Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104689 articles
Browse latest View live

NEW SONG:SIKILIZA NA DOWNLOAD MB DOG – UMENUNA


PAUL MAKONDA “NAUNGA MKONO ONGEZEKO LA POSHO LA BUNGE LA KATIBA”

$
0
0
1. Laki tatu(300,000) haitoshi, na mimi nasimamia hilo hadi iongezwe hii kazi ni ngumu. watu wamekuja na wanasheria wasaidizi ili kuwasaidia na kuwashauri.
2. Malipo ya dereva.
3. Nyumba Dodoma zimejaa sana si chini ya elfu arbaini(40,000).
4. Mafuta ya gari.
5. Mtu umeacha kazi zako na familia unakaa dodoma kwa miezi miwili(2).
6. Ada za shule.
7. taarifa za watoto kuumwa. nk.
kwa kweli wakitaka watu watulize mawazo yao kwenye katiba waongeze pesa kidogo, watu wasiwe waoga na nalisema wazi.

THE PHOTOS THAT HAVE SPARKED VICTORIA KIMANI & DIAMOND PLATNUMZ DATING RUMORS

$
0
0
The PHOTOS That Have Sparked Victoria Kimani & Diamond Platnumz Dating Rumors
The One ‘Do Agric’ campaign has brought together atleast 22 African artistes to promote Agriculture among them our very own Victoria Kimani, Tanzania’ s finest artistes Diamond Platnumz, AY, Mwana FA among others but it is the closeness between Vicky and Diamond that has got their fans talking.
After Victoria Kimani uploaded two photos of her with Diamond via her instagram page, most of the fans noted the chemistry between them and with that came the speculations.What is funny is the fact that Diamond Platnumz cannot be spotted with any hot female without dating rumours arising but that can be blamed on the reputation he has with women.

Diamond’s love life has always kept him in the limelight especially because he has dated some of Tanzania’s finest women. Diamond and Victoria are just having a great time working together but you cant blame their fans for trying to have fun because truth be told, they do look good.

While you are at it, make sure you get the message which they are trying to send which is ‘DO AGRIC, IT PAYS!’.Here is another photo

SIRI ZA FREEMANSON TANZANIA ZA FICHUKA!

$
0
0
Tanzania ina wanachama hai zaidi ya 600 wa kundi la watu wenye imani ya siri ya Freemasons wakiwa wanatokana na watu wa kada mbalimbali wakiwemo maarufu, huku ikielezwa kwamba miongoni mwao hakuna viongozi wakuu wa serikali.
Hayo yalibainishwa na Kiongozi wa kundi la Freemasons katika eneo la Afrika Mashariki, Jayantilal Keshavji Chande maarufu kama Sir Andy Chande.
Kiongozi huyo Mtanzania mkazi wa Dar es Salaam mwenye asili ya Kiasia, alisema licha ya Tanzania kuwa na wanachama hao, kwa sasa idadi ya wanachama duniani inapungua tofauti na inavyoonekana sasa kuwa wanaongezeka kutokana na kuibuka maneno mengi kuhusu kundi hilo. Alisisitiza kuwa si rahisi kumjua mwanachama wa kundi hilo, bali wenyewe ndio wanaofahamiana, akisema ni siri na kwamba wenyewe wanakutana katika vikao mbalimbali mara moja kwa mwezi au zaidi.
Alisema nchini kuna wanachama zaidi ya 600 wakiwemo wafanyabiashara, watumishi serikalini, walimu pamoja na wanataaluma mbalimbali wanaoheshimika sana na kusisitiza kuwa kuna maneno mengi yanayosemwa kuhusu kundi hilo, ambayo siyo ya kweli.
Alisema idadi ya wanachama wake duniani inazidi kupungua kutoka milioni nane hadi sasa wako milioni sita, tofauti na wengi wanaodhani kuwa idadi hiyo inaongezeka.
Chande alizungumza na mwandishi wa habari hizi katika Shule ya Sekondari ya Shaaban Robert ambako yeye ni Mwenyekiti wa Bodi ya shule alipozungumzia maadhimisho ya miaka 50 tangu kuanzishwa kwake.
Alisema duniani kuna watu wazito wengi ambao ni wanachama wa kundi hilo kama majaji wakubwa na hata Binamu wa Malkia Elizabeth wa Uingereza ni kiongozi mkubwa wa kundi hilo.
Akizungumzia masharti ya kujiunga na kundi hilo, Chande alisema ni lazima mwanachama huyo awe anaamini katika Mungu bila kubagua iwapo ni Mkristo au Muislamu.
Alisema pia ni lazima anayetaka kujiunga awe na umri unaozidi miaka 21 na walio chini ya umri huo hawaruhusiwi kujiunga na lazima familia ya anayetaka kujiunga na wanandugu wafahamu kuwa umejiunga na kundi hilo.

NANI ANASEMA POSHO YA SH 300,000 KWA SIKU HAZITOSHI BUNGE LA KATIBA

$
0
0
Hata kabla ya kupita wiki moja tangu Bunge Maalumu la Katiba kuanza rasmi shughuli zake, wajumbe wake wameendelea na vituko kiasi cha kutupa wasiwasi kama kweli wengi wa wajumbe hao wanastahili kutuwakilisha katika chombo hicho kufanya kazi ya kihistoria ya kutunga Katiba Mpya. Tulisema jana kupitia safu hii kwamba wengi wa wajumbe wa Bunge Maalumu la Katiba hawaonyeshi kama kweli wanatambua nafasi na hadhi waliyonayo kama wawakilishi wetu katika chombo hicho, kwani vitendo na kauli zao vinajenga picha tofauti. Ndiyo maana tulionya kwamba Bunge linapoanza shughuli zake kwa kutawaliwa na vioja na vituko haliwezi kamwe kufikia malengo yaliyokusudiwa.

Ni jambo la kusikitisha kuwa, pamoja na angalizo letu kwa wajumbe wa Bunge hilo, jana na juzi tulishuhudia mwendelezo wa vitendo vya aibu ambavyo kwa vyovyote vile siyo tu vimekidhalilisha chombo hicho, bali pia vimeibua maswali mengi miongoni mwa wananchi ambao wamehoji kama kweli Bunge hilo limeundwa na watu wenye sifa na hadhi ya kuitwa wajumbe wa Bunge Maalumu la Katiba. Kilele cha vioja na vitimbi hivyo ni pale wajumbe wengi walipozusha zogo mithili ya watoto wa chekechea kwa madai kwamba posho ya Sh300,000 wanazopewa kila siku hazitoshi na badala yake wanataka wapewe Sh420,000.

Ni kichekesho cha karne kwamba akili za wajumbe wengi, badala ya kuelekezwa kwenye ufanisi wa shughuli za Bunge hilo kama kudai wapewe makabrasha yenye nyaraka zilizoandaliwa vizuri au nakala za kutosha za Rasimu ya Mabadiliko ya Katiba pamoja na Sheria ya Mabadiliko ya Katiba, zimeelekezwa kwenye fedha na kuchumia matumbo yao. Tayari wamesahau kwamba waliteuliwa kuingia katika Bunge hilo kujitolea na kujitoa mhanga ili kuhakikisha inapatikana Katiba Mpya na siyo kugeuza uwakilishi wao katika Bunge hilo kuwa ajira.

Kichekesho kingine ni kwamba madai hayo ya kipuuzi waliyatoa wakati wa semina waliyoandaliwa kwa ajili ya kupatiwa rasimu ya Kanuni zitakazoongoza shughuli za Bunge. Badala ya kuzungumzia rasimu hiyo, wajumbe walilifanya suala la posho kuwa kipaumbele chao na kutaka walipwe viwango vya posho kama makamishna wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba walivyolipwa, huku wakipuuza ukweli kwamba makamishna hao na madereva wao walistahili kulipwa viwango hivyo kwa sababu walisafiri nchi nzima, tena katika mazingira magumu na kufanya kazi usiku na mchana. Uzoefu wetu umetuonyesha kwamba wengi wa wajumbe wa Bunge hili watatumia muda mwingi kuchapa usingizi au kukacha vikao. Ndiyo maana wanataka walipwe posho hata wasipohudhuria vikao.

Kwa sababu ya woga usiokuwa na msingi wowote, uongozi wa Bunge umesikiliza upuuzi huo na kuteua kamati ya watu sita eti kwenda kuona ugumu wa maisha ulivyo mitaani. Badala ya kusimamia ukweli kwamba Sh300,000 ni nyingi sana kwa matumizi ya kila siku, uongozi wa Bunge na Serikali sasa utakuwa unaandaa mkakati wa kuongeza posho hizo. Hii ni kinyume na hali ya uchumi wa nchi yetu ilivyo, kwani Serikali imeelemewa na Deni la Taifa la zaidi ya Sh27 trilioni, kwa maana ya Sh20.23 likiwa deni la nje na Sh6.81 trilioni likiwa deni la ndani ambalo Serikali imeshindwa kulilipa. Tusisahau kwamba ukarabati wa Ukumbi wa Bunge umegharimu zaidi ya Sh8 bilioni.
Credits:Mwananchi

MBWANA SAMATTA AMWAGIA SIFA KEDE KEDE MRISHO NGASSA LIGI YA MABINGWA AFRICA

$
0
0
Mshambuliaji wa kimataifa mtanzania anayekipiga  TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, Mtanzania Mbwana Samatta, amesema Mrisho Ngassa wa Yanga amefanya kitu cha maana kwa kupiga ‘Hat-Trick’ mbili mfululizo kwenye Ligi ya Mabingwa Afrika.
Samatta alisema idadi hiyo ya mabao si kazi rahisi kwenye mashindano makubwa kama hayo.
Yanga iliifumua Komorozine ya Comoro mabao 12-2 na kuiondosha kwenye mashindano na sasa itaikabili Al Ahly ya Misri ambayo Samatta amesema si timu ya ajabu lakini si laini kama hakuna mipango ya maana.
Akizungumza na Mwanaspoti kwa simu kutoka Lubumbashi, Samatta alisema: “Mabao sita ni mengi sana kufunga katika Ligi ya Mabingwa Afrika, ni dalili nzuri kwake na kwa timu.
“Pia yanaashiria mambo mazuri kikubwa, lakini asibweteke kwani anaweza kufanya kitu kikubwa katika mashindano hayo endapo Yanga itafanikiwa kusonga mbele.
“Ngassa ni mchezaji mzuri na mwenye uzoefu, kwangu sioni kitu cha ajabu sana kufunga mabao matatu kwenye mchezo mmoja kwa sababu nafahamu uwezo wake, lakini inaashiria pia kwa sasa yuko vizuri sana kimwili na kiakili.”
Kuhusu Yanga na Al Ahly, Samatta alisema: “Al Ahly ni timu kubwa na kama ulivyoona ni mabingwa, lakini mpira ni mchezo wa ajabu, nina imani kama Yanga watajituma, wanaweza kuwavua ubingwa na wao wakasonga mbele.”
Mazembe nayo imo kwenye michuano hiyo na inajiandaa na mechi dhidi ya Astres de Douala ya Cameroon. Kuhusiana na mchezo huo, Samatta ameweka wazi kuwa maandalizi yao ni ya nguvu.
Story kwa hisani ya Mwanaspoti

ALICHOSEMA BERNARD MEMBE JUU YA MGOGORO WA MPAKA KATI YA TANZANIA NA MALAWI

$
0
0
Tanzania bado ipo kwenye mgogoro na nchi ya Malawi juu ya mpaka halisi wa nchi,Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mh Benard Membe amesema hatma juu ya mgogoro huo inategemewa kutolewa mwezi march.
Hukumu hiyo itaamuliwa baada ya jopo la Usuluhishi litakapokaa na kusikiliza pande zote mbili ambalo litaongozwa na Rais wa zamani wa Msumbiji Joachim Chisano
Kupatikana kwa suluhu ya mgogoro wa mpaka huo kutawatoa hofu wananchi wanaoishi pembezoni mwa Ziwa hilo ambao wamekuwa wakitegemea shughuli za uvuvi wakiwemo wakazi wa kijiji cha Manda Jimbo la Ludewa mkoani Njombe.
Wakazi wa eneo hilo wamesema kwa hivi karibuni tangu kutulia kwa vuguvugu la mgogoro huo wamekuwa wakiendelea shughuli zao za maendeleo kama kawaida ikiwemo uvuvi.

VAZI HILI LA DIAMOND LASABABISHA VIDEO YA MSANII DULLY SYKES KUFUNGIWA

$
0
0
Wote tumemsikia Prince Dully Sykes akiongelea kufungiwa kwa video yake ya kabinti special na Baraza la Sanaa Tanzania(BASATA) . Kuna sababu kuu mbili zilizosababisha video hii kufungiwa na ya kwanza  ni kitendo cha msanii Diamond Platnumz kuvaa T-shirt iliyoandikwa neno ambalo ni tusi  . Hii ingekua kwa nchi za mbele basi ungekutwa t-shirt hii wanaifanyia kitu kinaitwa “blurring” yaani
wanayafanya maneno yasisomeke lakini wabongo wakaona isiwe tabu na director akaamua kuacha video irushwe ikiwa katika hali hii.Sababu ya  pili ni vazi la ufukwe yule demu alilovaa kitu ambacho dully ameona haikua mbaya.


HOW TO TEXT A LADY YOU LIKE AND MAKE HER LIKE YOU BACK

$
0
0
So you finally got the number of that lady you’ve been chasing for a while and now another challenge looms. How do you text her in a way that she’ll see you as really cool? Whether it’s through WhatsApp or normal SMS texting, the first few texts are very crucial. They can determine the kind of relationship the two f you will have. They can determine whether you’ll have her n your bed the next weekend, whether you’ll have a long lasting relationship, whether you’ll be ruled out or whether you’ll be put on the friend’s list.   Here are a few tips on how to go about texting a lady you like.

1.      Go ahead and text her….don’t hesitate

Don’t overthink it. You’ll get tensed hence end up saying stupid things, When a lady gives you her number, she wants you to communicate, so do so. Say whatever is on your mind but avoid irrelevant things or common questions like, “What you upto?”

Make sure you keep your text message short, sweet and structured in a query way. By query way I mean that it should not really be a question but it should be put in a way that she’s obligated to respond. Some ladies hate being asked too many questions, especially by guys they don’t know so well. So avoid multiple questions. A simple text won’t just let her know that you are thinking about her and her well-being, it will make her fond of you.

2.      Make her miss you

Don’t be that guy who tests all the time….you’ll become a boring puppy and a nuisance. After the two of you have been texting or WhatsApping each other for a while, go MIA. Stop replying to all her messages or take time before you reply. If she’s a little angry when you get back to her, apologize and tell her about something cool you had to do. Her anger will soften into soft admiration. And you know what they say, there’s no better way to woo a lady than to give her mixed emotions..

3.      Employ emotions

Tell her about something crazy or sad that just happened to you but you were able to handle it. She will sympathise with you and feel some sort of emotions gearing towards you. Do not tell her about something you were unable to handle because she might see you as weak or in desperate need of help. And ladies don’t like guys who come with loads of problems..

4.      Timing is key

Know the appropriate times to text her depending on what she does for a living or depending on the kind of person she is. Texting her when she’s busy will only make her more disinterested. If you are dealing with a busy lady, evenings are the best times to text. Evenings are usually the times when single ladies desire affection the most. Tell her sweet things that she can fantasize about. Make her laugh, then don’t text again until the following evening. Not unless she misses you and decides to text sooner.

MATOKEO KIDATO CHA NNE 2013 HAYA HAPA SASA

MWANAFUNZI AJICHOMA KISU BAADA YA MATOKEO YA KIDATO CHA NNE [2013] KUTOKA

$
0
0
Kijana ambae jina lake halija famika mpaka sasa,aneishi mwananyamala
 dar es salaam anae semekana kuwa ni mwanafunzi ambae alimaliza kidato
cha nne mwaka jana yan elfu 2013 alikutwa amejichoma kisu shingoni na
 kuwahishwa hospital ,huku chanzo kikisemekana kuwa ni matokeo yako ya
 kidato cha nne,matokeo yake hayakuwa mazuri maana amefeli kwa kupata
 ziro...

Tutazidi kuwapa taarifa

FULL MITEGO YA MREMBO ALIYENASWA FARAGHA NA MSANII DAVIDO WA NUMBER 1 REMIX...NI SHIDAAAA

$
0
0





Huyu Ndio Mdada anayesemekana ndio Girl Friend wa Mwanamuzi Davido kutoka Nigeria ...
Cute Eehhh?

EXCLUSIVE: MGANGA WA DIAMOND YAMEMKUTA

$
0
0
Stori: CHANDE ABDALLAH NA DENIS MTIMA
KIBAO kimegeuka! Yule mganga anayejitapa kumtengenezea nyota ya mvuto staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’, Ustadh Yahya yamemkuta mazito.

Habari za uhakika zilizolifikia gazeti hili zinaeleza kuwa jamaa huyo anahenyeshwa na polisi akiwa mahabusu kufuatia madai ya wizi wa gari aina Toyota Rav 4 ‘milango mitatu’.
Kwa mujibu wa chanzo makini, gari hilo liliibwa wiki kadhaa maeneo ya Msimbazi-Kariakoo jijini Dar.

HABARI ZA AWALI
Habari za awali zilidai kuwa gari hilo lilifika mikononi mwa Ustadh kutoka kwa mwanamke aliyetajwa kwa jina moja la Mwanahamis ambaye ilisemekana kwamba alikuwa akichukua dawa kwa mganga huyo.

Ilidaiwa kuwa mwanamke huyo naye alihongwa gari hilo na mume wa mtu huku akiwa hajui kuendesha hivyo aliliweka poni kwa Ustadh ambaye alimpa dawa ambayo aliipeleka Kigoma kuwauzia watu wake.

Hata hivyo, ilizidi kudaiwa kwamba mwanamke huyo alichukua dawa za shilingi milioni 3 lakini akashindwa kurudisha fedha hizo na riba waliyokubaliana na mganga huyo.
Ikazidi kudaiwa kuwa, Ustadh alimuongezea dawa nyingine mwanamke huyo hadi kufikia deni la shilingi milioni 6 ndipo akaamua kulichukua gari hilo.

NI UZEMBE?
Ukiacha stori hizo za awali ambazo zilikosa ‘balansi’, kuna habari nyingine kuwa gari hilo mali ya Edric Magayane liliibwa baada ya kuachwa eneo la tukio likiwa ‘sailensi’ bila mtu ndani.
Ilielezwa kwamba aliyekuwa na gari hilo aliingia dukani kununua vitu na alipotoka alichanganyikiwa akidhani gari hilo lilikuwa limevutwa na watu wa ‘breki dauni’ waliokuwa wakivuta magari yaliyoegeshwa hovyo katikati ya jiji.
Habari zinasema kuwa mhusika alikwenda kulitafuta katika ‘yadi’ zinakopelekwa magari yaliyovutwa lakini hakuliona.

POLISI
“Alichokifanya ni kwenda kuripoti polisi ambao walianza kulisaka Dar bila mafanikio.
“Wakati polisi wakiendelea kulisaka kuna mtu akasema amemuona Ustadh akitanua nalo.
“Yule mwenye gari (Magayane) alimtafuta Ustadh hakumpata. Akaelekezwa nyumbani kwake, Kigogo Luhanga, Dar au Urambo, Tabora.
“Jamaa alipatafuta nyumbani kwa Ustadh, Kigogo hadi akafika akiwa na polisi waliovalia kiraia lakini hawakumkuta.

ALITAKA KULIRUDISHA?
“Waliambiwa amesafiri Tabora. Pia walihakikishiwa kwamba kweli Ustadh alikuwa na gari hilo. Jamaa akaambulia namba za simu.
“Alipompigia simu Ustadh alimwambia kama gari limeibwa ana uwezo wa kutumia uganga wake kulirejesha kwa kuwa ni mtaalam wa mambo hayo.
“Ustadh aliomba apewe fedha ili afanye mambo yake gari lirudi. Kweli alitumiwa fedha, lakini akawa anazungusha huku akijiita majina lukuki kama Maimuna na mengine,” kilisema chanzo hicho cha kuaminika.

MKOKO WATAFUTIWA MTEJA
Baadaye polisi walifanya uchunguzi na kubaini kuwa, gari hilo lilikuwa likitafutiwa mteja mkoani Tabora lakini ilishindikana kutokana na kukosa ‘dokyumenti’ muhimu.

GARI LAKAMATWA
Habari zilizidi kutiririka kwamba, wakati Ustadh akikatiza na gari hilo Tabora mjini ndipo alipokamatwa na polisi kisha kuwekwa nyuma ya nondo za mahabusu kabla ya kusafirishwa jijini Dar kwa hatua zaidi za kisheria.

MASHITAKA MAWILI
Habari za uhakika zilieleza kuwa, Ustadh alipofikishwa Kituo cha Polisi cha Kati (Central), Dar alifunguliwa mashitaka mawili; wizi wa gari na kujipatia fedha kwa njia isiyo halali.
Baada ya kujikusanyia habari hizo, juzi gazeti hili lilishuhudia polisi wakipekuwa nyumbani kwa Ustadh kisha kumrejesha kituoni kwa ‘difenda’ huku amepigwa pingu mikononi.

MMILIKI ANENA
Akizungumza na gazeti hili juzi, mmiliki wa gari hilo, Magayane alikiri maelezo yote juu ya habari hiyo.
Alipoombwa namba ya jalada la kesi aliitaja kuwa ni MS/RB/827/ 2014-WIZI WA GARI NA KUJIPATIA FEDHA KWA NJIA ISIYO HALALI.
Jitihada za gazeti hili kuzungumza na Ustadh juu ya msala huo mzito ziligonga mwamba kwa kuwa simu yake ilikuwa haipatikani na bado alikuwa mahabusu huku ikelezwa kwamba soo limemkalia vibaya.

DIAMOND KAINGIA MITINI?
Kwa mujibu wa chanzo kingine, Diamond amekuwa akiombwa kumsaidia jamaa lakini akaingia mitini kwa madai kuwa hapendi kuhusishwa na Ustadh ambaye aliahidi msanii huyo kupata majanga makubwa baada ya kumkimbia na kwenda kwa waganga wengine.
Diamond alipotafutwa juzi kwa njia ya simu hakupatikana huku mmoja wa watu wa timu yake akisema yupo Afrika Kusini ‘Sauzi’ kwa ajili ya kufanya kolabo na D’Banj wa Nigeria.
Credits:Global Publishers

MAPENZI YA RAY, CHUCHU HANS NI PIGO!

$
0
0
Stori: Gladness Mallya na Hamida Hassan
Ni pigo kubwa! Ile ndoa inayodaiwa kukaribia kufungwa kati ya nyota wa filamu Bongo, Vincent Kigosi ‘Ray’ na Miss Tanga 2006 aliye pia msanii wa filamu Bongo, Chuchu Hans imepingwa isifungwe mpaka mambo f’lani yakae  sawa.
Kwa mujibu wa mtonyaji wetu, Ray na Chuchu wako mbioni kufunga ndoa wakati wowote kuanzi Mei, mwaka huu, lakini mjadala mzito uliopo mbele yao kwa sasa ni uhalali wake.
“Unajua wanachofahamu wao (Ray na Chuchu) wanaweza kufunga ndoa kwa ulaini kabisa, lakini ukweli ni kwamba kuna ugumu mkubwa.

UGUMU ULIPO
“Kanisa analosali Ray, viongozi wanasema wao si wa dunia hii mpaka wakubali kufunga ndoa ambayo mmoja wa wahusika ana ndoa yake,” kilisema chanzo hicho.
Kikaendelea: “Kwa hiyo kama wako tayari kufunga ndoa hiyo lazima Chuchu akubali kubadili dini yeye ndipo ataruhusiwa kungia kanisani kufungishwa ndoa.”

KANISA LA RAY
Juzi Alhamisi, Risasi Jumamosi lilifunga safari hadi kwenye Kanisa la Living Water-Makuti Kawe, Dar ambako mpaka mwaka uliopita magazeti pendwa yaliandika Ray anaabudu huko.
Lengo la Risasi Jumamosi lilikuwa kuonana na Mtume na Nabii Onesmo Ndegi lakini hakuwepo ofisini, ila msaidizi wake mmoja alipopatikana alikiri kumfahamu Ray.
Msaidizi:  Ray alishasali hapa, lakini sijamwona siku nyingi, sijui ana matatizo gani?
Risasi Jumamosi: “Oke, tukiacha hilo la kutofika kwa siku nyingi. Lililopo sasa hivi ni kwamba anataka kufunga ndoa na dada mmoja anaitwa Chuchu Hans ambaye ana ndoa tayari, hajaachika na mumewe yu hai. Unasemaje kuhusu hilo?
Msaidizi: “Sisi hatuamini katika kuachana. Kama alishafunga ndoa na mume yupo hai, hao wametengana tu, lakini ndoa yao ipo.
“Huyo mwanamke alishajifunga, kifungo chake kitatenguliwa pale tu mumewe atakapoondoka duniani (kifo).

KANISA LA MTAKATIFU MAXIMILIAN KOLBE
Baada ya kuondoka kanisani hapo, mapaparazi wetu walikwenda Kanisa Katoliki Parokia ya Mtakatifu Maximilian Kolbe, Mwenge, Dar es Salaam.
Risasi Jumamosi liliambiwa Baba Paroko hakuwepo kwa wakati huo, lakini muumini mmoja aliyesema yeye ni mwalimu alipoulizwa kuhusu nafasi ya Ray kufunga ndoa na Chuchu Hans alisema:
“Maandiko yako wazi. Sasa kama huyo mwanamke ana mume wake tena mmesema yupo nje ya nchi, siku akija si atamshika ugoni kwa mke wake?
“Huwezi kufunga ndoa kama bado una ndoa. Mungu hajaagiza hivyo. Ndiyo maana sisi (Wakristo) huwa tunatoa siku ishirini na moja za kutangaza ndoa ili kama kuna mwenye pingamizi ajitokeze na kulianika.
“Watu waongo siku hizi. Wapo wachumba wanakuja kuandikisha ndoa kumbe mmoja bado yupo kwenye ndoa halali.”

IMANI YA KIISLAM INASEMAJE?
Mapaparazi wetu hawakuchoka, walimtafuta Shehe Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Alhadi Musa Salum ambaye kuhusu Ray na Chuchu kufunga ndoa alifunguka hivi:
“Kama Chuchu ni Muislam, itabidi Ray abadili dini awe Muislam, si vinginevyo.”
Risasi Jumamosi: Chuchu alifunga ndoa Bomani na mume Mkristo, ila yeye Muislam. Inakuwaje hapo?
Sheke Mkuu: “Itakubalika kama Ray atabadili dini tu, maana hiyo ndiyo ya Bomani, Kiislam siyo.”

JOHARI, MAINDA WAPATANA
‘Johari’ ambaye ni Blandina Chagula na ‘Mainda’ mwenye uhalisia wa jina la Ruth Suka (zamani Mwanaid), wawili hao sasa ni mashosti wakubwa baada ya kuwa na bifu la miaka 8 kisa kikitajwa  kuwa ni ‘kaka mkubwa’ huyo (Ray) kuwachanganya kimapenzi.
Kwa mujibu wa chanzo, mastaa hao wanaotamba kwenye filamu za Bongo kwa miaka mingi wameamua kumaliza tofauti zao huku wengi wakitafsiri kuwa, wanashikamana kwa sababu ya  kuumaliza uhusiano wa Chuchu na Ray. Haikufafanuliwa.

MADAI MENGINE
Pia ilidaiwa kuwa, Mainda aliamua kumaliza bifu na Johari kwa sababu mchungaji wake alimtaka  kufanya hivyo.
“Niliwakuta kambini wakishuti filamu, Mainda akaniambia aliitwa kushiriki filamu hiyo kama mpambaji, Johari yeye amecheza baadhi ya  vipande ndipo Mainda akamtaka mwenzake wamalize tofauti zao,” kisema chanzo chetu.
Hivi karibuni, Risasi Jumamosi liliinasa picha iliyotundikwa mtandaoni na Mainda akimwonesha yeye, Johari na Mtangazaji wa StarTV, Sauda Mwilima.
Mainda aliisindikiza picha hiyo na maneno  yaliyosema: “Nimejifunza kitu katika maisha, kusamehe.”
KAKA MKUBWA RAY
Juzi, Risasi Jumamosi lilimpigia simu ya mkononi Ray lakini hakupokea. Akatumiwa meseji, hakujibu!
CHUCHU HANS
Baada ya kusomewa mashitaka yote, alijibu kwa ufupi: “Sina cha kuongea.”
JOHARI
Johari naye hakupokea simu yake ya mkononi licha ya kuita kwa muda mrefu na kukatika kisha kupigwa tena. Akatumiwa meseji, hakujibu!
MAINDA
Na yeye simu yake iliita sana bila kupokelewa, akatumiwa meseji, hakujibu!
Credits:Global Publishers

MIMI NILIACHWA HIVI..JE WEWE ULIACHWA VIPI NA MPENZI WAKO?

$
0
0

Katika haya mahusiano ya Kimapenzi, ktk kuachwa na wapenzi, nyie mliachwa kwa style gani? Mimi ktk mahusiano kadhaa niliachika hivi:


Kuna mmoja tulipendana sana, yaani sana, huyu nilisoma nae A- level, na kikubwa nilichomvutia ni upstairs, nilikuwa nakimbiza sana ktk combination yng ambayo na yeye, alikuwa anasoma! Tulikuwa boarding school, pamoja na mapenzi ya dhati ambayo nilipendwa na huyu kiumbe, F 5 na 6 sikuwahi kupewa papuchi.


Alikuwa na kauli yake "kuwa na subira J, katika siku ya ajabu, nitakupa vitu vya ajabu" Nilikuja kuachwa siku ya kwanza ya Orientation ya 1st yr kisa nilihoji kwa nini anaambatana na mkaka 1 na kila nikiwakuta wanaongea ki-external (kilugha) Niliambiwa mwanzo na mwisho wako leo kunifuatilia!


Huyu alikuwa wa kitaani Moro, nikiwa chuo DSM, alikuwa akija kuniletea papuchi! aalinipigia simu nirudi moro, kuna shida ya dharula, nikafikia hotel badala ya home. Alikuja kunipa penzi chupu chupu niwehuke! Kuanzia saa 4 usiku mpaka saa 9, kila nikilala, naamshwa! mpk nikamuuliza ******** una nini leo? mbona si kawaida yako? Asubuhi akaniogesha kwa mara ya kwanza, tusharudisha chumba tunatembea, akanambia "leo home inasomwa barua yangu ya posa" nilikuwa natafuta namna ya kukuaga! Mimi hoi!


Mwenzangu , naomba kupata mbinu zilizotumika wakati unaachwa kwa namna 1 ama nyingine! Kama vp pita kimya kimya!

BUNGE LA KATIBA-POSHO WANAZOTAKA ZAPINGWA KILA KONA

$
0
0
Wakati maombi ya baadhi ya wajumbe wa Bunge Maalumu la Katiba ya kuongezewa posho yakipingwa kila kona, uongozi wa muda wa Bunge hilo umeunda kamati kuchunguza uhalali wa maombi hayo.

Juzi, ndani ya kikao cha Bunge hilo, baadhi ya wajumbe walieleza mahitaji yao ya posho kuongezwa wakisema kiwango cha Sh300,000 (Sh80,000 za kujikimu na Sh220,000 kwa kikao), hakitoshi.

Baada ya maombi hayo, Mwenyekiti wa Muda wa Bunge, Pandu Ameir Kificho aliahidi kuliwasilisha suala hilo serikalini ili lifanyiwe kazi, lakini jana aliamua kuunda timu ya wajumbe sita kuchunguza uhalali wa posho hizo.

Posho kupingwa

Baadhi ya vyama vya siasa, wanaharakati na wananchi wa kawaida wameshangazwa na maombi hayo ya posho, wakisema wajumbe wamesahau kilichowapeleka bungeni na kukimbilia kutetea masilahi yao.

Vyama vya Chadema na CUF kwa nyakati tofauti, vilisema kuwa vitaanzisha juhudi za kuwataka wabunge wao ambao ni wajumbe wasusie agenda yoyote inayotaka kuongezwa kwa posho hizo.

Tamko la vyama hivyo limetolewa huku Chama Cha Mapinduzi (CCM), ambacho wajumbe wake ndio wanaodaiwa kupigia debe mpango huo, kikisema kitatoa ufafanuzi juu ya hoja hizo baada ya kupata ‘taarifa rasmi’.

Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Willibrod Slaa alisema jana kuwa wajumbe hao hawakupaswa kudai nyongeza ya posho kwa vile hawakutumwa kwenda Dodoma kudai marupurupu ya fedha.

Alisema kuanza kujadili suala la nyongeza ya posho badala ya kuzungumzia hoja za msingi zilizopo kwenye Rasimu ya Katiba, ni sawa na kuwapuuza wananchi ambao wanasubiri kupata Katiba Mpya.

“Wametoka kwenye hoja na kutupeleka kwenye mambo mengine ambayo hayana msingi wowote. Sisi kama Chadema tunapinga na tunataka wabunge wetu watambue hilo,” alisema.

Alisema wale wanaolalamika kwamba Sh300, 000 hazitoshi wanajaribu kupindisha ukweli, kwani kuna baadhi ya watumishi wa Serikali wanalipwa kiasi hicho ikiwa ni mshahara wao wa kila mwezi.

Alisema Chadema kimewataka wabunge wake kutojiingiza kwenye malalamiko hayo badala yake wazingatie kile walichotumwa na wananchi kwenda Dodoma.

DIAMOND KUHUDHURIA TUZO AFRIMMA ZITAKAZO FANYIKA MAREKANI TEXAS

$
0
0
July 26 mwaka huu, wasanii wengi wakubwa Afrika kutoka katika mataifa ya 17 watakutana Dallas, Texas, Marekani kuhudhuria utoaji wa tuzo za kiafrika zinazojulikana kama ‘AFRIMMA Awards’, na tayari Diamond Platinumz tayari ameshaonesha uthibitisho wa kuwa katika daftari la mahudhurio siku hiyo.

Diamond amepost kwenye Instagram video inayomuonesha akifanya promo maalum iliyoandaliwa na watayarishaji akiwaambia mashabiki kwa swag za kimarekani kuwa atakuwepo siku hiyo, na kisha akaisindikiza na maneno yanayosomeka, “Yess! i'll be ryt there....Afrimma Awards 26/07/2014 Texas, Dallas (USA).”

Tuzo hizo zilizoandaliwa na Big A Entertainment na African Muzik Magazine, zimelenga katika kuwatunuku wasanii mbalimbali wakubwa wa Afrika waliopo duniani kote na itagusa nyanja mbalimbali za burudani ikiwa ni pamoja na wasanii wa muziki, wachezea santuri aka Dj’s, watayarishaji wa muziki, mameneja na watu wanaousapoti utamaduni wa Afrika.

Tuzo hizo zinatarajiwa kusindikizwa na vicheko vya mara kwa mara kwa kuwa mshereheshaji wa shughuli hiyo ni mchekeshaji maarufu wa kimataifa, The Basket Mouth na atakuwa na muigizaji mrembo wa Nollywood, Juliet Ibrahim.

WIZKID AWA MSANII WA KWANZA AFRICA KUFIKISHA FOLLOWERS MILIONI MOJA KWENYE TWITTER

$
0
0
Ayodeji Ibrahim Balogun aka Wizkid, amekuwa msanii wa kwanza wa Naija kufikisha wafuasi millioni moja kwenye mtandao wa kijamii wa Twitter.

Msanii huyo mwenye umri wa miaka 23, amefikisha idadi hiyo Februry 19, 2014 huku akiwaacha wasanii wenye majina makubwa na waliotangulia kufahamika kwenye game duniani kabla yake.

D’Banj anafuatia akiwa na wafuafi zaidi ya 816,000, Don Jazzy 719,000, 2face Idibia 686,000 na muigizaji wa kike Genevieve Nnaji 542,000.

HII NDIO IDADI YA TEMBO WALIO BAKI MBUGA YA SELUU

$
0
0
Meno ya tembo bado ni ishu kubwa na stori zake bado zinazidi kumiliki headlines kutokana na ukweli kuhusu wanyama hawa wanavyoshambuliwa na majangili mbalimbali,February 20 Meneja uhusiano wa hifadhi ya Seluu ametoa idadi kamili ya Tembo waliobaki.
February 20 2014 mara baada ya kukabidhiwa zaidi ya Milioni 42.5 kutoka hotel zilizopo Seluu Mr Benson Kibonde ambaye ndiye Meneja uhusiano wa mbuga ya Seluu amesema>> ‘Hali  hii si nzuri kabisa licha ya hatua mbalimbali zinazochukuliwa na serikali’
Ingawa mpaka sasa haijatoka idadi kamili ya mbuga zingine jumla ya tembo waliuwawa lakini kwa mbuga ya Seluu peke yake imebakisha tembo 13,000 tu kutoka 70,000 waliokuwepo mwaka 1990 kwa mujibu wa Mr Kibonde.

Miongoni mwa sababu alizozi-amplify Mr Kibonde ni kuhusu majangili hao ambao amesema ujangili ni tatizo kubwa ambalo unafanywa na watu wenye fedha nyingi na wana mtandao wa kimataifa hali inayosababisha kazi hiyo kuwa ngumu.
Bado mbuga zetu za Tanzania zina changamoto nyingi ambazo miongoni mwa alizozieleza Mr.Kibonde ni pamoja na kufanya kazi kwenye mazingira magumu,mafuta ya magari kutojitosheleza, chakula na vitendea kazi vingine kukosekana.

WAYNE ROONEY AJIFUNGA MANCHESTER UNITED..ASAINI MKATABA WA KUICHEZEA MPAKA 2019

$
0
0
Wapenzi wa Manchester united hii itakuwa habari ya nzuri kwao kwasababu mtu muhimu kwenye kikosi chao amesaini mkataba wa kuendelea kuichezea timu hiyo kwa muda mrefu zaidi.
Rooney amesaini mkataba wa kuendelea kuwa na club ya Manchester united kwa miaka 4 zaidi ambapo atakuwa hapo hadi 2019.
Picha kwenye instagram ya Man united ambayo inamuonyesha Rooney akisaini mkataba huo pembeni ya kocha wake imepewa caption hii “Great news for #mufc as Wayne Rooney signs a four-year contract extension keeping him at #mufc until June 2019. #rooneymufc”
Viewing all 104689 articles
Browse latest View live




Latest Images