Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104747 articles
Browse latest View live

Dk. Cheni Afunguka Kumuoa Lulu!

$
0
0
Tangu wakati ule msanii maarufu wa filamu, Mahsein Awadh ‘Dk. Cheni’ aamue kupambana kumsaidia Elizabeth Michael ‘Lulu’ kwenye kesi ya mauaji iliyokuwa inamkabali, yaliibuka madai kuwa wawili hao ni wapenzi lakini leo limeibuka la ndoa, Ijumaa lina kila kitu.

Madai ya uhusiano wa Lulu na Dk. Cheni yamekuwa yakienea chinichini kiasi cha kuwafanya baadhi ya watu kuamini kuwa, huenda lisemwalo lipo na kama halipo laja.

Lakini Cheni ana mke

Hata hivyo, madai hayo yanakuja ikiwa inafahamika kabisa kuwa, Dk. Cheni ana mkewe aitwaye Sabrina Zahrain ambaye wanaonekana kupenda licha ya kwamba imani yake haimzuii kuona mke wa pili.

Madai ya ndoa

Wakati tetesi za mastaa hao kuwa wapenzi zikizidi kushika kasi, hivi karibuni mtu wa karibu wa ‘wauza sura’ hao alilipenyezea gazeti hili umbeya kuwa, eti uhusiano wao umeshamiri na wana mpango wa kuona.

Chanzo hicho kilichoomba hifadhi ya jina lake kilinyetisha kuwa, hata mashabiki wa wasanii hao wakisikia kuwa siku f’lani ndoa inafungwa wasishangae kwani ni jambo ambalo Cheni ameona siyo baya kwake.

“Ukaribu wa Lulu ni zaidi ya nyie mnavyojua, Cheni anaingia pale kwa Lulu masaa 24 na ninachojua Dk. Cheni anataka kumuoa Lulu mke wa pili, sasa kama mnataka kujua undani wa hili fuatilieni,” kilidai chanzo hicho.

Dk. Cheni atafutwa

Kufuatia madai hayo Ijumaa lilifanya jitihada za kuongea na Dk. Cheni ambapo alipopatikana alifunguka kama ifuatavyo:

“Hivi jamani mimi nikimuoa Lulu kuna shida gani? Yeye si mwanamke na mimi ni mwanaume, sasa tatizo liko wapi, hebu acha mambo yako bwana.

“Halafu ujue mimi ni Muislam naruhusiwa kuoa mke zaidi ya mmoja. Hilo la kwenda nyumbani kwake ni kwamba pale naingia masaa 24, kwani nani wa kunizuia?”

Lulu anasemaje?

Ijumaa baada ya kuongea na Dk. Cheni lilimtafuta pia Lulu kupitia simu yake lakini hakupokea kila alipopigiwa na hata alipotumiwa sms hakujibu. Paparazi wetu pia akafika nyumbani kwake maeno ya Mbezi jijini Dar lakini akaambiwa na mfanyakazi wake wa ndani kuwa ameenda kwenye mishemishe zake.

Chanzo: GPL



MADNESS! Which Dance Style Is This Now? Some People Are Crazy (LOOK)

$
0
0

This is Madness Now, hey dancers please explain which dance style this is!

What this LADY Did In Her Wedding Has Left Everyone Speechless (VIDEO)

$
0
0


Although many ladies may have done all manner of evils before settling down, they pretend to be saints during their Wedding Day.

But there is this lady who decided to show her true colours on her special day and what she did has left many people speechless.

Just watch the video below.


VUNJA-MBAVU: Staili Tofauti za CCM za Kuomba Kura 2015

$
0
0
Mambo yakiwa magumu unahitajika kuwa mbunifu. Zifuatazo ni staili tofauti zinazotumika na wanaCCM kuomba kura tena kwa wananchi. Wanatia huruma sana. Staili hizi huwezi kuzikuta Ukawa. Cheka kidogo basi




Taasisi ya Kiislam yatoa Tamko Dhidi ya Lowassa na Gwajima, Kuhusu Uchaguzi Mkuu 2015

$
0
0
TAMKO LA TAASISI YA KIISLAMU YA IMAM BUKHARY JUU KAULI ZA NDUGU EDWARD LOWASSA NA ASKOFU GWAJIMA WA KANISA LA UFUFUO NA UZIMA

Ndugu Wanahabari,

Assalaam Alaykum,

Hivi karibuni Taifa letu limetikiswa na maneno ya hatari yaliyotoka katika vinywa vya watu wawili mashuhuri hapa nchini. Maneno ambayo endapo yatapuuzwa yatasababisha mpasuko mkubwa wa kijamii na pengine maafa, na hatimaye kubomoa misingi imara ya taifa iliyojengwa na waasisi wa Taifa hili. kauli hizo ni zile zilizotolewa na mgombea urais wa CHADEMA Ndugu Edward Lowassa na kiongozi wa Kanisa la ufufuo na uzima, Askofu Josephat Gwajima.

Mgombea Urais kwa tiketi ya CHADEMA Ndugu Edward Lowassa amenukuliwa akiwa Kanisani Mkoani Tabora akiwaomba Waumini wenzake wa Madhehebu ya Kilutheri kumuombea sana awe Rais wa Taifa letu kwa hoja kuwa nchi hii haijawahi kupata Rais Mlutheri.

Naye Askofu Josephat Gwajima ambaye ni mshirika wa karibu wa Lowassa amenukuliwa pia akielezea ndoto yake ambayo bado haijatimia ya Kuiona Misikiti ya Tanzania ikigeuzwa kuwa “Sunday Schools” za watoto, pamoja na Masheikh na Maimamu kukimbizana kwenda mbele ya msalaba wa Bwana Yesu Kristo (AS).

Maneno haya ya Ndugu Lowassa na yale ya Askofu Gwajima yakitazamwa kwa idadi ni machache sana, lakini kwa uzito wake ni mabaya tena yenye hatari kubwa kwa umoja wetu wa kitaifa.

Maneno hayo yanaweza kulisambaratisha taifa kwa vile yanaonyesha dhamira mbaya waliyo nayo viongozi hao katika kuibomoa misingi ya Utaifa ya umoja na mshikamano, na badala yake kujenga misingi ya udini katika siasa na utawala.

Kadhalika matamshi hayo yanaonyesha dhamira yao ovu ya kujenga utawala wenye kufuata misingi ya ubaguzi wa kidini endapo watafanikiwa kushika uongozi wa nchi, ikiwa ni pamoja na kuhakikisha kuwa Uislamu unafutika kabisa katika nchi hii.

Ndugu Wanahabari, tujikumbushe kwamba Edward Lowassa anaomba awe Rais wa Tanzania kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) na mchakato wa kumfikisha huko umeratibiwa na Askofu Gwajima. Kila mmoja kati yao ameweka wazi dhamiri yake.

Wakati Ndugu Lowassa amejikita katika fikra za kupandikiza dhana ya ubaguzi wa kidini kuwa kigezo cha kuchaguliwa katika uongozi wa nchi, mwenzake Askofu Gwajima anatabiri kuwa mara tu baada ya kufanikiwa kushika hatamu za utawala, kitu cha kwanza kitakachotokea ni Misikiti kugeuka kuwa vituo vya kuwafundishia watoto imani ya Kikristo na Masheikh wote watapanga mistari kwenda kubatizwa kuwa Wakristo. Kwa maana nyingine Uislamu utafutika kabisa hapa nchini katika utawala wa Lowassa.

Ndugu wanahabari, Ushirikiano na ukaribu wa Lowassa na Askofu Gwajima si wa kuutazama kwa jicho moja tu. Tukumbuke kwamba ni Askofu Gwajima huyu huyu aliyekerwa kwa kuona Sehemu ya kuswalia Waislamu katika Uwanja wa ndege wa kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere wakati akieleza porojo zake za dhamira ya kujengwa Msikiti katika ofisi za Mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali CAG.

Ni Askofu Gwajima huyu huyu aliyekerwa na mchakato wa Mahakama ya Kadhi hadi akalazimika kutoa lugha zisizo na staha kwa watu wazima wakiwemo viongozi wakuu wa kidini hapa nchini.

kwa upande wake ndugu Lowassa huyu ndiye aliyefanikisha mkataba kati ya Serikali na Makanisa (MoU), mkataba ambao Waislamu tunaulalamikia mpaka leo hii.

Wanaposhirikiana wawili hawa pamoja na historia ya matukio yao hayo ya ‘KIBAGUZI’ kisha kila mmoja akatamka bayana maneno yanayotikisa misingi ya Utanzania na kuweka mbele ajenda zao za udini, si busara kuwanyamazia kwa maslahi ya Umoja wetu wa Kitaifa.

Haiwezi kuwa busara kwa Jamii ya Waislamu na watanzania wanaopenda amani, kukaa kimya wakati viongozi wa kisiasa na kidini kama walivyo Askofu Gwajima na Ndugu Lowassa wanatangaza hadharani nia yao ya kuivunja misingi ya utaifa na pia kukamia kuifuta dini yetu hapa nchini na kuwabatiza Masheikh nchi nzima, na kisha baada ya hapo kuigeuza Misikiti kuwa Sunday Schools za watoto wa kikristo. Hii ni dharau iliyochupa mpaka kwa dini tukufu ya Kiislamu na kwa waislamu wenyewe.

Ndugu Wanahabari, Taasisi yetu ya "Imam Bukhary Islamic Foundation" imekaa kimya kwa muda mrefu ikitafakari matukio hayo mawili ili kuona ni hatua gani stahiki zitachukuliwa kutokana na “cheche” hii ya moto wa hatari wa ubaguzi. Mwishowe tumeona tutahadharishe na kuwakumbusha Waislamu pamoja na Watanzania kwa ujumla yafuatayo:

(1) Kwa sauti ya juu Watanzania wote tumkemee na kumpinga Ndugu Edward Lowassa katika mpango wake wa kuona urais wa Tanzania unastahiki kwa zamu za Madhehebu ya dini, na tumwambie asiwagawe Watanzania kwa misingi ya kiimani

(2) Tuwakumbushe Ndugu Lowassa na Ndugu Gwajima kwamba Waislamu kamwe hawajasahau namna mchakato wa Mahakama ya Kadhi ulivyovurugwa kwa kuwatumia maswahiba wao, ambao leo hii wamejidhihirisha kuwa pamoja kwenye kambi zao za kampeni katika kuutafuta huo urais wa Tanzania, kwa dhana mbaya eti lau mchakato ule ungefanikiwa basi ungembeba mmoja kati ya wagombea wa urais.

(3) Tamko la Gwajima kuwa katika utawala ujao misikiti itageuzwa kuwa Sunday Schools za Watoto na Masheikh watakwenda kubatizwa na hivyo Uislamu kufutika hapa nchini, si tu kwamba ni maneno ya uchochezi, chuki na dharau kwa Waislamu, bali pia ni kipimo tosha kwa watanzania wote kutambua kuwa kundi hili halifai kiuongozi na ni wajibu wa kila mtanzania kumhadharisha mwenzake juu ya kumpigia kura Ndugu Lowassa na kundi lake.

(4) Kila Mtanzania anapaswa kufahamu kuwa, kumpigia kura Lowassa ni hatua moja katika kuvunja misingi ya amani na utangamano wa nchi yetu, kutokana na dhamira yake ya kuutazama uongozi wa nchi katika sura ya udini na umadhehebu. Lakini pia kila Mwislamu atambue kuwa kumpigia kura Lowassa itakuwa ni kuutimiliza utabiri wa Askofu

Gwajima wa kuwabatiza Masheikh wote Tanzania na kuigeuza Misikiti kuwa Sunday Schools kwa watoto wa kikristo.

Ni vizuri sisi Waislamu ambao ni waathirika wa mbinu chafu iliyotumika kuikwamisha Mahakama ya Kadhi, tumuulize Ndugu Lowassa: ameahidi kutatua kero kadhaa akiingia Ikulu, lakini kwanini hajapatapo kuitaja Mahakama ya Kadhi? Je, Lowassa hujui kuwa kutokuwepo kwa Mahakama ya Kadhi ni kero kwa Waislamu?

(5) Tuendelee kuhubiriana udugu wetu wa kitanzania na wale wote wenye nia mbaya tuwakemee na tuwazuwie kufikia kilele cha madaraka kitakachowawezesha kutimiza dhamira zao bila woga ili amani yetu idumu.

(6) Taasisi inajipanga kuandaa Semina maalum kwa Maimamu na baadhi ya Masheikh ili kujadili njia iliyo bora zaidi ya kujikinga na njama za wale wote ambao wanataka kulipasua Taifa letu kwa maslahi yao binafsi, wasifikie kwenye malengo yao hayo maovu.

Na tunawaomba Masheikh na Maimamu wa Misikiti yote Tanzania pamoja na Waislamu wote kushiriki kuwazindua Waumini kila pahala kote nchini kuwazindua Wananchi kwa ujumla juu ya hatari ya kuwaweka juu ya uongozi wa nchi yetu watu wenye dhamira ya kujenga dhambi ya ubaguzi wa kidini ambayo ni kansa itakayokula mwili wa Taifa na hatimaye kuliangamiza kabisa.

Ahsanteni kwa kunisikiliza.

Sheikh Khalifa Khamis

MWENYEKITI,
TAASISI YA KIISLAMU YA IMAM BUKHARY
(IMAM BUKHARY ISLAMIC FOUNDATION)
24/09/2015

Picha za MAFURIKO Ya Magufuli Kahama............Maelfu Wahudhuria Mkutano Wake

$
0
0

Mgombea wa Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kutoka Chama Cha Mapinduzi Dk. John Pombe Magufuli akiwasili kwenye uwanja wa Milango 10 tayari kuhutubia maelfu ya wakazi wa mji wa Kahama waliojitokeza kwa wingi kwenye mkutano wa kampeni za CCM.
  Mgombea wa Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kutoka Chama Cha Mapinduzi Dk. John Pombe Magufuli akiruka kutoka kwenye gari wakati akiwasili kwenye uwanja wa mkutano mjini Kahama.
  Mgombea wa Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kutoka Chama Cha Mapinduzi Dk. John Pombe Magufuli( wa tatu kutoka kushoto) akiongoza meza kuu kumuombea mapumziko mema mgombea wa Ubunge wa Jimbo la Ulanga Mashariki Mhe. Celina Kombani aliyefariki nchini India tarehe 25 Sept.
  Mgombea wa Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kutoka Chama Cha Mapinduzi Dk. John Pombe Magufuli akiwachangamsha wakazi wa Kahama kwa kuimba nao nyimbo za hamasa wakati wa mkutano wa hadhara wa kampeni za CCM uliofanyika kwenye uwanja wa Milango 10.
  Mgombea wa Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kutoka Chama Cha Mapinduzi Dk. John Pombe Magufuli akienda sambamba na wakazi wa mji wa Kahama.
 Wananchi wakiwa wamebanana kabisa kumuona  Mgombea wa Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kutoka Chama Cha Mapinduzi Dk. John Pombe Magufuli
  Mgombea wa Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kutoka Chama Cha Mapinduzi Dk. John Pombe Magufuli akihutubia wakazi wa mji wa Kahama na kuwaahidi ataubadilisha mji huo na kuwa wa kisasa na wenye maendeleo zaidi.
  Mgombea wa Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kutoka Chama Cha Mapinduzi Dk. John Pombe Magufuli akiwaambia wananchi wa Kahama kuwa atawafanyia kazi Watanzania wote bila kujali Itikadi zao za vyama.
 Hivi ndivyo mkutano wa Kahama wa  Mgombea wa Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kutoka Chama Cha Mapinduzi Dk. John Pombe Magufuli ulivyofurika.
 Wakazi wa Kahama mjini wakiwa wametosha kwenye mkutano wa kampeni za  Mgombea wa Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kutoka Chama Cha Mapinduzi Dk. John Pombe Magufuli
 Chegge na Temba wakitumbuiza kwenye mkutano wa kampeni za  Mgombea wa Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kutoka Chama Cha Mapinduzi Dk. John Pombe Magufuli kwenye uwanja wa Milango 10.
 Chegge na Temba wakishambulia jukwaa kwenye mkutano wa kampeni za  Mgombea wa Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kutoka Chama Cha Mapinduzi Dk. John Pombe Magufuli
 Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi na Mjumbe wa Kamati Kuu CCM Taifa Ndugu Alhaji Abdallah Bulembo akiwahutubia wakazi
 Mjumbe wa Kamati ya Kampeni za CCM Mhe.Samuel Sitta akihutubia wakazi wa Kahama mjini wakati wa mkutano wa kampeni wa  Mgombea wa Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kutoka Chama Cha Mapinduzi Dk. John Pombe Magufuli
Wasanii wa Yamoto Band wakitumbuiza kwenye mkutano wa kampeni za  Mgombea wa Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kutoka Chama Cha Mapinduzi Dk. John Pombe Magufuli.

Shuhudia GHARIKA La LOWASSA Ndani Ya Mji wa Mereraji,Simanjiro Mkoani Manyara Jana

$
0
0

Mgombea Urais wa Tanzania wa UKAWA kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Edward Lowassa, akiwahutubia wananchi wa Mji wa Mererani, katika Mkutano wa Kampeni zake, uliofanyika kwenye uwanja wa Machinjioni, Simanjiro Mkoani Manyara jana Septemba 25, 2015.

Sehemu ya Wananchi wa Mji wa Mererani, Jimbo la Simanjiro Mkoani Manyara wakionyesha furaha yao mbele ya Mgombea Urais wa Tanzania wa UKAWA kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Edward Lowassa, wakati akiwahutubia katika Mkutano wa Kampeni zake, uliofanyika kwenye uwanja wa Machinjioni, Mererani, jana Septemba 25, 2015.
Meneja wa Kampeni za Mgombea Urais wa Tanzania wa UKAWA kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Edward Lowassa, John Mrema akizungumza na Wananchi wa Mji wa Mererani, Jimbo la Simanjiro Mkoani Manyara. 
Waziri Mkuu wa Zamani, Mh. Fredrick Sumaye, akipokea kadi za wanachama wa CCM walioamua kurudisha kadi na kujiunga na UKAWA, wakati wa Kampeni za Mgombea Urais wa Tanzania wa UKAWA kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Edward Lowassa, uliofanyika kwenye uwanja wa Machinjioni, Mji wa Mererani, Simanjiro Mkoani Manyara jana Septemba 25, 2015.

Waziri Mkuu wa Zamani, Mh. Fredrick Sumaye, akizikusanya kadi hizo baada ya kuzipokea.

Utafiti wa TADIP Urais 2015 wampa Lowassa ushindi Lowassa kwa 54.5% dhidi ya Magufuli (40%)

$
0
0
 Utafiti wa TADIP Urais 2015 wampa Lowassa ushindi Lowassa kwa 54.5% dhidi ya Magufuli (40%)
Katika Utafiti huo uliosomwa Jana Mbele ya Waandishi wa Habari Pale Hotel ya Regency

Lowassa Ameongoza kwa Asilimia 54.5% , Magufuli 40%, Anna Mughwira 2%, Rashidi Rungwe 0.4%, Chief Yemba 0.1%, Sijui 3%


Kwa Haya Anayonifanyia Shemeji Ananitaka au Mawazo Yangu Tu?

$
0
0
Wadau nipo nyumbani kwa takribani mwezi sasa baada ya kumaliza mkataba wangu na kampuni flani.sasa hapa nyumbani ninaishi na wife na kidi wangu wa miaka 3..na nimekuta wife kamleta mdogo wake wa kike ambaye amemaliza chuo mwaka jana anasubiria ajira,sasa wadau wife wangu ni mfanyakazi so mida mwingi anashinda job,mimi nipo tu home na shemeji yangu,kid anapelekwa shule asubuh mpska jioni.shem huyu wadau ni mrembo sana ana figure matata sana na ni mzuri kwa kweli..yani mitihani ninayoipata ni mikubwa sana..mana nguo anazo vaa zinaonenya umbo lake namba 8 lilivyo,juzi asubuh nilikuwa nimelala akagonga chumbani kwangu anatafuta kitu wakati kavaa khanga tu.jamani naombeni ushauri wenu nifanyaje je?maana uzalendo unaelekea kunishinda asee.maana sasa imefika wakati naliota umbo lake na uzuri wake nimechanganyikiwa.naombeni ushauri weni wadau.

Asanteni

By Fukara

Nay wa Mitego Amvaa January Makamba..Adai January Ndio Mnunuzi Mkuu wa Akina Dr Slaa, Lupumba, Twaweza na Wasanii

$
0
0
Msanii  wa  bongo  fleva, Nay  wa  Mitego  amemvaa  mjumbe  wa  kamati  ya  Kampeni  ya  CCM,January  Makamba  na  kudai  yeye  ni  mnunuaji  mkuu  wa  tafiti  na  wasanii  kwa  lengo  la kukisaidia  chama  chake.

Nay  alimjibu  January  Makamba  aliyepost  ujumbe  ukionyesha  kushangaa  tuhuma  dhidi  ya  CCM  kuwa  imekuwa  ikinunua  wanasiasa,tafiti  pamoja  na  wasanii  kwa  lengo  la  kuulaghai  umma.

"Zitto kanunuliwa. Slaa kanunuliwa. Lipumba kanunuliwa. Twaweza imenunuliwa. Synovate imenunuliwa. Wasanii wamenunuliwa. Tuwe creative kidogo"Aliandika  January  Makamba.

"Ni kabisaa kwani uongo? We ndo mnunuzi mkuu. Bro kama ubunifu ni hela basi we Master wa Ubunifu... @JMakamba Ongeza ubunifu bro" Alijibu  Nay  wa  Mitego




Picha: Tiffah alivyoiongezea furaha familia ya Zari Afrika Kusini

$
0
0
Pamoja na kuwa ni watoto wa baba tofauti, watoto wa kiume wa Zari wamempokea kwa furaha kubwa Tiffah, mtoto wa Zari the Bosslady.
11356678_969639193088473_1391727929_n
Zari kwenye picha hii ameandika: If anybody ever said perfect doesn’t exist, they were wrong. It surely does!!!! Look at my ‘perfect’ lil life
Baada ya Tiffah kufikisha siku 40, sasa ni muda wa kuonana na kaka zake hao watatu wanaoishi nchini Afrika Kusini.
12063067_504973169676808_876703061_n
Mrembo huyo wa Uganda mwenye makazi yake South ameendelea kushare picha zinazowaonesha wanae wakicheza kwa upendo mkubwa na mdogo wao Tiffah.
10818117_470942569733664_1896259450_n
Katika picha nyingine aliyoshare jana Zari aliandika, “Someone didn’t move an inch… spent half of his night just staring,” ameandika Zari kwenye picha hiyo.
Zari na Tiffah walielekea Afrika Kusini wiki hii baada ya kukaa Tanzania kwa kipindi cha miezi takriban mitatu tangu akiwa mjamzito.
928864_131838347170081_262449761_n
Tiffah akifurahia usingizi kwenye ndege wakati yeye na mama yake wakiwa safarini Afrika Kusini

Magufuli Aigeuzia Kibao Taasisi ya Utafiti Iliyompa Ushindi wa Urais..Adai Amepunjwa Asilimia

$
0
0
Kahama. Mgombea urais wa CCM, Dk John Magufuli amesema waliofanya utafiti wamempunja asilimia kwani ana uhakika wa kushinda kwa asilimia 95 na si 65 kama zilivyotajwa kwa kuwa wananchi wanampenda, naye yuko tayari kufanya kazi ili kuwaletea maendeleo.

Akizungumza jana mjini Kahama, Dk Magufuli alisema: “Wapo wanaosema nimeshinda kwa asilimia 65, mimi ninasema nitashinda kwa asilimia 95, ninachoomba mjitokeze kwa wingi siku ya kupiga kura ili nitangazwe mshindi, ninawaahidi kwamba nitawatumikia na kujenga Tanzania mpya.”
Hivi karibuni, taasisi ya Twaweza ilitoa utafiti wake uliompa nafasi ushindi wa asilimia 65 huku mpinzani wake, Edward Lowassa akipata asilimia 25 na mgombea wa ACT –Wazalendo akipata asilimia 0.3.
Baadaye, taasisi ya Ipsos (Synovate) ilitoa utafiti wake ukionyesha kwamba alishinda kwa asilimia 62 huku Lowassa akipata asilimia 31 na Anna Mghwira akipata asilimia 0.3.


Esther Bulaya..Kwa Sasa Nimemdhibiti Wassira Pamoja na Mbinu zake Chafu za Kunipoteza Kisiasa

$
0
0
MGOMBEA ubunge anayewakilisha Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA) jimbo la Bunda mjini, mkoani Mara, Esther Bulaya anajivuna kuwa amefanikiwa kumdhibiti mpinzani wake mkubwa katika uchaguzi mkuu, Stephen Wassira.

Akizungumza na MwanahalisiOnline, Bulaya ambaye alikuwa mbunge wa Viti Maalum akitokea Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM), amesema kwamba amedhoofisha ngome ya Wassira, ambaye amekuwa kiongozi serikalini tangu awamu ya kwanza ya Mwalimu Julius Nyerere.

“Kulikuwa na matukio ya mikutano yetu kuvamiwa, wafuasi wetu kuvamiwa na kubambikiziwa kesi, hata hivyo tulijipanga na kudhibiti huku tukishirikiana na Jeshi la Polisi,” anasema akizungumzia mikakati iliyopangwa kumkwamisha kukubalika kwa wananchi.

“Ninavyoongea na wewe gari yangu ipo Polisi kwa madai kuwa imehusika na uhalifu wa kutumia silaha, dereva wangu pia anashikiliwa lakini wananchi kwa hasira wamenipatia gari sita za kampeni,” anasema Bulaya aliyejiunga Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) baada ya kuhama CCM mara tu bunge lilipovunjwa.

Bulaya ambaye pia kitaaluma ni mwandishi wa habari, amesema mpaka jana ameshafanya kampeni katika Kata 14 za jimbo hilo huku akipita kila kijiji na kila kitongoji na sasa anatarajia kuanza awamu ya pili ya kampeni akiwa ameimarika zaidi.

Kuhusu upinzani anaokumbana nao kutoka kwa Wassira, Bulaya anasema “pamoja na mbinu chafu dhidi yangu nipo imara sana, ninamkabili kisawasawa na anakosa watu kwenye mikutano mingi.”

Jimbo la Bunda mjini ni moja ya majimbo yenye upinzani mkali likishikiliwa na Wassira ambaye ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Uhusiano), aliyewahi kuwa NCCR-Mageuzi na kushinda ubunge kabla ya kuvuliwa na Mahakama Kuu kwa kosa la kununua kura. Alikuwa ameshindana na Joseph Warioba wa CCM.

Sumaye Ampa Makavu Magufuli......Lowassa Aahidi Kudhibiti Rushwa Ndani ya Siku 100

$
0
0
Jana  ilikuwa ni Septemba 26  ambapo  UKAWA waliendelea  na  mikutano  yao  ya  kampeni  za kuomba  ridhaa  ya kuchaguliwa na  wananchi .Jana  ilikuwa  ni  zamu  ya  wakazi wa Wilaya ya Hai ambapo  Waziri  Mkuu  wa  zamani, Fredrik Sumaye aliendelea na kazi ya kupangua mashambulizi ya CCM.


Sumaye aliitumia siku ya jana kumjibu Dk Magufuli aliyesema kuwa utafiti uliofanywa na Twaweza unaoonyesha anaongoza kwa asilimia 65, umempunja ushindi aliostahili.

Sumaye alisema Dk Magufuli hawezi kupata hata asilimia 40 ya kura na ndiyo maana amekuwa akitofautiana na mwenyekiti wake Rais Jakaya Kikwete.

Akizungumza katika mkutano huo wa kampeni uliofanyika Rundugai, Jimbo la Hai, Sumaye alisema Dk Magufuli amekuwa akikisahau hata chama chake na kuwataka wananchi wachague Tanzania ya Magufuli, huku akiomba wananchi wasichome godoro lote lenye kunguni badala yake waue kunguni waliopo kwenye godoro hilo.

“Haiwezekani mkalalia kitanda chenye kunguni si ndiyo,” alihoji Sumaye na kuitikiwa na wananchi “ndiyoooooo”.

“Amesahau hata kusema chagua CCM, anasema chagua Tanzania ya Magufuli,” alisema Sumaye na kuongeza kuwa Tanzania haiwezi kuwa ya Magufuli, bali ni ya Watanzania wote.

Sumaye alisema kuwa hali ya CCM ni mbaya na ndiyo maana wananchi wamechoka na hali zao ni mbaya.

“Wananchi wanataka mabadiliko, hakuna vita itakayotokea kama wanavyohubiri huo ni upuuzi mtupu,” alisema Sumaye.

Sumaye aliwaambia wananchi hao wa Rundugai kuwa nchi nyingi duniani zinapata mabadiliko kwa kubadilisha mfumo uliopo, hivyo wananchi wasiogope kwa kuwa CCM siyo mama yao, bali ni chama cha siasa.

Lowassa  Aahidi  Kudhibiti  Rushwa  Ndani  Ya  Siku 100
Wakati Sumaye akisema hayo ,mgombea urais kwa tiketi ya Chadema, Edward Lowassa  aliahidi kuhakikisha  anapambana na tatizo la rushwa ambalo limekuwa chanzo cha umasikini nchini.

"Siku 100 za serikali ya Chadema, tutaunda chombo kila wilaya ambacho kitakuwa ‘one stop centre’. Ukienda mjini kwa shughuli za kiserikali huduma zote zitakuwa sehemu moja, hii itaondoa urasimu na rushwa." Alisema  Lowassa.

Huku akionekana kujiamini kushinda katika chaguzi ujayo,Lowasa alisema atahakikisha anaongoza nchi kwa misingi ya haki na usawa huku akiahidi kutumia vema ilani ya ukawa kuhakikisha anapambana na rushwa.

Alisema kwa mara ya kwanza nchini Tanzania upinzani utachukua nchi  na  akasisitiza  kuwa  CCM  lazima  Ing'oke  mwaka  huu.

"CCM  lazima  ing'atuke  mwaka  huu, lakini  itang'atuka  kwa  kura  zenu, hivyo  nawaombeni  mtunze  sana  vichinjio  vyenu." Alisema  Lowassa  na  kuongeza;

“Wale wenzangu waliochukia mimi kuondoka CCM, sasa wameanza kukubali uamuzi wangu kwa kuwa CCM imeshindwa kuongoza nchi, haifai tena kuongoza kama Sumaye alivyosema.Hali ya wananchi ni mbaya sana."

Lowassa aliendelea kurudia ahadi zake za elimu bure kuanzia msingi hadi chuo kikuu, pia kuboresha maisha ya Watanzania waondokane na umaskini ambao kila siku amekuwa akisema anauchukia.

Katika mkutano huo, Lowassa alimsihi Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe kuendelea kuambatana naye kwenye kampeni ili aongeze nguvu kwenye timu yake.

Lowassa alisema Mbowe anaweza kufanya kampeni zake kwenye Jimbo la Hai na kuweka timu ambayo itamsaidia wakati atakapokuwa nje ya jimbo kumpigia kampeni mgombea urais.

Akizungumza kwenye mkutano huo, Mbowe aliiponda CCM akisema kwa sasa haijielewi kwa kuwa iko hoi.

Alisema katika uchaguzi huu hawatakubali kuibiwa kura huku akiwaomba askari wakae pembeni ya siasa na kulinda amani ili wanasiasa wacheze ngoma yao wenyewe.

“Askari wetu lindeni amani tuachieni CCM tucheze nao msipendelee upande wowote,” alisema Mbowe.

Makongoro Nyerere Awakera Wapiga Kura Kwa Matusi yake Jukwaani..Adai Ikulu Hakuna Makaburi, Lowassa Anaumwa Kuna Uwezekano Akafikia Ikulu

$
0
0
BAADHI ya wakazi wa mji wa Dodoma wameeleza masikitiko yao juu ya matusi na kashifa zinazotolewa na viongozi wa CCM dhidi ya wahasimu wao Chadema.

Hali hiyo ilijitokeza juzi ambapo Makongoro Nyerere aliweka sera za CCM pembeni na kuanza kutoa kashfa kwa wagombea wa vyama vya siasa hususani Mgombea Urais wa Chadema, Edward Lowassa na mgombea Ubunge Benson Kigaila.

Akihutubia katika mkutano wa Kampeni wa mgombea ubunge CCM katika viwanja vya Kikuyu Kusini, Makongoro badala ya kutangaza sera za chama chake alianza kwa kashfa na kudai Ikulu hakuna makabuli hivyo Lowassa anaumwa na kuna uwezekano akafia Ikulu.

Makongoro akimnadi Anthon Mavunde, alitumia muda mwingi kutoa kashfa kwa wagombea wa UKAWA huku akidai Lowassa asichaguliwe kuwa rais kwani afya yake mbaya hivyo anaweza kutofanya majukumu yake.

Mbali na hilo amesema Ikulu siyo wodi ya wagonjwa na sehemu ya makaburi hivyo ni vyema mtu anayetakiwa kwenda Ikulu ni mtu mwenye nguvu.

“Mimi sasa sitaki kuendelea kumsema Lowassa maana akifa watasema mimi ndiye niliyemuua hata hivyo nawashangaa watu wa UKAWA wana roho ngumu sana kutembea na   mtu ambaye amechoka vile.

“Chadema wanatakiwa kushitakiwa ni maajabu sana kuona na watu wasivyo na huruma wanamtesa sana baba wa watu hata hawezi kuzungumza majukwaani na sera anamwachia Lissu (Tundu),” amesema Makongoro.

Kutokana na hali hiyo wakazi wa Dodoma wamesema watanzania wanataka kusikiliza sera na siyo vinginevyo.

Mmoja wa wananchi wa Kikuyu Kaskazini ambaye alijitambulisha kuwa ni kada wa CCM na kukataa jina lake litajwe alisema ana mashaka na wana CCM huenda wana mpango wa kuua chama.

Alisema haiwezekani viongozi wa CCM badala ya kutangaza sera wao wanajielekeza katika matusi na kashifa,mambo ya afya ya mtu anaijua Mungu mwenyewe.

Here is That Video of CORAZON KWAMBOKA That Kenyan Men Must See in Their Privacy

$
0
0

After that drama last week from her father and the gossip around her family life, Corazon Kwamboka will want Kenyans to forget how embarrassed her father is and the best thing to do for her is to shake what her mama gave her for men.

Watch this video below;


Magufuli Awataja LIVE WanaCCM Wanaomsaliti Huku Wakimsanifu Kuwa Wanamuunga Mkono

$
0
0
Mgombea Urais kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM), Dk. John Magufuli, jana aligeuka mbogo baada ya kuamua kuwataja hadharani watu wanaohujumu kampeni zake kwa kujifanya mchana wako pamoja na usiku wakigeukia upande wa upinzani.

Akiwahutubia wananchi wa mkoani Shinyanga jana katika mkutano wake wa kampeni uliofanyika katika Uwanja wa CCM Kambarage, Dk. Magufuli, alisema kuna mamluki wanaokihujumu chama hicho katika kuelekea uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 25, mwaka huu.

Dk. Magufuli aliwataja hadharani baadhi ya makada hao ambao wamekuwa wakiipigia kampeni CCM mchana na usiku wakiwapigia wapinzani.

 “Kuna baadhi ya wana-CCM wanatujuhumu sana, wengine nawajua hata majina yao bahati nzuri huwa sisemi uongo bali ukweli, kuna huyu Gasper mchana tunakuwa naye CCM lakini usiku anaungana na wapinzani,” alisema.

Hata hivyo, kauli hiyo ya Dk. Magufuli ilipokelewa kwa mshangao na  baadhi ya wananchi na wanachama waliokusanyika uwanjani hapo, kwa kuwa baadhi ya makada hao walikuwa wameketi jukwaa kuu wakifuatila hotuba yake.

Mwandishi wa habari hizi alimshuhudia meneja kampeni wa mgombea huyo, Abdallah Bulembo, akimfuata Magufuli na kumnong’oneza ghafla Magufuli alibadilisha na kudai msaliti ni Gasper Anthony wala si Gasper Kileo aliyetajwa awali.

Hata hivyo, Magufuli  baada ya kumaliza hotuba yake alimfuata kada huyo na kumkumbatia huku akimtuliza na kuendelea na msafara wake.

Kada huyo aliyetajwa kuwa msaliti anadaiwa awali kuwa mpambe wa mgombea wa urais kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Edward Lowassa, anayeungwa mkono na vyama vinavyunda Umoja wa Katiba (Ukawa).

Akizungumza katika mkutano huo wa kampeni, Kileo alisema alimuunga mkono Lowassa akiwa CCM, lakini kwa sasa anamuunga mkono mgombea urais wa chama hicho, Dk. Magufuli na wala kwa kilichotokea hatarajii kukihama chama.

Akiwahutubia mkoani Shinyanga, Magufuli amesema hashangai wananchi kuanza kumwita rais kwasababu hata yeye anajua kuwa ndiye atakayeibuka na ushindi mnono kwenye Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 25, mwaka huu.

Alisema wagombea wengine wa nafasi ya urais ni wasindikizaji tu kama walivyo wapambe wa kwenye harusi.

Swizz Beatz ameikubali ‘Nana’ ya Diamond Platnumz, amepost video mtoto wake alivyoicheza.. (+Video)

$
0
0
Rapper na producer wa muziki toka Marekani, Swizz Beatz ni kama midundo ya Afrika ameanza kuikubali sana sasahivi.. kuna siku alipost yeye pamoja na mpenzi wake, Alicia Keys vipisi vya video wakienjoy midundo ya kwenye album ya staa wa Muziki toka Nigeria, Wizkid.

Muda mfupi uliopita jamaa kapost tena kipande cha video ya mtoto wake akiwa anacheza wimbo wa Diamond Platnumz, ‘Nana’ Feat. Mr. Flavour… kwenye post hiyo Swizz ameandika >>> “Vibes 💃👸 song by@diamondplatnumz #goodvibes” >>> @therealswizzz
A video posted by therealswizzz (@therealswizzz) on

Magufuli Azomewa Jijini Mbeya.....Wananchi Wasema Wanamtaka Lowassa. Hapa kuna Video Mbili

$
0
0





Katika  hali  isiyo  ya  kawaida,Mgombea  Urais  kwa  tiketi  ya  CCM, Dr. John Magufuli  leo  alijikuta  katika  wakati  mgumu  baada  ya  kukutana  na zomea zomea  ya  kundi  la  vijana  waliovamia  msafara  wake  akiwa  njianI  kuelekea  Mbarali  na kuanza  kuimba wakidai  Lowassa  ndo  Rais  wao....Tazama  Video hii

Pamoja  na  kadhia  hiyo,Magufuli  alifanikiwa kufika  Mbarali  na  kuhutubia  maelfu  ya  wananchi  ambao  amewaahidi  kushughulikia  migogoro  yao  ya  muda  mrefu  ambayo  imekuwa  kete  ya  kuombea  kura  kwa  baadhi  ya  wanasiasa  wenye  uchu  wa  madaraka. Tazama Na Hii

Dr. Magufuli  leo  pia  amefanya  mikutano  kadhaa  ya  kampeni  mkoani  Iringa  ambako  alilazimika  kumalizia  viporo  hivyo vilivyokuwa  vimebaki  mkoani  humo. 
Wananchi kwa maelfu wakimsikiliza Mgombea Urais kwa tiketi ya CCM Dkt. John Pombe Magufuli akihutubia huko Makambako mkoani Iringa ambako alipita leo kumalizia viporo vya mkoa huo kwenye kampeni zake.



Wagombea wa nafasi mbalimbali wa Mafinga wali-Magufulika mbele ya Mgombea Urais kwa tiketi ya CCM Dkt. John Pombe Magufuli katika jimbo la Mafinga mkoani Iringa ambako alipita leo kumalizia viporo vya mkoa huo kwenye kampeni zake.

Source:Mpekuzi Huru

RAY: Heshimuni Maamuzi Yangu ya Siasa...Nyinyi Tukaneni Mpaka Mchoke Maana Hata Mkwaruzo Sijapata

$
0
0
(  FREEDOM OF SPEECH )
Nyinyi tukaneni mpaka mchoke maana tangia muanze kutukana matusi hata mkwaruzo sijapata msinilazimishe kupenda mnachokipenda nyinyi. Heshimuni maamuzi yangu kwani kila mtu ana haki ya kufanya maamuzi anayoyaona kwa upande wake ni sahihi, nasema hivi wananchi wana akili timamu hawawezi kuwapa ridhaa ya kuongoza nchi hii kama wenyewe kwa wenyewe mnagombana mtaweza ongoza nchi hii mnavyoona watu wanajaa kwenye mikutano yenu mnafikiri mnapendwa hao wamekuja kuwashangaa mawaziri wakuu wawili waliohama chama tawala alafu kabila moja nasemaje kama umeshindwa kuiongoza familia yako utaiweza ya mwenzako amuwezi pata madaraka ya nchi. komaeni kwanza kisiasa labda miaka amsini ijayo ndio tuwafikirie kuwapa nchi baada ya kujiridhisha kama mshakomaa kisiasa. Over....Ray

Viewing all 104747 articles
Browse latest View live




Latest Images