Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104712 articles
Browse latest View live

Kauli ya Kwanza Baada ya Zitto Kabwe Kuibuka Kidedea Ubunge Kupitia Chama cha ACT Wazalendo..Adai Hajui Ataingiaje Bungeni Bila Deo Filikunjombe

$
0
0


Zitto Ameandika Haya Kwenye Ukurasa Wake wa Faceook Baada ya Taarifa za ushindi wake:

Manispaa ya kwanza kuwa chini ya chama cha ACT Wazalendo - Kigoma Ujiji Municipal Council

Kwa Heshima ya ndugu yangu Deo Haule Filikunjombe. Kwangu mimi baada ya kifo cha ndugu yangu uchaguzi huu haukuwa na maana yeyote. Hata sijui nitaingiaje bungeni bila Deo. Asante watu wa Kigoma kwa kumpa heshima kubwa Deo wangu

This how VERA SIDIKA dressed for her Nigerian sponsors during a pool party, Oh MY!

$
0
0

Nairobi’s most popular socialite, Vera Sidika, is currently in Nigeria where she is headlining a pool party event organized in one of the most expensive clubs in Lagos.

The private pool party is organized by elderly Nigerian businessmen who have a lot of money to throw around and as usual, Vera is killing them with her flesh as she smiles all the way to the bank.

This is how she stepped out to the pool party.

Vibanda vya Mama Lishe na Mitumba Vyachomwa Moto Mkoani Njombe......Polisi Yawataka Wananchi Kuwa Watulivu Wakati Wakisubiri Matokeo

$
0
0
Moto ambao chanzo chake hakijajulikana hadi sasa umeteketeza baadhi ya mabanda ya mama lishe na mitumba karibu na kituo cha mabasi mkoani Njombe.

Hata hivyo, kikosi cha Zimamoto mkoani humo kimefanikiwa kuuzima moto huo usiku wa kuamkia leo ambapo polisi wamesema uchunguzi wa tukio hilo unaendelea.

Kwa mujibu kikosi hicho, mabanda mengine yamesalimika katika ajali hiyo.

Hata hivyo, kikosi hicho kimewataka wananchi kuwa watulivu wakati huu wakisubiri matokeo ya uchaguzi ambayo yanatarajiwa kutolewa muda wowote mkoani humo.

Kwa mujibu wa kituo cha luninga cha AzamTV, polisi mkoani humo wamesema uchaguzi mkoani humo ulifanyika kwa utulivu na hsata moto huo ulipotokea, wananchi wengi walikuwa majumbani mwao.

Kauli ya Kwanza Kabisa Kutoka Kwa Mwigulu Nchemba Baada ya Taarifa za Awali kuwa Ameshinda Ubunge Iramba

$
0
0
Asanteni wanairamba kwa kunituma tena,Nakwenda kufanya kazi ya Jimbo na Taifa langu.Asanteni kwa kura za kutosha kwa Rais mtarajiwa Magufuli,hakika awamu ya tano ni kazi tu.

“Some Africans Are Lazy Fools Only Good At Eating, Lovemaking and Stealing” – Donald Trump

$
0
0

Once again, US business magnate Donald Trump has expressed his deep disgust for Africans by referring to them as lazy fools only good at eating, lovemaking and thuggery. Speaking in Indianapolis, Trump who is also the republican Presidential torch bearer reiterated his promise to deport Africans especially those of Kenyan origin including their son Barrack Obama.

“African Americans are very lazy. The best they can do is gallivanting around ghettoes, lamenting how they are discriminated. These are the people America doesn’t need. They are the enemies of progress. Look at African countries like Kenya for instance, those people are stealing from their own government and go to invest the money in foreign countries. From the government to opposition, they only qualify to be used as a case study whenever bad examples are required. How do you trust even those who have ran away to hide here at the United States hiding behind education? I hear they abuse me in their blogs but I don’t care because even the internet they are using is ours and we can decide to switch it off from this side. These are people who import everything including matchsticks. In my opinion, most of these African countries ought to be recolonized again for another 100 years because they know nothing about leadership and self governance” Explained Donald Trump bitterly as he illuminated how he plans to reconstruct America and restore its lost glory.

“I promise to make America great again by restoring our dignity that we have since lost through Obama. The more reason why I still believe that he, and his Kenyan brothers and sisters should be deported back to Kenya to make America safe”

Sources have indicated that Trump’s thrush did not augur well with the Carson Camp and they have since distanced themselves from Trump words.

Zanzibar: Vijana Wawili Wapigwa Risasi Na Vikosi Vya Usalama

$
0
0
Kutoka Hospitali ya Mnazi Mmoja, taarifa ni kwamba wamepokelewa watu watatu waliojeruhiwa, wawili kati yao wakiwa wamepigwa risasi ambapo mmoja tayari anafanyiwa operesheni baada ya risasi kupitia ubavuni kuelekea ubavu mwengine.
 
Ripoti kutoka eneo la Jang'ombe zinaeleza kuwa vikosi vya usalama vilipita eneo hilo na kuwashambulia vijana waliokuwa wamejikusanya mitaani.
Chanzo : DW Swahili

CCM yakabiliwa na upinzani mkali kutoka kwa UKAWA

$
0
0
Watu wamejitokeza kwa wingi katika uchaguzi wa Tanzania unaotajwa kuwa na ushindani mkubwa huku muungano mpya wa upinzani ukijaribu kukiondoa madarakani chama tawala CCM kilichoshikilia madaraka kwa miaka 54.
Katika maeneo mengine ,upigaji kura uliongezewa mda ili kuwapatia fursa wale walio katika milolongo mirefu kupiga kura.
Kura ya maoni imekiweka chama tawala cha CCM kifua mbele lakini matokeo hayo yanatarajiwa kuwa ya ushindani mkubwa.
Vyama vinne vya upinzani vinamuunga mkono mgombea mmoja ,aliyekuwa waziri mkuu.
Kujitokeza kwa wingi kwa raia ili kushiriki katika uchaguzi huo kunamaanisha kwamba Watanzania wanaamini kwamba uamuzi wa maisha yao ya baadaye uko mikononi mwao.
Hi ni tofauti na uchaguzi mingine iliopita ambapo CCM ilitarajia ushindi kutokana na upinzani uliodhoofika na kugawanyika.
Lakini siasa zimebadilika nchini humo kufutia kubuniwa kwa muungano wa Ukawa ambao unaamini una fursa kubwa ya kuibuka mshindi.
Rais Jakaya Kikwete ambaye anaondoka madarakani ametaka kuwepo kwa amani wakati na hata baada ya uchaguzi,huku akionya kwamba mtu yeyote atakayejaribu kuathiri amani ataadhibiwa vilivyo.
Katika eneo la kimara ambapo wapiga kura waliyachoma makaratasi ya kupigia kura,maafisa wa uchaguzi wamerudi na sasa raia wanatarajiwa kupiga kura.

Matokeo ya Awali urais, Ubunge Yaanza Kutolewa

$
0
0
Wagombea urais wa vyama vya CCM na Chadema wanachuana vikali kwa mujibu wa matokeo ya awali yaliyotangazwa kwenye vituo mbalimbali nchini baada ya wananchi kupiga kura jana.

Matokeo hayo ya awali yanaonyesha kuwa Dk John Magufuli wa CCM na Edward Lowassa wa Chadema wanapishana kwa kura chache kwenye vituo ambavyo kura zimeshahesabiwa, huku kukiwa na tofauti kubwa kwenye kura za ubunge.

Katika Jimbo la Musoma Mjini, Beldina Nyakeke anaripoti kuwa matokeo ya urais kituo cha CGS Shule ya Msingi Musoma B, Dk John Magufuli, CCM amepata kura 169, Edward Lowassa wa Chadema (124), Anna Mgwira, ACT-Wazalendo (1), Chief Yemba, ADC (1), Janken Kasambala, NRA (0), Fahmi Dovutwa, UPDP (0), Macmillan Lyimo, TLP (0) na Hashim Rungwe, Chaumma (0).

Kura zilizopigwa 297 zilizoharibika 2

Kwa upande wa kura za ubunge katika kituo hicho Vedastus Mathayo wa CCM (173), Vincent Nyerere, Chadema (119), Eliud Esseko, ACT Wazalendo (1), Gabriel Ocharo, CUF (1), Chrisant Nyakitita (DP) 0, Maimuna Matola (ADC) 0, Ibrahimu Selemani, Tadea (0), Rutaga Sospeter, AFP (0) na Makongoro Jumanne, UMD (0). Kura zilizopigwa ni 297 na zilizoharibika 3.

Katika kituo cha Kitaji, Ofisi ya Kata Jimbo la Musoma Mjini matokeo ya ubunge, Vedastus Mathayo (CCM ), 167, Vincent Nyerere, Chadema (102), Eliud Esseko, ACT Wazalendo (1), Gabriel Ocharo, CUF (0), Chrisant Nyakitita, DP (0), Maimuna Matola, ADC (0), Ibrahimu Selemani, Tadea (0), Rutaga Sospeter, AFP (1) na Makongoro Jumanne, UMD (0).

Kwa upande wa matokeo ya urais, katika kituo cha Kitaji ofisi ya Kata, Dk Magufuli (167), Lowassa (104), Mgwira (1), ADC, NRA, UPDP, TLP na Chaumma hazijapata kura.

Katika kituo cha John Bosco, Dk Magufuli (143), Lowassa (82), Mgwira (3), Yemba (1) na Rungwe (1).

Kwa upande wa ubunge, Mathayo (145), Nyerere (79), Eliud Esseko (2), na Gabriel Ocharo (1).

Katika Jimbo la Monduli Peter Saramba anaripoti kuwa matokeo ya ubunge katika kituo cha NMC B, Namelok Sokoine wa CCM (58), Julius Kalanga wa Chadema (137), Navaya Ndaskoi, ACT-Wazalendo (1).

Katika kituo hicho matokeo ya urais Mghwira wa ACT-Wazalendo (2), Lowassa (Chadema) 150, Dk Magufuli (CCM) 39, Rungwe (Chaumma) 01.

Kwenye kituo cha NMC A matokeo ya ubunge ni Namelok Sokoine (CCM) 38, Julius Kalanga (Chadema) 169, Navaya Ndaskoi (ACT-Wazalendo) 01.

Kwa upande wa urais kituo cha NMC A, Mghwira (ACT-Wazalendo) 0, Lowassa 178, Dk Magufuli (CCM) 30, Lyimo 0.

Kutoka Dodoma Mjini, Sharon Sauwa anaripoti kuwa katika matokeo ya urais kituo cha Mwangaza-1, Mghwira (2), Dk Magufuli (156) na Lowassa (131).

Kwa upande wa ubunge kituo hicho, Christina Alex wa ACT Wazalendo (5), Antony Mavunde, CCM (144) na Kigaila Singo, Chadema (135).

Salma Said anaripoti kutoka Pemba kuwa katika Kituo cha Skuli ya Bwagamoyo, Jimbo la Mtambwe wilayani Wete, Pemba katika Kituo Namba 1, Maalim Seif Sharrif Hamad amepata kura 317 na Dk Mohamed Shein 5, wakati kituo Namba 2- Maalim Seif (220), Dk Shein (2).

Katika kituo cha Gombani Station (1),(2) na (3) jimbo la Wawi, Mkoa wa Kusini Pemba, Kelvin Matandiko anaripoti kuwa kituo cha Station 1, Dk Shein (18), Maalim Seif (258), Hamad Rashid (4). Jumla ya kura 282 na zilizoharibika 2.

Katika kituo cha Station 2, Dk Shein (21), Maalim Seif (246), TLP (1), ADC (1), ACT (1), Tadea (1) na SAU(1). Jumla ya kura ni 275 na zilizoharibika ni 3. Matokeo hayo yalitolewa na msimamizi mkuu wa kituo cha Gombani Stadium, Abubakar Shaame Faki.

Katika Jimbo la Shinyanga Mjini, Suzy Butondo anaripoti kuwa mtokeo ya awali ya urais katika kituo cha Uwanja wa Soko Mageuzi kuwa Dk Magufuli (134), Lowassa (104), Mghwira (1) na wagombea wengine hawakupata kura.

Kwa upande wa ubunge katika kituo hicho, Steven Masele wa CCM (112), Patrobas Katambi, Chadema (127), Nyangaki Shilungushela wa ACT Wazalendo (1).

Katika jimbo la Moshi Mjini kituo cha Shule ya Msingi Mawenzi- 1, Mngwira (1), Dk Magufuli (89), Lowassa (131) na Lyimo (1).

Kwa upande wa ubunge katika kituo hicho Jafary Michael, Chadema (150), Davis Mosha, CCM (83) na Marchel Kitali, (UDP (1).

Katika kituo cha Shule ya Msingi Mawenzi-2, Lowassa (143), Dk Magufuli (94) na Rungwe (1).

Kwa upande wa ubunge katika kituo hicho, Buni Ramolewa ACT Wazalendo (1), Mosha, CCM (78), Michael, Chadema (139).

Katika jimbo la Nyamagana, Midraji Ibrahim anaripoti kuwa matokeo ya ubunge kituo cha Calfonia Majengo Mapya B, Chaha Okong’ wa ACT Wazalendo (1), Mabula Stanslaus, CCM (152), Wenje Ezekia, Chadema (99), Faida Hassan, CUF (1), Mohamed Juma, Jahazi Asilia (0), Ahmed Mohamed, NRA (2) na Ramadha Uhadi wa UDP hakupata kitu.

Kwa upande wa urais Mgwira (0), Dk Magufuli (170), Lowassa (85) na waliosalia wamepata 0.

Hawa Mathias anaripoti kutoka Mbeya Mjini kuwa katika kituo cha Mwasyoge kura za urais Dk Magufuli (85), Lowassa (128).

Kwa upande wa ubunge Joseph Mbilinyi wa Chadema (147) na Shambwee Shitambala wa CCM (63).

Katika kituo cha Kajigili, kura za urais Dk Magufuli (105) na Lowassa (96).

Kwa upande wa ubunge Joseph Mbilinyi (105), na Shambwee Shitambala (95).

Katika kituo cha Mifugo B, Lowassa (104) Magufuli (139), na Mghwira (7).

Kutoka Pemba, Salma Said anaripoti kuwa matokeo ya awali katika Kituo cha Skuli ya Bwagamoyo Wilaya ya Wete, Pemba , Kituo namba moja, Jimbo la Mtambwe, Maalim Seif amepata 317 na Dk Mohamed Shein (5).

Kituo Namba 2, Maalim Seif (220) na Dk Shein (2).



Ester Matiko (Chadema) Atangazwa Rasmi kuwa Mshindi wa Kiti cha Ubunge Tarime Mjini

$
0
0
Msimamizi wa uchaguzi jimbo la Tarime Mjini, Mwanjombe limemtajngaza rasmi Ester Matiko (Chadema) kuwa mshindi katika kinyang’anyiro cha ubunge wa jimbo hilo.

Matiko amekuwa mbunge wa kwanza kutangazwa rasmi huku akiweka histori kubwa katika wilaya ya Tarime mjini kuwa mwanamke wa kwanza kuwa mbunge katika wilaya hiyo inayosadikika kuwa na historia ya mfumo dume hususan katika ngazi ya familia.

Bi. Matiku  amepata kura 20,017 na kumshinda mpinzani wake wa karibu Kembaki Michael Mwita wa CCM aliyepata kura 14,025

Meet The Handsome Young Man Who Has Been Eating HUDDAH MONROE …. He Is Rich Too

$
0
0

Huddah Monroe has finally revealed the identity of the man whose cars she has been flossing with on social media.

The mysterious guy uses the handle @Romeoluuv and he is a sight to behold for ladies.

See him;



Tume Ya Taifa Ya Uchaguzi Yaanza Kutangaza Matokeo ya Urais......Majimbo Matatu yametangazwa na Yote Yamechukuliwa na CCM

$
0
0
Tume  ya  Taifa  ya  Uchaguzi  imeanza  zoezi  la  kutangaza  Matokeo  ya  Urais  ambapo  mpaka  sasa  majimbo  matatu  yametangazwa.  Majimbo  Yaliyotangazwa  ni  Jimbo  la  Makunduchi,Pache  na  Lulindi

Katika  majimbo  yote  matatu  yaliyotangazwa, Dr Magufuli  ameongoza  kwa  mbali  dhidi  ya  mpinzani  wale  Edward  Lowassa.



Swizz Beatz ampongeza Diamond kwa kumuita ‘King’ baada ya kushinda tuzo za MTV EMA, soma pongezi za mastaa wengine hapa

$
0
0
Diamond ameutafuna mfupa uliowashinda wengi.
Hakuna msanii yeyote kutoka Afrika Mashariki, Magharibi na Kusini aliyewahi kushinda kipengele cha Worldwide Act, Africa/India kwenye tuzo za MTV EMA. Ushindi huo mkubwa unaomfanya sasa awe msanii namba moja Afrika.

“Hii sio tunzo yangu ni tunzo ya wewe na mimi maana bila kura yako nisingeweza kabisa kushinda,” anasema Diamond. “Naomba niwashukuru sana sana kwa kura zenu Mashabiki zangu pendwa, wasanii wenzangu, media, uongozi pamoja na familia.”

Bahati mbaya kutokana na harakati za uchaguzi hatutaweza kuwa na mapokezi ila ukipita tutaandaa siku maalum kwa wote tuweze piga picha nayo,” ameandika kwenye Instagram.

Kutokana na ushindi huo, mastaa wengi wameendelea kumpa pongeza muimbaji huyo akiwemo mtayarishaji maarufu wa Marekani, Swizz Beatz aliyempongeza kwenye comment kwa kumuita king.


Hizi ni pongezi za wasanii wengine:

Mr Blue

Hongera mwanangu nasseeb mungu akubariki sana..na endeleza hasira hizo hizo…haina kuremba @diamondplatnumz

Navio

Hailing from East Africa…MTV Europe’s Best Worldwide Act- @diamondplatnumz. CONGRATS BRO! Apart from one other artist, I’ve never had more support from an EA artist than him. And hes not even Ugandan! While other big artists in the industry bicker, surplant and pull down their brothers, he always shows us as EA artists support and realness. He deserves it! Look at what supporting each other and Unity can do!

Banana Zorro

Congratulation Brother….u did it…u made it…..hatua kubwa saaana…stay blessed…@diamondplatnumz …and the team

Willy Paul Msafi

Ladies and gentlemen, @teamdiamondplatnumz has made Africa proud… congrats for winning #mtvema best world wide act/India… anything is possible…@diamondplatnumz

Vanessa Mdee

Diamond man, God got you kid. Nothing is impossible #NeverEver give up #WorldwideAct #Africa #MTVEMA WINNER!!!! ASANTE TANZANIA

Salama Jabir

Salama Zalhata Jabir ‏@EceJay 4h4 hours ago View translation
Hongera Pia Kwa Bwana Nasibu Abdul, Naona Mdosi Kanyooka! 😂😂 Kwetu Pazuri Bwana
@diamondplatnumz @Sallam_SK

Chairman HKN (Kaka yake Davido)

Congrats @diamondplatnumz on Winning Best world Act Africa/India #MTVEMA pretty sure he’s the first African Artist to do so big ups!

Uchumba wa Jack Wolper Wavunjika

$
0
0
ULE uchumba wa mwigizaji Jacqueiline Wolper na Mkongo ambao ulipamba vyombo vya habari kwa miezi kadhaa iliyopita, hatimaye umevunjika rasmi huku daktari wa Kitengo cha Sayansi na Tiba Asili kilichopo Mbezi-Afrikana, Dk. Fadhili Emily akitajwa, Ijumaa Wikienda linakupa mchapo kamili.

Wolper alivalishwa pete ya uchumba kwa mbwembwe katika hoteli moja moja maarufu jijini Dar ambapo mwanaume huyo raia wa Jamhuri ya Demokrasia ya Kongo aliahidi kumuoa hivi karibuni huku akijiweka karibu na ndugu wa Wolper.

Kwa mujibu wa mtu wa karibu na Wolper, kabla Dk. Fadhili hajatia ‘saundi’, tayari Wolper alikuwa ameshapishana na Mkongo huyo hivyo Dk Fadhili alipata kazi rahisi kuvunja uchumba huo maana amekuta unasuasua.

“Wolper alikuwa ameshatofautiana na jamaa, lakini jamaa alikuwa hakubaliani na matokeo akawa anaendeleza uchumba kwa tabutabu sasa alipotokea Dk. Fadhili na kuingiza nyavu, fasta tu Wolper akawa amevunja uchumba wa awali na kuunga uchumba mpya,” alisema mtu huyo wa karibu na Wolper.

Mara baada ya ubuyu huo kutua kwenye dawati la Ijumaa Wikienda, mwanahabari wetu alimtafuta Wolper ili aweze kuzungumzia taarifa hizo ambapo alipopatikana alikiri uchumba wake na kutofafanua vizuri kama uchumba huo umevunjwa na Dk. Fadhili.

“Ndiyo uchumba umevunjika kwani tatizo liko wapi? Kuhusu suala la nani ameuvunjia mbona sioni umuhimu wake, iwe ni huyo dokta (Dk. Fadhili) au mwingine yeyote sawa tu kwani haya si ni maisha yangu binafsi,” alisema Wolper.

ULE uchumba wa mwigizaji Jacqueiline Wolper na Mkongo ambao ulipamba vyombo vya habari kwa miezi kadhaa iliyopita, hatimaye umevunjika rasmi huku daktari wa Kitengo cha Sayansi na Tiba Asili kilichopo Mbezi-Afrikana, Dk. Fadhili Emily akitajwa, Ijumaa Wikienda linakupa mchapo kamili.

Wolper alivalishwa pete ya uchumba kwa mbwembwe katika hoteli moja moja maarufu jijini Dar ambapo mwanaume huyo raia wa Jamhuri ya Demokrasia ya Kongo aliahidi kumuoa hivi karibuni huku akijiweka karibu na ndugu wa Wolper.

Kwa mujibu wa mtu wa karibu na Wolper, kabla Dk. Fadhili hajatia ‘saundi’, tayari Wolper alikuwa ameshapishana na Mkongo huyo hivyo Dk Fadhili alipata kazi rahisi kuvunja uchumba huo maana amekuta unasuasua.

“Wolper alikuwa ameshatofautiana na jamaa, lakini jamaa alikuwa hakubaliani na matokeo akawa anaendeleza uchumba kwa tabutabu sasa alipotokea Dk. Fadhili na kuingiza nyavu, fasta tu Wolper akawa amevunja uchumba wa awali na kuunga uchumba mpya,” alisema mtu huyo wa karibu na Wolper.

Mara baada ya ubuyu huo kutua kwenye dawati la Ijumaa Wikienda, mwanahabari wetu alimtafuta Wolper ili aweze kuzungumzia taarifa hizo ambapo alipopatikana alikiri uchumba wake na kutofafanua vizuri kama uchumba huo umevunjwa na Dk. Fadhili.

“Ndiyo uchumba umevunjika kwani tatizo liko wapi? Kuhusu suala la nani ameuvunjia mbona sioni umuhimu wake, iwe ni huyo dokta (Dk. Fadhili) au mwingine yeyote sawa tu kwani haya si ni maisha yangu binafsi,” alisema Wolper.

Chanzo:GPL

Mabomu ya Machozi Yarindima Zanzibar Kuwatawanya Wafuasi wa CUF Walioingia Barabarani Kushangilia Ushindi wa Maalim Seif Sharif Hamad

$
0
0
Hali  ya  Usalama  Zanzibar  sio  nzuri, Polisi amelazimka  kutumia  mabomu  ya  machozi  kuwatawanya wafuasi  wa  CUF  walioingia  barabarani  kushangilia  ushindi  wa  Maalim Seif Sharif Hamad  ambaye  amejitangazia  ushindi  hata  kabla  ya ZEC  kumaliza kutangaza  matokeo.

Mabomu  ya  machozi  yamepigwa  kwa  wingi  katika  mji  wa  Chakechake  baada  ya  wananchi  kukaidi  amri  halali ya  Polisi  ya  kuwataka  watawanyike


Maneno ya LOWASSA Alipoongea na Waandishi Habari Kuhusu Usomaji wa Matokeo Kumpendelea Magufuli na Vijana wa Chadema Waliokamatwa

$
0
0
Nimewaita kueleza masikitiko yetu mawili haswa katika upande wa jeshi la Polisi. Tuna vijana wetu wanaofanya kazi za IT kwa kujitolea maeneo ya kinondoni na kijitonyama jumla ya vituo vitatu.

Hawa vijana wanafanya uzalendo,kushiriki katika uchaguzi wa nchi yao,na kujenga historia moya ya nchi yao,tendo la kuwakamata si la haki kabisa

Wamewavamia na kuwakamata kwa kosa la human trafficking ambalo ni kosa kubwa na halifanani na kazi wanazofanya. 
  
Nimeona taarifa zao za matokeo ya kura wameanza kuonyesha watu taratibu zinazompendelea Magufuli.

Ningependa kuwashauri tume watoe matokeo yote kwa pamoja, Sio kufanya kama hivi wanavyotoa kidogo kidogo yanayoongelea upande wa pili kushinda,wanafanya maandalizi ya kisaikolojia (psychological preparedness) kudhoofisha morali ya wafuasi wa UKAWA ambayo si haki

Swali;
Give us your view So far on the tallying

Jibu;
So far so good. Ila napenda kutoa pongezi kwa wananchi waliojitokeza kwa wingi kupia kura,Wamekua watulivu na kuheshimu sheria na kanuni.

Swali;
You said the main tallying station has been raided, Do you have an alternative?

Jibu;
We have no alternative, we have been handicapped
They have been so unfair .I wish i could charge them in ICC

Swali;
Chadema ina mpango gani kuwatoa hao waliokamatwa?

Jibu;
Jumla yao walikua 191 wanajumlisha kura, Sisi hatuna hatua stahiki zaidi ya kuongea na nyie waandishi wa habari mpeleke taarifa hizi duniani, kwamba huu ni uonevu mkubwa.



EDWARD Lowassa Confident But Doubtful About Result Delays

$
0
0
By Henry Mwangonde
Dar es Salaam. The opposition Presidential candidate Mr Edward Lowassa has requested that the  National Electoral Commission (NEC)  be diligent in releasing election results especially in parts of the country where he believes his party has won.

Lowassa added that  he fears that delay in releasing results in some parts of the country saying the move could be aimed at favoring CCM candidate Dr John Pombe Magufuli.

 “I have seen the results released by NEC so far and I thought there could be some changes but they are still favouring CCM candidate contrary to the reality on the ground,” he said.

Commenting on the election process Mr Lowassa said:  “So far good, but there is a problem with the way NEC is handling the results because they're a long  time to announce the results while the voting process has ended."

The former prime minister told journalists today at a press conference held at the opposition coalition’s headquarters that he is confident he will win the General election and commended Tanzanians for turning out in large numbers to vote.



MATOKEO YA AWALI: Dk Magufuli Anaongoza Majimbo Tisa, Lowassa Manne

$
0
0
By Emmanuel Mtengwa, Mwananchi Digital
Dar es salaam.Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) jioni hii imeendelea kutoa matokeo ya awali ya urais katika majimbo 13 ambapo mgombea wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk John Magufuli anaongoza kwa majimbo tisa wakati Mgombea wa Chadema, Edward Lowassa anaongoza majimbo manne.

Matokeo hayo yametangazwa na Mwenyekiti wa Tume hiyo, Jaji Mstaafu Damian Lubuva kwa awamu mbili, ambapo asubuhi  mwenyekiti huyo alitangaza majimbo matatu ambayo ni  Paje, Makunduchi na Lulindi ambayo yote Dk Magufuli ameongoza.

Majira ya alasiri , Jaji Lubuva alitangaza majimbo mengine 10 ambapo kati ya hayo majimbo sita yalionyesha Dk.Magufuli anaongoza huku majimbo manne yakionyesha Lowassa anaongoza.

Majimbo hayo ni pamoja na Jimbo la Ndanda (Dk Magufuli), Nsimbo (Dk Magufuli), Kiwani (Lowassa), Chambani (Lowassa), Mtambile (Lowassa), Mkoani (Lowassa), Kibaha Mjini (Dk Magufuli), Bumbuli (DK Magufuli), Donge (DK Magufuli) na Jimbo la Kiwengwa (Dk Magufuli)

Jaji Lubuva amesema kuwa matokeo ya majimbo mengine ambayo yatakuwa tayari yatatolewa leo saa mbili usiku.

UPDATES za Matokeo ya Urais..John Magufuli Aendelea Kumgaragaza Edward Lowassa..Sasa CCM Inaongeza Majimbo 17

$
0
0
Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) Usiku huu imeendelea kutoa matokeo ya awali ya urais katika majimbo 27 ambapo mgombea wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk John Magufuli anaongoza kwa majimbo 17 wakati Mgombea wa Chadema, Edward Lowassa anaongoza majimbo 10.

Matokeo hayo yametangazwa na Mwenyekiti wa Tume hiyo, Jaji Mstaafu Damian Lubuva kwa awamu tatu, ambapo asubuhi  mwenyekiti huyo alitangaza majimbo matatu ambayo ni  Paje, Makunduchi na Lulindi ambayo yote Dk Magufuli ameongoza.

Majira ya alasiri , Jaji Lubuva alitangaza majimbo mengine 10 ambapo kati ya hayo majimbo sita yalionyesha Dk.Magufuli anaongoza huku majimbo manne yakionyesha Lowassa anaongoza.

Usiku  huu  majira  ya  saa  mbili , Jaji Lubuva ametangaza majimbo mengine 14 ambapo kati ya hayo majimbo 8 yalionyesha Dk.Magufuli anaongoza huku majimbo 6 yakionyesha Lowassa anaongoza.

Majimbo hayo ni kama  ifuatavyo:
Matokeo ya Urais Singida Mjini
Kura: 56,558
Magufuli (CCM): 36,035
Edward Lowassa (Chadema): 19,007

Matokeo ya Urais Jimbo la Lindi Mjini
Kura: 38,992
Magufuli (CCM): 21,088
Edward Lowassa(Chadema): 17,607

Matokeo ya Urais Jimbo la Njombe Mjini
Kura: 55,772
Magufuli (CCM): 33,626
Edward Lowassa(Chadema):20,368

Matokeo ya Urais Jimbo la Peramiho
Kura:45,374
Magufuli (CCM): 32,505
Edward Lowassa (Chadema): 11,291

Matokeo ya Urais Jimbo la Mkinga
Kura: 39,788
Magufuli (CCM): 23,798
Edward Lowassa (Chadema): 15,142

Matokeo ya Urais Jimbo la Moshi Mjini
Kura:79,814
Magufuli (CCM): 28,909
Edward Lowassa (Chadema): 49,379

Matokeo ya Urais Jimbo la Nanyamba
Kura: 44,437
Magufuli (CCM): 24,904
Edward Lowassa (Chadema): 16,992

Matokeo ya Urais Jimbo la Mbinga Mjini
Kura: 42,717
Magufuli (CCM): 29,295
Edward Lowassa (Chadema):11,695

Matokeo ya Urais Jimbo la Kisarawe
Kura: 38,012
Magufuli (CCM): 24,086
Edward Lowassa (Chadema): 13,093

Matokeo ya Urais Jimbo la Mgogoni
Kura: 7,539
Magufuli(CCM):710
Edward Lowassa (Chadema): 6,506

Matokeo ya Urais Jimbo la Mtambwe
Kura: 7,620
Magufuli (CCM): 428
Edward Lowassa (Chadema): 6,937

URAIS Jimbo la Kojani
CCM - kura 1561
CHADEMA - kura 9982

URAIS Jimbo la Wete
CCM - kura 958
CHADEMA - kura 5119

URAIS Jimbo la Gando
CCM - kura 881
CHADEMA - kura 5903
10. URAIS Jimbo la Lindi Mjini
Jaji Lubuva amesema kuwa matokeo ya majimbo mengine ambayo yatakuwa tayari yatatolewa kesho  saa  tatu  asubuhi.

Matokeo Rasmi Ya Ubunge Jimboni Kwa TUNDU LISSU Haya Hapa

$
0
0
Jimbo la Singida Mashariki: Tundu Lissu wa Chadema, ameshinda kwa jumla ya kura 25010, dhidi ya mpinzani wake wa karibu Jonathan Njau wa CCM, aliyepata kura 18614.‪

KAULI ya Mgombea Julias Mtatiro Baada ya Kushindwa Ubunge Segerea Yawagusa Wengi..Adai Kilichotokea Kiwe Funzo Kwa UKAWA

$
0
0

HATUWEZI KUSHINDA UBUNGE SEGEREA...
Ndugu zangu, kwa moyo mkunjufu kabisa napenda kuwajulisha kuwa hatuwezi tena kushinda ubunge wa jimbo hili kwenye uchaguzi uliofanyika jana.
Matokeo ya majumuisho ya kila kata yanaonesha kuwa mgombea wa Chadema, Bi. Anatropia Theonest ana wastani wa kura 2000 - 2500 kwa kila kata.
Mimi nina wastani wa kura 4000 - 5000 kwa kata na mgombea wa CCM ana wastani wa kura 5000 hadi 6000 kwa kata.
Hii ina maana kuwa kura za UKAWA kama zingelipigwa kwa mgombea halisi wa UKAWA tungeishinda CCM kwa zaidi ya kura 20,000 lakini kwa sababu zimepigwa kwenda vyama viwili tunaweza kushindwa kwa wastani wa kura 5000 hadi 10,000.
Haya yaliyotokea hapa Segerea ni funzo kubwa kwa vyama vyetu na wanasiasa wetu kuheshimu na kusimamia makubaliano, kuwa na roho ya kufikiria mustakabali wa taasisi na watu wetu kuliko MASLAHI BINAFSI. Kwa hatua ya sasa sitaeleza hujuma za ndani kwa ndani tulizofanyiana ndani ya UKAWA hadi kufika hapa.
Nachoweza kusema ni Asante Mungu na asante wana Segerea, asante watu wote waliojitoa kufa na kupona kutusaidia, lakini pia asante kwa wale wote waliotusaliti kimya kimya ili kuchochea mgawanyiko wa kura hizi.
Naahidi kushiriki katika hatua zote za kumsaidia mshindi wa uchaguzi wetu ili atangazwe rasmi kuwa mbunge wa wana Segerea. Mimi nitaendelea na majukumu mengine lukuki ya kulijenga taifa letu.
Kwa sababu yaliyosababisha kukosa ushindi wetu ni mambo ya ndani ya vyama vyetu, sitachukua hatua zozote wala kukata rufaa kwa sababu wananchi hawakutunyima ushindi, tumeugawanya wenyewe.
Nawapongeza madiwani wa UKAWA walioshinda kwenye kata zote 13 za jimbo letu, tulishirikiana na kupambana pamoja hadi kuleta ushindi huu, nawataka wachape kazi kufa na kupona na waisimamie manispaa ya Ilala bila woga, nawaomba wakatumie mipango na ushauri tuliowahi kupanga pamoja ili kuwatendea wana Segerea yale waliyoyatarajia.
Mwisho, nataka kuwaeleza watanzania wote kuwa sina kinyongo na mtu yeyote kwa matokeo haya. Mimi ni kati ya watu wanaoamini kuwa SIASA SI AJIRA...Nitaendelea kuwatumikia watanzania kwa njia zote muhimu nje ya vyombo vya maamuzi.
Nataka kuwaambia wananchi wa Segerea kwamba niko imara sana, sijayumba wala kutetereka, nawapenda sana nyote na poleni na MSHTUKO wa matokeo haya na muda si mrefu tutayaweka hapa.
Ni mimi,
Mtatiro Julius,
Segerea.
Viewing all 104712 articles
Browse latest View live




Latest Images