Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104432 articles
Browse latest View live

Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) Yaingilia Kati Ugomvi wa UKAWA na CCM Uliosaabisha Mauaji

0
0
Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imesema imepokea kwa masikitiko taarifa za kutokea kwa mauaji katika Kijiji cha Mangucha, Wilaya ya Tarime wakati wa kampeni za uchaguzi ambapo mkazi wa kijiji hicho,

Mwita Waitegi aliuawa na imelaaani vikali mauaji hayo pamoja na kuwahimiza viongozi wa vyama vya siasa kuwa makini na wananchi wanawaongoza
Katika taarifa kwa vyombo vya habari iliyotolewa leo na kusainiwa na Mwenyekiti wa NEC, Jaji Damian Lubuva, inasema tume inakemea vikali na kwa nguvu zote ukiukwaji wa maadili unaosababisha uvunjifu wa amani na kusababisha vurugu.

“Kwa mujibu wa taarifa zilizopokelewa na tume, pamoja na mambo mengine, kwa kiwango kikubwa kifo kilisababishwa na fujo, vurugu na purukushani kati ya wafuasi wa vyama vya CCM na Chadema. Vurugu na fujo hizo ni kinyume kabisa cha maadili ya uchaguzi ya 2015 yaliyotiwa saini na vyama vyote vya siasa,” inasema taarifa hiyo.

Aidha, taarifa hiyo inasema maadili ya uchaguzi yanazuia mtu yeyote kuwa au kubeba silaha yoyote ikiwa ni pamoja na silaha za jadi au zana yoyote inayoweza kumdhuru mtu katika mkutano wa Kampeni au mkusanyiko wowote wa kisiasa.

“Kutokana na kutozingatiwa kwa Maadili ya Uchaguzi, 2015 kifo kimetokea na baadhi ya wananchi, wanachama wa vyama hivi vya siasa kuumia, tume kwa mara nyingine imekumbusha na kusisitiza vyama vyote vya siasa na wanachama wao kuzingatia Maadili ya Uchaguzi ya 2015.”

CCM Wamekosea Kutumia Neno na Logo ya M4C Kumnadi Magufuli

0
0
Tangu jana kumekuwepo na mijadala sehemu mbalimbali kuhusiana na matumizi ya logo ya M4C kwa chama cha Mzpinduzi (CCM). Wengine wakisema ni sawa lakini wengine wakisema si sawa.

Sikutaka kulizungumzia hili lakini naona kuna upotoshaji (wa makusudi) unaoendelea, hivyo nimeona nitumie uzoefu wangu ktk taaluma ya Mahusiano (Public Relations) na uelewa mdogo wa Sheria nilionao kutoa ufafanuzi juu ya jambo hili.

Lakini kabla sijaendelea nimpongeze sana mwanasheria wa CHADEMA John Mallya kwa kutoa msimamo wa Chama kuwa wataifikisha CCM mahakamani kwa kitendo cha kurudufu nembo yao.

Kwa uelewa wangu kinacholalamikiwa si logo tu, kinacholalamikiwa ni kitendo cha CCM kutumia nembo ya utambulisho ya chama kingine (Corporate Identity) ya CHADEMA, while are two oponent parties.

Muaasisi wa Taaluma ya Public Relations, Arthur Page alisema ili kutengeneza utambulisho wako kwa jamii (Corporate Identity) unahitaji kuwa alama zitakazokutambulisha.

Alama hizo ni pamoja na Nembo (Logo), Jina (brand name), Rangi (corporate colour), Mundo wa maandishi (designing) kama ilivyo Cocacola, etc.

Vyote hivi ndio vinatengeneza kinachoitwa utambulisho wa kampuni/shirika/asasi/chama etc.

Nembo ya M4C ni Corporate Identity ya Chama cha Demokrasia na maendeleo na imesajiliwa hivyo. Kwa hiyo CCM au chama kingine kutumia nembo hiyo bila ridhaa au makubaliano maalumu na CHADEMA ni kosa kisheria (Criminal Fraud).

KWANINI CCM WAMEKOSEA.

Sheria zinazolinda haki miliki Tanzania (The copyright and neighbouring Act, ya mwaka 1999 na The Trade and Service marks Act, ya mwaka 1986) pamoja na Sheria za kimataifa zinazolinda haki miliki zinataka kuwe na utouti wa utambulisho kati ya asasi moja na nyingine, bidhaa moja na nyingine, shirika moja na jingine etc.

Utofauti huo unakuwa kwenye maeneo mengi lakini kwa uchache ni kama ifuatavyo;

1. Jina/Brand name.
Jina moja haliwezi kutumiwa na asasi mbili tofauti zinazofanya kazi za kufanana. Kwa mfano Kampuni ya bia ya TBL ikizindua kinywaji kiitwacho "Burudani" kampuni ya Serengeti haipaswi kuanzisha kinywaji chenye jina kama hilo. Sheria inazuia ili kutowachanganya wateja na kulinda haki ya mwanzilishi wa hiyo "brand name".

Kwa hiyo kitendo cha CHADEMA kusajili nembo ya M4C kama "operation brand name" yake kinazuia chama kingine cha siasa kutumia jina hilo. Kwa hiyo CCM kutumia M4C ni kosa kisheria.

2. Muundo/Designing.
Muundo wa maandishi una hati miliki kisheria. Kwa mfano muundo wa neno Cocacola ulivyo ni tofauti na muundo wa neno Pepsi. Cocacola wanaandika kwa kucharaza. Hiyo ni designing yao. Pepsi hawaruhusiwi kuiga muundo huo unless kuwe na makubaliano maalumu na Cocacola.

Sasa CCM kwa ujinga wa kiwango cha "PhD" wameiga muundo wa neno M4C. Bora hata wangeandika kwa muundo mwingine, kwa mfano M-FOR-C, au m4c au namna nyingine itakayotofautisha brand name yao na ya CHADEMA. Lakini wamecopy na kupaste. Hapa haihitaji degree ya sheria kujua kuwa CCM wamekosea.

3. Rangi/Corporate colour.
Unaposajili bidhaa yako au kampuni yako ni vizuri kusajili na rangi yako ya utambulisho.

Kwa mfano hati ya usajili ya Chama cha mapinduzi inatambua rangi za kijani na njano kama rangi zao za utambulisho (corporate colour). Chadema rangi zao ni Blue, nyekundu, nyeupe na nyeusi.

Ukisajili rangi yako ya utambulisho ni kosa kisheria kutumia rangi ya mshindani wako hasa kwenye ulimwengu wa leo wa ushindani wa kimasoko wa "Oligopoly Marketing"

Simba hawaruhusiwi kuvaa jezi za Njano kwa sababu sio rangi yao ya utambulisho, vivyo hivyo Yanga kuvaa nyekundu.

Japo Sheria inatoa ruhusa kubadili rangi ikiwa unaona kuna haja ya kufanya hivyo. Yani ukiona "clients" wako au "audience" wako hawaridhiki na rangi yako unaweza kubadili kwa kufuata taratibu za kisheria. Na si rangi tu bali hata logo au muundo (design).

Ndio maana Vodacom ilianza na rangi ya Blue na nyeupe, lakini wakachange na sasa wanatumia nyekundu na nyeupe. Sheria inaruhusu kubadilisha.

Lakini CCM hawakufanya hivyo. Bado hati yao ya usajili inaonesha rangi zao za utambulisho ni Kijani na Njano, lakini leo wamekurupuka kutengeneza logo ya M4C kwa rangi ambazo si zao. CCM hawana utambulisho wa rangi nyekundu, blue, nyeupe wala nyeusi. Wamezitoa wapi?

Haihitaji elimu ya sheria kujua hawa watu wamekurupuka. Yani baba Njano, mama Kijani halafu mnazaa mtoto mwekundu au mweupe.. haya ni maajabu ya 8 ya dunia.

Haiwezekani baba awe Punda, mama awe Nyumbu halafu mnazaa mtoto Twiga?? Hakuna "cross genetics" ya aina hiyo. CCM u have proved failure.

Nisiwachoshe sana lakini kwa kifupi CCM wamekurupuka mno. Ni kukosa umakini kwa kiwango kikubwa. CCM ina wataalamu wa Sheria, ina wataalamu wa PR and Marketing, ina wataalamu wa Communication, kwanini wanafanya "Technical Mistake" ya kitoto namna hii? Hizi ndio akili za kushauriwa na kina Lusinde (standard seven) na kupuuza wataalamu. Poor u.!

Malisa GJ.

TAARIFA Rasmi Kutoka CHADEMA Kuhusu Mbowe Kusafiri na Kukutana na Dr Slaa Marekani

0
0
Kuna taarifa ya kutunga inasambazwa kwa njia za mawasiliano ya mitandao ya kijamii hususan Facebook na WhatsApp ikieneza habari za uongo kuhusu Mwenyekiti wa Chama Taifa, Freeman Mbowe na Mgombea Urais wa CHADEMA anayeungwa mkono na vyama vinavyounda UKAWA, Edward Lowassa.

1. Chama hakijatoa taarifa yoyote kuhusu kuwepo kwa safari ya Mwenyekiti wa Chama Taifa, Freeman Mbowe. Hatujatoa taarifa hiyo kwa sababu hakuna habari ya Mwenyekiti Mbowe kusafiri.

Mwenyekiti Mbowe amekuwa kwenye campaign trail (field) ya Mgombea Urais katika maeneo kadhaa kabla ya kuendelea na shughuli zingine za campaign trail nje ya field, ofisini kwake jijini Dar es Salaam ambazo anaendelea nazo hadi sasa na leo Jumamosi, Septemba 19, atakuwa na mkutano na waandishi wa habari.

Ukiangalia kwa makini pia, taarifa hiyo ambayo imeitwa ni Barua ya Wazi kwa Vyombo vya Habari, haiko katika mwonekano wa taarifa sahihi na rasmi za chama ambazo huwa zinatolewa na/kwa uratibu wa Idara ya Habari na Mawasiliano ya Chama.

2. Mgombea Urais wa CHADEMA anayewakilisha pia vyama washirika wenza vinavyounda UKAWA (CUF, NCCR-Mageuzi na NLD) anaendelea na ziara za kampeni mikoani akiwafikia wananchi wa vijijini na mijini. Habari zingine tofauti na hizo ni mwendelezo wa wapinzani wetu yaani CCM kutaka kuhamisha mjadala wa uchaguzi wa MABADILIKO ili wapiga kura wajadili vitu vingine visivyokuwa muhimu kwenye wakati ambapo Watanzania wanajiandaa kuandika historia mpya katika nchi yao.

Kubadili mjadala ndiyo mbinu ambayo CCM wameamua kuitumia ili eti kuwachanganya wapiga kura ambao wamejikita kutaka kusikia UCHAGUZI wa MABADILIKO. Si mabadiliko ya sura ndani ya CCM ile ile, bali mabadiliko ya kiutawala na kimfumo, kwa kuiondoa CCM madarakani na kukabidhi dhamana ya uongozi wa serikali na nchi kwa vyama vinavyounda UKAWA.

Kujikita kujadili porojo na uzushi kwa sasa badala ya agenda za uchaguzi huu unaolenga Mabadiliko, ni kuisaidia CCM inayopoteza uhalali wa kisiasa kadri uchaguzi unavyokaribia ili hata uhalali wa kisheria ilionao sasa, ukahitimishwe hapo Oktoba 25, mwaka huu.
Hatutawaachia wapumue kwa sisi kuanza kujadili uongo wanaozusha. Wananchi wana matumaini makubwa na UKAWA. Wanaimba mabadiliko na Lowassa, Lowassa na Mabadiliko. Wanasubiri mabadiliko kutoka kwa CHADEMA, CUF, NCCR-Mageuzi na NLD.

Tunasimamia hapo kusonga mbele.

Makene

NEC: Matokeo Ya kura za Urais Yatabandikwa Vituoni Ili Kuondoa Malalamiko Ya Kura Kuibiwa

0
0
Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imesema kuanzia sasa itaanza kubandika matokeo ya kura za urais kwenye vituo vya kupigia kura katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu ili kuongeza uwazi na kupunguza malalamiko ya wizi wa kura.

Mpango huo umeelezwa na Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Jaji mstaafu Damian Lubuva alipozungumza na viongozi wa dini jijini Dar es Salaam ambao walimueleza hoja hiyo kuwa moja ya vigezo vitakavyokamilisha mchakato huo kwa amani na utulivu na kuwaridhisha wagombea na wafuasi wa vyama.

Alisema licha ya kubandikwa vituoni, utangazaji wa matokeo utafanyika kama kawaida katika kila ngazi, udiwani kwenye kata, ubunge wilayani na urais Tume makao makuu.

Jaji Lubuva aliwahi kunukuliwa siku za nyuma akisema kuwa “hakuna haja ya kuwa na shaka wala kuandaa vijana wa kulinda vituo. Hakutakuwa na nafasi hiyo kwa sababu kura zote zitahesabiwa na kubandikwa huko.

“Kila mtu atajua diwani gani kapata kura ngapi, na mbunge na hata rais aliyemchagua. Itakuwa tofauti na zamani ambapo zilikuwa zinasafirishwa na kuhesabiwa wilayani ambako watu wengine walidhani yanabadilishwa,” alisema.

Wanaume Mnao Jisifia Mnajua Mambo Sita kwa Sita Mnaboa Wengi Si lolote..One Minute Man

0
0

Umekutana na Jamaa very Handsome...Very Smart..Kajazia misuli UKAMTAMANI...Yaani kila ukimwangalia Pichu inajaa udambwidambwi...Unampatia Picha Ukimpa Mzigo jinsi atakavyoimanua vizuri...SIKU YA SIKU UMEJIANDAA UMEMPA SHOO....Jamaa yuko bize anapiga mikelele ya shangwe kuita wazungu wakati wewe wala huoni anachofanya and ur wondering,"WHAT IS THIS NIGGA DOING ON TOP OF ME"
Imewahi kukutokea???
Halafu MBAYA ZAIDI baada ya kukuru kakara zisizo na faida yoyote kwako na kupakwa shombo la maana na kuwa disappointed jamaa linashuka na kukuuliza
"BABE HOW WAS IT"..Teh teh,Hapa wanaume tunapewaga jibu la kisiasa tu IT WAS FINE...halafu ananyanyua gagulo lake anaenda bafuni akirudi utasikia
"I think we should go,Nimekuta Missed call za Mum"
HUPEWI TENAAAAAA....Wanaume ukiona umepewa mara 1 ukiomba tena unazungushwa kama unafuatilia TIN NUMBER ofisi ya TRA ujue ULIFELI DAY 1...Akupe tena ili iweje??
UKIPEWA PAKUA HASWA..Ukishuka mtu alale kama masaa2 hivi ndo akumbuke kuna mama home...Sio mtu unashuka nae anabeba taulo..HUJAFANYA KITU BLOO!
poooooooo imejipost

I Need a Tanzanian Matured Man to Love Me

0
0
Mambo! Mimi ni binti,umri wangu ni miaka Ishirini na tano,mrefu,mweusi na mwembamba ni mkristo pia,elimu yangu ni chuo kikuu na ni mfanyakazi. Lengo langu hapa natafuta mwanaume,wa kuanza naye urafiki,mapenzi na mengine tukielewana.Awe mrefu,mwembamba,mwenye afya bora,mwonekano mzuri wa sura na mtanashati,asiwe mnywaji wa kilevi kupitiliza wala asivute sigara! Awe ana chanzo cha mapato cha kueleweka,matured,broadminded na alietayari kuingia kwenye mahusiano ya mapenzi na mwanamke,sexually active kwa njia ya kawaida ya kimaumbile!Elimu chuo kikuu...karibuni,alie tayari awache Mawasiliano yake! Sitaki mzaha,kebehi wala nyodo...!kama unajua hayakuhusu usinivuruge!
I Used to live in USA now Am Back
Note:I only Need Tanzanian Man Not Otherwise...
Call Me Sandra Kileo

Mambo Manne Mazito Aliyozungumza MBOWE Mchana wa Leo

0
0
Mh MBOWE akizngumza na wahabari mapema leo Jijini Dar es salaam
Umoja wa Katiba ya wananchi UKAWA leo umeitaka Tume ya taifa ya uchaguzi kutoa tamko kuhusu kauli iliyotoleawa na mmoja wa viongozi wa CCM kuwa chama hicho hakipo tayari kuondoka ikulu hata kama kitashindwa katika uchaguzi ujao mwaka huu.
Kauli hiyo ilitolewa katika kampeni za Urais mkoani kigoma na mmoja kati ya viongozi wa chama hicho ndugu ABDALA BULEMBO ambapo alisema kuwa hakuna njia inayoweza kuwaondoa ikulu na chama cha mapinduzi hakiwezi kuachia IKULU kwa njia yoyote kauli ambayo imeanza kuibua mijadala mbalimbali nchini Tanzania.

Akizungumza na wanahabari mchana wa leo mwenyekiti wa chama cha Democrasia na maendeleo chadema ambaye pia ni mwenyekiti mwenza wa UKAWA ndugu FREMAN MBOWE amesema kuwa kauli hiyo imewashtua sana wao kama vyama vya upinzani na kuanza kuwa na wasiwasi kama uchaguzi huo utakuwa na amani kwa kuwa chama chenye serikali kimeapa kufanya njia yoyote ili tu kisiachie ikuluMh MBOWE amesema kuwa kauli hiyo inaweza kuchukuliwa kawaida lakini ni kauli nzito na yenye mafumbo makubwa ambayo yanaweza kusababisha vurugu kubwa na hadi sasa hakuna mtu yoyote wa chama hicho wala tume ya uchaguzi aliyejitokeza kutolea ufafanuzi kauli hiyo.
Amesema kuwa kama kauli hiyo ni kauli ya chama cha mapinduzi ni ukweli kuwa vyama vya upinzani havitaweza kuwa na imani na uchaguzi huo kwa kuwa tayari chama tawala kimesema hakiko tayari kuachia ikulu huku akienda mbali na kusema kuwa kwa kauli hizo hakuna haja ya kuendelea kuwa na uchaguzi ambao chama tawala kinangangania ikulu
Mh MBOWE amesema sasa UKAWA unaitaka tume ya taifa ya uchaguzi kukitaka chama cha mapinduzi kutolea ufafanuzi kauli hiyo kwani kama ndio kauli yao watangaze kabisa kuwa hakuna uchaguzi kwa kuwa utakuwa ni upotevu wa rasilimali za taifa wakati tayari chama tawala hakiko tayari kukubali matokeo..

MGOGORO WA NCCR MAGEUZI.
Aidha katika hatua nyingine mwenyekiti huyo wa chadema amesma kuwa sakata linaloendelea ndani ya chama cha NCCR MAGEUZI ni mwendelezo wa baadhi ya viongozi wa vyama hivyo kuendelea kufika bei ya kutaka kuisaliti ukawa na hakuna lingine.
Hivi juzi viongozi kadhaa wa chama cha NCCR waliibuka na kudai kuwa chama chao kimekuwa kikiyumba kutokana na mwenyekiti wao kufanya kazi za chadema kuliko za chama huku wakidai kuwa wamekosa majimbo mengi ambayo walikuwa wanayatarajia ambapo Mh mbowe amesema kuwa hiyo sio hoja kwani lengo la UKAWA sio chama kuwa na majimbo mangapi bali ni kuhakikisha kuwa wanaibuka na majimbo mengi bila kujali vyama vyao.
Mh mbowe amesema kuwa swala la mgawanyo wa vyama lilienda sambamba na kuangalia uwezo wa chama husika katika jimbo na kusimamisha mtu ambaye anakubalika katika eneo husika ili kuweza kupata ushindi katika majimbo mengi na sio kutoa majimbo hata kwa watu ambao hawakubaliki katika majimbo hayo.

MPANGO WA KUMSHAMBULIA MBATIA
Katika hatua nyingine mwenyekiti huyo ameibua swala ambalo amesema kuwa wamelipata kuwa kuna mipango ya vijana kutoka chama cha mapinduzi kujifanya ni vijana wa CHADEMA na kumpiga Mbatia wakidai kuwa hawamtaki katika chama hicho jambo ambalo amesema ni mipango mfu kwani tayari chama hicho kimezipata.
Mh mbowe amesema kuwa mipango kama hiyo imekuwa ikipangwa na chama cha mapinduzi na na imekuwa wazi na wamekuwa wakiripoti sana kwenye vyombo vya dola lakini kumekuwa hakuna msaada wowote wanaoupata lakini wamejipanga kiulinzi kwa viongozi wao wote na wanahakikisha kuwa wanakua salama salimini.

MBOWE KUTOROKA NCHI
Akizungumza huku akicheka kwa mshangao mkubwa Mh MBOWE amesema kuwa kuna baadhi ya propaganda ambazo zimekuwa zikienezwa na baadhi ya viongozi wa chama cha mapinduzi na maadui wa UKAWA kuwa yeye ameikimbia nchi na haonekani katika kampeni za Mh LOWASA ambapo amesema kuwa ni utaratibu wa kupokezana kazi na sasa Ilikuwa zamu ya MH LISSU na baadae atapokea Mh WENJE ili kupeana nafasi za kufanya kazi za majimbo yao.
Mh mbowe amesema kuwa kuna baadhi ya jumbe za kutengeneza za EMAIL zikimuonyesha MBOWE akiwasiliana na Dk SLAA ambapo amesem ni uongo uliotukuka na hajawahi kufanya hivyo na hajatoka nje ya Tanzania kwenda popote kama wanavyosema huku akisema kuwa kuzushwa kwa mambo hayo ni kutokana na wapinzani wao kuishiwa sera na kuanza kuwadanganya watanzania.

Picha 9: Mafuriko ya LOWASSA Bukoba Mjini na Misenyi, Kagera


JB Aanza Kupata Changamoto za Kisiasa Katika Kazi zake

0
0
Msanii mkongwe wa filamu Jacob Stephan maarufu kama JB ameanza kuathiriwa na vuguvugu za kisiasa katika kazi zake za filamu.

JB ambaye amekuwa akionekana katika kampeni za Chama Cha Mapinduzi, amejikuta katika wakati mgumu kwenye mitandao ya kijamii baada ya kupokea matusi na kejeli alipotangaza ujio wa kazi mpya marehemu Adam Kuambiana ambaye anadaiwa alikuwa Chadema.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram JB ameandika:

Narudia tena siasa sio vita…marehemu Adam alikuwa Chadema kuliko wengi wenu, mpaka alikuwa campaign manager wa mkewe Janet kule Kawe kwenye udiwani, mbona tulikuwa tunashirikiana? Wasani mbona wengine wako UKAWA lakini bado ni marafiki, nina ndugu ambao wako UKAWA na nyinyi pia mna ndugu wako CCM mnagombana nao? hamshirikiani nao ? au mme ona sinema zetu tu…vitu vyote mnavyo nunua madukani vimetengenezwa na ukawa? acheni siasa za kijinga. sitaki utoto nikitangaza kazi zangu…kama hupendi piga kimya.

Lowassa:Richmond Kujulikana Oktoba 25

0
0
Hiyo ni kauli ya Lowassa.

Sumaye nae ahoji kama Richmond ni ya Lowassa kwanini inalipwa?

Lowassa anapiga kampeni za kisayansi, walitegemea atawajibu kuhusu Richmond sasa itabidi waendelee kusubiri hadi siku ya kupiga kura watakapopata majibu wanayoyataka.

Na sisi wananchi tuko tayari kumjibia siku hiyo.


Chanzo:TanzaniaDaima

Edward Lowassa Kuiteka tena Dar es Salaam LEO

0
0
MGOMBEA urais wa Chadema na anayeungwa mkono na vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA), Edward Lowassa anatarajia kuliteka tena Jiji la Dar es Salaam leo  katika mikutano mitatu.

Lowassa anarejea tena jijini Dar es Salaam mara baada ya kufanya mikutano kwenye majimbo ya Kawe na Kibamba Septemba 7 mwaka huu na kunadi wagombea wa majimbo hayo.

Lowassa alimnadi John Mnyika wa Kibamba na Halima Mdee wa Kawe kabla ya kuelekea visiwani Zanzibar katika uzinduzi wa Kampeni za Urais za Maalim Seif wa CUF.

Jijini Dar es Salaam leo Lowassa anatarajia kufanya mikutano yake katika Jimbo la Ukonga, Kigamboni na jimbo jipya la Mbagala ambapo maandalizi tayari yamekamilika.

Lowassa ataanzia Jimbo la Kigamboni saa 3:00 asubuhi, saa 6:00 mchana atakuwa katika Jimbo la Mbagala na atamalizia kwenye Jimbo la Ukonga saa 9:00 alasiri.

Sambamba na viongozi wengine Lowassa ataambatana na timu nzima ya kampeni ya UKAWA akiwemo Waziri Mkuu Mstaafu, Fredrick Sumaye; aliyekuwa Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Shinyanga, Hamis Mgeja; meneja wa kampeni John Mrema pamoja na mwenyekiti wa Chadema-Taifa, Freeman Mbowe.

Lowassa anaingia Dar es Salaam akiwa tayari amezunguka kwenye mikoa 15 ya Tanzania ikiwemo Dodoma, Geita, Kagera, Geita, Shinyanga na Iringa huku mikoa ya Lindi, Mtwara, Pwani, Arusha na mingeneyo ikiwa bado kufikiwa.

Kwa Wanandoa Tu: Ni Halali Kupokea Simu ya Mumeo/Mkeo Akipigiwa?

0
0

In case mumeo/mkeo yuko mbali kidogo na simu yake halafu ikatokea akapigiwa simu na mtu ambaye aidha ni namba ngeni au iliyohifadhiwa kwenye simu, na wewe upo karibu na simu yake, Je, unaweza kumpokelea!
Nawasilisha!

VIDEO: Mbowe Ajibu Malalamiko ya Viongozi wa NCCR-Mageuzi

0
0
MWENYEKITI Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) ambaye pia ni mwenza wa vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananachi (UKAWA), Freeman Mbowe amesema, wanaoleta chokochoko ndani ya umoja huo walitaka upendeleao.

Kauli ya Mbowe inakuja siku mbili baada ya Makamu Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi, Leticia Ghati Musore na katibu mkuu wa chama hicho Mosena Nyambabe kudai kwamba “Chadema imejipa umiliki wa UKAWA.”

Wakizungumza mbele ya waandishi wa habari viongozi hao wa NCCR-Mageuzi walimtuhumu mwenyekiti wao James Mbatia ‘kutekwa’ na Chadema na kwamba, ameshindwa kukitetea chama chao kwa kile walichosema kumezwa katika umoja huo.

Akizungumza na waandishi jana, Mbowe alisema viongozi hao wana jambo lingine nje ya yale waliyoyatamka hadharani na kwamba, kubwa ni kutaka kupewa upendeleo wa kugombea majimbo licha ya kukosa sifa.

“Tulikubaliana kuwa ili chama kipewe jimbo tutaangalia matokeo ya chama 2010, tutaangalia madiwani wa chama husika katika jimbo, mtandao wa chama pia matokeo ya uchaguzi wa vijiji na mitaa 2014 pamoja na mtandao wa ushindi wa mgombea” alisema Mbowe.

Mbowe alisema majimbo ambayo Nyambabe na Leticia wamekuwa wakiyang’ang’aniwa kugombea licha ya kutokuwa na sifa ni Segerea la jijini Dar es Salaam ambalo walipewa CUF na Jimbo la Serengeti lililopo Mara ambalo limekabidhiwa kwa Chadema.

“Nyambabe alihitaji kugombea Jimbo la Serengeti ambako Chadema ilishinda vijiji 38 lakini NCCR haikushinda hata kijiji kimoja katika uchaguzi wa vijiji, Chadema ina madiwani 8 NCCR haina hata mmoja, Nyambabe amegombea jimbo hilo mara mbili kwa vyama tofauti lakini hakupata hata asilimia 5, tungempaje hapo?” alihoji Mbowe.

Kwa upande wa Musore, Mbowe alieleza kwamba mwanamama huyo aliomba aachiwe kugombea katika Jimbo la Segerea ambako NCCR haina mtandao wa ushindi wala nguvu “jambo hili UKAWA tulilipinga.”

“Musore tunamfahamu aliwahi kuwa diwani wetu Tarime, hakujijenga wala kujenga NCCR, katika Jimbo la Segerea pia lakini akawa anataka tumzawadie jimbo kama makamu mwenyekiti taifa, hapana! tunataka kushinda hatuwezi kufanya uamuzi tunaojua wananchi wataukataa,” alisema Mbowe.

Hata hivyo alisema UKAWA bado wanaendelea na utatuzi wa migogoro iliyojitokeza katika majimbo na kwamba mambo yatakuwa mazuri muda si mrefu.

“Huu ni muungano wa vyama vinne, lazima kutofautiana kuwepo lakini kamwe hatuwezi kushindwa kuelewana katika maeneo machache yaliyobaki na hivi tunavyoongea Profesa Baregu, Salum Mwalimu, Bashage na viongozi wa CUF taifa wameelekea majimbo yenye shida,” alisema  Mbowe.

Baadhi ya majimbo yaliyo na utata ni Mtwara Mjini, Kigamboni, Itilima (Simiyu), Masasi, Mtama (Lindi), Ngara na Sikonge.

Msikilize Mbowe akiongea

Vijana na Watafutaji Tuna la Kujifunza Kupitia Dalas na Jack Wolper

0
0
MOYO huhifadhi mengi mazito hasa ya kuumiza! Staa mkubwa wa sinema za Kibongo, Jacqueline Wolper Massawe amejikuta akimwaga machozi wakati akianika siri tano nzito kuhusu mapenzi katika mahojiano (exclusive interview) na Amani kwa takriban saa mbili.

Katika ‘intavyu’ hiyo iliyofanyika Jumatatu iliyopita kwenye Ofisi za Global Publishers, Bamaga-Mwenge jijini Dar kuanzia saa 8:44 alasiri hadi saa 10:44 jioni, Wolper alifunguka vitu vingi.

KISA/MKASA
Akizungumza kwa masikitiko, uchungu na majuto, Wolper alisema hawezi kumsahau mwanaume huyo ambaye ni Abdallah Mtoro ‘Dallas’ kwa namna alivyomwingia kijanja na kutaka kumvunjia heshima aliyoijenga karibia miaka kumi nyuma.


ALIANZIA WAPI NA DALLAS?
“Siku ya kwanza Dallas alinipigia simu na kuniambia aliniona Magomeni (Dar). Naikumbuka sana siku hiyo, ilikuwa baada ya mizunguko yangu, mwanzoni sikupokea simu yake kwa sababu ilikuwa namba ngeni kwangu.
“Nilimsikiliza sana. Jamani yule mwanaume anaongea kwa ushawishi wa hali ya juu mno. Nilishangaa aliponieleza kila kitu kuhusu familia yangu na nyumbani kwetu. Kumbe tayari alishaunda urafiki na baba yangu (mzee Massawe).


“Mwanzoni nilidhani ni tapeli. Nikamkatia simu. Akaendelea kunipigia na nilipoona imekuwa kero kubwa nilipokea. Ili kuthibitisha anawajua wazazi wangu, alinitajia namba zao za simu ambazo ni za kweli.
“Pamoja na hilo nilimfanyia nyodo, si unajua mtoto wa kike? Lakini aliniongelesha kwa upole hadi nikapunguza nyodo zangu.

“Aliniuliza nataka anifungulie biashara gani. Nikamwambia biashara ya nguo. Akaniuliza nataka mtaji kiasi gani. nikamwambia dola laki moja kwa sababu nilikuwa sitaki fremu moja, nilitaka nyumba nzima. Akaniambia hakuna tatizo.
“Pia aliniuliza naishi wapi? Nikamwambia Sinza (Dar) alionesha dharau kwenye simu akaniambia atanihamishia Mbezi Beach.


“Aliniuliza natembelea gari gani? Nikamwambia Toyota Noah. Akaniambia ningependa aninunulie gari gani? Nikamjibu Toyota Discovery lakini yeye akasema ataninunulia Toyota Harrier.

“Kweli baada ya siku mbili-tatu nililetewa Toyota Harrier nyeusi nyumbani. Niliogopa isijekuwa mtego nikaingia kwenye matatizo hivyo nilimzungusha mtu aliyeniletea hadi Sinza-Mori nikamwambia apaki kwenye kituo cha teksi, nikaenda na dereva nikalichukua hadharani ili lolote likitokea nipate msaada


“Nilikabidhiwa funguo za lile gari na documents zake, nikaondoka nalo hadi nyumbani kwangu. Kesho yake Dallas alimtuma mtu aniletee dola za Kimarekani 15,000 (zaidi ya Sh. milioni 24). Nilipouliza za nini aliniambia ni kwa ajili ya shopping ya kutembelea Harrier niachane na zile swaga za kwenye Noah (fedha inaongea). Kisha akanitumia cheni ya dhahabu.

“Siku iliyofuata alinitumia Sh. milioni 15 nipeleke nyumbani nikawaambie wazazi nimepata mchumba ambaye angeenda kujitambulisha baadaye. Niliwaambia ni Dallas ambaye walikiri kumfahamu kwa sababu alishawapigia simu na kujitambulisha kuwa ni mkwe wao.”


AMESHAKUTANA NA DALLAS?
“Hadi hapo nilikuwa sijamuona Dallas kwa sura na fedha nilikuwa natumiwa kila siku.
“Wakati hayo yakiendelea akaagiza nihamishiwe Mbezi Beach na kununuliwa lile gari lililoibua mzozo BMW X6.
“Nakumbuka siku niliyokabidhiwa lile gari nililia sana. Sikuamini macho yangu kwa sababu Dallas aliniambia amenitumia kazawadi kumbe ni BMW X6 (lina stori ndefu inakuja)!

“Kumbuka mwanzoni nilikuwa na boyfriend ambaye tulipendana sana lakini hatukupanga kufunga ndoa. Nilimweleza kila kitu akakubaliana na mimi japokuwa aliumia.
“Maskini! Kuanzia hapo nikawa nimeachana na yule boyfriend wangu lakini hakukuwa na namna kwa sababu niliamini nimepata mchumba wa kunioa.

ATAKIWA KUBADILI DINI
“Baadaye Dallas aliniambia nimeshakuwa mchumba wake hivyo nibadili dini. Kweli nilibadili nikawa Muislam na jina langu likawa Ilham. Hicho kilikuwa kipindi kigumu sana maishani mwangu kwa sababu nilionekana ni muasi katika dini yangu ambayo mama ni mzee wa usharika na mwimba kwaya, baba ni mtu wa kanisani sana.”

NINI KILIFUATA?
“Siku moja nilikuwa Tanga nashuti filamu, nilikuwa nikitoka hapo niende Morogoro. Dallas alinipigia simu akaniambia yupo Nairobi (Kenya) anakuja Tanzania. Nilimwambia nipo Tanga akaniambia atanifuata kule. “Niliendelea kupiga mzigo. Zilipita saa nyingi, baadaye nikiwa na kruu yangu, Dallas alinipigia simu akaniambia ameniona.
“Nilikataa, akaniambia namna nilivyo, nguo nilizovaa na watu niliokuwa nao, alipatia. Kumbe alikuja na Toyota Prado.

WOLPER MORO, DALLAS DAR
“Tulipomaliza kurekodi Tanga tulikwenda Morogoro, yeye aliniambia anaelekea Dar. Tulikuwa tunawasiliana. Nilipomaliza kurekodi Moro nilirejea Dar. Hapo ndipo vituko vikawa juu ya vituko.

“Niliambiwa mara kaonekana sehemu akiwa na mwanamke au wanawake. Mimi sikujali kwa sababu nilipomuuliza aliniambia hatuwezi kuonana kwa sababu kipindi hicho alikuwa katika swaumu hivyo akionana na mimi nitamharibia. (ulikuwa mwezi mtukufu).

BADO HAWAJAKUTANA?
“(Mguno) Hapo bado hatujakutana lakini yupo mjini na amejaa tele kwenye kumbi za starehe.
“Baada ya kumaliza swaumu, siku moja aliniambia anakuja nyumbani Mbezi Beach. Niliwaalika marafiki zangu tukapika vyakula, tukafanya usafi na kufukiza udi chumbani. Nilitandika mashuka meupe kitandani na kujipara kisha nikavaa ushungi kuanzia mchana nikakaa kama malkia nikimsubiri mchumba.

“Huwezi amini, hadi giza linaingia Dallas hakutia mguu. Nilipataje aibu kwa rafiki zangu waliotaka kumuona huyo mchumba? Ninyi acheni tu!
“Nilipomuuliza aliniambia alipata dharura kuna biashara alikuwa anafanya

HATIMAYE WAKUTANA LAKINI…
“Nilikasirika sana, nikasema huyu ni mchumba gani asiyetaka kuja kwangu? Nikampa muda wa siku tatu aje nyumbani na alete nguo zake zote. Kweli, siku ya tatu, asubuhi nilimsikia mtu akiita ‘Ilham Wolper Dallas’. Nilishajua sauti yake kupitia simu hivyo nilimkaribisha na nguo zake nikaingiza ndani. Lakini cha kushangaza alikuja na pikipiki!

“Alishinda nyumbani siku hiyo maana kuna ndugu zake walikuja. Hatukufanya chochote. Dallas aliishia kunibusu shavuni kisha jioni akaondoka.



“Mjini kukawa hakukaliki. Natumiwa picha akiwa na wanawake tofautitofauti. Mmoja wa wanawake hao niliambiwa eti ana ‘ngoma’! Jamani hii dunia ina kichaa!

“Muda ukasonga, vitimbi vikawa vingi. Dallas simuoni. Muda wa kukaa kwenye ile nyumba uliisha hivyo nikahama na nikamwambia akachukue nguo zake.

UCHUMBA WAVUNJIKA, SASA ANAPUMZIKA HAPA
“Baadaye uchumba ukavunjika tena mimi ndiyo nilimwambia simtaki tena. Nilikaa muda hadi baadaye nilipopata mwanaume wangu wa sasa. Anani-control vizuri kwa sababu kanipita umri na ana busara. Tunapendana sana. Najuta kumfahamu Dallas. Siwezi kusahau tukio hilo katika maisha yangu. Dallas alicheza na hisia za moyo wangu. (akaangua kilio) Niliteseka sana. Ni Mungu tu anajua…

VIPI KURUDIA UKRISTO?
“Nimekaa muda siendi kanisani. Nilikuwa najifungia ndani nalia kama mama yangu alivyokuwa anafanya. Siku moja nilimwambia mwanaume wangu akaniambia kuliko kulia kila siku bora nirudi kanisani. Ndipo nikarudia ukristo. Kwa sasa nasali Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Usharika wa Kijitonyama, Dar,” alisema.

Mtazamo: Hollywood Movies na Suala la Ushoga!

0
0
Nimependa kushare na nyie mtazamo wangu kuhusu movies na series za siku hizi toka kwa wazungu.

Nimekuwa nikishangazwa sana na movies hizi ambazo kwa ujumla stori yake inaweza kuwa nzuri tu lakini baadhi ya wahusika wamekuwa wakioneshwa wakijihusisha moja kwa moja na masuala ya ushoga au usagaji! Tena unakuta ni wahusika muhimu wanaofanya yao yakaenda.

Je,kuna nini nyuma ya haya yote? Hivi sio mpango ili tuyaone mambo haya kuwa ni ya kawaida tu? Sio mpango wao kutuonesha mtu anaweza kuwa na matendo haya machafu na akafanya mambo makubwa tu kwenye jamii? Wanatumia characters(wahusika) wenye mvuto mkubwa kwenye hiyo "story" ili kuiaminisha dunia kuwa hayo ni mambo ya kawaida tu, yaani mtu yeyote anaweza akawa "gay" na maisha yakaenda kama kawaida.

Je, wanataka kutufundisha nini? Ushoga ni LAANA kubwa kwa MUNGU ni jambo lisilotakiwa kabisa hata na tamaduni zetu za kiafrica. Watoto wetu wanajifunza nini kutoka kwenye filamu hizi? Tunajenga jamii ya sasa na ya badaye yenye mtazamo upi?

Kwa hali ya kawaida kile tunachokiona na kukisikia huathiri moja kwa moja fikra zetu na mitazamo yetu kisha tabia zetu. Mtakumbuka zamani ilikuwa ni jambo la ajabu tena la aibu kuona watu wakikiss hadharani lakini sasa ni jambo la kawaida tu, haya yote ni baada ya mitazamo yetu kubadilishwa taratibu na kile tunachokitazama.

Mtakuwa mashahidi zangu kwa series/movies kama Orphan Black, Empire, Sense 8, etc.. baadhi ya wahusika wake wamejihusisha na mambo haya maovu tena yanaoneshwa wazi wazi.

Hii ni hatari kubwa katika maadili ya jamii yetu ya sasa na ya badae. Kama tukikubali kubadili mitazamo yetu kwa kutazama mambo haya machafu, tutawezaje kuyapinga?

Hebu tuwe makini sana na kile tunachochagua kukitazama ama kukisikia. Zaidi tuwe makini na kile kinachotazamwa majumbani na watoto/wadogo au ndugu zetu.

Msomi wa Chuo Kikuu Auawa Kisa Chips

0
0
RIP! Kijana aliyefahamika kwa jina la Shelitiael Steven Mbise, aliyekuwa akisoma Chuo Kikuu cha Dodoma (Udom) amefariki dunia kwa kuchomwa kisu na muuza chipsi kufuatia kutofautiana.

Kwa mujibu wa chanzo kutoka Dodoma, denti huyo alikuwa akichukua masters akiwa kwenye mwaka wake wa kwanza.
“Marehemu alikuwa amepanga chumba nje ya chuo, Mtaa wa Chako ni Chako lakini kipindi hiki chuo kimefungwa alikuwa hapa na mara nyingi alikuwa akionekana yuko bize na masomo kwani alikuwa akienda chuoni na kurudi.

“Kuna sehemu alishawahi kupanga chumba na rafiki yake lakini baadaye akahama na kwenda kupanga chumba chake mwenyewe,” kilieleza chanzo hicho kwa sharti la kutotajwa jina.Chanzo kiliendelea kuweka wazi kuwa siku ya tukio, Alhamisi ya Septemba 10, mwaka huu Mbise alikwenda kwenye chipsi ambapo ni jirani na anapoishi. Ndipo kukatokea mgogoro ulisababisha muuza chipsi kumchoma kisu.

“Kulikuwa na ugomvi kati ya marehemu na muuza chipsi. Sasa mashuhuda wanadai, msomi huyo aliomba chenji yake baada ya kula, muuza chipsi akasema hajalipa na akamtaka alipe. Wakazozana, mwishowe msomi aliamua kuondoka, ndipo mtu wa chipsi akamfuata kwa nyuma na kumchoma kisu sehemu ya juu ya mgongo. Mbise alianguka na kupoteza maisha palepale huku mtuhumiwa akishikiliwa,” kilisema chanzo.

Kikaendelea: “Baada ya hapo, taarifa ziliufikia uongozi wa chuo na mwili ulichukuliwa na kupelekwa Hospitali ya Mkoa wa Dodoma kwa ajili ya uchunguzi na kisha Ijumaa usiku ulisafirishwa kwao jijini Arusha.”

Kupitia simu ya mkononi, mwandishi wetu alimpigia afisa habari wa chuo hicho ambaye alijitambulisha kwa jina moja la Beatrice. Yeye alithibitisha kutokea kwa kifo cha mwanafunzi huyo akisema:

“Ni kweli yule alikuwa mwanafunzi wetu wa mwaka wa kwanza na kipindi hiki chuo kimefungwa lakini yeye alikuwa maeneo ya jirani na chuo kwa ajili ya kuonana na supavaiza wake. “Siku ya tukio marehemu alikuwa akienda mjini, akapita sehemu wanayouza chipsi kwa ajili ya kupata chakula ndipo ukatokea ugomvi uliosababisha yeye kuchomwa kisu lakini kesi tayari ipo polisi na yule mtuhumiwa anashikiliwa katika Kituo Kikuu cha Polisi Dodoma.Mwili wa Steven Mbise ulihifadhiwa kaburini Jumamosi iliyopita. Mungu ailaze roho yake mahali pema peponi. Amina.

UVCCM yamshangaa Sumaye kumpigia debe Lowassa

0
0
KATIBU Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), Shaka Hamdu Shaka amesema anamshangaa Waziri Mkuu mstaafu, Frederick Sumaye kusaidia kampeni mgombea urais kwa tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Edward Lowassa.

Amesema uamuzi huo wa Sumaye ni sawa na pwagu kumfanyia kampeni pwaguzi. Shaka alitoa matamshi hayo jana katika mkutano wa hadhara wa uzinduzi wa kampeni za ubunge na madiwani jimbo la Mtwara Vijijini wakati akimnadi mgombea wa jimbo hilo kupitia CCM, Hawa Ghasia.

Mkutano huo wa kampeni ulifanyika katika kijiji cha Mo Pacha Nne mkoani hapa.

Alisema ni kituko kwa viongozi hao, ambao waliwahi kuwa viongozi wa juu wa serikali ya CCM na kushindwa kuleta ufanisi na matokeo chanya, sasa wakiwa Chadema kughilibu wananchi wakidai wana ubavu wa kuleta mabadiliko na maendeleo.

“Sumaye anapomfanyia kampeni Lowassa awe Rais ni sawa na pwagu kumfanyia kampeni pwaguzi, hawajui wafanyalo, hawatambui kama majina yao hayaheshimiki mbele ya jamii, walipewa nafasi za juu wakashindwa kuisukuma nchi kimaendeleo,” alisema Shaka.

Alisema Sumaye akiwa Waziri Mkuu wa Serikali chini ya awamu ya tatu ya Rais Benjamni Mkapa, usimamizi wake alisababisha halmashauri nyingi za wilaya nchini kupata hati chafu kwa mujibu wa ripoti za Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali.

Aidha, Shaka alifichua siri ya jina la Lowassa kukatwa na vikao vya CCM katika mbio za urais, huku akisema halikuwa jambo la bahati mbaya.

ZARI HASSAN and DIAMOND already disagreeing on this

0
0


On Sunday, Zari and Diamond will release photos of Princess Latiffah’s face and disclose companies that have endorsed her but the two are still teasing their fans with half photos of Tiffah.

Check her out sporting a boyish look;

My sweet potato….Her dad loves seeing her looking boyish, mama loves her all dolled up in pink with ribbons. Blame this look on dad…she got a signature lip pause too, my lil diva in the making



SHOCKER! Church exposes JULIANA KANYOMOZI and how she sacrificed her only son to Satan

0
0

Just a week after Juliana Kanyomozi refuted claims that she started a cult in Uganda and is harboring h@m@s*x#@ls in her new organization, there are new allegations from a church which says that she sacrificed her son, Keron.

In a statement to Ugandans, Worldwide Apostolic Church says that Juliana is a member of Illuminati and she sacrificed Keron for fame and money. The post has however not gone down well with some of her fans.

Read part of it below;

Juliana you know very well how the devil forced you to sacrifice your son Keron? And of course that was supposed to cement your fame forever and keeping you at the Top of the celebrity in Female Artists in Uganda by giving blood of your own child. Juliana don’t fool people, anyway you may fool others but you will not fool them forever because the Truth has come up to be known by everybody and therefore you must accept it”

“but also you are to cause the Spirit of Lust and Lesbianism in people who are your fans and as well as those listen to you. Therefore you know very well that as an Illuminati member you are supposed to keep sacrificing in order to keep your Fame and your songs being loved by everyone. ”



Magufuli Afunika Chato........Maelfu ya Wananchi Wahudhuria Mkutano wake LEO

0
0

Mgombea wa Urais kupitia CCM Dk. John Pombe Magufuli akiwasili kwenye uwanja wa michezo wa Mazaina Chato tayari kuhutubia wakazi wa Chato.

 Umati wa wakazi wa Chato wakiwa wamefurika kwenye viwanja vya mkutano kwa ajili ya kumsikiliza Mgombea wa Urais kupitia CCM Dk. John Pombe Magufuli.
 Mgombea wa Urais kupitia CCM Dk. John Pombe Magufuli akizungumza na Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Geita Joseph Musukuma na Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi na mjumbe wa kamati kuu ya CCM Alhaji Abdallah Bulembo.


 Hii ndio meza kuu.
 Shilole akitumbuiza kwenye mkutano wa kampeni za CCM Chato
 Chege na Temba wakitumbuiza kwenye mkutano wa kampeni za Chato CCM.
 Mr.Blue akiwapagaisha wakazi wa Chato kwenye mkutano wa kampeni.


 Original Komedi wakitumbuiza wakazi wa Chato kwenye mkutano wa kampeni za CCM.
 Joti akipeana mkono na Mgombea wa Urais kupitia CCM Dk. John Pombe Magufuli mara baada ya kumaliza kutumbuiza.
 Yamoto Band wakitumbuiza kwenye uwanja wa michezo Chato kabla ya kuanza mkutano wa kapeni za CCM.



 Khadija Kopa akitumbuiza wakazi wa Chato
 Ali Star wa TOT akitumbuiza kwenye jukwaa la CCM Chato wakati wa mkutano wa kampeni za CCM
 Fid Q akishusha mistari kwenye jukwaa la kampeni za CCM Chato.
Bushoke akitumbuiza wakazi wa Chato kwenye mkutano wa kampeni za Mgombea wa Urais kupitia CCM Dk. John Pombe Magufuli
Viewing all 104432 articles
Browse latest View live




Latest Images