Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104776 articles
Browse latest View live

Breaking News: Kada Mwingine wa muda mrefu wa CCM Ametangaza Kukihama Chama Hicho

$
0
0
Akiongea na waandishi wa habari jioni hii kada wa muda mrefu mpanga Sera na mikakati wa CCM na mshauri wa chama Dr Eve Hawa Sinare ametangaza kukihama chama hicho na kujiunga na Ukawa. Huyu ni mtu muhimu sana kwa CCM na msomi aliyekuwa anashauri mikakati ya ushindi kwa JK katika chaguzi zilizopita.

`TUHUMA za Mbowe Kuhamamisha Mabilion ya Hela Kutoka Kwenye Accont yake Kwenda Nchi za Nje....CHADEMA Wazungumzia Tuhuma Hizo

$
0
0
CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimekashangwazwa na tuhuma za uongo zilizotolewa na baadhi ya vyombo vya habari dhidi ya Mwenyekiti wa chama hicho Freeman Mbowe za kuhamisha fedha katika akaunti za nje.

Akizungumza na waandishi wa habari  jana, msemaji wa chama hicho, Tumaini Makene alieleza kuwa hakuna sheria inayomkataza mtu kutofanya biashara na kuhamisha fedha zake binafsi.

Akitaja vyombo hivyo alisema kuwa ni Magezeti ya Jambo Leo, Uhuru na Raia Tanzania ambayo alidai yana maslahi ya kisiasa kwani habari hiyo imeonekana kuhaririwa na mhariri mmoja kutokana na kutokuwa na uthibitisho wala ushahidi wa upande wa pili.

Mimi ni mwandishi mwenzenu, naifahamu taaluma hii, ukisoma habari hiyo utaona inafanana kwa kila mstari, nukta hadi koma, inaelekea iliandikwa na mwandishi mmoja na kusambazwa kimaslahi kwa magazeti yote matatu na wahariri wakapachika” alisema Makene.

Alisema kuwa mwenyekiti huyo ni mfanyabiahara wa kimataifa ambaye anafanya biashara zake halali nje na ndani ya nchi zinazojulikana na serikali.Alisema magazeti hayo yanaandika ili kuwaondoa wananchi kwenye ajenda kubwa ya Uchaguzi sababu chama cha Mapinduzi kimeelemewa.

Jana Magazeti matatu yaliandika kuwa Freeman Mbowe, anatuhumiwa kuhongwa ili kumpitisha Edward Lowassa, kuwa mgombea urais wa chama hicho, yakimtuhumu kufanya uhamisho wa mabilioni ya fedha kwenye akaunti yake hivi karibuni.

Kwa mujibu wa Uhuru, Jambo Leo na Raia Tanzania yaliandika kuwa zilikuwa ni njama za Mbowe, kufanya uamuzi wake wa kumpitisha Lowassa kuwania urais pasipo kushindanishwa na mtu ndani ya chama chake na ndani ya muda mfupi, uamuzi unaodaiwa kukigawa chama hicho,

Magazeti hayo kwa pamoja yaliandika kuwa Mbowe anahamisha hela hizo wakati wagombea kupitia chama chake hawana hela.

Hata hivyo Makene alifafanua kuwa hakuna sera ya Chadema kutumia pesa za mtu binafsi na biashara zake kwa ajili ya kusaidia wagombea, isipokuwa hela zinazopatikana kutokana na ruzuku hutumika kwa shughuli za chama na hesabu zake zinajulikana.

KIMENUKA..CHADEMA Wamshitaki Rais Kikwete UN, AU na Katika Mahakama ya Kimataifa ya uhalifu wa kivita (ICC)

$
0
0
CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo Chadema kimemshitaki Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Jakaya Mrisho Kikwete.

Akizungumza na waandishi wa habari  jana mchana ukumbi wa Kisenga uliopo Millenium Tower, wakili wa Chadema, John Mallya alisema Rais  Kikwete ameshitakiwa Umoja wa Mataifa, Umoja wa Afrika na Mahakama ya kihalifu Uholanzi kwa sababu anatumia madaraka yake vibaya kutisha wananchi kuelekea uchaguzi mkuu.

Mallya alisema kuwa Mashitaka hayo yameelekezwa Umoja wa Mataifa lakini pia nakala za tuhuma dhidi ya Rais Kikwete zimepelekwa pia Umoja wa Afrika (AU) na Mahakama ya Kimataifa ya uhalifu wa kivita iliyopo The Hegue Uholanzi.

Kwa mujibu wa wakili huyo wa Chadema, barua hiyo ya tuhuma dhidi ya Rais Kikwete imesainiwa na Makamu Mwenyekiti wa chama hicho Prof. Abdallah Safari.

Mashataka haya yanakuja ikiwa ni miezi miwili tangu Rais Kikwete ailaumu  Mahakama hiyo ya kihalifu kwa kusema kuwa viongozi wa Afrika hawafurahii kwa namna ambavyo mahakama hiyo inavyofanya kazi zake kwa kuwashughulikia zaidi viongozi wa mataifa ya Afrika.

Kauli hiyo ya Rais Kikwete aliitoa jijini Dar es Salaam wakati akifungua mkutano wa 16 wa Umoja wa Wanasheria wa Jumuiya ya Maendeleo ya Uchumi Kusini mwa Afrika-SADC,

Hiyo ilikuwa ni siku moja baada ya ICC kueleza kwamba inafuatilia mwenendo wa uchaguzi nchini Tanzania.

Mwendesha Mashtaka Mkuu wa ICC, Fatou Bensouda, alikaririwa na vyombo vya habari vya Aljazeera na Gambia Today akisema kuwa Mahakama hiyo inatazama kwa umakini mkubwa yanayotokea Tanzania kuelekea Uchaguzi Mkuu kama ilivyofanya katika nchi za Kenya, Ivory Coast na Congo na kwamba itachukua hatua za haraka kama kutakuwa na uvunjaji wa haki za binadamu.

Kauli hiyo ya Bensouda ilitanguliwa na ile iliyotolewa na mgombea urais wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), anayeungwa mkono na Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), Edward Lowassa.

Lowassa alilazimika kusema hayo katika ziara ya kutafuta wadhamini katika mikoa ya Arusha na Mwanza  kwa  kulitahadharisha Jeshi la Polisi juu ya uwepo wa Mahakama ya ICC kutokana na kitendo chake cha kutumia nguvu dhidi ya wapinzani kwa kuupiga mabomu msafara wake.
Mpekuzi blog

Kyela Kimenuka. Lowassa amfutilia mbali Mwakyembe Jimboni Mwake..Apokelewa Kama Mfalme

$
0
0
Kyela jana jioni. Laigwanan wa kimasai afuta jina Mwakyembe mjini Kyela. Mafuriko ni kama kawaida yake... Apokelwa Kifalme Jimboni Kwa Mwakyembe Huko Kyela Jijini Mbeya.....

Lowassa: I am Prepared To Lead Nation As 5th President

$
0
0
CHADEMA presidential candidate, Edward Lowassa has said he is well prepared and organised to lead the nation as the Union government's fifth president.

Lowassa  also promised Mbeya residents to provide free education from kindergarten to university levels with just 1.4trn/- in collected revenue.

He said the government has a lot of finances with several untapped revenue sources from natural resources.

Lowassa, who leads the rainbow coalition better known as Ukawa said last year's tax exemptions amounted to 1.6trn/- which could be enough to finance the country's education budget.

On employment the Chadema candidate who is supported by the Coalition of Peoples Constitution (Ukawa) said secondary school graduates will be deployed in the National Service whereby apart from patriotism the youths will be equipped with vocational skills.

He made the pledges when addressing the full-packed campaign rally held at Rwanda-Nzovwe grounds a few kilometers from Mbeya city centre.

Before the rally, Lowassa addressed similar rallies in Chunya and Mbarali districts.

He said the National Service capacity will be increased five times of the current size and capacity.  He said farmers will be enabled to practice modern agriculture as well as to sell their produce outside the country.

“I will form a common-man friendly government and establish a special bank for small scale entrepreneurs,” said Lowassa amid applause from the crowd.  He however pledged to improve health services and upgrade regional hospitals to referral hospitals.

Former prime minister Frederick Sumaye called upon residents to vote for the coalitions' candidate since the ruling party has failed to implement the promises it made to Tanzanians during the 2010 General Election.

He said the current government has failed to improve social services specifically education and health.

Sumaye, who was premier during the third phase period, noted that once voted into power, Lowassa will put a check on corruption and misuse of public funds as the two contribute to poor social services delivery. “Corruption is a critical problem ... Ukawa is determined and ready to control it for the betterment of Tanzanians,” Sumaye said.

Chadema National Chairman Freeman Mbowe said he has no trust with the National Electoral Commission (NEC).

He said Ukawa members will secure their votes by staying 200 meters from the polling stations.

According to Mbowe, the fifth government will be formed by Chadema because wananchi have already decided to opt for change.

He urged the police to implement their duties by adhering to work ethics and respect human rights before and after the elections.

“Elections mean your life ... we only has seven days to go, you should not make a mistake you must vote for Lowassa," Mbowe said.

Former CCM Chairman for Shinyanga Region, Khamis Mgeja urged the residents to weigh political parties by their election manifestos.

According to Mgeja, CCM promised better life to Tanzanians but todate millions of people live under extreme poverty.

He said Chadema will ensure better life for pastoralists, farmers, workers and other societal groups.

Former Home Affairs minister Lawrence Masha said they made a brave decision to cross to Chadema. He insisted on the electorate to observe the country’s laws during the elections.

Long time politician Kingunge Ngombale-Mwiru said the ruling party is about to split due to violation of its own constitution.

He said CCM can longer rule the nation calling on the residents to vote for Chadema.

“Chadema is very strong and determined to bring about change in the country... every citizen supports change,” said Ngombale-Mwiru, adding that he decided to leave the party even after serving it for 60 years.

Facts: Kwanini Magufuli Kamshinda Lowassa Ndani na Nje ya CCM

$
0
0
Mgombea wa CCM ametumia masaa mengi kufafanua ilani ya Chama Chake.

Mgombea wa CCM amewafikia mamilioni ya watanzania katika vijiji na wilaya zao na pia kwa kupitia media mbalimbali.

Mgombea wa CCM amesaidiwa vyema na Mgombea Mwenza katika kufika majimbo yote Tanzania na kuamsha matumaini ya kina mama na watoto...hajaenda bar kumwaga sera za kilevi!!

Mgombea wa CCM ameibeba ajenda ya taifa ya kupambana na ufisadi na pia amerejesha ajenda ya kitaifa kwamba nchi hii si ya kibepari bali ni ya wakulima na wafanyakazi.

Mgombea wa CCM ameongelea ahadi zake kwa kuangalia vision 2025 na sio ahadi za kutoa wafungwa magerezani.

Mgombea wa CCM ameligusia suala nyeti la Migogoro ya Ardhi iliyosababishwa na mabwanyenye yanayogombea urais kupitia UKAWA.

Mgombea wa CCM amewaombea kura vizuri Wabunge na Madiwani wa CCM na hivyo kuacha hazina ya watu watakaoelimisha wananchi juu ya kumchagua hata baada ya kumaliza kampeni za majimbo.

Mgombea wa CCM ameomba na kusisitiza kuomba kura kwa wananchi wote kutoka vyama vyote.

Mgombea wa CCM yuko na anaonekana kuwa mkakamavu kuweza kuwa Amir jeshi Mkuu.

Mgombea wa CCM ndiye Mgombea pekee aliyeiongelea amani ya mama Tanzania mara nyingi kuliko mgombea yoyote.

Mgombea wa CCM ndiye mgombea pekee aliyefanya kazi kama waziri na kazi yake kugusa kila wilaya Tanzania hii.

Mgombea wa CCM ndiye mgombea pekee aliyeeleza kwa ufasaha kwamba muelekeo wa kiuchumi wa Tanzania ni kutoka tulipo na kuingia kwenye uchumi wa viwanda.

Mgombea wa CCM ndiye mgombea pekee aliyeweza kufurahi na audiance yake ikiwa ni pamoja na kucheza,kupiga pushups na kupiga drums.

Ni mgombea pekee anayeamini katika kazi kuwa msingi wa kujinasua na umasikini.

Mgombea wa CCM ndiye mgombea pekee aliyekiri changamoto za serikali na chama chake na hivyo kuahidi kuzitatua...yuko honest.

Mgombea wa ccm ndiye mgombea pekee alionesha kuwa hatobabaishwa au kupelekwapelekwa na watakaomzunguka...alionesha ukali palipostahili kukemewa.

Mgombea wa CCM hajatumia fedha kuhonga washabiki.

Mgombea wa CCM ametumia muda wa miezi miwili tu kuiteka jamii kwa hoja na msisimko.

Mgombea wa CCM amevunja makundi yaliyoitafuna CCM kwa miongo kadhaa.

Ameweza kuzipasua ngome za Chadema kama Arusha mjini,Moshi na Hai.

Mgombea wa CCM anawaacha mbali sana wasindikizaji katika kinyanga'nyiro hiki.


#hapakazitu

Zikiwa zimebaki siku tano, Home Shopping Centre yasitishwa uwepo wake

$
0
0
Sasa ni wazi hali imeanza kuwa tete kwa wafanyabiashara washirika wa vigogo wa serikali na watoto wao... Kampuni ya Home Shopping Centre washaanza kufungasha virago na kukimbia kusikojulikana.

Ikumbukwe kampuni hiyo imekuwa ikihusishwa na moja wa mke wa kigogo hapa nchini, pamoja na mtoto wa kigogo hapa nchi.(Mama na Mtoto).... Home Shopping centre wamekuwa wakishutumiwa zaidi kwenye sakala la ukwepaji kodi, ambapo kwa siku inakadiriwa walikuwa wanakwepa zaidi ya billioni 12 kwa bidhaa wanazoingiza nchini...

Kwa wale wadau wa Kariakoo watakuwa wanakumbuka sakata la hawa majamaa vizuri sana....

Myatake: Serikali ya Ukawa isinyamazie hili jambo. Lazima wawajibishwe kwa ukwepaji kodi hata kama wakisepa....

Source:Jamii Forums

Man Caught In The Act Of Rubbing His Private Organ Against A Female Passenger In A Train!

$
0
0
A video of an unidentified man, rubbing his crotch against a female passenger in the middle of a busy train carriage, has recently emerged on Chinese media sites.

The video starts with the man leaning into an unsuspecting woman, in front of him on a moving train.

It appears, that the man had already been grinding his crotch, into the woman's back for some moments, when the camera started recording.

Initially, it seemed that the man was just another passenger, but it soon appears, that the man was slowly, but deliberately rubbing himself against the woman, who was wearing a short skirt.

At one point, the woman, turned around briefly to look at him, and then moved forwards, but the man soon closed the gap.

Eventually his victim moved away, and the man covered up his dignity, with a shoulder bag he was carrying.

It is not clear when the video was taken, or whether the woman has decided to press charges, for the sexual harassment.

Watch the video below...

Girls Want To Snatch My Man Because He Is Gorgeous: Linah Sanga

$
0
0
Linah Sanga had been in unsuccessful relationships in the past, however months ago he fell in love with Ugandan William Bugeme who is also Zari's brother. But it seems Linah is still in pressure as girls are chasing Bugeme's love tirelessly. In a candid chat with E-NEWS of EATV the Ole Themba star says she is challenged as ladies wants her man because he is gorgeous and Sexy.

"Great of all are challenges I face, So I care my man because he is good-looking and he is a man every woman wants to have, To me they are just challenges and I'm proud of him coz he is cool, I can't plan what God plans for him, everyone wants to reach far in a relationship" said Linah

Ujumbe wa Paul Kagame kwa Jakaya Kikwete, ni Mtihani Kwa CCM

$
0
0
UJUMBE MUHIMU WA KAGAME KWA JAKAYA KIKWETE KUELEKEA UCHAGUZI MKUU!!

"Kuhubiri kuhusu demokrasia ni jambo moja na kusimamia demokrasia ni jambo jingine!!Kama Nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki tunafuatilia yale yanayoendelea Tanzania wakati ikielekea katika Uchaguzi wao Mkuu; hivyo tuna hamu ya kuona rafiki yetu na Mwenyekiti wetu anayesimamia jumuiya yetu akithibitisha kwetu namna demokrasia inavyotakiwa kusimamiwa kwa vitendo nchini Tanzania ili ajitofautishe nami ama na Nkurunzinza"...Kagame, Paul....


Je unakubaliana na Paul Kagame kwa niaba ya Viongozi wenzake wa Afrika Mashariki? Unadhani Jakaya Kikwete anatakiwa kuwathibitishia namna gani demokrasia inavyotakiwa kutekelezwa hapa Tanzania?..Je kunaviashiri vyovyote vya demokrasia kuvunjwa na haki kuzimwa chini ya Usimamizi wa Jakaya Kikwete?..Usiogope TIRIRIKA!!

King Lawrence Finally Reveals Ivan Semwanga Still Loves Zari The Boss Lady And He Can't Move On.

$
0
0
Many agreed Ivan Semwanga didn't move on after separation with his baby mama of his three boys Zari The Boss Lady while Zari started new life by dating superstar Diamond Platnumz and recently they were blessed with baby girl. However, after lots of dramas on social media at last, King Lawrance, a close friend to Ivan admitted the Ugandan tycoon based in S.Africa still loves Zari.

Lawrence took to instagram to flaunt his new girlfriend and saying if Ivan had a hot girl like his it would be easy to forget Zari. "I think Ivan can find a beautiful girl like @therealmissrose(his girlfriend), then he can move on from @zarithebosslady"
 King Lawrence with his new lady love....


TCRA Yatoa Onyo Kwa Vyombo Vya Habari Kuhusu Kutangaza Matokeo

$
0
0
MAMLAKA ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imevionya vyombo vya habari vitakavyotangaza matokeo ya uchaguzi mkuu kinyume cha sheria na taratibu kwamba haitasita kuviadhibu.

Mbele ya wanahabari jana jijini Dar es Salaam, Mwenyekiti wa Kamati ya maudhui ya vyombo vya habari, Injinia Magreth Munyagi alionya kuwa utangazaji wa matokeo ya uchaguzi kabla ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) ambao umekuwa ukizungumzwa na baadhi ya wanasiasa lazima uzingatie taratibu zilizowekwa na tume tofauti na hapo hatua kali zitachukuliwa na TCRA.

Kumekuwa na mvutano baina ya Tume na vyama vya upinzani hususani vile vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA) kuhusu utangazaji wa matokeo ya uchaguzi mkuu mwaka huu huku Tume ikisisitiza kuwa ndiyo yenye mamlaka ya kutangaza matokeo na vyama hivyo vikisema hakuna sheria inayovizuia kutangaza matokeo ya vyama vyao.

Wiki tatu zilizopita, Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Bara), John Mnyika alisema “hakuna sheria inayotuzuia kutangaza matokeo ya kura zetu na ndio maana tunasisitiza tutayatangaza matokeo yetu wenyewe iwapo tutamaliza kujumlisha kabla ya masaa 72 ambayo NEC inasema itakuwa imemaliza.”

Akijibu swali la mwandishi iwapo vyombo vya habari kutangaza matokeo yatakayokuwa yametolewa na chama au vyama vya siasa ni kosa kisheria, Injinia Munyagi alisema “Tumeshaeleza kwamba utangazaji matokeo lazima uzingatie sheria na taratibu za NEC.”

Baadhi ya adhabu zilizotajwa kutumika kwa atakayethibitika amevunja sheria ni kuonywa, kupigwa faini, kufungiwa kwa muda na kunyang’anywa leseni ya utangazaji.

Pia Mamlaka kupitia kamati hiyo ya maudhui ya vyombo vya habari, ilieleza kuridhishwa kwa ‘wastani’ na utolewaji wa matangazo ya habari za kampeni.

“Mpaka sasa tumeridhishwa kwa wastani na kazi iliyofanywa na vyombo vya habari katika kampeni za uchaguzi mkuu, taarifa za uchochezi na kutia hofu zimepungua na waandishi wanajitahidi kutafuta vyanzo sahihi vya habari zao,” alieleza mwenyekiti injinia Munyagi.

Kamati ya Maudhui huteuliwa kisheria na waziri mwenye dhamana ya masuala ya habari jukumu kubwa la kamati hiyo likiwa ni kufanya tathimini za mara kwa mara kuhusu maudhui ya utangazaji na kupokea maoni au malalamiko juu ya maudhui ya vipindi hivyo.

Dr. John Pombe Magufuli Awasha Moto Mkoani Geita (Nkome)..Atembelea Kaburi la Babu na Bibi yake

$
0
0
Zikiwa zimebaki siku chache wa Tanzania wapige kura ya kumchagua Raisi wa awamu ya Tano. Jana Dr. John Pombe Magufuli alikuwa na mkutano mkoani Geita (Nkome).

Pia Dr. John Pombe Magufuli alitembelea kaburi la bibi yake na babu yake katika kijiji cha Katoma.

Kilichojiri Mahakamani Muda Huu Kesi ya Wapiga Kura Kukaa Mita 200

$
0
0
MAHAKAMA Kuu ya Tanzania, imehairisha kesi namba 37 ya mwaka huu, ya mlalamikaji kuiomba mahakama itoe tafsiri ya kifungu cha 104 kidogo cha (1) cha Sheria ya Uchaguzi kama kinazuia ama la wananchi kukaa umbali wa mita 200 baada ya kupiga kura katika vituo. Anaandika Josephat Isango … Jopo hilo la majaji linaongozwa na Jaji Sakieti Kihiyo pamoja na Lugano Mwandambo na Aloysius Mjujulizi limeahirisha kesi ya kikatiba iliyofunguliwa na mgombea ubunge Viti Maalum kupitia Chadema, Ammy Kibatala.

Kesi hiyo sasa itasikilizwa kesho saa 3 asubuhi baada ya upande wa serikali kudai kuwa walikuwa hawajamaliza kujibu hoja au kuweka pingamizi sababu walipokea notisi ya walalamikaji muda wa jioni hivyo hawakujiandaa.

“Mheshimiwa Jaji, tunaomba tupewe muda kwani tulipokea nyaraka hizi muda wa kazi ukiwa umekaribia kwisha hivyo hatukujiandaa, tunaomba tupewe muda kama ikiwezekana tulete majibu saa 8:30 Mchana leo kama mahakama itaona inapendeza,” alisema Wakili wa Serikali Obadia Kameya.
Kabla Majaji hawajatolea uamuzi ombi hilo walimshauri Wakili wa mlalamikaji, Peter Kibatala kubadilisha mashtaka na kumshtaki Mkurugenzi wa Uchaguzi kwani ndiye mtendaji mkuu wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi badala ya Mwenyekiti wa Tume hiyo.

Uamuzi huo ulifikiwa baada ya kuangalia katiba Ibara ya 74, kifungu kidogo cha 7, inayosomeka “Kwa madhumuni ya utekelezaji bora wa majukumu yake yaliyoainishwa katika ibara hii, Tume ya Uchaguzi itakuwa ni idara huru inayojitegemea, itafanya maamuzi yake rasmi kuhusu utekelezaji wa majukumu yake kwa vikao, na mtendaji wake mkuu atakuwa ni Mkurugenzi wa Uchaguzi ambaye atateuliwa na kufanya kazi kwa mujibu wa masharti ya sheria iliyotungwa na Bunge.”
Baada ya marekebisho hayo, kesi hiyo iliyovutia watu wengi iliahirishwa mpaka kesho saa 3
Mawakili upande wa mlalamikaji ni Peter Kibatala na Omary Msemwa, huku upande wa walalamikiwa ambayo ni Mwanasheria Mkuu na Tume ya Uchaguzi ni Obadia Kameya na Alecia Mbuya.
Katika kesi hiyo, mgombea huyo ambaye pia ni mpiga kura mwenye maslahi na uchaguzi mkuu ujao, ameomba mahakama kwa mujibu wa kifungu hicho sura ya 343 iliyofanyiwa marekebisho mwaka 2010 ifafanue kuhusu haki za wapiga kura.

Mlalamikaji anaitaka mahakama iseme na kutafsiri kifungu hicho kinamaanisha nini kuhusu haki hiyo kufuatia kauli iliyotolewa na NEC pamoja na Rais Jakaya Kikwete kwamba wananchi wakishapiga kura hawaruhusiwi kukaa eneo la vituo vya kupigia kura umbali wa mita 200.
Aidha, anaitaka mahakama itamke kama ni halali kwa Rais na Tume ya Uchaguzi (NEC) kuzuia wananchi kukaa kwa utulivu umbali huo ama la.
MWANAHALISI ONLINE

MTABIRI: Chama Kitakachoshindwa Ndiyo Utakuwa Mwisho Wake!

$
0
0
MTABIRI maarufu nchini, Maalim Hassan Yahya Hussein amesema chama cha siasa kati ya vyama viwili vikubwa nchini kitakachoshindwa katika uchaguzi mkuu mwaka huu ndiyo utakuwa mwisho wake.

Akizungumza na gazeti hili katika mahojiano maalum jana, Maalim Hassan alisema Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) vina wakati mgumu na vinashikwa kinyota kutokana na wagombea wake kutofautiana.

“Mwaka huu ulianza Alhamisi ambayo kinyota asili yake ni moto na wagombea wao, Edward Lowassa wa Chadema jina lake linaanzia L , nyota yake ni Mshale ambayo asili yake ni moto na (Dk. John) Magufuli wa Chama Cha Mapinduzi ambaye jina lake linaanza na M, nyota yake ni ya samaki ambayo asili yake ni maji, majina hayo yana maana sana kinyota.

“Kwa kawaida maji huzima moto lakini pia maji yakizidi, moto huzimika, hii maana yake ni kwamba chama ambacho mgombea wake ana nyota asili ya maji kikishinda, basi kile cha mgombea ambaye asili yake ni maji kitakufa na moto ukizidi unaweza kukausha maji, hivyo kiutabiri chama kitakachoshindwa kitakufa moja kwa moja au kufifia sana,” alitahadharisha.
Chadema mwenyekiti wake ni Freeman Mbowe wakati CCM mwenyekiti wake ni Rais Jakaya Kikwete.

Uchaguzi mkuu nchini unatarajiwa kufanyika Oktoba 25, mwaka huu na Tume ya Taifa ya Uchaguzi imetangaza kwamba matokeo ya urais yatatangazwa ndani ya saa 72.

Sababu za Rais Kutovunja Baraza la Mawaziri Mpaka Muda Huu Zawekwa Wazi

$
0
0
Mwanasheria Mkuu wa Serikali, George Masaju ametoa mwongozo wa kisheria kufuatia sintofahamu iliyoibuka kwa baadhi ya watanzania kuhusu sababu zilizosambaa kwenye mitandao ya kijamii kuhusu kutovunjwa kwa baraza la mawaziri hadi muda huu huku zikiwa zimebaki siku tano kufanya uchaguzi mkuu.
Masaju alieleza kuwa kisheria bado sio muda muafaka wa kuvunja baraza la mawaziri kwa kuwa waziri hupoteza sifa za kuwa waziri wa serikali ya Tanzania punde kabla ya rais mpya kupatikana.
“Mara tu kabla rais mteule hajashika madaraka hayo, ndipo waziri anapoteza nafasi yake ya kuwa waziri. Kwahiyo sasa hata uchaguzi hatujafanya,” alisema.

Aliongeza kuwa suala la siku chache zilizobaki bado liko kisheria kwa kuwa rais mpya bado hajapatikana.
“Japokuwa ni siku tano sasa zimebaki, lakini uchaguzi ukishafanyika na rais akapatikana, mara tu huyu rais mteule hajashika madaraka hayo ndipo waziri anapoteza sifa ya kuwa waziri,” aliongeza.


Majibu ya kisheria ya mwanasheria mkuu wa serikali yamekuja wakati ambapo taarifa zilizosambaa kwenye mitandao ya kijamii na vijiweni zikieleza kuwa huenda kutovunjwa kwa baraza la mawaziri kunacheleweshwa kwakuwa kuna hofu ya mawaziri wengi kukihama Chama Cha Mapinduzi.

Balozi Juma Mwapachu alikoleza tetesi hizo wakati alipokuwa akirudisha kadi ya Chama Cha Mapinduzi katika ofisi za chama hicho zilizoko Mikocheni, Dar es Salaam baada ya kueleza kuwa uamuzi wake unaungwa mkono na mawaziri wengi wa serikali ya awamu ya nne.

MAGUFULI: Mabadiliko Ya Kweli Hayawezi Kuletwa Kwa Kuzungusha Mikono

$
0
0
MGOMBEA urais wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk. John Magufuli, amesema mabadiliko ya kweli hayawezi kuletwa kwa kuzungusha mikono, bali yatakuja kwa kufanya kazi.

Kutokana na hali hiyo, amesema yeye ndiye anayeweza kuleta mabadiliko ya kweli yanayokwenda na vitendo katika kujenga uchumi wa nchi na watu wake.

Dk. Magufuli alitoa kauli hiyo jana kwa nyakati tofauti, alipokuwa akizungumza wakati wa  mikutano ya kampeni iliyofanyika katika majimbo ya Buchosa, Geita na Busanda.

Katika mazungumzo yake, Mgufuli aliwataka Watanzania wasidanganywe na baadhi ya wanasiasa wanaowataka wasiipigie kura CCM.

Alisema kwamba, pamoja na baadhi ya wanasiasa kukesha wakihamasisha mabadiliko kwa kutoichagua CCM, jambo hilo halitawezekana kwa kuwa ni sawa na ndoto za mchana.

“Ninasema hapa, eti kuna watu wanahangaika kuzungusha mikono na kusema wanaleta mabadiliko, ni lazima wajue mabadiliko hayawezi kuja kwa mtindo huo.

“China hivi sasa inatisha kwa kuwa na uchumi wa daraja la kwanza duniani na kuna hatari hata ya kutaka kuizidi Marekani.

“Kwa mfumo wao huo, hawakukiondoa madarakani chama tawala ila walifanya mabadiliko ya ndani ya chama na Serikali.

“Ndiyo maana Magufuli ninakuja na mabadiliko ya kwenda ndani ya Serikali na ndani ya CCM. Katika hili, sina mchezo ndugu zangu Watanzania, naomba mniamini,” alisema Dk. Magufuli.

Kwa kuwa Watanzania wameshaamua kumpa urais Oktoba 25, mwaka huu, jambo atakalo anza nalo ni kuunda mahakama ya mafisadi.

Alisema, amezaliwa katika familia maskini na hatakuwa tayari kuona wajasiriamali wadogo wakinyanyaswa na hata kutozwa ushuru ambao umekuwa ukiwakandamiza katika biashara zao.

Alisema anajua eneo la Nkome ni maarufu kwa kilimo cha mananasi daraja la kwanza, lakini bado wakulima wamekuwa wakikosa soko la uhakika.

Kutokana na hali hiyo, atatimiza mkakati wa Serikali yake kwa kujenga kiwanda cha juisi katika  eneo hilo.

“Ni aibu kwa nchi yetu inayozalisha matunda kwa wingi, kukosa kiwanda cha kusindika matunda.

“Napenda kuahidi hapa, nitajenga kiwanda cha juisi kitakachosaidia wakulima wa mananasi kuwa na soko la uhakika badala ya kwenda Geita mjini au Mwanza.

“Tukijenga kiwanda hapa, tutatoa ajira kwa vijana na tutatengeneza juisi yetu badala ya kila siku kuagiza kutoka nje ya nchi, hii ni aibu,” alisema.

Source:Mpekuzi blog

Mkuu wa Majeshi DAVIS MWAMUNYANGE Ajitokeza Hadharani Kwenye Uzinduzi wa Uwanja wa Ndege za Kivita Morogoro

$
0
0
Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Rais JAKAYA KIKWETE amezindua awamu ya pili ya ujenzi wa uwanja wa ndege za vita uliopo katika kamandi ya jeshi la anga iliyopo NGERENGERE mkoani MOROGORO.

Akizindua ujenzi huo,Rais KIKWETE amesema mazingira bora ya uwanja huo pamoja na kutumika kwa shughuli za kijeshi, yatawawezesha watu kufanya kazi kwa bidii na kuchochea uboreshwaji wa huduma mbalimbali za kijamii katika eneo hilo.

Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Dkt. HUSSEIN MWINYI amesema kukamilika kwa mradi huo itakuwa ni hazina kwa jeshi la wananchi na taifa zima huku akisisitiza suala la matumizi ya uwanja huo kuboreshwa.

Naye Mkuu wa Majeshi ya ulinzi na usalama Jenerali DAVIS MWAMUNYANGE ameeleza mikakati iliyopo ya kuboresha jeshi hilo, huku mkuu wa jeshi la anga Meja Jenerali JOSEPH KAPWANI akisema uwanja huo utakuwa bora katika nchi za Kusini mwa AFRIKA.

KIMENUKA: Madereva wa Malori Wafunga Barabara ya Morogoro Baada ya Mwenzao Kupigwa Risasi

$
0
0
Madereva wa magari makubwa aina ya Lori wafunga Barabara ya Morogoro baada ya mwenzao kupigwa risasi na Bosi wake-Yadaiwa dereva alikula njama kuiba mafuta kisha kutaka kulichoma gari.abari za asubuh hii zinasema Madereva wa Malori wameamua kuacha Magari yao njiani, ni baada ya mwenzao kukwatuliwa Risas Bandarini jana, Magari hayatembei kabisa toka Kibaha kuja Ubungo.Kamanda wa Polisi wa mkoa wa kipolisi Kinondoni, Camillius Wambura,ameithibitisha kupokea taarifa za mgomo huo na kwamba anafuatilia ili kujua kama taarifa hizo zina ukweli kiasi gani. Atatoa taarifa kamili baada ya muda

SIRI IMEFICHUKA: Helkopta iliyomuua Filikunjombe na Wenzake Ilikuwa ni Mbovu Isiyofaa Kutumika Wala Kufanyiwa Matengenezo

$
0
0
Gazeti la The Star la nchini Kenya limeripoti kuwa chopa hiyo yenye uwezo wa kubeba kilo 1,000 na kuruka futi 20,000 ilithibitishwa na Taasisi ya Usalama wa Ndege kuwa mbovu, isiyofaa kwa matumizi wala matengenezo.

Dar es Salaam. Chopa iliyopata ajali katika pori la akiba la mbuga za Selous na kuua watu wanne akiwamo aliyekuwa mbunge wa Ludewa, Deo Filikunjombe ni ya Makamu wa Rais wa zamani wa Kenya, Kalonzo Musyoka.

Msemaji wa Musyoka, Dennis Kavisu aliliambia gazeti la Daily Nation la Kenya kuwa chopa hiyo ni mali ya Musyoka aliyekuwa makamu wa rais wa zamani wa Kenya.
Gazeti la The Star la nchini Kenya limeripoti kuwa chopa hiyo yenye uwezo wa kubeba kilo 1,000 na kuruka futi 20,000 ilithibitishwa na Taasisi ya Usalama wa Ndege kuwa mbovu, isiyofaa kwa matumizi wala matengenezo

Chopa hiyo, yenye namba za usajili 5Y-DKK na namba za utengenezwaji 7027 Ecureuil ilikuwa ikitumiwa na Filikunjombe kwa kampeni zake za ubunge mwaka huu.
Wengine waliokufa katika ajali hiyo ni rubani, Kapteni William Silaa, Egid Nkwera na Plasdus Haule.
Kwa mujibu wa gazeti hilo, chopa hiyo ni miongoni mwa nyingi zinazokodishwa kutoka Kenya na marais na wabunge wa nchini kwa kampeni. Kadhalika taarifa kutoka Kenya zinaonyesha Musyoka alinunua chopa hiyo mwaka 2013 baada ya Uchaguzi Mkuu na amekuwa akiikodisha ndani na nje ya nchi.

Mkurugenzi wa usalama na sheria wa Mamlaka ya Anga nchini (TCAA), Redemptus Bugomola hakutaka kuzungumza lolote kuhusu chanzo cha ajali ya chopa hiyo na mmiliki wake. “Bado nawasiliana na wenzangu wanaofanya uchunguzi, wakimaliza tutatoa taarifa rasmi kwenu kuhusu mmiliki na chanzo cha ajali,” alisema.

Katika mahojiano na gazeti hili wiki iliyopita, Mchunguzi Mkuu wa ndege wa Wizara ya Uchukuzi, John Nyamwihura alisema chanzo cha ajali za chopa ni makosa ya kibinadamu yanayosababishwa na rubani, hali ya hewa na mazingira ya chombo chenyewe

Mtandao wa usalama wa ndege unaeleza chopa mpya kama hiyo inagharimu kiasi cha Sh 7.3bilioni. Kwa kawaida chopa huuzwa zikiwa vipande na huunganishwa baada ya kufika zilikonunuliwa.
Kenya ina jumla ya chopa 400 zinazomilikiwa na watu binafsi wakiwamo wafanyabiashara na wanasiasa
.
MWANANCHI
Viewing all 104776 articles
Browse latest View live




Latest Images