss Lady’, baba mzazi wa mwanamuziki huyo, Abdul Jumaa ‘Baba D’ amekataliwa kumuona mjukuu wake huyo, Risasi Mchanganyiko lina habari kamili.

ILIKUWAJE?
Kwa mujibu wa baba Diamond, baada ya Tiffah kuzaliwa Agosti 6, mwaka huu, mama mzazi wa nyota huyo, Sanura Kassim a.k.a Sandra alimpigia simu mzazi mwenzake huyo na kumjuza kwamba wamepata mjukuu, jambo ambalo walilifurahia kwa pamoja.

Wakiwa katika mazungumzo hayo kwenye simu, baba Diamond alimuuliza kuhusu sura ya mtoto kama kweli ni wa kwao au siyo kama tetesi zinavyozagaa kwamba siyo wao ambapo alihakikishiwa na mama huyo kuwa Tiffah ni damu yao kwani anafanana na mtoto wao Diamond hasa mdomo.

BABA DIAMOND AFURAHIA
“Nilifurahi sana nilipopigiwa simu na mama Diamond na kuniambia tumepata mjukuu tulipongezana, pia nikamuuliza kuhusu wasiwasi wa kwamba siyo damu yetu kama wengi wanavyodai ambapo alinihakikishia kwamba ni damu yetu,” alisema baba Diamond.

AKATALIWA KUMUONA, APIGWA CHANGA
Baba Diamond alifunguka kuwa, wakiwa wanaendelea na mazungumzo, alimtaka mzazi mwenzake huyo amwelekeze nyumbani ili akamuone mjukuu wake, Tiffah lakini mama D alimpiga ‘changa la macho’ na kumwambia hawapo wameshasafiri kwenda nchini Afrika Kusini ‘Sauz’.

“Niliumizwa sana na maneno hayo kwani yalionesha wazi kwamba, mama D hataki niende kumuona, kwani nyombo vya habari kila siku vinaripoti kwamba Zari na mwanaye wapo hapa Bongo lakini nikaona isiwe shida nikapiga kimya tu,” alisema baba Diamond.
Hata hivyo, baba D alisema kuwa, kutokana na kupigwa changa hilo la macho, hakuweza kwenda kwani hajawahi kufika hata nyumbani kwa Diamond alikohamia huko Madale-Mivumoni jijini Dar na anaona sawa tu kwani hana la kufanya.

UKWELI NI HUU
Kwa mujibu wa mtu wa ndani kwenye familia ya Diamond, ukweli ni kwamba, Zari na mwanaye Tiffah mpaka sasa wako nyumbani kwao na hawajasafiri kwenda Sauz kama alivyoelezwa baba

Diamond mwenyewe hakuweza kupatikana kuzungumzia jambo hilo kwani muda wote simu yake ya mkononi haikupatikana hadi tunakwenda mitamboni.
Source:Globalpublishers

Siasa yamtia Akili Baby Madaha..Amekata Shauri Kuachana na Skendo na Utoto ili.........

$
0
0
Baby Madaha Katika Pozi
BAADA ya kushuhudia wasanii wenzake wakijiingiza katika siasa na kuanguka, staa wa muziki na filamu, Baby Madaha ametia akili na kusema sasa atatulia kwani ni imani yake siku moja atajiingiza katika jukwaa hilo.

Alisema sasa ameamua kuachana na maisha ya skendo za kila siku kwani aliumizwa sana na madai ya kutumia dawa za kulevya, kitu kilichomuumiza hadi mama yake mzazi.

Ninajiandaa kuwa kiongozi wa kisiasa miaka ijayo, unajua hata wenzetu walioingia kugombea uongozi wa siasa na kushindwa, ilichangiwa na historia ya maisha yao ya kisanii, sisi ni watu wa skendo tu, nimejifunza kitu kutokana na hilo, nimeamua kuacha utoto, sitaki tena skendo,” alisema Baby Madaha.
Source:Globalpublishers

Magufuli Apata Wakati Mgumu Kuwanadi Wabunge

$
0
0
Mgombea wa urais kupitia CCM, Dk John Magufuli ameanza kuonja shubiri ya kuwanadi baadhi ya wabunge wa chama hicho baada juzi, akiwa Kalambo mkoani Katavi, baadhi ya wananchi kuguna pale alipompandisha jukwaani mgombea ubunge wa jimbo hilo, Josephat Kandege.

Baada ya kuona hali hiyo, Dk Magufuli alisema: “Nawaombeni jamani, hatuchagui malaika, kila mtu ana tatizo lake. Inawezekana wengine mmechoka hata kumwangalia, lakini mkitaka mimi nifanye kazi vizuri nileteeni huyu bwana,” alisema akimnadi mgombea huyo.

Kwa nyakati tofauti tangu aanze kampeni mikoani, mgombea huyo amekuwa akiwaambia wananchi kuwa baada ya kumchagua yeye, wawachague wabunge hao na kuwasamehe makosa yao ili apate urahisi wa kuunda Serikali na kuleta maendeleo.

Alisema anatambua wakati wa mchakato wa kura za maoni, kulikuwa na wagombea wengi wa ubunge lakini wananchi wasife moyo kwa sababu kuna kazi nyingi za kufanya iwapo atachaguliwa kuwa rais.

Ili kumaliza kabisa miguno iliyokuwapo, Dk Magufuli alimwita mmoja wa waliokuwa wagombea wa ubunge ili kuwaeleza kuwa anamuunga mkono Kandege na alipopanda jukwaani na kusalimia wananchi walimshangilia kwa nguvu.

Akiwa Sumbawanga Mjini juzi, Dk Magufuli alimnadi mgombea ubunge wa jimbo hilo, Aeshi Hilaly kwa kumuita jembe huku akiwataka wananchi “wampigie tena kura hata kama amewakosea.”

“Nimesema hatuchagui malaika kila mtu ana kasoro zake. Tuache kasoro, tuangalie maendeleo. Nataka Sumbawanga muwe maalumu mkinichagulia huyu (Aeshi),” alisema Dk Magufuli wakati akihutubia katika Uwanja wa Nelson Mandela juzi.

Katika Jimbo la Kwela – Rukwa, aliwataka wananchi wamsamehe mgombea ubunge, Ignas Malocha kwa makosa aliyowatendea na kuwa atafanya kazi vizuri kwenye utawala wake.

“Msianze kugombana baadaye mkakosea kwa kumchagua mtu mwingine kwa sababu nahitaji mtu atakayeniambia shida katika wilaya yake.
 
"Hatuchagui malaika ndugu zangu, hatuchagui sura, hata mimi sura yangu ni mbaya sana na nywele zinatoka lakini Watanzania wamenichagua,” alisema Dk Magufuli akiwa katika Kijiji cha Laela.
 
“Tumsamehe, tumjaribu afanye kazi mimi nikiwa rais tuone kama hatafanya kazi vizuri.”

Kauli hiyo ya kumnadi Malocha ilijitokeza tena alipokuwa Kata ya Lusaka aliposema wampigie kura hata kama amewakosea, wamsamehe ili apate kiunganishi kwani asipopita atashindwa kufanya kazi.

“Wewe nenda tu hata kama humpendi fumba macho lakini umpigie nani?” aliuliza Dk Magufuli na kujibiwa “Malochaaa”

Baadhi ya wakazi wa Laela walimwambia mwandishi wetu kuwa wanampenda Dk Magufuli lakini Malocha hajawatekelezea ahadi nyingi alizotoa.
 
Akiwa katika Jimbo la Momba mkoani Mbeya, Dk Magufuli alimpigia kampeni kwa muda mrefu mgombea wa CCM, Dk Lucas Siame na madiwani wa eneo hilo na kuwataka wananchi wasifanye makosa safari hii, bali wachague chama tawala.

Akihitimisha ziara yake mkoani Rukwa, Dk Magufuli aliahidi kuanzisha mamlaka maalumu ya kusimamia masilahi ya polisi.

Akizungumza na wakazi wa Mji wa Laela, Dk Magufuli alisema anataka kuboresha masilahi ya askari ili waache vitendo vya rushwa na kudhibiti wimbi la majambazi na wizi... “...unamwona huyo ofisa amekonda kama mimi ni kwa sababu anafanya kazi,” alisema Dk Magufuli huku akimwonyesha mmoja ya polisi waliokuwapo mkutanoni hapo.

Alisema atawaongezea mishahara hata wafanyakazi wengine ili waweze kufanya kazi kwa ufanisi na kuondoa vitendo vya kutamani rushwa na kuwaonea wanyonge.

Tofauti na siku tatu zilizopita, msafara wa mgombea huyo ulisimama mara nyingi kusalimia wananchi, hasa baada ya baadhi ya wanavijiji kufunga barabara ili awasalimie.

Hata hivyo, aliposimama katika Kijiji cha Ndalambo wilayani Momba jana, kilizuka kikundi cha vijana wasiozidi 40 na kuanza kunyoosha vidole kwa alama ya V inayotumiwa na Chadema na wakati Dk Magufuli akiendelea kumwaga sera kikundi hicho kiliendelea kupiga kelele na kupinga baadhi ya ahadi kuwa hataweza kuzitekeleza huku wengine wakisema “Lowassa, Lowassa.”

Hata hivyo, mgombea huyo hakuwajali na kuendelea kuwahutubia waliokuwa wakimsikiliza na kumshangilia hasa aliposema ataunda Serikali na kuleta maendeleo ambayo hayatabagua watu kwa itikadi za vyama, dini, makabila wala mahali watokako.

Katika eneo la Tunduma alipata mapokezi makubwa hadi akasema: “Mapokezi haya ni ya hatari, ni tsunami. Kama ni ya namna hii leo nitalala kwa raha.”

Updates: Mkutano wa Edward Lowassa na wanawake wa DSM kutoka Ukumbi wa Millenium Tower

$
0
0
Kama tulivyowatangazia jana rais matarajiwa wa awamu ya tano Kamanda mpambanaji asiyechoka na mzee wa maamuzi magumu Edward Ngoyai Lowassa atalihutubia Taifa kupitia wanawake wa mkoa wa Dar es Salaam.

Waziri Mkuu huyo mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania anatarajiwa kusikiliza kilio cha wanawake wa Tanzania na atatoa mwelekeo wa UKAWA kwa wanawake na Taifa kwa ujumla baada ya kushika dola mwezi Oktoba.

Mkutano huo unatarajiwa kuanza rasmi saa 8 mchana na utarushwa moja kwa moja na kituo bora cha Televsheni Tanzania cha ITV.

Kati ya wanaotarajiwa kuhudhuria ni wanawake wajasiriamali,mama ntilie,wafanya usafi,akina mama wa nyumbani,wanaoishi katika mazingira magumu,wenye ulemavu na waliojariwa kwenye sekta rasmi na isiyo rasmi.

Mgombea huyo wa Urais kupitia UKAWA atakutana na wanawake hao ikiwa ni siku moja tangu serikali ya CCM kumpiga marufuku kukutana na wafanyabiahsra mbalimbali masokoni,wagonjwa mahospitalini na pia kumzuia kupanda daladala.

Wakati Lowassa akitendewa hayo mgombea mwenza wa CCM Samia Suluhu amekuwa akisindikizwa na polisi kutembelea wagonjwa mahospitalini na ni juzi tu alikuwa katika hospitali ya HUruma Mkuu Rombo ambapo alikutana na wagonjwa na wafanyakazi wa hospitali hiyo na kusababisha shughuli katika hospitali hiyo kusimama kwa zaidi ya saa tatu.

Timu ya wanahabari wa UKAWA imeshafika hapa Ukumbini na tunatarajia kuwaletea kila kitakachojiri kabla na wakati wa mkutano.

Karibuni..

UKAWA Mnaniharibia Mwanangu, Nakosa Raha Nyumbani Kwangu Mwenyewe

$
0
0
Kila nikitaka kwenda nyumbani kwangu,nasitasita. Natafakari namna na kujibu mapigo ya mpigo toka kwa mwanangu. Kijana wangu huyu aliye Chuo Kikuu,akiwa likizoni sasa,ananitambia na kunibeza katika nyumba yangu mwenyewe.

Najuta kumpa uhuru wa kidemokrasia tangu akiwa Shule ya Msingi. Kila akiniona ananitambia kuhusu UKAWA na kukwama kwetu kama CCM.

Nimejaribu kumwambia kuwa mimi sipo tena kwenye kampeni za CCM. Bado ananing'ang'ania. Ananibakisha CCM na kunihusisha moja kwa moja na kampeni za wagombea wetu kuanzia Dr.Magufuli, Mama Samia, wale wa Ubunge na Udiwani.

Nyumba yangu mwenyewe imegeuka uwanja wa tambo na vikumbo vya kikampeni. Yeye amejipambanua kuwa ni mfuasi wa UKAWA kupitia CHADEMA.

Leo, ameshanipigia simu kujiproud kuwa Lowassa anaibomoa ngome ya CCM pale Millenium Towers. Anadai kuwa Lowassa atawateka wanawake wa Tanzania na kuifanya CCM ibaki na wazee tu kama wapigakura wake.

Akajinasibu kuwa wanawake wa Tanzania wanaiacha mkono CCM na inaelekea kuyumba pamoja ya karata yake ya kumsimamisha Mama Samia kama mgombea mwenza.

Leo pia, amenidokeza kuwa watanzania hawa si wale. Amesema kuwa ana tafiti zilizo fiti zikionesha kuwa UKAWA ndiyo dawa. Ananisubiri anioneshe nikifika nyumbani jioni.

Lengo lake nalijua. Ni kuninyanyasa kisiasa lakini kisasa. Kwa hoja za haja bila kubadili lahaja. Najiandaa,kwa kujisomea nyaraka za haraka na baraka,kwenda kupindua tafiti zake. Nikifika nyumbani, kampeni za chumba kwa chumba zitaanza.

UKAWA mmeniharibia mwanangu. Kwasasa hadi ana kibwagizo chake: MAGUFULI APIGE KAMPENI, LOWASSA ATAPIGIWA KURA! Kazi kwelikweli.

Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam

UKAWA Kutumia Viwanja wa Jangwani Jumamosi

$
0
0
Malalamiko ya vyama vinavyounda UKAWA ya kakatazwa kutumia uwanja wa jangwani kuzindua kampeni yameanza kufanyiwa kazi na tume ya taifa ya uchaguzi na taarifa zilizotolewa na mkuu wa idara ya mawasiliano ya CHADEMA Bw.Tumaini Makene imesema kuwa

Ghafla hiyo itafanyika kwenye uwanja huo kama ilivyokuwa imepangwa.
Bw.Makene ametoa taarifa hiyo kwenye mkutano wa baraza la vijana la vyama vinavyounda UKAWA na waandishi wa habari ambao pia viongozi hao wametumia nafasi hiyo kuiomba tume ya uchaguzi kuwakemea viongozi na watendaji wa serikali kufanya kazi za siasa kwa lengo la kukibeba chama tawala.

Viongozi hao wa vijana wamesema hatua ya viongozi na watendaji wa serikali ya kujihusisha moja kwa moja na kampeni za CCM huku wengine wakitumia rasilimali za umma na vyombo vya dola kukandamiza vyama vya upinzani inathibitisha ukweli wa malalamiko yao.

Baada ya Kufunguliwa Kamati Mpya ya Miss Tanzania yawekwa Wazi..Jokate Ndani....

$
0
0
Baada ya kufunguliwa kwa mashindano ya kumtafuta Miss Tanzania na Baraza la Sanaa la Tanzania (BASATA), Kamati ya Maandalizi ya Michuano hiyo imekuja na mikakati ya kurejesha hadhi na heshima ya mashindano hayo makubwa ya kusaka walimbwende nchini.


Katika kuboresha mashindano ya Miss Tanzania, Mkurugenzi wa Kampuni ya Lino Agency, Hashim Lundenga leo ametambulisha mbele ya waandishi wa habari kamati mpya yenye wajumbe 12, ambayo itakuwa inaratibu mashindayo hayo kwa sasa.
Lundenga amesema kuwa kamati hiyo inayoanza kazi zake hii leo, itashughulikia mapungufu yote yaliyojitokeza na kurejesha imani ya wananchi kwa mashindano hayo ikishirikiana kwa karibu na wadau mbalimbali pamoja na Basata.
Akizungumza na waandishi wa habari baada ya kutambulishwa Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Jokate Mwegelo ametoa shukrani kwa niaba ya kamati yake kwa kuamininiwa kupewa jukumu hilo na kuahidi maboresho makubwa na mikakati endelevu ya kurejesha hadhi ya Miss Tanzania.

Kamati Mpya ya Miss Tanzania inaundwa na wajumbe wafuatao:

1.Juma Pinto – Mwenyekiti
2.Lucas Rutta – Makamu Mwenyekiti
3.Doris Mollel – Katibu Mkuu
4.Jokate Mwegelo – Msemaji wa Kamati
5.Hoyce Temu – Mjumbe
6.Mohamed Bawazir – Mjumbe
7.Gladyz Shao – Mjumbe
8.Magdalena Munisi 0 Mjumbe
9.Shah Ramadhani – Mjumbe
10.Hamm Hashim – Mjumbe
11Khalfani Saleh – Mjumbe
12.Ojambi Masaburi – Mjumbe

Kwa upande wa Sekretariet tunao wajumbe 4 ambao ni:

1.Dr.Ramesh Shah
2.Hidan Ricco
3.Yasson Mashaka
4.Deo Kapteni

Tazama Picha za Mafuriko ya Wanawake Waliojitokeza Millenium Tower Kumsikiliza Lowassa, Wengi Wamekosa Nafasi na Kubakia Nje

$
0
0


Ni mkutano wa wanawake wa ukawa na mh lowasa hapa jengo la millenium TOWER Dar es salaam,hizi ni picha za awali,hizi ni picha za awali ambazo nimekuwekea hapa kutoka katika mkutano huo.LOWASA bado hajawasili hapa ila idadi ya wanawake waliojitokeza hapa ni wengi sana kiasi cha kutokutosha katika jengo hili na sasa watu wanasubiri hatma yao kama watahamisha mkutano au italazimu wengine kuwa wapole na kusubiri nje kidogo.
Picha kamili za tukio hili zitakujia baadae kadiri muda unavyozidi kwenda msomaji wetu





























VERA Sidika Ajibu Mapigo ya Huddah Monroe Kwa Kuweka Picha Hii ikionyesha Chuchu zake zilivyo

$
0
0
If these socilates are not posting nudes they are busy calling out each other online. Well it’s barely a week since Vera played therapist by asking Huddah to tone down on her cocaine after a photo her naked boobs surfaced online.


Vera has shared a similar photo but the difference between the two is that she covered them. Braless though. She might not be the first lady walking around braless but is this the in thing? The last time i checked these two were out travelling to outdo each other but the tables keep turning.

Maimartha, Wema Sepetu Kumekucha>>>Hadi Polisi Waingilia>>>Kisa na Chote Ingia Hapa

$
0
0
KUMEKUCHA! Hivyo ndivyo unavyoweza kusema kufuatia mtifuano kati ya mtangazaji maarufu wa televisheni, Maimartha Jesse na staa wa filamu, Wema Sepetu baada ya bifu la wawili hao kufika jeshi la polisi.

Akipiga stori na gazeti hili, Maimartha alisema Wema alikuwa na nia ya kumdhalilisha kwani baada ya kumtafuta na polisi na kumkosa, waliamua kumpigia simu na kumuita kituoni Kijitonyama (Mabatini) ambako alisomewa mashtaka ya kumtukana Wema katika mtandao wa kijamii wa Instagram.

Yaani Wema alitaka kunidhalilisha ndiyo maana polisi walikuja kibao kwenye gari lao hapa dukani kwangu na waliponikosa ndiyo wakanipigia simu kwamba niende mwenyewe kituoni, nikaenda nikatoa maelezo yangu ila sasa nitakula naye sahani moja kwani watu wake wanaendelea kunitukana sana mtandaoni nami siwezi kukubali,” alisema Maimartha.

Chanzo: Globalpublishers

Hatimaye UKAWA Wakubaliwa Kutumia Uwanja wa Jangwani Jumamosi hii Kuzindua Kampeni zao

$
0
0
Lowassa Akizungumza na Wahandishi wa Habari
Malalamiko ya vyama vinavyounda UKAWA ya kakatazwa kutumia uwanja wa jangwani kuzindua kampeni yameanza kufanyiwa kazi na tume ya taifa ya uchaguzi na  taarifa zilizotolewa na mkuu wa idara ya mawasiliano ya CHADEMA Bw.Tumaini Makene zimesema kuwa uzinduzi huo utafanyika kwenye uwanja huo kama ilivyokuwa imepangwa.

Bw.Makene ametoa taarifa hiyo kwenye mkutano wa baraza la vijana la vyama  vinavyounda UKAWA na waandishi wa habari ambao pia viongozi hao wametumia  nafasi hiyo kuiomba tume ya uchaguzi kuwakemea viongozi na watendaji wa  serikali kufanya kazi za siasa kwa lengo la kukibeba chama tawala.

Viongozi hao wa vijana wamesema  hatua ya viongozi na watendaji wa serikali ya kujihusisha moja kwa moja na kampeni za  CCM huku wengine wakitumia rasilimali za umma  na vyombo vya dola kukandamiza vyama vya upinzani inathibitisha ukweli wa  malalamiko yao.

Angalia Video Jinsi Nyumba iliyoteketea kwa Moto na Kuua Watu 9 Buguruni Malapa

$
0
0
Watu tisa wa familia moja wameteketea kwa moto usiku wa kuamkia leo huko Buguruni Malapa jijini Dar es Salaam.
Tukio hilo la kusikitisha limetokea Mtaa wa Ulam ambapo, bibi, watoto watatu wa kike na wajukuu watano waliokuwa wanaishi nyumba namba 40 wameteketea.

Video Hii Hapa:

Mhe. Lowasa Hukukidhi Kiu ya Wanawake! Nilichotegemea Sikukipata

$
0
0
Nimefatilia kwa karibu sana sana hotuba ya Mhe. Mgombea u Rais kupitia UKAWA aliyoitoa hapa LAPF kwenye kongamano la wanawake BAWACHA na kubaini jambo moja kubwa sana.

Kauli mbiu ya kongamano ni "LOWASA NA HATMA ZA CHANGAMOTO ZA WANAWAKE TANZANIA"

Nimesikitika kuwa nilitegemea kwenye hotuba Yake ataweza kuelezea mikakati ya ukombozi huo wa mwanamke. Nasikitika kuwa sikuona mahali popote akiongelea changamoto hizo na jinsi ya kuzitatua.

Ameishia kuimba Wimbo wa Mhe. Magufuli "Alinselema Hadija, mchaka mchaka chinja" na kuzungumza mambo ya MAHABA!!!!!!!!

Nasikitika kusema mimi kama mwanamke nimeondoka na kiu yanguuuu!!!!!!!!!! Ngoja nimsubiri mzee original wa Alinselema. I hope atatuondolea kiu hii!!!!!! Tunataka kuona SERA za ukweli za kumkomboa mwanamke, sio MAIGIZO.

Naomba kuwasilisha.
Viewing all 104747 articles
Browse latest View live




Latest Images