Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104789 articles
Browse latest View live

HABARI KAMILI Kuhusu Abiria Aliyeuawa Kwa Kupigwa Risasi Kwenye Daladala Jijini Dar na Wengine Kujeruhiwa

$
0
0
Mtu mmoja amefariki dunia na mwingine kujeruhiwa wakati watu wanaosadikiwa kuwa ni majambazi waliposimamisha daladala eneo la Jangwani na kuingia ndani kupora mkoba unaosadikiwa kuwa na fedha.Askari na wasamaria wema wakiwa wamebeba mwili wa abiria aliyepigwa risasi na majambazi akiwa ndani ya daladala eneo la Jangwani, Dar es Salaam jana. Daladala hilo lilikuwa likitoka Kariakoo likielekea Ubungo Mawasiliano. Picha na Edwin Mjwahuzi Watu hao, waliokuwa na pikipiki aina ya boxer, walikuwa wakifuatilia basi hilo linalofanya safari zake kati ya Kariakoo na Mwenge na kulisimamisha eneo la Jangwani saa 7.30 mchana na baadaye kuwaamuru abiria wote wainame kabla ya kuelekea kiti cha nyuma alikokuwa amekaa mtu huyo aliyekuwa amebeba mkoba.
Mmoja wa abiria wa daladala hilo, Rehema Michael alisema wakati basi lao likiwa linaenda taratibu, alimuona mtu aliyekuwa amepakizwa kwenye pikipiki akishuka na kumfuata dereva na kisha kumuelekezea bastola usoni, akimtaka asimamishe gari.

Alisema dereva wao alitaka kukunja kona kuelekea Jangwani, lakini akatii amri na ndipo dereva wa bodaboda alipokwenda nyuma ya daladala na kumtaka mmoja wa abiria aliyekuwa amekaa nyuma ya daladala kutoa begi, huku mwingine akipiga risasi hewani, lakini hakupewa mkoba huo.
“Baada ya kuona yule abiria anakaidi agizo lao, mmoja wa majambazi hao alimpiga risasi ya kichwani na kifuani na kuanguka chini huku yule abiria mwenzake ambaye alipewa begi hilo alishike alilitupa chini na mmoja wa majambazi aliingia ndani ya daladala na kulichukua,” Hashim Ally.

Shuhuda mwingine, Richard Urio alisema wakati uvamizi huo ukitokea abiria walikuwepo ndani ya daladala hiyo akiwemo konda walilazimika kulala chini baada ya kusikia milio ya risasi zilizokuwa zikipigwa hewani, na kwamba baada ya kuchukua lile begi walimpiga risasi abiria mwingine ambaye alikuwa karibu na marehemu baada kuhisi alikuwa akizuia begi lisitolewe.
“Siti ya nyuma walikuwa wamekaa abiria wanne, na wawili kati yao walikuwa wamasai ambao mmoja wapo alikuwa amevaa begi mgongoni ambalo lilichukuliwa na majambazi baada ya kumuua mmoja wa wamasai huku mwingine akijeruhiwa na bastola shavuni,”Urio.

Shuhuda mwingine, Regina Mateso alisema yeye alipanda daladala hiyo eneo la Shakilango na kuwakuta wamasai hao ambao inasemakana walikuwa na fedha nyingi kutokana na maongezi yao.
“Wale wamasai walikuwa wanapigiana mahesabu na wapi kwa kwenda kubadilisha fedha. Yule aliyefariki alikuwa anamwambia mwenzake ukibadilisha hizi dola unapata Sh16 milioni, hivyo inawezekana wale abiria walikuwa na kiasi hicho cha fedha ambacho walikuwa wameweka katika begi la mgongoni,” Mateso.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Polisi Ilala, Lucas Mkondya alisema tukio hilo limetokea na wanalifanyia kazi .

“Na sisi polisi tumelipata sasa hivi ndio kwanza tunalifanyia kazi likikamilika tutatia taarifa,” Mkonya

ZITTO KABWE: Magufuli Kwenye Majukwaa Anaongea Nini ? Anasema Barabara tu Utafikiri Anagombea Uwaziri wa Barabara

$
0
0

Kumekucha...Zitto Amchana Magufuli..."Magufuli Kwenye Majukwaa Anaongea Nini ? Anasema Barabara tu Utafikiri Anagombea Uwaziri wa Barabara"

Taswira za Picha Nyingine Kutoka Jagwani Nimekuwekea Hapa...Kuna Nyomi la Kufa Mtu....

Angalia Jinsi Warembo wa Bongo Movies Wakiwa Ndani ya Gwanda la Chadema Tayari Kwa Mkutano Jagwani

$
0
0

Angalia Jinsi Warembo wa Bongo Movies Wakiwa Ndani ya Gwanda la Chadema Tayari Kwa Mkutano Jagwani

Tanzania imeshikilia nafasi ya 10 katika orodha ya Nchi za Afrika zenye Uchumi Mkubwa

$
0
0
The African continent has always been referred to as “The Sleeping Giant.” Such a terminology usually points at the great potential Africa has. It is well endowed with resources of all kinds. This applies to natural as well as human resources. In the recent past, African economies have been flourishing with the following countries making up the list of the top 10 largest economies in Africa.

10. Tanzania
GDP – $49 billion
Per Capita – $720
Tanzania completes the list of the top ten economies in the African continent with a GDP of $49 billion. As of 2014, Tanzania’s gross domestic product (GDP) was an estimated $43.8 billion, or $86.4 billion on a purchasing power parity (PPP) basis. Tanzania is a middle-power country, with a per capita GDP of $1,813 (PPP) which was 32% below the average of $2,673 for the 45 sub-Saharan African countries[87] and ranked 23rd among those countries.

From 2009 through 2013, Tanzania’s per capita GDP (based on constant local currency) grew at an average of 3.5% per year. Tanzania’s population of 47.4 million (2014) is highly diverse, composed of numerous ethnic, linguistic, and religious groups.

9. Ethiopia
GDP – $55 billion
Per Capita – $859
About three decades ago, the whole world came in aid of Ethiopia. The country was going through a dreadful famine. Three decades down the lane, Ethiopia is emerging as one of the top economies in the region. With a GDP of $55 billion dollars, Ethiopia holds the 9th slot. Its economy mainly depends on agriculture. It is the second largest producer of maize in the continent. Coffee and horticulture (flowers) have been doing quite well recently.

8. Sudan
GDP – $64 billion
Per Capita – $2,417
Until the mid 2008, Sudan was infamous for civil wars. This greatly devastated the country. However, after 2008 the country’s economy sprang back to action. As of 2014, the Eastern Africa country had a GDP of $64 billion. Its main economic activities are agriculture, gold and petroleum mining. It is the 3rd largest producer of sesame in the world. Other products include cotton, coffee, cotton seed, wheat, sugarcane, tobacco, peanuts and more.

7. Libya
GDP – $ 67 billion
Per Capita – $11,354
Libya has an estimated GDP of $ 67 billion dollars. The main economy of the country is petroleum mining. It has among the largest oil reserves in the entire world. Better world prices have certainly favoured the desert country in the recent past. Libya also has some substantial deposits of steel ore.

Interestingly, despite Morroco’s position here, it is the country that has the highest per capita income in this list. This could be attributed to her small population side
Also see: 10 African Minerals of Highest Economic Value

6. Morocco
GDP – $107 billion
Per Capita – $5,765
The Kingdom of Morocco has for many decades featured among the top economies in the continent. This has largely been attributed to good policies and stable political structures. Its annual GDP in 2014 is valued at $ 105 billion dollars. The main economic activities include fishing, agriculture, and mining. Morocco is among the top producers of cannabis. It also has a good reserve of lead, phosphates, and silver.

5. Angola
GDP – $131 billion
Per Capita – $2,829
A few years back, Angola was always in the news for civil wars and political unrest. However, it seems like the 25 year war has finally ceded to peace. The once war-torn country overtook the Kingdom of Morocco to become the fifth largest economy in Africa. Its GDP is valued at $ 131billion dollars. Its main economic activities are mining of diamonds and petroleum oil % gas.

4. Algeria
GDP – $214 billion
Per Capita – $7, 095
Algeria has always been a regional rival to Egypt. The GDP of the North African country is estimated to be $ 214billion. The main economic activities driving the country comprise of agriculture, fishing and mining. The country is well gifted with quite a number of valuable minerals.

They include iron, copper, zinc, mercury, lignite, calamine, antimony and phosphate. Algeria was able to make the 3rd position, based on her Per Capita income which is $7, 095; a step upward from her GDP position.

3. Egypt
GDP – $292 billion
Per Capita – $4,282
Egypt famously known as “the jewel of the Nile” was convincingly placed at the third position. Its average GDP annually is estimated at $ 292 billion dollars. For many skeptics, this came as a major surprise taking into account the political unrest in recent years. In fact, many expected the economy to take a dip. Egypt relies heavily on its mineral resources such as copper, natural gas, aluminium, steel and iron ore.

It also has a thriving horticultural, and tourism industry. Her Per Capita which is $4,282 is not too bad, occupying the 5th position; just two steps down.
Read: 10 Common Reasons Why New Startup Businesses Fail

2. South Africa
GDP – $353
Per Capita – $11,035
South Africa which has always been revered as the top economy in Africa was finally beaten to second place by Nigeria. The southern Africa state had its GDP valued at approximately $ 350 billion dollars. In the recent past, the South Africa’s economy has been struggling. This has especially been witnessed in the mining industries where reserves for precious minerals such as gold, platinum, palladium, and diamond have been dwindling.

Commendably, South Africa retained its #2 position in terms of per capita. With a per capita of $11,035. South Africa is still in essence, the richest African country.

1. Nigeria
GDP – $569 billion
Per Capita – $2,700
Nigeria has always been referred to as the giant of Africa, both in terms of economy and population. Since 2014, Nigeria has been topping the list of richest African countries in terms of Gross Domestic Product (GDP). The country had overtaken South Africa which had for many decades had an iron grip at the helm. The GDP of Nigeria is currently valued at $521 billion. This is majorly attributed to its vast reserves of oil and gas.

Unfortunately, the exploding population of Nigeria has rendered the citizens and inhabitants at large poor in the midst of plenty. Even with all the wealth and first position on the list of biggest economies, Nigeria slips down to #7 with a GDP Per Capita as poor as $2,700.

Kama Kipimo Cha Ushindi ni Idadi ya Watu, Lowassa Ndiye Rais Wetu!. CCM Chali!, Imeshindwa Vibaya!.

$
0
0
Wanabodi,

nimepita hapa Jangwani kwenye uzinduzi wa kampeni za UKAWA, mchana huu saa 8:45, kitu nilichokishuhudia, Kama Kipimo Cha Ushindi ni Idadi ya Watu, then, Lowassa Ndiye Rais Wetu!. Kwa upande huu wa idadi ya watu wa leo, nikilinganisha na idadi ya watu siku ya ufunguzi wa Mkutano wa CCM, then, CCM imepigwa chini, imeangushwa Chali!, Imeshindwa Vibaya!.

Hii inamaanisha, kama umati huu wote wamejiandikisha, na wote watajitokeza kupiga kura hiyo siku ya uchaguzi, hata CCM waibe vipi kura, kwa kuitumia NEC, kura hazitatosha, mshindi wa uchaguzi huu bado atakuwa ni Edward Lowassa!.

Lakini kama ni kweli, hawa wenye boda boda, bajaj na umati uliojitokeza wamehongwa pesa ili kuleta tuu ujazo wa wingi wa watu, lakini hawajajiandikisha kupiga kura na sii wapiga kura, then hakuna ubishi, mshindi ataendelea kuwa ni CCM!.

Pasco wa jf, sio mwanachama, mfuasi au mshabiki wa chama chochote cha siasa, au mgombea yoyote, bali ni mkereketwa wa demokrasia ya kweli ndani ya bunge, ambaye anaamini kwenye ukweli na uwazi!.

Pasco

TANESCO Wamekata Umeme Sehemu Kubwa ya Nchi ya Tanzania, Leo 29th Aug 2015

$
0
0
Maeneo ya Moshi mjini umeme umekatwa tangia saa 3 asubuhi. Umeme umekatwa jijini Dar es salaam, na maeneo mengi nchini.
Yote Hii ni hujuma na mwendelezo ule ule wa kuinyonga demokrasia na kuwafanya watanzania kuwa watumwa miaka yote....

Je Kukatwa Huku kwa Umeme Kuna Mahusiano yoyote na Ufunguzi wa Kampeni za Ukawa Jagwani?

Edward Lowassa Avunja Rekodi ya Umati wa Watu Jangwani

$
0
0
Mkutano wa Ukawa wa Kuzindua Kampeni za Uchaguzi 2015 umemalizika huku wakiacha rekodi mpya ya  Avunja Rekodi ya Umati wa Watu Jangwani........

Hotuba ya Sumaye Jagwani ni Noma, Aongelea Ugonjwa wa Lowassa na Habari za Ufisadi Anazosingiziwa

$
0
0
Sumaye: Kwa ajili ya muda nitasema kwa kifupi sana, nimetoka chama cha mapinduzi, katibu mkuu alisema sisi ambao hatukuteuliwa hatukuwa na maadili, mimi nasema kama kipimo cha maadili ni mheshimiwa Kinana, mimi nitakuwa mtakatifu, CCM wamekuwa wakiongoza siasa ya chama kimoja kwa ngozi ya vyama vingi, mmekunjika kwa miaka yote.

 Tulitaka kufanya mabadiliko kulekule, kukawa na tatizo ndani ya CCM, ukitaka kufanya lolote wanakuzingira. Wanawajaza watanzania uoga wa usilolijua, mkiwapa wapinzani wataharibu nchi, kila binadamu ana uoga wa asilolijua.

Lowassa kwa kuliona hilo, kwa kuwa watanzania wanamfahamu aliona uoga wa aina hiyo haitakuwepo, na mimi nimekuja kwa sababu hiyo. Watanzania leo elimu yetu inashuka sana, tunashusha alama za kufaulu wanafunzi ionekane wamefaulu wengi, pia ukienda katika afya. Tunataka tubadilishe hali hiyo.

Leo Lowassa ametoka CCM ameonekana hafai, lakini ni KIkwete aliemfanya waziri mkuu wake, kuna Rais anaweka kiongozi ambae hafai? Lakini ni LOwassa huyuhuyu ndie aliemuingiza KIkwete Ikulu, Kwamba watanzania wanampenda Lowassa, halina mjadala.

Mmewasikia kwenye kampeni zao, fisadi mkubwa huyo amechukua fedha za matajiri, Lowassa amechukua ustaarabu wa kuwajibika. Waziri anachukua mzigo ili kumuokoa Rais na serikali yake. Asanteni sana.

Nyerere wakati anastaafu, kwenye kikao kimoja nafikiri cha halmashauri kuu. Alisema hajaona mtu mvumilivu kama Kawawa, alibeba mizigo aliyostahili kubeba yeye, ndiyo kazi aliyofanya Lowassa.

Vichwa vya treni vinavyonunuliwa, Lowassa alikuwepo? Wajenzi wa barabara nchi hii wanaidai serikali trilioni 1.4, kudai si tatizo katika hizo bilioni 900 ni pesa za adhabu, huo si ufisadi, mbona hawasemi? Serikali hii ni dhaifu sana na alituthibitishia katibu mkuu, mwenyewe kusema kuna mawaziri mizigo.

Mwisho wanalomsema nalo, Escrow Lowassa alikuwepo, kile kipande cha Lugemalira tulijua waliokula, kile kipande cha Habinder ni nani aliekula, tangu lini benki ikaruhusiwa kutoa cash kwa mabilioni. Wamejenga kibr, hawajali tena maumivu ya wananchi, naomba mwaka huu msikubali, watanzania mfurahie mabadiliko ya ndani ya vyama vingi.

Wanasema mgonjwa, mimi nataka niwaulize, kwani Magufuli mzima? Wanaenda kufanya nini Ulaya kama ni wazima, mtu yeyote ukishavuka miaka 50 hauwezi kuwa wazima kwa asilimia 100, hivi Rais mkapa alipokuwa madarakani hakwenda kufanyiwa operashi Ulaya, nchi ilidorora? Alienda akarudi akaikuta nchi usalama.

Kwani KIkwete alivyokuwa madarakani hakwenda kufanyiwa upasuaji mkubwa Markani??

 Rais si kazi ya kubeba zege Ikulu, anatakiwa kuwake timu nzuri ya kazi, yeye ni meneja tu, naomba sana tumchague itakapofika tarehe 25 Oktoba. Asanteni sana, nawashukuru.

LOWASSA Amesikia Vilio vya Watanzania Kuhusu Babu Seya na Mashehe wa Kiislam Walioko Jela...

$
0
0
Leo Jagwani Katika Uzinduzi wa Kampeni za Ukawa Lowassa Amewagusa Wengi baada ya Kuzungumzia Suala la Babu Seya ambaye yupo jela amefungwa kifungo cha Maisha yeye na mtoto wake ..Lowassa Amesema kuwa amesikia kilio cha wengi kutaka aachiwe huru hivyo atakapo ingia madarakani atalitazama swala hilo....
Pia Lowassa Ameongelea kuhusu Mashehe wa Kiislam ambao wako Mahabusu na wengine Jela nakusema kuwa atashughulikia endapo atapewa nafasi ya kuwa Rais.....

Rais Kikwete Awatahadharisha UKAWA Kuhusu kauli za uvunjifu wa amani

$
0
0
Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Rais Jakaya Kikwete amesema baadhi ya kauli zinazotolewa na Umoja wa Vyama vya Upinzani (Ukawa), zinaashiria uvunjifu wa amani pindi matokeo ya kura yatakapoanishwa baada ya zoezi la upigaji kura Oktoba 25 mwaka huu.

Rais Kikwete alisema baadhi ya kauli hizo zimekuwa zikionyesha wazi viashiria vya uvunjifu wa amani na upotoshaji kwa kundi kubwa la vijana ambao wanapiga kura kwa mara ya kwanza.

Akizungumza wakati akizindua Kampeni ya Mama Ongea na Mwanao jijini Dar es Salaam Rais Kikwete alisema;

“Wamediriki kusema wazi bila kificho kwamba patakuwa hapatoshi, hizi ni kauli zinazoashiria uvunjifu wa amani. Tunachokisema CCM ushindi kwetu ni lazima na tutashinda kwa kishindo na kwenda nginja nginja mpaka Ikulu.”

Kikwete alisema CCM imejipanga kuhakikisha inapata ushindi katika Uchaguzi Mkuu ujao na kuongeza kuwa ili kufanikisha hilo wamepanga kikosi kazi ambacho kitatembea nyumba kwa nyumba, chumba kwa chumba, mtu kwa mtu ikiwa kwa sasa tayari wameshaanza kufanya kampeni zao kupitia mtandao ya simu za mkononi.

Katika hafla hiyo ya kuzindua kampeni hiyo inayoratibiwa na msanii wa filamu na Miss Tanzania mwaka 2006, Wema Sepetu, Rais Kikwete aliwataka wanawake kaungalia mazuri yote yaliyofanywa na Serikali ya CCM katika kumuinua mwanamke.

Mwanangu Alifukuzwa Shule Kwa Kumpiga Mwenzie Aliyemtania Baba yake ni Teja – Q Chief

$
0
0
Q Chief amedai kuwa aliumia mno pale mtoto wake alipofukuzwa shule baada ya kupigana na mwanafunzi mwenzake aliyemtania kuwa baba yake ni teja!
10956351_663821843741171_1618248528_n
Q-Chief alikuwa akizungumza na BBC Swahili hivi karibuni.
1391193_700453833312677_2145510502_n
Mtoto wa Q Chief
“Siku moja mwanangu alikuja analia sana, akaniambia baba mwanafunzi mmoja amesema baba yake si teja tu. Nikamwambia kwahiyo ukafanyaje akaniambia ‘nimempiga ndio maana nimefukuzwa’, nikamuuliza ‘kwanini umempiga?’ akasema nimejisikia uchungu sana,” alisema.
“Kwahiyo nikaona kama mtoto wa miaka tisa anaweza kusikia uchungu, amenyimwa haki zote za malezi ya baba. Nikajiuliza sio watu wote wananijali zaidi lakini huyu ni doctor kesho au ni lawyer au atafanya kazi BBC, napaswa kuwa mfano mzuri kwake, nikaamka asubuhi nikasema inatosha.”
Source:Bongo5

Lulu Amechumbiwa? Picha Hii Yazusha Maswali Mengi

$
0
0
Elizabeth Michael aka Lulu amewaacha mashabiki wake njia panda baada ya kuweka picha inayoonesha amevaa pete ya uchumba.

Picha aliyoweka Lulu na kuibua maswali kibao kutoka kwa mashabiki wake

Kupitia ukurasa wake wa Instagram, mrembo huyo aliweka picha ya mitego ikiwa na caption ‘N.U.D.I’ na hivyo kuwaweka njia panda mashabiki wake.

Hizi ni baadhi ya comments za mashabiki:

Aubrey_bittoria. Is she engaged?

Ms_gikaro. Engagés or?

Richi_manyota. Ww lulu unatuuwa bhna

January Makamba Ampa MAKAVU Lowassa

$
0
0
Aliyekuwa mgombea Urais wa CCM ambaye pia ni Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya chama hicho, Januari Makamba, jana alimshukia mgombea urais kwa tiketi ya Ukawa, Edward Lowassa kwamba ni mroho wa madaraka.

Makamba alitoa kauli hiyo katika viwanja vya Barafu mjini Dodoma wakati akimnadi mgombea ubunge wa Jimbo la Dodoma Mjini, Anthony Mavunde. January alisema kuwa Lowassa ameivuruga demokrasia ndani ya Chadema na kupeleka mizengwe itakayokiua chama hicho na umoja wao.

“Yale siyo mabadiliko kama wanavyojinadi bali ni uroho wa madaraka kwa mtu mwenye uroho na chama chenye uroho, lakini hawezi na hawawezi kushika madaraka ya kuongoza nchi,” alisema Makamba.

Alisema kinachoendelea kwa vyama vinavyounda Ukawa ni maigizo na siyo mabadiliko ya kweli kwa sababu mgombea urais ametoka CCM na Sera za CCM na mgombea mwenza ametoka CUF na sera za huko, hivyo hawawezi kuungana kwa pamoja kwa sababu hawajui nini maana ya kile wanachogombea.

Hata hivyo, Makamba alikiri kuwa uchaguzi wa mwaka huu ni mgumu kuliko uchaguzi wowote uliowahi kutokea katika mfumo wa vyama vingi na akawataka wana CCM kujiandaa kikamilifu.

Alisema CCM kinapaswa kuwa makini na imara wakati wote ili kutoyumba na wakifanya hivyo watajikuta wanapata mchanganyiko ambao utaleta shida katika maendeleo.

Kwa upande wake mgombea ubunge Mavunde alijipachika jina la Mr Makao akisema lazima ataipelekea Dodoma hadhi ya kweli katika kufikia makao ambayo yamekuwa yakisemwa kama hisani.

Mavunde aliomba wananchi kumwamini na kumpa nafasi hiyo kwani ana uhakika kwa miaka mitano ataifanya Dodoma kupaa kiuchumi huku akisema atashughulika na watu wenye kipato cha chini pamoja na kumaliza migogoro ya ardhi.

Aliyekua Waziri wa Elimu Joseph Mungai na Mkewe Watangaza Kuhama CCM na Kujiunga na CHADEMA

$
0
0
Aliyekua Waziri wa Elimu Joseph Mungai na mkewe wametangaza kuhama CCM na kujiunga na CHADEMA Mafinga leo ambapo mgombea urais kupitia UKAWA /CHADEMA Edward Lowassa yupo mkoani Iringa kwaajili ya kampeni

Diamond Platnumz Atoa Wimbo Mpya wa Kumpigia Kampeni Magufuli wa CCM, Usikilize Hapa– CCM No-1

$
0
0
Diamond kaamua kuja na hii mpya, ameipa jina CCM No-1 ikiwa ni maalum kwa ajili ya kampeni za uchaguzi mkuu mwaka huu. Isikilize hapa….

Lowassa AFUNIKA Iringa.....Maelfu Wahudhuria Mkutano wake, Awataka Wafuasi wake Wazilinde Kura Zisiibiwe

$
0
0
Mgombea Urais kwa tiketi ya Chadema, Edward Lowassa amesema amechoshwa na manyanyaso wanayoendelea kuyapata wakulima hapa nchi kwa kukopwa mazao yao na kutozwa ushuru na serilkali bila ya wao kupata faida yoyote.


Lowassa alisema punde atakapochaguliwa kuongaza nchi kitu kikubwa atakachokifanya kuwasaidia wakulima ni kufuta ushuru wote wa mazao kuhakikisha wakulima wananufaika na jasho wanalolitoa wakati wa kilimo.



Lowasa ameyasema hayo leo wilayani Mufindi alipofanya mkutano wa hadhara wa kampeni katika Uwanja wa Shule ya Msingi Wambi, mjini Mafinga.



Lowassa alisema watu wamekuwa wakizungumza kuwa CCM ni wezi wa kura kwasababu ni wajanja sana katika kufanya michezo michafu katika chaguzi na maneno hayo si yakuyabeza wala kuyafumbia macho.



“Mimi nataka kila mtu akihifazi vizuri kichinjio chake (kadi ya kupigia kura) na siku ya kupiga kura ikifika nawaomba wanawake na wanaume wajitokeze kwenda kupiga kura ila wakina baba nawaomba mkishapiga kura fanyeni kazi ya kuzilinda kura zenu” alisema Lowassa



Katika mkutano huo, waziri wa zamani wa Elimu, Joseph Mungai alipanda jukwaani na kumnadi Mgombea Ubunge wa Jimbo la Mafinga Mjini kupitia Chadema, William Mungai ambaye ni mtoto wake.



Mungai aliwahi kuwa mbunge kwa miaka 35 kupitia CCM na aliweza kuteuliwa nafasi mbalimbali za uwaziri ikiwamo Wizara ya Kilimo, Mambo ya Ndani na Wizara ya Elimu.



Mungai alisema wananchi wa jimbo hilo wanatakiwa kumchagua William Mungai kwa sababu mbunge aliyemaliza muda wake katika jimbo hilo hakuweza kuongoza kama alivyofanya yeye.


Fanya Haya! Unapotokea Kumpenda Mtu aliye na Mpenzi Wake

$
0
0
Tumshukuru Mwenyezi Mungu ambaye ametuwezesha kuonana tena wiki hii tukiwa wazima. Lakini pia tumshukuru kwa kutuletea kitu kinachoitwa mapenzi. 

Mapenzi yamekuwa yakichukua nafasi kubwa sana katika maisha yetu ya kila siku na yamekuwa yakichangia kwa kiasi kikubwa furaha kwa kila mtu.

Kama huamini, angalia wale waliotokea kupenda na wao wakapendwa, utabaini nyuso zao zimetawaliwa na furaha isiyo na kifani. Lakini mapenzi hayo hayo yamekuwa ni chanzo cha vilio kwa baadhi ya watu.

Mpenzi msomaji wangu, kupenda hakuna macho! Moyo ukishapenda hausikii la kuambiwa. Katika hili ndiyo maana unaweza kumuona mwanaume kazimika kwa demu ambaye hawaendani kabisa lakini moyo wake ndiyo umeshapenda.

Ilishawahi kutokea msichana akampenda kijana mmoja ambaye ni fukara kupita maelezo. Yeye akawa ndiyo anamhudumia kwa kila kitu. Akamfanyia mpango wa ajira na mwisho wake wakafunga ndoa.

Sasa hivi wanaishi maisha ya furaha na amani. Wamegeuka mfano wa kuigwa kwa jinsi wanavyopendana lakini huko nyuma msichana huyo alikuwa akichekwa kwa kutoa penzi kwa mwanaume asiye na mbele wala nyuma.

Hayo ndiyo mapenzi jamani! Lakini pia katika kufurukuta kumtafuta mpenzi wa kuwa naye maishani, mwanaume anaweza kujikuta unaangukia kwa demu ambaye tayari ana mpenzi wake. 

Moyo wako unakuambia yeye ndiye mtu sahihi katika maisha yako lakini tayari ana mtu wake, unafanyaje? 

Utapambana kuhakikisha unapata kile ambacho moyo wako umekipenda au utakubaliana na ukweli kwamba huwezi kuwa naye kwa kuwa ana mtu wake? Inapofikia hatua hiyo unaweza kujikuta upo njia panda hasa pale ambapo huyo mwenye mtu wake naye anaonesha kuwa na chembechembe za mapenzi kwako.
Kuna mambo kadhaa ya kukusaidia kukabiliana na hali hii.

Chunguza
Tumia muda wako mwingi kuchunguza juu ya uhusiano wake. Uhusiano wao umesimama na wanaonekana ni watu wenye ‘future’? Nasema hivyo kwa sababu, yawezekana uhusiano wa huyo uliyetokea kumpenda ni wa kuzuga tu na huenda wewe ndiye mwenye ‘future’ naye. Ndiyo maana nikasema chunguza uhusiano wake kwanza.

Usitafute uadui
Baada ya kuchunguza, ukibaini kwamba uhusiano wao hauko ‘siriasi’, vuta subira, lolote linaweza kutokea na likaufurahisha moyo wako. Lakini kama utaona ni watu walio siriasi na wanaelekea kuoana, usitafute uadui bure, kaa pembeni.

Una nafasi kwake?
Sawa umetokea kumpenda msichana aliye na mtu wake, umeshawahi kujiuliza kama una nafasi ndani ya moyo wake? Anaonesha dalili fulani za kukupenda kama unavyompenda na ni mtu anayeonesha kukumisi anapokuwa mbali na wewe? Utakapobaini una nafasi kwake, uamuzi wa kumpotezea hautakuwa na nafasi.

Ni rahisi kubadili uamuzi wake?
Unadhani huyo uliyetokea kumpenda anaweza kubadili maamuzi ya kumuacha huyo aliyenaye kama kweli hawana ‘future’? Utagundua hilo kwa kuongea naye na kumsikia kama anaweza kufanya maamuzi hayo ili awe na wewe.

Pingana na moyo wako
Ifike wakati upingane na moyo wako. Unajua moyo wako kukuambia kuwa unataka kuwa na uhusiano na demu ambaye tayari ana mpenzi wake wakati mwingine utakuwa unakupotosha. 

Kwa hiyo ukiona vipi, pingana nao. Acha kumng’ang’ania msichana mwenye mpenzi wake licha ya ukweli kwamba, huenda wewe ndiye mwenye nafasi ya kuwa mume wake na siyo huyo aliye naye.

Urafiki ni poa?
Umempenda sana na hauko tayari kumkosa katika maisha yako lakini imetokea kwamba tayari yuko na mtu na umebaini huna nafasi kwake kabisa? Usiumie, omba angalau urafiki. Siyo urafiki wa kivile sana ila angalau pale unapotaka kusikia sauti yake kwa kumsalimia tu, upate nafasi hiyo.

Usiumie, yupo mwingine
Haina haja ya kujitafutia vidonda vya tumbo bure kwa kuwa tu umebaini uliyetokea kumpenda tayari ana mtu. Chukulia ni hali ya kawaida, mademu wazuri ambao wanaishi singo wapo kibao huko mtaani, ni suala la wewe kutulia tu. Amini yupo mwingine ambaye atayafanya maisha yako yawe ya furaha.

Naomba nihitimishe kwa kusema kwamba, unapotokea kumpenda mtu fulani, pambana kuhakikisha unampata kwa sababu ukimkosa maisha yako yanaweza kuwa gizani. Ila pale utakapoona uwezekano wa kuwa naye haupo, usilazimishe ndugu yangu. Kumbuka haya ni maisha tu!

Wakili Maarufu Peter Kibatala Aeleza Mantiki Ya Lowassa Kuwatoa Masheiks & Babu Seya

$
0
0
Babu Seya na Mwanawe Wakiwa Chini ya Ulinzi wa Magereza
Kuna watu wanajaribu kupotosha nini hasa mantiki ya Mgombea Edward Lowassa kuahidi kushughulikia suala la Sheikhs wa Zanzibar na suala la Babu Seya.
Suala la Sheikhs wa Zanzibar liliihusisha Chadema kabla hata Lowassa hajahamia huku. Binafsi niliombwa na Dr Slaa kulishughulikia, lakini bahati mbaya nilikuwa nina cases kadhaa zilizonifanya nikwame. Lakini cha muhimu zaidi ni kwamba wana Wakili, tena Wakili mahiri tu na ambaye ni Mwanachama wa Chadema. Amepambana sana, na anaendelea mpaka leo.

Issue yao ni complicated, na ni mfano tu wa issues zinazo athiri haki za wananchi kwa kukosekana tu utashi sahihi wa kisheria na kiutawala.
Mojawapo wa pertinent issues ni mgogoro wa iwapo wanatakiwa kishtakiwa Bara, au Zanzibar inakosemekana walitenda huo ugaidi. 
Na kuna masuala ya Sheiks wale kulalamika kutendewa kinyume wakiwa chini ya ulinzi. 
Kuna suala pia la ucheleweshaji wa upelelezi, hata kama tuna-assume case dhidi yao ina mashiko.
Asiyefahamu anaweza kudharau uzito wake, lakini ni suala linaloleta hisia kali kwa sehemu ya waumini wa kiislamu. 
Lowassa atakuwa Rais wa ajabu kama vision yake ya kisheria haitajumuisha suala pertinent kama hilo. Huwezi jadili general concepts bila kuchagua specifics kadhaa kama mfano. 
Pia, Lowassa hajasema atamtoa Babu Seya kwa stroke ya pen on a whim. Wala hajasema hiyo ni priority yake above all else kwa upande wa sheria. Alichosema within the limited confines za muda ni kwamba serikali yake itakuwa makini sana na masuala ya utawala wa sheria. Issue ya Babu Seya na hao Sheiks ni representation tu ya matatizo yaliyopo. Na malalamiko yaliyopo. Issue ya Lawrence Masha na wale vijana 19 wa 4U Movement tuliowapigania juzi, imepigia mstari.
Pamoja na kwamba ni suala linalogawa opinion, ni naivety kujidai eti issue ya Babu Seya si moja ya issues zinazoleta mjadala wa kisheria na kihisia mpaka leo hii. Suala la ni namna gani linashughulikiwa, ni suala la ushauri wa kisheria kutoka kwa wataalamu wa Rais Lowassa (kipindi hicho).

LOWASSA Asema anahitaji Kura Milioni 10 tu ili Awe Rais wa Tanzania........Asisitiza Tena Watu Wakipiga Kura Wabaki Wazilinde Zisiibiwe

$
0
0
Mgombea urais wa Chadema anayeungwa mkono na vyama vinavyounda Ukawa, Edward Lowassa amesema kama Watanzania watashindwa kufanya mabadiliko kwa kupiga kura kuing’oa CCM madarakani mwaka huu, hawataweza kufanya hivyo tena, huku akihoji kama vyama tawala mbalimbali katika nchi za bara la Afrika vimeng’oka madarakani: “Kwa nini isiwe CCM”.

Akizungumza katika mkutano wa hadhara wa kampeni katika Uwanja wa Gangilonga Iringa Mjini uliohudhuriwa na mamia ya wakazi wa mji huo, Lowassa aliyeambatana na Waziri Mkuu wa zamani, Frederick Sumaye alisema vyama tawala vilivyokuwa rafiki na CCM vimeshang’oka madarakani na kwamba hivi sasa ni zamu ya chama hicho tawala kuondolewa.

“Nataka kura nyingi ili hata wakiiba tushinde, asilimia 90 ziwe zetu hizo 10 waache waibe. Msipoiondoa CCM mwaka huu hatutaiondoa tena, CCM na Tanu walikuwa na marafiki zao lakini karibu wote wameondoka.

“Chama cha Kanu cha nchini Kenya kimeshaondoka madarakani, kile cha Malawi (Malawi Congress Party) nacho kimeondoka, UNIP (The United National Independence Party cha Zambia) nacho imeondoka na kile chama cha Mzee Obote (Dk Militon) cha Uganda kimeondoka, tunaona pia jinsi Rais wa Zimbabwe (Robert Mugabe) anavyohangaika,” alisema Lowassa.

Katika mkutano huo, Lowassa alirudia vipaumbele vya ilani ya uchaguzi ya Ukawa, huku akimponda mgombea ubunge wa Jimbo la Iringa Mjini kwa tiketi ya CCM, Frederick Mwakalebela kuwa hawezi kushinda kwa maelezo kuwa amepanda gari bovu.

Sumaye alieleza ufisadi mbalimbali uliotokea tangu Lowassa alipojiuzulu mwaka 2008, huku akihoji yalipo majina ya wauza dawa za kulevya na majangili ambayo alidai kwa nyakati tofauti Rais Jakaya Kikwete amenukuliwa akisema kuwa anayo.

Mkutano huo ulihudhuriwa na idadi kubwa ya wananchi ambao walianza kufika uwanjani saa nne asubuhi kutoka maeneo mbalimbali ya mkoa huo. 

Baada ya kumalizika kwa mkutano huo saa 11.58 jioni, baadhi ya wananchi hao walilisukuma gari la Lowassa na mgombea ubunge wa Iringa Mjini kwa tiketi ya Chadema, Mchungaji Peter Msigwa hadi katikati ya mji huo kabla ya magari hayo kushika kasi na kuwaacha wakiendelea kukimbia barabarani huku wakiimba nyimbo mbalimbali.

Baadhi yao walionekana kubeba kitu mfano wa jeneza na kukivisha bendera ya CCM huku wakisema mwisho wa chama hicho tawala ni Oktoba 25.

Aomba kura milioni 10
Akiwa Mafinga Mjini, Lowassa alisema anahitaji Watanzania wampigie kura si chini ya milioni 10.2 ili awe rais na kumaliza kilio cha wakulima nchini.

Akiwa katika siku ya kwanza ya kampeni zake mikoani hapa, Lowassa aliwaeleza wananchi wa Mafinga kuwa amechoshwa na manyanyaso ambayo wakulima wanaendelea kuyapata ikiwamo kukopwa mazao yao na kutozwa ushuru na Serikali bila ya wao kupata faida yoyote.

Lowassa alisema mara atakapochaguliwa kuongoza nchi, kitu kikubwa atakachokifanya kuwasaidia wakulima ni kufuta ushuru wote wa mazao na kuhakikisha wananufaika na jasho wanalolitoa wakati wa kilimo.

Katika mkutano huo uliofanyika katika Uwanja wa Shule ya Msingi Wambi, Mjini Mafinga, Lowassa alisema: “Nakataa wakulima kuendelea kukopwa mazao yao na kutozwa ushuru, kuendelea kufanya hivi ni kuwanyonya na kutaka waendelee kuwa maskini wakati wao wanafanya kazi kwa kujituma sana.”

Alisema hayo yatafanyika iwapo wananchi watampigia kura za kutosha na kuzilinda huku akigusia madai kwamba CCM ni wezi wa kura na kubainisha kuwa maneno hayo si ya kubeza wala kuyafumbia macho.

“Mimi nataka kila mtu akihifadhi vizuri kichinjio chake (kadi ya kupigia kura) na siku ya kupiga kura ikifika nawaomba wanawake kwa wanaume wajitokeze kwenda kupiga kura ila kina baba ninawaomba mkishapiga kura fanyeni kazi ya kuzilinda kura zenu,” alisema Lowassa na kuongeza: “Kweli CCM ni wajanja sana kazi tunayotakiwa kufanya ni kuziba mianya yote, hata kama tukipigwa chenga wawe wamepata asilimia 10 ili asilimia 90 zibaki kwetu.”

Sumaye: Tunataka wabunge 300
Akizungumza katika mkutano huo, Sumaye aliwataka wananchi wa Mafinga kutokuwa na shaka na Ukawa kwa sababu wamejipanga vizuri kuhakikisha wanapata ushindi katika uchaguzi wa Oktoba 25, licha ya CCM kujipanga kupata ushindi wa goli la mkono.

“Tunawaomba Watanzania wachague Ukawa kwa sababu umefika muda wa mabadiliko, tunataka tupate wabunge 300, hizo nafasi nyingine wagawane vyama vingine vilivyo nje ya Ukawa,” alisema Sumaye.

Alisema Serikali ya sasa ni dhaifu kwa sababu wamekuwa wakipeana nafasi ya uongozi kindugu na ushikaji, hali inayofanya wananchi kuendelea kupata shida.

“Tumemwambia Lowassa akichaguliwa anatakiwa kuunda Serikali inayowajibika kwa umma tofauti ya Serikali iliyopo sasa madarakani, chama kinapokuwa madarakani kwa muda mrefu kinajenga kiburi na dharau kwa wananchi wake na ndivyo inavyofanya CCM sasa, ni muda wake kuondoka madarakani,” alisema Sumaye.

Sumaye alisema amekuwa akisikia CCM wakisema Magufuli hana utani na rushwa wakati amekuwa waziri wa ujenzi kwa miaka kadhaa na bado kumekuwa na tuhuma za rushwa katika sekta ya ujenzi.

“Nataka kumuuliza Magufuli, yeye ni waziri wa ujenzi, ameshindwa kitu gani kuondoa rushwa katika wizara yake halafu anakuja kusema akiwa rais ataweza?” alihoji Sumaye.

Katika mkutano wa pili wa Lowassa uliofanyika katika Uwanja wa Maendeleo wa (FDC), Ilula katika Jimbo la Kilolo, aliwataka wananchi wamchague ili awaondolee kero zinazowakabili ikiwamo ya ukosefu wa maji.

Katika uwanja huo uliofurika huku wananchi wakiwa na mabango mbalimbali yanayoeleza kero zinazowabali, Lowassa aliwataka wasiwe na hofu na yeye katika kutatua kero za maji na kama wanabisha wawaulize wananchi wa Mkoa wa Shinyanga ambao walihangaika kwa muda mrefu na kero ya maji lakini aliwezesha mkoa huo kupata maji kutoka Ziwa Victoria.

Alisema atahakikisha elimu inapanda kwa kasi ili kupunguza umaskini. “Najivunia na ujenzi wa shule za kata nchini kwani Mkoa wa Iringa ulikuwa maarufu kwa kutoa wasichana wanaokwenda kufanya kazi za majumbani, lakini kwa sasa kuwapata imekuwa shida baada ya kupatikana shule hizo ambazo zimeleta mapinduzi hayo,” alisema Lowassa.

Kuhujumiwa
Lowassa alisema Ukawa wamekuwa wakihujumiwa katika mchakato wa uchaguzi ikiwamo kukataliwa kufanya mambo kadhaa na kukatwa umeme pindi mikutano ya hadhara ya chama hicho inapokuwa ikirushwa moja kwa moja na televisheni.

“Hata wakikakata umeme, CCM hawatatuweza, wamezoea kutuhujumu ila tarehe 25, mwezi Oktoba hawawezi kukata umeme kwenye vichwa vya watu wanaotaka  mabadiliko."
Viewing all 104789 articles
Browse latest View live




Latest Images