Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104702 articles
Browse latest View live

Shilole kuchora tattoo nyingine ya Nuh Mziwanda kalioni!

$
0
0
Hivi karibuni Zuwena Mohamed ‘Shilole’ alichora tattoo yenye jina la boyfriend wake Naftari Mlawa ‘Nuh Mziwanda’ kwenye kifua chake, ikiwa ni ishara ya kuwa mapenzi yao yanazidi kushamiri.
shilole-2
Kama vile haitoshi Shishi bado ana mpango wa kuongeza mchoro mwingine kwenye sehemu za siri.
Akizungumza na Global Publishers, Staa huyo wa mduara, Shishi amesema ana mpango wa kuchora tena jina la mpenzi wake, Nuh kwenye moja ya kalio lake ikiwa ni njia mojawapo ya kuonyesha mapenzi yake ya dhati kwake.
shilole-1
“Mimi bado tattoo moja ya muhimu sana ambayo nataka kuchora kwenye kalio ili kuonyesha ni jinsi gani nampenda mpenzi wangu Nuh,” alisema Shilole.
Nuh Mziwanda ndiye aliyekuwa wa kwanza kuchora tattoo zenye majina ya Shilole kwenye mwili wake, kitendo kilichomshawishi mpenzi wake Shishi naye kuchora.
Source: GPL

Lulu Michael Alia Kwa Uchungu Akisimulia Jinsi Mama Yake Alivyompigania Akiwa Jela

$
0
0
Muigizaji wa filamu, Elizabeth Michael aka Lulu amelia kwa uchungu baada ya kukumbuka jinsi mama yake alivyompigania wakati yupo jela alikopelekwa kwa kusababisha kifo cha marehemu Steven Kanumba.

Akizungumza Ijumaa hii kwenye kipindi cha Uhondo cha EFM, Lulu alisema mama yake alifanya kila njia ili kuhakikisha mtoto wake anakuwa salama.

Mama yangu ana mapenzi pili ni jasiri,” alisema. “Ni mtu ambaye anaweza kusimama kwa kitu anachotaka kufanya na akafanikiwa. Sio mzazi mwenye mapenzi ya kumharibu mtoto. Hajali wewe ni Lulu wewe ni nani, Lulu mwisho getini, ukiingia ndani wewe ni mtoto,” aliongeza.

Tumepitia maisha fulani ambayo sio marahisi sana, kwahiyo nyakati tunazo nyingi lakini wakati ambao ulikuwa mgumu sana na akasimama wakati dunia nzima ilikuwa against, ni kitu ambacho kinanifanya niwe proud of her. Kipindi cha kesi yangu ni kipindi ambacho alitukanwa aliongelewa vibaya, ushirikina lakini alikubali akasema vyovyote vile lakini huyu ni mwanangu na akapigana na mpaka leo maisha yanaendelea,” alikumbushia Lulu huku akilia kwa uchungu.

Hivi Ndivyo Helikopta Ilivyomuua Shujaa Deo Filikunjombe...Mashuhuda Waelezea Kilichotokea

$
0
0
Chopa
Polisi na wananchi wakiwa eneo la tukio  baada ya Chopa kuteketea kwa moto.
AJALI ya chopa (helikopta) iliyotokea usiku wa kuamkia jana, Oktoba 16, 2015 katika Hifadhi ya Selous, eneo la Msolwa mkoani Morogoro, imeyakatisha maisha ya aliyekuwa Mbunge wa jimbo la ludewa, Mhe. Deo Filikunjombe (43), pamoja na watu wengine watatu waliokuwa ndani ya helikopta hiyo.
Deo-Filikunjombe
Deo Filikunjombe.
Kwa mujibu wa taarifa zilizothibitishwa na Kamishna wa Oparesheni na Mafunzo wa Jeshi la Polisi, Paul Chagonja, Mhe. Filikunjombe aliyekuwa akitetea ubunge wa jimbo hilo kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), alikuwa na watu wengine watatu kwenye helikopta hiyo, akiwemo rubani, Kepteni William Silaa ambaye ni baba wa Jerry Silaa, Vitalis Blanka Haule anayetajwa kuwa ndugu wa Filikunjombe na Egdi Mkwera, Ofisa Tawala wa Mkoa wa Tarime na mtaalam wa mifugo.
chopa 2
Chopa (helikopta) aliyokuwa akitumia Mbunge wa jimbo la ludewa, Mhe. Deo Filikunjombe (43).
Chagonja alieleza kuwa helikopta hiyo yenye namba za usajili, 5Y-DKK ilikuwa ikitokea jijini Dar es Salaam kuelekea kusini huku taarifa nyingine zikieleza kuwa ilikuwa ikielekea jimboni kwake, Ludewa kabla ya kupata hitilafu ya injini ikiwa angani, baadaye ikaanguka na kulipuka, ikisababisha eneo lote la ajali kugubikwa na vumbi na moshi mzito.
chopa
Deo Filikunjombe akiwa kwenye helkopta anayodaiwa kupata nayo ajali.
Habari zisizo rasmi zilizolifikia gazeti hili, zilieleza kuwa helikopta hiyo iliondoka jijini Dar es Salaam majira ya saa 9 alasiri. Kabla ya kuruka angani, vyanzo vyetu vinaeleza kuwa helikopta hiyo ilipata hitilafu ndogo za kiufundi ambazo hata hivyo zilirekebishwa na safari ikaanza bila matatizo.
“Ilipofika kwenye Hifadhi ya Selous, rubani aligundua kwamba kuna hitilafu kwenye injini, akawa anajaribu kutafuta sehemu ya kutua kwa dharura ndani ya hifadhi hiyo lakini kabla hilo halijatimia, helikopta ilipoteza mwelekeo kabla ya kudondoka na hatimaye kulipuka,” kilieleza chanzo chetu kwa sharti la kutotajwa jina gazetini.
12107262_10203566066031418_6703966378237878945_n (1)
...Wakiendelea kufanya uchunguzi eneo la tukio.
Habari nyingine zinazosambaa kwenye mitandao ya kijamii, zinaeleza kuwa helikopta hiyo ilianza kuwaka moto ikiwa angani kabla ya kuanguka kandokando ya Mto Ruaha unaopita ndani ya hifadhi hiyo ambapo baadhi ya maoni yalidai huwenda chopa hiyo ilihujumiwa na hivyo kutaka uchunguzi zaidi. 
Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu usiku wa kuamkia jana, aliandika kuhusu ajali hiyo kupitia mitandao ya kijamii ambapo alieleza kupata taarifa kutoka kwa askari wa wanyamapori ndani ya hifadhi hiyo kubwa kuliko zote nchini Tanzania na kueleza hatua zilizochukuliwa:
“Mashuhuda wa ajali ya helikopta iliyotokea Selous walikuwa kitalu R2 na walishuhudia ikianguka na kulipuka ng’ambo ya Mto Ruaha Kitalu R3, maafisa na askari wanaelekea eneo la tukio kutokea Msolwa na Matambwe na tumeagiza vikosi vilivyo kwenye doria Selous kushiriki uokoaji.”
Habari zaidi kutoka vyanzo vyetu, zinaeleza kuwa kutokanana jografia ya eneo ajali hiyo ilipotokea, iliwachukua muda mrefu maafisa usalama na askari kufika eneo hilo, kutokana na ugumu waliokutana nao kuvuka Mto Ruaha hasa wakati huo wa usiku. Hata hivyo, askari na maafisa hao waliendelea kuhangaika usiku kucha mpaka siku iliyofuatia (jana Ijumaa), walipofanikiwa kufika eneo la tukio lakini tayari walikuwa wamechelewa kwani Mhe. Filikunjombe, Kepteni Silaa na wenzao wawili, tayari walishakata roho.
Naye Jerry Silaa, Meya wa Manispaa ya Ilala ambaye pia ni mtoto wa rubani wa helikopta hiyo, jana mchana aliandika kupitia ukurasa wake wa Instagram: “Kwa masikitiko makubwa nimepokea taarifa rasmi kutoka kwa timu ya uokoaji iliyofanikiwa kufika eneo la ajali na kukuta abiria wote na rubani wamepoteza maisha.
12065789_952647898130144_658653796879178835_n (1)
Kifo cha Filikunjombe, kimetokea siku 9 kabla ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania na muda mfupi baada ya vifo vya wanasiasa wengine wawili, aliyekuwa Waziri wa Viwanda na Biashara, Dk. Abdallah Kigoda na Dk. Emanuel Makaidi, aliyekuwa Mwenyekiti wa Chama cha NLD na Mwenyekiti Mwenza wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa).
Baadhi ya wananchi wa gazeti hili waliopata nafasi ya kutoa maoni yao kufuatia mfululizo huo wa vifo vya viongozi wa kisiasa, walionesha wasiwasi mkubwa na kuhoji kinachoendelea nchini huku wengine wakihisi ni mambo ya kafara.
Enzi za uhai wake, ukiachilia mbali ubunge, Mhe. Deo Filikunjombe alipata kuwa Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) iliyosimamia kidete sakata la ufisadi wa Escrow na kusababisha viongozi kadhaa wakubwa serikalini kung’oka kwenye nyadhifa zao. Mungu azilaze roho za marehemu wote mahalipema peponi, Amen!

Source:GPL

Sad News: Askari Aliyekuwa Akiongoza Msafara wa Magufuli Afariki Dunia Kwa Ajali

$
0
0

Askari aliyekuwa akiongoza msafara wa mgombea urais wa CCM Dr.John Pombe Magufuli amefariki baada ya kugongana na bodaboda eneo la ubungo jijini Dar es Salaam.

Kamanda wa Polisi kikosi cha usalama Barabarani Mohamed Mpinga amethibitisha kutokea kwa kifo cha Askari huyo.

Dk Magufuli amefanya kampeni katika jimbo la Segerea leo  jijini  Dar  es  Salaam  kabla  ya  kuruka  na  kuelekea  jijini  Mwanza  ambako  amefanya  mkutano  mkubwa  wa  hadhara  katika  viwanja  vya  Furahisha

REVEALED: Why All Women Should Stop Wearing Bras

$
0
0

Science has revealed the hazards involved in wearing bras for women.

'National No Bra Day' is observed annually on October 13. It is a day set aside for women to let off their bras at home in order to raise awareness for breast cancer.

Since the emergence of bras, they have come in handy for women across the world. While majority of them use them as a tool to look 'firm' and shield the boobs from dangling all around unnecessarily, a smaller divide of the woman race wear bras for other different purposes, all best known them. However, a notorious research on bras and breasts came out a couple of years ago.

According to IFLScience, a sport science researcher and a professor, Jean-Denis Rouillon, conducted a 15-year research on the effect of bras on 330 women aged 18 to 35 and the outcome was mind boggling! The research was geared towards knowing the changes that occur to the breasts yearly when a bra is worn regularly and otherwise, using a slide rule and a caliper.

The research opined that when a young girl wears a bra from an early age, it does not help support the chest, reduce back pain or prevent breast sagging, as against popular belief. "Medically, physiologically, anatomically – breasts gain no benefit from being denied gravity. On the contrary, they get saggier with a bra," Professor Rouillon told France Info in an interview.

According to the research, young women get toned breasts and supporting breast tissue if no bra were used. Women that stopped wearing bras – through choice, not as a requirement of the study – had a 7-millimeter (0.3-inch) lift in their nipples compared with their other counterparts. This is because it is claimed that bras have a way of slowing down circulation and reduce breast tone with time.

A doctor who was not a part of the research, Stafford Broumand, also confirmed the research, saying: "For younger women, not wearing a bra will lead to increased collagen production and elasticity, which improves lift in a developing breast."

However, the research team cautioned on drawing general conclusions from the research, saying that the women in the study are not a representative of the population as a whole.

Hatimaye Lowassa Ashindwa Kuhutubia Tunduma..Licha ya Umati wa Wananchi Kufurika

$
0
0
Lowassa ameshindwa kuhutubia leo Tunduma kisa Vyombo vinasumbua.

Katika team yake ya kampeni hakuna aliepanda jukwaani zaidi ya Mbowe kwa dakika moja kuwaeleza wananchi kuwa tatizo ni vyombo.

Dr. Slaa akimbilia tena Marekani, awatakia Watanzania uchaguzi salama

$
0
0
Baada ya kutapatapa huku na kule na kushuhudia jinsi alivyoshusha heshima yake na kudharauliwa na wananchi Dr. Slaa kaamua kukimbilia tena Marekani na kuwatakia watanzania uchaguzi mwema.

Dr. Slaa hapa karibuni heshima yake ilishuka sana, baada ya kuanza kutumiwa na CCM. Maskini saizi baada ya kuona hana impact tena wameamua kuachana naye jumla na yeye kuamua kurudi Marekani kwa aibu...

Mytake: Hiyo ndio dhambi ya usaliti. Kamwe hawezi kuishi kwa furaha

Source: Raia Tanzania... 16.10.2015
By by Ocampo four

Breaking News: Two People Died After CHADEMA & CCM Fight at Tunduma Today

$
0
0


Breaking News: Two People Died After CHADEMA & CCM Fight at Tunduma Today


Two People Died After CHADEMA & CCM Fight



Breaking News: Wafuasi wa CCM na CHADEMA Wachomana Visu Tunduma.......Watu wawili Wapoteza Maisha

$
0
0
Watu wawili wamefariki  dunia  baada  ya  vurugu  kubwa  kutokea kati  ya wafuasi  wa  CCM  na  CHADEMA  katika  mji  mdogo  wa  Tunduma  Mkoani  Mbeya.

Vurugu  hizo  zimetokea  baada  ya  wanachama wa CCM kuweka mawe barabarani ili wafuasi wa CHADEMA wasipite  kuhudhuria  mkutano  wa  Lowassa.

Hali  hiyo  iliwafanya  wafuasi  wa   CHADEMA kushuka  ili kutoa mawe hayo, ndipo akatokea kijana  mmoja wa CCM na kumchoma kisu kijana mmoja wa CHADEMA  ambaye  alifariki  dunia  papo hapo.

Baada  ya  tukio  hilo, vijana wa CHADEMA nao walijibu mapigo kwa  kumshambulia  na  kumuua kijana huyo.

Picha  Zinatisha....Kuziona  Bonyeza=>HAPA

Is Diamond Platnumz Africa's Biggest Superstar?

$
0
0
Since Tanzanian music star, Diamond Platnumz blew up on the continent, his star power has known no bounds. Giving the Nigerians (who normally dominate the African music scene) a run for their money, Diamond has caused several upsets in numerous pan-African awards, leaving Nigerian fans asking why or how?


Tanzania’s estimated 50 million population is nothing compared to Nigeria’s estimated 180 million population, but one thing that Diamond Platnumz has working for him is the seeming support from East Africa (especially Swahili speaking territories) .

According to my recent interaction with some journalists from Kenya, I found out that the biggest and trendiest form of social media in Tanzania is Instagram. It is not surprising therefore that Diamond has some 1.1 million followers on Instagram ( He has over 800,000 fans on Facebook and just over 241,000 followers on Twitter). Davido also has 1.1 million followers on Instagram, while Wizkid has 1 million. What’s more interesting with Diamond’s Instagram presence is the fact that his 3-month old baby, Tiffah has 157,000 followers on Instagram. I remember once checking out the accounts of the ‘children’ of US rapper, The Game wondering why those kids had so many followers, now we have a similar African story.

Clearly Diamond Platnumz’ fans are loyal – isn’t that what great superstars are made of? I remember flying to Dubai from Mauritius with several of the African stars, and Diamond was the one who was swamped by airport staff for photos- right after going through security.

SOURCE : ameyaw debrah Blog
(Award winning Ghana top blog)


Vincent Nyerere Amenusurika Kufa Siku ya Leo....Bomu Lakutwa Kwenye Gari yake

$
0
0
Bomu La kutengenezwa lilitegwa kwenye gari no T720 ANP.

Toyota land cruiser ya Mhe Vincent Nyerere mgombea ubunge CHADEMA Musoma mjini Leo kwa ajili ya kuondoa maisha yake, Mungu amekataa hila chafu, uchunguzi wa tukio hilo bado linaendelea kuchunguzwa na jeshi la police...
Source:Vicent Nyerere Facebook

Nyumba Ya James Mbatia Yateketea Kwa Moto

$
0
0
Nyumba ya makazi ya mwenyekiti wa chama cha NCCR-Mageuzi, James Mbatia imeteketea kwa moto siku ya Jumamosi, majira ya saa saba u nusu mchana, kwa kile kilichoelezwa kuwa huenda ni hitilafu ya umeme unaosemekana kukatika asubuhi na kurejea mchana kwa nguvu kubwa.

Akizungumza na Channel TEN, kaka wa Mbatia, Felix Kessy amesema hadi sasa wanachoweza kueleza ni uharibifu uliotokea kutokana na moto huo, kwani hawakuwepo wakati wa tukio, ingawa anawashukuru majirani walioweza kuokoa baadhi ya vitu vya ndani.

Amesema ni mapema mno kuzungumzia aina ya uharibifu kwani atakayeweza kujua zaidi ni mkewe na Mbatia ambaye kwa wakati huo Channel TEN ilipofika, haikuweza kuzungumza naye kwa sababu alikuwa amepandwa na shinikizo la damu kutokana na tukio hilo.

Mkuu wa oparesheni hiyo kutoka kikosi cha zima moto na uokoaji kwa wakati huo nyumbani hapo sajenti Haji Madulika amesema kikosi chake kiliwahi eneo la tukio ingawa kutokana na ukubwa wa moto, walishindwa kuokoa baadhi ya vitu. 
  
Aidha ameoneshwa kushangazwa kwake na tabia ya watu kuwashutumu askari wa zimamoto kwa kuchelewa huku wananchi wakielewa hali halisi ya barabara na miundombinu.


Mpekuzi blog

Nicki Minaj Shares New Sexy Photos

$
0
0

Nicki Minaj shared sexy photos of herself and her bestie. Another photo after the cut..




Magufuli Aliteka Jiji la Mwanza.......Hapa Kuna Picha Kadhaa za MAFURIKO Yake-Octoba 17

$
0
0
Mgombea Urais Kutoka chama cha mapinduzi CCM Dr. John Pombe Magufuli ameweka historia katika jiji la Mwanza maarufu kama Rock City. Maelfu ya watanzania wameonesha msimamo wao wa kumuunga mkono Mgombea wa CCM Dr. John Pombe Magufuli.








Men Do You Respect These Kind Of Ladies ?

$
0
0
 So my question now do you respect ladies that smoke?? Are They Wife Material?




Helkopta Nyingine ya Mgombea Ubunge CCM Yapata Hitilafu..Mgombea Ashtukia Aaapa Kuto Ipanda Tena.....

$
0
0
Mgombea ubunge wa Jimbo la Mtera (CCM), Livingstone Lusinde ameapa kutotumia tena usafiri wa anga katika kampeni, baada ya helikopta aliyokuwa anatumia kupata hitilafu na kushindwa kuruka katika Kijiji cha Idifu wilayani hapa, juziLusinde maarufu kwa jina la Kibajaji alithibitisha kuwa helikopta hiyo ilishindwa kuruka baada ya rubani kubaini ilikuwa na hitilafu, na ilikuwa imetua katika eneo la kichaka kijijini hapo.


Jana asubuhi alifika mtaalamu wa ndege kutoka Afrika Kusini na kuirusha hadi Dodoma Mjini.
“Ni kweli kuna tatizo hilo na hadi sasa (juzi) tunasubiri mafundi kutoka Dar es Salaam ili waje kuikagua na kujua tatizo lake nini,” alisema Lusinde, ikiwa ni siku moja baada ya helikopta nyingine kuanguka na kuua abiria wanne akiwamo mgombea ubunge wa Jimbo la Ludewa, Deo Filikunjombe.
Kutokana na hali hiyo, Lusinde alisema, “Hata wakinipa ndege nyingine siwezi kuitumia tena, nimeamua kuwa ardhini na kama kufa bora nifie chini lakini siyo angani. Nasema katika kampeni hizi situmii anga tena na sababu kubwa ni kuwa zaidi ya wananchi wangu 500 wamepiga simu kunisihi nisitumie usafiri wa anga kipindi hiki”. Mgombea huyo ambaye ni mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM na mmoja wa wajumbe wa timu ya kampeni za mgombea urais wa chama hicho, alisema wakati ndege hiyo ikishindwa kuruka alikuwa amefanya mikutano mitatu jimboni kwake na alitarajia kumaliza kisha kuendelea katika mikoa aliyopangiwa kumnadi Dk John Magufuli.

Aliwataja waliokuwamo kwenye helikopta hiyo kuwa ni Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake (UWT) Wilaya ya Chamwino, Devotha Mbogoni; Katibu Mwenezi wa CCM wilaya, Marietha Mkuya; Mwenyekiti wa CCM wa Kata ya Mvumi Mission, Mathias Lusano na yeye na kwamba, wote walitoka wakiwa
CHANZO MWANANCHI

Viashiria Vya Uvunjifu Wa Amani Wiki Moja Kabla Ya Uchaguzi

$
0
0
TAMKO LA ASASI ZA KIRAIA KUHUSU VIASHIRIA VYA UVUNJIFU WA AMANI WIKI MOJA KUELEKEA TAREHE YA UPIGAJI KURA KATIKA UCHAGUZI MKUU TANZANIA TAREHE 25.10.2015

Asasi za Tanzania tumeendelea kufuatilia mchakato wa uchaguzi mkuu 2015 tangu uandikishaji wapiga kura, uhamasishaji hadi kampeni zinazoendelea kwa umakini mkubwa. 

AZAKI tumefanya hivyo tukiamini kuwa uchaguzi  ni sehemu kuu ya michakato ya kidemokrasia hapa nchini kama ilivyo duniani kote. Sisi asasi za kiraia Tanzania, tukiwa watetezi na wasimamizi wa demokrasia, utawala bora na haki za binadamu, hatumuungi mkono mgombea yeyote wala chama chochote cha kisiasa kinachotafuta kuingia madarakani wala hatulengi kuchukua dola.

Kwa ujumla wake, uchaguzi hufanikishwa na wadau wengi tukiwemo sisi AZAKI, Vyombo vya usalama, viongozi wa Dini, Taasisi za Umma kama Tume na Vyombo vya habari. Lakini makundi makuu mawili ya wahusika wakuu ni wapiga kura na wapigiwa kura. 
  
 Ili wapiga kura waweze kuchagua kiongozi atakayeweza kusimamia maendeleo ya nchi na kuhakikisha amani ya nchi inazidi  kudumu  ni lazima viashiria vyote vya uvunjifu wa amani na mazingira ya vitisho kwa wapiga kura  vijadiliwe na wadau na vidhibitiwe mapema.

Usalama na amani wakati wote wa uchaguzi ni suala la muhimu sana na ndio maana Asasi za Kiraia (AZAKI) nchini zimekuwa mstari wa mbele kuhakikisha kuwa uchaguzi mkuu wa mwaka 2015 unakuwa wa kidemokrasia, wa haki  na wa amani.  
  
Tanzania ni Taifa lenye amani kwa muda mrefu sasa, lakini tusipokuwa makini katika kuhakikisha uchaguzi unafanyika katika mazingira ya haki na usawa huenda tukalitumbukiza taifa hili katika machafuko. 
  
Angalizo hili ni muhimu zaidi kwa mwaka huu ambapo hamasa na mashindano vimekuwa kwa kiwango cha juu kuliko miaka mingine yoyote ya nyuma.

Ili kuweza kuhakikisha uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2015 unafanyika kwa  usalama na amani AZAKI   zimeona ni vyema kuanisha masuala mbalimbali yanayoweza kupelekea uvunjifu wa amani nchini  kama angalizo kwa  sekta na taasisi husika kuchukua hatua stahiki mapema.
  
 Mchakato huu umejaa changamoto mbalimbali ambazo kama hakutakuwa na jitahada za ziada basi ni wazi kuwa tutakwenda kufanya uchaguzi tukiwa katika hali tete zaidi. Kati ya hizo changamoto nyingi zinazojitokeza, sisi wana AZAKI tumeanisha mambo sita makubwa yanayohitaji ufumbuzi wa haraka kabla ya tarehe 25 oktoba. Mambo hayo ni kama yafuatayo;

(i) Matumizi Makubwa ya nguvu ya Vyombo vya Usalama

AZAKI  zimegundua kuwa vyombo vya usalama kama Jeshi la Polisi na makundi mengine ya usalama Tanzania Bara na Zanzibar zimekuwa zikilalamikiwa sana kwa kuona kuwa tishio kwa wananchi badala ya kuwa msaada kwa wananchi. Kwa mfano, majeshi haya  yamekuwa yakifanya mazoezi waziwazi  na karibu na makazi ya watu  suala linalopelekea kujenga  uoga na hofu kwa wananchi .
  
 Pia baadhi yao  wameonekana wakitapakaa kwenye makazi ya wananchi huku wakiwa wamevaa sare zao. AZAKI zinatambua umuhimu wa vyombo hivi kipindi cha uchaguzi,  AZAKI tunataka vyombo hivi kufanya kazi zao bila kujenga hofu kwa wananchi na kwa mujibu wa Sheria.

Wito Wetu kwa Vyombo vya Ulinzi na Usalama
  •  Vyombo vya ulinzi na usalama kufanya kazi zake kwa uweledi na tahadhari ya kutowatia hofu wananchi na wapiga kura. Vyombo vya ulinzi visitumie vitisho, nguvu, na silaha za kivita wakati wa mikutano ya kampeni na siku ya kupiga kura.
  • Vyombo vya usalama  kwa namna yoyote   visiegemee  upande wowote wa chama cha siasa bali vitende haki kwa vyama vyote na wananchi wote wakiwemo wagombea mmoja mmoja na wala visikubali kuyumbishwa na mamlaka yoyote nje ya sheria inayovipa mamlaka kutekeleza wajibu wao.
  • Tunalishauri Jeshi la Wananchi wa Tanzania kutojihusisha na mchakato wa uchaguzi kuanzia kipindi cha maandalizi,  cha kampeni,  upigaji kura  na baada ya upigaji kura.

(ii) Daftari la Wapiga Kura na Taarifa za Msingi

 Kwa mujibu wa Katiba na Sheria, Uchaguzi wa Tanzania unasimamiwa na Tume ya Taifa ya  Uchaguzi (NEC) na Tume ya Uchaguzi Zanzibar( ZEC).  AZAKI zimebaini pia pamoja na kufanya vizuri katika hatua zingine Tume za Uchaguzi kwa sasa zimeonyesha udhaifu mkubwa katika eneo la utoaji wa taarifa za msingi kwa wadau na umma kwa ujumla. 
 
Tumeshudia ukinzani wa taarifa mbalimbali zinazotolewa na Tume kama taarifa za idadi halisi ya wapiga kura walioandikishwa pamoja na idadi ya vituo vya kupigia kura. Ukinzani wa takwimu za muhimu kama hizi ni jambo linaloweza kupelekea uvunjifu wa amani kama lisipo simamiwa vyema. 
  
Mambo haya pamoja na mengine yanawaweka wananchi katika hofu kubwa kwa kutokujua kama watapiga kura ama la na endapo idadi halisi ya wapiga kura ni ipi. Hofu inaongezwa na ukweli kuwa Sheria za uchaguzi Tanzania haziruhusu kulalamikia matokeo ya uchaguzi hususani katika ngazi ya urais.
 
Wito wetu kwa Tume za Uchaguzi
  • Tume ya Taifa ya uchaguzi na Tume ya Uchaguzi Zanzibar zitimize  majukumu yao kisheria  kwa kutangaza rasmi takwimu za mwisho  za idadi ya vituo vya kupigia kura na kujibu hoja zinazaoibuliwa na wanasiasa badala ya kuwabeza na kuwapuuza.
  • Tume Itoe Daftari la wapiga kura  lenye vigezo vyote  kwa wadau wote na wanachi kwa ujumla mapema iwezekanavyo ili kutoa fursa ya kurekebisha makosa yatakayobainika.
  • Tume ibandike majina ya wapiga kura kwenye vituo vyote wiki moja kabla ya siku ya kupiga kura kama ilivyoahidi kwa ajili ya wapiga kura kujua vituo watakavyopigia kura.
  • Tume za uchaguzi zifanye kazi kwa uhuru, kufuata sheria, kusimamia kanuni walizokubaliana na vyama vya siasa na kujiepusha kwa namna yoyote kukipendelea chama chochote wakati wote wa mchakato wa uchaguzi.
  • Tume zinapaswa kuhakikisha kuwa zimewapa mafunzo ya uhakika maofisa na wasidizi wa uchaguzi na kuchunguza mienendo yao kabla hawajawakabidhi vituo vya kazi ili kuepusha makosa yaliojitokeza wakati wa kuandikisha wapiga kura.
  • Tume za Uchaguzi zinapaswa kufanya maandalizi mapema, pia kusambaza vitendea kazi vinavyotakiwa kwa wakati ili kuepusha usumbufu unaoweza kujitokeza siku ya upigaji kura pamoja na hisia kuwa baadhi ya maeneo yanacheleweshewa vifaa kwa makusudi.
  • Tume zihakikishe kuwa watu wote wenye sifa na kustahili kupiga kura ambao hawakuandikishwa katika vituo waliko siku ya upigaji kura wanawezeshwa kufaidi haki yao ya kupiga kura kwa mujibu wa sheria.
  • Tunazitaka Tume ziruhusu mawakala wa vyma vya siasa kuingia kwenye chumba cha mwisho cha ujumlishaji wa kura za urais (National Tallying Centre) ili kuondoa hofu ya kuibiwa kura. Ifamike kuwa matokeo ya urais yakishatangazwa hayawezi kupingwa mahakamani.  Ni kinyume na taratibu za uchaguzi kuwazuia mawakala wa vyama vya siasa kuingia kwenye kituo kikuu cha kitaifa cha ujumlishaji wa kura.
  • Tume zitangaze matokeo sahihi bila ya kuchelewesha ili kuepusha kutokea kwa vurugu zinazoweza kujitokeza.

(iii)Mgogoro wa Kusubiri Matokeo katika umbali usiopungua Mita 200

AZAKI tumebaini kuwa jambo lingine linaloweza kuchangia uvunjifu wa amani ni  mgogoro uliobuka kuhusu uhuru wa wapiga kura kubaki vituoni katika umbali usiopungua mita 200. 
  
 Kwa mujibu wa  sheria ya Taifa ya Uchaguzi ya Mwaka 1985 sura ya 343 ya sheria za Tanzania kama zilivyopitiwa mwaka 2010  mpiga kura anapewa haki ya kupiga kura na kuondoka kuendelea na shughuli nyinginezo au kubaki kituoni kusubiri matokeo ili mradi anafanya hivyo katika umbali usiopungua mita 200 toka kituoni na kwamba hafanyi mkutano. Kwa tafsiri hii, mpiga kura hajalazimishwa kurudi nyumbani baada ya kupiga kura wala hajakatazwa kuwepo nje ya eneo la katazo la kisheria kwa mujibu wa kifungu cha 104 (1).
 
Sheria inamtaka mpiga kura asionekane ndani ya eneo la  kituo cha kupiga kura baada ya kumaliza kupiga kura(within the vicinity) na haimlazimishi mwananchi arudi nyumbani mara baada ya kupiga kura au asogee umbali wa mita 200 bali sheria ya uchaguzi inaweka bayana kwa wananchi/mpiga kura kutokupiga kampeni au kuvaa nguo zenye alama au nembo ya chama chochote katika siku hiyo.

Wito Wetu kwa Tume za Uchaguzi na Jeshi la Polisi

  • Kwa kuwa hili limekuwa  kawaida sasa katika chaguzi zilizopita hapa  Tanzania wananchi kubaki vituoni na  kusubiri matokeo karibu na vituo kwa umbali wa mita 200, na  kutokana na ufinyu wa muda usioweza kutoa mwanya wa kurekebisha sheria hii, Tunazitaka Tume za  uchaguzi  zitumie busara  katika kuamua  suala hili kwa kupima faida na hasara za kuzuia wananchi kubaki vituoni kwa umbali wa mita 200 kama walivyozoea katika  chaguzi zilizopita.
  •  Pia, Tume zitoe maelekezo yenye kuangalia zaidi maslahi ya Taifa kwa wananchi  badala ya kusikiliza upande wowote kati ya wanaovutana kuhusu suala hili.  Ushauri wetu kuhusu jambo hili ni kuwa wapiga Kura waamue kuendelea na shughuli zao baada ya kupiga kura lakini wanaotaka waweze kubaki vituoni kwa umbali wa mita 200 kwa kadri ya mapenzi yao huku wakiepuka kufanya kinachofanana na mikutano.
  • Mahakama isadie kutatua mgogoro huu wa tafsiri ya kisheria ili kuepusha  machafuko katika Taifa hili yanayoweza kutokana na imani kuwa kukatazwa kubaki vituoni kuna nia ya kutaka kufanya ujanja Fulani kuhusu kura zao ikiwemo kuziiba.
  • Pia tunataka Jeshi la Polisi wasitumie nguvu yoyote kwa wananchi endapo itafika siku ya kupiga kura bila suala hili kupatiwa ufumbuzi. Hii ni kwa sababu kwa jinsi Sheria ilivyo, imeruhusiwa wananchi kubaki umbali wa mita 200 kutoka vituoni.
  • Pia tunawataka wapiga kura endapo wataona umuhimu wa kukaa umbali wa mita 200  kusubiri matokeo, basi wafanye hivyo kwa unyenyekevu mkubwa ili kulinda amani na pia kuepuka kuzuia wananchi wengine kutumia haki zao.
(iv) Suala la Wanafunzi wa Vyuo Vikuu na watumishi waliohamishwa vituo vya kazi

Ni kwa mara nyingine sasa katika uchaguzi mkuu wanafunzi wa vyuo vikuu wanakoseshwa haki yao ya kupiga kura  kwa sababu zisizoridhisha.
  
 Wanafunzi wengi walijiandikisha katika maeneo ambayo hawatakuwepo siku ya kupiga kura na hawataweza kupiga kura zote tatu kutokana na kwamba vyuo vitakuwa vimefungwa siku hadi tarehe ya upigaji kura. 
  
Aidha, baadhi ya watumishi wa umma waliohamishwa vituo vya kazi katika miezi na siku za karibuni nao wamejikuta katika hali ya ugumu waliyonayo wanafunzi na wanavyuo.

Wito Wetu kwa Tume za Uchaguzi
    • Asasi za kiraia zinasisitiza watanzania walio katika makundi hayo mawili wapewe  fursa ya kuwezeshwa kufanya taratibu za kisheria kuwawezesha kupiga kura ya Rais siku ya tarehe 25 Oktoba. Aidha, katika miaka ijayo, Tume zihakikishe kuwa technolojia ya habari inawezesha upigaji kuwa wa waliojiandikisha popote nchini bila matatizo yoyote kwa kuwa mfumo ni wa kielektroniki.
    • Asasi za Kiraia hazioni ulazima wa Tamko la Tanzania Commission for Universities (TCU) kwamba vyuo vikuu visifunguliwe mpaka baada ya uchaguzi  kwani amri hii inanyima wanafunzi wa vyuo hasa wale wachache walijiandikisha vyuoni  haki yao ya kikatiba ya kupiga kura na kinaweza kuwa ni kichocheo cha uvunjifu wa amani.  Suala hili linapaswa liangaliwe upya kwa miaka ijayo.
      (v) Kauli za Vitisho na Lugha Chafu
      Kwa muda huu mchache uliobaki, vyama vya siasa na wanasiasa  vinapaswa kuendesha kampeni za kistaarabu zinazoheshimu misingi ya sheria na siasa za ushindani ambazo zinatambua kuwa kuna kushinda na kushindwa.
        
      Kwa hivyo, kusiwepo na kampeni za vitisho, matusi na ubaguzi wa aina yoyote na badala yake kuwepo kampeni za kistaarabu zinazoheshimu na zinazozingatia maadili ambayo vyama vyote vya siasa vimesaini ili kuliepusha Taifa hili na Machafuko.

      Tunazitaka Tume zote mbili kuchukua hatua haraka iwezekanavyo kwa wale watakaotoa vitisho kwa wananchi ama kwa wagombea. Tumesikitishwa na kitendo cha Tume kuacha kuchukulia hatua baadhi ya wanasiasa wanaotumia lugha za vitisho kwa wananchi au vyama vinavyokiuka muda wa kumaliza kampeni za uchaguzi.

      Aidha, tunavitaka vyombo vya habari vya umma kuacha mara moja kutoa fursa kwa chama kimoja tu wakati tunafanya uchaguzi wa vyama vingi. 
        
      Taarifa za kila wiki za Baraza la Habari na  Taarifa ya Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu zinaonyesha   kuwa toka kampeni zianze vyombo vya Umma hasa TBC na Habari leo vimekuwa zikionesha wazi wazi kukipendelea zaidi chama Tawala katika habari zake na kuziacha ama kuzipa uzito mdogo taarifa za vyama vingine.

      Tunakemea na kuvitaka pia baadhi ya vyombo vya habari vya binafsi kuacha kutoa taarifa za kichochezi na za uongo kwa wiki moja hii kuelekea siku ya kupiga kura ili kulinda amani ya Taifa. 
        
      Kipekee, tunapenda kuvipongeza vyombo vya habari ambavyo vimefuatilia na kutoa taarifa za kampeni za uchaguzi wa Tanzania 2015 kwa uhuru na haki wakati wote wa mchakato huu. 
        
      Kwetu, tunaona kuwa vyombo hivyo vimechangia kudumisha amani na vinastahili tuzo maalum.
       
      Pia kwa umoja wetu tunatoa tahadhari kwa AZAKI  na viongozi wake kutokushiriki katika shughulizi za kampeni za vyma na wagombea ili waweze kutimiza wajibu wa uwaanngalizi bila kukiuka maadili ya AZAKI.

      Tunawasihi viongozi Wakuu wa Kitaifa  wastaafu  hasa Marais kutokuonyesha upande kipindi cha uchaguzi na nyakati zingine zote ili waweze kuwa wasuluishi endapo hali ya amani na usalama itapotea.
        
      Taifa linahitaji wasuluhishi wa ndani hivyo ni vyema viongozi wakuu wastaafu wakalizingatia hili ukizingatia Tanzania  tumekuwa tukisifika kwa kuwa wasuluishi wa majirani zetu.

      Mwisho
      Sisi ni Asasi za Kiraia (AZAKI) za nchini Tanzania zilizoundwa na kutambulika kisheria na  zinazofanya kazi katika masuala mbalimbali ya kisheria, kijamii, kiuchumi, kisiasa na kiutamaduni. 
        
      Kwa umoja wetu tunasimamia na kuhimiza utawala wa sheria na haki za binadamu na masuala yote ya kimaendeleo ili kuhakikisha maisha ya watanzania yanakuwa bora katika nyanja zote.
        
       Kwa sababu hiyo, tunajiona tukiwa na jukumu kubwa la kukemea na kuvitaka vyombo husika kufanyia kazi viashiria vyote vya uvunjifu wa amani ili kulinusuru Taifa letu. Kamwe hatuwezi kunyamazia uovu wala kunyamazishwa!

      Imetolewa kwa niaba ya AZAKI 300 nchini na  asasi miavuli zilizofanya mikutano mikuu ya mashirika wanachama kati ya tarehe 14 na 17 Oktoba 2015,

      Dar es Salaam
      Tarehe 17/10/2015 na:
      Ismail Suleiman
      Katibu Mkuu
      Baraza la Taifa la Asasi za Kiraia

      MKE Alininyanyasa Sana Nilipofukuzwa Kazi, MUNGU Ameniona, Sasa Yamegeuka

      $
      0
      0
      Siku moja nisiyopenda kuikumbuka nilitwa ofisini kwa bosi wangu na kukabidhiwa barua ya kufukuzwa kazi
      Hiyo ilikua ni baada ya uchunguzi wa miezi kdhaa wa kosa nililokua nimelifanya bahati mbaya. Miezi mitatu nyuma nilimuingizia pesa mteja kimakosa kwenye akaunti yake kiasi cha million mia tatu na hamsini ambazo alitakiwa kuwekewa Mteja mwingine halali kupata pesa hizo.

      Kama humu ndani Kuna banker ataelewa nachokisema, kwamba makosa kama haya benki ni kawaida sana. Ukigundua kosa kama hili unawahi una reverse hiyo entry una m-credit anaetakiwa shida ni kama uliemwekea kimakosa akawahi kuzichukua ndipo yanakukuta yaliyonikuta mimi.

      Baada ya kufukuzwa kazi mke wangu alibadilika kabisa
      Nilishuhudia yafuatayo:-

      (1) Alitamka mimi ni mjinga ndio maana nimefukuzwa kazi.

      (2) Chake kikawa chake tu.

      (3) Akawa anawaambia wazi watoto kuwa kitu fulani kimenunuliwa na yeye na sio mimi.

      (4) Muda wa kurudi home ukabadilika sasa anarudi usiku mwingi, nampa kipigo cha nguvu anazira na kukimbilia kwao, kwenye usuluhishi anawaambia wasuluhishi kwamba mimi namuonea wivu kwa kuwa ana kazi mimi sina.

      (5) Niliuza Gari zangu mbili ili nipate mtaji wa kufanya biashara hivyo nikawa sina Gari nilijua maadam wife ana Gari tutatumia wote maana hata yeye wakati hana Gari alikua akitumia magari yangu.

      Kinyume na matarajio hakutaka kabisa niguse Gari lake mimi nikawa mtu wa miguu.Majirani wakawa wanashangaa mfumo wetu wa maisha.

      (6) Life yetu ya bedroom ikawa imekufa no intimacy no love making nothing. Alianza kidogo kidogo leo mara aseme anaumwa, kesho kachoka, hadi mwezi unaisha. Nikaamua isiwe tabu nikaacha kuulizia tena, nae akawa amepotezea moja kwa moja.

      Hata wazazi wangu aliwa mistreat sana wakawa hawaji tena kwangu, mama yangu akawa ananitumia vitu kwa njia basi kutoka nyumbani kama mchele, maharage, unga na kadhalika ili na mm nionekane nachangia.Wakuu siku ya kufa nyani miti yote huteleza. Kila nilichojaribu kukifanya ili nijinasue kinakwama, nakuta mtaji wote unakata naanza moja.Ilikatika miaka minne nikiwa kwenye hali hii maana nilipata matatizo 2010. Mwaka Jana kuna Dada mmoja tulisoma wote primary school akaamua kunisaidia, huyu dada tulikutana Posta accidentally tukapeana contact
      mimi nilishamsahau ila yeye alinikumbuka.

      Baadae akaniunganisha na mumewe ambae ni HR manager kwenye shirika fulani, nikamwelezea ukweli wote na akaniingiza kaziniWife sikumwambia kuwa nimepata kazi akaanza kuona nakuja na mahitaji ndani, nikawa naondoka zangu alfajiri narudi usiku mwingi. Nikaita mafundi wakabomoa ukuta wote wa fensi uliokua umeoza waliiba sana cement wakati wa ujenzi ukajengwa upya, vitu vyote vilivyochoka ndani nikabadilisha. Wife alishangaa sana ila akashindwa kuniuliza maana hadi hapo tulikua hatuongeleshani zaidi ya salam za asubuhi na jioni tu basi.

      Wana jf siwezi kuwaficha sehemu niliyopata naingiza hela Mara kumi ya ile kazi yangu ya benki, hii sikutokana na mshahara bali njia mbali mbali katikati ya mwezi kitengo chetu tupo wanne,hali ikiwa nzuri huwa tunagawana hadi laki mbili kila siku, kama hali ni mbaya tunagawana laki moja kwa siku hii ni mbali na ile tunayogawana mwisho wa mwezi kama million 3 each person mshahara ni mdogo tu ni laki saba tu kwa mwezi.Maana mshikaji alisema anaweza kuniingiza kazini ila kama mfanyakazi wa kawaida kwa kuwa benki nilifukuzwa hakukua na reference wala background check so nikaamua kufuta kwenye CV kuwa nilifanya bank.

      Nimeanza mchakato wa talaka kupitia mwanasheria mmoja rafiki yangu, mwezi January mwaka huu amemwandikia barua ya kumtaarifu uamuzi huo na copy Ustawi wa jamii pia, baadae tutafungua shauri la talaka.Kinyume na matarajio yangu wife kwa kuwa alishañichoka na hakuna kinachoendelea kati yetu nilijua angekubali tu. Cha ajabu hivi sasa kupitia wazee wake wameniita kikao zaidi ya Mara 6 sasa ili tusuluhishe tofauti zetuKawa mpole sana, alidhan nitaendelea kuteseka milele

      Wakuu sasa sipo nyumbani kwa hasira ya mambo aliyonitendea hivi sasa sipo nyumbani nimepanga upande wa nyumba nimeanza ujenzi ili nihamie. Kila siku lazima nipite kwa watoto niwaone ndo niondoke. Nimesimama njia panda, mm binafsi nilishaamua simtaki tena huyu mwanamke ila wazee na viongozi wa dini tunakoabudu wanasema turudiane juzi mke wangu alinipigia magoti tukiwa kikaoni kwamba nimsamehe, nifute kusudio la kuomba talaka mahakamani. Wazazi wangu hawataki kusikia kabisa neno msamahakwa matendo aliyotufanyia.


      NB: Nimetaja kipato ili kuwapa mwanga na uelewa wa tatizo isichukuliwe vinginevyo

      Nimesikia amepata matatizo kazini ila sina uhakika na taarifa hizo

      Naomba ushauri wenu

      By Christo devries/Jamii Forums

      Wagombea Urais wa CCM na CHADEMA Waukacha Mdahalo wa Laivu Ulioandaliwa na Twaweza

      $
      0
      0

      Wagombea urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM) Dk John Magufuli, pamoja na Edward Lowassa wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), wameshindwa kushiriki mdahalo maalum wa wagombea urais ulioandaliwa na Taasisi ya Twaweza pamoja na wadau wengine.

      Mdahalo huo ambao umefanyika kwenye Ukumbi wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam leo, ulirushwa moja kwa moja na kituo cha televisheni cha Star TV. Anna Mghwira kutoka Chama cha ACT-Wazalendo na Chief Lutasola Yemba wa ADC na mgombea kutoka CHAUMMA, Hashim Rungwe ndiyo wagombea pekee wa urais waliopewa mualiko rasmi na kushiriki mdahalo huo.

      Hata hivyo, Rungwe alifika wakati mdahalo huo ukiwa unaelekea ukingoni ambapo awali ilitaarifiwa kuwa angefika kwa kuchelewa kwa kuwa wakati mdahalo umeanza yeye ndio alikuwa akiwasili Uwanja wa ndege wa Julius Nyerere akitokea Mtwara.

      Katika mdahalo huo, maswali mbalimbali yaliulizwa ikiwemo dhana nzima ya mabadiliko ambayo awali ilikuwa ikitumiwa na Chadema kisha kuenea kwenye vyama vingine, imepata tafsiri tofauti kutoka kwa wagombea urais wa ACT-Wazalendo Anna Mghwira na Chief Yemba wa ADC.

      Kwa mujibu wa Mghwira, dhana ya mabadiliko katika ACT-Wazalendo ni hoja mbadala inayolenga kushughulikia matatizo ya jamii. Alisema ACT-Wazalendo imebuni mikakati madhubuti wa kuongeza uzalishaji kupitia  rasilimali za nchi kama vile misitu, madini na uwekezaji kwenye kilimo.

      “Matumizi bora ya rasilimali na uwekezaji katika kilimo vitasaidia kuongeza pato la taifa na  hivyo itarahisisha utoaji wa huduma bora za jamii kama vile elimu na afya,” alisema Mghwira.

      Kwa upande wake, Chief Yemba alisema dhana ya mabadiliko kwa mujibu wa ADC ni kuondoa maradhi, ujinga na umasikini. Alisema mabadiliko siyo kuiondoa CCM madarakani na kisha kuiongoza nchi kwa misingi ileile ya CCM.

      Kuhusu Muungano, Chief Yemba alisema ADC itapitia kero zote ili Muungano uweze kutoa haki sawa kwa watu wote tofauti na ilivyo sasa. Alisema Muungano unapaswa kusimamia na kutekeleza hoja ya haki sawa kwa wote kama vile kutoa huduma za jamii kwa usawa kwa pande zote za Muungano.

      “Sisi ACT-Wazalendo tunasema Muungano ni lazima utokane na ridhaa ya wananchi kikatiba tofauti na ilivyo sasa. Hoja za wananchi kudai serikali ya Tanganyika au Zanzibar yenye mamlaka kamili, zinaonyesha wazi kwamba Muungano tulionao unahitaji marekebisho ili wananchi wenyewe waridhie,” alisema Mghwira.

      Mgombea urais kupitia Chama cha TLP, Maxmilian Lyimo, pamoja na kwamba hakuwa mmoja wa wazungumzaji kwenye mdahalo huo, alipata fursa ya kujibu baadhi ya hoja za wananchi kama vile afya bora. Alisema serikali yake haitafanya dawa kweye hospitali za umma kuwa bidhaa adimu kama ilivyo sasa.

      JOYCE KIRIA Kashindwa Kuvumilia...Awapa Mchambo wa Nguvu Watu Wanaomponda na Elimu yake

      $
      0
      0
      'Matusi yenu kwangu ni Elimu yangu ndogo ya darasa la saba! 
      Ivi ni watanzania wangapi wameishia la saba? Ivi ni watanzania wangapi hawajafika hata darasa la saba? Ivi ni Watanzania wangapi ni maskini walioshindwa kuwapa Elimu watoto wao?
      Haya kwa nyie wasomi uchwara! Ivi wasomi wa Taifa hili wameisaidiaje nchi yetu?
      Ivi ni wasomi wangapi wanadigrii na hawana kazi iwe ya kuajiriwa au kujiajiri?

      Ivi kusoma ni kutukana watu na kuwadhalilisha huku unatamba wewe ni msomi!!! Nini maana ya Elimu? Ivi ukisoma na kuwa rais unakuwa na Haki kuwatukana wanyonge? Hadi Rais anatukana???? Ngachokaaaaaaaaa

      Baba Lowassa anajua fika hata mnaojinadi mmesoma, lakini nyie ndo mambumbumbu! Yuko tayari kujenga upya Kizazi cha Taifa letu kwa kuwapa Elimu Bora sana!
      Ndo Maana tunaotukanwa hatujasoma tumeamua kufanya Mabadiliko bila woga ili kila Mtanzania apatiwe Elimu Bora itakayoweza kuleta Maendeleo katika Taifa letu! Elimu ya Kufanya Maendeleo, tuachane na Elimu ya kutukana watu bila sababu! 

      Tumebakiza siku 5 tuu tuingie Kanani kila mtu atasoma bure! Elimu Bora! Amen
      Tangazo tangazo! Kwa Mimburula na misukule Hii ni page yangu, naandika nikitakacho! Makelele yako peleka kwenye acc yako, vinginevyo ntakunyoosha kama kawa! Mimi ni binadamu wa kawaida kama wengine kipaji cha uvumilivu sina unikomeeeeeee mxiuuuuuuuuuuu
      Sitembelei nyota ya mtu yeyote! Ni mimi na Mungu wangu tuu!'Joyce Kiria
      Viewing all 104702 articles
      Browse latest View live




      Latest Images