Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104776 articles
Browse latest View live

Mke Wangu Kapata Bwana Instagram

$
0
0
Habari zenu,

Najuta mke wangu kujua haya masimu ya kufuta futa.Yani mwanzo kwa hela yangu nilimnunulia simu hiyo ya kisasa ili aendane na wenzake akaja akaiuza kwani ilikuwa inajizima na istack akarudi kwenye tochi nikaona afadhali tukakaa miezi kadhaa akawa hana simu.

Sasa dada yake akaja akamnunulia simu pana kubwa hapo ndio balaa ilipoanzia yaani amekuwa mgonjwa wa simu yuko instagram kila saa hadi usiku ni huko huko hakuna cha mapenzi wala nini salama labda iishe charge na umeme uwe umekatika.

Nina siku 14 na zaidi hakuna cha mapenzi wala nini akishapika anaingia kwenye simu,mume wake amekuwa simu hasa instagramu.

Sasa nifanyeje?

Picha za Mwigizaji Jack Wolper Kwenye Mkutano wa Lowassa Leo...Apewa Mike na Kusizitiza Jina lake sasa ni Jack Lowassa

$
0
0
 Katika Mkutano wa Lowassa leo na Wanawake wa Chadema , Mwigizaji Jack Wolper Alipewa Nafasi ya Kuongea Kuwawakilisha wasanii na Kusizitisha kuwa kwa sasa jina lake ni Jack Lowassa Kama Alivyoandika kwenye ukurasa wake wa Instagram siku kadhaa zilizopita...
Jack Lowassa akisistiza jambo pembeni ni Aunt Ezekiel na katikati ni Shamsa Ford
Msanii wa Filamu Bongo Movies Jack Wolper akisalimiana na Lowassa mara baada ya kumpatia keki,ambapo jana mh.Lowassa alikuwa anatimiza miaka kadhaa toka azaliwe

Hutaamini Alikokuwa Akiishi Nuh Mziwanda Kabla ya Kuhamia Kwa Shilole

$
0
0
Nuh Mziwanda alikuwa akiishi kwenye studio ya muziki kabla ya kuhamia kwa mpenzi wake Shilole.

Muimbaji huyo amekiambia kipindi cha Hatua Tatu cha Times FM kuwa awali hakuwa na makazi maalum mpaka alipohamia kwa Shishi.

Nilikuwa nalala studio, nashinda studio tu. Zamani makazi yangu yalikuwa studio, nilikuwa producer studio moja hivi Ilala, so siku niliyoenda kwa Shilole nilienda na begi tu,” alisema.

Kwa upande mwingine Nuh alidai kuwa maisha ya vituko wanayoishi na mpenzi wake wameyachagua.

Bongo5

Kipindupindu Chanyemelea Nyumbani Kwa Wema Sepetu

$
0
0
Mrembo Wema Sepetu
Taarifa za ugonjwa wa kipindupindu zimebadili mfumo wa maisha ya watu wengi ikiwa ni pamoja na kuhakikisha maeneo wanayoishi ni masafi lakini nyumbani kwa msanii wa filamu Bongo, Wema Sepetu, Kijitonyama jijini Dar hali ni tofauti.

Mwandishi wetu akiwa kwenye mishemishe zake hivi karibuni, alikuta uchafu mwingi nje ya geti la nyumba ya msanii huyo hali iliyoelezewa na majirani kuwa ni kuukaribisha ugonjwa huo hatari.
Uchafu huo ulikuwa umezagaa katika eneo hilo ukiwa kwenye mifuko ya plastiki na kutoa harufu mbaya huku kunguru na paka wakipata pa kuponea njaa.

Akizungumza na Ijumaa mmoja wa majirani wa Wema alisema kuwa, ni kweli uchafu huo haukustahili kuwepo katika eneo hilo hasa katika kipindi hiki lakini akadai huenda uliwekwa na watu.
“Ni kweli kwa hatari ya ugonjwa huu wa kipindupindu uliolipuka, uchafu kama huu si sahihi kuwepo hapa lakini ninachohisi labda wale wavuta unga wanaozoa taka wamemuwekea usiku,” alidai jirani huyo.
Mwandishi wetu alifanya jitihada za kuzungumza na Wema lakini geti lake lilipogongwa halikufunguliwa na alipopigiwa simu hakupokea.

Source:Globalpublishers

Chadema, CCM Vita Kali..Wachuana Vikali Matangazo ya Televisheni

$
0
0
Vyama vya Chadema na CCM vimeingia katika mchuano wa kuwania nafasi ya kurusha matangazo ya moja kwa moja ya kampeni za wagombea urais katika televisheni Jumamosi hii.
Wakati Chadema ikitaka muda wa kurusha matangazo ya uzinduzi wa kampeni za mgombea wake, Edward Lowassa kutokea jijini Dar es Salaam, CCM inataka kurusha matangazo ya mkutano wa kampeni ya mgombea wake, Dk John Magufuli kutoka jijini Mbeya.

Ofisa Habari wa Chadema, Tumaini Makene alisema jana kuwa kumekuwa na njama za CCM kutaka kuzuia fursa ya Chadema kurusha kampeni za mgombea wake kwa kutaka siku hiyo irushe kampeni za Dk Magufuli.

Akizungumzia madai hayo, Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye alikiri chama hicho kutaka kurusha matangazo ya mgombea wake na kuhoji; “tatizo liko wapi kama Chadema imechelewa kulipia?”

Ni kweli mgombea wetu wa urais akiwa Mbeya tutarusha matangazo ya kampeni zake moja kwa moja kwenye runinga, sasa ni runinga ngapi siwezi kujua maana kuna watu wanalifanyika kazi suala hilo. Lakini kama Chadema walijua wana tukio lao kwa nini wasingewahi kulipia?” alihoji.
Chanzo cha habari kutoka kituo kimoja maarufu, kimeeleza kuwa kwa nyakati tofauti, CCM na Chadema waliomba muda wa kurusha vipindi vyao, lakini CCM ndiyo waliofanikiwa kupata.
Ninachojua hao wote walikuja kwa nyakati tofauti kuomba muda na CCM ndiyo waliofanikiwa kupata,” alidokeza mmoja wa wafanyakazi wa telesheni hiyo ambaye hakutaka kutaja jina kwa maelezo kuwa siyo msemaji.

Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa Azam TV, Tido Mhando alisema CCM na Chadema vilikuwa vimeomba kurushiwa matangazo yao na vyote vimelipia. Alisema kila moja kitapata fursa hiyo kwa kuwa kituo chake kina channel nyingi.

Hata hivyo, mmoja wa wahariri wa Kituo cha Televisheni ya Taifa (TBC1), alisema: “Sisi tunarusha vipindi vyetu kulingana na matukio na mahitaji ya jamii, hatuko fixed.” Alieleza kuwa ameamua kutoa jibu hilo rahisi kwa kuwa alijua kwa nini mwandishi aliuliza.

Sisi hatuna utaratibu wa kurusha live (moja kwa moja), wanaofanya hivyo ni watu wa radio tena huwa hilo linafanywa kibiashara. Kwamba wateja wanaomba kutangaziwa vipindi vyao na kulipa fedha,” kilieleza chanzo kutoka kituo kingine.

Habari zimeeleza kuwa kituo kimoja kikubwa cha televisheni kimethibitisha kurusha matangazo ya mgombea wa Chadema.
Awali, Makene alisema hadi jana, chama hicho kilikuwa kimefanikiwa kupata vituo vinne na radio nne.

Ukawa Wakatazwa kujenga Jukwaa Jangwani-Hii sasa Vita Police vs Ukawa

$
0
0
Hvi sasa kuna watu (wazee wa wapigwe tu) wamefika viwanja vya jangwani na kuwataiti mafundi wanaondelea na maandalizi ya uwekaji jukwaa kwaajili ya uzinduzi wa kampeni za UKAWA hapo kesho 29-08-2015 , hao wana usalama wamewataka mafundi hao kuwaonyesha kwanza kibali kinacho waruhusu wao kufanya kazi hiyo , lasivyo hakuna kujenga jukwaa hilo. more news and pictures to come, stay tuned. Aluta Continua...

Petit Man Amuanika Mrithi wa Esma Platnumz

$
0
0
Mpambe wa staa wa Filamu Bongo, Wema Sepetu, Hamadi Manungwa ‘Petit Man’, juzikati alimuanika rasmi mrithi wa aliyekuwa mkewe, Esma Abdul ‘Esma Platnumz’ baada ya hivi karibuni kuingia kwenye mgogoro wa ndoa.

Baada ya gazeti hili kuanika habari ya kuvunjika kwa ndoa hiyo wiki iliyopita huku Wema akitajwa kuwa chanzo ambapo yalizuka mambo mengi mpaka watu kupelekana polisi, hivi karibuni Petit Man alimuanika mwanamke mwingine akidai ndiye wa kuchukua nafasi ya Esma.

esmaBaada ya picha hizo kuzagaa mtandaoni, mwandishi wetu alizungumza na Petit Man ambaye alisema: “Niko kwenye mchakato wa kutoa talaka kwa vile sipendi kuwekwa kwenye mitandao na kudhalilishwa kila wakati, baada ya talaka nitaoa haraka.”

Esma kwa upande wake alisema anachosubiri ni talaka yake tu kwani ameshachukua baadhi ya vitu vyake kwenye nyumba waliyokuwa wakiishi na Petit Man.

Source:Global Publshers

Nani Kuhamia Ukawa/Chadema Kesho- Kingunge na Serukamba?

$
0
0
Jamani kesho kwa kutumia haki yao ya kidemokrasia kuna watanzania wenzetu watahama kutoka CCM kwenda UKAWA/CHADEMA. Kwenye list hiyo, nawaona Kingunge Ngombale Mwiru na Peter Serukamba ni watu ambao kimwili wako CCM lakini kifikra wako UKAWA. Sio vibaya 'kuspeculate' kwani siasa zetu za ovyo ovyo ndio zimetufikisha hapa. Kwa wale wenye taarifa za 'chumbani' si vibaya mkaanza kuwatayarishia waandishi wa habari vichwa vya habari vya kesho kwa kutujuza.

NEC Yakabidhi Polisi Majina ya Watu 52,000 Waliojiandikisha Zaidi ya Mara Moja Katika Daftari la Kudumu la Wapiga Kura

$
0
0
Mkurugenzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), Kailima Ramadhan (kushoto), akimkabidhi Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP), Benedict Wakulyamba orodha ya majina 52,078 ya watu waliojiandika katika daftari la kudumu la wapiga kura kwa mfumo wa BVR zaidi ya mara mbili Dar es Salaam jana, kwa ajili ya uchunguzi na baadae hatua za kisheria zichukuliwe kwa wahusika.

Picha hii ni baadhi ya watu waliojiandikisha zaidi ya mara mbili katika daftari hilo.

TUME ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imelikabidhi jeshi la polisi orodha ya majina ya watu zaidi ya 52,000 ambao wamebainika kujiandikisha zaidi ya mara moja kwenye daftari la kupigia kura kwa mfumo wa Biometric Voters Registration (BVR), akiwemo Diwani wa Kata ya Kimara, Pascal Manota (Chadema).

Idadi hiyo ilibainishwa Dar es Salaam jana na Mkurugenzi wa NEC, Ramadhan Kailima wakati wa ziara na waandishi wa habari katika bohari ya utayarishaji wa vitambulisho vya kupigia kura kwa mfumo wa BVR

UKAWA Kuzundua Kampeni Kesho Bila Dr. Slaa

$
0
0
MRATIBU wa Maandalizi ya Kampeni Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Deogratia Munishi amesema maandalizi ya mkutano wa ufunguzi wa kampeni yamekamilika kwa asilimia 90.

Akizungumza na waandishi wa habari leo katika viwanja hivyo vya Jangwani, Munishi amesema kila kitu kipo tayari katika maandalizi hayo na wanachosubiri ni mkutano.

Munishi amesema mkutano huo wa ufunguzi wa kampeni umepangwa kuanza saa 4 asubuhi na kumalizika saa 12 jioni.

Amesema, mkutano utahudhuliwa na watu kutoka sehemu mbalimbali nchini wakiwemo wanachama kutoka nje ya nchi kama Zambia na sehemu nyingine duniani.

Aidha, amewataja viongozi watakaohutubia katika mkutano huo kuwa, Mgombea urais kupitia Chadema, Edward Lowassa, Mgombea Mweza, Juma Duni Haji, viongozi wakuu wa UKAWA na wawakilishi kutoka makundi mbalimbali.

Kuhusu uwepo wa wasanii katika mkutano huo amesema: “Wasanii watakuwepo lakini hawatapamba mkutano kama kule kwa wenzetu, sisi tunakuja kutangaza sera na sio tamasha la wasanii.”

Naye Afisa Habari wa Chadema, Tumaini Makene ametoa ratiba ya Mgombea urais na mgombea mwenza kuwa, mara baada ya uzinduzi wa kampeni hizo wataanza ziara mikoani.


Amesema Lowassa, Jumapili ataanza ziara yake Mkoani Iringa na kufanya mikutano ya hadhara minne ambapo ataanzia Mufindi, Kilolo, Karenga, na Iringa Mjini kila sehemu mkutano mmoja.

Kwa Upande wa Babu Duni, amesema ataanzia Mtwara katika wilaya ya Newala, Tandahimba, Mtwara vijijini na Mtwara mjini.

Aidha, kuhusu tetesi za uwepo wa Katibu mkuu Chadema, Dk. Willbrod Slaa viwanja vya jangwani Makene amesema: “Hizo ni tetesi tu. Hakuna ukweli wowote. Dk. Slaa (Willbrod) amepumzika acheni kumzushia maneno.”

Ameongeza, mkutano utakuwa laivu katika televisheni na radio zisizopungua tano kuanzia saa 9 hadi 12 jioni.

UKAWA Wakishindwa Mwaka Huu, Nani Ataweza?

$
0
0
Siasa za mwaka huu ni kali, tena sana. Utamu na ukali wake umenogeshwa na mambo matatu hasa moja ni jambo ambalo watanzania walikua wakisema sana kuwa vyama vya upinzani vikiungana ndipo vitaweza kuitoa CCM ikuli, hilo limetokea mwaka huu. Pili ni ile hali ambayo haikuzoeleka ya wana CCM wakubwa kama Lowassa, Sumaye na wengineo kuhama CCM na kuenda upinzani, hilo limetokea na kunogesha siasa za mwaka huu. Tatu ni jinsi wagombea wa urais toka CCM na yule wa ukawa walivyo na nguvu katika Jamii, woote wanakubalika na ni vigumu kusema nani ni zaidi ya mwingine, hapo ndipo utamu unakolea zaidi na zaidi.

Najiuliza tu, je, ukawa wakishindwa kuitoa ccm madarakani mwaka huu,nani au chama gani kitakuja kufanikiwa? Au hilo litamaanisha hakuna upinzani mioyoni mwa watanzania na hivyo upinzani utaparaganyika?

Pale Unapokuta Mkeo Katuma Picha zake za Uchi kwa Mwanaume Mwingine

$
0
0
Nimeishi na mke wangu wa ndoa kwa miaka kama 10 hivi sasa. Ila ndani ya muda huo ndani kumekuwa na migogoro ya hapa na pale ya kutoaminiana.

Ila katika hali hiyo yeye ndiyo alikuwa ananishutumu mimi kuwa nina michepuko na yeye kujiona yupo innocent kama malaika. Lakini juzi kati hivi, katika pita pita yangu nikgundakuna mwanaume yupo nae busy ofisi kwake.

Nilipomuuliza akaribu kutoa utetezi ambao sikuridhika nao, nikaanza kumfutilia kimyakimya kenye simu zake na email zake. Siku ya siku nikkutana na chats kwenye whatsap baina yake na huyo mwanaume na mke wangu akimtumia huyo mwanume picha zake akiwa mtupu kigia kwenye kitanda chetu.

Hebu nipeni ushauri, maana hatua ya kwanza niliyoichukua ni kumrudisha kwa wakati natafakari maamuzi ya kudumu. Mpaka sasa yupo kwa mjomba wake.

Advice please guys

Majambazi wenye silaha wamevamia daladala inayofanya safari zake Ubungo-Kariakoo

$
0
0
Majambazi wamevamia daladala Ubungo Kariakoo maeneo ya Jangwani, mtu mmoja (abiria) aliyekuwa amebeba mfuko amepigwa risasi, watu kadhaa wamejeruhiwa. Majambazi haya yalikuwa na Pikipiki aina ya Boxer , kabla ya kupiga risasi walitaka abiria atoe hilo fuko la fedha yeye akagoma akiaangalia kama atapata msaada kutoka kwa abilia ndipo walimwambia dereva kusimama na kutwanga risasi huyo abiria akaachia fuko linalosemekana kuna fedha, haijajulikana ni fedha au ni dhahabu/Tanzanite maana abiria alikuwa awezi tena kuongea.

Taarifa kamili zitawajia

TCRA yatoa onyo kali kwa TBC1 kwa kuzikwepa habari za UKAWA na Kupendelea CCM

$
0
0
MAMLAKA ya mawasiliano nchini (TCRA) imekipa onyo kali  kituo TBC1 kwa kosa  la  kubagua kusoma taarifa zinazohusiana na UKAWA.

Hukumu hiyo ilitolewa jana jijini Dar es Salaam na kamati ya maudhui ya utangazaji, katika ofisi za Mamlaka ya Mawasiliano na Kaimu Mwenyekiti wa Kamati hiyo Walter Bugoya wakati wa mkutano na waandishi wa habari.

Bugoya alisema kamati hiyo imebaini TBC one imekiuka sheria ya utangazaji ya mwaka 2005  pamoja na sheria ya uchaguzi ya mwaka 2015 kwa kufanya upendeleo wa vyama katika taarifa zake kwenye kipindi.

Alidai katika kipindi cha Jambo Tanzania kilichorushwa tarehe 15 mwezi huu majira ya saa 12 asubuhi hadi saa tatu, katika kipingele cha uchambuzi wa magazeti mtangazaji wa kipindi hicho alikuwa anayasoma magazeti huku akiruka kusoma habari kuu husika.

Alisema Mtangazaji huyo alipokuwa anachambua gazeti la Majira na Nipashe alidanganya umma jambo ambalo amedai ni kosa.

Bugoya alitaja makosa hayo  kuwa ni wakati  mtangazaji huyo alipokuwa anasoma Gazati la Majira  ukurasa wake wa mbele alisema habari kubwa ni “CCM yazidi kuwaumbua wanaomfuata lowassa” wakati habari  kubwa ilikuwa inasomeka hapo ni ile inayosema “Mbeya kwafurika”, huku picha ya gazeti hilo likionyesha picha ya umati watu pamoja na mgombea wa Urais wa chadema Edward lowassa akihutubia.

Alisema mtangazaji huyo pia alifanya kosa lingine kama hilo pia wakati akisoma Gazeti la Nipashe ambapo alisema Habari iliyopewa uzito wa kipekee ni  “Mbalawa atoa sheria ya mitandao”  ambapo habari iliyopewa uzito ilikuwa ni ile “Mafuriko Mbeya” na sio aliyokuwa anaisoma yeye.

Alisema baada ya Kamati yake kubaini makosa hayo waliwasiliana na mkurugenzi wa TBC one Bwana Mshana.

Mkurugenzi huyo alitoa utetezi wake kwenye kamati hiyo akisema mtangazaji huyo hakufanya kosa kwakuwa alikuwa hajaridhika na taarifa zilizokuwa zimeandikwa kwenye magazeti hayo.

Sanjari na hayo Mshana alizidi kujitetea akidai kuwa hata mtangazaji huyo  asingesoma habari ile lakini picha iliyokuwa inaonekana kwenye magazeti hayo tayari mtazamaji alikuwa ashajua kwahiyo amedai haikuwa na ulazima wa kusomwa.

Bugoya alisema baada ya kusikiliza upande wa TBC one ndio wakabaini kituo hicho kilikiuka sheria ya utangazaji ya Mwaka 2005 ambayo inavitaka vituo vyote vya utangazaji nchini kuripoti taarifa kwa kutokuwa na upendeleo wowote.

Alisema Kamati imefikia uamuzi wa kuipa onyo kali TBC one na endapo wataendelea basi Mamlaka hiyo haitasita kuwachukulia hatua kali zaidi.

Mwakyembe Amshambulia LOWASSA Kuhusu Sakata la Richmond...........Mwigulu Nchemba naye Adai Lowassa Ni Mpiga Dili Tangu Kijana

$
0
0
Mwakyembe Akihutibia Umati
Aliyekuwa mwenyekiti wakamati teule ya bunge ya kuchunguza kashfa ya mkataba tata wa Richmond iliyomuondoa madarakani aliyekuwa waziri mkuu Mh Edward Lowassa, Mh Harrsion Mwakyembe amewahakikishia watanzania kuwa walijiridhisha pasipo shaka kuhusika kwa Edward Lowassa katika sakata la Richmond na kwamba hawakumsingizia kama anavyojitetea hivi sasa.

Mwakyembe aliyasema hayo mbele ya maelfu waliojitokeza katika mkutano wa hadhara wa mgombea urais wa CCM, Dk John Magufuli katika viwanja vya Luandanzovwe jijini Mbeya, jana.

Akizungumzia madai ya kwa nini baadhi ya wahusika hawakupelekwa mahakamani kama kuna ushahidi, mhadhiri huyo wa sheria alisema kosa la jinai, halina ukomo na wakati wowote linaweza kufunguliwa mashitaka, huku akiapa kuwa anaweza kumfungulia mtu mashitaka hata kesho.

Alionya viongozi na makada wa Chadema na vyama vinavyowaunga mkono katika umoja wa Ukawa wanaozindua kampeni zao leo jijini Dar es Salaam, kwamba wasithubutu kujibu hoja zake.

Dk Mwakyembe alisema ikilazimika kusema ukweli, ataweka hadharani uchafu wote uliofanyika, ambao alisema bungeni kuwa asingeuanika na kuifanya Richmond hoja ya kila siku mpaka Watanzania waelewe kilichofanyika.

“Tunao ushahidi. Hawa walitakiwa kuwa jela badala ya kuimba nyimbo za ajabu,” alisema Dk Mwakyembe katika mkutano huo uliorushwa moja kwa moja nchi nzima na kuongeza kuwa Dk Magufuli akiingia madarakani, anakwenda kuanzisha Mahakama ya Ufisadi.

Alisema yeye na wenzake walipewa kazi ya Bunge kuchunguza ilikuwaje viongozi waandamizi wakaamua kuipa kampuni hewa zabuni ya mabilioni ya fedha, ambayo imesababisha mpaka leo kuna shida ya umeme nchini.

Dk Mwakyembe alikumbusha kuwa walikwenda mpaka Marekani kuchunguza uwepo wa kampuni hiyo iliyodaiwa kutoka katika nchi hiyo, na kukutana na kampuni ya kuchapisha kadi za harusi.

Kwa mujibu wa Dk Mwakyembe, baada ya kubaini ubadhirifu huo, aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa, alishinikizwa kujiuzulu na kumaliza suala hilo na hivyo hatua ya kiongozi huyo kutaka kwenda Ikulu, wazalendo hawawezi kuikubali.

“Hatutaruhusu watumie demokrasia kuingia Ikulu na hiyo ndiyo shida ya kuazima wagombea,” alisema Dk Mwakyembe akimaanisha kuwa chama cha Chadema, kimeazima mgombea bila kumfahamu.
 
 Dk Mwakyembe alisema suala hilo lilishafungwa bungeni, lakini anashangaa kusikia linarejeshwa kinyemela.

Mwigulu
Naye Naibu Waziri wa Fedha na Uchumi, Mwigulu Nchemba, alisema mgombea wa Ukawa, Lowassa, tangu akiwa kijana alikuwa ‘mpiga-dili’.

Kwa mujibu wa Mwigulu, Rais Kikwete alipoingia madarakani, alidhani kuwa Lowassa alikuwa ameonewa, akamteua kuwa Waziri Mkuu, lakini kabla ya kumaliza miaka miwili, akaendeleza tabia yake ya ‘kupigadili’.

Mwigulu alionya kuwa, Watanzania wakimpeleka ‘mpiga-dili’ Ikulu, shida yake na wenzake si changamoto za watu wa Mbeya wapate maji, huduma bora za afya na nyingine bora za umma, bali kurejesha fedha walizotumia wakati wa kutafuta urais.

“Mkimpeleka mpiga dili Ikulu, ‘wapiga-dili’ wenzake hawatalipa kodi, mtalipa nyie wanyonge ili wale ‘wapigadili’ warejeshe fedha zao,” alisema na kufafanua sababu za vyama vya Chadema, CUF, NCCRMageuzi na NLD kuungana pamoja katika Ukawa.
 
Kwa mujibu wa Mwigulu, kilichowaunganisha ni maslahi ya aina mbili; moja aliyetoa fedha kwa ajili ya kwenda Ikulu, ambaye anatafuta nafasi hiyo ili arejeshe madeni yake na wengine ni waliouza vyama ambao ‘wameshakunja’ chao.

“Nawaambia mwisho wa mbwembwe na maigizo, ni Oktoba 25 na baada ya hapo ni kazi tu,” alisema Mwigulu na kuhoji iweje Lowassa apande daladala leo, ambalo hakulipanda miaka 40 iliyopita?
 
 Mwigulu alisema Watanzania wana siku 60 za kujadili hatima ya taifa lao na katika hilo, hakuna namna zaidi ya kuelezana ukweli mtupu.

Mwigizaji Lulu Michael, Mama Kanumba Wapigana Vikumbo

$
0
0
MAKUBWA! Mama wa aliyekuwa nguli wa filamu Bongo, Steven Kanumba, Flora Mtegoa amejikuta kwenye simanzi nzito baada ya kukutana na mwigizaji Elizabeth Michael ‘Lulu’ ambaye alikuwa mpenzi wa mwanaye kumpita bila kumsalimia.

Tukio hilo lilijiri mwishoni mwa wiki iliyopita ndani ya Ukumbi wa Makumbusho ya Taifa, Posta jijini Dar kulipokuwa na fainali za shindano la vipaji vya kuigiza lijulikanalo kama Tanzania Movie Talents (TMT 2015) ambapo Lulu alimpita mama huyo kama hawajuani kitendo ambacho kilisababisha minong’ono ukumbini hapo.
FrolaMtegoa“Inastaajabisha sana yaani huyu Lulu ndiyo kafikia hatua ya kumdharau mama Kanumba kiasi hiki, siyo siri hamtendei haki huyu mama sijui ni kitu gani kikubwa ambacho alimkosea,” alisikika mmoja wa mashabiki.

Mama Kanumba alipohojiwa na paparazi wetu ukumbini hapo, alisema anashindwa kumuelewa Lulu kwani hata ukiondoa undugu wake, bado kiumri ni mtoto anayepaswa kuheshimu wakubwa.
“Nimestaajabu sana kuona Lulu hanisalimii na isitoshe alijifanya kama hana habari na mimi utasema kuna kitu nimemkosea, wakati yeye ndiye anatakiwa ajishushe kutokana na yale yaliyotokea, ni dharau kubwa amenionyesha wakati aliwahi kuniomba msamaha huko nyuma kuhusu matukio yake hayahaya ya kuninunia,” alisema mama Kanumba.

Alipotafutwa Lulu, simu yake haikuwa hewani na hata alipotumiwa ujumbe mfupi, hakujibu.

Source:Globalpublishers

Madai Mtoto si wa Diamond, Zari Aitwa Kwao Uganda

$
0
0
KIMENUKA! Baada ya madai kwamba mtoto Latifah ‘Tiffah’ si damu ya Mbongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’ huku shemeji wa zamani wa Zarinah Hassan ‘Zari’ (mama Tiffah), King Lawrence naye kusema mtoto huyo ni wake, kuna taarifa mpya zinazodai kuwa, Zari ameitwa kwao, Uganda ili akamalize ubishi juu ya suala hilo, Risasi Jumamosi limenasa mchapo kamili.
Hivi karibuni baada ya Zari kujifungua, King Lawrence alijitokeza na kudai kuwa, mtoto huyo ni wake na kusema kama kuna anayebisha kiitishwe kipimo cha vinasaba (DNA), hivyo kuibua mkanganyiko na taarifa zilizozagaa awali kuwa, mtoto huyo ni wa aliyekuwa mume wa Zari, Ivan Ssemwanga.

TUJIUNGE NA CHANZO
Kwa mujibu wa chanzo makini, hivi karibuni, Zari alipigiwa simu na mama yake mzazi, Halima Hassan akimtaka aende nyumbani kwao ili akawaeleze ukweli ndugu zake ambao wamekuwa njia panda baada ya kuibuka kwa taarifa kwamba Tiffah si wa Diamond ambaye familia inamtambua kwa sasa.
“Taarifa zinawafikia tofauti. Kuna zile za awali kwamba mtoto huyo ni wa Ivan, mara zikaibuka nyingine kwamba ni wa King Lawrence hivyo mama amemuita Zari ili akategue kitendawili hicho kumaliza ubishi.

ATAKIWA KWENDA NA UKWELI
“Amemtaka aende na ukweli moyoni maana yeye (Zari) ndiye anayeujua. Hata hiyo DNA haina maana. Ameambiwa kwamba siku zote mama ndiye anayejua ukweli wa mtoto ni wa nani,” kilisema chanzo hicho.

ATAKIWA AMUOGOPE MUNGU
Chanzo kilizidi kunyetisha kuwa, mbali na kumtaka aende na ukweli, familia imemtahadharisha atakapofika aseme ukweli kwa kumuogopa Mungu maana vinginevyo dhambi hiyo itamhukumu maisha yake yote.
“Ametahadharishwa na familia kwamba anapaswa kumuogopa Mungu maana ni dhambi mtoto wa baba huyu kumpa baba huyu. Wao Kama familia wanajua Tiffah ni wa Diamond. Sasa wanakangaywa na hao wanaodai wao ndiyo haswa wahusika.

HAWAHOFII KAMA SI WA DIAMOND
“Familia imesema haina shida hata kama itakuwa mtoto si wa Diamond lakini wanachotaka wao ni kujua ukweli tu.” Chanzo.

DIAMOND ANASEMAJE?
Katika mazungumzo yake na mwandishi wetu hivi karibuni baada ya King Lawrence kuibuka na barua ya wakili kuitisha kipimo cha DNA akidai mtoto ni wake, Diamond alisisitiza kwamba mtoto huyo ni damu yake hivyo hana muda wa kubishana na mtu.

“Huyo jamaa (King Lawrence) atakuwa anatafuta kiki katika vyombo vya habari. Huyohuyo ndiye alianza kusema mtoto si wangu ni wa Ivan mara amegeuka tena na kusema ni wake yeye, hata haeleweki. Siwezi kujibishana naye.
“Hata hiyo barua aliyosema ni ya wakili ya kutaka DNA, haijatufikia! Nasikia tu kwenye vyombo vya habari na mitandao ya kijamii,” alisema Diamond.

KUHUSU SAFARI
Alipotafutwa Diamond ili aeleze kuhusu taarifa za mama Tiffah kuitwa nchini Uganda ili akaeleze ukweli, alisema hayo ni mambo ya kifamilia zaidi na hata hivyo haoni tatizo ndugu kumwita Zari kwani ukweli Tiffah ni damu yake na hakuna mabadiliko yoyote yatakayotokea.
“Tiffah ni damu yangu hata akienda hakuna kitakachobadilika. Sina wasiwasi maana mimi najua mahesabu yake yote na ninajua mpaka tarehe niliyokutana naye na mtoto akawepo,” alisema Diamond huku akisema, Zari hana nafasi ya kuongea na vyombo vya habari.

NCHINI UGANDA
Nchini Uganda, bado baadhi ya vyombo vya habari vimekuwa vikiripoti mkanganyiko wa mtoto wa Diamond ambapo baadhi ya magazeti yametaka Zari aende akapime DNA ili kujiridhisha kuhusu uhalisia.

AFRIKA KUSINI
Nazo habari kutoka nchini Afrika Kusini ambako ndiko kwenye makazi ya Zari, baadhi ya Wabongo wanaoishi jirani na Zari walisema wanatambua uwepo wa Diamond kama mpenzi mpya wa Zari kwa hiyo hakuna shaka kuwa yeye ndiye baba (biological father) wa Tiffah.
Akizungumza na Risasi Jumamosi kwa njia ya simu juzi, mkazi mmoja wa eneo hilo aliyejitambulisha kwa jina moja la Steve, alisema amekuwa akimfuatilia kwa karibu King Lawrence kupitia Instagram yake akidai kwamba yeye ni baba wa Tiffah, lakini sehemu kubwa ya watu wenye ujirani na Zari kule wanaamini, Diamond ndiye baba husika.

“Kuhusu Diamond kuwa baba wa Latifah hilo halina ubishi. Hata sisi huku tunajua hivyo. Hili suala liangaliwe kwa macho matatu. Nahisi kuna ‘vita’ ya sisi Watanzania na Waganda kuhusu mtoto,” alisema Mbongo huyo.

Source:Globalpublishers

PICHA:Maandalizi ya Mkutano wa UKAWA/CHADEMA Wwanja wa Jangwani..Hili Hapa Jukwaa Ukawa Watakalo Litumia leo

$
0
0
PICHA:Maandalizi ya Mkutano wa UKAWA/CHADEMA Wwanja wa Jangwani..Hili Hapa Jukwaa Ukawa Watakalo Litumia leo...
Kaa Mkao wa Kule na kusikia sera za UKAWA ...ili kufanya uamuzi ulio sahihi...

Harrison Mwakyembe Adai Mgombea Urais Edward Lowassa Alihusika Kwenye Ufisadi wa Richmond

$
0
0
Mhe Mwakyembe amkaanga Lowassa kuhusu kadhia ya Richmond na kusema kuwa asikwepe maana tume ya Bunge ilimkuta na hatia na ikabidi ajiuzulu Uwaziri Mkuu.

Ameeleza hayo kwenye mkutano wa kampeni wa Mgombea Urais kupitia CCM Mhe JPM leo huko Kyela katika mfululizo wa kampeni za mgombea huyo. Mhe Mwakyembe kaeleza kadhia hiyo kwa maelfu ya wananchi waliokuwa wakishangilia tangu mwanzo hadi mwisho na wameahidi na kuapa kutotoa kura zao kwa Lowassa!

Alieleza kuwa leo waTanzania wanalipia umeme kwa bei ya juu kutokana na uroho wa Fisadi huyo kwavile Tanesco iliingizwa kwenye mkataba mbovu na pia gharama za mabilioni zilizolipwa kufuatia mkataba mbovu na kesi zilizojiri baada ya mkataba kusitishwa!

Wakati huo huo aliyekuwa mkuu wa mkoa wa Mbeya Mhe Mwakipesile, aliyestaafu ameuambia mkutano huo kuwa yeye hawezi kukihama chama cha Mapinduzi kilichomsomesha na kukulia kama mwanachama.

Hii inavunja uongo uliozushwa dhidi yake kuwa kakihama chama hicho na kuhamia UKAWA!

Source:Jamii Forums

Picha zingine 4 Nimekuwekea Hapa Zikionesha Jinsi Hali ilivyo Uzinduzi wa Kampeni Jagwani..

$
0
0

Maelfu  ya  wananchi  wakiendelea  kuwasili  viwanja  vya  Jangwani
Jukwaa  Litakalotumika

Viewing all 104776 articles
Browse latest View live




Latest Images