Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104429 articles
Browse latest View live

Completely Shocking! This is What University Girls are Doing Behind Closed Doors

0
0

Do you have a daughter or a sister who is currently in University? If yes, then be very weary. You might think they are busy studying but that might not be the case.

These University girls are busy doing all manner of things which would even make the devil’s jaw drop all the way to the ground.

 Things that would make you start thinking the world is coming to an end.

This is what I’m talking about:


Ben Pol Aeleza Kwanini Hataki Kuonekana na Mpenzi Wake kila Wakati

0
0
Ben Pol amesema ataamua kutembea kila sehemu na mpenzi wake baada ya kuona anakaribia kufunga naye ndoa.

Ben Pol ameiambia Bongo5 kuwa, kitu anachoogopa ni kuonekana mara kwa mara na mtu halafu siku chache watu wasikie wameachana.

Kusema ukweli nahisi bado,” amesema. “Unajua mpaka uanze kutembea na mtu kwenye public mpaka ujiridhishe vitu fulani fulani na labda muwe kuna hatua fulani mmefika. Uchumba nini ndoa, sio unatembea na mtu na kumuonyesha kumbe mna migogoro. Kwahiyo lazima vitu muhimu vifanyike kwanza, mauchumba na pete na baadaye ndoa inakaribia ndio mnaweza kufanya hivyo,” ameongeza Ben Pol.

UTABIRI wa Mgombea Urais TZ Kufariki Kabla ya Oktoba 25 Umetimia?! Haya Ndio Majibu ya MAALIM Hussein!

0
0
MTABIRI maarufu nchini, Maalim Hassan Yahya Hussein, amesema utabiri wake alioutoa mwaka 2014 kwamba mgombea urais mmoja atafariki dunia ghafla kabla ya uchaguzi, umetimia baada ya kifo cha Mchungaji Christopher Mtikila na kuwaacha salama wagombea Edward Lowassa na Dk. John Magufuli.
Maalim Hassan aliyasema hayo alipozungumza na gazeti hili juzi ambapo alisisitiza kuwa utabiri wake alioutoa Desemba 28, 2014 katika mkutano wake na waandishi wa habari ofisini kwake, haukumlenga mtu.

Mchungaji Mtikila ambaye alikuwa akigombea urais kupitia Democratic Party (DP) kabla ya kuenguliwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (Nec), alifariki dunia Oktoba 4, 2015 kwa ajali ya gari kijijini Msolwa, Chalinze, mkoani Pwani akitokea Njombe.
“Nilipoutoa utabiri ule mengi yalisema na watu wakawataja wagombea fulani, lakini niliwaambia kwamba utabiri haulengi mtu na sasa umempata Mchungaji Mtikila.
“Mtikila alikuwa mgombea urais, alichukua fomu na watu wakaona akiwa na mkoba kama wa wagombea wenzake, akakataliwa na tume lakini akakata rufaa… angeweza pia kushinda rufaa yake,” alisema Maalim Hassan.
Aliongeza kuwa, mara baada ya utabiri wake alipigiwa simu na makada wa vyama viwili – Chama cha Mapinduzi (CCM) waliodai kuwa mgombea wao Dk. Magufuli haumhusu na wale wa Chadema nao wakasema mgombea wao, Lowassa hawezi kuchuliwa hivyo – akawajibu wote kwamba utabiri wake haumlengi mtu.
“Niwahakikishie wananchi kwamba, kinyota wagombea wote wa urais waliobaki sasa wako salama na watashiriki kuchagua viongozi Oktoba 25, mwaka huu,” alisema Maalim Hassan.

Christopher Ole Sendeka Akerwa na Tabia ya Vijana Kupiga Deki Barabara Ili LOWASSA Apite.......Asema Huo ni Sawa na Utumwa

0
0
Mjumbe wa kamati ya kampeni ya chama cha  Mapinduzi, Christopher Ole Sendeka amelaani kitendo cha mgombea urais wa Chadema, Edward Lowassa kuruhusu vijana kusafisha barabara ya lami ili msafara wake upite akidai  kuwa  huo  ni  utumwa.

Ole Sendeka  alitoa  kauli  hiyo  jana  wakati  akiwa katika mkutano wa kumnadi mgombea mwenza wa CCM, Samia Suluhu Hassan mjini Geita.

Juzi mjini Musoma na jana Jijini Mwanza walijitokeza vijana na kupiga deki barabara ili Lowassa apite, wakisema hawataki apate mafua.

Sendeka jana alikemea kitendo hicho katika mikutano kadhaa mkoani Geita akisema, “Lowassa anatumia umaskini wa vijana wetu kuwalipa fedha ili wamwage maji kwenye barabara ya lami kusafisha barabara msafara wake upite. Huo ni utumwa si utumwa?” aliuliza Sendeka na kujibiwa na wananchi kwa sauti, “Ni utumwa.”

“Namtaka Lowassa asitumie nafasi yake ya ugombea urais kudhalilisha utu wa vijana kwa sababu ya fedha zake, tena ambazo hakuzipata kihalali kuwalipa vijana wetu eti wakamsafishie barabara ya lami apite,” alisema.

Sendeka alisema kitendo hicho cha aibu kimeona matairi ya gari la Lowassa yana thamani kuliko utu wa vijana.

“Kama kweli hakufadhili mpango huo wa kulipa vijana wafanye hivyo kwa nini hakuwakataza alipoona wanamwaga maji ili msafara wake upite,” alihoji.

Shindano la Serengeti Masta Lawasha Moto Ulaya Ulaya Bar ya Manzese

0
0

Mshereheshaji wa shindano la Serengeti Masta Razani Kapalatu akitoa zawadi ya fulana kwa mkazi wa Manzese na mpenzi wa bia ya Serengeti Premium Lager Rodgers Robert wakati wa promosheni ya kumtafuta Serengeti Masta iliyofanyika katika baa ya Ulaya Ulaya ya Manzese jijini Dar es salaam. Promosheni hiyo ya bia ya Serengeti Premium Lager imezifikia baa zaidi ya mia tano kwa mikoa minne ambayo ni Dar es salaam, Arusha, Mwanza na Mbeya na kufanikiwa kutoa elimu juu ya bia hiyo na ubora wake.

Mkazi wa Manzese jijini Dar es salaam Joachim Mwale (kushoto) akishiriki  kwenye droo ya kumtafuta “Serengeti Masta” wa baa ya Ulaya Ulaya iliyopo Manzese jijini Dar es salaam wakati promosheni hiyo ilipofunga kambi ndani ya baa hiyo mwishoni mwa wiki. (Kulia) ni Mshereheshaji wa shindano hilo Masta Razani Kapalatu.
Mshereheshaji wa shindano la Serengeti Premium Lager liliopewa jina la “Serengeti Masta” Razani Kapalatu akiwa pamoja na mabalozi wa bia ya Serengeti premium Lager ambao kwa pamoja walitoa maelezo kwa wateja wa bia hiyo waliofika kushiriki katika shindano la kumtafuta Serengeti Masta ndani ya baa ya Ulaya Ulaya iliyopo Manzese jijini Dar es salaam mwishoni mwa wiki. Shindano hilo limedumu jijini Dar na mikoani kwa takriban muda wa miezi miwili sasa na kuweza kuzifikia baa mbalimbali ambapo zawadi mbalimbali kama fedha taslim, fulana na bia za bure zimekuwa zikitolewa katika kuwahamasisha wateja wa bia hiyo kuendelea kuwa pamoja.

Mshereheshaji wa shindano la Serengeti Masta Razani Kapalatu( akionyesha kiasi cha Tsh. 50,000/= alichomkabidhi mshindi wa shindano la Serengeti Masta ambaye aliitambua ladha halisi ya bia ya Serengeti Premium Lager wakati wa promosheni hiyo iliyofanyika katika baa ya Ulaya Ulaya iliyopo Manzese jijini Dar es salaam. (Kushoto) ni mteja aliyeibuka “Serengeti Masta” wa baa hiyo ambaye alifahamika kwa jina la Doris Frances.



Mshindi wa shindano la Serengeti Masta Doris Frances (kushoto) kwenye picha ya pamoja na marafiki zake mara baada ya kuibuka bingwa wa kuitambua ladha halisi ya bia ya Serengeti na kukabidhiwa zawadi ya Tsh 50,000 wakati wa promosheni hiyo iliyofanyika mwishoni wa wiki katika baa ya Ulaya Ulaya iliyopo Manzese jijini Dar es Salaam.

Breaking News: Balozi Juma Mwapachu Leo Ametangaza Kujivua Uanachama wa CCM. Amedai Chama Kimepoteza Dira

0
0
Treni ya mabadiliko inazidi kuongeza speed katika hizi dakika za lala salama. Kesho Balozi mwenye heshima tele ndani na nje ya Tanzania, Juma Mwapachu anaachana na Chama Cha Mapinduzi.

Hii ni siku kadhaa baada ya Mkongwe wa TANU/CCM Kingunge Ngombale Mwiru kukimbia ndani ya chama hicho kwa kile alichokisema CCM imechoka, hakiwezi kuleta mabadiliko hivyo ni lazima ipumnzishwe kwanza ili ipate pumzi upya.

Mwapachu ni moja wa wasomi, na balozi mwenye heshima kubwa ndani na nje ya nchi. Na kwa kweli kuondoka kwake ni pigo kubwa sana kwa CCM, hasa linapokuja suala la kumanage mabalozi wa nje. Mwapachu anaheshimika sana na mabalozi wa nje hasa Marekani na nchi za Ulaya.

Treni la mabadiliko linazidi kuongeza kasi zaidi. Huku CCM hali ikizidi kuwa tete.


TAMKO RASMI LA BALOZI JUMA V. MWAPACHU.

NAJIVUA UANACHAMA WA CCM

Ndugu zangu,

Kesho ni siku muhimu katika kalenda ya Taifa letu. Tunamkumbuka marehemu Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere aliyetutoka miaka 16 iliyopita. Nadhani ni siku mwafaka kwangu kufanya maamuzi magumu katika maisha yangu ambayo yanahusu uanasiasa wangu. Mimi ni mwanachama wa CCM tangu mwaka 1967 wakati nilipojiunga na TANU Youth League. Nimepata fursa ya kuwa kiongozi ndani ya Chama hiki. Lakini kuanzia kesho mimi si mwanachama wa CCM tena. Natoa maelezo yafuatayo:

Kwa kipindi chapata mwezi na nusu hivi sasa mmekuwa mkisoma makala zangu kuhusu msimamo na mwelekeo wangu katika masuala ya siasa za hapa nchini hususan kuhusu uchaguzi mkuu na mstakabali wa demokrasia nchini mwetu. Nyote mnatambua kwamba kuanzia mchakato wa kumpata mgombe wa Urais ndani ya CCM kule Dodoma, ambako nilipiga kambi, sijayumba katika msimamo wangu kwamba Edward Ngoyai Lowassa ndiye chaguo langu katika kampeni za kumpata Rais mpya wa Taifa letu.

Chaguo langu si ndoto wala mlipuko wa mapenzi juu ya Lowassa. Nimemfahamu Lowassa tangu miaka ya 90 nikiwa cadre wa Chama cha Mapinduzi kwa mahusisho katika majukumu ya Kichama. Lowassa amejaaliwa nuru na uwezo wa kuongoza na wa kupendwa na watu. Ni msikivu pamoja na kwamba ni kiongozi asiyependa ukiritimba na utovu wa nidhamu, iwe kwa upande wa watumishi au wananchi wenyewe. Kubwa kwake ni ucha Mungu wake ambao unamsaidia sana katika uongozi unaojali na kuheshimu utu, ukweli na uwazi. Wanaodhani au kutaharuki kwamba eti anaweza au ana hulka ya kulipiza kisasi kwa jambo lolote lile ni waongo; wanajilinda.

Lowassa ni chaguo la wengi na CCM, katika busara yake ya kumuengua katika mchakato wa kumpata mgombea wa Urais, kimedhihirisha kutokuwa Chama kinachoendeshwa kwa misingi ya demokrasia. Dalili za Chama hiki kupoteza lengo la kuwa Chama cha watu, na kuwa cha viongozi wachache zilianza siku nyingi na hasa katika kipindi cha uongozi wa Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete. CCM kimebadilika na kuwa Chama cha makundi na migawanyiko yakupambana, si kwa malengo ya itikadi na ujenzi wa Chama, bali ya kumalizana na kutaka kufukuzana.

Lowassa angeweza kufukuzwa miaka mingi tu iliyopita! Aliweza kushinda vita hivyo kutokana na kupendwa na wengi ndani ya CCM. Hivyo, kujitoa kwake uanachama wa CCM hivi karibuni ni sahihi kabisa kwasababu CCM si Chama tena cha watu. Kimetekwa. Na mimi nakubaliana na msimamo wa Lowassa na hao waliyofuata kutoka nadani ya CCM.

Niliwahi kuandika makala katika ukurasa huu nikimnukuu mshairi mmoja wa Uingereza aliyeandika kwamba, ‘there comes a time when the door opens and allows the future in’. Mlango huo sasa umefunguka usoni mwangu na huu uamuzi wangu maana yake ni kukubali kwamba wakati mpya umewadia; ni wakati wa mabadiliko. Kuendelea kujihisi kwamba ningali mwana CCM wa kadi ni kukubali kujidanganya mwenyewe. Si sawa. Kama marehemu Baba wa Taifa alivyowahi kusema, ‘CCM si mama yangu’.

Hivyo ndugu zangu, kuanzia kesho mimi si mwana CCM tena. Nitarejesha rasmi kadi yangu kupitia ofisi ya CCM ya kata yangu Mikocheni, Dar-es-Salaam. Kwa sasa sijaamua kujiunga na Chama kingine. 

Mwenyezi Mungu anilinde.

I'm Looking For A Husband To Settle Down With: Sabby Angel

0
0

Actress and singer Sabby Angel is tired being lonely and she is looking for a husband to settle with as she turns 25 on her birthday this October 21st.  Sabby has been in unsuccessful relationships in the past and this time the mother of one seems to be serious looking for a man to be her husband and not a boyfriend to waste her time.
Anyhow, who could be the lucky dude to date the screen goddess..?, watch this space for more...

Milioni Waondolewa Kwenye Daftari la Wapiga Kura Tanzania

0
0
Tume inayosimamia uchaguzi nchini Tanzania (NEC), imefuta majina ya wapiga kura zaidi ya milioni moja kutoka kwenye orodha ya watu waliojiandikisha kupiga kura.
Awali tume hiyo ilikuwa imetoa idadi ya wapiga kura milioni 23.7 waliojiandikisha kwenye daftari la kudumu kupitia kwa mfumo wa kielektroniki (BVR).
Mwenyekiti wa NEC, Jaji mstaafu Damian Lubuva, alisema idadi hiyo imepigwa kalamu kufuatia shughuli ya kuhakiki majina ya watu wote waliojiandikisha.

Majina ya watu milioni moja, 1,031,769 waliopatikana kuwa na makosa moja au zaidi yaliondolewa.
Jaji Lubuva alisema kuwa wengine waliojiandikisha zaidi ya mara moja, wengine hawakutimiza vigezo vya kuitwa Watanzania huku waliosalia wakiwa watu waliokosa sifa nyingine muhimu.
Kufuatia shughuli hiyo , Jaji Lubuva alisema wapiga kura watakaoruhusiwa kushiriki katika uchaguzi mkuu ujao watakuwa ni watu milioni 22,251,292.

Kisiwani Zanzibar wapiga kura wapatao laki 503,193 wataruhusiwa kushiriki uchaguzi mkuu tarehe 25.
Watu 181,452 walijiandikisha zaidi ya mara moja.
Wengine 845,944 waliandikishwa na wahudumu 74,502 waliokuwa kwenye mafunzo kabla ya kuanza shughuli kuu ya uandikishaji

Aidha majina ya watu 3,870 yalibainika kuwa watu waliokosa sifa za Mtanzania.
Wakati huohuo idadi ya vituo vya kupigia kura pia vimetangazwa.
Kutakuwa na vituo 65,105 vya kupigia kura katika uchaguzi ujao.
Vituo vya kupigia kura 63,525 vitakuwa Tanzania bara huku Kisiwa cha Zanzibar kikitengewa vituo 1,580 vya kupigia kura.

Sad Photos: Father Cradles, Kisses His Dead 3Year Old Killed in Israeli Airstrike (photos)

0
0
A Palestinian father cradled, kissed and cried as he said goodbye to his 3 year old daughter, Rahaf who was killed alongside her pregnant 30-year-old mum, Noor Hassan in an Israeli air strike near Gaza City, on Sunday, October 11, when their house collapsed. The Israeli army said that its planes were targeting two Hamas weapons-manufacturing sites in the area and not civilians. The mother and child were buried today. See more photos





King LAWRENCE Flaunts His New Lover After Eating And Dumping ZARI & HUDDAH (PHOTO)

0
0

After having s3x with aging Ugandan socialite, Zari Hassan, and later dumping her like garbage and doing the same to Kenya’s Huddah Monroe, flashy Kampala businessman, King Lawrence, has flaunted his new s3xy lover.

He describes her as the boss of all bosses and way richer than Zari and Huddah combined. From the look of things, this controversial Ugandan businessman has a taste for beautiful women.


See her in the photo below.:

Magufuli Kasema Chanzo cha Mgao wa Umeme Nchini ni Wagombea Urais wa Upinzani Ambao Wamepiga Dili na Kampuni za Umeme

0
0
Mgombea urais kwa tiketi ya CCM, Dkt. John Magufuli amesema kuwa tatizo la umeme linaloendelea nchini limesababishwa na baadhi ya wagombea wa vyama vya upinzani.

Mgombea huyo wa CCM aliyasema hayo katika mkutano wa kampeni uliofanyika jana mkoani Lindi na kuhudhuriwa na umati mkubwa wa wafuasi wa chama hicho, ambapo alisema kuwa baadhi ya wagombea wa vyama vya upinzani ndio chanzo cha tatizo la umeme nchini kwa kuwa ‘walipiga deal’ kupitia makampuni ya ufuaji umeme.

Katika hatua nyingine, Dkt. Magufuli, alisema amepata taarifa kwamba kuna njama zinaandaliwa kwa lengo la kumuangusha mgombea ubunge Jimbo la Mtama kwa tiketi ya chama hicho, Nape Nnauye.

Dk. Magufuli aliyasema hayo jana wakati akizungumza kwenye mkutano wa kampeni katika Jimbo la Mtama mkoani Lindi.

Alisema Nape anaandaliwa njama ili asipite katika kinyang’anyiro cha ubunge jimboni humo kwa sababu aliwataka baadhi ya wana-CCM wajivue gamba wakati chama hicho kikiwa katika mchakato wa kufanya mabadiliko.

Hata hivyo, Dk. Magufuli alisema Nape ni kiongozi mzuri ambaye endapo yeye (Dk. Magufuli), angekuwa na uwezo wa kumhamisha,  angemhamishia kwenda kugombea katika jimbo lake la Chato.

DR Mtikila Aliuawa Kabla ya Ajali....DP

0
0
MAPYAA! Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrati (DP), Abdul Juma Mluya ameibuka na kusema mazingira ya kifo cha aliyekuwa mwenyekiti wa chama hicho, Mchungaji Christopher Mtikila yamejaa utata huku akiweka wazi kwamba, inavyoonekana aliuawa kabla ya ajali yenyewe.
Mtikila alifariki dunia katika ajali ya gari aina ya Toyota Corolla namba T189 ARG, Oktoba 4, 2015 iliyotokea kwenye Kijiji cha Msolwa, Bagamoyo, Pwani. Wengine watatu walijeruhiwa.
mtikila2
Mti ambao gari liliugonga kwa juu kabla ya kupinduka.
Akizungumza na Uwazi mwishoni mwa wiki iliyopita kwenye ofisi ndogo ya chama hicho nyumbani kwa marehemu, Mikocheni B jijini Dar, Mluya alisema hata watu waongee vipi, lakini uchunguzi wao umeonesha kwamba, kiongozi wao aliuawa tofauti na eneo la ajali na mwili kwenda kutupwa pale.
ROHO YAKE ILIWINDWA KWA SIKU 40
Mluya alisema: “Ndugu mwandishi, Mchungaji Mtikila kama kufa alikuwa afe muda mrefu sana pengine siku arobaini zilizopita (mpaka siku ya kifo cha kweli), kwa sababu amewindwa na watu ambao hatujajua lengo lao kubwa lilikuwa nini!
“Kila alikokwenda kwa shughuli za kichama kulikuwa na timu ya watu inayomfuatilia.”
mtikila4
...Baada ya Kupinduka
MARA YA KWANZA
“Tarehe siikumbuki, lakini ni Septemba mwanzoni. Tulikuwa Bunda, Mara kwenye shughuli za chama, kuna watu ambao walikuwa hawaeleweki walitufuata mpaka hotelini.
“Baada ya kubaini hilo, nilimuuliza mwenyekiti kuhusu ratiba aliyokuwa nayo ya kuzungumza kwenye runinga ya Staa TV.
“Alinipa ratiba. Baada ya kumaliza kuzungumza, nilimwambia Bunda si mahali pa kulala hivyo nilimshauri aondoke, aende Mwanza. Na nilimwambia dereva wake aondoke bila kuaga.”
mtikila4 (2)
WAKIWA NJIANI
“Lakini cha ajabu, wakiwa njiani wakielekea Mwanza kuna gari liliwafuata kwa nyuma kwa mwendo ambao waliutulia shaka. Dereva wa mwenyekiti alipokuwa akiongeza mwendo, naye anaongeza, akipunguza naye anapunguza.
“Ilibidi dereva amwambie mwenyekiti naye akamtaka dereva aongeze kasi hadi Mwanza.”
“Katika ratiba yetu tulitaka kufanya ziara za kichama kuanzia  Oktoba 18,  mwaka huu kwa kuanzia mkoa wa Kigoma na kwingineko. Pamoja na kufuatiliwa kote kule mwenyekiti hakuwa na roho ya uoga hata kidogo. Alimtanguliza sana Mungu.
“Kwa hiyo wasiwasi mkubwa wa kufuatiliwa na watu hao ulianza Mara na Mwanza kwa nyakati tofauti.
“Septemba 11, mwaka huu ndiyo tarehe ambayo sasa nilianza kukariri matukio hayo hatua kwa hatua. Siku hiyo tulikwenda kwenye Kijiji cha Usangu mkoani Pwani kwa ajili ya kufanya kampeni ya mgombea udiwani. Baada ya kumaliza tuliamua kurudi Dar lakini njiani dereva akasema kuna watu hawajui wanakuja nyuma yetu.”
WAPOTEA NJIA KWA KUFUATILIWA
“Tulijikuta tukipotea njia na kutokea mjini Kisarawe (Pwani). Pale tulifika kituo cha mafuta ambapo tulikuta gari aina Toyota Land Cruiser VX limepaki kama vile ni watu pia walikuwa wakitufuatilia.
“Lengo la kusimama pale lilikuwa kupata chakula lakini hatukufanya hivyo kulingana na mazingira. Tukaanza safari ya kurudi Dar. Tulipofika Pugu Sekondari, gari lile lilitupita kwa kasi na kupotea.
“Tulipofika Tazara gari lile lilionekana na wakati huo yalikuwa mawili. Kilichotushangaza ni upya wa magari lakini eti namba zinaanzia na A. Mimi nilifikiria kwamba, pengine ni za idara  ya  usalama  wa  taifa  zilikuwa doria  mbalimbali hasa kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi.
“Ndugu mwandishi, mimi ninafanya kazi ya siasa, niko makini sana. Niliwaambia wenzangu kuwa tunafuatiliwa.
“Ndani ya gari sisi tulikuwa na viongozi wa kuwapeleka Temeke. Lakini baada ya kufika huko lile VX tulikutana nalo. Tulipomuacha yule tuliyempeleka kule, tukawa tunampeleka mchungaji nyumbani kwake (Mikocheni) lakini bado lile gari lilikuwa likitufuatilia.”
WAPIGA CHENGA
“Tulipofika maeneo ya Msasani kwa Mwalimu (Julius Nyerere) dereva alikunja kona kuelekea kwa mchungaji na lile gari likakunja kona na kurudi lilikotoka.”
SIKU NYINGINE
“Siku iliyofuata tulipanga mipango yote ambapo sasa tulisema Oktoba 18, mwezi huu tuanze ziara ya mkoa wa Kigoma  na maeneo  mengine ya Kanda ya Ziwa.
“Mimi niliondoka kuelekea Shinyanga, yeye (Mchungaji) aliandaa safari ya kwenda Njombe kwenye kampeni ya mgombea Ubunge Jimbo la Njombe.”
OKTOBA 2, 3, 2015
“Mwenyekiti aliondoka Dar Oktoba 2, kuelekea Njombe. Oktoba 3, alinipigia simu asubuhi na kunijulisha kuwa  jana yake walipata ajali maeneo ya Makambako wakati wanakwenda.
“Nilimuuliza alipata matibabu, akajibu kuna viongozi wa Njombe walifika na kumchukua hivyo yuko sawasawa.”
TAARIFA YA AJALI
“Siku hiyo hiyo walifanya kampeni na jioni yake walianza safari ya kurejea Dar. Walipofika Mkoa wa Pwani, saa kumi na moja alfajiri, Mchungaji Mgaya alinipigia simu na kuniambia walikuwa njiani wanarudi Dar, wamepata ajali mbaya sana. Lakini hakuniambia kama mchungaji amefariki dunia.
“Nilianza kufuatilia tukio hilo na kuuliza kama kuna msaada wowote wameupata, akasema mpaka muda huo polisi walikuwa hawajafika. Mimi napenda sana kufungua mitandao ya kijamii, nilipofungua nikakuta picha zilishasambaa kwenye mitandao kitu ambacho nilijiuliza usiku huo huyo mpigapicha alikuwa wapi?”
SHAKA KUBWA YA DP
“Sisi DP, mashaka yetu makubwa ni mazingira mazima ya namna kiongozi huyo alivyofariki dunia. Hata mtoto hawezi kudanganywa kwa namna hiyo. DP ina taasisi ya kufanya uchunguzi iitwayo Liberty International Foundation iliyokuwa ikisimamiwa na marehemu. Ipo kazini kwa sasa ili kubaini ukweli wa kifo cha mwenyekiti na tutaweka wazi kila kitu.”
“Laini pia tunaitaka serikali kufanya uchunguzi na kutoa taarifa hadharani.”
MWENYEKITI KIJIJI AIBUKA NA YAKE
Uwazi pia lilifika aneo la ajali na kujionea kwa macho mazingira yake na kupata maelezo kutoka kwa baadhi ya mashuhuda.
Joshua Mohamed Msigala ni Mwenyekiti wa Kijiji cha Msolwa, Chalinze, Pwani palipotokea ajali. Yeye anasimulia mambo aliyoelezwa na mmoja wa majeruhi, Mchungaji Patrick Mgaya siku ya tukio.
“Kwanza kabisa waandishi wa habari mmefanya vizuri kufika eneo la tukio na kujionea hali halisi. Nawaeleza hali halisi ilivyokuwa mpaka mimi kufika eneo la ajali.
“Siku hiyo asubuhi ya saa kumi na moja na nusu kama sikosei, nikiwa nyumbani nilipigiwa simu na dereva mmoja wa lori anayenijua. Akasema ameona ajali maeneo yangu lakini hajui kama kuna waliokufa au la!”
MWENYEKITI AWAHI NA BODABODA
“Kusikia hivyo, nilichukua bodaboda ili niwahi. Nilifika ndani ya dakika kama kumi tangu kutokea kwa ajali. Nilikuta mwili wa Mtikila umelala pembeni ya gari huku wengine watatu waliodai walikuwa ndani ya gari wakiwa wamesimama tu.
“Ila kati ya hao watatu, mmoja alijitambulisha kuwa ni Mchungaji Mgaya, yeye wakati nafika alikuwa akiongea kwa simu.”
ALICHOAMBIWA NA MCHUNGAJI
“Nilimuuliza mchungaji ilikuwaje? Akasema wakati wanapata ajali hiyo, marehemu Mtikila na wengine wawili walichomoka ndani ya gari hali iliyosababisha kifo cha Mtikila. Hata hivyo, kwa upande wangu sikuamini kama wote walichomoka kutoka kwenye gari bali mazingira yalionesha walitoka wenyewe.
“Mchungaji alizidi kuniambia kuwa, gari lilipaa juu zaidi ya futi kumi na kugonga mti kisha likapinduka na kulalia paa (kwenye Uwazi siku ya tukio, mchungaji alisema gari lilibiringika).
“Lakini pia siamini, kwani pamoja na kuona alama katika mti sikubali kama zilisababishwa na ajali kwani kama ni hivyo gari lingekuwa limepondeka zaidi juu lilikoangukia tofauti na lilivyokuwa likionekana.”
KILICHOMSHANGAZA ZAIDI MWENYEKITI
Mwenyekiti huyo alizidi kusimulia kushangaa kwake: “Kitu kingine kinachonishangaza ni kwamba, kwa maelezo yao gari liliacha barabara likawa linaendeshwa pembeni kwa umbali wa meta mia moja (urefu wa uwanja wa mpira). Kwa nini dereva asipunguze mwendo ambapo angefanya hivyo gari lisingefika kwenye mti.”
“Kinachoshangaza kingine ni kwamba, hakuna majeraha yaliyoonekana kwa macho kwa walionusurika hata kuonesha kwamba walikatwa na vioo wakati wakirushwa nje kutoka ndani ya gari. Hata viti vya mbele vilikuwa vilevile, havikuharibika na kama majeruhi walirushwa nje walipitia wapi?”
WALIOFIKA AWALI
Mwenyekiti huyo alisema anawashukuru askari wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ) wa Kambi ya Kizuka na Sangasanga waliokuwa wakipita ambapo walifika kutoa msaada.
“Baadaye mimi nilifanya mawasiliano na Polisi wa Kituo cha Chalinze (Bagamoyo) ambapo walifika eneo la tukio. Pia polisi wa mkoa nao walifika na saa 12:30 asubuhi majeruhi na mwili wa marehemu walipelekwa Hospitali Teule ya Rufaa Tumbi.”
Naye Ofisa Mtendaji wa Kijiji cha Msolwa, Joseph Hamad kwa upande wake alisema alipokea taarifa saa 3 asubuhi na alipowasiliana na mwenyekiti alimwambia yupo katika eneo la tukio.
Baadhi ya wananchi wa kijiji hicho waliohojiwa na Uwazi walisema wameshangazwa na ajali hiyo iliyosababisha kifo cha Mchungaji Mtikila na kuitaka serikali kufanya uchunguzi wa kina.
SIMU YA MTIKILA YAZUA UTATA
Mpaka tunakwenda mitamboni, familia ya Mtikila ilisema, jana ilitarajia kufuatilia simu ya marehemu kwani haijulikani ilipo na pia kujua walipo dereva (George Ponella) na msaidizi wake (Ally Mohamed) ambapo awali, dereva alishikiliwa na jeshi la polisi.
Habari imekusanywa na Makongoro Going, Haruni Sanchawa na Issa Mnali.

Source:GPL

Rayuu Afunguka Kuhusu Wanaume Wanne Waliomfanyia Mbaya Kisha Kumtosa Bila Kumuoa

0
0
NYOTA wa filamu Alice Bagenzi ‘Rayuu’ amesema anajihisi kama mwanamke mwenye mkosi baada ya wanaume wanne alioshiriki nao mapenzi kuonesha nia ya kumuoa, lakini ghafla waliingia mitini na kupeperusha ndoto yake ya kuwa mke wa mtu.

Akipiga stori na gazeti hili, muigizaji huyo alisema umri wake unamruhusu kuolewa na anafanya kila njia ikiwa ni pamoja na kutii maelekezo yote ya mwanaume ili kumvutia aingie naye katika ndoa, lakini kinachomshangaza hubadilika ghafla na kumpotezea kabisa.
“Siyo siri naumia sana, huenda nimerogwa nisiolewe, mwanaume anajitambulisha hadi kwa wazazi na kuanza mchakato wa ndoa lakini baadaye anaingia mitini,” alisema Rayuu
GPL

Mzindakaya Nae Afunguka Makubwa Kuhusu CCM na Waliondoka CCM

0
0
MWANASIASA mkongwe nchini, Chrisant Mzindakaya amewataka viongozi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na wagombea wao wa nafasi mbalimbali, wasigombane na waliohama chama hicho kwa kusisitiza kwamba wakifanya hivyo, watakuwa wanakosea.

Mzindakaya alisema, CCM ni chama chenye heshima kubwa duniani na chenye Ilani ya Uchaguzi bora, yenye heshima. Alisisitiza kuwa rais bora wa awamu ya tano atatoka katika chama hicho.
Alisema hayo juzi akiwawakilisha wazee wa mkoa wa Rukwa kwenye mkutano wa kampeni ya kuwanadi wagombea urais, ubunge na udiwani kwa tiketi ya CCM uliofanyika katika viwanja vya Shule ya Msingi Ndua, Manispaa ya Sumbawanga.

Mkutano huo wa kampeni ulihudhuriwa na Mjumbe wa Kamati Kuu CCM Taifa na Halmashauri Kuu, Mizengo Pinda ambaye pia ni Waziri Mkuu. Wengine ni pamoja na viongozi waandamizi wa CCM mkoa na wilaya.

“Sisi wazee wa mkoa huu tunasema chama cha siasa chenye heshima kubwa duniani ni CCM ambapo bila wasiwasi ndiko atakakotoka rais wa awamu ya tano ambaye ni Dk John Magufuli …

FLORA MBASHA Akiri..Mwanangu si wa Emmanuel Mbasha

0
0
OHOOO! Kimenuka tena. Mwimbaji wa nyimbo za Injili, Flora Mbasha amesema mwanaye mdogo (jina linahifadhiwa) hahusiani hata kidogo na aliyekuwa mumewe, Emmanuel Mbasha huku akidai kuwa anamtambua mwanaume huyo kama mzazi mwenzake kwa mtoto mmoja tu (Liz), Risasi Jumatano linakupa zaidi.

Akizungumza na waandishi wetu kwa njia ya simu mwishoni mwa wiki, Flora alisema amechoshwa na manenomaneno yanayosemwa juu yake na Emmanuel na kwamba kama mumewe huyo ameamua kumwaga ugali, yeye yupo tayari kumwaga mboga.

Mwimbaji huyo alisema kwamba kauli aliyoitoa hivi karibuni kuwa anampenda mumewe na kwamba yupo tayari kuishi naye haikutoka moyoni, isipokuwa alifanya hivyo kwa huruma tu, kwa sababu mwanaume huyo ni mtu katili, mwenye roho mbaya na asiyemuogopa Mungu.
“Mtu mwenyewe alimtelekeza mtoto (Liz) kwa zaidi ya mwaka mmoja, ni mtu mbaya sana, sina mapenzi na Mbasha hata kidogo, ni afadhali niolewe na chizi anayeokota makopo kuliko kurudiana na mtu katili na mnyama kama huyo, namheshimu kama mzazi mwenzangu kwa Liz,” alisema.
Mtoto anayedaiwa kuibua mazito.

“Huyo mwanaume hafai kabisa, ni katili, namfananisha na shetani, anajifanya mwema kwa watu wakati hajawahi kuiomba msamaha familia, sikubaliani kabisa na hukumu ya mahakama, ukweli anaujua kwamba alibaka na hata mkimtaka huyo binti mumhoji nitamleta, isitoshe sasa hivi hata mtoto wake hamjali, hajui anasoma vipi, hajawahi kulipa hata shilingi ya ada, mimi mwenyewe ndo nahangaika kumlea mwanangu Liz ambaye anasoma kidato cha kwanza.


“Hastahili kabisa kuitwa baba sababu mzazi mwenye akili hawezi kutelekeza familia hata kama tumegombana, nimemwachia nyumba niliyojenga kwa pesa yangu na pesa zote aliweka kwenye akaunti yake na zote nilimwachia lakini kashindwa kuihudumia familia.”


Flora anajulikana kuwa na watoto wawili, mdogo akiwa ni yule aliyezaliwa wakati wanandoa hao wakiwa katika mzozo uliosababisha watengane hadi hivi sasa. Alipoulizwa kwa nini anadai aliyekuwa mumewe kumtelekeza mtoto mmoja tu, badala ya wawili, alifunguka.
“Huyu mwanangu mdogo hausiki naye kabisa, tena asiwe anamtaja kabisa kwa sababu hamhusu, hajui hata matumizi yake yakoje, mengine kaka achana nayo tu,” alisema Flora.
Mwimbaji huyo mwenye kipaji alipoulizwa sababu za kufuta kesi ya kudai talaka, aliyoifungua hivi karibuni katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, wakati anadai hamtaki na hawezi kurudiana naye, alisema alifanya hivyo baada ya kushinikizwa na mtu ambaye hata hivyo, alikataa kumtaja.
Mwimba Injili Bongo, Flora Mbasha.\

Flora alisema familia yake haijaridhishwa kabisa na suala la kesi ya ubakaji iliyokuwa ikimkabili mumewe kumalizika kwa kuachiwa huru na kwamba wanajipanga kwa ajili ya kukata rufaa.“Hiyo kesi imeisha kisiasa, Mbasha aliwahi kukiri kuwa ni kweli alifanya kitendo hicho, iweje leo aonekane hana hatia? Tutakwenda kukata rufaa ili haki itendeke.”

Baada ya kuzungumza na Flora, mwandishi wetu alimtafuta Mbasha kwa lengo la kumuuliza kuhusu madai ya mtoto yule mdogo kutohusika naye kama alivyosema mkewe, naye bila ‘kutafuna maneno’, alisema hata yeye hamtambui huyo mtoto mdogo, ila anaomba arudishiwe mtoto wake mkubwa, Liz na maisha mengine yaendelee.
“Hata mimi simtambui huyo mwingine, ninachoomba anirudishie tu mtoto wangu mkubwa Liz, huyo mwingine sihusiki naye kabisa kama alivyosema, yeye (Flora) ndiye anajua mhusika wa huyo mtoto, lakini si mimi na wala hajakosea kusema hivyo, nililitambua hilo tangu zamani, anipe tu mwanangu wa kwanza,” alisema Mbasha.

Source:GPL-meandikwa na Brighton Masalu, Mayasa Mariwata na Gladness Mallya

Diamond Opens Up About How Fathering Princess Tiffah Has Changed Him

0
0
Diamond and Zari Hassan’s daughter, Latiffah Nasibu Abdul aka Princess Tiffah has not only made the Dangote’s a tight-knit family but also changed her father’s life in a big way.

Speaking to Tanzania’s leading radio station, Clouds FM, the singer who just bagged three awards at the just concluded 2015 AFRIMMA awards, said that he has been trying to be conduct himself in  a more disciplined manner as he would not like his daughter to see ratchet pictures of her father grinding on women because she would be saddened by them.


He went on to say that he fears tomorrow more than before, so he has decided to reduce the drama in his life as such things would confuse his daughter in future.

January Makamba Adai Magazeti Yanampendelea LOWASSA Kwa Kumpigia Kampeni

0
0
Mjumbe wa Kamati ya Kampeni ya CCM, January Makamba ameonesha kutokubaliana kwake na ripoti za kinachojili kwenye mikutano ya mgombea urais wa Chadema, Edward Lowassa na kueleza kuwa  Magazeti hutumiwa kupiga kampeni.

Makamba ameeleza hayo kupitia mtandao wa Twitter baada ya mtu mmoja anaetumia jina la ‘Gachanja Muigai’, kumueleza kuwa kutokana na kile wananachokisoma, inaonekana kuwa wananchi wengi wanamuunga mkono Lowassa. Na akataka kupata maoni ya Makamba kutokana na hali hiyo kama anadhani wataweza kushinda.

“@JMakamba @MagufuliJP From what we read here, it seems #Lowassa is resonating with Wananchi. Una hakika si wakati wa kuvuka sakafu?” Aliuliza.

Makamba alimjibu kuwa wapinzani wanatumia baadhi ya magazeti kama sehemu ya kampeni zao lakini tafiti na hali halisi nchini inaeleza tofauti.

“They’ve turned some newspapers into their campaign fliers. But the polls & mood across Tanzania tell another story.”

Mgombea Ubunge wa Kahama Mjini James Daudi Lembeli apata ajali

0
0
 Mgombea Ubunge Kahama Mjini Chadema, James Lembeli na Joyce Multan wamepata ajali wakitokea Arusha kwenda simanjiro .hakuna aliepoteza maisha

Maduka ya Uchumi Supermarket yafungwa Tanzania na Uganda

0
0
Uongozi wa Uchumi Supermarket umetangaza kufunga shughuli zake katika maduka yake yaliyopo Tanzania na Uganda ili kutoa nafasi ya kuzuia mtikisiko wa kifedha unaoikumba kampuni hiyo.

Ofisa Mtendaji Mkuu wa Uchumi, Dk Julius Kipng'etich, amesema Bodi imeamua kufunga vitengo vya kikanda ili kuimarisha shughuli zake nchini Kenya baada ya kupata hasara katika maduka yake ya Uganda na Tanzania.

"Maduka yetu ya Uganda na Tanzania huchangia asilimia 25 tu ya gharama za uendeshaji. Matawi hayo mawili hayajapata faida yoyote kwa zaidi ya miaka mitano iliyopita jambo linaloyumbisha shughuli zetu," amesema Dk Julius

"Tuna uhakika kwamba tunaweza kuigeuza Uchumi kwa kulenga asilimia 95 ya biashara ambazo zinaleta fedha kwa wanahisa ambao wana matumaini kwamba tutafanikisha hili ndani ya muda mfupi," ameongeza Dk Kipng'etich.

Kwa upande wa Tanzania, juzi wafanyakazi zaidi ya 400 waligoma kwa kujifungia ndani ya ofisi zao kwa zaidi ya saa 20 wakitaka kujua hatma yao kwenye makao makuu ya duka hilo yaliyopo katika jengo la Quality Center jijini Dar es salaam.

Rais Kikwete Awaonya Wanaopanga Kulinda Kura Vituoni

0
0
Rais Jakaya Kikwete amesema watu wanaopanga kubaki katika vituo vya kupigia kura baada ya kumaliza zoezi hilo kwa lengo la kulinda kura kunaashiria uvunjaji amani, hivyo serikali imejipanga kupambana na hali hiyo siku ya uchaguzi.

Rais amesisitiza kwamba wanaopaswa kulinda kura ni mawakala pekee na si wafuasi wa mgombea ama vyama.

Akizungumza jana katika sherehe za Kilele cha Mwenge wa Uhuru zilizofanyika Uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma, kiongozi huyo anayemalizia muda wake madarakani alisema viongozi wanaowaagiza wafuasi wao kulinda kura wana nia mbaya dhidi ya amani ya nchi.

“Mnatakiwa muondoke kwenye vituo baada ya kupiga kura….kura utazilindaje? Mawakala ndio pekee wanaoweza kulinda. Mkikaidi hilo, hatutawavulimia. Serikali imejipanga kupambana na wale wote watakaokaidi agizo la Tume ya Uchaguzi (NEC),” alisisitiza Rais Jakaya Kikwete.

Katika shehere hizo za mwenge zilizoendana sambamba na maadhimisho ya siku ya kumuenzi Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere, Rais Kikwete aliwataka Watanzania kuchagua watu waadilifu ambao wana dhamira ya kupambana na rushwa kwa vitendo.

“Tumchague mtu ambaye hana ukabila, udini na ubaguzi wa rangi…tumchague kiongozi atakayetetea maslahi ya makabila yote 126,” alisema rais huku akimnukuu Mwalimu Nyerere aliyefariki miaka 16 iliyopita.

Sherehe hiyo ilihudhuriwa pia na Spika wa Bunge anayemaliza muda wake, Anne Makinda, wakuu wa mikoa na viongozi wengine wa ngazi tofauti serikalini na kupambwa na nyimbo za makabila na wanafunzi wa shule mbalimbali mjini Dodoma.
Viewing all 104429 articles
Browse latest View live




Latest Images