Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104775 articles
Browse latest View live

Uwezi Amini Rais Magufuli Awa Gumzo Kubwa Nchini Kenya...Watamani Awe Rais Wao...Wamkosoa Uhuru Kenyatta

$
0
0
Uchapakazi wa Rais Dkt John Magufuli unatuma ujumbe si kwa maafisa wa Tanzania pekee, bali na nchi za jirani pia na kuwaacha viongozi wa nchi hizo kwenye wakati mgumu.

Kenya ambayo imekuwa ikifuatilia siasa za Tanzania tangu wakati wa kampeni, imeonesha kupenda mbinu za Magufuli na wananchi wake wanatamani mtu kama yeye.

Kwa kipindi kifupi alichoingia madarakani, Magufuli amefanya mambo makubwa na wananchi wamependa.

Ziara yake ya kushtukiza kwenye hospitali ya Muhimbili ilifichua uovu mwingi na kupelekea kufutwa kwa bodi ya wakurugenzi wa hospitali hiyo na kumuondoa Kaimu Mkurugenzi wake, Dk Hussein Kidanto.

Ili kupunguza matumizi makubwa ya fedha za serikali kwaajili ya kugharamia safari za nje za viongozi wa nchi, Magufuli aliamua kuzisitisha mara moja.

Dkt Magufuli pia alielekeza kiasi cha shilingi milioni 225 zilichangwa kwaajili ya kugharamia hafla ya wabunge kupongezana mjini Dodoma zipelekwe kwenda kununua vitanda. Badala yake shilingi milioni 15 pekee zilitumika kwaajili ya sherehe hiyo.

Siku chache baadaye vitanda hivyo na vifaa vingine vilinunuliwa na kupelekwa Muhimbili.

Jumatatu hii Magufuli alitangaza kuondoa sherehe za maadhimisho ya siku ya Uhuru December 9 na fedha za maandalizi hayo zitumike kwa mambo mengine muhimu.

Hayo na mambo mengine yamefanya Dkt Magufuli atrend nchini Kenya.

Hizi ni baadhi ya tweets za wakenya:

Kaka Hana Uwezo wa Kupata Mtoto, Je Naweza Kumsaidia Kumpa Mkewe Ujauzito?

$
0
0
Najua hapa kuna wenye ujuzi na hekima na busara.

Hoja ni jee ikiwa kaka yangu wa baba na mama mmoja ana mke, na ameishi nae kwa miaka zaidi ya tisa lkn hawajapata mtoto. ila huyu mwanamke ana mtoto aliempata kwa mnmumewingine kabla ya kuolewa na kaka mimi nimeoa miaka sita ilopita na tayari mke wangu ana watoto wawili.

Sasa ktk ndoa ya kaka tayari kuna minong'ono kuwa kaka ndie tatizo maana jamaa hajawahi hata kusingiziwa mtoto mitaanirafiki wa familia yetu mmoja amenishauri nifanye mpango wa siri na shemeji ili ikiwezekana nihakikishe anapata uja uzito uhusiano wangu na shemeji yangu ni mzuri na niwakaribu. na mara nyingi tunapotoka na wife huongozana nae kwasababu ya majukumu yake.


Je, naweza kukubali ushauri huo kwa siri ili kurejesha amani ya kaka? Lakini ili kulinda heshima ya familia yetu, inabidi angalao shemeji atuletee mtoto.

Wandugu, niambieni naweza kumsaliti kaka kulinda heshima ya familia?

NAFASI ZA AJIRA>>WWW.AJIRAYAKO.COM

Update Toka Mahakamani: Familia ya Alphonce Mawazo na CHADEMA Washinda Kesi ya Pingamizi la Polisi, Sasa kesi ya Msingi kusikilizwa

$
0
0
Jaji wa Mahakama Kuu Kanda ya Mwanza, Lameck Mlacha, ametupilia mbali mapingamizi yaliyowekwa na RPC wa Mwanza na Mwanasheria Mkuu wa Serikali dhidi ya kesi iliyofunguliwa jana na familia ya Marehemu Alphonce mawazo kuomba tafsri ya mahakama baada ya jeshi la polisi mkoani Mwanza kupiga marufuku mikusanyiko ya kuuaga mwili wa marehemu.

Katika mapingamizi hayo, mwanasheria mkuu wa serikali  alidai kuwa mleta maombi ambae ni Baba mdogo wa Mawazo hana uhalali wa kisheria wa kuleta maombi hayo mahakamani  kwa kuwa yeye si baba mzazi wa marehemu, na kuwa hajaleta hoja za kubishaniwa kwenye maombi hayo.

Upande wa utetezi unaoongozwa na mawakili John Mallya, James Millya na Paul Kipeja ulijibu hoja hizo kuwa katika hatua hiyo masuala ya kubishaniwa hayana sababu ya kuletwa kwa kuwa ni hatua ya awali sana.

Kuhusu uhalali wa kisheria wa baba mdogo wa marehemu, majibu yalikuwa kwamba baba mdogo kwa kuwa ndiye aliemlea Marehemu Mawazo, anayo mamlaka na uhalali wa kisheria wa kuleta maombi hayo.

Mahakama imekubaliana na hoja za mawakili wa mleta maombi na kuamua kuruhusu kesi ya msingi kufunguliwa kama ilivyoombwa, na kutupilia mbali mapingamizi ya RPC na mwanasheria mkuu.

Upande wa wapeleka maombi utawasilisha maombi ya kesi ya msingi leo hii mchana, kisha utasubiri maelekezo ya Mahakama kuwa kesi hiyo itaanza kusikilizwa lini kisha uamuzi wa kesi hiyo.

Alphonce Mawazo  alikuwa ni mwenyekiti wa chadema mkoani Geita kabla ya kuuawa kikatili kwa kukatwa mapanga na mashoka na watu wasiojulikana Novemba 14 mwaka huu katika kijiji cha katoro wilayani Geita.

NAFASI ZA AJIRA>>WWW.AJIRAYAKO.COM

Mchakato wa Serikali Kunyang’anya Mashamba na Viwanda Kwa Wawekezaji Walioshindwa Kuviendeleza waanza

$
0
0
Mchakato wa kunyang’anya mashamba na viwanda kutoka kwa wamiliki walioshindwa kutekeleza masharti waliyopewa na Serikali umeanza.

Taarifa tulizozipata zimeeleza kuwa miongoni mwa mashamba na viwanda hivyo ni kutoka mkoani Morogoro, Lindi, Arusha, Mbeya, Tanga, Kilimanjaro na Dar es Salaam.

Wiki iliyopita, Ofisi ya Msajili wa Hazina ilitoa tangazo kwa wawekezaji walionunua viwanda na mashamba ya Serikali ikiwakumbusha kurejea kwenye mikataba yao.

Taarifa hiyo iliyosainiwa na Msajili wa Hazina, Lawrence Mafuru (pichani) ilieleza kuwa inarejea mikataba yote ya mauzo ya viwanda na mashamba iliyoingiwa kupitia Mpango wa Ubinafsishaji na kwamba kuna wawekezaji wamekiuka masharti ya mikataba yao.

Miongoni mwa masharti hayo yaliyokiukwa ni kutoendelezwa viwanda na mashamba kwa mujibu wa mikataba, kushindwa kutekeleza mpango wa uwekezaji, baadhi ya wanunuzi kuuza mashine walizozikuta bila kurudisha mashine mbadala, kutokamilisha malipo ya ununuzi wa viwanda na mashamba na kubadilisha matumizi ya viwanda na mashamba bila idhini.

Ninawaagiza wawekezaji wote walionunua viwanda na mashamba yaliyokuwa yanamilikiwa na Serikali kwa ajili ya uwekezaji wawasilishe taarifa zao za sasa ndani ya siku 30, kinyume na hapo Serikali itachukua hatua stahiki ikiwamo kurejesha viwanda na mashamba hayo kwenye miliki yake,”ilisema taarifa hiyo.

Lakini zikiwa zimebaki siku 24 kwa tangazo hilo kufika kikomo taarifa zinaeleza kuwa tayari mashamba yameanza kurejeshwa kwenye umiliki wa Serikali, kwa madai ni utekelezaji wa agizo la Serikali.

Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Alphayo Kidata akizungumzia taarifa hizo za kuanza kurejeshwa kwa baadhi ya mashamba alisema hawezi kutoa maelezo kuhusu madai hayo kwa kuwa hana taarifa nayo.

Lakini alisema anatambua kwamba mambo yanaendeshwa kwa sheria na taratibu zake tofauti na madai ya taarifa hizo.

Sidhani kama mtu anaweza kuamka tu na kusema hili lifanyike. Lazima taratibu zifuatwe,” alisema Kidata.

Hata hivyo, Kidata alifafanua kuwa wizara hiyo imekuwa ikiendesha ikirejesha ardhi serikalini kutoka kwa wamiliki walioshindwa kuendeleza masharti.

Alisema mtu anapopewa dhamana ya kumiliki ardhi, dhamana hiyo huambatana na masharti ikiwamo kuendeleza na anaposhindwa hunyang’anywa.

Lakini kabla ya kufanya hivyo hupewa notisi na asipoifanyia kazi uamuzi wa mwisho ni kuichukua,”alisema Kidata.

Alisema Serikali chini ya wizara hiyo itaendelea kufanya hivyo kama wamiliki watakiuka masharti wanayotakiwa kufuata.

Kwa upande wake, Mafuru alisema serikali imetoa tangazo hilo na kuwapa wahusika siku 30 ili ndani ya muda huo, wajipange na kuandaa taarifa za utekelezaji wa miradi waliyopewa kuiendesha.

NAFASI ZA AJIRI>>WWW.AJIRAYAKO.COM

Waziri Mkuu Mpya Aanza Kumwaga Cheche..Aitaka TAMISEMI Kujieleza Kwanini Mabasi Yaendayo Kasi Hayajaanza Kufanya Kazi

$
0
0
Waziri Mkuu Mh.Majaliwa ameitaka TAMISEMI kujieleza ni kwanini mradi wa mabasi yaendayo kasi DART haujaanza hadi sasa.

Ameagiza watendaji wote wa wizara ya TAMISEMI, akiwemo Katibu Mkuu wa Wizara ya TAMISEMI kufika Ofisini kwake kesho asubuhi kueleza kwa nini mabasi hajaanzana kazi wakati miundombinu imeshakamilika.

Ameyasema hayo leo alipotembelea Wizara ya TAMISEMI na kuongea na watendaji wa wizara hiyo.

TAZAMA VIDEO:

NAFASI ZA AJIRA>>WWW.AJIRAYAKO.COM

Taifa Stars Yafanya Kweli Kombe la Challenge....Yaingia Robo Fainali Kwa Kishindo

$
0
0
TANZANIA Bara imejihakikishia kwenda Robo Fainali ya michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika Mashariki na Kati, CECAFA Challenge baada ya kushinda 2-1 dhidi ya Rwanda katika mchezo wa Kundi A jioni ya leo Uwanja wa Taifa wa Addis Ababa, Ethiopia.

Ushindi huo, unaifanya Tanzania Bara iongoze Kundi A kwa kufikisha pointi sita na mabao sita, huku ikiwa imefungwa bao moja na sasa itamaliza na wenyeji Ethiopia ikiwa ‘haina presha’.
Kilimanjaro Stars leo ilipata bao lake la kwanza kupitia kwa kiungo wa Simba SC, Said Ndemla kwa shuti la mpira wa adhabu dakika ya 22 baada ya Nahodha John Bocco ‘Adebayor’ kuchezewa rafu na mchezaji mwenzake wa Azam FC, Jean Baptiste Mugiraneza.

Winga wa Yanga SC, Simon Msuva na mfungaji bora wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara – akaifungia Stars inayofundishwa Alhaj Abdallah Athumani Seif ‘King Kibaden’ bao la pili dakika ya 78.

Rwanda ilipata bao lake la kufutia machozi kupitia kwa Jacques Tuyisenge dakika ya 85. Sasa Amavubi iliyoifunga Ethiopia 1-0 katika mchezo wa kwanza, itamaliza na Somalia waliofungwa 4-0 na Kili Stars.  
 
Kikosi cha Tanzania Bara kilikuwa; Aishi Manula, Shomary Kapombe, Mohammed Hussein ‘Tshabalala’, Kevin Yondan, Salum Mbonde, Himid Mao/Jonas Mkude, Simon Msuva, Said Ndemla, John Bocco, Elias Maguri na Deus Kaseke.

Diamond Tops 15 African Artists of 2015, Wizkid, Olamide Follow, Vanessa Mdee Makes It Too.

$
0
0

African Muzik Magazine has released their list of top 15 African artists of 2015, interestingly Tanzanian Diamond Platnumz is in the number 1 while Tanzanian Vanessa Mdee is in number 12. Nigerian Wizkid is placed 2 , Olamide in third place while Davido is placed fourth. Below is what they said about Diamond and Vanessa Mdee.....

1.Diamond Platnumz

Your guess is as good as ours, Diamond Platnumz the golden boy of East Africa and Tanzania’s own music crown prince tops our list of Top 15 African Artists of 2015 .Flamboyant, exciting and creative Diamond Platnumz has emerged as the new face of East African music and the undisputed King of Bongo flava. Never before has an artiste dominated the Tanzanian musical landscape like Diamond is presently doing lifting the East African flag to lofty heights on the world stage. Seen as a spoilt child by his siblings with the way his mother took him around to tale to shows every time and wait for him till late in the night for him to perform, Diamond has gone on to justify the unshaken faith of his mother in his musical ability emerging as one of Africa’s brightest music stars.

Born on October 2nd, 1989 as Nasibu Abdul Juma in Dar REs Salam, Diamond Platnumz started his music career as a rapper dreaming of becoming a rap star and getting all the girls but he found fame as a singer with his special brand of bongo lava. The very prolific artist has recorded more than 140 songs in his music career and is seen as the poster boy of Tanzanian/East African music. The song ‘Number One’ and the subsequent remix featuring the flaming Davido has catapulted Diamond to the top of the African music game with his popularity soaring more than ever before. The energetic performer has shut down venues all over Africa and beyond with fans yearning for more.
Diamond is a music person who listens to music all the time and is absolutely loved and adored by his fans while setting an unprecedented record of winning 7 Tanzanian Music Awards in one go. The BET Awards 2014 nominee stormed AFRIMMA with multiple nominations and he won in the Best Male East Africa category before going on stage to rekindle his partnership with Davido on the ‘Number One’ remix. 2015 has seen Diamond Platnumz cement his status as Africa’s number one artist with multiple awards including MTV EMA’s and AFRIMMA 2015 Artist of The Year Award.
A fan favorite anyday, Diamond is poised to cross boundaries with his music and his energetic as well as creative performances.

12. Vanessa Mdee
Coming up at number 12 of our Top 15 African Artists of 2015 is the petite East African vocal siren Vanessa Mdee aka V-Money. Born Vanessa Hau Mdee on June 7, 1988 in Arusha, Tanzania the third largest city in the country, she got grips different cultures in hear formative years. Vanessa grew up in New York, Paris, Nairobi and Arusha bagging a law degree at the Catholic University of East Africa. Vanessa Mdee has always had the knack for the creative and performing arts.
Little wonder that she is today a recording artist, songwriter, youth activist, TV and radio host.Vanessa Mdee created her own piece of history by becoming the first ever Tanzanian MTV VJ and he gained prominence as radio and TV host, hosting Epic Bongo Search and Dume Challenge for ITV Tanzania. Music took over she signed to B’Hits Music Group in late 2012 and her rise to the top echelons of African music has been astronomical.

After joining B’Hits Music Group, Mdee collaborated with Tanzanian rapper A.Y. on a record ‘’Money’’ and Ommy Dimpoz, a Bongo Flava artist on a record Me and You that was later voted Song of the Year during the 2013 Kilimanjaro Music Awards.
She received an even bigger buzz with the release of her first solo single “Closer”, which in its first week was downloaded over 30,000 times, a feat achieved by no other Tanzanian artist. “Closer” remained on the charts for over 13 weeks. She bagged three nominations at the prestigious Kilimanjaro Tanzania Awards in 2014.
Vanessa Mdee has kept her buzz up in 2015 by consistently doing better at what she does best. She released her fifth single Nobody But Me in March this year where she joined forces with heavy hitting South African rapper K.O. on a song that topped charts across the continent. The Vanessa Mdee brand solidified the more this year as she attracted loads of corporate attention eventually signing up as Brand Ambassador for Samsung Tanzania.

On the back of winning the Best Female Entatiner award at Kilimanjaro Tanzania Awards 2015, she went ahead to claim the AFRIMMA Best Female East Africa award as well as dropping the hot fire single ‘Never Ever to cap an impressive year for one of Africa’s finest female entertainers.

Walisema Hataweza Kuleta Mabadiliko Ndani ya Mfumo wa CCM, Sasa Wanadai Anatekeleza ilani yao

$
0
0
Hawa marafiki zetu wa upinzani kwa maoni yangu ni watu wa kutafuta tafuta sababu za kujitetea!
Wakati CCM inampitisha Magufuli kuwa mgombea urais, jamaa wakajaribu kuja na hoja kwamba hata aje malaika hataweza kuleta mabadiliko Kwasababu ya mfumo uliopo!!

Hoja yao ikawa Magufuli anafaa kuwa Raisi lakini mfumo ulio chini ya chama cha Mapinduzi utakuwa kikwazo kwake kuleta mabadiliko ambayo Magufuli alikuwa akiya nadi wakati wa kampeni! Ajabu ni kwamba hawakutuambia wakati ule kwamba mabadiliko aliyokuwa anayanadi Magufuli wakati wa kampeni yako kwenye ilani yao. Wao walichokiona na kutuaminisha wananchi ni kwamba ilani ya CCM iliweka mabadiliko ambayo Magufuli atashindwa kuyaleta akiwa ndani ya mfumo huu!!
Kichekesho sasa!!!

Baada ya wananchi kutokuwaamini wapinzani na kumuamini Magufuli na wakamchagua kuwa Raisi.
Na Magufuli huyo akaanza kuzifanyia kazi zile ahadi za mabadiliko alizozitoa wakati wa kampeni, wale jamaa wanarudi tena na hoja nyingine,
Eti Magufuli ameamua kuifuata ilani yao na kuiacha ilani ya CCM aliyoinadi!!!
Hivi hizi ni akili timamu kweli????
Wamesahau kwamba wakati Magufuli akiinadi hiyo ilani wakati wa kampeni, hao hao waliiona ni nzuri lakini wakajaribu kuwaaminisha watz kwamba Magufuli atashindwa kuitekeleza Kwasababu ya mfumo!!

Leo Magufuli anawaonyesha kwamba mfumo hauwezi kumzuia kuitekeleza ilani hiyo ya CCM na mabadiliko iliyoya ainisha, wanasema hayo unayo yafanya yako kwenye ilani yetu!!!!
Hivi mabadiliko Yale mliyo sema atashindwa kuyaleta Kwasababu ya mfumo ni yapi????
Magufuli amewathibitishia kwa vitendo kwamba siku zote mko wrong!!!!
Inabidi mfikirie tena!!!!

Magufuli Tafadhali Tuondolee Mbio za Mwenge, Hazina Faida Kwa Taifa zaidi ya Kutafuna Mabilioni Kila Mwaka

$
0
0
Tarehe 27 mwezi May, mwaka 2014 siku ya Jamanne majira ya saa 4 asubuhi, kwenye kipindi cha maswali na majibu, Naibu waziri wa habari vijana, utamaduni na michezo Juma Nkamia alieleza makadirio ya gharama za kukimbiza Mwenge wa Uhuru nchini.

Nkamia alisema "serikali kuu hutenga kiasi cha fedha kulingana na mahitaji na gharama halisi ya wakati husika.. Mwaka 2012 jumla ya shilingi Bilioni 43 zilitumika ambapo kati ya hizo Bilioni kumi na moja (11) zilitengwa na serikali na Bilioni 32 zilichangwa na mashirika, taasisi, makampuni na wadau mbalimbali walioombwa kuchagia kwa ajili ya kuadhimisha uzinduzi na kilele cha mbio za mwenge wa uhuru." Taarifa zinaonesha kuwa mwaka 2014 inakadiriwa jumla ya Shilingi Bilioni 120 zilitumika kama gharama ya kukimbiza Mwenge nchi nzima.
CALCULATION.

Bilioni 120 zinazotumika kukimbiza mwenge nchini (mwaka huu huenda zikaongezeka), zinatosha kufanya yafuatayo;

1. Kununua mashine 60 za MRI na CT Scan kwa ajili ya kuhudumia wagonjwa wenye kuhitaji vipimo hivyo. Ikumbukwe hospitali ya Taifa ya Muhimbili kuna mashine moja tu ya MRI na moja ya CT Scan ambazo zote ni mbovu. Fedha za Mwenge zinaweza kununua mashine 60 za aina hiyo.

Rais Magufuli alijaribu kuhimiza ukarabati wa mashine hizo lakini zilifanya kazi kidogo tu kisha zikafa tena. Kwa sasa hakuna huduma za Vipimo vya MRI Hospitali ya Muhimbili, hadi imefikia hatua wagonjwa wametunga kirefu cha MRI kuwa ni;
-Magufuli -Rudi -Imeharibika tena.

2. Shilingi Bilioni 120 zinazotumika kukimbiza Mwenge zinatosha kulipia mikopo ya wanafunzi 61,624 wa vyuo vya Elimu ya Juu nchini. Hadi sasa takribani wanafunzi 40,000 walioko vyuoni hawajapata mikopo. Kumbe fedha za Mwenge zingeweza kuwalipia mikopo wanafunzi wote waliobaki na chenchi ikabaki (61624 -40000) x 1,960,000 = 4,238,304,000. Ikabaki chenchi ya Bilioni 4.2

3. Bilioni 120 za Mwenge zinatosha kujenga Zahanati 3,870 kwa gharama ya Mil.41 kila Zahanati. Kwa mujibu wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi mwaka huu Tanzania ina jumla ya Kata 3,802. Kwahiyo Bil.120 za Mwenge zinatosha kujenga Zahanati kila Kata nchini na chenchi ikabaki. (3870-3802) × 41,000,000 = 2,788,000,000. Ikabaki chenchi ya Bilioni 2.7

4. Bil 120 za Mwenge zinatosha kununua Boti 13 za kisasa za majini kama ile ya Bakharesa (Kilimanjaro 5). Ikumbukwe ukiondoa boti za Bakhresa, serikali haina usafiri wa kueleweka wa kwenda Zanzibar. Meli mbili za Mv. Spice Islanders na Mv.Scagget zilizama na kuua maelfu ya watanzania kutokana na uchakavu wa meli hizo. Kwahiyo Bil.120 za Mwenge zingeweza kununua meli mpya za kisasa kwa ajili ya usafiri wa Zanzibar na nchi jirani ktk bahari ya Hindi kama Msumbiji, Comoro na Kenya. Hii ingekua njia ya kuongeza pato la taifa kupitia sekta ya usafiri majini.

On other hand tungenunua Boti za kisasa tungeweza kupromote utalii wa fukwe (Beach Tourism). Nchi ya Mauritius inaingiza zaidi ya Shilingi Trilioni 10 kwa mwaka (nusu ya bajeti ya Tanzania) kupitia utalii wa fukwe tu. Mauritius hawana Mbuga za wanyama, hawana mlima mrefu kama Kilimanjaro, lakini wanapata Trilioni 10 kwa mwaka kupitia utalii wa fukwe, Tanzania tuna vivutio vya kila aina lakini tunaingiza Trilioni 1.7 tu kupitia sekta ya utalii.

Kwahiyo tukitumia fedha za Mwenge tunaweza kuboresha utalii wa fukwe na kuvutia watalii wengi zaidi na kupata mapato makubwa zaidi kutokana na sekta ya utalii.

5. Bil 120 za Mwenge zikikusanywa kwa miaka mitano (120 bil x 5 = 600 Bil) zinatosha kununua Ndege kubwa za kisasa zipatazo 10 angalau na sisi tukawa na Shirika letu la ndege. Kwa mujibu wa mtandao wa www.aircraftcompare.com bei ya ndege aina ya Boeing 737 yenye uwezo wa kubea abiria 240 ni USD 43 Million sawa na Shilingi za kitanzania Bil.80.
Kwahiyo Bil.600 za Mwenge (kwa miaka mitano) zinaweza kununua ndege kama 10 hivi angalau na sisi tukafufua Air Tanzania yetu tukaanza kushindana na Kenya Airways, Rwandan Air au Ethiopian Airways.

Kwa ujumla yako mambo mengi sn fedha za Mwenge zinaweza kufanya ikiwa zitatumiwa vzr. Hizi nilizotoa ni alternatives chache tu lakini kama viongozi wetu wakiwa makini wanaweza kufanya makubwa zaidi ya haya.

Written By Malisa GJ

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumatano Ya Tarehe 25 Novemba

$
0
0

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumatano Ya Tarehe 25 Novemba

Vikwazo Vitano Vyatajwa Kwenye Agizo la Rais Magufuli Kufuta Safari za Nje

$
0
0
Agizo la Rais John Magufuli la kusitisha safari za nje linakabiliwa na ugumu katika utekelezaji wake kutokana na nchi kuwa na balozi 36 tu ambazo zitatakiwa kufanya kazi maeneo mbalimbali duniani.
Muda mfupi baada ya kuapishwa na kuanza utekelezaji wa majukumu yake ya mkuu wa nchi, Rais alifuta safari zote za nje kwa watumishi wa Serikali na viongozi ili kuokoa fedha zinazotumika kwa ajili hiyo na kuagiza shughuli hizo zifanywe na mabalozi.

Rais alisema safari hizo zitadhibitiwa na Ikulu ambayo itatoa kibali kwa safari maalumu, ikiwa ni pamoja na kuweka masharti ambayo mtumishi anayetakiwa kusafiri atatakiwa kuyatimiza kabla ya kupewa kibali.

Lakini utekelezaji wa agizo hilo unakabiliwa na vikwazo vingi, hasa vikubwa vitano ambavyo ni uchache wa balozi za Tanzania nje ya nchi, ukomo wa madaraka ya mabalozi, wigo wa ufahamu wa mambo ya kitaalamu na ukosekana kwa mazungumzo endelevu iwapo suala moja litawakilishwa na watu wawili tofauti kwenye mikutano miwili tofauti.

Takwimu za Umoja wa Mataifa (UN), zinaonyesha kuwa hadi sasa chombo hicho kina wanachama 193 ambao nchi zinazaweza kuwa na uhusiano nazo wa kidiplomasia, kwa mujibu wa makubaliano ya wanachama wa umoja huo. Kwa mujibu wa wakosoaji, uchache huo utasababisha mabalozi hao kusafiri sehemu mbalimbali duniani kushiriki kwenye shughuli ambazo viongozi wa umma walitakiwa kwenda, hali ambayo itasababisha safari kuwapo kama kawaida isipokuwa wanaosafiri ndiyo watakaobadilika.

“Ni kweli kwamba idadi ya watu wanaosafiri itapungua, lakini ile dhana ya safari itabakia vilevile,” alisema mmoja wa wakosoaji ambaye hakutaka jina lake litajwe.
“Kwa mfano, mkutano wa Jumuiya ya Madola unaofanyika Malta, Balozi wa Tanzania nchini Uingereza ndiye atatakiwa kwenda. Kwa hiyo ni safari pia.”
Bara zima la Amerika Kusini lina ofisi moja tu ya ubalozi iliyoko Brasilia, Brazil, wakati bara la Amerika Kaskazini lina balozi tatu, mbili zikiwa Marekani--Umoja wa Mataifa jijini New York na Washington--, huku Ulaya yenye nchi 50 ikiwa na balozi nane, wakati Asia, Arabuni pamoja na Australia kuna ofisi nane za ubalozi.

Bara la Afrika lenye nchi 52, ndiko kuna balozi nyingi zaidi, kukiwa na ofisi 14.
Ugumu katika utekelezaji unaosababishwa na idadi ndogo ya mabalozi pia ulidokezwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Liberata Mulamula mapema mwezi huu.
Akizungumzia suala hilo, Katibu Mkuu Kiongozi, Ombeni Sefue ambaye alikuwa akijibu maswali kuhusu vikwazo vitano vya utekelezaji wa agizo hilo la Rais, alisema suala hilo linaweza kujibiwa vizuri zaidi na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.
Lakini msemaji wa wizara hiyo, Mindi Kasiga alisema atumiwe ujumbe wa barua pepe ili ajibu suala hilo.

Ukomo wa madaraka ya mabalozi
Suala jingine linalozungumziwa ni ukomo wa mabalozi katika mamlaka yao, hasa pale wanapotakiwa kumuwakilishi Rais wakati hawabebi madaraka hayo ya mkuu wa nchi. Mara nyingi wakuu wa nchi huona umuhimu zaidi wa kuwa na mazungumzo baina yao kuliko na mabalozi inapotokea wamekutana kwenye mikutano ya mikubwa kama ya Jumuiya ya Madola, Umoja wa Mataifa, Sadc na mingine inayoweka maazimio muhimu kuhusu masuala kama ya mazingira, afya, na ya kibiashara.
Lakini Balozi Sefue alisema Rais atakuwa akihudhuria mikutano michache na hivyo uamuzi huo hautaathiri nchi. “Ni mikutano michache sana ambayo wanahudhuria wakuu wa nchi,” alisema Balozi Sefue. “Pale ambapo tutajiridhisha kuwa ubalozi hauwezi kutuwakilisha vizuri, basi tutaruhusu mtu atoke hapa nyumbani. Hiyo itakuwa ni baada ya kujua ni nani atakayekwenda na atakwenda kufanya nini,” alisema Balozi Sefue.

Kwa uzoefu wake, alisema hata viongozi watakaopewa ruhusa hawatakuwa na misafara mirefu kama ilivyokuwa awali kwa kuwa wapo baadhi yao ambao wanakuwa hawafanyi chochote huko waendako.
“Nilipokuwa Washington niliwahi kushuhudia. Kuna msafara ulikuja, mkubwa sana na kwa kipindi chote walichokaa pale, wapo baadhi hawakupata nafasi ya kufanya chochote. Hili nalo ni miongoni mwa mambo yatakayozingatiwa katika vibali vitakavyokuwa vinatolewa kwa wale watakaokidhi masharti,” alisisitiza.

Kuhusu ukubwa wa ujumbe ambao kiongozi anaruhusiwa kuambatana nao aendapo nje ya nchi, msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje, Mindi Kasiga amewahi kufafanua kuwa, kwa mujibu wa itifaki, kila mmoja ana maelekezo yake.
“Msafara wa Rais hauwezi kulingana na wa makamu wake, Waziri Mkuu au waziri wa kawaida ambao pia hutofautiana na makatibu wakuu au wakuu wengine wa idara na vitengo vya Serikali,” alisema Kasiga wakati akitoa ufafanuzi juu ya gharama za safari za nje wakati wa Serikali ya Awamu ya Nne.


Uwakilishi wa mamlaka ya Rais
Mbali na vikwazo hivyo, suala jingine ni mabalozi kubeba majukumu ya Rais kwenye mikutano ya nje jambo ambalo wakosoaji wanasema litawawia vigumu hasa watakapotakiwa kufanya uamuzi kwa madaraka ya mkuu wa nchi.
Lakini Balozi Sefue alisema mabalozi watakaotumwa kwenye mikutano hiyo watabeba kofia hiyo ya mkuu wa nchi na taarifa itakayotumwa nchini itakuwa na uzito unaostahili hivyo suala hilo halitaathiri ushiriki wa nchi.

Mabalozi kutokuwa na utaalamu
Uwezo wa mabalozi kushiriki kikamilifu kwenye masuala ya kitaalamu pia ni moja ya mambo yanayoonekana kuwa kikwazo kwa agizo la Rais Magufuli kuzuia safari za nje.
Lakini Balozi Sefue alisema matukio yanayohusu masuala ya kitaalamu kama kilimo, mazingira, afya, madini na mawasiliano ambayo yanahitaji watendaji waliobobea kwenye fani hizo, yatawekewa utaratibu licha ya kuwa changamoto kwa mabalozi.
“Kila ubalozi una wataalamu wa masuala mbalimbali ambao wanaweza kutoa mchango unaostahili kwa lolote linaloweza kuhitajika,” alisema.
“Si rahisi kukosa mtu mwenye uwezo wa kumsaidia balozi kutekeleza majukumu yake kiasi cha kuhitaji mtu mwingine kutoka nyumbani. Lakini likijitokeza hilo, tutatuma mwakilishi.”
Akizungumzia suala hilo, Balozi Mulamula alisema mapema mwezi huu kuwa utekelezaji huo utachukua muda kidogo kutokana na balozi nyingi kukosa fedha na watalaamu.
Suala la fedha kwenye balozi za Tanzania limekuwa kilio kikubwa kila wakati wa Bunge la Bajeti na mwaka huu suala hilo liliibuka kwenye hotuba ya kambi ya upinzani iliyosema kiasi cha Sh30 bilioni ziloizotengwa kwa wizara hiyo hazikutosha kuwawezesha mabalozi kufanya kazi yao kwa ufanisi.
Suala la weledi pia lilizungumzwa kwenye hotuba ya kambi ya upinzani ya mwaka 2014/15 ikisema uteuzi holela wa mabalozi usiozingatia sifa, unalikosesha Taifa fursa nyingi za kiuchumi kwa kuwa wengi hawana ufahamu wa fursa zilizoko kwenye nchi wanazokwenda.
Lakini mapema mwezi huu, Balozi Mulamula alisema suala hilo sasa litaangaliwa kwa jicho la karibu zaidi, hasa uteuzi wa mabalozi.

Alisema watatoa mwongozo ambao utawataka wawakilishi hao wasibweteke katika utendaji wao kwa kuwa kuna mpango wa kuanzisha utaratibu wa kupima matokeo ya utendaji wao kwa kila baada ya kipindi kitakachoelekezwa.
“Kwa sasa tutakuwa tunawapima mabalozi wetu kwa malengo tuliyokubaliana nao ambayo yanaweza kuwa ya mwaka au zaidi.
Tutakuwa tunamuuliza balozi umeweza kuleta watalii au kuwahamasisha wawekezaji wangapi nchini?” alisema.

“Hii ni kwa sababu zamani tulikuwa tunakwenda kienyeji lakini kwa sasa hapa kazi tu.”
Kikwazo kingine kinachoonekana kwenye utekelezaji wa agizo hilo ni kukosekana kwa mazungumzo endelevu iwapo suala moja litawakilishwa na watu wawili tofauti kwenye mikutano miwili tofauti.
“Mfano iwapo kutakuwa na mkutano wa suala fulani la Jumuiya ya Afrika Mashariki nchini Kenya, kwa agizo hilo la Rais, atakayewakilisha ni balozi wa Tanzania nchini Kenya,” alisema mkosoaji huyo na kuongeza:
“Iwapo suala hilo litaendelezwa kwenye mkutano mwingine wa jumuiya nchini Uganda, ni dhahiri atawakilisha balozi wa Tanzania nchini humo ambaye hakuwapo kwenye mkutano wa Kenya. Kwa hiyo kutakuwa na upungufu.”

Balozi Sefue hakutaka kufafanua kuhusu hoja hiyo na badala yake akaielekeza kwa Wizara ya Mambo ya Nje, ambayo alisema ina nafasi nzuri zaidi ya kulizungumzia.

WEMA Sepetu na Kajala Acheni Utoto..Maisha Yenu Tunayajua A-Z, Tengenezeni Pesa Kupitia Sanaa Zenu na si Kuhongwa na Kuja Kututambishia

$
0
0
Wema Sepetu
KWENU warembo wa Bongo Movies, Wema Sepetu ‘Madam’ na Kajala Masanja. Habari zenu binafsi? Bila shaka ni wazima wa afya na mnaendelea na majukumu yenu ya kila siku. Kitambo kidogo sijawaona lakini naamini pumzi ya bure mnaendelea kuivuta ndiyo maana nasikia matukio yenu kwenye vyombo vya habari.

Mkitaka kujua afya yangu, mimi ni mzima. Namshukuru Mungu naendelea na shughuli zangu kama kawaida. Mungu ni mwema sana, anaendelea kubariki kazi ya mikono yangu, namuomba yeye aendelee kunibariki zaidi na zaidi.

Dhumuni la kuwaandikia barua hii ni kutaka kuwakumbusha kwamba nyinyi kwa sasa ni watu wazima. Umri wenu unatosha kabisa kusema haufanani na yale matukio yasiyokuwa na kichwa wala miguu. Mara kadhaa nimewahi kuwaambia, hata yale mashindano yenu ya kumwaga fedha ukumbini, nyakati hizi si zake.

Mambo ya kuibiana mabwana kama yalishatokea, itoshe sasa kusema ulikuwa ni ujana. Kwa kuwa ilitokea, hakuna namna zaidi ya kuyasahau na kuchapakazi. Soko lenu la filamu bado haliridhishi, lakini mnapaswa kukomaa ili angalau mtengeneze fedha kupitia kazi zenu na si kuhongwa.
Binafsi sikufurahishwa na tukio lenu la kukutana ukumbini na kuzinguana mbele ya kadamnasi lililoripotiwa wiki iliyopita na magazeti Pendwa. Lilikuwa tukio linaloonesha kwamba bado hamjakua kitu ambacho sitaki kukiamini.
Wema na Kajala

Kama nilivyotangulia kusema hapo awali, huu siyo wakati wa nyinyi kuoneshana ubabe wa fedha. Kwamba eti kwa kuwa mwenzako kaenda kutunza msanii jukwaani, na wewe lazima utunze nyingi zaidi ili uonekane wewe ni zaidi.

Ndugu zangu, bahati nzuri maisha  yetu tunajuana. Kwa kiasi kikubwa natambua maisha ya wasanii wetu nchini hususan warembo. Wengi wenu hamtegemei sanaa kuendesha maisha yenu. Wengi mnategemea  mapedeshee au ‘mabwana’ kutamba mjini.
Niwashauri hizo fedha mnazozipata ni bora mngewekeza kwenye sanaa yenu. Mkajizatiti vizuri ili ziweze kuzaliana. Mnapigana ili iweje? Mnatambiana mbele za watu inawasaidia nini. Wenzenu wanapigana siku hizi wanaingiza fedha.

Nyinyi kazi yenu si ubondia. Kazi yenu ni uigizaji. Igizeni kwelikweli na Watanzania wawaunge mkono kwa kununua kazi zenu. Sanaa yenu ina changamoto nyingi, mnawezaje kuzishughulikia ikiwa hamna umoja.

Mtawezaje kutatua changamoto hizo ikiwa hamna upendo kati yenu? Si rahisi kutatua changamoto hizo wakati mna chuki. Ili mfanikiwe, mnahitaji kushirikiana. Shirikianeni ili muweze kuisogeza sanaa mbele, acheni vita ya kipuuzi mnayoendelea kuifanya.

Mkizingatia hayo niliyowaambia, hakika tutaona mabadiliko kwenu na sanaa kwa ujumla. Nina imani nyinyi ni watu wazima na mtajipanga upya na mtaanza kuchapa kazi kama kauli mbiu ya rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. John Pombe Joseph Magufuli, ‘Hapa Kazi Tu’.

Ni mimi mtu wenu,
Erick Evarist.

Kasi ya Magufuli Yamzindua Usingizini Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta.....Nae Awapiga Chini Mawaziri Wote Wenye Kashfa Za Ufisadi

$
0
0
Uhuru Kenyatta
Rais wa Kenya, Uhuru Kenyatta amefanya mabadiliko katika Baraza la Mawaziri na kuwapiga chini mawaziri wote ambao wizara zao zinakumbwa na kashfa za ufisadi.

Uamuzi wa Rais Kenyatta umekuja siku moja baada ya kutangaza ufisadi kama tishio la usalama wa kitaifa huku akiazimia kufanya mabadiliko makubwa kwenye ofisi ya Rais hivi karibuni.

Katika mabadiliko hayo, Kenyatta ameongeza pia idadi ya wizara kutoka 16 hadi 20 na kuongeza idara mpya chini ya wizara hiyo, kutoka idara 26 hadi 41 kwa kile alichoeleza kuwa ni kusaidia wizara kutekeleza majukumu yao bora zaidi.

Baadhi ya mawaziri walikuwa tayari wamekwisha jiondoa kwenye wizara zao kwa tuhuma za ufisadi huku wengine wakiwa na kesi za kujibu mahakamani.

Hivi karibuni, Waziri wa Ugatuzi, Anne Waiguru alikuwa wa mwisho kujiondoa kwenye wizara akiwa na kashfa zilizopata umaarufu zaidi kwa kipindi cha hivi karibuni za kununua kalamu moja kwa shilingi zaidi ya 200,000 za Tanzania.

Hata hivyo, Uhuru Kenyatta hakuwa na budi ya kuvunja baraza lake na kuunda upya kwa kuwa katiba ya nchi hiyo inataka idadi ya mawaziri isiwe chini ya 14. Baada ya Waiguru kujiuzulu nafasi ya uwaziri, baraza la mawaziri lilibaki na mawaziri 13 pekee.

Baraza la Mawaziri: Magufuli Kefyeka Nusu ya Wizara za Kikwete

$
0
0
Dr John Magufuli 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. John Magufuli, anatarajiwa kuzifuta wizara 15 kati ya zilizopo sasa na kubaki na baraza dogo litakalokuwa na wachapakazi makini ili kutimiza dhamira yake ya kubana matumizi na kuinua maisha ya Watanzania.

Kadhalika, inaelezwa kuwa Dk. Magufuli aliyeahidi kuleta mabadiliko ya kweli wakati akiomba kura kwa Watanzania kabla ya kuibuka na ushindi wa asilimia 58.46 dhidi ya wapinzani wake katika uchaguzi mkuu Oktoba 25, sasa yuko mbioni kutangaza baraza lake la mawaziri litakalokuwa na wizara 15, idadi inayofanana kwa kiasi kikubwa na ile ya Baraza la Mawaziri la miaka ya 1980 lililoundwa na Rais wa Awamu ya Kwanza, Baba wa Taifa hayati Mwalimu Julius Nyerere.

Serikali ya awamu ya nne ya Rais Jakaya Kikwete, ilimaliza muda wake Novemba 5, 2015  ikiwa na Wizara 30. Kadhalika, alipoingia kwa mara ya kwanza mwaka 2005, Rais Kikwete alikuwa na serikali kubwa yenye mawaziri na naibu wao zaidi ya 60.  

Kufikia leo, Rais Magufuli aliyeapishwa Novemba 5, mwaka 2015, tayari ameshamteua Mbunge wa Ruangwa, Kassim Majaliwa, kuwa Waziri Mkuu wa serikali yake ya awamu ya tano na Ijumaa iliyopita alizindua rasmi Bunge la 11.

Chanzo kimoja cha uhakika kimedokeza jana kuwa hivi sasa, tayari Rais Magufuli kwa kushirikiana na wasaidizi wake, ameshakamilisha sehemu kubwa ya mchakato wa kuunda baraza lake la mawaziri na kwamba, kinachosubiriwa sasa ni kulitangaza wakati wowote kuanzia sasa.

Chanzo hicho kilidai kuwa Dk. Magufuli ambaye amejichimbia mjini Dodoma tangu mwishoni mwa wiki iliyopita, anatarajiwa kutangaza baraza lake dogo la mawaziri wakati wowote kuanzia leo.

“Halitakuwa sawa na hili alilomaliza nalo Rais Kikwete… na wala halitakuwa na watu wengi kama lile aliloingia nalo kwa mara ya kwanza Rais Kikwete mwaka 2005. Ni baraza dogo tu na wizara kadhaa hazitakuwapo,” kilisema chanzo hicho.

Kwa mujibu wa ibara ya 55 (1) ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, mawaziri wanakuwa wajumbe wa Baraza la Mawaziri na pia kwa mujibu wa ibara ya 54, mawaziri huteuliwa na rais baada ya kushauriana na Waziri Mkuu.

“Kuna mambo madogo bado hayajakamilika… baada ya hapo Mheshimiwa Rais atalitangaza Baraza la Mawaziri siku yoyote kuanzia leo. Kimsingi mkakati wake ni kuwa na baraza dogo lenye wizara 15,” kilieleza chanzo hicho.

Aidha, ilielezwa zaidi kuwa sura kadhaa katika baraza hilo dogo zitakuwa mpya na kwamba, mawaziri waliokuwamo katika serikali ya awamu ya nne wana nafasi ndogo ya kuteuliwa katika baraza hilo.

“Kwa kiasi fulani Baraza hili jipya linafanana na lile la Serikali ya Mwalimu Nyerere miaka ya 1980… lina wizara chache sana, zenye lengo la kubana matumizi ya serikali lakini likiwa na uhakika wa kuchapa kazi usiku na mchana ili kutimiza lengo la Rais Magufuli katika kuwaletea maisha bora Watanzania,” chanzo kiliongeza.

Kumbukumbu zinaonyesha kuwa miaka ya 1980, Mwalimu Nyerere alikuwa na serikali yenye wizara 15; ambazo ni Wizara ya Elimu; Wizara ya Mipango; Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa; Wizara ya Mambo ya Ndani; Wizara ya Ujenzi; Wizara ya Mawasiliano na Uchukuzi na Wizara ya Kazi na Ustawi wa Jamii.

Wizara nyingine wakati huo ni Wizara ya Habari na Utamaduni; Wizara ya Afya; Wizara ya Nishati, Madini na Maji; Wizara ya Sheria;  Wizara ya Viwanda na Biashara; Wizara ya Kilimo na Wizara ya Fedha.

Jacqueline Wolper Aeleza Jinsi Anavyompenda Mpenzi Wake...Awapa Wadada wa Mjini za Uso

$
0
0
Muigizaji wa filamu za Bongo, Jacqueline Wolper baada ya kuvalishwa pete ya uchumba na mpenzi wake miezi miwili iliyopita, jana amemwandikia ujumbe mzuri wa siku yake ya kuzaliwa kuonesha jinsi anavyompenda.

Kupitia ukurasa wa Instagram wa Wolper ameandika: “100% Comfort zone… Who else understands and accepts all of me? Who else can I count on for comfort and security? Who else can I call at any hour of the day or night? Who else rallies behind me in my good decisions and are there to help me through the consequences of the bad ones? Not many people are as blessed as I am with someone like you in their lives. I bless the heavens for the wonderful gift of you my PUTIN.
Thanks for completing me.. HAPPY BIRTHDAY MY ROCK”

Katika hatua nyingine Wolper aliweka post nyingine na kuandika: “Nasikia mjini kuna nyakunyaku sasa jamani mtu mzima unanyakuliwaje? me nasema ukininyakulia nikakuachia labda kama simpendi lakini kama nimempenda anyakuliwi mtu ubabisha jaribu shuwainiiii ….na nyie wadada wamjini acheni habari zakuibiana mabwana na kutangazana insta kma umeshindwa kumuifadh bwanaako vzuri akanyakuliwa basi tulia tulii… tafuta mnyonge nawe umnyakulie syo maneno kila sku tukitagiwa kwenye umbea ukisoma ni mambo ya nyaku nyaku sasa we ulinyakuliwa ulikua wapi? paka unyakuliwe nyakuliwa danga maana kila mtua analitaka hilo danga lkn usinyakuliwe bwana maana paking mjini shida… kila mtu ataki kua side chick sasa vipi ulegee unanyakuliwa tuu…so wapenzi wangu nimeongea yote haya kwa sababu ya nyie mashushu wakunitag kwenye umbea wamabwana kunyakuliwa mwanamke kwanza anayegombania bwana me naona soko litakua limeshuka ndo maana unalalamika sawa inauma kwakua umemzoea lkn aina sababu yakugombana kama mwenzio kakuzidi we kata mti panda mti ananyakuliwa nawenyakua maisha yaendelee..unalilia ndani nn nakutoa siri zako kwa mashoga wakat mashoga wenyewe wanafk tuu mfyuuu …nyakua nikunyakulie…mada yaleo hyo haya wakunyakua nakunyakuliwa tiririkeni hapa.”

Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Awasweka Rumande Maofisa Ardhi 10 Kwa Masaa 6

$
0
0
Paul Makonda
Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Paul Makonda leo amewaweka ndani kwa saa sita maofisa ardhi zaidi ya 10 huko Kawe baada ya kuchelewa kufika eneo walilokubaliana kukutana.

Makonda jana alikuwa amewataka Maofisa hao  kufika eneo la Nakasangwe Kata ya Wazo leo asubuhi kutoa ufafanuzi wa mgogoro wa ardhi lakini wao wakafika saa 5.

Semina Na Makongamano Yote Ya Serikali Kufanyika Online Kwa Tele-conferencing......... Hakuna Tena Posho Za Vikao Wala Viburudishaji

$
0
0
SERIKALI kupitia Menejimenti ya Utumishi wa Umma Ofisi ya Rais imesema haitagharamia gharama zozote za kuendesha vikao kazi na watendaji wake kuanzia sasa, badala yake vikao hivyo vitaendeshwa kwa kutumia Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHEMA).

Wahusika wakuu wa vikao kazi hivyo ni pamoja na Wakurugenzi, Makatibu Tawala wa Mikoa na Maafisa Utumishi wa Mamlaka za Serikali za Mitaa.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Jijini Dar es Salaam, Florence Temba, Mkuu wa Kitengo cho Mawasiliano Serikalini na Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma, amesema kuwa, kupitia utaratibu huo washiriki wa vikao hivyo watabaki katika maeneo ya kazi ambapo wataunganishwa na mtandao wa pamoja kwa mfumo wa kuonana na kuongea uso kwa uso.

“Tulianzisha mfumo huo ili kupunguza gharama zisizo na ulazima ambapo awali ilitakiwa kila kunapokuwa na kikao lazma watumishi wasafili kuja Dar es Salaam kwaajili ya mkutano lakini kwa sasa tutatumia Video Conference iliyounganishwa kwenye mikoa yote nchini. Tumeokoa gharama za nauli, mafuta, chakula na malazi,” amesema Temba.

Temba ameeleza kuwa, hatua za utekelezaji wa teknolojia hiyo ulianza kufanyika tangu mwishoni mwa mwaka 2013 hadi sasa ambapo umekamilika na kufanyiwa majaribio yaliyofauli kwa kufanya mikutano kumi ambayo iliunganisha mikoa yote kasoro mitatu ambayo ni mipya ambayo ni, Njombe, Geita na Simiyu.

Kuhusu miondombinu ya mawasiliano amewatoa hofu watumishi kwa kusema: “Mfumo huo ni salama hakuna haja ya kuhofia kuhusu kukatika kwa umeme au hali ya hewa kwani mpango huo unaratibiwa na serikali hivyo ikitokea hali kama hiyo kutakuwepo na umeme wa ziada au kwa kutumia mkongo wa Taifa wa mawasiliano.”

Mtazamo wa Kisheria wa Sakata la Mkuu wa Wilaya Kuwasweka Rumande Maofisa Ardhi.........Hapa Kuna Video Pia ya DC Makonda Akitoa Sababu za Kuwatia Ndani

$
0
0
Na. Julius Mtatiro,
Nilipo- post juu ya jambo hilo mjadala mkubwa wa wananchi umekuwa ni kutaka kujua sheria inaelekeza nini kwa mamlaka ya wakuu wa wilaya. Kwa uelewa wangu wa shahada ya kwanza ya sheria nimeona niwawekee hapa ufafanuzi wa kisheria kwa ajili ya faida yenu na mjadala mwingine tena.

SHERIA INASEMAJE?
Sheria ya Tawala za Mikoa ya mwaka 1997 (The Regional Administration Act) kwenye kifungu cha 15 (1) imeweka sharti muhimu kwa Mkuu wa Wilaya ikiwa atahitaji kutumia mamlaka ya kuamrisha mtu akamatwe, kifungu hicho kinamtaka afanye hivyo pale tu ambapo atakuwa amejihakikishia kuwa kosa lililotendwa na mhusika athari yake huwa ni kukamatwa na kushtakiwa na tena sheria imeweka masharti ya namna ya kushtaki.

JE KISHERIA DC MAKONDA ANA HAKI YA KUWAWEKA NDANI WATAALAM HAO?
Hapana, kisheria hana mamlaka hayo, Kosa walilotenda watalaam hawa wa ardhi ni la kuchelewa kwenye eneo la kazi, kosa la kuchelewa mahali kwenye majukumu ya kawaida ya kupima ardhi haliwezi kamwe kumfanya mtu ashitakiwe hadi pale ambapo kuchelewa huko kutakuwa kumesababisha madhara makubwa na yanayoweza kuthibitishwa mahakamani.

Kwa hiyo kama Makonda amewaweka ndani anawajibika kwa mujibu wa sheria hii kuwapandisha kizimbani haraka kesho (Jambo ambalo atalikwepa kwani hawana kosa ambalo lina ?amount to being arrested and tried? yaani ?kukamatwa na kushtakiwa?).

JE, MAKONDA AKISHTAKIWA ANAWEZA KUPEWA ADHABU GANI?
Bahati nzuri, sheria hiyohiyo katika kifungu cha 15 (1) imeeleza kuwa ikiwa mkuu wa wilaya atatumia mamlaka yaliyowekwa na kifungu husika kwa maana ya kutumia madaraka yake vibaya, atakuwa ametenda kosa na anaweza kushtakiwa kwa mujibu wa kifungu cha 96 cha Sheria ya Kanuni ya Adhabu (Penal Code).

Kifungu hicho cha 96 (1) na (2) kinaeleza kuwa Mtu yeyote ambaye ameajiriwa kwenye utumishi wa umma (akiwemo Mkuu wa Wilaya) anayetenda au kuamrisha utendekaji wa jambo kwa kutumia vibaya madaraka ya kazi yake, kitendo chochote cha dhuluma ambacho kinazuia haki ya mwingine atakuwa ametenda kosa na akitiwa hatiani anaweza kufungwa miaka mitatu jela.

JE WATAALAM HAO WA ARDHI WANAWEZA KUMSHITAKI MAKONDA?
Ndiyo, wataalam wa Ardhi waliotendewa amri hiyo wanaweza kumshitaki Paul Makonda kwa kitendo chake cha kutumia vibaya madaraka yake lakini bahati mbaya itakayowakuta ni kwamba Sheria hiyo hiyo ya Kanuni ya adhabu kwenye kifungu cha 96 (3) imeweka sharti lingine kuwa Uendeshaji wa shitaka kwa husika hautaanzishwa mpaka kitakapotolewa kibali cha Mkurugenzi wa Mashitaka (Kesi ya Nyani amekabidhiwa ngedere).


Upande wa Pili Wa Shilingi
Kwa nini  mkuu  wa  wilaya  aliamua kuwatia ndani? Wananchi wa eneo husika walikichukuliaje kitendo hicho??

===>>Tazama Video Hii Ya DC  Makonda akitoa sababu za kuwatia nyuma ya Nondo

Rais Magufuli Afuta sherehe za Maadhimisho ya siku ya UKIMWI Kitaifa......Aagiza Fedha za Maandalizi ya Sherehe Hizo Zikanunulie Dawa za Waathirika

$
0
0
Rais John Magufuli amesitisha  maadhimisho ya siku ya Ukimwi kitaifa ambayo yalikuwa yafunguliwe mkoani Singida jana na kufikia kilele chake Desemba mosi mwaka huu mjini humo.

Badala yake Rais Dk Magufuli ameagiza fedha zote ambazo zilitengwa na serikali pamoja na wahisani mbalimbali kwaajili ya maadhimisho hayo zielekezwe kununua dawa kwaajili ya waathirika wa Ukimwi na  vitendanishi.

Akizungumza na moja kwa moja na Televisheni ya Taifa (TBC), Mwenyekiti Mtendaji wa Tume ya Taifa ya Kudhibiti Ukimwi (TACAIDS), Dk Fatma Mrisho, amesema serikali imetoa agizo hilo jana wakati tayari mkuu wa Mkoa wa Singida akiwa ameshafungua maonesho ya maadhimisho hayo.

“Serikali imesitisha maadhimisho ya mwaka huu Singida na badala yake fedha zilizopangwa kwaajili ya maadhimisho ziende zikanunue dawa za virusi vya Ukimwi, dawa za kudhibiti maambukizi ya ukimwi na vitenganishi,” amesema Mrisho.

Dk Mrisho amesema kuwa tayari taarifa za kusitisha maadhimisho hayo zimesha wafikia washiriki na wale walio kuwa njiani kuelekea Singida wamegeuza.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake Dar es Salaam juzi kabla ya sherehe hizo kusitishwa, Mwenyekiti Mtendaji wa Tume ya Taifa ya Kudhibiti Ukimwi (TACAIDS), Dk Fatma Mrisho alisema maadhimisho ya mwaka huu yalikuwa yatanguliwe na maonesho ya wadau yatakayojumuisha huduma mbalimbali zikiwamo za utoaji elimu na burudani.

Dk Mrisho alisema huduma nyingine zilizopangwa kutolewa katika maadhimisho hayo ya wiki moja ni upimaji wa hiari wa watu zaidi ya 3,500  wanaoishi na virusi vya Ukimwi na utoaji ushauri nasaha, upimaji wa shingo ya uzazi, sukari, uzito, damu na kupata elimu itakayotolewa kupitia vikundi vya sanaa na burudani.

Maadhimisho ya mwaka huu yanachagizwa na kaulimbiu ya ‘Tanzania bila maambukizi mapya ya VVU, vifo vitokanavyo na Ukimwi na ubaguzi na unyanyapaa inazewekana.’

Mkuu wa Mkoa wa Singida, Dk Parseko Kone aliwaambia waandishi wa habari ofisini kwake hivi karibuni kuwa maadhimisho hayo yanatarajiwa kuanza Novemba 24 mwaka huu kwenye viwanja vya Peoples Club ambapo uzinduzi utakuwa Novemba 25 kabla ya kilele, Desemba mosi.

Hii ni mara ya tatu tangu Rais Dk Magufuli aingie madarakani kuzuia maadhimisho yanayogharimu fedha nyingi za  sherehe na fedha zake kuelekeza ikanunulie vifaa tiba mahospitalini.

Awali Rais aliagiza fedha zilizotengwa kwaajili ya hafla ya uzinduzi wa Bunge zaidi ya shilingi Milioni 225 ziende kununulia vitanda vya hospitali ya taifa Muhimbili.

Aidha Rais pia alisitisha maadhimisho ya siku ya Uhuru Desemba tisa mwaka huu na badala yake watu wafanye kazi katika maeneo yao ya kazi hasa usafi wa mazingira.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Alhamisi ya Novemba 26, Ikiwemo ya Magufuli Kuzidi Kukaza Uzi Kwa Watumishi wa Serekali

$
0
0
Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Alhamisi ya Novemba 26


Viewing all 104775 articles
Browse latest View live




Latest Images