Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104776 articles
Browse latest View live

MSIMAMO WA ZITTO KUHUSU KATIBA MPYA HUU HAPA

$
0
0
Katiba ni mwafaka wa kitaifa. Kitendo cha CCM kuweka msimamo wa Serikali mbili kwenye muundo wa Muungano kinaua kabisa maana ya kuwepo na mjadala. 'Caucus' za vyama kwenye kazi nyeti kama ya kuandika katiba ya nchi iwe marufuku. Kuna kundi lina lengo la kuzuia katiba Mpya kupatikana. Kwa vyovyote vile lazima tuwashinde wapinga mabadiliko hawa kwa kuunganisha nguvu za wananchi. Tusirudi nyuma
"Forward ever, Backward never" - Nkrumah

MAAJABU:ANGALIA SEHEMU YA PUA KATIKA PICHA HII KWA SEKUNDE 15 ALAFU ANGALIA PEMBENI UNIAMBIE UMEONA NINI

$
0
0
Embe na wewe Angalia Sehemu ya pua ya hiyo picha hapo juu alafu angalia pembeni mwa hiyo picha hapo kwenye weupe uniambie umeona nini?

NIMEFANYA MAPENZI NA SHEMEJI YANGU KWA BAHATI MBAYA..PLEASE HELP

$
0
0
Naombeni ushauri wa hali na mali katika hili , Siku kadhaa zilizopita hapa nyumbani kwetu tulifanya sherehe ya birthday ya mtoto wetu kutimiza miaka mitano tuliwaalika ndugu wengi hapa home kwa ajili ya sherehe hiyo, Mgeni mmoja wapo ni mdogo wa mume wangu ambae alikuwa ametoka mkoani so alifikia kwetu, sasa siku ya birthday katika sherehe hiyo tulikunywa sana kila mtu akawa safi mume wangu pombe zilimzidi ilipofika saa sita usiku akaniaga anaenda kulala, mimi nikabaki na baadhi ya ndugu tunakunywa, ilipofika saa saba nami nikajikokota kwenda kulala, nikaingia chumbani nikajitupa kitandani bila kuwasha taa mme wangu alinipokea kwa mahaba tukabinjuka, baada ya kumaliza kiu kikanisha nikaamka niende kunywa maji ile kuwasha taa nikakuta kumbe nilikosea chumba na niliye fanya nae mapenzi ni mdogo wa mume wangu nae alizania nimemtunuku mambo basi hakufanya ajizi akanipa dozi ya uhakika...Hichi kitu kinanisumbua akilini sana mpaka naona sina raha je nimweleze mume wangu kilichotokea ili nipate amani ama nitaharibu zaidi?

KAULI YA MWANASHERIA KUHUSU SAKATA LA OKWI KUICHEZEA YANGA

$
0
0
Mwanasheria WA TFF, Allex Mgongolwa amesema kuwa mshambuliaji Emmanuel Okwi yupo huru kucheza Yanga na wala Sakata lake lisipotoshwe. Mgongolwa alisema watu wamekuwa wakipotosha kuhusu Sakata la mchezaji huyo "Hicho kipengele wanachosema kama amecheza klabu mbili kwenye mashindano husika haruhusiwi kucheza klabu ya tatu, kipengele hicho kingepata nguvu kama kungekuwa na zuio la muda, lakni hakuna zuio lolote, ndio maana Fifa wakamruhusu" source Mwananchi

TANZANIA TUNAHITAJI RAIS MWENYE U DIKTETA KAMA KAGAME AJE KUBADILISHA MINDSET TUPATE MAENDELEO

$
0
0
Pamoja na propaganda niite za kitoto zinazoendeshwa na viongozi wa Tanzania pamoja na Baadhi ya watanzania dhidi ya Rais Paul kagame wa Rwanda kwa mtizamo wangu anaendelea kuwa Rais Bora barani Africa.

Ni rais pekee africa anaye weka mbele maslahi ya nchi yake kuliko kitu chochote. Kutokana na hiyo nia ya dhati amefanikiwa kwa kiasi fulani kupunguza saratani ya ukabila ndani ya Rwanda ndani ya miaka 20 tu. Si katika kuondoa ukabila tuu bali amefanikiwa kuboresha elimu na utoaji wa huduma za jamii hasa afya kwa kiwango kikubwa sana ukilinganisha na nchi yeyote ya Africa. Kwa aliyebahatika kwenda Rwanda kabla ya Kagame atakubaliana na mimi jinsi rais kagame alivyo fanikiwa kwenye miundo mbinu, barabara , njia za mawasiliano etc.

Kuna wanao sema mafanikio hayo yameletwa na pesa zinazopatikana kutokana na uporaji wa madini Congo, Je ni nchi gani yenye kiongozi mwenye akili na commited kuleta maendeleo nchini kwake na wananchi wake haipori utajiri toka nchi nyingine?? Kwani marekani ilienda Iraq kuwasaidia wa Iraq?? ama waingereza na wafaransa walienda afganstan kuwasaidia wale waarabu???Mnajua wanawake na watoto wangapi wanakufa majeshi ya marekani yanapokuwa yanaenda kutafuta resources kwenye nchi nyingine??? Kwani hii mikataba mibovu tunayo lalamikia kila siku ya madini na makampuni , serikari za nchi yanako toka makampuni haya hawajui tunaibiwa?? Ama mnadhani Obama alikuja Tanzania kwa sababu anatupenda sana Wa Tanzania?? Rais mwenye akili anaye wapenda wananchi wake na nchi yake will do whatever it takes to bring about prosperity to his/her country. Eti Tanzania tunaenda kupigana Congo kwaajili ya kuwasaidia...Nchi za kusini mwa jangwa la sahara hususan South africa, Msumbiji etc tulizo zisaidia kupata uhuru wa kweli zinatusaidia nini leo hii zaidi ya kutushukuru tuu???


Tanzania inahitaji Rais mwenye u dikteta kama kagame aje kubadilisha mindset za watanzania kama tunataka maendeleo ya kweli vinginevyo hizi ngonjera tunazoimba kila siku hazita tupeleka kokote...Mtu yeyote anaye jaribu kuvuruga kilichojengwa anawekwa za kichwa kama yule generali aliyeuwawa hivi majuzi...Kiongozi yeyote mwenye vision anafanya hivyo kwa mvuruga nchi yeyote....Bongo kituko wanauwawa watu ki majungu majungu..mwangosi etl

WATANZANIA MAJUNGU NA WIVU WA KIKE HAUTA TUFIKISHA POPOTE
Source:Jamii Forums

INSTAGRAM KIMENUKA KWA MASOGANGE NA WOLPER WAPEWA MAKAVU LIVE

$
0
0
Mtandao wa Instagram umekuwa ndio uwanja wa kuchambana hasa kwa hawa mastaa embu jionee huyo alivyowapa live live Agness Masogange na Jackline Wolper 




LINEX "ISSUE YA MIMI KUTOKA NA AGNESS MASOGANGE IMENISABABISHIA MATATIZO NA FAMILIA YANGU"

$
0
0
Msanii kutoka Kigoma na memba wa kampuni ya Leka Dutigite Linex Sunday Mjeda ameendelea kutoa kilio chake juu ya uzushi ulioenezwa siku kadhaa zilizopita baada ya kupost picha mbalimbali akiwa na video vixen maarufu wa hapa bongo Agnes Gerald aka Masogange.

Baada ya picha hizo kusambaa Linex alikana habari zilizoandikwa na baadhi ya blogs kuwa ana uhusiano wa kimapenzi na mrembo huyo.
“ni kweli watu wa blog mnapush sana kazi zetu but nimesikitishwa na habari hii iliyoandikwa na blog kadhaa mtasababisha tutashindwa ata kukaa na Dada zetu au marafiki zetu Uliza b4 Hujaandika ujinga am single na sina haraka ya kua na mpenzi.” Aliandika Linex kwenye akaunti yake ya facebook.



Kupitia Facebook jana mwimbaji huyo wa ‘Kimugina’ ameendelea kulalamika juu ya matokeo ya habari hizo za uzushi:
“Daaah Uzushi ulioenezwa na baadhi ya blog miyeyusho umesababisha Umenitofautisha na familia yangu ndugu jamaa na marafiki wish kama Mungu awafunue ndugu jamaa marafiki washabiki wangu waujue ukweli bado naendelea kupokea cm nyingi za maswali japo nilishaongea b4 kwamba sina mahusiano na Masogange daaaaah.”  

Credits:Bongo5

TOP C ADAI KUPOKEA VITISHO KUTOKA KWA CANDY RECORDS, APIGWA MKWALA ASIKANYAGE KENYA

$
0
0
Muimbaji wa Lofa, Top C amesema tangu atangaze kutaka kujiondoa kwenye label ya Candy n Candy ya Kenya, ameanza kupokea vitisho kutoka kwa wasanii waliosalia wanaomchimba mkwara asikanyage tena nchi Kenya.

 Top C alikuwa akiongea na mtangazaji wa kipindi cha Street Bamiza cha Nuru FM ya mjini Iringa, Nelly Calocy Msamila aka Nelly B.

“Kuna dogo mwingine wa pale pale anaitwa Imrani ambaye yeye yupo karibu sana na bosi ndo alikuwa akielezaeleza sijui ‘utaona usikanyage show za Kenya’ mimi nikamwambia ‘mimi nilikuja Kenya ndo nikapatana na hii kampuni,” amesema Top C.

Amesema kampuni hiyo inamtaka arudishe gharama ilizotumia kwake lakini anadai hakuna gharama kubwa iliyotumika kwaajili yake na kuongeza kuwa kwa sasa hana mpango tena wa kuwa chini ya usimamizi wa kampuni nyingine.

“Sasa hivi ntafanya kila kitu kimpango wangu, wanazingua hawa washkaji ila kuhusu mambo hayo ntakuwa macho sana sasa hivi. Yaani tunaingia sehemu tu unakuta mtu anakuchekea pale mnapoanza kuonana na tayari ukishaingia kunakuwa issue tena.”

Top C amesema kwenye kampuni hiyo anayepewa kipaumbele peke yake ni Baby Madaha ambaye ana uhusiano na boss wa kampuni hiyo.

Credits:Bongo5

MUME NA MKE WAZUA BALAA BUNGE LA KATIBA

$
0
0
Chama cha National League for Democracy (NLD) Zanzibar kimemtaka, Rais Jakaya Kikwete kufuta uteuzi wa wajumbe wa Bunge Maalumu la Katiba kupitia chama hicho kwa madai kuwa walioteuliwa katika chama hicho ni mtu na mkewe na kufanya uteuzi huo kukosa sura ya Muungano.

Tamko hilo limetolewa na Naibu Katibu Mkuu wa NLD - Zanzibar, Khamis Haji Mussa katika taarifa aliyoisambaza kwa vyombo vya habari mjini hapa juzi, kuwa Mwenyekiti wa chama hicho, Dk Emmanuel Makaidi amewasilisha majina mawili, la kwake na la mkewe, Modesta Ponera kwa ajili ya uteuzi.

Alisema NLD - Zanzibar kilianza kufuatilia taratibu za uwasilishaji wa barua tangu Desemba 27, mwaka jana kwa kumwandikia barua Katibu Mkuu Kiongozi wa SMZ baada ya kupokea maelekezo ya Ikulu ya Tanzania kwamba majina ya Zanzibar yatafanyiwa kazi visiwani na ya Bara yangepelekwa Ikulu Dar es Salaam.

Alisema kwa mujibu wa utaratibu huo, vyama vyote vyenye usajili wa kudumu vilitakiwa kila kimoja kutoa mtu mmoja kutoka Tanzania Bara na mwingine Zanzibar ili kuwa na sura ya kitaifa, lakini Dk Makaidi alikiuka utaratibu huo.

Makaidi ajitetea

Akizungumzia tuhuma hizo, Dk Makaidi alikiri kuwa Ponela ni mke wake, lakini akasema ni mwanachama wa NLD, hivyo ana haki ya kuteuliwa.

Alisema alipeleka majina manne Ikulu na kwamba upande wa Zanzibar ulitakiwa kufanya hivyo kupitia Ikulu ya Zanzibar... “Walifanya uzembe, hawakupeleka majina ya wanachama wa NLD, matokeo yake nikapeleka majina manne, tukapata uwakilishi.”

 Alisema mkewe ni mwanachama wa NLD hivyo ana haki ya kuchagua na kuchaguliwa katika nafasi yoyote kulingana na sifa zake... “Wanalalamika nini hata chama tawala cha CCM, Rais Jakaya Kikwete ni Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa (Nec) na Mkewe Salma pia ni mjumbe wa Nec.”

Alisema Ponela kuwa mkewe hakumfanyi akose haki zake za msingi na kwamba sifa zake na elimu ndivyo vilivyomfanya Rais amteue.

Kaimu Katibu Mkuu Kiongozi, Florens Turuka alipoulizwa alisema Ikulu haina taarifa za suala hilo lakini wanaamini vyama vya siasa vilikaa na kupendekeza majina manne na kuyawasilisha Ikulu, ndipo Rais alipoteua wajumbe mawili kati yake.


WATOTO WALIO ZALIWA WAMEUNGANA WAREJEA DAR BAADA YA KUTENGENISHWA

$
0
0
Watoto pacha, Elikana na Eliud waliokuwa wameungana wamerejea nchini jana wakitokea India walipokuwa kwa ajili ya kutenganishwa, tayari kwa kusherehekea kumbukumbu yao ya kutimiza mwaka mmoja leo.

Waliwasili katika Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere saa 10:30 kwa ndege ya Shirika la Ndege la Oman, wakiwa na mama yao, Grace Joel (20) ambaye muda wote alionekana mwenye furaha.

Elikana na Eliud walizaliwa Februari 20, mwaka jana wilayani Kyela, Mbeya wakiwa wameungana na baadaye kuhamishiwa katika Hospitali ya Mkoa wa Mbeya ambako walipata rufaa ya kwenda Hospitali ya Taifa Muhimbili.

Juni mwaka jana, Serikali iliwapeleka Hospitali ya Chennai, India ambako Desemba 16, mwaka jana walifanyiwa upasuaji mkubwa wa kuwatenganisha.

Akizungumza baada ya kutua jana, Grace alisema: “Nina furaha ya ajabu, sijui nimshukuru vipi huyu Mungu wangu, ni mkuu mno. Ninawashukuru sana madaktari wa India, ninawashukuru madaktari wa Muhimbili na sana naishukuru Serikali yangu kwa kunipa msaada huu mkubwa. Siamini kama leo ningekuwa narudi salama na watoto wangu kila mmoja akijitegemea,” alisema Grace.

“Kesho (leo) ni birthday yao, wanatimiza mwaka mmoja, ni furaha ya ajabu niliyo nayo, siwezi kuelezea. Siku nilipoambiwa watoto wangu watafanyiwa upasuaji mkubwa na watapumulia mashine kwa wiki moja, nilichanganyikiwa kwa kweli, sikutamani tena hata hiyo operesheni ifanyike ila sikuwa na jinsi zaidi ya kumwomba Mungu.”

Akizungumza uwanjani hapo, Dk Glory Joseph kutoka Hospitali ya Rufaa Bugando ambaye aliongozana na watoto hao kurudi nchini alisema: “Watoto wamerejea salama na wanaendelea vizuri ila watakuwa Moi (Hospitali ya Mifupa Muhimbili), kwa uangalizi maalumu mpaka hapo madaktari watakapoona inafaa ndipo watapewa ruhusu ya kurudi nyumbani kwao Mbeya.

“Agosti watarudishwa tena India kwa ajili ya upasuaji katika njia ya mkojo na kufunga sehemu ya utumbo,” alisema.

Msemaji wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Nsachris Mwamwaja alisema upasuaji wa watoto hao ulichukua saa 18. Katika muda huo, saa 13 zilitumika kutenganisha viungo vilivyoungana sehemu ya chini ya uti wa mgongo, sehemu ya utumbo mpana, njia ya mkojo, kibofu na sehemu ya uume, wakati saa tano zilitumika kuunganisha sehemu zilizotenganishwa.

Pacha hao walifanyiwa upasuaji na madaktari 20 na wataalamu wengine wa afya ambao walitumia saa 18 kuwatenganisha. Kiasi cha Sh100 milioni kilitumika.

Meneja wa Huduma za Wagonjwa wa Kimataifa wa hospitali hiyo, Senu Sam alizungumza na gazeti dada la Mwananchi, The Citizen juzi na kusema wamefanya sherehe kwa ajili ya mafanikio ya upasuaji huo.

Sam alisema pacha hao wameonana ana kwa ana kwa mara ya kwanza, wiki tatu baada ya upasuaji... “Imekuwa faraja kuwaona wakitazamana. Eliudi alivishika vidole vya mkono wa Elikana na kuvichezea. Wanaonekana kufurahia mazingira mapya,” alisema Sam.

MZIMU WA POSHO WALITESA BUNGE LA KATIBU..WAKATAA POSHO YA SH LAKI TATU KWA SIKU

$
0
0
Siku mbili baada ya kuanza kwa Bunge hilo, baadhi ya wajumbe wametaka waongewe posho kwa maelezo kuwa kiasi wanachopewa sasa cha Sh300,000 kwa siku hakiwatoshi kutokana na kupanda kwa gharama za maisha Dodoma.

Wajumbe hao walitoa kauli hiyo jana katika kikao cha kuwasilisha na kujadili rasimu ya kanuni za Bunge hilo ambacho kilianza saa nne asubuhi.Kwa kiasi kikubwa, kikao hicho ambacho awali waandishi wa habari walizuiwa kuingia, kilitawaliwa na hoja ya kuongezwa kwa posho za wajumbe na kuungwa mkono na wajumbe wengi bila kufuata utaratibu maalumu uliokuwa ukisisitizwa na Mwenyekiti wa Muda wa Bunge la Katiba, Pandu Ameir Kificho.

“Wajumbe wengi walikuwa wakisimama na kutaka kuzungumza bila kufuata utaratibu maalumu. Jambo hilo liligeuza ukumbi wa Bunge kuwa kama soko,” kilisema chanzo chetu. Baadhi ya wajumbe waliopata nafasi ya kuzungumzia nyongeza ya posho hizo ni Mbunge wa Kishapu (CCM), Suleiman Nchambi na Mbunge wa Sumve (CCM), Richard Ndassa.

Katika ufafanuzi wake kwa waandishi wa habari, baada ya kikao hicho kuahirishwa kwa muda, Ndassa alisema: “Bunge ndiyo linalotengeneza Katiba ya nchi. Nasikitika kuwa kiwango cha fedha ambacho tunalipwa ni kidogo na hakitoshi kwa sababu kuishi katika Mji wa Dodoma ni gharama kubwa.”

Ndassa alisema kati ya Sh300,000 wanazolipwa wajumbe hao, posho ya kikao ni Sh220, 000 na 80,000 ya kujikimu na kwamba kiasi hicho hakitoshi.

“Mfano ni siku ya Jumamosi na Jumapili. Katika siku hizo mbili wajumbe wote hawalipwi Sh220,000 za posho za kikao na wakati huohuo wanatakiwa kuwalipa madereva wao, kununua mafuta ya gari, chakula na malazi,” alisema.

Aidha, alisema kitendo cha wajumbe kutakiwa kulipwa Sh220, 000 baada ya kusaini katika kitabu cha mahudhurio mara mbili kwa siku ni sawa na udhalilishaji.

“Nilimweleza mheshimiwa mwenyekiti kwamba wajumbe tupo 600 na kulingana na hali halisi wote hatuwezi kuhudhuria kikao kila siku, zipo siku ambazo baadhi yetu wanakuwa na shughuli nyingine na wapo watakaougua, sasa na hao wasilipwe Sh220,000 kweli?” alihoji.

Alisema Serikali inatakiwa kulitazama suala hilo kwa kina kwa maelezo kuwa linaweza kuibua mvutano unaoweza kusababisha wajumbe hao kushindwa kuijadili Rasimu ya Katiba kama inavyotarajiwa na wengi.

“Wajumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba walikuwa wakilipwa Sh500,00 kwa siku, lakini wajumbe wa Bunge Maalumu la Katiba wanalipwa Sh220,000 tena mpaka wahudhurie kikao. Hii siyo sawa kabisa,” alisema.

Alisema madereva wa Tume hiyo ya Katiba walikuwa wakilipwa Sh220,000 kwa siku... “Posho yangu ni sawa na aliyokuwa akilipwa dereva wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba. Sielewi kabisa maana hata viwango vyetu vya posho ni tofauti na wajumbe wa Bunge la Katiba kutoka Zanzibar, wao wameongezewa posho.”

Alisema jambo hilo litaibua ubaguzi kwa sababu wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wanaweza kuwasilisha malalamiko yao kwa Spika wa Bunge, Anne Makinda na kuongezewa posho lakini wajumbe 201 walioteuliwa na Rais hawana mahali pa kulalamika ili kuongezewa posho.

Pamoja na Ndassa kutotaka kuweka wazi, kumekuwa na madai kuwa wajumbe kutoka Zanzibar wameongezewa Sh120,000 na Baraza la Wawakilishi, hivyo kuwafanya kupata Sh420,000 kwa siku.

Hata hivyo, Katibu wa Baraza hilo, Yahya Khamis Hamad alikana madai hayo akisema hakuna fedha za ziada walizolipwa.

Alisema malipo waliyosaini wakiwa Dodoma yaliyotokana na kuhudhuria vikao vya Kamati za Baraza, lakini si nyongeza ya posho.

Akizungumzia suala hilo Nchambi alisema: “Sisi tumeshazoea maisha ya Dodoma na tunaishi hivyohivyo tu licha ya kuwa fedha ni ndogo. Ila hawa wenzetu ambao ni wageni hali zao ni mbaya.

“Wajumbe wapo hapa kwa ajili ya kutengeneza moyo wa nchi yao na wakati tunakuja hapa Dodoma tulielezwa wazi kuwa tusiende kuishi katika nyumba za wageni za vichochoroni. Sasa kwa mantiki hiyo hiki kiwango cha fedha tunacholipwa kitatosha kweli?

“Hapa bungeni wapo maprofesa walioacha kazi zao zinazowaingizia fedha nyingi na kuja kuandika Katiba. Kitendo cha kuwalipa fedha kidogo kinaweza kuwakatisha tamaa.”

Kificho alihitimisha mjadala huo kwa kusema suala hilo la posho litawasilishwa serikalini kuona namna ya kulifanyia kazi.

Baada ya wabunge kutoka kwenye mjadala huo, Mjumbe, Kabwe Zitto alisema anasikitika kwamba tangu siku ya kwanza, suala la posho linashika kasi... “Kiukweli inavunja moyo sana… Ni dhahiri wajumbe lazima walipwe lakini malipo ya posho ndiyo kipaumbele kweli?”

Imeandikwa na Mwinyi Sadallah, Raymond Kaminyoge Fidelis Butahe na Freddy Azzah.

MAKUBWA! MAMA WEMA AKESHA AKIOMBA DIAMOND AFUMANIWE

$
0
0
Mayasa Mariwata na Shani Ramadhani
MAMA wa Miss Tanzania 2006 aliye pia staa wa muvi za Bongo, Wema Sepetu, Mariam Sepetu amesema anamwomba Mungu bintiye huyo amfumanie mpenzi wake asiyemkubali, Mbongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’, Amani  lina picha kamili.

Akizungumza na mapaparazi wetu juzikati jijini Dar es Salaam, mama Wema alisema:
“Najua kwa sasa sina tena mamlaka ya kuingilia mapenzi ya binti yangu kwani mambo hayo yamenichosha, yananiumiza na kichwa.

“Lakini naomba sana kwa Mungu itokee siku moja Wema amfumanie Diamond akiwa na mwanamke mwingine labda ndiyo itakuwa kikomo chao cha kuwa wapenzi kwani ndiyo ndoto ninayoiota kila siku.”

KWA NINI ANAOMBA DUA BAYA?
Mama Wema alikwenda mbele zaidi kwa kusema kwamba, amegundua binti yake huyo hana ubavu wa kuachana na Diamond hata kama atasikia ana mwanamke mwingine.

MAGAZETI PIA YAMESHINDWA
Mwanamke huyo anayemwogopa Mungu tu, alikwenda mbele zaidi kwa kusema kwamba, kuna wakati baadhi ya magazeti pendwa nchini yaliandika Diamond kuwa na demu mwingine lakini Wema hakukasirika wala kuachana na staa huyo wa muziki wa kizazi kipya.

MSIKIE MWENYEWE
“Kwa hiyo mchezo mzuri ni yeye (Wema) kumfumania huyo Diamond wake, maana magazeti tu  kuandika kwamba ana uhusiano na mwanamke mwingine mwanangu alivyofanywa mjinga wa kutupwa, hatamwacha.

“Mimi najua Wema anashindwa kukaa chonjo kwa sababu ndumba zimemtawala, amefunikwa labda baadaye atafunguka,” alisema mama Wema.

AIGUSA SAFARI YA DIAMOND NCHINI NIGERIA
Mama Wema akaanika jambo ambalo halijawahi kujulikana kabla. 
Alisema: “Huyo Diamond ndo maana alikwenda Nigeria akashindwa kupiga muziki kwa sababu hakwenda na Wema, sasa ameona ampumbaze ili aweze  kwenda naye nchi za nje kwa masilahi yake binafsi, ataishia kumuahidi tu hana uwezo wa kumnunulia Wema kitu chochote chenye thamani kubwa, ni mpenda misifa tu.   
“Si mnamjua huyo ni mtoto wa Tandale? Anajiita yeye m...(alitaja jina la kinyesi) na kweli yuko hivyo.
NDUGU WA DIAMOND WAMEJAZANA KWA WEMA
“Ndugu zake walivyo washamba wamejazana hovyo pale kwa Wema. Wajinga mno, maana mshamba siku zote ni mshamba,”     alisema mama huyo.

HATAKI KUSIKIA WEMA ANA MIMBA YA DIAMOND
Katika hali iliyoonesha kwamba kweli hampendi Diamond, Bi. Mariam alisema hataki kusikia binti ana ujauzito wa msanii huyo.

Alisema: “Mbegu (uzao) gani atakayoileta kwangu, huyo mjukuu si atakuwa balaa, siwezi kuharibiwa wajukuu. Mtoto asiyeeleweka siwezi kumshika.”

ACHIMBA MKWARA
“Halafu nataka kuwaambia enyi watu wa magazeti, haya mambo ya kumwongelea huyo domo acheni mara moja, dunia itamnyoosha,” alisema.

AJIRUDI KWA MWANAYE
Mama Wema alisema hawezi kumlaumu sana binti yake  kwa vile akili si yake, yeye (Wema) ni mwanake na atabaki kuwa mwanamke, ila siku zote lenye mwanzo halikosi kuwa na mwisho.

DIAMOND SASA
Juzi, Amani lilimtafuta Diamond kwa njia ya simu na kumjulisha kuhusu ndoto za mama mkwe wake huyo ambapo aliishia kucheka.
“Teh! Teh! Teh! Thubutu.”
HAIJAWAHI KUTOKEA
Kumbukumbu za makabrasha ya Amani zinaonesha kwamba, katika historia ya wapenzi wa Wema, mzazi huyo hakuwahi kutokea kumkubali Diamond hata siku moja tu.
Amekuwa akimshukia mara kwa mara, madai yake siku zote ni kwamba, katika maono yake hajawahi kuona mapenzi ya kweli ya Diamond kwenda kwa Wema.

Japokuwa pia hajawahi kusema kama kuna mapenzi ya kweli ya Wema kwa Diamond.
Wema amewahi kuwa na uhusiano wa kimapenzi na marehemu Steven Kanumba, Jumbe Yusuf, Chalz Baba na Clement ‘kigogo wa ikulu’. Pia amewahi kudaiwa kutembea na TID na Mr Bluu.
Credits:Global Publishers

ALIYEZAA NA SHILOLE AIBUKA, WAONYESHANA MALAVIDAVI HADHARANI

$
0
0
Denis Mtima, aliyekuwa Igunga, Tabora
KWA mara ya kwanza, mzazi mwenza na msanii wa muziki na filamu Bongo, Zuwena Mohamed ‘Shilole’, Elias Makala ameibuka na kujinadi hadharani wilayani Igunga, Tabora.

Tukio hilo lilitokea Februari 14, mwaka huu (Valentine’s Day) ambapo Shilole aliyekuwa amekwenda kufanya shoo mkoani humo, alishindwa kuzuia hisia zake baada ya mzazi mwenzake huyo kujitokeza na kujikuta wakioneshana mahaba mbele za watu.

Pozi hilo la kimahaba liliwashangaza watu na kuanza kudhani kuwa huenda wawili hao wakarudisha penzi lao lililokufa miaka mingi iliyopita.

“Mh! Kweli mtalaka hatongozwi, hebu ona Shilole alivyorembua alipomuona jamaa yake, pale Makala kumchukua ni kama kumsukuma mlevi,” alisema shuhuda mmoja
Baada ya paparazi wetu ‘kuusoma mchezo’ huo, aliamua kumuuliza staa huyo kama penzi lao limerudi upya au laa?

“Hahahahaa! Kwa kweli unanichekesha kuniuliza kama nimerudisha penzi kwa mzazi mwenzangu, huyu ni baba wa mwanangu Joyce, itabaki kuwa hivyo. Siwezi kumtenga na sioni ajabu kupiga naye picha, hakuna kinachoendelea,’’ alisema Shilole.

Licha ya kufafanua hivyo, usiku wa siku hiyo, Shilole alipokuwa jukwaani akipagawisha mashabiki kwa shoo kali, alimpandisha jukwaani mzazi mwenziye huyo hali iliyozua mtafaruku mkubwa kwa mpenzi wa sasa wa Makala aliyefahamika kwa jina la Maguno.

Baada ya shoo kuisha, Maguno aliyekuwa na jazba kwa mpenzi wake kupandishwa jukwaani, alimsaka Shilole kwa udi na uvumba kutaka kumtembezea kichapo lakini bahati haikuwa yake, hakuweza kumpata hadi msanii huyo aliporejea jijini Dar siku iliyofuata.
Credits:Global Publishers

HILI BUNGE LA KATIBA LIMEJAA WAHUNI NA WASHENZI SIJAWAHI KUONA TOKA TUPATE UHURU

$
0
0
Mchungaji Mtikila leo huyu jamaa amekandia bunge lote la katiba na kusema anasikitka soon atalicha bunge hilo mana limechaguliwa kihuni.

Nasema hivi wambieni kabsa nimesema hili ni bunge la kihuni limechaguliwa kihuni ndio maana unakutana na mambo ya kishenzi mnayoendelea kuyaona.

Nasema tangia uhuru sijapata kuona bunge la kihuni kama hili.

Sitoshangaa maamuzi ya kihuni na kishenzi kutokea siku tunaagana pale nje.

Huyo ni rev. Christopher Mtikila.

Source: BBC swahili

ZITTO AMWOMBA RAIS ASIONGEZE POSHO WANAZOLILIA WABUNGE WA BUNGE LA KATIBA

$
0
0
Ishu ya posho za bunge la katiba ndiyo inayoongelewa sana hivi sasa ambapo pamoja na headlines zote za Wabunge, haya ni mawazo ya Mbunge wa Kigoma Kaskazini Zitto Kabwe kuhusu hii posho.IANGALIA HAPA


FACEBOOK WAINUNUA WHATS APP, WAMILIKI WAWA MABILIONEA

$
0
0

San Fransisco. Mtandao wa kijamii wa Facebook umenunua programu ya huduma za meseji ya WhatsApp kwa dola za marekani bilioni 19 (TSh 30.9 trilioni) katika taarifa iliyotoka mapema leo.
Ununuzi huo wa WhatsApp umetengeneza mabilionea wapya angalau watatu, akiwemo mwanzilishi wa WhatsApp, Jan Koum, ambaye atajiunga na bodi ya wakurugenzi ya Facebook.
Mwanzilishi mwenza wa WhatsApp, Brian Acton, naye anaingia katika orodha ya mabilionea wapya vijana.
Miaka 4 iliyopita, Acton alijaribu kuomba kazi Facebook na Twitter baada ya kupunguzwa kutoka Yahoo, inaripoti blogu ya teknolojia ya Techcrunch.
Hakufanikiwa.
Leo hii, program aliyoitengeneza na rafikiye wa Yahoo, Koum, inagombaniwa na kampuni zilezile zilizomkataa na hatimaye, imenunuliwa kwa mabilioni ya dola na Facebook.
Wengine walioula ni wawekezaji wa kwanza wa WhatsApp toka kampuni ya uwekezaji ya Sequoia.
Techcruch inaripoti vijana wa Sequoia wametengeneza zaidi ya dola bilioni 3 (TSh 4.9 trilioni) – mara 50 ya pesa waliowekeza – katika ‘dili’ hilo.
Facebook, ambao ni mtandao mkubwa kuliko yote duniani ukiwa na wanachama zaidi ya bilioni 1, inaamini kuwa WhatsApp itasaidia kuongeza uwepo wake katika masoko mbalimbali duniani, hasa katika nchi zinazoendelea Afrika, Asia na Amerika Kusini ambapo teknolojia ya simu za mkononi imeshika hatamu.
Uamuzi huo unaipa Facebook nafasi ya kuongeza idadi ya watumiaji wa mtandao wake, itarithi zaidi ya watumiaji milioni 450 wa WhatsApp.
Mwanzilishi na Mkurugenzi Mtendaji wa Facebook, Mark Zuckerberg anaamini uamuzi wa kuinunua WhatsApp kwa dola bilioni 19 ni wa busara, kwa kuwa “[WhatsApp] ni mtandao unaokuwa kwa haraka, ambayo itafikia watumiaji zaidi ya bilioni moja hivi punde.”

UGANDA YAPIGA MARUFUKU UVAAJI WA VIMINI NA MAVAZI YA NUSU UCHI ATAKAYE KUTWA FAINI JELA MIAKA 10

$
0
0
Rais wa Uganda Yoweri Musen Amesign Mswada wa kuzuia wanawake kuvaa nguo fupi zijulikanazo kama vimini ama nguo zozote za nusu uchi, Kuanzia sasa mtu yoypte atakaye kutwa amevaa hivyo atachukuliwa sheria ikiwemo adhabu ya kufungwa jela miaka 10 mpaka 15 ...Je unaonaje na kwetu Tz ikiletwa Adhabu Hii Maana daaaa Kumezidi?/

"MSIMAMO WANGU, SAKATA LA POSHO BUNGENI"JOSHUA NASSARI

$
0
0
MSIMAMO WANGU, SAKATA LA POSHO BUNGENI.

Nimeona nukuu kwenye gazeti la nipashe la leo. Kimsingi ike nukuu si ya kwangu ni nineshazungumza na Mhariri wa jipashe Bw. Kwayu.
Sijui kama nukuu ile imewekwa kwa kukosea au kwa makusudi, wameahidi kurekebisha makosa lakini ni vyema nikaweka msimamo wangu hapa.

Kwa hali halisi ya maisha ya kawaida ya Mtanzania wa shilingi laki 3 ni fedha nyingi. Na taasisi ya Bunge ndiyo inayopaswa kuwapigania hawa watanzania ili vipato vyao vipande lakini taasisi hii siku zote imekubali kuwa upande wa serikali badala ya kuisimamia serikali kwa niaba ya wananchi.
Fedha hiyo bado ni nyingi mno kama kipato cha mtanzania kinabaki kuwa hapo kilipo.

Kabla ya kupigania ongezeko ambalo linaweza wakati mwingine likawa na mantiki, ni vyema wabunge wakaifanya kwanza kazi yao ya kupigania maisha bora na maslahi bora kwa wananchi hiki hiyo mantiki yao kama ya kufanya mabadiliko ya posho ya shilingi elfu arobaini 40,000/= atakayolipwa mbunge iwapo ataugua akiwa Dodoma iweze kuonekana. Otherwise na sisi wabunge tutakuwa ni sehemu ya dhambi ya mateso na hali ngumu ya maisha ya watanzania ambao bado wanajifungulia sakafuni na hawana maji safi ya kunywa. 

Joshua Nassari (MB) na mjumbe wa bunge maalum la katiba.

NAPE "WANAOTAKA SEREKALI TATU NI WAHUNI"

$
0
0
"Wanaotaka serikali tatu ni wahuni" Nape Nnauye:Hii kauli ya Katibu wa Itikadi na Uwenezi wa CCM,Nape kumtukana Mwenyekiti wa chama chake na Raisi wa nchi.

Tume inayongozwa na Jiji Warioba,iliteuliwa na Raisi hivyo kuwaita wanaotaka serekali tatu ni wahuni,afahamu kwamba kamtukana mkuu wake na sio mwingine.

Na kama raisi alipokea maoni rasimu iliyokuwa na serekali tatu,ambazo Nape anaita ni wahuni,sasa asilimia 63% ya watz ni wahuni?

JK hataki misimamo ya vyama bungeni, nyie serekali mbili mnatoa wapi?

Maoni ya watanzani yanatakiwa kuheshimiwa na kulindwa kwa gharama yoyote hata ikibidi,kumwajika kwa damu,Lengo kuheshimu Sauti ya Umma

SNURA AMBWATUKIA SHILOLE

$
0
0
Na Brighton Masalu
MAMA wa majanga, Snura Antony Mushi kwa mara ya kwanza amejitokeza hadharani na kuzungumzia kauli ya  msanii mwenzake wa muziki wa mduara, Zuwena Yusuf Mohamed ‘Shilole’ juu yake kuwa ameisha kimuziki ndiyo maana ameamua kukimbilia muziki wa Taarab.

Akizungumza na mwandishi wetu hivi karibuni, Snura ambaye anawika mitaani kwa ngoma kali kama Majanga na Nimevurugwa, alisema kitendo cha Shilole ‘kuponyokwa’ na maneno hayo ni ishara tosha kuwa anamkubali na kufuatilia kazi zake kwa ukaribu mkubwa.

“Sina tatizo na maneno ya Shilole, hiyo ni ishara kuwa anafuatilia na kuzikubali sana kazi zangu, wala hawezi kunizuia kufanya kazi zangu kwa namna ambavyo nafikiria, yeye afanye yake, nami nishike ‘hamsini zangu’, alisema Snura.
Viewing all 104776 articles
Browse latest View live




Latest Images