Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104429 articles
Browse latest View live

Wanawake Acheni Kuvaa Mawigi Hampendezi Wala Kuvutia-Say NO to Fake Hair.

0
0
Mwanamke anapendeza na kuvutia zaidi anapokuwa na nywele zake za asili wala sio mawigi. Hiyo ni FACT.

Mawigi yanaboa na yanatupunguzia hisia, mfano pale mwanaume unavyozishika au kujaribu kuzichezea alafu kwa ndani anakutana na mabutu yaliyotumika kushonea wigi...Inaboa Hasa

Ni kama likofia fulani hivi linalovaliwa au kushonwa kichwani kwa mwanamke, ambayo pamoja na kwamba KIUHALISIA halimuongezei mwanamke mvuto (hata kama ni la Laki Moja), linatakiwa libadilishwe kila baada ya muda fulani.

Wanawake bakini na nywele zenu za asili, zipeni matunzo na usafi wala hamna haja ya kuhangaika na kubadilisha mawigi maana wanaume {99.99%} hatuzipendi. Zinaboa hata kuangalia. 

Cha kushangaza, utamkuta mwanamke wa kibongo eti naye anahangaika kuweka liwigi lake vizuri kanakwamba linamzuia kuona vizuri wakati ni FAKE HAIR na yeye mwenyewe kaliweka hivyo kwa makusudi kuiga Wazungu.

Say NO to Fake Hair.

Magufuli 'Alivyoivua Nguo' Serikali Ya Rais Kikwete...... Aanika Jinsi Mabilioni ya Safari Ne Yalivyoumiza taifa.

0
0
Uamuzi wa Rais Dk. John Magufuli kueleza kwa kina namna safari holela za nje ya nchi zinavyoligharimu taifa mabilioni ya fedha, umeianika wazi Serikali iliyopita ya Awamu ya Nne chini ya Rais Jakaya Kikwete na kuibua mjadala mkubwa miongoni mwa baadhi ya wafuatiliaji wa masuala ya siasa nchini.

Wachambuzi mbalimbali wa masuala ya kiasiasa wanasema kuwa ujasiri wa Rais Magufuli kueleza bila kificho jinsi safari za nje zinavyogharimu taifa kabla ya kutangaza msimamo mkali wa kuzidhibiti umedhihirisha pasi na shaka kuwa rais huyo mpya amedhamiria kubana matumizi holela ya fedha za serikali na badala yake kuzielekeza katika shughuli za maendeleo kwa nia ya kuboresha maisha ya Watanzania.

Wakati akilihutubia Bunge la 11 Ijumaa iliyopita kisha kulizindua rasmi, Rais Magufuli aliwataka wabunge na Watanzania wote wamuunge mkono katika uamuzi wake wa kupiga marufuku safari holela za nje huku akisisitiza kuwa kwa kufanya hivyo, fedha nyingi zinazopotea zinaweza kutumiwa katika kuboresha huduma za jamii.

Akitaja kwa mifano jinsi safari hizo za vigogo nje ya nchi zinavyoligharimu taifa, Magufuli alisema katika mwaka wa fedha 2013/2014 na 2014/2015 peke yake, taifa lilitumia Sh. bilioni 356.324 kugharimia safari hizo; kiasi ambacho kwa maelezo yake, kingetosha kujenga barabara ya lami ya urefu wa kilomita 400 na pia kufanikisha miradi mbalimbali ya maendeleo ikiwamo ya maji, elimu na afya.

Alisema mgawanyo wa matumizi ya fedha hizo ulikuwa ni tiketi za ndege (Air ticket) Sh. bilioni 183.160, mafunzo nje ya nchi Sh. bilioni 68.612 na posho za kujikimu (Per Diem Foreign) Sh. bilioni 104.552.

Magufuli alizitaja wizara na taasisi za umma zilizoongoza kwa kutumia fedha nyingi kwa ajili ya safari za nje ya nchi kuwa ni Bunge, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikano wa Kimataifa, Wizara ya Fedha, Ofisi ya Waziri Mkuu, Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi wa Hesabu za Serikali (NAOT) na Wizara ya Mambo ya Ndani.

Kwa mujibu wa Rais Magufuli, sasa safari hizo ni marufuku na pale inapolazimu, ni lazima kibali kitoke kwake au kwa Katibu Mkuu Kiongozi Ikulu, na kwamba, kuanzia sasa watakaokuwa wakijumuishwa kwenye misafara ya lazima nje ya nchi ni watu muhimu tu wanaohitajika katika safari husika.

“Hizi fedha zingeweza kutumika vizuri kuboresha huduma za wananchi wa maisha ya chini, kama afya, maji, elimu na umeme. Mfano, fedha hizi zingetosha kutengeneza kilomita 400 za barabara za lami. Tujiulize, zingeweza kutengeneza zahanati ngapi? nyumba za walimu ngapi? Madawati mangapi?” alihoji Rais Magufuli wakati akielezea suala hilo bungeni na kuongeza:

“Hivyo tunapodhibiti safari za nje tunawaomba Waheshimiwa Wabunge na Watanzania wote mtuelewe na mtuunge mkono.”

Alivyo "Ivua Nguo" Serikali ya Awamu ya nne
Hotuba ya Rais Magufuli aliyoitoa mwishoni mwa wiki inaonyesha wazi kuwa misafara ya mara kwa mara ya viongozi mbalimbali kwenda nje ya nchi ilikuwa ikiligharimu taifa kwa kiasi kikubwa kwani fedha hizo zingefanya mambo mengi kwa manufaa ya nchi badala ya kunufaisha vigogo wachache.

Wakati fedha nyingi zikitumika kwa safari hizo, bado hali ni mbaya katika utoaji wa huduma mbalimbali za kijamii; mambo ambayo Magufuli amesisitiza kuwa kamwe hatakubali kuyaruhusu katika serikali yake ya awamu ya tano.

Fedha hizi zilizotafunwa na viongozi mbalimbali kupitia safari za nje (Sh. bilioni 356) zingeweza kufanikisha mambo mengi ya maendeleo kwa taifa kama ifuatavyo.

1. Madawati 3,098,469
Bei ya dawati moja linalochukua wanafunzi watatu wa shule za msingi huwa ni kati ya Sh. 80,000 hadi 150,000, wastani wake ukiwa ni Sh. 115,000.

Kwa sababu hiyo, ikiwa fedha zilizotumika kwa safari za vigogo (Sh. bilioni 356) zingetumika kununua madawati, maana yake yangepatikana madawati 3,098,469 na hivyo kumaliza tatizo hilo katika shule za msingi nchini.

2. Visima vya maji safi 35,632
Kwa mujibu wa vyanzo mbalimbali, gharama za kuchimba kisima cha maji safi huwa ni kati ya Sh. 50,000 hadi Sh. 100,000 kwa kina cha mita moja, kutegemeana na jiografia ya eneo husika.

 Kwa sababu hiyo, kama kisima kitakuwa na urefu wa mita 100 na kitachimbwa kwa Sh. 100,000 kwa kila mita moja, maana yake kiasi cha fedha kitakachohitajika ni Sh. milioni 10.

Hivyo, ikiwa fedha za safari za nje (Sh. bilioni 356) zingetumika kuchimba visima vya maji safi vya thamani hiyo, maana yake vingepatikana visima 35,632. Visima hivyo vingegawanywa sawa katika wilaya 133 nchini, maana yake kila wilaya ingepata mgawo wa visima 268.

3.Mikopo  ya wanafunzi wa elimu ya juu
Mwanafunzi wa mwaka wa kwanza wa shahada ya uhandisi wa madini katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) anayepata mkopo wa asilimia 100 hulipwa na  Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) jumla ya Sh. 4,219,500 kwa mwaka. Mchanganuo wa mkopo huo kwa mwaka wote wa masomo ni Sh. 2,099,500 kwa ajili ya chakula na malazi, Sh. 200,000 ya vifaa, Sh. 620,000 kwa ajili ya mafunzo ya vitendo, ada Sh. milioni 1.3.

Kwa sababu hiyo, ikiwa fedha za safari za nje alizozitaja Rais Magufuli zingetumika kuwapa mikopo wanafunzi wa elimu ya juu kama wa mwaka wa kwanza wa shahada ya uhandisi wa madini wanaolipwa asilimia 100, maana yake wanufaika kwa mwaka wangekuwa wanafunzi 84,447.

4.Magari ya kubebea wagonjwa
Mwaka jana, Agosti 28, kampuni ya Biolands International ilikabidhi msaada wa gari la kubebea wagonjwa (ambulance) aina ya Nissan Patrol kwa Halmashauri ya Wilaya ya Kyela lenye thamani ya takriban Sh. milion 76.

Kwa sababu hiyo, ikiwa fedha zilizotajwa na Rais Magufuli kuwa zilitumika kusafirisha vigogo nje ya nchi zingeelekezwa katika kununua magari ya wagonjwa kama walilopata msaada Halmashauri ya Wilaya ya Kyela, maana yake taifa lingepata magari mapya ya wagonjwa 4,688.

5.Zahanati  4,454.
Septemba 16 mwaka huu, Mbunge wa Jimbo la Bumbuli mkoani Tanga, January Makamba, alisema kuwa katika jimbo lake, wamekamilisha ujenzi wa zahanati za vijiji kadhaa kwa wastani wa Sh. milioni 80 kwa kila moja.

Kwa sababu hiyo, kama fedha za safari alizozitaja Rais Magufuli kuwa zilitumika kusafirisha vigogo nje ya nchi (Sh. bilioni 356) zingetumika kujengea zahanati kama za jimbo la Bumbuli, maana yake taifa lingepata zahanati mpya takriban 4,454.

6.Maabara shule za Sekondari 6,122
Mkuu wa Shule ya Sekondari Tandika, Hussein Mpungusi, aliwahi kukaririwa Aprili 20, 2015, akisema kuwa shuleni kwake walikamilisha ujenzi wa maabara mojawapo kwa Sh. milioni 58.2.

 Kwa sababu hiyo, kama fedha za safari kusafirisha vigogo nje ya nchi wakati wa Rais Kikwete mwaka juzi na mwaka jana zilizotajwa na Magufuli (Sh. bilioni 356) zingetumika kujenga maabara za shule za sekondari kama Sekondari ya Tandika, maana yake zingejengwa maabara 6,122 na kumaliza tatizo hilo nchini.

7.Mikopo kwa wajasiriamali( Kila  mmoja 500,000)
Miongoni mwa changamoto zinazowakabili wajasiriamali wanawake ni ukosefu wa mitaji kwa ajili ya kukuza biashara zao.

Hata hivyo, kama ingetokea serikali ya Rais Kikwete ingesitisha matumizi ya fedha za safari za nje kwa viongozi alizozitaja Rais Magufuli (Sh. bilioni 356) na badala yake kuzielekeza katika kuwakopesha mitaji wajasiriamali wanawake kwa kiasi cha Sh. 500,000 kila mmoja, maana yake wanufaika wangekuwa ni kina mama 712,648.

8.Bodaboda aina ya Boxer
Bei ya juu ya pikipiki aina ya Boxer zinazotumika kwa biashara ya bodaboda ni Sh. milioni 2.5.

Kwa sababu hiyo, ikiwa fedha za posho za safari alizozitaja Magufuli kuwa zilitumika katika miaka ya fedha ya 2013/2014 na 2014/2015 (Sh. bilioni 356) kwa ajili ya safari za vigogo nje ya nchi zingeelekezwa katika kununulia pikipiki hizi kwa ajili ya kuwakopesha vijana wanaotoa huduma ya usafiri wa bodaboda, maana yake zingepatikana pikipiki za aina hiyo takriban 142,530.

9.Vipimo CT-Scan 356
Vyanzo mbalimbali vinaeleza kuwa mashine za kipimo maarufu cha CT-Scan, aina ya Phillips huuzwa kwa wastani wa Sh. milioni 600 hadi bilioni moja.

Hivyo, kama Sh. bilioni 356.324 alizozitaja Rais Magufuli kuwa zilisafirisha vigogo nje ya nchi zingeelekezwa kununua vipimo hivyo, maana yake zingepatikana CT-Scan 356 za thamani ya Sh. bilioni moja  kila moja na kufungwa katika hospitali zote za rufaa nchini na nyingine nyingi zikaelekezwa katika hospitali za wilaya na pia vituo vya afya.

10.Daladala Toyota Coaster  6,089.
Kwa mujibu wa mtandao wa Trade Car View, bei ya kununua gari aina ya Toyota Coaster iliyotumika lakini iliyo katika hali nzuri ni dola za Marekani 27,896, sawa na takriban Sh. 58,513,255.

Kama fedha zilizosafirisha vigogo nje ya nchi katika miaka ya fedha ya mwisho ya Rais Kikwete (Sh. bilioni 356) zingetumika kununulia gari hizi kwa ajili ya kuwapatia wajasirimali wanaotoa huduma ya usafiri wa daladala nchini, maana yake zingepatikana daladala 6,089.

Chanzo: Nipashe

Saed Kubenea Kumburuza Mahakamani Spika wa Bunge Job Ndugai Kwa Kuvunja Kanuni Na Kuwaruhusu Polisi Kuingia Bungeni

0
0
Mbunge wa Ubungo (Chadema), Saed Kubenea amesema atamfikisha mahakamani Spika wa Bunge, Job Ndugai kwa kuvunja kanuni baada ya kuwaingiza polisi ndani ya ukumbi wa chombo hicho.

Polisi hao waliingia ndani ya ukumbi huo wiki iliyopita wakati Rais John Magufuli alipofika kwa ajili ya kuhutubia Bunge.

Kubenea alisema kitendo cha askari kuingia ndani ya Bunge kwa mara ya mwisho kilitokea nchini Uingereza mwaka 1930 na hakijawahi kutokea tena isipokuwa nchini.

Alisema kuwa kesi hiyo anatarajia kuifungua Mahakama Kuu wiki ijayo kwa ajili ya kutaka tafsiri ya kanuni hiyo.

Hata hivyo, mkurugenzi wa shughuli za Bunge, John Joel alisema hakuna kanuni iliyovunjwa kwa askari hao kuingia ndani ya Ukumbi wa Bunge.

Wakati Kubenea akiandaa mpango huo, Kamati ya Wabunge CUF imesema Spika Ndugai ndiye chanzo cha yaliyotokea bungeni.

Ijumaa wiki iliyopita wakati Rais akiingia kutoa hotuba ya kuzindua Bunge, wabunge hao walipiga kelele wakitaja jina la mgombea urais wa Zanzibar kwa tiketi ya CUF, Maalim Seif Sharif Hamad, kuonyesha msimamo wao dhidi ya uamuzi wa kufutwa kwa matokeo ya uchaguzi wa visiwa hivyo.

Walipiga kelele hizo wakati Rais wa Zanzibar, Dk Mohamed Shein akiingia kwenye ukumbi huo na baadaye wakati Dk Magufuli akiingia ukumbini na wakagoma kunyamaza hadi walipotakiwa kutoka nje na askari kuitwa ndani.

Wabunge wa upinzani wanadai kuwa Dk Shein si Rais wa Zanzibar, wala makamu wake wa pili, Balozi Seif Ali Iddi na Spika wa Baraza la Wawakilishi, Pandu Ameir Kificho kwa madai kuwa muda wao uliisha Novemba 2, baada ya Uchaguzi Mkuu.

Jana wabunge wa CUF chini ya Mwenyekiti wake, Juma Hamad Omary walitoa tamko lililokemea na kutoa tahadhari kwa mambo mawili huku wakimtaka Ndugai kutoyumbishwa na Serikali.

Katibu wa Umoja huo, Hamudu Hassan Bobal alisema vurugu zisingetokea endapo Bunge hilo lingezingatia tamko la barua ya Ukawa na kusikilizwa hoja ya mbunge wa Singida Mashariki (Chadema), Tundu Lissu aliyeomba mwongozo akitaka kujua Dk Shein na wenzake wanaingiaje bungeni wakati madaraka yao yaliisha tangu Novemba 2.

The HARD TRUTH! Why Kenyan Men Will Sleep with Nairobi Women And Not Marry Them.

0
0

Many single city women are crying foul because eligible bachelors are unwilling to settle down, even though these same guys date and sleep with them. To my fellow sisters, here is why men would rather spend the time with you in the sack, but not consider marriage.

Lifestyle 

When you earn Sh20,000 and live on the other side of Uhuru Highway, paying rent in excess of Sh30k, you will resort to soliciting money from men to maintain your expensive lifestyle. This paints you as an extravagant, careless and greedy chick, if not a gold-digger. Many men would shy away from a high maintenance woman, a woman who insists on holidaying in Dubai even when the man is up to his eyeballs in debt.


If you are that woman who knows all entertainment joints in the city and its environs, and probably can even identify their staff by name, you should not complain about not being hitched. Men don’t want to receive a money-milking text every Wednesday asking, “Babe what’s the plan today” A party animal cannot make a good wife. You are the type likely to leave the kids at the mercy of the neighbors or house help.

Then there’s your fashion sense. Yes, he may be proud to introduce you to his boys in your hot little number. But have you ever wondered why he’s never thought of taking you to meet his mum There can only be one Kim Kardashian, so don’t expect him to pull a Kanye and propose to you when you are always dressed like a stripper! Seems like there’s a very thin line between classy and trendy and trashy and ratchet.

Misplaced priorities

Here you are with a certificate or diploma in an inconsequential course from a city college atop a pub, yet you seem quite content with yourself. A level-headed man would rather marry an emancipated, ambitious woman. Not the likes of you who splurge on Peruvian hair every two weeks! How about you reduce your expenses and instead enroll for a degree or master’s programme. If school is beyond you, there’s still the option of starting a business.



Our clueless city women would rather save money for VVIP concert tickets. Then they still have the nerve to make an SOS call the following morning begging that you bail them out with rent money. Jeez woman, have you looked at your jewellery collection and how much it is worth! Really, how do you expect a man to take you seriously Drop the pettiness of instant gratification and consider investment. Plus, learn how to cook, because it’s just a matter of time before the man gets tired of your favorite Chinese take-outs. And you wonder why plain girls always seem to bag the man!

An intelligent woman makes for a stimulating life companion, not one whose claim to knowledge is the next plot in reality drama series.

Irresponsibility

Equality is not about fighting for the right to pee while standing, it is about knowing your place as a woman without your rights being infringed. When all you care about is asserting your ‘rights’ even in simple matters like house chores, you are definitely going to end up only with cats as your life companions!

Responsibility includes learning how to cook basic, decent meals and doing house chores. It does not matter how you were brought up or if you are a career woman, every man wants to come home to a warm, nicely prepared meal by his wife, not the mboch. If you delegate all duties to the house help, including making your bed because your manicure is too expensive to spoil, don’t complain if your man chooses the ‘auntie’ over you for a wife
Quit bugging the pastor with the same prayer request for a husband. All the prayers and fasting in the world will bear no fruit if you don’t want to be a woman. Stop tearing up every time you watch a wedding show and wish you were the bride. You won’t be, unless you change and do something. If you ever wish to be walked down the aisle, you need to be worth it.


Schophie Aoko Atieno

Mimba ya Jokate Yazua Balaa, Familia Yashtuka

0
0
Kwani kimenuka? Siku chache baada ya kubumburuka kwa habari ya kunasa mimba ikimhusisha ‘mtoto mzuri’ Bongo, Jokate Mwegelo ‘Kidoti’ huku mhusika mkuu akitajwa kuwa ni msanii nguli wa Bongo Fleva, Ali Kiba, ishu hiyo imezua balaa kufuatia familia ya mrembo huyo kushtushwa na hali hiyo, Ijumaa Wikienda limenyetishiwa.

TWENDE OYSTERBAY
Mwishoni kwa wiki iliyopita, ‘kijumbe’ wa gazeti hili alitua getini nyumbani kwa akina Jokate, Oysterbay jijini Dar kwa lengo la kutaka kujua nini kinaendelea juu ya binti yao kunasa mimba nje ya ndoa ilihali familia hiyo inasifika kwa misingi bora na maadili ya kidini.

Gazeti hili lilipotia timu nyumbani hapo, lilifanikiwa kuzungumza na mmoja wa wanafamilia hiyo aliyekuwa nje akifanya usafi ambaye bila simile ‘alifunua kinywa’ na kuweka hadharani mambo mazito.

GAZETI LA IJUMAA LAIBUA MAMBO
Kama anayeogopa jambo fulani, memba huyo wa familia ya Jokate alisema kuwa, mrembo huyo alikuwa akifanya siri kubwa juu ya ujauzito wake huo, lakini baada ya gazeti pacha la hili, Ijumaa, kuibua habari hiyo, familia hiyo, hususan mama yake mzazi (jina lipo), alizua utata mkubwa kwa binti huyo na kwamba alishtushwa na hali hiyo na kumlazimu kumkalisha ‘kitako’ Jokate ampe ukweli.

“Jokate alikuwa akifanya siri sana, lakini ninyi mlipoandika habari hiyo, hapakutosha, mama yake alimuitisha kikao na baadhi ya ndugu wengine, lakini Jokate hakutaka kuweka wazi juu ya hali hiyo.

“Ninavyosikia, kuna uwezekano mkubwa wa Jokate kuhama hapa nyumbani akajitegemee ili kuififisha aibu hii kwani familia inadai amewatia aibu kwa kitendo chake cha kubeba mimba nje ya ndoa,” alidai mhusika huyo.

JOKATE ATOWEKA
Mnyetishaji wetu huyo aliendelea kudai kwamba, baada ya kuona anabanwa, alitoweka nyumbani hapo kwa siku mbili kabla ya kurejea na kuondoka kisha kurejea tena.

Kama kawaida ya gazeti hili kujiridhisha kwa kila habari kabla ya kuichapisha na kuwapelekea wasomaji wake, ‘kiranja mkuu’ wa dawati la Ijumaa Wikienda, mashine kubwa kwa habari za ndani za mastaa wa Kibongo, alimtafuta mrembo huyo kupitia simu ya mkononi na alipobaini kuwa mpigaji ni mwandishi wetu alishindwa kusema chochote zaidi ya kuiacha simu hewani na baadaye kuikata.

ATUMIWA SMS
Hata hivyo, ili kujizolea ushahidi madhubuti, mwanahabari wetu alimtumia ujumbe mfupi wa maandishi (sms) na kumsomea madai hayo, lakini hakujibu ujumbe huo licha ya simu ya mwandishi wetu kuonesha kuwa ujumbe ulikuwa umepokelewa (delivered).

KIBA KIMYAA
Pia, kwa upande wa Ali Kiba, simu yake ilionekana kutokuwa hewani muda mwingi, lakini mwandishi wetu alituma ujumbe wa kutaka kusikia chochote kutoka kwake ili akiiwasha simu akutane na ujumbe huo, lakini hadi gazeti hili linaenda kuchapishwa, hakuwa amejibu ujumbe huo achilia mbali kupiga simu hivyo jitihada zinaendelea.

Hata hivyo, mashabiki wa mastaa hao wameendelea kuwapongeza kwa namna ambavyo wamekuwa wakioneshana mahaba na kwamba suala la kupata mtoto ni jambo la heri bila kujali wamefunga ndoa au la.

Chanzo: GPL

Breaking News: Rais Magufuli Afuta Sherehe za Uhuru Disemba 9..Atoa Agizo Hili..

0
0
Katibu mkuu kiongozi Ombeni Sefue amesema rais.John Pombe Magufuli amefuta maadhimisho ya siku ya Uhuru December 9 na kuagiza fedha zilizopangwa kwa shughuli hiyo zitengwe kwaajili ya kufanyia shughuli nyingine na pia akaagiza siku hiyo kutumika kwaajili kufanya usafi nchi nzima kwaajili ya kukabiliana na ugonjwa wa Kipindupindu.

Baraza la Mawaziri la Raisi Magufuli...Unaambiwa Wabunge Sasa Hivi Matumbo Joto

0
0
WAKATI Rais John Pombe Magufuli akitegemewa kutangaza Baraza la Mawaziri wakati wowote kuanzia sasa, matumbo ya wabunge yamepata moto wakijiuliza kama watawezana na kasi yake endapo watateuliwa kuwemo.

Magufuli, ambaye Rais Mstaafu Jakaya Kikwete alimuita Tingatinga, ameweka wazi katika hotuba yake kwa Bunge kuwa hatamvumilia mtu mzembe na mvivu na kwamba watakaobainika kujihusisha na rushwa au ufisadi, watashughulikiwa.
Ingawa wabunge karibu wote walikuwa wakimshangilia kwa nguvu wakati wa hotuba yake hiyo, inadaiwa hamu ya kupata ulaji wa uwaziri inawafanya baadhi yao kuingiwa na woga, kwani ufanyaji kazi wa mazoea ndiyo unaowatesa.

“Nakuambia hapa wabunge, hasa wale wenye ndoto za kuteuliwa uwaziri wana wasiwasi kama wataweza kweli kwenda na kasi ya huyu jamaa, maana anaonekana kuwa siriaz sana na kazi. Hili liko wazi maana wengi walizoea kuona nafasi za juu kiuongozi wanazitumia kwa masilahi yao,” kilisema chanzo chetu katika viwanja vya Bunge mjini Dodoma.

Inadaiwa wengi wa wanaotegemea kupata uwaziri wana hofu kwa sababu wanaamini mzigo watakaopewa utakuwa mkubwa kuliko tabia na hulka zao.

Rais Magufuli ameahidi kuteua Baraza dogo la Mawaziri litakalokuwa limesheheni wachapakazi na katika kukabiliana na vitendo vya rushwa na ufisadi, alisema kazi hiyo ataifanya kwa dhati.
Hata hivyo, mbali na jina la Tingatinga hivi sasa mtaani amepewa jina jipya la Mtumbua majipu licha ya kuwa kitendo hicho huleta maumivu.

Huyu Ndio Mbunge Mwanamke Mwenye Umri mdogo Tanzania Kuliko Wabunge Wote

0
0
Bi Halima Abdallah Bulembo, 24, anayetoka Kagera ndiye mbunge mwanamke mwenye umri mdogo zaidi katika bunge la kumi na moja la Tanzania.


Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumanne ya Nov. 24 2015, Ikiwemo ya Tinga tinga la Magufuli Kuzoa Vigogo Taasisi 18

Lowassa Awatembelea Wahanga Waliookolewa Mgodini Baada ya Kufukiwa Kifusi Kwa Siku 41

0
0
Mgombea urais kwa tiketi ya CHADEMA Edward Lowassa Jana alitoa shilingi milioni mbili kwa wahanga waliookolewa katika mgodi wa Nyangalata wanaopatiwa matibabu katika hospitali ya halmashauri ya mji wa Kahama mkoani Shinyanga.

Akikabidhi fedha hizo kwa wahanga hao, Lowassa alisema ametoa fedha hizo kama msaada ili ziwasaidie kwa matibabu kwa muda wote watakapokuwa hospitalini hapo, ambapo kila mmoja amepatiwa shilingi laki tano.

Mmoja wa wahanga hao, Joseph Burule alisema kitendo cha Lowassa kuwatembelea hospitalini hapo kimewapa faraja kubwa, kwani tangu waokolewe na kuanza kupatiwa matibabu hakuna kiongozi mkubwa aliyefika kuwajulia hali pamoja na kuwapa pole.

Burule alisema kitendo hicho kinatakiwa kuwa mfano wa kuigwa kwa viongozi pindi linapotokea jambo la kusikitisha kama hilo, na kusema kuwa fedha hizo zitawasaidia kujikimu hospitalini hapo.

Kwa upande wake Mbunge wa viti maalumu Mkoa wa Shinyanga kupitia CHADEMA Salome Makamba aliwaambia wananchi waliojitoza kumsabahi Lowassa kuwa, Lowassa amekuja kuwapa pole wahanga hao na hakuja kwa masuala ya kisiasa.

Novemba 15, 2015 wahanga 5 kati ya 6 waliofukiwa na kifusi katika machimbo ya nyangalata wilayani kahama waliokolewa wakiwa hai baada ya kukaa ndani ya mashimo kwa siku 41, ambapo juzi mmoja kati yao alifariki dunia.

Ni hivi karibuni baada ya kuokolewa mmoja wa wahanga hao alikaririwa akimuulizia Lowassa kama alishinda urais wa  Tanzania kwenye uchaguzi na baada ya kuambiwa hakushinda alikosa raha.

Julius Mtatiro Afunguka Kuhusu kesi ya Kupinga Ushindi wa CCM Segerea

0
0
Napenda kutoa taarifa hii rasmi na ya awali kwa wananchi wa Segerea na watanzania wote ambao walipigana kufa na kupona ili kuhakikisha UKAWA tunashinda madiwani, mbunge na kuongoza kura za Rais hapa jimboni. Kwa bahati mbaya tulifanikiwa kushinda madiwani wote, kuongoza kura za Rais lakini tukashindwa kwenye Ubunge.

Baada ya jimbo letu kwenda CCM nilishauriwa nisisaini kukubali matokeo na nikatekeleza ushauri huo, lengo lilikuwa ni kuwapa muda wanasheria wetu na mawakili waweze kushauri ikiwa kuna kesi ya kufungua kupinga ushindi wa CCM.

Baada ya mashauriano ya wiki kadhaa yaliyohusisha mawakili na wataalam wa sheria wa ngazi mbalimbali, tumejiridhisha na kushauriwa kwamba hatutakuwa na kesi ya kufungua, na kwamba tukiifungua kwa kulazimisha au "kwa kusukumwa na upepo wa wananchi" tutashindwa mahakamani mapema.

Wanasiasa wengi hukimbilia mahakamani wanaposhindwa uchaguzi si kwa sababu wana kesi zenye ushahidi wenye mashiko, bali huogopa maneno na tuhuma wanazoweza kupewa kuwa "wamenunuliwa na wagombea wa CCM", mimi kwa bahati nzuri sijakumbwa na upepo huo na natambua wananchi wa Segerea wananiamini kiasi cha kutosha.

Baada ya wiki moja kutoka sasa, ntatoa taarifa rasmi na ya kina juu ya hoja na sababu zilizopelekea wanasheria na mawakili wetu washauri tusihangaike kufungua kesi na kupoteza muda wa matumaini ya wananchi.

Mtatiro Julius,
Segerea.

Mgogoro wa Zanzibar Watua IKULU ya Marekani

0
0
Na Swahilivilla, Washington
Wakati vikao vya siri vya kutafuta suluhu ya mzozo wa kisiasa visiwani Zanzibar vikiwa vimeripotiwa, juhudi za kuupatia ufumbuzi mzozo huo zimehamia kutoka Ikulu ya Zanzibar na kufika Ikulu ya Marekani (White House).


Mnamo tarehe 21 mwezi huu, Wazanzibari waishio nchini Marekani waliandamana hadi kwenye Ikulu ya nchi hiyo katika juhudi za kutafuta uingiliaji kati wa kimataifa ili kuupatia suluhisho mzozo huo.

Akizungumza na waandishi wa habari mbele ya Ikulu hiyo, Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazanzibari Waishio nchni Marekani (ZADIA) iliyoandaa maandamano hayo Bwana Omar Haji Ali, alisema kuwa maandamano hayo yanakuja katika juhudi za Jumuiya hiyo za kutafuta uingiliaji kati wa kimataifa katika kuukwamua mgando wa kisisas visiwani Zanzibar.

Aliendelea kusema kwamba maandamno hayo pia yana lengo la kumkumbusha rais Barack Obama wa Marekani kutekeleza ahadi yake ya kuilinda demokrasia Barani Afrika.

"Katika hotuba yake aliyoitoa kwenye Makao Makuu ya Umoja wa Afrika mapema mwaka huu, rais Obama alisema '.. pale ambapo raia hawawezi kutekeleza haki zao, basi ulimwengu una jukumu la kukemea. Na Marekani itafanya hivyo, hata kama wakati mwingine itakuwa inauma'..", alikumbusha Bwana Ali.

Aliongeza kuwa "Wananchi wa Zanzibar wameshindwa kutekeleza haki yao kwa zaidi ya nusu karne sasa. Wakati umefika sasa kwa ulimwengu kuchukua jukumu lake. Wakati umefika sasa kwa Marekani siyo tu kukemea, lakini pia kuchukua hatua za kivitendo ili kuhakikisha kuwa sauti za Wazanzibari zinasikilizwa na kuheshimiwa"

Alipoulizwa ni hatua gani watakazochukuwa iwapo Serikali ya Marekani haikuchukua hatua yoyote kusaidia kumaliza mgando wa kisiasa Zanzibar, Bwana Ali alisema;
 
"Tuna imani na rais Obama, na tumemfikishia barua ya malalamiko yetu, na tunasubiri jibu lake, na imani yetu ni kuwa atachukua hatua madhubuti khususan ikizingatiwa kuwa Ubalozi wa Marekani nchini Tanzania ulikuwa wa mwanzo kutoa taarifa kuelezea kuwa uchaguzi wa Zanzibar ulikuwa wa haki na huru"
 
Alidokeza kuwa, iwapo hali itaendelea kubakia kama ilivyo, basi ZADIA itaelekea kwenye Umoja wa Mataifa.

Katika maandamano hayo yaliyowashirikisha pia wapenda amani na demokrasia kutoka sehemu mbalimbali ulimwenguni, waandamanaji walibeba mabango yaliyokuwa na maneno kama vile "Mshindi wa uchaguzi atangazwe", "maamuzi ya Wazanzibari yaheshimiwe", "bila haki hakuna amani' na mengineyo.

Aidha, waandamanaji hao walipiga makelele wakidai "tunataka matokeo yetu ya uchaguzi.."

Akizungumza na Swahilivilla, raia mmoja wa Marekani aliyeshiriki kwenye maandamano hayo alisema "Nilimpeleka mwanangu kwenda kusoma kule, bado ana mapenzi na Zanzibar, na amenisimulia habari nzuri za amani, utulivu na ukarimu wa watu wake. Amekuwa akifuatilia hali ilivyo, na kwa hamasa kubwa alipopata habari za maandamano haya, akaniomba tuje kuwaunga mkono Wazanzibari katika kudai haki yao"

Itakumbukwa kuwa, wananchi wa Zanzibar walipiga kura mnamo tarehe 25 Oktoba mwaka huu, lakini Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC) Bwana Jecha Salum Jecha akatangaza kufutwa kwa uchaguzi huo Mkuu visiwani humo, kitendo ambacho wataalamu wa Sheria wamesema kuwa kinakwenda kinyume na Katiba ya Zanzibar.

Wachambuzi wanaona kuwa hatua hiyo ya Bwana Jecha ilikuja wakati asilimia kubwa ya matokeo yaliyokuwa yametangazwa yalikuwa yanampa ushindi mgombea wa urais wa Zanzibar kutoka chama cha upinzani cha Wananchi (CUF) Maliim Seif Shariff Hamad.

Kitendo cha kufutwa kwa uchaguzi huo ambao wachunguzi wa nje na ndani waliulezea kuwa ulikuwa wa haki na huru, kimezua mtafaruku wa kisiasa visiwani Zanzibar, na juhudi za ndani na nje zimekuwa zikifanyika ili kumaliza mgogoro wa kisiasa visiwani humo.

Maandamano ya ZADIA ni katika juhudi za hivi karibuni kabisa za kimataifa za kusaka suluhu za mgogoro huo kwa njia za amani.

Wimbo Mpya wa Christian Bella na Ali Kiba Washindwa Kufanya Vizuri Kwenye Radio Kama Ilivyotarajiwa..Christian Bella Afunguka

0
0
Mkali wa masauti, Christian Bella amekiri wimbo wake mpya aliomshirikisha Alikiba ''Nagharamia'' haupo kwenye mzunguko mzuri kwenye redio kama ilivyotarajiwa na kwamba ukipewa airtime utakuwa mkubwa.

Akizungumza na Bongo5 leo, Bella alieleza sababu ya kwanini wimbo huo umeshindwa kufanya vizuri kama ilivyotarajiwa ukilinganisha na ukubwa wa wasanii waliomo.

Ngoma bado haina mzunguko kusema kweli, kwa sababu ilitambulishwa redio moja tu na bado haijakaa bado kwenye promotion,amesema.

Ngoma ni nzuri na itafanya vizuri, kwa sababu kuna ngoma nyingine inatambulishwa inafanya vizuri kwa siku za mwanzoni halafu inapotea lakini hii nina uhakika itafanya vizuri kutokana na muziki mzuri tulioimba.

Ngoja video itoke halafu watu wanajua nazungumzia nini kwa sababu mapokezi ni mazuri na watu wanahitaji kinachohitajika ni promotion tu.

Pia mimi wakati wimbo unatambulishwa sikuwepo, kwahiyo mimi naona ni promotion na wiki ijayo tunapokea video, aliongeza.

Chanzo: bongo5

Kuhusu Mwanamuziki Diamond Kuanza Kuimba Kingereza Kwenye Nyimbo zake Mpya...

0
0
Muziki ni lugha ya dunia, ndio sababu kuna wanamuziki wengi wanaimba lugha za kwao lakini bado wanafanya vizuri katika nchi nyingine zisizoongea lugha hizo.

Diamond Platnumz ametokea kuwa balozi mzuri wa lugha ya Kiswahili, kwasababu mafanikio aliyonayo sasa ya kufanya vizuri ndani na nje ya Afrika yametokana na nyimbo za Kiswahili alizotoa hadi sasa.

Baada ya kugundua kuwa kinachoweza kusababisha wimbo upendwe kimataifa sio lugha, hit maker huyo wa ‘Nana’ hana mpango kabisa wa kurekodi nyimbo za Kiingereza, licha ya kuwa ameshawahi kutoa wimbo wa Kiingereza, collabo yake na Iyanya ‘Bum Bum’ ambayo hata hivyo haikufanya vizuri kama nyimbo zake za Kiswahili.

“Hatuwazi kabisa kufanya nyimbo ya kizungu kwasababu Kiswahili ndicho kimetufanya tukavuka boda,” alisema Babu Tale ambaye ni meneja wa Diamond kupitia 255 ya XXL. “sio ushamba kutokuimba kizungu…Cabo Snoopy haimbi kizungu yule anaimba kikwao, wapo wakubwa kibao ambao wanaishi Ufaransa wanaimba Kifaransa wanaoishi Portugal wanaimba ki Portuguese, yaani hivyo, unatokea Tanzania imba Kiswahili, hata tukifika Nigeria wakimwona Diamond anafanya Interview ya kizungu wanamshangaa, wapo wanaokwenda pale hawajui hata kuongea kizungu…basi sometimes wanamuomba awafundishe maneno machache ya Kiswahili, ni dalili nzuri ya kutangaza lugha yetu.” alisema Tale.

Tale aliendelea kusema;

“Anayedharau asili yake hawezi kuvuka, tumekubalika kusikika Nigeria, Uganda wapi sehemu ambazo hazina Kiswahili kwasababu ya ‘Number 1 Remix’ ambayo Diamond aliimba Kiswahili mwanzo mwisho, na ‘Nasema Nawe’ imepata tuzo juzi Nigeria na ni ya Kiswahili typical. Kwahiyo tumesema si tunataka tupewe ubalozi wa kutangaza lugha yetu, na huwezi ukaimba kizungu R.Kelly akaimba kizungu halafu mkafananishwa, R.Kelly mwenye kizungu chake ndio ataonekana number One. Tukasema sisi haitatokea Diamond nyimbo hata moja kuimba kizungu na tunafanikiwa…Watu kibao waliwahi kuwaza huwezi kuwa International artist kama hujaimba kizungu, Diamond juzi ameshinda tuzo ile ya MTV Europe, hana nyimbo ya kizungu yoyote hana.” Alimaliza Babu Tale.

Msanii mwingine wa Afrika ambaye ameshaweka msimamo kuwa hatatumia kiingereza kwenye nyimbo zake ni rapper Sarkodie wa Ghana.

Sarkodie hutumia lugha ya kwao kwa kuchanganya na Kiingereza kidogo sana, lakini ni msanii ambaye ameshashinda tuzo mbalimbali kubwa kama ya BET Awards 2012 ‘Best International Act’, na ameshapata nominations za MTV MAMA, Channel O Music Awards, MOBO, AFRIMMA na zingine, kutokana na nyimbo hizo hizo.

Wachezaji Mbali Mbali Wajinyakulia Zawadi Katika Michuano ya Gofu ya Waitara

0
0
Mkurugenzi Mkuu (Mstaafu) wa Kampuni ya bia ya Serengeti Steve Ganon akizungumza kwenye hafla ya jioni kwa washiriki wa michuano ya gofu ya Waitara ambayo ilifanyika katika viwanja vya gofu vya Lugalo mwishoni mwa wiki jijini Dar es salaam. Michuano hiyo hudhaminiwa na Kampuni ya bia ya Serengeti ambayo hufanyika mara moja kila mwaka kwa madhumuni ya kuenzi mchango wa kimichezo wa Mkuu wa Majeshi (Mstaafu) Jenerali George Waitara kwa kuasisi uwanja wa gofu wa Lugalo golf club.


Mkurugenzi Mkuu (Mstaafu) wa Kampuni ya bia ya Serengeti Steve Ganon (kulia) akiwasilisha zawadi yake kwa Mkuu wa Majeshi (Mstaafu) Jenerali George Waitara (Kushoto). Aliyeshika zawadi hiyo ni balozi wa pombe kali ya Johnnie Walker Winfrida Kimario. Michuano hiyo hudhaminiwa na Kampuni ya bia ya Serengeti ambayo hufanyika mara moja kila mwaka kwa madhumuni ya kuenzi mchango wa kimichezo wa Mkuu wa Majeshi (Mstaafu) Jenerali George Waitara kwa kuasisi uwanja wa gofu wa Lugalo golf club.



Mshindi wa michuano ya gofu ya Waitara kwa wachezaji wakongwe wanawake Priscilla Karobia (Katikati) akikabidhiwa zawadi yake baada ya kuwapiku wenzake kwa mikwaju 82. Akikabidhi zawadi hiyo kushoto ni Mwenyekiti wa bodi ya (NIC) Dk. Edmund Mndolwa. Michuano hiyo hudhaminiwa na Kampuni ya bia ya Serengeti ambayo hufanyika mara moja kila mwaka kwa madhumuni ya kuenzi mchango wa kimichezo wa Mkuu wa Majeshi (Mstaafu) Jenerali George Waitara kwa kuasisi uwanja wa gofu wa Lugalo golf club.

Mkuu wa Majeshi (Mstaafu) Jenerali George Waitara (Kushoto) akipokea zawadi ya wiski ya Johnnie Walker (Platinum Label) iliyotolewa na Kampuni ya bia ya Serengeti katika kuthamini mchango wake kimichezo kwa kuasisi uwanja wa gofu wa Lugalo. Anayekabidhi zawadi hiyo ni balozi wa pombe kali ya Johnnie Walker Winfrida Kimario.

Mgeni rasmi wa michuano ya gofu ya Waitara Mhe. Jaji Mstaafu Mark Bomani (katikati) akikabidhi zawadi kwa mshindi wa pili wa jumla wa michuano ya gofu ya Waitara Bw. Michael Obare (wa kwanza kulia). Pamoja na Mgeni rasmi ni Mkuu wa Majeshi Mstaafu Jenerali George Waitara(wa kwanza kushoto) na Meneja chapa wa vileo vikali wa Kampuni ya bia ya Serengeti Shomari Shija (wa pili kulia). Michuano ya gofu ya Waitara hudhaminiwa na Kampuni ya bia ya Serengeti na hufanyika mara moja kila mwaka kwa madhumuni ya kuenzi mchango wa kimichezo wa Mkuu wa Majeshi (Mstaafu) Jenerali George Waitara kwa kuasisi uwanja wa gofu wa Lugalo golf club.

Mshindi wa jumla wa michuano ya gofu ya Waitara George Nyakundi (katikati) akiwa na nyuso ya furaha baada ya kutangazwa rasmi kama mshindi wa jumla wa michuano hiyo ambapo alikabidhiwa kikombe pamoja na zawadi mbalimbali. (wa pili kushoto) ni Mgeni ramsi wa michuano hiyo Jaji (Mstaafu) Mark Bomani na (wa kwanza kushoto) ni Mkuu wa majeshi (Mstaafu) George Waitara na wa kwanza kulia ni Meneja chapa wa pombe kali wa Kampuni ya bia ya Serengeti Shomari Shija. Michuano ya gofu ya Waitara hudhaminiwa na Kampuni ya bia ya Serengeti na hufanyika mara moja kila mwaka kwa madhumuni ya kuenzi mchango wa kimichezo wa Mkuu wa Majeshi (Mstaafu) Jenerali George Waitara kwa kuasisi uwanja wa gofu wa Lugalo golf club.

 Mshindi wa jumla wa michuano ya gofu ya Waitara George Nyakundi akionyesha zawadi yake ya kikombe mara baada ya kutangazwa rasmi kama mshindi wa jumla wa michuano hiyo iliyofanyika katika viwanja wa gofu vya Lugalo jijini Dar es salaam. (Kushoto) ni Mkuu wa majeshi (Mstaafu) George Waitara. Michuano ya gofu ya Waitara hudhaminiwa na Kampuni ya bia ya Serengeti na hufanyika mara moja kila mwaka kwa madhumuni ya kuenzi mchango wa kimichezo wa Mkuu wa Majeshi (Mstaafu) Jenerali George Waitara kwa kuasisi uwanja wa gofu wa Lugalo golf club.

Mkurugenzi Mkuu wa Abstrat Limited Abdallah Singano kutoka klabu ya (Gymkhana) Dar es salaam akishiriki kikamilifu katika michuano ya gofu ya Waitara ambayo yalifanyika katika viwanja vya gofu vya Lugalo jijini Dar es salaam mwishoni mwa wiki. Michuano hiyo ambayo huandaliwa na kudhaminiwa na Kampuni ya bia ya Serengeti hufanyika mara moja kila mwaka kwa madhumuni ya kuenzi mchango wa kimichezo wa Mkuu wa Majeshi (Mstaafu) Jenerali George Waitara kwa kuasisi uwanja wa gofu wa Lugalo golf club.


Michuano ya gofu ya Waitara yanayodhaminiwa na Kampuni ya bia ya Serengeti kupitia pombe yake kali ya Jonnie Walker imefana na kumalizika vizuri siku ya jumamosi ambapo MCHEZAJI George Nyakundi ameibuka mshindi wa jumla wa mashindano ya kila mwaka ya Kombe la Waitara yalilofanyika kwenye Viwanja vya gofu vya Klabu ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ) Lugalo jijini Dar es Salaam.
Nyakundi anayecheza katika kiwango cha ubora wa mchezo wa gofu (handicap) 22 alionesha kiwango cha juu zaidi katika mashindano hayo kwa kupiga mikwaju nett 65 na kuwashinda wachezaji zaidi ya 118 waliokuwa wakiwania Kombe hilo.
Nafasi ya pili ya jumla ilikwenda kwa Michael Obare ambaye alichuana vikali na mshindi akirejea na mikwaju nett 66.
Akizungumza na waandishi wa habari waliofika katika viwanja hivyo, Meneja Chapa wa pombe kali wa kampuni ya bia ya Serengeti Shomari Shija alisema kuwa wamedhamini mashindano hayo kwa mara ya tano sasa ili kuendelea kuenzi heshima ya muasisi wa klabu hiyo Jenerali Mstaafu George Waitara.
Akitangaza matokeo ya washindi mbalimbali katika makundi tofauti Kapteni wa klabu ya gofu Lugalo Japhet Masai alisema katika kundi la wachezaji wa viwango vya Daraja A ambao ni wa kiwango cha juu katika mchezo huo mchezaji chipukizi Suleiman Kessy mwenye handicap 9 alishinda kwa kupiga mikwaju nett 69, Jumanne Ally handicap 8 alishika nafasi ya pili akiwa na mikwaju 70, wakati Juma Likuli mwenye handicap 8 alimaliza nafasi ya tatu akiwa na mikwaju 70 pia.
Mchezaji Nicolaus Chatanda handicap 11 alishinda kombe kwa wachezaji wa Daraja B akiwa na mikwaju 68, akifuatiwa na nahodha wa Klabu ya Gymkhana Dar es Salaam, Akhil Yusufali handicap 16 akiwa na mikwaju 71 na Priscus Nyoni handicap 12 alishika nafasi ya tatu akiwa na mikwaju 72.
Kelvin Manuhwa handicap 19 alishinda kwa kundi la wachezaji wa Daraja C akiwa na mikwaju 72 na kufuatiwa na R. Rwiguza handicap 24 aliyepiga 74.
Kundi la wachezaji waandamizi wanaume kombe lilikwenda kwa Joseph Tairo handicap 13 mikwaju 73, nafasi ya pili alikuwa Jenerali Mstaafu Mirisho Sarakikya handicap 19 aliyepiga mikwaju 73 pia , wakati Edmund Mndolwa handicap 9 alipiga mikwaju 74 na kumaliza nafasi ya tatu.
Pricilla Karobia handicap 17 alishinda kwa upande wa wachezaji wakongwe wanawake akiwa na mikwaju 82 na Lina Nkya handicap 15 alishika nafasi ya pili baada ya kurejea na mikwaju 88.
Kwa upande wa kundi la wanawake Tayana William handicap 24 aliibuka mshindi kwa kupiga mikwaju 72, akifuatiwa na Vailet Peter handicap 13 akiwa na mikwaju 74 na Vicky Elias handicap 13 alishika nafasi ya tatu baada ya kurejea na mikwaju 76.
Mbali na wachezaji wa ridhaa mashindano hayo pia yalihusisha kundi la wachezaji wa kulipwa ambapo Geofrey Leverian alirejea na mikwaju 75 gross na kuibuka mshindi wa kundi hilo lililohusisha wachezaji 18. Nafasi ya pili na tatu ilikwenda kwa mchezaji mkongwe Mbwana Juma na Nuru Mollel waliopiga mikwaju 76 na 77.
Kwa upande wake muasisi wa michuano hiyo Mkuu wa Majeshi mstaafu Jenerali George Waitara aliwashukuru washiriki wote kwa kuonyesha ni jinsi gani wameendelea kuthamini michuano hiyo na kuwataka kuendelea na moyo huo.
Waitara pia alitumia nafasi hiyo kuishukuru Kampuni ya bia ya Serengeti na kumpongeza Mkurugenzi Mkuu (mstaafu) wa Kampuni hiyo Bw. Steve Ganon ambaye mara zote hakusita kudhamini michuano hiyo na kuomba wadau wengine kuiga mfano huo.
Naye Mgeni rasmi wa michauano hiyo Jaji (Mstaafu) Mark Bomani alitoa changamoto ya wadau wa mchezo huo kushiriki katika kuongeza viwanja vingi zaidi vya mchezo huo huku akianisha maeneo kama Dodoma, Mwanza na Mbeya ambapo wadau hao wanaweza kuendeleza mchezo huo.
Mashindano ya gofu ya Mkuu wa Majeshi mstaafu Jenerali George Waitara huandaliwa na kufanyika kila mwaka kwa madhumuni ya kuenzi mchango wake wa kimichezo nchini kwa kuasisi uwanja wa gofu wa Lugalo golf club. Uwanja huo ulianzishwa mwaka 2006 kwa mchango mkubwa uliotolewa na Jenerali mstaafu George Waitara kipindi alichokuwapo madarakani, pia kuendelezwa na Mkuu wa Majeshi aliyefuata na aliyeko madarakani kwa sasa Jenerali Davis Mwamunyange.

Mambo Bado Zanzibar: Dr Shein na Maalim Seif Kukutana Tena Leo Kwa Mara Ya Tatu

0
0
Mazungumzo ya kutafuta muafaka wa mgogoro wa Uchaguzi Mkuu wa Zanzibar, yataendelea kufanyika leo Ikulu Mjini Zanzibar leo.

Mazungumzo ya kikao hicho ambacho ni cha tatu, kitaongozwa na Rais wa Zanzibar, Dk. Ali Mohammed Shein.

Wajumbe wa kikao hicho ni Marais wastaafu wa Zanzibar, Dk. Salmin Amour, Amani Abeid Karume, mgombea urais wa Zanzibar kwa tiketi ya Chama cha Wananchi (CUF) ambaye pia ni Makamu wa Kwanza wa Rais, Maalim Seif Sharif Hamad na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi.

Mazungumzo hayo yanasubiriwa kwa hamu kubwa na wananchi baada ya Tume ya Uchaguzi Zanzibar (Zec), kufuta matokeoi ya Uchaguzi Mkuu visiwani humu Oktoba 28, mwaka huuu na kuibua mgogoro mkubwa wa Kikatiba.

Naibu Katibu Mkuu wa CUF Nassor Ahmed Mazrui, amesema kuwa hadi sasa mazungumzo hayo bado siri kubwa hata viongozi wa ndani ya chama chake, hawafahamu kinachoendelea tangu viongozi hao wa kitaifa kuanza kukutana.

Amesema inasikitisha mno vikao vyote vitatu vilivyofanyika pamoja na hicho kinachotarajiwa kufanyika leo, upande mmoja unawakilishwa na watu watano wakati upande mwingine ukiwa na uwakilishi wa Maalim Seif peke yake.

Amedai kuwa mashariti yaliyowekwa katika muongozo wa mazungumzo, ni magumu kwa kuwa hakuna mtu mwingine anayeruhusiwa kushiriki katika mazungumzo ya kutafuta muafaka wa uchaguzi wa Zanzibar zaidi ya Maalim Seif pekee.

NAFASI ZA AJIRA>>WWW.AJIRAYAKO.COM

MUGABE Again 'I Don’t Care About Racism As Long As I Use White Tissue Paper To Wipe My Black B.utt

0
0

If you missed Zimbabwean President Robert Mugabe’s speech on racism, here an excerpt;

"Racism will never end as long as white cars are still using black tires. 

Racism will never end if people still use black to symbolise bad luck and white for peace. 

Racism will never end if people still wear white clothes to weddings and black clothes to funerals. 

Racism will never end as long as those who don't pay their bills are blacklisted not whitelisted. 

Even when playing snooker, you haven't won until you've sunk the black ball, and the white ball must remain on the table. 

But I don't care, as long as I'm still using white toilet paper to wipe my black b()tt , I'm fine"


Victory! AL SHABAAB Leaders Blown Into Pieces as US Drone Strike Kills Several Commanders

0
0

Somalia based Al Qaeda affiliate terror group, Al Shabaab, suffered heavy casualties over the weekend after their top commanders were killed in a US drone strike on Saturday night in Southern Somalia.

Three senior commanders were killed alongside 11 other Al Shabaab fighters who were bombed as they were taking one of their senior commanders for medical attention at Baladul Amin in Lower Shabelle region.

Among Al Shabaab commanders killed on Saturday is Sheikh Mohamed Abdalla, who is the overall commander of Lower Shabelle region.


The killing of these three top commanders of the Al Qaeda affiliated jihadist group is a big blow to the militants who have been suffering from one blow after another in the hands of Kenya Defence Forces (KDF) who are currently wiping them out of their only hideout in Boni Forest.

The attack comes barely a week after US announced a hefty reward offer of upto 27 million US dollars on any information leading to the killing or capturing of the senior Al Shabaab figures in Somalia.

Ushauri: Mchumba Wangu Anaishi na Jini na Linataka Limuoe

0
0
Mimi ni mvulana wa miaka 28, Nina mchumba wangu ambaye nimeshalipa gharama ya mahali kama robo 3 ila siku hizi nipo karibu sana na huyo mchumba wangu.

Siku moja alikuwa ananisimulia maisha yake, kitu kilichonitisha amesema yeye kuanzia 2014 anaishi na Jini subiani naikipita siku hajaswali basi usiku yule jini anamtokea na anasex na kubwa zaidi hiyo jini ndiye aliyemtoa bikra na akisex nae asubuhi anakuta mbegu ukeni.

Miezi michache iliyopita Jini alikuwa anambembeleza amuoe ila binti amekataa, sasa hii kitu mi inanitsha sana coz nahisi kama huyu jini ata nimaliza mimi coz atajua ndo sababu ya yeye kukataliwa.

Ushauri wenu coz niliplan tufunge ndoa mwezi 3 mwakani

NAFASI ZA AJIRA>>WWW.AJIRAYAKO.COM

Wanawake: Kama Unampenda Mumeo, Mpende na Mama Mkwe

0
0
Habari wakuu,

Kumekua na tabia kwa baadhi ya wanawake ya kupenda waume zao na kuwachukia wazazi wa kike wa wawaume zao.

Hii tabia imekithiri katika baadhi ya ndoa nyingi, wanawake hao wamekua wabinafsi sana, hawataki kuendeleza mahusiano ya mume wake na familia ya mumewe.

Mfano, unakuta mtoto huyo wa kiume ni tegemeo la nyumbani kwao au wakati mwingine sio tegemeo ila lazima atume kiasi flani cha matumizi nyumbani kwao, lakini mkewe akiona hivyo anazuia hataki pesa zitumwe kwa mama mkwe.

Wakati mwingine mama huyo anaumwa na anahitaji kuja kutibiwa kwa mwanae, lakini mwanamke anakasirika na kumwambia mumewe asije kupata matibabu nyumbani kwao.

Wanawake wengine wamekua wakigombana na mama wa waume zao bila hata aibu, lakini eti akiwa na mumewe anampenda. Wanawake wenzangu tujifunze kuwaheshimu mama wa waume zetu na tuwapende kama mama zetu.

Kama unampenda mumeo, mpende na mama mkwe
Viewing all 104429 articles
Browse latest View live




Latest Images