Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104414 articles
Browse latest View live

Lori Lavamia Msafara wa Magufuli na Kugonga Magari Matatu

0
0
MSAFARA wa mgombea urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk. John Magufuli, umenusurika kupata ajali, baada ya lori la mizigo kuuvamia na kugonga magari matatu likiwamo lililokuwa limembeba mpiga debe wa chama hicho, Amon Mpanju.

Ajali hiyo ilitokea jana asubuhi katika eneo la Njia Panda jirani  kilomita chache kabla ya kuingia Maswa mjini.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Simiyu, Gemin Mushi jana alikiri kutokea kwa tukio hilo.

Alisema wakati msafara huo ukitoka wilayani Meatu, askari polisi waliokuwa wakiuongoza msafara huo walimuaru dereva wa lori hilo lenye namba za usajili T 217 DDY kuegesha pembeni gari lake, lakini alikaidi.

“Msafara wa mgombea urais ulikuwa jirani kuingia Maswa, dereva wa lori aliamuriwa kuliweka pembeni akakaidi, tena kibaya akaongeza mwendo hali iliyosababisha ajali.

“Lori hili ni mali ya Kampuni ya Dilchadri Mill Ltd ya jijini Mwanza, liligonga magari matatu likiwamo gari lenye namba za usajili T 217 CYM aina ya Toyota Land Cruser ambayo iliharibika vibaya na kushindwa kuendelea na safari.

“…Baada ya tukio hili, dereva amekimbia na polisi wanamsaka ili  afikishwe mbele ya vyombo vya sheria,” alisema Kamanda Mushi.

Kutokana na ajali hiyo, Kamanda  Mushi amewataka madereva kuzingatia sheria za usalama barabarani.Alisema hakuna mtu aliyeumia katika ajali hiyo.

Wakati huo huo, mgombea huyo aliendelea na mikutano yake katika wilaya za Maswa, Kishapu na Igunga.

Kwa nyakati tofauti katika mikutano hiyo, Dk. John Magufuli, aliwataka Watanzania kuchagua wabunge ambao watatetea masilahi yao badala ya wale wanaotoka bungeni kila zinapowasilishwa bajeti.

Alisema endapo atachaguliwa anataka kuona Bunge linalotimiza wajibu wake, ikiwemo kupigania  kero za waliowachagua.

“Haiwezekani wakati wa kujadili hoja za wananchi, wenzako wanatoka nje wanafanya hivi kwa kumkomoa nani?

“Maswa ninyi ni mashahidi kwa muda mrefu hamkuwa na mtu wa kuwasemea tatizo la maji, barabara na hata huduma za afya. Maana kila zinapopangwa bajeti wao wanatoka nje je waziri atajuaje kama kuna tatizo eneo husika.

“Hii si demokrasia hata kidogo ila ni kuwatesa wananchi, kwa hali hiyo sasa Watanzania wote chagueni wabunge wenye masilahi kwenu na watakaosemea shida zenu na si wale wanaotoka nje kila wakati (Ukawa),” alisema Dk. Magufuli

Aonya lugha chafu
Alisema ni vema viongozi wa vyama vya siasa kuepuka kampeni za matusi, kwani hazina tija kwa Taifa.

“Matusi si hoja, ndiyo maana kila ninaposimama situkani mtu, najenga hoja. Tunahitaji kujenga nchi yetu iwe ya amani siku zote,” alisema.

PICHA ya Lowassa Mgombea Urais wa Ukawa Yazua Gumzo Mtandaoni

0
0
Picha ya Mgombea Urais kwa tiketi ya UKAWA Mh. Lowassa akisaidiwa kupanda jukwaani Manyoni Singida kwenye kampeni zake za Urais, Huko Mitandaoni Kila Mmoja Ameongea lake..Je wewe Unasema Kuhusu Hii Picha ?


Mke wa Dr Slaa Azua Gumzo Marekani...

0
0
Wetu WAKATI nyumbani Bongo moto mkubwa umewashwa na mumewe aliyekuwa Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk. Wilbrod Slaa, Josephine Mushumbusi amekuwa gumzo Marekani.

Kwa mujibu wa Mbongo aishiye nchini humo akitumia mtandao wake wa Instagram, mara baada ya Josephine kutua nchini humo akiwa na familia, baadhi ya Wabongo waishio humo walipata habari kupitia mitandao ya kijamii, wakaanza kumtafuta.

“Jamani! Nimesikia kwamba, Dk. Slaa na mke wake wapo hapa Marekani. Sasa hamna namba zake? Maana tunataka kuwasiliana na mkewe,” alisema Mbongo huyo.
Baadhi ya wachangiaji walimuuliza kisa cha kumtafutia, alijibu: “Unajua tulisoma kwenye mitandao kuhusu madai ya Mchungaji Gwajima (wa Kanisa la Ufufuo na Uzima) kwamba, yeye (Josephine) amewahi kuanguka mapepo mara kadhaa.

“Lakini sasa hatujawahi kumsikia Josephine mwenyewe akijibu. Maana Gwajima alikuwa akimjibu Dk. Slaa, akaingiza na mambo ya mkewe. Sasa tunataka kujua mke naye anamjibu nini Gwajima?”
Habari zaidi zilidai kuwa, mke huyo amekuwa gumzo kwenye mitandao mbalimbali na mada kuu ni mke wa Dk. Slaa kuwa nchini humo, wengine wakitaka kujua kafuata nini.
Wengi wamehoji kama safari yake nchini humo na mumewe ni kwa sababu ya kujificha baada ya Gwajima kumwanika au kuna lingine.Hata hivyo, Mbongo mwingine alitupia kwenye mtandao wake wa Instgram akisema kuwa, ameshakutana na mke wa Dk. Slaa kwenye mgawaha mmoja akila maisha.

“Jamani, mke wa dokta nimekutana naye laivu. Anakula raha tu. Wabongo kule wao bado wanawashiana moto kwenye kampeni,” sehemu ya ujumbe huo ulisomeka hivyo.
Wakati f’lani mwanzoni mwa mwaka huu, mwanamke huyo akiwa na mume wake walikuwa nchini humo ambapo alionekana akiwa kwenye eneo la starehe akiendesha baiskeli.
Hata hivyo, wakati wa kuondoka nchini, Dk. Slaa mwenyewe alisema anakwenda Marekani kwa ajili ya mapumziko na kwamba atatumia kipindi hicho kujiendeleza katika kozi ya lugha na sheria.

Ninatafakari hatima ya CCM kama Lowassa angekuwa ni mgombea Urais wa CCM

0
0
Kuna mengi sana yamesemwa kuhusu mchakato wa kumpata mgombea wa Urais kwa tiketi ya CCM uliofanikisha kumpata John Magufuli kuwa mgombea Urais.

Kwa kuangalia kwa nje kabla ya kumteua Magufuli, CCM ilikuwa inakabiliwa na hali yenye mashaka na hatari (awkward situation) kuhusu hatima ya Lowassa.

Kwa kuangalia kwa nje, maamuzi yoyote kuhusu Lowassa ndani ya CCM yalikuwa yanaiweka CCM katika wakati wa aina yake kwenye uchaguzi.

Kwa sasa ni zaidi ya mwezi mmoja tokea mchakato wa kumpata mgombea Urais ndani ya CCM umalizike. Katika muda huu majibu ya maswali mengi yameanza kupatikana.

Kwa sasa ninaweza kusema, kama mgombea wa Urais kwa tiketi ya CCM angekuwa ni Lowassa, CCM ingekuwa imeishashindwa kabla hata ya kuanza kampeni za Uchaguzi Mkuu.

Ndani ya mwezi mmoja akiwa CHADEMA, Lowassa ameonyesha udhaifu mkubwa pamoja na kusaidiwa na CHADEMA/UKAWA kulibeba/kulishusha zigo la ufisadi ambalo amelibeba kwa miaka mingi. CCM wasingeweza kuhimili hoja kutoka upinzani huku wakiwa wamebeba zigo lote la ufisadi na hasa ikichukuliwa hata uwezo wa Lowassa ni mdogo katika kuhimili jukwaa la kisiasa achilia mbali afya yake.

Lowassa akiwa mgombea wa CCM asingeweza kusema maamuzi ya kuendelea na mkataba wa Richmond yalitoka kwenye mamlaka ya juu ili kukabiliana na hoja za wapinzani. Wapinzani kama walivyo watu wengine wasingeamini haya maneno mepesi yasiyokuwa na chembe ya ukweli kiutendaji kwa Waziri Mkuu ambaye aliwahi kusema hawajakutana barabarani na Rais Kikwete.

Kuna wapinzani wengi tu wanaamini maneno ya Lowassa ni uwongo lakini kwa vile Mbowe na genge lake amewaletea Lowassa kama mgombea Urais, wanajikuta hawana njia nyingine zaidi ya kumkubali kama mgombea Urais. ndiyo maana kwa sasa kuna hoja ambazo wanadai wanamtumia tu Lowassa ili kushinda uchaguzi mkuu kwa sababu ana nyenzo fedha.

Kukatwa kwa Lowassa na Uthubutu wa kuihama CCM na kujiunga na CHADEMA kumefanya CCM wapumue na kulifanya zoezi la kumpata Rais wa Tanzania lichukue sura nyingine.

Wahenga walisema, Usilolifahamu ni kama...

Lowassa Utusamehe Sisi Wana CCM, ni Kosa Lipi Lisilohitaji Msamaha?

0
0
Ndugu wanaCCM wenzangu, huu ni ukweli. Tabia ya ukweli ni kuumiza mioyo ya watu, kama ambavyo hapa wanaCCM wenzangu watakapoumia mioyo yao na kuanza kunitukana.

Ni hivi, nilikuwa mbishi sana na siku zote nimekuwa nikiamini kuwa CCM tutashinda katika uchaguzi mkuu, nimefatilia kwa umakini mkubwa mikutano ya CCM pamoja na mikutano ya UKAWA, kiukweli kabisa CCM TUMEKWISHA.

Lowassa tulikukosea, tulikusingizia mengi na tunafahamu kuwa kuna watu walikuhujumu. Tunakuomba utusamehe urudi nyumbani (CCM). Ni kweli tumefanya makosa lakini adhabu unayotupa hatustahili Lowassa.

Ndugu wana CCM wenzangu popote pale mlipo mjitokeze tumuombe msamaha mheshimiwa Lowassa, mpaka muda huu Lowassa amekwisha chukua nchi, October 25 asubuhi anakabidhiwa na JK.

By MCHUNGUZI HURU/JF

High School Madness > Rotten Girls Caught On Camera Doing Stuff Well Preserved For Huddah Monroe And Vera Sidika

0
0
The last time I checked, secondary education was still not free. Parents cough substantial amounts to send their sons and daughters to high schools but the things some students do…


Just the other day high school students were busted smashing each other, smoking bhang and doing other unimaginable stuff in a bus.

Even before that disturbing memory could fade, another video has popped up showing high school girls reenacting scenes best seen at night clubs.

The girls are seen hauling up their skirts to expose their not so pleasing panties before they shook their bones infested butts.

Surprisingly there were also dudes present who were daggering them!

Watch the clip below:

Ray C....Kuna Watu Wanataka Kuniua

0
0
Yamekuwa hayo tena! Staa wa muziki Bongo, Rehema Chalamila `Ray C’ yupo kwenye hofu nzito ya kutaka kuuawa kwa kile alichodai ni chuki za binadamu wasiomtakia mema.

Wikiendi iliyopita Ray C alitupia ujumbe mzito mtandaoni uliosomeka: “Nacheka lakini sina furaha ila najua kabisa mpango wao kwangu ni kuniua kabisa nipotee! Sitakufa bali nitaishi! Nashukuru kuwa ninajua haki yangu!

“Ndiyo chanzo chote cha chuki na fitina! Ila kumbukeni na ninyi mna watoto pia muombeni Mungu awaepushie hili balaa ndani ya familia zenu ila kumbukeni tu kuwa malipo ni hapahapa duniani tena siku wala si nyingi.”

Ilielezwa kwamba, Ray C alitoa ujumbe huyo akiwalalamikia watu ambao wamekuwa wakimnyima dozi ya Methadone ya kuondoa sumu ya madawa ya kulevya mwilini.Akichati na gazeti hili, Ray C alisema hiyo yote ni mtihani tu kwa binadamu. Source:GPL

Dk Kigwangala Apata Wakati Mgumu Kuitetea CCM Katika Mdahalo

0
0
Mwakilishi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika mdahalo wa MkikiMkiki unaohusu Uchaguzi Mkuu uliofanyika jijini Dar es Salaam, Dk Hamis Kigwangala jana alikuwa na wakati mgumu kutetea sera za chama hicho tawala katika sekta za elimu na afya.

Dk Kigwangala ambaye pia ni mgombea ubunge jimbo la Nzega Mjini kupitia CCM alitetea serikali ya chama chake na jinsi kinavyoshughulikia sekta hizo katika mdahalo huo uliorushwa moja kwa moja na kituo cha luninga cha Star Tv.

Mdahalo huo pia uliwashirikisha wawakilishi wengine na vyama vyao kwenye mabano ni Samson Mwigamba, (ACT Wazalendo), Rajab Hoza (UPDP),  Jacob Samwel (ADC) na Nderakindo Kessy (NCCR Mageuzi).

Dk Kigwangala alianza kupata wakati mgumu baada ya kuzungumzia mkakati wa CCM kuondoa tatizo la msongamano wa wagonjwa katika hospitali za serikali ambapo ilielezwa kuwa hali ilivyo sasa, kitanda kimoja kinalaza wagonjwa watatu huku kina mama wajawazito wakilala sakafuni.

Dk Kigwangala alianza kwa kupuuza madai hayo akisema kuwa ni kauli za kisiasa, hivyo kuwataka wananchi wazungumze mambo yenye uhalisia.

“Mimi nimekuwa daktari katika hospitali ya Muhimbili na baadaye Mwananyamala, sikumbuki ni mara ngapi nimewahi kuona wagonjwa watatu wakilala kitanda kimoja. Hizo ni siasa tu siyo tatizo kubwa,” alisema.

Hata hivyo, alifafanua kuwa serikali ya ijayo chini ya Dk John Pombe Magufuli itakuja na utaratibu wa kutoa matibabu bure kupitia mifuko ya bima ya afya.

Kauli hiyo ilipingwa na wawakilishi wengine katika mdahalo huo ambao kwa nyakati tofauti walisema  kauli ya Dk Kigwangala inawakilisha mtazamo wa chama dola ambacho hakijali wananchi wake.

“Mimi sijawahi tu kuona wagongwa watatu wakilala kitanda kimoja, nimewahi pia kuona wagonjwa wakilala chini. Mama yangu alipokuwa akijifungua mtoto wa sita alijifungulia kichakani,” alisema Mwigamba ambaye alieleza kuwa ACT-Wazalendo itakuja na sera ya kuongeza bajeti ya afya kukabiliana na hali hiyo.

Kwa upande wake, Kessy alimshanga Dk Kigwangala akieleza kuwa hii ni dalili ya chama hicho kutowajali wanananchi.

Hoja nyingine iliyompa wakati mgumu Dk Kigwangala ni swali lililotaka aeleze kama kuna uhalali wa walimu kuwachapa wanafunzi kwa sababu ya wazazi wao kushindwa kutoa michango na kama ni halali kwa baadhi ya walimu kutoa mafunzo ya ziada.

Akijibu swali hilo, Dk Kigwangala alitaka jamii kutowadharau walimu akisema kuwa wanafanya kazi nzuri na ndiyo maana wameongeza ufaulu wa wanafunzi.

“Napenda tuwaheshimu na kuwatia moyo walimu badala ya kuwakatisha tamaa. Siyo vibaya walimu kuwa wajasiriamali katika maeneo ya kazi,” alisema Kigwangala.

Wakati daktari huyo wa magonjwa ya binadamu akieleza kuwa kila Mtanzania ana haki sawa ya kutibiwa nje ya nchi, wawakilishi wengine walidai fursa hiyo inatolewa kwa viongozi wa serikali ya CCM pekee.

“Hizi ni chuki za kisiasa ambazo watu wanaeneza kuwa ni viongozi pekee ndio wanaotibiwa nje. Ukweli ni kwamba, ili mtu akatibiwe nje, lazima madaktari watatu wathibitishe na hili linafanyika kwa Watanzania wote,”alisema Dk Kigwangala.

Diamond Platnumz na Zari Boss Lady Kisa Mtoto wao Tiffah

0
0
MVUTANO! Ndivyo unavyoweza kusema baada mastaa wapendanao, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ na Zarinah Hassan ‘Zari The Boss Lady’ kujikuta wakipishana kauli kutokana na mvutano wa kibiashara unaohusu Sherehe ya Arobaini ya mtoto wao mchanga, Latiffah Nasibu ‘Tiffah’ ambaye amedhaminiwa Sh. Mil. 40 na makampuni mbalimbali yanayojishughulisha na bidhaa za watoto, Ijumaa Wikienda lina ‘full’ stori.


TUJIUNGE NA CHANZO
Kwa mujibu wa chanzo, mvutano wa wawili hao umeanzia katika suala la kujadili eneo la kufanyia sherehe hiyo inayotarajiwa kufanyika Septemba 20, mwaka huu ambapo Diamond anataka sherehe ifanyikie katika ukumbi mkubwa kama yalivyopendekeza makampuni hayo yanayogombea ubalozi na kudhamini tukio hilo lakini Zari anataka ifanyike nyumbani.
Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’.

“Diamond amefuata biashara zaidi. Makampuni yanayodhamini shughuli hiyo yamemwambia ili azma yao ya kutangaza bidhaa zao itimie, inabidi wafanyie kwenye ukumbi mkubwa ili watu wengi waweze kuhudhuria katika tukio hilo la kihistoria na wao waweze kutangaza bidhaa zao.


ZARI ASIMAMIA MILA ZA KWAO
“Zari ametaka shughuli hiyo ifanyikie nyumbani kwani mila za kwao Uganda zinataka shughuli hiyo ya kumtoa mtoto ifanyikie nyumbani na si katika ukumbi. Sasa Diamond alisukumwa na sababu za kibiashara na kujaribu kumshawishi mama la mama (Zari) naye akubali kupindisha mila za kwao ndipo walipotofautiana,” kilivujisha ubuyu chanzo chetu.


DIAMOND ADATA
Chanzo hicho kilizidi kujipambanua kuwa, kufuatia kupishana huko, Diamond alichanganyikiwa maana tayari makampuni yameshaanguka saini na yanahitaji shughuli hiyo ifanyike kwenye ukumbi ili malengo yao yatimie waweze kuwafikia watu wengi.

“Diamond amechanganyikiwa, anakosa jibu la moja kwa moja kwa makampuni japo anaweza kuzungumza nao wakamuelewa lakini kama akifanyia kwenye ukumbi atawafurahisha zaidi wadhamini,” kilisema chanzo hicho.


MAJIRANI WAMSHAURI
Ndugu wa karibu na Diamond ambaye hakupenda jina lake lichorwe gazetini alipenyeza habari kuwa, kuna majirani walishauri kama ikiwezekana shughuli hiyo waifanyie nyumbani siku moja kabla ya Septemba 20 ili ikifika Septemba 20, watafute ukumbi maalum kwa ajili ya sherehe hiyo.

“Yeah! Kuna majirani hapa wameshauri tufanye sherehe hii hapa nyumbani kabla ya tarehe 20 ila siku hiyo kuwe na ulinzi maalum watu wasiweze kuvujisha picha ambazo zinatakiwa kuonekana rasmi Septemba 20 kwa idhini ya wadhamini, Diamond na Zari wanaufanyia kazi pia ushauri huo,” alisema ndugu huyo wa Diamond.


DIAMOND ANASEMAJE?
Alipotafutwa Diamond kuhusiana na mvutano huo, alikiri kutokea na kuweka bayana kuwa suala hilo limemchanganya sana.

“Daah hili suala limenichanganya sana. Kuna watu wanashauri tufanye ukumbini, wengine wanakataa, wengine wanataka tufanye nyumbani na ukumbini.

“Kuhusu ukumbini dini inakataa, sherehe hii inapaswa kufanyikia nyumbani nitajua cha kufanya siku zikikaribia nitakujuza utaratibu kamili,” alisema.

Source:Global Publishers


AY Akutana na Mdogo Wake Kwa Mara Kwanza Baada ya Miaka 16

0
0
Rapper Ambwene Yessayah aka AY amekutana na mdogo wake wa kiume kwa mara ya kwanza baada ya miaka 16.AY ameiambia 255 ya XXL kupitia Clouds FM kuwa kuonana na mdogo wake huyo kunaenda sambamba na siku ambayo baba yake mzee Yessayah anatimiza miaka 12 toka afariki dunia.
“Tulikuwa hatujawahi kuwasiliana na wala kuongea kwenye simu na vitu vilikuwa complicated kidogo,” amesema. Ni mdogo wangu na leo ilikuwa siku special kuonana naye na pia leo ni siku ya kumbukumbu ya Mzee Yessayah. Mimi mwenyewe binafsi nimekuwa na furaha kuonana na mdogo wangu wa kiume.”

Nay wa Mitego na Diamond Wayapeleka Mabishano yao ya Muziki Kwenye Siasa, Soma Vijembe Walivyotupiana

0
0
Kampeni za uchaguzi zimewatengenisha maswahiba kwenye muziki, Nay wa Mitego na Diamond Platnumz.

Wawili hao waliohit na wimbo wao ‘Muziki Gani’ wapo kwenye kampeni za pande mbili zenye nguvu kwenye uchaguzi wa mwaka huu, Ukawa na CCM.

Na sasa ubishani wao umehamia kwenye siasa.

Kupitia Instagram, Diamond amepost kipande cha video cha show yake ya Zanzibar kwenye kampeni za chama cha mapinduzi na kuandika: Bado wewe tu @naytrueboy kurudi nyumbani….kama nayaona vile yale maselfie yetu na nguo za kijaniblushlaughingsweat_smile #AboutYesterday.”

Nay amemjibu Diamond kwa kuandika:

Nimekataa siendi popote. Wanasema huu ndo muda wa Wasanii kupiga hela ni kweli, ila mi kwangu itakua tofauti kidogo. Mi ni moja kati ya Wasanii wachache wafanya biashara. Ila kwa kipindi iki cha uchaguzi nimeweka pembeni kidogo maswala ya biashara now ni #Harakati huwezi kumnunua mwanaharakati wa kweli coz ata pesa anajua kuitafuta nje ya #Harakati. Uchaguzi ukiisha we leta izo Deal sasa za mamilioni mia tutafanya, ila kwa sasa tunapigania Maslahi ya nchi na kile wanachotaka watanzania Wengi. Naamini #Mabadiliko2015. @diamondplatnumz hujui kusoma, ata picha huoni?! Watanzania wanataka #Mabadiliko2015.”

Mtuhumiwa Kinara wa Ugaidi wa Kupora Silaha Kwa Polisi Awatoroka Polisi na Kujirusha ghorofani

0
0
POLISI Kanda Maalumu ya Dar es Salaam imewakamata watuhumiwa 26 wanaojihusisha na vitendo vya ugaidi, huku Ally Ulatule anayetajwa kama kinara wa vikundi hivyo akijaribu kutoroka au kujiua kwa kujirusha kutoka ghorofa ya tatu wakati akihojiwa na polisi.

Aidha, Polisi Kanda hiyo kwa kushirikiana na vikosi maalumu tangu ianze operesheni ya kuwasaka watuhumiwa waliovamia vituo vya Polisi na kujihusisha na ugaidi, wamefanikiwa kuwakamata jumla ya watuhumiwa wanaojihusisha na vitendo hivyo 64 huku silaha 27 zilizoporwa katika vituo mbalimbali vya polisi zikipatikana.

Akizungumza na waandishi wa habari jana ofisini kwake, Kamanda wa Kanda hiyo, Kamishna Suleiman Kova alisema, katika operesheni hiyo ambayo inashirikisha mkoa wa Pwani na iliyo jirani walifanikiwa kuwakamata watuhumiwa hao pamoja na silaha mbili ambazo ziliporwa katika vituo vya Polisi vya Kimanzichana na Ikwiriri mkoani Pwani.

Alisema silaha ya kwanza ni SMG yenye namba TZPL 26686 ambayo iliporwa Juni 21, mwaka jana katika kituo cha Kimanzichana na nyingine yenye namba TZPL 26706 iliyotambuliwa kuporwa katika kituo cha Ikwiriri.

“Pamoja na silaha hizo pia zilipatikana risasi 23 za SMG na magazine mbili za bunduki hizo, katika kijiji cha Mandimkongo, wilaya ya Mkuranga,” alisema Kamishna Kova.

Akizungumzia kuhusu tukio la Ulatule, Kamishna Kova alisema, mtu huyo jana saa 4 asubuhi wakati akihojiwa katika Kituo Kikuu cha Polisi (Central) aliomba kwenda chooni na ndipo alipojirusha kutoka katika ghorofa ya tatu kwa lengo la kujiua au kutoroka.

Soma Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumanne ikiwemo ya Jakaya Kumtaja Mtuhumiwa wa Ufisadi wa Richmond

0
0




















Soma Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumanne ikiwemo ya Jakaya Kumtaja Mtuhumiwa wa Ufisadi wa Richmond

Kauli ya Sumaye Kuhusu Tuhuma za Kutishiwa kunyang’anywa Mashamba yake

0
0
Akizungumza kwenye uzinduzi wa kampeni za ubunge wa Jimbo la Ubungo jijini Dar es Salaam, Waziri Mkuu Mstaafu, Frederick Sumaye, alisema kwa sasa hakuna njia au mtu atakayeweza kuifufua CCM.

Sumaye alisema wamezunguka maeneo mengi ya nchi kila walipokuwa wakienda wamebaini Watanzania hivi sasa wanahitaji mabadiliko na hawana mpango wa kuongozwa tena na CCM.

Aidha Sumaye alipingana na wale wanaosema amejiunga Ukawa kwa uchu wa madaraka, na kusema kuwa uchu wake wa kujiunga Ukawa ni kutaka kuing’oa CCM.

Sikuja UKAWA kutafuta cheo kwa sababu nimeshakuwa waziri mkuu na hata hapa Ukawa hakuna nafasi ninayotaka kwa sababu nafasi ya urais yupo Lowassa na nafasi ya waziri mkuu siwezi kupata kwa sababu sijagombea ubunge ila ninachofanya ni kuhakikisha CCM inaondoka madarakani,

Sumaye alisema kwa kuingia kwake UKAWA, amejikuta akipata vitisho kutoka serikalini:.

Suala la kunitisha kuninyang’anya mashamba yangu ni kunikomaza zaidi kwa kuwa naamini suala hilo ni sawa na kumpiga chura teke.”

Tusker Fanyakweli Kiwanjani Yawakuna Wakazi wa Mbezi Beach na Kimara Wiki Hii

0
0
Mkazi wa Mbezi Beach jijini Dar es salaam, Mlai Abraham akipokea zawadi ya fulana toka kwa Msimamizi wa Mauzo ya Kampuni ya bia ya Serengeti kanda ya Mbezi beach Obedi Salema katika hafla ya kuipongeza baa ya Coast Pub ya Mbezi Beach jijini Dar es salaam ambayo iliibuka mshindi wa wiki kwenye promosheni inayoendelea ya Tusker Fanyakweli Kiwanjani.

Mpenzi wa bia ya Tusker na mkazi wa Mbezi Beach jijini Dar es salaam, Jane Jeva (katikati) akipokea zawadi yake ya mfuko wenye fulana toka kwa Msimamizi wa Mauzo ya Kampuni ya bia ya Serengeti kanda ya Mbezi beach Obedi Salema (Kushoto) katika hafla ya kuipongeza baa ya Coast Pub Tangi Bovu-Mbezi Beach jijini Dar es salaam mara baada ya baa hiyo kuibuka mshindi wa wiki kwenye kampeni ya Fanyakweli Kiwanjani inayoendeshwa na bia ya Tusker.

Mteja wa bia ya Tusker Bi. Elizabeth Ulomi (katikati) akizungumza na mshereheshaji wa kampeni ya Fanyakweli Kiwanjani Gadner Habash (kushoto) kabla ya kupokea zawadi yake ya mfuko na fulana wakati wa hafla ya kuipongeza baa ya Coast Pub iliyopo Tangi Bovu-Mbezi beach jijini Dar es salaam ambayo iliibuka mshindi wa wiki kwenye kampeni ya Fanyakweli Kiwanjani inayoendeshwa na bia ya Tusker. Akijiandaa kutoa zawadi hiyo (kulia) ni Msimamizi wa Mauzo ya Kampuni ya bia ya Serengeti kanda ya Mbezi beach Obedi Salema. Tofauti na jiji la Dar, kampeni hiyo pia inaendelea mikoa mbalimbali nchini kama Arusha, Moshi, Mwanza, Morogoro na Mbeya.

Mpenzi wa bia ya Tusker na mkazi wa Kimara-Korogwe Bw. Edward Ukawa akipokea zawadi yake ya fulana sambamba na bia ya bure toka kwa Msimamizi wa Mauzo ya Kampuni ya bia ya Serengeti kanda ya Ubungo Victor Mhindi katika hafla ya kuipongeza baa ya Miti Mitatu ya Kimara-Korogwe jijini Dar es salaam mara baada ya baa hiyo kuibuka mshindi wa wiki kwenye kampeni ya Fanyakweli Kiwanjani inayoendeshwa na bia ya Tusker. Edward aliimwagia sifa bia hiyo kuwa ni laini na humburudisha pindi anapoitumia.

Mkazi wa Kimara Steven Kiswanta (Katikati) akizungumza na mshereheshaji wa kampeni ya Fanyakweli Kiwanjani Gadner Habash (kushoto) kabla ya kukabidhiwa zawadi yake ya fulana na bia za bure katika hafla ya kuipongeza baa ya Miti Mitatu iliyopo Kimara-Korogwe jijini Dar es salaam ambayo iliibuka mshindi wa wiki kwenye kampeni ya Fanyakweli Kiwanjani inayoendeshwa na bia ya Tusker. (Kulia) ni Msimamizi wa Mauzo ya Kampuni ya bia ya Serengeti kanda ya Ubungo Victor Mhindi.

Bi. Margret Adeli akizungumza na Mshereheshaji wa promosheni ya Tusker Fanyakweli Kiwanjani Gadner Habash (kulia) kabla ya kukabidhiwa zawadi yake ya fulana, mfuko wa kufanyia manunuzi na bia za bure katika hafla ya kuipongeza baa ya Miti Mitatu iliyopo Kimara-Korogwe jijini Dar es salaam ambayo iliibuka mshindi wa wiki kwenye kampeni ya Fanyakweli Kiwanjani inayoendeshwa na bia ya Tusker. (Kushoto) ni balozi wa bia ya Tusker Veronica Mbilinyi.

Why Would A LADY do This in The Gym? A Must Watch VIDEO for men.

0
0

Some ladies have perfected the skill of tempting men but this bootylicious lady has decided to take things to another level.

One even wonders whether she had gone to the gym for a work-out or to s3duce men.
Just click play and see what she did.


Ukimya Wa Mke wa Magufuli Unatia Shaka....Kunani?

0
0
Jamani Mke wa Magufuli mbona haonekani kwenye Campaign kama ilivyokua kwa Mama Salma, Mama Anna Mkapa na Mama Regina Lowassa. Kuna nini hapa katikati.

John Mnyika amtetea vikali Dr.Slaa Adai Yaliyotokea ni Kama Samsoni kwa Delila.

0
0

Mnyika amemtetea vikali Dr.Slaa na kupingana na wale wanaomkejeli na kumuona hana mchango CHADEMA.

Mnyika anasema Dr.Slaa anao mchango wake na yaliyomkuta ni mambo kama yaliyowahi kumkuta Samsoni kwa Delila.

Naomba kuisha hapa.

Rais Kikwete Amtaja Mhusika wa Sakata la Richmond....Asema ni Yule Anayetembea na Tundu Lissu Kila Siku Kwenye Kampeni

0
0
Rais Jakaya Kikwete amesema anashangazwa na Mwanasheria wa Chadema, Tundu Lissu kumtaka amtaje mhusika wa Richmond wakati mwenye Richmond yupo na anatembea naye mikoani.

Kikwete aliyasema hayo jana wakati akiwaaga wananchi wa Kigoma katika Uwanja wa Lake Tanganyika na kumtaka Lissu amtaje mwenye Richmond.

“Endapo Tundu Lissu atashindwa kumtaja mwenye Richmond, nitatoka hadharani na kumtaja mwenyewe,” alisema Kikwete.

Kabla ya mkutano huo, Rais Kikwete alifungua jengo la Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii, (NSSF) ambalo limejengwa kwa Sh7 bilioni.

Akifungua jengo hilo, aliwaomba wawekezaji na mifuko ya kijamii kuiga mfano wa NSSF kwa kuwekeza katika sekta ya majengo kwa kuwa yanapendezesha mji.

Kadhalika, Rais Kikwete alizindua jengo la Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) pamoja na nyumba 36 za bei nafuu zilizopo katika eneo la Mlole, Kigoma Mjini.

Suala la Richmond imekuwa moja ya ajenda za CCM katika kampeni za urais hasa baada ya Waziri mkuu wa zamani Edward Lowassa aliyejiuzulu wadhifa huyo kwa kashfa hiyo kuhamia upinzani.

Kila sehemu ambako mgombea urais wa CCM anakwenda, suala hilo limekuwa likiibuliwa, huku Lowassa akisema yeye hakuhusika, bali alijiuzulu kuiokoa Serikali isianguke kwa kuwa ulikuwa uamuzi wa wakubwa.

Mgombea urais wa CCM, Dk John Magufuli amekuwa akienda mbali zaidi akisema akichaguliwa ataanzisha mahakama maalumu ya kushughulikia mafisadi wanaosababisha umaskini nchini.

Zitto Kabwe: CCM Imeoza.....Haiwezi Kubadilika Hata Akija MALAIKA Kuiongoza

0
0
KIONGOZI wa Chama cha ACT Wazalendo, Zitto Kabwe, amesema Chama Cha Mapinduzi (CCM) hata kipate malaika hakiwezi kubadilika, hivyo dawa pekee ni kukiondoa jumla madarakani.

Akizungumza juzi wakati wa mkutano wa kampeni uliofanyika katika kituo cha basi Tabata Segerea, Zitto alisema matatizo mengi ya nchi yamesababishwa na sera mbovu za CCM ambazo baadhi ya wagombea wake ndio waliokuwa wakizitunga, kuzitetea na kuzitekeleza.

Kuna ambao wamekuwa watawala tangu tupate uhuru na bado wanataka waendelee kutawala, ukiwauliza wanasema tupeni tena kipindi kingine.

Sisi tunataka wote waondoke, tunataka tuweke mwanzo mpya katika nchi hii ndio maana hata ilani yetu imejikita kutatua changamoto mbalimbali zinazotukabili,” alisema Kabwe.

Zitto aliyewasili viwanjani hapo saa 10:14 jioni na kuanza kuhutubia saa 11:13 jioni, alisema taifa linakabiliwa na changamoto kuu nne ambazo ni umaskini, huduma mbovu za jamii, kukosekana kwa umoja wa kitaifa na ufisadi.

Leo hii tumekua na uchumi ambao hauzalishi ajira na kusababisha vijana wengi wanaomaliza masomo yao kuhangaika kutafuta kazi. Ni kwanini uchumi ambao unakua kwa kasi hauzalishi ajira,?” alihoji Kabwe.

Alisema hivi sasa nchi imekuwa na matabaka kwenye huduma za jamii kama vile elimu na afya na kusababisha Taifa kuwa la masikini na matajiri.

Leo hii watoto wa masikini na matajiri hawakutani, wa matajiri wanasoma shule zao halikadhalika na wa masikini…matajiri wanafundishwa elimu bora wanaandaliwa kuja kuwatawala masikini.

“Rushwa kubwa ndio inalitafuna taifa hili, mwaka jana zilitengwa Sh bilioni 546 kwa ajili ya kununulia madawa muhimu lakini ni Sh bilioni 36 tu ndizo zimetolewa, kuna wajanja wachache wamezifanyia ufisadi zile fedha,” alisema.

Kiongozi huyo wa ACT, alisema wamejipanga vizuri na wamesimamisha wagombea ubunge 219 nchi nzima hivyo akawataka Watanzania kuwapima kulingana na uwezo wao kisha kufanya uamuzi.

Awali mgombea ubunge katika Jimbo la Segerea, Mohamed Mwikongi, alisema akifanikiwa kushinda kiti hicho ataanzisha mfuko wa maendeleo wa Segerea na kuwahamasisha wananchi wajiunge katika vikundi ili wapate mikopo.

Nitaangalia upya mfumo wa wazazi kuchangia gharama za elimu katika shule za umma na kuzipunguza ili ziendane na hali halisi ya utendaji,” alisema Mwikongi.

Naye mjumbe wa chama hicho, Terry Gbemundu, alisema Watanzania wengi wameaminishwa kuwa ni masikini lakini hakuna umasikini wowote nchini.

“Tunaaminishwa hivyo ili tuibiwe tuzidi kukandamizwa, akili zimedumazwa lakini sasa uamuzi mnao kwenye sanduku la kura.

Atakayechagua kijani (akimaanisha CCM) ambayo imetawala kwa miaka 54 bila mafanikio sijui itabidi tukapimwe akili,” alisema Gbemundu.
Viewing all 104414 articles
Browse latest View live




Latest Images