Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104684 articles
Browse latest View live

Mazoezi ya Kuapishwa Rais Mteule Dk. John Pombe Magufuli Yapamba Moto Dar‏...Angalia Picha Hapa

$
0
0

Kibanda cha kitakachotumika wakati wa kuapishwa kwa Rais Mteule, Dk John Magufuli kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kesho kutwa kwenye Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam.
Askari wa Jeshi la Wananchi akiigiza kama Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi nchini, Jenerali Davis Mwamunyange na mwingine akiigiza kama Rais anayemaliza muda wake, Jakaya Kikwete wakati wa mazoezi ya sherehe za kuapishwa Rais wa Awamu ya Tano, Dk John Magufuli kwenye Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam.Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Davis Mwamunyange (wa pili kulia), Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, Ernest Maangu (wa tatu kulia) na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Said Sadick wakipiga saluti ulipokuwa unaimbwa wimbo wa Taifa wakati wa mazoezi ya sherehe za kuapishwa Rais wa Awamu ya Tano, Dk John Magufuli kwenye Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam.Maofisa mbalimbali wakiwa katika kibanda cha kiapo wakipanga jinsi viongozi watakavyokaa wakati wa sherehe za kuapishwa Rais wa Awamu ya Tano, Dk John Magufuli kwenye Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam.

Kikundi cha sarakasi kikitumbuiza wakati wa maandalizi hayo
Wasanii kutoka Zanzibar wakicheza ngoma ya kibati wakati wa mazoezi hayo.
Mtu aliyeigiza kama Rais Jakaya Kikwete, akiwa amesimama alipokuwa akipigiwa mizinga ikiwa ni ishara ya kuagwa kwa rais huyo kabla ya kuapishwa Rais mpya wa Awamu ya Tano, Dk John Magufuli wakati wa mazoezi hayo.
Viongozi mbalimbali wakiwemo wa vyombo vya ulinzi na usalama wakiwa Jukwaa Kuu wakati wa maandalizi hayo.
Baadhi ya wananchi wakiwa wamesimama wakati wimbo wa Taifa ukipigwa na Bendi ya Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) wakati wa maandalizi hayo.
Mtu aliyeigiza kama Rais Jakaya Kikwete, akielekea kukagua gwaride la heshima la kumuaga wakati wa mazoezi hayo.

Mwanachama wa CCM Awajeruhi Kwa Panga na Shoka Wanachama Wawili wa CUF.....

$
0
0
Jeshi la Polisi mkoani Tanga limemtia mbaroni mwanachama wa chama cha mapinduzi Jullius Joseph kufuatia kuwajeruhi vibaya wafuasi wawili wa chama cha wananchi CUF kwa kuwakata kwa kutumia shoka na panga na kuwajeruhi vibaya ambapo hivi sasa wamelazwa katika hospitali ya rufaa ya mkoa wa Tanga ya Bombo kwa ajili ya matibabu.
Chanzo ITV

Breaking News: CCM Wampitisha Mtoto wa Marehemu Abdallah Kigoda Kuwania Ubunge Jimbo la Handeni Mjini

$
0
0
Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa CCM  wamempigia kura na kumchagua tena mgombea ambae alishinda awali Omari Abdallah Kigoda katika uchaguzi uliofanyika wilayani humo leo baada ya kamati kuu ya CCM Taifa kutaka urudiwe.

Akitangaza matokeo hayo Mwenyekiti aliyesimamia uchaguzi huo Dk Maua Daftari alisema kuwa wajumbe wote kwenye mkutano walikuwa 690 na waliopiga kura ni 660 na uchaguzi ulikuwa wa wazi na haki na hakukuwa na tatizo lolote.

Alisema Omari Kigoda amepata kura 402 na mgombea mwenzake Hamisi Mnondwa alipata kura 257 huku kura moja ikiharibika na kufanya jumla ya kura zote kuwa ni 660 hivyo kumtangaza Omari kuwa mshindi katika kura halali 259.

Awali kabla ya uchaguzi huo mjumbe wa kamati kuu ya chama hicho Taifa Abdallah Bulembo alisema kuwa sababu kubwa ya kurudiwa uchaguzi huo ni kutokana na mshindi wa kwanza na aliyemfuatia kushindwa kuvuka nusu ya idadi ya wapiga kura hivyo hawakufika katika vigezo vinavyotakiwa.
Mgombea huyo anatarajiwa kwenda kuchukua fomu ya kugombea ubunge kwa msimamizi mkuu wa uchaguzi jimbo la Handeni Mjini kesho na kuirudisha ambapo tarehe tano wataanza kampeni rasmi.

Mchungaji TB Joshua Awa Gumzo Mitandao ya Kijamiii Baada ya Kutua Tanzania...Hivyo Ndivyo Watu Wanasema

$
0
0

Baada ya Ujio wa Mchungaji Maarufu Kutoka Nigeria TB Joshua Hapa Tanzania Siku ya Jana Kila mtu Anaongea yako kuhusu ugeni huo, Soma Hapa chini:


filbertmbwambo 
 Maswali magumu!
TB Joshua
1. Amekuja tz kushuudia kuapishwa kwa Magufu!?
2. Amekuja kuleta upatanisho!??
3. Amekuja kutoa maelekezo kuwa nani ni Rais halali??



mrekebishatabia
Ooh TB Joshua karibu tena na tena Tanzania...hata yeye pia hajakutana na EN Lowassa barabarani.
Tena bora amekuja maana nina list ndefu ya maombi maalumu. Huyu mtu nadhan si mchezo...si mnaona shati alilovaa?? Anafaa kabisa kutuombea watanzania hasa wenye mapepo ya Rangi mbali mbali.

udakutz_
TB Joshua baada ya kutua tu katika ardhi ya Tanzania alivua viatu na kanyaga ardhi ya bongo akiwa na soksi tu!! Hii ina maana gani?

linda_ukawa_supporter 
Naomba niwajuze kilichomleta TB Joshua kwa mujibu nilivyoelezwa na mtu wa karibu na Mbatia muda huu nikwamba kaja kunatafrija leo jioni na lengo lake kubwa ni kuwaeleza viongozi husika ukweli wa mambo kuwa mshindi wa urasis ni lowassa na km wanaweza wamuachie nchi maana kuna mapigo Mungu kamuonyesha kuwa watayapata kwa hiyo kaleta ujumbe wa Mungu ili kunawa mikono watakapo kaidi sauti ya Mungu.then km watakaidi pia wakimualika kwenye kumuapisha Magu atahudhuria km wageni wengine.maana yupo nchi kwa siku

mdaku_wa_town 
 IF THIS IS A STATE VISIT BASI LAZIMA SERIKALI ILIO IN POWER NDO IMPOKEE!. MIE SIMJUI HUYU JAMAA BUT NAISI NI MTU MWENYE POWER KWENYE AFRICAN SOCIETIES MIONGONI MWA VIONGOZI WA DINI. SO I GUES THATS WHY KAPATA MAPOKEZI YA KISERIKALI EVEN THOUGH KAJA KUTOA MESSAGE YAKE......PLUS HE WAS MORE COMFORTABLE KWA LOWASA KULIKO IKULU. CCM NI KUJISHAUWA TU WAMEMPOKEA BUT HAKUJA KI CCM. NI MAMBO YA PROTOCOL
Read more at http://websta.me/n/mdaku_wa_town#qRZiIzo8l0ig9zmj.99

SAMWELI SITTA Ajitosa Uspika wa Bunge..Awa Kada wa Kwanza Kutoka CCM Kuitaka Nafasi Hiyo...Amesema Haya

$
0
0
Samweli Sitta, 
WAZIRI wa Uchukuzi, Samuel Sitta ametangaza kuwa atawania nafasi ya Spika ili kuliongoza Bunge la 11. Sitta aliyewahi kuwa Spika wa Bunge la Tisa amekuwa kada wa kwanza wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kujitosa katika mchuano wa kuwania nafasi hiyo nyeti wakati huu ambao Bunge limevitaka vyama vya siasa viwe tayari kwa ajili ya kupeleka majina ya wateule wao wa nafasi hiyo mara itakapotangazwa kuwa wazi.

Msemaji wa Spika huyo mstaafu, John Dotto alisema jana Dar es Salaam kuwa Sitta amemua kuwania nafasi hiyo kutokana na uwezo na uzoefu alionao wa kuendesha Bunge. Alisema Sitta anaamini kuwa uwezo wake aliouonesha katika kuendesha Bunge la Tisa akitumia kaulimbiu yake ya ‘Spika wa Kasi na Viwango’ itamfanya aendane na kasi ya utendaji wa Rais Mteule, Dk John Magufuli.

Sitta alijizolea sifa wakati akiwa Spika wa Bunge la Tisa kuanzia mwaka 2005 hadi 2010, ikiwamo Bunge hilo kufanyia marekebisho ya kanuni mbalimbali zilizolifanya liwe na makali na kuibua kashfa nzito ikiwamo ya Richmond ambayo ilisababisha Waziri Mkuu, Edward Lowassa kujiuzulu na alilirejeshea makali Bunge.

Tayari Bunge la Jamhuri ya Muungano limetangaza kuanza kwa mchakato wa kumpata Spika mpya wa Bunge, atakayerithi mikoba ya Spika Anne Makinda.

 Kaimu Katibu wa Bunge, John Joel akizungumza na vyombo vya habari Dar es Salaam mapema wiki hii alisema kuwa mgombea wa nafasi ya Spika, anaweza kuwa Mbunge au mwanachama yeyote wa chama kwa masharti kwamba kama si Mbunge, jina lake lazima liwasilishwe kwanza Tume ya Taifa ya Uchaguzi siku tano kabla ya uchaguzi kujiridhisha kuwa mgombea huyo ana sifa za kuwa Mbunge.

Bunge hilo la Tisa lilipata ufanisi na mafanikio kadhaa kutokana na ubunifu na ujasiri wa baadhi ya wabunge wakiongozwa na utayari wa Sitta ambaye wakati akishika nafasi hiyo aliahidi kuwa ‘spika wa kasi na viwango.’

Mafanikio yaliyopatikana katika Bunge hilo ni pamoja na kutungwa kwa Kanuni mpya za Bunge za mwaka 2007, ambazo zimeelezwa kuwa zilisaidia kwa kiasi kikubwa kuliwezesha lifanye kazi kwa ufanisi kama vile kuondoa ukiritimba wa serikali kuwa ndiyo pekee inayoweza kupeleka muswada bungeni.

Kanuni hizo mpya za mwaka 2007 ambazo zilitokana na kufanyia marekebisho makubwa kanuni za Bunge za mwaka 2004, zilitoa mamlaka kwa kamati za kudumu za Bunge kuwa na uwezo wa kupeleka mswada kwa ajili ya kujadiliwa bungeni na hatimaye kuwa sheria.

Katika Hali Isiyo ya Kawaida...Chadema ‘Wajigamba’ Kufawafanyisha Polisi Maandamano Bila Kujijua

$
0
0
Katika hali isiyo kuwa ya kawaida Chama cha Demokrasia na Maendeleo mkoani Shinyanga leo kimedai kwamba Jeshi la Polisi mkoani humo limefanya maandamano ya Chadema bila kujijua.

Kwa mujibu wa baadhi ya viongozi wa chama hicho walidai kupokea taarifa kutoka kwa uongozi wa juu wa chama hicho ukiwataka kufanya maandamano leo nchi nzima  ya kupinga ushindi wa Dkt. John Pombe Magufuli kwa madai kuwa demokrasia imebakwa katika mchakato mzima wa uchaguzi  mkuu uliofanyika tarehe 25 oktoba 2015.

Katibu wa Chadema wilaya ya Shinyanga mjini George Kitalama amesema kwamba chama hicho kimefanikiwa kufanya maandamano kupitia  jeshi la polisi lililozunguka mji mzima kuwasaka wanachama wa chadema na kuambulia patupu.

“Tulipanga kufanya maandamano leo Novemba 03,2015 mji mzima wa Shinyanga lakini polisi ndiyo wamejitokeza kufanya maandamano wakiwa na magari yao kila mtaa.”Alisema Kitalama.

Kufuatia taarifa  ya Chadema kutaka  kufanya maandamano katika maeneo mbalimbali nchini Askari wa Jeshi la Polisi wamekuwa  katika misururu ya magari yakiwemo ya maji ya kuwasha wakizunguka kuwasaka waandamanaji kutoka chama hicho ambao hawakufanikiwa kufanya maandamano hayo.

Jijini Dares salaam Askari Polisi wakiwa kwenye punda na wengine wa doria wameonekana katika maeneo mbalimbali ikiwemo maeneo nyeti na yenye ofisi nyingi za Serikali ikiwemo Posta.

Wanafiki Wote Walioihujumu CCM Wakati Wa Kampeni Kutimuliwa

$
0
0
WANACHAMA na viongozi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) waliohusika kwa namna moja ama nyingine kukihujumu chama hicho wakati wa kampeni za uchaguzi mkuu na kukikosesha ushindi katika kata na majimbo kadhaa, wametakiwa kutafuta pa kwenda kabla ya kufukuzwa uanachama.

Kauli hiyo imetolewa juzi na Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Tabora Mjini, Abdulrahman Nkonkota alipokuwa akihutubia mkutano wa hadhara wa wana CCM kutoka maeneo mbalimbali ya mji huo wa kumpongeza Rais Mteule wa awamu ya tano, Dk John Magufuli kupitia chama hicho.

Alisema ili CCM iendelee kupata kibali kwa wananchi na kushika dola ipo haja ya kusafisha chama kwa kuondoa wanafiki na wasaliti walioko ndani ya chama.

Alisema hao kwa kuwa wanadumaza maendeleo ya chama pamoja na serikali huku akibainisha wazi kuwa wataanza operesheni safisha chama ili kiweze kutekeleza malengo yake yapatayo 19.

“Naunga mkono kauli ya Rais wetu Mteule Dk Magufuli ya kuwaondoa wanafiki katika chama ambao wamerudisha nyuma maendeleo ya chama chetu hali iliyowafanya baadhi yao kupoteza imani kwa chama chao”, alisema.

Awali Katibu wa CCM wilaya ya Tabora Mjini, Kameth Ndaghine alisoma tamko la wana CCM wa wilaya hiyo la kumpongeza Dk Magufuli na mgombea mwenza Samia Suluhu Hassan kwa kuibuka na ushindi wa kishindo katika uchaguzi mkuu uliofanyika nchini kote Oktoba 25 mwaka huu.

Alisema wanaamini uwezo mkubwa walio nao viongozi hao utawavusha Watanzania na kuwaondoa katika dimbwi la umasikini sambamba na kuongeza ajira kwa vijana.

Aidha alimwomba Magufuli mara tu atakapoapishwa ahakikishe anaanza kutekeleza ahadi zake hasa kwa kujenga mahakama ya mafisadi na kuwachukulia hatua kali wala rushwa ambao wamelifikisha taifa pabaya.

Ndaghine alisema pamoja na kuanzisha mahakama ya mafisadi awashughulikie watumishi wa umma wanaoendekeza uzembe na wale wanaofanya kazi kwa mazoea ili kurudisha imani kwa Watanzania waliomwamini na kuiamini CCM hadi kuipa ushindi wa kishindo.

Hali si Shwari Kivuko cha Kigamboni..Baadhi ya Watu Watumia Mitumwi ya Wavuvi Kuvuka

$
0
0
Kivuko cha MV Magogoni leo asubuhi kimepata hitilafu na hivyo kushindwa kufanya kazi ya kuvusha watu kutoka na kwenda Kigamboni

Hali hii imesababisha baadhi ya watu kutumia mitumbwi ya wavuvi kuvuka

TB Joshua Azua Jambo! Akanyaga Ardhi ya Tanzania Bila Viatu..Je Unajua Maana yake?

$
0
0
TB Joshua Azua Jambo! Akanyaga Ardhi ya Tanzania Bila Viatu..Jambo lililoleta Maswali Mengi Sana Kwa Watanzania....Je Unajua Maana yake?

Habari zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumatano Nov 4.....

$
0
0
Habari zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumatano Nov 4.....

Taarifa ya Serekali Kuhusu Taarifa za Kifo cha Rais Mstaafu, Benjamin Mkapa Zilizozagaa Mitandaoni

$
0
0
Msemaji  Mkuu wa Serikali ya Tanzania, Assah Mwambene amekanusha taarifa zinazosambaa katika mitandao ya kijamii kuhusu Rais Mstaafu, Benjamin Mkapa kuwa amefariki Dunia.

Akizungunza na waandishi wa habari katika ukumbi wa Habari Maelezo jijini Dar es Salaam, Mwambene amesema Rais Mkapa yupo salama na mzima wa afya na hakuna maradhi yoyote yanayomsumbua.

Mwambene amewaasa watumiaji wa mitandao mbalimbali hasa Blogs kuacha kuitumia mitandao hiyo kwa kupotosha umma na kuandika nambo yasiyo na ukweli ili kuepusha mifumuko ya habari za upotishaji.

Si jambo jema na wanaofanya hivyo waache mara moja kabla ya hatua stahiki hazijachukuliwa,” amesema Mwambene.

Amesema kuwa jambo la kumzushia mtu kifo si jambo zuri ambalo amelizungumza kama ‘uchuro’ kwa mtu husika na kumtabiria mabaya.

Mkapa yupo hai na kesho pia atakuwepo katika sherehe za kumuapisha Rais mteule wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, John Magufuli,” amesema Mwmbene na kuongeza.

Serikali italishughulikia hili na tayari imeshaanza kukamata baadhi ya watu mbalimbali ambao wanatoa taarifa za uongo zinazopelekea umma kupotoka.

Amesema kuwa vyombo vya habari vifanye kazi kwa uweredi ili kazi ya uandishi wao iwe ya usawa na kufuata misingi ya uandishi, jambo ambalo wengi hukiuka kutokana kutofuata weredi wa kazi zao.

Rais Jakaya Kikwete Atangaza Kuwa Kesho ni Siku ya Mapumziko Tanzania..

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete ameamua na ameitangaza kesho, Alhamisi, Novemba 5, mwaka huu, 2015, kuwa Sikukuu na siku ya mapumziko.

Rais Kikwete amefanya uamuzi huo, ili kuwawezesha Watanzania kushiriki katika sherehe za kuhitimisha Uongozi wa Serikali ya Awamu ya Nne na kuingizwa madarakani Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli kuwa Rais wa Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa Dar es Salaam leo Jumatano, Novemba 4, 2015 na Ofisi ya Katibu Mkuu Kiongozi (KMK) Balozi Ombeni Yohana Sefue, Rais Kikwete ametoa uamuzi huo kwa mujibu wa mamlaka aliyo nayo chini ya Kifungu cha 3 cha Sheria ya Sikukuu za Kitaifa.

Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu,
DAR ES SALAAM.

4 Novemba, 2015

Rais Kikwete Afanya Mazungumzo na Mgombea Urais wa Zanzibar, Maalim Seif - Ikulu ya Dar

$
0
0
Rais Jakaya Mrisho Kikwete wa Tanzania amefanya mazungumzo na makamu wa rais wa kwanza kisiwani Zanzibar ambaye ndiye mgombea Urais kupitia tiketi ya chama cha upinzani (CUF) Maalim Seif katika Ikulu Jijini Dar es Salaam.

Hatua hiyo inajiri wakati ambapo kuna tofauti za kisiasa kisiwani Zanzibar baada ya Tume ya Uchaguzi(ZEC) kufuta matokeo ya uchaguzi uliofanyika . 

Video:

Masanja Mkandamizaji Achukua Form za Kugombea Ubunge Ludewa na Ktangaza nia Kuchukua Nafasi ya Marehemu Filikunjombe

$
0
0
Masanja Mkandamizaji
MSANII maarufu na mwigizaji Emmanuel Mgaya maarufu kwa jina la (Masanja mkandamizaji) ameahidi kuvaa viatu vya Deo H. Filikunjombe kwa kuwaletea maendeleo wananchi wa jimbo la Ludewa na kusema ana uwezo mkubwa na kasi kama ya marehemu Filikunjombe ambaye alikuwa rafiki yake.

Ameyasema hayo alipokuja kuchukua fomu ya kugombea kupata ridhaa ya Chama cha Mapinduzi,jumla ya watu tisa akiwemo mdogo wa marehemu Fillipo Filikunjombe ambaye ni mwanasheria wa TCRA wamechukua fomu ili kuweza kuomba ridhaa.

Kimenuka: Asimilia 82 ya Wanafunzi Wakosa Mikopo 2015/16

$
0
0
Asimilia 82 ya Wanafunzi Wakosa Mikopo 2015/16

Zaidi-ya wanafundi 50,000 watashindwa kuendelea na masomo ya elimu ya juu kutokana na kushindwa kupata mikopo kutoka katika Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu (HESLB).

Hayo yamebainika ikiwa ni siku tatu tangu HESLB kutoa majina ya wanafunzi waliofanikiwa kupata mikopo kwa mwaka wa masomo 2015/2016, huku idadi kubwa ikiwa haimo katika majina hayo.Katika mwaka huu wa masomo bodi ya mikopo imeweza kuwapatia mikopo wanafunzi 12,000 pekee sawa na 17.1% ya waombaji zaidi ya 70,000, hivyo kufanya idadi ya wanafunzi waliokosa mikopo kufikia asilimia 82.9 ya waombaji wote.

Wanafunzi waliokosa mikopo ya kuwawezesha kujiunga na elimu ya juu na hivyo wazazi wao kutakiwa kugharamia elimu hiyo wameelezea kusikitishwa na hali hiyo huku wakiitaka serikali kuwaangalia kwa jicho la kipekee kwani hawana uwezo wa kuanza masomo pasipo kufadhiliwa na serikali.

Wanafunzi hao walionekana kukata tamaa ya kutimiza ndoto yao ya kujiunga na elimu ya chuo kikuu, wamefika makao makuu ya bodi hiyo huku wakiongozana na baadhi ya viongozi wa serikali ya wanafunzi kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) kutaka kujua hatima yao.

Nimetokea Tabora, wazazi wangu walinipa Sh. 100,000 ya kutumia wakiamini tunapewa mikopo na serikali, lakini tumenyimwa na hatujui hatima yetu, nimebakiwa na Sh. 6,000, naomba serikali ituhurumie, isikie kilio chetu hatustahili kuteseka hivi,?-ameeleza Abdul Omary mwanafunzi mteule UDSM.Fatuma Bakari, mwanafunzi mwingine kutoka UDSM, amesema:-

Siwezi kujiunga na Chuo bila mkopo, tumefika hapa ili kuomba bodi ya mikopo itusaidie hatuna tumaini lolote zaidi ya kuomba Mungu atusaidie tuweze kupata mikopo na kuanza masomo.

Waziri wa Mikopo serikali ya wanafunzi (Daruso), Shitindi Venance ameeleza kutokukubaliana na majibu waliyopewa na uongozi wa juu wa bodi ya mikopo kwani yanakatisha tamaa na kuzima ndoto za wanafunzi wa masikini kusoma chuo kikuu.?Hapa UDSM ni wanafunzi 600 tu waliopata mikopo kati ya wanafunzi 7,000 waliopangiwa kuanza masomo, hili ni janga kubwa kwa watoto wa masikini kwani hawawezi kujisajili chuoni wala kupata makazi katika mabweni mpaka walipe ada na wengi wametoka mikoani.

Tunachukua hatua moja mbele na kuamua kulifuatilia suala hili kwa katibu mkuu wa wizara ya elimu na katibu mkuu wa wizara ya fedha kwa sababu bodi bado wanasisitiza tuwe na subira ilihali muda umeenda na wanafunzi wanateseka ameeleza Shitindi.

Mkurugenzi wa Habari, Elimu na Mawasiliano wa HESLB, Omega Ngole amewaambia wanahabari waliofika ofisini kwake kuwa bodi haistahili kulaumiwa kwani serikali kupitia wizara ya fedha na wizara ya elimu ndio yenye uwezo wa kutenga kiasi cha fedha kulingana na mahitaji ya wakati husika.

Lengo la bodi ya mikopo ni kuwawezesha wanafunzi wa vyuo vikuu kusoma kwa ufadhili wa serikali na wala sio kuwakwamisha, tunaendelea kujadiliana na serikali kuona kama itatuongeza fedha ili tuweze kutoa awamu ya pili ya majina ya wanafunzi waliopata mikopo, tunawaomba wanafunzi wavute subira,?-anaeleza NgoleHata hivyo Ngole amesema hawezi kusema lini watatangaza majina ya awamu ya pili kwani hilo linategemea ni lini serikali itatoa fedha kwa ajili ya wanafunzi wa awam ya pili.

Katika mwaka uliopita wa masomo 2014/2015 serikali ilitoa mikopo kwa wanafunzi 30,000 sawa na 51.7% ya waombaji wote 58,000 na hivyo kufanya waliokosa mikopo kuwa wanafunzi 28,000 sawa na 49% pekee tofauti na mwaka huu ambapo waliokosa wamefikia asilimia 82.9

Chanzo: Mpekuzi blog

Diamond Platnumz Ex Girlfriend Wema Sepetu’s New Ride Will Leave East African Women Dying Of Jealousy (PHOTOS)

$
0
0

Wema Sepetu has finally settled down with her new beau Luis Munana. The actress cum model seems to have accepted and moved on from her relationship with her ex Diamond Platnumz.

The sexy lady is currently said to be enjoying her life with her new lover and recently, photos of her new 2015  range rover sport surfaced online, but it is not clear if she bought it herself or it was given to her by Luis, her hubby.

Wema Sepetu once had a Nissan Murano, which she was bought for by her ex-boyfriend but later sold it at the beginning of the year.


The face of the Tanzanian acting industry is the latest East African female celebrity to own the heavy machine after controversial Kenyan socialite Vera Sidika

Wema Sepetu has been a key campaigner in the just concluded Tanzania elections.



Lulu And Wema Sepetu End Their Cold War !

$
0
0
Recently it was reported Lulu Elizabeth Michael and Wema Sepetu are't in good terms  but it seems the two famous actresses have buried the hatchet as Lulu was invited at Wema's Royal Birthday over the weekend and she showed up and even took photos together.





Jukwaa la Wahariri Walaani Tukio la Kuzomewa Dk Reginald Mengi na Wafuasi wa CCM

$
0
0
JUKWAA la Wahariri (TEF), limelaani kitendo cha kuzomewa na kudhalilishwa kwa waandishi wa habari wa ITV, katika Ofisi Ndogo za Makao Makuu ya CCM, Dar es Salaam, Oktoba 30 mwaka huu.

Akizungunza na waandishi wa habari Katibu wa Jukwaa hilo, Neville Meena amesema kuwa kitendo hicho si cha kukaliwa kimya kutokana na kukwaza utendaji wa kazi na kudhalilisha utu wa waandishi hao mbele ya jamii.

Meena amesema kuwa waandishi na wafanyakazi wa kituo hicho walikuwa katika ofisi hizo za CCM, wakirusha na kuandika habari za tukio la mapokezi ya Dk. John Magufuli baada ya kukabidhiwa hati ya ushindi wa urais na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) katika hafla iliyofanyika siku hiyo katika ukumbi wa Diamond Jublee.

“Kuzomewa kwa waandishi hao katika ofisi za CCM ni muendelezo wa kile kilichoanzia Diamond Jubilee ambapo wafuasi wa Chama cha Mapinduzi CCM, walionekana wakiwazomea wafanyakazi wa ITV na baadaye kumzonga Mwenyekiti Mtendaji wa IPP, Dk Reginald Mengi ambaye ni mmliki wa kituo hicho,” amesema Meena.

Ametoa onyo kwa kuwataka wafuasi hao waache vitendo hivyo, akisema kuwa utafiti mdogo waliofanywa na Jukwaa hilo kuhusu vitendo hivyo vinatokana na wafuasi hao kuchukizwa na jinsi kituo hicho kilivyoripoti, matukio ya kampeni na kuwapa fulsa wagombea wa vyama vingine vya siasa.

Amesema kuwa kituo hicho ni miongoni mwa vyombo vya habari vilivyofanya kazi zake kwa weredi wakati wa kampeni za wagombea wa vyama vyote nchi nzima ambapo Dk. Magufuli na Mgombea Mwenza, Samia Suluhu walikuwa na wandishi wa kituo hicho miongoni mwao ni Emmanuel Buhohera na Halfan Liundi ambapo umma wa watanzania ulipata kufahamu kinachoendelea katika mikutano yao ya kampeni.

Meena ameongeza kuwa hilo sio tukio la kwanza kufanywa na chama hicho kwani wakati wa kampeni za mgombea urais kilimfukuza katika msafara wa Dk. Magufuli mkoani Mbeya, mwandishi wa gazeti la Mwananchi, Peter Elias kwa madai ya kutofurahishwa na habari aliyoandika kuhusu mgombea wao.

Amesema kuwa matuko hayo siyo ya kiungwana na hayatakubalika katika jamii ya watu wastaarabu. Ikiwa waandishi wa habari au vyombo vya habari vinafanya makosa zipo njia za kisheria za kushughulikia makosa hayo pamoja na kufanya mazungumzo kupitia taasisi za waandishi wa habari.

“Tunachukua fulsa hii kuvitaka vyama vya siasa kama taasisi viongozi, wanachama na wapenzi wake kuacha mara moja vitendo vya kuwashambulia waandishi wa habari kwa sababu zozote zile. Tusingependa ifike hatua kutangaza kwamba matukio ya chama fulani ni hatari kwa waandishi wa habari,” amesema Meena.

Kadhalika tunachukua fursa hii kuvitaka vyama vya siasa na watu binafsi wanaoandaa mikutano inayowahusisha waandishi wa habari kuhakikisha kuwa waandishi wanakuwa salama wanapo hudhuria kwenye mikutano yao na kuchukua hatua ya kukemea.

“Tunasikitika kwa ukimya wa chama hicho ulionyesha kufurahishwa kwa tukio hilo kutokana na kutotoa kauli yoyote,” amesema Meena.

T.B Joshua Akutana na UKAWA Nyumbani Kwa Lowassa

$
0
0
Muhubiri wa Kimataifa kutoka nchini Nigeria, T. B. Joshua (shati la miraba), akizungumza jambo na wenyeji wake, aliekuwa Mgombea Urais wa Tanzania kwa tiketi ya CHADEMA kupitia mwamvuli wa UKAWA, Edward Lowassa na viongozi wakuu wa UKAWA,Freeman Mbowe,  James Mbatia pamoja na mwanasiasa mkongwe nchini, Mzee Kingunge Ngombale Mwiru, wakati alipofika nyumbani kwa Lowassa, Masaki jijini Dar es Salaam kwa mazungumzo maalum.



Kinyang'anyiro cha Uspika wa Bunge...Samweli Sita na Zungu Kushikana Mashati ...Wengine ni Hawa Hapa

$
0
0
Wakati Bunge la Kumi na Moja likitarajiwa kuanza vikao vyake wiki ijayo mjini Dodoma, Samuel Sitta  na Anne Makinda, waliokalia kiti cha Spika wa mabunge mawili yaliyopita, wanatajwa kuwamo kwenye mchuano mwingine wa kuwania nafasi hiyo ya kuongoza chombo hicho cha kutunga sheria.

Majina ya makada hao wawili wa CCM, ambao mwaka huu hawakugombea ubunge kwenye majimbo yao, ni miongoni mwa watu kadhaa wanaotajwa kuwania kuongoza Bunge la 11 ambalo linatarajiwa kuanza vikao vyake wiki ijayo.

Kada mwingine wa CCM ambaye amekuwa akitajwa kwa muda mrefu ni mbunge wa Ilala, Mussa Hassan Zungu ambaye anatarajiwa kutoa upinzani mkubwa kwa wawili hao endapo ataingia kwenye mchakato wa kuwania nafasi hiyo.

Wengine wanaotajwa kuitaka nafasi hiyo ni mbunge mteule wa Peramiho, Jenister Mhagama, mbunge mteule wa Kibakwe, George Simbachawene na Job Ndugai ambaye ni Naibu Spika wa Bunge lililomaliza muda wake.

Kiti cha spika kinaweza kuwaniwa na mtu yeyote ambaye atapitishwa na chama chake bila ya kujali kama ni mbunge.  CCM hutoa fursa kwa wanachama wake kuomba nafasi hiyo na baadaye kikao cha wabunge wa chama hicho hukutana kupitisha jina la mgombea mmoja.

Iwapo mgombea hatakuwa mbunge mteule, ni lazima jina lake lipitishwe na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC).

Iwapo wawili hao wataingia kwenye kinyang’anyiro hicho, Sitta, aliyeongoza Bunge la Tisa ambalo linasifika kwa kuruhusu hoja zilizoibana Serikali, na Makinda, aliyeongoza Bunge la Kumi lililoibua kashfa zilizolazimisha mawaziri kujiuzulu, watakuwa wakipambana kwa mara ya pili baada ya kukutana mwaka 2010 wakati CCM ilipomtosa Sitta kwa hoja ya “kutaka Spika mwanamke”.

Habari kutoka kwa watu walio karibu naye zinasema Sitta, ambaye ni Waziri wa Uchukuzi, atapeleka jina lake CCM kwa ajili ya kuteuliwa kuwania nafasi hiyo.

Taarifa hizo zilithibitishwa na msemaji wa mbunge huyo wa zamani wa Urambo Mashariki, John Dotto ambaye alilieleza gazeti hili kuwa Sitta atawania nafasi hiyo kutokana na uwezo na uzoefu alionao wa kuendesha Bunge.

 Alisema Sitta anaamini kuwa uwezo wake aliouonyesha katika kuendesha Bunge la Tisa (2005 hadi 2010) akitumia kaulimbiu yake ya “Spika wa Kasi na Viwango”, utamfanya aendane na kasi ya utendaji wa Rais Mteule, Dk John Magufuli.

Habari zaidi zinaeleza kuwa Sitta ana nafasi kubwa ya kuibuka mshindi kutokana na rekodi yake na pia kukubalika na wabunge wengi wa CCM na hata wa vyama vya upinzani.

Hata hivyo, Sitta hakupatikana kueleza kiundani kuhusu suala hilo kutokana na kuwa nje ya nchi. Alitarajiwa kurejea jana jioni.

Baada ya kuongoza Bunge lililomlazimisha Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa kujiuzulu, Sitta alijaribu kutetea nafasi yake mwaka 2010, lakini akagonga mwamba.

Baadhi ya watu walimuona kuwa ni mtu aliyekuwa akiruhusu mijadala ya kuibana Serikali, kitu kilichofanya ajijengee uadui na baadhi ya vigogo.

Wakati alipowania nafasi hiyo mwaka 2010 alijikuta akipambana na Andrew Chenge, mpinzani aliyeonekana kuwa na sifa na nguvu inayolingana naye ndani ya CCM, hali iliyokifanya chama hicho kupata mwanya wa kutumia hoja ya “zamu ya wanawake” na wote wawili wakakosa nafasi.

Sitta, ambaye amekuwa mbunge kwa vipindi tofauti kati ya mwaka 1975 na 2015, alipambana tena na Chenge kuwania uenyekiti wa Bunge la Katiba mwaka 2013.

Kabla ya kuanza kwa kampeni za uchaguzi huo, Chenge alijitoa na kumuachia Sitta ambaye aliwashinda kirahisi wagombea wengine. Makinda hakutarajiwa kuingia kwenye kinyang’anyiro hicho mwaka 2010, lakini alipoingia mara moja akawa anapewa nafasi kubwa.

Watu wa karibu na Makinda, ambaye kwa mara kadhaa alikuwa akilaumiwa na wabunge wa upinzani bungeni kwa kile walichodai ni kuibeba CCM, walilithibitishia Mwananchi kuwa Spika huyo wa Bunge la Kumi atawania tena nafasi hiyo. “Subiri tu utaona, pengine anaweza kutangaza ama akajitosa tu kimya kimya. Anaonekana kuitaka nafasi hii,” alisema mtu aliye karibu naye ambaye aliomba jina lake lihifadhiwe.

Kwa kawaida Makinda si mzungumzaji sana na vyombo vya habari, hasa kwa masuala yake binafsi.

Kwa upande wa Zungu, ambaye alikuwa mmoja wa wenyeviti wa Bunge la Kumi, hakutaka kukanusha wala kuthibitisha suala hilo alipoulizwa na gazeti hili.

Zungu aliliambia gazeti hili jana kuwa chama chake bado hakijatoa mwongozoo wowote hadi kufikia jana jioni na hivyo hawezi kuzungumzia suala hilo.

Mtu mwingine anayetajwa kwenye kinyang’anyiro hicho ni Naibu Spika anayemaliza muda wake, Job Ndugai, ambaye pia hakutaka kuzungumzia suala hilo kwa madai kuwa bado anauguza ‘majeraha’ ya Uchaguzi Mkuu.

Ndugai, ambaye amerudi bungeni akiliwakilisha Jimbo la Kongwa, alisema wiki hii atavieleza vyombo vya habari kama atawania nafasi hiyo.

Jibu kama hilo lilitolewa na Mhagama, ambaye pia alikuwa mwenyekiti wa Bunge la Kumi kabla ya kuteuliwa kuwa waziri. Mbunge huyo wa Peramiho alisema hawezi kuzungumzia  vyema suala hilo kwa sababu yupo katika matayarisho ya hafla fupi ya kuapishwa kwa Rais Mteule.

Juhudi za kumpata Simbachawene ziligonga ukuta.

Kuhusu kupitisha wagombea wa kiti hicho, makamu mwenyeki wa CCM, Philip Mangula alisema mchakato wa chama hicho kupokea majina ya wanaotaka kugombea uspika, bado haujaanza kutokana na kutotangazwa rasmi.

Wakati hali ikiwa haijapamba moto ndani ya CCM, mwanasheria mkuu wa Chadema, Tundu Lissu jana alisema vyama vinavyounda Ukawa-Chadema, NCCR-Mageuzi, NLD na CUF- havijaanza mikakati ya kupitisha mtu atakayegombea uspika, badala yake vinaandaa kambi imara ya upinzani  kwa ajili ya kuibana Serikali bungeni.

Akizungumzia utaratibu wa kumpata Spika, mkurugenzi wa shughuli za Bunge, John Joel alisema wagombea wanaruhusiwa kutoka vyama mbalimbali vya siasa na kwamba mchakato huo utaanza baada ya rais kuapishwa na kuitisha Bunge.

“Nafasi hii haigombewi na mgombea binafsi. Ni lazima apitishwe na chama. Kama ni mbunge mteule jina lake linaletwa moja kwa moja katika ofisi za Bunge ila kama ni mwanachama wa kawaida lazima athibitishwe na NEC kuona kama ana sifa,” alisema Joel.

Alisema rais akishaitisha vikao vya Bunge, chombo hicho cha kutunga sheria ndio kitaanza mchakato wa uchaguzi wa spika na kazi ya kwanza itakuwa kupokea majina ya wagombea kutoka vyama mbalimbali.

Viewing all 104684 articles
Browse latest View live




Latest Images