Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104776 articles
Browse latest View live

Aunty Ezekiel Afunguka Makubwa Kwanini Ameamua Kuondoka UKAWA na sasa Kuisupport CCM

$
0
0
"Nimeamua kuondoka Chadema na vuguvugu la Ukawa kwa sababu mbalimbali: moja ni ubovu wa kimfumo katika uongozi, uratibu na misimamo. Fujo: Wafuasi wengi Ukawa bado wana muhemko kwenye kufanya mambo. Naamini uongozi wa nchi unahitaji busara kuhimili kazi. Tumefeli hilo. Kwa siku 39 zilizobaki nitaongea na mamilioni ya mashabiki wangu kuhusu msimamo wangu. Naondoka Chadema, nitamuunga mkono Magufuli". Hayo ni baadhi ya maneno aliyoandika Aunt Ezekiel

Neno moja kwa Aunt Ezekiel.

She Claims to Have a Big Behind than Ageness Masogange And it’s Natural (PHOTO)

$
0
0
Irene
She Claims to Have a Big Behind than Ageness Masogange And it’s Natural (PHOTO)..Do you Agree?

Masogange


Gaidi wa Kisomali Auawa na Kuzikwa Kwa Siri Kwenye Msitu wa Mkuranga

$
0
0


MTU ambaye ametajwa kuwa ni gaidi mwenye asili ya Kisomali (jina lake halikupatikana) ambaye imeelezwa alijeruhiwa kwa risasi katika mapambano kati ya magaidi na 
askari wa Kituo cha Polisi Stakishari, Dar Julai 12, mwaka huu, amefariki dunia na kuzikwa kwa siri, Uwazi liko kazini.
Baada ya kifo hicho, inadaiwa magaidi wenzake waliuzika mwili wake kwenye kaburi hilo lililopo kwenye msitu wa Kijiji cha Mamndikongo, Mkuranga, Pwani bila wanakijiji kujua.
UWAZI LIMECHIMBA HIVI
Taarifa zilizopatikana toka vyanzo vyetu makini katika kijiji hicho zinadai kwamba, kaburi la gaidi huyo liligundulika Jumatatu iliyopita. Na hatua chache mbele zikapatikana bunduki mbili aina ya SMG sanjari na risasi kadhaa kufuatia msako mkali ulioendeshwa na wanakijiji kwa ushirikiano wa polisi.
Askari na wananchi eneo la tuikoMara baada ya taarifa hizo, Uwazi lilifunga safari hadi kijijini hapo kwa lengo la kuujua ukweli ambapo Mtendaji wa Kijiji cha Mamndikongo, Issa Said Mchalaganga alikuwa na haya ya kusema:
“Ni kweli kuna msako mkali unaoendeshwa na askari polisi, vyombo vya usalama kwa ujumla na wananchi wa kijiji hiki ambapo Jumatatu iliyopita tulifukua sehemu tuliyoitilia shaka na kukuta mwili wa mtu mwenye asili ya Kisomali.”
HALI YA MAITI
“Maiti tuliikuta imevaa t-shirt yenye alama ya pundamilia, jaketi lenye maandishi ya King Lion (mfalme simba), bukta, pensi, trak’suti ya kuteleza na raba na ilionesha ni mtu mwenye asili ya Somalia kutokana na nywele na sura. Pia alikuwa na madevu.
“Alikuwa pande la mtu, mwenye kifua kipana. Tulipomwangalia vizuri alionekana kuwa na urefu wa kama futi 5.8 na umri tulioukadiria kuwa ni kati ya miaka 45 hadi 50.”
KISA CHA MSAKO
“Tulianza msako mkali katika maeneo ya mashamba ya watuhumiwa hao ambao baadhi yao wamekamatwa na wengine kukimbia nyumba zao baada ya kugundua kuwa, wanasakwa na polisi. Hii ni kufuatia kurejea kwao kijijini hapa nyakati za usiku wa saa tatu kwa siku tatu kabla ya maiti hii kupatikana.
“Taarifa tulizozipata ni kuwa, siku hiyo walifika usiku na pikipiki zaidi ya sita na kuziegesha sehemu iliyokuwa makazi yao kwa lengo la kwenda kwenye maskani yao ya zamani. Lakini walipofika karibu na nyumba ya mtu anayeitwa Joseph Chacha, mbwa wa hapo alibweka wale magaidi wakampiga risasi na kufa. Waliposonga mbele walimuona mbuzi akipita, wakafikiri ni mbwa, naye wakampiga risasi, akafa.”


WAKUTA MAZINGIRA TATA
“Taarifa tulizozipata ni kwamba waliposonga mbele walikuta mazingira ya sehemu waliyokuwa wakiishi yamebadilika. Kulifyekwa hali ilyowafanya wapatwe na hofu na kuamua kuondoka.
“Baada ya taarifa hizo, ndipo sisi tuliwasiliana na polisi na kwenda kuangalia kilichowaleta. Sasa katika msako wa kutafuta tukaona hilo kaburi.”



BENDEJI YAZUA MASWALI
Mtendaji huyo alizidi kusimulia: “Pia tulifukua dawa na bendeji ambayo ilikuwa na masalia ya damu hali iliyoashiria kwamba, alikuwa akitibiwa majeraha ya risasi akashindwa kupata nafuu kwani. Sehemu za mwili wake hasa zile zilizoingia risasi ziliharibika sana.




Silaha zilizokutwa karibu na kaburi la gaidi huyoMAGAIDI WANA DAKTARI WAO
“Daktari alikuja akaufanyia uchunguzi mwili kisha akaruhusu uzikwe tena. Lakini pia kwa upande wao, inasemekana watu hao pia wana daktari wao ambaye alikuwa akiwatibu pale wanapojeruhiwa wakati wa mapambano, sasa na yeye ametoweka.”
KWA NINI MAGAIDI BADO WANARUDI KIJIJINI?
“Watu hao wanaonekena kutafuta namna ya kurudi hapa kijijini kwa sababu kuna vitu vyao, zikiwemo silaha walizoficha ardhini sehemu mbalimbali ila wanashindwa kuja moja kwa moja.”
WANAKIJIJI WASHINDA KWA HOFU
Naye Mkufunzi wa Mgambo Kata ya Bupu na Kamanda wa Kijiji cha Mamndikongo, MG 357062 Abdallah Twalib Mandale alisema kwa sasa wananchi wa kijiji hicho wana hofu kiasi kwamba wanashindwa kuendelea na shughuli zao ili kushiriki katika msako wa silaha za magaidi hao.
WANAKIKIJI WAPONGEZA
Hata hivyo, wanakijiji hao walimpongeza Kamishna wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Suleiman Kova na vyombo vyote vya ulinzi na usalama ambavyo vimekuwa vikiendesha oparesheni hiyo ambayo imeleta mafanikio makubwa pia wameiomba serikali kuwapatia vyakula na maji askari wanaojihusisha na zoezi hilo kwani wamekuwa wakifanya kazi porini kwa muda mrefu bila kula wala kunywa maji jambo ambalo ni hatari.

Breaking News: Mtangazaji wa Clouds FM DJ Fetty Atangaza Kuacha Kazi Clouds

$
0
0
September 15 2015 Show ya XXL inaandika Historia nyingine tofauti ambapo DJ Fetty ametangaza kuacha kazi ya Utangazaji na kuingiza nguvu yake zaidi kwenye masuala ya Biashara… wakati Fetty anatangaza hivyo, presenter mwingine pia Kened the Remedy ameungana na Timu ya XXL kwa mara ya kwanza.

Dada Zangu wa Kichaga Jisafisheni Kimapenzi Maana Sehemu Kubwa ya Jamii inawaogopa Kimapenzi

$
0
0
Ukipata mchumba hasa mmachame wanafamilia wanakuwa wagumu kubariki mahusiano yenu.Hii imetokana na baadhi ya jamii kutendwa baada ya kuoa wachaga.Lakini naamini kuna baadhi ya dada zangu wa kichaga ni wema kabisa na wanamtegemea Mungu na upendo wao unaweza kufuta mabaya yaliyojengeka ktk jamii zetu kwa vizazi vilivyopita.

Hapo awali wanaume wa kikurya walikuwa wanaogopwa na mabinti wengi sana kwa sababu ya kutoa kichapo lakini siku hizi baada ya jamii kuona baadhi ya wadada wameolewa na watu hao na wamepewa mapenzi ya dhati jamii imewakubali.Leo hii ukipata mchumba wa kikurya halafu ukampeleka nyumbani anakubalika.

Hivyo dada zangu jisafisheni kufuta mfumo dume uliojengeka ktk jamii pia mnaweza kutujuza tatizo liko wapi mpaka jamii inaogopa?

Kisa Pombe; Johari Azima, Akombwa Kila Kitu

$
0
0
Kisa pombe! Mwigizaji wa kitambo Bongo, Blandina Chagula ‘Johari’ anadaiwa kupiga mitungi hadi akazima kisha kukombwa mkoba uliokuwa na kila kitu zikiwemo fedha taslimu Sh. 285,000/= na simu ya ‘tachi’ ya bei mbaya.

Akizungumza na Ijumaa Wikienda, wikiendi iliyopita kwa njia ya simu akiwa mkoani Tabora ambako Johari na baadhi ya mastaa wengine wapo kwa kazi maalum, mmoja wa wasanii hao alitonya kuwa tukio hilo lilijiri Alhamisi usiku, wakati wakiwa wanagida pombe, jambo lililozua taharuki kwake na wenzake.

Mtonyaji huyo alifunguka kuwa, wakiwa wanaendelea kunywa, Johari alifika wakati akazima ambapo walikuja watu waliojiita mashabiki wake, wakawa wanamvizia hivyo alipozinduka akaenda maliwatoni na kuacha mkoba wake, aliporudi ndipo akagundua kuwa mkoba wake haukuwepo, hali iliyomfanya aangue kilio cha uchungu.

Baada ya kupata ‘ubuyu’ huo, mwandishi wetu alimtafuta msanii rafiki wa damu na Johari (jina tunalo) ambapo aliombwa kumpa simu Johari ili kuzungumza naye ndipo Johari akakiri kukumbwa na masaibu hayo.

“Ni kweli tulikuwa tumekaa mahali ndipo nikalizwa mkoba wangu uliokuwa na vitu vyangu vyote,” alisema Johari.Kisa pombe! Mwigizaji wa kitambo Bongo, Blandina Chagula ‘Johari’ anadaiwa kupiga mitungi hadi akazima kisha kukombwa mkoba uliokuwa na kila kitu zikiwemo fedha taslimu Sh. 285,000/= na simu ya ‘tachi’ ya bei mbaya.

Akizungumza na Ijumaa Wikienda, wikiendi iliyopita kwa njia ya simu akiwa mkoani Tabora ambako Johari na baadhi ya mastaa wengine wapo kwa kazi maalum, mmoja wa wasanii hao alitonya kuwa tukio hilo lilijiri Alhamisi usiku, wakati wakiwa wanagida pombe, jambo lililozua taharuki kwake na wenzake.

Mtonyaji huyo alifunguka kuwa, wakiwa wanaendelea kunywa, Johari alifika wakati akazima ambapo walikuja watu waliojiita mashabiki wake, wakawa wanamvizia hivyo alipozinduka akaenda maliwatoni na kuacha mkoba wake, aliporudi ndipo akagundua kuwa mkoba wake haukuwepo, hali iliyomfanya aangue kilio cha uchungu.

Baada ya kupata ‘ubuyu’ huo, mwandishi wetu alimtafuta msanii rafiki wa damu na Johari (jina tunalo) ambapo aliombwa kumpa simu Johari ili kuzungumza naye ndipo Johari akakiri kukumbwa na masaibu hayo.

“Ni kweli tulikuwa tumekaa mahali ndipo nikalizwa mkoba wangu uliokuwa na vitu vyangu vyote,” alisema Johari.

Chanzo:GPL

Aunti Ezekiel na Vincent Kigosi Kutoka UKAWA Wajiunga na Kampeni za CCM

$
0
0
Zikiwa zimebaki takribani siku 39 kuelekea siku ya Kupiga kura. Wasanii wawili wa tasnia ya Maigizo waliokuwa katika Kampeni za Mh Edward Lowassa wa CHADEMA ghafla wameamia kwenye Kampeni za Mh John P. Magufuli wa CCM.

Hii imethibitishwa na mmoja wa wasanii hao, yaani Anti Ezekiel kupitia kwenye ukurasa wake wa Twitter.      (Auntezeofficial)

Ni stori ya kisiasa ambayo ilianza kuchukua headlines kwenye mitandao mbalimbali kuhusu wasanii wawili wa Bongo Movies, Aunt Ezekiel na Vicent Kigosi aka Ray kuondoka UKAWA na kuhamia chama cha Mapinduzi.

Baada ya taarifa hizo kuchukua nafasi kubwa kwenye mitandao sasa ripota wa millardayo.com amezungumza na Steve Nyerere ambaye ni mwenyekiti wa kampeni ya Mama ongea na Mwanao…’Ndugu zetu wakina Vicent Kigosi na Aunt Ezekiel walitoroka wamerudi CCM kabla hawajatangaza lakini watatangaza wamerudi kwa kishindo kikubwa wanaamini bila hapo walipofika bila nguvu ya Mh Jakaya Mrisho Kikwete wasingiweza kufika‘ – Steve Nyerere

‘Kwa hiyo nataka kuwaambia watanzania kuwa hao watu wamerudi katika chama cha mapinduzi na wala msidanganywe pilika pilika za huku na kule hawa watu ni wanachama wa CCM hai walitoroka na sifa ya kutoroka ni kukosa nidhani kwa sisi wazazi ambao tuna watoto , mtoto akitoroka unatakiwa umpe adhabu ili siku nyingi afahamu njia ya sahihi na njia sahihi ni chama cha Mapinduzi ambacho kina Dkt John Pombe Magufuli na Mama Samia Suluhu’ – Steve Nyerere

Chanzo: JF by DemiGod

OFFER OFFER Kutoka Markson Beauty Products..Dawa Zisizo na Madhara za Kukufanya Uwe Mrembo zaidi na Muonekano wa Kupendeza

$
0
0
OFFER,OFFER,OFFER
         MARKSON BEAUTY PRODUCTS 
Katika kusherehekea miaka kumi na nne ya kampuni hii tumetoa punguzo kubwa la bei kama shukran kwa wateja wetu. Bidhaa zetu zimetengenezwa kwa mimea na matunda na hazina kemikali wala madhara.
    TUNAZO ZA:-
1.Kerefusha nywele na kuzuia kukatika ovyo @80,000/=
2.Kuongeza shepu (hips na makalio) @120,000/=
3.Kuondoa mvi milele zisirudi @100,000/=
4.Kupunguza unene na manyama uzembe
@100,000/=
5.Kuongeza uume pamoja na nguvu za kiume kwa (a)Gely ya kupaka @90,000/=(b)Vidonge maalum @100,000/= (c)Handsome up original (@)170,000/=
6.Kuongeza unene wa mwili mzima na uzito @90,000/=
7.Kupunguza tumbo  (kitambi) na nyama za pembeni kwa :- (a)Dawa ya kunywa au kupaka @80,000/=  (b)Mkanda wa kawaida  @80,000/=  (c)Micro-computer belt @300,000/= 
8.Kuwa mweupe na soft mwili mzima  @90,000/= 
9.Kubust maziwa na kuyasimamisha  @90,000/=
10.Kushepu miguu na kuwa minene @90,000/=
11.Kuondoa mipasuko mwilini (michirizi) @80,000/=
12.Kubana uke na kuongeza hamu ya tend la ndoa kwa mwanamke @80,000/=


      NB...Matokeo ni garantii na hakikisha unapata risiti yake ili kukuhakikishia kufanikiwa kwako. Popote ulipo utapata huduma zetu.
      Wasiliana nasi kwa no (+255) 0767-447444  na 0714-335378

10 things you didn’t know about DIAMOND’s lover ZARI, her real age may shock you.

$
0
0
Diamond’s lover, Zari Hassan, is arguably one of the most popular female celebrities in East Africa.

From the men she beds, the clothes she rocks and the vehicles she drives, Zari Hassan is news any day. Even though her life is there in the limelight for her fans to see, there are some little known facts that are not known to the public.

Take a look.

1.She used to be a musician

Majority of people who know Zari Hassan know her because of showbiz rather than her music. Zari used to sing and  was even nominated for a channel O award in 2007  in the best East African video category.

2. She Was Born in 1980 (35 Years ago)

Zari Hassan is 35 years of age. We have to give it to her for maintaining such a youthful years despite being in her mid thirties. Zari Hassan is currently in a relationship with Tanzanian music heartthrob Diamond Platinumz who is only 25 years of age. Talk of the classical cougar.


3. Zari Hassan Has Four  Children

Her real name is Zarinah Hassan and has 4 children namely, Pinto, Quincy  Did and newly born Queen Latifah.

4. She Is From Jinja

Zari Hassan is from the source of the Nile. She grew up in Jinja and attended Jinja Girls High school for her secondary education. Those who know her back in the days say she was ratchet as hell.

5. She is educated in London 

If you thought that it was only beauty without brains then you are wrong. Zari Hassan is London educated with a Diploma in Cosmetology. That explains a lot because she is always on point with her makeup.

6. She Is From 3 Different countries

Her heritage is confusing and you can’t really tell whether she is Ugandan , Burundian or Indian. According to her official website, her grandfather from her maternal side is Indian while the grandfather from paternal side Somalian while the grandmother is from Burundi. So what’s Zari Hassan’s nationality?

7. She is a Channel O Award Winner

She had been nominated for the best East African video  in 2006. In 2008, Zari Hassan won a channel O Video award for the best East African award. Yes, even though she is not singing anymore, Zari Hassan has been there and done that.

8. She has s3x Tape

It was released just the other week and has received mixed criticism. We had written an article on Ugandan celebrities that should release their s3x tape and it did not take a week before her video was leaked.

9. She Is Dry as a Rock

Social media was awash with negative comments when Zari’s intimate video was released. Everyone was saying Zari Hassan is as dry as a rock. Even Isaac Luggede a former lover confirmed the allegations.

10. She Doesn’t Give a Damn

Zari Hassan is a strong woman. She doesn’t give 2 sh#ts on what the media has to say about her. She has been involved in several controversies and is always calm when addressing them. There you go, that is Zari Hassan for you.

Ukitongoza Mwanamke Mrembo Usithubutu Kumwambia Unafanya Kazi Hizi, Atakukataa Mchana Kweupe!

$
0
0
1.Ualimu
2.Askari magereza
3.Fundi ujenzi
4.Kondakta/utingo
5.Mgambo


Ila ukisema unafanya kazi maeneo haya, utakubaliwa asubuhi na mapema
1.Migodini
2.Siasa
3.Ikulu
4.Bandarini
5.Viwanja vya ndege
6.Bank
7.Mahospitalini.
6.Ubalozini.

Baada ya kununua Prado, Nay wa Mitego asema ‘kinachofuata ni Range Rover’

$
0
0
Nay wa Mitego amesema akimaliza ujenzi wa nyumba yake mpya ya kifahari iliyopo Tabata jijini Dar es Salaam, atanunua gari aina ya Range Rover.

Nay ambaye amenunua gari mpya, Prado Land Cruiser hivi karibuni, ameiambia Bongo5 kuwa lengo lake ni kumiliki Range.

“Bado sijapata gari ninayoihitaji, mpango wangu ni Range nikimaliza nyumba yangu ya Tabata,” alisema Nay.

“Hii Prado ni mpya lakini ina kazi maalum. Hii ni kwaajili shows za mikoani. Nimenunua milioni 60, ni mpya kabisa ndio maana unaona hata namba haina ila ikikamilika kila kitu itakuwa barabarani soon.”

NEC Yafungua Milango kwa Wasimamizi wa Nje Hawata Ruhusiwa Siku ya Kupiga na Kutangaza Matokeo ya Kura

$
0
0
TUME ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imesema waangalizi wa uchaguzi mkuu utakaofanyika 25 Oktoba, mwaka huu wataruhusiwa kushiriki katika uangalizi wa hatua zote za upigaji kura, kuhesabu na kutangaza matokeo ya uchaguzi katika vituo vya kupigia kura.

Waangalizi wa kimataifa 600 wanatarajiwa kusimamia zoezi la uchaguzi mkuu wa tano tangu kurudishwa mfumo wa vyama vingi nchini mwaka 1992 ambapo uchaguzi wa ulifanyika kwa mara ya kwanza mwaka 1995.

Katika uchaguzi wa mwaka huu, Watanzania wapatao milioni 23.7 ndani ya nchi na waliotimiza masharti ya kupiga kura, wanatarajiwa kuchagua viongozi ngazi za udiwani, ubunge na urais.
Uchaguzi huo unatarajiwa kuwa na ushindani mkubwa kutokana na kuungana kwa vyama vinne vya upinzania vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA).

Vyama hivyo ni Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), National League for Democracy (NLD), Chama cha Wananchi (CUF) na NCCR – Mageuzi.
Pia sababu nyingine inayotajwa katika kuchochea ushindani mkali ni mawaziri wakuu wastaafu wawili, Edward Lowassa na Frederick Sumaye kujiunga na upinzani wakitokea Chama Cha Mapinduzi (CCM) ambacho ndio chama tawala.

Akizungumza katika mahojiano maalum na MwanaHALISI Online, leo mchana, Kaimu Mkurugenzi wa Sheria NEC, Emmanuel Kawishe amesema “Kati ya watu watakao ruhusiwa kuingia ndani ya chumba cha kupigia kura ni waangalizi wa uchaguzi kutoka ndani na nje ya nchi.

“Watazamaji hawa watashiriki katika kila hatua za upigaji kura, kuhesabu na kutangaza matokeo katika vituo vya uchaguzi, ili mradi wawe na kibali kinachowatambulisha kutoka NEC,” amesema Kawishe.
Hata hivyo Jumanne wiki iliyopita, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe akizungumza na mabalozi wanaoziwakilisha nchi zao Tanzania aliwataka waangalizi hao kutotoa tamko lolote linalohusu kampeni au uchaguzi kabla ya NEC kufanya hivyo.

Kawishe amesema watu wengine watakaoruhusiwa kuingia ndani ya chumba cha kupigia kura ni msimamizi mkuu wa uchaguzi katika kituo na wasaidizi wake wawili kutoka NEC na mawakala wa vyama vya siasa ambapo kila chama kinachoshiriki katika uchaguzi kitawakilishwa na wakala mmoja.
“Pia nje ya kituo kutakuwepo na askari polisi. Askari hawa hawataruhusiwa kuingia ndani ya chumba cha kupigia kura. Watakaa nje kuangalia hali ya usalama. Na ataruhusiwa kuingia ndani ya chumba cha kupiga kura iwapo atatakiwa kufanya hivyo na msimamizi wa uchaguzi katika kituo na si vinginevyo,” amesema Kawishe.
Aidha, nje ya kituo kutakuwepo na karani mmoja kutoka NEC ambaye atakuwa na kazi ya kutoa maelekeo kwa wapiga kura ikiwemo ni hatua gani wafuate baada ya kufika katika kituo cha kupigia kura.

Tundu Lissu Afunguka: Richmond ni ya Rais Kikwete..Nataka Nimnyamazishe

$
0
0
Mwanasheria wa CHADEMA, Tundu Lissu akihutubia Leo Mkutano wa kumnadi Edward Lowassa mgombea Urais wa CHADEMA (UKAWA) amesema Richmond ni ya Rais Jakaya Kikwete.

Aidha, amesema richmond sio ya mtu anayeongozana nae kwenye kampeni.

Magazeti leo yalimkariri Rais Kikwete alipokuwa Kigoma akisema mhusika wa Richmond ni yule anayeongozana na Lissu kwenye Kampeni.

Katika video hiyo,Tundu Lissu anasikika akisema maneno yafuatayo;

"Ndugu zangu wa Morogoro, Richmond ni ya Kikwete.. Richmond ni ya Kikwete narudia.. Richmond sio ya huyu anayetembea na Lissu kwenye kampeni, Richmond ni ya Kikwete. Sasa nimesema nataka nimnyamazishe. Sasa nipeni masikio yenu...."

Reginald Mengi Ajitoa Rasmi Kwa Lowassa

$
0
0
Tangu mbio za Urais zianze kushika kasi mkurugenzi wa IPP Media ndugu Regnald Mengi alionekana wazi wazi kuiunga mkono timu ya UKAWA

Ghafla Mkurugenzi huyo ameamua kujitoa kwenye timu hiyo baada ya kuona anapoteza nguvu zake wakati ana uhakika wa 100% kuwa Magufuli ndiye Rais wa awamu ya tano. Mengi amesema haoni faida ya kupoteza muda wake kumuunga mkono mtu mwenye uhakika wa kushindwa. Mengi amekubali wazi kuwa ushindi wa kiti cha Urais 2015 ni wa Magufuli... "kama hawa jamaa watashinda nafasi ya Urais basi ni baada ya miaka 10 siyo hivi sasa, huu mwaka ushindi utakuwa wa Magufuli tu tutake tusitake"

Pigo kubwa kama hilo limeambatana na kuondoka kwa wasanii mbalimbali waliotimkia kambi ya Ndugu Magufuli akiwemo Aunt Ezekiel, Ray na Juma Nature. Mshirika wake mkuu Hussein Bashe nae amejiweka pembeni na kuutangazia umma kuwa "ili wananchi wawe salama ni lazima kiti cha urais kikabidhiwe kwenye mikono salama, kinyume chake wananchi hawatokuwa salama, na mikono salama ni ya ndugu Magufuli tu"

Mwaka wa kufa nyani miti yote huteleza, EDO keshaanza kufa na miti yake pia imeanza kuteleza taratibu

By Aisha Idd/Jamii Forums

Kati ya Magufuli na Lowassa, ni Nani atatufaa Kwa siasa za Nje?

$
0
0
“Msifanye mabadiliko kwa pupa kama watu wa Libya. Walimuondoa madarakani rais Saddam, hapana rais Gaddafi maana Saddam alikuwa rais wa Kuwait!!”.

Sikuamini masikio yangu kwamba haya ni maneno yaliyotoka kinywani mwa mgombea urais kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi (CCM), Dk John Pombe Magufuli.

Alikuwa akiongea na wananchi wa Tanga katika mkutano wa kampeni akiwahadharisha Watanzania wasivichague vyama vya upinzani, kwa lengo la kufanya mabadiliko kwa sababu kufanya hivyo ni kuchagua bora mabadiliko wakati mabadiliko bora yatapatikana.

Nia yangu siyo kumfedhehesha mgombea huyu anayesifika kwa uadilifu na uchapakazi, lakini hivi kuna asiyejua kuwa Saddam Hussein hakuwa rais wa Kuwait bali Iraq? Kila mtu anajua hivyo, nashangaa tu kwamba mgombea wangu wa urais ama kweli hajui hili au hayuko makini katika masuala ya kimataifa.

Ninachokusudia ni kujaribu kuwahadharisha Watanzania kwamba zama hizi rais wa nchi haongozi ndani ya mipaka ya nchi hiyo pekee, bali anakuwa kiungo muhimu kati ya nchi yake na jamii ya kimataifa katika ulimwengu huu ambao sasa ni kama kijiji.

Moja ya mafanikio ya rais wa nchi yeyote ile duniani ni jinsi gani anazicheza karata zake kwenye medani ya kimataifa. Siasa za kimataifa siku hizi ni mchezo hatari, kiasi kwamba kama rais hazijui vizuri siasa za kimataifa kuna hatari ya kushindwa kutekeleza ilani na sera za chama chake awapo madarakani, kwa sababu ya misuguano na wale waitwao washirika wa maendeleo ambao ni nchi zilizoendelea.

Ukubwa wa hatari hii unazidi pale nchi yetu inapoingia katika uchumi wa mafuta na gesi asilia. Rasilimali mbili hizi zimeyaingiza mataifa yenye rasilimali hizo katika machafuko.

Kwa mujibu wa andiko, Oil and Diamonds as causes of civil war in sub-Saharan Africa, rasilimali ya mafuta na gesi zinaweza kuitia nchi katika machafuko. Lakini hilo hutegemea wingi wa rasilimali hiyo, sera na mikataba ya nchi husika kwa mataifa na mashirika wahitaji wa rasilimali hiyo kwa lugha rahisi wawekezaji.

Jingine ni uwezo wa kidiplomasia ya uchumi wa viongozi wa nchi yenye rasilimali kumudu hila, njama, migandamizo na vishawishi vya wawekezaji hao. Kwa maneno mengine, uwezo wa rais aliye madarakani katika kuongoza diplomasia na mataifa ya nje.

Mbali na rasilimali, uwezo wa rais katika diplomasia na mataifa ya nje ni mtaji muhimu katika kuvutia wawekezaji katika kile kijulikanacho kama mitaji ya moja kwa moja kutoka nje au ‘foreign direct investment (FDI)’, misaada mbalimbali kwa nchi na hata haiba ya nchi kimataifa.

Kwa kweli Rais wa Tanzania anayemaliza muda wake ameipaisha Tanzania katika medani ya kimataifa, ingawa mwishoni mwa utawala wake mataifa na wadau wa maendeleo walifikia kuzuia misaada yao kupinga kashfa mbalimbali, ikiwamo kashfa ya Tegeta Escrow iliyolitikisa Taifa.

Hatari iliyoko mkipata rais asiyejua changamoto zinazolikabili taifa katika siasa za kimataifa ni kuchukua maamuzi yanayoweza kuliingiza taifa katika hasara na hata katika migogoro ya ndani na nje.

John Perkins anaandika katika kitabu chake “The confession of an economic hitman” kwamba mashirika ya kimataifa hususan yale ya uchimbaji mafuta na gesi, huyaingiza mataifa katika lindi la madeni, umaskini na vita vya wenyewe kwa wenyewe.

Hapo ndipo unapoonekana umuhimu wa kuwapima wagombea wetu ili kuona ni nani anafaa kwa siasa za nje?
  
 Mwandishi wa makala katika gazeti mmoja litokalo kila siku hapa nchini, alimsifia Dk John Magufuli kwamba katika kipindi chake cha miaka 20 ya utumishi serikalini, amesafiri kwenda nje ya nchi mara nne !

Hii inaonyesha kuwa si mtu mbadhirifu kwani uchache wa safari za nje unathibitisha kuwa yeye siyo mwenye kufanya matumizi ya ovyo ovyo. Japo hili ni jambo zuri kwa upande mmoja, kwa upande wa kukuza uelewa wake katika medani za kimataifa, si jambo la kujivunia. Ziara za nje hupanua uelewa wa mtu katika diplomasia ya kimataifa.

Magufuli Vs Lowassa

Kupitia hotuba zake za kampeni mtu anaweza kupata wasiwasi juu ya uwezo wa Dk Magufuli kuhusu siasa za nje. Ule mfano wake maarufu wa kulinganisha mabadiliko ya Tanzania na yale yaliyotokea Libya umetoa picha hasi kwamba hajui vyema siasa za kimataifa.

Ukichanganya na kauli yake “mimi sifanyagi (sifanyi) siasa na kwa bahati mbaya naweza kuwa si mwanasiasa mzuri,” unapata shaka kama kweli atamudu siasa za kimataifa zilizojaa ulaghai, hila na mizengwe dhidi ya nchi changa. Ili kuwa rais zama hizi, inabidi uzijue vizuri siyo siasa za ndani bali hata zile za kimataifa.

Hili la kutokujua au kujichanganya kuhusu Saddam alikuwa rais wa nchi gani linaweza kuonekana jambo dogo, lakini kwa watu makini haiwezekani kwa mtu msomi wa kiwango cha uzamili tena aliyekuwa katika uongozi wa nchi kama waziri kwa muda mrefu, awe hajui Saddam alikuwa rais wa nchi gani. Ni dalili kwamba kuna upungufu mkubwa kwenye uelewa wa mambo ya kimataifa kwa mgombea wetu huyu.

Lowassa kwa upande wake hatujamsikia akizungumzia lolote kuhusu masuala ya kimataifa, licha ya kuwa amewahi kuwa Waziri Mkuu na waziri wa kawaida kwa miaka mingi.

Nafasi hiyo bila shaka ilimpa uzoefu fulani katika medani ya kimataifa, kwa kuwa Waziri Mkuu ni msaidizi wa karibu wa rais kwenye mambo yote likiwamo la ushirikiano wa kimataifa. Aidha, Lowassa amesafiri mara nyingi nje ya nchi jambo linalompa fursa ya uelewa mpana kuhusu masuala ya nchi za nje.

Katika kampeni zake, tumemsikia akisema “sitosubiri misaada kutoka nje”. Hii ni kauli nzito kwa kuwa nchi hizi changa kama Tanzania haziwezi kabisa kuepuka misaada kutoka nje, ingawa pia hazitakiwi kuwa tegemezi kwani zina rasilimali nyingi.

Kuwa kwake Mkurugenzi wa Kituo cha Mikutano cha Kimataifa Arusha (AICC), bila shaka kulimwezesha kukutana na wanadiplomasia wengi wa kimataifa wakiwamo mabalozi, mawaziri wakuu, makamu wa marais na hata marais waliowahi kuhudhuria mikutano ya kimataifa katika ukumbi huo.

Tukumbuke kwamba, mchakato wa Ushirikiano wa Jumuiya ya nchi za Afrika Mashariki, utakuwa unaingia katika kipindi nyeti cha ushuru wa pamoja wa forodha na mamabo mengine ambapo masilahi ya nchi yetu itabidi yalindwe ipasavyo.

Ni wazi marais wa nchi jirani wanasubiri kwa hamu ni nani ataibuka Rais wa Tanzania, nchi ambayo ‘kistratejia’ imekaa vizuri kuliko nchi zote za Afrika Mashariki, lakini isiyokuwa na mikakati mizuri ya kufaidika na uwepo wake kijiografia.

Mataifa na mashirika ya nje kama vile Umoja wa Mataifa, Umoja wa Ulaya na mengineyo yatakuwa yanafuatilia kwa karibu uchaguzi wa Tanzania. Kwa hiyo wakati tukishangilia kauli za wagombea kuhusu jinsi watakavyoendesha siasa za ndani ya nchi, tusisahau kuna siasa za kimataifa ambazo zinaweza kukwamisha hata mipango yetu ya maendeleo, iwapo rais atakayechaguliwa hatokuwa na uzoefu au uelewa wa kutosha. 
  
Mwandishi:Mpunta Wadinya; dinyampuntaz@yahoo.com

Ajali ya Basi Yaua Watu Watano.....Chanzo cha Ajali ni Dereva Kusinzia

$
0
0
Watu watano wamekufa na wengine 39 kujeruhiwa vibaya baada ya basi walilokuwa wakisafiria la kampuni ya Metro kuacha njia na kupinduka katika eneo la Manga, mpakani mwa mikoa ya Tanga na Pwani, chanzo kikidaiwa dereva alikuwa akisinzia.

Waliokufa katika ajali hiyo iliyotokea jana ni Joseph John (45) na Joseph Shayo (41), wakazi wa Moshi, mkoani Kilimanjaro na Zakaria Kintupa, mkazi wa Lutindi na mwanawe ambaye jina lake halikufahamika mara moja.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga, Zuberi Mwombeji, amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo na kwamba  miili ya marehemu na majeruhi wa ajali hiyo wamepelekwa katika Kituo cha Afya cha Mkata, wilaya ya Handeni, mkoani Tanga.

Kwa mujibu wa Kamanda Mwombeji, ajali hiyo  ilitokea saa 5.00 asubuhi wakati basi hilo likitokea Dar es Salaam kuelekea Rombo, mkoani Kilimanjaro.

Alisema basi hilo lilipinduka baada ya dereva kushindwa kumudu kona kali na hivyo kuacha njia na kuingia kwenye korongo.

Hata hivyo, baadhi ya abiria waliokuwa wakisafiri na basi hilo walidai ajali hiyo ilitokea kutokana na dereva kuendesha huku akisinzia.

Kamanda Mwombeji alisema dereva wa basi hilo ambaye jina lake halikufahamika alitoroka baada ya ajali hiyo kutokea na kwamba polisi wanaendelea kumsaka, huku mmiliki wa basi akihojiwa na kwamba uchunguzi wa ajali hiyo ili kujua chanzo chake halisi unaendelea.

Yaliyojiri Mkutano wa CCM na Waandishi wa Habari, Ofisi ndogo ya CCM, Lumumba Dar 16 Sept 2015

$
0
0

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Tumewaita kuwaomba mtusaidie kufikisha ujumbe ufuatao kwa Watanzania:

MWENENDO WA KAMPENI ZA CCM

Hadi jana, tarehe 16 September 2015, Mgombea Urais wa CCM, Dr. John Pombe Magufuli, alikuwa amekwishafanya kampeni katika mikoa 12 na Majimbo 94. Amekwishafanya mikutano mikubwa ya hadhara 76 na mikutano ya barabarani 381. Amekwishatembea, kwa gari, jumla ya kilomita 13,720. Kwa ujumla amekwishakutana, moja kwa moja, na asilimia zaidi ya 30 ya wapiga kura. Kwa kuwa baadhi ya mikutano yetu inatangazwa moja kwa moja na redio za kijamii na luninga, wapiga kura waliopata nafasi ya kumsikia wanakadiriwa kufikia asilimia 70.

Tunafarijika na idadi kubwa ya watu wanaokuja kwenye mikutano ya kampeni zetu. Tunafarijika pia kwamba karibu Watanzania wote wanaopata fursa ya kumuona na kumsikia wamemuelewa na wamepata matumaini ya Tanzania Mpya kupitia kwake. Utafiti wetu wa ndani, tulioufanya kwa kipindi cha siku kumi zilizopita katika majimbo 246 kati ya majimbo 269, unaonyesha kwamba Dr. Magufuli atapata ushindi wa asilimia 69.3 Tunaamini kwamba asilimia hizi zitaongezek kadri Watanzania wengi zaidi wanavyopata fursa ya kumsikiliza Dr. Magufuli na kusikiliza Ilani na sera za CCM.


Kwa upande wa kampeni zetu za Ubunge, zaidi ya robo tatu ya wagombea Ubunge wa CCM wamekwishazindua kampeni zao na wanaendelea vizuri. Sekretarieti ya Kampeni ya CCM inaanda program maalum ya kampeni katika majimbo yenye changamoto mahsusi.

Napenda kuchukua fursa hii kuwajulisha wana-CCM kwamba viongozi na makada wengine wa CCM, waliopo madarakani na wastaafu watapita tena, jimbo kwa jimbo, nchi nzima katika siku 30 za mwisho katika jitihada za kuongeza ushindi wa CCM na Dr. Magufuli.

MIDAHALO YA WAGOMBEA

Wiki tatu zilizopita, CCM, na kwa hakika vyama vingine pia, ilipokea mwaliko wa Mgombea Urais wa CCM, Dr. John Pombe Magufuli, kushiriki kwenye mdahalo wa wagombea Urais uliondaliwa na Baraza la Habari Tanzania (Media Council of Tanzania) kwa kushirikiana na taasisi nyingine kadhaa, ikiwemo Twaweza. Dr. Magufuli amekubali kushiriki katika mdahalo huo. Kwa msingi huo, kauli ya UKAWA iliyotolewa jana na Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi, Ndugu James Mbatia, kwamba UKAWA inaomba mdahalo ni njia ya kuwahadaa Watanzania tu kwa kuwa mwaliko wa mdahalo ulikwishatolewa mapema kwa vyama vyote na wanaotakiwa kushiriki ni wagombea Urais wa vyama.

CCM inafurahishwa na utamaduni wa midahalo ambao unaanza kujitokeza katika chaguzi zetu. Na inaamini kwamba midahalo ya Wagombea Urais ni
sehemu muhimu ya kuwashirikisha wapiga kura katika mchakato wa uchaguzi na kuwasaidia waamue nani wamchague kwa misingi ya hoja na sera na sio kwa ushabiki, kwa mihemko, na kwa propaganda. Mdahalo unatoa fursa ya wagombea kuulizwa maswali ya moja kwa moja na kutoa ufafanuzi wa kina kuhusu sera na ahadi zao, fursa ambayo hawaipati kwenye mikutano ya hadhara kampeni.

Hatukubaliani na kauli ya UKAWA kwamba mdahalo usiwe baina ya wagombea bali uwe baina ya Wenyeviti wa Vyama. Tunaamini hoja hii ni kichekesho. Haijawahi kutokea popote duniani kwenye utamaduni wa midahalo, kwamba wagombea wasishiriki bali watu wengine ndio wafanye midahalo kwa niaba yao. Tunaamini mdahalo huu unapaswa kuwa baina ya wagombea. Wao ndio wanaoomba dhamana. Wao ndio wanaopaswa kujibu maswali na kufafanua kuhusu ahadi zao.

CCM inaamini kwamba ili mdahalo huu uwe na tija, wagombea Urais wote, hasa wa vyama vikuu, wawepo na washiriki. Mdahalo hautakuwa na maana
kama mgombea mmojawapo wa vyama vikuu atatengeneza kisingizio ili asishiriki.

UCHAGUZI WA AMANI

CCM inasikitishwa na kauli zinatolewa na baadhi ya viongozi wa UKAWA zenye kuashiria fujo na vurugu. Kauli kwamba kura zitaibiwa hazina msingi wowote. Kauli hizi zinaashiria maandalizi ya kushindwa na maandalizi ya kufanya vurugu baada ya matokeo ya kushindwa.

Utaratibu wa uchaguzi wetu unajulikana na umekubalika na vyama vyote. Kura zinapigwa kituoni na kuhesabiwa kituoni mbele ya mawakala wa vyama vyote, wasimamizi wa uchaguzi na waangalizi wa uchaguzi wa ndani na nje ya nchi. Baada ya kura kuhesabiwa, matokeo yanajazwa katika fomu ambayo kila wakala anasaini na kupewa nakala. Nakala ya matokeo hayo pia inabandikwa nje ya kituo cha kupiga kura. Kila Chama, na kila Mtanzania, kina fursa ya kujumlisha matokeo yake kwenye kila kituo na kupata jumla kuu. Matokeo ya nchi nzima yanajumlishwa mahala pamoja huku kukiwa na waangalizi wa uchaguzi wa ndani na nje ya nchi, pamoja na wawakilishi wa vyama vyote na wao wakiwa na fomu zao za kila kituo nchi nzima.

Tunapenda kuwasihi Watanzania wasikubali vishawishi vya kufanya vurugu. Mara nyingi, viongozi wanaohamasisha vurugu wanakuwa na ulinzi au walinzi au uwezo wa kukimbilia pahala penye utulivu zaidi huku wakiwaacha wafuasi wao katika wakihangaika.

UCHAGUZI NA UMOJA WA KITAIFA

CCM pia inapenda kusisitiza imani yake kwamba uchaguzi haupaswi kutugawa kama taifa. Uchaguzi ni tukio la kupita. Kuna maisha baada ya uchaguzi. Kuna taifa baada ya uchaguzi. Lazima taifa liendelee kubaki moja, tuendelee kubaki wamoja. Tusitoe kauli za kupitiliza zenye mrengo wa kujenga chuki katika jamii na kuhatarisha umoja na amani ya nchi yetu.

Kama Chama kilichoasisi umoja wa taifa letu, tunaendelea kuasa kwamba wanasiasa wasijinadi kwa misingi ya udini, ukabila wala ukanda. CCM haina mpango kuendeleza mjadala wa kauli ya Mgombea wa UKAWA Ndugu Edward Lowassa aliyoitoa kanisani Tabora tarehe 6 September 2015
kwamba nchi ilishapata viongozi Wakatoliki na kwamba sasa ni zamu ya Walutheri kuchukua nafasi hiyo. Tunaamini mjadala huo hauna tija. Tunaamini kwamba Watanzania wengi, wa dini na madhehebu yote, hawaamini katika siasa za namna hii. Tuliamini kwamba UKAWA ingetumia fursa ya mkutano wao na waandishi wa habari jana kuomba radhi kwa Watanzania. Kwakuwa hawakufanya hivyo, tunapendekeza mjadala wa jambo hili ufungwe. Itoshe tu kwamba Ndugu Lowassa amesema hivyo, Tume ya Uchaguzi imemuonya, na yeye hajajitokeza kuomba radhi wala kufafanua. Watanzania wamemjua ni kiongozi wa aina gani na watatoa hukumu yao tarehe 25 Oktoba 2015.

Imetolewa na:-

January Y. Makamba,

MJUMBE WA HALMASHAURI KUU YA TAIFA YA CCM
MJUMBE WA KAMATI YA KAMPENI YA CCM
16/9/2015

Alinipa Penzi ili Nimuingize Kazini, Imebuma, Anatishia Kuja Kazini Kuharibu na Kumwambia Wife

$
0
0
Nawasalim wote katika bwana

Wapendwa, yupo msichana mmoja, alimaliza chuo mwaka jana, anakaa mtaa wa nyuma yetu, anatufaham sana mm na mke wangu, lakini zaidi ya yote tunaabudu pamoja, yaani kanisa moja, nilipoanza kuabudu hapo, yy tayari alikua mwenyeji Wa kanisa hilo na familia yake kwa muda sasa

Mara baada ya Mimi kujiunga na kanisa hilo, huyo binti ndie alinipokea, nilijiunga peke yangu, wife yeye aliendelea na kanisa lake la zamani, amehamia kwetu recently

Basi, tukawa tumebadilishana namba zetu na binti, tukaulizana na kuongea mambo mengi ya maisha, nilipomtajia ninapofanya kazi akaomba nimtafutie kazi kwenye shirika letu, nikamwambia nitajitahidi, baade akaniletea CV zake nikazipeleka kwa hr wetu na kumuomba anisaidie nafasi ikitokea, akakubali

Baadae binti akaja na laki mbili kutoka kwa wazazi wake, kwamba nimpelekee hr ya chai ili mambo yaweze kwenda HR akazipokea na kuniomba niwe mvumilivu.

Wakati tunaendelea kusubiri, huyu binti alizidisha sana ukaribu, tukawa wakati mwingine tunachat vitu vya ndani sana, Akawa ananiuliza kama najua hiki au kile ktk love making, Nikawa namjibu kwamba sijui, Basi akadai atanifundisha, ndipo nikashangaa atanifundishaje bila kufanya hilo jambo?
Isitoshe wote tumeokoka. 

Nikamwambia kwanza hatupaswi hata kujadili mambo hayo, Pia sikuwahi kutembea na mwanamke mwingine zaidi ya mke wangu baada ya kuoa, akasema ndio maana hujui vitu vingi, tutafundishana taratibu

Kwa kweli sielewi kilitokea nini kuja kuzinduka, bahati mbaya tukawa tumeshafahamiana Mara kadhaa hivi, ukichukulia kwamba nilikua na mgogoro flani na wife kwa kipindi kirefu, kwa ujumla tukawa tumeshafahamiana kama Mara 12 hivi tangu mwanzo Wa mwaka huu

Yule HR wetu kila siku ananipiga kalenda tangu mwezi wa 11 mwaka Jana inakimbilia mwaka sasa, binti ikafika pahala akaanza kusema nimemtapeli, tumekua na ugomvi mkubwa, na unaendelea kukua siku hadi siku, juzi kanitumia sms akidai kwamba eti alimsaliti mchumba wake na kunipa tunda mimi ili nichakarike apate hiyo kazi sasa nimemuingiza mkenge,

Cha kusikitisha zaidi, hili suala linakaribia kumfikia wife maana hapo mtaani kuna watu wamenifuata na kuniuliza.Nashangaa sana, maana hata hilo la kula tunda ni yeye ndio alinirubuni.

Kuhusu hela yake, anadai nimrudishie kwamba wazazi wanaulizia, wakati hela yenyewe alidai tumpe hr ya chai, sasa wadau hela ya chai huwa inarudishwa?Na mimi yule HR tunaheshimiana sana, ni bosi wangu, siwezi kumkoromea, wala kumuimba anirudishie hela yeye anadai nafasi ikipatikana atamuingiza, sasa binti anaona kama ni utapeli muda umekua mrefu

Yote tisa, kumi anadai atakuja kwa bosi wangu kueleza jambo hilo ili aniharibie, na atafanya liwezekanalo mke wangu ajue

Wapendwa msaada wenu please

Wolper Awatoa Hofu Mashabiki, Asisitiza Kubaki Kuwa Jacqueline Lowassa

$
0
0
Staa wa Bongo Movies, Jacqueline Wolper ambaye amejipambanua siasa kuwa anaunga mkono madadiliko kupitia UKAWA na kushiriki katika harakati za kumpigia kampeni Mh Edward Lowassa ambaye ni mgombea urasi kupitia UKAWA kwa tiketi ya CHADEMA, amewatoa hofu mashabiki wao kuwa hakuna bifu miongoni mwao kwani siasa zikiisha wataendelea na maisha yao kama kawaida tofauti na baadhi ya mashabiki wanavyodhani hasa baada ya wasanii hao wa bongo movies walivyotafautiana kimitazamo ya kisiasa kwakipindi hiki hadi kufia  kutoleana lugha kali miongoni mwao.

"Msijali Mashabiki siasa zikiisha maisha yetu yanaenda kama kawaida Maana sisi zetu kamera siyo viti vyekundu ila hapa pipozii tuu paka kieleweke"–Wolper aliandika kwenye mtandao wa instagram.

Pia kwenye moja ya posti zake wkkenyemtandao huo huo wolper alisisitiza kubaki kuwa team mabadiliko

“...Ni bora kuwa kaisari kuliko kuwa yuda mimi nitabaki kuwa Jacq Lowassa”

Am In Love With My Sister. Please Help Me!

$
0
0
Dear Admin,

I hope this meets you well and I beg of you to post it.

What I’m about to say is considered a taboo in Africa but to us it’s not. I’m in love with my sister. We are in love with each other. My blood sister .She is 23 and I’m 27.

We have been dating each other for 2 years and people mistake our closeness for brotherly/sisterly love. It started after my ex-girlfriend of 5 years broke my heart in 2010 and left me for my friend.

My sister was my comforter and before we knew it, things became romantic. No one should judge us because it’s real love.

She was a virgin and she gave it to me. It’s a shame we found love in a hopeless place.

The problem is how to break the news to our parents that we want to get married. Our plan is to go another country where this is not a taboo and get married.

Please Advice us

Viewing all 104776 articles
Browse latest View live




Latest Images