Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104745 articles
Browse latest View live

Zitto Afunguka..Asema Nguvu ya Lowassa ilikuwa Kubwa Sana Kiasi cha Kuwavurugia ACT Wazalendo Katika Uchaguzi

$
0
0
Kiongozi wa Chama cha ACT Wazalendo, Zitto Kabwe amesema nguvu ya aliyekuwa mgombea urais kwa tiketi ya Chadema, Edward Lowassa ilivuruga mpango wake wa kupokea wabunge 50 kabla ya Uchaguzi Mkuu.

Alisema Lowassa aliyekuwa akiungwa mkono na vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) alikuwa na nguvu kubwa kiasi cha kufanya ACT pia ishindwe kupata wabunge wengi katika Uchaguzi Mkuu uliofanyika nchini Oktoba 25.

Zitto alitoa kauli hiyo alipotakiwa kueleza sababu za ACT kushindwa kutimiza azma yake ya kupokea wabunge 50 kutoka vyama mbalimbali, kabla ya Uchaguzi Mkuu na kupata wabunge wengi baada ya uchaguzi huo kama alivyoahidi miezi michache kabla ya kuanza kwa kampeni.

Alibainisha kuwa chama chake kilifanya mazungumzo na wabunge wengi waliokuwa CCM na Chadema ambao walikubali kujiunga nacho na kushiriki uchaguzi kupitia chama hicho. Lakini mpango huo ulibadilika baada ya Lowassa kujiunga na Chadema na baadaye kuwania urais akiungwa mkono na Ukawa.

“Wabunge wengi walikubali kuungana nasi, wamo wa CCM na wabunge wa upinzani… lakini upepo wa Lowassa uliwabadilisha na hili tusingeweza kulidhibiti kwa kipindi kile,” alisema Zitto na kuongeza kuwa:

“Katika mazingira ya kawaida Lowassa ndani ya Chadema ni watu wachache sana wangekwepa upepo wake. Kwanza haikutegemewa kuwa (Lowassa) anakwenda wapi. Wapo walioamini kuwa anakuja kwetu (ACT), lakini ukweli ni kuwa hatukuwa na mazungumzo kati yetu (ACT) na Lowassa, ingawa kulikuwa na wish (matakwa) ya kuwa na coalition (umoja) kubwa zaidi ya kuunda kambi ya upinzani.”

Kwa nini ACT haikujiunga Ukawa
Zitto alisema sehemu kubwa ya waliounda ACT walitoka Chadema, hivyo kulikuwa na mazingira magumu ya kufanya kazi pamoja tena.

“Sisi tuliweka sharti moja, katika mazingira yoyote ya kufanya kazi pamoja, kwa matokeo yoyote yatakavyokuwa, moja ya ajenda ilikuwa kurejesha miiko ya uongozi jambo ambalo wenzetu hawakuwa tayari kutangaza mali,” alisema Zitto.

Lakini, mwisho baada ya majadiliano, ACT waliona kwa chama hicho ambacho kinaanza, kikiingia kwenye muungano na vyama vikubwa kingeweza kumezwa hivyo ni vizuri kwenda wenyewe ili wapate fursa ya kujitangaza kwa kuweka wagombea katika kila jimbo.

Ulikuwa uchaguzi wa ovyo
Akitoa maoni yake kuhusu uchaguzi uliopita, Zitto alisema ulikuwa mgumu, usioeleweka na uliokosa ajenda za wananchi. Badala yake, ulilenga mapambano ya wagombea na si sera.

“Uchaguzi ulikuwa kati ya CCM na Ukawa, ulikuwa ni kati ya (John) Magufuli na (Edward) Lowassa. Ulikuwa kuhusu personalities (watu) na siyo issues (hoja), naweza kusema ulikuwa miongoni mwa uchaguzi wa ovyo kweli kuwahi kutokea nchini,” alisema Zitto.

Aliongeza kuwa uchaguzi wa mwaka huu ulikuwa tofauti na wa miaka ya nyuma kutokana na kuwa wagombea wote wenye nguvu walikuwa ndani ya mfumo.

“Usingeweza kuwatofautisha wagombea wote waliokuwa au waliotokana na mfumo uliopo… ilikuwa vigumu kuacha kumfananisha mgombea wa CCM na yule wa Ukawa, wote ni walewale usingetegemea chochote. Kwa hiyo sisi (ACT) hata tungejitahidi tusingeweza kufanya kitu ni mara chache sana tulikuwa tukisikika,” alisema.

Kwa mujibu wa Zitto, uchaguzi uliopita ulikuwa mgumu na usio na ajenda ikilinganishwa na wa mwaka 2010.

“Kumbukeni uchaguzi wa mwaka 2010, vyama vilibishana kuhusu ajenda, baada ya uchaguzi watu walikuwa na ajenga ya uchaguzi, lakini angalia sasa wapinzani au vyama wanajadili nini, hakuna,” alisema.

Alisema ajenda ya kupinga ufisadi na rushwa iliyokuwa ikitumiwa na wapinzani, sasa imechukuliwa na Rais Magufuli.

“Sasa watu wanasubiri kusikia Rais atasema nini, watu wamesahau kwamba hakuna Baraza la Mawaziri, lakini nchi inakwenda… hata ile hoja ya Ukawa ya kutomtambua Magufuli haipo tena,” alisema.

Upinzani umepoteza
Zitto anasema anachokiona ni wapinzani umepotea kutokana na ajenda yao ya ufisadi kuchukuliwa na Rais Magufuli.

“Sasa unasikia Magufuli anakuwa mkali sana kuhusu rushwa na ufisadi jambo ambalo zamani halikuwapo naweza kusema tumebadilishana. Zamani ilikuwa wapinzani wanazungumzia rushwa na CCM wanaitetea Serikali, lakini sasa majukumu yamebadilika,” alisema.

Alisema kwa sasa sauti ya wapinzani katika hoja haisikiki na badala yake anasikika Rais Magufuli pekee ambaye amekuwa Serikali na upinzani wakati mmoja.

“ Hii itaimarisha zaidi demokraia kwa sababu kwa muda mrefu upinzani umekuwa ukitegemea matukio kujenga au kufanya siasa, itabidi sasa upinzani uendane na hoja katika siasa… lakini mwisho wa siku tunaangalia mwananchi anafaidika na nini? ” alihoji.

Nafasi ya wapinzani siasa za Tanzania
Zitto alisema kwa ujumla wapinzani wameanza vizuri kwani licha ya kuwa anachofanya Rais Magufuli kuhusu rushwa kinaonekana kukonga nyoyo za Watanzania, ukweli unabaki kuwa CCM imechokwa.

“Upinzani una wabunge wengi sana ndani ya Bunge, 122, kwahiyo tunaweza kujipanga na kufanya kazi ya kuionyesha Serikali matatizo yake wakati wote na hiki ndicho tulichokuwa tukifanya…Lakini tunayoiona sasa hivi ni kuwa hatujui, je, nguvu ya Magufuli, ni yake peke yake au ni nguvu ya taasisi? Na kama ni yake CCM itakuwa ni ile ile na mashambulizi dhidi ya CCM yatakuwa yaleyale,” alisema.

Mtazamo wake kwa Rais Magufuli
Zitto anamwona Rais Magufuli kama kiongozi aliyekosa msingi, kwani alichaguliwa bila makundi, hivyo kila anachofanya kinapaswa kuwafurahisha wananchi ili apate kuungwa mkono.

Alisema kwa muda mrefu wabunge walionekana kuwa na nguvu kwa kuwa pale Bunge lilipokuwa likipambana na Serikali, wananchi walikuwa nyuma ya Bunge, lakini sasa hali inaweza kuwa tofauti.

“Kwa namna ya uongozi wa Magufuli, Bunge linaweza kukosa nguvu kwani likijaribu kumkwamisha atatetewa na wananchi. Wakimpinga (Magufuli) wananchi watawapinga (wabunge). Na Magufuli alivyo anaweza kusema turudini kwenye uchaguzi, maana akivunja Bunge tunarudi kwenye uchaguzi kwani ana uhakika yeye atashinda, lakini wabunge hawatakubali kuingia kwenye gharama za uchaguzi tena.”

Tutampima Magufuli kwa posho
Wabunge wanataka kukopeshwa Sh 130milioni badala ya Sh90milioni, je Zitto anasemaje?

“Tumuangalie, Je, atasalimu amri kwa shinikizo la wabunge la kuongezewa mkopo wa gari au atatia mguu kwenye kiasi ambacho wabunge walilipwa mwaka 2010… akisalimu amri ina maana ni mtu ambaye atataka ushirikiano na Bunge, lakini akitia mguu ina maana ana msimamo,” alisema na kuongeza: “Wabunge huwa wanakimbilia kusema tutazuia bajeti, Je, atatishika. Bado tuna muda wa kutosha wa kuweza kumsoma Magufuli na kuona ni jinsi gani wanakwenda.”

Kuna uamuzi ambao tayari ameanza kuhusu kurejesha mashamba ambayo hayajaendelezwa, lakini lipo suala la viwanda. Je, anafanya nini kuhusu nguo kutoka nje, kuna ukwepaji mkubwa sana wa kodi na viwanda vya Tanzania,

Zitto anaenda mbali kwa kusema kwa Rais wa aina ya Magufuli ni lazima kuwe na namna ya kumdhibiti kwani Watanzania watajikuta wanatengeneza ‘dikteta’.

Alisema ili kuendana na kasi ya kiongozi huyo wa nchi, inatakiwa kuwa na Bunge imara.

“Bunge ni lazima libadilike, liache kushambulia watu na badala yake lijikite kwenye hoja na kwa jinsi Magufuli alivyo wapo wabunge wengi wataathirika na maamuzi yake… wapo wabunge ambao wapo kwenye matukio ya rushwa, wafanyabiashara ambao wataguswa na maamuzi yake, kwa hiyo kwa mwaka mmoja tutashuhudia mengi, ” alisema.

Zari wa Diamond na Mama Diamond ni Vita Kwa Kwenda Mbele....Mama Hamtaki Mkwe, Zari Atoa Masharti

$
0
0
NI vita! Baada ya staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’ kwenda nchini Afrika Kusini ‘Sauzi’ kumwangukia mzazi mwenzake, Zarinah Hassan ‘Zari’ kufuatia kuwepo kwa figisufigisu kati yao huku mama wa msanii huyo, Sanura Kassim ‘Sandra’ akihusishwa, mazito yameibuka.

TUJIUNGE NA CHANZO
Habari kutoka chanzo cha ndani ya familia ya Diamond zinamwagika kwamba, Zari amekubali kuja Bongo lakini akatoa sharti: “Nakuja Bongo, Desemba 8, lakini mama (mama mkwe) aondoke pale nyumbani (Tegeta-Madale, Dar).”

ZARI ATIA NGUMU, AKUBALI
Chanzo hicho kilimwaga ‘ubuyu’ kwamba, awali Zari alimtilia ngumu Diamond lakini baadaye alikubali kurejesha amani kama ilivyokuwa zamani hivyo watakuja wote Bongo baada ya kujiachia vya kutoka huko Sauzi nyumbani kwa mwanadada huyo.


DIAMOND KICHEKO SAUZI
Kuhusu kuweka mambo sawa na kuwa atarejea Bongo na Zari na mtoto wao, Latiffah ‘Tiffah’, Diamond alilidokeza gazeti hili kwamba, sasa ni ‘full’ kicheko na anamshukuru Mungu kwa kufanikisha kufanya mambo kuwa kama mwanzoni.
Alitamba kuwa atatinga Bongo wiki hii au mapema wiki ijayo akiambatana na familia yake kwani kwa sasa wapo poa na hakuna manenomaneno tena.
“Nakuja na familia yangu. Kwa sasa tupo poa sana na maisha yanaendelea. Kiukweli huku South (Sauzi) tuna amani sana,” Diamond aliliambia gazeti hili wikiendi iliyopita.

TURUDI KWA CHANZO BONGO
Ilidaiwa kwamba, baada ya mama Diamond kusikia kuwa, mwanaye atarejea Bongo, Desemba 8, mwaka huu akiambatana na Zari alianza kuhaha kwa vile alishamtolea maneno makali akidai kuwa, mkwewe huyo alikuwa analeta uzungu kwenye familia yake.
“Unaambiwa ndugu wanapomuonesha mama Diamond picha za Zari akijiachia na Diamond na mtoto wao, Tiffah, anaamini kweli anaweza kuja Bongo jambo ambalo hataki kulisikia,” kilisema chanzo hicho.

MAMA DIAMOND KAMA MAGUFULI
Kufuatia hali hiyo ilitonywa kuwa, mama Diamond alifunguka kimipasho:
“Hata kama akija ataondoka kurudi kwao kama alivyokuja kwani ‘Hapa Kazi Tu’ kama ilivyo kauli mbiu ya Rais John Pombe Magufuli.”
Ili kupata mzani wa habari hiyo, mmoja wa vijumbe wetu alimtafuta mama Diamond kwa njia ya simu ambapo aliwaka mara tu baada ya kuulizwa ishu hiyo.
Katika majibu yake ya hasira, mama Diamond alisema haogopi lolote na yupo tayari kwa lolote.

MSIKIE MWENYEWE
“Siogopi chochote Zari kurudi hapa, kama atakuja, atakuwa amekuja kama alivyokuja mwanzoni na ataondoka hivyohivyo kama alivyoondoka awali.
“Sasa kwani nina hofu gani wakati niko nyumbani kwangu hapa? Watu watuache na waache unafiki wa kufuatilia mambo ya watu,” alisema mama D kisha akakata simu.

TUJIKUMBUSHE
Mapema baada ya Zari kujifungua mtoto wa Diamond, kuliibuka maneno ya mama mkwe huyo kutoelewana na mama Tiffah ambapo mara tu baada ya sherehe ya 40 ya mtoto huyo, Zari alitimka Bongo kwa maelezo kwamba hatarejea lakini sasa anaweza kuja kupambana tena na mama mkwe wake anayeonekana bado ana jambo moyoni.

Imeandikwa na Gladness Mallya, Mayasa Mariwata na Musa Mateja
GPL

Nafasi za Ajira Tanzania Women's Bank PLC, Application Deadline 04 December, 2015

$
0
0
Tanzania Women's Bank PLC
Position Advertisement

Tanzania Women's Bank is seeking to recruit dynamic, honest, result oriented and committed to fill the following roles:

Bonyeza Hapa Kusoma Ajira zote zilizotangazwa na Bank hiyo leo =>WWW.AJIRAYAKO.COM


Au Bonyeza HAPA

Rais Magufuli kaamua Bilioni zilizokua zitumike sherehe za uhuru 9 Dec matumizi yake yawe kama ifuatavyo.

$
0
0

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli ameamuru fedha zilizopaswa kutumika kugharamia shamra shamra za siku ya Uhuru ambazo zingefanyika tarehe 09 Desemba 2015, kutumika kufanya upanuzi wa barabara ya Mwenge hadi Morocco jijini Dar es Salaam yenye urefu wa kilometa 4.3 kwa kuongeza njia mbili za barabara za lami.

Tayari fedha hizo kiasi cha shilingi bilioni nne zimepelekwa kwa wakala wa barabara hapa nchini TANROADS kwa ajili ya utekelezaji wa agizo hilo, linalopaswa kuanza mara moja
Akizungumza na Mtendaji Mkuu wa TANROADS Mhandisi PATRICK MFUGALE Ikulu Jijini Dar es Salaam, Dkt. Magufuli ametaka ujenzi wa barabara hiyo uanze haraka ili kukabiliana na adha ya msongamano wa magari katika barabara hiyo

Kujengwa kwa njia hizo kutaifanya barabara ya Morroco hadi Mwenge kuwa na njia tano.

Wakati huo huo, Rais John Magufuli amekutana na kufanya mazungumzo na Mwenyekiti Mstaafu wa Chama Cha wananchi (CUF) Prof. Ibrahim Lipumba Ikulu Jijini Dar es salaam.

Katika Mazungumzo hayo Prof. Lipumba amempongeza Dkt. Magufuli kwa kuchaguliwa kuwa Rais wa awamu ya tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na pia kwa kutoa hotuba nzuri ya uzinduzi wa Bunge la 11 la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania iliyokonga nyoyo za Watanzania.

Kwa Upande wake Rais Magufuli amempongeza Prof. Lipumba kwa msimamo wake thabiti wa kupinga ufisadi na amemtakia heri katika shughuli zake.

Gerson Msigwa
Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano, IKULU.
Dar es Salaam.
30 Novemba,2015

Rais John Magufuli na Waziri Mkuu Majaliwa Wamuibukia Samia Suluhu Hassan Ofisini Kwake

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli (kushoto) akiagana na Makamu wake, Mhe. Samia Suluhu Hassan (katikati) na Waziri Mkuu, Majaliwa Kassim Majaliwa (kulia) baada ya mazungumzo yao yaliyofanyika Ofisini kwa Makamu wa Rais Ikulu jijini Dar es Salaam, leo Nov 30, 2015. Wa pili (kulia) ni Naibu Katibu wa Makamu wa Rais, Mohamed Khamis
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli, (kushoto) akizungumza na Makamu wake, Mhe. Samia Suluhu Hassan (katikati) na Waziri Mkuu, Majaliwa Kassim Majaliwa, wakati Rais na Waziri Mkuu walipomtembelea Makamu Ofisini kwake Ikulu jijini Dar es Salaam, leo Nov 30, 2015 kwa mazungumzo.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli, (kushoto) akizungumza na Makamu wake, Mhe. Samia Suluhu Hassan (katikati) na Waziri Mkuu, Majaliwa Kassim Majaliwa, wakati Rais na Waziri Mkuu walipomtembelea Makamu Ofisini kwake Ikulu jijini Dar es Salaam, leo Nov 30, 2015 kwa mazungumzo.

Nafasi za Kazi Tanzania Posts Corporation, Assistant Postal Officers (8 Posts) And Senior Economist II

$
0
0

Ingia Kwenye Website Ifuatayo Uweze Ku Apply Kazi Hizo zilizotangazwa Katika Gazeti la leo la Daily News =>> www.ajirayako.com

Zitto Kabwe Ayafungukia Makampuni Makubwa Tanzania Ambayo Yanakwepa Kodi....

$
0
0
By Zitto Kabwe
Kutoka Hotuba ya Waziri Mkuu 26.08.2011 – Makampuni yanayoogoza kwa kulipa kodi

Note: (Highlights)
Only one Mining company (the smallest i.e. - Resolute Mining), only one telecom company(Airtel Tanzania).
Household names like: 
MeTL, Bakhresa/Azam, IPP, VodaCom, Coca cola, Pepsi(SABCO), Serengeti Breweries, Barrick Gold, ACACIA, AngloGold Ashanti not seen. No oil marketing companies pia.
One can conclude that, TBL is the most profitable company in Tanzania, NMB is the most profitable Bank.
A public debate is needed. Hili ni tatizo kubwa.
Here under is the an extract from the Prime Minister speech; Sehemu ndogo ya hotuba ya Waziri mkuu.
Mheshimiwa Spika,
1. Nitumie nafasi hii kuwapongeza baadhi ya Walipakodi Wakubwa kwa Serikali na ambao wamefanya vizuri kati ya kipindi cha mwaka 2005 na 2011. Kwa kipindi hicho, Makampuni yaliyoongoza kwa kulipa kodi ni pamoja na:
  1. Tanzania Breweries Ltd. (Tshs 165.4b)
  2. National Microfinance Bank (Tshs 108.6b);
  3. Tanzania Cigarette Company (Shilingi Bilioni 92.1);
  4. National Bank of Commerce (Shilingi Bilioni 89.9);
  5. CRDB Bank Ltd. (Shilingi Bilioni 79.2);
  6. Tanzania Ports Authority (Tsh 76.8b);
  7. Tanzania Portland Cement (Tshs 73.4b);
  8. Airtel (T) Ltd. (Shilingi Bilioni 63.6);
  9. Tanga Cement Company Ltd. (Tshs 43.6 b);
  10. Standard Chartered Bank Ltd. (Tshs 40.0b );
  11. Citibank (T) Ltd. (Shilingi Bilioni 35.7);
  12. Resolute (T) Ltd. (Tshs 32.1b );
  13. Tanzania International Container Terminal Services (Shilingi Bilioni 25.9);
  14. Tanzania Distillers Ltd. (Tshs 13.4 b); na
  15. Group Five International (PTY) Ltd. (Tshs Bilioni 9.5).

2. Napenda kutoa rai kwa Makampuni yote Nchini kuiga mfano huu mzuri. Wito wangu kwa Makampuni, Wafanyabiashara Wakubwa kwa Wadogo na Wananchi wote ni kuongeza juhudi katika kufanya biashara zao ili zizalishe kwa wingi na kupata faida kubwa zaidi. Faida kubwa itachangia katika kuongeza Mapato ya Serikali kwa njia ya Kodi na hivyo kusaidia kukuza uchumi, kuongeza Pato la Taifa na la Mwananchi mmoja mmoja na kuondoa Umaskini. Niwadhihirishieni kwamba, Serikali inatambua umuhimu wao kwa maendeleo ya Nchi yetu na itahakikisha inaongeza juhudi zake za kuweka Mazingira Wezeshi kwa Makampuni hayo kufanya shughuli zao vizuri ili kuwezesha kulipa Kodi kwa mujibu wa Sheria.
Issues, issues, issues

Upotevu wa Makontena 349 Bandarini: Watu 12 Watiwa Mbaroni na Jeshi la Polisi

$
0
0
Kufuatia agizo la Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa la kuwataka watuhumiwa wa wizi wa makontena 329 katika bandari ya Dar es salaam kuchukuliwa hatua na Jeshi la Polisi, tayari Jeshi hilo limewashikilia watuhumiwa kumi na mbili wanaohusika na wizi huo.

Akiongea na waandishi wa habari leo Jijini Dar es salaam,  Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (CP) Diwani Athumani amesema kuwa, uchunguzi unaofanywa na wataalamu waliobobea katika makosa ya uhalifu wa kifedha umeweza kuwabaini watu kumi na mbili  ambao wamehusika na wizi huo.

“Kati ya watuhumiwa hao kumi na mbili, watano wanashikiliwa na Jeshi la Polisi na saba bado wapo katika upepelezi na upelelezi utakapokamilika watafikishwa mahakamani,” alisema Kamanda Athumani.

Wanaoshikiliwa kutokana na tuhuma mbalimbali ni Kamishna wa Idara ya Forodha na Ushuru TRA Bw. Tiagi Masamaki, Meneja Kitengo cha Huduma za Ushuru  na Bi.  Habib Mponezia, Msimamizi Mkuu wa Kitengo cha Ushuru wa Forodha.

Watuhumiwa wengine ni pamoja na Bi. Eliaichi Mrema, Msimamizi Kitengo cha Mawasiliano ya Kompyuta  Bw. Haroun  Mpande na Mchambuzi Mwandamizi wa Masuala ya Biashara Bw. Hamis Omary.

Aidha Kamanda Athumani amewaomba wananchi wenye taarifa za ubadhilifu wa mali za Umma kuendelea kulisaidia Jeshi la Polisi katika kutekeleza majukumu yake.

Unajua Athari za Kuitana Sweet, Dear na Baby Kwa Watu Ambao Sio Wachumba ama Mke na Mume?

$
0
0
BABY ni neno la Kiingereza lenye maana ya mtoto, tena mara nyingi linatumika kwa mtoto mdogo. Pia lina maana nyingine ya mpenzi. Ni neno maarufu sana siku hizi; hata wazee kabisa, utasikia wanaitana baby!

Mbali na hilo, yapo maneno mengine kama sweet, dear, honey na mengine mengi. Maneno yote hayo ya Kiingereza, yana maana zaidi ya moja, lakini kubwa zaidi ni kumaanisha mpenzi, mpendwa (hutumika katika kuonesha mapenzi ya dhati kwa mwingine).

Leo nataka kukupa kitu kipya kabisa kichwani mwako. Unahitaji utulivu wa hali ya juu ili kujifunza hili. Ni maneno mazuri sana, ya kipekee lakini kwa upande mwingine ni hatari kwa sababu hukaribisha matatizo ambayo hayakutarajiwa na mtumiaji.

HUTUMIKA WAPI HASA?

“Dear, naomba uniamshe saa 12:00 asubuhi, kesho nina vikao vingi sana asubuhi,” inaweza kuwa kauli ya mume akimwambia mkewe, ambaye naye anamjibu: “Sawa sweet, usijali.”

Kwa hakika ndipo sehemu sahihi zaidi kutumika. Ni maneno yenye mshawasha mkubwa na huonesha penzi la dhati lililopo moyoni mwa mhusika kwenda kwa mpenzi wake.
Husisimua na kuongeza ladha ya mapenzi ya kweli. Kumuita mpenzi wako kwa majina ya kimapenzi 

huongeza zaidi upendo na msisimko wa moyo. Mwenzi hujiona wa kipekee na mapenzi huzidi kukua.
Kwa maana hiyo basi, ni sahihi zaidi kwa wapenzi kuitana majina niliyotaja hapo juu na mengine yanayofanana na hayo kwa lugha yoyote ile, ila iwe inatambulika vizuri na anayetamkiwa.

ATHARI SASA!

Kwa upande mwingine kuna athari za kutumia maneno hayo. Zama hizi, maneno hayo yanaonekana ya kawaida tu. Mtu yeyote anaweza kumuita yeyote mpenzi, honey, baby n.k. Hapo ndipo kwenye tatizo lenyewe.

Kwa ujumla wanawake ndiyo wanaongoza zaidi kuitana majina hayo. Wakati mwingine huenda mbali zaidi na kuwaita hata wanaume majina hayo ya kimapenzi. Si rahisi kuona athari zake kwa haraka na moja kwa moja, lakini zipo na wengi zimewasababishia matatizo. Ngoja tuone..

HUPUNGUZA THAMANI


Kama nilivyotangulia kusema awali, maneno 
niliyotaja hapo juu husisimua na kuongeza mapenzi. Kwa kuyatumia vinginevyo, basi kwa kiasi kikubwa huanza kukuathiri na kupunguza thamani ya neno lenyewe.

Kama unaweza kumwita mfanyakazi mwenzako dear, mtu wa jinsi sawa na wewe sweet ni wazi hata utakapomuita mpenzi wako au wewe kuitwa na yeye, halitakuwa na nguvu sana ya mapenzi kwa sababu ni neno ulilolizoea kila wakati.

HUKARIBISHA USALITI
Wakati mwingine unaweza kujikuta umeingia kwenye usaliti bila kutarajia. Veronica, mfanyakazi wa saluni moja ya kiume iliyopo Sinza, Dar alitoa ushuhuda ufuatao:
“Mimi naishi na mchumba wangu, tuna mtoto mmoja mwenye miaka mitatu. Nafanya kazi saluni. 

Tangu nimeanza hii kazi, nimejifunza kutumia maneno matamu ya kumfurahisha mteja na wakati mwingine kumfanya akupe tipu baada ya kumaliza kazi.

“Kuna kaka mmoja nilizoeana naye sana. Kama kawaida, huwa namkaribisha kwa kumuita dear au sweet. Wakati nikiendelea kumfanyia scrub, mazungumzo yetu hutawaliwa na dear, sweet, nikajikuta nimezidi kumzoea.

“Kwa sababu tulibadilishana namba, mara akaanza kuwa na mazoea ya kunitumia meseji, akija ananipa pesa, anaondoka. Mazoea yakazidi. Nikajikuta nimemzoea na kuna siku ambayo siwezi kuisahau kabisa.

“Ni siku niliyomsaliti mchumba wangu...mbaya zaidi na huyo jamaa naye ana mke wake. Niliumia sana, lakini naamini kama nisingekuwa na mazoea ya kumuita majina ya kimapenzi nadhani nisingeingia mtegoni. Moyo wangu unauma sana, najuta kumsaliti mpenzi wangu.”

Unaweza usione athari hii moja kwa moja, lakini ndugu zangu chukua jambo hili leo; wanaume wengi wakiitwa kwa majina ya kimapenzi husisimka sana – hujiona wenye bahati na mara hushawishika kuingia mapenzi.

Kama mwanamke hatakuwa makini atajikuta ametumbukia. Ya nini yote hayo, wakati unaweza kubadilisha mazoea hayo? 

ANGALIA TOFAUTI
Rafiki zangu, kati ya maneno niliyoyataja, kuna ambayo yanakubalika kutumiwa na wasio na uhusiano lakini wawe na undugu wa damu. Mathalani baba, mama, kaka, dada, shangazi nk.

Hakuna tatizo kumuita mtu mpendwa, lakini siyo baby, sweet, mpenzi na mengine yenye maana ya moja kwa moja ya kimapenzi. Umenipata? Akili za kuambiwa, changanya na zako kisha unazifanyia kazi! Chukua kinachokufaa!
Hadi wiki ijayo kwa mada nyingine. Wewe ni muhimu sana kwangu. 

TOA MAONI YAKO JE NI KWELI NIYASEMAYO?

Madhara ya Kutofanya Tendo la Ndoa Muda Mrefu.

$
0
0

Habari zenu, nimeona niwaletee hili nina imani mtajifunza hasa kwa wale wasiofahamu,Ukikaa Muda Mrefu bila Kufanya tendo la Ndoa madhara yake ni kama haya:
• Hasira za mara kwa mara katika mambo madogo,
• kupendelea sana kuangalia picha za uchi,
• Kusahausahau,

• Kupendelea story za mapenzi,
• Kutokwa damu nyingi wakati wa hedhi (Mke),
• Kupenda kurukiarukia mambo ya watu wengine (tabia ya kufuatilia mambo
yasiyokuhusu),
• Kuumwa na kichwa,
• Kukakamaa mgongo (wanaume),
• Kuingiliwa kirahisi na jini mahaba,
• Kupoteza umakini ktk kazi (efficiency),
• Siku ukikutana kimwili na mwenye virusi bila kinga utaambukizwa kirahisi mno,
• Waweza ku-develop tabia mpya ambayo hukuwahi kuwa nayo ili iwe mbadala
kama ulevi n.k.

Kenyan Guy Narrates The Trick a Desperate Single Mother Used to Seduce Him To S£X (PICTURED)

$
0
0

A Kenyan guy has narrated how he visited a desperate single mother, who happens to be his side-dish, and the trick she used to lure him to s3x.

This is what he had to say;



Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumanne ya Tarehe 1 Disemba...Ikiwemo ya Miss Tanzania Atajwa Ufisadi wa Sh 1.3 Trilioni

$
0
0
Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumanne ya Tarehe 1 Disemba...Ikiwemo ya Miss Tanzania Atajwa Ufisadi wa Sh 1.3 Trilioni










KIMENUKA..Miss Tanzania Atajwa Ufisadi wa Sh1.3 Trilioni

$
0
0
 Aliyekuwa ofisa mwandamizi wa benki ya Stanbic tawi la Tanzania, Shose Sinare amehusishwa na mipango ya kifisadi ambayo imeisababishia Serikali ya Tanzania hasara ya Sh1.3 trilioni kati ya mwaka 2012 na 2013.

Taarifa ambazo gazeti hili limepata kutoka Uingereza na hapa nchini, mwanadada huyo ambaye alikuwa mrembo wa Tanzania mwaka 1996, alishirikiana na aliyekuwa Mkurugenzi Mtendaji wa benki hiyo, Bashir Awale.

Sinare hakupatikana kufafanua suala hilo ilhali Awale alifukuzwa nchini hivi karibuni.

Alipoulizwa jana kuhusu tuhuma hizo, Mkurugenzi Mkuu wa Takukuru, Dk Edward Hosea alisema anatambua suala hilo,  linafuatiliwa na taasisi yake na hakutaka kutoa maelezo zaidi.

Taarifa kwamba Serikali imetumbukia katika kashfa nyingine kubwa ya ufisadi zimebainika baada Taasisi ya Uchunguzi wa Makosa Makubwa ya Ufisadi ya Uingereza (SFO) kuwasilisha mahakamani ushahidi wake kwamba kiasi cha Sh1.3 trilioni kilipotea wakati wa uuzwaji wa hati fungani za Serikali kwa benki ya Stanbic inayomilikiwa na Standard Group ya Afrika Kusini.

Mwanasheria wa SFO, Edward Garnier aliiambia Mahakama ya Southwark Crown ya jijini London, Uingereza inayosikiliza shauri hilo la kibiashara kwamba wakati wa mchakato wa benki kununua hati fungani Awale na Sinare walihusika.

Garnier alisema Awale alifukuzwa kazi Agosti 2013 baada ya kushindwa kutoa ushirikiano kwa timu ya uchunguzi ya ndani na Sinare alijiuzuru Juni 2013 na hivyo naye alifanikiwa kukwepa uchunguzi.

Katika uchunguzi huo, Garnier alisema maofisa hao waliwataka maofisa wa Serikali ya Tanzania wawapatie kwanza kiasi cha Dola za Kimarekani 6 milioni (Sh13 bilioni) ili waweze kufanikisha mkopo wa Dola 600 milioni (Sh1.3 trilioni) na ziingizwe kwenye akaunti za maofisa binafsi wa Serikali. Dola 6 milioni ni asilimia moja ya mkopo huo wa Dola 600 milioni. Garnier alisema mpaka sasa hakuna anayefahamu fedha hizo zipo mikononi mwa nani.

Hii ni mara ya pili SFO inafanikiwa kuibua ufisadi wa mabilioni ya dola kwa maofisa wa Serikali ya Tanzania baada ya ule wa mwaka 2002 ambapo maofisa waliongeza Sh73 bilioni katika bei halisi ya rada kutoka kampuni ya vifaa vya kijeshi ya Uingereza ya BAE Systems.

Watanzania walipopata habari hizo walipiga kelele maofisa waliohusika wachukuliwe hatua lakini Serikali ilikataa. Baadaye yalifanyika makubaliano maofisa wasishtakiwe na BAE pia isishtakiwe, lakini fedha zilirejeshwa nchini.

Katika shauri hili yanataka kufanyika makubaliano kama hayo ya awali kwamba Stanbic inayonilikiwa na kampuni ya Standard Group ya Afrika Kusini ambayo ni kampuni tanzu ya Industrial and Commercial Bank of China (ICBC) inatakiwa kulipa Dola 32.2milioni sawa na Sh69 bilioni, ikiwa ni pamoja na kuwalipa SFO Dola 16.0 milioni sawa na Sh36.3 bilioni. Pia inatakiwa kulipa faini ya Dola 6 milioni (Sh12.9) na riba Dola 1 milioni (Sh2.1bilioni) kwa Serikali ya Tanzania.

Zitto Kabwe

Akizungumzia sakata hilo, Kiongozi Mkuu wa ACT Wazalendo, Zitto Kabwe aliitaka Serikali kuwakamata na kuwafikisha katika vyombo vya sheria wote waliohusika na ufisadi huo.  Zitto, kupitia taarifa kwa vyombo vya habari aliyoitoa jana alisema kati ya mwaka 2012/2013, Serikali kupitia Wizara ya Fedha iliuza hati fungani zenye thamani ya kiasi hicho cha fedha, ambapo dhamana za Serikali zilinunuliwa na benki ya Stanbic  inayomilikiwa na benki ya Standard Group ya Afrika Kusini.

“Hata hivyo, sehemu ya fedha hizo hazikuingia kwenye akaunti za Serikali ya Tanzania na pia gharama za bond (hati fungani) hiyo zilipaishwa kupitia wakala wa kati kati (middle men) na hivyo kupelekea rushwa ya takribani $60 milioni (Sh129 bilioni) kutolewa kwa maafisa waliothibitisha biashara hiyo,” alisema.

Stanbic

Hii itakuwa mara ya pili benki ya Stanbic kuingia katika mgogoro baada ya mwaka jana kutuhumiwa kupitisha kiasi kikubwa cha fedha kilichotokana na mgawa wa Sh306 bilioni kutoka Akaunti ya Tegeta.

Baadhi ya maofisa, mawaziri na watu maarufu waliopewa fedha zinazoaminika zilitoka Tegeta Escrow kupitia benki ya Mkombozi walijulikana na wakafikishwa katika Baraza la Maadili, lakini waliopokea fedha kutoka Stanbic hawajulikani ingawa uchunguzi uliofanywa na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) aligundua kwamba watu hao walichukua kwa mifuko ya sandarusi na plastiki.

Source:Mwananchi

Kimbunga cha Magufuli chatua Mashirika ya Umma, ATCL, TRL And Tazara Matumbo Moto

$
0
0
Msajili wa Hazina, Lawrence Mafuru amezitaka taasisi na mashirika ya umma nchini kuacha utegemezi kwa Serikali, badala yake kupunguza matumizi na wafanyakazi ili kuongeza mapato na ufanisi.

Mafuru alisema Serikali imebeba mzigo wa taasisi na mashirika hayo kwa kutegemea izipatia fedha kutoka Hazina kwa ajili ya kujiendesha, na kulipa mishahara ya wafanyakazi na kusababisha ufanisi wao kuwa mdogo.

Mafuru pia alitangaza kufuta posho za wabunge katika bodi za mashirika na kuanzisha mchakato wa kuwaondoa katika mashirika hayo, ili wabaki na jukumu lao la msingi la kuikosoa Serikali badala ya kuingia katika utendaji.


Kuhusu uzalishaji

Msajili huyo alisema inashangaza kuona kwamba mpaka sasa kuna mashirika ya umma ambayo bado yanaitegemea Serikali kulipa mishahara ya wafanyakazi wake.

Aliyataja mashirika hayo kuwa ni Shirika la Ndege Tanzania (ATCL), Kampuni ya Reli Tanzania (TRL), Kampuni ya Hifadhi za Reli (RAHCO) na Mamlaka ya Reli Tanzania na Zambia (Tazara).

Alisema hakuna haja kwa Serikali kuendelea kuwa na mizigo hiyo isiyozalisha ikiwamo kubeba gharama za kuendesha mashirika hayo.

“Wenyeviti na wajumbe wa bodi, pamoja na watendaji wakuu wa kila shirika mkae chini mjitafakari, kwa nini muendelee kuongoza mashirika hayo wakati mmeshindwa kuzalisha. Rais ameniagiza kuwakumbusha kwamba mrejee malengo ya kuanzishwa kwa taasisi zenu,” alisema.

Mafuru alisema taasisi ambazo uzalishaji wake umeshuka lakini gharama za uendeshaji ziko juu, hazina budi kupunguza wafanyakazi ili kulingana na mapato yake.

“Kama hawataweza kufanya hivyo, watafute njia nyingine ya kuongeza uzalishaji kwa kutumia wafanyakazi walionao. Kwenye sekta binafsi, kampuni ikianza kufanya vibaya inapunguza matumizi yake na moja ya njia wanazotumia ni kupunguza wafanyakazi. Huku serikalini utasikia mtendaji mkuu akiandika barua, siyo proposal (mradi), kuomba fedha kwa ajili ya mtaji. Hatuwezi kwenda mbele,” alisema.

Mafuru aliyasema hayo jana katika mkutano maalumu ulioitishwa kwa maagizo ya Rais John Magufuli ili kuwakumbusha watendaji mbalimbali wa taasisi na mashirika ya umma nchini, juu ya wajibu wao katika kuwahudumia wananchi.

Mkutano huo uliwahusisha wenyeviti wa bodi, wajumbe wa bodi na watendaji wa taasisi na mashirika mbalimbali ya umma ambayo kwa sasa yamefika 216, yakiwa na mali zenye thamani ya Sh20 trilioni.

Hata hivyo, alisema pamoja na mtaji huo, taasisi na mashirika ya umma yamekuwa yakichangia Sh185 bilioni kwenye Pato la Taifa.

“Kwa mtaji wa Sh20 trilioni, hicho ni kiasi kidogo sana ambacho kinarudi serikalini. Kwa wenzetu wa sekta binafsi, ukimpatia mtaji huo basi baada ya muda fulani unamkuta kapata mara mbili ya mtaji aliopewa,” alisema Mafuru ambaye amefanya kazi kwenye taasisi za benki kwa miaka 15.

Alisema Rais Magufuli amemtuma kuwakumbusha kila mmoja kwenye taasisi yake ahakikishe anapunguza kero zote zinazopatikana kwa kutumia rasilimali alizonazo.

Alisisitiza kuwa kila mmoja atambue kwamba anawajibika katika kuleta maendeleo ya Taifa hili.

Msajili huyo aliongeza kuwa Serikali imekuwa hainufaiki na mashirika ya umma ambayo ndiyo yangekuwa msaada mkubwa wa kupunguza mikopo ambayo inadaiwa.

Hata hivyo, alisema mashirika yamekuwa yakiiacha kulipa madeni hayo licha ya kwamba yanapata faida kubwa kila mwaka.

“Siyo lazima faida inayopatika kwenye taasisi na mashirika ya umma irudi serikalini, lakini mashirika yenyewe yanaweza kusaidia katika shughuli mbalimbali za maendeleo ambazo Serikali ilitakiwa kufanya” alisema.

Mafuru alitoa mfano wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) akisema linapopata faida kubwa, linaweza kuamua kujenga kipande cha reli kutoka Dar es Salaam mpaka Morogoro na kuisaidia TRL na Serikali.



Wabunge kutopewa posho

Mafuru alisema wabunge ambao ni wajumbe wa bodi za mashirika hayo, hawatalipwa posho za vikao vya bodi kwa sababu wanalipwa posho hizo kwenye kamati zao.

Alisema kuendelea kufanya hivyo ni sawa na kuwalipa posho mara mbili kwa kazi moja, jambo ambalo halikubaliki.

Alisema kuna mpango wa kuwaondoa wabunge kwenye bodi hizo ili washiriki kikamilifu kuisimamia Serikali na kwamba mbunge anapokuwa sehemu ya bodi anakosa uhuru wa kufanya kazi yake kama mwakilishi wa wananchi.

“Shirika linapofanya vibaya wajumbe wote wa bodi wanahusika bila kujali ni mbunge au la. Kuna mbunge mmoja alipata msukosuko wakati wa sakata ya Tanesco, kwa hiyo tunajaribu kuwalinda ili wafanye kazi yao kikamilifu,” alisema.

Kuhusu uteuzi wa wenyeviti wa bodi, Mafuru alisema Rais anawateua kwa sababu anaamini wana uwezo wa kusimamia na kuongoza bodi hizo ili kuleta matokeo chanya.

Alisema wenyeviti wengi wamekuwa wakichukulia nafasi wanazopewa kama zawadi na kushindwa kusimamia majukumu ya mashirika au taasisi husika.

Alisisitiza kuwa uenyekiti ni jukumu kubwa ambalo linahitaji kuifahamu taasisi vizuri ili kutoa maamuzi sahihi.

Aliwataka wenyeviti wa mashirika ya umma kutambua wajibu wao na kuondokana na dhana kwamba wanapoteuliwa basi wanapewa ‘ulaji’.

Kwa upande mwingine aliyataka mashirika hayo kufanya ukaguzi wa hesabu zao na kuwasilisha ripoti katika ofisi yake.

Akitoa maoni yake kuhusu uendeshaji wa mashirika ya umma, Mkuu wa Taasisi ya UsiMamizi wa Fedha (IFM), Profesa Emmanuel Mjema, alisema Wakala wa Manunuzi ya Serikali (GPSA) amekuwa tatizo ambalo linapaswa kuangaliwa. Pia, alisema Wakala wa Huduma za Ufundi na Umeme (Temesa), nao wamekuwa ni tatizo kwa kutopeleka magari kwa ajili ya kufanyiwa matengenezo huku wakitoza fedha, lakini wanaambiwa wapeleke magari hayo GS Motors.

Mafuru alisema amepokea maoni hayo na kuongeza kuwa ofisi yake imekuwa ikipata malalamiko kutoka mashirika mbalimbali kuhusu GPSA na kuahidi kufuatilia na kuyapatia ufumbuzi wa kudumu.

Mkurugenzi Mkuu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS), Albina Chuwa alitaka mishahara ya watendaji wa taasisi na mashirika ya umma iangaliwe upya kwa sababu wapo wanaopata mikubwa kiasi cha Sh36 milioni wakati wengine wanapokea Sh3 milioni.


Sheikh Ponda: Haki yangu imechelewa Kutolewa..Nimekaa Mahabusu Miaka Miwili Bila Kosa

$
0
0
Baada ya kukaa mahabusu kwa zaidi ya miaka miwili kwa kesi ya uchochezi iliyokuwa ikimkabili, Mahakama ya Hakimu Mkazi Morogoro jana ilimuachia huru Sheikh Ponda Issa Ponda, baada ya kukosekana ushahidi wa kumtia hatiani.

Mara baada ya kuachiwa huru, Sheikh Ponda alisema pamoja na uamuzi huo wa mahakama, amekaa mahabusu kwa muda mrefu kutokana na dhamana yake kuzuiwa na Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP), hivyo haki yake imechelewa kutolewa.

 Alisema ipo haja ya Katiba kufanyiwa marekebisho kwa kupunguza mamlaka ya DPP, yakiwamo ya kuzuia dhamana kwa kuwa yeye alikaa mahabusu ilhali hakuwa hana hatia.

Vilio vya furaha vilisikika kutoka kwa wafuasi wa Sheikh Ponda wakiwamo wanawake baada ya Hakimu Mkazi Mfawidhi wa mahakama hiyo, Mary Moyo kumuachia huru.

 Kiongozi huyo wa Taasisi na Jumuiya za Kiislamu aliachiwa huru chini ya kifungu namba 235, cha sheria ya mwenendo wa makosa ya jinai sura ya 20 marejeo ya mwaka 2002.

Hakimu Moyo alisema upande wa mashtaka ulishindwa kuthibitisha  kwa namna gani maneno aliyoyatoa Sheikh Ponda, yameumiza imani za dini na kushawishi watu kutenda kosa.

  Wakili Abubakar Salimu ambaye alikuwa akimtetea Sheikh Ponda pia alisema mahakama imechelewa kutoa haki kwa mteja wake, na kwamba muda alioupoteza mahabusu hakuna mtu anayeweza kuulipa.

 “Sheikh Ponda amekaa mahabusu kwa miaka miwili na miezi mitatu na katika kipindi hicho amefiwa na mama yake mzazi pamoja na baba mkwe wake, na hivyo kushindwa kuhudhuria mazishi, pia alitenganishwa na familia yake, ifahamike kuwa haki inayocheleweshwa ni sawa na haki inayonyimwa” alisema Wakili Salimu.

 Mawakili wa Serikali, Sunday Hyera na George Mbalasa wao walisema kwa nyakati tofauti kuwa hawana cha kuzungumza, kwani tayari kesi imemalizika na mahakama imetoa maamuzi.

 Kabla ya kusomwa kwa hukumu hiyo, Sheikh Ponda alifikishwa mahakamani hapo saa 2:30 asubuhi, akisindikizwa na polisi na askari wa kikosi maalumu cha Magereza waliokuwa na silaha za moto na mabomu ya machozi.

Kiongozi huyo alionekana akijiamini na aliposhuka kwenye gari alikuwa mwenye furaha na baadaye alianza kusoma gazeti.

 Wafuasi wachache wa Ponda waliruhusiwa kuingia ndani ya mahakama hiyo, huku wengine wakizuiwa nje ya uzio kutokana na sababu zilizoelezwa kuwa ni za kiusalama na kuifanya mahakama iwe katika utulivu.

Mashtaka

Awali, ilidaiwa na upande wa mashtaka kuwa Agosti 10, 2013 saa 12.45 jioni Uwanja wa Shule ya Msingi Kiwanja cha Ndege mkoani Morogoro, Sheikh Ponda alikaidi  amri halali ya mahakama, kutoa maneno yenye kuumiza imani za dini na kushawishi watu kutenda kosa.  Mashtaka ambayo aliyakana.

Hata hivyo, shtaka la kwanza na kutotii amri ya mahakama liliondolewa mahakamani hapo, baada ya Sheikh Ponda kushinda rufaa na hivyo kubaki na mashtaka mawili.

Katika kesi hiyo upande wa mashtaka ulikuwa na mashahidi tisa pamoja na vielelezo saba, ikiwamo kamera ambayo ilimrekodi Sheikh Ponda alipokuwa akitenda makosa hayo wakati upande wa utetezi ulikuwa na shahidi mmoja.



CCM Yakanusha Taarifa za Kuridhia Kuapishwa kwa Maalim Seif Kuwa Rais wa Zanzibar

$
0
0
Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimekanusha taarifa iliyosambazwa kupitia mitandao ya kijamii ya kuridhia Mgombea wa Chama Cha (CUF) Maalim Seif Sharif Hamad atangazwe kuwa Rais wa Zanzibar.

Akiongea na waandishi wa habari ofisini kwake Kisiwandui mjini hapa Naibu Katibu Mkuu wa chama hicho Zanzibar, Vuai Ali Vuai, alisema wamepokea kwa msikitiko makubwa taarifa hizo alizoziita za uzushi.

Alisema chama chake hakipo tayari kuvunja katiba wala sheria kwa kuridhia kuwa Maalim Seif atangazwe, kwani uchaguzi uliofanyika tayari umefutwa rasmi na Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC) kupitia Gazeti la Serikali.

"Mtandao huo wa kijamii ulidai kuwa mimi Naibu Katibu Mkuu niliwataka wananchama na wananchi wote kuridhia hatua hiyo iliyofikiwa ya chama chetu kuridhia kuapishwa Maalim Seif , huku nikisisitiza kwa kuwataka wananchi wote wajitokeze kwa wingi katika sherehe za kuapishwa rais", alisema Vuai.

Aliongezea kusema, "mbali ya hayo pia tarifa hizo zilinisingizia nimesema kwa kuwataka wananchi waridhie kuwa Dk Ali Mohamed Shein kuwa ni Makamo wa kwanza wa Rais wa Zanzibar mara bada ya kuapishwa kwa Maalim Seif kuwa Rais".

Alidai taarifa zote hizo zinaonekana kuwa zimeaandaliwa na kundi maalum lenye kutaka kuivuruga (CCM) na wananchama wake na pia kuvuruga mshikamano.

Alisema wanatarajia kukutana na wanasheria wa Chama hicho ili kufanya utafiti juu ya waliotoa taarifa hizo na wakigundulika hatua za kisheria zitachukuliwa.

Kwa upande wa mazungumzo ya kukwamua hali tete ya kisiasa Visiwani, yanayoendelea kati ya Dk Ali Mohamed Shein na Maalim Seif Sharif Hamad, Vuai alisema, wao kama Chama wanayapongeza kwa nguvu zote.

Alisema kuwa ni matarajio yao kuwa mazungumzo hayo yanaweza kuleta tija kwa jamii na taifa kwa ujumla huku akisisitiza kuwa mazungumzo hayo hayataweza kuwa mbadala wa sheria.

Alifafanua kwa kusema kuwa mazungumzo hayo hayataweza kwenda kinyume na sheria ya nchi kwa kuendelea kutangazwa matokeo ya uchaguzi uliofutwa bali inaonekana kuwa yana lengo la kudumisha amani ya nchi kwa viongozi hao.

Alisema kuwa kwa hivi sasa Chama Chao kinajiandaa kwa nguvu zote katika kushiriki uchaguzi wa marudio na kusema kuwa wako tayari kwa kupiga kura wakati wowote.

 "Chama chetu kimo katika harakati za kurejea uchaguzi mara tu Tume itakapoutangaza”,alisema.


Nafasi ya Kazi World Bank Tanzania, Application Deadline 08 December 2015

Sakata la Makontena: Polisi Kwa Kushirikiana na TRA Wakamata Makontena 9

$
0
0
Maofisa wa Jeshi la Polisi  Dar es Salaam kwa kushirikiana na TRA, wanayashikilia makontena 9   Mbezi Tanki Bovu baada  ya  kuyatilia shaka kuwa yalikuwa yanasafirishwa kinyememela usiku wa kumakia leo

Kashfa Nzito ya Ufisadi Wa Trioni 1.2/- Katika Serikali ya JK Yaibuliwa na Zitto Kabwe

$
0
0
Serikali ya Uingereza kupitia shirika lake la kuchunguza makosa ya jinai (AFO), imeibua kashfa ya rushwa katika ununuzi wa dhamana (hati fungani) ya serikali katika kipindi cha uongozi wa aliyekuwa Rais Jakaya Kikwete.

Madai hayo yametolewa jijini Dar es Salaam jana na Kiongozi Mkuu wa Chama cha ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe, katika taarifa yake aliyoisambaza kwenye vyombo vya habari jana.

Katika taarifa yake hiyo, Zitto alidai kuwa biashara hiyo iliyofanyika kati mwaka 2011 na 2012, iliyohusisha serikali na benki ya Standard Group ya Afrika Kusini kupitia Stanbic ya Tanzania ilikuwa na thamani ya Dola za Marekani milioni 600 (sawa Sh. Tanzania trioni 1.2).

Benki ya Standard Group ambayo ni benki mama ya Stanbic Tanzania, imekiri makosa hayo na kukubali kulipa faini ya Dola milioni 25.2 (sawa na Sh. bilioni 54 ) kwa kosa hilo.

Ilikubali kulipa faini hiyo mbele ya Jaji Lord Justice Leveson, wakati shauri hilo liliposikilizwa jana kwenye Mahakama ya Southwark nchini Uingereza.

Benki hiyo ilikubali shauri hilo limalizwe kwa njia ya muafaka baada ya kukiri ilitoa kiasi cha fedha ili kuwahonga maofisa wa Tanzania kinyume na Sheria ya Rushwa ya Uingereza ya mwaka 2010 kufanikisha mpango wao.

Pia benki hiyo imekubali kulipa kiasi cha Dola milioni saba (sawa na Sh. bilioni 15.1) kwa Serikali ya Tanzania kama fidia ya shauri hilo baada ya kubainika walihonga baadhi ya maofisa wa Tanzania kufanikisha mpango huo.

Hata hivyo, fedha hizo hazitakabidhiwa moja kwa moja kwa Serikali ya Tanzania bali zitapitishwa kwenye Wizara ya Maendeleo ya Kimataifa ya Uingereza ili kupangiwa kazi ya kufanya.

Pia benki hiyo inatakiwa kulipa kiasi cha pauni 300,000(sawa na Sh. milioni 974) ikiwa ni gharama za shauri hilo kusikilizwa nje ya mahakama.

Katika taarifa yake, Zitto alitaka mamlaka zenye kuchunguza sakata hilo ikiwamo Benki Kuu ya Tanzania, Kitengo cha Kudhibiti Biashara Haramu ya Fedha (FIU) Tanzania na Taasisi ya Kupambana na Kuzuia Rushwa nchini (Takukuru) waungane na SFO kutoa  taarifa za chunguzi huo na sababu ya kutoziweka hadharani mapema.

Aliomba vyombo vya sheria kuwachukulia hatua wote waliohusika na upotevu fedha hizo za Watanzania.

Alisema hati fungani hiyo ya serikali iliuzwa na serikali kupitia Wizara ya Fedha kwa benki hiyo ya kigeni ambayo ni miongoni mwa kundi la mabenki ya Afrika ya Kusini, yenye makao makuu yake London, Uingereza.

Alisema ni jambo la kawaida duniani serikali kuuza dhamana zake za hati fungani, lakini kwa Tanzania uligubikwa na harufu ya rushwa na kuisababishia nchi hasara.

Alidai kuwa kwa mujibu wa uchunguzi huo, sehemu ya fedha hizo hazikuingia kwenye akaunti za Serikali ya Tanzania na pia gharama za hati fungani hiyo zilipaishwa kupitia wakala wa kati.

Kutokana na upaishaji wa gharama hizo, takriban Dola milioni 60 zilitolewa kwa maofisa waliothibitisha biashara hiyo.

Zitto alimuomba Rais Dk. John Magufuli, kuingilia kati suala hilo akisema jambo hilo lina maslahi mapana ya nchi, hasa ikizingatiwa na uzoefu katika masakata kama hayo yanayohusisha nchi za kigeni, kama ununuzi wa rada, vyombo vya uchunguzi vya hapa nchini, vilitoa majibu ya kutokuwapo kwa rushwa na kisha kuja kuthibitishwa na Serikali ya Uingereza.

“Baada ya kuthibitishwa na Uingereza, serikali yetu ilirudishiwa sehemu ya fedha zilizozidi kwenye manunuzi ya rada, ni vyema Rais Magufuli akaliingilia kati,” alisema Zitto.

Alisema ACT-Wazalendo inasubiri taarifa ya makubaliano kati ya SFO na benki mama ya iliyonunua hati fungani hiyo ili ashauri zaidi hatua za kuchukua.

“Ikumbukwe kuwa Benki ya…(anaitaja jina), ilihusika na kashfa ya Tegeta Escrow na mpaka sasa haijachukuliwa hatua zozote kama ilivyoagizwa na Bunge. Benki hiyo imewaficha waliochota fedha za Escrow mpaka leo,” alisema Zitto.

Alisema kashfa hiyo iliwafanya washauri uongozi wa benki hiyo hapa nchini kuondolewa na kurejeshwa nchini Uingereza kwa hatua zaidi.

Kwa upande wake, Katibu Mkuu Hazina, Ramadhani Kijja, alisema kuwa halifahamu suala hilo na kwamba kwa sasa hana maelezo yoyote juu ya jambo hilo.

“Kama Zitto ndiye katoa hiyo taarifa, mimi sina na wala siwezi kuizungumzia kwa sasa,” alisema Kijja.

Magufuli Azipiga Chini Posho za Wabunge......Posho za Mikutano ya Bodi Ya Mashirika Ya Umma Nazo Zimepigwa Chini

$
0
0
Mpango wa Serikali ya Awamu ya Tano ya Rais Dk. John Magufuli, kupunguza matumizi yasiyo ya lazima ili fedha zitumike kuboresha huduma za jamii, umetua kwa Wabunge wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambao sasa wameondolewa malipo ya posho wakati wanapokuwa katika vikao vya kamati zao mbalimbali za kisekta.

Kwa muda mrefu sasa, imezoeleka kwa wabunge kupokea posho kutoka kwenye mashirika na taasisi mbalimbali za umma wanapoketi kutekeleza wajibu wao ndani ya kamati za Bunge.

Hata hivyo, posho hizo hazitakuwapo tena baada ya Msajili wa Hazina, Lawrance Mafuru, kutangaza jana kuwa sasa posho hizo hazitatolewa tena kwani wanachokifanya wabunge ni sehemu ya kazi zao.

Msajili alitoa agizo hilo wakati wa mkutano wake na wakuu wa taasisi na mashirika ya umma na pia wenyeviti wa bodi zao. Msajili Mafuru alisema agizo hilo limetoka kwa Rais Magufuli, na kwamba sasa kinachotakiwa ni kuona utekelezaji wake.

Bodi zafutiwa Posho za Vikao
Kadhalika, Mafuru alisema serikali imefuta posho za mikutano ya bodi ambazo wamekuwa wakilipwa wajumbe na kuagiza kwamba badala yake, kuanzia sasa watakuwa wakilipwa malipo ya bodi peke (board fees), huku maelekezo mengine yakitaka vikao hivyo vya bodi vipunguzwe kutoka kufanyika karibu kila mwezi na sasa vya idadi ya juu vibaki kuwa vinne pekee kwa mwaka.

Kuna mambo ya hospitality allowances (posho za takrima).  Tumepata taarifa kwamba wabunge wanapofanya kazi za kamati,  huwa wanalipwa fedha na Bunge. Hivyo  kuwapa pesa tena ni double invoice… tunahitaji kuacha hii,” alisema Mafuru.

Alisema zipo taarifa kwamba kuna tatizo la baadhi ya wabunge kuwa katika katika bodi zaidi ya moja na kwamba, utaratibu huo siyo mzuri na unaweza kuathiri utendaji kazi.

Kuna wakati mwingine unakuta mtu mwingine anakaa kwenye bodi hata tano au saba. Sasa inapotokea anatakiwa kuwajibika katika bodi nyingine, anakuwa hawezi kutekeleza wajibu wake kwavile anakuwa amebanwa na ratiba. Ila tunashukuru kwamba sasa hivi kuna effort (jitihada) nzuri zimefanyika kwa kuruhusu kumuondoa mbunge kwenye bodi,” alisema.

Kadhalika, Mafuru alifichua kuwa baadhi ya Bodi za mashirika na taasisi za umma husafiri na kundi la wabunge kwenda nje ya nchi, lakini mwishowe wabunge hao huwa hawafiki eneo la tukio linalowapeleka nje.

Unakuta baadhi ya bodi zinasafiri na kundi la wabunge, halafu tunasikia wengine hawafiki eneo la tukio. Kama ni mbinu ya kutaka wabunge wafichefiche madudu, sidhani kama wabunge wa sasa wananunulika. Mtaenda nao huko nje, lakini wakirudi ndani watawalipua tu,” alisema Mafuru.
Viewing all 104745 articles
Browse latest View live




Latest Images