Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104776 articles
Browse latest View live

Temptation Kibao! Imagine If This LADY Was Your Secretary (VIDEO)

$
0
0

Many secretaries go to work dressed to kill and that’s why their bosses fall into temptation.

A case in point is this lady said to be working as a secretary, who decided to flaunt her curvaceous figure by wearing a black s3xy dress that left her big b()()ty well exposed for all to see.

Just watch the video below; what if you were the boss?



I'm Not Old...No Man Can Resist My Body Even After 4 Children …… DIAMOND’s wife Zari

$
0
0

Diamond’s wife, Zari Hassan, has rubbished her haters who keep saying that she is an old woman and those who have been pushing a rumour on social media that she is now in her 40s.

Zari says that she started giving birth when she was still young and having many children does not translate to one being old.

Here is what she posted;

Ati she has 4 kids she is old blah blah…. Had ma 1st baby when I Was 23. Having kids doesn’t make one old coz you might have had them while young.





Mkazi Mmoja wa Mkoa wa Morogoro Amejikata Kidole Chake Baada ya Lowassa Kukosa Urais

$
0
0
Mkazi mmoja wa mkoa wa Morogoro amejikata kidole chake kidogo cha mkono wa kushoto ambacho huingizwa kwenye wino baada ya kupiga kura ikiwa ni hasira ya Lowassa kukosa uraisi.
Mkazi huyo pia ameharibu kadi yake ya kupiga kura na kuahidi kutopiga kura tena katika maisha yake.

NANI Alisema Dr John Magufuli Ajui Kuongea Kingereza..Sasa Hapa Nimekuwekea Video Akimwaga Kingereza Mpaka Utafurahi

$
0
0
NANI Alisema Dr John Magufuli Ajui Kuongea Kingereza..Sasa Hapa Nimekuwekea Video Akimwaga Kingereza Mpaka Utafurahi Nimekuwekea
VIDEO HAPA CHINI:

Zigo la Z’bar ni la Magufuli au Kikwete?

$
0
0
Wakati majadiliano ya kina yanaendelea visiwani ili kufikia mwafaka wa kuendelea na mchakato wa kutangaza matokeo ya uchaguzi mkuu Zanzibar uliofanyika Oktoba 25 au kurudiwa upya, imeelezwa kuwa suala hilo linaweza kupata ufumbuzi iwapo litashughulikiwa na Mwenyekiti wa CCM Taifa, Jakaya Kikwete au Rais wa Awamu ya Tano, Dk John Magufuli.

Kikwete ametupiwa zigo hilo kwa sababu ya wadhifa wake wa uenyekiti wa chama tawala ambacho kwa Zanzibar kinapambana na chama cha upinzani cha CUF.

Hata hivyo, kundi jingine linasema suala la Zanzibar linaweza kutatuliwa na Rais wa Tanzania, Dk Magufuli kwa sababu ndio mwenye dola.

Lakini baadhi ya wasomi wamesema jambo hilo litamalizwa na Wazanzibari wenyewe.

Wakitoa maoni yao kuhusu mtanziko wa kisiasa uliovikumba visiwa vya Unguja na Pemba tangu Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC), Jecha Salum Jecha alipotangaza kufuta matokeo ya uchaguzi mkuu, wiki iliyopita wamesema hali ya sasa inafafana na iliyotokea miaka ya nyuma ambapo ilimalizwa kwa aliyekuwa Rais wa Zanzibar, Amani Karume na Katibu Mkuu wa CUF, Seif Sharrif Hamad kukutana na kumaliza tofauti zao.

Baada ya viongozi hao kujali maslahi ya Wazanzibari walikubaliana kurekebisha Katiba ya Zanzibar ambapo vyama vilivyotofautiana kwa asilimia ndogo ya ushindi vishiriki kuunda Serikali. Mwafaka huo ndio uliozaa Serikali ya Umoja wa Kitaifa (SUK) ambayo ilimaliza mpasuko na uhasama wa kisiasa uliokuwapo awali.

Profesa Kopoka

Profesa wa Chuo Kikuu cha Dodoma, Peter Kopoka amesema viongozi wa vyama vya siasa vya CCM, CUF, na vingine vinavyohusika pamoja na ZEC, hawana budi kufikia mwafaka kwani mgogoro wowote ulimwenguni humalizwa na pande husika hivyo wakae na kumaliza wenyewe na siyo kutegemea zaidi watu wa nje.

“Wazungumze bila kulala wao kwa wao kupitia ZEC. Isitumike nguvu zaidi ya busara na kwa hali ilivyo wangefikia mwafaka hata leo,” alisema Profesa Kopoka.

“Kadri muda unavyokwenda bila kupatikana mwafaka ndivyo hatari inavyokuwa kubwa na huo ndiyo ukweli, hivyo Wazanzibari wenyewe wayamalize na hawa watu wa nje wawe ni wa kutoa mapendekezo tu.”

Dk Benson Bana

Mhadhiri wa Chuo Kikuu Dar es Salaam, Dk Benson Bana amesema kuwa tatizo la Zanzibar ni zaidi ya uchaguzi. “Kinachotokea Zanzibar kwa sasa ni aina ya muundo wa Muungano tu na si kingine,” alisema.

Kwa mtazamo wake ili migogoro ya kisiasa imalizike visiwani humo lazima upatikane muundo mwafaka ambao ni Muungano wa Serikali Moja badala ya huu wa sasa.

“Nje ya Serikali moja ‘makandokando’ hayataisha. Mjadala wa Serikali moja unaweza kufanyika taratibu tu na Dk Magufuli, Samia (Suluhu Hassan-Makamu wa Rais) na Maalim Seif mpaka mwafaka utapatikana. Busara iliyotumika kuunda Serikali ya Umoja wa Kitaifa itumike kumaliza sintofahamu iliyofanywa na Jecha. Mvutano huu wala hauwezi kumalizwa na mataifa ya nje ni Wazanzibari wenyewe na Watanzania,” alisema

Dk Bana alisema kuwa hata mwaka 2010, Maalim Seif alilalamika kuwa amepokonywa ushindi, lakini mazungumzo yalifanyika na hali ikawa shwari.

Dk Ave Semakafu

Mratibu wa Umoja wa Wanawake Wanasiasa Tanzania (Ulingo), Dk Ave Maria Semakafu alisema mwenendo unaoendelea kutatua mgogoro huo ndiyo sahihi kwa kuwa pande zinazohusika zimeonekana kuchukua hatua stahiki na subira zaidi inahitajika.

Alisema ni wazi kuwa katika uchaguzi huo kulikuwa na tatizo la msingi ambalo mojawapo ni uvunjaji wa Sheria ya Uchaguzi kwa mmoja ya wagombea kujitangazia ushindi, hivyo mazungumzo baina ya pande hizo yanahitajika na kuongozwa na busara.

“Kwa hali ilivyo ni heri tuwaache wajadili wenyewe, watafakari kwa kina ili watakapokuja na mwafaka uwe unajitosheleza na kumaliza kabisa mgogoro, hakuna haja ya kuharakisha mazungumzo hayo,” alisema.

Aidha, alisema mgogoro huo hautakiwi ujadiliwe na kuchukulia kama wa watu binafsi, yaani wa Maalim Seif na Dk Shein badala yake uangaliwe kwa mustakabali wa Wazanzibari wote.

Profesa Mpangala

Profesa Gaudence Mpangala wa Chuo Kikuu cha Ruaha alisema vyombo vya juu vya CCM vikiongozwa na Mwenyekiti wao, Rais Kikwete vina dhamana kubwa ya kutatua mgogoro huo.

Alisema matatizo yanayoendelea Zanzibar yanaeleweka kwa kuwa CCM huwa hawapo tayari kuachia madaraka hivyo hata kama mazungumzo yataendelea baina ya pande hizo mbili au kutekelezwa kwa uamuzi wa ZEC wa kurudia uchaguzi, hakutakuwa na matunda yoyote.

 “CCM ngazi ya taifa waamue kukubali hali halisi, iwapo wameshindwa katika uchaguzi wakiachie chama kilichoshinda zaidi ya hapo mgogoro wa Zanzibar unakuzwa bila sababu. Kwa maana hiyo ZEC isitishe kufuta uchaguzi, iendelee na kutangaza matokeo na aliyeshinda apatiwe madaraka kwa kuwa kurudia uchaguzi siyo utatuzi sahihi,” alisema Profesa Mpangala.

Profesa Penina Mlama

Mwenyekiti wa Kigoda cha Taaluma cha Mwalimu Nyerere, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Profesa Penina Mlama amesema kuwa mvutano huo utamalizwa na watu kutoka nje ya Zanzibar.

“Sidhani kama Wazanzibari wenyewe wanaweza kufikia muafaka wa suala hili. Rais Kikwete bado ni Mwenyekiti wa CCM, yeye pamoja na Rais Magufuli wanaweza kuweka mambo sawa. Bila shaka kuna mazungumzo yanaendelea sidhani kama viongozi wako kimya. Kama wakishindwa wanaweza kuwashirikisha viongozi wakuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki maana hata Tanzania huwa inasuluhisha migogoro ya nchi nyingine,” alisema.

Historia

Hii ni mara ya tatu unatokea mgogoro wa kisiasa Zanzibar ukihusisha matokeo ya uchaguzi mkuu. Mwaka 1995 ulizuka mgogoro mkubwa lakini Jumuiya ya Madola ilipatanisha na viongozi wa CUF na Serikali walitiliana saini lakini mwafaka haukuheshimiwa.

Baada ya uchaguzi mkuu wa 2005, Rais Kikwete alianzisha rasmi juhudi za kupatanisha na zilipoelekea kukwama Rais Karume na Maalim Seif walikutana, wakajadiliana, wakaafikiana kubadili Katiba na baada ya uchaguzi mkuu wa 2010 ikaundwa SUK.

Mvutano wa sasa ulizuka baada ya Jecha kufuta matokeo yote ya uchaguzi wote wa urais, wawakilishi na madiwani uliofanyika Oktoba 25, kwamba utarudiwa ndani ya siku 90.

Jecha alitaja sababu za kufuta uchaguzi huo kuwa ni baada ya kujiridhisha kuwa kulikuwa na ukiukwaji mkubwa wa sheria na taratibu na kwamba mmoja wa wagombea urais, Maalim Seif alishajitangazia matokeo yanayompa ushindi.

Uamuzi huo wa Jecha ulipingwa na watu wa kada mbalimbali, wakiwamo makamishna wa ZEC, jumuiya za kimataifa; waangalizi wa uchaguzi wa kimataifa na wa ndani pamoja na CUF wote wakishinikiza Tume iendelee na mchakato wa kumtangaza mshindi.

Tayari Maalim Seif, na Rais wa Zanzibar, Dk Ali Mohamed Shein wamekutana kujadili suala hilo. Kilichojadiliwa hakijawekwa wazi lakini viongozi wa CUF wamekuwa wakisisitiza kuwa hawatakubali kurudiwa kwa uchaguzi huo.

Nuh Mziwanda Adai Aliambiwa ili Asaidiwe Kimuziki Inabidi Asafirishe Unga

$
0
0
Baada ya Shilole kudai kuwahi kushawishiwa kujihusisha na biashara ya madawa ya kulevya katika muziki wake, mpenzi wake Nuh na yeye amekiri kukutana na changamoto hiyo hiyo.

Akizungumza kwenye kipindi cha Planet Bongo cha East Africa Radio, Nuh alisema kama angekuwa anataka mafanikio ya haraka angekuwa ameshapotea.

Wengi waliokuja walikuwa wananiambia issue za kuuza madawa ya kulevya, nianze kusafiri ili niweze kupata pesa ya kuendeleza muziki wangu,” alisema Nuh.

Aliongeza, “Mimi ni mwanaume niliyekamilika na nilichagua kuishi katika maisha yangu, sikuchagua maisha ya kuuza madawa ya kulevya, nimechagua maisha ya kuishi mimi ni mwanamuziki na kupata pesa kupitia muziki wangu. Kwahiyo maisha pia ni chaguo lako wewe mwenyewe ambaye unaishi. Kama umechagua kuishi maisha yako kwa shortcut utapata vitu kwa shortcut na maisha yako yatakuwa shortcut vile vile.”

Rais Magufuli akabidhiwa rasmi ofisi Ikulu na Rais Mstaafu Kikwete

$
0
0
MAKABIDHIANO YA TAARIFA RASMI IKULU.
 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, leo katika Ikulu ya Dar es Salaam amepokea taarifa rasmi ya makabidhiano ya Ofisi kutoka kwa Rais Mstaafu Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete.

Makabidhiano hayo yamefanyika leo mchana na kushuhudiwa na Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan, Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue na Maafisa wa Ofisi Binafsi ya Rais.

Utaratibu wa kukabidhiana Ofisi katika Ofisi Kuu hapa nchini ni jambo la kawaida na hivyo imebidi makabidhiano hayo kati ya Rais anayeondoka na anaye ingia madarakani kufanyika.

“Umeanza vizuri, baki na msimamo huo huo utasaidia sana wananchi” . Mhe. Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne amemueleza Mhe. Rais Magufuli wakati wa hafla hiyo ya makabidhiano.

Mhe. Rais Mstaafu amekabidhi taarifa rasmi yenye kurasa 53, ambayo kwa ujumla inaelezea kazi zilizokwisha kufanyika, ambazo zinasubiri kukamilika na zile ambazo zinasubiri maamuzi ya utekelezaji. Mengine ni hali halisi ya nchi katika nyanja zote za kiuchumi, kisiasa na kijamii.

Mhe. Rais Dkt. Magufuli amemshukuru Rais Mstaafu ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi kwa muongozo wake siku zote .“Nikushukuru kwa kuiacha nchi salama na itaendelea kuwa salama, nikushukuru kwa muongozo wako, na taarifa ya muelekeo na ninaahidi kuwa Hapa ni Kazi Tu”.
 
Mhe. Rais amesema na kumueleza Rais Mstaafu kuwa ametengeneza mazingira mazuri ambayo nchi nyingi zimeshindwa kufanya na hivyo basi kuahidi kuendelea kuchota hekima na busara kwa Marais wote wastaafu wakiwemo Mhe. Benjamin William Mkapa wa Awamu ya Tatu na Mzee Ally Hassan Mwinyi wa Awamu ya pili.

Wakati huo huo Mhe. Rais Magufuli ameendelea kupokea salamu za pongezi kutoka Kwa Msimamizi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) Bibi Helen Clark.

“Chini ya uongozi wako, tunatarajia kuzidi kuimarisha ushirikiano baina yetu, demokrasia, kushughulikia masuala ya umaskini na ajira kwa vijana , kukuza uchumi, na kulinda na kuhifadhi mazingira, masuala ambayo Tanzania na UNDP tumekuwatukishirikiana kuyaendeleza na kuyatimiza” amesema Bi Clark.

Salamu zingine ni kutoka kwa Rais wa Shirikisho la Uswiss, Mhe. Simonetta Sommaruga, Rais wa Jamhuri ya Italia Mhe. Sergio Mattarella, Rais wa Jamhuri ya Shirikisho la Ujerumani Mhe. Joachim Gauck na pia kutoka kwa Rais wa Finland Mhe. Sauli Niinisto.

Pongezi zingine zimetoka kwa Rais wa Jamhuri ya Urusi, Mhe. Vladimir Putin, Rais wa Jamhuri ya Sudan Kusini, Mhe. Salva Kiir Mayardit, Rais wa Jamhuri ya Korea Mhe. Park Geun-hye na kutoka kwa Rais wa Jamhuri ya Watu wa China, Mhe. XI Jinping.

Salamu pia zimemfikia Mhe. Rais Dkt. Magufuli kutoka kwa Rais wa Taifa la Eritrea Mhe. Isaias Afwerki na kutoka kwa Rais wa Ufaransa Mhe. Francois Hollande.Katika ujumbe wao, viongozi hao mbali na kumpongeza Mhe. Rais Dkt. Magufuli kwa kuchaguliwa kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, wamesisitiza kuendeleza na kuimarisha ushirikiano baina ya Tanzania na nchi zao.

Pia wameipongeza Tanzania kwa kudumisha demokrasia imara na Watanzania kwa ujumla kwa kuimarisha amani na utulivu wakati wa Uchaguzi Mkuu.

Imetolewa na:
Premi Kibanga,
Mwandishi wa Habari wa Rais, Msaidizi.
Ikulu,
DAR ES SALAAM.
12 Novemba, 2015

Rais Dkt John Pombe Magufuli akipeana mikono kwa furaha na Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne Dkt Jakaya Mrisho Kikwete aliyefika Ikulu jijini Dar es salaam kukabidhi rasmi Ofisi ya Rais
Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne Dkt Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue alipofika Ikulu jijini Dar es salaam kukabidhi rasmi Ofisi ya Rais
Rais Dkt John Pombe Magufuli akimsikiliza Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne Dkt Jakaya Mrisho Kikwete aliyefika Ikulu jijini Dar es salaam kukabidhi rasmi Ofisi ya Rais. Kulia ni Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue
Rais Dkt John Pombe Magufuli akimsikiliza Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne Dkt Jakaya Mrisho Kikwete wakati akiongea kabla ya kukabidhi rasmi Ofisi ya Rais Ikulu jijini Dar es salaam
Rais Dkt John Pombe Magufuli akipokea kwa furaha hati ya makabadhiano ya Ofisi kutoka kwa Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne Dkt Jakaya Mrisho Kikwete Ikulu jijini Dar es salaam leo Novemba 12, 2015

Rais Dkt John Pombe Magufuli akipokea kwa furaha hati ya makabadhiano ya Ofisi kutoka kwa Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne Dkt Jakaya Mrisho Kikwete Ikulu jijini Dar es salaam leo Novemba 12, 2015
Rais Dkt John Pombe Magufuli akiiangalia kwa furaha hati ya makabadhiano ya Ofisi aliyoipokea kutoka kwa Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne Dkt Jakaya Mrisho Kikwete Ikulu jijini Dar es salaam leo Novemba 12, 2015
Rais Dkt John Pombe Magufuli, Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne Dkt Jakaya Mrisho Kikwete, Makiamu wa Rais Mhe Samia Suluhu Hassan na Katibu Mkuu Kiongozi baada ya hafla ya makabidhiano rasmi ya Ofisi Ikulu jijini Dar es salaam kukabidhi rasmi leo Novemba 12, 2015
Rais Dkt John Pombe Magufuli, Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne Dkt Jakaya Mrisho Kikwete, Makiamu wa Rais Mhe Samia Suluhu Hassan baada ya hafla ya makabidhiano rasmi ya Ofisi Ikulu jijini Dar es salaam kukabidhi rasmi leo Novemba 12, 2015.

Gazeti la Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ) Lachapisha Taarifa ya Kufuta Rasmi Uchaguzi Wa Zanzibar

$
0
0
Wakati mazungumzo ya kutafuta ufumbuzi wa mgogoro wa uchaguzi mkuu wa Zanzibar yakiwa yamepamba moto, uamuzi wa kufutwa matokeo ya uchaguzi umetangazwa rasmi katika Gazeti la Serikali la Novemba 6, mwaka huu, hivyo kumaanisha uchaguzi huo sasa ni rasmi utarudiwa.

Kwa mujibu wa gazeti hilo, uamuzi huo umechapwa chini ya kifungu 119 (10) na Sheria ya Uchaguzi Namba 11 ya Mwaka 1984.

Gazeti hilo pia limetolewa kwa kuzingatia kifungu cha 3(1) na 5(a) vya Sheria ya Uchaguzi ya Zanzibar.

Aidha gazeti hilo la serikali limeeleza kuwa, matokeo yote ya Uchaguzi Mkuu yamefutwa kuanzia Oktoba 25, mwaka huu.

Kifungu cha 3 (1) cha Sheria ya Uchaguzi kinasema:  “Kanuni, maelezo na matangazo yote ambayo tume ina mamlaka ya kutunga au kutoa, itajaaliwa kuwa yametungwa au yametolewa kisheria kama yametiwa sahihi na Mwenyekiti wa Tume au Mkurugenzi wa Uchaguzi.”

“Mimi Jecha Salim Jecha, Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar kwa kuzingatia masharti ya kifungu cha 119 (10) cha Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984 na kwa mujibu wa vifungu vya 391) na 5 (a) vya Sheria ya Uchaguzi namba 11 ya mwaka 1984, natangaza uamuzi wa Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar kufuta matokeo yote ya Uchaguzi Mkuu wa Zanzibar wa tarehe 25, Oktoba,” gazeti hilo la serikali lilieleza.

Tangazo hilo kwenye Gazeti la Serikali  limetiwa saini na Mwenyekiti wa Zec Oktoba 28 mwaka huu na kwa msingi huo wananchi wa Zanzibar watatakiwa kuingia tena katika uchaguzi ndani ya siku 90.

Kabla ya kuchapwa kwa gazeti hilo, wajumbe saba wa Zec walikutana na kujadili kufutwa matokeo ya Uchaguzi Mkuu lakini kulitokea mvutano mkubwa kabla ya kuamuliwa kwa kutumia akidi ya wajumbe wengi waliounga mkono.

Katika kikao hicho, wajumbe wanne waliunga mkono uchaguzi kufutwa na wajumbe watatu walipinga kufutwa kwa matokeo ya uchaguzi huo, akiwamo Makamo Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Jaji Abdularhakim Issa Ameir.

Wajumbe wengine waliopinga matokeo kufutwa ni, Ayub Bakar (Cuf) na Nassor Khamis (Cuf) na wajumbe waliounga mkono walikua ni, Omar Ramadhan Mapuri (CCM), Salmin Senga (CCM) na Haji Ramadhan (Sau).

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais, Mohamed Aboud, alisema baada ya tume kuchapa Gazeti la Serikali juu ya kufutwa kwa matokeo ya uchaguzi mkuu, kinachosubiriwa ni tume kutangaza tarehe ya uchaguzi mkuu wa marudio visiwani humo.

Alisema serikali itahakikisha uchaguzi huo unafanyika kwa wakati kwa kuzingatia sheria na katiba ili wananchi wapate haki yao ya msingi ya kuchagua viongozi wao kwa haki na utaratibu wa kidemokrasia.

Alisema serikali imeanza kujipanga katika matayarisho ya gharama za uchaguzi huo, ikiwamo utoaji wa elimu ya uraia kwa wananchi kabla ya kufanyika.

Hata hivyo, Kiongozi Mwandamizi wa Muungano wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), Janeti Fussi, alisema umoja huo haukubaliani na uamuzi wa kurudiwa Uchaguzi Mkuu wa Zanzibar.

 “Tunamtaka Mwenyekiti wa Zec arudi kazini akamilishe uchaguzi wa Oktoba 25 na kumtangaza mshindi wa uchaguzi huo,” alisema Fussi ambaye ni Katibu wa Chadema Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja.

Naye Mkurugenzi wa Mawasiliano na Kampeni wa Cuf, Ismail Jussa, alisema Mwenyekiti wa Zec katika Gazeti la Serikali ameshindwa kuonyesha kifungu cha katiba au sheria kinachompa uwezo wa kufuta matokeo ya uchaguzi mkuu.

Alisema kifungu cha katiba namba 119 (10) cha Katiba ya Zanzibar alichokitumia kinazungumzia kiwango cha mikutano ya tume na kila uamuzi lazima uungwe mkono na wajumbe walio wengi na siyo kufuta matokeo ya uchaguzi.

Alisema msimamo wa Cuf upo palepale Zec itengue uamuzi wa mwenyekiti wake warudi kazini kukamilisha utaratibu wa kuhakiki na kutangaza matokeo ya majimbo yaliyobakia na kumtangaza mshindi wa uchaguzi huo.

Gazeti la Serikali la kufuta matokeo ya Uchaguzi Mkuu limetoka wakati viongozi wakuu wa Zanzibar wakiendelea na mazungumzo ya kusaka ufumbuzi wa mgogoro wa uchaguzi huo, akiwamo Rais Dk. Ali Mohamed Shein (CCM) na mgombea mwenzake kupitia Cuf, Maalim Seif Sharif Hamad ambaye anadai yeye ndiyo mshindi kabla ya matokeo kufutwa.

Lowassa kumnadi Godbless Lema Arusha Mjini Jumamosi hii....Pia Atalitumia Jukwaa Hilo Kuwashukuru Watanzania

$
0
0
Aliyekuwa mgombea wa urais wa tiketi ya Chadema, Edward Lowassa anatarajiwa kupanda jukwaani Jumamosi kumuombea kura mgombea wa ubunge wa Chadema Jimbo la Arusha Mjini, Godbless Lema.

Akizungumza katika mkutano wa uzinduzi wa kampeni za ubunge katika jimbo hilo uliofanyika Soko Kuu jana, Lema alisema Lowassa atazungumza na Watanzania na kuwashukuru pia kwa kura nyingi walizompa.

Awali, mbunge mteule wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi ‘Sugu’ alieleza kuwa Lowassa na viongozi wa Chadema watatoa tamko zito siku hiyo na kuwataka wakazi wa Arusha na Watanzania kutega masikio.

Lema ambaye pia ni mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema, aliwataka wakazi wa Arusha, kutokatishwa tamaa na kuendelea kuwa na huzuni kutokana na matokeo ya urais yaliyotangazwa na kuwa bado kuna harakati za chama hicho kusaka haki.

“Ndugu zangu msikate tamaa, tumesikia wengine wametupa shahada zao, hapana, kazi ndiyo imeanza na lolote linaweza kutokea kwa uwezo wa Mungu,” alisema.

Alisema huzuni ya matokeo yaliyotangazwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), haipo kwa wananchi tu, bali hata wajumbe wote wa kamati kuu.

“...Kwenye kikao cha kamati kuu, kuna wajumbe walimuomba Lowassa atoe tamko...  kama angetoa tamko la kupinga matokeo na kukubali watu kuingia mitaani, Tanzania ingekuwa imeingia katika machafuko makubwa.

“Tunaendelea kutumia taasisi za kimataifa kudai haki, ndiyo sababu mnaona Zanzibar wameshindwa kujitangazia matokeo, hii ni kazi kubwa ya Ukawa,” alisema.

Katika mkutano huo, Lema alieleza njama alizosema zinapangwa kumnyima ushindi na akaonya kuwa hatakuwa tayari kuona ameshinda lakini mwingine akatangazwa kushinda.

“Najua Arusha nitashinda kwa kura nyingi, lakini kama wakitaka kunipora ushindi sitakubali,” alisema Lema.

Aliwaomba wakazi wa Arusha kujitokeza kwa wingi Desemba 13 kumpigia kura nyingi, ili pia kuwezesha Chadema kupata viti viwili zaidi vya wabunge wa viti maalumu.

Makonda Afuata Nyayo za Dk John Magufuli Azindua ‘Sukuma Twende’ Kinondoni Kuwakomesha Watendaji Wabovu wa Serekali

$
0
0
MKUU wa Wilaya ya Kinondoni Paul Makonda kwa kushirikiana na kampuni ya Push Mobile leo wamezindua mfumo mpya wa utoaji taarifa ya uzembe unaofanyika katika sekta muhimu zilizopo wilayani humo.

Huduma hiyo itawahusu wananchi waishio Wilaya ya Kinondoni tu. Wananchi hao watapata fursa ya kutuma ujumbe kwa njia ya simu ya mkononi ambao utamfikia Makonda moja kwa moja na hivyo kumwezesha kushughulikia kero husika.

Akizungumza na waandishi wa habari leo ofisini kwake Jijini Dar es Salaam, Makonda amesema, wananchi wanatakiwa kutoa taarifa kuhusu kero za huduma muhimu kuanzia tiba mahospitalini, usafiri barabarani, mahakamani, masuala ya ardhi, polisi na maeneo ya biashara.

“Kwa mfano mtu uko eneo la biashara au uko katika kituo cha polisi umekaa kwa muda mrefu hakuna huduma, ukiuliza unajibiwa vibaya, au upo mahakamani kesi yako inazungushwa kwa muda mrefu mahakimu hawapo. Kuanzia hapo hapo ulipo unaweza kutuma malalamiko yako kwa kuandika neno ‘Kinondoni’ kisha unaacha nafasi, halafu unaandika kero yako kwa kifupi kwenda namba 15404. Ujumbe huo utanifikia moja kwa moja nami nitachukua hatua stahiki,” amesema Makonda.
“Nimewaandaa vijana wangu wasiopungua watano ambao nitafanya nao kazi watakuwa wakipokea ujumbe kutoka kwa wananchi na kuweza kutambua kama ni ukweli au uongo. Tutamtambua mtu huyo aliyetuma ujumbe eneo alipo kwa kutumia kompyuta zilizounganishwa kwenye mitambo maalumu na kisha tutafuatilia”. Amesema Makonda.

Makonda alisema kwamba, mkakati huo utakuwa ni endelevu ambapo wananchi wa Kinondoni watatuma ujumbe kwa masaa 24.  Mkakati huu umepewa jina la “Sukuma twende”.
Kila wiki nitakuwa nakutana nafanya tathmini ili kuangalia ni sekta ipi imelalamikiwa sana. Ikionekana ipo iliyobeba kero nyingi nitawaandikia barua za onyo, au kuagiza watumishi wabadilishwe vitengo kwa kupelekwa hata kijijini, kama sio kuwafukuza,” amesema Makonda.

KIMENUKA..Maduka ya Dawa Karibu na Hospitali zote za Serekali Kuondolewa

$
0
0
SERIKALI imesema ipo katika hatua za mwisho kuanzisha maduka ya dawa katika hospitali zake zisizokuwa nayo na kuweka maduka mapya ya Bohari Kuu ya Dawa (MSD), hatua itakayohakikisha dawa zinapatikana katika hospitali hizo.

Aidha, imesema ili kufanikisha hilo, inafanya mazungumzo na wamiliki binafsi wa maduka ya dawa yaliyo nje ya hospitali zote za serikali ili yahamishwe kuondoa mgongano wa kimaslahi baada ya kubaini maduka mengi ni ya watumishi wa afya.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Dk Donan Mmbando, aliyasema hayo jana, alipozungumza na waandishi wa habari baada ya kufanya ziara katika Hospitali ya Saratani ya Ocean Road na kufafanua zaidi kwa simu alipozungumza na gazeti hili baada ya ziara hiyo.

Dk Mmbando alisema changamoto ya dawa ipo katika maeneo mengi ya nchi, hivyo serikali imeandaa utaratibu wa kuweka maduka ya dawa ya serikali ndani ya hospitali zake ambayo yatasaidia upatikanaji wa dawa kwa wepesi na kwa bei rahisi. “Maduka ya dawa hayapo katika hospitali zote.

Tuliruhusu kuwepo kwa maduka binafsi ili kuongeza ushindani wa dawa, lakini baadhi ya watumishi wasio waaminifu wanawaandikia wagonjwa dawa wanazojua katika duka la hospitali hakuna, na kumwagiza aende duka la nje ambalo ni lake ama la mwenzake.

“Mpango tunaouzungumza hapa ni kuweka maduka katika hospitali za serikali zisizo nayo na pia kuanzisha maduka ya MSD ndani ya hospitali moja kwa moja ili kuhakikisha dawa stahiki zote zinapatikana kwa wakati,” alifafanua Dk Mmbando.

Alisema hatua hiyo itaondoa ucheleweshwaji wa kupata dawa kwa wakati na itaongeza ufanisi. Kadhalika alisema hivi sasa utekelezaji wa mpango huo unaendelea hatua kwa hatua. “Hilo suala limezungumzwa vizuri pia katika bajeti tunayoitekeleza katika mwaka huu wa fedha (2015/2016) na tutaeleza utekelezaji wake mwakani,” alisema Dk Mmbando.

“Wananchi wamekuwa wakilalamika kukosa dawa ndani ya hospitali na kutakiwa kununua katika maduka ya nje, jambo ambalo limeleta sintofahamu kwa wananchi, hivyo kwa sababu maduka yote ya dawa yamesajiliwa kisheria tunataka kuyaondoa kwa maana ya kuyahamisha ili kuondoa huo mgongano,” alibainisha Dk Mmbando.

Katika hatua nyingine, Serikali imezitaka hospitali zake zote nchini kuhakikisha zinatenga bajeti itakayowasaidia kufanya marekebisho ya vifaa tiba pindi vitakapoharibika ili kuondoa usumbufu kwa wagonjwa.

Dk Mmbando alisema hospitali hizo zinapaswa kuweka bajeti ya vifaa tiba itakayowasaidia wao kama hospitali kufanya marekebisho na kuacha kusubiri mpaka serikali itoe fedha za marekebisho ya vifaa hivyo.

“Hospitali hizi tunajua zinapata fedha, hatutegemei kusikia malalamiko ya vifaa kuharibika, lazima wachukue hatua wao wenyewe za kuhakikisha vifaa vinarekebishwa ili kuondoa usumbufu kwa wagonjwa na kuwanyima haki ya msingi ya kupatiwa huduma bora,” alisema Katibu Mkuu huyo.

Alisema amefurahishwa na utoaji huduma katika Hospitali ya Ocean Road licha ya kuwepo kwa changamoto mbalimbali, ikiwemo kukosekana kwa dawa za saratani. “Hospitali inafanya huduma kwa ushirikiano, wafanyakazi wanafanya kazi kama timu, jambo ambalo limenipa nguvu,” alisema na kuaigiza MSD kuhakikisha wanahifadhi dawa za kutosha kwa ajili ya wagonjwa wa saratani ili kusaidia wagonjwa hao kupata huduma bila kuwepo vikwazo.

Pia aliwataka wakurugenzi wa Idara ya Tiba na Famasia waliopo wizarani watunze asilimia ya fedha kwa ajili ya kununua dawa za wagonjwa wa saratani. Dk Mmbando alisema serikali pia imeandaa mwongozo wa huduma za tiba ambao utatumika katika hospitali za umma utakaosaidia kujua gharama za matibabu kwa wananchi.

“Mwongozo huo umekamilika katika rasimu ya kwanza tunasubiri waziri atakayekuja aweze kupitia, kuuzindua na kutangazwa rasmi,” alisema Dk Mmbando. Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Hospitali ya Ocean Road, Diwani Msemo alisema amefurahishwa na ujio wa Katibu Mkuu huyo, kwani amekuwa na maagizo mazuri ambayo yanalenga kusaidia hospitali hiyo.

Pia alisema maagizo ya Katibu kuhusu upatikanaji wa dawa yatawasaidia kwani wamekuwa na changamoto kubwa ya dawa, jambo ambalo linasababisha usumbufu kwa wagonjwa.

Soma Story ya Kusikitisha ya Huyu Dada, Mume Wake Anamlazimisha Kufanya Mapenzi ya Watu Watatu na Amegundua Kuwa ni Shoga Pia

$
0
0

Kutoka Instagram:

MMH DUNIA HII INA MAMBO KWAKWEL.COZZ LEO NIKO KI EMOTION ZAID EMBU NGOJA NI SHARE NA NYIE BAADHI YA STORY NAZO POKEA INBOX...kuna dada nilikuwa naongeaga nae ila kutokana na sababu zangu nisingependa mtaja jina...naomba nikuletee Story yake ya kusikitisha Hapa Chini:
.
Masta hata ukinipost kweny wall yako mungu nishaidi ila tangu nimekujua umekuwa mkarimu sana kwangu ndio maana leo hii nimeamua kukufungukia ili unisaodie tu kimawazo maana kadri siku zinavyo zidi kwenda ndivyo nazid changanyikiwa...

Kama nilivyo kwambia nimeolewa huu mwaka wa 3 mimi na mume wang tumejuana huu unaenda mwaka wa 5,masta ilianza kama utan baada nilipo jifungua mtoto wang wa kwanza alipo fikisha miez 8 skumoja mume wng alinitamkia habar ya ku invite 3 person in our bedroom nilijua utani so tukajibizana na alipoona sikupenda idea akaanza jichekesha na kusema he was joking yakaisha...ila baada ya miez kadhaa aliirudia hii mada tena ila this time alijipanga na kuni Converse sana yan alinipa darasa la uwakika nikajikuta nakubali,masta kesho yake kwel akaja na mdada mashallah mpaka nyumban chumban kwangu kikatokea cha kutokea ila baada ya hapo nilijiona mjinga sana nililia siku nzima but nilikuwa dhaifu cz usiku wake baby akanileta pochi jipya la prada nikaridhika...

Mchezo ulikuwa ni huo kwa takriban kama miez 6 nahis nilijikuta nazoea mpa nilipo jikuta nina mimba, for his respect mwenyewe alinitamkia kuwa we need to stop..ila skumoja rafiki yake alikuja home amelewa na walikuwa wamegombana baada ya kutapeliana na alianza kumcharukia huku akimwita GAY sikutilia maanan cz nilijua ni mikwaruzano tu na pombe masta baada ya kujifungua mtoto wangu wa 2 in 6 month ananitamkia tena huo mchezo this time nilikuwa mkali coz tayari mtoto wang wa 1 alishaanza kuongea na sikutaka kaone huo ujinga pili habari zilikuwa zinasambaa kuwa mimi na mume wang tunahuo mchezo..basi Masta nyumba ikaanza waka moto kila siku kelele iskumoja alinitamkia kuwa either i like it or not ataendelea kufanya coz hiyo ndio furaha yake...

Wakat nimerudi Tanzania kwaajiri ya holiday siku ya kurudi marekan tulichelewa ndege Transit na coz hatukuwa na simu ya mawasiliano mimi na wanangu tulirudi home kwa kumshtukia baada ya kuingia ndani nilimkuta mume wangu akifanya mapenzi na watu wawili mmoja alikuwa mwanamke yule wa mwanzo ambae alimleta first time mwengine mwanaume, that was the most painful thing nimewahi shuudia Masta nilihisi moyo umestop nilianguka chini huku nikiwa nimembabe mtoto wangu mdogo kifuani...nimekuja stuka niko hospital.

Kinacho niuma zaidi dada yangu baada ya kutoka hospital nilikuwa tayari kumsamehe mume wangu kama angeliniomba msamah lakini haikuwa hivyo baada ya Two Montn ananiambia nichague moja NIENDELEE KUWA NA YEYE NA NIKUBALI MATAKWA YAKE YA KUINGIZA WATU NDANI AU TUACHANE...Masta nilikosa jibU na kujikuta natoa machozi aliniambia kuwa ananipa muda nijifikilie lakini sasa masta maneno ya watu kusema kuwa ni gay yalikuwa ya kizidi ila sababu sikuwa na uelewa mzuri wa haya mambo nilikuwa nikibisha coz mume wang alikuwa na uwezo wa kunibebesha mimba...mpaka siku nyingine tena nilimfumania kweny gari lake akiwa na mwanaume mwenzie wakifanya uchafu wao...

Dadangu roho inaniuma na siku nyingi sana nilikuwa natafuta njia ya kutoa hili dukuduku moyon coz sijawah muelezea mtu masta naogopa walimwengu watanicheka coz always huwa wananisema naringa na kujifanya kuwa nina pesa kisa navaa vitu vya gharama...baada ya hilo tukia mume wangu kwa mdomo wake alinitamkia kuwa yeye anai enjoy kufanya mapenz na wanaume pamoja na wanawake at the same time so kama mke anataka nimsapoti...hivi navyo kwambia atanaka divorce kisa nimekataa kukubaliana na yeye na kuhusu watoto he doesnt seems to care masta wanangu bado wadogo na wakiume wameshazoea kila siku daddy daddy daddy coz ana waspoil mume ananambia nikiachana nae hataki kujua anything about me na watoto atakuwa anatuma tu pesa...shida sio pesa masta NISAIDIE NIFANYE NINI NAHISI NAKUWA KICHAA SOON...naogopa kuwaadisia ndugu na rafiki zangu Masta
.
.
MWISHO...DUH EMBU TUMSAIDIE HUYU DADA KIMAWAZO

Kuhusu Emmanuel Nchimbi: Kama Hatakiwi kuwa Spika, kwanini Alipewa Fomu?

$
0
0
Ifike mahali CCM, kama chama chetu na chama tawala, kijitenge na siasa za ulaghai, uongo na maigizo. Hasa kwenye mambo nyeti ya nafasi za kiuongozi. Tangu Emmanuel Nchimbi alipochukua fomu ya kugombea Uspika wa Bunge la 11, amekuwa gumzo kwa viongozi na wanachama wa CCM. Kuanzia Makao Makuu ya CCM hapa Dodoma hadi Ofisi Ndogo za Lumumba Dar es Salaam, Nchimbi anasemwa kama asiyefaa na kibaraka.

Anakandiwa na kusingiziwa kuwa bado ni mfuasi wa Lowassa pamoja na kushiriki kampeni za Rais Magufuli. Nchimbi anafanyiwa na kusemewa vitimbi. Yote haya ni kuonesha kuwa Emmanuel Nchimbi hatakiwi kuwa Spika. Kwanini alipewa fomu ya kugombea? Hivi bado CCM yetu inategemea 'vijihela' vinavyotokana na kutoa fomu za kugombea nafasi mbalimbali kupitia chama?

CCM ikumbuke kuwa Dr. Kalokola, yule aliyedai milioni moja yake ya fomu ya Urais, amechukua tena fomu ya Uspika. Huyu aweza kuungana na watu aina ya akina Nchimbi kudai hela yao ya fomu za Uspika. Itakuwa aibu kwa CCM zaidi kuliko kwa wagombea husika. Chama kitaonekana ni cha kitapeli,kilaghai na kimaigizo. Waliochukua fomu za Uspika waachwe wapambane kichama na mmoja wao awe mgombea wetu wa Uspika. Majungu hayajengi chama!

By Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Dodoma)

Muda Wowote Kuanzia Sasa Dk Magufuli Kuteua Wabunge........

$
0
0
Rais John Magufuli anatarajiwa, wakati wowote kuanzia sasa, kuwateua baadhi ya watu wenye sifa kuwa wabunge ili aweze kuwapa majukumu ya kuongoza wizara atakapopanga safu ya Baraza la Mawaziri, hivi karibuni.

Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 inampa Rais mamlaka ya kuteua wabunge wasiozidi 10 kutoka miongoni mwa wananchi ambao anaona wanaweza kumsaidia katika utekelezaji wa majukumu yake katika baadhi ya maeneo kama vile afya, elimu, kilimo, nishati na sheria.

Ibara ya 66 (1) inasema, bila ya kuathiri masharti mengine ya ibara hii, kutakuwa na aina zifuatazo za wabunge, yaani (e) wabunge wasiozidi 10 walioteuliwa na Rais kutoka miongoni mwa watu wenye sifa kwa mujibu wa ibara ya 67, isipokuwa sifa iliyotajwa katika ibara ya 67(1) (b).

Baraza hilo jipya linatarajiwa kuwa na sura nyingi mpya ambazo zitaendana na kasi yake kutekeleza kaulimbiu ya “Hapa Kazi Tu.” Pia, baraza litakuwa na sura mpya kutokana na ukweli kwamba baadhi ya mawaziri waliangushwa kwenye kura za maoni, wengine wakati wa Uchaguzi Mkuu na wengine, japokuwa wamerejea bungeni ni walionekana kuwa mzigo awamu iliyopita.

Kati ya mawaziri 55 waliokuwamo katika Baraza lililopita, waliorejea katika Bunge la 11 ni 23 tu wakiwamo 20 wa majimbo na watatu wa viti maalumu. Kupungua kwa idadi hiyo kutampa Dk Magufuli fursa ya kusuka baraza hilo kutoka miongoni mwa wabunge 188 wa majimbo, 64 wa viti maalumu na 10 atakaowateua ili wamsaidie.

Haijulikani baraza litakuwa na mawaziri wangapi ila wakati wa kampeni amewahi kukaririwa akisema litakuwa dogo ikilinganishwa na lililopita.

Katika muhula wa pili wa utawala wake, Rais Kikwete aliwateua wabunge 10, kati yao sita aliwapa wizara za kuongoza, utaratibu ambao huenda Dk Magufuli akautumia ili kupata mawaziri kulingana na mahitaji ya Serikali atakayoiunda.

Kwanza Rais Kikwete alimteua Profesa Makame Mbarawa na akamfanya Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia; na Shamsi Vuai Nahodha ambaye alipewa Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa. Pia, alimteua Zakhia Meghji lakini hakumpa wizara, na Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi, James Mbatia (sasa mbunge mteule wa Vunjo).

Baada ya kufanya mabadiliko ya Baraza la Mawaziri mwaka 2012, Rais Kikwete aliwateua Profesa Sospeter Muhongo (sasa mbunge mteule wa Butiama) akampa Wizara ya Nishati na Madini; Janet Mbene na Saada Salum Mkuya akawafanya manaibu waziri katika Wizara ya Fedha. Janet ambaye baadaye aliteuliwa kuwa Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara ameshinda ubunge katika Jimbo la Ileje na Mkuya anasubiri hatima yake katika Jimbo la Kijitoupele, Zanzibar. Aidha, alimteua Dk Asha-Rose Migiro kuwa Waziri wa Katiba na Sheria na hivi karibuni alikamilisha orodha kwa kuwateua Dk Grace Puja na Innocent Sebba.

Baraza la Mawaziri litajulikana baada ya wabunge kula kiapo wiki ijayo mbele ya Spika wa Bunge ambaye anatarajiwa pia kuchaguliwa wiki ijayo.


Kisa Siasa, JACK WOLPER Atelekeza Tasnia ya Filamu, Aamua Kujiimarisha Kwenye Ulimwengu wa Siasa

$
0
0
UPO? Habari ikufikie kuwa ‘mtoto mtamu’ anayesumbua katika tasnia ya filamu Bongo, Jacqueline Wolper Massawe ameweka pembeni masuala ya uigizaji kwa muda usiojulikana kwa kile alichodai ni kujipa muda wa kupumzika na kujikita zaidi kwenye mambo ya siasa.

Rafiki wa karibu na Wolper aliyeomba hifadhi ya jina lake mwanzoni mwa wiki hii, aliliambia gazeti hili kuwa Wolper kwa sasa amekolea sana kwenye mambo ya siasa na kuona kama amekuwa akipoteza muda mwingi kwenye mambo ya uigizaji.

Baada ya kupata ‘ubuyu’ huo, mwandishi wetu alimtafuta Wolper ambaye alikiri kuamua kupumzika kidogo mambo ya uigizaji huku akishindwa kuweka wazi atajikita kwenye nafasi gani ndani ya ulingo wa kisiasa.

Aah, kila mtu ana mipango na malengo yake, ni kweli kwa sasa nina mambo mengi ya kufanya kupitia siasa, nimejifunza vitu vingi mno vya msingi na muhimu, nimeweka kando kwa muda uigizaji, muda ukifika wa kuendelea na fani hiyo, nitasema,” alisema Wolper.

Source:Globalpublishers

Ommy Dimpoz Atoa Sababu za Wasanii wa Tanzania Kutumia Models wa nje Kwenye Video Zao

$
0
0
Ommy Dimpoz ni kati ya wasanii wa Bongo ambao wameshoot video zao kadhaa nje ya Tanzania kwa kutumia waongozaji pamoja na video models wa nje.

Wengi wanaamini upo uwezekano wa wasanii kuamua kusafiri na models kutoka nyumbani kama ambavyo husafiri na dancers wao kwenda kushoot video nje, lakini Ommy Dimpoz ana sababu za kwanini hushindwa kufanya hivyo.

Mara nyingi models wa nje wako proffesional wanaweza kucheza character zote ambazo wamepangiwa,” alisema Ommy Dimpoz kupitia Planet Bongo ya East Africa Radio.

“huku unajua kidogo kuna scene ambazo mtu anatakiwa acheze lets say amevaa swimming costume, unajua huku kumpata msichana ambaye anaamua kujiachia hivyo ni wachache sana, hata kama ikitokea mnaweza mkajikuta msichana huyo huyo atatumika kwenye video za watu wote”. Alisema Ommy.

Ommy pia ameongeza sababu nyingine kuwa ni kupunguza gharama ya kusafiri na watu wengi zaidi.

Kikubwa ni kupunguza gharama, huko wako kibao utawakuta wengi sana, kwa hiyo ndo mana nasema hiyo nayo inachangia, pia ni vigumu kuondoka na watu wote kwenda nao kushoot nao nje, kwa sababu kule unawapata kwa bei rahisi alafu ukilipia video ina maana unalipia kila kitu”,

Siku chache zilizopita mwigizaji wa filamu za Bongo Jacqueline Wolper alihoji kupitia Instagram, kwanini wasanii wetu wanatumia zaidi models wa nje kwenye video zao (Ingia hapa)? Sina shaka Ommy Dimpoz amejibu swali la Wolper.

Kasi ya Dk John Magufuli Kupambana na Watu Sasiowajibika Kwenye Ofisi za Umma Yatikisa Kila Kona

$
0
0
Kasi aliyoanza nayo Rais John Magufuli ya kupambana na watu wasiowajibika kwenye ofisi za umma, imeanza kutikisa sehemu nyingi baada ya taasisi tofauti kutoa maagizo ya kuongeza ufanisi, huku nyingine zikieleza ni kwa jinsi gani zimeitikia wito huo.

Wakati Wizara ya Afya na baadhi ya taasisi zake zikitoa maelezo ya kushughulikia vifaa vya tiba vilivyokuwa vibovu kwa muda mrefu, Wizara ya Madini imeeleza ni jinsi ilivyochukua hatua za kuongeza uwajibikaji, huku Wizara ya Habari ikihimiza utendaji na Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni akifungua kituo cha kusikiliza kero za wananchi.

Rais Magufuli alikuwa akihimiza wakati wote wa kampeni yake kuwa wavivu na wazembe waanze kukusanya virago na baada ya kuapishwa, alitembelea Wizara ya Fedha, Hospitali ya Taifa ya Muhimbili na kufanya kikao na makatibu wote wa wizara kutoa mwelekeo wa “Serikali ya Magufuli”, ikiwa ni pamoja na kusitisha safari za nje na kukusanya kodi bila ya upendeleo. Pia, aliiondoa Bodi ya Muhimbili pamoja na kaimu mkurugenzi na kuteua mpya, uamuzi ambao unaonekana kuzua taharuki kwenye taasisi za umma.

Jana, Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Dk Donan Mmbando aliwataka viongozi wote wa hospitali nchini kutoka maofisini na kusikiliza shida za wagonjwa na kuwaeleza huduma zinazotolewa kwenye vituo vyao vya afya na kwamba wazembe watachukuliwa hatua.

Dk Mmbando aliwaambia wanahabari jana baada ya kutembelea Taasisi ya Saratani ya Ocean Road (ORCI), kuwa mpango huo wa kutoa huduma bora wataufanya kwa kushirikiana na Tamisemi.

Katika kuanza kutekeleza mabadiliko hayo, Dk Mmbando aliagiza Bohari Kuu ya Dawa (MSD) kutenga kiwango maalumu cha dawa kwa ajili ya kutibu wagonjwa wa saratani wa ORCI na kuhakikisha hospitali hiyo haikosi dawa.

“Ni mwisho kuanzia sasa kusikia mgonjwa wa saratani anasumbuliwa kwenda kununua nje wakati tunaweza kuweka utaratibu mzuri na dawa zikapatikana ndani ya hospitali,” alisema.

Alitoa agizo hilo baada ya kuelezwa na wagonjwa pamoja na menejimenti kuwa taasisi hiyo haina dawa na wagonjwa kununua kwenye maduka binafsi.

Mmoja ya wagonjwa waliolazwa ORCI, Felix Kessy alisema kwa sasa huduma zinaendelea vizuri hospitalini hapo, lakini ukosefu wa dawa unawalazimisha kwenda kununua mitaani ambako baadhi huuzwa kati ya Sh18,000 na Sh28,000.

Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa ORCI, Dk Diwani Msemo alisema ukosefu wa dawa ni changamoto kubwa kwa kuwa hospitali hiyo inatoa matibabu bure hivyo ni vigumu kukabiliana na uhaba huo.

Alisema katika bajeti ya mwaka wa fedha wa jana 2014/15, Serikali ilipanga kuwapatia Sh6 bilioni kununua dawa, lakini wamepokea Sh2 bilioni tu.

Katika kukabiliana na tatizo la kifedha, Dk Mmbando aliagiza hospitali zote nchini kutumia sera ya ubia baina ya Serikali na Sekta Binafsi (PPP) katika kutekeleza miradi ambayo itasaidia kutatua matatizo.

“Kusiwe na sababu ya kumiliki kifaa tiba kama Serikali. Kuwe na makubiliano ya namna fulani ili mtengenezaji wa kifaa husika awe ndiyo mhudumiaji ila kitakuwa kikifanya kazi saa 24,” alisema.

Mwenendo wa CT-Scan ya Muhimbili

Kuhusu mashine ya kuchukua vipimo ya CT-Scan iliyoko Muhimbili, alisema tatizo hilo litatatuliwa na mafundi waliopo Uholanzi na kwamba ndani ya siku mbili itaanza kufanya kazi.

Ili kuzuia hali iliyojitokeza Muhimbili ya kuharibika vifaa, Dk Mmbando aliagiza hospitali zote ziwe na mpango kinga wa kutengeneza mitambo yao na zipange bajeti maalumu za matengenezo kwa kuwa wanakusanya mapato.

Alisema wameshailipa kampuni ya Philips Sh3 bilioni kati ya Sh7 bilioni wanazodaiwa kwa ajili ya matengenezo ya mashine hizo nchi nzima na kwamba wanaamini kwa sasa wataendelea kuhudumiwa bila kikwazo chochote.

Muhimbili yaingia hasara

Wakati hayo yakiendelea, Hospitali ya Muhimbili imeshindwa kukusanya zaidi ya Sh225 milioni katika muda wa siku 75 ambazo mashine za uchunguzi wa magonjwa za CT Scan na MRI zilikuwa mbovu kuanzia Agosti.

Ubovu wa mashine hizo umezuia huduma kwa zaidi ya wagonjwa 50 kwa siku ambao hufanyiwa uchunguzi hospitalini hapo na hivyo kufanya idadi ya wagonjwa waliokosa huduma hiyo kufikia 3,750.

Akizungumza na vyombo vya habari hospitalini hapo jana, Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Muhimbili, Aminiel Aligaesha alisema vipimo vya CT Scan vilikuwa vinatoa huduma kwa wagonjwa 40 hadi 60 kwa siku na hutakiwa kulipia Sh50,000.

Alisema MRI ilikuwa ikitoa huduma kwa wagonjwa 10 hadi 15 kwa siku kwa gharama ya Sh100,000 kila mmoja anayetumia kadi za bima za afya, wakati wanaolipia hutozwa Sh150,000.

Mashine hizo zilitakiwa kufanyiwa matengenezo na kampuni ya Philips lakini hayakufanyika kutokana na deni.

Wakati huohuo, mfanyabiashara wa Dar es Salaam, Mohamed Razak Dewji ametoa msaada wa vitanda 30 na magodoro 30 kwa hospitali hiyo ili kusaidia kupunguza adha ya wagonjwa kukosa vitanda.

Profesa Ole Gabriel na ‘Hapa Kazi Tu’

Kwingineko, Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Profesa Elisante Ole Gabriel jana alitembelea mitambo ya kurushia matangazo ya Shirika la Utangazaji Tanzania(TBC) iliyoko Kisarawe mkoani Pwani kwa lengo la kufahamiana na wafanyakazi na akawahimiza kufanya kazi kwa bidii

Profesa Elisante alitembelea taasisi tatu zilizo chini ya wizara hiyo ambazo ni Baraza la Sanaa la Taifa (Basata), Shirika la Magazeti la Serikali (TSN) na Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) ikiwa ni kutimiza kaulimbiu ya “Hapa Kazi Tu”.

Jana, Mwananchi ilishuhudia pilikapilika kwenye baadhi ya ofisi za umma, ikiwamo Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii pamoja na Nishati na Madini.

Msemaji wa Wizara ya Nishati na Madini, Badra Masoud alisema watumishi wa wizara hiyo wapo tayari kufanyiwa ziara ya kushtukizwa kwa kuwa wanafanya kazi muda wote wa kazi.

“Hata Rais akija sasa hivi atakutana na ‘Hapa Kazi Tu’ wakati wa kazi. Kinachoendelea hapa wizarani ni uchapaji wa kazi. Kila mtu anatekeleza wajibu wake kwa vitendo,” alisema.

Katika kuonyesha hayo yanatendeka taasisi zilizo chini ya wizara hiyo zimeagizwa kutochelewa kushughulikia maombi ya wawekezaji wanapoonyesha dhamira ya kuwekeza nchini.

Agizo hilo amelitoa wakati wa kikao chake na watendaji wa Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (Ewura) pamoja na mwenyekiti wa bodi ya taasisi hiyo.

Makonda, Natty wakoleza moto

Kasi hiyo ya Dk Magufuli haijatikisa wafanyakazi pekee.

Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Paul Makonda na mkurugenzi wa manispaa hiyo, Mhandisi Mussa Natty jana walitoa maelekezo ya utendaji kazi na ufuatiliaji wa matatizo ya wananchi kwenye eneo lao.

Makonda, ambaye mara baada ya kuteuliwa alitenga muda kwa kusikiliza matatizo ya ardhi wilayani kwake kila Ijumaa, jana alizindua namba ya simu itakayotumika kusikiliza kero za wananchi na kuzitatua.

Wakazi wa Kinondoni na wengine wanaotaka huduma wilayani humo, watatakiwa kutuma ujumbe mfupi wa maneno kwenye namba hiyo na kueleza tatizo walilonalo na itapokewa na wafanyakazi maalumu watakaokuwa na kazi ya kuushughulikia.

“Tunatazamia kupunguza vitendo vya rushwa sambamba na kuongeza ufanisi kwa watumishi. Zamani kulikuwa na masanduku ya maoni, lakini hivi sasa hayapo tena. Kwa kutumia namba 15404 wananchi watawasilisha malalamiko yao sehemu salama,” alisema Makonda.

Alisema wapokeaji ujumbe huo watawasiliana na wakuu wa idara husika ili washughulikie kero hizo.

Wakati Makonda akizindua huduma hiyo, Natty, ambaye alikuwa mgeni rasmi katika hafla ya kupokea msaada wa dawa za kipindupindu na vifaa tiba vilivyotolewa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF), alitumia dakika zisizozidi sita kwenye shughuli hiyo akitaka watu kurejea kazini.

“Kila mtu anajua kuwa sasa tupo katika kipindi gani. Hapa ni kazi tu. Hatupaswi kupoteza muda katika vikao,” alisema. “Amri si ya kuzuia kusafiri nje pekee, bali kukaa mikutano isiyo na tija pia haitakiwi. Hivyo tunapaswa kulimaliza hili na kuendelea na shughuli zetu za utendaji wa kazi kama kawaida.”

Baada ya kusema hayo, Natty aliutaka ujumbe wa taasisi hiyo kumkabidhi msaada huo jambo lilofanywa kwa haraka na Mkurugenzi wa Fedha, Mipango na Uwekezaji, Deusdedit Rutaza aliyesema msaada huo wenye thamani ya Sh5 milioni unahusisha dawa za ugonjwa wa kipindupindu, glovu na dawa kuzuia mazalia ya wadudu katika mitaro ya maji machafu.

“Shughuli imeisha,” alisema. “Kila mfanyakazi arudi ofisini kwake mara moja. Nitakuja kukagua kama kila mtu anafanya majukumu yake. Muda wa kuzungukazunguka haupo tena.”

Wafanyakazi wazungumza

Dereva wa Wizara ya Nishati na Madini, Derick Samson alisema wafanyakazi wengi wanafika ofisini mapema kufanya shughuli zao, jambo ambalo ni tofauti na hali ilivyokuwa awali. Alisema wafanyakazi walikuwa wanafika ofisini muda wowote bila kuulizwa.

Mhudumu wa mapokezi wa Hazina, Beatrice Mvungi alisema wapo wanaolalamikia mabadiliko hayo.



     

SIKILIZA na Download Wimbo Mpya Toka Kwa Mkali Bayo the Great-Kitimtim

$
0
0
Kitimtim ni wimbo wa kuchezeka wenye mahadhi ya mduara uliochagizwa na vionjo vya ragga/dancehall kutoka kwa rapper na mwimbaji wa dancehall @bayothegreat.

Unaweza kudownload Kitimtim hapa Chini:

Hii ni ngoma ya pili ya Bayo kwa mwaka huu wa 2015. Ngoma kabla ya hii inaitwa "Nielewe" yenye mahadhi ya sweet reggae. Unaweza kutizama nielewe hapa:

https://www.youtube.com/watch?v=6QB_OVby0D0

Wimbo wa kwanza kutoa Bayo kama solo artist unaitwa Jina Kapuni akiwashirikisha Watu Pori pamoja na Hussein Machozi. Bayo kwa sasa ni mfanyakazi wa shirika la VSO visiwani Zanzibar.

No Stopping! Agness Masogange Still Displaying Her Meat to Tanzanian Men (PICS)

Msemaji wa TANAPA Akanusha Kuhusu Picha Zilizogaa Kwenye Mitandao ya China Zikionyesha Simba Wamevamia Gari la Watalii na Kutoboa Matairi

$
0
0
Baada ya habari kusambaa kwenye mitandao mbali mbali ya Kijamiii zikionyesha Simba Wamevamia Gari la Watalii....



Msemaji wa TANAPA ndugu Shelutete ametoa statement kukanusha kuwa picha ile si ya Serengeti na wala gari zile si za Tanzania.

Hivyo tukio lile halikutokea TANZANIA na wala si SERENGETI NATIONAL PARK.Kama lilivyokuwa limewekwa humu leo ktk link hii

Mbuga ya wanyama ya Serengeti yang'ara kwenye mitandao ya kijamii (CHINA)

Taarifa ya TANAPA kwa mujibu wa Msemaji wake ni hii;

This information is not true. Iam the official Spokesperson for Tanzania National Parks (TANAPA), the custodian of Serengeti National Park and below is the copy of the statement: TANZANIA NATIONAL PARKS OFFICE OF THE DIRECTOR GENERAL P.O.BOX 3134, ARUSHA PRESS RELEASE SERENGETI NATIONAL PARK SAFE FOR TOURISTS On 10th November, 2015, the UK based blog Mail online came out with a story titled ?Meals from wheels: Terrified tourists watch as lion eats their vehicle?s tire during Safari in South Africa.?

The story further pointed out that the pictures of the tourists whose vehicle was attacked by lions were taken in Serengeti National Park in Tanzania. The news is now circulating very fast in various social media globally.

Tanzania National Parks would like to categorically state that the incident did not happen in Serengeti National Park as reported.

The registration number of the vehicle seems to be of South Africa and we do not have it on our records.

Tourists visiting Serengeti National Park must be aware that the place is safe for them and we have a good number of park wardens to take care of their security while in the park.
Issued by Corporate Communications Department Tanzania National Parks12th November


Viewing all 104776 articles
Browse latest View live




Latest Images