Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104429 articles
Browse latest View live

Diamond Beats Wizkid, Patoranking And Tiwa Savage To Win Best African Act Ugandan Entertainment Awards.

0
0
Diamond Platnumz has just won best African act award at the recently concluded Ugandan Entertainment Awards 2015, The superstar beat Wizkid,Tiwa Savage and Patoranking to win the award...


"My People!!! Jus Wanna thank you for your Vote and let you know that have won the BEST AFRICAN ACT OF THE YEAR on@uganda_entertainment_awards ... S/O to my bro @tommyleeafrica for representing me and the whole@wcb_wasafi ... Lastly wanna thank@uganda_entertainment_awards for recognize my Efforts...please keep VOTE for me on other Awards"




Edward Lowassa Leo Kufunga Bara Bara za Dar Kwa Mafuriko...Kufanya Mikutano Miwili Kwa Mpigo Leo

0
0
Zamu ya Jiji la Dar Leo ..Soma Hapa Ujumbe alioandika LowassaKuhusu Kampeni zake Jiji Dar es Salaam


CCM Wako Bize Wanamsema Lowassa Badala ya Kuwaambia Wananchi ni Lini Watawaondoa Katika Maisha ya Ufukara

0
0
Nilidhani watanzania (wapiga kura) walitaka kusikia zaidi ni kwanini wao ni masikini ilhali nchi hii ina rasilimali za kuwafanya waishi maisha bora. Serikali ya awamu ya 4 ilikuja na slogan "Maisha bora kwa kila mtanzania". Katika ziara za wagombea urais Nchi imezungukwa na nyumba nyingi za nyasi yani kwa kifupi bora hata yale mahema ya muda ya wakimbizi. Unawasikia mapambe wa mgombea urais wa CCM wako bize wanamsema ENL badala ya kuwaambia wananchi ni lini watawaondoa katika maisha ya ufukara. Ni ajabu sana kuanzia rais wa awamu ya 4, wapambe kasoro mgombea urais wote hofu yao ENL wakati wao ndio walio madarakani na wanaweza pia kutumia sheria zilizopo kutaifisha wanachohisi si halali yake. Iweje washindwe leo aweze wa awamu ya 5? Iweje Chama hicho hicho kijinandi kitaweza na akijaweza kupambana na mafisadi? 

Iweje Chama hicho hicho kinajinadi kitageuza uchumi wa nchi hii kuwa wa viwanda wakati kilimo kwanza kimeshindikana?(yaani uchumi wa raw materials), iweje Wanachama hao hao waendelee kupiga kelele wakiwatolea wapinzani kashfa wakati wao ndiyo wazazi wa mafisadi? Inaniwia vigumu kuielewa CCM na viongozi wake na pengine kukiamini chama hicho kwani ni chama kinachowataka watanzania kuwa watu fukara hata baada ya miaka 53 ya unyonyaji wa haki, kodi na mali zao. Wameshindwa kabisa kueleza ni vipi watatuondolea umasikini. Badala yake wanatoa majibu mepesi ya tutatoa elimu bure mpaka form 4, tutatoa milioni 50 kwa kila kijiji (Tafakari kijiji kina watu 15,000 ina maana mtauondoa umasikini kwa kila mmoja kupata shilingi 3,333/-? acheni masihara. ## Tafakari chukua hatua##

By Philip Mlay

Mke Acharuka na Kusema ..Jack Wolper Niachie Mume Wangu ..

0
0
Chanzo makini kimelieleza Ijumaa Wikienda kwamba, baada ya habari na picha za Wolper na Mkongomani huyo kuripotiwa na gazeti ndugu na hili, Risasi Jumamosi, mke wa ndoa wa mwanaume huyo alijitokeza na kuvunja ukimya akimtaka mwigizaji huyo aachane na mumewe huyo mara moja kabla hajamchukulia hatua za kisheria kwa sababu ameingilia ndoa yake.

“Unajua baada ya ninyi (Global) kuanika picha za Wolper kwenye gazeti na mitandao mbalimbali ya kijamii akivishwa pete ya uchumba na Mkongomani, mke wake ameshindwa kuvumilia hivyo amelazimika kumtumia ujumbe Wolper akimtaka aachane na mume wake  kwani kama alikuwa hana taarifa kuanzia leo (Jumamosi) atambue kwamba huyo mwanaume ni mume halali wa mtu na ana watoto ndani ya ndoa.

“Yaani mke wa Mkongomani amemjia juu Wolper akimtaka amwachie mumewe, ajiweke pembeni mara moja na kama alidanganywa kuwa huyo mwanaume hajaoa, basi atambue kwamba tayari alishafunga naye pingu za maisha, tena kanisani na tayari ana familia ya watoto wawili, haoni sababu ya kumnyamazia maana ameumia sana hivyo anamtahadharisha ili baadaye asije akaanza kulia akisema hajaambiwa,” kilisema chanzo hicho.

MSIKIE WOLPER

Ili kuweka mzani wa habari hiyo, Ijumaa Wikienda lilimtafuta Wolper ili kujua kama ameshayapata malalamiko hayo ambapo alifunguka kuwa, kuna maneno mengi yanazungumzwa juu ya tukio hilo lakini ukweli wa mambo zaidi anaufahamu yeye na mchumba’ke huyo hivyo haoni sababu ya kumwambia kila mtu maana mpaka anafikia uamuzi wa kuvishwa pete tayari walishajadiliana vya kutosha.

“Naweza kusema kwamba ni moja ya historia katika maisha ya mchumba wangu hivyo hata nilipoona hizo picha za mkewe hakuna jambo lililonishtusha kwani tayari alikuwa ameshaniambia juu ya misukosuko aliyoipitia kwenye ndoa yake huko nyuma.

“Hadi anafikia hatua ya kunivisha pete basi watu wanatakiwa kujua tu kwamba kila jambo liko sawa na zaidi wao wanatakiwa kusubiri hadi siku ya ndoa yetu waone kama itafungwa au lah.

“Siku hizi dunia imekuwa kama kijiji hivyo huwezi kuwazuia watu kuongea jambo, mchumba wangu ananijua na mimi ninamjua kwa kina, pamoja na kwamba watu pia wamekuwa wakimletea maneno kuhusu mimi lakini nimemwambia aachane nao kwani hakuna sababu ya kujibizana nao, kwa sababu kila mtu ana uhuru wa kutumia kinywa chake jinsi anavyoweza maana ningekuwa sijui background (maisha ya nyuma) yake kweli baada ya kuona hizo picha za mkewe na maneno ya watu wanayosema ingeniuma sana.

“Nafikiri watu wanachotakiwa kujua juu yetu ni kwamba Mungu akishapanga jambo kamwe binadamu hawezi kulipangua hata iweje na kwa maana hiyo sasa hata mwanaume akishakupenda ni ngumu kumsikiliza mtu mwingine maana upendo wa mtu ni moyo na nafsi yake mwenyewe ndiyo inayoweza kumuongoza kwa kila hali.

“Watu wameshafanya kila juhudi za kutugombanisha lakini sasa ameshazoea hadi anavichukulia kama burudani tu, hata mimi haya ninayaona kama matangazo ya biashara hivyo hakuna linaloniumiza kichwa,” alisema Wolper.

ETI ANA GUNDU?

Kutokana na kitendo hicho wadau mbalimbali walifika mbali na kudai kwamba mwanadada huyo inawezekana ana gundu kwani ameshakuwa na wanaume tofauti na wengine kumvisha pete ya uchumnba na kutambulishana kwa wazazi lakini ikawa ndivyo sivyo.

“Wolper anatakiwa kujiangalia sana na kumuomba Mungu kwani siyo mara ya kwanza kuwa na wanaume wa watu, kinachowaponza hawa mastaa wetu wana tamaa sana ya fedha ambazo huwasababisha kuwa na mtu kwenye uhusiano bila kumchunguza vizuri,” alisema mdau mmoja mkazi wa Mwenge, Dar.

TUJIKUMBUSHE

Kwa Wolper, kuvishwa pete ya uchumba siyo mara ya kwanza kwani awali aliwahi kuvishwa na aliyekuwa mpenzi wake, Abdallah Mtoro ‘Dallas’ lakini hawakufikia hatua ya kufunga ndoa wakaachana solemba.

Watu Wawili Wafa Kwenye Mkanyagano Mkutano wa Magufuli Morogoro

0
0

Watu wawili wamepoteza maisha na wengine kujeruhiwa kutokana na mkanyagano uliotokea jana Uwanja wa Jamhuri, Morogoro katika mkutano wa kampeni za mgombea urais wa CCM, Dk John Magufuli.

Tayari leo, Mwenyekiti wa CCM taifa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jakaya Kikwete amewatembelea majeruhi hao waliolazwa Hospitali ya Mkoa Morogoro.

Mganga Mkuu wa Hospitali hiyo, Dk Ritha Lyamuya amesema walipokea watu 19 waliokuwa na majeraha yakiwemo ya kuvunjika maeneo mbalimbali ya mwili na kuongeza kuwa miongoni mwao, wawili walikufa kutokana na kuumia vibaya.

Aidha Dk Lyamuya alisema kuwa wagonjwa ambao bado wamelazwa wako 10 na wengine saba walitibiwa na kuruhusiwa.

Dk Lyamuya alisema kuwa waliokufa ni pamoja na mwanamke anayekadiriwa kuwa na umri wa miaka 42 na mtoto wa umri wa miaka 12 aliyejulikana kwa jina la Ramadhan Abdalah.

Uwanja wa Jamhuri jana ulifurika watu wakati mgombea urais kwa tiketi ya CCM John Magufuli alipokwenda kwa ajili ya kufanya kampeni.

Mara tu baada ya Magufuli na viongozi wengine kuondoka uwanjani hapo, ndipo hali ya kusukumana na kukanyagana ilitokea getini wakati watu wakitoka.

Siku Lowassa Akiamua Kufungua Mdomo Kuhusu Ricmond Nchi itatetemeka

0
0
Wanasema usimrushie mawe mwenzio wakati unaishi nyumba ya vioo, wanadhani Lowassa hawezi kusema anayojua kuhusu Richmond wanajidanganya.

Inasemekana washauri wake wamemwambia akae kimya kwanza muda ukifika atasema na siku hiyo kuna watu watakuwa kama wamevuliwa nguo ila waswahili wanasema muungwana akivuliwa nguo huchutama.

'We Would Rather Vote For A Stone Rather Than CCM Which Has Since Independence Been Falling Us' Karatu Residents

0
0
Karatu. Karatu residents said attacks their one-time MP, Dr Willibrod Slaa, directs to Chadema’s presidential candidate, Mr Edward Lowassa, will not change their resolve to see the ruling CCM voted out in the forthcoming General Election.


Dr Slaa served as Karatu MP for 15 years since 1995 and Chadema secretary general before he announced recently he was quitting politics to protest the move by his party to embrace Mr Lowassa, the man he had for many years branded the kingpin of corruption.

He has also terrmed Mr Lowassa a liability to the opposition. Dr Slaa has made a name as a firm anti-corruption crusader and won the hearts of many people in Karatu where he comes from.

But some Karatu residents told ‘The Citizen’ in separate interviews on Saturday that Dr Slaa’s allegations would not change their resolve to see the country’s leadership overhauled.

A Rhotia Ward resident, Isack Philip said the determination of all Karatu residents was to see CCM is ejected and nothing will change their stance. “We would better have a couple of corrupt leaders in the Opposition rather than the over 100 ones CCM is still embracing,” he said.

Another resident, Mr Samaytu Ephraim, said Dr Slaa, who was eyeing the presidency on the Chadema ticket, was being troubled by envy.

A bodaboda roperator, Mr Emmanuel Bayo said Karatu residents will not buy Dr Slaa’s “misplaced allegations” against their leaders. “We would rather vote for a stone rather than CCM which has since independence been failing us,” he said, stressing that whoever is vying for Karatu seat on the coalition’s ticket will win.

Former CCM chairman Herman Daffo, however, defended Dr Slaa, saying he deserved praise for using constitutional right to express his views and enlightening fellow Tanzanians.
Source:Citizen


Aunty Ezekiel Amkingia Kifua Iyobo Kuhusu Kumzidi Umri

0
0
KUFUATIA kuwepo kwa madai na minong’ono mingi ya msanii wa filamu Bongo, Aunt Ezekiel kumzidi umri mzazi mwenzake, Moses Iyobo, muigizaji huyo ‘amewaka’ na kuwataka watu wasiingilie uhusiano wao na kwamba suala la umri kwao ni namba tu.

‘Akibananishwa ukutani’ na mwandishi wetu kwa maswali magumu hivi karibuni, Aunt alisema amekuwa akiumizwa na maneno yanayoendelea juu ya kumzidi umri Iyobo, na kusema hayuko tayari kuona uhusiano huo ukivunjwa kwa maneno ya aliowaita “wakosa kazi”.

“Kwani wakati tunatongozana hatukujua kuwa tunazidiana umri? Mbona watu wanashindwa kufanya mambo ya msingi na kukalia majungu? Kwetu sisi suala la umri ni namba tu, labda nikuulize, ulishaona mtoto anambebesha mwanamke mimba? Maneno ya mimi kumzidi umri Iyobo yananiumiza sana kwa kweli, lakini nitaulinda uhusiano huu hadi mwisho,” alisema Aunt Ezekiel

Chanzo: GPL

Zari is in South Africa…..She Shares These Photos With Her All 4 children

0
0
Raphael_rich21...so calm and collected. He ma main soldier



And finally with ma Manchester soccer academy player @pinto_bitw. The most shy person ive ever known, very humble and very smart. Mummy is very short soon y'all be looking in ma head...... where ma high heels at???

SUMAYE: Walioficha fedha nje watazirudisha; Magufuli haiingii Ikulu 2015

0
0
Fredrick Sumaye
Waziri Mkuu mstaafu, Fredrick Sumaye,   amesema kama Lowassa atafanikiwa kuingia madarakani Watanzania walioficha fedha nje ya nchi watazirudisha.Sumaye alitoa kauli  hiyo jana alipohutubia mkutano wa kampeni katika Uwanja wa Laini Polisi mjini Nzega, Mkoa wa Tabora.

Kwa mujibu wa Sumaye, fedha hizo ambazo Serikali ya CCM imeshindwa kuzirudisha zitatakiwa kurudi kwa sababu ni mali ya Watanzania.

“Jana (juzi) mmemsikia Magufuli (Mgombea urais wa CCM, Dk. John Magufuli), akisema atakapoingia madarakani atarudisha mashamba ya wananchi yaliyoporwa.

“Kwanza kabisa namwambia Magufuli kwamba Ikulu haingii, lakini sisi tutakapoingia madarakani  tutahakikisha walioiba fedha za Watanzania na kuzificha huko Ulaya au Uswisi wanazirudisha,” alisema Sumaye.

Sumaye pia alizungumzia suala la rushwa nchini na kusema kama CCM wangekuwa waungwana wasingemsimamisha mtu yeyote kugombea urais kwa sababu wameshindwa kuwaletea maisha bora Watanzania.

“Magufuli anasema akiingia madarakani atakomesha rushwa sasa kama ana uwezo huo kwa nini ameshindwa kuikomesha wakati na yeye ni waziri katika Serikali iliyokithiri kwa rushwa?

“Magufuli anasema akiingia madarakani atakuza uchumi, kama kweli ana uwezo wa kukuza uchumi kwa nini ameshindwa kuukuza kupitia Serikali ya CCM ambayo yeye ni waziri?

“Magufuli hana lolote, msimchague kwa sababu ameshiriki kununua feri mbovu inayotoka Bagamoyo  kwenda Dar es Salaam,” alisema Sumaye.

Katika maelezo yake, Sumaye alizungumzia pia taarifa za viongozi wa CCM wanaodaiwa kuwatisha wananchi wasimchague Lowassa kwa kisingizio kwamba nchi itaingia katika vita kama ilivyotokea Libya na katika nchi nyingine za Afrika Kaskazini.

Sumaye alisema hakuna vita itakayotokea  wapinzani watakapoingia madarakani na kwamba vita hiyo itatokea kama Serikali ya CCM haitataka kuondoka madarakani.

MBOWE: Ulofa na Upumbavu Wetu ni Kwa Sababu ya CCM

0
0
Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe
Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe, amesema ili umasikini unaowakabili Watanzania uweze kuondoka lazima washirikiane kuiondoa madarakani CCM.

Amesema ulofa na upumbavu wanaodaiwa kuwa nao Watanzania umesababishwa na Serikali ya CCM kwa kuwa haiwajali Watanzania.

Mbowe  alitoa kauli  hiyo jana alipohutubia mkutano wa kampeni katika Uwanja wa Laini Polisi mjini Nzega, Mkoa wa Tabora  ambapo  pia alilazimika kuwapigisha kura za mikono wananchi wa Nzega waliohudhuria mkutano huo ili kutatua mvutano wa wagombea wa ubunge katika Jimbo la Nzega Mjini lililokuwa na wagombea wawili wa Ukawa.

Wakati wa kura hizo, mgombea wa Chadema, Charles Mabura, aliibuka mshindi dhidi ya mgombea wa Chama cha Wananchi (CUF), Meza John.

Mgombea wa Ukawa alieteuliwa kuwania Ubunge wa Jimbo la Nzega Mjini kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Charles Mabula (kulia) akipeana mkono na aliekuwa Mgombea wa nafasi hiyo kwa Jimbo la Nzega mjini, Mezza Leonard (kati) akiekubali kushindwa baada ya kupigwa kura ya wazi na wananchi wa Nzega Mjini, jana Septemba 6, 2015.Kushoto ni Mwenyekiti wa CHADEMA, Mh. Freeman Mbowe.

SHOCK! House help caught using her URINE to cook for her employers (See PHOTOs)

0
0
The house help in the photos below was caught with urine that she had stored and which she uses to cook food for her employer.

The bottles of urine were found in one of the cabinets in the kitchen and her employer says that she confessed that she uses it to cook for them

Check this out;


Kwaheri Dr Slaa Huwaminiki Tena Mzee...Hatujui Kesho Tena Utasema Nini, Utakuwa Wapi na Nani

0
0
Dr Slaa
 Sisi wote ni wanafunzi na wahanga wa Dr. Slaa kifikra na kisiasa. Dr. Slaa umetufundisha watanzania wote kuwa CCM haifai na ndio chanzo cha ufisadi, ubadhilifu, wizi, matumizi mabaya na sera mbaya zisizotekelezaka na zilizosababisha maisha ya watanzania kuwa mabaya. Ukiwa na wenzako wa chadema kwa kutumia kampeni za sangara, M4C, redio na tv, ulitufundisha kuikataa CCM na tulikuelewa vizuri, tuliamini na tukafanya hivyo kwa moyo, kwa nguvu na kwa akili zetu zote. Wewe ndiye uliyesababisha taifa lote liichukie na kuikataa CCM kwa moyo na nguvu zote, watu wameshalielewa somo lako kuhusu ubaya wa CCM kwetu. Ulitufungua akili tuliokuwa hatujui siasa za chama cha CCM. Tulifanya hivyo kwakuamini kwamba wewe ni msomi mzuri na mtumishi wa Mungu husemi uongo na utakuwa umefanya utafiti mzuri kuhusu uhusiano uliyopo kati ya maisha ya watanzania na sera, utekelezaji wa sera na utawala wa CCM. Uliamsha hamasa na ari ya watanzania katika siasa na kufikiri juu ya maisha yao. Sasa tumeelimika sana kupitia wewe na wenzako wa chadema kuhusu ubaya wa CCM kwetu na kwa taifa, watu hawataki tena kusikia habari za CCM mitaani na maofisini. Ahsante sana baba!

Sasa wafuasi wako tumeanza kushikwa na butwaa kubwa kukuona wewe tena unakipigia debe CCM kiendelee kubakia madarakani!!!!@***&.com???. Hapa kuna mawili, ama wewe unataka kutugeuza sisi kichwa chini miguu juu, au wewe ndo umegeuka mwenyewe kichwa chini miguu juu. Tunajiuliza nini kimetokea kwa mwalimu wetu Dr. Slaa hadi kufanya hivi? Kama shida ni Lowassa kuhamia chadema basi hata wewe hukupaswa kuwa na uhalali wa kukilaumu CCM kwa ufisadi, ubadhilifu na huduma mbovu kwa wananchi, badala yake ulipaswa kuwalaumu viongozi waliotokana na CCM tu peke yake wasiofanya vizuri na sio chama chote cha CCM kuwa hakifai. Vinginevyo wewe ulikuwa katibu mkuu wa chadema hivyo ungeweza kuhakikisha kuwa rais (Lowassa) anayetokana na chama cha chadema angeongoza nchi kwa mujibu wa kanuni, taratibu na maadili ya chadema tu basi. Hivyo ukiwa kama katibu mkuu wa chadema hukuwa na sababu za msingi za kumuogopa Lowassa 'fisadi' kuhamia chadema au kugombea urais kupitia chadema maana chama chini ya katibu mkuu (wewe) kingemnyoosha na kumfanya kuongoza nchi kwa mujibu wa chadema. Kama hili limeshindikana kwako na kwa chadema kwanini ulitaka hili liwezekane kwa CCM? Ulikuwa unatudanganya kuhusu ubaya wa CCM? Ulipaswa kuwalaumu viongozi na watendaji wabaya wa CCM na sio chama cha CCM chote kama chama. Unapaswa kuwaomba samahani CCM hadharani kwa kukisema chama chao vibaya badala ya kumsema mwanachama/kiongozi wa CCM ambaye ni mwizi, mbadhilifu, fisadi, n.k, pili, uwaombe radhi watanzania kwa kuwapotosha kuhusu ubaya wa CCM kama chama.

Kama wewe ukishindwa kuyafanya haya yote mawili kwapamoja taifa hili litakuwa juu ya kichwa chako kwa kuliyumbisha na kutaka kulipasua vipande. CCM wanafunzi wako tunakuona kama mwalimu usiyekuwa na msimamo, uliyehongwa, mwenye ubinafsi wa kuwa rais kwa gharama yoyote, unayependa porojo, usiyependa maamuzi ya pamoja ndani ya chama, mpotoshaji, muongo, usiyejali wafuasi na familia yako, na usiyefaa kusikilizwa tena na watu wenye shida za maisha kama sisi. Hatujui kesho tena utasema nini, utakuwa wapi na nani. Kwaheri huwaminiki mzee!!!

By Kavulata-JF

Mwaka Huu Nimewajua Wasanii Waliokuwa na Akili na Wasiokuwa na Akili-Ray

0
0
"(FREEDOM OF SPEECH)
Kuna vitu vingi sana nimegunduakwenye uchaguzi wa mwaka huu nimewajua baadhi ya wasanii waliokuwa na akili na wasiokuwa na akili japokuwa nami nawezakuwa mmoja wapo katika hao wasiokuwa na akili. Why nasema hivi na samahani kama nitakuwa nime2mia lugha kali, Unajua nashanga sana sasa hivi kumekuwa na vita baina ya wasanii wanaosapoti (CCM) Na (UKAWA)

Jamani siasa ni democracy kila m2 ana haki yakuwa upande anayeuona yeye unamfaa. Mimi nilidhani badala ya kuwa na tofauti nilitegemea kuwa 2ngekaa pamoja nakujua madhaifu ya chama na chama gani kitatufaa ili kiweze kutusaidia maslahi ye2 pamoja na maslahi ya wananchi wanaoishi maisha ya tabu kwenye nchi yenye kila aina ya utajiri badala yake 2napambana wenyewe kwa wenyewe. Jamani wasanii mmesahau shida zetu zote kwa kipindi hiki kifupi cha uchaguzi kumbukeni siasa si kazi yetu kazi yetu ni sanaa tusiwe wajinga huu ndio wakati wa kuwafunza viongozi waliokuwa wanaidharau tasnia ya sanaa na wananchi waliokuwa wakiwaona ni sawa na box lisilo na bidhaa ndani yake najua wasanii wenzangu kwamba kipindi hichi ni cha mavuno lakini tuangalie tusije tukala mpaka mbegu na kuzipata tena mbegu zingine mpaka miaka mitano ijayo sasa sijui kipindi chote hicho maisha yatakuwaje? Maana kuna maisha mengine baada ya uchaguzi.

WAZUNGU WANASEMA HIVI. To be a rich is not what you have in your account but what you have in your heart. Sijui nimepatia hiki kizungu haya walimu twende".

Vicent Kigosi ‘Ray ‘ @raythegreatest on instagram

Your work is going to fill a large part of your life, and the only way to be truly satisfied is to do what you believe is great work. And the only way to do great work is to love what you do. If you haven't found it yet, keep looking. Don't settle. As with all matters of the heart, you'll know when you find it. Steve Jobs

Habari zilizopo katika Magazeti ya Leo Jumanne ya Septemba 8

0
0
Hapa Nimekuwekea Habari zilizopo katika Magazeti ya Leo Jumanne ya Septemba 8



















LOWASSA 'Aitikisa Tena Dar...KIBAMBA Yatapika People's.....Wamwambia 'ULIPO TUPO'

0
0



Mh. Lowassa na viongozi wengine wa UKAWA, wakiwa jukwaani mbele ya umati wa watu

Wananchi wakionyesha alama ya mabadiliko inayotumiwa hivi sasa na UKAWA

Mh. Lowassa, na Mwenyekitin wa CHADEMA, Mh. Mbowe, wakiwasili kwenye eneo la mkutano huko Kibamba



Mgombea kiti cha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia vyama vinavyounda UKAWA, Mh. Edward Lowassa, leo tena amelitikisa jiji la Dar es Salaam, hususan maeneo ya Kibamba kulikofanyika mkutano wa kihistoria wa kampeni ambapo maefu ya wananchi walifurika wengine wakikaa juu ya mapaa ya nyumba za madarasa, wengine kwenye miti, kutokana na kukosa eneo zuri la kuweza kushuhudia "live" mkutanonukiendelea. Changamoto ya maeneo ya kufanyia mikutano ya kampeni ndiyo inayoonekana kuikumba UKAWA, kutokana na kuongezeka kwa idadi ya watu wanaohudhuria mikutano hiyo. Pichani mfuasi wa UKAWA, akiwa amejichora rangi za bendera ya CHADEMA akiambatanisha maneno maarufu yanayotumiwa na wafuasi wa Mh. Lowassa kwa sasa, yaani "Ulipo tupo".







Mh. Lowassa, akimnadi mgombea ubunge jimbo la Kibamba, John Mnyika.(Picha zote na Othman Michuzi)





Diamond Platnumz Reveal The Date Tiffah Dangote's Face To Be On Public.

0
0
"On the 20th of September 2015 my Daughter's face@princess_tiffah will be Exclusively shown for the first time to the public... would you like to know which companies have sponsored her first video and photo??? Apart from being@MsasanicityMall and @PuguMall#BABYSHOP brand Ambassador would you like to know which companies have endorsed her??? Stay with me!!!" said Diamond


Mgombea Urais wa CCM John Magufuli Kutatua Migogoro ya Ardhi Kisayansi

0
0

 
 Mgombea wa Urais kwa tiketi ya CCM Dk. John Pombe Magufuli(katikati) akiwanadi Mbunge wa Handeni Mjini Dk. Abdallah Kigoda (kulia) na Mgombea wa Ubunge Jimbo la Handeni Vijijini Ndugu Mboni Mhita kwenye mkutano wa kampeni uliofanyika kwenye uliofanyika kwenye uwanja wa Azimio Center.
 Mgombea wa Urais kwa tiketi ya CCM Dk. John Pombe Magufuli akimkabidhi mgombea wa ubunge jimbo la Handeni mjini Dk. Abdallaha Kigoda.
 Mgombea wa Urais kwa tiketi ya CCM Dk. John Pombe Magufuli akimnadi mgombea wa ubunge jimbo la Handeni Vijijini Ndugu Mboni Mhita.Mgombea wa Urais kwa tiketi ya CCM Dk. John Pombe Magufuli akisoma bango la vijana wafanya biashara ndogo ndogo wa eneo la Dumila maarufu kama Feri wakati akielekea mkoani Tanga ikiwa muendelezo wa mikutano ya kampeni za CCM .
 Wananchi wanaoishi eneo la Dumila wakimsikiliza Mgombea wa Urais kwa tiketi ya CCM Dk. John Pombe Magufuli 
 Mgombea wa Urais kwa tiketi ya CCM Dk. John Pombe Magufuliakimnadi mgombea wa ubunge jimbo la Mvomero Sadiq Murad kwenye mkutano wa kampeni za CCM uliofanyika Mvomero, mkoani Morogoro.
 Wanachama wa CCM wakionyesha mabango ya mgombea wao wa Ubunge Ndugu Sadiq Murad kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye uwanja wa Kihalawa,Turiani mkoani Morogoro.
 Mzee Yusuph Makamba akihutubia wakazi wa Turiani mkoani Morogoro kwenye mkutano wa kampeni za kumnadi mgombea wa CCM pamoja na sera za CCM kwa wananchi wa Turiani.
 Kikundi cha akina mama wahamasishaji kikiingia uwanjani kwenye eneo la mkutano wa kampeni za CCM Turiani ambapo Mgombea wa Urais kwa tiketi ya CCM Dk. John Pombe Magufuli alihutubia.
 Wazee wa Turiani wakimsikiliza kwa makini Mgombea wa Urais kwa tiketi ya CCM Dk. John Pombe Magufuli.
 Mgombea wa Urais kwa tiketi ya CCM Dk. John Pombe Magufuliakihutubia wakazi wa Turiani mkoani Morogoro na kuwaambia atahakikisha migogoro ya ardhi inamalizika na kuileta jamii kuishi kwa amani na upendo.
 Mgombea wa Urais kwa tiketi ya CCM Dk. John Pombe Magufuliambapo aliwaambia wananchi hao ataunda baraza dogo la mawaziri lakini pia atahakikisha barabara zinakamilika kwa kiwango cha Lami.
 Wakazi wa Turiani mkoani Morogoro wakimsikiliza Mgombea wa Urais kwa tiketi ya CCM Dk. John Pombe Magufulikwenye mkutano wa kampeni.
 Wananchi wakiinua mikono kuonyesha kukubaliana na Mgombea wa Urais kwa tiketi ya CCM Dk. John Pombe Magufuli 
 Mgombea wa Urais kwa tiketi ya CCM Dk. John Pombe Magufuli akimkabidhi ilani ya uchaguzi mgombea ubunge wa jimbo la Mvomero Ndugu Sadiq Murad.
 Mama akifurahia jambo kwenye mkutano wa kampeni za CCM uliofanyika Turiani mkoani Morogoro.
 Wakazi wa Kwaluguru wakimsubiri Mgombea wa Urais kwa tiketi ya CCM Dk. John Pombe Magufuli afike na kuwasalimu wakazi hao.
 Mgombea wa Urais kwa tiketi ya CCM Dk. John Pombe Magufuli akimnadi mgombea ubunge jimbo la KilindiOmari M. Kigua wakati wa mkutano wa kampeni uliofanyika Kwaluguru.
 Wakazi wa kijiji cha Bandari kata ya Kimbe wakimsikiliza Mgombea wa Urais kwa tiketi ya CCM Dk. John Pombe Magufuli.
 Wakazi wa Songe wakifurahia ujio wa Mgombea wa Urais kwa tiketi ya CCM Dk. John Pombe Magufuli 
 Mgombea wa Urais kwa tiketi ya CCM Dk. John Pombe Magufuli akihutubia wakazi wa Songe ambapo aliwaambia wananchi hao katika uongozi wake atasimamia haki kwa wananchi wote na kuhakiisha huduma zote za msingi zinapatikana.
 Mgombea wa Urais kwa tiketi ya CCM Dk. John Pombe Magufuli akihutubia wakazi wa Kibirashi
 Msafara wa Mgombea wa Urais kwa tiketi ya CCM Dk. John Pombe Magufuli ukiwasili Kwediboma.
 Mgombea wa Urais kwa tiketi ya CCM Dk. John Pombe Magufuliakihutubia wakazi wa Kwediboma.
Wananchi wa Handeni wakishangilia jambo kwenye mkutano wa Kampeni za CCM uliofanyika kwenye uwanja wa Azimio Center mkoani Tanga.

Taarifa za Uhamiaji kuchunguza uraia wa Zitto Kabwe

0
0
Akizungumza kwenye moja ya mikutano ya kampeni Kigoma, mgombea urais kwa tiketi ya ACT-Wazalendo ambaye pia ni mwenyekiti wa chama hicho Anna Mghwira amesema, anawashangaa Uhamiaji leo kuanza kuchunguza uraia wa Zitto wakati ameshawahi kuwa mbunge wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Habari zaidi soma gazeti la Majira la leo.

Nuh Mziwanda: Sioni Tatizo kwa Msanii Kuonesha Mahaba kwa Chama Anachokipenda

0
0
Nuh Mziwanda amewataka wasanii kuwa wazalendo kwa kuonyesha hisia zao za vyama vya siasa na kuonyesha ushirikiano katika kuhamasisha.

Akizungumza na Planet Bongo ya East Africa Radio leo, Nuh alisema maendeleo yatakayopatikana ni manufaa kwa watanzania wote kwa ujumla.

Wewe ukiwa msanii sio kwamba sio mwananchi wa kawaida,” alisema.

Wewe pia unahitaji kutawaliwa vizuri. Unahitaji utawala mzuri ambao utaongoza hata kazi zako ziende vizuri. Kwahiyo ni vyema mtu ukajua upo upande gani. Huo ni upendo wa nchi yako na ni mzalendo. Kila binadamu anapenda uongozi mzuri ndio maana kila mtu akiwa na akili timamu ana haki ya kuchagua chama anachokitaka,” aliongeza.

Lakini sisi wasanii tusijisahau tukawa tunashindwa kuweka hisia zetu kwaajili ya maslaHi ya nchi yetu. Unaogopa kuweka wazi wewe ni chama gani, unampenda mwanasiasa gani! Sisi ni vioo vya jamii tunaangaliwa pia na watu na kuna watu wahitaji ushauri au ufafanuzi juu ya viongozi waliotangaza nia. Kwa sisi inatubidi tuwe mfano kwanza kabla ya wananchi.”

Your work is going to fill a large part of your life, and the only way to be truly satisfied is to do what you believe is great work. And the only way to do great work is to love what you do. If you haven't found it yet, keep looking. Don't settle. As with all matters of the heart, you'll know when you find it.

Steve Jobs




Viewing all 104429 articles
Browse latest View live


Latest Images