Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104663 articles
Browse latest View live

STEVE NYERERE UENYEKITI WA BONGO MOVIES WAANZA KUMTOKEA PUANI..WAWA MCHUNGU

$
0
0
Steve Nyerere Amesema Inamuwia vingumu kufanya kazi kutoka na kukosa ushirikiana kutoka kwa wana bongo Movies wenzake ..Amehabarisha kuwa kuna baadhi walio mchagua kuwa mwenye kiti wao ili wamzalilishe na kuona kama ataweza , na hilo analiona sasa kwani kuna baadhi waliomchagua wananyima ushirikiano....

AY AKANUSHA KUMTUNGIA NYIMBO JAGUAR...APINGA KUWA DIAMOND NI TISHIO KWAKE

$
0
0
Msanii wa HipHop kutoka Tanzania, Ambwene Yesaya amekanusha uvumi uliokuwa umezagaa nchini Kenya wa kumuandikia baadhi ya nyimbo mkali wa Kioo kutoka Kenya, Jaguar.

Katika mahojiano aliyofanyiwa nchini Kenya alikokuwa ameenda hivi karibuni, AY amesema hajawai kumuandikia wimbo wowote Jaguar na hata wimbo wao ‘Nimetoka Mbali’ kila mtu aliandika mashairi yake.

“Jaguar ni mmoja wa marafiki zangu. Tumefanya kazi pamoja na hakuna ukweli wowote kuhusiana na tetesi za mimi kumuandikia mashairi ukizingatia amekuwepo kwa muda mrefu kwenye gemu ya muziki hivyo kumfanya kuwa miongoni mwa wasanii wenye uzoefu wa kutosha na kufanya vizuri hata ukitazama ngoma niliyowahi kufanya nae ya Nimetoka Mbali, kila mmoja wetu aliandika mashairi yake kivyake hivyo huna haja ya kubisha kwa uwezo mkubwa alionao na naamini ni ushahidi tosha,” alisema.

Pia AY amepinga muziki wake kuathiriwa na Diamond kwakuwa kila mtu ana malengo yake katika muziki wake.

“Kila msanii ana mipango na mikakati yake ya kufikia malengo aliyojiwekea, sipo kujilinganisha na mtu yoyote, ushindani wangu ni kwa yule anayetaka kujaribu kutengeneza mkwanja mkubwa kushinda wangu, huo ndio ushindani wa kweli, hata hivyo siwezi kuwa juu milele.”

Source:Bongo5

PICHA MBALI MBALI ZA NICK MINAJ AKIWA BILA WIGI...SHE IS CUTE I LIKE HER LIKE THIS

$
0
0
 Jionee Mwenye Mtoto Alivyo Bomba ...Hapo kaweka Usela wote pembeni na yale mawigi yake ya kishetani pembeni ...mtoto unywele Anao ...Dahhhh She is Cute ......
Check picha alafu ucomment




MVUA ILIYOAMBATANA NA UPEPO MKALI DSM HUENDA IKAENDELEA HADI JUMATANO

$
0
0
Mvua iliyoambatana na upepo mkali uliovuma usiku wa kuamkia leo jijini Dar es Salaam umesababisha umeme kukatika kwa zaidi ya saa sita katika sehemu kubwa ya jiji hilo,miti kuanguka pamoja na wavuvi kusitisha shughuli za uvuvi ili kunusuru maisha yao huku mamlaka ya hali ya hewa ikisema upepo kama huo huenda ukaendelea kutokea nchini hadi Jumatano ijayo.
ITV imepita katika sehemu mbalimbali za jiji la Dar es salaam majira ya asubuhi na kushuhudia miti ikiwa imeanguka pembezoni  mwa barabara pamoja na nguzo za umeme zikiwa katika hali ya kutaka kudondoka .
Katika sehemu kubwa ya jiji la Dar es Salaam umeme ulikatika wakati upepo huo ukivuma  ambapo  mafundi wa  shirika la umeme Tanzania -Tanesco wameonekana  majira hayo ya asubuhi wakiwa katika harakati za kurejesha umeme.
 Nao baadhi ya wavuvi waliokuwa baharini wakivua wakati upepo huo ukivuma wamesema  waliamua kusitisha shughuli zao na kuzielekeza mashua na boti walizokuwa wakizitumia katika sehemu zilizo salama ili kunusuru maisha yao.
Kwa upande wao mamlaka ya hali ya hewa kupitia mkurugenzi wake mkuu Agness Kijazi amesema upepo huo umesababishwa na mgandamizo mdogo wa hewa uliopo katika eneo la kusini/magharibi mwa Madagascar ambapo sasa wanalazimika kupata hewa kutoka misitu ya nchi ya jamhuri ya kidemokrasia ya Congo,na hivyo kusababisha upepo mkali unaoambatana na unyevunyevu katika sehemu ambazo hewa hiyo inapita na kwamba hali hiyo huenda ikaendelea mpaka Jumatano ijayo. ITV

ROSE NDAUKA AMUWEKA HADHARANI MTOTO WAKE....VERY HEALTH BABY

$
0
0

Star wa filamu Swahiliwood, Rose Ndauka amemuweka hadharani mtoto wake aliyejifungua hivi karibuni na kumpa jina la Naveen yeye na baba mtoto wake Malick Bandawe(Chiwaman). Kupitia 
mtandao mmoja wa kijamii Rose aliweka picha ta mwanae jioni hii na kuandika "nachukua nafasi hii kuwashukuru wote mlioweza kuwa na mimi na mpaka sasa tumepata mtoto wetu anayeitwa naveen na leo ikiwa tunasogelea arubaini yake tarehe 9/02/2014 basi nawaomba dua zenu na hii ndio zawadi niliopata kwa mungu nashkuru sana kwa zawadi hii shukran mama yangu mzazi na malick kwa zawadi hii... nawapenda sana"

DIRECTOR ADAMU JUMA AKUTA USO KWA USO NA DIRECTOR NISHER LEO...WALIZIKA BEEF LAO

$
0
0
Katika mechi ya kikapu leo kati ya team Adam Juma na team Karabani kulikuwa na vitu vingi vizuri sana moja wapo ilikuwa ni hili, baada ya mechi kuisha na team ya Adam Juma kuondoka na ushindi watu wengi walikuwa na furaha sana moja wapo ni hili la Director Nisher alipotoka sehemu alipokuwa akitizama mechi hii na kwenda hadi katikati ya uwanja na kumfuata Director Adam Juma na kumpongeza kwa kile kilichofanyika na kuzungumza mambo mengine na kuacha tofauti zile zilizotokea na hadi watu kujua kuwa kuna BEEF la chini chini linaendelea.
Nimefurahi sasa mimi kama DJ CHOKA na vitu kama hivi vinatakiwa viwe poa kwasababu hawa ndio wanaopeperusha bendera yetu mbali kwenye upande wa video za wasanii wa kibongo so tofauti zinapotokea haina budi kuzimaliza. One

TIPS ON HOW TO FORGIVE A CHEATING PATNER AND SAVE YOUR RELATIONSHIP

$
0
0
Tips On How To Forgive A Cheating Partner And Save Your Relationship
I understand that I am on that drake tip right now but Valentine’s Day is around the corner. Some things have to be said and some problems have to be solved. So here we go.

.Many people will agree that nothing hurts as much as the discovery of a partner’s affair. An affair doesn’t have to close the curtains in a relationship. In fact, it can be a new beginning of reevaluation and fresh impetus. It can bring a couple closer than ever. One important thing is that you should only be ready to forgive when you are sure you really love your partner and can’t do without him or her. If the cheating has broken you to a point of no return, don’t forgive just because they are begging.

There serious are things to watch out for along the way if you are ready to forgive and want a healthy, lasting relationship post-infidelity. Here are tips for couples who are trying to pull through from infidelity on one partner’s side;

1. Understand the reality of this affair.

The fact and issue is it happened and with the facts you have (make sure you are not just suspecting things, be sure)…and once you both know the truth, the next thing is to understand what really matters. What really happened?

If she did have sex with him, that is really difficult to get over, but it can be done if it isn’t a behavioral pattern. The rule of thumb with affairs is this: if it happens once, you can get over it. If it happens twice or more, it’s a pattern, and you can’t get over it because it will happen again….so what do you do?

2. Make a decision about your partner’s character.

If you believe that your partner is fundamentally untrustworthy, and will continue romping off even after forgiving her several times, move on. You will always feel like you’re settling and they will feel like they can never prove herself.

However, if you believe that your partner made this one mistake, but overall you know him or her to be a person of integrity and someone you can trust, then embrace the person you know her to be. Set aside the mind-chatter about what they did with the other person and return to your previous mindset of who they are — a person you can trust and love.

Guard your thoughts and feelings about them and never let yourself doubt them again. Your love and trust will lift them up and they will shine.

3. Take responsibility for your side of this.

You didn’t cause their behavior, but affairs are often a symptom of underlying issues in the relationship that have not been addressed.

Look hard in the mirror and ask yourself what, if anything, you may have done or not done that contributed to them seeking intimacy with another person. If you can work on your side of the fence, it will only strengthen your relationship going forward.

And one very strong emotion you will use and need is love.

Does your partner love you all through this and is willing to fight for this love and earn your trust again? Do you still love them yourself and still hurt because of that love? Love concurs all. Mend things if you can, or move on if you just can’t forgive.

MH. LOWASSA AKANA UMILIKI WA KURASA ZA MITANDAO YA KIJAMII

$
0
0
Kumekuwa na kurasa (accounts) mbalimbali zenye jina la Mh. Edward Lowassa Waziri Mkuu Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika mitandao ya kijamii Kama vile Facebook,Twitter,Instagram nk.
Zinazoonye kuwa mmiliki wake ni Mh. Edward Lowassa.
Ukweli ni kwamba hizo kurasa zote hazimilikiwi na Mh. Lowassa.
Kwa maana hiyo chochote kinachoandikwa au kuchapishwa kwenye kurasa hizo,hazihusiani kwa namna yoyote na Mh. Lowassa.
Hata hivyo Mh. Lowassa anawashukuru wote wenye kumiliki account hizo bila ya ruhusa yake, kwani anaamini wamesukumwa na mapenzi yao kwake.
Imetolewa na 
Ofisi ya Mh. Edward Ngoyai Lowassa 
Mbunge wa Jimbo la Monduli.

SHILOLE AYAZUNGUMZIA MAKAVU LIVE ALIYOPEWA NA BABY MADAHA.

$
0
0
Baada ya msanii wa Candy n Candy, Baby Madaha kufunguka akimchana wazi msanii mwenzake wa kike, Shilole aka Shishi Bybee kwa kudai kuwa nyimbo zake haziwezi kulinganishwa na nyimbo anazofanya Shilole, Shilole nae kakikalia kiti kile kile na kuyajibu makavu hayo.

Shilole amedai kuwa hawezi kupoteza muda kumzungumzia Baby Madaha, na kwamba yeye anaamini hana tatizo naye lakini anashangaa kuona anamzungumzia.
Udaku Specially
“Ni kama Baby Madaha anavyonizungumzia mimi, mmekua mkiona na wengine mliumia mkasema sana kwa nini ananizungumzia mimi. Baby Madaha sina tatizo naye lakini nashangaa amekuwa mtu wa kunizungumzia everyday, I don’t know why.” Amesema Baby Madaha.

Mkali huyo aliamua kumpa ushauri Baby Madaha kwa kile alichokiita kumsema yeye vibaya ni kupoteza muda wake.

“Wewe mwanamke, mimi mwanamke mwenzio nafanya kazi, umeshaniona hata siku moja naenda kukuzungumzia somewhere? Muogope Mungu kukaa unamzungumzia mtu ambaye hana time, hana shida na wewe. Hebu tubadilike wanawake tupendane tuache kuzumziana vibaya.” Shilole ameeleza.

“Kwani ukinizungumzia mimi vizuri utapata nini, najua kuna vitu vingi nimekuzidi lakini usikae unamzungumzia vibaya. Wanawake tupendane tupeane sapoti. Ndio maana hatufiki mahali tunabaki tu kulalamika ‘ooh nimerogwa’, hujarogwa umejiroga mwenyewe.” Shilole anakaririwa.

Chanzo: Channel 10

NAJIONA NIPO TOFAUTI NA WANAWAKE WENGINE..ILA I ADMIRE MY PERSONALITY

$
0
0
Kama kichwa cha habari kinavyosomeka hapo juu,najiona natofautiana kimtazamo na wanawake wengi hapa duniani.
1. Wanawake wengi hawapendi kuadhibiwa na waume zao au wapenzi wao. Lakini mimi huwa napenda nikifanya kosa niadhibiwe. Nikisema kuadhibiwa simaanishi kupigwa hadi kudhalilishwa,No! namaanisha nikifanya kosa au ku behave tofauti mpenz wangu anigombeze na ikiwezekama kama nimemkasirisha sana hata anizabe kibao kimoja. Kwa kufanya hivi huwa nahisi ananipenda na ananijali.

2.Napenda sana mpenzi wangu awe "possesive towards me". Nikisema kuwa possessive toward me namaanisha mwanaume awe "ananimiliki".napenda mpenzi wangu anichukulie kama mimi ni mali yake, na si ya mtu mwingine.Kwahyo awe na authority na mimi, ajue nipo wapi? na nani? Nafanya nn?.Awe na wivu na mimi.Ila wanawake wengi, hulalamika kuwa wanafuatiliwa sana, kama mwanaume aki act hivi.
This is all I wanted to share with you friends! Enjoy your weekend!
From Malkia wa Urembo JF

SUGU AWAPA MAKAVU LIVE BILA CHENGA KINANA NA NAPE

$
0
0
Akihutubia mkutano wa kufunga kampeni za udiwani kata ya malindo wilayani rungwe,Sugu amesema yeye kajenga ghorofa jijini mbeya na wala si mpangaji kama adhanivyo nape pia kamwambia kinana kuwa karibu na wakulima ni kuwapa mbolea na si kupiga picha na wakulima kisha kutoa gazetini. Akizungumzia hoja ya nape aliyesema sugu ni mpangaji jimbo la mbeya mjini sugu amekosoa hoja hiyo,pia kuhusu mgogoro ndani ya chadema kasema imebaki historia ila wana ccm wana gogoro linalokua kila siku.hakika nguvu ya umma hakuna kulala!

BAO 5-1 ZAMCHANGANYA ARSENE WENGER APIGA MWELEKA WA NGUVU-PHOTOS

$
0
0
Kipigo cha bao tano cha jana kilimchanganya kabisa Arsene Wenger mpaka akapiga mweleka wa nguvu alipokuwa anaondoka katika mjio huo baada ya kutembezewa kichapo hicho ...Aibu ya Mwaka kwa Arsenal ..Tuwazomeeee

JAKAYA KIKWETE ATEUWA MAJINA YA WABUNGE WA BUNGE LA KATIBA

$
0
0
Hatimaye Rais Jakaya Kikwete amekamilisha uteuzi wa majina ya Wajumbe 201 wa Bunge Maalumu la Katiba, litakaloanza vikao vyake Februari 18 mjini Dodoma.

Kupitia uteuzi huo amewarejesha bungeni wanasiasa wakongwe akiwamo Kingunge Ngombale Mwiru na Paul Kimiti na kuwakumbuka pia wanasiasa wakongwe ambao hawakuwahi kuwa wabunge.

Baadhi ya wanasiasa hao ni pamoja na Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF), Profesa Ibrahim Lipumba, Mwenyekiti wa Chama cha (NLD) Dk Emmanuel Makaidi na Mwenyekiti wa Chama cha Ustawi Tanzania (Chausta) James Mapalala.

Pia wamo Mwenyekiti wa Chama cha Democratic Party (DP), Mchungaji Christopher Mtikila na John Chipaka ambaye ni Mwenyekiti wa Chama cha Tadea.

Bunge hilo litajumuisha wabunge wote 357 wa Bunge la Jamhuri ya Muungano, wajumbe 82 wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar pamoja na 201 waliotangazwa jana na kufanya idadi yao kuwa 640.

Akitaja majina hayo jana Kaimu Katibu Mkuu Kiongozi, Dk Florens Turuka alisema wajumbe hao wameteuliwa kutoka katika makundi 10 ya kijamii.

Aliyataja makundi hayo na idadi ya walioteuliwa katika mabano kuwa ni Taasisi zisizo za Kiserikali (20), Taasisi za Dini (20), Vyama vya Siasa (42), Taasisi za Elimu (20), Makundi ya Walemavu (20), Vyama vya Wafanyakazi (19), Vyama vya Wafugaji (10), Vyama vya Wavuvi (10), Vyama vya Wakulima (20) na Makundi yenye Malengo yanayofanana (20).

“Taasisi 554 kutoka Tanzania Bara na 178 kutoka Zanzibar ziliwasilisha mapendekezo yao yaliyojumuisha majina 2,762 kwa upande wa Bara na upande wa Zanzibar yalihusisha watu 874,” alisema na kuongeza:

“Majina yote yalikuwa 3,636, lakini kinyume na sheria watu 118 walipendekeza wenyewe na kufanya idadi ya majina yaliyopendekezwa kuwa 3,754. Taasisi hizo zilileta majina mengi na kazi ya kuyachuja mpaka kubaki 201 ilikuwa ngumu,” alisema Turuka.

Alisema uteuzi huo umezingatia umri wa waombaji na kwamba wenye umri kuanzia miaka 22 hadi 35 wapo 35, wenye umri wa miaka 36 hadi 60 ni 145 na kuanzia miaka 65 na kuendelea wapo 21.

“Wameteuliwa kwa kuangalia umri, jinsi, uzoefu, sifa na mahali anapotoka mjumbe husika. Wanawake wapo 100 na wanaume wapo 101, wajumbe waliotokea Zanzibar ni 67 na waliotokea Tanzania Bara ni 134,” alisema.

Alisema katika kila kundi wajumbe kutoka Tanzania Bara wapo theluthi mbili na wale kutoka Zanzibar theluthi moja.

RAISI UHURU KENYATTA WA KENYA AWASHANGAZA WENGI BAADA YA KUTEMBEA MJINI BILA MSAFARA WA WAWALINZI

$
0
0
Hii imetokea kwenye mji mkuu ambao ni Nairobi pale Rais Uhuru Kenyatta alipotumia gari moja tu bila msafara akitokea Ikulu kwenda kwenye hoteli moja kwa ajili ya kukutana  na Wanafamilia.
Unaambiwa toka amechukua madaraka, Rais Uhuru amekua na tabia hii mara kwa mara tofauti na Rais Kibaki ambae kila sehemu aliyotia mguu ni lazima aambatane na msafara hata kama ni maeneo ya karibu na Ikulu.
Askari mmoja wa usalama barabarani alipigwa butwaa pale alipojikuta kasimamisha gari ambalo ndani yupo Rais Uhuru bila msafara ambapo President mwenyewe alimwambia >>> “Ni mimi ofisa, fungua”. akimaanisha ni yeye amfungulie njia aendelee na safari.
Askari wa Usalama barabarani nchini Kenya wanasifia uongozi wa Rais Uhuru kwamba hata kukiwa na msafara huwa hawawekwi barabarani kwa muda mrefu kuusubiria upite manake wakati wa Mwai Kibaki ilikua inawalazimu wakae barabarani kwa saa kadhaa kabla ya msafara kupita.

MAONI:MCHEZA MPIRA CHUJI ANAFAA KUWA MFANO WA KUIGWA

$
0
0
KWA kipindi kirefu sasa kiungo nyota wa Yanga, Athuman Idd maarufu ‘Chuji’ amekuwa katika matatizo yatokanayo na utovu wa nidhamu.

Hali imekuwa hivyo katika klabu yake pamoja na timu ya Taifa. Suala la nidhamu limekuwa likimuweka pabaya.

Katika miaka ile akiwa na tatizo Taifa Stars chini ya kocha Marcio Maximo wengi waliona kwamba uchanga wake nao ulichangia kuwapo matatizo hayo hivyo wakati wote kilichozungumzwa na kwamba anahitaji nafasi.

Wako ambao walimlaumu Maximo na kuona kwamba hakuwa sahihi kwa jinsi alivyoyasimamia matatizo ya Chuji.

Pamoja na yote ambayo Chuji amekuwa akikutana nayo bado nafasi yake katika klabu na hata Taifa Stars ni kubwa, makocha wanamhitaji, wachezaji wenzake wanamhitaji na mashabiki wanamkubali.

Yote hiyo ni kutokana na kipaji chake na uwezo wake wa kufanya kazi uwanjani kwa ufanisi jambo ambalo baadhi ya wachezaji limekuwa likiwashinda. 

Hata hivyo tunadhani kwamba huu ni wakati sahihi kwa Chuji kufahamu kwamba imetosha na badala yake mashabiki watapenda kumuona akifanya mambo uwanjani tu na si vinginevyo.

Mashabiki hawatopenda kusikia habari za Chuji kusimamishwa kwa mambo ambayo kwa uzoefu alionayo haipendezi kuyafanya.

Matatizo yote yahusuyo nidhamu na mengineyo yamewachosha mashabiki na kwa muda ambao amekuwa katika soka ni wazi kwamba anatakiwa kubadilika, anatakiwa kuwa msaada kwa wachezaji chipukizi.

Tumekuwa tukishuhudia mara kadhaa wachezaji kukerwa mara wanapotolewa na makocha wao kabla ya dakika 90 za mchezo kumalizika.

Hili ni jambo la kawaida, si kwa wachezaji wa Bongo tu bali hata wale wanaocheza soka Ulaya kama kuna jambo hawalipendi basi ni kutolewa kabla ya muda.

Hata hivyo pamoja na kutolipenda jambo hilo lakini wachezaji hao wanafahamu ukweli kwamba wanatakiwa kwenda kwenye benchi kuungana na wenzao na si kwenda sehemu nyingine.

Mchezaji ambaye anatolewa kabla ya wakati na hapaswi kwenda kwenye benchi ni yule ambaye anapewa kadi nyekundu.

Hili tunaamini Chuji alilifahamu na hivyo tulishangaa kulikoni alipotolewa katika mechi ya Mtani Jembe kati ya Yanga na Simba akaacha kwenda kwenye benchi la Yanga kama utaratibu unavyotaka.

Ni vyema Chuji akatambua kwamba kinachomlinda sasa katika Yanga na hata Tafa Stars ni kipaji chake, kipaji ndicho kinachowafanya makocha wamhitaji na mashabiki wamhitaji na kumuunga mkono.

Hatuoni ni kwa nini anawaangusha makocha na mashabiki hawa kwa mambo ambayo yeye mwenyewe anayafahamu, Chuji anafahamu utaratibu wa mchezaji pindi anapotolewa na kocha wake.

Kutolewa na kocha na kutokwenda katika benchi si jambo zuri hata kidogo, ni kumdharau kocha na wachezaji wenzako ambao kwa kawaida wanapotolewa pamoja na hasira lakini wanajumuika na wenzao katika benchi.

Tunafahamu kwamba Chuji ni mzoefu na anazijua taratibu hizi na ndio maana tunashangaa ni kwa nini aliamua kuzipuuza kwa makusudi.

Kwa mantiki hiyo tunapenda kumkumbusha Chuji kwamba huu ni wakati wake wa kuwa mfano wa kuigwa katika klabu ya Yanga na hata Taifa Stars.

Bado anayo nafasi na ni vyema akaitumia nafasi hiyo kwa mambo yatakayomfanya akumbukwe vizuri.

MALINZI:TUMERITHI ZIGO LA MADENI TOKA KWA TENGA

$
0
0
SHIRIKISHO la Soka Tanzania (TFF), limesema changamoto kubwa linaloikabili sasa ni madeni ya mamilioni ya fedha waliyoyarithi kutoka uongozi uliopita wa Rais, Leodegar Tenga.

Akizungumza na Mwanaspoti katika tathimini yake ya siku 100 tangu alipochaguliwa kuwa rais mpya wa shirikisho hilo, Jamal Malinzi, alisema madeni hayo ni makubwa ukilinganisha na kipato cha TFF kinachotegemea zaidi mapato ya milangoni ya mechi mbalimbali.

“Madeni tuliyoyakuta ni makubwa, lakini mengine tumegundua ni hewa, hivyo yanafanyiwa uhakiki ili tujue madeni halisi ili tuweze kuyalipa,” alisema Malinzi aliyeingia madarakani Oktoba 27, mwaka jana.

“Pia tunafanya mazungumzo na watu wanaoidai TFF ili watupe masharti nafuu ya kulipa madeni hayo.”

Kauli ya Malinzi imekuja ikiwa imepita miezi sita tangu TFF ipate aibu ya mabasi yake kukamatwa na Kampuni ya Udalali ya Flamingo ili kufidia deni la zaidi ya Sh50 milioni.

USHOGA WA DK.CHENI HUU HAPA FILAMU YAKE YAZUIWA

$
0
0
Stori: Brighton Masalu
SIKU chache baada ya Bodi ya Filamu Tanzania (TFB) kuzuia filamu ya mkongwe katika sinema za Kibongo, Mahsein Awadh Said ‘Dk. Cheni’ ijulikanayo kwa jina la Nimekubali isiingie sokoni kwa madai kuwa imekiuka maadili ya Kitanzania, msanii huyo ameibuka na kueleza kinagaubaga, Risasi Jumamosi limenasa sauti yake.

Akizungumza na mwandishi wetu Jumatano ya wiki hii maeneo ya Mlimani City jijini Dar, msanii huyo alisema amesikitishwa na maamuzi ya bodi hiyo huku akidai kuwa lengo la filamu hiyo ni kukemea tabia za kishoga zinazoendelea kuibuka kwa vijana ikiwa ni pamoja na kupinga uhalali wa ndoa za jinsia moja

Katika maelezo hayo, DK. Cheni ambaye huzitendea haki filamu zake kwa kuvaa uhusika halisi, alisema moja ya kigezo ambacho bodi hiyo imekitumia kuzuia filamu hiyo ni pamoja na muonekano wa bango la filamu hiyo ambalo linamuonesha msanii huyo akiwa amevaa vazi la shera huku akiwa amejiremba kwa madai kuwa ni kuchochea ushoga jambo ambalo msanii huyo amelipinga vibaya.

“Eti ushoga wangu uko kwenye kujiremba sana, hakika wamenionea sana, lengo letu ni kuonya na kukemea vikali vitendo vya ushoga na ndoa za jinsia moja, huwezi kuelimisha bila kuonesha madhara yake kwa vitendo kama ilivyo ndani ya filamu hiyo.

“Lakini, ndani ya filamu hiyo, kuna kipande ambacho kinaonesha kiongozi wa serikali akikemea kitendo hicho, sasa hapo ushoga wangu uko wapi? Kuvalia shera kwenye kava? Siyo sahihi,” alisema Dk. Cheni.
Mbali na kava hilo, msanii huyo alidai haoni kosa lolote katika filamu hiyo hivyo ataendelea kupigania haki yake na kwamba hayuko tayari kuonewa.

Jitihada za kumpa mkurugenzi wa bodi ya filamu,  Joyce Fissoo ili kuelezea juu ya sekeseke hilo, ziligonga mwamba hadi gazeti hili linaingia mtamboni lakini imedaiwa kuwa bodi hiyo itasimamia msimamo wake.
Source:Global Publishers

NCHI HII INAPOTEZA MWELEKEO WASOMI MKO WAPI?

$
0
0
Ni ukweli usiopingika nchi hii inapoteza uelekeo tofauti na miaka ya 60. Miaka ya 60 hatukuwa na wasomi wengi sana kama maprofesa, madoctor, masters, na bachelors ukilinganisha na ilivyo sasa, chakushangaza nchi ndio inazidi kutumbukia kwenye kila aina ya uovu, na kwa bahati mbaya hakuna hata anayefanya utafiti na kujua tatito ninini.

Miaka ya 60 ilikuwa nafuu kulikuwa na uadilifu tofauti na ilivyo sasa, hivi sasa watoto wanazaliwa wanaanza elimu ya msingi mpaka kufikia vyuo vikuu wakiona wizi, chuki, uongo, fitna.... nikitu cha kawaida tofauti na miaka ya 60. Ukosefu wa uadilifu umefanya ongezeko la wahuni mtaani, mpaka kufikia hatua mtu anashindwa kutofautisha msomi na asiye msomi.

kwa bahati mbaya wahuni hao wanaanza kuingilia polepole sector nyeti ya siasa hapa nchini.

Kila anayelala na kuamka anakwambia namimi nataka kugombea ubunge, matokeo yake tunakuja kupata wahuni wa kisiasa kazi kurushiana matusi majukwani mfano halisi ni mh. Lusinde alipokuwa kwenye kampeni huko Arusha. Pia matokeo yake utakuja kuona wahuni wa kisiasa walivyotaka kuivuruga chadema na kuitana wasaliti huku wakipandikiza chuki kwa wanchi huku sisi tunabaki tunashabikia tukiwapoteza watu muhimu katika ukombozi kwa walio masikini.

Hivi sasa msema kweli ndiye muongo na msema uongo ndiye mkweli.Niseme kwamba chadema ni chama makini sana ila kikihendekeza wahuni wanashinda humu Jf wakipandikiza chuki ndani ya jamii kitapoteza uelekeo.

Umuhimu wa kuwasomesha wanafunzi huku hatuoni faida yao uko wapi? Wengi wanaishia kuwa wanywa pombe, na watu wa vijiweni. Kila aina ya raslimali tunazo wameshindwa hata kutupatia elimu zao tukazalishe, wamesubili ajira wakale rushwa au nao kutamani ubunge wakawe wezi na kupata kiinua mgongo.
By  mayange from JF

WADAU HIVI HILI KWELI LINAWEZEKANA AMA NIMEINGIA CHAKA KWA BINTI HUYU?

$
0
0
Leo nimekutana na kali ya kufungua mwaka. Kwa muda mrefu tu tumekuwa tukiwasiliana na kuchat kiasi cha kuzoeana na msichana fulani hivi lakini hatukuwahi kuonana. Sasa tukapanga tuonane siku ya leo. Nikamshtua mtrotro mapema leo, nikamwambia aje pande za huku kwetu. Mida ya flani jioni nikawasili maeneo ya kituoni hapa, nikamkuta ananisubiri. Kumuona mtrotro mashallah.. Kiukweli mimi sijajaliwa sura yenye mvuto na kimuonekano pia ni wa kawaida tu. Nikaenda nae maeneo tukapiga story 2.. 3.. Then nikamuingiza majaribuni, nikamuomba tuzini. Cha kushangaza akakubali wakati ndo kwanza tumeonana leo. Nikajilia vyangu kiulainiii, nikamsindikiza. Nikarudi home na viulizo..!! Huyu binti yuko sawa kweli au ndo wale wa buguruni..!!? Au ni kawaida tu, kwamba inawezekana sex at first sight.

DIAMOND SI MCHAWI..BALI ANA JITAMBUA NA ANA WASHAURI WAZURI

$
0
0
Msanii nguli  katika kuiga sauti za watu maarufu  MC Babu Ayoub aliyewahi kutamba na wimbo wa chaja ya kobe ameibuka na kusema mkali wa ngololo Diamond si mchawi.
Mkali huyu wa kibao cha chaja ya kobe  ambaye pia aliwahi kushiriki katika wimbo wa ndiyo mzee wa Prof.J alifunguka mbele ya mwandishi wetu.

ALisema “Diamond si mchawi ila anajithamini kama msanii,anajua umuhimu wake anajitambua na hata kama hajitambui basi anawashauri wazuri kwa maana ya menejiment.anajituma kwani anajua kucheza na muda na yuko kibiashara zaidi si kama wasanii wengine waliowahi kuhit,jamaa najua pia kucheza na media ,ukimpa nafasi hafanyi makosa.Aidha msanii huyu anayetegemea kuja na kibao chake kipya amedai msanii Diamond ana haki ya kuwa hapo alipo lakini pia itakuwa ni fundisho kwa wasanii wengine waliohiti na watakaohit.
Viewing all 104663 articles
Browse latest View live




Latest Images