Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104415 articles
Browse latest View live

Mgombea Urais wa CCM Dr John Magufuli Amfagilia Mwanamuziki Diamond Platnumz

0
0
MGOMBEA urais wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), John Magufuli amemmwagia sifa lukuki, mkali wao ndani ya muziki wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’ kutokana na ushindi wa tuzo tatu za Afrimma zilizofanyika wikiendi iliyopita nchini Marekani
Tukio hili lilitokea katika Viwanja vya Shule ya Msingi Mpilipili mkoani Lindi baada ya staa wa Bongo Fleva, Ali Saleh Kiba kushuka jukwaani kukamua kwenye kampeni za mgombea huyo wa urais, ndipo Magufuli alishika kipaza sauti na kumsifia Diamond aliyeshinda tuzo za Msanii Bora wa Kiume Afrika Mashariki, Msanii Bora wa Mwaka na Utumbuizaji Bora wa Video.

“Ukweli nampongeza sana msanii Diamond kwa jinsi anavyojituma na kuipeperusha vyema bendera ya taifa letu…,” alisema Magufuli huku pia akiwapongeza Ommy Dimpoz na Vanesa Mdee walioshinda tuzo tofauti katika kinyang’anyiro hicho.

Aidha, katika kampeni hizo Magufuli aliwaahidi wakazi wa mji huo kuwajengea Lindi mpya ambayo itakuwa ya neema kupitia gesi inayopatikana kwenye ukanda huo, unafuu wa vifaa vya ujenzi ikiwemo saruji ‘cement’ iliyoanza kupatikana kwa bei ya shilingi 8,000 kwenye kiwanda cha Dangote kilichopo Mtwara, zao la korosho ambalo Magufuli alijinandi kuwa na digrii ya zao hilo.

MAMBO HADHARANI: Hatimaye AGNESS MASOGANGE Afungukia Penzi la DAVIDO

0
0
VIDEO Queen mwenye umbo tata Bongo, Agness Jerald ‘Masogange’ alifungukia penzi lake na staa wa muziki kutoka Nigeria, Davido.

Akizungumza na Amani Masogange alisema kuwa kuna uvumi unaovumishwa na baadhi ya watu kwamba amekuwa akitoka kimalovee na Davido jambo ambalo halina ukweli wowote.

“Kwanza kabisa Davido ni shemeji yangu lakini pia kuna ‘project’ kubwa ambayo tunaiandaa. Mtakuja kuelewa tu hapo mbeleni na si jambo la kusema ni wapenzi bila kuthibitisha,” alisema Masogange.

Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi CCM Mh. Abdulrahman Kinana akiwa KATAVI

0
0


Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi CCM Mh. Abdulrahman Kinana akiwa KATAVI

Video: These Are The Things House Girls Do While Alone At Home

0
0

Have you ever imagined what these ladies do while they are left all alone in the house when their bosses are out for work? They do crazy things that can shock you.

We have heard cases of some some assaulting young kids.Some even remain nak3d in front of the kids and tell the kids to f!nger them down there.

Here is a video of one who called her hubby next door to record her twerking and later they headed to the bedroom for the next session of the unthinkable.

Lulu, Wema Wafika Pabaya! Kisa Uhusiano na Diamond…

0
0
Pamoja na wenyewe kudai hawajui kilichotokea, mastaa wawili wenye sura za mauzo kunako sinema za Kibongo, Elizabeth Michael ‘Lulu’ na Wema Isaac Sepetu, kwa sasa wanadaiwa kufikia pabaya kufuatia bifu zito linalofukuta kati yao.

Habari za mjini zinadai kwamba, Wema amekuwa akishtushwa na kuchukizwa na kitendo cha Lulu kuwa upande wa aliyewahi kuwa mwandani wake, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ kiasi cha kwenda nyumbani kwake, Madale-Tegeta jijini Dar, usiku wa manane na kujiachia na jamaa huyo anavyotaka.

“Kama mtakumbuka, kabla ya kifo cha Kanumba (Steven), Wema na Lulu walikuwa ni mashosti kama ilivyokuwa kwa Wema na Snura (Mushi) au Wema na Kajala (Masanja) au Wema na Aunt (Ezekiel).

“Lakini baada ya jamaa (Kanumba) kuondoka na kisa kizima cha Lulu ndipo Wema akavunja urafiki na Lulu kwa sababu Kanumba aliwahi kuwa ‘mtu’ wa Wema kama ilivyo kwa Diamond.

“Ulipita ukimya wa muda mrefu bila Wema na Lulu kuwa mashosti zaidi ya salamu.

“Lakini mambo yalianza tena kuwa mabaya baada ya Lulu kumponda Wema alipokuwa akigombea Ubunge wa Viti Maalum kupitia CCM (Chama Cha Mapinduzi).

“Sasa hivi ishu ni kitendo cha Lulu kujiachia na Diamond kwenye birthday ya Rome Jones (binamu na DJ wa Diamond) kisha ile pati ya birthday Diamond kuifanyia nyumbani kwake huku (Lulu) akitupia picha za mafumbo yaliyoelekezwa kwa Wema.

“Hicho ndicho kinachoendelea na unaambiwa hali ni tete mno,” kilisema chanzo hicho ambacho ni mtu wa karibu wa mastaa hao.

Baada ya kupata ‘ubuyu’ kamili, Amani lilimtafuta Wema na kummwagia data ambapo alionesha kushtushwa na kudai kwamba hata yeye anashangaa ni nini kimetokea.

Kwa upande wake Lulu hakupatikana hewani lakini kwa mujibu wa mahojiano aliyofanya hivi karibuni juu ya uhusiano wake na Wema, mwanadada huyo alikiri kuwa rafiki wa Wema kitambo hicho lakini akasema hajui ni nini kilichotokea zaidi ya kwamba huwa wanasalimiana tu wanapokutana.

Kabla ya mambo kwenda mrama, Lulu na Wema walikuwa mashosti wakubwa ambapo gazeti hili liliwahi kuwashuhudia wakiwa lokeshi na kulala pamoja chumba kimoja kama mtu na dada au mtu na mdogo wake.

Chanzo: GPL

Christian Bella Adai Fedha Alizotunzwa Kwenye Fainali ya BSS ni Shilingi Milioni 3.2

0
0
Christian Bella amesema show yake ya fainali ya Bongo Star Search Ijumaa iliyopita, ilimuingiza fedha za kutunzwa nyingi zaidi kuliko show zote alizowahi kufanya.

Bella ameiambia Bongo5 kuwa ni mara yake ya kwanza kutunzwa zaidi ya shilingi milioni 3 na hivyo anawashukuru watanzania kwa upendo wanaomwonyesha.

“Unajua mimi nimekuwa nikitunzwa pesa nyingi lakini haikuwahi kufika kiasi kile. Nakumbuka katika uzinduzi wa wimbo wangu ‘Nashindwa’ nilitunzwa milioni 2, lakini ile ya BSS ndio imevunja rekodi, milioni 3 na laki mbili ni nyingi sana. Nawashukuru sana watanzania. Hii inaonyesha wanakubali ninachokifanya,” alisema Bella.

TANZIA: Mzee Emanuel Makaidi, Mwenyekiti mwenza wa UKAWA afariki dunia

0
0
Mwenyekiti wa NLD, ambaye ni mwenyekiti mwenza wa vyama vya upinzani vinavyounda Ukawa, Dkt. Emmanuel Makaidi amefariki leo majira mchana katika hospitali ya Nangao mkoani Lindi.

Taarifa za uhakika zinaeleza kuwa Dkt. Makaidi ambaye alikuwa mgombea ubunge katika jimbo la Masasi alikuwa akisumbuliwa na ugonjwa wa shinikizo la damu.

Dkt. Makaidi ni mgombea ubunge wa tano kufariki katika kipindi hiki cha uchaguzi mkuu.

Mpekuzi inatoa pole kwa familia, ndugu na jamaa wa Dkt. Emmanuel Makaidi na taifa kwa ujumla.

Mbowe Amshukia Rais Kikwete Kuhusu Idadi ya Wapiga Kura na Zuio la Wananchi Kulinda Kura Vituoni

0
0
Mwenyekiti  wa  Chadema, mh Freeman Mbowe  amemtaka Rais Kikwete kutovuruga amani ya nchi na badala yake   amemtaka aondoke  madarakani  na kuiacha  nchi ikiwa  salama.

Mbowe alitoa  kauli hiyo jana jioni  katika mkutano  wa kampeni uliofanyika Mbogwe, wilayani Geita.

Alisema Rais Kikwete  anatakiwa aondoke madarakani salama kama walivyofanya marais wenzake wastaafu.

“Rais Kikwete ameamua kuwa mpiga debe wa Magufuli (mgombea wa CCM), sasa mimi naomba nimjibu yeye kama mpiga debe na si rais,”alisema Mbowe.

Alisema Rais Kikwete ameamua kuwaaminisha  Watanzania kuwa wapiga kura wapo milioni 28 badala ya milioni 22 kama ilivyotangazwa na Tume ya Taifa ya Taifa ya Uchaguzi (Nec).

“Sasa nataka kumuuliza Rais Kikwete hao wapiga kura wengine milioni sita wametoka wapi?” alihoji Mbowe na kuongeza:

“Naomba kumwambia Rais Kikwete kuwa hii nchi si yake, hii nchi si ya CCM na hii nchi si ya familia yake...hii ni nchi ya Watanzania,” alisema.

Alisema hatua ya Rais Kikwete na CCM inayoungwa mkono na Nec kuwataka wananchi wapige kura na kuondoka vituoni haiwatendei haki Watanzania.

“Kikatiba Watanzania wana haki ya kulinda kura zao kwa sababu zile ni kura zao, nashangaa Rais Kikwete anawaambia watu waondoke,”alisema.

Mbowe, aliwaomba Watanzania wote kwenda kwenye vituo kwa ajili ya kupiga kura ikiwa ni pamoja na kuzilinda kura zao.

Pia alisema anashangazwa na kauli ya Rais Kikwete ya kuliagiza Jeshi la Polisi kuwaondoa wananchi kwa nguvu katika vituo vya kupigia kura.

“Hao askari walioagizwa na Rais Kikwete, nao wana watoto na familia zao, naomba nikwambie Rais Kikwete kuwa huwezi kuzuia mabadiliko. Zimebaki siku 11, Mungu atajibu maombi yetu...nawaambia wananchi nendeni mkapige kura kaeni mita 200 lindeni kura zetu,” alisema.

Akiwa  mjini Dodoma jana  wakati wa kilele cha Mwenge wa Uhuru kilichoenda sanjari na kumbukumbu ya miaka 16 ya kifo cha Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, Rais  Kikwete  alitaja  idadi  kubwa  ya  wapiga  kura  kuliko  iliyotolewa  na Tume  ya  Taifa  ya  Uchaguzi.

Hata  hivyo, jana  jioni  Ikulu  ililitolea  ufafanuzi  suala  hilo  na  kudai  kuwa  idadi  kamili  ya  wapiga  kura  ni  milioni 22  na  si  vinginevyo.

"..... Katika Kilele cha mbio za mwenge wa uhuru , kumbukumbu ya Baba wa Taifa , Mwalimu JULIUS Nyerere na wiki ya vijana Kitaifa, Rais  Jakaya Mrisho Kikwete katika hotuba yake amezungumzia idadi ya watu waliojiandikisha kupiga kura.

"Kwa uhakika amesema kuwa idadi ya wapiga kura ni 22,751, 292 kwa upande wa Bara na 503,193 wa Zanzibar.  Hii ndiyo idadi kamili ambayo imo kwenye hotuba ya Mheshimiwa Rais na hii ndiyo idadi kamili kama ilivyotolewa na Tume ya Uchaguzi Tanzania.."  Ilisema  Sehemu  ya  Tamko  hilo  la  Ikulu  jana.

Tiddo Muhando Tutakuwa Live Kuripoti Kila Kitu Muda Wote wa Uchaguzi

0
0
Azam TV itatenga channel moja dedicated kuripoti kila tukio siku ya uchaguzi live....tutatumia chopa mbili na drones kukusanya taarifa na matukio,.satelite uplink zaidi ya 50 na maripota nchi nzima....pia matokeo kadri kura zitakavyondikwa vituoni...utashuhudia nyumbani kwako....tutakua live usiku na mchana kwa masaa 72, kuanzia oktoba 25....

Tiddo Muhando,
CEO AZAM TV

Baada ya Kujitoa CCM, Balozi Juma Mwapachu Atoa Mpya..Adai Hata Nyerere Angekuwa Hai Angejitoa CCM

0
0
Siku moja baada ya kutangaza kujitoa CCM, kada mkongwe wa chama hicho, Balozi Juma Mwapachu amesema uamuzi alioufanya ni sahihi ambao hata Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere angekuwa hai angeufanya kwa sasa.

Balozi Mwapachu alieleza hayo jana katika mahojiano maalumu na kuongeza kuwa chama chake cha zamani kimepoteza mwelekeo kwa kuwa kinara wa kuvunja katiba na taratibu kitendo ambacho Nyerere alikichukia katika maisha yake.

Alisema anafahamu fika kuna watu watakosoa uamuzi wake huo lakini hatababaishwa na maneno yao na atasimamia msimamo wake huo huku akieleza kuwa anajisikia amani kujitoa katika siku ya kumbukumbu ya miaka 16 ya kifo cha Nyerere.

Mwapachu alitangaza kujitoa CCM juzi akisema kilivunja taratibu wakati wa mchakato wa uteuzi wa mgombea wa urais uliofanyika Julai ambao Dk John Magufuli alichaguliwa.

“Nimefanya makusudi kujitoa wakati huu kwa sababu hata Nyerere mwenye angekuwapo hai leo hii angefanya uamuzi kama niliofanya. Hata yeye alikuwa ameshachoshwa na chama chake kwa uvunjaji wa kanuni, taratibu na katiba na alikwishaona kuwa kinaanza kupitwa na wakati.”
 
Alisema mengine yanayojitokeza kwa sasa ndani ya CCM yanaonyesha bayana kuwa chama hicho hakiendi na wakati na kilijisahau na kuendesha mambo kama kipo kwenye mfumo wa chama kimoja wakati ni wa vyama vingi.

Alisema CCM ya sasa siyo ile aliyojiunga nayo akiwa chuo kikuu, ndiyo maana amejitoa kutokana na kutekwa na watu wachache ambao humpiga vita mtu ambaye si mwenzao.

Prof. Kitila Mkumbo Awarushia Dongo Mwalimu Nyerere Foundation, Adai Waache Kuchanganya Wananchi...Soma Hapa

0
0
"Nimefuatilia kwa kiasi mazungumzo ya ndugu Butiku, Mama Mongela na Ndugu Polepole. Nayaita mazungumzo na sio mdahalo kwa sababu hapakuwa na hoja kinzani.Hata hivyo nina angalizo. Kwa takribani miaka kumi tangu JK aingie madarakani Mwalimu Nyerere Foundation walikuwa vinara wa kuinanga CCM na kutuonyesha jinsi chama hiki kilivyobadilika na kuwa cha ovyo. Mimi naamini mlimaanisha na wala hamkuwa na chuki binafsi na JK. Sasa itakuwa vizuri mkatueleza watanzania wenzenu ni lini hasa chama hiki kiliacha yale mabaya mliyotueleza katika miaka kumi iliyopita.Anyway mna haki ya kubadilika kwa sababu tumeambiwa hiki ni kipindi cha mabadiliko. Lakini naomba sana baada ya uchaguzi msitumie MNF kutuhubiria tena ubaya wa CCM. Tafadhalini sana, msichanganye tena wananchi kwa kutumia taasisi takatifu ya Mwalimu Nyerere".

Ameandika hivyo Prof. Kitila Mkumbo ambaye ni Mhadhiri Mwandamizi wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam
Nini maoni yako hapo?

Lamar Odom Has 50/50 Chance For Survival, Took Several Sex Pills Before His Crisis

0
0
According to a report by TMZ, former NBA star Lamar Odom has a 50/50 chance of survival. They also confirmed that Khloe is still married to him and is now making all the decisions on his behalf.

Sources at the hospital tell us doctors are now saying Lamar has a 50/50 chance of surviving after enduring multiple medical problems ... the apparent result of complications from drug use.Our sources say doctors are saying 4 of Lamar's organs, including his kidneys, are failing. As we reported, he's had a series of strokes in the hospital and has heart problems as well.
The doctors are saying with each failing organ the chances of survival go down significantly.
We're also told doctors are having trouble determining the extent of any brain damage because the organ issues make it difficult to test and get an accurate reading on brain function.

Another TMZ report below...


Lamar Odom took 10 Reload pills over the course of 3 days before he fell into unconsciousness -- according to people at the brothel -- and the FDA says the pills are so dangerous they've advised consumers to throw them away IMMEDIATELY.
The FDA determined Reload contained sildenafil, the active ingredient in Viagra. The label does not reveal the presence of that ingredient, which is normally restricted to prescriptions monitored by a doctor.
The FDA says sildenafil can "lower blood pressure to dangerous levels."

The FDA sent a warning to consumers in 2013, saying, "Consumers should stop using this product immediately and throw it away."
The brothel sold Reload and Lamar got it when he arrived. The Sheriff seized the remaining inventory of Reload from the display case.
We tried to get in touch with the company that makes Reload, but it looks like it went out of business.


UKAWA: Daftari La Wapiga Kura ni Chafu

0
0
WAKATI Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) ikiwa ndio kwanza imelikabidhi Daftari la Kudumu la Wapiga Kura kwa vyama vya siasa na wadau wengine wa uchaguzi, ili kufanyiwa uhakiki, uchunguzi umeonesha daftari hilo ni chafu na haliaminiki. Anaandika Charles William … (endelea).
Siri hii inafichuka siku tisa tu kabla ya Oktoba 25 ambapo Watanzania wapatao milioni 22 wanatarajiwa kujitokeza vituoni kupiga kura ya kuchagua Rais wa Jamhuri ya Muungano, Wabunge na Madiwani.
Kwa Zanzibar, kutakuwa pia na uchaguzi wa Rais wa Zanzibar, Wajumbe wa Baraza la Waakilishi na Madiwani.
Hatua hiyo inakuja siku moja tangu Tume ya Uchaguzi iruhusu vyama vya siasa kuchukua daftari hilo ndani ya shinikizo kubwa za viongozi wakuu wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA).
Mbele ya waandishi wa habari leo, Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Profesa Abdallah Safari pamoja na Mkurugenzi wa Uchaguzi wa chama hicho, Reginald Munisi, walisema kumebainika “madudu na upungufu mwingi kwenye daftari. Kwa hakika haliaminiki.”
“Tumeanza kulifanyia ukaguzi daftari la Tume baada ya kulipata jana Jumatano, na kwa tuliyoyaona, sasa tumeelewa ni kwanini walikuwa hawataki kulitoa mapema,” amesema Prof. Safari ambaye ni wakili wa Mahakama Kuu nchini.
“… ni wazi Tume hii ambayo si tume huru imejiandaa kuhujumu uchaguzi kwa kuwa katika kituo kimoja tu tulichokagua tumeona majina feki mengi yakiwa yameingizwa,” ameongeza Munisi ambaye amesema ukaguzi ulifanywa katika jimbo la Dodoma mjini.
Dosari za msingi zilizobainika katika ukaguzi huo ni
  • Majengo kuandikishwa kama wapiga kura. Katika hali ya kushangaza picha za majengo, ikiwemo migahawa zimeonekana kuwa ni sehemu ya majina ya wapigakura wa jimbo la Dodoma Mjini huku zikibeba majina ya watu na namba ya kitambulisho cha mpiga kura.
  • Baadhi ya vitambulisho kuonekana vikiwa na picha mbili: kumekutwa baadhi ya vitambulisho vinachoandamana na picha ya halisi za watu wengine nyuma.
  • Raia wa kigeni kuandikishwa: Kumekutwa majina ya wasiokuwa raia wa Tanzania wamejumuishwa kwenye daftari, majina mengine yakiwa yasiyoeleweka; picha za raia wanaoonekana kuwa wageni kama Wachina na Wazungu zimeonekana zikiwa sehemu ya wapigakura wa Tanzania; na majina yenyewe yana herufi tupu zisizo na irabu na hivyo kushindwa kusomeka. Kwa mfano limekutwa jina lililoandikwa LHPG SVWTN.
  • Picha za pikipiki kutokeza kama majina ya wapigakura: kumekutwa picha za pikipiki zikiwa ni sehemu ya majina ya wapigakura huku majina na picha hizo yakiwa na namba za vitambulisho vya wapigakura.
  • Majina yalioainishwa kuwa ni ya wanaume yana picha za wanawake: baadhi ya majina yalioneshwa kuwa ni ya kiume na kitambulisho kuonesha kuwa jinsia inayomiliki kitambulisho ni ya kiume lakini picha ni za wanawake.
  • Picha za wapigakura kupigwa katika maeneo tofauti ikiwemo sehemu zenye mabati na mbao badala ya kitambaa kimoja kilichokuwa kikitumiwa kwenye vituo vya Tume:picha za baadhi ya wapigakura zimeonekana kwa mwonekano tofauti wa nyuma (background), ikiwemo kupigwa kwenye sehemu za mabati na mbao hivyo kuzua hofu kuwa huenda uandikishwaji uliendelea katika maeneo mengine baada ya muda wa uandikishaji kumalizika.
Prof. Safari amesema kufuatia uchafu wa daftari, wanaandaa barua kwenda jumuiya za kimataifa ili kuzitahadharisha namna ambavyo serikali ya Chama Cha Mapinduzi inavyoshirikiana na Tume ya Taifa ya Uchaguzi kuvuruga uchaguzi.
“Leoleo tunaandika barua na kuzituma mahakama ya kimataifa ya uhalifu wa kivita ICC, tunaipelekea pia Jumuiya ya Madola, Umoja wa Ulaya, Umoja wa Afrika pamoja na Umoja wa Mataifa kuwajulisha waone mbinu chafu za CCM kutafuta ushindi wa goli la mkono… wanajiandaa kuiingiza nchi katika machafuko,” ameeleza Prof. Safari.
Munisi amesema wanaitaka tume ya taifa ya Uchaguzi kutoa majibu juu ya daftari hilo na kulirekebisha haraka sana kabla hawajatangaza uamuzi mwingine watakaouchukua iwapo hawataridhishwa na hatua za NEC.

HABARI Kuhusu Helikopta ya CCM Iliyoanguka Mbugani Ikiwa na Mbunge Deo Filikunjombe

0
0
Usiku wa kuamkia leo October 16 2015 majukwaa  ya siasa Tanzania yametawaliwa na ajali ya Helikopta ambayo imeanguka na kulipuka kwenye mbuga ya Wanyama ya Selous ambapo Waziri wa maliasili na utalii Lazaro Nyalandu alithibitisha kwamba mmoja wa waliokuwemo ndani ni Mbunge wa Ludewa Deo Filikunjombe (CCM).

Kupitia  ukurasa  wake  wa  Twitter,Nyalandu  aliandika;
"Tumetuma vikosi vya maafisa na maaskari katika eneo la Selous kulikotokea ajali ya helikopta katika harakati za uokozi, ajali ya helikopta imetokea katika kitalu R3 ndani ya mbuga ya Selous na mashuhuda wanasema ilianguka na kulipuka ng’ambo ya mto Ruaha

"Mashuhuda wa ajali ya helikopta iliyotokea Selous walikuwa kitalu R2 na walishuhudia ikianguka na kulipuka ng’ambo ya mto Ruaha Kitalu R3, Maafisa na Maaskari wanaelekea eneo la tukio kutokea Msolwa na Matambwe na tumeagiza vikosi vilivyo kwenye doria Selous kushiriki uokoaji

"Mashuhuda wa ajali ya helikopta Selous walikuwa Kitalu R2 wanasema ilianguka baada ya majira ya saa 12 jioni na kulipuka, serikali kupitia wizara ya maliasili na utalii inachukua hatua zote kuwafikia wahanga na majeruhi wa ajali ya helikopta Selous usiku huu

"Nimeagiza section 2 zenye askari 16 kutoka Matambwe na Msolwa (Selous) kwenda eneo la tukio, RPC Morogoro na mkuu kanda ya Msolwa (Selous) wanashirikiana, hatujui kitakachokuwa kimewapata wasafiri ndani ya helikopta iliyoanguka akiwepo Mh, Filikunjombe, tuungane kuwaombea kwa Mungu"

Katika taarifa nyingine kutoka upande wa CCM iliyotolewa na naibu waziri wa mawasiliano sayansi na teknolojia January Makamba mida ya saa sita usiku ilisema:  "Tumesikia habari za chopa kuanguka huko Selous. Mungu aepushe kusiwe na majeruhi. Chopa zote zinazotumiwa na CCM kwenye kampeni ziko salama"

Baadae aliandika :"Kwakuwa ilisemekana kuwa chopa ya kampeni ya CCM imeanguka, tulifuatilia/kubaini/kuripoti kuwa tulizokodi kama Chama hakuna iliyoanguka". Hiyo ndio ilikua tweet ya mwisho kuandikwa na January Makamba usiku lakini badae aliretweet kilichoandikwa na Waziri Nyalandu na Zitto Kabwe.

Zitto aliandika:"Naomba utulivu.(1) ajali ya helkopta imethibitishwa (2) kuwaka hakujathibitishwa (3) ndugu yangu Deo alikuwamo (4) hakuna uthibitisho wa madhara, naomba utulivu mpaka tupate taarifa rasmi zilizothibitishwa na mamlaka husika, naomba sana hilo ili kuepuka sintofahamu"

Baadhi Ya 'Vituko' Vilivyopo Ndani ya Daftari la Wapiga Kura.....Picha Zimepigwa jana Wakati UKAWA Wakiongea na Waandishi wa Habari

0
0
Huyu  Kaandikishwa  kwa  jina  la  GGGHUH  GGJGJHGHG GGHGGGHG

Mwangalie  vizuri  mzungu    na  majina  yake. Picha  ya  pembeni  kulia  ni  kitu  cheusi  na  siyo  sura  ya  mtu
Angalia  Jina  na  hiyo  picha. Kwa  kuiangalia  sidhani  kama  ni  picha  ya  binadamu
Tazama  majina  na  picha
Hizi  picha  mbili  za  kulia  sio  za  binadamu. Moja  ni  kama  ya  mlango, nyingine  ni  weusi tu  unaonekana

Mpekuzi blog

Alichokiandika Zitto Kuhusu Rafiki Yake Deo Filikunjombe

0
0
Zitto aliandika >>> ‘Naomba utulivu.

1) ajali ya helkopta imethibitishwa 

2) kuwaka hakujathibitishwa

3)ndugu yangu Deo alikuwamo 

4)hakuna uthibitisho wa madhara, naomba utulivu mpaka tupate taarifa rasmi zilizothibitishwa na mamlaka husika, naomba sana hilo ili kuepuka sintofahamu

Jerry Silaa Aandika Haya Kuhusu Ajali ya Helkopta ya CCM..Kumbe Baba yake Naye Yumo Katika Hiyo Ajali

0
0

Jerry Silaaa Ameandika Haya Katika Ukurasa Wake wa Instagram

@jerrysilaa - Baba yangu Capt.William Silaa akiwa na Mhe.Deo Filikunjombe na abiria wengine walipata matatizo ya engine ya helicopter 5Y-DKK jana jioni wakitokea Dar kuelekea Ludewa. Taarifa za mwisho ilionekana imeanguka kwenye msitu wa Selous. Hakuna mawasiliano ya simu. Usiku kucha vyombo vyote vya serikali vimeendelea na jitihada za kufika eneo la tukio na jitihada kubwa zaidi zinaendelea asubuhi hii.
Nawaomba wote kuwa watulivu kwani jambo hili linahitaji umakini wa hali ya juu na ushirikiano wa taasisi nyingi za wizara tofauti.
Tuwaombee wote Mungu awanusuru. 

Lowassa Aionya Tume ya Uchaguzi Kwa Kinachoendela Kuelekea Uchaguzi Mkuu 25 Oct

0
0
Mgombea urais anaesubiri kuapishwa Edward Lowassa akiwa katika jimbo la Magu ameitaka tume ya uchaguzi kuwa makini kama kweli tume hiyo iko huru la sivyo wataiingiza nchi katika matatizo makubwa ambayo hayajawahi kutokea nchini.

Lowassa amewataka tume kuwa makini pasipo kuyumbishwa kwa kuwa amani ya nchi hii iko mikononi mwao.Alisema anasikitishwa sana na maelezo yanayotolewa na tume hiyo huku akihoji wapi uhuru wa tume hiyo kama walivyodai mwanzo kuwa wako huru.

Lowassa pia ameitaka serikali ya CCM kutocheza na amani ya nchi hii.

This Is What a Tanzanian Witchdoctor told RAILA ODINGA About RUTO And His ICC mess

0
0

In March this year, Mbita MP, Millie Odhiambo, claimed that Homa Bay Women Representative, Gladys Wanga once told him that former Prime Minister Raila Odinga uses witchcraft to keep his supporters around him without taking them anywhere.

Millie, who made these remarks during an interview with Radio Ramogi, claimed that Wanga told her that Raila visits various witchdoctors’ in Tanzania and Nigeria and that is why he easily wins elections in many parts of the country.

Since visiting witchdoctors and traditional medicine-men is synonymous with ODM party leaders, there are whispers within ODM circles that Raila Odinga met a Tanzanian medicine-man, who gave him the right “ingredient” to win the 2017 elections.

A source in ODM says that MPs with the opposition are speculating that Raila was told that the secret to winning the 2017 General Elections is by courting Deputy President William Ruto because he has the key to State House.

Raila was told to court Ruto again if he wants to win the 2017 elections like he did in 2007 only to be rigged out by former President, Mwai Kibaki.

“They are saying he was told he must court Ruto and the Kalenjin nation again if he wants to sleep in State House,” a source said.

Over the past two weeks, a number of ODM MPs led by Dr Oburu Odinga, Homabay Town MP, Peter Kaluma, and Ugunja MP, Opiyo Wandayi, have been camping in Kalenjin land trying to woo locals to the opposition side.

What is shocking is that the ODM MPs have been saying how they will rescue Ruto from the jaws of ICC, something they haven’t done for seven years Ruto has been appearing at The Hague.

Kenyan post

Shindano la Serengeti Masta Lahitimishwa Jijini Mbeya na Arusha

0
0
Mkazi wa Arusha na mpenzi wa bia ya Serengeti Premium Lager Laota Elias akishiriki katika shindano la mwisho la kumtafuta Serengeti Masta wa jumla kwa mkoa wa Arusha katika kuitambua ladha halisi ya bia ya Serengeti Premium Lager. Mashindano hayo ya mwisho yalifanyika katika baa ya Bondeni iliyopo Kijenge juu jijini Arusha ambapo yaliwakutanisha washindi mbalimbali wa baa za mkoa huo waliofika kuchuana vikali ili kumpata mshindi wa jumla. Kampeni hiyo imefikia tamati jijini humo baada ya kudumu kwa takribani miezi miwili ikizunguka baa kwa baa kusaka washindi waliopewa jina la “Serengeti Masta”.

Mkazi wa Arusha Cleophas John akifurahi pamoja na marafiki zake baada ya kupita kwenye ngazi ya kwanza ya shindano la kumtafuta “Serengeti Masta” wa mkoa wa Arusha linaloendeshwa na bia ya Serengeti Premium Lager toka SBL wakati wa  shindano hilo ambalo lilifanyika katika baa ya Bondeni-Kijenge juu jijini Arusha. Shindano hilo limefikia tamati jijini humo baada ya kudumu kwa takriban miezi miwili (2) ikiwaburudisha na kuwazawadia wateja wa bia hiyo na kuwafundisha wahudumu wa baa mbalimbali juu ya utoaji huduma kwa wateja

Mratibu wa mashindano ya kumsaka Serengeti Masta Yassin Khalfan (katikati) akiwa na baadhi ya washiriki wa shindano hilo kutoka Baa mbalimbali jijini Mbeya kushoto ni Faraji Mbwambo kutoka Gambino Bar na Ibrahim Allan kutoka Liz Pub. Kampeni hiyo ya Serengeti Masta imewakutanisha wateja na mameneja wa bia hiyo katika kujifunza kwa undani kuhusiana na bia ya Serengeti Premium Lager ambapo mameneja hao walitoa zawadi mbalimbali kwa washindi walioweza kuitambua ladha halisi ya bia hiyo katika kipindi chote cha kampeni ambapo pia waliweza kuwafikia wahudumu wa baa zaidi ya 4000 katika miji tofauti.

Mshiriki wa shindano la Serengeti Masta na mkazi wa Arusha Daniel Mwakasungule akionja ladha tofauti za bia zilizo mbele ya meza yake ili kuitambua ladha halisi ya bia ya Serengeti Premium Lager katika shindano la kumpata Serengeti Masta wa mkoa wa Arusha ambalo lilifanyika katika Baa ya Bondeni, Kijenge juu jijini Arusha mwishoni mwa wiki hii.

Mshindi wa jumla wa shindano Serengeti Masta kwa jiji la Mbeya Faraji Mbwambo kutoka baa ya Gambino jijini Mbeya akionesha kitita cha fedha sh. 100,000 alizotunukiwa baada kuibuka mshindi wa jumla wa kuitambua ladha ya bia ya Serengeti Premium Lager kati ya vinywaji vitano vinavyozalishwa na kampuni ya SBL. Kampeni hiyo ya Serengeti Masta imewakutanisha wateja na mameneja wa bia hiyo katika kujifunza kwa undani kuhusiana na bia hiyo ambapo mameneja hao walitoa zawadi mbalimbali kwa washindi walioweza kuitambua ladha halisi ya bia hiyo katika kipindi cha kampeni
Mmoja wa wateja na mnywaji maarufu wa bia ya Serengeti Premium Lager Tuntufye Mwakaje maarufu kwa jina la “Tupac” akiburudika na bia hiyo wakati wa shindano la kumsaka Serengeti Masta wa jumla kwa wakazi wa jiji la Mbeya lililofanyika  kwenye baa ya Mbeya Pazuri.
Viewing all 104415 articles
Browse latest View live




Latest Images