Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104432 articles
Browse latest View live

NAY WA MITEGO NA MPENZI WAKE MAMBO MOTO MOTO AMNUNULIA MKOKO WA NGUVU

0
0
 True Boy Aonyesha upendo alio nao kwa mpenzi wake kwa kumnunulia gari .....check hapa chini:


ARUSHWA GOROFANI BAADA YA KUFUMANIWA AKIFANYA MAPENZI

0
0
Mzee mmoja mwenye hasira kali, Deji Kamoru, amejikuta akitiwa mbaroni baada ya kumfuma binti yake Aishat chumbani kwake na kuuamua kumrusha kupitia dirishani ghorofa ya 3, mkasa huo kwa mjibu wa walioshuhudia ulitokea pale mzee huyo aliporudi nyumbani kwake na kumkuta binti yake mwenye umri wa miaka 14 akiwa chumbani kwa baba yake akila uroda na boyfriwnd wake, kwa mjibu wa shuhuda wa tukio hilo  mzee huyo aliamua kumfunga mikono binti yake huyo na kumchapa kisha kumrusha dirishani... binti huyo alipofika chini alipigiza kichwa na kupoteza fahamu.. mpaka sasa binti hajitambui na yuko ICU katika hospital ya taifa ya nigeria... mzee huyo ameachiwa kwa dhamana ili aweze kumhudumia mwanae hospital kwani mama yake waliishatarakiana siku nyingi

BABY MADAHA AKIRI UCHAWI UPO BAADA YA KUPIGWA JUJU NA KUSINGIZIWA KUJIUZA

0
0
Mwanamuziki na muigizaji baby Joseph madaha amefunguka na kusema kuwa kweli ameamini uchawi na kupigana juju vipo kwenye gemu kwani mambo yaliyomtokea hivi karibuni haelewi hata imekauje.

Chanzo nini?

Hapo siku za nyuma baby Madaha alipatikana na dhahama ya kukumbwa na kashfa nzito sana ya kujiuza kwa dau la milioni kumi kwa jamaa mmoja hivi mitaa ya Dar es Salaam Jambo lilolopelekea yeye kupigwa chini na Record label yake ya Candy and Candy ya huko Kenya na kupokonywa gari aina ya AUDI TT aliyokuwa akitembelea huku akiharibu pia uhusiano wake na bosi wa record label hiyo - Joe kairuki ambaye pia anadaiwa kuwa mpenzi wake.

Je ni Kweli alijiuza?

Baby Madaha ambaye amerudi nchini hivi karibuni tokea Nairobi alipoenda “ku-solve” ishu yake hiyo na label hiyo anasema yani hata haelewi kitu gani kilitokea siku hiyo ingawa mpaka akaandikwa kama alienda kujiuza, anachokumbuka ni kupigiwa simu na mtu asiyemfahamu an kumwambia anataka wafanye naye kazi ya kusambaza filamu yake mpya ya Gal Bladder ambaye inatikisa soko kwa sasa.

Baada ya kufika hapo waliongea vizuri na kuondoka ghafla kabla ya kuja kusoma kesho yake kuwa alikuwa anajiuza kitu ambacho ansema hajui kimetoka wapi.

“Yani hata sielewi ilikuaje nikaenda kukutana na yule jamaa, ilikuwa ni kama muujiza hivi, mwanzo nilisita sana ila nikashangaa nimefika tu pale bila kujielewa, ni vitu vya ajabu sana” alieleza baby Madaha.

Uhusiano wake na Label hiyo ukoje sasa?

Akizungumza na bongomovies, baby amesema kwa sasa kila kitu kipo sawa kwani alipoenda Kenya waliongea vizuri na bosi wake huyo na kumaliza tofauti zao na sasa amerudi nchini kusambaza filamu yake hiyo mpya ya Gal bladder huku akijiindaa kupiga show kwenye tour yake aliyoiandaa  jina la Top Up and Refill itakayofanyika mwezi ujao wa tatu.

Mwenyewe anasemaje zaidi?

Hata wafanyaje, waniroge, wanichafue, i'm a bad gal, na sibabaishi na vijimaneno vya watu hata kidogo, sitoki candy and Candy hata waloge kwa waganga wote duniani. Kama walifikiri nimeumbuka, wajue watasubiri sana. Nikitoka kenya naenda Holywood tu!

Bongomovies

WEMA SEPETU AWASHANGAA WANAO MPONDA JOKATE..

0
0
Mwigizaji Wema Sepetu, amewashangaa wanaomponda Jokate Mwegelo kwa kumaliza tofauti baina yao akisema kuwa hawatendi haki na wanaingilia uhuru wa wasanii hao.

Kauli ya Wema imekuja siku chache baada ya Jokate kufika kwa kushtukiza katika onyesho lililofanywa na Wema mkoani Arusha hivi karibuni na kumaliza tofauti zao.

Wawili hao wanadaiwa walikuwa wakimgombea mwanamuziki nyota na tajiri, Diamond Platinum.

“Sikuona kioja wala ajabu, kwa kuwa tulikuwa marafiki na kilichotokea ni ujana. Kila mmoja amekaa na kuona hakuna haja ya kuwa na bifu zisizokuwa na faida. Nimemuunga mkono Jokate kwa kuwa ameonyesha kukua na kukomaa kiuamuzi, hakuna haja ya kumbeza kwa maneno ya kijinga,”alisema Wema.

TASWIRA YA TANZANIA YACHAFUKA NCHINI UINGEREZA

0
0
Wakati Rais Jakaya Kikwete akijiandaa kwenda London Uingereza kuhudhuria mkutano wa kuokoa viumbe vilivyo hatarini kutoweka duniani ukianza wiki hii, tatizo la ujangili limeweka wingu zito kwa Tanzania.

Rais Kikwete ni kati ya viongozi wa nchi 50 watakaohudhuria mkutano huo, utakaokuwa chini ya wenyeji wa mwana wa Wales na Waziri wa Mkuu wa Uinegerza, David Cameron,

Taarifa ya gazeti la The Mail on Sunday la Uingereza la Februari 8, limeitaja Tanzania kama kinara wa ujangili kwa kuua zaidi ya tembo 11,000 kwa mwaka, huku Rais wake (Jakaya Kikwete) akielezwa kufumbia macho.

Pia, gazeti hilo limemhusisha Rais Kikwete kuwa na urafiki na wafanyabiashara ya meno ya tembo, huku likiwahusisha wafadhili wa Chama cha Mapinduzi (CCM) katika biashara hiyo.

“Utawala wa Rais Kikwete umetawaliwa na mauaji ya tembo yaliyovunja rekodi katika historia ya nchi yake. Kibaya zaidi, wahifadhi wanasisitiza kuwa, ndani ya Serikali kuna viongozi wanaoshiriki biashara hiyo,” imesema sehemu ya taarifa hiyo.

Katika mkutano huo, viongozi wa nchi 50 na mawaziri wataweka mikakati dhidi ya biashara haramu ya wanyamapori, yenye thamani ya pauni 6 bilioni za Uingereza kwa mwaka zinazotumika kufadhili magaidi.

Taarifa hiyo inasema kuna wafanyabiashara wakubwa wa Dar es Salaam wanaohusika na ujangili.

“Miongoni mwao ni  matajiri wakubwa nchini, wafadhili na wanachama wa CCM na ndugu wa karibu wa Rais Kikwete. Lakini wanao marafiki wakubwa, huku majaji, waendesha mashtaka na polisi hurubuniwa kwa urahisi,” inasema sehemu ya taarifa hiyo.

Pia, taarifa hiyo inadai kuwapo kwa idadi kubwa ya Wachina wanaofanya biashara ya mafuta nchini, huku baadhi yao wakihusika na ujangili.

Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Ikulu, Salva Rweyemamu alikiri kuona taarifa hiyo na kwamba, Rais Kikwete atahudhuria lakini aliipuuza taarifa hiyo.

“Ni kweli Rais Kikwete atahudhuria huo mkutano, lakini taarifa ni ya None sense, crap and malicious (ya kishenzi, kipuuzi na ovu),” alisema Rweyemamu.

Juhudi za kumpata Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu hazikufanikiwa baada ya simu yake kuita  muda mrefu bila kupokelewa.

TATHMINI YA MATOKEO YA UCHAGUZI WA MADIWANI BAADA YA CCM KUIBUKA KIDEDEA JANA

0
0
Hakika nimepata mshituko mkubwa kuona matokeo ya uchaguzi wa udiwani katika kata mbalimbali yameenda ndivyo sivyo kwa upande wa chadema. Katika kata 27 ukitoa 1 zinabaki 26.

Katika kata hizi CHADEMA imepata kata 3 tu huku NCCR ikiendelea kupata hisani ya kata 1 kwenye Jimbo la Zitto Kabwe. Zilizobakia zote CCM imechukua. Sasa hapa ndipo mshituko wangu ulipoanzia.

Lakini zipo sababu kadhaa zilizopelekea matokeo haya.CHADEMA na ujazaji wa watu kwenye mikutano yake Itakumbukwa kwamba hivi karibuni uongozi wote wa juu ulipita katika mikoa kadhaa kufanya mikutano na wananchi.

Japo agenda kuu haikuwa uchaguzi huu wa madiwani lakini walitumia nafasi hiyo pia kuwanadai wagombea udiwani wake. Kwa mahudhurio tuliyokuwa tunayaona kupitia ITV na mitandao ya kijamii tungeamini kuwa hii ilikuwa nafasi ya ushindi wa kishindo safari hii. Lakini mambo yameshtua zaidi. Nadhani tujitatmini upya.

Tubadilishe mbinu za kushambulia adui. Je wahudhuriaji wote ni wapiga kura? Nilichobaini kwa mtazamo wangu ni kuwa wale wote wanohudhuria mikutano ya CHADEMA si wapiga kura halali wanaotambulika na NEC. Wale ni wapiga kura wetu wasio rasmi. 

Chukua mfano wa kata ya Nyasura huko Bunda ambayo tuliambiwa toka awali kuwa tayari CCM ipo katika hali mbaya. Lakini matokeo yamekuwa tofauti. Labda palipokuwa na ukweli ni huko Njombe mjini tu ambako CHADEMA imeshinda. Nini tatizo hapa? Kwa mtazamo wa haraka haraka unakubaliana na hoja ya CHADEMA waliyokuwa wanaililia.

Hoja ya uboreshaji wa daftari la wapiga kura. Hapa ndipo CCM ilipokuwa inatumia mwanya adhimu kabisa. Ni ukweli kuwa kuna wananchi wengi hawana vitambulisho vya kupigia kura. Vijana wengi nawafahamu katika eneo langu ambao ni wakereketwa wa CHADEMA hawana vitambulisho hivi.

Kwa hiyo basi, Tume ya Uchaguzi itakapoliboresha daftari hili naamini Chadema itapata mtaji mkubwa mkononi. CCM ina wapiga kura? Ndio.Hapana. Majibu yote ni sahihi kwa sasa. 

CCM ina wanachama na wapiga kura waliozeeka. Kwanini? Ukiwatazama wapiga kura wengi wa CCM ni wale wanachama wao ambao si wengi. Lakini wanafanikiwa kupata kura hizo kwa sababu CHADEMA haina wapiga kura wa kutosha ukilinganisha na idadi kamili ya wahudhuriaji wa mikutano yake.

Akina mama ndio wapiga kura namba moja kwa CCM. Idadi hii itazidiwa pindi daftari la wapiga kura litakpoboeshwa. Ni kweli CCM inanunua wapiga kura? yawezekana kweli lakini binafsi napingana na hoja hii. 

Hivi tunaposema wananunua wapiga kura kwa kuchukua shahada zao, wao wenyewe wahusika wanakuwa wamejitoa ufahamu? Madai haya nayasikia kwa muda mrefu sana. Lakini mbona mimi katika eneo langu hawaji kunishawishi kununua hiyo shahada? Au wanaangalia na mtu mwenyewe wakiona unajitambua wanakuruka? Wananchi ndio wajinga kwa kukubali kuuza shahada hizo kwa bei ya kujidhalilisha. 

Ushauri wangu CHADEMA tujipange upya. Tujitathmini. Kwa mwenendo ninaouona kwa sasa, chaguzi za serikali za mitaa tutapata aibu kubwa na hapo ndipo ndoto ya Ikulu itakapoyeyuka.

Nimeshauri sana kwa baadhi ya viongozi wa mkoa kujikita zaidi vijijini ambako mwamko umeanza kujitokeza kwa kuunga mkono upinzani. Sasa tusiwakatishe tamaa. Viongozi hatupendi kwenda kufanya mikutano vijijini.

Tayari mjini watu wameshaelewa umuhimu. Tusahihishe makosa yetu. Kipimo kikuuu cha CHADEMA kuingia Ikulu kitatokana na namna tutakavyojipanga kwenye serikali za mitaa. Hadi hivi sasa tunakosa wagombea wa serikali za mitaa. Hatujajipanga. Tukiendelea kulalamika tu kwa mbinu chafu wanazofanya CCM tutaishia kulia kila siku.

Kumbukeni kuwa Jeshi la Polisi hasa viongozi wake wakuu wote wapo CCM. Huwezi kupata cheo serikalini kwa sasa kama wewe si mwanachama wa CCM.

Hivyo basi, kufikiri jeshi la polisi hasa viongozi wake kuunga mkono upinzani ni ndoto kubwa ambayo hatupaswi kuota usiku wala mchana. Ni hayo tu kwa sasa. Nimesikitika sana kwa matokeo haya.
Source:Ngalikivembu wa JF

NI SAHIHI KUMUOA X-GIRL WA RAFIKI YAKO WA KARIBU

0
0
Nilitokea kumpenda sana binti mmoja lakini sikuwa na uwezo wa kuingia kwenye uhusiano naye kipindi hicho na najua alijua kuwa nampenda lakini kulikuwa na vizuizi flani flani.

Binti alikuwa anakaa hostel ya mabibo na nina rafiki yangu sana walikuwa wanasoma naye baadae akamtokea jamaa kagharamia sana wakawa kwenye uhusiano, na jamaa akaniambia lakini binti hakuniambia coz wote nilikuwa nawasiliana nao, sasa nilionana na binti kanisani na nikamuuliza kuwa najua wapo na uhusiano lakini akaniambia waliachana miezi 6 iliyopita, baadae sanaa siku za mbele nikamuuliza jamaa naye akasema ni kweli waliachana japo jamaa ameongea kinyonge na kwa wasiwasi (nahisi kwa sababu alikuwa anajua nampenda yule msichana na inaonekana yeye bado anampenda sana na yeye ndio alimwagwa). 

Basi mimi nikawa nawasiliana na yule binti na kwa sababu nilimpenda siku nyingi nikamwaga sera zangu na binti kanielewa na kwa sasa tumeshaanza rasmi uhusiano japo kimya kimya, kusema kweli natamani kumuoa huyu binti lakini pia namfikiria huyu rafiki yangu, naombeni mnishauri wana MMU, je ni sahihi kumuoa binti aliyeachana na rafiki yako wa karibu?

WALIO TANGAZA NIA CCM KIKAANGONI

0
0
Baadhi ya makada wa CCM ambao wataitwa mbele ya Kamati ya Maadili na Usalama ya chama hicho, wanakabiliwa na shtaka la kutoa rushwa kwa lengo la kushawishi kukubaliwa kwao, Mwananchi limebaini.

Makada hao ni wale wanaodaiwa kuwa katika harakati za kuwania urais wa 2015, hatua ambayo imekigawa chama hicho katika makundi yasiyo rasmi ya yanayowaunga mkono wagombea hao.

Tovuti hili imedokezwa kuwa mgombea mmoja wa nafasi hiyo mwenye ushawishi mkubwa aligawa fedha Sh200,000 zilizoambatana na kadi za kuwatakia heri ya Krismasi na Mwaka Mpya 2014 idadi kubwa ya wajumbe wa Mkutano Mkuu wa CCM.

Kadhalika, habari kutoka ndani ya chama hicho zinasema baadhi ya wanaojiwinda kwa ajili ya uongozi, pia waligawa fedha kwa kigezo cha kuwashukuru wajumbe waliowachagua kuingia katika Halmashauri Kuu ya CCM (NEC), zaidi ya mwaka mmoja uliopita.

Hata hivyo, taarifa zaidi zinasema baadhi ya wajumbe waliopelekewa kadi hizo na fedha, walitoa taarifa kwa uongozi wa juu wa CCM pamoja na kuzirejesha, huku wakitaka wahusika wachukuliwe hatua.

“Kumekuwa na shinikizo kubwa kutoka kwa baadhi ya watu ndani ya chama kwamba ugawaji wa fedha nyingi kiasi hicho haupaswi kuvumiliwa hata kidogo, kwa hiyo ni dhahiri kwamba suala la chama kuchukua hatua halina mbadala, lazima hatua zichukuliwe,” alisema mmoja wa watendaji wa CCM makao makuu Dodoma na kuongeza:

“Waliorejesha hizo kadi na fedha hatukuwaruhusu waondoke hivihivi, bali tuliwataka waandike barua za malalamiko maana tunaweza kuwahitaji kwa ajili ya kutoa ushahidi mbele ya Kamati ya Maadili.”

Uchunguzi unaonyesha kuwa miongoni mwa waliorudisha fedha na kadi hizo ni wenyeviti wa wilaya na wajumbe wa NEC wa wilaya ambao ni sehemu ya walioshinikiza kuchukuliwa kwa hatua.

Akizungumzia suala hilo mwishoni mwa wiki iliyopita, Makamu Mwenyekiti wa CCM (Tanzania Bara), Philip Mangula alisema mwanachama yeyote wa chama hicho hatakiwi kutoa michango, misaada, zawadi kwa mtu au katika shughuli yoyote bila kupata ridhaa ya uongozi.

“Kufanya jambo hilo ni kwenda kinyume na kanuni za chama. Ndani ya chama kila ngazi ina Kamati ya Maadili, wote ambao wameanza kwenda kinyume na kanuni za chama watahojiwa katika kamati hizo,” alisema Mangula na kuongeza:

“Hairuhusiwi kuwasafirisha wajumbe, kuwapa malazi, chakula, vinywaji na ukifanya hivyo utakuwa unakwenda kinyume na utaratibu uliowekwa na Kamati ya Sheria, Katiba na Kampeni.”

Akihutubia kilele cha maadhimisho ya miaka 37 tangu kuzaliwa kwa chama hicho, Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete aliziagiza Kamati za Maadili na Usalama, kuwachukulia hatua stahiki viongozi na wanachama wake wanaomwaga fedha ili kupata uongozi. Kadhalika, Rais Kikwete alipozungumza na wajumbe wa Halmashauri ya CCM ya Mkoa wa Mbeya, alisema kuanza kwa kampeni kabla ya wakati wake ni moja ya mambo yanayosikitisha na kwamba suala hilo limekabidhiwa kwa Mangula kwa hatua zaidi za kinidhamu.

Watakaowekwa kikaangoni

Mangula alisema wanaCCM watakaowekwa kikaangoni wapo katika makundi matatu, wakiwamo wale waliogawa fedha kwa lengo la kutaka kuungwa mkono katika harakati zao za kusaka uongozi wa nchi.

Alitaja makundi hayo kuwa ni wagombea wanaomwaga fedha kwa wanachama, mawakala wanaotumiwa na watu wanaoutaka urais 2015.

JOKATE AFICHUA SIRI YA KUPATANA NA WEMA

0
0
THE big boss wa Kidoti, Jokate Mwegelo ambaye pia ni staa wa sinema na Bongo Fleva, amefichua siri ya kupatana na Wema Isaac Sepetu akisema kuwa sababu ya yeye kuonekana kwenye jukwaa moja na aliyekuwa hasimu wake huyo ni kutafuta amani ya moyo aliyokuwa ameikosa si kweli kwamba alisukumwa na nguvu ya pombe.…
Wawili hao walipatana hivi karibuni wakiwa jijini Arusha.
Akizungumza na gazeti namba moja la burudani Bongo, Ijumaa Wikienda, Jokate alisema ilipokaribia siku ya kwenda Arusha, Wema alimkaribisha kwenye shoo yake iliyofanyika jijini humo lakini alimwambia kuwa amebanwa ila akamuahidi kwamba akimaliza mambo yake atakwenda kumsapoti.
“Wema aliondoka bila kujua kama nitakwenda lakini nilipopanga ratiba yangu ikakaa sawa, niliamua kwenda na kumfanyia ‘sapraizi’ na si kweli kwamba nilisukumwa na nguvu ya pombe,” alisema Jokate.
Jokate alisema kwamba hakushauriwa wala kujadiliana na mtu yeyote isipokuwa aliamua mwenyewe kufanya jambo hilo ambalo lilikuwa likimkosesha faraja kwa muda mrefu.
“Nimeamua kumaliza mabifu kwa sababu nilikosa amani ninayoitaka kwa muda mrefu. Ukweli Wema alinikaribisha, nikaona ndiyo sehemu ya kutimiza lengo langu la kupatana naye,” alisema Jokate ambaye aliingia kwenye gogoro na Wema baada ya kutembea na mpenzi wake, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’.
Global Publishers

PENZI LA RAY NA CHUCHU SI SIRI TENA...WENYEWE WAITANA BABY FACE

0
0
Penzi kati la waigizaji wawili maarufu ndani ya bongo movie, Vicent Kigosi – Ray na Mwanadada Chuchu Hans limekuwa sio siri tena baada ya hivi majuzi mwanadada Chuchu hans kuweka picha mbalimbali za Vicent kigosi na yeye kwenye mtandao mmoja wa kijamii huku akiandika “I love my babyface NO MATTER WHAT (TOO MUCH)” akimaanisha kuwa anampenda sana mwigizaji huyo  kwa hali yoyote ile na anampenda sana.

Penzi hilo limekuwa la utata baada ya kuleta mtafaruku hapo siku za awali baina ya waigizaji Johari na chuchu Hans kudaiwa kuzitwanga wakimgombania muigizaji huyo.
Source:Bongo Movies

LULU AAMUA KUVUNJA UKIMYA BAADA YA STORY KUSAMBAA KUWA KAPATA MCHUMBA

0
0
BINTI anayeshikilia Tuzo ya Mwigizaji Bora wa Kike ya Ziff 2013, Elizabeth Michael maarufu Lulu ameweka wazi kuwa amepata mchumba na kwamba taratibu za kujitambulisha na mahari vitafuata baadaye.
“Unajua mimi ni binadamu na ili nitulie na kujiepusha na majanga, ni vyema kuwa na mpenzi mmoja  mwaminifu, anayenijali mimi na kazi yangu hapo nitasimama na kusema kwamba nimepata sehemu ya kutulia na kuanza maisha mapya ya uhusiano na ndoa,” anasema Lulu.
Hata hivyo anasema yeye na mchumba huyo (ambaye hakutaka kuweka wazi jina lake) wana mikakati mingi katika kuyafikia maisha ya uhusiano yaliyo wazi na yenye baraka za wazazi.
“Siwezi kukutajia jina kwa sasa itafika wakati atajulikana tu, hata hivyo bado hatujafikia hatua muhimu ikiwa ni pamoja na kujitambulisha kwa wazazi na masuala ya mahari na ndoa. Vitu kama hivi vitafanyika baadaye mwaka huu, hata hivyo wazazi wangu sidhani kama watakuwa na pingamizi katika hili kwani mimi ni mtoto wa kike na nimekua sasa,” anasema.
Kuhusu Mama Kanumba Lulu anasema: “Huyu ni mama yangu hana tofauti na mama Lulu hivyo anajua kila kitu na amenipa baraka zake zote, yaliyopita si ndwele kinachotakiwa ni kuganga yajayo, namshukuru mama kwani amenionyesha upendo wa kweli na kunishauri katika maisha, bila yeye nisingekuwa na ujasiri nilionao sasa.
“Mama Kanumba ni rafiki yangu wa ukweli, ana mapenzi mazito sana kwangu amekuwa mstari wa mbele kunishauri na kunipa mwongozo wa maisha ni nini na wapi nilipokosea na natakiwa kufanya nini ili kuwa na maisha yaliyonyooka,” anasema mwigizaji huyo anayetamba na filamu ya Foolish Age.
Lulu mwenye miaka 19, anasema haikuwa rahisi kwake kufikiria kutulia kiuhusiano ila amepewa mwongozo bora unaomfanya afikirie kufanya hivyo kwa sasa.
“Mimi ni binti na kama ujuavyo nina mapenzi yangu moyoni, si kazi rahisi kuamua kwa sasa lakini nimepewa mwongozo bora na kuona nini natakiwa kufanya. Kama binti napaswa kuzingatia maadili, mimi ni kioo cha jamii, inafika hatua inabidi niishi katika maadili hilo ndilo ninalolifanya sasa.”
Anasema wazazi wake wamempa baraka zote kuhusu uhusiano wake wa sasa: “Wazazi wangu sasa wanafahamu kwamba nimepata mchumba, kwa kweli wamenipa baraka zao zote, pande zote hata Mama Kanumba. Nimekua sasa na mimi nina uamuzi wangu, ni vema kuangalia ninataka nini lakini kikubwa wananishauri.”
Anasema wazazi wake hawakubali kila anachokitaka: “Sina wazazi wa kukubali kila ninachokitaka ila nina wazazi waelewa, wenye kuangalia jambo kabla hawajaniambia sasa unaweza kuendelea, mama yangu ni mkali sana, hana mchezo hasa pale anapoona kwamba nayumba kimaisha,” anasema Lulu.
Kuhusu tetesi zilizoenea kwamba ana uhusiano na msanii wa hip hop Young Dee, Lulu alikana na kusisitiza kwamba hajawahi hata kuwa na ukaribu na msanii huyo.
“Nashangaa taarifa hizo watu wanazitoa wapi na mpaka leo nashangazwa na uvumi ulioenea kwamba tulifumaniwa, usiku ule nilikuwa sehemu nyingine tofauti kabisa, ukweli ni kwamba sijawahi kuwa na ukaribu na Young Dee, wala hata kumfikiria kama ninaweza kuwa na uhusiano naye. Bado, hatulingani kwa kweli,” anasema.

KLYNN AWEKA PICHA YA FAMILIA YAKE MTANDAONI..ATOA UJUMBE MZITO

0
0
 See beautiful Message to her Family ...Very Niceeee

RAY AFUNGUKA"MASHABIKI WANGU MNANICHANGANYA HIVI MNATAKA NIWE MNENE AMA MWEMBAMBA?"

0
0
 Ray C aomba Ushauri ....Embu Soma Message yake hapa chini:

JAYDEE AOMBA USHAURI KUBADILISHA JINA LA BAND YAKE, HATAKI TENA MACHOZI

0
0

Muimbaji wa kike wa muziki wa kizazi kipya nchini Lady Jaydee afikiria kubadilisha jina la band yake kutokana na machozi yaliyokuwa yakimliza kipindi hicho yameshafutika.

Amefikiria kubadilisha jina hilo la bendi yake na isiitwe Machozi Band kama ilivyozoeleka kutokana na sasa hatoe tena machozi kama ilivyokuwa hapo awali.

Kupitia ukurasa wake wa Facebook aliandika hivi " Nafikiria kubadilisha jina la band sababu Machozi Machozi niliolia zamani yashafutika. Mnashaurije???" alitupia swali hilo kwa mashabiki wake.

SIKILIZA NA DOWNLOAD WIMBO MPYA WA AY-ASANTE

0
0
Si vibaya, siku moja ukikaa na umpendae na kumwambia asante kwa yote alokufanyia, mko wote long time mnapendana, mnaheshimiana, hayo ni maneno ya AY yakisikika kwenye intro ya wimbo wake Brand new aliouachia

MELI ILIYONASWA NA ‘UNGA’

0
0
Stori:  Waandishi Wetu
WIKI iliyopita Jeshi la Polisi Kikosi Kazi cha Wanamaji Tanzania, walikamata shehena ya madawa ya kulevya ‘unga’ wenye thamani ya mabilioni ya shilingi zikiwa ndani ya meli.

Taarifa za uhakika zinadai kuwa meli hiyo ambayo ni mali ya Kampuni ya  Almansoor SA ya Iran ilikamatwa Jumanne iliyopita katikati ya bandari za  Zanzibar na Dar es Salaam.

Meli hiyo ilikamatwa baada ya askari waliokuwa doria kuilitilia shaka na  kufuatilia kwa karibu ili kujua ilikuwa imebeba nini.

Vyanzo vilivyokuwa katika eneo la tukio  vinasema kuwa meli hiyo ilikuwa na watu 12 na baada ya kupekuliwa ndipo walikuta kilo 201 za madawa ya kulevya aina ya heroine.

Watu waliokamatwa katika meli hiyo ni Mohamed Hassan (30), Abdul Nabii (30), Fahiz Muhamad (34) na  Rahi Baksh (30), wote raia wa Pakistani.

Wengine ni Abdulsamad Badreuse (47), Hazra Azat (60),
Nahimu Musa (25), Khalid Ally (35),  Kher Murad (38), Said Mohamed (34), Murad Gwaharam (38) na Ayub Hot (50) ambaye ni nahodha wa meli, wote raia wa Iran.

Meli hiyo ilikuwa na mtazamo wa kivuvi na lengo la wahusika ilikuwa wasishtukiwe kirahisi.
“Ilikuwa si rahisi kuigundua kama uwezo wako wa kufikiri ni mdogo lakini askari wetu wana akili sana na ndiyo maana meli ile ilihisiwa mara moja,” alisema mtoa habari mmoja kutoka jeshi la polisi.

Naye Kamanda wa Kikosi cha Wanamaji Tanzania, ACP Mboje Kanga alisema ilikuwa ni kazi kubwa kuibaini meli hiyo ilikuwa imebeba nini lakini kwa kutumia mbinu za kiintelijensia waliweza kuitilia shaka na kuipeleka bandari ya Dar es Salaam.

Kwa mujibu wa uchunguzi wa Uwazi, unga huo ulikuwa utue katika maeneo ya Ilala jijini Dar ambapo baadaye ungesambazwa kila kona ya nchi ya Tanzania.

“Ndugu waandishi, Ilala kuna maeneo ambayo ni maarufu sana kwa biashara kama hiyo, ule unga ulikuwa upelekwe Ilala halafu upelekwe nchi nzima,” kilisema chanzo chetu.

Kwa upande wake Kamanda wa Kikosi cha Kupambana na Kudibiti Madawa ya Kulevya Tanzania, Godfrey Nzowa akizungumza na gazeti hili kuhusu madawa hayo, alisema kama yangefanikiwa kutua Dar na kusambazwa nchini watu milioni 3 mpaka 4 wangetumia, hasa vijana.

Kamanda Nzowa alisema meli hiyo ilitiliwa shaka  kutokana  na kutokuwa na utambulisho wa nchi husika, yaani bendera kama  meli zingine.

Akasema baada ya upekuzi waligundua  zaidi ya kilo 201 za heroin zenye thamani zaidi ya shilingi bilioni 9.

“Mpaka sasa upelelezi unaendelea ili kubaini mwenyeji wao ambaye angewapokea Dar es Salaam ni nani maana kwa vyovyote yupo, tukimbaini amekwisha,” alisema Nzowa
GPL

HEE.... VIP TENA MCHUNGAJI MASANJA MKANDAMIZAJI NA DEMU WA PREZZO

0
0


Masanja Mkandamizaji Akiwa na Starlisha Aka Chaggabirbie....Wamependezajeee....Mwee Prezzo Akizengua Masanja Kamata mzigo ..hahaha

NAPE"CHADEMA NI MZIGO KWA TAIFA"

0
0
Chama ca Mapinduzi (CCM) kimewashukuru watanzania kwa kukiamini na kukipatia ushindi katika uchaguzi mdogo wa udiwani uliofanyika katika kata 27 na kushinda kata 23.

Kimesema siri ya kuimwaga CHADEMA ni uadilifu katika kuwatumikia wananchi na kwamba kushindwa kwa chama hicho ni ushahidi tosha kwamba hakikubaliki na Watanzania.



Katibu wa NEC ya CCM, Itkadi na Uenezi, Nape Nauye, amesema hayo na kuongeza kuwa matokeo hayo ni ushindi kwamba CCM inakubalika zaidi na Watanzania wengi.
Akizunguma kushindwa kwa CHADEMA, amesema wamehukumiwa kutokana na vurugu za kupiga watu kwenye kampeni za uchaguzi ndiyo maana wametumia gharama kubwa na helkopta tatu na kuambulia kata tatu.
“Watanzania hawapendi vurugu wamezoea Amani na utulivu sasa wamewaadhibu kwa kuwanyima kura na huo ni ushahidi kwamba Watanzania hawakiamini chama hicho,” amesema.

Katika uchaguzi huo CCM ilishinda katika kata 23 za Kibinduna Magomeni (Pwani), Kiwalala na Namikage (Lindi), Ubwage (Shinyanga), Ibumu na Nduli (Iringa), Kiomoni na Mtae (Tanga), Nyasura (Mara), Malindo na santillya (Mbeya). Zingine ni Partimbo (Manyara), Mkwiti ( Mtwara), Tungi na Ludewa (Morogoro) na Mrijo ( Dodoma).

Source, Uhuru

STEVE NYERERE"WASANII WENGI WA BONGO MOVIES HAWAJITAMBUI"

0
0
Mwenyekiti wa kundi la Bongo Movie Unity, Steven Mangere ‘Steve Nyerere’ amesema wasanii wengi wa filamu hawajitambui, mbumbumbu na wabinafsi katika kila kitu, jambo linaloleta ugumu katika harakati zao za kujikwamua.
Steve Nyerere ambaye pia ni mwigizaji na mchekeshaji, amesema wasanii wengi wanakosa umoja wa kudai haki zao kutokana na uelewa mdogo walionao huku wengine wakitazama maendeleo yao binafsi.
“Wasanii tumekuwa mbumbumbu wa kila kitu, tumeyumba kwa kuuza na kuibiwa kazi zetu na maharamia. Dada zetu nao wanafanya Bongo Movie ni sehemu ya kufanyia ukahaba.
Pia amesema yeye kama kiongozi anapigania haki za wasanii zisisahaulike katika mchakato wa katiba mpya ili waweze kupata nafuu ya kazi zao.

Source, Mwanaspoti

UKWELI KUHUSU TELEX FREE KUTOKA WIKIPEDIA..BRAZIL KIMENUKA

0
0
Mimi sina mengi wala siandikii mate Mange Jana Kaandika about TelexFree Watu wamemjia juu kuwa ni uongo ..ila ki ukweli hiyo Kitu ina walakini ....Embu jisomee hapa kutoka Wikipedia..Jinsi ilivyozuiliwa huko Brazil...


"From Wikipedia, the free encyclopedia....
Telexfree is a trade name owned by Telexfree Inc, that became best known for its operations in Brazil held by Ympactus Comercial Ltda after it was involved in an ongoing investigation for allegedly operating a Ponzi scheme. The Brazilian court of Acre State suspended the company's operations in that country
Telexfree Inc. owns the rights to the TelexFREE brand worldwide. The company was created by Carlos Roberto Costa, Carlos Nataniel Wanzeler and James Matthew Merrill after the change of its former corporate name "Common Cents Communications Inc.", which was incorporated in Massachusetts, USA.According to the Company Registration Office of Massachusetts, Telexfree Inc. started to use this corporate name on February 15, 2012.
Telexfree Inc. is a sister company of many other companies that operates TelexFree Marketing Plan, which belongs to the same founders and also share the same website. It includes a Brazilian company named "Ympactus Comercial Ltda", which was suspended on June 13, 2013, by Brazilian authorities.
Telexfree Brazilian operations was regarded as one of the largest financial frauds in Brazil's history, according to Brazil's Ministry of Justice and the Federal Public Ministry.The number of investors—labelled as "promoters" by Telexfree—has not yet been determined; by the end of August 2013, just after companies' suspension, Carlos Roberto Costa (Company Director) said that the company had 1,049,619 active promoters in Brazil.The company is currently under investigation by Brazilian authorities, which led the Court to freeze the company's and its owners' assets in Brazil and maintain, despite numerous appeals, the suspension of its operations in Brazil. Telexfree Brazil (Ympactus Comercial Ltda) denies the accusations, saying that it operates under the Multi-level marketing structure, commercializing VoIP services. The final trial and judgement will likely be held in 2014, and the company assets will probably remain frozen before that, according to the Public Ministry of Acre State.
Telexfree and BBOM, both companies suspected of operating Ponzi Schemes and suspended by the Brazilian justice, were featured among the top 10 most searched terms on Google during the year of 2013 in Brazil. Telexfree was ranked 2nd place, just after "BBB"
Read More HERE
Viewing all 104432 articles
Browse latest View live




Latest Images